Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

Uzinduzi Wa Tawi Jipya Benki Ya Exim: BOT Yaipongeza Exim Kwa Ukuaji.

$
0
0
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imeipongeza benki ya Exim Tanzania kwa jitihada na mafanikio inayoyapata katika kujitanua ndani na nje ya nchi huku ikitoa wito kwa benki hiyo kuhakikisha inawekeza zaidi katika kutoa huduma maalumu na zenye ubunifu kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati ili waongeze nguvu katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse wakati akifungua rasmi tawi jipya la benki ya Exim Tanzania lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam ikiwa ni baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania. Katika uzinduzi huo, Dk Kibesse alimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango.

“Ni fahari kwetu kuona benki ya kizalendo inafanya mambo makubwa kama haya. Mmekuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa mabenki hapa nchini jinsi inavyojizatiti kujiimarisha ndani na nje ya mipaka ya nchi.Hatua hii ni sawa na kuitikia kilio cha wadau wa huduma za kifedha hapa nchini wanaohitaji huduma zinazokidhi mahitaji yao pia huduma zinazolingana na zile za kimataifa na kwenye mazingira yaliyobereshwa.’’ Alisema.

Alitoa wito kwa benki hiyo kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara wadogo na wa kati ili waweze kuongeza nguvu katika kuleta mabadiliko ya kiuchumi nchini ili kulisaidia taifa kufikia malengo yake ambayo ni pamoja na kufikia pato la kati ifikapo mwaka 2025.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu alisema hatua hiyo inakwenda sambamba na msimamo wa Rais Dk John Magufuli ambae amekuwa akisisitiza juu ya umuhimu wa kuwa na benki kubwa zaidi na ndogo nchini kwa kuwa ni hatua muhimu kwa afya ya kifedha katika ukuaji wa uchumi hususani katika kutoa huduma kamili na zenye ubunifu kwa wateja.

“Aidha ufunguzi wa matawi mapya kama hili utasaidia kuimarisha uwepo wa Benki ya Exim kiushindani katika maeneo mbalimbali ili kutoa kwa urahisi huduma zetu kwa wakazi na wamiliki wa biashara wa maeneo haya’’

"Tunafurahi kuwakaribisha wateja wa Benki ya UBL, wafanyakazi na jamii yote ya UBL kwenye familia ya Benki ya Exim. Hatua hii si tu inaongeza uwepo wetu kwenye soko kubwa bali pia inatuongezea timu kubwa ya wafanyakazi wenye weledi katika masuala ya kibenki,’’ alisema.

Alisema Dar es salaam ni soko muhimu kwa Benki ya Exim na tawi hilo jipya la Mkwepu limeambatana na matumzi ya teknolojia mpya na muundo ambao utawasaidia wateja wa benki hiyo kuwasiliana na maafisa wa benki hiyo kwa njia inayowafaa na katika mazingira ambayo ni bora na salama zaidi.

Akielezea mpango wa benki hiyo Bwana Matundu alisema kuwa wanalenga kutoa kasi ya juu katika suala la utoaji huduma ili kuhakikisha kuwa wateja wanapata huduma haraka na zisizo na usumbufu kwa kuzingatia mahitaji ya wateja na hali ya soko.

Ikiwa na jumla ya matawi 33 kwasasa Benki ya Exim Tanzania ni moja wapo ya benki kubwa nchini. Katika kipindi kifupi cha zaidi ya miaka 22 ya uwepo wake benki hiyo imetoa huduma za kifedha kwa wateja wa wadogo, wa kati na wakubwa.


Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse (Kulia) akijipongeza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu (Kushoto) wakati akifungua rasmi tawi jipya la benki ya Exim Tanzania lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania. Wengine ni pamoja na maafisa waandamizi wa benki hiyo, wateja na wageni waalikwa.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse (Kulia) akipongeza na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu (Kushoto) wakati akifungua rasmi tawi jipya la benki ya Exim Tanzania lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse akzungumza wakati wa hafla hiyo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu (katikati) akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Huduma ya Rejareja wa benki ya Exim, Bw. Andrew Lyimo akizungumza kwenye hafla hiyo.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse (wa nne kulia) pamoja na na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu (katikati) wakiwa kwenye picha ya pamoja na maafisa waandamizi wa benki ya Exim, wateja na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.

Vodacom yakutanisha Wadau kujadili ustawi wa huduma ya pesa kwa njia ya simu ya mkononi Afrika

$
0
0
Mkurugenzi wa M-Pesa Ltd, Epimack Mbeteni akizungumza kwenye kongamano hilo 
Mwakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania Albert Cesari (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Mkurugenzi mkuu wa Vodacom Tanzania Plc, Hisham Hendi (wa kwanza kulia), Mtendaji mkuu, Sheria na Udhibiti kutoka Vodacom Group, Judith Obholzer (wa kwanza kushoto) na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano, Rosalynn Mworia wakati wa kongamano na uzinduzi wa ripoti kuhusu kuhakikisha ukuaji wa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi jijini Dar Es Salaam.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Rosalynn Mworia (kulia) na Mtendaji mkuu, Sheria na Udhibiti kutoka Vodacom Group, Judith Obholzer (katikati) wakizungumza na mdau wa huduma za kifedha aliyehudhuria kongamano hilo.

*************************************

Novemba 19, 2019, Dar es Salaam. Wawakilishi kutoka zaidi ya nchi 8 Afrika wanakutana leo katika kongamano maalumu lililoandaliwa na Vodacom kujadili mwenendo na maendeleo kwaajili ya kuboresha sekta ya huduma ya pesa kwa njia ya simu ya mkononi Afrika. Kampuni hiyo inayoongoza kwa teknolojia ya mawasiliano pia imetoa ripoti yake ya kuhakikisha ukuaji wa Huduma
za Kifedha kupitia simu za mkononi katika kongamano hilo.

Ripoti hiyo ambayo ni ya kwanza ya Mwendelezo wa Sera ya Umma kwa Vodacom, inafafanua jinsi ambayo huduma ya pesa kwa simu ya mkononi inayoendesha ukuaji wa uchumi na kuinua kiwango
cha maisha kupitia huduma ya kifedha.

Mkurugenzi Mtendaji, Sheria na Udhibiti wa Vodacom Group, Judith Obholzer, alisema Nchi za Afrika zilizoko Kusini Mwa Jangwa la Sahara ikiwamo Tanzania zimeshuhudia ukuaji wa haraka katika huduma za pesa kupitia simu ya mkononi, sambamba na uvumbuzi na kuwezesha ushiriki mpana wa utoaji wa huduma za kifedha.

Kusini mwa Jangwa la Sahara ni kinara ambapo watu wazima wengi wanamiliki akaunti za simu ya mkononi kuliko zile za taasisi za kifedha. Mabadiliko haya katika ukanda huo yanazidi kuendesha kukua kwa uchumi na faida za kijamii kwa kutoa huduma za kifedha kwa mamilioni ya watu wanaomiliki simu ya mkononi, lakini pia wakiwa umiliki mdogo sana wa akauti za benki.

“Lengo letu ni kutoa jukwaa kwa wataalamu wa sekta hii kutoa maoni yao jinsi ya kuboresha sekta.Sekta hii inaendelea kukua kwa kasi, watunga sera pamoja na wasimamizi wana jukumu la kuweka mazingira ya biashara hii ya kifedha,” alisema Obholzer.

Mwakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania ambaye ni Meneja Msaidizi katika idara ya Mifumo ya Malipo ya Taifa, Bwana Albert Cesari alieleza umuhimu wa huduma za kifedha zinazotolewa na makampuni za simu katika utowaji wa fursa pamoja na ajira na ukuwaji wa uchumi.

“ Serikali imeweka mazingira bora na endelevu kuhakikisha huduma za kifedha zinaendelea kuleta mabadiliko chanya ya kiuchumi ikiwemo ajira na mabadiliko katika mfumo wa ulipiaji huduma nchini. Kanuni za malipo ya simu kupitia simu ya mkononi hutolewa ili kuongoza soko bila kuzuia ubunifu au kukwaza mafanikio ambayo yanaletwa na wavumbuzi hawa.”

M-Pesa imekuwa moja ya huduma bora zaidi ya pesa ya simu ya mkononi barani Afrika. Tafiti zinaonesha kwamba huduma ya pesa kupitia simu ya mkononi imechangia kwa kiasi kikubwa katika uwezeshaji wa jamii, kukua kwa uchumi na kupunguza umasikini.

Inatoa huduma kwa njia salama, Uhakika na ya bei nafuu kwa kutuma na kupokea pesa, kuongeza muda wa maongezi, kufanya malipo ya bili, kupokea mishahara na kupata mkopo wa muda mfupi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa utafiti mpya juu ya matumizi ya huduma ya pesa kupitia simu ya mkononi Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi, alisema “ Huduma ya pesa kwa simu ya mkononi imeongezwa nguvu matumizi ya simu ya mkononi, imeonekana kuwa kama jukwaa la kutoa fursa kiuchumi na kubadlisha mazingira ya huduma za kifedha na hasa katikabara la Africa,”

Hendi aliongeza kusema kuwa, “Nimefurahi kwamba ripoti hii inaleta pamoja michango ya wataalam wanaoongoza na ndio wazungumzaji katika mada hizi tatu pana. Wana maoni na mitizamo tofauti, ili kuleta msukumo wenye tija na wa kujenga.”

