Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

WANAWAKE WAPEWA MBINU ZA KUGOMBEA NA KUSHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

$
0
0
 Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Theresia Sawaya akizungumza katika mafunzo ya uongozi kwa wanawake watia nia ya kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa kutoka vitongoji na vijiji kwenye baadhi ya kata wilaya Kishapu mkoani Shinyanga. 


Mtandao wa Jinsia Tanzania 'TGNP Mtandao' umetoa mafunzo ya uongozi kwa Wanawake,vijana na watu wenye ulemavu waliotia nia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24,2019 ili kuwajengea uwezo,ujasiri,mbinu na mikakati ya kuingia katika kinyang'anyiro cha uchaguzi na kushinda.

Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza leo Jumatano Oktoba 23,2019 kwenye ukumbi wa BM uliopo katika kata ya Maganzo wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga na kukutanisha watia nia 65 kutoka baadhi ya kata za wilaya ya Kishapu.

Mwezeshaji wa mafunzo hayo,Theresia Sawaya ambaye ni Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wanawake,vijana na watu wenye ulemavu waliotia nia kugombea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ili waweze kugombea na kushinda kwa kishindo.

"Tumekutana na watia ni kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi ili kuwafundisha kuhusu dhana za jinsia na namna zinavyotumika na athari zake katika masuala ya uongozi lakini pia kuwajengea uwezo namna ya kufanya kampeni kwenye uchaguzi,namna ya kupata rasilimali fedha na ulinzi na usalama wa wagombea",alieleza Sawaya.

Alisema kupitia mafunzo hayo wanatarajia wanawake ambao katika miaka ya nyuma wamekuwa nyuma kushiriki kwenye masuala ya uchaguzi watahamasisha na kupata ujasiri wa kugombea na kushinda katika uchaguzi na kushiriki katika ngazi mbalimbali za maamuzi.

Kwa upande wake, Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Eva Hawa ambaye pia ni mwezeshaji katika mafunzo hayo aliwataka wanawake watia nia kugombea kwenye uchaguzi kuhakikisha wanawashirikisha waume zao ili kupata matokeo mazuri zaidi.

"Wanawake tunapogombea madaraka ni vyema kuwashirikisha watu wanaotuzunguka,washawishini waume zenu wawaunge mkono ikibidi muwaombe wawe makampeni meneja wenu,wataongea na wanaume wenzao ili wawape kura na mtapata ushindi mnono",alisema Juma.
Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Theresia Sawaya akielezea kuhusu mafunzo ya uongozi kwa wanawake watia nia ya kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa kutoka vitongoji na vijiji kwenye baadhi ya kata wilaya Kishapu mkoani Shinyanga.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Theresia Sawaya ambaye ni Mwezeshaji katika mafunzo ya uongozi kwa wanawake watia nia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa akiwahamasisha wanawake kujiamini kwani wanaweza kuongoza jamii kutokana na kwamba mwanamke ni kiongozi kuanzia ngazi ya familia.
Wanawake watia nia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini. Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Eva Hawa ambaye pia ni mwezeshaji katika mafunzo ya uongozi kwa wanawake watia nia kugombea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa akiwasisitiza kuepuka rushwa ya ngono kwenye uchaguzi. 
Mwanasheria kutoka TGNP Mtandao Eva Hawa akizungumza wakati wa mafunzo ya uongozi kwa wanawake watia nia kugombea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa akiwasisitiza kuepuka rushwa ya ngono kwenye uchaguzi.
Diwani wa Kata ya Mwadui Luhumbo,Mhe. Sarah Masinga akiwatia moyo wanawake waliotia nia kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa kuwa wajiamini,wamtangulize Mungu na kushirikiana na jamii ili kushinda katika nafasi wanazogombea.
Washiriki wa mafunzo hayo wakisiliza nasaha mbalimbali.
Mwenyekiti wa vituo vya taarifa na maarifa wilaya ya Kishapu Rahel Madundo akiwasisitiza wanawake kupendana na kuacha tabia ya kukwamishana wao kwa wao.
Mtia nia ya kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa,Mary Richard Nzingula akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa ukumbini.
Mlezi wa wanawake watia nia ya kugombea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa wilaya ya Kishapu,Mhe. Suzana Makoye ambaye ni Diwani wa Viti Maalum kata ya Maganzo akiwasisitiza wanawake watia nia kutokata tamaa pale wanapokutana na changamoto mbalimbali.

Tigo yaifikisha promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo Jijini Arusha

$
0
0

Kaimu mkurugenzi wa kampuni ya simu za mkononi,Aidan Komba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo iliyofanyika Jijini Arusha.Pembeni yeke ni Mtaalamu wa huduma za Kidigitali wa Tigo,Fabian Felician
Mtaalamu wa huduma za Kidigitali wa Tigo,Fabian Felician akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo iliyofanyika Jijini Arusha.Pembeni yeke ni Kaimu mkurugenzi wa kampuni ya simu za mkononi,Aidan Komba


Wateja wa Tigo wanaoshiriki katika promosheni ya Tigo Fiesta 2019 Chemsha Bongo kwa mara ya kwanza wana nafasi ya kushinda hadi Sh1 milioni kila wiki huku mshindi wa jumla ataweza kujinyakulia gari mpya aina ya Renault Kwidyenye thamani ya Sh23 milioni.


Meena Ally akitoa maelezo jinsi ya kushinda Gari mpya (0kms) aina ya Renalt Kwid kwenye promosheni ya #TigoFiestaChemshaBongo. Tuma Neno "Muziki" kwenda 15571


SBL yatimiza miongo miwili ya ukuaji kwa kuzindua nembo mpya

$
0
0
 Waziriwa Viwanda na Biashara Mh. Innocent Bashungwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa nembo mpya ya Kampuni ya Serengeti Breweriers kwenye hoteli ya Coral Beach jana.

 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya SBL John Ulanga akizungumza wakati wa uzinduzi wa nembo mpya ya Kampuni ya Serengeti Breweriers kwenye hoteli ya Coral Beach jana.



 Mkurugenzi mtendaji wa SBL Mark Ocitti akizungumza wakati wa uzinduzi wa nembo mpya ya Kampuni ya Serengeti Breweriers kwenye hoteli ya Coral Beach jana.
 Nembo mpya ya Serengeti Breweries ikizinduliwa
 Cheerrsssss baada ya uzinduzi




Baadhi ya wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika uzinduzi huo.

Ikiwa ni zaidi ya miongo miwili tangu ianze kufanya shughuli zake hapa nchini, kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), leo imezindua nembo mpya itakayoitambulisha na kuonyesha historia ya ukuaji wake tangu ianzishwe mwaka 1996.

