Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46379 articles
Browse latest View live

Watengenezaji wa vifaa vya jikoni wazindua duka la kwanza Afrika mjini Dar

$
0
0

Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam

Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam
Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam
Meneja wa Sachsenküchen –Tanzania, Ronald Harold akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam


Meneja wa Sachsenküchen –Tanzania, Ronald Harold akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam
Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akizungumza na wageni na waandishi wa habari waliohudhuria kwenye uzinduzi wa duka jipya la kisasa la vyombo vya jikoni .


Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akielezea kuhusu ubora wa bidhaa walizonazo kwa wateja waliojitokeza kwenye duka jipya lakisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen lililoko Mikocheni jijini Dar es salaam
Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa duka jipya la kisasa la vyombo vya jikoni la Sachsenküchen, Mikocheni jijini Dar es salaam jana. Pembeni ni Meneja wa Sachsenküchen –Tanzania, Ronald Harold
Novemba 9, 2019, Dar es Salaam:

Kampuni ya Kitanzania, Power Systems (T) Ltd, imeshirikiana na wasanifu na watengenezaji wanaotambulika kimataifa wa vifaa vya jikoni, Sachsenküchen, kusambaza bidhaa zenye viwango kwenye soko la Tanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa moja ya maduka yake Mikocheni, jijini Dar es Salaam, Meneja wa Biashara za Nje wa Sachsenküchen, Dominik Shulze Doring, amesema kwamba ukaribu na wateja utarahisisha kufikisha huduma zao kwa wateja wa Tanzania.

“Kwa kuzindua duka la Sachsenküchen, ikiwa ni la kwanza barani Afrika, tunawaletea Watanzania bidhaa mbalimbali ambazo tunazizalisha. Pia tunaleta huduma za usanifu wa majiko kutokana na mahitaji ya mteja,” Doring ameelezea.

Meneja wa Sachsenküchen –Tanzania, Ronald Harold nae amesema: “Tunafuraha kwa kuweza kushirikiana na watengenezaji wa vyombo vya jikoni wanaotambulika duniani ili kuweza kuleta bidhaa zenye ubora wa hali ya juu kwenye soko. Tanzania pia itafaidika kwa kupata uzoefu na ujuzi watakaoleta washirika wetu kutoka Ujerumani ambao wana uzoefu wa zaidi ya miaka 100”

Harold pia ametoa wito kwa Watanzania kutembelea duka hilo jipya la Sachsenküchen kujionea wenyewe bidhaa bora na kufurahia huduma hiyo mpya.“Jikoni ni mahali ambapo mtu anatakiwa kufanya shughuli zake kwa furaha. Bidhaa zetu zimetengenezwa kuhakikisha matumizi mazuri ya nafasi huku pia zikiwa ni za kisasa, zenye kuvutia na kuridhisha wateja,” ameongeza Harold.

“Hapa Sachsenküchen kila kitu kinapewa kipaumbele, hususan ubora wa bidhaa ambazo zinabadilisha na kulifanya liwe ni sehemu halisi ya kuishi,” amesema.Sachsenküchen ni kiwanda kipo Dippoldiswalde, karibu na Dresden, Ujerumani, na wamekuwa wakisanifu majiko na kutengeneza vifaa vya jikoni kwa zaidi ya miaka 100.

Tokea miaka ya 1990, Sachsenküchen imekuwa ikikua huku ikiwa na wafanyakazi 220 na inasavifirisha zaidi ya asilimia 50 ya bidhaa zake nje ya nchi, mapato ya Euro milioni 40 kwa mwaka huu faida ikiwa ni asilimia 12.

Serikali yaipongea Taasisi ya CCBRT kutoa huduma kwa jamii kwa miaka 25

$
0
0
Taasisi ya CCBRT Tanzania imetimiza miaka 25 ya kutoa huduma za tiba kwa watoto wenye matatizo ya macho, miguu pinde, mgongo wazi na afya ya uzazi ikiwemo fistula.

Akizungumza na waandishi wa habari na wageni waalikwa, Rais wa bodi ya CCBRT Tanzania, Dkt. Wilbrod Slaa alisema tulianzisha hospitali ya CCBRT mwaka 1994 mwezi wa Nne tukiwa na malengo ya kusaidia watoto wenye ulemavu, lakini wazo lilikuja nikiwa na Dan Wood tukiwa Zanzibar baada ya ajali ya ndege iliyotokea Rwanda 

" Nakumbuka mwanzo tulikuwa tunapita mitaani kwenye nyumba na kukuta watoto wenye matatizo ya miguu na macho, kuna nyumba tulikuta mtoto ambaye alikuwa hana uwezo wa kuona mchana lakini usiku anaona vizuri wataalamu wanakumbuka , huyu ndio alikuwa mgonjwa wetu wa kwanza". alisema Slaa. Kina mama wengi ilikuwa tukipita mitaani walikuwa wanalia kuomba msaada wa watoto wao wenye matatizo mbalimbali na tuliweza kuwasiadia 

Tulipata changamoto ya kupata sehemu ya kufanyia operesheni, ikabidi tuende hospitali ya Mwananyamala na kuomba kupewa ruhusa ya kuwafanyia operesheni wagonjwa wetu wakaturuhusu na changamoto nyingine ilikuwa mahali pa kulaza wagonjwa wetu, na ilibidi tukiuke taratibu na kwenda kuwapangishia kwenye nyumba ya kulala wageni ambazo tulikodi kwa wagonjwa tu, na kwa bahati waziri wa afya kipindi hicho, mhe. Anna Abdallah alitoa baraka zake wagonjwa waweze kuwekwa kwenye nyumba hiyo. Aliendelea kusema Dkt. Slaa

Tunashukuru serikali ya Tanzania kuwa mdau mkubwa sana wa CCBRT kwa kutoa ardhi kubwa bure  kuwezesha kujenga hospitali na kupandisha hadhi hospitali yetu kuwa ya rufaa (zonal referral) alisema Dkt. Slaa

Pia tunatoa huduma zetu kulingana na wagonjwa tunaowapokea, hii inategemea mgongwa private au sio private na gharama tunazowachaji wagonjwa wa private zinaenda kutibia wagongwa wasio na uwezo gharama za matibabu alimaliza kusema Dkt. Slaa

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, alisema, Naomba kuchukua nafasi hii kuwapongeza Taasisi ya CCBRT kuadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwake nchini. Najua mmepitia changamoto nyingi sana pindi mlipoanza kama alivyokwisha kusema Rais wa bodi ya Taasisi ya CCBRT Dkt. Wilbrod Slaa.

Pia niwapongeze kwa kuwa na huduma za mkoba (mobile outreach) ambazo zimekuwa na ubia na hospitali mbalimbali nchini kama vile Bombo mkoani Tanga, Seko Toure Mwanza, Mnazi Mmoja Zanzibar, Kabanga Kigoma, Bagamoyo na Ikwiriri hii inaonyesha jinsi gani mmeweza kuwa bega kwa bega nasi serikali alisema Mhe. Mwalimu.
Nachukua fursa hii pia kuwapongeza, kituo cha CCBRT Moshi ambacho kinafanya kazi nzuri sana, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1996 kimeweza kuhudumia watoto wenye ulemavu na familia zao zaidi ya 10,000 na kuwarejeshea matumaini aliendelea Mhe. Mwalimu

Nimepewa taarifa CCBRT ndani ya miaka 9 mnashirikiana na timu ya usimamizi na uendeshaji wa huduma za afya mkoa wa Dar es salaam kutoa mafunzo kwa watoa huduma zaidi ya 900 kila mwaka hasa kwa madaktari na wauguzi. Na mradi wa kuwajengea uwezo watumishi kwenye vituo vya afya na zahanati 22 katika manispaa zote tano za mkoa wa Dar es salaam na Pia mradi huu umewekeza kiasi kikubwa cha miundombinu, ukarabati wa wodi za wazazi, ikiwemo ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi 1,895,615,400 na uwekezaji wa vyumba maalum vya watoto njiti, vyoo maalum kwa wenye ulemavu, utambuzi wa mapema wa watoto wenye ulemavu na kina mama wenye fistula ya uzazi aliendelea kusema Mwalimu.

Kwenye fistula wastani ya akina mama 800 kwa mwaka walipata huduma ya upasuaji, takwimu zinaonyesha akima mama takribani 2000 hadi 3000 hupata fistula ya uzazi nchini , CCBRT kushirikiana na MUHAS, Chuo kikuu Dodoma, KCMC kumewezesha kutoa mafunzo na Taasisi ya kimataifa ya madaktari bingwa magonjwa ya kinamama na wajawazito,(figo) kuwa miongoni mwa vituo vya mafunzo ya upasuaji fistula duniani, na mpaka kufikia mwezi 10 mwaka 2019 watakuwa wamefanya upasuaji fistula kina mama wapatao 10,000 alimaliza kusema.

Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB kwa kununua picha iliyouzwa kwenye mnada kwa thamani ya shilingi millioni 4.5 huku Dkt. Wilbrod Slaa akimpongeza mmoja kati ya wafanyakazi wa benki hiyo.
Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wageni waalikwa kwenye tafrija ya maadhimisho ya miaka 25 ya taasisi ya  hospitali ya CCBRT jana jijini Dar es Salaam 
 Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangi akizungumza na wageni waalikwa
 Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa PWC kwa kununua picha iliyouzwa kwenye mnada kwa thamani ya shilingi millioni 2 ili kuchangia gharama za matibabu kwa wasiojiweza

 Rais wa bodi ya Taasisi ya hospitali ya  CCBRT, Wilbrod Slaa akibadilishana mawazo na  Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangi

 Rais wa bodi ya Taasisi ya hospitali ya  CCBRT, Wilbrod Slaa (kulia) akimkabidhi picha ya zawadi kwa mchango alioutoa kwa taasisi hiyo Makamu wa zamani wa Rais bodi ya CCBRT, Biharilal Tanna , kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangi

 
 Baadhi ya wakina mama waliopokea vyeti vya kutambua mchango wao kwa CCBRT wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangina Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangi

 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye tafrija ya CCBRT usiku wa jana

 Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wapili kushoto waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa bodi ya Taasisi ya hospitali ya CCBRT, Wilbrod Slaa (wapili kulia waliokaa) Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Dkt. Brenda Msangi na Makamu wa Rais wa zamani wa bodi hiyo, Biharilal Tanna na wadau mbalimbali kwenye tafrija ya maadhimisho ya miaka 25 ya taasisi ya  hospitali ya CCBRT  jijini Dar es Salaam jana.

Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na  wafanyakazi wa Taasisi ya hospitali ya CCBRT jana kwenye tafrija ya maadhimisho ya miaka 25 ya taasisi hiyo.

WATU 250 KUHUDHURIA MKUTANO WA SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UUNIFU NCHINI LEO

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Amos Nungu katikati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusiana na mkutano wa kubadilishana uzoefu wa  Masuala ya Sayansi Techinolojia  na Uzoefu unaoanza leo hapa nchini kulia ni Ofisa Mtafiti wa Costech, Neema Tindamanyire na kushoto ni Meneja Sayansi Hai kutoka Costech, Hulda Gideon.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimzikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Amos Nungu.

WAGENI 250 kutoka nchi mbalimbali duniani wamewasili hapa nchini kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa viongozi wa Baraza la Sayansi Kanda ya Afrika kwa lengo la kubadilishana uzoefu pamoja kujifunza kuhusu masuala ya sayansi, teknolojia na ubunifu.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Dk. Amos Nungu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu mkutano huo ambao unaoanza leo.

Alisema mada inayotawala mkutano huo ni sayansi wazi na shirikishi katika utafiti na ubunifu wa maendeleo, hivyo Costech kama mratibu wa masuala hayo ya utafiti, teknolojia na ubunifu imepewa dhamana ya kuandaa mkutano huo.

“Kupitia mkutano huu tutabadilishana uzoefu pamoja na kujifunza kutoka kwa kila mmoja, pia kujenga mahusiano pale inapowezekana,” alisema Dk. Nungu.

Dk. Nungu alisema, Tanzania ipo kwenye sera ya uchumi wa viwanda hivyo katika mkutano huo watajifunza mambo mengi kutoka kwa wengine kwa kuwa nchi 16 za Afrika zinashiriki pamoja na mataifa makubwa karibu kila bara.

Katika mkutano huo, Dk. Nungu alisema Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu, Dk. Joyce Ndalichako atafungua.

Kwa upande wa Meneja Sayansi Hai kutoka Costech, Hulda Gideon alisema mkutano huo utazungumzia sayansi wazi kwa maana kuwa mawazo yote yanayotolewa yawe shirikishi, andiko pamoja na utafiti unaofanyika kuwa wazi na mwishoni taarifa ziwe wazi kwa ajili yaw engine kuzitumia.

Alisema sayansi wazi haiangali maandiko tu ya utafiti bali hata vifaa vinavyotumika ambavyo vinaweza kusaidia wengine ambao hawana vifaa hivyo.

Alisema Tanzania ni mojawapo ya nchi zinazokuza sayansi nayo imeshiriki kwenye utafiti na data katika sekta ya afya na maliasili ambavyo kwa Tanzania inaongelewa kuwa ina viumbe hai wengi.

“Inabidi sayansi ilivyofanyika ikatumika kuwaambia watu kuwa kuna utafiti huo umefanyika. Hata kwa upande wa dawa unakuta mimea mingi ipo kwa nchi za Afrika ambazo ni maskini utafiti ukifanyika huku kama hakuna uwazi, yale maandiko yatabakia nchi zilizoendelea wataingia kwenye viwanda vyao na kuzalisha dawa halafu sisi tunasubiri kununua dawa kutoka kwao.

“Lakini kama tukiwa ile sayansi wazi watajua kuwa dawa zile pamoja na kuwa zimetengenezwa kwenye viwanda vya nje lakini zilitokea Afrika ni rahisi kushare ile keki iliyotokana na dawa hizo,” alisema.

Alisema hiyo ndiyo maana halisi ya kuhamasisha Tanzania kuingia kwenye michakato yote ya kuwa na sayansi hai inayokuwa na uwazi zaidi.

“Lengo kubwa la kuwa na sayansi hai ni kukuza sayansi yenyewe, kama Afrika au nchi zinazoendelea hatujafika kule lakini tukiifanya ile sayansi ikawa wazi ina maana wale wenzetu kule nje wanachokifanya na sisi tutakijua, tukikijua hatuna haja ya kuanza kitu upya tutatumia vile ambavyo wamevifanya na kuvileta huku kwetu kwa ajili ya kuviendeleza,” alisema.

 Sayansi wazi pia inasaidia kupunguza gharama hivyo mtu anayefanya utafiti wa aina hiyo nchini hatakuwa na haja ya kununua kifaa kinachohitajika ikiwa ni pamoja na kukuza ushirikiano baada ya kujua mwingine ana nini au anafanya nini.

Hata hivyo Ofisa Mtafiti wa Costech, Neema Tindamanyire alisema hadi kufikia jana nusu ya wageni walioalikwa walikuwa wameshafika.


Katika mkutano huo takribani sh. milioni 500 zitatumiwa na wageni hao kama gharama za kwenye hoteli, vyakula na huduma mbalimbali watakazozipata nchini ikiwa ni pamoja na kutembelea vivutio mbalimbali

KAMPUNI YA KIMATAIFA YA ELIMU NA SAYANSI YAONESHA NIA YA KUSHIRIKIANA NA ZANZIBAR KUIMARISHA ELIMU

$
0
0

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Ujumbe wa Viongozi wa Kampuni ya Kimataifa ya Elimu na Sayansi kupitia Mfumo wa Kisasa wa Mtandao wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano {VM Ware} kutoka California Nchini Marekani.Kulia ya Balozi Seif ni Mkurugenzi Mkurugenzi Muandamizi wa Mipango na Mikakati anayesimamia Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Kampuni hiyo Bwana Thomas Mackay, Msaidizi wake Bwana Kamau na Bibi Evan.Kushoto ya Balozi Seif ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanziar Mh. Simai Mhamed Said, Naibu Katibu Mkuu Nd. Abdullah Mzee Abdulla na Mkurugeni wa Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ya Wizara ya Elimu Nd. Omar Said Ali.Picha na – OMPR – ZNZ.



Kampuni ya Kimataifa ya Elimu na Sayansi kupitia Mfumo wa wa Kisasa wa Mtandao wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano {VM Ware} kutoka California Nchini Marekani tayari imeonyesha nia ya kushirikiana na Zanzibar katika kuimarisha Sekta ya Elimu Nchini.

Mkurugenzi Muandamizi wa Mipango na Mikakati anayesimamia Elimu, Sayansi na Teknolojia wa Kampuni hiyo Bwana Thomas Mackay alitoa kauli hiyo wakati akibadilishana mawazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar.

Bwana Thomas Mackay alisema Taasisi yake imejitolea kusaidia nguvu za Kitaaluma katika Miradi ya Elimu kutokana na jitihada kubwa zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali katika uimarishaji wa Miundombinu ndani ya Sekta hiyo muhimu kwa Maendeleo ya Taifa lolote Duniani.

Alisema mazingira ya maumbile ya Watu wa Visiwa vya Zanzibar yaliyojaa ukarimu yameushawishi Uongozi wa Kampuni hiyo kujitolea kusomesha mbinu na mikakati itakayowezesha kuibua kwa fursa za Taaluma kwa Vijana na Wasomi wa Zanzibar kupata mwanga zaidi wa hatma yao ya baadae katika mfumo wa Kisasa wa Teknolojia.

Bwana Thomas Mackay alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Taasisi hiyo inayokwenda Kitaalamu zaidi imekuwa ikitoa mafunzo katika Mataifa mbali mbali Ulimwenguni na mkakati wao kwa sasa ni kuona fursa hiyo adhimu inawanufaisha Wananchi wa Zanzibar.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema wazo la Uongozi wa Kampuni ya VM Ware limekuja wakati ambao Zanzibar imeshaanza hatua za awali katika kuhakikisha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano inawafikia Wananchi walio wengi Mjini na Vijijini.