Hafla hiyo iliwashirikisha wawakilishi kutoka kwa waendeshaji wa mitandao ya simu wakiwamo wadau wa mawasiliano, watoa huduma za kifedha, benki, Asasi za Kiraia na washiriki wengine walioshiriki kuchangia mada mbalimbali kama vile; Uthibitisho wa baadaye wa Uwepo wa Huduma za Kifedha za simu ya Mkononi, Mfumo wa Ushirikiano, Mfumo wa Malipo, Ushirikiano wa kikanda
na fursa za mipaka, Jinsi ya kutatua matatizo ya kisheria, Tabia ya kupeana mawazo na fursa za ushindani.

MKAZI WA IRINGA ASHINDA KITITA CHA MILIONI 393 za M-Bet,

$
0
0
Mkazi wa mkoa wa Iringa, Salvatory Kambaulaya amejishindia kitita cha Sh 393,200,750 baada ya kubashiri kiusahihi mechi 12 za mchezo wa Perfect 12 unaondeshwa na kampuni ya M-bet Tanzania.

Kambaulaya ambaye ni shabiki wa Simba na Manchester City alisema kuwa hakuwa na wasiwasi mara baada ya kupigiwa simu na Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet, Allen Mushi kuwa ni mshindi wa fedha hizo.

“Niliamini kuwa ni mshindi kwani mimi siyo mtu wa kwanza kushinda droo ya Perfect 12 ya M-Bet kutoka mkoa wa iringa, kuna mwanafunzi alishinda na kupatiwa fedha zake,

“Niamini M-Bet kwa kuwa na washindi wa uhakika katika michezo yao, ndiyo maana nilicheza ‘mikeka’ saba, mmoja nikipatia mechi tisa na mwingine mechi 12,” alisema Kambaulaya. Alisema kuwa kiasi cha fedha alichoshinda ni kikubwa sana na anatakiwa kutuliza akili ili kujua nini anafanya kwa upande wa maendeleo.

“Nimeshinda zawadi ya kwanza, lakini nimeumia sana na matokeo kati ya timu yangu, Manchester City ilipofungwa na Liverpool, niliweka Manchester kuwa ni washindi, hata hivyo alifungwa mchezo huo. Meneja Masoko wa M-Bet Tanzania, Allen Mushi alisema kuwa Kambaulaya ambaye ni afisa polisi mkoani Iringa ataweza kubadili maisha yake kupitia mchezo wao wa Perfect 12.

Mushi alisema kuwa M-Bet itaendelea kuwa nyumba ya mabingwa ambao wamefaidika na msemu huo tokea kuanza kwa ubashiri. “Tumetoa washindi wengi mpaka sasa ambao wamejishindia mamilioni ya fedha na kuweza kubadili maisha yao ya kila siku,” alisema Mushi.
 Mshindi wa Sh milioni 393 wa mchezo wa kubashiri wa Perfect 12 wa kampuni ya M-Bet Tanzania, Salvatory Kambaulaya ( wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Meneja Masoko wa kampuni ya M-Bet Tanzania Allen Mushi (wa pili kushoto) mara baada ya kukabibidhiwa mfano wa hundi kwa kushinda kitita hicho cha fedha. Wengine katika picha ni Chiku Saleh kutoka bodi ya michezo ya kubashiri na Kulia ni Shabani Mwanga, Mkuu wa Kitengo cha Kodi za Michezo ya Kubahatisha (TRA), mkoa wa kodi wa Ilala.

Rais Magufuli ateua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa TMA

BENKI YA TPB YAMWAGA VIFAA SHULE MBILI ZA SEKONDARI MBILI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania(TPB) Sabasaba Moshingi wa tatu kushoto akikabidhi moja kati ya meza 100 na viti 100 vyenye thamani ya shilingi Ml 4.8 kwa Mkuu wa wilaya ya Mbinga Cosmas Nshenye kwa ajili ya shule mbili za Sekondari za Mbambi na Makita zilizopo Halmashauri ya Mji Mbinga mkoani Ruvuma,kushoto Afisa mahusiano wa Benki hiyo Novas Moses. 
****************
BENKI ya Posta Tanzania(TPB) imetoa msaada wa meza 100 na viti 100 vyenye thamani ya shilingi Ml 4.8  kwa shule mbili za Sekondari za Mbambi na Makita zilizopo katika Halmashauri ya Mji Mbinga mkoani Ruvuma.

Akikabidhi samani hizo za Shule,Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Sabasaba Moshingi alisema, Benki hiyo imekuwa na utaratibu wa kutenga kiasi fulani cha fedha  kila mwaka na kusaidia jamii hasa katika sekta ya Elimu katika mikoa mbalimbali hapa Nchini.

Alisema,  mwaka wa fedha 2019 Benki ya Posta imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya kuchangia huduma za jamii na itaendelea kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazo fanywa wananchi na Serikali.

Moshingi alisema, Benki ya Posta Tanzania inajivunia sana kuona imekuwa sehemu ya mafanikio katika sekta  ya Elimu hapa Nchini  na sio mara ya kwanza kuchangia sekta ya elimu kwani mwaka jana ilitumia kiasi cha shilingi milioni 50 kukarabati shule ya Msingi Kindimba iliyopo katika wilaya hiyo.

Amewataka wanafunzi wa shule hizo, kuhakikisha  wanatumia meza na viti hivyo kusoma kwa bidi na kujiepusha na mambo yanayoweza kukatisha safari yao ya maisha na kuwataka Watanzania wengine kuunga mkono juhudi zinazo fanywa na Benki ya Posta na Serikali ya awamu ya tano ya kumarisha miundombinu ya Shule.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya hiyo Cosmas Nshenye,amewataka wakazi wa  Mbinga  kuwa wazalendo, na wenye mapenzi mema kwa  kumaliza baadhi ya changamoto zinazoikabili wilaya hiyo badala ya kutegemea misaada ya Serikali na wafadhili.

 Nshenye ametoa kauli hiyo jana wakati akiongea na wanafunzi,walimu na baadhi ya wananchi katika hafla ya kupokea msaada wa viti 100 na meza 100 zilizotolewa na Benki ya Posta Tanzania kwa shule mbili za  Sekondari za Mbambi na Makita wilayani humo.

Alisema, sio  jambo la kufurahisha na haipendezi hata kidogo kwa jamii  ya wana Mbinga kuona wanashindwa  kuchangia ujenzi wa miradi na huduma mbalimbali za kijamii, kwani wana uwezo mkubwa wa kifedha,lakini inasikitisha kuona  kazi kubwa ya kuijenga wilaya hiyo imeachwa kwa Serikali na wadau wengine wa maendeleo.

Nshenye alisema, wakati umefika kwa wakazi wa wilaya ya Mbinga kubadilika na kujitolea nguvu kwa kuchangia  ujenzi wa miradi  ikiwemo miundombinu ya Elimu,Afya,Maji na mingineyo hatua itakayochochea na kuharakisha maendeleo ya Nchi yetu.

Kwa mujibu wake,ni aibu wilaya kama ya Mbinga ambayo wananchi wake wana nguvu kubwa ya kiuchumi inayotokana na zao maarufu la kahawa bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa madawati,viti na meza huku baadhi ya wanafunzi wa shule wakilazimika kubeba viti kutoka nyumbani kwao.

Aidha Mkuu wa wilaya ameishukuru Benki ya Posta kwa msaada wa viti na meza ambazo zinakwenda kupunguza  mahitaji ya samani  kwa shule hizo mbili, ambapo ameyataka makampuni mengine kuiga mfano wa Benki hiyo ambayo imekuwa msaada mkubwa katika kuchangia miundombinu ya shule kwa wilaya ya Mbinga.

Amewataka wanafunzi  kutumia meza na viti hivyo  kusoma kwa bidii, hali itakayowasaidia kufikia malengo waliyojiwekea katika safari yao ya maisha nan a viti na meza hizo wazitumie kama chachu ya mafanikio.

Awali Mkuu wa shule ya Makita Wilson Msengi alisema, shule hiyo ina upungufu wa viti 62 na meza 58,lakini msaada huo  uliotolewa na Benki ya Posta utapunguza sana changamoto hiyo.

Alisema,samani hizo zinakwenda kuhamasisha suala zima la kujifunzia na kufundishia darasani na pia kuchochea taaluma kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Heri ya Siku Ya Mtoto Duniani kutoka Benki ya NMB

$
0
0

 Heri ya #SikuYaMtotoDuniani

Katika kuadhimisha #SikuYaMtotoDuniani, jengo letu la Benki ya NMB Makao Makuu liliwasha taa za bluu kuunga mkono Shirika la uniceftanzania katika maadhimisho ya kumbukizi ya miaka 30 ya Mkataba juu ya Haki za Mtoto

Ni wakati wa kuwaunga mkono na kuwawezesha watoto na vijana ambao wanasimamia na kudai haki zao kote Ulimwenguni ni sasa.

#KwaKilaMtoto, Kil haki inatimizwa!

TCRA Kanda ya Mashariki yaendelea kutoa elimu Mkoa wa Morogoro

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Morogoro

Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Lawi Odiero  amesema kuwa Wananchi wote watasajili laini za simu kwa alama za vidole kutokana na jitihada walizoweka kwa kushirikiana na wadau katika kufanikisha usajili huo.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro, Odiero amesema zoezi la elimu pamoja na usajili wa laini za simu kwa alama za vidole linafanyika katika mkoa wote wa Morogoro kwa kupita kila Kata.

