Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46369 articles
Browse latest View live

Benki ya NBC yajipanga kutoa huduma bora msimu mpya wa ununuzi wa korosho Mtwara

$
0
0
Na Mwandishi wetu,Mtwara

WAKATI wakulima wa korosho wakiendelea na msimu mpya wa korosho kwa mwaka 2019/20 Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesema itaendelea kuwahudumia na kuwahakikishia usalama wa fedha zao huku ikisogeza huduma hizo karibu zaidi badala ya kusafiri umbali mrefu.

Akizungumza wakati wa Kongamano la Uwekezaji na Maonyesho ya Biashara mkoani Mtwara mwishoni mwa wiki, Meneja wa NBC Mkoa wa Mtwara, Job Nshatsi alisema wameendelea kuwa mstari wa mbele kutuoa huduma za kibenki, ushauri na mafunzo ya kifedha na biashara yanayowezeha wateja wake ikiwemo wakulima na wafanyabiashara wa korosho.

Alisema katika kuhakikisha wakulima wananufaika na huduma zake tayari wameendelea kuongeza mtandao wao wa mawakala katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha wakulima wanapata fedha kwa wakati lakini pia kwa usalama kwa kuepuka kusafiri na fedha umbali mrefu kwenda palipo na tawi la benki hiyo.

“NBC tunatoa huduma za kibenki maalumu kwa ajili ya kukuza na kuendeleza kilimo-biashara (agribusiness) kwa kushirikiana na Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kilimo nchioni (PASS), tukiangalia sekta ya kilimo na mnyororo mzima wa thamani katika kilimo, na kwa Mtwara tutaendelea kutoa huduma ili kusaidia kukuza uzalishaji, uongezaji wa thamani na uuzaji wa zao la korosho,”alisema Nshatsi

Aidha alisema NBC kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) wanaendelea kutoa elimu za kifedha kwenye vikundi mbalimbali vya wajasiriamali lengo ikiwa ni kuwawezesha wajasiriamali hao kupata mbinu mbalimbali katika kuendesha biashara zao.

Nshatsi alizidi kueleza kuwa ili kuhakikisha watu wengi wanafikiwa na huduma za kibenki wamerahisisha ufunguaji wa akaunti kupitia akaunti ya NBC Fasta ambapo mteja anahitajika kuwa na kitambulisho kimoja au barua ya mtendaji na kufunguliwa akaunti.

Wakizungumza baadhi ya wananchi waliohudhuria kongamano hilo waliziomba taasisi za kifedha kuendelea kuwapa elimu ya matumizi sahihi ya fedha hasa katika kipindi hiki cha msimu wa mavuno ya korosho.

“Tunapohudhuria makongamano tunatumaini tutapata elimu mbalimbali lakini watu wa benki waendelee kutoa elimu ya matumizi sahihi ya  fedha ili kuwa endelevu hasa kipindi hiki ambacho wakulima wanauza korosho wasaidiwe wajue baada ya kuuza fedha wanazozipata wanatakiwa kuziendeleza kwenye miradi mingine ya maendeleo,”alisema Asha Chimae

Naye mwanachi mwengine Hansi Chilumba alisema “Wananchi wapo tayari kufanya kazi lakini kinachokosekana ni ujuzi na mtaji, ni vizuri benki kuendelea kutuwezesha hata mmoja mmoja ili kutimiza malengo kwa sababu kila mtu anakuwa na malengo yake lakini tunapounda kikundi inakuwa ngumu kwa wote kukubali wazo la mmoja ili kulifanyia kazi.


Ofisa Huduma Wateja wa Benki ya NBC Tawi la Mtwara, Lulu Mutayoba (katikati), akitoa maelezo kuhusu huduma za kibenki zotolewazo na NBC wakati wa Kongamano la Uwekezaji na Maonyesho ya Biashara Mtwara yakiyofanyika katika Viwanja vya Chuo cha Elimu Mtwara mwishoni mwa wiki. 



Ofisi 127 za serikali za mitaa sasa kupokea malipo kupitia Vodacom M-Pesa.

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), Mh. Suleiman Jaffo (kulia), Mkurugenzi wa M-Pesa (katikati) Epimack Mbeteni pamoja na Mkurugenzi wa Vodacom Business, Arjun Dhillon (kushoto) wakizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa Ushirikiano baina ya
TAMISEMI na Vodacom ambao utawezesha Ofisi 127 za serikali za mitaa kupokea malipo kupitia M-Pesa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), Mh. Suleiman Jaffo (kulia), Mkurugenzi wa M-Pesa Epimack Mbeteni (katikati) pamoja na Mkurugenzi wa Vodacom Business, Arjun Dhillon (kushoto) wakizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa Ushirikiano baina ya
TAMISEMI na Vodacom ambapo zaidi ya wateja milioni 14 watanufaika na matumizi ya M-Pesa katika malipo ya halmashauri na manispaa kote nchini.

************************************

· Zaidi ya wateja milioni 14 kunufaika na matumizi ya M-Pesa katika malipo ya halmashauri na manispaa kote nchini.

Novemba 3, 2019. Dar es Salaam: Wateja zaidi ya milioni 14 wa Vodacom watanufaika na huduma ya malipo kwa M-Pesa kwenda halmashauri na manispaa mbali mbali nchini. Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na ofisi ya TAMISEMI wamefanikisha kuimarisha mfumo wa malipo ya kifedha kwa kusogeza huduma ya malipo kwa M-Pesa kwa ofisi zaidi ya 127 za serikali za mitaa nchini. Uzinduzi wa huduma hiyo, ulifanyika ofisi za Makao Makuu ya Vodacom, Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI), Mheshimiwa. Suleiman Jaffo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mh Jaffo alisitiza umuhimu wa kutumia njia za kidigitali kama M-pesa kufanya malipo na kukusanya mapato kwani itaboresha uwekaji wa kumbukumbu, utoaji wa taarifa, kupunguza uvujaji na ubadhirifu wa pesa za umma pamoja na kuongeza mapato kwa idara mbalimbali za Serikali za mitaa.

“Malipo kutumia njia hizi za kidijitali yanapunguza muda mwingi tuliokuwa tunatumia kupanga foleni kufanya malipo. Sasa tuna M-Pesa naamini muda huu tutaupeleka moja kwa moja kwenye kujenga taifa na shughuli za maendeleo. Napenda kuwapongeza Vodacom kwa kutukumbuka na sisi huku TAMISEMI. Ninatumaini kwamba huduma hii itawarahisishia malipo, si tu kwa wananchi bali hata nyinyi viongozi katika kutunza hesabu zenu, usalama wa fedha pamoja na ukusanyaji fedha kwa ujumla,” aliongeza Jaffo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa huduma ya M-Pesa, Bwana Epimack Mbeteni alisema kupitia M-Pesa, Vodacom inategemea kufikia taasisi nyingi za serikali na binafsi ili kuwezesha mfumo wa malipo kuwa rahisi, fanisi na salama zaidi.

“Asilimia kubwa ya Watanzania wanatumia M-Pesa kufanya miamala mbalimbali kama Luku, bili za maji, faini za barabarani, ndio maana tukaona fursa kubwa ya kurahisisha malipo kwa serikali za mitaa kutumia M-Pesa,” aliongeza Mbeteni.

Ushirikiano huu baina ya TAMISEMI na M-Pesa utawawezesha wateja wa mtandao wa Vodacom kufanya zaidi ya malipo 205 ya serikali za mitaa kwa urahisi na usalama zaidi. Malipo kama vile leseni za biashara, vibali vya ujenzi, malipo ya maegesho na nyinginezo.

“Wote tunashuhudia jinsi M-Pesa inavyoendelea kubadilisha mfumo wa malipo nchini, ni tegemeo letu kwamba, malipo katika serikali za mitaa yatakuwa rahisi na salama zadi,” alisema Mbeteni.

Ili kulipa kupitia M-Pesa unapiga *150*00# halafu chagua lipa kwa M-Pesa, halafu malipo kwa serikali kisha weka namba ya kumbukumbu ambayo utapewa na ofisi za serikali za mtaa au unaweza kutumia APP ya M-Pesa kufanya malipo wakati wowote,” alifafanua Mbeteni.

Tigo yatangaza kuungana rasmi na Zantel

$
0
0
Hatua hiyo itasaidia kuboresha zaidi huduma na kukuza sekta ya mawasiliano nchini.

Kampuni ya Mawasiliano ya MIC Tanzania Public Limited Company (Tigo), leo imetangaza rasmi kuungana na kampuni ya Zanzibar Telecom Public Limited Company (Zantel) baada ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria na kiumiliki ambapo lengo kuu ni kukuza na kuboresha huduma za mawasiliano nchini.

Pamoja na kupata vibali kutoka mamlaka zinazohusika, mchakato wa kuhamisha hisa na umiliki kamili kutoka Zantel kwenda Tigo sasa umekwisha kamilika. Kufuatia kukamilika kwa zoezi hili sasa makampuni haya yataunganisha shughuli zake za kiutendaji Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar. 


