Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

MSAADA TUTANI: DJ JOHN DILLINGA A.K.A DJ JD AONGEA

0
0
Disck Jockey Mkongwe DJ JOHN DILLINGA A.K.A DJ DJ akiongelea mustakabali wa Disco nchini Tanzania na Isumba Lounge

KAMPUNI YA ISSERE SPORTS YATOA JEZI KWA SHULE YA SEKONDARI YA KEREZANGE

0
0




KAMPUNI ya kuuza vifaa vya michezo, Issere Sports imetoa jezi mipira na soksi kwa timu ya soka ya Shule ya Sekondari Kerezange, iliyoko Kivule Ilala, Dar es Salaam.

Akikabidhi jezi hizo mchezaji wa zamani wa Simba, Qureshy Ufunguo aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Issere, Abbas Ally alisema michezio inafanya wanafunzi kuondokana na maradhi. 

Ufunguo aliyekubali kufundisha timu ya soka ya shule katika mashindano ya shule za Sekondari (UMISETA) alisema atatumia uwezo wake kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika mashindano hayo.

Mkuu wa Shule hiyo. Kirundu Mgeni alisema vifaa hivyo ni chachu ya wachezaji wa shule yake kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali ya ndani na nje ya wilaya yao ya Ilala. 

Awali Mwalimu wa michezo wa shule hiyo, Baraka Mololo alisema shule yake ina wachezaji wengi wenye vipaji ambao wakiendelezwa wanaweza kuchezea timu za Simba na Yanga na hata Taifa.

Alisema hivi karibuni shule hiyo ilifanya vizuri katika mashindano ya kirafiki na shule za jirani na kuibuka washindi hivyo ana matarajio makubwa ya kutwaa ubingwa wa UMISETA mwaka huu.

Chama cha Mapindunduzi ni chama chenye kuleta maendeleo na kinapinga ubaguzi

0
0
 Katibu wa CCM Mkoa wa Mjini Mwangi Rajabu Kundya akimnadi mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mahmoud Thabit Kombo katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki zilizofanyika Mbweni Wilaya ya Magharibi Unguja. (Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar).
 Mgombea Uwakilishi wa Jimbo la Kiembe Samaki  kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM) Mahmoud Thabit Kombo akiwahutubia wananchi waliofika katika kampeni zake Mbweni Wilaya ya Magharibi Unguja.
========  =======  ============
Na Miza Kona – Maelezo Zanzibar    
Chama cha Mapindunduzi ni chama chenye kuleta maendeleo ambacho kinapinga ubaguzi  na kuwatetea wananchi haki zao za msingi.

Hayo yameelezwa jana huko Mbweni na Katibu wa CCM Mkoa wa Mjini Mwangi Rajab Kundya katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki. Amesema kuwa kuna baadhi ya vyama Vya upinzani vinachochea kuleta ubaguzi nchini kwa kisingizio cha kutaka Zanzibar iwe na mamlaka yake kamili kinyume na matakwa yao.

Aidha amesema kuwa Zanzibar imeshapata mamlaka yake tangu baada ya Mapinduzi na kuundwa kwa chama cha Afro Shirazi Party ASP ambapo tayari ina viongozi kamili na sifa zake zote za kupata maamlaka hayo. “Mamlaka kamili tayari yamepatikana tangu ilipoundwa ASP hivyo wanataka mamlaka gani tena”, aliuliza Kundya.

Katibu huyo ameeleza kuwa Zanzibar itaendelea kudumisha Muungano ambao unatetea wazanzibar na kuwaletea maendeleo ambayo wananchi wananufaika na matunda yake.

Amefahamisha kuwa CCM sio chama chenye kuleta ubaguzi kwa wananchi  kwani kiko makini katiika kuwaletea maendeleo ya nchi. Amesema CCM ina viongozi makini ambao ni wataalam wa uongozi hawayumbishwi na watu wasiopenda maendeleo ya nchi.

“Kiongozi wa watu lazima ajitie katika  makundi ya watu ili aweze kujua shida zao kwa lengo la kutatua matatizo ya watu wao lakini wapinzani hawana utaala huo”, alifahamisha bwana Kundya.

Aidha Katibu huyo amewataka wananchi wa Jimbo la Kiembesamaki kumchagua kiongozi wa CCM kwani ndiye atakaeweza kusimamia Muungano, kupigania haki ya wanzibari  na maendeleo kwa jumla.

Nae mgombea uwakilishi wa chama hicho Mahmoud Thabit Kombo ameahidi kuimarisha matawi ya CCM kwa kinamama na jumuiya za wazazi pamoja na kuwaimarisha na kuwashajihisha vijana katika mambo ya ajira.   

MASHINDANO YA NGUMI MKOA WA DAR ES SALAAM YAPAMBA MOTO

0
0
Bondia Cosmas Peter kushoto akipambana na Hfidhi Bamtula wakati wa mpambano wao uliofanyika Dar es salaam jana kwenye mashindano ya Mkoa ambayo yanachagua bondia atakaewakilisha Mkoa wa Dar es salaam Bamtula alishinda kwa Point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Hafidhi Bamtula kushoto akitupa ngumi ambayo imeenda hewani bila mafanikio alipokuwa akipambana na Cosmas Peter wakati wa Mashindano ya Mkoa wa Dar es salaa ambayo wanachagua mabondia wa mkoa huo, Bamtula alishinda kwa point mpambano huo.

Bondia Emillian  Patrick kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Hamad Furahisha wakati wa mashindano ya mkoa wa Dar es salaam Patrick alishinda kwa point mpambano huo .

