Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

SHIRIKA la Compassion Internation Tanzania LAJIKITA ZAIDI KWA WATOTO

0
0

 Mkurugenzi wa Nchi wa shirika la Compassion Internation Tanzania Mch.Joseph Mayalaakizindua jengo jipya la jiko la kisasa lenye majiko matatu pamoja na stoo ya kuhifadhia chakula katika kituo cha P.A.G kilichopo njiro mkoani Arusha jana kilicho gharimu shilingi mil.17(picha na pamela Mollel)
Mkurugenzi wa Nchi wa shirika la Compassion Internation Tanzania Mch.Joseph Mayala akiimba na watoto wanaoishi katika mazingira magumu muda mchache baada ya kuzindua jiko jipya la kisasa lenye majiko matatu pamoja na stoo ya kuhifadhia chakula katika kituo cha P.A.G kilichopo njiro mkoani Arusha jana kilicho gharimu shilingi mil.17(picha na pamela Mollel)
=====  ======= ===== =====
Na Pamela Mollel,Arusha

Shirika la Compassion Internation Tanzania pamoja na washirika wenza wanampango wa kuwahudumia watoto zaidi ya laki mbili na nusu kwa mawaka wa fedha 2012-2013 ifikapo 2020 hapa Nchini.

Mkurugenzi wa Nchi wa shirika la Compassion Internation Tanzania Mch.Joseph Mayala alitoa kauli hiyo jana wakati akizindua jiko jipya la kisasa lenye stoo ya kuhifadhia chakula cha watoto katika kituo cha P.A.G kilichopo njiro Mkoani Arusha

Mch.Mayala alisema kuwa lengo hasa la kuwahudumia watoto ni kuwajengea maarifa zaidi na uwezo wa kufanya mambo mbalimbali hasa katika maeno ya uongozi sanjari na kukuza teknolojia ya habari na mawasiliano kwa watoto wanaohudumiwa  katika vituo kwa kuhakikisha vinakuwa na mtandao

Pia alitaja lengo jinge kwa mwaka huu wa fedha kuwa ni pamoja na vituo kuwa na kompyuta pamoja na madarasa ili kuwajengea uwezo wa kuhimili teknolojia sambamba na kuimarisha ushirika wenza na makanisa kwa kuhakikisha kwamba wanawaandaa ili leo na kesho waweze kuwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika eneo lao husika kutokana na kujengewa uwezo wa awali.

Hata hivyo aliweka wazi juu ya elimu ya sekondari kwa vijana na watoto kuwa mwaka jana waligundua matokeo hayakuwa mazuri hivyo wameamua kuwa na mikakati ya kuwa na madarasa ya ziada kwaajili ya vijana waliopo sekondari ili waweze kupata msaada katika maeneo ambayo wanakutana na changamoto kielimu.

“Tumegundu kuwa tunamfadhili mtoto ndiyo lakini kuna umuhimu wa kuijengea pia uwezo familia ili leo na kesho kutwa au compassion hawapo inakuwa rahisi familia kumudu kumsomesha motto”alisema 

Hata hivyo alisema kuwa tayari wameshafungua vituo vipya 8 mkoa wa Dar es salama huku akidai kuwa wanampango wakuanzisha vituo vingine  vipya mkoa wa Kigoma na katika baadhi ya maeno ya wilaya ya Tabora vijinini

Kwa uapnde wake Mkurugenzi wa kituo cha P.A.G Amani Simon Msemo alisema kiasai cha million 17 zimetumika katika ujenzi wa jengo pamoja na  majiko matatu ya kutumia kuni na stoo ya kuhifadhia chakula.

Msemo alisema kuwa wataondokana na changamoto kubwa waliyokuwa nayo ya awali ya kupika nje jambo ambalo lilikuwa likiwapelekea kushindwa kwenda na ratiba hasa nyakati za mvua

“Matumizi ya kuni yalikuwa makubwa hivyo kuchangia katika uharibifu wa mazingira unaotokana na ukataji mkubwa wa kuni katika maeno mbalimbali ya Nchi yetu”alisema Msemo

Pia alitoa shkurani kwa uongozi mzima wa kanisa,Shirika la Compassion pamoja na muwezeshaji wa kituo  Esther Mgimba na wenzake kwa kitendo cha kukamilisha huduma hiyo.

Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Makamu wa Rais lafanya kikao chake Mkoani Morogoro

0
0
  Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mh. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais mara baada ya kufungua mkutano wa siku mbili katika hotel ya Hilux mjini Morogoro. (Picha zote na Lulu Mussa)
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mh. Samia Suluhu Hassan (katikati) akifungua kikao cha siku mbili cha Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais. Kikao hicho kinafanyika Mkoani Morogoro. Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Ndg. Sazi Salula na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Ngosi Mwihava.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wakimsikiliza Mgeni Rasmi Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mh. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili katika Hotel ya Hilux mjini Morogoro.

Castle Lite yataja watakaomshuhudia Kanye West

0
0

Meneja wa kinywaji cha castle lite Pamela kikuli akimpongeza mshindi wa shindano laFeel the Beet of Sub Zero’ nchini Afrika ya kusini , Caroline Lupilli lililoendeshwa kwa kuwashirikisha washiriki wa mtandao wa facebook 
===== ======= ========

WATANZANIA watatu waliobahatika kuhudhuria tamasha kubwa la muziki lijulikanalo kama ‘Feel the Beet of Sub Zero’ wamejulikana.

Tamasha hilo la kimataifa linaloandaliwa na kinywaji cha Castle Lite, linatarajiwa kufanyika Johannesburg, Afrika Kusini Februari 2, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Bia ya Castle Lite inayozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Pamela Kikuli, alisema watu hao watalipiwa kila kitu ikiwa pamoja na nauli ya kwenda na wenza wao watakaowachagua.

Pamela aliwataja watu hao ambao walipatikana kupitia shindano lilikuwa likiendeshwa katika kurasa ya Castle Lite kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, kuwa ni Caroline, Edger na Eric.

“Hii ina maana kuwa Castle Lite itawalipia watu sita ikiwa ni gharama za kwenda huko, kwani tulisema kila mmoja ataenda na rafiki yake atakayemchagua.

“Tumefanya hivi ikiwa ni kurudisha fadhila kwa jamii, maana kwa kiasi kikubwa imetuunga mkono katika mambo mbalimbali,” alisema.
Mwanamuziki maarufu atakayetumbuiza katika tamasha hilo ni Kanye 

YALIYOJIRI SAFARI YA KITALII KWENYE HIFADHI YA MIKUMI JAN 26, 2013

0
0


Safari ya kitalii ya kwenda katika hifadhi ya taifa ya Mikumi iliyoandaliwa na kampuni ya utalii ya Landland Africa jumamosi wiki iliyopita imekuwa ya mafanikio baada ya watalii kuona idadi kubwa ya wanyama wakiwemo simba, chui na wanyama wengine.

Mbali na kuona wanyama hao watalii walilala kwenye kambi namba moja huku wakizungukwa na idadi kubwa ya wanyama. Kabla ya kulala watu wote tuliuzunguka moto (camp fire) na kuanza kupiga soga ambapo kila mtalii alitoa simulizi yake, ilikuwa safi sana…kwa picha zaidi tembelea facebook page yetuwww.facebook.com/lakelandafrica.

Wiki hii Lakeland inakuletea safari ya siku moja kwenye mji wa kihistoria Bagamoyo; utapata historia ya mji huo, utaogelea kwenye beach safi, utakula, utakunywa, utaburudika na hutataka kuondoka!
Kwa ratiba kamili ya safari za kitalii za kila mwisho wa wiki tembelea tovuti yetu www.lakelandafrica.com/safaris/scheduled-trips

mtanzania kumvaa mghana machi 8 kugombea ubingwa wa jumuiya ya madola

0
0

Mtanzania Fadhili Majia sasa atamvaa Mghana Isaac Quaye tarehe 8 March kutafuta nafasi ya kugombea mkanda wa ubingwa wa Jumuiya ya madola (CBC) ambayo unashikiliwa na bondia Kevin Satchell  wa Uingereza.
 

Mpambano wa Majia na Quaye umemsogezwa mbele kwa kuwa mashindano ya ubingwa wa Afrika yanayoendelea nchini Afrika ya Kusini yanarushwa na televisheni ya Super Sports ambayo ndio wafadhili wakubwa wa mpambano wao.
 
Wakati huo huo bondia Richard Commey wa Ghana atamvaa Mghana mwenzake Bilal Muhammed kugombea mkanda wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati uzito wa lightweight siku hiyo hiyo March 30. Aidha bondia Frederick Lawson wa Ghana atazichapa na bondia Isaac Sowah wa Ghana kugombea mkanda wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati  katika uzito wa Welterweight. Mapambano hayo yatasimamiwa na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi
 
Mtanzania mwingine atakaye peperusha bendera ya taifa siku hiyo ni pamoja na Allan Kamote atakayezichapa na bingwa wa zamani wa IBF wa mabara na ambaye ndiye bingwa wa sasa wa WBA wa mabara Emmanuel Tagoe katika pambano lisilo la ubingwa.
 