Akizungumza kuhusu muungano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari alisema hatua hiyo ina manufaa makubwa kwa Taifa; “Ninaamini kuwa kuunganishwa kwa kampuni hizi - Tigo na Zantel kutajenga huduma jumuishi kwa watanzania wote siku za usoni. Wateja wote wa Tigo na Zantel wataweza kufurahia huduma bora kutoka kwenye soko imara litakalosaidia kuchochea ubunifu kwenye sekta ya mawasiliano,” alisema Karikari.

Muunganiko wa makampuni haya mawili utasaidia katika kuimarisha utoaji wa huduma kwa wateja wa Tigo na Zantel waliopo kote Tanzania Bara na Visiwani. Aidha, muungano huu utawezesha kupanua wigo wa huduma zetu pamoja na kuongeza ubora wa upatikanaji wa mawasiliano katika maeneo ya mijini na vijijini. Vile vile muungano huu utasaidia katika usambazaji wa huduma za mawasiliano kwa makampuni na taasisi mbalimbali nchini na pia kupanua huduma za kifedha kwa njia ya simu za mkononi.

Tunategemea mafanikio chanya kutokana na muunganiko wa makampuni haya mawili wenye lengo la kuchangia kwenye maendeleo ya Taifa.

Zoezi la kuunganisha taratibu za kiutendaji wa makampuni haya mawili zinatazamiwa kuanza hivi punde. Aidha, wateja wa Tigo na Zantel wataendelea kupata huduma bila usumbufu wowote kutoka mtandao husika kwani namba na laini za wateja hazitabadilika.




Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari 

NCHI 23 WANACHAMA WA SHIRIKA LA NGUVU ZA ATOMIKI DUNIANI ZASHIRIKI WARSHA YA KINGA NA UDHIBBITI WA VYANZO VYA MIONZI AFRIKA JIJINI ARUSHA

$
0
0
 
 Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) katikati mwenye suti ya kijivu akiwa akiongea na watalamu  wa kitaifa wa Kinga na Udhibiti  wa mionzi kutoka  katika nchi 23 za bara la AFrika waoaohudhuria  mkutano huo unaofanyika jijini Arusha.
 Baadhi ya washiriki wakiwa mkutanoni.
Wataalamu wa kitaifa wa kinga na udhibiti wa mionzi kutoka nchi 23 za bara la AFRIKA akiwa katika picha ya pamoja na mkurugenzi wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania(TAEC) mwenye suti ya kijivu mstari wa chini mara baada ya kufungua warsha ya siku tano ya majadiliano ya utekelezaji  wa viwango vya kimataifa  vya kinga na udhibiti wa mionzi vilivyotolewa  mwaka 2014 na Shirika la kimaitaifa la Nguvu za Atomiki Duniani(IAEA).



Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) inaendesha warsha inayohusisha wataalamu wa kitaifa wa kinga na udhibiti wa mionzi kutoka katika nchi 23 kutoka katika Bara la Afrika ambao ni wanachama wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani

Lengo la warsha hii ilionza hivi leo, ni kujadiliana uzoefu wa nchi za Afrika zilizopata kutekeleza viwango vya kinga na udhibiti wa mionzi vilivyotolewa mwaka 2014 na shirika la kimataifa la Nguvu za Atomiki Duniani na pia kujadili changamoto zilizowahi kujitokeza na kuzifanyia marekebisho.

Akifungua mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania Prof. Lazaro Busagala amewataka watalaamu hao kujadiliana na kutoa mapendekezo sahihi yatakayosaidia kuwakinga wananchi na mazingira katika nchi zao dhidi ya madhara yanayoweza kusababishwa na mionzi.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha mionzi katika Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA) Bwana Tony Colgan amesema kuwa washiriki wa mkutano huo wanapaswa kujadiliana na kupata mbinu zitakazowezesha kuboresha ulinzi na usalama katika mionzi. Amesistiza kuwa IAEA inapenda kupata mrejesho wa uzoefu wa nchi hizo katika kutumia viwango hivyo vya kimataifa.


Imetolewa na;

Peter G. Ngamilo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Azania Benki yatangaza washindi wa mwisho wa promosheni ya ‘Amsha Ndoto’

$
0
0
 Meneja wa mauzo ya rejareja wa Azania Bank Limited, Jackson Lohay  (katikati) akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam muda mfupi kabla ya kuwatangaza washindi wa promosheni ya Amsha Ndoto iliyoendeshwa na benki hiyo kwa lengo la kuwahamasisha wateja wake kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba.


Benki ya Azania (ABL) leo imewatangaza washindi wa awamu ya tatu na ya mwisho wa promosheni yake ya ‘Amsha Ndoto’ ambayo ina lengo la kuwahamasisha wateja wake na umma wa watanzania kujenga utamaduni wa kuweka akiba itakayowasaidia kuwa na maisha ya baadaye yaliyo imara kifedha.

Promosheni hii ambayo ni ya mizezi mitatu ilianza rasmi tarehe 27/06/2019 na ilifika tamati tarehe 27/09/2019 huku ikihusisha wateja wa Azania Benki wa zamani na wale wapya na ilijikita zaidi katika bidhaa mbili kuu za uwekaji akiba, ambazo ni: Ziada Akaunti pamoja na Watoto Akaunti.

Mwezi Agosti, droo ya kwanza ya promosheni hii ilifanyika ambapo jumla ya washindi watatu walipatikana ambao wote kwa pamoja walijishindia jumla ya shilingi millioni 8. Vivyo hivyo, droo iliyofuata ilifanyika mwezi Septemba ambapo pia washindi watatu walipatikana wakijishindia jumla ya kiasi cha shilingi milioni 8.

Akitangaza washindi kwenye droo ya tatu na ya mwisho ambayo imefanyika leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Mauzo ya Reja Reja wa Benki ya Azania, Jackson Lohay, amesema benki imetimiza ahadi ya kuwapatia zawadi washindi walioshoriki kwenye promosheni na kwamba zawadi wanazopewa zinawasaidia kutimiza ndoto zao. “Katika droo mbili zilizopita tulipata washindi kutoka Amaeneo mbalimbali ya nchi yetu ya Tanzaniana wote walipewa zawadi zao kama walivyostahili, kwa ujumla washidni wote sita waliweza kujishindia kiasi cha shilingi milioni 16,” amesema Lohay.

Kwa mujibu wa Lohay, washindi wa droo ya mwisho ya promosheni hii ambao wamepatikana baada ya droo kufanyika ni; (kiasi cha fedha walichojishindia kwenye mabano);

1. Frank Godfrey Nyange (Tsh2.2m)
2. Anna Said Lyimo (Tsh 3m)
3. Venancy Benny Loshia (Tsh 3m)

Akitoa pongezi kwa washindi wa promosheni, Lohay amewahasa wateja wa ABL kuendelea na utamaduni wa kujiwekea akiba kwani kwa kufanya hivyo wanakuwa wanajihakikishia kuwa na fedha za kutosha kwenye akaunti zao kwa ajili ya matumizi yao ya siku za usoni.

NBC PROFITS TRIPLE

$
0
0
The National Bank of Commerce (NBC) the country’s oldest bank, with
over 50 year of serving the financial sector in Tanzania, has posted
impressive profits during the third quarter of the year. According to the third
quarter financial statement, that was released on 30 th October 2019, NBC
has attained impressive growth of 367% on its Profit After Tax (PAT)
compared to last year.

“Our impressive performance for the last nine months is mainly attributed to
our ongoing cost savings and efficiency drive, increased fee income from
transactional activities and improved quality of the loan portfolio,” said Mr.
Theobald Sabi NBC Managing Director.

Taking a closer look, at the NBC third quarter financial statement, as at end
of September 2019, NBC had Net Loans and Advances to the tune of TZS
987 Billion and Customer Deposits worth TZS 1.717 Trillion.

“Our total net loans and advances increased quarterly by 3.7%, mainly
contributed by additional loan bookings from our Corporate, Retail and
Business Banking clients, whilst our overall customer deposits increased by
19.3%” added Mr. Theobald Sabi.

“Our continued focus of onboarding quality loans has started to pay off
resulting in lower impairment charges for the third quarter of the year. In
addition, Non-Performing Loans (NPLs) ratio has continued to decline to
6.9% down from 10.1% as at September 2018” said Mr. Sabi.

The NBC Digital Transformation agenda continued to deliver impressive
results, which have contributed to our bottom line. Our Mobile Banking
transactions have grown by 50% compared to last year alone. This
represents that our customers are effectively utilizing our electronic
offerings and thus reducing the time required to conduct transactions in the
branches.

“Our purpose is to provide convenient services to our customers and
clients. We want our customers to be able to bank or transact wherever
they are without visiting branches. We also want our customers to enjoy
the different services and products that we have built in our digital
platforms,” said Mr. Theobald Sabi

The Online and Mobile Banking proposition have become popular
electronic channels widely used by Retail (Individual) and Corporate
clients. The online transactions are safe and secure allowing Bulk
Payments, Local and International Payments.

