AFTER PARTY YA LADY IN RED KUFANYIKA FEB 22
↧
↧
KALAMA NYILAWILA ASAINI MKATABA WA KUCHEZA NA BINGWA KATI YA MASHALI AU KASEBA MEI MOSI
Promota wa ngumi nchini Ali Mwazoa akipeana mkono na Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi baada ya kumsainisha bondia Kalama Nyilawila katikati anaetarajia kuzipiga mei mosi. |
Promota wa ngumi nchini Ali Mwazoa akipeana mkono na Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ostadhi baada ya kumsainisha bondia Kalama Nyilawila katikati anaetarajia kuzipiga mei mosi Picha na www.superdboxingcoach. |
========== ========= =======
Bondia Kalama Nyilawila ameingia mkataba wa makubaliano na promota Ali Mwazoa wa Tanga kwa ajili ya mpambano wa Mei Mosi mwaka huu ambapo anasubiri mshindi wa mpambano kati ya Thomasi Mashali na Japhert Kaseba ambao watazichapa March 29 katika ukumbi wa PTA Sabasaba ambapo mshindi atacheza na
Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo bondia Kalama Nyilawila alijitapa kwa kusema iwe Mashali awe Kaseba yoyote atakae kutana nae ato kuwa na masihara nae atampiga kipigo cha mbwa mwizi kwani nafasi hiyo alikuwa anaitafuta siku nyingi baada ya kupoteza huwezo wake katika masumbwi hivyo sasa wakae mbali na mimi kwani nakuja kwa nguvu mpya kabisa akisema atakuwa hatari kama 'Mbeya City' timu ambayo inatoka mkoani kwao na kufanya maajabu kwa kuitawala ligi kuu ya Tanzania bara ndivyo na mimi nitakavyofanya
Kalama katika harakati zake za kuhakikisha anarudi katika chati kama zamani mechi yake ya mwisho katika kuukaribisha mwaka 2014 alimsambalatisha bondia Ibrahimu Maokola bila huruma kwa kumpiga K,o ya raundi ya pili mpambano uliofanyika katika ukumbi wa Msasani klabu
Nae promota wa mpambano huo Mwazoa amesema kila kitu kinaendelea vizuri ikiwemo mapambano ya utangulizi yenye mabondia bora wanaotamba kwa sasa ambao wapo kwenye kiwango cha ali ya juu kwa kuwa mwaka huu ni wa masumbwi nchini Tanzania nimeanza na nitaendelea kusapoti na kupromot mchezo wa ngumi popote nchini
akizungumza kwa niaba ya chama kilichopewa dhamana ya kusimamia mchezo huo wa mei mosi Rais wa TPBO Yassini Abdallah 'Ostadhi' amesema watanzania wana bahati sana kwa kujitokeza promota mwenye uchu wa maendeleo kwa mabondia kwana mabondia wote wame saini mkataba na kupewa posho ya kufanyia mazoezi isipokuwa bondia mmoja tu kati ya watakaocheza march 29 ni Kaseba au Mashali jibu ndio tunasubili siku hiyo nani zaidi na atakaepata nafasi ya kuchapana na Kalama
↧
WASANII WAWAOMBA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA KUZINGATIA MASUALA YA WASANII
Mjumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta (mwenye koti jeusi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi kutoka mashirikisho mbalimbali ya wasanii wa nchini . Viongozi hao walikuwa mjini Dodoma jana kwa ajili ya kuwaomba wajumbe wa mkutano huo kuzingatia masuala ya wasanii katika maboresho ya rasimu ya Katiba mpya.
Baadhi ya viongozi kutoka mashirikisho mbalimbali ya wasanii wa nchini wakibadilishana mawazo jana wakati walipofika kwenye eneo la Mkutano Maalum wa Bunge Maalum kwa lengo la kuwaomba wajumbe wa mkutano huo kuzingatia masuala ya wasanii katika maboresho ya rasimu ya Katiba mpya.
Wajumbe wa Mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Stephen Ngonyani (kulia) na Dkt. Hamis Kigwangalla (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi kutoka mashirikisho mbalimbali ya wasanii wa nchini . Viongozi hao walikuwa mjini Dodoma jana kwa ajili ya kuwaomba wajumbe wa mkutano huo kuzingatia masuala ya wasanii katika maboresho ya rasimu ya Katiba mpya. Picha na MAELEZO-Dodoma
↧
ZANZIBAR NA OMAN KUSHIRIKIANA KIELIMU
Na Maua Ally .
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imetaja majina ya wanafunzi saba wa Zanzibar waliochaguliwa kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza katika fani mbali mbali kupitia mpango wa masomo unaodhaminiwa na Serikali ya Oman (OAF).
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Mazizini baada ya kumaliza ziara ya siku nne nchini Oman, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna amesema wanafunzi hao wamepatikana baada ya kuwafanyia mchujo zaidi ya vijana 300 walioomba nafasi hizo.
Amesema kamati kutoka pande mbili, Zanzibar na Oman, ilikaa pamoja kupitia majina ya wanafunzi wote walioomba na kuchangua vijana saba waliofanya vizuri zaidi katika mitihani yao na hivi sasa wanatafutiwa vyuo vya kusoma katika nchi za Ulaya na Marekani .