Naye bondia wa Kenya Michael Odhiambo atachuana vikali na Mghana George Ashire katika mpambano usio wa ubingwa uzito wa lightweight.
  
Mapambano hayo yote yatakuwa ni ya utangulizi katika mpambano wa ubingwa wa dunia kati ya bondia maarufu wa Ghana anayeishi nchini Marekani Joseph Agbeko na Luis Mendelez kutoka nchini Columbia.


IBF/Afrika inawaomba watanzania kwa ujumla wao wawaombee mabondia wake ili waweze kupeperusha vyema bendera ya taifa.

Imetolewa na:

UTAWALA
International Boxing Federation Africa
DAR-ES-SALAAM

Airtel kuchezesha Droo ya mwezi ya milioni 30 kesho

0
0

             Wateja wawili wa Airtel kujinyakulia  kitita cha shilingi milioni 15
•              Promosheni ya amka millionea bado inaendelea

Jumatatu Januari 28, 2013 Kampuni ya simu za mkononi Airtel bado inaendelea kuwazawadia wateja wake kupitia promosheni ya Amka Millionea ambapo imetangaza kuchezesha droo ya pili ya mwisho wa mwezi kesho jumanne tarehe 29 itakayowawezesha wateja wake wawili kuibuka na kitita cha shilingi million 15 kila mmoja

Akizungumza juu ya droo hiyo Meneja Uhusiano wa Airtel bwn Jackson Mmbando alisema, “tangu ilipozinduliwa mwanzoni mwa mwenzi December mwaka jana tumekuwa tukiwazawadia wateja zawadi za pesa taslimu kila siku, kila wiki na kila mwenzi. Droo ya kwanza ya mwenzi wa December ilifanyika  na kushuhudia  Agnes Hassani Chakame mwenye umri wa miaka 27, mkulima na makazi wa Rufiji pamoja na Rickson Richard Kilonzo  mwanafunzi wa kidato cha 5, umri wa miaka 19 ambae ni mkazi wa Arusha wakiibuka mamilionea  kila mmoja akiondoka kitita cha shilingi milioni 15”.

“Na leo tunayofuraha kuwatangazia droo ya mwenzi Januari ambapo wewe pia una nafasi ya kuibuka kuwa mshindi, droo hii itafanyika kesho saa tano hapa makao makuu ya Airtel Moroco na washindi kutangazwa mara baaada ya droo hiyo Ikiwa hujashiriki unaweza kujaribu bahati yako sasa!

Ili mteja aweze kushiriki inabidi atume neno WIN/SHINDA kwenda namba
15595 bure , Baada kujiunga mteja atapata ujumbe kutoka 15656 na kupata maswali ambayo atajibu na akipata sahihi atapata ponti 20 akikosea atapata ponti 10. Na kwakila ujumbe atakaotuma atatozwa kiasi cha shilingi 350 pamoja na kodi.

Airtel tunaahidi kuendelea kuboresha huduma zetu na kuendelea kuwazawadia wateja wetu kupitia promosheni mbalimbali huku tukiwapatia huduma nafuu kupitia mtandao ulioenea zaidi nchini. Aliongeza Mmbando

Mbali na promosheni hii kabambe,  Airtel pia imekuwa mstari wa mbele kutoa gharama nafuu za mawasiliano kwa wateja wote nchini, Airtel imeimepunguza gharama za kutuma sms, ujumbe mfupi pamoja na gharama za kupiga simu ambapo kwa sasa mteja wa Airtel atatozwa shilingi 1 kwa sms moja siku nzima mara baada ya kutuma ujumbe mfupi wa kwanza kwa shilingi 125, na pia  gharama za kupiga simu kwenda Airtel kwa Airtel sasa ni senti 10 mara baada ya dakika mbili za kwanza. 

sekretarieti ya ccm taifa yafanya ziara kijiji cha nguruka na uvinza mkoani kigoma leo.

0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na Wazee wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo,wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji viwili vya Wilaya hiyo ya Uvinza.



Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza mkoani Kigoma leo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana (UVCCM),Martin Shigella akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Nguruka,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Uvinza,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma leo,waliojitokeza kwa wingi kumsikiliza na pia kusikiliza shida zao wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji viwili vya Wilaya hiyo ya Uvinza.

Mzee wa Makamo akitabasamu wakati akimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana (hayupo pichani) wakati alipokuwa akihutubia.

 Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Uvinza,Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma mapema leo jioni.
 Pichani juu na chini ni Sehemu ya Wakazi wa mji wa Uvinza,wilayani Uvinza mkoani Kigoma wakiwa wamejitokeza kwa wingi na kuupokea ujumbe wa wajumbe wa Sekretarieti ya CCM Taida,ilioongozwa  na  Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana 


Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akijadiliana jambo na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye.

Msanii wa Muziki wa kizazi kipya,Dokii akiimba moja ya nyimbo zake alizozitunga kwa ajili ya CCM.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa pamoja na Katibu wa CCM katika kata ya Nguruka,Asha Baraka wakati wa matembezi ya kuingia kwenye kijiji hicho cha Nguruka mkoani Kigoma leo.
Katibu wa CCM katika kata ya Nguruka,Asha Baraka akiwasalimia wananchi wake.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwasalimia wananchi waliokuwa wamejipanga barabarani kumuona.
Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiimba nyimbo na wananchi wa kijiji cha Nguruka.

lulu arejeshwa tena rumande,dhamana yake kujulikana kesho.

0
0

Msanii wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama  ‘Lulu’ akitoka Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,  licha ya dhamana yake kuwa wazi, lakini alishindwa kutoka kwasababu ya kukosekana kwa Msajili wa Mahakama Kuu. Msanii huyo sasa atatoka kesho baada ya kurudishwa tena mahakamani kwa ajili ya kuangalia kama ametimiza masharti ya dhamana yake.

Pamoja na hayo, mwonekano wa msanii huyo unazidi kutia wasiwasi. Handeni Kwetu ilipokea simu nyingi zinazotaka kujua kama kweli mwanadada huyo ni mjamzito. Hata hivyo, wataalamu wa mambo wanaweza kuchunguza vyema wakati na sisi tunasubiri kupata kauli yake au vipimo vya daktari.
Lulu akipanda gari lililomleta Mahakamani.
Hili ndilo gari lililomleta Mahakamani.
Hapo Vipi?
Hapo Lulu anapanda gari.Picha zaote kwa hisani ya Handeni Kwetu Blog

sekretarieti ya ccm taifa yatembelea mradi mkubwa wa ujenzi wa daraja la malagarasi leo mkoani kigoma

0
0
Wajumbe wa Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi  (CCM) wakiongozwa na Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana leo wamembelea na kukagua mradi mkubwa wa  ujenzi wa Daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi lililopo wilayani Uvinza Mkoani Kigoma.

Ziara hiyo ya Wajumbe hao ni moja ya shamra shamra za maadhimisho ya Miaka 36 ya CCM ambayo mwaka huu inaadhimishwa Mkoani Kigoma kitaifa, na Wajumbe hao wameamua kukagua miradi kadhaa ya Maendelea ambayo iliahidiwa na Chama hicho tawala wakati wa Kampeni zake za Uchaguzi mwaka 2010.

Katika ziara hiyo Kinana ameambatana na Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Katibu wa UVCCM taifa,Martin Shigela.

Ujenzi wa daraja hilo  lenye urefu wa mita 275 linatarajiwa kumalizika mnamo Oktoba ambapo Rais Kikwete ndiye atakayekuja kulizindua rasmi.

Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana akiongoza Wajumbe wake wa Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi  (CCM),leo akifafanua jambo mbele ya Wanahabari mara baada ya kumaliza kutembelea na kukagua mradi mkubwa wa  ujenzi wa Daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi lililopo wilayani Uvinza Mkoani Kigoma,shoto ni Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha Rose Migiro na kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Mh Issa Machibya.
Mmoja wa Wakandarasi wa ujenzi wa daraja hilo kutoka kampuni ya Hanil Engeneering  pichani kulia kutoka nchini Korea,akitoa ufafanuzi kwa Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana,

Sehemuu ya daraja la Malagarasi kama lionekavyo.

Mmoja wa Wakandarasi wa ujenzi wa daraja hilo kutoka kampuni ya Hanil Engeneering  pichani kati kutoka nchini Korea,akitoa ufafanuzi kwa Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana,pichani shoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma,Mh Issa Machibya.

 Sehemu ya Mto Malagarasi kama uonekanavyo pichani.
Baadhi ya wajenzi wa barabara inayounga daraja la Malagarasi,imbayo inatarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami,yenye urefu wa kilometa 76.6 wakiendelea na kazi.

masumbwi ngumi mawe yalivyofanyika tandale

0
0
Bondia Charles Mashali kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Adam Ngange wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumb i wa CCM Tandale Dar es salaam jana Mashali alishinda kwa point .