“Nembo mpya ya SBL inasimama ikiwakilisha ubora, ubunifu, utaalaum, urafiki na kujiamini. Nembo hii pia inaonyesha kuwa kampuni yetu inatengeneza bia zake kwa viungo asilia,” Mkurugenzi mtendaji wa SBL Mark Ocitti aliwaambia wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa nembo hiyo mpya jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, nembo hiyo ni kielelezo cha historia pamoja na vipindi ilivyopitia kampuni hiyo kwa miaka yote tangu ikimiliki kiwanda kimoja kidogo cha kuzalisha bia jijini Dar es Salaam hadi kufikia kampuni kubwa inayomiliki viwanda vitatu vilivyopo Dar es Salaam, Moshi na Mwanza huku ikitoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja zaidi ya 800.

Bia zinazozalishwa na SBL ni pamoja na Serengeti Premium Lager, Serengeti Lite, Pilsner Lager, Kibo Gold, Guinness pamoja na Senator. Bia hizi zimefanikiwa kushinda tuzo mbali mbali za kitaifa na kimataifa kutokana ubora pamoja na ubunifu unaotumika kuzitengeneza. SBL pia inasambaza pombe kali zinazoongoza kwa ubora na mauzo duniani kama Johnnie Walker, Smirnoff, White Horse, Gordons, Baileys na nyinginezo.

IIkijulikana kama mdhamini mkuu wa timu ya taifa (Taifa Stars), SBL katika kipindi cha miaka 10 imetekeleza miradi 17 ya maji nchi nzima kwa kuchimba visima kwenye sehemu zenye shida ya maji na kuwawezesha watu zaidi ya milioni 2 kupata maji safi na salama. Kwa mujibu wa Ocitti, kampuni hiyo inashirikiana na Wizara ya Kilimo kuwasaidia wanafunzi wanaofanya vizuri kutoka familia za wakulima kupata elimu ya chuo kupitia ufadhili chini ya mpango wa SBL Kllimo-Viwanda Scholarship.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa nembo hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya SBL John Ulanga alisema nembo hiyo mpya inaakisi lengo jipya la ukuwaji wa kampuni hiyo na kuongeza kuwa SBL imewekeza Paundi za Uingereza milioni 14 katika shughuli zake na upanuzi. “Uwekezaji huu mkubwa, utasaidia kutengeneza ajira mpya zaidi, utaongeza mchango wa SBL kwenye kodi kwa Serikali,”alisema.

Tukio la uzinduzi lilifanywa na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa aliyeelezea kuridhishwa kwake na mchango wa SBL kwa uchumi wa nchi na kuahidi kuwa Serikali itandelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara kwa ajili ya malkampuni pamoja na biashara. Bashungwa alisema maboresho yanayaofanywa kwa sasa kwenye sera yanalenga kuondoa urasimu usio wa lazima kwa taasisi za umma ambao ni kikwazo kwa maendeleo na ukuaji wa biashara.

TAARIFA MUHIMU KWA UMMA UPATIKANAJI WA NIN KWA AJILI YA USAJILI WA KUHUISHA KAMPUNI NA MAJINA YA BIASHARA

TAARIFA MUHIMU KWA UMMA KUHUISHA TAARIFA ZA MAKAMPUNI NA MAJINA YA BIASHARA NDANI YA SIKU 90

Dun&Bradstreet wazindua alama ya mkopo kurahisisha utoaji wa mikopo nchini

$
0
0
Taasisi inayoongoza kuandaa taarifa za mikopo nchini Dun & Bradstreet Credit Bureau Tanzania Ltd. imezindua mfumo wa alama ya kwanza ya utabiri wa deni la mteja ili kuwawezesha wakopeshaji kama vile benki na taasisi za huduma ndogo za fedha kupata taarifa sahihi za wakopaji.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Afisa Mkuu Mtendaji wa Dun & Bradstreet Credit Bureau, Miguel Llenas alisema kuwa alama hiyo imezinduliwa ili kutatua changamoto zinazowakabili wadau wote katika soko la mikopo nchini.

Alisema mfumo wa alama hiyo utaongeza uwajibikaji katika kukopesha na kukopa, pia utasaidia wakopeshaji na wadai kusimamia vitabu vyao vya mkopo na kuhakikisha viwango vya riba hulingana na maelezo husika ya mkopaji na kukuza bidhaa za mkopo katika soko la wakopeshaji.

Alisema Alama ya Mikopo hutoa faida nyingi kwa mkopaji kwani humwezesha kujua kama anavyo vigezo vya kukopa au kutokukopa.

“Pia inapunguza muda wa kupata mkopo kulingana na taarifa za mkopo zilizopo kwenye ripoti zake hivyo kukuwezesha kama dhamana ya mkopo wako mpya na kukupatia mkataba bora na wenye kiwango stahiki cha riba.

"Inampa mkopeshaji taarifa sahihi za mchakato wa utoaji wa mikopo; ujumbe na mwongozo wa tathmini ya mkopaji, pia kuwezesha kasi ya utoaji mkopo na usimamizi wa wateja husika. "Pia mtoaji wa huduma anaweza kuongeza kasi ya upatikanaji wa wateja, kuelekeza na kusimamia mipaka ya mkopo yao na kuboresha utoaji wa huduma hizo.

Akifafanua zaidi kuhusu huduma hizo, Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Adebowale Atobatele alisema lengo lao kila wakati limekuwa kutoa suluhisho la usimamizi kuelekea mikopo isiyolipika katika sekta mbalimbali na kutoa taarifa sahihi kwa watoa mikopo kufanya maamuzi sahihi ya kutoa au kutokutoa mikopo.

"Lakini pia kuharakisha kasi yao ya kuchukua maamuzi; kurahisishaji upatikanaji wa haraka wa bidhaa za mikopo kwa kampuni zinazostahiki, watu binafsi na hivyo kukuza fursa za ukuaji kwa uchumi kwa wote.

“Pia tutaendelea kufanya kazi kwa karibu na wadau wote na wahusika wote nchini ili kusaidia kurahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi za mkopo nchini, "alisema. Alisema alama ya mkopo ni maelezo ya kihesabu ambayo wakopeshaji hutumia, pamoja na ripoti ya mkopo kutathmini hatari ya kutoa mkopo.

"Alama za mkopo ni njia muhimu za kukopesha ambayo inaweza kuamua ikiwa unapata mkopo, viwango gani vya riba unalipa kwa deni husika, "alisema.

Naye Ofisa Mkuu wa masuala ya Ufundi wa kampuni hiyo, Kelyn Pena alisema alama ya mkopo ya watumiaji wa D & B ni ya kipekee nchini Tanzania kwa sababu inatoa taarifa halisi za kitakwimu. "Alama hii ya mkopo ni rahisi kutumiwa na taasisi za kifedha na watumiaji kwa jumla kwani iko thabiti katika mpangilio wa wakati na utofauti wa historia ya mikopo ya watumiaji. " alisema.


Mkuu wa kitengo cha usimamizi wa fedha kutoka BOT, Jerry Sabi akizungumza namna mfumo wa alama za mkopo kwa wakopaji na wakopeshaji unavyosaidia kukuza sekta ya fedha na uchumi nchini.


Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Dun&Bradstreet Credit Bureau, Miguel Llenas akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa alama ya mkopo kwa wakopaji na wakopeshaji nchini. Mfumo huo umezinduliwa jijini Dar es Salaam kuwawezesha wakopeshaji kuwa na taarifa sahihi za wakopaji.

Meneja Mkuu wa kampuni ya Dun&Bradstreet Credit Bureau, Adebowale Atobatele akifafanua namna mfumo wa alama kwa mteja unavyozisaidia taasisi zinazokopesha wateja kupata taarifa sahihi za mkopaji.
 

WANANCHI WAASWA KUWEKEZA KWENYE TAFITI ZA DAWA ASILI

$
0
0


 Mkurugenzi wa Utafiti wa tiba asili, Joseph Otieno akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, Profesa Mohammed Sheikh na Mtafiti Mkuu Kiongozi waTume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Khadija Malima. 
 Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sayansi na Utafiti wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Profesa Mohammed Sheikh aikungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mtafiti Mwandamizi wa utafiti wa Mradi wa Fellow, Dk. Francis Machumi na katikati ni Mtafiti Mkuu Kiongozi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dk. Khadija Malima. 
 Mtafiti Mkuu Kiongozi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Khadija Malima akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia, Profesa Mohammed Sheikh na Mtafiti Mkuu Kiongozi wa Taasisi ya Dawa asili, Dk. Khadija Malima. 

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii
KUNA haja ya kuwekeza katika tafiti za ya dawa asilia nchini kwani Tanzania inamalia asili nyingi ambazo zitaweza kuimalisha afya ya kila mtu.

Hayo yamesemwa na Mtafiti Mkuu Kiongozi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dk. Khadija Malima jijini Dar es Salaam leo wakati akingumgumza na waandishi wa habari ikiwa ni kuelekea mkutano wa mabaraza ya kitafiti utakaofanyika jijini Dar es Salaam Novemba 11 hadi 15 unaondaliwa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH).

"Ili kuhakikisha dawa asilia ni salama kwa binadamu, dawa hizo zinaweze kutibu na kuondoa matatizo ya magonjwa, dawa hizo zinatakiwa kufanyiwa utafiti na zitengenezwe ka kiwango cha hali ya juu na kwauwingi".

Khadija Amesema kuwa viwanda vikishiriki katika utafiti wa dawa asilia tuweze kupata dawa na kufungua soko la dawa asilia kwa nchini za Afrika mashariki na katika na nchi za kusini mwa jangwa la sahara.

Hata hivyo amesema kuwa tunaweza kujikita katika matumizi ya fedha za uuma kwaajili ya kwaajili ya kufanya tafiti ambazo zitatupatia dawa za asili lakini sio lazima ziwe zifikie kiwango cha vidonge kwani hiyo itachukua miaka mingi, lakini tukitumia maliasili  tuliyokuwa nayo tunaweza pia kuwekeza ili kujiletea maendeleo.

"Ili kuhakikisha hizo dawa ni salama kwa binadamu, ziweze kutibu na kuondoa matatizo ya magonjwa,zinatakiwa zitengenezwe kwa kiwango cha hali ya juu na kwa uwingi".

Hata Hivyo Mkurugenzi wa taasisi ya dawa asili, Joseph Otieno amesema kuwa biashara ambayo mtu anaweza kuwekeza ni kwenye kitengo cha dawa asili kwani dawa huzi zinatafutwa na nchi za nje ikiwepo Marekani, Uholanzi, ujerumani, China na Kolea.

" Watu hawa wanakuja hapa Muhimbili katika Taasisi ya tiba asili wakihitaji tuweze kushirikiana nao ili waweze kujua dawa zinazotokana na miti dawa zinazoweza Kuendelezwa ili kupambana na maradhi yanayoongezeka duniani ambayo yamekuwa sugu na hayawezi kutibika kirahisi kwa dawa ambazo tayari zimevumbuliwa".

Otieno amesema kuwa Tanzania inamiti zaidi ya elfu 12 lakini kati ya hiyo zaidi ya asilimia 25 imesharekodiwa  kwamba ni ya dawa lakini kinachokosekana ni utafiti ambao unahusisha waganga wa asili, kuungwa mkono na serikali kuhakikisha kwamba hii miti inafanyiwa utafiti kwaajili ya kutibu magonjwa yanayotusumbua.

Barclays Bank continues to invest in Tanzania’s key growth sectors as the bank transitions into Absa

$
0
0



Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed addresses participants during the bank’s Corporate Clients Economic Forum held in Dar es Salaam on Wednesday.
Barclays Bank Tanzania (BBT) Board Chairman, Simon Mponji (left), shakes hands with Absa Group Deputy Chief Executive Officer, Peter Matlare, as the bank’s Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed looks on, during the Barclay’s corporate clients economic forum held in Dar es Salaam on Wednesday.
Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed (right), chats with Barclays Kenya Head of Corporate & Investment Banking, James Agin (left), while Engen Petroleum (T) Ltd Chief Executive Officer, Paul Muhato looks on, during Barclays’s corporate clients economic forum held in Dar es Salaam on Wednesday.
Absa Group Deputy Chief Executive Officer, Peter Matlare (left), greets Chief Executive Officer of UAP Old Mutual Insurance Tanzania Limited Stephen Lokonyo, during Barclays Bank Tanzania’s corporate clients economic forum held in Dar es Salaam on Wednesday. Looking on is BBT Corporate Banking Director, Brian Kalero.
Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed (left), chats with corporate executives during the bank’s corporate clients economic forum held in Dar es Salaam on Wednesday. Engrossed in the conversation from his left is BBT Corporate Banking Director, Brian Kalero, Chief Executive Officer of Kagera Sugar Limited, Ashwin Rana and Barclays Kenya Head of Corporate & Investment Banking, James Agin

Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed (left), talks to Barclays Kenya Head of Corporate & Investment Banking, James Agin (right) and Kagera Sugar Chief Executive Officer, Ashwin Rana, during Barclays corporate clients economic forum held in Dar es Salaam on Wednesday.


Barclays Bank Tanzania Limited (BBT) was joined by Senior Executives, Mr. Peter Matlare, the Absa Group Deputy Chief Executive Officer and Mr. Saviour Chibiya, the Regional Managing Director for the Absa Africa Operations on Wednesday, 23rd of October at Serena Hotel in Dar es Salaam, to host some of its customers to a cocktail event.

The event was not only a platform to appreciate the continued support of its customers but was also used to provide an opportunity for clients to join BBT in its transition journey and be informed of the expected milestones as the Bank prepares to rebrand into Absa.

In addition, BBT also offered clients access to Absa research on the current Global and Tanzania macroeconomic environment. The report, presented by Mr. Ridle Markus, Absa's macroeconomist for Sub Sahara Africa, commended Tanzania’s impressive growth rate in recent years despite a number of global and domestic challenges. Ridle also provided customers with insights on the increasingly challenging global macroeconomic backdrop.