Amesema katika utoaji wa elimu wanashirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA),Watoa Huduma wa Kampuni za Simu za Mkononi ,Wakala wa Usajili wa Vifo na Vizazi (RITA) kwa kupata Wananchi huduma kwa pamoja.

Amesema Wananchi watumie muda wao kutafuta viambatanisho vinavyohitajika kwa wadau wengine ili waweze kusajili laini zao kwa alama za vidole.Katika utoaji elimu hiyo wamepita katika vituo vya radio vya Mkoa wa Morogoro kutoa elimu hiyo watu kujitokeza kusajili laini za simu kwa alama za vidole.

Aidha amesema utoaji elimu unakwenda katika mikoa yote iliyopo katika kanda ya Mashariki ambapo zoezi hilo lilishamalizika katika Mkoa wa Pwani na kutaka Wananchi wa Mkoa huo ambao hawana vitambulisho vya Taifa kufanya utaratibu wa kupata katika Ofisi za NIDA ili waweze kusajiliwa.
Kwa upande mwananchi Amina Salumu wa Manispaa ya Morogoro amesema TCRA wamefanya vizuri kuhamasisha kwa kuungana na watoa huduma wote  katika usajili wa laini za simu kwa alama za vidole.

Aidha amesema kuwa tatizo lingine ni wao Wananchi kushindwa kufuata taratibu za kuweza kupata vitambulisho kwa wakati kwa kizingizio cha majukumu yao.

Salumu ameshauri kuwa zoezi hilo lifanyike mara kwa mara ili wote waweze kujisajiliwa wasisubiri laini zifungwe ndipo waanze kuhangaika.
Wananchi wakipata huduma ya usajili wa laini za simu kwa alama za vidole katika Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro.
 Mwananchi akisubiri kupewa namba ya kitambulisho cha Taifa kwa kuangalia mfumo aliyessjiliwa na NIDA.
 Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Lawi Odiero aliyesimama akiangalia kazi data waliosajiliwa na Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa ajili ya Namba waweze kujisajili laini za simu kwa alama za vidole katika utoaji wa elimu katika Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro.
 Wananchi wakisajili laini za simu kwa alama za vidole kwa watoa huduma wa Kampuni za Simu katika utoaji elimu  Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro.
Afisa wa TCRA Kanda ya Mashariki Vaoleth Esseko akimkabidhi kitabu Cha mkataba kwa Wateja Cha TCRA wakati utoaji elimu Kata ya Lukobe Manispaa ya Morogoro.

Man Mo: Msanii aliyeingia kanisani ili atoke kimuziki

$
0
0
*Familia yake ikamkalia kooni
*Sasa achomoka na 'Mapenzi Kazi'

HAKUNA jambo lolote linaloanza kwa utelezi hapa duniani. Kila kazi ina changamoto na msoto wake. Na katika kupitia changamoto hizo, baadhi yao wanafikia kukata tamaa kabisa, licha ya kuwa na kila kitu kinachoweza kuwapatia mwangaza katika mambo wanayopigania.

Hata katika sanaa ya muziki wa kizazi kipya tunachoshuhudia vijana wengi wakichanua na kujimudu kiuchumi, pia una suluba na changamoto lukuki, msoto mzito unaowakumba wasanii wengi tangu siku walipoamua kujiingiza kwenye tasnia hiyo.

Katika kuangalia vijana hao wanaopitia katika msoto mzito ni Maneno Mohamed 'Man Mo'. Kijana huyu mwenye uwezo wa juu wa kuimba na kutunga nyimbo za muziki wa kizazi kipya, anapitia katika tanuri la moto, barabara yenye miba mikali kiasi cha kuwahi kukata tamaa ya kuendelea na sanaa yake.

Ndio, hii ni kwa sababu msanii huyo licha ya kuwa kwenye sanaa kwa muda mrefu sasa, lakini mlango wa mafanikio ulionekana kuchelewa kufunguka, licha ya kuwa na kipaji cha uimbaji na utunzi wa nyimbo kali, ukiwamo wimbo wa 'Nasimama' ulioimbwa na msanii nyota Judith Wambura 'Lady JayDee', ambao uliandikwa na Man Mo.

Katika mazungumzo na Gazeti hili, Man Mo anasema kwamba alianza kujihusisha na muziki tangu alipokuwa mdogo, akimfuatilia mama yake Bi Salama Mussa Kaduga, aliyekuwa anajihusisha na sanaa katika Matukio mbalimbali haswa ya kisiasa, huko kijijini kwao Kimange, mkoani Pwani.

"Muda mwingi nilikuwa namfuatilia mama yangu katika sanaa yake, jambo ambalo lilichochea kwa kiasi kikubwa mimi kupalilia kipaji changu cha kimuziki na kuweka nia kubwa ya kuja kuwa msanii nyota duniani kama wengine.

"Pamoja na mambo mengine, msanii mwingine ambaye kwa namna moja ama nyingine aliendelea kukuza kipaji changu ni Ali Kiba, ambaye muziki wake niliuelewa, haswa nilipofanikiwa kukutana naye katika studio za Sharobaro Records za jijini Dar es Salaam zilizokuja kuvuma kwa kutoa wasanii wengi mahiri, akiwamo Bob Junior, Diamond Platnumz, Shetta, Rich Mavoco na wengineo kibao ambao mara kwa mara walikuwa wakikutana kwenye studio hizo,"Alisema Man Mo.

Msanii huyo mwenye kiu kubwa kisanaa anasema rasmi kuingia kwenye sanaa ilikuwa ni mwaka 2010 ambapo kama vijana wengine, aliamua kuondoka kijijini kwao na kuvamia jiji la Dar es Salaam, akiwa na matarajio makubwa ya kuvuna kwa kupitia muziki wa kizazi kipya.

Kwa bahati mbaya jiji lilimlaki vibaya na kumchoma na jua tangu alipofika na kuamua kukimbilia kwenye kiwanda Cha nguo Cha Urafiki ili apunguze makali ya kimaisha kwa kufanya kibarua katika kitengo cha kuchambua nyuzi.
 
Mkali huyo wa kizazi kipya anasema licha ya kufanya kibarua Urafiki, lakini hamu ya kimuziki ilikuwa kubwa na kujikuta akienda Sharobaro kurekodi wimbo wake kwa pesa yake, hata hivyo baadae uongozi wa Studio hizo ulimpa ahueni kwa kumtaka awe chini ya Sharobaro Records ili akue kimuziki. 
 
Hata hivyo anakiri uamuzi huo pia ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na bidii yake pamoja na kujituma kwa kila aina ikiwamo kufanya usafi kwenye studio hizo, akitafuta upenyo wa kuchomoka kisanaa.

"Nikiwa Sharobaro Records nilifanikiwa kurekodi nyimbo nyingi na kupata marafiki wengi ambao naweza kusema nilikua kwa kiasi kikubwa mno kulinganisha na wakati ule natokea kwetu kijijini nikiwa sina mtandao wowote kisanaa na hata kula yangu ikawa ni mashaka matupu.

"Nyimbo ambazo nilitengeneza wakati ule ni Binti wa Kibara, Binti wa Kimasai na nyingine nyingi ambazo hazikuachiwa hewani bila kusahau zile nilizoandikia wasanii wengine ukiwamo ule wa dada yangu Lady JayDee uliojulikana kama Nasimama ambao ulifanya vizuri mno katika ulingo wa Bongo Fleva,"Alisema.

Wakati anaamini anaelekea pazuri, ghafla mambo yalibadilika na kurudi tena kwenye msoto ambapo kila alilopanga lilishindwa kutimia, ikiwamo kuwapata mameneja ambao bila wao ni ngumu msanii kutokea peupe. Anasema wakati anaelekea kuchoka, akapata meneja aliyempa sharti la kuimba muziki wa injili na sio muziki wa kidunia.

"Huyu ndugu yangu alikuwa anaitwa James Albert Katagira anayemiliki shule za Tusiime, ambaye alinionea huruma na msoto wangu na kunishawishi nihamie kwenye injili ili anisimamie jambo ambalo nililitekeleza haraka, kwa sababu lengo langu lilikuwa ni sanaa.

"Nilifanikiwa kurekodi nyimbo mbili na video zake ambazo ni Jicho Langu na Nimuimbie, ambazo zilifanya vizuri katika muziki wa injili na kuanza kupata shoo nyingi katika mikoa mbalimbali kwa kuunganishwa na wasanii wengi wa muziki huo bila kusahau kushiriki makongamano mengi ya kidini,"Alisema.

Man Mo anasema muziki huo ulikuwa unampa mwelekeo mzuri, licha ya kufikia kutengwa na familia yake kwa madai alitokea katika chimbuko la waumini wa dini ya Kiislamu, hivyo jamii ilishindwa kumuelewa, wakiwamo marafiki zake waliomkosoa kwa kitendo chake cha kuacha Bongo Fleva na kukimbilia injili.

Ili jamii imuelewe akiwamo mama yake mzazi, alitumia muda mwingi kuzungumza nao, huku akikiri kuwa aliingia kanisani na kuimba injili kama njia ya kumfikisha kileleni na sio nia ya kubadili dini, ingawa anasema katika kipindi chote hicho, jamii ya kikristo na wasanii hao wameishi kwa upendo na kushirikiana kwa kiasi kikubwa, akiwamo Madame Frola ambaye alishiriki naye katika matamasha kadhaa likiwamo la Tanga Mjini akiwa kama mwimbaji wa injili.