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali amesema vijana waliotakiwa kuomba nafasi hizo ni waliomaliza kidato cha sita mwaka 2013 na kupata daraja la kwanza na la pili. Amewataja vijana hao kuwa ni Adam Kassim Ali atakaesoma Uhandisi wa uchimbaji mafuta, Al- Kassim Mohd Nassor El Mazrui atakaechuka fani ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano na Khadija Hilal Al Habsy atakaesoma Sayansi na Hesabu.
Wengine ni Mize Burhan Omar na Juwairia Mohd Ali ambao watasoma Medicine, Ahmed Makame Mwadini na Salma Mohd Ali watakaochukua masomo ya ufamasia. Waziri Shamhuna amewapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa na kuongeza kuwa kuteuliwa kwao kunatokana na uwezo uliotokana na matokeo mazuri ya mitihani yao.
Ametoa wito kwa wanafunzi wengine wa kidato cha sita ambao watafanya mitihani yao mwaka huu wajitahidi kusoma kwa juhudi na kufanya vizuri ili waweze na wao kuomba nafasi hizo za masomo na hatimae kuchaguliwa.
Waziri wa Elimu amesema Serikali ya Oman itaendelea kugharamia nafasi za masomo kwa wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar SUZA na wafanyakazi wengine ambapo watakaporejea watafanya kazi SUZA.
“Nafasi hizo za masomo zitakuwa katika vyuo vikuu mashuhuri Duniani ambavyo pia wanafunzi wa Oman wanasoma,”alieleza Waziri Shamhuna.
Ameongeza kuwa tayari wazanzibari watano wameshajiunga na vyuo vikuu kwa masomo ya shahada ya uzamili na uzamivu na wengine sita wanakamilisha taratibu ili na wao waweze kujiunga mwaka huu.
Amesema kufuatia ziara hiyo, Serikali ya Oman imekubali kuongeza nafasi zaidi kwa wanafunzi kutoka Zanzibar kusoma katika Vyuo Vikuu vya Oman na kwa mwaka huu mwanafunzi Omar Juma Omar ameshajiunga na Chuo Kikuu nchini Oman.
Aidha amesema wamekubaliana kuongeza ushirikiano katika utoaji wa mafunzo kwa walimu wa masomo ya sayansi, Hesabati na Kiingereza kwa Skuli za Sekondari na wahudumu wa maabara.
↧
NINATOA TAMKO LA KUPINGA NA KUKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOFU NA UHARIBIFU WA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA- ALEX KASSUWI
NDUGU ZANGU ASANTENI KWA KUNIPIGIA SIMU NYINGI SANA NA KUNITAKIA KHERI. NILIKUWA SAFARINI. ASANTENI KWA SUPPORT.
NINATOA TAMKO LA KUPINGA NA KUKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOFU NA UHARIBIFU WA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA MIMI BWANA ALEX KASSUWI MMILIKI WA SWAHILI TV NINAKANUSHA HABARI ZA UPOTOFU KWA JAMII NA UHARIBIFU ULIOKUSUDIWA KUNICHAFUA KWA UPUUZI KABISA. HABARI ZILIZOTOLEWA SIO ZA KWELI.
CHANZO CHA YOTE NI KUDAI HAKI ZANGU KATIKA SWAHILI TV NA HAKI ZA WATOTO WANGU KATIKA WIZI ULIOFANYWA NA BWANA AUGUSTINO MALINDA KUIBA HELA ZA MICHANGO YA MSIBA NA TAMAA ZA BWANA DICKSON MKAMA KWANZA NAPENDA UMMA UELEWE KWAMBA MIMI BWANA ALEX KASSUWI NDIO MMILIKI HALALI WA SWAHILI TV NA SWAHILI TV BLOG NA DOCUMENT ZOTE NINAZO. NILIANZISHA NA KUSAJILI KIHALALI KWA KUFUATA TARATIBU ZOTE ZA KISHERIA KAMPUNI YANGU SWAHILI TV NA KAMPUNI ZINGINE
TANZU HAPA MAREKANI ZAMANI HATA KABLA SIJAMJUA NA NILIKUWA SIJAWAHI KUKUTANA NA BWANA AUGUSTINO MALINDA NA BWANA DICKSON MKAMA. SWAHILI TV MBALI NA KUWEKA VIPINDI ONLINE, INAZALISHA NA KUUZA VIPINDI KATIKA TV ZINGINE, HAPA AWALI NIKIWA PEKE YANGU NILIWEZA KUANDAA VIPINDI MBALIMBALI VINGINE VIKIWA ONLINE NA VINGINE VINGI HAVIJATOKA BADO VIKO MITAMBONI. SWAHILI TV ILIANZA KUFANYA VIPINDI MAARUFU VYA MAHOJIANO MBALIMBALI NA KUWA NA KIPINDI CHA WEEKEND SPECIAL KUTOKEA HAPA WASHINGTON DC.