“Our Digital Banking Facilities provides individuals, SMEs, Government
Agencies, and Corporates with convenient and efficient Cash Collections
and Payment solutions,” said Mr. Sabi.

Another fast growing electronic channel is the NBC Agency Banking (NBC
Wakala) that now has a membership of over 2,000 agents spread across
the country. Customers are now able to access their accounts and make
payments with greater convenience through the growing NBC footprint of
agents. NBC Wakala agents are now GePG compliant and thus customers
can settle their dues to the Government through the NBC Wakala network.

NBC is now one of the leading banks in respect of Government Revenue
Collections through GePG.

Our electronic channels are Government Electronic Payment Gateway
(GePG) compliant, thus allowing our customers the choice to settle
government levies and fees through our convenient electronic channels,”
said Mr. Sabi.

Benki ya NBC yaendeleza jitihada zake katika kusaidia huduma za jamii

$
0
0
 Picha mbalimbali za tukio la mashindano ya gofu ya hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari na kudhaminiwa na          Benki ya NBC. Mashindano hayo yalikuwa na lengo la kukusanya fedha na kusaidia wenye mahitaji maaalumu katika jamii ikiwa ni pamoja na mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo na kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao katika Shule ya Sekondari Mtakuja iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yaliwashirikiosha zaidi ya wacheza gofu 104. 

 Picha mbalimbali za tukio la mashindano ya gofu ya hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari na kudhaminiwa na          Benki ya NBC. Mashindano hayo yalikuwa na lengo la kukusanya fedha na kusaidia wenye mahitaji maaalumu katika jamii ikiwa ni pamoja na mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo na kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao katika Shule ya Sekondari Mtakuja iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yaliwashirikiosha zaidi ya wacheza gofu 104.  
Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo (katikati) akipokea cheti  kutoka kwa Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya Mshindano ya Gofu ya Hisani yaliyoandaliwa na Klabu ya Rotari ya Bahari, Hemaly Jethwa kwa kutambua udhamini wa benki hiyo katika mshindani hayo yaliyofanyika katika Viwanja cha gofu vya Gymkhana jijini Dar es Salaam hivi karibuni yakiwa na lengo la kukusanya fedha kusaidia wenye mahitaji maaalumu ikiwa ni pamoja na mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo na kituo cha mafunzo kwa njia ya mtandao katika Shule ya Sekondari Mtakuja iliyopo Kunduchi jijini Dar es Salaam. . Kushoto ni Meneja Mahusiano wa NBC, Joseph Lema. Mashindano hayo yaliwashirikisha zaidi ya wacheza gofu 104. 
  
Maofisa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), wakipiga picha ambapo pamoja na kutoka huduma za maji na kofia kwa wakimbiaji, washiriki pia walipata nafasi ya kujulishwa huduma mbalimbali za kibenki zitolewazo na benki hiyo. 


KATIKA kuendeleza jitihada zake za kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii, Benki ya NBC imedhamini hafla maalumu ya kuchangisha fedha  iliyoandaliwa  na Klabu ya Rotari ya Bahari jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
 Hafla hiyo iliandaliwa na klabu hiyo ili kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wenye mahitaji maalumu katika jamii ya watanzania ikiwemo mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama, vyoo na ujenzi wa kituo cha kufundishia kwa njia ya mtandao katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja iliyopo eneo la Kunduchi jijini Dar es Salaam.
 Akizungumza na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo na wa Kati wa NBC, Evance Luhimbo alisema NBC kwa miaka kadhaa imekuwa ikishughulisha katika kusaidia shughuli za jamii katika maeneo  mbalimbali kama vile elimu, afya na masuala ya ujasiriamali,
 “Sisi ni jukumu letu kama benki kurudisha katika jamii sehemu ya faida tuipotayo katika biashara yetu, NBC ni benki kongwe yenye uzoefu katika kutoa huduma bora za kibenki kwa zaidi ya miaka 52, hivyo tutaendelea kusapoti miradi kama hii yenye kuleta tija katika jamii”, alisema.
 Pamoja na hayo alisema mara baada ya kupokea maombi ya kuchangia hafla hiyo kutoka Klabu ya Rotari, benki yao haikusita kuitikia wito kwani ni imani jamii ikiwezeshwa kiuchumi na kielimu na jamii ikiwa na afya bora inaweza kuchangia vizuri katika kuleta maendeleo ya Taifa kwa ujumla.    
 Aidha Bwana Lhimbo aliitaja baadhi ya shughuli za kujamii ambayo NBC imefaya ikiwa ni  pamoja na kutoa vifaa vya  ujenzi wa madarasa katika shule za mkoani Lindi, Zanzibar, msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa Morogoro pamoja na kutoa elimu ya masuala ya kifedha na ujasiriamali katika shule mbalimbali nchini.
 Baadhi ya miradi ambayo imeshafanikishwa na Klabu ya Rotari ya Bahari ni pamoja na matibabu ya moyo kwa watoto katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), ukarabati wa maktaba katika shule ya msingi buyuni, upanuzi wa kituo cha mafunzo ya ufundi stadi katika kituo cha masista cha Carmel, Kurasini, ukarabati wa maktaba katika Shule ya Sekondari ya Mtakuja  pamoja na kutoa misaada ya aina tofauti katika vituo vingine vya walemavu na wasiojiweza.

‘Tigo Business’ yachochea mageuzi ya kidigitali kwenye biashara Tanzania

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari akizungumza na wangu waalikwa katika Hafla ya uzinduzi wa huduma na bidhaa zilizoboreshwa zaidi pamoja na tovuti inayompa mteja mamlaka ya kujihudumia na kudhibiti matumizi ikiwa na lengo la kuzisaidia kampuni mbalimali kukuza huduma zao kidigitali.Hafla hiyo ilifanyika mapema Jijini Dar Es salaam.
Kandambara Maita..Mkuu wa Mauzo- Tigo business. akifafanua jambo kwa wageni waalikwa ( hawapo pichani) katika Hafla ya uzinduzi wa huduma na bidhaa zilizoboreshwa zaidi pamoja na tovuti inayompa mteja mamlaka ya kujihudumia na kudhibiti matumizi ikiwa na lengo la kuzisaidia kampuni mbalimali kukuza huduma zao kidigitali.Hafla hiyo ilifanyika mapema Jijini Dar Es salaam.
 Kampuni ya Tigo kupitia kitengo cha Tigo Business leo imezindua huduma na bidhaa zilizoboreshwa zaidi pamoja na tovuti inayompa mteja mamlaka ya kujihudumia na kudhibiti matumizi ikiwa na lengo la kuzisaidia kampuni mbalimali kukuza huduma zao kidigitali.

Aidha tovuti hiyo itawasaiidia wateja kujua matumizi yao kwa wakati na kuwapa wateja mamlaka ya kusimamia akaunti zao.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari alisema “Tigo business ni huduma inayokua kwa kasi ikiwalenga hasa wafanyabiashara na inaongoza katika huduma zenye ubunifu kwenye soko la mawasiliano.Pia, ni washirika wa teknolojia na washauri wa kimkakati kwa baishara za aina zote.”

Karikari alisema Tigo kama kampuni ya kidigitali ipo mstari wa mbele katika ukuzaji wa teknolojia na kuwa imejizatiti katika kuhakikisha kampuni zinafikia malengo ya kutoa huduma zao kidigitali sokoni.

“Bidhaa zetu ni pamoja na huduma za sauti, data, IoT pamoja na jumbe (Bulk SMS) zinazomruhusu mteja kuwasiliana na wateja wake kwa viwango nafuu.Tovuti hii pia inatoa intaneti mahsusi kwa kampuni ambazo zinahitaji suluhisho kubwa ili kuongeza ufanisi kwenye taasisi. Biashara ambazo zina matawi mengi zinaweza kuunganisha data, mifumo yake na uendeshaji kwa kutumia huduma ya ‘inter-branch connectivity solutions” aliongeza Karikari.

Tigo business inamiliki na kuendesha kituo cha data cha Kimataifa (Tier III Certified Data Center) Tanzania, kinachoruhusu kampuni za ndani kuhifadhi data zao na programu za biashara kwa usalama kupitia miundombinu iliyothibitishwa na mamlaka za kimataifa.

“Ukweli ni kwamba tunaishi kwenye dunia ambayo taarifa au data zimepungua thamani hivyo zinahitaji kuhifadhiwa na kuchakatwa kwa ufanisi mkubwa ili kusaidia kampuni kufikia malengo ya biashara na ndiyo maana Tigo business imewekeza katika kuhakikisha inatoa suluhisho zenye kukidhi mahitaji na bajeti za kampuni,” alisema.

Kupitia miundombinu yenye usalama inatoa uhuru kwa wateja kuunganishwa na huduma za uhakika kupitia kwa watoa huduma wengine au moja kwa moja na Tigo na pia inatoa uhakika wa huduma kwa asilimia 99.982% hivyo kuzifanya biashara kuzalisha zaidi jambo linalochochea ukuaji wake.