Man Mo anasema msoto haukumuacha, kwani msaada wake uligota, hivyo kuamua kuachana kabisa na muziki, akiingia katika biashara ya kilimo pamoja na kuuza kuku, biashara ambazo zilitokana na umri kuendelea kumtupa mkono huku akishindwa kutokea peupe.

Kijana huyo mwenye ndoto na maneno mengi mdomoni mwake anasema baada ya kukaa kwa miezi kadhaa bila kujihusisha na lolote linalohusu muziki, alishtushwa na simu kutoka kwa Belo Master, aliyekuwa anafanya wimbo kwenye Studio za classic Sound chini ya mtayarishaji wake Monagenster za Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
"Wakati ananipigia simu, sikuwa na ari, lakini kwakuwa jamaa anajua uwezo wangu na alitaka nikamuimbie kiitikio, hivyo nikaenda Studio kurekodi kama alivyotaka, jambo ambalo lilianza upya kunitekenya rohoni mwangu. 

"Kwakuwa niliimba vizuri kwenye wimbo ule, viongozi wa Monagenster walivutiwa na mimi na kunivuta karibu ili waendelee kuangalia uwezo wangu ambapo walinikubali zaidi haswa kwa uwezo wangu wa kuandika nyimbo kali, ukizingatia wengi nilikuwa nawatungia, hivyo kupata upenyo rasmi,"Alisema.

Kijana huyo anasema kwa Sasa anasimamiwa kazi zake chini ya Kampuni ya African Network Entertainment (ANE) kwa kushirikiana na Monagenster kwa kupitia classic Sound ambapo hadi sasa nimeachia nyimbo mbili kali pamoja na video matata ambazo ni 'Tike na Mapenzi Kazi zinazofanya vizuri katika ulimwengu wa muziki.

Msanii huyo anayetokea kwenye familia ya watoto wanne, huku yeye akiwa wa kwanza kuzaliwa mwaka 1994 huko Kimange, anawataja wadogo zake kuwa ni Mwahija, Sauda na Muhsin huku kiwango chake cha elimu kikiwa ni kidato cha nne, akiishia kiwango hicho kutokana na kuhangaikia muziki licha ya baba yake kutamani mtoto wake asome sana, aliishia njiani.

Man Mo alisoma elimu ya msingi katika shule mbili za Kimange na Bagamoyo, wakati elimu ya Sekondari aliipata katika shule ya Air wing ya Banana, jijini Dar es Salaam, huku akisema kuwa maisha ya muziki kabla ya kutoka ni magumu yanayoweza kukatisha tamaa wasanii wengi wenye vipaji.

"Kwa sasa sina ninachokifanya zaidi ya kusikiliza ushauri wa viongozi wangu wa ANE, nikiamini kuwa uwezekano wa kupasua anga ni mkubwa kutokana na Kampuni kuwa na watu wanaojua muziki na ndoto za sisi vijana kufika mbali.

"Lengo langu ni kufanya muziki mzuri wa kibiashara, nikitumia uzoefu wangu na kipaji changu cha kuimba na kuandika nyimbo kali ili nipate mafanikio ya kutimiza ndoto zangu, ukizingatia kuwa nimesota sana, nimekula ngarambe nyingi, hivyo hakuna kinachoweza kuniweka chini tena,"Alisema Man Mo.

Man Mo anasema kuwa licha ya muziki kuwa na ushindani mkubwa, lakini ukiweka bidii unafanikiwa, huku akisema kuwa anataka kuwa msanii 'simple' kama Ali Kiba lakini afanye muziki mzuri wa biashara kama Diamond Platnumz jambo linalompa utajiri mkubwa.

Msanii huyo anaendelea kusema kwa kuwataka wasanii kufanya juhudi kubwa kuutangaza muziki wao pamoja na chipukizi kukaza msuri ili nao wafikie malengo licha ya kwamba wasanii wachanga wengi huishia njiani kwa kushindwa kwenda na kasi ya msoto katika sanaa.

Man Mo anakumbuka jinsi alivyoshindwa kuwa na maelewano mazuri na baba yake kiasi cha kununiana, kisa kuwa kwenye muziki huku maisha yakiwa magumu kwa mtoto wao, ambapo juhudi za mama yake zilikuwa zinamlainisha mzee wake japo kwa uchache.

Mwimbaji huyo mwenye ndoto kubwa anasema muziki umezidi kupiga hatua kutokana na juhudi za wasanii wenyewe wanaokwenda na mabadiliko, ikiwamo mbinu ya kutumia vizuri mitandao ya kijamii kama Facebook, Instagram, YouTube nk, ambapo kama ilivyokuwa kwa wasanii wengine, Man Mo pia anamiliki akaunti mbalimbali zinaoenda kwa jina la manmoofficial katika mitandao mbalimbali kwa ajili ya kutangaza muziki wake pamoja na kupata ulingo wa kujadiliana na mashabiki wake.

Anasema hali hiyo umeufanya muziki kuwa biashara nzuri licha ya msoto kabla ya kutoka kuwa pale pale, jambo linaloongeza hamasa ya kufanya vizuri kwa wasanii wote nchini Tanzania, ambapo nyimbo zake zinapatikana kwenye YouTube kwa akaunti ya Kampuni ya Africa Network Entertainment pamoja na kupatikana pia Audiomack, Boomplay, Spotify na kwingineko.

Kuhusu serikali, Man Mo anaitaka iendelee kushirikiana na wasanii wote sanjari na kuwatafutia upenyo katika muziki wa Dunia, bila kusahau kufanikisha wasanii wa ndani kutoka nje mara kwa mara ili wakaongeze wigo mkubwa katika sanaa yao, akisisitiza kuwa bila wasanii wa ndani kupata maonyesho ya Kimataifa muziki wao hautapiga hatua.

Huyo ndiye Man Mo, mmoja ya wasanii waliopokewa na msoto na mwenye ndoto lukuki za kisanaa.

Infinix YAZINDUA Infinix S5 SIMU YA KWANZA YENYE 32 CLEAR SELFIE NA Infinity-O Display

$
0
0



Infinix, baada ya kuliteka soko na toleo pendwa la Infinix S4, Infinix imezindua rasmi Infinix S5, kinamara wa toleo la S series kwa sasa ikiwa na Infinity-O Display na 32MP. Ujio wa Infinix S5 umeambatana msimu wa sikukuu za Christmas na Mwaka mpya hivyo Infinix kusheherekea msimu huu kwa kuzindua rasmi promotion itayoanza rasmi tarehe 25/11/2019 na zawadi mbalimbali kama vile Vacuum Cleaner, Deep Flyer, Subwoofer Radio.
Akizungumza na vyombo vya habari wakati wa uzinduzi wa Infinix S5, Afisa wa mahusino wa kampuni ya Infinix, Aisha Karupa alisema, “Infinix ikiwa ni kampuni yenye ushawishi mkubwa katika mfumo wa kidigitali tunawahakikishia wateja wetu bidhaa zenye teknolojia ya hali ya juu kwa bei Rafiki”,
Vile vile Aisha aligusia kuhusiana na sifa za simu hiyo kwa kusema, “na pamoja ya kuwa na selfie kali yenye 32MP lakini pia inasifa lukuki kama vile teknolojia ya Artifficial Intelligence kwenye kamera 4 za nyuma ambazo ni 16MP+5MP+2MP+AI Lens, lakini pia Infinix S5 ina memory card ya ukubwa wa GB 4 kwa GB64 yenye uwezo wa kutunza kumbukumbu nyingi pasipo huitaji ya memory card ya ziada na kwa upande wa design Infinix S5 imekuja katika muonekano wa kitofauti wenye kuvutia kutokana na namna kamera ya mbele ilivyopachikwa ndani ya Display kwa jina la kitaalamu Infinity-O Display na kwa wale wenye matumizi mengi Infinix S4 inauwezo wa kukaa na chaji kwa muda mrefu kutokana na ujazo mkubwa wa Battery wenye mAh40,000”.
Pia Infinix wametumia nafasi hiyo kutambulisha rasmi promotion ya msimu wa sikukuu inayoenda sambamba na uzinduzi wa Infinix S5. Akizungumza meneja wa mauzo wa Infinix Bwana Fredy Kadilana alisema kwamba, katika msimu huu wa sikukuu za Christmas na mwaka mpya Infinix imezindua rasmi promotion itakayompa nafasi mteja wa Infinix S5 au mteja wa simu yoyote ya Infinix kujishindia zawadi mbalimbali kama vile Vacuum Cleaner, Deep Flyer, Subwoofer Radio na nyengine nyingi lakini pia Infinix haijasahau wadau wake wa wanaotembelea kurasa @infinixmobiletz kwa kuitambulisha challenge ya #S5showitoff itayoanza rasmi mwishoni mwa wiki hii”.

Kwa maelezo zaidi tembelea

www.infinixmobility.com

kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA yawafikia wakazi wa Mkoani Singida

$
0
0

 Mkuu wa Kanda ya Kati wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Anthony Manyanda akizungumza na Wananchi wakati wa utoaji wa elimu ya usajili wa laini za Simu kwa alama za vidole wakati wa Kampeni ya Mnada Kwa Mnada iliyofanyika Viwanja vya Stendi ya Zamani ya mabasi mkoani Singida.

WAKAZI wa Mkoa  Singida na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Idara ya Uhamiaji  kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Kampeni tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 18 lengo kuu ni nchi nzima kufikiwa na Kampeni hiyo.