In an update on rebranding, the bank’s Managing Director, Mr. Abdi Mohamed said, “Our brand and name change to Absa is proceeding as planned. We have taken a sequenced approach and expect some branches to reflect several elements of the new brand by mid-November, while some branches will retain the current look. The intention is to take our customers and the public with us through the transformation journey visually. We will however continue to operate and trade as Barclays Bank Tanzania Limited until our name officially changes, as approved by the Regulator.”

Speaking on the bank’s commitment to Tanzania, Mr. Mohamed said, “Barclays is committed to serving its customers and we are proud of the momentum we have built over the past 3 years. Our commitment to our clients has been demonstrated in the successful execution of key financing transactions amounting to TZS 529bn, across sectors such as Oil & Gas, Public Sector, Manufacturing and Agriculture. In addition, our non-funded strategy and focus has been reaffirmed by The Asian Banker 2019 recognition of BBT as the best ‘Cash Management Bank in Tanzania’.

Further, the bank’s Corporate Director, Mr. Brian Kalero highlighted that ‘’BBT is geared to supporting the private and public sector customers in driving sustainable economic growth across various sectors. As our customers grow their businesses, we are well positioned to continue to support their various funding requirements and provide digitally led transactional banking solutions which are aimed at creating efficiency in the way we do business.”

Mr. Brian was also honored to announce the Bank’s wins at the 12th EMEA Finance African Banking Awards 2019, where BBT was awarded the ‘Best Investment Bank in Tanzania’ for the second year in a row, demonstrating BBT’s continued growth and the differentiated proposition of our Global Markets business. “Awards such as these demonstrate our capability to go to extraordinary lengths to overcome unique challenges, regardless of how intricate the deals are or scale to bring our client’s goals and possibilities to life.” Brian remarked.

In conclusion, Mr. Mohamed; called for clients to remain vigilant, saying “We will not ask any customer for additional information during this time, and all customer account details will remain the same before and after the transition. Customers will continue to bank with us as safely as they always have.”

Wafanyakazi wa Benki ya NMB wachangia damu kwa wagonjwa 240 wenye uhitaji

$
0
0

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam Badru Idd (wa pili kulia) akiwaongoza wenzake kuchangia damu katika Hospitali ya Ocean Road.

Taasisi ya Saratani ya Ocean Road inakabiliwa na uhaba wa damu hali inayosababisha wakati mwingine huduma kushindwa kutolewa kwa ufanisi.

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Tiba wa Ocean Road, Dk. Mark Mseti, amesema kwa siku za hivi karibuni hospitali hiyo imekuwa ikikabiliwa na uhaba mkubwa wa damu hali inayokwamisha utoaji huduma kwa wahitaji.

Mseti alisema mahitaji ya damu katika hospitali hiyo ni makubwa kutokana na tiba zote za mionzi kuhitaji wagonjwa kuwa na damu ya kutosha ili ziweze kufanya kazi sawasawa .

“Tunahitaji chupa za damu 40 hadi 50 kila siku, kuna wakati Mpango wa Taifa wa Damu Salama unaileta kwa kiwango kinachostahili tunapata chupa 50 au 40 na tunaweza kufanya kazi kama inavyostahili lakini hivi karibuni kwa takribani wiki mbili hivi kumetokea uhaba mkubwa wa damu kwenye taasisi yetu. Kwa mfano jana na juzi tulipata chupa zisizozidi 20 kwa siku,” amesema Dk Mseti.

Katika kujaribu kukabiliana na changamoto hiyo wafanyakazi wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam wametumia huu mwezi wa Huduma kwa Wateja kwa kuchangia uniti 97 za damu.Dk. Mseti amesema kiasi hicho cha damu kitatumika kwa wagonjwa 240 wenye uhitaji wa tiba hiyo.

Meneja wa NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd, amesema lengo la kushiriki zoezi hilo ni kuangalia jinsi ya kuokoa maisha ya watanzania wenzao wenye uhitaji.Amesema kupitia zoezi hilo walilolifanya,anatoa rai kwa Watanzania wengine kushiriki kuokoa maisha kwa kuchangia damu

“Nimetembezwa hospitalini unakuta hata hiyo damu inayohitajika haipo au ni kidogo, watanzania tujitolee kuokoa maisha ya wenzetu,” amesema

KAMPUNI YA MAFUTA YA ENGEN YAADHIMISHA WIKI YA USALAMA

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Paul Muhato (wa pili kulia) akifafanua jambo kwa baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wakikagua moja ya kisima cha mafuta ikiwa ni sehemu ya kilele cha Wiki ya Usalama ambayo huadhimishwa kati ya tarehe 21 mpaka 25, Oktoba Duniani kote, ambapo kwa upande wa Engen wamefanya kilele hicho kwa kutembele na kukagua sehemu za usalama katika Kituo chao cha Mikocheni Jijini Dar es salaam leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya Engen Tanzania, Paul Muhato akikagua moja ya mitundi ya kuzimia moto, katika Kituo cha mafuta cha Engen Mikocheni ikiwa ni sehemu ya kilele cha Wiki ya Usalama ambayo huadhimishwa kati ya tarehe 21 mpaka 25, Oktoba Duniani kote, ambapo kwa upande wa Engen wamefanya kilele hicho kwa kutembele na kukagua sehemu za usalama katika Kituo chao cha Mikocheni Jijini Dar es salaam leo. 











PUMA ENERGY, SELCOM NA MASTERCARD WAUNGANA KUHAMASISHA MALIPO YA KIELEKTRONIKI

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Dominic Dhanah akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Bomba Weekend katika kituo cha kuuza mafuta cha Puma Energy Upanga jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Selcom Paytech LTD, Sameer Hirji, akizungumza na waandishi wa habari katika kituo cha mafuta cha Puma Energy Upanga jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya BombaWeekend kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Dominic Dhanah.

Baadhi ya wateja wakikaribishwa na wafanyakazi wa Puma Energy kwa ajili ya kujaza mafuta kwa kutumia kadi ya Master Card kwenye kituo cha kuuza mafuta cha Puma Energy Upanga.
Bw. Modestus Chambu mmoja wa wateja wa kampuni ya Puma Energy akijaziwa mafuta kwa kadi ya Master Card kwenye kituo cha kuuza mafuta cha Puma Energy Upanga jijini Dar es salaam.
Wateja wakiendelea kuhudumiwa na wafanyakazi wa Puma Energy Upanga jijini Dar es salaam.
Bw. Modestus Chambu mmoja wa wateja wa kampuni ya Puma Energy akiwaelezea waandishi wa habari faida anazozipata kwa kujaza mafuta kutumia mfumo wa Kielektroniki Master Card.


KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania, Selcom Paytech LTD na Mastercard kwa wamezindua kampeni ya pamoja iitwayo BombaWeekend yenye lengo la kurejeshea asilimia tano ya fedha watakayotumia watakapojaza mafuta katika vituo vya Puma Energy endapo watalipia kupitia Mastercard QR.