Balozi Seif alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Taasisi za Kitaifa na Kimataifa inaendelea kujenga miundombinu ya Madarasa ya masomo ya Mtandao wa Teknolojia katika ngazi ya Msingi ili kuwarahisishia ufahamu wa awali Wanafunzi wake wa kujiandaa na Taaluma hiyo waingiapo Elimu ya juu.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisema mfumo wa sasa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano unaotumika Duniani umekuwa ukirahisisha kazi za Mwanaadamu katika harakati zake za Kimaisha na kuifanya Dunia hivi sasa kuwa Kiganja badala ya Kijiji.

Mapema Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mheshimiwa Simai Mohamed Said alisema Teknolojoa ya Habari na Mawasiliano inayobadilika kwa kasi Duniani kamwe haiwezi kuiacha nyuma Sekta ya Elimu ambayo ndio mzizi wa Maendeleo yoyote.

Mh. Simai alisema katika kuthamini ujio wa Viongozi hao wa Kampuni ya VM Ware ya Marekani Vikao maalum vimendaliwa vitakavyo washirikisha Watendaji wa Masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Taasisi za Umma na zile Binafsi kujadili fursa zitakazopatikana kutokana na ujio huo.

Stanbic Bank hosts 5th Zanzibar Paddling Challenge

$
0
0
 A paddler crossing the Indian ocean during the Zanzibar paddle race held over the weekend in starting from Dar Yatch Club to Zanzibar, Tanzania. This epic paddle was founded in 2015 and sponsored by Stanbic Bank Tanzania with the aim of promoting beach tourism in the country.
Paddlers and TanzaCat sailors celebrating after finishing the Zanzibar paddle race held over the weekend, starting from Dar Yatch Club to Zanzibar, Tanzania. This epic paddle was founded in 2015 and sponsored by Stanbic Bank Tanzania with the aim of promoting beach tourism in the country.

Vodacom Tanzania imeongeza pato lake kwa asilimia 6.5 katika kipindi cha miezi sita.

$
0
0
Vodacom Tanzania PLC imerekodi ongezeko la mapato kwa asilimia 6.5% kufikia shilingi bilioni 528,962 kwa kipindi cha miezi sita.

Ongezeko hili limechagizwa na ukuaji wa wateja wetu wa msingi, ukuaji wa mapato ya M-Pesa na data za simu pamoja na uwekezaji uliolenga kupanua mtandao wetu wa data na kusambaza huduma ya 4G nchini kote na huduma za kifedha kupitia M-Pesa.

Uwekezaji mkubwa wa shilling bilioni 78.7 katika kupanua mtandao wa 4G na kuongeza ubora wa mtandao pia umechangia kuongeza wateja na kufikia milioni 14.8 ambayo ni ongezeko la asilimia 5.5.

Mkuu wa Uhusiano wa Uwekezaji na Miradi Maalumu Vodacom Tanzania Plc, Robin Kimambo akifafanua kuhusu matokeo ya mapato na matumizi ya nusu mwaka ya kampuni hiyo kwa wahariri wa habari za biashara waliohudhuria wakati wa utangazaji matokeo hayo jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mhariri wa gazeti la The citizen, Mnaku Mbani akiuliza swali kwenye mkutano wa wahariri wa habari za biashara kuhusu matokeo ya mapato na matumizi ya nusu mwaka ya kampuni ya Vodacom Tanzania Plc wakati wa utangazaji matokeo hayo jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki.
Wahariri wakimsikiliza mtoa mada, Robin Kimambo kwenye mkutano wa wahariri wa habari za biashara kuhusu matokeo ya mapato na matumizi ya kampuni ya Vodacom Tanzania Plc wakati wa utangazaji matokeo hayo jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki.

Mkuu wa Mipango na Uwekezaji wa Vodacom Tanzania Plc, Hilda Bujiku akifafanua kuhusu matokeo ya mapato na matumizi ya nusu mwaka ya kampuni hiyo kwa wahariri wa habari za biashara waliohudhuria wakati wa utangazaji matokeo hayo jijini Dar Es Salaam mwishoni mwa wiki.

SERIKALI YAOKOA BILIONI 34 /- KWA KUTUMIA MFUMO WA UNUNUZI KWA NJIA YA KIELETRONIKI-KATIBU MKUU

$
0
0
SERIKALI imesema imeokoa wastani wa Sh.bilioni 34 katika miaka mitano ya kwanza kutokana na kutumia mfumo  wa ununuzi kwa njia ya kieletroniki.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam leo Novemba 11,2019,  Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali Doto James amesema kwa kuzingatia mfumo huo imeiagiza Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) kuhakikisha ifikapo Desemba 31 mwaka huu kuwa taasisi zote za ununuzi nchini ziwe zimeungwa katika mfumo wa ununuzi kwa njia ya kieletroniki na kuanza kuutumia bila kisingizio chochote.

Katibu Mkuu James amesema kuwa kuzingatia kwa fedha zitumikazo katika utekelezwaji wa miradi ya Serikali kwa kiasi kikubwa hutumika kupitia mifumo ya ununuzi wa umma na kwamba jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanyika kuliimarisha eneo hilo ili kuiwezesha Serikali kupata thamani halisi ya fedha zinazotumika kupitia  ununuzi wa bidhaa.

Amesema taasisi za  umma  ambazo tayari  zimeunganishwa  katika mfumo wa ununuzi kwa njia ya kieletroniki ni jumla ya taasisi nunuzi 418 kati ya taasisi 540 sawa na asilimia 77.4 ya taasisi nunuzi zilizopo nchini zimeunganishwa na mfumo huo.

James amesema tangu kuanza kwa mfumo huo kumeongeza ushindani kwenye michakato  ya ununuzi ,kuongeza ufanisi na hivyo kupunguza muda unaotumika katika michakato ya zabuni  pamoja kuongeza uwazi hivyo kupunguza vitendo vya rushwa.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) Mhandisi  Leonard Kapongo amesema baada ya kupewa maagizo na Serikali waliingia kazini kuongeza katika kutoa mafunzo kuhusiana na mfumo kwa maafisa  Ununuzi na Tehama wa Taasisi za Umma.

Amesema hawataruhusu taasisi za umma kufanya nunuzi nje ya mfumo wa ununuzi kwa njia ya kieletroniki kufikia Januari 31 mwaka ujao.

Mhandisi Kapongo amesema taasisi ambazo hazjaunganishwa wajiunge ikiwa ni pamoja na kugharamia mafunzo maakumu ya namna ya kutumia mfumo wa ununuzi kwa njia ya kieletroniki.

 Pichani kati ni Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali-Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James akizungumza na Waandishi wa Habari jana jijini Dar,kuhusu kuanzishwa kwa mfumo wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya Kielektroniki (TANePS)  ikiwa pamoja na Utekelezaji wa Maagizo ya Waziri wa Fedha kuhusu matumizi ya mfumo huo.Pichani kulia ni Mwenyekiti wa Bodi  wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA),Balozi Dkt Matern Lumbanga na kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA),Mhandisi Leonard Kapongo.
 Katibu Mkuu na Mlipaji Mkuu wa Serikali-Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James akiwaonesha Waandishi wa Habari moja ya Nyaraka iliyokuwa na maelekezo ya uanzishwaji mfumo wa Ununuzi wa Umma kwa njia ya Kielektroniki (TANePS),ambapo amesema Serikali imeagiza Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA) ifikapo Disembe 31,2019 ihakikishe taasisi zote za ununuzi hapa nchini ziwe zimeungwa katika mfumo huo na kuanza kuutumia bila kisingizio chochote. 
 Waandishi wa habari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano huo.

Airtel Africa yaingia ushirikiano na Mastercard kuwezesha wateja wa Airtel Money kufanya malipo kidigitali

$
0
0
• Wateja wa Airtel Money, hata wale ambao hawana akaunti za benki kwa sasa wanaweza kufanya malipo ya kimtandao/kidigitali wakiwa popote duniani kwa kutumia Airtel Money virtual card

Kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania  imetangaza kuingia ushirikiano na Mastercard kwa kuzindua huduma ya Airtel Money Mastercard Virtual card ambayo itawawezesha wateja wa Airtel Money kulipia huduma, bidhaa, applikesheni, hoteli, gharama za usafiri pamoja na kulipia huduma za mtandao (kama Netflix) wakati wowote kidigitali zaidi kupitia watoa huduma wote waliounganishwa au wanaokubali malipo kwa Mastercard. Wateja wa Airtel Tanzania wataweza kufurahia huduma hii ya kipekee kutokana na usalama na uhakika kwa kufanya malipo kidigitali popote kupitia ushirikiano huu.

Vile vile, wateja wa Airtel Money wataweza kufanya malipo binafsi kwa watoa huduma popote kwa kutumia huduma ya Quick Response (QR) kwa wauzaji wa bidhaa mbalimbali au watoa huduma kupitisha QR akaunti ya Airtel Money au kuandika namba ya wakala/mtoa huduma anaekubali malipo kwa Mastercard .

Uzinduzi wa huduma hii unalenga kuendelea kukuza sekta ya fedha hapa Tanzania huku taarifa za hivi karibuni za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zikionesha kuwa, nchini Tanzania watumiaji wa huduma za fedha kupitia mitandao ya simu za mkononi wanaongezeka ambapo hadi kufikia mwezi machi mwaka huu wamefikia takribani milioni 22 wakiwa wamefanya miamala inayofikia thamani ya zaidi ya TZS trilioni 8. 