 Mkuu wa Kanda ya Kati  wa TCRA  Anthony Manyanda amesema ni fursa kwa wananchi wa Mkoa Singida kufika Stendi ya zamani ya mabasi kwa ajili ya kusajili kwa alama za vidole pamoja na kujiandikisha kupata usajili wa vitambulisho vya Taifa  kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Manyanda amesema kuwa  Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa ya Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa alama za vidole pamoja Huduma zingine za mawasiliano..

Manyanda  amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika  huduma  za simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi na kuongeza kuwa muda ni huu na kuacha kusubiri mwisho wa mwezi Desemba.

Amesema  kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.

Manyanda amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata ili waweze kusajili laini za simu kwa kwa  alama za vidole na huduma nyinginezo za Mawasiliano hayo.

Hata hivyo amesema kuwa
 kuna watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kutoa elimu kuhusiana  makosa ya jinai ya matumizi ya simu yasiofuata sheria.

Aidha amesema Kampeni hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha kila mwananchi anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha taifa.

Amesema  TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili watumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu tunayotoa.

Hata hivyo amesema kuwa wananchi wajitokeze katika kujisajili kwa alama za vidole kabla ya Desemba 31 na muda uliobakia ni mdogo tangu tangazo lilipotolewa.

"TCRA tutahakikisha tunawafikia katika wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" amesema.Manyanda.

Manyanda amesema kuwa Kampeni hiyo imeanza kwa Mikoa yote iliyopo katika kanda ya Kati.

Nae Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili laini za simu kwa alama za vidole.

Masasi amesema kuwa Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA kupata elimu na baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika mamlaka husika kupata vitambulisho.
 Afisa Habari Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mabel Masasi akitoa elimu ya usajili wa laini za Simu kwa alama za vidole ikiwa ni Kampeni ya Mnada kwa Mnada iliyofanyika Viwanja vya Stendi ya Zamani ya mabasi mkoani Singida.
 Wananchi wakiwa wamepanga foleni kwa ajili ya kuangalia namba ya vitambulisho katika mfumo wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada iliyofanyika Viwanja vya Stendi ya Zamani ya mabasi mkoani Singida.


 Matukio mbalimbali katika picha katika usajili wa laini za Simu kwa alama za vidole katika Viwanja vya Stendi ya Zamani ya mabasi mkoani Singida.
Mwananchi akisoma fomu ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA ili kuweza kukamilisha usajili wa laini za Simu kwa alama za vidole,Kampeni ya Mnada kwa Mnada iliyofanyika Viwanja vya Stendi ya Zamani ya mabasi mkoani Singida.

Mkurugenzi Mtendaji wa Tigo azishauri taasisi za kifedha kuwekeza katika teknolojia

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji (Tigo), Simon Karikari, akiwasilisha mada juu ya kukuza maendeleo ya sekta ya fedha kupitia mifumo ya kidigitali katika mkutano wa 19 wa taasisi za kifedha nchini unaoendelea jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye.



Mkurugenzi Mtendaji (Tigo), Simon Karikari, akiwasilisha mada juu ya kukuza maendeleo ya sekta ya fedha kupitia mifumo ya kidigitali katika mkutano wa 19 wa taasisi za kifedha nchini unaoendelea jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye.

M-BET yamwaga vifaa Ruvuma Vijana Cup

$
0
0
Dar es Salaam. Kampuni ya michezo kubashiri ya M-BET Tanzania imedhamini mashindano ya soka ya Ruvuma Vijana Cup ambayo yanashirikisha timu za wilaya zote sita za Mkoa wa Ruvuma.

Msemaji wa M-BET Tanzania, David Malley alisema kuwa kampuni yao imetoa vifaa mbalimbali vya michezo ikiwa pamoja na Jezi na Mpira kwa timu mbalimbali zinazoshiriki katika mashindano hayo.

Malley alisema kuwa mbali ya jezi, soksi na mipira kwa timu , pia M-BET imedhamini vifaa vya mazoezi kama bips.

Alisema kuwa jezi hizo zitagawiwa kwa timu zitakazofuzu hatua ya 16 bora ya mashindano ambapo fainali yake itafanyika Desemba 15 kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Sokoine.

“Huu ni mwendelezo wa mchango wa kampuni yetu katika kuendeleza michezo, tulianza na KMC ambayo tumeidhamini kwa Sh 1 billioni kwa miaka mitano,” alisema Malley.

Kwa upande wake, mratibu wa mashindano hayo, Raymund Mhenga alisema kuwa mashindano hayo yalishirikisha jumla ya timu 32 ambapo sasa yapo katika hatua ya mtoani kuelekea hatua ya 16 bora.

“Tunawashukuru M-BET Tanzania kwa msaada huu ambao utahamasisha maendeleo ya soka mkoani Ruvuma ambapo mwaka jana, wachezaji 10 walisajiliwa na timu inayoshiriki ligi daraja la kwanza ya Majimaji,” alisema Mhenga.

Mhenga alisema kuwa mashindano hayo yanazidi kushika kasi na mipango yao ni kuyafanya kuwa ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Alisema kuwa mipango yao ni kuziharika timu za Yanga na KMC kushuhudia mashindano hayo ili kusaka vipaji kama ilivyokuwa kwa Majimaji.
 
Msemaji wa Kampuni ya michezo ya kubashiri ya M-BET, David Malley (kulia) akimkabidhi mpira mratibu wa mashindano ya Ruvuma Vijana Cup, Raymund Mhenga baada ya kampuni hiyo kutangaza kudhamini mashindano hayo. 

RAIS DKT MAGUFULI AWEKA MAWE YA MSINGI KATIKA MIRADI YA HOSPOITALI YA UHURU, SOKO KUU, NYUMBA ZA POLISI NA STENDI KUU YA MABASI JIJINI DODOMA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelezo toka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo kuhusiana na Ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini Dodoma alikoiwekea jiwa la msingi leo. Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe
kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai akifunua pazia kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini Dodoma alikoiwekea jiwa la msingi leo Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugaio baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini Dodoma alikoiwekea jiwa la
msingi leo. Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Ally Mwalimu  baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini
Dodoma alikoiwekea jiwa la msingi leo. Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipata maelekezo ya  maendeleo ya ujenzi kutoka kwa Mkuu wa JKT Brigedia Jenerali Charles Mbuge  baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini
Dodoma alikoiwekea jiwa la msingi leo Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya
kisasa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Mkuu wa JKT Brigedia Jenerali Charles Mbuge  na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Daud Kondoro baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali Kuu ya Uhuru inayojengwa maeneo ya Chamwino jijini Dodoma alikoiwekea jiwa la msingi leo Ujenzi wa Hospitali hiyo umewezekana baada ya Rais Magufuli kuelekeza kiasi cha Shilingi Milioni 995.18 ambazo zilipangwa kutumika kwenye maadhimisho ya siku ya Uhuru mwaka jana zipelekwe kwenmye ujenzi wa hospitali hiyo ya kisasa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro akiwasili  eneo la Nzuguni jijini Dodoma Leo Tayari kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makazi ya Askari Polisi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akipata Maelezo  ya maendeleo ya Ujenzi wa Nyumba za makati ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijini Dodoma Leo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro akifunua pazia kuashiria uwekaji wa  jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makaki ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijin Dodoma Leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro baada ya kweka  jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makazi ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijin Dodoma Leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola baada ya kweka  jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makazi ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijin Dodoma Leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akikagua moja ya Nyumba za makazi ya askari baada ya kweka  jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makazi ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijin Dodoma Leo. Pamoja naye ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe.
Kangi Lugola, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani Meja Jenerali Jacob Kingu na IGP Simon Sirro.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kweka  jiwe la Msingi la Ujenzi wa Nyumba za makazi ya Askari Polisi eneo la Nzuguni jijin Dodoma lor ametoa jengo la Kwa adili ya Makao Makuu ya na kukabidhi nyaraka za jengo hilo kwa  Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola na IGP Simon Sirro.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimsikiliza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Mhe. Godwin Kunambi akitoa Maelezo kuhusiana na maendeleo ya Ujenzi wa Soko kuu la jiji la Dodoma ambalo litaitwa Soko Kuu la (Spika wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Job
Ndugai eneo la Nzuguni
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akifunua kitambaa kuweka jiwe la Msingi la  Ujenzi wa Soko kuu la jiji la Dodoma ambalo litaitwa Soko Kuu la (Spika wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai eneo la Nzuguni
 Muonekano wa  Soko Kuu la (Spika wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai eneo la Nzuguni jijini Dodoma
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiondoka baada ya kuweka jiwe la Msingi la  Ujenzi wa Soko kuu la jiji la Dodoma ambalo litaitwa Soko Kuu la (Spika wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai eneo la Nzuguni jijini Dodoma leo.PICHA NA IKULU

TCRA YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA SHULE YA SEKONDARI ILBORU

$
0
0

 Mkuu wa kanda ya Kaskazini Imelda Salum akizungumza katika hafla ya Makabidhiano ya vifaa katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Ilboru iliyopo Mkoani Arusha leo.
 Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega akizungumza na wageni waalikwa na wanafunzi katika shuke ya Sekondari Ilboru katika hafla ya Makabidhiano ya vifaa vya Tehama vilivyotolewa na TCRA.
Mkurugenzi mtendaji wa Ausha DC Alvera Ndabagoye akizungumza katika hafla hiyo Wakikadidhiana karatasi za  Makabidhiano ya vifaa kati ya Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TCRA Mhandisi Imelda Salum pamoja na Mkuu wa Shule ya Ilboru Dennis Otieno yakiendelea
Uwekaji sa saini katika karatasi za makabidhiano kati ya Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TCRA Mhandisi Imelda Salum pamoja na Mkuu wa Shule ya Ilboru Dennis Otieno yakiendelea .
Wakibadilishana karatasi za makabidhiano kati ya Mkuu wa Kanda ya Kaskazini TCRA Mhandisi Imelda Salum pamoja na Mkuu wa Shule ya Ilboru Dennis Otieno yakiendelea ,Wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega na Mkurugenzi wa halmashauri ya Arusha 
 Baadhi ya washiriki katika hafla hiyo katika ukumbibwa shule hiyo
Mkuu wa Shule ya sekondari ya ILBORU Dennis Otieno akizungumza katika hafla ya Makabidhiano ya vifaa vya TEHAMA vilivyotolewa na TCRA.