Bondia Adam Ngange kushoto akioneshana umaili wa kutupiana makonde na Charles Mashali wakati wa mpambano wao uliofanyika kwa mala ya kwanza katika ukumbi wa CCM Tandale Dar es salaam jana.
Bondia Athumani Pendeza kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Kalama Nyilawila wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa CCM Tandele nyilawila alishinda kwa K,O raundi ya tatu .

Bondia Kalama Nyilawila kushoto akipambana na Athumani Pendeza wakati wa mpambano uliofanyika katika ukumbi wa CCM Tandale Dar es salaam jana Nyilawila alishinda kwa K,o raundi ya tatu.
Baazi ya wadau wa mchezo wa ngumi wakiwa na mabondia kutoka kushoto ni Kaike Silaju, Nassoro Choro,Selemani Kidunda, Thomas Mashali na Kibavu wakifatilia masumbwi
Bondia Fadhili Majia kushoto akikwepa konde la Antoni Mathias wakati wa mpambano wao uliofanyika CCM Tandale Dar es salaam jana Majia alishinda kwa K,O raundi ya pili .
Bondia Hassan Mandula kushoto akimlushia makonde James Martini  wakati wa mpambano wao uliofanyika jana Mandula alishinda kwa point picha na www.superedboxingcoach.blogspot.com

NGOWI MSIMAMIZI MKUU UBINGWA WA MABARA NCHINI GHANA

0
0

Rais wa Shirikisho la Ngumi la Kimataifa IBF bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi atakuwa msimamizi mkuu wa mapambano ya ubingwa wa yatakayofanyika nchini Ghana tarehe 8 na 30 March 2013.

Mapambano hayo ni yale yanayowakutanisha mabondia Richard Commey akipambana na Mgana mwenzake Bilal Mohammed wakigombea mkanda wa IBF Afrika na Ghuba ya Uajemi (IBF AMEPG) katika uzito wa Lightweight.  Mabondia wote wawili wana rekodi zinazovutia, Commey ana makazi yake katika jiji la London nchini Uingereza.

Mpambano wa pili siku hiyo utawakutanisha mabondia wawili wa Ghana Fredrick Lawson akipambana na bondia machachari Isaac Sowah. Wote wanaishi nchini Ghana.

Mapambano yote yatafanyika wakati bingwa wa dunia wa zamani wa IBF Joseph Agbeko atakapochuana na bondia Luis Melendez wa Mexico kugombea ubingwa wa dunia wa IBO katika uzito wa bantam.

Mpambano mwingine ambao Ngowi atasimamia ni kati ya bondia Helen Joseph wa Nigeria na Fatuma Zarika wa Kenya ambao watagombea mkanda wa IBF wa mabara wa wanawake. Helen Joseph ni mkazi wa Ghana wakati Fatuma Zarika anaishi nchini Ujerumani.

Maofisa wengine watakaomsaidia Ngowi katika mapambano hayo ni pamoja na: Refarii: Rodger Barnor, Jaji namba 1 ni Fred Ghartey, Ghana, Jaji namba 2  ni Confidence Hiagbe na jaji namba 3 ni May Mensah Akakpo, Ghana     

Mapambano haya ni kati ya mapambano 100 ambayo IBF imepania kuyafanya katika ukanda wa Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati mwaka huu 2013.

Imetolewa na:

UTAWALA
 
International Boxing Federation Africa
Dar-Es-Salaam, Tanzania

Serikali Yataja Manufaa kwa Wana-mtwara Gesi Ikipelekwa Dar

0
0

SERIKALI imetaja manufaa na faida ambazo wanatarajia kuzipata wananchi wa Mtwara pamoja na Lindi endapo gesi itasafirishwa kwenda Jijini Dar es Salaam.

Imesema Mkoa wa Mtwara ndipo utakapo jengwa mtambo mkubwa wa kusafishia gesi hiyo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Dar es Salaam kwa matumizi ya uzalishaji umeme na matumizi ya moja kwa moja viwandani.

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alipokuwa akizungumza katika Kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Radio One jijini Dar es Salaam.

Naibu waziri huyo ameweka wazi kuwa mkoani Mtwara licha ya Serikali kupanga kujenga viwanda vingine kadhaa, inajenga mtambo wa megawati 250 ambao utakuwa ukizalisha umeme na mwingine kujengwa mkoani Lindi eneo la Somanga Funga utakao kuwa ukizalisha megawati 520.