Bondia Kasimu Mbutike kushoto akimtupia konde la mkono wa kushoto Yusufu Said wakati wa mashindano ya mkoa Wa Dar es salaam yaliyofanyika katika ukumbi wa panandi panandi Ilala Bungoni Said alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

MO plans to build a USD 5 billion empire out of Dar

0
0
942331_578714148840668_773339795_n

.At the age of 38, Mohammed Dewji employs 24,000 people and claims to contribute 3.5% to Tanzania's GDP. Within the next 5 years, he plans to build a $5 billion empire out of Dar es Salaam.

by Kristin Palitza
What most entrepreneurs don’t achieve in a lifetime, he did in just over a decade. Mohammed Dewji single-handedly turned his father’s trading business into Tanzania’s largest import-export group. He grew Mohammed Enterprises Tanzania (MeTL) 30-fold and increased revenues from $30 million to $1.1 billion by diversifying into a multitude of sectors, including manufacturing, distribution, logistics, financial services, real estate, cement, energy and mobile telephony.

It’s not surprising that many people have a hard time imagining the humble beginnings Dewji comes from. His family, which stems from Gujarat state in western India and was blown in the proverbial dhow across the Indian Ocean, started out with very little. His grandmother opened a small trading shop, which she runs out of their home in Singida, a poverty-stricken town in central Tanzania. In this simple house, built from sand and mud, Dewji was born with the help of a traditional midwife.

“That wasn’t very smart. My mother and I almost died because I had the umbilical cord wrapped around my neck,” he recalls. But from then on, his fortunes changed. His father, Gulam Dewji, who had by the mid-70s turned his mother’s shop into a flourishing import-export business, was able to sent his six children to good schools, first in Tanzania’s third-largest city Arusha and later in capital Dar es Salam. In their free time, Dewji and his siblings played tennis and golf.

“My father spent a lot of money educating us. He also believed sport creates discipline. He didn’t want us to just play a sport for fun. He wanted us to push ourselves. We probably have a thousand trophies at home that we won,” he says. Until this day, there is almost nothing Dewji undertakes purely as a hobby. He either aims for success, or he doesn’t bother with it. And so he ploughs millions of Dollars into Tanzania’s national soccer team, the Taifa Stars instead of being content watching the odd game or kicking around a ball on a Sunday.

“I have no moderation. My wife always complains. She says, ‘Mohammed, why don’t you do things in the middle?’ It’s either very much or nothing at all,” he laughs.

His favorite sport has always been golf. Dewji spent many afternoons on Dar es Salaam’s golf course, not only because he was good it – he had 3 handicap – but also because he realized from early on that many high-profile business deals are concluded on the world’s 18-hole-lawns.“I already liked to network as a very young guy. I was told that the golf course is a good place to meet important people. So I started playing golf. At one time, I even wanted to become a golf professional,” he says.

When his father saw that his son showed potential, he enrolled him at the legendary Arnold Palmer Golf Academy in Orlando, Florida, where Dewji also attended Saddlebrook High School. A few years later, when it became clear that Dewji wasn’t going to make the cut as a professional golfer, he decided to study international business and finance with a minor in theology at Georgetown University, an elite tertiary institution in Washington D.C., which has a long list of notable alumni, including former US president Bill Clinton, former Philippines president Gloria Arroyo and Jordan's King Abdullah.