Uzinduzi huo umefanyika jijini Dar s Salaam na itaendeshwa kwa wiki 11, kila Ijumaa hadi Jumapili kuanzia saa 10 hadi 12 jioni kupitia mtandao wa Puma wenye vituo 52 nchi nzima. Pamoja na dhumuni la kuzawadia watumiaji wa huduma hiyo, Bomba Weekends ina dhamira ya kuchangia katika juhudi za serikali za kurasimisha malipo na kuhamasisha uchumi wa malipo ya kieletroniki ili kufikia malengo ujumuishaji wa kifedha wa nchini Tanzania.

Pia imeelezwa kwamba mchakato mzima wa kurudishia pesa wakati wa Bomba Weekends unaendeshwa kupitia huduma ya zawadi kwa wateja ya Qwikrewards iliyoundwa na Selcom Paytech LTD mahususi kwa watumiaji wa Mastercard QR.

Na kwamba Qwikrewards inamuwezesha mtu yeyote kukusanya pointi au kupata pesa taslim kupitia akaunti iliyounganishwa na namba yake ya simu kila afanyapo malipo kutumia Mastercard QR. Watumiaji Qwikrewards wanaweza kukomboa pointi walizokusanya kwa kupiga 150*15 na kuzitumia katika maeneo zaidi ya 30,000 nchini ambapo Mastercard QR inakubalika kama njia ya malipo.

Aidha Mastercard QR imepiga hatua kubwa tangu kuanzishwa kwake nchini mwaka 2018 hadi sasa kupelekea kukubalika na watoa huduma mbali mbali zaidi ya 30,000 kuwa na uwezo wa kupokea malipo kutoka mitandao yote 7 ya simu na benki 15 nchini.

Akizungumza kwa kina kuhusu kampeni hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania Dominic Dhanah amesema "Bomba Weekends inahamasisha wateja we kulipia mafuta katika vituo vyao kwa kutumia njia rahisi, haraka na salama zaidi na kunufaika papo hapo kupitia Qwikrewards kutoka Puma.

Amesema ushirikiano huu unadhahiri kwamba Puma ni kiongozi wa katika sekta ya mafuta inapofikia kujiunga na suluhisho bunifu za malipo ambazo hurahisisha malipo kwa wateja wetu na kutuwezesha kutoa huduma bora zaidi katika vitu vyetu."

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Selcom Paytech LTD, Nd. Sameer Hirji, alionyesha matumaini makubwa kuelekea uchumi wa malipo ya kielektroniki akisisitiza kuwa ni lazima taasisi ambazo zinaongoza mchakato huo kuongeza thamani kwa wateja ili kuwapa hamasa zaidi kutumia malipo ya elektroniki.

"Kupitia Bomba Weekends tukishirikaina Puma Energy pamoja na Mastercard QR tumedhamiria kuwazawadia wateja watakaolipa kielektroniki katika matumizi yao ya kila siku, mafuta yakiwa sehemu kubwa ya matumizi hayo.

" Tunaamini kwamba tunavyozidi kurahisisha na kuimarisha upatikanaji na upokeaji wa malipo ya kieletroniki ndivyo tutazidi kuwajengea Watanzania imani ya kutoka nyumbani bila pesa taslim. Tukiwa na Qwikreward na maeneo zaidi ya 30,000 ambapo Mastercard QR inakubali kitaifa tunaamini tunaongoza mabadiliko kuelekea malipo ya kielektroniki na malengo ujumuishaji wa kifedha nchini Tanzania,”amesema .

Wakati huo huo wadau mbalimbali wanatumia mfumo wa malipo kwa njia ya kieletroniki wamesema wamefurahishwa na uamuzi wa kampuni hizo kuungana kuhakikisha wanahamasisha ulipaji wa fedha kwa njia hiyo ambayo ni salama na yenye kurahisisha malipo.

Wamesema katika kipindi hiki cha kampeni hiyo wataitumia vema ili kupata asilimia tano ambayo imetolewa kama sehemu ya kupata fedha ambayo Puma wameamua kuirejesha kwa Watanzania.

Benk ya NBC yasaidia ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu jijini Mbeya

$
0
0
 .Naibu waziri Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa (wa tatu kulia) akipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kutoka kwa Meneja wa Benki yua NBC Kanda ya Kusini, Salema Kileo (wa pili kushoto), pamoja na baadhi yua wafanyakazi wenzake iliyotolewa na NBC kwa ajili ua ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu katika Jiji la Mbeya. Hafla ya makabidhiano ilifanyika jijini Mbeya jana.

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais MenejimentI ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa (katikati),  akizungumza wakati akipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kutoka kwa Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kusioni, Salema Kileo (wa pili kushoto), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake iliyotolewa na NBC ank ya NBC kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu katika Jiji la Mbeya. Hafla hiyo ilifanyika jijini humo jana.

 Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa akizungumza wakati akipokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kutoka Benki ya NBC kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu katika Jiji la Mbeya. Hafla hiyo ilifanyika Mbeya jana. Kulia ni Meneja wa NBC Kanda ya Kusini, Salema Kileo na kushoto ni Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Mwashikindi.
  Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Mwashilindi akizugumza wakati wa hafla ya kupokea msaada wa mifuko 600 ya saruji kutoka Benki ya NBC kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu jijini humo. Katikati ni  Naibu waziri Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa na kulia ni Meneja wa NBC Kanda ya Kusini, Salema Kileo.


 Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kusini, Salema Kileo akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wa mifuko 600 ya saruji kwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk Mary Mwanjelwa (kulia kwake), iliyotolewa na benki hiyo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya afya na elimu jijini Mbeya.  Mbeya,
Naibu waziri Ofisi ya Rais Menenjimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dk. Mary Mwanjelwa (katikati), Meya wa Jiji la Mbeya, Mchungaji David Mwashilindi (kushoto kwa naibu waziri), wakipozi kwa picha ya kumbukumbu mara baada ya hafla hiyo jijini Mbeya jana.

Viongozi Waandamizi NMB wawahudumia wateja matawini

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Biashara Benki ya NMB – Donatus Richard (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mohamed Mussa ambaye ni NMB Wakala katika Mtaa wa Livingstone, Kariakoo.

MKUU wa Masoko wa Benki ya NMB – Rahma Mwapachu (wapili kushoto) akimhudumia mteja wa benki – Petra Karamagi katika Tawi la Oyster Plaza.


Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya NMB – Omari Mtiga (katikati) akimsaidia mteja kujaza fomu ya kuweka fedha katika Tawi la Zanzibar.
Mkuu wa Idara ya Biashara za Serikali NMB – Vicky Bishubo, akizungumza na mteja wa benki hiyo – Nyamate Mayunga, alipomtembelea dukani kwake.Kushoto ni Meneja wa Tawi la Gongo la Mboto – Rehema Mwibura.

************************************

Benki ya NMB imeendelea kuadhimisha mwezi wa huduma kwa wateja kwa kuwafikia kwa ukaribu zaidi wateja wao.

Viongozi Waandamizi wa benki hiyo wameingia kwenye matawi mbalimbali yaliyopo kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar kuwahudumia wateja waliofika kupata huduma.

Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar – Idd Badru amesema programu hiyo waliyoiita ‘Make A Difference’ imelenga kuwaweka karibu watendaji wa benki na wateja wao wa kada zote.

Amesema kupitia njia hiyo wameweza kukutana na wateja wao na kujua kitu gani wanahitaji ili kuendelea kuboresha huduma wanazozitoa.

“Imekuwa ni siku nzuri kwanza wateja wamefurahi, wamekutana na viongozi wetu Waandamizi na wamewahudumia katika matawi yao na kuwatembelea katika maeneo yao ya biashara ”

“Pili imetupa fursa ya kusikiliza changamoto wanazokumbana nazo na imekuwa rahisi pia kuzipatia ufumbuzi kwa kuwa wengine wamekutana na wafanya maamuzi. Mengine yamechukuliwa yataenda kufanyiwa kazi kupata ,” amesema Badru

Akizungumzia hilo mfanyabiashara wa Tandika Gamsa Moniko amesema hatua hiyo imewapa furaha wateja na kujiona wa thamani kwa benki ya NMB

“Mimi ni mteja wa kawaida Ila kwenye biashara yangu nilitembelewa na Meneja wa tawi pamoja na watu kutoka Makao Makuu, binafsi ilinipa faraja kwamba wamenitambua na kuona mchango wangu kiasi cha kunitembelea,” amesema Moniko

Naye Richard Njau ambaye ni Wakala wa NMB ameeleza kuwa kupitia programu hii ameweza kuwasilisha changamoto zake moja kwa moja kwa watendaji wa benki.

Kwa upande wake Mkuu wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo Abella Tarimo amesema kitengo chake kitaendelea kuyafanyia kazi maoni ya wateja ikiwa ni pamoja na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka changamoto zilizoainishwa kwa kuwahakikishia wateja kuwa Ubora Upo NMB.

#NMBKaribuYako

RAIS DKT. MAGUFULI AONGOZA MAPOKEZI YA NDEGE MPYA YA BOEING 787-8 DREAMLINER JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Kepteni saidi Hamadi mmoja wa Marubani walioleta ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner kuoka Seattle Marekani alipoipokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo kwenye viti vya marubani wa Boeing 787-8 Dreamliner alipoipokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019
Mke wa Rais Mama janeth Magufuli na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakifurahia jambo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuipokea ndege mpya ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ndani ya Boeing 787-8 Dreamliner alipoipokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kuaga baada ya kuongoza mamia ya wananchi katika mapokezi ya ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi wengine na wadau akikata utepe kuashiria kupokewa kwa ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo wakisiliza maelezo toka kwa Kepteni Dennis Mshana mmoja wa Marubani walioileta ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner kutoka Seattle Marekani hadi katika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine katika picha ya pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama alipoongoza wananchi katika mapokezi ya ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine katika picha ya pamoja na marubani na wanaanga waliokuja na ndege wakati alipoongoza mamia ya wananchi katika mapokezi ya ndege hiyo mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine katika picha ya pamoja na Viongozi wa Dini alipoongoza mamia ya wananchi katika mapokezi ya ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine katika picha ya pamoja na Wakuu wa Wa Taasisi Mbalimbali za Umma na Binafsi alipoongoza wananchi katika mapokezi ya ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezwa na Mzee Omary Mkali, mmoja wa wazee waliofika katika mapokezi ya ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika kiti cha rubani Boeing 787-8 Dreamliner alipoipokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Jumamosi Oktoba 26, 2019

PICHA NA IKULU

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI MISA TAKATIFU DOMINIKA YA 30 MWAKA “C” KANISA KATOLIKI LA MTAKATIFU PETRO PAROKIA YA OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Mkate wa Ekaristi alipoungana na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki kushiriki Misa Takatifu Dominika ya 30 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Oktoba 27,2019.
 


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakishiriki Misa Takatifu Dominika ya 30 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Oktoba 27,2019.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waumini wengine wa Kanisa Katoliki wakishiriki Misa Takatifu Dominika ya 30 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam. Ibada iliyoongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Oktoba 27,2019.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya Waumini wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mtakatifu Joseph baada ya Misa Takatifu Dominika ya 30 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Oktoba 27,2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Paroko Msaidizi Padre Dkt. Alista Makubi pamoja na Mzee wa Kanisa Dkt. Adelhelm Meru baada ya Misa Takatifu Dominika ya 30 ya Mwaka “C” iliyofanyika katika kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Paroko Msaidizi Padre Paul Haule, Oktoba 27,2019.

PICHA NA IKULU


PanAfrican Energy Tanzania Limited yasaini makubaliano na Shirika la Tumaini la Maisha kusaidia watoto wenye saratani Lindi

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa PAET, Andy J Hanna (kulia) na Mwenyekiti wa bodi ya TLM Gerald Mongella (kushoto) wakisaini mkataba wa makubaliano kusaidia watoto wenye saratani mkoani Lindi.


Kampuni ya uzalishaji gesi ya PanAfrican Energy Tanzania Limited (PAET) imesaini mkataba wa makubaliano (MoU) na Shirika la kuhudumia watoto wenye saratani la Tumaini la Maisha (TLM) kwaajili ya kusaidia utoaji wa huduma za matibabu kwa watoto wenye saratani katika Hospitali ya rufaa ya Sokoine mkoani Lindi.

Makubaliano hayo yalisainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa PAET, Andy Hanna na Mwenyekiti wa bodi ya TLM, Gerald Mongella ambapo pande zote mbili zilieleza kuwa na imani na hatua hiyo ambayo ni mwanzo katika kufikisha huduma hiyo katika maeneo mengine ya nchi.

“Ushirikiano huu utasaida katika utambuzi wa magonjwa ya saratani kwa watoto hususani kwenye maeneo yasiyofikika kwa urahisi hapa nchini baada ya kazi hii kufanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam. Tunafarijika kuunga mkono jitihada hizi ambazo ni msaada mkubwa kwa rika la watoto hapa Tanzania,” alisema Hanna.

Aliongeza “Ushirikiano huu utaanza na uanzishwaji wa kituo cha matibabu hapo mkoani Lindi ili kuleta huduma karibu na wahitaji.Tunaamini kuwa huu ni mwanzo tu wa ushirikiano utakaofanya kufikisha huduma hizi maeneo mengi ya nchi siku za karibuni.”

Msaada huu utasaidia kuhakikisha watoto wanapata matibabu bora na ya uhakika karibu na makazi yao.

Msaada huu wa PAET kwa TLM katika utoaji wa huduma za matibabu kwa watoto ni sehemu ya uwajibikaji kwa jamii ambapo kwa kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa afya, kampuni inategemea kuleta mchango chanya katika kuokoa maisha ya watoto wenye saratani nchini.

Tumaini La Maisha, ni shirika lisilo la kiserikali lenye lengo lakutoa huduma za matibabu bure kwa watoto wenye wenye saratani nchini ili kupunguza idadi ya vifo vinavyosababishwa na ugonjwa huo.