Akifafanua zaidi Simbachawene alisema eneo la Mikindani katika Kijiji cha Msijute mkoani Mtwara kinatarajiwa kujengwa kiwanda kikubwa cha saruji Afrika Mashariki na Kati chenye uwezo wa kutoaji ajira kwa watu 6000 jambo ambalo ni manufaa ya Wanamtwara.

Alisema pia tayari kuna wawekezaji wa viwanda vya mbolea wamejitokeza kujenga viwanda mkoani Mtwara na Serikali itaviacha vinu vya kuchimba na kusindika gesi eneo hilo jambo ambalo bado ni manufaa makubwa kwa wananchi.

“Viwanda vya kusindika gesi hii vimepangwa kujengwa maeneo ya Lubasi, Kishere, Mchinga Bay, Lindi, Sudi Bay, Airport pamoja na Mikindani…viwanda vyote hivi vitatoa ajira kubwa sana,” alisema Naibu Waziri.

Alisema licha ya manufaa hayo, gesi itakapopelekwa Dar es Salaam itazalisha umeme wa uhakika pamoja na kutumika moja kwa moja viwandani jambo ambalo litailetea taifa tija kubwa ikiwa ni pamoja kupunguza ukali wa maisha.

“Ni kweli gesi imepatikana Mtwara lakini ni lazima uipeleke sokoni ili iweze kupata soko (wateja)…Dar es Salaam ndio kwenye soko, huwezi ukaiacha Mtwara ambako hakuna soko; mbali na kuzalisha umeme kuna viwanda 37 na hoteli kadhaa zinataka ziitumie moja kwa moja ni lazima iletwe huku, Mtwara pale hakuna soko,” alisema.

Aidha alitolea mfano kuwa zipo nchi mbalimbali ambazo zimegundua gesi lakini zimelazimika kuisafirisha kwa mabomba kwenda eneo la soko. Alibainisha kuwa nchi ya Urusi inasafirisha gesi yake hadi nchini Ujerumani huku Iran ikisafirisha hadi India gesi yake kutafuta soko lilipo.

Alisema miundombinu mikubwa ya umeme ipo jijini Dar es Salaam hivyo kuna kila sababu ya gesi hiyo kuletwa jijini humo ili iweze kuzalisha umeme na matumizi ya viwandani moja kwa moja pamoja na matumizi mengine, ambapo tayari wateja wamepatikana.

Aidha aliongeza kuwa uzalishaji umeme wa kutosha kwa kutumia gesi utapunguza bei ya umeme na kuuzwa kati ya senti 6 na 8 za Marekani jambo ambalo litapunguza ugumu wa maisha na pia bei ya bidhaa nchini.

Pamoja na hayo amevitaka baadhi ya vyama vya siasa na taasisi zisizo za Serikali (NGO’s) zinazowapotosha Wanamtwara juu ya mradi huo kuacha kitendo hicho kwani hakuna asiyejua umuhimu wa gesi hiyo kuja Dar es Salaam.

“Hivi ni nani asiyejua kuwa tatizo la kutokua na umeme wa uhakika nchini ndilo linalokwamisha uchumi wa nchi…Tanzania inapoteza bilioni 4.5 kwa ajili ya kununua mafuta ya kuzalisha umeme kwenye mitambo yake, sasa gesi itaokoa fedha hizi,” alisema Simbachawene.

Hata hivyo amesema Serikali haiwezi kutekeleza mradi huo kwa nguvu bali itaendelea kuwaelimisha Wanamtwara umuhimu na manufaa ya gesi hiyo kuletwa Dar es Salaam na inaimani wataelewa na malumbano kumalizika.

*Imeandaliwa na www.thehabari.com

mdingi nae pia ana jukumu la kuilea familia yake.

0
0
Mkazi mmoja wa kijiji cha Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma akiwajibika kifamilia kama uonavyo pichani,pamoja na Wababa wengi wanadai kuwa na majukumu mengi ya kikazi,lakini bado ana nafasi kubwa ya kuilea na kuijenga familia yake katika mapenzi bora kabisa.

eneo la kwanza kutambulika kimataifa lipo mkoani kigoma

0
0

Watoto wakishangaa jambo .

0
0


haina kushangaa hiyo,na mzigo unafika.!

0
0

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AFUNGUA MKUTANO WA KANDA, WA MASHAURIANO WA BARAZA LA VIJANA WA JUMUIYA YA MADOLA.