MALENGO YANGU YA KUANZISHA SWAHILI TV NA SWAHILI TV BLOG HAPA MAREKANI NI
KUITANGAZA TANZANIA NA KUILETEA SIFA NCHI YANGU, KUENDELEZA LUGHA YA KISWAHILI NA KUDUMISHA MAHUSIANO NA WATU WA MAREKANI KIJAMII, KITAMADUNI, KIBIASHARA NA BURUDANI.
KUANZA NA KUFA KWA MMK MMEDIA GROUP BAADA YA MUDA MREFU KUPITA NIKIWA MWENYEWE NIKAKUTANA NA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA. NILIFANYA KOSA KUBWA KUFANYA UBIA NA WATU NISIOWAJUA BACKGROUND ZAO. TUKAANZISHA MMK MEDIA GROUP. (M=MALINDA,M=MKAMA,K=KASSUWI). TUKIWA MMK MEDIA GROUP TULIJITANGAZA SANA, TULITAMBULIKA HIVYO KWA JAMII, UBALOZINI NA KATIKA VYOMBO MBALIMBALI VYA HABARI.
MAKUCHA YA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA YAKAJIONYESHA MUDA MFUPI SANA. NIKAONA MAONO/VIZION YANGU NA WAO NI TOFAUTI MAPEMA. HAWA WATU SIO WAAMINIFU NA WANAPENDA SIFA ZA KIJINGA, NA MABOBLISHI YASIYO NA MAANA, KUJIKWEZA KWA KIJINGA. AUGUSTINO MALINDA ALISEMA ANAFANYA KAZI DC TV NA AKA AHIDI KUWA SWAHILI TV ITAKUWA INAONEKANA LIVE PALE DC TV.
MIMI MUDA MFUPI NIKAGUNDUA KUWA AUGUSTINO MALINDA SIO MFANYAKAZI WA DC TV NA TAYARI KESHA NIINGIZA MKENGE. NIKIWA MMK MEDIA GROUP NILI-INJINIA SWAHILI RADIO ONLINE TULIWEZA KUFANYA MATANGAZO BILA KUWA NA OFISI, TULIFANYA KUTOKEA NYUMBANI KWANGU KISHA NYUMBANI KWA DICKSON MKAMA, SWAHILI RADIO NA MMK MEDIA GROUP HAIJAWAHI KUSAJILIWA POPOTE PALE NA HAIJAWAJI KUWA NA OFISI WALA VIFAA VYA KAZI, WALA AKAUNTI KATIKA BENKI YOYOTE ILE.
MBALI NA MMK MEDIA GROUP KUTOKUWA NA VIFAA VYA KAZI NA FEDHA, TULIENDESHA MMK MEDIA GROUP KUTOKA KATIKA MIFUKO YETU PESA ZETU BINASFI, TULIKUWA TUKIKODI STUDIO NA VIFAA TOKA SEHEMU NYINGINE KUFANYIA KAZI ZA MMK MEDIA GROUP NA USHAHIDI UPO. KUTOKANA NA SIFA ZA HAWA NDUGU KUWA MBAYA KATIKA JAMII NA MISIFA ISIYO NA MSINGI, IKAWA NGUMU KWA MIMI KUPIGA HATUA NA MBAYA ZAIDI HATA MIMI MWENYEWE
KUNITAPELI.
SWAHILI MEDIA GROUP NI KITU GANI?
KATIKA MUDA MFUPI TULIOKAA PAMOJA KILA SIKU NILISHAURI TUISAJILI HII KAMPUNI YA MMK MEDIA GROUP KISHERIA HAPA MAREKANI ,LAKINI BWANA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA WAKANIZUNGUKA MCHANA KWEUPE NA KUANZISHA KAMPUNI AMBAYO MIMI SIIJUI NA SIIELEWI INAYOITWA SWAHILI MEDIA GROUP. BAADA YA KUOMBA MAELEZO KWA NINI
WAMEAMUA HIVI NA KUSHINDWA KUTOA MAJIBU, WAKAWA WANANIKIMBIA NDIPO NIKAMUA KUJIONDOA NA UMOJA HUU WA MASHAKA. W
ATAZAMAJI WETU MTAKUMBUKA TULIJITAMBULISHA KATIKA UMMA KUWA SISI NI MMK MEDIA GROUP. MMK MEDIA GROUP HAIKUWAHI KUSAJILIWA POPOTE PALE. NI MIMI PEKEE BWANA ALEX KASSUWI NDIYE NILIYESAJILI SWAHILI TV NA JINA LA SWAHILITV NEMBO HAPA MAREKANI. NDIO SABABU NILIYOJIENGUA NA BWANA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA BAADA YA KUNITAPELI.
MBALI NA SIFA ZAO KUWA MBAYA HAWANA UJUZI KATIKA TELEVISION NA TEKNOLOJIA YA KUENDESHA MITAMBO KAMA WALIVYONIDANGANYA HAPO MWANZO, NDIPO NILIPO AMUA KUACHANA NAO RASMI, NILIPOWAPA TAMKO RASMI LA KUACHANA NAO HARAKA WAKAIBA PASSOWRD YA BLOG YANGU NA KUIBADILI. NA KUANZA KUITUMIA HIYO BLOG KUNICHAFUA MIMI.
