Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

MWANDISHI WA HABARI ASHEHEREKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KWA KUWAPA ZAWADI AKINA MAMA WALIOJIFUNGUA HOSPITALI YA MKOA WA SHINYANGA

$
0
0
 Mwandishi wa habari wa kituo cha matangazo Radio Faraja FM Stereo iliyopo Shinyanga Mjini Josephine Charles, amesheherekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa zawadi kwa wazazi ambao wamejifungua kwa njia ya upasuaji kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga.


Tukio hilo limefanyika leo Julai 23, 2019 ambapo ni siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka kadhaa hapa duniani, ambapo ametembelea kwenye wodi ya wazazi ambao wamejifungua kwa njia ya upasuaji, wodi ambayo na yeye alijifungua mtoto wake Desemba 23,2018 kwa njia hiyo Christian Alex ambaye ametimiza miezi saba sasa. 

Zawadi alizotoa kwa akina mama hao ni taulo za kike, sabuni za kufulia, kuogeshea watoto pamoja na poda, huku akitoa wito kwa wanawake kujenga utamaduni wa kuhudhuria kliniki mapema na kwa wakati pamoja na kujifungulia watoto wao kwenye huduma za kiafya mahali ambapo ni salama kuliko majumbani. 

“Nimeamua kusheherekea siku yangu ya kuzaliwa kwenye wodi hii ya wazazi waliojifungua kwa njia ya upasuaji, wodi ambayo na mimi nilijifungua mtoto wangu kwa njia hii, ili kutoa hamasa kwa akina mama kupenda kujifugulia kwenye vituo vya afya na kuweza kupunguza tatizo la vifo vya mama na mtoto vitokanavyo na uzazi mkoani Shinyanga,” amesema Charles.

 “Nasema haya kwa sababu siku ambayo mimi nililazwa kwenye wodi hii kwa ajili ya kujifungua mtoto wangu, alikuja mama mmoja akiwa hoi ambapo alipohojiwa ili kuchukuliwa taarifa zake aligundulika hakuwahi hata siku moja kuhudhuria kliniki, na alipozidiwa ndipo akaona aje hospitali kupatiwa huduma kitendo ambacho ni hatari kwa maisha yake,”amesema Charles. 

"Pia natoa wito kwa watu wengine ambao wana nafasi wasiwe wanasheherekea siku zao za kuzaliwa kwa kufanya vitu vya anasa, bali wawe wanatumia fursa hiyo kusaidia watu ambao wana uhitaji ili na wao wasione kama jamii inayowazunguka imewatenga",ameongezaCharles.

 Nao baadhi ya wazazi waliojifungua watoto wao kwa njia hiyo ya upasauaji akiwemo Dotto Jumanne na Winfrida Joseph ambao ni wakazi wa mkoani Shinyanga, wameshukuru kupewa zawadi hizo huku wakipongeza huduma ambayo wanapatiwa hospitalini hapo, ambapo wameweza kujifungua watoto wao salama. 