PanAfrican Energy Tanzania (PAET) ni kampuni ya uzalishaji gesi asilia inayowajibika kulinda mazingira pamoja na jamii ikijidhatiti kuleta matokeo chanya katika ukuaji wa sekta ya gesi nchini kwa wateja pamoja na jamii zinazozunguka maeneo ya uendeshaji.

Ikiwa na shabaha ya afya na elimu, kampuni hii imeendelea kufanya uwekezaji kwenye sekta hizo huku ikichochea uvumbuzi, miradi yenye kuleta manufaa kwa nchi.

Miaka 20 ya kuwekeza kwenye sekta ya gesi nchini.

Kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa zaidi ya miaka 20, PanAfrican Energy ni kampuni yakitanzania inayoongoza katika uzalishaji,uwekezaji pampoja na uendelezaji wa gesi asilia nchini.

ROSTAM, Dogo janja WAFUNIKA Tigo fiesta saizi yako 2019 Arusha

$
0
0

Msanii wa Bongofleva Roma akiwajibika jukwaani wakati akitumbuiza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta SIZe Yako liliofanyika jana Jijini Arusha.
Msanii wa Bongofleva Mario akiwajibika jukwaani wakati akitumbuiza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta SIZe Yako liliofanyika jana Jijini Arusha.
Roma na Stamina Wasanii wanaounda kundi la Rostam wakitumbuiza katika jukwaa la Tamasha la Tigo Fiesta SIZe Yako liliofanyika jana Jijini Arusha
Msanii Rosaree akitumbuIza kwenye Tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia leo Arusha
Msanii wa bongoflava Jux akiwa jukwaani katika tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia leo jijini Arusha.
Msanii wa bongoflava DogoJanja akinogesha wimbo na Roma jukwaani katika tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia Leo Arusha.



NA Ally Mvungi, Arusha

TAMASHA la Muziki, Msimu wa Tigo Fiesta2019 jana liliwafurahisha wana chugga kwa kishindo jijini Arusha huku Rostam likifunika kwa kuwapagawisha washabiki luluki waliojitokeza kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha.

Mbali na wasanii hao kukonga vilivyo nyoyo za washabiki wa muziki wa kizazi kipya wasanii wengine walikuwa Rosa Ree, Juma Jux,Ruby, Country boy,Fid Q,Weusi.

Washabiki waliojitokeza kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid walishindwa kujizuia kutokana na makamuzi ya nguvu yaliyowaacha hoi yaliyofanywa na kundi la Rostam, na huku Dongo janja akijiunga nao kufanya makamuzi ya kipekee.

Tamasha hilo limefanyika Arusha lilikuwa na mvuto na msisimko mkubwa ambapo mashabiki kutoka viunga vya jiji hilo la kitalii walisuuzika nyoyo na mara kadhaa walishiriki kuimba nyimbo za wasanii mbalimbali hasa kundi la Rostam.

Akizindua tamasha hilo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema waandaaji wa Tigo Fiesta 2019 kwa ubunifu na uamuzi wao wa kuzindua tamasha hilo hawakukosea ikizingatiwa jiji hilo ni kitovu cha utalii kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kati.

“Arusha ni kisima cha burudani kutoka na kuwa na wapenzi wengi wa muziki wa kizazi kipya hivyo niwapongeze Clouds na Tigo kwa ubunifu wao wa kuandaa na kuzindua tamasha lao hapa.Sisi kama mkoa tutaendelea kuwaunga mkono.Pia tamasha hili mbali na kutoa burudani lina umuhimu kiuchumi, linatoa ajira za muda mfupi,linaongeza kipato cha wananchi wetu na waandaaji nao wananufaika,”alisema Gambo.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Kaskazini, Aidan Komba, kampuni hiyo ya mawasiliano itaendelea kushirikiana na kuiunga mkono Clouds ili kuhakikisha wanawapatia Watanzania burudani yenye vionjo na ladha tofauti tofauti.

Tamasha hilo sasa linaelekea mjini Tanga.

ACHA,TRW KUWAPELEKA WAANGALIZI 215 UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2019, KUTOA ELIMU YA MPIGA KURA

$
0
0

Na Ripota Wetu, Michuzi TV

ASASI mbili za kiraia za Action for Change(ACHA) na The Right Way (TRW) zinatarajia kupeleka waangalizi jumla ya 215 katika Wilaya zote za Tanzania Bara kwa ajili ya kufuatilia mwenendo wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajia kufanyika Novemba mwaka huu.

Pia imeelezwa ACHA na TRW kwa pamoja wanadhamiria kuendesha mpango wa pamoja wa kutoa elimu ya uraia na uangalizi wa uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa mwaka 2019 sanjari na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ili kuzifanya chaguzi hizo kuwa huru zaidi, za haki za kuaminika Tanzania.

Akizugumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2019 na Uchaguzi Mkuu wa 2020,Ofisa Mradi wa ACHA Jackson Sikahanga amesema wanatarajia kupeleka waangalizi hao kuhakikisha wanafuatilia mchakato mzima wa uchaguzi wa Serikali za mitaa.

"ACHA TRW tuna matarajio kwamba uchaguzi huu utakuwa huru, haki , kuaminika , tulivu na wenye amani.Pia utakuwa wa uwazi na utakaoshirikisha makundi maalumu , mfano watu wenye ulemavu, wanawake, vijana na wazee.

"Ni dhahiri kuwa uangalizi wa uchaguzi huu utafanyika pia kwa kutumia vifaa vya teknolojia ya kisasa na mafunzo bora yatakayotolewa kwa wakati katika nyanja zote za michakato ya uchaguzi na hata baada ya uchaguzi,"amesema na kuongeza uangalizi na umakini huo katika utoaji taarifa vitabainisha maeneo yenye ucdhaifu kwa marekebisho kwa siku zijazo

Sikahanga amesema ACHA na TRW zinalenga kuona mchakato wa uchaguzi unaofuata viwango vya kitaifa na kimataifa, kama ambavyo Tanzania imeridhia na zile zilizopo kwenye sheria za manispaa , kanuni na miongozo kutoka vyombo mbalimbali vya kusimamia uchaguzi ikiwemo Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC).

Pia amesema uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu mwaka 2020 ni fursa nyingine kwa Watanzania kushuhudia ukuaji wa utawala wa demokrasia. Aidha amesema ipo haja ya ushiriki mpana wa wananchi wote katika mchakato wa uchaguzi, kaunzia kipindi kabla ya uchaguzi kwa mfano uandikisha waji wa wapiga kura, elimu ya mpira kura na uteuzi katka vyama.

"Mchakato huu unahitaji mfumo wa mwenendo thabiti wa elimu kwa wananchi katika zoezi zima, ambalo litafanya elimu kwa mpiga kura kuwa thabiti na wenye tija , mwamko huu wa wananchi kupitia elimu kwa umma na programu ya mpiga kura , ambayo imeandaliwa mahususi kwa ajili ya kuwadaidia wananchi kutambua kuwa ushiriki katika uchaguzi ni haki yao,"amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TRW Rhoda Kamungu amesema upo ushahidi usiojitosheleza unaunga mkono umuhimu wa vyombo katika kuhakikisha Serikali inawajibika juu ya utawala bora ,haki na misingi yote ya haki za binadamu na kwa wananchi wake.