During his time at Georgetown, Dewji learned what he says were key lessons in leadership. “Georgetown really molded me. It took me a step forward. I understood that you need to be dreaming, but not daydreaming. You need to try to dream a reality. Then you have vision,” he explains.
Pietra Rivoli, deputy dean of Georgetown University’s school of business, who taught Dewji in international finance, remembers him as a student whose energy was boundless and whose positive enthusiasm was contagious.
“While other students tried to stay awake through discussions of exchange rates, Mohammed would stay after class to talk about how the readings might pertain to the Tanzanian Schilling, and how Tanzania could address its economic challenges. Even at the age of 20 or so, he was thinking about how to improve life in his country,” she remembers.
Dewji never questioned if he should return to Africa after his graduation in 1998. He joined his father’s business, which had by then become a million Dollar trade and transport group, as chief financial controller. Five years later, at the age of 29, he was promoted to managing director, expanding his father’s business hard and fast. “I went into manufacturing and value-addition. I built a distribution system and created branches,” he says.
Today, MeTL Group is buying and selling more than 200 commodities in east, central and southern Africa, from sugar to rice, salt, fertilizer, second-hand clothing, motorcycles, bubblegum, yeast and ballpoint pens. The group also distributes 50 of its own brands, taking advantage of the fact that Tanzania borders on eight countries and is thereby an ideal import-export gateway.
“The goods that I am mainly dealing in are FMCGs [fast moving consumable goods]. It’s goods that touch people’s lives, that are needed by the common man,” he says.
The distribution of FMCGs is not an easy task in a vast country like Tanzania, which measures a million square kilometers and where 80% of the population lives in remote, rural areas. But with more than a hundred trade outlets countrywide, MeTL Group has managed to undercut multi-national consumer goods giants like Unilever and drive them out of the east African nation.
“I have a big basket of goods. I have warehousing and logistics. I have over a thousand trucks. It’s all complimenting each other. It’s very difficult for people to come from the outside and compete with me,” Dewji explains.
He invests in whatever sector he sees opportunity and growth potential. Or to say it differently: the only two industries Dewji is not involved in are beer and tobacco.
Agriculture is another key sector for MeTL Group, which with a workforce of 24,000 people is also the country’s biggest employer, and with 50,000 hectares of arable land, the largest private landowner. Dewji’s sisal farms, tea gardens and cashew fields are the drivers of his FMCG export business. A good 99% of the cashew kernels he produces, for example, are shipped to the United States.
Always thinking two steps ahead, Dewji has been making plans for how to profit most from his land, while helping to solve the challenges of Dar es Salaam’s rapid urbanization, a city of 4.4 million people. He is busy turning a 17,000 acre plot he bought cheaply several years ago, just 25 kilometers outside of the capital, into a dry-port with an internal container depot and a railway connection that will feed into Dar es Salaam’s massive, natural harbor, which is slowly but surely running out of space. It will, of course, also generate huge profits.
Since MeTL Group already contributes 3.5% of Tanzania’s GDP, it is fast outgrowing national boundaries.
“If you compare, for example, Tata and the MeTL Group, we are like Mickey Mouse. But if you look at their contribution to India, vis-à-vis my contribution to Tanzania, mine is bigger. You end up competing with everybody in your own country, and I don’t think that’s healthy. It’s a risk area. It’s a good time for us to replicate what we are doing in Tanzania in other countries,” he explains his expansion plans.
A workaholic at heart, Dewji never thinks small. “Slowly, slowly, I am planning to take on the whole continent. I am very bullish,” he says about himself. His five-year-plan is to turn MeTL Group into a $5 billion empire.
“We have to constantly revisit our visions, because we are outgrowing them so quickly. Who would have thought we could turn our business from $30 million to $1.1 billion in only 12 years? I believe that by 2018, we will be a $5bn business. Easy. It’s a no-brainer. If you look at the business we are in and the growth potential that there is, it’s amazing. My philosophy as a businessman is not to be satisfied with what I have got, but to always work harder to achieve more,” he says.
It’s been quite some years now that MeTL Group, under Dewji’s helm, has expanded so drastically that it has outgrown the loan potential of Tanzania’s banks. Dewji has found a solution to this problem, too. He goes to one of the continent’s powerhouses, South Africa, to finance new ventures. Most recently, he secured a $100 million syndicated loan through a grouping of banks.
“If I think of a top African businessman, Mohammed comes to mind. He works very long hours, is always on the move, has an eye for opportunity and a very good business sense. He is levelheaded and pays extremely close attention to detail,” says Helmut Engelbrecht, head of Investment banking in Africa at Standard Bank, one of the financial institutions that has been working closely with MeTL Group.
Whatever venture Dewji pursues links closely into his country’s national policy framework. When Tanzania’s government launched a national strategy for economic growth and poverty reduction in 2005 that was geared, among other things, towards boosting entrepreneurship to achieve value addition and employment creation, Dewji immediately saw opportunity.
“I bought a lot of sick industries, including soap production, grain milling, rice and sugar blending. I also went into the edible oil business and the textile industry,” he says.
He first expanded MeTL Group’s edible oil refining capacity from 60 to 600 tons. This year, Dewji almost quadrupled the business when he purchased an additional 1,650-ton refinery, increasing his total output to 2,250 tons of edible oil. It comes as little surprise that he has caught the attention of some of Africa’s wealthiest investors.
“I am being approached by many big boys, by multi-national companies that want to partner with me or buy me out. But I am not ready to sell yet. I can see so much more opportunity for growth. I don’t want to be paid based on what I am earning today, because I can see the tremendous potential. I am always looking five, ten years ahead,” he explains.
Another ailing sector Dewji rescued is Tanzania’s textile industry. Knowing that the east African nation is the continent’s third largest cotton producer, he decided to buy and refurbish four run-down mills, three in Tanzania and one in Mozambique. His next step will be to move into Zambia and Malawi, he says, considering Ethiopia as a potential fifth standpoint.
“We were quite lucky. Tanzania’s previous, socialist government had invested hundreds of millions of Dollars in infrastructure to build textile mills. But under socialism everything collapsed. So we were able to acquire these industries very cheaply. Obviously the machinery was all run-down, the technology obsolete. We had to rehabilitate the mills by investing in top European and American machinery,” says Dewji.
He has turned MeTL Group into sub-Sahara Africa’s largest textile player, integrating the entire value-addition chain from ginning to spinning, weaving, processing and printing.
“This year, we are going to produce more than a hundred million meters of cloth. That is more than 2,500 times the circumference of the earth,” Dewji says with pride.
Due to his entrepreneurial vigor, Tanzania is able to compete with the world’s largest and cheapest textile producer, China – at least within its own borders where government policies, including import tariffs on textiles and a standard value added tax (VAT) of 18% help protect the industry.
“Today, overall textile production is cheaper in Tanzania than in China. Labor is competitive in terms of pricing. Tanzania’s big advantage is that we have cotton, while China has to import cotton. So they cannot compete with me in my market,” Dewji explains.
His success speaks for itself. This year alone, he will earn at least $85 million after taxes, he says. But he is far too humble to take credit for the entirety of his achievement.
“People often ask me: ‘Who is smarter, you or your father?’ I ask them back: ‘Is the person who goes from zero to ten smarter, or someone who goes from ten to a thousand?’ Obviously, it’s much easier to go from ten to a thousand than to start from zero. So I believe that my father is much smarter than me,” he says.
Nothing could be further from his mind than taking it easy, or even early retirement.
“People in Tanzania look at my wealth and think I must be sunbathing and playing golf all day. But I work really hard. I put in a hundred hours a week. It’s a never stopping game. You can never say, ‘I’ve worked hard enough now’,” says Dewji, who has 60 divisional board meetings every month, or two per day.
Every morning, Dewji, who lives in with his wife, daughter and two sons in one of Dar es Salaam’s best neighborhoods, starts work at 6AM, spending the first hour responding to emails and reading commodity reports. He then runs meetings until lunch, by which time he has already put in almost seven hours of work.
“When I feel my energy levels starting to drop, I drive to the gym near my house. Every day, I run three kilometers and lift weights. I like to keep fit,” says Dewji, who is of slender built and the proud owner of a ‘six-pack’.
After gym, he goes home for lunch and to play 15 minutes with his three children before he returns to the office until late at night. The only days he takes off are Sundays, he says, when he spends time with his family and totally shuts off from work.
“Until about four years ago, I also used to work on Sundays, until my wife almost divorced me,” he jokes.
Dewji is not only growing his own empire. He is putting Tanzania on the map, making sure the east African nation – which boasts the continent’s third largest gold reserves, recently discovered uranium and gas reserves as well as a flourishing tourism industry combined with long-term political stability – will become one of sub-Sahara Africa’s big economic players, together with South Africa, Nigeria, Ghana and Kenya.
Already, Dar es Salaam is the second fastest growing African city after Lagos. And Tanzania, which boasts an average of 7% national economic growth over the past decade, has become one of the fastest growing economies in the world. According to World Bank, Tanzania’s per capita GDP more than doubled from $730 in 2000 to $1,500 in 2012.
“There’s no doubt that the country’s purchasing power is increasing,” notes Dewji, who believes the whole of sub-Saharan Africa, which currently has an overall growth rate of 4.8%, could achieve double-digit growth figures if countries are well-governed, politically stable and create conducive environments to attract investment.
As if Dewji didn’t already have enough on his plate, he is also in politics. The decision was made when he visited Singida, the town and district he grew up in, after returning from the US. As he walked the city’s streets, he encountered an old man who was scooping yellowish water out of a dirty puddle. It was his family’s only access to drinking water.
“A lot of people die from water-born diseases in rural Tanzania. But every life has the same value. So I decided to run in the next elections to change the dire situation these people live in. I was 24 years old. My parents thought I was crazy,” he remembers.
Whatever Dewji sets his mind to, he turns into a success. In 2005, he was elected as a Member of Parliament in the National Assembly of Tanzania. Five years later, he was re-elected in a landslide victory with 80% of votes. Not being a fan of ‘politicking’, Dewji, who is fluent in both English and Kiswahili, says he decided to put his own spin on the role of an MP.
“I don’t really have time for politics. I don’t go to parliament, and I don’t get involved in national politics, because I don’t want it to conflict with my business interests. All I do is serve my constituency because I believe people see hope in me,” he explains.
He puts his money where his mouth is. Every year, he donates half a million Dollars of his own money to help the people of Singida, with focus on three areas: education, health care and water. And with tangible success. In years Dewji has been representing the central Tanzanian district, access to clean water has jumped from 23% to 75%, while the number of secondary schools increased from two to 18.
“I studied theology as a minor because I feel that religion is complimenting me. It makes you strive to become a better person. I am very conscious of everything I do. If you get too engrossed in making money, you lose focus on life. Life is very short. I don’t want to die with all this money,” he explains.
Even though he makes millions, he has little interest in living a life of utter luxury, employing only a driver, a butler and private security.
“You have to live well, but you don’t have to live lavishly to the extreme. You need to be humble. I could buy a plane, a Rolls Royce or a Bentley. But I don’t. If drilling a borehole costs $20,000, you tell me to buy a watch for $20,000? To make a decision that has an impact on people’s lives is a one-second decision for me. If you get too egocentric, you lose your vision. It deceives you.”