Kwa upande wake Daktari wa wodi hiyo ya akina mama wanaojifungua kwa njia ya upasuaji Dkt. Amoni Amoni, alitoa wito kwa wadau wa afya mkoani humo kuendelea kutoa elimu kwa wakina mama juu ya umuhimu wa kuhudhulia Klinik mapema na kwa wakati pamoja na kujifungua watoto kwenye huduma za kiafya. Na Marco Maduhu - Malunde1 blog  Mwandishi wa habari kutoka kituo cha matangazo Radio Faraja Shinyanga Mjini Josephine Charles akizungumza nje ya wodi ya wazazi ambao wamejifungua watoto kwa njia ya upasuaji kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga, mara baada ya kumaliza kutoa zawadi kwao ikiwa ni siku ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa leo Julai 23,2019. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog  Mwandishi wa habari wa kituo cha matangazo Radio Faraja Shinyanga Mjini Josephine Charles (kwanza kushoto) akiwa na wanafamilia, waandishi wa habari wa Radio Faraja pamoja na baadhi ya wauguzi wa hospitali ya mkoa wa Shinyanga wakifungua zawadi kwa ajili ya kuwapatia wazazi.  Josephine Charles akitoa zawadi kwa wazazi ambao wamejifungua kwa njia ya upasuaji kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga wakati wa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa, wodi ambayo na yeye alijifungua mtoto wake kwa njia hiyo ya upasuaji.  Josephine akiendelea kutoa zawadi.  Josephine akiendelea kutoa zawadi kwa akina mama waliojifungua watoto kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga kwa njia ya upasuaji.  Josephine akiendelea kutoa zawadi.  Josephine akiendelea kutoa zawadi kwa akina mama walijifungua watoto wao kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga , ikiwa anasheherekea siku yake ya kuzaliwa.  Zawadi zikiendelea kutolewa.  Josephine akiendelea kutoa zawadi huku akiwa amembeba mtoto wake Christian Alex ambaye alijifungua kwenye wodi hiyo kwa njia ya upasuaji.  Josephine akitoa pia zawadi kwa wauguzi wa wodi ya wazazi wanaojifungua kwa njia ya upasuaji kwa kutoa huduma nzuri na kuhakikisha wazazi wanajifungua salama na kupunguza vifo vya uzazi.  Mzazi Dotto Jumanne akishukuru zawadi hizo ambazo zimetolewa na Josephine Charles katika siku yake ya kuzaliwa.  Daktari wa wodi ya akina mama ambao wanajifungua wa njia ya upasuaji Dkt Amon Amoni, akitoa wito kwa akina mama kuhudhuria kliniki mapema na kwa wakati pamoja na kujifungulia kwenye huduma za kiafya, sabambamba na elimu itolewe zaidi kwa akina mama juu ya umuhimu wa kujifungulia kwenye huduma za afya mahali ambapo ni salama.  Dkt. Justice Minofu mwenye shati jekundu akimpatia zawadi ya siku yake ya kuzaliwa Josephine Charles ambaye amefikisha miaka kadhaa hapa duniani na kumtakia maisha mema na marefu.  Awali Josephine Charles akiwa na wafanyakazi wenzake wa Radio Faraja wakiwasili kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kutoa zawadi kwa wazazi ikiwa ni siku ya sherehe yake ya kuzaliwa.Kushoto ni Steve Kanyefu akifuatiwa na Joseph Edward.  Josephine Charles akipiga picha na familia yake, waandishi wa Radio Faraja na wauguzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ,katika wodi ya wazazi waojifungua kwa njia ya upasuaji wakati wa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa wazazi hao.  Josephine Charles akipiga picha ya pamoja na familia yake, waandishi wa Radio Faraja na baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ,katika wodi ya wazazi waojifungua kwa njia ya upasuaji wakati wa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa wazazi hao. Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog.

UBA GROUP SETS TO PROJECT AFRICAN ENTREPRENEURS TO THE GLOBAL MARKET VIA ITS SECURED ECOMMERCE PLATFORM - ‘UBA MARKETPLACE’:

$
0
0


‘UBA Marketplace’ is a secure online marketplace that allows businesses (small and medium scale) have an online store where they can advertise and sell their products or services across the continent and beyond. The UBA Marketplace is owned and managed by United Bank for Africa, a leading Pan-African financial institution in Africa with over 12 million customers. The Marketplace offer businesses personalized e-commerce site with their own unique store name to showcase their goods online thereby reaching potential customers across the globe irrespective of their physical locations.

As part of the process of enhancing the business network of African entrepreneurs, UBA Group also organizes an annual gathering of the ‘UBA Marketplace’ registered merchants, vendors, customers and other stakeholders for a two day exhibition in Nigeria. This year’s event is scheduled to hold at the iconic Transcorp Hilton Hotel, in Nigeria’s capital city of Abuja on the 26th and 27th of July 2019 with the theme “Empowering African Entrepreneurs”. This Africa’s largest gathering of business owners and entrepreneurs, promises to be the ideal forum for the enhancement of Tanzanian entrepreneurs business connections as over 5,000 visitors and over 100 registered exhibitors across 20 African countries, plus top private and public sector players will be gracing this annual historical event.

The UBA Market is available https://www.ubagroup.com/nigeria/market-place-africa/


On UBA Marketplace, there are different ways to sell your products such as listing on the marketplace, offering deals or listing as an auction. The E-commerce platform features categories such as electronics, fashion, jewelry, health and beauty, groceries, household goods, perfumes and more.