Afisa Mkuu wa Tigo business, Pavan Ramdhani aliwaarifu wateja wa Tigo business wakati wa uzinduzi kuwa “Tovuti hii mpya itasaidia wamiliki wa makampuni kutumia muda mwingi katika biashara zao kwa kuwapa nafasi ya kujihudumia na kupata thamani halisi kupitia chaneli wanazopenda.Hii itawapa uwezo wateja na kutoa huduma bora kwa wateja wao,”

Aliogeza “Wateja wanaweza kusimamia akaunti zao, kuuliza na kupata ripoti ikiwamo za ankara pamoja na kupata huduma kwa wakati.Pia, tovuti inaruhusu wateja kusimamia na kudhibiti gharama za mawasiliano pamoja na kupanga rasilimali kwa watumiaji kulingana na mahitaji.Tovuti ni rahisi kutumika na inapatikana kupitia link https://tigobusiness.tigo.co.tz/Login/Tz.”

Tigo business inatoa suluhisho kwa biashara zote bila kujali ukubwa wake na kuzisaidia kampuni kujikita kwenye mambo ya msingi kwenye biashara kwa mustakabali wa baadaye. Tupigie 0711 100 101 au tutumie e-mail kupitia: tigobusiness@tigo.co.tz kupata huduma kwaajili ya biashara yako kwa gharama nafuu.

Zantel yazindua simu janja ijulikanayo kama SMARTA yenye uwezo wa 4G na gharama nafuu nchini

$
0
0

Mkuu wa Bidhaa na Bei wa Zantel, Aneth Jamila Muga (Julia),akionyesha simu janja na ya gharama nafuu ya SMARTA iliyozinduliwa na Zantel mjini Zanzibar. Simu hii inayonunuliwa ikiwa na GB 12 intaneti inayowezesha matumizi ya mwaka mzima inapatikana kwa shilingi 39,999/- nchini pote. Wengine pichani ni wafanyakazi wa Zantel

Katika jitihada zake za kuongeza wigo wa watumiaji wa simu janja nchini Tanzania, Zantel imezindua simu janja yenye uwezo wa 4G na gharama nafuu sana sokoni ijulikanayo kama SMARTA.

Akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi, Mkuu wa Bidhaa na Bei wa Zantel, Aneth Jamillah Muga, alisema simu iliyozinduliwa imetengenezwa kwa teknojia zinazowezesha matumizi ya programu za simu janja zinazowezesha kupata programu za kuelimisha na kuburudisha kama vile, WhatsApp, Facebook, YouTube, Google na inapatikana kwa bei nafuu ya shilingi 39,999/-.

Alisema simu ya SMARTA ni aina mpya ya simu katika soko la Tanzania inayowezesha kuongeza idadi ya watumiaji wa simu janja nchini kote na kuleta mabadiliko ya kidigitali kwenye jamii.

“Tumezindua simu aina ya SMARTA katika soko kuwezesha wananchi wengi kumudu kumiliki simu janja sambamba na kuwapatia fursa ya kufurahia maisha ya kidigitali kupitia mtandao wa 4G+ wa Zantel”. Alisema Muga.
Muga, alisema kuanzia sasa simu janja zijulikazo kama SMARTA zinapatikana katika maduka yote ya Zantel yaliyopo Pemba, Unguja, na Tanzania bara na zinanunuliwa zikiwa tayari zimeunganishwa na intaneti ya bure yenye GB 12 itakayowezesha mteja kuitumia kwa kipindi cha miezi 12.

Mkuu wa Zantel Zanzibar,Mohammed Mussa Buacha, alisema kuzinduliwa kwa simu mpya za SMARTA ni moja ya mkakati wa Zantel kuleta mapinduzi ya kidigitali na kuwezesha kupatikana teknolojia za kisasa kwa gharama nafuu nchini kote. Alisema Zantel inaamini kuwepo kwa bidhaa za kisasa kwa matumizi ya huduma za kidigitali kunabadilisha maisha ya wananchi kuwa bora.

‘’Kupitia mapinduzi ya kidigitali yanawezesha kupata elimu, taarifa za afya, burudani, huduma za kifedha na kwenye intaneti inawezesha kujua mambo mbalimbali yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku. Dira ya Zantel ni kuwezesha upatikanaji wa huduma za kidigitali kwa manufaa ya wateja wetu wapya na wa zamani”. alisisitiza Mussa.

Alisema kupatikana kwa simu za gharama nafuu za SMARTA, ni suluhisho la kuwezesha watanzania wengi kuweza kumudu kumiliki simu janja nchini na kuwezesha kuendeleza matumizi ya huduma za kidigitali Zanzibar “Kuanzia sasa Watanzania hawana sababu ya kuwa na vikwazo wanapotaka kununua simu janja”.

Zantel imekuwa mstari wa mbele kuwekeza katika ubunifu kwendana na ongezeko la watumiaji wa huduma za data na kuunganishwa kwenye intaneti yenye kasi kubwa ambapo ili wengi wafurahie huduma hizo kunatakiwa kuwepo simu janja za gharama nafuu.

NMB YATOA MISAADA YA MILIONI 110 UKEREWE,TABORA,SONGEA

$
0
0
Siriel Mchemba (Mwenye miwani) akipokea moja ya vifaa tiba kutoka kwa Meneja wa NMB Kanda ya Mashariki – Baraka Ladislaus kwa ajili ya kituo cha afya Gairo mkoani Morogoro. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Gairo, Agnes Mkandya na Mganga M.fawidhi wa kituo cha afya Gairo, Dk. Dastan Mshana.
Janeth Shango akikabidhi msaada wa bati 175 kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea- Pololet Mgema kwa niaba ya shule ya Msingi Ndelenyuma katika Halmashauri ya Madaba wilayani Songea.


Sospeter Magese, Akikabidhi msaada wa Bati za Shule za Sekondari na Msingi kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Erick Komanya. Benki ya NMB ilikabidhi viti na meza kwa shule za sekondari, vifaa vya unjenzi – bati 216, mbao na misumari kwaajili ya shule za msingi Kanyenye, Kalunde na Ikomwa vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 30.

Cornel Magembe akipokea vitanda na mashuka kutoka kwa Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa – Abraham Augustino (aliyevaa suti), wakati wa hafla ya makabidhiano yaliyofanyika juzi wilayani Ukerewe. Benki hiyo imekabidhi msaada wa vitanda na mashuka kwa Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe, viti na meza za shule na chuo cha Murutunguru,vifaa vya ujenzi kwa Zahanati ya Bwasa na shule za msingi na Sekondari za wilaya ya Ukerewe vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 75.
………………

NA MWANDISHI WETU

KATIKA kuunga juhudi za utatuzi wa changamoto zinazoikabili Sekta ya Afya na Elimu nchini, Benki ya NMB wiki iliyopita ilikabidhi misaada mbalimbali yenye thamani ya Shilingi Milioni 110 katika wilaya za Songea, Tabora na Ukerewe.

Thamani ya misaada hiyo ya vifaa vya ujenzi na vifaa tiba, vinaifanya Benki ya NMB kutumia zaidi ya Sh. Mil. 900 kununulia na kukabidhi vifaa hivyo kwa Shule za Msingi, Sekondari, Zahanati na Vituo vya Afya nchini kwa mwaka huu. – 2019

Wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, NMB imekabidhi misaada ya vifaa vya ujenzi, elimu na afya yenye thamani ya Sh. Mil. 75 kwa shule 14 za msingi na sekondari, Chuo cha Ualimu Marutunguru na Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe.

Msaada huo, ulitolewa na Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa, Augustino Abraham na kupokelewa na Mkuu wa Wilaya hiyo (DC), Corneli Magembe, ambaye aliishukuru benki hiyo kwa uwezeshaji huo, alioutaja kama unaoenda kumaliza tatizo la uhaba wa vifaa kwa taasisi husika.

Mkoani Tabora, NMB imekabidhi viti na meza wenye thamani ya Sh. Mil. 30 kwa shule sita za Manispaa ya Tabora, tatu zikiwa ni za sekondari na nyingine tatu za msingi, msaada ambao ulipokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Erick Komanya.

Hafla hiyo ilifanyika Sekondari ya Wavulana Tabora, ambako Meneja wa NMB Kanda ya Magharibi, Sospeter Magese, alikabidhi mabati 216, mbao na misumari vyote vikiwa na thamani ya Sh. Mil. 15, kwa ajili ya Shule za Msingi Kanyenye, Kalunde na Ikomwa.

Aidha, NMB ikatoa msaada wa mabati 175 ya geji 28, yenye thamani ya Sh. Mil. 5, kwa ajili ya Shule ya Msingi Ndelenyuma, iliyopo katika Halmashauri ya Madaba, wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza kabla ya kukabidhi bati hizo katika hafla ambayo ilifanyika katika Shule ya Msingi Ndelenyuma, Meneja wa NMB Kanda ya Kusini, Janeth Shango, alisema kwa miaka kadhaa sasa NMB imekuwa mstari wa mbele kuchangia miradi ya mbalimbali ya maendeleo.