NISHATI NA MADINI YAWAPIGA MSASA WACHIMBAJI WADOGO IKIWA NI PAMOJA NA VIONGOZI NA WATENDAJI WA WILAYA NA MADIWANI HUKO TUNDURU MKOANI RUVUMA

0
0
Mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mhandisi Dkt. Crispin Kinabo akiwasilisha mada juu ya utunzaji wa mazingira kwenye migodi wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika mapema leo katika wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma. Mafunzo hayo yalishirikisha viongozi na watendaji wa wilaya, madiwani, wakuu wa vitongoji na wachimbaji wadogo lengo lake likiwa ni kuwapa uelewa wa kanuni za uchimbaji bora wa madini.
Mmoja wa wakilishi wa wachimbaji wadogo ambaye ni mmiliki wa mgodi katika eneo la Mhesi Mapinduzi lililopo wilayani Tunduru Bi Sofia Hamdan akichangia mada wakati wa mafunzo hayo.
Mpepo Ismail ambaye ni mmoja wa wachimbaji wadogo na mmiliki wa machimbo ya shaba Mbesa akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho. Ameitaka Serikali kuangalia uwezekano wa kuwasaidia wachimbaji wadogo kwa kuwakopesha vifaa vya kuchimba madini.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinawasilishwa na watoa mada kwa nyakati tofauti (hawapo pichani).

BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI

SMZ yaombwa kuipatia fedha Wizara ya Kilimo na Maliasili kwa ajili ya kulipa deni wanalodaiwa na wakulima

0
0
Na Miza Kona  -Maelezo Zanzibar 

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeombwa kuipatia fedha Wizara ya Kilimo na Maliasili kwa ajili ya kulipa deni wanalodaiwa na wakulima wa mbegu za mpunga nchi

Akiwasilisha Ripoti ya Kamati ya Fedha Biashara na Kilimo katika Ukumbi wa Baraza La Wawakilishi Chukwani,  Mwenyikiti wa Kamati hiyo Salmin Awadh Salmin amesema Wizara hiyo inadaiwa jumla ya sh milioni 240 na wakulima wanaozalisha mbegu za mpunga katika mabonde mbalimbali ya kilimo hicho.

Alifahamisha kuwa wakulima hao wanadai fedha  hizo zaidi ya miezi minne hali inayopelea kurudisha nyuma maendeleo ya kilimo hicho na kukosa kujikimu kimaisha.