To further advance the course of entrepreneurs in the continent, 3 African leaders on day 2 of the event, will be engaging an audience of 5,000 people and watched around the globe through TEF forum, courtesy of the founder of TEF, Tony O. Elumelu, the Group Chairman of UBA Plc.

There will be plenary sessions which will highlight entertainment and music industries. Likewise, fashion, a big cultural and revenue attraction on the continent, will be showcased with the designs of 10 leading African labels. The event will provide a unique opportunity to shop, eat, play, network and party at the Africa’s largest fair of entrepreneurs as the African renowned artist “Wizkid” will be leading others; Niniola, DJ Cuppy, DJ Neptune to provide live music concert.

A good number of Tanzanian entrepreneurs are poised to grace the trade fair and will be showcasing Tanzanian products and culture. With this event, UBA seeks to touch base with small business owners while positively affecting the lives of entrepreneurs doing business in its countries of operations and beyond’.

Furthermore, this Forum presents the largest single annual opportunity for entrepreneurs and policy makers to interact directly and all sessions at the Forum have private sector and public sector leaders anchored in panel discussions, master classes, and a dynamic pitching competition that will engage an audience of start-up entrepreneurs, development institutions and policymakers.


The Managing Director of UBA Tanzania, Usman Isiaka explained various benefits as to why the entrepreneurs should embrace this golden business opportunity: UBA Marketplace reach wider audience through Internet penetration with increasing number of internet users and online shoppers; it is cost effective as it offers an effective low cost channel for SMEs in Tanzania to drive sales online through new customer acquisition; it leverages on the support of a trusted bank with over 12 million customers; customers will be able to create their store url to share with their buyers (example: Omary.ubamarketplace.com) where “Omary” is the store name; ability of entrepreneurs to auto post their products on Facebook and sell them from own business page; secure transaction using one of the highest Secure Socket Layer Encryption on the platform with a payment gateway which is Payment Card Industry Data Security Standard (PCI DSS) compliant and reliable logistics managed by DHL.

As part of its initiative of supporting African entrepreneurs, UBA Group has developed a Young Entrepreneurs Finance (YEF) Scheme which is being rolled out in phases across our 20 presence countries in Africa. The product provides existing TEF Alumni and other African Entrepreneurs above 18 years with qualifying business plans, opportunity to get up to $50,000.00 loan with 6 months deferred interest.
UBA Bank Tanzania Managing Director Usman Isiaka speaks in Dar es Salaam today during an event to ECOMMERCE PLATFORM - ‘UBA MARKETPLACE’ which gives an opportunity to allow businesses (small and medium scale) have an online store where they can advertise and sell their products or services across the continent and beyond 

RAIS DKT MAGUFULI APOKEA DHAHABU NA FEDHA ZILIZOKAMATWA NCHINI KENYA

$
0
0
  Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisaidia kuhesabu vipande vya dhahabu huku akishuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi aliyevipokea kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Balozi Monica Juma Dhahabu pamoja na pesa zilizokamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi zikitoroshwa kutoka Tanzania kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Julai 24, 2019.
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi akipokea kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Balozi Monica Juma Dhahabu pamoja na pesa iliyokamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi zikitoroshwa kutoka Tanzania kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Julai 24, 2019

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya kushuhudia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi akipokea kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Balozi Monica Juma Dhahabu pamoja na pesa xzilizokamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi zikitoroshwa kutoka Tanzania kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Julai 24, 2019
 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akisalimiana kwa simu ya mkononi na Rais wa Jamhuri ya Kenya Mhe Jomo Kenyatta baada ya viongozi hao kushuhudia Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi akipokewa kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Balozi Monica Juma Dhahabu pamoja na pesa iliyokamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi zikitoroshwa kutoka Tanzania kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Julai 24, 2019. Kushoto ni Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan akifuatiwa na Mhe Monica Juma. Kutoka kulia ni Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko akifuatiwa na Profesa Kabudi na Mwendesha Mashataka Mkuu wa Serikali Mhe Biswalo Mgangha
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Mhe. Balozi Monica Juma baada ya kukabidhi Dhahabu pamoja na pesa iliyokamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi zikitoroshwa kutoka Tanzania kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Julai 24, 2019 PICHA NA IKULU