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifungua Mkutano  wa  Mashauriano wa Kanda wa  Baraza la Vijana wa Jumuiya ya Madola uliofunguliwa leo Januari 29, 2013 katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara, akizungumza wakati wa Mkutano  wa  Mashauriano wa Kanda wa  Baraza la Vijana wa Jumuiya ya Madola uliofunguliwa leo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiteta jambo na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel, wakati wa ufunguzi wa Mkutano  wa  Mashauriano wa Kanda wa  Baraza la Vijana wa Jumuiya ya Madola uliofunguliwa leo, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Dkt. Mohammed Gharib Bila, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo leo, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Dkt. Mohammed Gharib Bila, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo leo, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Dkt. Mohammed Gharib Bila, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo leo, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo, wanaowakilisha makundi mbalimbali ya vijana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo, wanaowakilisha makundi mbalimbali ya vijana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo, wanaowakilisha makundi mbalimbali ya vijana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mkurugenzi wa Maendelea ya Vijana wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel, baada ya kufungua mkutano wa  Mashauriano wa Kanda wa  Baraza la Vijana wa Jumuiya ya Madola uliofunguliwa leo, katika Hoteli ya White Sands  jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Fenella Mukangara.  .Picha zote na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

UNIC YASHIRIKISHA VIJANA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA WAHANGA WA MAUAJI YA KIMBARI YA HOLOCAUST

0
0

Afisa Habari Ngazi ya Taifa wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkoma akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon katika Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka wahanga wa Mauaji ya Kimbari ya Holocaust kwa vijana wanafunzi wa shule za sekondari na baadhi ya vyuo. Amesema katika siku hii ya kimataifa, tuwakumbuke watu wote wasio na hatia ambao walipoteza maisha wakati mauaji ya kimbari ya Holocaust.

Ameongeza kuwa vilevile tuhamasishe na wale ambao walikuwa na ujasiri wa kujali watu wa kawaida ambao walichukua hatua zisizo za kawaida kulinda heshima ya binadamu. Mfano wao unaweza kutusaidia sisi kujenga dunia bora zaidi leo. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Uokoaji wakati wa Mauaji ya Kimbari: Ujasiri wa Kujali”.

Pichani Juu na Chini ni baadhi ya Wanafunzi wa shule za sekondari na vyuo wakimsikiliza kwa makini Bi. Usia Nkoma (hayupo pichani) alipokuwa akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wakati wa Siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka wahanga wa Mauaji ya Kimbari ya Holocaust iliyofanyika jijini Dar leo katika ukumbi wa British Council.

Wanafunzi wa shule za Sekondari, vyuo na wafanyakazi wa UN wakifuatilia Filamu 'The Rescuers' inayosimulia kwa undani kuhusiana na stori zinazowahusu wanadiplomasia 13 waliofanya vitendo vya kishujaa na kijasiri ambao waliowaokoa maelfu ya Wayahudi wakati wa vita vya pili vya Dunia. Filamu hiyo imetengenezwa na mtayarishaji wa filamu maarufu na mshindi wa tuzo EMMY Michael King.



Mjumbe wa Chama cha Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA) Bernadetha Mshana akisoma shairi lenye ujumbe wa kupiga vita mauaji na kuhamasisha vijana kudumisha amani.

Burudani ya ngoma za asili.

Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo akiendesha mjadala na wanafunzi wa shule mbalimbali za sekondari kutoka katika vilabu vya UN kuhusiana na siku ya kimataifa ya kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya kimbari ya Holocaust baada ya kutazama filamu iliyokuwa ikielezea mauaji hayo inayoitwa “ The Rescuers” iliyotengenezwa na mtengenezaji filamu maarufu Michael King.

Dakika moja ya ukimya: kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya Kimbari ya Holocaust.

Baadhi ya vijana wa UN Clubs wakimsikiliza kwa makini Bi. Stella Vuzo.

Pichani Juu na Chini Wanafunzi wakitoa maoni yao baada ya kutazama filamu hiyo wakati wa Mjadala ulioendesha na Afisa Habari wa ngazi ya kimataifa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi Stella Vuzo (hayupo pichani).

Bi. Usia Nkoma akitoa neno la shukrani kwa washiriki.