Vile vile, kwa miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na maendeleo makubwa katika baadhi ya huduma kama utumaji wa fedha kupitia mitandao mbalimbali kutoka ule wa zamani uliokuwa ukifanyika kwa kumtuma mtu ili kusafirishae fedha ndani au nje ya nchi, ubunifu umefanyika hata kwenye kununua muda wa maongezi kwa mtandao na hivyo kufanya huduma ya fedha wa njia ya mtandao kuwa moja ya huduma yenye tija katika sekta ya kifedha nchini.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua huduma hiyo ya Airtel Money Mastercard Virtual card, Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchuda alisema “Kwa sasa tunaishi kwenye dunia ambapo malipo yanafanyika kila sekunde. 

Ushirikiano wetu na Mastercard unatufanya tuendelee kukamilisha dhamira yetu ya kutoa huduma na bidhaa ambazo ni za kipekee na zenye unafuu zaidi ili kukidhi mahitaji ya kila siku ya wateja wetu.’ Alisema Nchunda huku akiongeza kuwa uzinduzi wa Airtel Money Mastercard Virtual card unaonyesha ni kiasi ngani Airtel inaunga mkono juhudi za Serikali za kurahishisha na kupanua sekta na huduma za kifedha hapa nchini.

Airtel Money Mastercard inamuwezesha mteja wa Airtel kufanya malipo kwa urahisi kwenye sehemu zote ambazo Mastercard inakubalika hata kama mteja huyo hana akaunti ya benki au kadi ya malipo. Ili mteja wa Airtel Money aweze kupata Airtel Money Mastercard Virtual card piga *150*60# chagua 6 kisha 1 na ufuate maelekezo kuapata Airtel Money Mastercard Yako. Pale Airtel Money Mastercard inapokamilika pia inakuwa tayari kwa malipo ya kupitia mtandao.

Kwa upande wake, Makamu Rais na Mkurugenzi wa Biashara Afrika Mashariki wa Mastercard Adam Jones alisema “Ushirikiano wetu na Airtel utarahishisha huduma za kifedha kwa mamilioni ya Watanzania. Kwa kupitia ushirikiano wetu huu wa huduma za kidigitali, nia yetu ni kuendelea kuboresha utoaji huduma kiditali zaidi kwa kuzingatia urahisi, unafuu na usalama ili kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kidigitali. 

Mastercard ni njia ya malipo kwa mtandao inayotumia teknolojia ya kisasa kwa kushirikiana na washirika wake ukanda wa kati pamoja na bara la Afrika kwa lengo la kumfanya mteja kufurahia huduma za kimataifa za malipo”.

“Huduma za fedha kwa mitandao ya simu imesaidia sana kupuguza gharama za miamala na kuongeza ukuaji wa uchumi kwa kuondoa gharama za kusafiri mpaka kwenye matawi ya benki ili kufanya miamala ya malipo. Airtel Money Mastercard sasa itapanua wingo wa matumizi ya akaunti za Airtel Money kufanya malipo kwa njia ya mtandao, alisema Jones.

Airtel Money Tanzania kwa sasa imeunganisha kwa zaidi ya watoa huduma 1000 pamoja na taasisi za kifedha zaidi ya 40 kwa kumfanya mteja kutoa na kuweka fedha. Vile vile, Airtel inazidi kutanua wigo wake hapa nchini kwa kuwa na Zaidi ya Airtel Money branch 80ambazo zinatoa huduma na bidhaa za Airtel.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Selcom Sameer Hirji alisema taasisi yake imejipanga vyema na kwakudhihirisha hilo kwa inaendelea kuwekeza kwenye miundo mbinu na kujiweka kwenye sehemu nzuri kwenye soko ili kuendelea kutoa huduma ya malipo ya uhakika kwa washirika wake kama Mastercard na Airtel ambao dhamira zao ni kutoasuluhisho kwenye huduma za malipo. 

“Selcom imekuwa moja ya taasisi imara kwenye huduma ya malipo kwa zaidi ya muongo mmoja na kutoa mageuzi makubwa kwenye malipo ya kimtandao hapa nchini na wakati tukiendelea kukua tunakua pamoja na washirika wetu kwenye kurahshisha malipo ykidigitali.

“Matokeo ya uzinduzi huu wa Airtel Money Mastercard ni mafanikio makubwa sana kwa kuwa utarahisisha mambo mengi kwa wateja wa Airtel Money”.alimaliza kusema Sameer.
Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchuda akiongea leo jijini Dar es Salaam wakati wa kuingia ushirikiano na Mastercard kwa kuzindua huduma ya Airtel Money Mastercard Virtual card ambayo itawawezesha wateja wa Airtel Money kulipia huduma, bidhaa, applikesheni, hoteli, gharama za usafiri pamoja na kulipia huduma za mtandao wakati wowote kidigitali zaidi kupitia watoa huduma wote waliounganishwa au wanaokubali malipo kwa Mastercard. 
Makamu Rais na Mkurugenzi wa Biashara Afrika Mashariki wa Mastercard Adam Jones wakati wa kuingia ushirikiano na Mastercard kwa kuzindua huduma ya Airtel Money Mastercard Virtual card ambayo itawawezesha wateja wa Airtel Money kulipia huduma, bidhaa, applikesheni, hoteli, gharama za usafiri pamoja na kulipia huduma za mtandao wakati wowote kidigitali zaidi kupitia watoa huduma wote waliounganishwa au wanaokubali malipo kwa Mastercard. 
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akisisitiza jambo wakati wa kuingia ushirikiano na Mastercard kwa kuzindua huduma ya Airtel Money Mastercard Virtual card ambayo itawawezesha wateja wa Airtel Money kulipia huduma, bidhaa, applikesheni, hoteli, gharama za usafiri pamoja na kulipia huduma za mtandao wakati wowote kidigitali zaidi kupitia watoa huduma wote waliounganishwa au wanaokubali malipo kwa Mastercard .

Wateja watano wajishindia bodaboda na Ibuka Kidedea na NBC Malengo

$
0
0

Meneja Masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Alina Maria Kimaryo (wa pili kushoto), akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo wakati NBC ikichezesha droo ya kwanza ya kampeni  ya akaunti ya Malengo ambapo wateja watano walijishindia zawadi ya bodaboda  kila mmoja.  Wengine pichani ni maofisa wa benki hiyo na kulia kabisa ni mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha .
Meneja Masoko wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Alina Maria Kimaryo (mbele kulia), akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati  NBC ikichezesha droo ya kwanza ya kampeni  ya akaunti ya Malengo ya NBC ambapo wateja watano walijishindia zawadi ya pikipiki aina ya Yamaha kila mmoja.  Washindi wa leo ni;  Augustine Hatari kutoka Pwani, Williumu Pendaeli Isack wa Moshi,  Scholastica Peter Yamawasa, Honest Christopher Kimaro na  Daudi Majani wote kutoka Dar es Salaam.


WATEJA Watano wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) wameibuka washindi wa bodaboda mpya aina ya Yamaha katika droo ya kwanza ya kampeni ya “IBUKA KIDEDEA NA NBC” kupitia akaunti ya Malengo ya benki hiyo kongwe hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kwenye droo ya kwanza ya kampeni hiyo iliyoanza mwezi wa Oktoba, Meneja Masoko wa benki hiyo, Alina Maria Kimaryo alisema kwamba akaunti ya malengo inampa mteja njia rahisi ya kuweka akiba kidogo na kupata faida kubwa kila mwezi.

“kwenye akaunti hii ya malengo kila Tsh 100,000 atakayoweka mteja kwenye akaunti hii inampa nafasi ya kushida zawadi kemkem ikiwemo bodaboda ambapo leo droo ya kwanza itashuhudia wateja hawa watano wakipata zawadi zao,” alisema Kimaryo.

Aliongeza kwamba katika kipindi chote cha kampeni bodaboda tano aina ya Yamaha zitatolewa kila mwezi na safari tatu za kwenda kufanya utalii Serengeti na safari tano za kwenda Seychelles mwezi wa Disemba na washindi wanaruhusiwa kwenda na mtu mmoja kwenye safari hizo.

“ukiwa na akaunti ya NBC malengo unapata faida nyingi ikiwemo ya kuhifadhi fedha kwa ajili ya kutimiza malengo na ndoto zako pamoja na mambo mengine ya kupata riba ya hadi asilimia 7 ya pesa uliyoweka kila mwezi,’ alisisitiza Kimaryo.

Washindi kwenye droo ya jana walikuwa ni Augustine Hatari kutoka Pwani, Daudi Majani, Dar es Salaam, Williumu Pendaeli Isack, Moshi Kibololoni, Scholastica Peter Yamawasa, Dar es Salaam, na Honest Christopher Kimaro wa Dar es Salaam.