“Mpaka ninavyoongea leo, kwa mwaka huu 2019 pekee, tayari NMB tumetoa misaada yenye thamani ya Shilingi Milioni 900, tumejikita zaidi kwenye miradi ya elimu, afya na majanga,” alisema Shango wakati wa hafla ya makabidhiano hayo yaliyofanyika wilayani Songea.

Tigo inavyorejesha tabasamu kwa wagonjwa wa mguu kifundo.

$
0
0

Mkurugenzi mtendaji (Tigo) Bw. Simon Karikari akimkabidhi mfano wa hundi ya Mil 110/- Ofisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT, Brenda Msangi.Hafla ya makabidhiano yalifanyika katika wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika hospitali ya CCBRT

Siku zote ni furaha pale mwanamke anapopata mtoto ambaye alimtarajia kwa takribani miezi tisa ya ujauzito.Hii ilidhihirika kwa Salma Hajj (29) baada ya kujifungua salama mtoto wake wa kwanza wa kiume miezi kumi iliyopita.


Hatahivyo, furaha ya Salma haikudumu.Baada ya muda mfupi, Salma ambaye ni mkazi wa Buza jijini Dar es Salaam furaha yake ilitokweka baada ya kugundua kuwa mwanae wa huyo alikuwa na tatizo la miguu kujikunja pasipo kujua ni nini tatizo.

Tatizo hilo linajulikana kama ‘mguu kifundo’ au kwa kiingereza linafahamika kama ‘Clubfoot’ ambalo kisayansi linalotokea hata kabla ya mtoto kuzaliwa.

Kila mwaka zaidi ya watoto 100,000 duniani huzaliwa na ugonjwa huu ambao humfanya mtoto kushindwa kutembea kwa kutumia unyayo na badala yake hutumia kifundo cha mguu.

Kwa Tanzania,inakadiriwa kuwa karibuni watoto 2,800 wanazaliwa na ugonjwa huu kila mwaka.Kati yao asilimia 50 wana athirika mguu mmoja huku waliobaki wakiathirwa miguu yote miwili.


Asilimia 80 ya wagonjwa wasiopata matibabu yake wanapatikana kwenye nchi zinazoendelea, ikiwamo Tanzania.Kama ugonjwa huu usipotibika unaweza kusababisha maumivu makali wakati wa kutembea na hatimaye husababisha ulemavu wa muda mrefu.

“Kiukweli ulikuwa ni wakati mgumu sana kwangu.Nilijisikia vibaya kwamba mwanangu hataweza kutembea vizuri na hatahivyo sikujua anasumbuliwa na tatizo gani kwa kipindi kile,” anasema Salma.

“Nilihisi kama ilikuwa mwisho wa dunia kwangu na mwanangu; nilijiuliza maswali mengi bila majibu kwamba atawezaje kutembea? ataonekanaje kwa watu? atasoma katika shule gani? nilichanganyikiwa sana,” anasema Salma.

Mmoja wa mtoa huduma (nesi) alimjulisha kuwa tatizo hilo linaweza kutibika katika Hospitali ya CCBRT iliyoko Msasani jijini Dar es Salaam bila malipo.Kilichofuata ilikuwa ni kutembelea hospitalini hapo ambapo madaktari walianza kutoa matibabu kwa mtoto wake kwa miezi michache tu.

Kwa mujibu wa daktari wa mifupa (Orthopedic) wa CCBRT, Dk. Zainab Ilonga, anasema chanzo cha ugonjwa huo bado hakijulikani.

Anasema hadi sasa sababu yake bado haijathibitika lakini wanaamini kuwa moja ya sababu ni matumizi ya pombe na matumizi mabaya ya madawa wakati wa ujazuzito au urithi wa vinasaba (genetic) na kwamba tafiti zaidi zitasaidia kutambua chanzo halisi cha tatizo hilo.

“Kuna njia mbili za kutibu ugonjwa huu wa mguu kifundo;moja ni kutumia njia ya Ponseti ambayo haihitaji kufanya upasuaji na nyingine ya kufanya upasuaji,” Dk Ilonga anasema na kuongeza

“Kwa Tanzania tunatibu watoto takribani 400 kwa mwaka sawa na asilimia 25 ya wagonjwa wote na hii inatokana na baadhi ya wazazi kuwanawaficha watoto wenye tatizo hili.”

Ignacio V. Ponseti ni njia ambayo imekuwa ikitumia kutibu mguu kifundo tangu miaka ya 1940.Moja ya kanuni ya njia hii ni kwamba tishu za mtoto ikiwamo tendoni, ligamenti na maungio yake yapo katika hatua ya ukuaji hivyo kufanya mguu kuungana baada ya kila wiki moja.

Kwa kutumia njia hii ndani ya wiki kadhaa hali ya mgonjwa inaweza kubadilika na kufanikisha kurekebisha mguu bila uhitaji wa kufanya upasuaji.Mtoto wa Salma alipitia hatua hiyo maarufu kama ‘gentle bone manipulations’ na ufuatiliaji (castings) ili kujua mabadiliko ya kibaolojia hasa misuli yake, maungio na tishu kwa lengo la kutibu tatizo alilokuwa nalo.

“Kuna wakati alikuwa anapitia wakati mgumu kwani alikuwa analia sana jambo lililonifanya na mimi kulia.Nilikuwa na wasiwasi juu ya maisha ya mwanangu siku za mbeleni,” anasema kwa huzuni.

“Nawashukuru sana Tigo na madaktari wa CCBRT kwa msaada wao mkubwa kwasababu saizi mtoto wangu ana miezi kumi na amepona kabisa,” anasema Salma huku akiwa na uso wa furaha.

Afisa wa Uwajibikaji kwa Jamii wa Tigo, Halima Okash anasema “Tuliona kuna umuhimu wa kusaidia wahitaji hawa kwasabau CCBRT inahudumia jamii yenye uhitaji na wasiojiweza katika kuwasaidia kupata huduma za matibabu.Tumeunga mkono jitihada hizi zinazofanywa na CCBRT kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata nafasi ya kutibiwa kwa gharama ndogo au bure kabisa,” anasema Okash.

Kupitia huduma za upasuaji kutoka hospitali ya CCBRT jumla ya watoto 1,509 wamenufaika katika kipindi cha miaka sita iliyopita.

“Haya ni mafanikio yanayotufanya sisi Tigo kujisikia faraja kwa kiasi kikubwa kwani kwa kutoa matibabu kwa watu wenye ulemavu,Tigo na CCBRT tunaleta matokeo chanya kwa maisha ya mtu mmoja mmoja, familia na jamii ya Tanzania kwa ujumla,” anasema Okash.

Tangu mwaka 2013, Tigo iliingia ubia na hospitali ya CCBRT kutoa matibabu kwa wagonjwa wa midomo sungura, kwa kutumia njia ya jumbe (SMS) zinazotumwa kwa wagonjwa wa CCBRT kuwakumumbusha kufuatilia matibabu na kutoa uelewa kuhusu huduma kwa umma.

Kupitia mpango huu, wagonjwa wanaweza kupata jumbe za matibabu kwa siku nne na siku moja kabla ya siku ya matibabu na hii imeisaidia CCBRT kupunguza idadi ya wagonjwa wanaokatisha matibabu.

Kwa msaada wa Sh110, 0000,000 kwa mwaka kutoka Tigo, CCBRT inaweza kutoa huduma za matibabu kwa njia Ponseti (bila upasuaji) kwa wagonjwa wapya zaidi ya 400 na wengine wanaoendelea na matibabu hospitalini hapo.

Benki Ya Exim Yakamilisha Rasmi Umiliki Wa Benki Ya UBL

$
0
0
Benki ya Exim Tanzania imeendelea kujitanua zaidi baada ya kufungua rasmi tawi lake jipya katika mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam kufuatia benki hiyo kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania.

Hatua hiyo inafanya Benki ya Exim Tanzania kuwa benki ya kwanza miongoni mwa benki za sekta binafsi hapa nchini zilizofanikiwa kuunganisha benki nyingine na hivyo kuifanya kuwa miongoni mwa benki tano kubwa hapa nchini ikiwa na ukwasi wa kiasi cha Tsh 1.7 Trilioni.

"Tunafurahishwa na ongezeko kubwa la wa wateja wa aina tofauti ambao watajiunga na familia ya benki ya Exim na tunawahakikishia kuwa tunafurahi kuwa nao kwenye safari yetu na tunajitoa kuhakikisha kwamba wanaendelea kufurahia huduma zenye ubunifu kutoka kwetu.''

''Wateja wakiwa ni sehemu muhimu zaidi ya biashara yetu, tunaahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wanafurahia huduma zetu,'' Alisema Bwana Jaffari Matundu, Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Exim.

Kwa mujibu wa Bw. Matundu hatua hiyo inakwenda sambamba na msimamo wa Rais Dk John Magufuli ambae amekuwa akisisitiza juu ya umuhimu wa kuwa na benki kubwa zaidi na ndogo nchini kwa kuwa ni hatua muhimu kwa afya ya kifedha katika ukuaji wa uchumi hususani katika kutoa huduma kamili na zenye ubunifu kwa wateja.