Na.Vero Ignatus,Arusha 

Mamlaka ya Mawasiliano Nchini(TCRA) imekabidhi vifaa vya TEHAMA katika shule ya Sekondari ya Ilboru iliyopo mkoani Arusha ambapo kigezo kikubwa ni ufaulu na kushika nafasi ya juu katika ngazi ya Taifa. 

Akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano Mkuu wa kanda ya Kaskazini Mhandisi  Imelda Salum ambaye amemuwakilisha Mkurugenzi mkuu wa TCRA Nchini Mhandisi James Kilaba amesema kuwa Mamlaka hiyo ina jukumu la kuhakikisha kuwa mawasiliano yanawafikia wananchi wale waliopo mjini na wale waliopo nje ya mji bila kusahau makundi yenye mahitaji maalumu.

''TCRA imeweka imeweka katika mpango mkakati wake utaratibu wa kusaidia utoaji wa vifaa vya vifaa vya Tehama kwa wenye mahitaji makundi maalumu kwa kuzingatia vigezo mbalimbali vinavyopangwa katika kila mwaka wa utekelezaji''alisema Mkuu wa Kanda.

Amesema lengo kuu la kutoa vifaa kwa wanafunzi ili waweze kutumia huduma za Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,katika kusaidia kupata mahitaji yao ya kimasomo, kama vile vitabu kwenye mtandao na rejea mbalimbali,sambamba na kutoa chachu katika kufikisha,kurahisisha upatikanaji kwa waalimu na wanafunzi,kuandaa masomo,kuwawezesha kuweka habari za shule kwenye mtandao.

Ametoa wito kwa uongozi wa shule hiyo kuhakikisha kuwa vifaa hivyo vya TEHAMA vinatumika katika matumizi salama ya mtandao ili yaweze kuleta tija kama ilivyokusudiwa,kwani vikitumika vibaya ni hasara.

''Naomba niweke msisitizo kwenye suala zima la matumizi salama ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano pamoja na matumizi sahihi salama ya mtandao,kwani mtandao ukitumika vizuri ni jambo zuri na lenye manufaa sana,lakini ikitumika vibaya ni hasara''Alisema Mhandisi Imelda.

Kwa upande wake Katibu Tawala mkoa wa Arusha Richard Kwitega ameishukuru TCRA kwa kutoa vifaa hivyo katika shule hiyo Maalumu ya ILBORU,ambapo ametoa wito kwa walimu na wanafunzi kujitahidi kutumia vifaa hivyo kwa makusudi maalum yaliyokusudiwa huku akiwataka kuvitunza vifaa hivyo ili vidumu.

Kwitega mesema kuwa Mkoa wa Arusha umejipanga kuboresha ufaulu katika shule zake na kuhakikisha kuwa ufaulu unakuwa nzuri kuanzia ngazi ya Kata hadi Kitaifa ili kuleta sifa njema.  

Pia amewaagiza Tehama ngazi ya mkoa kutoa sapoti ya kiufundi kwaajili ya kusaidia vifaa hivyo viendelee kufanya kazi kwa manufaa ya Elimu.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya seondari ya Ilboru Dennis Otieno ameishukuru TCRA kwa kuwapatia vifaa hivyo vya TEHAMA na ameahidi kuwa watavitumia kwa matumizi sahihi yaliyokusudiwa huku akisema vitawasaidia kutuma matokeo ya wanafunzi kwa wazazi,sambamba na wanafunzi kutumia vifaa hivyo kwaajili ya kujisomea na kufahamu mambo mbalimbali bila kuvunja sheria ya mtandao.

''Hapa shuleni tunao wanafunzi ambao ni watundu sana katika mambo ya mtandao,kunammoja aligundua kifaa cha kutambua kama mwanafunzi anayo simu shuleni na mwingine aligundua kifaa cha kutambua kama mwanafunzi anaumwa ambapo taarifa zinatumwa mapema kwa mzazi,hivyo kwetu sisi kupata vifaa hivi ni faraja sana.''Alisema mkuu wa shule

Katika mwaka wa fedha 2018/2019, Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA imeshatoa vifaa kwa shule tano nchini kwa kuzingatia vigezo vya ufaulu,matokeo ya mtihani wa Taifa mwaka 2015,ambapo shule ya Ilboru ni miongoni mwa shule hizo zilizofanya vizuri kitaifa na hivyo kuweza kukidhi mahitaji ya kupewa vifaa vya TEHAMA.

Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na Computer,UPS,Printer,utengenezaji wa tovuti za shule pamoja na kuunganisha kwenye mtandao ambapo vifaa hivyo viliwasilishwa na kufungwa shuleni hapo mnamo mwezi Agosti mwaka huu

GSM WAFUNGUA DUKA JINGINE LA SAMANI ZA NDANI MIKOCHENI, WATANZANIA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA

$
0
0
Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Duka jipya la GSM HOME lililopo Mikocheni A Barabara ya Mwai Kibaki jijini, Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Silent Ocean ,Salaa Mohamed amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi katika duka jipya na la aina yake la GSM Home ili kujipatia samani (fenicha) bora kabisa za kiwango cha kimataifa zinazoendana na kipato chao.
Mkurugenzi huyo aliyasema hayo Novemba 22, mwaka huu, wakati wa hafla ya uzinduzi wa duka hilo lililopo Mikocheni A barabara ya Mwai Kibaki jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi na wafanyakazi wa Kampuni ya GSM pamoja na wadau wengineo.

Kwa mantiki hii, napenda niwapongeze kwa ajili ya kuendelea kuwa wabunifu na kuja na wazo la kuanzisha duka hili kubwa la samani ambalo linasaidia watu pamoja na taasisi kupata samani zenye ubora hapa nchini.
“Napenda kuwahimiza Watanzania kufika katika duka hili jipya na la aina yake ili kuweza kujipatia samani bora na ambazo zitaendana na kipato chao. Napenda niwapongeze GSM kwa kuendelea kuwa wabunifu na kuja na wazo la kuanzisha duka hili kubwa la samani ambalo linasaidia watu pamoja na taasisi kupata samani zenye ubora hapa nchini,” alisema Mohamed.

Alisema kutokana na uwepo wa makampuni ya GSM, maelfu ya Watanzania wameweza kupata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja na hivyo kujipatia kipato kinachowasaidia kuendesha maisha yao.

“Makampuni ya GSM yamekuwa mdau muhimu na mwenye mchango mkubwa kwa nchi yetu na pia tunatarajia mchango wenu kuongezeka zaidi hasa katika utekelezaji wa lengo la kitaifa la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda pamoja na uchumi wa kati kufikia mwaka 2025,” alisema.

Aliongeza: “Napenda kuwahakishia kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, itaendelea kutengeneza mazingira mazuri na rafiki ya ufanyaji biashara ili kampuni kama GSM ziendelee kukua. Serikali imedhamiria kutekeleza mapendekezo yaliyopo kwenye waraka wa Blueprint yanayolenga kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini ili nchi yetu iweze kufika kwenye uchumi wa kati.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa GSM Group, Fatma Abdallah, lengo la kuzindua duka hilo ni kuziba pengo lililopo sokoni katika usambazaji wa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu, lakini pia kuwasogezea wananchi huduma zao.
“Duka hili jipya linatarajiwa kuhudumia na kukata kiu kwa watanzania wote kwani mahitaji haya ni muhimu sana katika jamii yetu, hususan fenicha za majumbani na maofisini zinazopatikana hapa GSM HOME kwa ubora wa kimataifa.

Alizitaja bidhaa zinazopatikana katika duka lao hilo kuwa ni ‘shelving’, sofa, kabati za ukutani, meza za kahawa, meza za chakula, vitanda na fenicha za chumba cha kulala, makabati ya nguo na nyinginezo za kupendezesha ofisi na nyumba.

“Napenda kuwahabarisha Watanzania kuwa fenicha zetu ni bora na za kisasa zikiwa zimetengenezwa kwa umakini wa hali ya juu na kufanyiwa tathmini ya kubaini ubora wake wa kimataifa,” alisema.

Alisema mbali ya fenicha, wanauza vyombo vya aina zote vya jikoni, bafuni na chooni vya chapa (brand) kutoka Italia pamoja na vifaa vya umeme.

Sambamba na uzinduzi huo, Fatma alisema kutakuwa na ofa na promosheni nyingi, ikiwemo punguzo la asilimia 10% kwa mwezi huu mzima wa Novemba kwa mteja atakayenunua mzigo wa thamani kuanzia sh 200,000.