DKT BASHIRU ATEMBELEA MKUTANO WA WATAALAMU WANAOJADILI MABORESHO YA MFUMO WA HAKI JINAI NCHINI

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally akizungumza na Wataalam wanaoshiriki majadiliano ya kufanyia maboresho ya sekta ndogo ya haki jinai nchini unaofanyika jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally akizungumza na Wataalam wanaoshiriki majadiliano ya kufanyia maboresho ya sekta ndogo ya haki jinai nchini unaofanyika jijini Dodoma.
Washiriki wa Mkutano wa Wataalam wa majadiliano yenye lengo la kufanyia maboresho sekta ndogo ya haki jinai nchini unaofanyika jijini Dodoma wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally (hayupo pichani ) alipokuwa akizungumza nao juu ya kazi hiyo wanayoifanya.
…………………..
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally ametembelea Mkutano wa Wataalam wanaoshiriki majadiliano ya kufanyia maboresho ya sekta ndogo ya haki jinai nchini unaofanyika jijini Dodoma na kuwataka wataalamu hao kushughulikia maeneo yanayotoa mianya ya rushwa, urasimu na ubwetekaji kwa taasisi zinazohusika na mfumo wa haki jinai ili kupata mfumo sahihi unaotoa haki kwa wananchi.

Amesema kazi ya maboresho ya mfumo wa haki jinai inapaswa kushirikisha taasisi zote zinazohusika na mfumo huo ikiwa ni pamoja na sheria zinazosimamia taasisi hizo ili kuziondoa katika mazingira ya ubwetekaji, urasimu na mazingira yanayotoa mianya ya rushwa.

“Huwezi kuwa na mfumo bora na thabiti wa utoaji haki nchini kama taasisi zinazosimamia na kutoa haki nchini zitakuwa zimebweteka, zina urasimu na kuwa na sheria ambazo zinatoa mianya ya rushwa, ni jukumu lenu kuangalia taasisi husika na sheria zao, na msipofanya hivyo hamuwezi kufikia lengo la kuwa na mfumo bora na thabiti utakaotoa haki kwa watu” amesema.

Amesema ni wazi kuwa taasisi nyingi zinazohusika na mfumo wa haki jinai nchini bado zinakabiliwa na kasoro hizo na kuongeza kuwa ili kuondokana nazo ni lazima taasisi zinazohusika ziondokane na vitu hivyo.

Amesema kama vitu hivyo visipozingatiwa lengo la kupata mfumo bora na thabiti wa utoaji haki kwa wananchi haliwezi kufikiwa na hivyo kukwamisha juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano ya kutoa haki kwa wananchi.
Amewataka Washiriki kuangalia maeneo yote ambayo yanatoa mwanya wa kufanyika kwa vitendo vya kijinai ambavyo ni vya kutengenezwa na hivyo kuwakosesha wananchi haki kwa kuwa wahusika wa taasisi hizo wana mianya hiyo.

“Muangalie maeneo yote ambayo yanawapa mianya watendaji katika taasisi husika kutengeneza vitendo vya kihalifu na kuwarushia wananchi ambao mwisho wa siku wanakuwa wamekoseshwa haki zao kutokana na kukabiliwa na vitendo hivyo vya kihalifu ambavyo ni vya kutengenezwa,” amesema.

Amesema kushamiri kwa vitendo hivyo kunafanya kuanguka kwa mfumo wa haki jinai nchini ambako pia kunamaanisha kwamba taasisi zinazohusika na mfumo huo pia zinakuwa zimefeli.

Dkt. Bashiru ametoa kauli hiyo jijini Dodoma alipotembelea mkutano wa Wataalam wanaoshiriki katika majadiliano ya kuboresha mfumo wa haki jinai jinai nchini ili iweze kuimarisha utoaji haki nchini kwa wote na kwa wakati.

Wataalam hao ambao ni kundi la pili wanapitia mnyororo wa haki jinai na kubainisha changamoto katika mfumo na kupendekeza hatua za namna ya kutatua changamoto hizo na hivyo kuwa na mfumo mpya wa haki jinai ambao utazingatia utoaji haki kwa wananchi..