"Tanzania ina benki nyingi ukilinganisha na mataifa mengine ikiwemo Afrika Kusini na Nigeria. Sekta ya benki imekuwa ikishuhudia uunganishwaji wa mabenki ambao mwisho wa siku utaziacha benki zikiwa na uwezo wa kusukuma ukuaji wa uchumi kikamilifu. ''

"Dar es salaam ni soko muhimu kwa Benki ya Exim na hivyo uwepo wa tawi jipya la Mkwepu ambalo lenye teknolojia, ubunifu na muundo ambao utawawezesha wateja kukutana na maafisa wa benki kwa njia ambayo inawafaa na katika mazingira ambayo ni yanafikika kwa wote,'' alisema.

Aidha Bw Matundu alisema mchanganyiko wa benki binafsi na zile za umma zilizosambaa kote nchini utahakikisha kuwa kuna mtiririko mzuri wa huduma za kifedha.

"Wajasiriamali watakuwa wamehakikishiwa upatikanaji wa kutosha wa mitaji inayohitajika kupanua biashara zao, ambayo itasababisha kasi kubwa ya ongezeko la ajira na hivyo kupunguza kabisa tatizo la ukosefu wa ajira nchini,'' alisema

Ujio wa tawi hilo jipya unaifanya benki ya Exim Tanzania kuwa kuwa na jumla ya matawi 33 kote nchini.

Kwa zaidi ya miaka 22, benki ya Exim imefanikiwa kupata hadhi ya kuwa benki kimbilio si tu Tanzania bali pia nje ya nchi ambapo imeweza kujitanua kwa kuanzisha matawi yake ikiwemo nchi za Djibouti, Comoros na Uganda.
 Ofisa Huduma kwa wateja na Uendeshaji wa Benki ya Exim Tawi la jipya la Mkwepu, jijini Dar es Salaam Bi Helen Muhenga (Kushoto) akimkaribisha mmoja wa wateja aliefika kwenye tawi hilo ili kupata huduma za benki hiyo. Tawi hilo jipya ni mkakati wa benki hiyo kujitanua zaidi baada ya kukamilisha taratibu za umiliki rasmi wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania.
Meneja wa Huduma kwa wateja na Uendeshaji wa Benki ya Exim Tawi la jipya la Mkwepu, jijini Dar es Salaam Bw Brian Bennet (Kushoto) akimkaribisha mmoja wa wateja wa benki hiyo aliefika kwenye tawi hilo ili kupata huduma za benki hiyo. Tawi hilo jipya ni mkakati wa benki hiyo kujitanua zaidi baada ya kukamilisha taratibu za umiliki wa iliyokuwa Benki ya UBL Tanzania.

SBL yaahidi makubwa kuelekea mechi ya Stars na Equatorial Guinea Na Mwandisdi Wetu

$
0
0
 Katibu Mkuu wa TFF Kidau Wilfred (kulia), akiongea na waandishi wa habari wakati wa kutangaza maandalizi ya Taifa Stars kuelekea mechi yake ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2021) dhidi ya Equatorial Guinea. Kulia kwake ni Meneja Masoko wa kampuni ya Bia ya Serengeti Anitha Msangi akifuatiwa na Haji Manara, mwenyekiti wa kamati ya uhamasishaji na Cliford Ndimbo, Afisa habari wa TFF.

 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari, wakifuatilia mkutano wa kutangaza maandalizi ya Taifa Stars kuelekea mechi yake ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2021) dhidi ya Equatorial Guinea utakachezwa jijini Dar es Salaam November 2019.
Mwenyekiti wa kamati ya uhamasishaji ya Taifa Stars Haji Manara (wa pili kulia) akiongea na waandishi wa habari wakati wa kutangaza maandalizi ya Taifa Stars kuelekea mechi yake ya kufuzu fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON 2021) dhidi ya Equatorial Guinea. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF Kidau Wilfred akifuatiwa na Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Anitha Msangi Na kushoto ni Afisa habari wa TFF Cliford Ndimbo.


Mdhamini mkuu wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries (SBL) kupitia bia yake ya Serengeti Premium Lager, imeahidi kuendelea kuwapa raha wapenzi wa soka hapa nchini kupitia udamini wake kwa Timu ya Taifa. 

Taifa Stars, inatarajia kucheza mechi yake ya kufuzu tiketi ya Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2021) dhidi ya Equatorial Guinea Novemba 15 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza wakati wa kutangaza maandalizi kuelekea mechi hiyo, Meneja Masoko wa SBL Anitha Msangi alisema SBL kupitia bia yake ya Serengeti Premium Lager ipo bega kwa bega na Timu ya Taifa pamoja na mashabiki wa soka. 

“SBL kupitia bia yetu ya Serengeti Premium Lager tutataendelrea kuwapa burudani mashabiki wa soka kwa kuhakikisha tunaiwezesha timu yetu ya taifa kufanya vizuri lakini pia kupitia bia ya Serengeti kuwafanya mashabiki wafurahie mechi pamoja na bia yao pendwa,” alisema 

Anitha alisema, ili kuhakikisha Watanzania wengi zaidi wanafurahia mechi hiyo, kampuni ya SBL itaweka skirini kubwa sehemu mbali mbali ambazo zitaonyesha mechi bure huku nafasi ya kufurahia bia ya Serengeti ikitolewa. 

“Tujitokeze kwa wingi kuishangia timu yetu huku tukifurahia bia yetu ya Srengeti Premium Lager ambayo ni fahari yetu,” alisema .Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Kidau Wilfred alisema timu itaingia kambini hivi karibuni kujiandaa na mchezo huo wa nyumbani.. 

Kidau alifafanua kuwa, mchezo wa pili wa kufuzu AFCON utachezwa ugenini ambapo Stars wataenya na Libya Novemba 19,2019, siku 4 tu baada ya kucheza mchezo wa kwanza. 

“Tunawaomba Watanzania kwa pamoja tuungane kwa ajili ya timu yetu ya Taifa. Tujitokeze kwa wingi siku ya mechi na kuishangilia kwa nguvu zetu zote ili kuwapa hamasa wachezaji wetu waweze kufanya vizuri,” alisema Ndimbo.

PETROBENA YATOA MIFUKO 100 YA SARUJI KUSAIDIA UJENZI WA MADARASA KATIKA MANISPAA YA TABORA

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala (kushoto) akipokea msaada mifuko ya mbolea kutoka Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena Peter Kumalilwa (kulia) kwa ajili ya kuunga mkono kampeni ya utunzaji wa mazingira katika Manispaa ya Tabora.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena Peter Kumalilwa akitoa maelezo mafupi leo kabla ya kukabidhi mifuko 100 ya saruji kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala(wa pili kutoka kushoto) .
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala akitoa maelezo mafupi leo kuhusu kampeni ya kuboresha miundombinu ya elimu kabla ya kupokea mifuko 100 ya saruji kutoka Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena.
Bwana shamba na Mauzo wa Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena Khaji Halidi akitoa maelezo leo kuhusu matumizi ya mbolea za aina mbalimbali wakati walipokabidhi mbolea za kukuzia miti kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala( mwenye shati nyeupe) 
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala (kushoto) akipokea msaada mifuko ya saruji 100 kutoka Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena Peter Kumalilwa (kulia) kwa ajili ya kuunga mkono kampeni ya uboreshaji wa miundombinu ya elimu katika Manispaa ya Tabora.PICHA NA TIGANYA VINCENT

……………………………………………………

KAMPUNI ya Petrobena East Ltd imetoa mifuko 100 ya saruji na mifuko 10 ya mbolea katika Manispaa ya Tabora ikiwa ni kuunga mkono juhudi Serikali za ujenzi wa madarasa na utunzaji wa mazingira.

Msaada huo umekabidhiwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Peter Kumalilwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala.

Alisema kuwa Kampuni hiyo imefurahishwa na juhudi za Serikali za kuboresha elimu nchini zinazoendelea na hivyo wameamua kushiriki katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira mazuri ya kujifunzia.

Kumalilwa alisema kuwa sanjari na utoaji wa saruji hiyo wameamua kutoa mbolea mifuko 10 kwa ajili ya kukuzia miti ambayo imepandwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Tabora ili kulinda mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala alisema kuwa msaada huo utasaidia kuunga mkono jitihada zao za kuboresha miundombinu ya elimu katika Manispaa ya Tabora kwa ya kuweka mazingira mazuri ya wanafunzi kupata elimu ikiwemo kuwapunguzia kutembea umbali mrefu kutafuta elimu.

Alisema mifuko 50 itakwenda kata ya Uyui na iliyobaki 50 itapelekwa Kata ya Ifucha ili kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Kitwala alisema wako katika kampeni ya kuhakikisha kuwa inaondoa tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa na kujenga hosteli kwa ajili ya wanafunzi ili kuwasaidia kutembea umbali mrefu kutoka kwao hadi shule , jambo linalodhofisha ufaulu wa wanafunzi.Aidha alisema kuwa pia wanampango wa kujenga Sekondari katika Kata ya Ifucha ambayo haina Sekondari.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Ifucha Juma Abdallah aliishukuru Serikali kwa hatua ya kuamua sehemu ya msaada uliotolewa na Petrobena kusaidia wananchi wa eneo hilo ili kuongeza vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi.