SI KWELI NI UZUSHI WA KIJINGA NAKANUSHA UZUSHI NA UPUUZI WA BWANA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA KUWA NILIBADHIRIFU AMA ETI KUIBA MALI ZENYE THAMANI YA $15,000. HABARI HIZI SI KWELI NA NI UONGO WA KUNICHAFUA. HIZI SIFA ZA KIJINGA.
KATIKA UMOJA WETU WA MMK MEDIA GROUP NA REJEA TENA HATUKUWAHI KUMILIKI OFISI WALA VIFAA VYA UZALISHAJI VIPINDI. VIFAA VYOTE TULIVYOTUMIA TULIKUWA TUNAAZIMA NA KUKODI KUTOKA SEHEMU MBALIMBALI. NILITUMIA VIFAA TOKA CHUO NINACHOSOMA NA USHAHIDI UPO NA PIA TULIKODI VIFAA TOKA SEHEMU MBALIMBALI.
NA BWANA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA HAWANA VIFAA VYOYOTE VYA KUZALISHA VIPINDI WALA UJUZI, NACHOJUA WANAKODI, NA HATA OFISI HAWANA. NA KAMA WAMEPATA VIFAA NA OFISI ITAKUWA JANA. AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA ACHENI MAMBO YA KIPUUZI, NYINYI NI WATU WAZIMA NA MNA FAMILIA. HATA WAKE ZENU WANAJUA NYINYI NI WAONGO, NA HELA HAMNA.
KIFUPI AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON MKAMA SIO WATU WAAMINIFU, WANA CREDIT CHAFU KATIKA JAMII YETU. NILISHAURIWA SANA KUACHANA NA HAWA WATU LAKINI NILIJUA WAMEBADILIKA LAKINI KUMBE BADO NI MATAPELI. WAMETUNGA NA KUZUSHA HABARI HII ILI KUNICHAFUA HASAA BAADA YA KUINDOA SWAHILI TV KATIKA USHIRIKA WAO.
HAWA WATU WANAWEZA KUUA MTU, WE FIKIRIA SWAHILI TV AMBAYO HAIJAANZA KUINGIZA MAPATO NA SWAHILITV BLOG AMABAYO PIA HAINA MAPAT0, HAINA HELA, HAINA VIFAA, HAINA OFISI, TUMEKUWA TUKIANDIKA HABARI NA KUWEKA PICHA KAMA HOBBY WANAZUSHA
UONGO HUU!! HAWA NI WATU HATARI SANA. NAWAJUA WATAFOJI, WATAFANYA CHOCHOTE HATA WATA FAKE DOCUMENT KU-SUPPORT UZUSHI WAO. DMK AMESHAFUNGWA JELA KWA UWIZI NA KU-FOJI/ KU-FAKE NYARAKA HAPA MAREKANI NA USHAHIDI UPO.
NITACHAMBUA KWA KINA DOUBLE FACES ZA AUGUSTINO MALINDA NA DICKSON KATIKA POST IJAYO NA VITUKO WALIVYONIFANYIA TOKA NIMEWAJUA, USIKOSE
KUSOMA NA PIA KUMSHIRIKISHA MWENZAKO ILI KUWEKA KILA KITU WAZI. KAMA HUPENDI DHULUMA TAFADHALI SHARE NA LIKE HII POST
↧
↧
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA
MATOKEO YA WATAHINIWA WALIOFANYA MTIHANI OKTOBA MWAKA JANA HAYA HAPA CHINI. BOFYA LINK HIYO HAPO CHINI KUYATAZAMA.
↧
KAMPUNI YA MONABAN YAKABIDHI MSAADA WILAYA YA HAI KWA AJILI YA WAHANGA WA MAAFA
Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga msaada wa Tani nne za unga wenye thamani ya shilingi Milioni 4.2,baada ya wilaya yake kupata maafa yaliyotokana na mvu zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha badhii ya watu kukosa nyumba za kuishi
Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga Arusha Philemon Mollel akiongea mbele ya wanakijiji(hawapo pichani)namna alivyoguswa na maafa hayo yaliyopelekea kutoa msaada huo huku kiwataka wafanyabishara,makampuni,watu binafsi kujitokeza kuwasaidia waanga wa maafa hao,mbali na msaada huo wa tani nne za unga pia alitoa shilingi Milioni moja kwaajili ya waanga.
Kina mama ambao ndio waathirika wa kubwa wa maafa hayo wakisubiria zoezi la kugawiwa chakula cha msaada
Mtendaji wa kijiji Bi.Trea Ramadhani akitoa shukrani zake za dhati kwa mmiliki wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichipo Arusha.