MCHEZA FILAMU WA MEXICO ATEMBELEA HIFADHI NNE ZA TAIFA

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Muigizaji wa Tamthilia maarufu ya ESMERALDA kutoka nchini Mexico, aliyekuja nchini kwa mapumziko ya siku saba na watoto wake, wakati Waziri Mkuu akiwa mkoani Arusha kwenye ziara ya kikazi. Julai 23.2019. Tokea kushoto ni watoto wa muigizaji huyo, Carlo Collado (14) na Luciano Collado (15).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na wafanyakazi wa hoteli ya The Retreat at Ngorongoro iliyoko wilayani Karatu, wakati akiwa mkoani Arusha kwenye ziara ya kikazi. Julai 23.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
………………..

*Zimo Ngorongoro, Serengeti, Manyara na Tarangire
*Ni Leticia Calderon, aliyeigiza filamu ya ESMERALDA

MUIGIZAJI maarufu wa filamu kutoka Mexico, Bi. Leticia Calderon (51) amesifia rasilmali ya hifadhi za wanyama ambayo Tanzania imejaliwa kuwa nayo.

Muigizaji huyo ambaye amefanya kazi hiyo kwa miaka 36, na ameigiza sinema maarufu ya ESMERALDA, yuko nchini kwa mapumziko ya siku saba kwenye hifadhi za wanyama za ukanda wa Kaskazini.

Akisalimiana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyekuwa mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi, Bi. Calderon amesema amevutiwa na uzuri wa hifadhi za Tanzania na idadi kubwa ya wanyama aliowaona kwenye hifadhi za Taifa za Tarangire, Manyara na Ngorongoro.

“Kwa miaka mingi nilikuwa natamani sana kuja Tanzania kuona wanyama. Tuliyoyaona yametufurahisha mimi pamoja na wanangu. Nchi yenu ina uzuri wa kustaajabisha. Watu wenu ni wema na wakarimu,” alisema Bi. Calderon.

“Ninafurahi kwamba ndoto yangu imetimia. Tulienda Tarangire, Manyara na Ngorongoro ma sasa tunajiandaa kwenda Serengeti. Tulipokuwa Ngorongoro, tuliona simba wanne, majike wawili na madume wawili. Tumefurahi sana na nikirudi nyumbani, nitawaonyesha picha marafiki zangu na kuwaalika waje kutembelea Tanzania,” alisema.

Bi. Calderon ambaye amefuatana na wanaye wawili Luciano Collado (15) na Carlo Collado (14) alisema wakimaliza mapumziko yao huko Serengeti watakwenda Masai-Mara kwa siku tatu na kisha wataelekea Paris, Ufaransa kumtembelea rafiki yake ambaye waliigiza filamu pamoja huko nyuma.

Bi. Calderon pia ameigiza tamthilia ndefu (soap operas) 29 katika jiji la Mexico City ambalo ni mji mkuu wa Mexico. Mbali ya Esmeralda, filamu nyingine maarufu ambazo ameigiza ni En Nombre del Amor (In the Name of Love); Amor Bravia (Valiat Love) na La Indomable (The Taming of the Shrew).

Waziri Mkuu alimshukuru mwanamama huyo na wanaye kwa kuichagua Tanzania kwa mapumziko yao na akawatakia heri katika safari yao ya mbugani.

Akizungumza na wafanyakazi wa hoteli ya The Retreat at Ngorongoro iliyoko Karatu ambako muigizaji huyo alikuwa amefikia, Waziri Mkuu aliwataka wafanyakazi wa hoteli hiyo na wengine walioko kwenye hifadhi za Taifa, wafanye kazi kwa bidii ili huduma zao ziwavutie watalii wengi zaidi.

“Tunampongeza mwenye hoteli kwa uwekezaji huu mkubwa lakini niwasihi wafanyakazi mchape kazi ili wageni wengi zaidi waweze kuvutiwa na huduma zenu,” alisema Waziri Mkuu.

“Sasa hivi tunapata watalii wengi na watu maarufu kama hawa, wamechagua kuja kupumzika Tanzania. Mheshimiwa Rais Magufuli ameshanunua ndege sita, nyingine mbili zinakuja, moja itawasili Oktoba, na nyingine Januari, mwakani. Na tayari kuna ndege tatu nyingine zimeagizwa. Lengo lake ni kuimarisha usafiri wa ndani kwa kutumia ndege,” alisema.

“Zamani ilikuwa ni vigumu sana kuja Tanzania moja kwa moja. Ili mtalii afike, ilibidi apitie nchi nyingine na huko akidakwa anaondokea hukohuko. Sasa hivi, akitoka kwao ataweza kuja Tanzania moja kwa moja, akitua KIA anakuja Karatu au Serengeti moja kwa moja,” alisema.