WAJASIRIAMALI WALIVYONUFAIKA NA SAFARI LAGER WEZESHWA

0
0
 Mjasiriamali Elizabeth Chami (26), akioka keki kwenye jiko la kisasa alilozawadiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia promosheni ya Safari Lager Wezeshwa 2012, kwenye karakana yake iliyopo Tabata Mawenzi, Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

 Elizabeth akikata lebal  ya kampuni yake tayari kubandika kwenye kasha la keki
 Mfanyakazi wa karakana hiyo, Happiness akiweka akioka keki kwenye jiko hilo la kisasa. 
 Mfanyakazi wa Kiwanda cha kutangeneza Shampoo  cha L & V Intergrated Firm, kilichopo Mikocheni, Dar es Salaam, Hashim Hussein akifungasha katoni za bidhaa hiyo. Kiwanda hicho kilisaidiwa chupa 15,000 baada ya mmiliki wa kiwanda hicho Valerian Luzangi (hayupo pichani) kuwa mmoja wa washindi wa promosheni  ya Safari Lager Wezeshwa 2012.
 Luzangi akisaidia kupanga vizuri chupa zilizojazwa shampoo. Kushoto ni mfanyakazi wa kiwanda hicho Stahabu Mwinyi.
 Mjasiriamali Valerian Luzangi (38), kulia, akipanga vizuri katoni za shampoo anazozalisha katika kiwanda chake cha L & V Intergrated Firm, kilichopo Mikocheni, Dar es Salaam juzi. Luzangi alisaidiwa chupa 15,000 baada ya kuwa mmoja wa washindi wa promosheni  ya Safari Lager Wezeshwa 2012, Kushoto ni mfanyakazi wake, Hashim Hussein. 
 Wajasiriamali Innocent Mberwa (kulia) na Gosbert Mugisha wakiwa sawa mfumo wa umwagiliaji katika moja ya mashamba  zao la matikiti maji ya Kampuni yao ya  Tin Wax eneo la Minondo, Kata ya Somangila, Kigamboni, Dar es Salaam juzi. Kampuni hiyo ilizawadiwa mfumo huo baada ya kushinda promosheni  ya Safari Lager Wezeshwa 2012,
 Mjasiriamali Innocent Mberwa akionesha tikiti maji katika moja ya mashamba ya Kampuni yao ya  Tin Wax yaliyopo eneo la Minondo, Kata ya Somangila, Kigamboni, Dar es Salaam juzi. Kampuni hiyo ilizawadiwa mfumo wa maji wa umwagiliaji baada ya kushinda promosheni  ya Safari Lager Wezeshwa 2012,
Wajasiriamali Innocent Mberwa (kulia) na Gosbert Mugisha wakiwa sawa mfumo wa umwagiliaji katika moja ya mashamba  zao la matikiti maji ya Kampuni yao ya  Tin Wax eneo la Minondo, Kata ya Somangila, Kigamboni, Dar es Salaam juzi. Kampuni hiyo ilizawadiwa mfumo huo baada ya kushinda promosheni  ya Safari Lager Wezeshwa 2012,
Baadhi ya vitunguu vinavyozalishwa katika shamba hilo. (PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG)

KINANA ATINGA WILAYANI KAKONKO MKOANI KIGOMA, APOKEWA NA DIWANI WA CHADEMA KATA YA KASANDA

0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwalisha kiapo cha utii Wanachama wapya 45 wa CCM mara baada ya kuwapa kadi za chama hicho kwenye mkutano uliofanyika Kata ya Kasanda, Kakonko mkoani Kigoma

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi ya CCM mwanachama mpya, Elizabeth Gwimo, alipokwa wanachama wapya 45, katika mkutano uliofanyika Kata ya Kasanda, Kakonko Kigoma


Wanachi wakishangilia jambo kwa pamoja
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi kwenye mkutano uliofanyika Kata ya Kasanda, Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na mabalozi wa mashina na wazee katika Kata ya Kasanda, Kakonko mkoa wa Kigoma.


Diwani wa kata ya Kasanda, Kakonko mkoani Kigoma, Dickson Barutwa (CHADEMA), akimpa maelezo ,Ndugu Kinana kuhusu ujenzi wa nyumba za zahanati ya kata hiyo unaofanywa na serikali.



zahanati ya kata ya Kasanda iliyojengwa na Serikali. 


Kinana akisalimiana na Wauguzi wa zahati hiyo ya Kasanda.


Kinana akipata maelezo  kwa Dc Kakonko, Peter Toima wakati akikagua mradi wa ujenzi nyumba za zahanati ya Kata ya Kasanda wilayani humo. Kulia ni diwani wa Kata hiyo Dickson Barutwa. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Kibondo,  Dk. Laurean Kanaganwa(kulia) akitoa maelezo ya zahanati ya kata ya Kasanda. Wapili kulia ni diwani wa Kasanda-Chadema, Dickson Barutwa 



Mjumbe wa Shina, Agnes Lukwavi akitoa maoni yake ya kuboresha C CM, wakati Kinana alipozungumza na mabalozi na wazee wa Kata ya Kasanda, wilayani Kakonko, Kigoma
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images