“Kamati ilielezwa kuwa wakulima wa mikataba wanaozalisha mbegu za mpunga katika mabonde mbali mbali wanaidai Wizara jumla ya Tsh milioni 240 baada ya Wizara kuchukua mpunga huo bila ya kuwalipa kwa zaidi ya miezi minne ambapo wakulima wa bonde la Mtwango pekee wanadai Tsh milioni 60,” aleleza Mwenyekiti huyo.

Ameeleza kuwa tatizo hilo linaweza  kuathiri uzalishaji wa mbegu hizo za mpunga kitendo ambacho kinawavunja moyo wakulima na kuathiri kilimo hicho.

Aidha Mhe Salmin ameitaka Wizara hiyo ya Kilimo na Maliasili kukipatia mtaalam wa maabara ya Mifugo na ulinzi wa uhakika  Chuo cha Kilimo kiliopo Kizimbani ili kiweze kufanya kazi zake kwa ufanisi.

Akichangia Ripoti ya Kamati hiyo Mwakilishi wa Viti maalum Asha Bakari Makame ameiomba Serikali kuweka Benki ya mikopo kwa wakulima kutokana na asilimia kubwa ya wazanzibari ni wakulima ili waweze kujikimu wakati wanapopata shida.  

UNIC yaendelea kutoa mafunzo ya mateso ya kambi za wayahudi

0
0
DSC_0014
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond juu ya umuhimu wa kujifunza mauaji ya kimbari ya wayahudi ya mwaka 1933.

=========  ===== ======

Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) kimeendelea kutoa mafunzo na elimu juu ya umuhimu wa kukumbuka maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya ukombozi wa kambi za mateso ya Auschwitz kwa wanafunzi wa sekondari na shule za msingi nchini.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi ya Diamond ya jijini Dar es Salaam leo asubuhi, Afisa habari wa kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama amesema kwamba ni muhimu kwa kizazi na kizazi kujifunza madhara ya mauaji na maangamizi ya moto dhidi ya wayahudi yaliofanywa na askari wa kinazi wa Ujerumani.

“Ni muhimu kutoa mafunzo kwa vijana wakitanzania wa shule za msingi na sekondari ili wajue kwamba tofauti za rangi na za kidini hazina nafasi ya kutugawa kama binadamu,” amesema Nkhoma.


MH. MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA MKOA WA NJOMBE

0
0
Naibu Waziri wa Fedha,Mh. Mwigulu Nchemba hii leo amekutana na Wafanyabiashara wa Mkoa wa Njombe kuzungumza nao Kuhusu Wajibu wao wa Kulipa Kodi,Matatizo wanayokumbana naYo kwenye Biashara na namna ya Kuinua Uchumi wao kama Wafanyabiashara wadogo na wakubwa ndani ya Mkoa wa Njombe na Taifa kwa Ujumla.Sehemu ya Wafanyabiashara waliofika kwenye Ukumbi wa Turbo hapa Njombe mjini kwaajili ya Kuzungumza na Naibu waziri wa Fedha Mh;Mwigulu Nchemba.Kubwa zaidi linaloendelea hapa ni Mkutano wa Kubadilishana mawazo kati ya Naibu waziri,Viongozi wa Uchumi Mkoa,TRA na Taasisi mbalimbali za Uchumi pamja na Wafanyabiashara wa Mkoa huu.

RAIS JAKAYA KIKWETE AWAAPISHA WAZIRI NA MANAIBU WAZIRI IKULU JIJINI DAR LEO

0
0
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Ummy Mwalimu, kuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha George Boniface Tuguluvala Simbachawene, kuwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Kaika Saning’o Telele, kuwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Eng. Dr. Binilith Satano Mahenge, kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal, na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakia katika picha ya pamoja na Waziri na Manaibu Waziri walioapishwa katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wapya na wa zamani wa Ofisi yake, baada ya kuapishwa wapya katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo. Kutoka (kulia) ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Muhangwa Kitwanga, ambaye kwa sasa ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano)Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Eng. Dr. Binilith Satano Mahenge, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu na aliyekuwa Waziri wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Terezya Huvisa, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Waziri na Manaibu Waziri, iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014. Picha na OMR. 

SASENI MEDIA WAIBUKA NA CHANGAMOTO KWA WAIGIZAJI WA FILAMU TANZANIA

0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Saseni Media, Bw. Issa Mbura akizungumza katika warsha hiyo kwa wasanii mbali mbali wa filamu hapa nchini.

Kampuni ya Saseni Media, kwa kupitia mpango wake wa kukuza vipaji vipya vya uigizaji na kuvisimamia, iliendesha kwa mafanikio makubwa zoezi la usaili kwa waigizaji wazoefu na wanaochipukia siku ya jumamosi, tar 25 Januari 2014.

Idadi kubwa ya watu ilijitokeza kujisajili na kufanyiwa usaili na kila mwigizaji alionekana kuwa ni mwenye shauku ya kutaka kupata fursa hiyo na hivyo kuonyesha umahiri wake katika uigizaji. Akizungumzia usaili huo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Saseni Media, Bw. Issa Mbura amesema

“Zoezi lilienda vizuri na pamoja na kupata vipaji kama lilivyokuwa kusudio letu, pia tumeshuhudia mambo kadhaa yakijitokeza kama changamoto kwa tasnia ya filamu inayotegemea sana waigizaji ili kufanya vizuri,” “Moja, ni kwamba Tanzania kuna waigizaji wengi wanaochipukia na kutafuta fursa za kuigiza kuliko wale wachache tuliozoea kuwaona kwenye luninga zetu,”anasema Mwl. Issa.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MAWAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, SAYANSI,ELIMU IKULU DAR

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha-Rose Migiro, wakati alipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014 kwa mazungumzo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014 kwa mazungumzo. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwakaribisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof Makame Mbarawa (katikati) wakati walipofika Ofisini kwake kwa Makamu Ikulu Dar es Salaam, leo Jan 30, 2014 kwa mazungumzo.Picha na OMR 