Mkuu wa wilaya Novatus Makunga akimkabidhi msaada uliotolewa na kampuni ya Monaban ,mtendaji wa kijiji cha kwa sadala Bi.Trea Ramadhani msaada uliogharimu zaidi ya milioni 4,Kushoto ni kaimu mkurugenzi Bw.Zabdieli Moshi
Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga akitoa shukrani zake za dhati kwa mmiliki wa kiwanda cha Monaban kwa kuweza kuwaletea chakula cha msaada na kuwataka makampuni,mashirika na watu binafsi kuiga mfano wa Monaban kwa kuwasaidia waanga wa maafa yaliyotokana na mvua zilizoambatana na upepo mkali na kusababisha watu kukosa makazi hivi karibuni ktika wilaya yake.
Mkuu wa wilaya ya Hai Mh.Novatus Makunga akiwa na ugeni mzito kutoka kampuni ya Monaban ofisini kwake,lengo la ugeni huo nikutoa msaada wa chakula kwa waathirika wa maafa ya mvua
Mkurugenzi wa Monaban kushoto Philemon Mollel akiongelea namna alivyoguswa na maafa hayo ambayo yalisababisha baadhi ya watu kukosa makazi ,
Afisa Tarafa Masama Bw.Nsajigwa Ndagile akisoma taarifa ya madhara yaliyotokana na mvua hiyo kuwa ni pamoja na kuezuliwa kwa mapaa ya nyumba,kubomolewa kwa kuta za nyumba na kuharibiwa kwa mazao hasa migomba hali iliyosababisha baadhi ya kaya kukosa mahali pa kulala hivyo kujihifadhi kwa majirani
Mama ambaye ni muathirika wa maafa hayo akitoa shukurani zake kwa mkurugenzi wa kampuni ya Monaban kwa kuweza kuwakumbuka kipindi cha shida na kudai kuwa akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli
Nyumba ya familia ya Bibi Aziza Mohammed baada ya kuezuliwa paa
↧
Article 6
↧
IN LOVING MEMORY OF OUR BELOVED MOTHER ESTHER NYIMBO BADI
No words can express the pain we felt when we lost you on Wednesday 22nd February 2012 at 6.30 p.m. Over the two years, precious memories of your beautifully life have been our only comfort.
We remember your affectionate smile, the sweet sound of your voice, your kind and most generous heart that would have a place for everyone.
We count our self lucky to have held a mother like you, and we thank GOD for the incredible times we shared. We miss you greatly, but we know you are happy in Heaven watching over us, and praying for us.
Affectionately remembered by your children, Blandina, Bertha, Stella, Gern, Lilian, John and Upendo. You’re in laws Cashmir, Modestus, James, Kenny and Afro and Your Grandson’s Joakim, Jeff, Abraham, Faith, Deborah, Caleb, Karen, Sara, Brandon, Dillan, Esther, Hilary, Suzana and Edson.
Rest in Peace Mummy.
↧
↧
DAKIKA 90 ZA DUNIA: Kwanini Facebook imetumia dola bilioni 19 kununua WhatsApp?
Photo: Mobile88.com
Kama wewe ni mmoja wa wanaotumia njia ya mawasiliano iliyojipatia umaarufu ya WhatsApp, basi ujue kuwa nawe ni miongoni mwa wateja takribani nusu bilioni walioufanya mtandao huo kuwa maarufu zaidi duniani kwa kipindi kifupi tu.
Ni umaarufu huu uliofanya kampuni kubwa ya mawasiliano ya Facebook wiki hii kuona umuhimu wa kutumia dola za kimarekani bilioni 19 kununua WhatsApp. Lakini kwanini kampuni itumie kiasi hicho kikubwa kwa kampuni kama hii?
Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM). Hii ilikuwa ripoti ya Februari 22, 2014
↧
PINDA AIASA JUMUIYA YA UMOJA WA WAZAZI NCHINI Lazima iwe na kitu cha kujivunia
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Jumuiya ya Wazazi nchini ni miongoni mwa jumuiya inayoongoza na kusimamia masuala yote yanayohusu elimu, malezi bora kwa vijana wa taifa letu hivyo lazima iangalie jinsi ya kuweza kujipambanua katika utekelezaji wa Umoja wa Jumuiya yao.
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumamosi, Februari 22, 2014), wakati akifungua rasmi semina ya siku tatu ya viongozi na watendaji wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi ngazi ya Taifa, Mikoa na Wilaya Tanzania inayofanyika kwenye Ukumbi wa NEC, Mkoani Dodoma.
Akizungumza katika ufunguzi huo, Waziri Mkuu Pinda aliwaeleza wana jumuiya hao kuangalia malengo wanayojipangia aidha yawe ya muda mfupi au mrefu ili kuyatekeleza kwa kuzingatia yale mambo ya msingi na yenye kipao mbele kwa wananchi.
“Changamoto kubwa iliyopo mbele yenu kama viongozi na watendaji wakuu wa Jumuiya hii ni namna ya kutimiza malengo mliyojiwekea“.
Alisema, dhana ya Jumuiya ya Umoja wa Wazazi nchini ni kuongeza na kuboresha masuala yote yanayohusu Sekta ya elimu hapa nchini: ‘‘Tumieni semina hii kujipima kwamba mmefikia wapi katika utelelezaji wa malengo yenu kwa kuangalia mapungufu na maboresho katika jumuiya yenu‘‘.