Aliongeza kuwa tayari wananchi wa endeo hilo wamekusanya vifaa mbalimbali kama vile mchanga na mawe wakisubiri kuungwa mkono ili nao waweze kujenga Sekondari yao ya Kata kwa ajili ya kuondolea adha ya kutembea umbali mrefu wanafunzi wanasoma Sekondari katika Kata jirani.

Naye Said Ntahondi aliishukuru Kampuni ya Petrobena kwa kutoa msaada huo ambao sehemu ya mifuko hiyo itasaidia kujenga vyumba vya madarasa katika Shule shikizi.

Alisema shule shikizi zinasaidia kupunguza tatizo la watoto kutembea umbali mrefu kutafuta haki yao ya kupata elimu.Aidha Ntahondi aliishukuru Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena kwa kuamua kushughulikia tatizo la zao la tumbaku ikiwemo usambazaji wa mbolea mapema.

KAMPUNI ya Petrobena East Ltd imetoa mifuko 100 ya saruji na mifuko 10 ya mbolea katika Manispaa ya Tabora ikiwa ni kuunga mkono juhudi Serikali za ujenzi wa madarasa na utunzaji wa mazingira.

Msaada huo umekabidhiwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Peter Kumalilwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala.

Alisema kuwa Kampuni hiyo imefurahishwa na juhudi za Serikali za kuboresha elimu nchini zinazoendelea na hivyo wameamua kushiriki katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira mazuri ya kujifunzia.

Kumalilwa alisema kuwa sanjari na utoaji wa saruji hiyo wameamua kutoa mbolea mifuko 10 kwa ajili ya kukuzia miti ambayo imepandwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Tabora ili kulinda mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala alisema kuwa msaada huo utasaidia kuunga mkono jitihada zao za kuboresha miundombinu ya elimu katika Manispaa ya Tabora kwa ya kuweka mazingira mazuri ya wanafunzi kupata elimu ikiwemo kuwapunguzia kutembea umbali mrefu kutafuta elimu.

Alisema mifuko 50 itakwenda kata ya Uyui na iliyobaki 50 itapelekwa Kata ya Ifucha ili kusaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Kitwala alisema wako katika kampeni ya kuhakikisha kuwa inaondoa tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa na kujenga hosteli kwa ajili ya wanafunzi ili kuwasaidia kutembea umbali mrefu kutoka kwao hadi shule , jambo linalodhofisha ufaulu wa wanafunzi.

Aidha alisema kuwa pia wanampango wa kujenga Sekondari katika Kata ya Ifucha ambayo haina Sekondari.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Ifucha Juma Abdallah aliishukuru Serikali kwa hatua ya kuamua sehemu ya msaada uliotolewa na Petrobena kusaidia wananchi wa eneo hilo ili kuongeza vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi.

Aliongeza kuwa tayari wananchi wa endeo hilo wamekusanya vifaa mbalimbali kama vile mchanga na mawe wakisubiri kuungwa mkono ili nao waweze kujenga Sekondari yao ya Kata kwa ajili ya kuondolea adha ya kutembea umbali mrefu wanafunzi wanasoma Sekondari katika Kata jirani.

Naye Said Ntahondi aliishukuru Kampuni ya Petrobena kwa kutoa msaada huo ambao sehemu ya mifuko hiyo itasaidia kujenga vyumba vya madarasa katika Shule shikizi.

Alisema shule shikizi zinasaidia kupunguza tatizo la watoto kutembea umbali mrefu kutafuta haki yao ya kupata elimu.

Aidha Ntahondi aliishukuru Kampuni ya Usambazaji wa Mbolea ya Petrobena kwa kuamua kushughulikia tatizo la zao la tumbaku ikiwemo usambazaji wa mbolea mapema.

Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania Foundation watembelea shule ya Sekondari Mtakuja ikiwa ni sehemu ya kukuza upatikanaji wa elimu bure nchini.

$
0
0

Mratibu wa Instant Schools Christine Lucas (kati) akiwagawia vitabu  wanafunzi wa shule ya sekondari Mtakuja ya jijini Dar es Salaam .


Mratibu wa Instant Schools Christine Lucas (kushoto) akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Mtakuja ya jijini Dar es Salaam kuhusu mfumo huo unavyofanya kazi wakati wafanyakazi wa Vodacom Tanzania Foundation walipofanya ziara katika shule hiyo. Mfumo huu unasaidia wanafunzi kujisomea popote wanapokuwa bila gharama yeyote ile. VTF ilitoa kompyuta 24 zilizounganishwa na intaneti vyote vikiwa na thamani ya shilingi 131,904,000/=

MAKAMU WA RAIS SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA MAWAZIRI WA AFYA WA NCHI ZA SADC

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Katibu Mtendaji wa SADC Dkt. Stergmena Tax  baada ya kufungua Mkutano wa siku tano kwa Mawaziri wa Sekta ya Afya na Ukimwi  kwa Nchi Kumi na Sita Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Unaojadili Mustakbali wa Masuala yote ya afya,  Mikakati dhidi ya Ukimwi, kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya Mwaka 1999,  Mpango Mkakati wa Kanda wa Masuala ya Afya na kuridhia kwa pamoja Maazimio mbalimbali yanayohusiana na  Afya kwa Nchi za SADC.  Mkutano huo Umefunguliwa leo Novemba 07,2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu alipowasili katika Ukumbi wa  Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT  CC) Jijini Dar es salaam leo Novemba 07, 2019 kwa ajili ya kufungua Mkutano wa siku tano kwa Mawaziri wa Sekta ya Afya na Ukimwi  kwa Nchi Kumi na Sita Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Unaojadili Mustakbali wa Masuala yote ya afya,  Mikakati dhidi ya Ukimwi, kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya Mwaka 1999,  Mpango Mkakati wa Kanda wa Masuala ya Afya na kuridhia kwa pamoja Maazimio mbalimbali yanayohusiana na  Afya kwa Nchi za SADC.  (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  (kushoto) akiwa ameambatana na Katibu Mtendaji wa SADC Dkt. Stergmena Tax  (kulia)  pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiondoka baada ya kufungua Mkutano wa siku tano kwa Mawaziri wa Sekta ya Afya na Ukimwi  kwa Nchi Kumi na Sita Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Unaojadili Mustakbali wa Masuala yote ya afya, Mikakati dhidi ya Ukimwi, kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya Mwaka 1999,  Mpango Mkakati wa Kanda wa Masuala ya Afya na kuridhia kwa pamoja Maazimio mbalimbali yanayohusiana na  Afya kwa Nchi za SADC.  Mkutano huo Umefunguliwa leo Novemba 07,2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es salaam. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Mkutano wa siku tano kwa Mawaziri wa Sekta ya Afya na Ukimwi  kwa Nchi Kumi na Sita Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Unaojadili Mustakbali wa Masuala yote ya afya,  Mikakati dhidi ya Ukimwi, kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya Mwaka 1999,  Mpango Mkakati wa Kanda wa Masuala ya Afya na kuridhia kwa pamoja Maazimio mbalimbali yanayohusiana na  Afya kwa Nchi za SADC.  Mkutano huo Umefunguliwa leo Novemba 07,2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT CC) Jijini Dar es salaam. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Baadhi ya Wajumbe baada yakufungua Mkutano wa siku tano wa Mawaziri wa Sekta ya Afya na Ukimwi  kwa Nchi Kumi na Sita Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Unaojadili Mustakbali wa Masuala yote ya afya,  Mikakati dhidi ya Ukimwi, kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya Mwaka 1999,  Mpango Mkakati wa Kanda wa Masuala ya Afya na kuridhia kwa pamoja Maazimio mbalimbali yanayohusiana na  Afya kwa Nchi za SADC.  Mkutano huo Umefunguliwa leo Novemba 07,2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es salaam.

TCRA kampeni ya Mnada kwa Mnada wilayani Mafia katika utoaji wa Elimu ya Usajili wa laini kwa kutumia alama za vidole.

$
0
0
Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Lawi Odiero akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Mafia katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya kuhamasisha usajili wa Laini za Simu kwa alama za Vidole katika uwanja wa Kilindoni Wilayani Mafia mkoani Pwani.
Mkuu wa Kitengo wa Huduma za Bidhaa za Mawasiliano wa TCRA Thadeo Ringo akizungumza na mwananchi wa Mafia katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada wilayani Mafia.
Wananchi wakisajili laini za simu kwa alama za vidole.
Mwananchi akisoma kitabu cha muongozo cha TCRA

**********************************

Wakazi wa wilaya ya Mafia na viunga vyake wamejitokeza kwa wingi katika kampeni ya Mnada kwa Mnada ambapo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikishirikiana na Kampuni ya simu, Jeshi la Polisi Kitengo cha Uhalifu Mitandaoni na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Idara ya Uhamiaji kwa ajili ya utoaji wa huduma za usajili wa laini za simu kwa kutumia vitambulisho vya kitaifa na kuhakikiwa na kampuni za simu kwa kuweka alama za vidole kwa laini za simu.