WAKALA WA BENKI YA NMB WAPIGWA MSASA

$
0
0

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Ndogo na za Kati wa benki ya NMB - Filbert Mponzi akimkabidhi Khalifa Kimaro-mmoja wa mawakala cheti cha ushiriki mafunzo ya uwakala.
Mmoja wa mawakala akiuliza swali kwa watoa mada
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam – Badru Idd akimkabidhi Betty  Rutihanda-mmoja wa mawakala cheti cha ushiriki mafunzo ya uwakala.
Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawakala – James Manyama akitoa mada 

**********************************

MAWAKALA wa Benki ya NMB Halimashauri za Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam wamepigwa msasa katika Semina ya kuwajengea uwezo na kuboresha huduma inayomfikia mteja wa NMB katika maeneo yao pamoja na kujilinda na uhalifu na utakatishaji fedha.

Katika semina iliendeshwa hivi karibuni katika maeneo ya Sinza na Ilala jijini Dar es Salaam,Mawakala wa Benki ya NMB walipata fursa ya kupewa elimu juu ya kumpatia mteja huduma bora, kuuliza maswali na elimu juu ya kujikinga na vitendo vya kihalifu ikiwemo kupitisha fedha chafu, ambapo ni kinyume na sheria za nchi.

Akizungumza katika Semina hiyo Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam – Badru Idd, alisema NMB Wakala ni njia inayomfikishia huduma mteja kwa urahisi zaidi na kwa wakati.

“Kwa nini tunawatumia mawakala, tumeona kwamba ni njia moja wapo inayoweza kutufanya tuwafikie wateja wetu ambao ni watanzania zaidi ya Milioni 60, hatuwezi kufika kila eneo huwa kidogo kuna ugumu wake lakini kupitia mawakala tunaweza kuwapata kila eneo wenye uwezo wa kuwahudumia wateja wetu kama vile ambavyo tumekusudia.

“Mteja wetu anaweza kutoa pesa, kuweka pesa, ataweza kulipia miamala mbali mbali, kama kulipia malipo ya maji, umeme, malipo ya serikali na ada za shule, tunasisitiza kwamba wateja wetu waendelee kutuamini kupitia mawakala wetu ambao wanaendelea kutoa huduma.

“Tumekuwa na semina mbali mbali, tukiwa tunaendelea kuwajengea uwezo mawakala ili waendelee kutoa huduma zetu kwa ukaribu Zaidi. Muhimu ni muongozo wetu kila mwaka tunataka tuwasikilize changamoto juu ya huduma zetu, tuwaulize maswali watuulize maswali wote kwa pamoja tuweze kuhakikisha huyu mtanzania anapata huduma zetu kokote kule anakopatikana kwa ufanisi mkubwa.

Badru alisema, sio kwa Dar es Salaam tu, bali wameendesha semina kama kwa zaidi ya maeneo 40 nchi nzima. Semina hizi zimeleta mafanikio makubwa sana, hasa kwa kuokoa muda wa mteja, kupata huduma ya uhakika na kwa urahisi.

“Sisi kwetu wateja ni wafalme na ndio maana tunaendelea kuwa na huduma za mbadala kama, wakala, masine za ATM, na NMB Mkononi ili kuweza kumfikia mteja wetu kiurahisi zaidi.”alisema Badru.

Naye Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawakala – James Manyama, alisema lengo la kukutana na Mawakala ni kuwapa muelekeo wa wapi Benki inaelekea kwa wakati na kuwapa mafunzo jinsi ya kujilinda na utakatishaji fedha pamoja na kuingiza fedha katika mikono ya gaidi.

“Kama Mawakala, tunawapa wajibu wa kutunza amana za wateja, kutunza usiri wa wateja, mawakala wetu wamethibitisha ubora wa huduma zetu na wameahidi kwenda kutoa huduma bora kwa wateja wetu” alisema Manyama.

Kwa upande wa Mawakala waliohudhuria semina hiyo walitoa kongole zao kwa NMB kwa jinsi ambavyo inawajali kwa kuwapaa elimu na fursa ya kutoa changamoto zao ili kuweza kuboresha huduma zao.

“Nafurahi sana kuwa karibu na NMB, nafurahia kuwepo katika hii semina, NMB wanatoa huduma nzuri, pia wako karibu na sisi mawakala wao, kila wakala anafanya kazi kwa ukaribu sana na tawi lake la NMB linalomhudumia, nashauri Watanzania wenzagu kuchangamkia fursa ya Uwakala wa NMB maana inalipa” Tedy Michael – Wakala NMB Makumbusho.

“Tunashukuru kwa semina hii ambayo imetupa elimu juu ya nini cha kufanya kwa wateja wetu, tumepata mbinu mbadala ya kutoa huduma bora kwa wananchi na tunawaahidi benki yetu pendwa ya NMB kuwa tutafanya kazi kwa weledi na kuhakisha wateja wanafurahia huduma zetu.” Alisema Khanifa Kimaro – Wakala NMB Kimara.

WAKALA WA BENKI YA NMB WAPIGWA MSASA

$
0
0

Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara Ndogo na za Kati wa benki ya NMB - Filbert Mponzi akimkabidhi Khalifa Kimaro-mmoja wa mawakala cheti cha ushiriki mafunzo ya uwakala.
Mmoja wa mawakala akiuliza swali kwa watoa mada
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam – Badru Idd akimkabidhi Betty  Rutihanda-mmoja wa mawakala cheti cha ushiriki mafunzo ya uwakala.
Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawakala – James Manyama akitoa mada 

**********************************

MAWAKALA wa Benki ya NMB Halimashauri za Ubungo na Kinondoni jijini Dar es Salaam wamepigwa msasa katika Semina ya kuwajengea uwezo na kuboresha huduma inayomfikia mteja wa NMB katika maeneo yao pamoja na kujilinda na uhalifu na utakatishaji fedha.

Katika semina iliendeshwa hivi karibuni katika maeneo ya Sinza na Ilala jijini Dar es Salaam,Mawakala wa Benki ya NMB walipata fursa ya kupewa elimu juu ya kumpatia mteja huduma bora, kuuliza maswali na elimu juu ya kujikinga na vitendo vya kihalifu ikiwemo kupitisha fedha chafu, ambapo ni kinyume na sheria za nchi.

Akizungumza katika Semina hiyo Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam – Badru Idd, alisema NMB Wakala ni njia inayomfikishia huduma mteja kwa urahisi zaidi na kwa wakati.

“Kwa nini tunawatumia mawakala, tumeona kwamba ni njia moja wapo inayoweza kutufanya tuwafikie wateja wetu ambao ni watanzania zaidi ya Milioni 60, hatuwezi kufika kila eneo huwa kidogo kuna ugumu wake lakini kupitia mawakala tunaweza kuwapata kila eneo wenye uwezo wa kuwahudumia wateja wetu kama vile ambavyo tumekusudia.

“Mteja wetu anaweza kutoa pesa, kuweka pesa, ataweza kulipia miamala mbali mbali, kama kulipia malipo ya maji, umeme, malipo ya serikali na ada za shule, tunasisitiza kwamba wateja wetu waendelee kutuamini kupitia mawakala wetu ambao wanaendelea kutoa huduma.

“Tumekuwa na semina mbali mbali, tukiwa tunaendelea kuwajengea uwezo mawakala ili waendelee kutoa huduma zetu kwa ukaribu Zaidi. Muhimu ni muongozo wetu kila mwaka tunataka tuwasikilize changamoto juu ya huduma zetu, tuwaulize maswali watuulize maswali wote kwa pamoja tuweze kuhakikisha huyu mtanzania anapata huduma zetu kokote kule anakopatikana kwa ufanisi mkubwa.

Badru alisema, sio kwa Dar es Salaam tu, bali wameendesha semina kama kwa zaidi ya maeneo 40 nchi nzima. Semina hizi zimeleta mafanikio makubwa sana, hasa kwa kuokoa muda wa mteja, kupata huduma ya uhakika na kwa urahisi.

“Sisi kwetu wateja ni wafalme na ndio maana tunaendelea kuwa na huduma za mbadala kama, wakala, masine za ATM, na NMB Mkononi ili kuweza kumfikia mteja wetu kiurahisi zaidi.”alisema Badru.

Naye Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawakala – James Manyama, alisema lengo la kukutana na Mawakala ni kuwapa muelekeo wa wapi Benki inaelekea kwa wakati na kuwapa mafunzo jinsi ya kujilinda na utakatishaji fedha pamoja na kuingiza fedha katika mikono ya gaidi.

“Kama Mawakala, tunawapa wajibu wa kutunza amana za wateja, kutunza usiri wa wateja, mawakala wetu wamethibitisha ubora wa huduma zetu na wameahidi kwenda kutoa huduma bora kwa wateja wetu” alisema Manyama.

Kwa upande wa Mawakala waliohudhuria semina hiyo walitoa kongole zao kwa NMB kwa jinsi ambavyo inawajali kwa kuwapaa elimu na fursa ya kutoa changamoto zao ili kuweza kuboresha huduma zao.

“Nafurahi sana kuwa karibu na NMB, nafurahia kuwepo katika hii semina, NMB wanatoa huduma nzuri, pia wako karibu na sisi mawakala wao, kila wakala anafanya kazi kwa ukaribu sana na tawi lake la NMB linalomhudumia, nashauri Watanzania wenzagu kuchangamkia fursa ya Uwakala wa NMB maana inalipa” Tedy Michael – Wakala NMB Makumbusho.