MWILI WA SHEKH WA MKOA WA MARA WAWASILI UWANJA WA NDEGE MUSOMA

0
0
 NDEGE ILIYOBEBA MWILI WA MAREHEMU SHEKH ATHUMANI MAGEE
 MKUU WA MKOA WA MARA JOHN TUPPA AKIELEKEA KWENYE NDEGE KUONGOZA WAOMBOLEZAJI
 RUBANI WA NDEGE AKIELEKEZA NAMNA YA KUTOA JENEZA LENYE MWILI WA MAREHEMU


 NDANI YA GARI MAALUMU LA JESHI LA WANANCHI WA TANZANIA(JWTZ)LILILOBEBA MWILI WA MAREHEMU
 WAUMUNI WA DINI YA KISSLAMU PAMOJA NA WANANCHI WA MJINI MUSOMA WAKIWA UWANJA WA NDEGE.


 AFIDH WAZIRI MMOJA WA WATU WALIOTOKA NA MWILI WA SHEKH MAGEE DAR AKIAGANA NA RUBANI WA NDEGE

 MWILI UKIONDOLEWA UWANJA WA NDEGE TAYARI KUPELEKWA NYUMBANI

 MSAFARA WA MWILI WA SHEKH MAGEE UKIPELEKWA NYUMBANI

 MKUU WA MKOA WA MARA NYUMBANI KWA SHEKH
 MWILI UKISHUSHWA NYUMBANI
 WAOMBOLEZAJI WAKIWA NYUMBANI

MKUU wa mkoa wa Mara Mheshimiwa John Gabriel Tuppa ameongoza maelfu ya Wananchi wa Mji wa Musoma kupokea mwili wa Shekh wa Mkoa wa Mara Athumani Magee aliyefariki dunia usiku wa januari 28 katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Shekh Athumani Magee alifikwa na mauti baada ya kugua kwa muda na mrefu na kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Bugando kwa muda kabla ya kuhamishiwa Muhimbili kwa uangalizi zaidi na akiwa njiani kupelekwa nchini India kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislam waliokuwepo kwenye uwanja wa ndege Musoma wakiusubili mwili wa shekh Magee wamesema  wamepata pigo kubwa kutokana na msiba huo kutokana na Shekh kuwa mstari wa mbele katika kuhimiza masuala ya dini.

Shekh wa mkoa wa Mara anatarajiwa kuzikwa kesho kabla ya swala ya adhuhur katika makabari ya Musoma Bus mjini Musoma.

   INNAH LILLAH WAINNAH ILLAH RAJIUUN

HABARI NA PICHA KWA HISANI YA SHOMARI BINDA

VYAMA VYA NGUMI ZA KULIPWA VYAUNGANA

0
0

vyama vya ngumi za kulipwa nchini  vimekubali  kuungana na wenzao TPBO kushiriki mkutano wa mapromota wa ngumi na mabondia wote wa Tanzania. Mkutano huo unaotarajiwa  kufanyika katika ukumbi wa vijana hall – kinondoni, siku ya jumamosi tarehe 1/2/2014 kuanzia  saa nne asubuhi. 


Mkutano huo ulioitishwa na TPBO chini ya udhamini wa KITWE GENERAL TRADERS ukiwa na lengo la kuweka mikakati ya sasa na ya baadae kwa ajili ya kuinua ngumi za hapa nchini,sanjali na kutambulikana kwa mapromota na mabondia wenyewe kwa kutengenezewa vyeti maalum na vitambulisho, vitakavyowafanya watambulike katika jamii ya wanamasumbwi wa hapa Tanzania na hata nje ya mipaka ya nchi yetu,hizo ni sehemu ya mada zitakazozungumzwa.
Ibrahim kamwe akizungumza na vyombo vya habari ,alisema ‘Mkutano huo ambao utawahusisha mapromota wote ,pamoja na viongozi wa vyama vya ngumi za kulipwa,makocha na mabondia wote wa ngumi za kulipwa, haijalishi wewe ni nani ili mradi ni mwalimu wa ngumi, mratibu wa ngumi au bondia ni vema ukafika katika mkutano huo ambao ni mara ya kwanza kufanyika  katika historia ya ngumi za kulipwa kuwakutanisha kwa pamoja waratibu, viongozi na mabondia wa nchi nzima kwa pamoja, pia mkutano huo utaendana na mapromota kupewa vyeti  na kurekebisha usajili wa mabondia ambao usajili wao haujakaa sawa

WAJUMBE WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII, WATEMBELEA CHUO CHA MAENDELEO YA JAMII, RUNGEMBA IRINGA

0
0
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Mhe.Saidi Mtanda (Mb.) wakikagua maeneo / miradi ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba na kutoa maelekezo kwa watendaji wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, katika baadhi ya maeneo yenye kuhitaji maboresho.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii leo wametembelea Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba kilichopo Wilayani Mufindi, Mkoa wa Iringa. Lengo la ziara hii ni kukagua utekelezaji wa shughuli za Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto katika utoaji wa Mafunzo ya Maendeleo ya Jamii kupitia chuo hiki. Katika ziara hii, wajumbe wa kamati walipata fursa ya kupokea taarifa ya chuo na kutembelea maeneo / miradi mbalimbali ya chuo.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe. Dkt. Pindi Chana (mb.) akiwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba kilichopo Wilayani Mufindi, Mkoa wa Iringa.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe. Dkt. Pindi Chana (Kati) pamoja na Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba, (Kulia, mwenye nguo ya kahawia) Bibi Santina Mbata wakiwapitisha Waheshimiwa Wabunge ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika Majengo / miradi ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba. 