Katika kampeni hii wateja watakao ongeza salio kwa kiasi Tsh milioni moja kwenye akaunti ya Malengo watapata nafasi ya kushinda zawadi kuu ya TOYO na jumla ya TOYO tatu zitatolewa kwenye kampeni hiyo ya “IBUKA KIDEDEA NA NBC MALENGO”

SBL mdhamini mkuu mashindano ya Waitara Gofu 2019

$
0
0
Meneja masoko wa SBL Anitha Msangi akizungumza na waandishi wa habari leo wakati wa kutangaza udhamini wa kampuni ya bia ya Serengeti kwenye mashindano ya Waitara Gofu ya mwaka 2019 yanayotarajiwa kufanyika siku ya jumamosi viwanja vya Lugalo jijini Dar es salaam. Wengine ni Mwenyekiti wa klabu ya Lugalo Gofu Brigedia Generali Mstaafu, Michael Luwongo (katikati) na Nahodha wa klabu ya Gofu ya Lugalo , Kapt. Japhet Masai
Meneja masoko wa SBL Anitha Msangi akipeana mkono wa pongeza na Mwenyekiti wa klabu ya Lugalo Gofu Brigedia Generali Mstaafu, Michael Luwongo mara baada ya kutangaza udhamini wa kampuni ya bia ya Serengeti kwenye mashindano ya Waitara Gofu ya mwaka 2019 yanayotarajiwa kufanyika siku ya jumamosi viwanja vya Lugalo jijini Dar es salaam. Wengine ni Nahodha wa klabu ya Gofu ya Lugalo , Kapt. Japhet Masai (kulia) na Afisa Utawala wa klabu hiyo Luteni. Samwel Mosha.



Jumla ya wachezaji 120 wa gofu kutoka sehemu mbali mbali hapa nchini, wanatarajiwa kuchuana vikali mwishoni mwa wiki katika mashindano ya Waitara Gofu ya mwaka 2019 yanayodhaminiwa na kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL).

Mashindano hayo ya siku moja, yatafanyika siku ya Jumamosi katika viwanja vya Gofu vya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Akitangaza udhamini huo jijini Dar es Salaam, Meneja masoko wa SBL Anitha Msangi aliwaambia waandishi wa habari kuwa udhamini wa SBL kwenye mashindano hayo maarufu, unalenga kuendeza mchezo wa gofu hapa nchini.

“Kampuni ya SBL kupitia bia yake pendwa ya Serengeti Premium Lager inayofuraha kuwa mdhamini mkuu wa mashindano ya gofu ya Waitara ya mwaka huu. Udhamini huu unaonyesha nia yetu ya dhati ya kuendeleza michezo hapa nchini,” alisema Anitha.

Kupitia bia ya Serengeti Premium Lager, kampuni ya SBL ni mdhamini mkuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars Serengeti na pia inadhamini ligi ya taifa ya wanawake kupitia bia yake ya Serengeti Lite.

Kwa upande wake, mwenyekiti wa klabu ya Gofu ya Lugalo Brigedia Jenerali mstaafu Michael Luwongo aliishukuru kampuni ya SBL kwa udhamini huo na kuyataka makampuni na taasisi nyoingine kuiga mfano wa SBL na kujitokeza kusaidia michezo wa gofu nchini.

“Tunaishukuru sana kampuni ya SBL kwa mchango wake kwenye kusaidia maendeleo ya michezo hapa nchini na hususani gofu. SBL imekuwa mdhamini mkubwa wa mashindano haya,” alisema.

Mashindano ya Waitara Golf hufanyikja kila mwaka yakilenga kutambua mchango wa Genelrali mstaafu George Waitara aliyekuwa mkuu wa majeshi kwa kuanzisha klabu ya golf ya Lugalo.

Klabu ya Golf ya Lugalo ilianza mwaka 2006 kutokana na mchango mkubwa wa Waitara ambo pia uliendelezwa na Generali Davis Mwamunyange ambaye alimfuatia baada ya kustaafu.

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YA RAIS MSTAAFU MHE. MKAPA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli akizindua kitabu cha Historia ya Maisha ya Rais Mstaafu wa
Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa akishuhudiwa na Rais wa
Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Marais wastaafu Alhaj Ally Hassan
Mwinyi, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Finland nchini Tanzania
Mhe. Antila Sinikka katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne Novemba 12, 2019
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William akihutubia
wakati wa uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Maisha yake katika Ukumbi
wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo
Jumanne Novemba 12, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli baada ya kuzindua kitabu cha Historia ya Maisha ya Rais
Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa akiwa na Rais waZanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Marais wastaafu Alhaj Ally Hassan
Mwinyi, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne Novemba
12, 2019





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akimpongeza kwa hotuba nzuri Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe.
Benjamin William Mkapa wakati wa uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya
Mhe. Mkapa huku akishuhudiwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed
Shein na Marais wastaafu Alhaj Ally Hassan Mwinyi, Dkt Jakaya Mrisho
Kikwete pamoja na Balozi wa Finland nchini Mhe. Antila Sinikka katika
Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam
leo Jumanne Novemba 12, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiongoza kunyanyua glasi na kumtakia maisha marefu Rais Mstaafu wa
Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa katika kuadhimisha siku ya
kuzaliwa kwake wakati wa sherehe za uzinduzi wa kitabu cha historia ya
Maisha ya Mhe. Mkapa. Wengine hapo meza kuu ni Rais wa Zanzibar Dkt.
Ali Mohamed Shein na Marais wastaafu Alhaj Ally Hassan Mwinyi, Dkt
Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Anna Mkapa katika Ukumbi wa Mikutano waKimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne Novemba
12, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin
William Mkapa baada ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Mhe. Mkapa.
Wengine ni Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Marais wastaafu
Alhaj Ally Hassan Mwinyi, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Balozi
wa Finland nchini Mhe. Antila Sinikka na Mama Anna Mkapa pamoja na
maafisa wa Ofisi Binafsi ya Mhe. Mhe. Mkapa katika Ukumbi wa Mikutano
wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne
Novemba 12, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin
William Mkapa baada ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Mhe. Mkapa
wakiwa na Marais wastaafu Alhaj Ally Hassan Mwinyi na Dkt Jakaya
Mrisho Kikwete katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne Novemba 12, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin
William Mkapa, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dkt. Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Spika wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai na Marais wastaafu Alhaj
Ally Hassan Mwinyi na Dkt Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuzindua
kitabu cha Historua ya Maisha ya Mhe. Mkapa katika Ukumbi wa Mikutano
wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne
Novemba 12, 2019 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin
William Mkapa baada ya uzinduzi wa Kitabu cha Historia ya Mhe. Mkapa.
Wengine ni Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Marais wastaafu
Alhaj Ally Hassan Mwinyi, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Balozi
wa Finland nchini Mhe. Antila Sinikka na Mama Anna Mkapa na familia ya
Mhe. Mkapa katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumanne Novemba 12, 2019

GSM to address nations’ thirst for good quality furnishing

$
0
0

Dar es Salaam based GSM group of companies, is set to launch its biggest furniture store dubbed ‘GSM HOME’, aimed at addressing the existing gaps in the market in supply of wide range of good quality furniture’s.

Occupying about 1,200 square feet space, the new store is located along Mwai Kibaki road in Mikoche B area and is expected to cater for growing needs of office and home furniture in the country.

Speaking at HQ in Dar es Salaam GSM group of Companies Chief Commercial Officer Mr. Allan Chonjo said, the plan to unveil of the new store is the company’s long-time dream that will come true.

“We are very excited that soon we will launch this great store in Dar es Salaam. In addition to offering customers a convenient shopping experience, GSM HOME will have a number of contemporary furniture including shelving, sofas, sideboards, coffee tables, dining furniture, beds & bed room furniture, wardrobes & a wide range of cash N carry items everything to make your house perfect,” he said.

Chonjo added “And for the Office, we have a large selection of fabulous office furniture including reception area, waiting area, chairs, ergonomics, tables, conferences, workstations, storage and filing cabinets,”

The CCO noted that, the contemporary furniture collections which will be found at GSM HOME are carefully chosen for value and practicality as well as design; with the ethos that good design must work as well as being great to look at adding that a considerable amount of time has been spent looking for just the right.

He urged people to be prepared to visit the new store shortly after the lunch which will be this month and enjoy new furniture shopping experience adding that the store has everything to cater for their furniture needs.

“When choosing furniture, it’s important to pick timeless, functional pieces that fit your space and budget! Choose from contemporary and modern, traditional or a bit of both in a unique eclectic mix – there are no rules, so don’t be afraid to get creative and buy furniture you love,” he said.

We have launched our two shops in Mlimani City as well as Pugu Mall, and this 3rd one will be our iconic version aimed at driving user experience. We have packages for both individuals as well as corporate clients – with facilities to pay by card so you don’t have to carry a lot of cash with you for security purpose.

MRADI WA KIWANDA KIKUBWA CHA DAWA TANZANIA WAVUTIA WAWEKEZAJI WA KIMKAKATI AFRIKA KUSINI

$
0
0

Na Benny Mwaipaja, WFM, Johannesburg 

Tanzania imewasilisha miradi 13 ya Kipaumbele kwa wawekezaji wa kimkakati wanaoshiriki kongamano la Jukwaa la Uwekezaji Mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango anayemwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Jukwaa hilo, amesema Mradi wa Ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza dawa mchanganyiko kitakachogharimu zaidi ya dola za Marekani milioni 408 umewavutia wawekezaji wengi.

Amewataja wawekezaji waliovutiwa na mradi wa ujenzi wa kiwanda hicho kitakachojengwa Kibaha mkoani Pwani, kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya aina 230 za dawa kwamba wanatoka nchi za Korea, Uturuki, taasisi za fedha za kimataifa na kwamba hadi kufika mapema mwakani (2020) mwekezaji mmoja au zaidi watakuwa wamepatikana kwa ajili ya kuanza kujenga mradi huo.