HALMASHAURI YA GEITA MJINI YATOA MKOPO WA BILIONI 1.6 KWA VIJANA, WANAWAKE NA WALEMAVU

$
0
0
Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu akizungmza kwenye mkutano kati ya wananchi na Mbunge kuhusu ahadi mbalimbali alizozitekeleza ikiwemo suala la utoaji mikopo wa shilingi bilioni 1.6 kwa vikundi mbalimbali wakiwemo vijana, wanawake na walemavu kwa lengo la kupunguza umasikini katika jamii kwenye mkutano uliofanyika katika kata ya Ihanamiro wilaya ya Geita mkoani Geita
Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Geita, Mhe.Mohamed Ali( wa pili kulia) pamoja na Diwani wa kata ya Ihanamiro, Joseph Lugaila wakiwa kwenye mkutano wa hadhara kabla Mhe. Kanyasu kuanza kuzungumza na wananchi wake katika kata ya Ihanamiro.
Baadhi ya wanachama wa CCM waliohudhuria mkuatano wa Mbunge wa Geita mjini, Mhe. Constantine Kanyasu wakimsikiliza wakatik akizungumza kwenye mkutano huo kuhusu ahadi alizozitekeleza kwa wananchi wake likiwemo suala la mikopo kwa wanawake, vijana na walemavu.
Baadhi ya Madiwani wa viti maalum walioshirki kwenye mkutano wa Mbunge wa Geita mjini, Mhe. Constantine Kanyasu wakimsikiliza wakati akizungumza na wananchi wake katika kata ya Ihanamiro.
Baadhi ya wananchi walioshiriki kwenye mkutano wa Mbunge wa Geita mjini, Mhe. Constantine Kanyasu wakimsikiliza Mbunge wao wakati alipokuwa akizungyumza nao katika kata ya Ihanamiro.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita, Mohamed Ali akizungumza na wananchi wa kata ya Ihanamiro kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na utalii ambaye pia ni Mbunge wa Geita mjini kabla ya kuzungumza na wananchi wa kata hiyo.