Jumuiya ya Wazazi ndio magwiji mnaoongoza kwa kuwa na shule nyingi hapa nchini, hivyo jumuiya yenu ijipange na kusimamia vema shule hizo ili kuwa vinara katika kuboresha masuala ya elimu hapa nchini. Akitoa mfano, alisema: “Kwanini shule za binafsi zinakuwa zinaongoza kuliko shule zilizopo ndani ya Jumuiya yenu, walau katika kumi bora iwepo shule moja kutoka Jumuiya ya Umoja wa Wazazi alisema Waziri Mkuu”.
Kutokana na kauli hiyo, Waziri Mkuu aliiambia Jumuiya hiyo kutumia dhana ya elimu kama ngao yao katika kuleta maendeleo katika Sekta hiyo kwani Ilani ya chama cha Mapinduzi imetamka wazi kuongeza kasi ya upanuzi wa Elimu ya Awali, Msingi na Sekondari lengo ambalo ni moja ya jukumu kuu la msingi la Jumuiya ya Umoja wa Wazazi.
Aliendelea kusema kuwa Jumuiya ya Wazazi inajukumu la kusimamia masuala yote yanayohusu maadili, jukumu ambalo halina tofauti sana na jukumu la madhehebu ya dini kuzungumza bayana masuala ya malezi ya watoto na vijana ambayo yamekuwa yakiporomoka kila kukicha, hivyo Waziri Mkuu alisema, jumuiya hii itumia jukumu na nafasi waliyopewa kuhakikisha watoto wote walio ndani na nje ya jumuiya wanafundishwa maadili.
Waziri Mkuu aliendelea kusema kuwa, Jumuiya ya Umoja wa Wazazi ina majengo, viwanja na ardhi inayofaa kwa kilimo na shughuli za kiuchumi, tumieni fursa hizi kwa kujenga vyuo, kuanzisha miradi ya maendeleo ambayo itawasaidia katika kuongeza kipato katika jumuiya yenu.‘‘Mnachotakiwa ni kupanga bajeti zenu vizuri na kusimaia utekelezaji pamoja kusimamia vizuri miradi na fursa zinazojitokea“
Pamoja na hayo, Waziri Mkuu aliiomba Jumuiya ya Wazazi kujitokeza kuzungumzia masuala ya Dawa za Kulevya kwa kusema kuwa, wako vijana ambao wametumbukia katika dimbwi la Dawa za Kulevya ambaa pia wanahatarisha maisha yao kwa kupata UKIMWI: “Ni matumaini yangu kwamba Jumuiya ya Umoja wa Wazazi itakuwa mstari wa mbele kuelimisha jamii, kutoa ushauri kwa vijana kuhusu athari za dawa za kulevya, UKIMWI na hata mkiweza kuanzisha vituo vya ushauri”, alisisitiza Waziri Mkuu.
“Ili kuweza kuwa na Jumuiya ya Wazazi imara ni dhahiri kuwa wanajumuiya wasimamie kanuni na maadili yanayoongoza jumuiya yao kwa kuwaasa kuacha kujiingaza katika makundi yasiyokuwa na msingi hasa kwa kutanguliza maslahi ya fedha katika kupata nafasi za uongozi katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu ambao huleta migawanyiko kati ya Viongozi na wanachama na wapiga kura”. Mzingatie masuala yanayohusu kujenga na kukuza utekelezaji wa jumuiya yenu ambayo itawasaidia kujenga jumuiya imara na kujenga chama imara kitakacho leta viongozi imara”alisisitiza Waziri Mkuu.
Mapema, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Taifa, Bw. Majura Bulembo, alisema lengo la semina hiyo ni kuwajengea uwezo na kuwaongeza ufanisi Jumuiya ya Wazazi katika utekelezaji kazi zao na kuwasisitiza kuhudhuria semina hiyo ipasavyo ili kuweza kukumbusha mapungufu na changamoto zinazojitokeza katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.
“Viongozi wamekuwa wakitumia vibaya nafasi za uongozi walizopewa kwa kujiona wao ndio viongozi wakuu kwa kujifanyia maamuzi yao, viongozi kama hao wataondolewa madarakani mara moja”.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 3021,
DAR ES SALAAM.
JUMAMOSI, FEBRUARI 22, 2014.
↧
YANGA YAIVURUGA VURU VURU RUVU SHOOTING 7-0
Mchezaji wa Yanga, Juma abdul akimtoka beki wa Ruvu Shooting, Said Madega.
Mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi akimpiga chenga kipa wa Ruvu Shooting, Abdalah Ramadhan na kuipatia timu yake bao la 3 kwa timu yake.
Dogo huniwezi.................
Sasa naenda kufunga......
Golikipa wa Ruvu Shooting, Abdalah Ramadhani akiwa ameshika kiuno baada ya Okwi kupachia bao.
Washambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi (kulia), na Hamis Kiiza wakishangilia moja ya magoli waliyoifungia timu yao wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya Ruvu Shooting uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga ilishinda 7-0 (Picha zote na Francis Dande)
↧
NAIBU WAZIRI DKT PINDI HAZARA CHANA AFANYA ZIARA YA KIKAZI KATIKA CHUO CHA MAENDELEO YA WANANCHI MUNGURI, KONDOA- DODOMA
Pichani juu Naibu waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto, Mhe. Dkt. Pindi Hazara Chana akikagua utoaji wa mafunzo katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Munguri, Kondoa, akiwa ameambatana na Uongozi wa Wilaya ya Kondoa.
Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana akiwa katika ziara hii ya Kikazi alipata fursa ya kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Munguri, kondoa ambacho ni miongoni mwa vyuo 55 vinavyotoa mafunzo ya elimu ya wananchi, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya ufundi stadi, VET
Wakati wa ziara hii Mhe. Naibu Waziri aliiasa jamii ya Kondoa kutumia fursa hii kuwahimiza vijana kuja kupata mafunzo na ujuzi mbalimbali utakao wawezesha kujiajiri na hatimae kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, na hata kiwango cha umaskini katika jamii.
Alisisitiza kuwa Serikali ina dhamira ya dhati ya kuimarisha utoaji mafunzo katika chuo hiki na vingine nchini, ili kufikia vijana wengi zaidi na kutekeleza kwa vitendo Ilani ya CCM ya mwaka 2010.
↧
↧
SONG JIPYA LA SNURA - USHAHARIBU
Kaa tayari kwa ajili ya wimbo huu mpya wa snura mushi. unaojulikana kama Ushaharibu, huu wimbo unawazungumzia watu wenye tabia ya kuiangalia leo na kuidharau kesho, kwa mfano kuna watu wamezungumziwa umo ndani kuwa ''Uliuza nyumba kwa ugumu wa maisha,huna pakulala shida umezizidisha,
na haya ndio mashahiri ya wimbo huu wa ushaharibu....
unatafuta kick na upo kwenye muziki,ndio kwanza unahit umetukana mashabiki ulikimbia wazazi ukayafanye mabaya,tena ulimwaga radhi na umepata miwaya ulitukana wakunga na wakati una mimba, ulijiona mjanja kumbe wewe ndio mjinga umeombewa kulala umekojoa kitandani,umetutia haibu kwenye chumba cha jirani
uliuza nyumba kwa ugumu wa maisha , una pakulala shida umezizidisha,
kuto kujiamini umetapatapa, umeliacha dume umelamba galasa.x 2
chorus
ndo basi tena ushaharibu,uuuhu
kujifanya mjuaji ushahaaribuuuuhu
umejitia ufundi ushaharibuuuuhu
jipange upya ushaharibuuuuuuhu x 2
vers ya 2
unataka heshima kutoka kwa wako wana , mbele ya watoto wako matusi unatukana, baba yupo ICU mmeukata umeme,tena mmeshaharibu wacheni mimi niseme. nilipokuwa chini ulikuwa unitaki,leo hii niko juu unataka urafiki. umechomwa sindano na umemeza vidonge, ulivyo na dharau eti umekunywa pombe.
uliuza nyumba kwa ugumu wa maisha , una pakulala shida umezizidisha,
kuto kujiamini umetapatapa, umeliacha dume umelamba galasa.x 2
chorus
ndo basi tena ushaharibu,uuuhu
kujifanya mjuaji ushahaaribuuuu
umejitia ufundi ushaharibuuuu
jipange upya ushaharibuuuuh x 2
Brige
ebu jaribu sasa kufikiria jambo usiharibu, umeharibu sasa limekushuka sura ina haibu, ebu chunga uchunge uchungweee usiharibu tena,hk chungwa uchungwe usiharibu tena, we Snura chunga uchungweeee,baby talha chungwa uchungweeeee, na mapacha chungwa uchungweeee msiharibu tenaa. ebu chungwa chunga uchungweee usiharibu tenaaaaaaaaaaaaaaaaa.
↧
Article 4
↧
Washindi wawili wa droo ya winda safari ya Brazili na Serengeti wakabidhiwa zawadi zao
Washindi wa droo ya winda safari ya Brazili na Serengeti Godbles Sehaba (kulia)na Karushe Mathias (kushoto) wakiwa na nyuso za furaha baada ya kukabidhiwa zawadi zao za king’amuzi cha azam walizoshinda baada ya kuchezeshwa droo hiyo siku ya jumatano.
mshindi wa king’amuzi cha azam katika promosheni ya winda safari ya Brazili na Serengeti Bw Godbles Sehaba katikati akikabidhiwa zawadi yake na meneja mauzo eneo la mabibo Bi Anna Gassembe (kushoto) na afisa mauzo Bi Anna Msonga (kulia).
Washindi wawili wa droo ya winda safari ya Brazili na Serengeti wamekabidhiwa zawadi zao jumamosi katika bar ya muleba iliyopo maeneo ya Mabibo Dar es Salaam, washindi hao Bw Godbles Sehaba na Karushe Mathias wakiwa na furaha walipokea zawadi hizo na kuishukuru kampuni ya bia ya Serengeti kwa kuwapa zawadi hiyo, wakiwa kama mashabiki wakubwa wa soka la nyumbani washindi hao wamefurahia kupata zawadi itakayowawezesha kuangalia ligi za mpira wa miguu ya nyumbani bila matatizo.