Kampeni tangu imeanzishwa imekwenda katika Mikoa 17 lengo kuu ni nchi nzima kufikiwa na Kampeni hiyo.

Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa TCRA Mhandisi Lawi Odiero amesema ni fursa kwa wananchi wa Wilaya ya Mafia kufika katika uwanja wa Kilindoni kwa ajili ya kusajili kwa alama za vidole pamoja na kujiandikisha kupata usajili wa vitambulisho vya Taifa kutokana na kuwa na mnyororo wadau wa mawasiliano.

Mhandisi Odiero amesema kuwa Mnada kwa Mnada TCRA ilianzisha ili kutoa fursa ya Wananchi kuhudumiwa hasa wakati huu usajili wa laini za simu kwa alama za vidole pamoja Huduma zingine za mawasiliano..

Aidha amesema Kampeni hiyo ni kuimarisha ulinzi katika huduma za simu pamoja kufanya mawasiliano kuwa salama katika nchi.

Amesema kuwa kampeni ya Mnada kwa Mnada ni kwa ajili ya kutoa elimu ya mawasiliano kwa kushirikiana na wadau katika kujibu changamoto wanazokutanazo katika utumiaji wa mawasiliano nchini.

Mhandisi Odiero amesema kuwa wananchi wasio kuwa na Vitambulisho vya NIDA wahakikishe wanapata katika usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole na huduma nyinginezo za Mawasiliano hayo.

Hata hivyo amesema kuwakuna watu wengine wanatumia mawasiliano ya simu bila kujua ambapo Jeshi Polisi lipo katika Kampeni ya Mnada kwa Mnada ili kutoa elimu kuhusiana makosa ya jinai ya matumizi ya simu.

Aidha amesema Kampeni hiyo ni endelevu katika kuwafikia ikiwa kuhakikisha kila mwananchi anajisajili laini yake kwa alama za vidole kwa kutumia kitambulisho cha taifa.Amesema TCRA iko kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi ili mtumie Mawasiliano kwa usalama kutokana na elimu tunayotoa.

Hata hivyo amesema kuwa wananchi wajitokeze katika kujisajili kwa alama za vidole kabla ya Desemba 31.“TCRA tutahakikisha tunawafikia katika wananchi katika utoaji wa elimu za utumiaji wa bidhaa za mawasiliano kwa kutatua changamoto katika huduma hiyo” amesema.Mhandisi Odiero.

Odiero amesema kuwa Kampeni hiyo imeanza kwa Mkoa wa Pwani hivyo wilaya zote zitakuwa.Nae Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa TCRA Mabel Masasi amesema kuwa mwitikio umekuwa mkubwa kwa Wananchi kutaka vitambulisho kwa ajili ya kusajili laini za simu kwa alama za vidole.
Masasi amesema kuwa Wananchi wa watumie Kampeni ya Mnada kwa Mnada ya TCRA kupata elimu na baada ya kuisha Mnada sehemu husika waende katika mamlaka husika kupata vitambulisho.

BENKI YA NMB ILIVYOJIKITA KUCHANGIA ELIMU MAENEO MBALIMBALI NCHINI

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Rorya  - Simon Chacha akiwa ameketi na wanafunzi  wa shule ya Msingi Minigo juzi (Jumanne) katika moja ya madawati yaliyotolewa na benki ya NMB  ili kusadia kupunguza uhaba wa madawati shuleni hapo. Wengine ni Kaimu Meneja wa Kanda ya Ziwa (Mwenye koti na Tai Nyeusi) – Amos Mubusi.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha - Mrisho Gambo(kushoto) akisalimiana na mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mrisho Gambo ya jijini Arusha wakati wa hafla ya kukabidhiwa meza na viti vyenye thamani ya shilingi 10 milioni vilivyotolewa na benki ya NMB. Katikati ni Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini - Aikansia Muro.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari Kihaka wilayani Kilolo - Iringa wakiwa wamebeba stuli za maabara muda mfupi baada ya kukabidhiwa na benki ya NMB.Benki ya NMB ilikabidhi meza na stuli 60 vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 10.
 Wanafunzi wa shule ya Msingi Maduma iliyoko Kata ya Maduma Wilayani Mufindi wakishangilia madawati waliyokabidhiwa na benki ya NMB juzi shuleni kwao.

NBC yazindua Klabu ya Biashara (NBC-B-Club) Mkoani Morogor

$
0
0

 Ofisa Uvuvi na Mifugo wa Manispaa ya Morogoro, Mohamed Chamzhim (wa tatu kushoto),  aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Morogoro katika uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya Benki ya NBC mkoani humo jana, akishikana mikono na Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassimu Hussein katika uzinduzi wa klabu hiyo Mkoani Morogoro jana. Klabu hiyo imeanzishwa kusaidia mahitaji ya wafanyabiashara wadogo na wa mkoa huo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Biashara NBC, Elvis Ndunguru, Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashra wa kati na Wadogo, Evance Luhimbo na Meneja wa Tawi la NBC Morogoro, Sophia Mwombelo.
  Ofisa Uvuvi na Mifugo wa Manispaa ya Morogoro, Mohamed Chamzhim (kushoto),  aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Morogoro katika uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya Benki ya NBC mkoani Morogoro,  akishikana mikono na Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassimu Hussein wakati akizindua rasmi klabu hiyo mkoani humo jana. Kulia ni Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Elvis Ndunguru.

  Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashra wa Kati na Wadogo wa Benki ya NBC, Evance Luhimbo akizungumza katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki hiyo kwa wateja wake wafanyabiashara  wadogo na wa kati Mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani humo.

 Ofisa Uvuvi na Mifugo wa Manispaa ya Morogoro, Mohamed Chamzhim (kushoto),  aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Morogoro katika uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya Benki ya NBC mkoani humo akikaribishwa na Mjumbe wa Bodi ya NBC, Dk. Kassimu Hussein wakati akiwasili kuzindua rasmi klabu hiyo mkoani humo jana. Katikati ni Meneja wa Tawi la NBC Morogoro, Sophia Mwombelo. Uzinduzi huo  ulitanguliwa na semina ya siku moja   juu ya kuwajengea uwezo wafanyabiasha wadogo na wa kati.
 Ofisa Biashara Mwandamizi Taarifa za Biashara na Takwimu kutoka Mamlaka ya Biashara Tanzania (Tantrade), Magdalena Shirima akitoa elimu kuhusu fursa za masoko ya nje ya nchi katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati Mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani humo.
 Ofisa Biashara wa Asasi ya Kusaidia Uwekezaji kwenye Kilimo (PASS), Irene Benedicto akizungumza katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wadogo na wa kati Mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani humo.

  Ofisa Mkuu Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Julius Mjenga akitoa elimu kuhusu kodi katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyabiashara wadogo na wa kati Mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani humo.
Baadhi ya wafanyabiashara wakifuatilia mada katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na benki ya NBC kwa wateja wake wafanyuabiashara wadogo na wa kati Mkoani Morogoro jana. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani humo.

Washindi wa 'Paka na Ushinde' wajinyakulia zawadi

$
0
0












KAMPUNI ya Rangi ya Plascon Tanzania, imewazawadia washindi mbalimbali wa promosheni ya 'Paka Rangi na Ushinde'.Promosheni hiyo sasa imefikia wiki ya tano, ambayo hadi sasa washindi 21 wamepatikana na kujishinda sh. milioni 1 kila mmoja.
Promosheni hiyo ilikuwa imepokea zaidi ya washindi 1,000 kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Rangi ya Plascon Tanzania, Hussein Jamal, alisema:“Tukiwa kama kampuni tulianza rasmi shindano hili Oktoba, kiukweli tumepata mwitikio mzuri. Promosheni ya Paka Rangi na Ushinde imethibitisha kuwa kampuni yetu hurudisha kwa uaminifu au fadhila kwa wateja wetu”.

Jamal pia alisema promosheni hiyo inaonesha jinsi gani Plascon inavyotimiza wajibu wake kwa Watanzania pamoja na dhumuni lao la kuongeza thamani ya soko la rangi kupitia bidhaa yao, katika ubora, uvumbuzi na kuwa suluhisho la rangi kwa watanzania.

Promosheni hiyo iliyopewa jina la 'Paka Rangi na Ushinde', ilianza Oktoba na itafikia ukomo Desemba 14 na kuwavutia mamia na maelfu kwa kila mshiriki kuwa na uhakika wa kujipatia muda wa maongezi wa sh.500 na bado anakuwa na nafasi ya kushinda sh. milioni moja.

Plascon hutoa zawadi ya sh. milioni 5 kila wiki kwa washindi mbalimbali.

Jamal aliongeza washiriki wanatakiwa kununua lita 20 ya rangi ya Plascon, na utapata utapewa kadi utakayoikwangua na kutuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda namba 15054, ili kuwa katika nafasi ya kushinda.

Viewing all 46369 articles
Browse latest View live




Latest Images