Mbunge wa Geita mjini, Mhe. Constantine Kanyasu (katikati) akiwa amekaa na wananchi wa kata ya Ihanamiro huku akiwa akiwa anazungumza nao kabla ya kikao cha ndani kuanza.
……………………….
Mbunge wa Geita mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Constantine Kanyasu amesema Halmashauri ya mji wa Geita hadi kufikia mwezi Julai mwaka huu tayari imeshatoa mkopo wa Shilingi bilioni 1.6 kwa ajili ya wakinamama, vijana na walemavu kwa lengo la kutimiza adhima ya Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais John Pombe Magufuli.
Amesema lengo la kutoa mkopo huo ni kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira na kuweza kuinua kipato cha wananchi kwa kunufaika na miradi mbalimbali na hatimae kuweza kujikwamua kiuchumi.
Hayo ameyasema kwenye mkutano wakati akizungumza na wananchi wake kuhusu ahadi mbalimbali alizozitekeleza ikiwemo ya kutoa mkopo wa shilingi bilioni 1.6 kwa vikundi mbalimbali kwa lengo la kupunguza umasikini katika jamii katika mkutano huo uliofanyika katika kata ya Ihanamiro wilaya ya Geita mkoani Geita.
Mhe.Kanyasu amewaeleza wananchi hao kuwa kutokana na uhusiano mzuri uliopo miongoni mwa madiwani katika Halmashauri hiyo wameweza kutoa mkopo huo. Hata hivyo amesema kuwa mikopo hiyo itasaidia katika uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia kutengeneza ajira na kukuza uchumi
Akizungumza katika mkutano huo,Mhe.Kanyasu amesema anajisika fahali ya kutoa mikopo hiyo kwa vikundi ikiwa ni moja ahadi alizozitimiza za kuhakikisha mwananchi wake wanajihusisha kwenye shughuli za kiuchumi ili kupunguza umasikini kuanzia ngazi ya familia hadi taifa
Amesema kuwa kutokana na changamoto zilizoko katika taasisi za fedha, ambazo hutoa mikopo kwa riba kubwa na kuhitaji dhamana ya nyumba na ardhi jambo ambalo linawakwamisha wakopaji hivyo serikali imeamua kutoa mikopo ya masharti nafuu.
Aidha amesema mikopo hiyo itawasaidia makundi hayo kuweza kuongeza mitaji na kutoa ajira ndani ya jamii.
Aidha, Mhe, Kanyasu amesema katika awamu ya pili ya utoaji mkopo wataongeza viwango vya mikopo kwenye vikundi ambapo kila kikundi kitakuwa na uwezo wa kukopeshwa hadi kufikia shilingi milioni 20 tofauti na ilivyokuwa awali
Kwa upande wake, Diwani wa kata ya Ihanamiro, Mhe. Joseph Lugaira amemueleza Mbunge huyo kuwa katika kata hiyo jumla ya vikundi 19 vimenufaika na mkopo huo kwa kuanzisha shughuli za kiuchumi.
Amesema vikundi hivyo vimekuwa vikifanya shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo biashara pamoja na kilimo ambapo anaamini wataweza kupata faida pamoja na kurejesha mkopo huo na kukopa tena.
Naye Diwani wa viti maalum, Mhe. Suzana Mashala amewahimiza wanawake wasiogope kukopa kwani hawawezi kujiendeleza kiuchumi pasipo kukopa.
Vile vile, Diwani huyo alitumia fursa hiyo kuwahimiza wanawake waliokopa wajitahidi kurejesha mikopo hiyo mapema ili mikopo hiyo iweze kuwasaidia watu wengine lengo likiwa ni kuondokana na umasikini.
Kwa upande wake, Emalio Nyangabo ambaye ni kiongozi wa Kikundi cha Tuinuane, amesema walipokea mkopo ambao umewasaidia kuinuka kiuchumi, na kuwawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali na kuachana na kujihususha na vitendo visivyofaa katika jamii
Naye, Godson Maduka ambaye ni miongoni mwa vijana walionufaika wa mkopo huo amesema mkopo huo umewasaidia vijana wengi kujiepusha kujiingiza kwenye utumiaji wa madawa ya kulevya na unywaji wa pombe kupita kiasi.

BALOZI WA UFARANSA AFURAHISHWA NA HUDUMA ZA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI MUHIMBILI

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akipokea maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha MUHAS wwakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwake ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu (katikati) akiambatana na Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe, wakwanza kushoto ni Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha MUHAS Prof. Said Aboud.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mikrobiolojia na Immunolojia chuo cha MUHAS Prof. Eliangiringa Kaale, wakati alipofanya ziara katika chuo hicho ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho, Kulia kwa Waziri Ummy ni Balozi wa Ufaransa Tanzania Frederic Clavier na wamwisho ni Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Andrea Pembe.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu akisisitiza jambo mbele ya Watumishi na Wanafunzi wa chuo cha MUHAS (hawapo kwenye picha) wakati alipofanya ziara ya kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti katika chuo hicho.
Wataalamu mbali mbali wa masuala ya tafiti pamoja na Watumishi wa Sekta ya Afya, wakifuatilia hotuba kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe Ummy Mwalimu wakati alipofanya ziara katika chuo cha MUHAS ili kujionea Maendeleo ya shughuli zakitafiti

……………………………………………………

NA WAJMW-DSM
Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania Bw. Frederic Clavier amefurahishwa na huduma zinazotolewa katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu mapema leo wakati wa kukagua na kufuatilia maendeleo ya ushirikiano kati ya nchi ya Ufaransa na Tanzania katika masuala ya utafiti mafunzo na utoaji wa huduma za Afya katika chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Muhimbili.

Kwa kiasi kikubwa Waziri Ummy pamoja na Balozi huyo wameridhishwa kwa kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Wataalamu katika chuo hicho ikiwemo utafiti, mafunzo na utoaji wa huduma za afya.

“Binafsi tumeridhishwa na kazi kubwa na nzuri zinazofanywa na wataalamu wetu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi cha Muhimbili, katika masuala ya utafiti tumeona kazi kubwa inayofanyika katika utafiti juu ya dawa za kuua wadudu”. Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema hakuna sheria nzuri za udhibiti wa dawa hizi nchini hivyo Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Muhimbili na Serikali ya Ufaransa itaendelea kufanya utafiti na kuona jinsi gani itapunguza madhara ya utumiaji wa dawa za kuua wadudu kwa binadamu.