Meneja mauzo eneo la mabibo hilo Bi Anna Gassembe ambaye alikabidhi zawadi kwa washindi amehimiza watu kuendelea kunya bia ya Serengeti kistaarabu ili wajishindie zawadi. "zawadi bado ni nyingi na zawadi kubwa ya safari ya Serengeti bado haijatolewa kwa hiyo muendelee kushiriki zaidi ili mjipatie zawadi mbalimbali" alisema Anna.
promosheni ya winda safari ya Brazili na Serengeti inaendelea na washindi wanaweza kujishindia zawadi za simu aina ya samsung galaxy tab, king'amuzi cha azam, pesa taslimu shilingi 5000 na 10000, bia za bure pamoja na zawadi kubwa ya safri ya kwenda Brazili.
↧
CHADEMA WAZINDUA RASMI KAMPENI ZA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KALENGA
Viongozi na wanachama wa CHADEMA wakielekea kwenye makumbusho ya Chifu mkwawa kabla ya kuanza kampeni hizo
Hapa wakitoka kwenye Makumbusho ya Chifu Mkwawa huku hali ya hewa ikiwa ni ya ubishi kutokana na mvua kubwa kunyesha.
Mgombea wa Ubunge kupitia chama cha CHADEMA Grace Tendega Mvanda akinadiwa na Katibu mkuu wa chama hicho Dr. W. Slaa wakati wa kampeni hizo zilizoanza hii leo katika jimbo la Kalenga.
↧
↧
RAIS KIKWETE ASAIDIA KUENDESHA HARAMBEE KUCHANGIA WODI YA DHARURA YA WATOTO NA VIFAA VYAKE HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa baada ya kuwasili katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibadilishana mawazo na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Radio One Bw. Deo Rweyunga akitangaza mchango wa makampuni ya IPP ya kununua kifaa cha thamani ya dola elfu 50 ) katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam. PICHA NA IKULU.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru mwakilishi wa NSSF Bw. Juma Kintu kwa mchango wa mfuko huo katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 10 toka kwa wawakilishi wa PPF ukiwa mchango wa mfuko huo katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru Bi Lucy Kimei kwa kuwasilisha shilingi milioni tatu kama mchango wa familia ya Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dkt Charles Kimei katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Rais mstaafu Mzee Benjamin William Mkapa akimshukuru mwakilishi wa taasisi ya WAMA Bi. Caroline Mthapula kwa mchango wa taasisi hiyo katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru mwakilishi wa UNICEF nchini kwa mchango wa dola za kimarekani 100,000 huku Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa wakishuhudia katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
↧
Article 24
↧
TAMASHA LA PASAKA KUJA KIVINGINE MWAKA HUU.
Tamasha la pasaka la Mwaka huu litakalozinduliwa rasmi April 20,jijini dar likibeba kaulimbiu ya "Tanzania kwanza haki huinua Taifa",litaemdendeshwa kwa namna ya Wadau wenyewe kuchagua waimbaji,aidha iwe kutoka ndani ama nje ya nchi ikiwemo sambamba na mgeni rasmi.
Hayo yalibainishwa jijini Dar,mwishoni mwa wiki na Mkurugenzi Mtendaji wa Msama Promotions,ambao ndio wandaaji wa tamasha.Alifafanua kuwa wapenzi wa muziki huo ndio watakaochagua waimbaji hao kwa kutuma ujumbe mfupi kupitia namba 15327, kwa kutumia mitandao yote ya simu.
"Tamasha la mwaka huu linakuja kwa mtindo wa kipekee kabisa,ambapo wapenzi wa muziki wa injili watakuwa na fursa ya kuwachagua wanamuziki watakao penda waje kutumbuiza ikiwemo na Mikoa litakapo fanyika tamasha hilo, tofauti na miaka mingine na wale wote watakao pendekezwa tutawaleta kutoa burudani",alisema Msama.
Alisema,licha ya kuweka utaratibu huo,kumekuwa na changamoto kubwa kwa wapenzi hao wa muziki wa injili ambao wanataka wanamuziki waliotoa burudani wakati wa tamasha la krimasi akiwamo Solly Mahlangu kutoka nchini Afrika Kusini.
Msama alisema,maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika na katika mazingira ya kwenda na wakati,limekuwa na kauli mbiu ya "Tanzania kwanza haki huinua Taifa".
Miongoni mwa waimbaji waliotikisa tamasha la Krismas ambalo lilizinduliwa rasmi Desemba 25,mwaka jana jijini Dar,kabla ya kuhamia mikoani,Ni Solly Mahlangu,Ephrahim Sekereti,Rose Muhando,Upendo Kilahirio,Upendo Nkone,Edson Mwasabwite na wengineo,wakiwemo vijana wa Acapella a.k.a The Voice.
↧
More Pages to Explore .....