"Pamoja na kupunguza tatizo la uhaba wa dawa na dawa bandia zinazoingizwa nchini, kiwanda hiki pia kitazalisha ajira kwa watanzania" alisema Dkt. Mpango. 

Dkt. Mpango amesema Serikali inatenga zaidi ya sh bilioni 230 kwenye Bajeti kila mwaka kwa ajili ya kununua dawa huku mahitaji halisi ya dawa nchini ni takriban shilingi trilioni 1.4 ndio maana mkazo umewekwa kwenye ujenzi wa kiwanda hicho kitakachotatua changamoto za upatikanaji wa dawa nchini.

Alifafanua kuwa miradi mingine 12 iliyowasilishwa mbele ya wawekezaji hao iko katika hatua za maandalizi na iko katika sekta za Nishati ya umeme unaotumia nguvu ya maji, viwanda vya kuchakata pamba ili kuiongezea thamani na hatimaye kuzalisha nguo, ambavyo vinaendana na dhamira ya Serikali ya ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake, Meneja Miradi kutoka Bohari ya Dawa ya Taifa Mhandisi Fredrick Pondamali ameeleza kuwa usanifu wa mradi huo wa kiwanda cha kuzalisha dawa mchanganyiko umekamilika pamoja na viwanda vingine viwili zaidi vinavyotafutiwa wawekezaji.

Alisema kuwa mradi wa kiwanda cha kuzalisha dawa ulichaguliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa lengo la kuupeleka mbele ya wawekezaji ili uweze kupata fedha kutokana na umuhimu wake kwa Tanzania na nchi jirani.

Jukwaa hilo la Uwekezaji Afrika linalofanyika kwa mwaka wa pili sasa limeandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB kwa kushirikiana na wadau wake mbalimbali ambapo mwaka huu limevuta wawekezaji wa kimkakati zaidi ya 4000 kutoka kila pembe ya dunia ikiwa na lengo la kuongeza uwekezaji kwenye ujenzi wa miundombinu ili kuchochea kasi ya mabadiliko ya kiuchumi katika nchi za Bara la Afrika.
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (kulia) akizungumza na Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania, Dkt. Alex Mubiru, kando ya Kongamano la Jukwaa la Wawekezaji Afrika (Africa Investment Forum), unaoendelea Mjini Johannesburg, Afrika Kusini
 Msimamizi wa Dawati la Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Said Nyenge (wa pili kulia) akimweleza Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika Dkt. Alex Mubiru (kulia) kuhusu miradi ya kipaumbele iliyowasilishwa na Serikali kwenye Kongamano la Jukwaa la Uwekezaji Afrika), linalofanyika Johannesburg, Afrika Kusini. Kulia ni Bw. Frank Sanga kutoka AfDB na wa pili kulia ni Mchumi kutoka Wizara ya Fedha na Mipangp Bw. Abel Philip.
 Mkuu wa Idara ya Huduma za Uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Abubakar Ndwata, akimweleza mwekezaji kutoka Kampuni ya Burhani Engineers kutoka Zoher Pirbhai kutoka nchini Kenya kuhusu fursa za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, wakati wa Kongamano la Jukwaaa la uwekezaji la Afrika, linalofanyika Johannesburg nchini Afrika Kusini,
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (aliyeipa mgongo kamera kushoto) akizungumza na wawekezaji wa kimkakati walioonesha nia ya kuwekeza kwenye Mradi wa Kiwanda cha kutengeneza dawa chenye thamani ya dola za Marekani milioni 408, kutoka nchi za Korea, Uturuki na taasisi za fedha za kimataifa, wakati wa Jukwaa la Africa Investment Forum), unaoendelea Mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Baadhi ya wawekezaji wa kimkakati kutoka nchini Korea, Uturuki na Taasisi za Fedha za Kimataifa, wakielezea nia yao ya kuwekeza kwenye Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda kikubwa cha dawa nchini Tanzania unaotarajiwa kugharimu dola za Marekani milioni 408, walipokutana na kufanya kikao na Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango,  Dkt. Philip Isdor Mpango, mjini Johannesburg, Afrika Kusini

VODACOM YABORESHA MFUMO WAKE WA HUDUMA KWA WATEJA

$
0
0

Yatambulisha menyu mpya ya USSD kwa huduma binafsi 

‘Customer Service’ sasa kuitwa ‘VODACARE’ 

Kampuni inayoongoza kwa teknolojia ya mawasiliano nchini, Vodacom Tanzania PLC, hivi karibuni iliadhimisha wiki ya huduma kwa wateja, kwa kutangaza mabadiliko katika mfumo wake wa huduma kwa wateja. Lengo la mabadiliko hayo ni kutoa uhuru kwa wateja wake kupata huduma kwa urahisi pale inapotakiwa.

“Tuna zaidi ya njia nane ambazo mteja anaweza kuzitumia kutufikia na leo tunaiongeza nyingine ambayo itampa mteja fursa ya kujihudumia; hii ni menyu ya USSD, ambayo inapatikana katika simu,” alisema Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Vodacom, Harriet Lwakatare

Kwa kupiga *149*01# mteja anaweza kufanya miamala ya M-Pesa, kuangalia taarifa za matumizi, kupata huduma muhimu kama vile kununua Luku, kuangalia salio, kifurushi cha intaneti na taarifa kuhusu bidhaa mbalimbali za Vodacom. 

“Kwa idadi ya zaidi ya wateja milioni 14, kitengo cha huduma kwa wateja ni kati ya vitengo vyenye kazi muda wote. Vodacom inaendelea kukua kiteknolojia na kuwapa huduma ya kidigitali wateja wake ili kutoa huduma endelevu kupitia njia kadha wa kadha 

“Tunajali mahitaji ya wateja kwa huduma ya haraka na nyepesi. Ndio maana hatujachoka kufanya kazi na kuendelea kuwapa wateja wetu kilicho chaguo kwao na hasa linapokuja suala la kuhitaji msaada. Tuna huduma kwa wateja kwa njia ya kidigitali kupitia WhatsApp, Mitandao ya kijamii, majibizano kwa njia ya sauti (IVR) na mawasiliano ya moja kwa moja. Na sasa tunawaletea menyu ya USSD kwaajili ya huduma binafsi kwa mteja,” alisema Harriet.

Katika hatua nyingine, Harriet alisema kuwa, kuanzia sasa njia zote za huduma kwa mteja zitakuwa zikifahamika kama VODACARE; hii ni ishara kwa Vodacom kuwa imeamua huduma binafsi na za kipekee kwa wateja 

“Tumebadilisha jina la ‘Customer Care’ kwenda ‘VODACARE’ sambamba na maboresho ya kipekee tuliyoyafanya katika kitengo cha huduma kwa wateja ya kwa kiwango cha hali ya juu,” alisema Harriet

Huduma za VODACARE zinapatikana kwa mteja kupiga 100/01 kwenda kituo cha huduma au kwa kutumia mitandao ya kijamii; WhatsApp, mawasiliano ya moja kwa moja au My Vodacom App, menu ya msaada binafsi na katika maduka yote ya Vodashops na kupitia dawati la huduma.

“Aliongezea kusema “Wiki hii Vodacom si kwamba inasherehekea nguvu ya huduma bora kwa wateja kama sehemu ya maudhui yake, ila tunasema kwamba ukiwa na Vodacom matumizi na upatikanaji wa msaada wa huduma kwa mteja ni rahisi wakati wote kupitia katika njia zetu zote za mawasiliano,” alimalizia kusema Harriet

NMB Bank Supports Chato Football Stadium

$
0
0

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Ziwa Abraham Augustino (katikati) akimkabidhi matofali Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhandisi - Charles Kabeho (wa pili kutoka kulia) kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu wa Chato. Kutoka kulia ni mwenyekiti wa halmashauri hiyo - Batholomeo Manunga na wa kwanza kushoto ni Diwani wa kata ya muungano - Johnson Kilimokwanza, hafla hiyo ilifanyika katika ofisi ya za mkuu wa wilaya Chato hivi karibuni
****************************

NMB Bank PLC has dished out construction materials worth 30m/- in support of a football Stadium Construction in Chato District, Geita region.

The materials handed over includes 500 bags of cement and 13,335 bricks promising to look into the possibility of dishing out more support for the project in the future.

In a brief handover ceremony of the materials in Chato over the weekend, the Bank( Manager for the Lake Zone – Abraham Augustino said the support of the materials is the bank’s recognition of the importance of sports in the promotion of good health among the people particularly the youths.

“This is in line with the Bank annual commitment to the public through its Corporate and Social Investment program which has spent over 900m/- for different projects countrywide so far,” said Mr Augustino.

Receiving the items, the Chato District Commissioner – Charles Kabeho and Chato District Executive Director (DED) Eliud Mwaiteleke expressed gratitude to partners like NMB for coming forward to support sports development in the district.

DC Kabeho said the construction of the stadium was part of the initiatives targeting to boost sports development among other strategic programs in the district.

On his side DED Mwaiteleke hinted that the 3000 capacity stadium would lead to bigger sports facilities in the future remaining optimistic giants like Simba, Young Africans, Azam and others may one day use it when on transit for Premier league encounters.