“Tunashukuru kwa semina hii ambayo imetupa elimu juu ya nini cha kufanya kwa wateja wetu, tumepata mbinu mbadala ya kutoa huduma bora kwa wananchi na tunawaahidi benki yetu pendwa ya NMB kuwa tutafanya kazi kwa weledi na kuhakisha wateja wanafurahia huduma zetu.” Alisema Khanifa Kimaro – Wakala NMB Kimara.

Benki ya Exim Yazidi kujitanua zaidi, Yaingia Ethiopia.

$
0
0
Benki ya Exim Tanzania imezidi kujitanua zaidi nje ya mipaka ya Tanzania kwa kufungua kituo cha huduma za benki hiyo (Commercial Representative Office ) katika jiji la Addis Ababa nchini Ethiopia.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse wakati akifungua rasmi tawi jipya la benki ya Exim Tanzania lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam ikiwa ni baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania. Katika uzinduzi huo, Dk Kibesse alimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango.
Kufuatia hatua hiyo Benki hiyo inakuwa taasisi ya kwanza ya kifedha nchini Tanzania kuendesha shughuli zake kwenye mtandao wa mataifa matano  ikiwemo  Ethiopia ambayo inatajwa kuwa ndio nchi ya pili kwa ukubwa wa idadi  ya watu barani Afrika. Mataifa mengine ambayo benki hiyo inaendesha huduma zake ni pamoja Uganda, Comoros na Djibouti.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na benki hiyo jijini Dar es salaam mapema leo ilisema kwamba benki hiyo imepata leseni ya kufungua na kuwa na Ofisi ya Mwakilishi wake nchini Ethiopia kupitia tawi lake la nchini Djibouti na imepanga kuanza kazi kutoa huduma zake nchini humo hivi karibuni.
"Tunatarajia kwamba huduma zetu zitaanza  kutolewa kikamilifu mapema mwezi Disemba, 2019 kupitia Ofisi ya Mwakilishi wetu kibiashara  iliyopo katika Jengo la Zouleka LKG, ghorofa ya 2, Sub City Bole, 2160 / B. Addis Ababa. '' alisema Bw Jaffari Matundu, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo kupitia taarifa hiyo.
Alisema upanuzi huo  wa Ethiopia unakuja kama sehemu ya mikakati wa upanuzi wa benki hiyo kwa ujumla katika kutimiza matarajio yake ya kuwa Benki ya Pan African. Aidha ufunguzi wa ofisi hiyo  ya uwakilishi utakuza mipango ya kimkakati katika kuongeza ushirikiano na nchi mbambali  za Afrika na inatoa jukwaa muhimu kwa Benki hiyo kuuza huduma zake za kipekee kwa biashara za nje.
"Hii ni hatua muhimu kwa Benki ya Exim ikiwa kama kikundi.'' Alisema Matundu  huku akibainisha kuwa ukuaji thabiti wa uchumi nchini Ethiopia ambao umechochewa na uwekezaji mkubwa wa umma na ongezeko la wateja ndio sababu nchi hiyo imekuwa kivutio kwa taasisi za kifedha kuwekeza katika taifa hilo.
Alisema kuwa Benki hiyo pia inakusudia kusaidia ufanyaji wa biashara baina ya Tanzania  na Ethiopia,  kusoma soko na fursa za uwekezaji zilizopo huku ikishiriki katika kuendesha ukuaji wa uchumi baina ya nchi hizo mbili.
Aliongeza kuwa Ethiopia imerekodi viwango vya juu zaidi vya ukuaji wa uchumi ulimwenguni kote katika miaka michache iliyopita na imeorodheshwa  miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi zaidi barani Afrika kulingana na takwimu za Shirika la Fedha Duniani (IMF).
"Tunatazamia fursa zaidi za ukuaji kupitia soko la Ethiopia, haswa kwa kuzingatia mageuzi yaliyofanyika hivi karibuni nchini humo. Tunaamini kwamba kuna fursa nyingi za ukuaji wa uchumi nchini Ethiopia, na Benki ya Exim kama kikundi tunataka kuwezesha hili. "Alisema.
Aidha ukuaji huo wa Benki ya Exim umeonesha kuivutia Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ambapo hivi karibuni, akifungua rasmi tawi jipya la benki hiyo lililopo katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam ikiwa ni baada ya benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Dk Bernard Kibesse aliipongeza benki hiyo huku akiahidi kuipa ushirikiano zaidi katika kufanikisha adhma yake ya kufungua matawi zaidi nje ya nchi.
“Ni fahari kwetu kuona benki ya kizalendo inafanya mambo makubwa kama haya. Mmekuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa mabenki hapa nchini jinsi inavyojizatiti kujiimarisha ndani na nje ya mipaka ya nchi.Hatua hii ni sawa na kuitikia kilio cha wadau wa huduma za kifedha hapa nchini  wanaohitaji huduma zinazokidhi mahitaji yao pia huduma zinazolingana na zile za kimataifa na kwenye mazingira yaliyobereshwa.’’ Alisema Kibesse.

Mtanzania Ateuliwa Nafasi Nyeti Umoja Wa Mataifa.

$
0
0
Mtanzania, Elizabeth Maruma Mrema, ameteuliwa kuwa Kaimu Katibu Mtendaji wa Sekretarieti inayosimamia Mkataba wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa wa tofauti za kibiolojia (CBD) yenye makao yake makuu Monteal, Canada kuanzia Disemba 1, mwaka huu.

Uteuzi huo umefanywa hivi karibuni na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw António Guterres kufuatia kujiuzulu kwa Bi Cristiana Pasca Palmer,raia wa Romania kutokana na sababu za kiafya.

Kulingana na taarifa iliyotumwa kwenye wavuti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira (UNEP), uteuzi huo unatajwa kuwa unaongeza matumaini katika uhifadhi wa masuala ya bayonuai ya kibaiolojia, matumizi endelevu ya baiolojia hizo, na ugawaji wa faida zitokanazo na rasilimali za kijenitiki kwa kuzingatia usawa na haki.

Kabla ya kuteuliwa kwake, Bi Mrema alikuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Makao makuu ya UNEP jijini Nairobi, Kenya ambapo amefanya kazi kwa zaidi ya miongo miwili.

Majukumu yake katika Idara ya Sheria ya UNEP ni pamoja na uratibu wa ujenzi wa uwezo, maendeleo, utekelezaji na pia kufuatilia utekelezaji wa sheria za mazingira na mikutano ya kimataifa ya mazingira. Pia aliongoza masuala yanayohusiana na utawala wa kimataifa wa mazingira.

Bi Mrema ni Mwanasheria kitaaluma na Mwanadiplomasia akiwa na Shahada ya Sheria (LLB) (Hons) kutoka Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam, Shahada ya Uzamili (LLM) kutoka Chuo Kikuu cha Dalhousie, Canada na Stashahada ya Juu katika masuala ya Uhusiano wa Kimataifa na diplomasia (Summa Cum Laude) kutoka Kituo cha Mahusiano ya Kigeni na Diplomasia jijini Dar-es-salaam.

Aidha, Bi Mrema amechapisha nakala kadhaa zinazohusiana na sheria za kimataifa za mazingira, ufuatiliaji na utekelezaji wa mikataba na maendeleo ikiwemo makubaliano kadhaa ya mazungumzo kuhusu hali mazingira ya kimataifa pamoja na miongozo inayotumika sasa na UNEP katika mipango yake ya kujengeana uwezo.

Kabla ya kujiunga na Kitengo cha Sheria cha UNEP mnamo Juni 2014, Bi Mrema alikuwa Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mazingira, anayesimamia uratibu, shughuli na utoaji wa programu kuanzia mwaka 2012 na kwa mwaka mmoja, pia aliwahi kuwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara hiyo.

Mnamo mwaka 2004 alipewa tuzo ya Meneja wa UNEP bora zaidi wa mwaka kuwahi kutokea, aliyotambulika kama Tuzo ya Wafanyikazi ya UNEP Baobab kwa utendaji bora na kujitolea kufikia malengo ya UNEP.

Mnamo mwaka wa 2009 aliteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa UNEP/ Sekretarieti ya Mkataba juu ya Uhifadhi wa wanyamapori wanaohama (CMS)

Kabla ya kujiunga na UNEP, Bi Mrema alifanya kazi na Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa nchini Tanzania na hadi anaondoka alikuwa Mshauri Mwandamizi wa Sheria.

Katika kipindi cha uhudumu wake kwenye Wizara hiyo Bi Mrema, pia alikuwa Mhadhiri wa Sheria ya Umma ya Kimataifa na Diplomasia ya Mkutano katika Kituo cha Uhusiano wa nje na diplomasia cha Tanzania.
 
 Bi. Elizabeth Maruma Mrema  

Benki ya NMB yakabidhi gawio la Shilingi Bilioni 10.48 kwa Serikali

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuliakipokea mfano wa hundi ya gawio la Shilingi Bilioni 10.48 kwa Serikali kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurungezi wa Benki ya NMB - Margaret Ikongo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NMB - Ruth Zaipuna (kulia) katika hafla ya upokeaji wa gawio na michango kwa Serikali iliofanyika Ikulu Chamwino, Dodoma mapema leo. Wakishuhudia kutoka kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango – Dkt. Philip Mpango na Spika wa Bunge la Tanzania -Job Ndugai.
Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia yaliokuwa yakijiri kwenye hafla hiyo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani a Dkt John Pombe Magufuli,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kupokea gawio na michango kutoka katika Taasisi, Makampuni na Mashirika ya Umma hafla hiyo imefanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo.



Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images