TAMKO LA MZEE JOHN MALECELA KUHUSIANA NA GUMZO LA MBIO ZA URAIS 2015 HAPA NCHINI

0
0


Ndugu zangu waandishi wa habari, awali ya yote naomba niwasalimie na niwapongeze kwa kufika -mwaka mpya 2014, pia naomba niwapongeze kwa kazi kubwa ambayo mmekuwa mkiifanya hasa kuhakikisha watanzania wanapata habari kwa kila jambo linaloendelea kila kona ya taifa letu la Tanzania.

Ndugu waandishi wa habari nimewaita hapa ili kuzungumza nanyi na mnisaidie kufikisha ujumbe kwa watanzania hasa kuhusu jambo hili ambalo limekuwa gumzo kwa watanzania wengi la mbio za urais 2015 kwa baadhi ya watu ndani ya chama changu cha mapinduzi (CCM), kilichonisukuma zaidi na kupata hamu ya kuongea nanyi ni baada ya kumsikia -na kumuona kijana wetu ndani ya chama cha mapinduzi bwana Paul Makonda akiwa na ujasiri wa kukemea vitendo mambo haya yanayofanywa na baadhio ya viongozi bila uwoga wowote naomba tuchukue fursa hii kumpongeza sana kijana huyu.

Nadiriki kusema nampongeza kijana huyu hasa kwa kauli zake nzito na za kijasiri kwa maslahi ya chama changu cha CCM ili chama kiendelee kupendwa na kuchaguliwa na watanzania.

Pia itakuwa si busara kama sitawapongeza vijana wangu katibu mkuu wa chama ndugu ABDULRAHMAN KINANA na NAPE NNAUYE kwa juhudi zao za dhati za kujenga chama na kuendelea kuwaeleza wananchi juu ya misingi bora ya chama cha mapinduzi (CCM) kwa kuwakemea viongozi wasiofaa bila kujali cheo na umaarufu wao ndani ya chama na serikali, nawaomba waendelee -na juhudi zao hizo nami naziunga mkono juhudi zao na kama kuna watru wanaowabeza naomba wasijali kwani kukemea viongozi wasiofaa ndani ya chama na serikali ni msingi wa chama chochote kilichounda serikali.

Aidha nawaomba watanzania wenzangu wazalendo wasikubali kukatishwa tama na kikundi cha watu wachache wasio na mapenzi mema na taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa kwa amani, upendo, utulivu na mshikamano urithi tulioachiwa na baba yetu wa taifa mwalimu julias kambarage nyerere ndani na nje ya mipaka ya bara letu la afrika.

Ndugu zangu waandishi wa habari naomba niwaambie kuwa msemaji wa UVCCM kijana wetu Paul Makonda namuunga mkono kwa -kitendo chake cha ujasiri cha kumkemea ndugu EDWARD NGOYAI LOWASSA bila uwoga kwa jinsi anavyokivuruga chama chetu kwa lengo la kutaka urais 2015 huku secretariet ya chama ikiwa imekaa kimya wakati inajua kuwa muda wa kuanza mbio hizi bado na kufanya hivi kwa sasa ni kukiuka misingi na katiba -ya chama. Hapa najiuliza kuwa ile misingi imara ya uongozi ndani ya chama chetu cha mapinduzi iko wapi? Mpaka tumuachie mototo ndio akemee haya? Je, hapa chama kiko wapi?

Ukweli ni kwamba wanachama wetu na vijana wamekuwa njia panda huku wakitamani kusikia tamko au karipio la chama juu ya suala hili la harakati za urais 2015 bila mafanikio.

Naomba niseme kuwa bila kuwa na karipio au tamko la chama, hawa wanaotumia pesa zao hadharani kwa lengo la kutafuta umaarufu na ushawishi kwa vijana ili kupata madaraka wanaharibu misingi yetu bora ya uongozi iliyowekwa na waasisi wetu ndani ya chama.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuona juhudu za uongozi wa sasa wa chama ngazi ya juu ikiwa ni pamoja na sekretarieti inayoongozwa na katibu mkuu ABDULRAHMANI KINANA na katibu mwenezi NAPE NNAUYE za kutetea chama hiki zinatiwa mchanga.

Ninaomba juhudi hizi zisibezwe na watu wenye nia njema na chama. Ukweli ni kwamba vijana hawa wamekuwa na juhudi kubwa sana ya kujenga na kuimarisha chama chetu -kwa wananchi kila pembe ya taifa letu kwa kukemea na kueleza misingi ya uongozi bora. Swali: Je! Chama hakioni haya mpaka vijana ndio waone?

Kwa hili ni lazima tubadilike ili kujenga chama chetu na naishauri -secretariet ya chama lazima ichukue hatua mara moja, kijana huyu paul makonda asingesema haya yote kama hana uhakika wa ushahidi wa wa haya aliyoyasema na nampongeza sana.

Vijana na wanachama wengi wa CCM wamekuwa na hamu kwa muda mrefu ya kutaka kujua msimamo wa chama chao bila mafanikio na ndio sababu ya baadhi ya-wengine kupoteza mwelekeo.

Sisi tulikijenga chama hiki kwa taabu sana hapakuwa hata mtu mmoja aliyediriki kutumia fedha zake kutaka madaraka. Nidhamu, busara na uchungu wa rasilimali za taifa hili kwa maslahi ya wananchi ndio vilituongoza kufuata misingi na maadili ya uongozi ndani ya chama na serikali, ndio maana tunaumia sana kuona chama sasa kinataka kutekwa na wenye fedha kwa uchu wa madaraka, mpaka tunashangaa na kujiuliza hizi pesa wanatoa wapi? Na haya madaraka wanayotaka kwa kununua ni kwa maslahi ya nani? Huku watanzania wakiendelea kuwa maskini.