“We are looking forward to hosting football giants like Simba and Young Africans who might decide to camp and train here as they travel for Premier league games. We ask for other supporters to join NMB and help us to complete the construction of this stadium,” he said.

GOBA KUNUFAIKA NA MRADI MKUBWA WA MAJI

$
0
0
 Maji yakititirika baada Mradi wa Maji kibululu Goba kukamilika..wananchi wa maeneo ya kibululu, Goba centre na Lasanza kunufaika na mradi huu.  Kukamilika kwa mradi huu kutanufaisha wananchi 5000 wa kata ya Goba na maeneo jirani

TCRA yapongezwa kwa Kusogeza huduma kwa Wananchi

$
0
0

Wananchi wakipata maelezo kuhusiana na usajili kwa alama za vidole katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
 MKuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman akikabidhiwa kitabu cha Muongozo wa Mawasiliano na Mkuu  wa Kanda ya Zanzibar wa  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  Esuphatie Masinga (katikati) wakati wa Kampeni ya a Mnada kwa Mnada wa TCRA katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.K kushoto ni Mkuu wa Kanda ya Mashariki TCRA Mhandisi Lawi Odiero na watatu kutoka kushoto Afisa Habari Mwandamizi wa TCRA Makao Makuu Mabel Masasi.
 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Hemed Suleiman akiweka alama ya vidole wa ajili ya usajili laini ya simu katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
 Afisa Habari Mwandamizi wa TCRA Makao Makuu Mabel Masasi akimpa maelezo mwananchi wakati wa Kampeni ya Mnada kwa Mnada Katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.
 Afisa Habari wa TCRA Judith Shao akitoa maelezo kuhusiana vitabu vya Muongozo wa Mawasiliano Katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba.

MKUU wa Mkoa  wa Kusini  Pemba Hemed Suleiman ameipongeza  Mamlaka ya  Mawasiliano Tanzania  kwa kuandaa kampeni ya Mnada kwa Mnada kwa kuwa inasaidia  sana wananchi  kupata  huduma  kirahisi

Mkuu huyo  ameyasema hayo wakati wa Kampeni ya Mnada kwa Mnada  wa TCRA katika Viwanja vya Gombani Mjini Pemba  amesema kwa kusogeza huduma zote  muhimu  pamoja  inawarahisishia wananchi kupata huduma jambo  ambalo  linamanufaa  kwa wananchi  na serikali kwa ujumla.

 Hemed Amewataka  wananchi kutumia vema  fursa ya kampeni huyo  inapofika katika  maeneo yao.

Kampeni ya Mnada kwa Mnada Pemba  katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole. 

Wakazi wa wilaya ya Pemba na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni  ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni  na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Idara ya Uhamiaji  kwa ajili  ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Kampeni tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 17 na Zanzibar lengo kuu ni nchi nzima kufikiwa na Kampeni hiyo.

 Mkuu wa TCRA Zanzibar Esuphatie Masinga amesema ni fursa kwa wananchi wa Pemba  kufika katika Viwanja vya Gombani  kwa ajili ya kusajili kwa alama za vidole pamoja na kujiandikisha kupata usajili wa vitambulisho vya Taifa  kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa  mawasiliano. 

Masung amesema kuwa  Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa ya Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa alama za vidole pamoja Huduma zingine za mawasiliano..

Aidha amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika  huduma  za simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi.

Mkuu huyo amesema  kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.

Masinga  amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe  wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole na huduma nyinginezo za Mawasiliano hayo.

Hata hivyo amesema kuwa
 kuna watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kutoa elimu kuhusiana  makosa ya jinai ya matumizi ya simu.

Aidha amesema Kampeni hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha kila mwananchi anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha taifa.
TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili watumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu wanayoipata katika Kampeni mbalimbali.

Hata hivyo amesema kuwa wananchi wajitokeze katika kujisajili kwa alama za vidole kabla ya Desemba 31.

"TCRA  tunawafikia katika wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo" amesema Masinga.

Nae Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili laini za simu kwa alama za vidole na kupata mwamko wa kutumia simu katika maendeleo.

Masasi amesema kuwa Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA kupata elimu na baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika mamlaka husika kupata vitambulisho.

Airtel yazindua Airtel 4G kuboresha mawasiliano nchini

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, George Mathen wakiwa wameshika nembo ya Airtel 4G baada ya uzinduzi wa Airtel 4G Dodoma. kulia ni Mwakilishiwa wa katibu mkuu wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiano Munamu Mulemwa, kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Airtel Bw Lekini Moleli . Airtel imezindua 4G ikiwa ni utekelezaji wa mipango ya uwekezaji iliyowekeana na serikali ili kutoa huduma bora kwa watanzania wote na kendendelea kuijenga Airtel mpya, hafla ya uzinduzi wa Airtel 4G ilifanyika jana jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki akizindua mtandao wa Airtel 4G mkoani Dodoma, Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, George Mathen na wengine katika picha wapili kutoka kulia ni mjumbe wa bodi ya Airtel Lekini Molel, Mwakilishiwa wa katibu mkuu wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiano Munamu Mulemwa, Mbunge wa viti maalum Mariam Ditopile . Airtel imezindua 4G ikiwa ni utekelezaji wa mipango ya uwekezaji iliyowekeana na serikali ili kutoa huduma bora kwa watanzania wote na kendendelea kuijenga Airtel mpya itakayoendelea kutoa gawio kwa wanahisa ikiwemo Serikali, hafla ya uzinduzi wa Airtel 4G ilifanyika jana jijini Dodoma.


  • Airtel yawekeza katika teknolojia ya mawasiliano ya 4G-LTE ili kutoa mawasiliano bora ya huduma za kimtandao
  • Uwekezaji wa Airtel katika teknolojia ya Mawasilaino kutachangia kufikia malengo ya serikali kwa kuchangia ukuaji wa uchumi kidigitali
    Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania leo imetangaza kuzindua huduma ya Airtel 4G ikiwa ni muendelezo wa kupanua wigo wa mtandao wake    nchini ili kutimiza dhamira yake ya kutoa huduma bora za kimtandao kwa wateja wake.

    Akizindua huduma hiyo ya Airtel 4G leo jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki alisema kuwa ni furaha kuona Airtel inatekeleza mipango ya uwekezaji na kuja na  huduma za mtandao wa Airtel 4G  kwa lengo la kukidhi mahitaji ya watanzania wote, hii ni ishara tosha inayoonesha mikakati ya kuijenga Airtel mpya itakayoendelea kutoa gawio kwa wanahisaikiwemo Serikali yetu.

    “Nimefarijika kusikia taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Airtel kwamba Airtel inatekeleza mikakati yao ya uwekezaji wa kuboresha huduma kwa kuanzisha huduma hii ya 4G/LTE ikiwa na wigo mkubwa wa kutoa huduma za mawasiliano, mimi kama Waziri mwenye dhamana ya uwekezaji inanipa ishara nzuri ya matokeo ya mazingira mazuri tuliyoyaweka ili wawekezaji wetu nchini waweze kutekeleza majukumu yao na kulifaidisha taifa, haya yote yanafanikiwa  chini ya uongozi wa Serikali yetu ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dokta John Joseph Pombe  Magufuli.

    “Wote tunatambua, Airtel Tanzania na Serikali yetu waliingia makubaliano mazuri hivi karibuni kwamba serikali yetu iwe na umiliki wa asilimia 49 wa hisa ndani ya Airtel Tanzania, kutokana na makubaliano hayo pia hadi leo Airtel Tanzania imeshailipa serikali jumla ya bilioni 8 kama sehemu ya makubaliano hayo na leo hii Airtel wanatekeleza upanuzi wa mtandao, hii ndio mikakati ya kuijenga Airtel mpya ili kuendelea kuleta tija kwa shughuli za kijamii na uchumi, alisema kairuki

    Mheshimiwa Waziri Kairuki pia alitoa pongezi kwa Airtel kutokana na taarifa yao inayoonesha  kasi ya kusambaza huduma hiyo ya Airtel 4G  katika miji mikubwa takribani 25 ambapo leo wamewasha mtandao wa Airtel 4G mkoani Dodoma. “ Naamini ya kwamba kwa uzinduzi huu wa mtandao wa Airtel 4G, Airtel itazidi kuwa imara sana na sisi serikali tuko tayari kuwaunga mkono kwa hili”. Kairuki aliongeza.

    Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji Airtel Tanzania Bw, George Mathen alisema kuwa uzinduzi huu wa huduma ya Airtel 4G ni moja ya malengo ya muda mrefu ya kuifanya kampuni ya Airtel kuwa na uwezo wa kutoa huduma bora ukizingatia sasa ni ulimwengu wa kidigitali.
    “ili mteja aweze kutumia huduma ya Airtel 4G anatakiwa kuwa na Simu ya Smatifoni yenye uwezo wakupokea mawimbi ya 4G na awe amewezesha laini yake ya simu kuwa ya Airtel 4G. Kupata uhakika kwamba simu yake inauwezo wa kutumia 4G piga *149*95#”
    Mathen alisema Uwekezaji na upanuzi wa mtandao kwa kuzindua huduma za Airtel 4G ni kutelekeza makubaliano baina wa wabia wetu ambao ni serikali ya kuhakikisha ya kwamba Airtel inaendeleza uwekezaji kwenye upanuzi wa mtandao kwa lengo la kuzidi kuwa na mtandao imara,

    Aliongeza kuwa huduma ya 4G itatoa nafasi kukuza teknolojia ya kidigitali hapa nchini kwa kuwa na huduma nafuu na zenye kasi za intaneti na hivyo kubadilisha maisha ya Watanzania. “Airtel tutaendelea kuzindua huduma na bidhaa nafuu kwa ajili ya Watanzania wa kila rika” Mathen aliongeza.