"Ni jukumu letu kuwajulisha wananchi kama nguzo muhimu kupitia vyombo vya habari katika kutoa jukwaa jumuishi la mjadala wa umma na majadiliano kuhusu kuhamasisha mijadala kwa kuzingatia Katiba,sheria,sera ,taratibu na miongozo.Utafiti unadhihirisha kuwepo idadi kubwa ya wapiga kura wasiofahamu kuhusu mchakato na utaratibu wa uchaguzi,"amesema.

Kuhusu kwanini elimu ya uraia, elimu ya mpiga kura na ungalizi ni muhimu, Kamungu amejibu kuwa ACHA na TRW kwa pamoja wanatamani kuona mchakato wa uchaguzi ambao unaongozwa na wananchi, shirikishi , wenye uwazi , huru na haki. "ACHA na TRW tutatoa elimu ya uraia, mpiga kura na uangalizi wa michakato ya uchaguzi kwa kuzingatia vigezo vilivyopo.
 Mkurugenzi wa The Right Away ,Rhoda Kamungu  akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam,mambo mbalimbali ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi mkuu,sambamba na namna  Asasi hizo zilivyojipanga kupeleka waangalizi  Wilaya zote za Tanzania Bara,ambapo ameeleza kuwa waangalizi wa Muda mrefu  wapatao 215 watapewa jukumu hilo ngazi ya majimbo na Waangalizi wa muda mfupi wapatao 3600 watapelekwa kwenye vituo mbalimbali vya uangalizi nchi nzima.
 Ofisa Mradi wa Action for Change   (ACHA) Jackson Sikahanga akizungumza na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu  namna walivyodhamiria kuendesha mpango wa pamoja wa kutoa elimu ya uraia,na uangalizi wa uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa mwaka 2019 sanjari na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, ili kuzifanya chaguzi hizo kuwa huru zaidi, za haki na kuaminika Tanzania.
 Ofisa Mipango wa ACHA na TRW akitolea ufafanuzi wa baadhi ya mambo yalitozungumza na Watangulizi wake kwenye mkutano huo na Waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam.

WAJASIRIA MALI 10 WAHUDHURIA KONGAMANO LA BIASHARA NCHINI CHINA KWA UFADHILI WA BENKI YA NMB

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB – Ruth Zaipuna akizungumza na wateja hao walipotembelea Makao Makuu ya NMB kujionea shughuli mbalimbali za kibenki zinazofanyika hapo
Mkuu wa Huduma Jumuifu –Nenyuata Mejooli akizungumza na wateja.
Afisa Mkuu Uendelezaji wa Bidhaa na Matumizi ya Digitali NMB – Pete Novat akizungumza na wateja
Mkuu wa Biashara Wateja Wadogo na wa Kati wa NMB –Filbert Mponzi katika picha ya pamoja na wateja walipotembelea Makao Makuu ya NMB.

…………………………………………

Wafanyabishara wadogo wameziomba taasisi za fedha kuwawezesha ili waanzishe viwanda na kupunguza safari za China kufuata bidhaa ambazo zingeweza kuzalishwa nchini.

Hayo yameelezwa na wajasiria mali 10 waliohudhuria kongamano la biashara nchini China chini ya ufadhili wa benki ya NMB.

Wajasiriamali hao wameeleza kuwa katika ziara hiyo wamebaini China ina viwanda vidogo vidogo vingi ambavyo ndivyo vinazalisha bidhaa wanazotumia gharama kubwa kuzifuata au kuagiza.

Mmoja wa wajasiriamali hao Arnod Mapunda anayejihusisha na uuzaji wa vifaa vya pikipiki amesema kinachowagharimu watanzania ni bidhaa nyingi kununuliwa nje ya nchi.Amesema ziara hiyo imemuzesha kutambua kuwa inawezekana kuanzisha kiwanja kidogo na ukapata matokeo makubwa.

“Vyote tulivyooona huko vinawezekana endapo tutaamua na hili walione wenzetu wenye taasisi za fedha, wawakopeshe wajasiriamali ili waweze kufanya uwekezaji tupunguze kuagiza kutoka nje,” amesema Mapunda

Naye mfanyabiashara wa maziwa mkoani Morogoro, Rehema Mmari amesema kupitia ziara hiyo ameweza kupata mawazo kadhaa ya biashara ambazo anaweza kuzifanya akipata fedha za kutosha.

Amesema, “ Nimefikiria biashara ya nywele maana nimeona mashine ya kutengeneza na vitu vingine vingi vizuri, hakuna sababu ya kununua mzigo nje ya nchi tukiwa na viwanda vidogo hapa nyumbani tunaweza kabisa,”

Kwa upande wake Mkuu wa biashara wa NMB, Donatus Richard amesema waliamua kuwawezesha wafanyabishara hao kuhudhuria kongamano hilo ili wakajifunze kutoka kwa wafanyabishara wa China namna wanavyoendesha biashara zao.

Sanjari na hilo ziara hiyo ililenga kujifunza ni namna gani wanaweza kufanya uwekezaji wenye tija hapa nchini ili kupunguza safari za kwenda China.“NMB huwa tuna klabu za wajasiriamali ‘NMB Business Club’ tunawafundisha masuala mbalimbali ya biashara, mwaka huu tukaona twende mbele tukawapeleka China wakajifunze zaidi kwa kujionea,”

“Wametembelea viwanda na kuhudhuria kongamano la bishara ni matumaini yetu wamejifunza vingi na watafundisha wenzao kile walichojifunza, maana wametoka katika mikoa ya kanda zote nane,” amesema Richard

Ziara hiyo ya siku 10 ilianza Oktoba 13 na kuhitimishwa Oktoba 23.

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO TOKA KWA MABALOZI WAPYA WA FINLAND, UMOJA WA ULAYA NA RWANDA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa Balozi mteule wa Jamhuri ya Rwanda nchini Meja Jenerali Charles Karamba kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Balozi mteule wa Jamhuri ya Rwanda nchini Meja Jenerali Charles Karamba baada ya kupokea hati yake ya utambulisho kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa Balozi mteule wa Jamhuri ya Finland nchini Mhe. Riita Swan kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Balozi wa Jamhuri ya Finland nchini Mhe. Riita Swan baada ya kupokea hati yake ya utambulisho kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea hati ya utambulisho toka kwa Balozi mteule wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Mhe. Manfredo Fanti kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifanya mazungumzo na Balozi mteule wa Umoja wa Ulaya (EU) Mhe.Manfredo Fanti baada ya kupokea hati yake ya utambulisho kwenye hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaa leo Jumatatu Oktoba 28,2019

PICHA NA IKULU
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live


Latest Images