Mfano hivi karibuni baadhi ya viongozi wa chama ngazi ya juu wamejibishana kwenye vyombo vya habari,vitendo hivi havina tija kwa chama na wala havileti umoja na mshikamano ambao umedumu ndani chama kwa muda mrefu.

Mwisho Ninaomba sekretarieti ichukue hatua haraka kama alivyoomba kijana wetu makonda na kweli kuchelewa kuchukua hatua jambo hili kumejionyesha wazi kwamba utaleta kutokuelewana ndani ya chama kusiko kuwa na lazima.


JOHN SAMWELI MALECELA

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

MSAADA WAKO UNAHITAJIKA KUOKOA MAISHA YA MTOTO MARYAM

0
0
Kuna mdada wa miaka 18 Ambae amejifungua binti anaeitwa Maryam kwa bahati mbaya sana mtoto Huyo alipozaliwa hakua na sehemu ya kutoa choo kikubwa hali ya Kua kwamba sehemu hiyo imefunga. Kwa ujuzi wa ma daktari wa muhimbili wamemtoboa hapo ubavuni ili atoe choo kikubwa kwa njia hii. 

Madaktari walimshauri mama mzazi mtoto atafanyiwa operation wa kufungua njia ya choo kikubwa akifika mwaka na nusu. Sasa amefika umri na mama mzazi yupo kwenye hali Duni sana na Hana hela ya kumfanyia mtoto operation huo. 

Nawaomba ndugu zanguni tumsaidie huyu mtoto, kwani hali hii Inaweza kumkuta mtu yoyote. Haya ni Maisha Yake nawaomba mjitokeze kwa Moyo mkunjufu tumsaidie huyu mtoto. 

Kama Una msaada Wowote ule tafadhali nipige mimi apa kwa kutumia number: +255719009004 au Kama upo nje ya Tanzania na umeguswa na hili na unataka kutoa sadaka yako tafadhali Tuma kwenye account yangu ya Barclays: Miss S.Yussuf sort code: 207103 acc: 73049328 pia unaweza kutuma njia ya wastern union. 

Kwa mlikuwepo Tanzania hiyo number yangu ya TIGO PESA. Ahsante sanaa

KUTOA NI MOYO SI UTAJIRI. MUNGU AWABARIKI SANA.

Bendi ya 'Sikinde' kutoa burudani ya nguvu leo Sinza, Meeda

0
0


Bendi ya Mlimani Park Orchestra almaarufu kama Sikinde inategemea kuburudisha wapenzi wa muziki wa dansi kutoka Dar es Salaam leo Ijumaa (31 Januari 2014) katika ukumbi wa Meeda Sinza wilayani Kinondoni.

Akizungumza kwa niaba ya bendi ya Sikinde, Katibu wa bendi hiyo Hamis Mirambo amesema “baada ya kukaa muda mrefu bila kufanya shoo yeyote katika wilaya ya Kinondoni ,bendi ya Sikinde sasa ipo tayari kuwakosha moyo za wapenzi wa muziki wa dansi katika wilaya hiyo pamoja na watu wa wilaya za jirani.”

“Tunapenda kuwaalika wapenzi wote wa muziki wa dansi wasikose kuhudhuria shoo yetu ambayo itaanza ukumbini Meeda kuanzia saa mbili usiku,” alisema Mirambo.

Aliongeza, “Karibuni mpate kuburudika na nyimbo za zamani na mpya kutoka bendi hii kongwe hapa nchini. Mpate kusikia kutoka kwa msanii Bichuka na wengine wengi…karibuni sana!”

Kwa hivi sasa bendi hiyo ya Mlimani Park Orchestra inamalizia kukamilisha albamu yao mpya iitawayo “Jinamizi la talaka” ambayo inabeba nyimbo kama Kibogoyo, Deni ntalipa, Ng’ombe haelemewi nunduwe, Kukatika kwa dole gumba, Tabasamu na Mkwezi. 

JIUNGE NA GLOBAL BREAKING NEWS SASA!

0
0
Kuwa wa kwanza kupata Breaking News za wasanii, watu maarufu na zingine kutoka Magazeti Pendwa ya IJUMAA WIKIENDA, UWAZI, RISASI, AMANI, IJUMAA na CHAMPIONI moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi kwa shilingi 100 tu kwa SIKU!

Kujiunga tuma GLOBAL kwenda 15778
Huduma hii ni kwa watumiaji wa Vodacom pekee. Kwa maelezo zaidi LIKE Ukurasa wetu wa Facebook hapa: http://on.fb.me/L0OSPD

KINANA, MANGULA WAWASILI MKOANI MBEYA KWA MAADHIMISHO YA MIAKA 37 YA CCM

0
0
 Makamu Mwenyekiti wa CCM,Phillip Mangula akisalimiana na Mbunge wa Viti Maalum, Dk. Mary Mwanjelwa baada ya kuwasili leo asubuhi kwenye Ofisi za CCM Mkoa wa Mbeya , tayari akwa maadhimisho ya miaka 37 ya CCM yatakayofanyika kitaifa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya Jumapili Februari 2. Kushoto ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.
 Mangula (katikati) akiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Godfrey Zambi.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akizungumza na Nape (kulia) pamoja na Zambi kwenye chumba cha watu mashuhuri (VIP) alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, Mbeya leo mchana, tayari kwa maadhimisho hayo.
 Nape (kulia) akizungumza na Kinana pamoja na Zambi kwenye Uwanja wa Ndege wa Songwe
Dk. Mary Mwanjelwa (kushoto) akijadiliana jambo na Makmu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Dogo Idd Mabrouk wakati wa mapokezi hayo.
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images