SBL yahimiza usalama barabarani kueleke msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka

$
0
0
 Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa kampuni ya Bia ya Serengeti, John Wanyancha( kushoto) akizungumza na waendesha boda boda mjini Moshi leo, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya 'Usinywe na Kuendesha' inayolenga kupambana na ajali za barabarani. Wengine ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani  mkoa wa Kilimanjaro, Zauda Mohamed (mbele kulia) na Mratibu wa Mafunzo Ofisi ya  Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa huo, Insp. Hamadi Hoza.
Mwenyekiti wa Bodaboda Manispaa ya Moshi,Hamad Bendera akizungumza na waendesha boda boda mjini Moshi leo, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya 'Usinywe na Kuendesha' inayolenga kupambana na ajali za barabarani. Wengine wanaosikiliza ni Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa kampuni ya Bia ya Serengeti, John Wanyancha (kushoto),  Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani  mkoa wa Kilimanjaro,Zauda Mohamed (mbele kulia) na Mratibu wa Mafunzo Ofisi ya  Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa huo, Insp. Hamadi Hoza.

Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo imetoa vifaa mbali mbali vya usalama barabarani pamoja na elimu kwa madereva wa mabasi na waendesha boda boda mjini Moshi, ikiwa ni mchango wa kampuni hiyo katika kupambana na ajali za barabarani

Hatua hiyo ni muendelezo wa kampeni ya nchi nzima ya kampuni ya SBL kutoa elimu kwa watumiaji wa barabara na hususani madereva inayojulikana kama ‘Usitumie Kilevi na Kuendesha Chombo cha Moto’ inayohamasisha madereva kuepuka kuendesha vyombo vya moto wanapokuwa wametumia kilevi.

Utoaji huo wa vifaa ulifanywa na Mkurugenzi wa Mahusiano kwa Umma wa kampuni hiyo, John Wanyancha na kushuhudiwa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani  mkoa wa Kilimanjaro, Zauda Mohamed. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na makoti ya usalama barabarani, stika, vipeperushi vyenye ujumbe juu ya usalama barabarani pamoja na programu za elimu zilizotolewa kupitia redio na kwenye vyuo vya elimu ya juu vilivyopo mjini Moshi.

“Tunapoelekea msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka, kampuni ya SBL inapenda kuwakumbusha wateja wake na umma kwa ujumla kusherehekea sikukuu zinazokuja kistarabu kwa kuhakikisha hawaendeshi vyombo vya moto baada ya kutumia kilevi,” alisema Wanyancha

Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Kilimanjaro aliishukuru kampuni ya SBL kwa kuandaa kampeni hiyo na kuongeza kuwa kwa kulishirikisha jeshi la Polisi kampuni hiyo inaiunga mkono Serikali katika kutoa elimu ya usalama barabarani na pia kupambana na ajali zinazosababishwa na unywaji usio wa kistarabu.

Kamanda Zauda aliwaonya madereva na watumiaji wengine wa barabara wanaotumia kilevi na kuendesha vyombo vya moto  bila kufikiria athari za kufanya hivyo na kusisitiza kuwa jeshi la Polisi halitawavumilia watu wa aina hiyo haswa katika kipindi hiki tunapoelekea msimu wa sikukuu.


NMB YAFANYA SEMINA KWA WAJASIRIAMALI WA KAZI ZA UBUNIFU NA UFUNDI JIJINI DAR

$
0
0
 Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (wa pili kushoto), akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa wabunifu wa mitindo aliyeshiriki semina ubunifu na ufundi iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa wajasiriamali.
 Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, akiangalia kazi za wabunifu wa mitindo wakati wa semina ya Ubunifu na Ufundi iliyofanyika Makao Makuu ya Benki ya NMB jijini Dar es Salaam.
 Mbunifu wa mavazi, Doris Mbwilo (kushoto), akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, wakati wa maonesho ya kazi za ubunifu na ufundi za wajasiriamali.
 Mkurugenzi wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (kulia), akizungumza na mbunifu wa mavazi, Doris Mbwilo, wakati wa maonesho ya bidhaa za ubunifu na ufundi.
 Baadhi ya wabunifu wa mitindo walioshiriki semina ya Ubunifu na Ufundi.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya NMB, Donatus Richard, akizungumza na wajasiriamali wa kazi za ubunifu na ufundi.



MKURUGENZI wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna, amewaasa wajasiriamali na wafanya biashara wadogo kada ya ubunifu na ufundi kutumia benki katika kukuza biashara zao, ameyasema hayo katika uzinduzi wa semina ya Ubunifu na Ufundi ni Nguzo ya Uchumi, iliyofanyika leo Makao Makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.


Ametoa wito kwa wajasiriamali hao kuyashika na kuyatendea kazi mafunzo waliyoyapata ili kuweza kufanikiwa katika malengo yao ya kukuza biashara zao kwa kuzifanya zenye kuaminika.

Amewataka kufungua akaunti za benki kama vile FANIKIWA zitawawezesha kulinda biashara zao na kuwafanya kuaminika na benki ili kuingia kwenye mfumo wa kibenki kupata mikopoa ambayo itawawezesha kukuza biashara zao.

“Kuna mambo matatu mnayokwenda kufundishwa, moja ni umuhimu kuwa na akaunti, pili umuhimu wa mauzo ya bishara zako kupitia kwenye akaunti zenu na tatu ni faida ya kuweka akiba katika kukuza biashara zenu.

“Mkiwa na mahesabu yanayoeleweka kwenye akaunti zenu ni rahisi kupata mikopo ya kibenki kuinua biashara zenu ili muweze kujiimarisha zaidi. Ubunifu mlionao kama mnaweka malengo na kuyasimamia na kuwa na mtiririko wa matumizi ya fedha yanayoeleweka mtaweza kuzilinda biashara zenu na kukuza ubunifu mlionao.”amesema Zaipuna na kuongeza kuwa.

“NMB imeamua kuwafikia wajasiriamali wadogo kada ya ubunifu kwani ni kada iliyosahaulika katika jamii katika uwezeshwaji, sisi tunaamini kuwa Ubunifu na Ufundi ni nguzo ya Uchumi hivyo tunadhamira ya dhati ya kuimaraisha Uchumi wa wajasiriamali wabunifu kupitia mafunzo na mikopo ya kibenki ambayo itatolewa.”amesema.

Kwa upande wa mtoa mada, Meneja wa wafanyabiashara wadogo wa NMB, Beatrice Mwambije ametoa wito kwa wajasiriamali hao kutambua kuwa kuna gharama ya kulipia ili kuweza kupata mafanikio wanayoyahitaji katika kazi zao.

“Katika biashara yoyote ni muhimu sana kuwa na akaunti ili kuweza kutunza kumbukumbu zako za manunuzi, mauzo na matumizi ili kukujengea uwazi na uwaminifu kwa benki kukupa mkopo utakao kuwezesha kukua katika biashara yako.

“Lakini katika mafanikio yoyote yale lazima kuna gharama ya kulipia ili uweze kuyafikia, unahitaji kuwa na watu sahihi ambao watakutoa sehemu moja hadi nyingine nao ni watu sahihi ambao fikra zao ni chanya na wakomavu zaidi.”amesema Mwambije.

Nae Mkurugenzi wa Kampuni ya Ubunifu wa mavazi ‘Speshoz Tanzania’ Jeffrey Jessey amewataka washiriki wa semina hiyo kuwa mstari wa mbele kujifunza vitu vipya, kuchangamana na watu na kuwekeza zaidi kwa kile wanachokipa ili waweze kufika mbali katika tasnia ya Ubunifu na Ufundi.

Kwa Upande wa washiriki wa semina hiyo wametoa kongole kwa NMB kwa kuwajali na kuwapa elimu ambayo itawatoa walipo na kupiga hatua zaidi katika kazi zao,

“Nimefurahi sana kuwepo hapa leo, mafunzo haya ni kitu kikubwa sana kwetu sisi wabunifu wachanga katika kupiga hatua zaidi, tumejifunza mambo mengi na mazuri ambayo tukiyatendea kazi basi naamini tutafika mbali zaidi,”amesema Addam Mtaullah Mwenyekiti wa Umoja wa Mafundi Nguo Mbezi Luis (UMANGUMBE.

“Kwanza niwapongeza NMB wametuletea jambo sahihi kwa wakati sahihi, lakini pia mafunzo tuliyopata hapa yametufungua akili kujua jinsi gani tunaweza kutumia njia za kibenki kukuza biashara zetu kwa kuwa na akaunti unaiweka pesa yako salama.”amesema Doris Mbwilo mshiriki wa semina hiyo.
Viewing all 46379 articles
Browse latest View live




Latest Images