Pamoja na hayo, Waziri Ummy amefurahi kuona ushirikiano ambao Serikali ya Ufaransa inaendelea kuutoa katika huduma za watu wenye tatizo la Seli nundu “Sickle Cell”.

“kwa Mujibu wa Tafiti tuna jumla ya watu 200,000 nchini ambao wana tatizo la seli nundu na watoto ambao wanazaliwa ni 11,000 kwahiyo tumejadiliana na Serikali ya Ufaransa kuona ni jinsi gani tunaweza kuboresha huduma za ugunduzi ili tuweze kuwatambua mapema watoto pale wanapozaliwa na tatizo hili na kuhakikisha huduma za matibabu zinapatikana ikiwepo dawa ya kupunguza maumivu inapatikana”. Amesema Waziri Ummy.

Kufuatia hatua hiyo Waziri Ummy amemuomba Balozi Frederic kushawishi makampuni makubwa ya kutengeneza dawa kutoka Ufaransa yaweze kusaidia katika kuzalisha dawa ya kupunguza maumivu ya Seli nundu inapatikana kwa Watanzania wengi.

TICTS DONATION AT ILELA SECONDARY SCHOOL, MLELE, KATAVI REGION

$
0
0
 Mr. Donald Talawa, TICTS Corporate Affairs Director handing over 1,200 bags of cement and 1,200 pieces of iron sheet worth Tshs 56 million to Mrs Rachel Kasanda Mlele District Commissioner, to assist with the construction of a girl's hostel at Ilela secondary school. The hostel is planned to accommodate 200 girls as the school is located 11 kilometers from Inyonga town in Mlele district, Katavi region and has a total of 485 students.
 Mr. Donald Talawa, TICTS Corporate Affairs Director, addressing the students Ilela secondary school after handing over a donation of 1,200 bags of cement and 1,200 pieces of iron sheets to assist with the construction of a girl's hostel which will accommodate 200 girls. On the right are Mrs. Rachel Kasanda Mlele district commissioner, and Mr. Alexius Kagunze, Mlele district executive director. On the left is Mr. Deus Bundala, Mlele district council chairman.
Ilela secondary school students, teachers, and parents looking on during the handover ceremony of 1,200 bags of cement and 1,200 pieces of iron sheet donated by TICTS to assist with the construction of a girls hostel. The donation which is worth Tshs 56 million was received on behalf of District government by Mrs. Rachel Kasanda, Mlele District Commissioner, Mr. Alexius Kagunze, Mlele District Executive Director and Mr. Deus Bundala, Mlele District Council Chairman.

Wateja wa Mpesa kuvuna zaidi Bahati nasibu ya Biko

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta akipeana mkono na Mkurugenzi Kitengo Cha biashara Arjuun Dhillon kuonesha msisitizo wa muungano wao kati ya BIKO na kampuni ya Vodacom Tanzania, kuhakikisha wachezaji wa mchezo huo wanatumia Mpesa kushinda zaidi kwa kuendeshwa droo maalum inayohusisha watumiaji wa Mpesa pekee.


Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta akizungumza jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar leo kuhusu Kampuni hiyo kuungana na kampuni ya Vodacom Tanzania kuhakikisha wachezaji wa mchezo huo wanatumia Mpesa kushinda zaidi kwa kuendeshwa droo maalum inayohusisha watumiaji wa Mpesa pekee,kushoto ni Mkuu wa Kitengo Cha Uzalishaji cha wateja wakubwa-Vodacom, Ali Z Ali na kulia na kulia ni Meneja Mauzo-Vodacom,Carolyn Lyimo
 
======== = =========    =========  ==========

Kampuni ya mchezo wa kubahatisha wa Biko, wameungana na Kampuni ya Mtandao wa Simu za Mikononi ya Vodacom Tanzania kwa kuhakikisha kwamba wachezaji wa mchezo huo wanaotumia Mpesa kushinda zaidi kwa kuendeshwa droo maalum inayohusisha watumiaji wa Mpesa pekee.


Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Biko, Charles Mgeta, alisema droo hiyo ni tofauti na zile za kawaida zinazofanyika kila Jumatano na Jumapili kwa watumiaji wa mitandao yote nchini Tanzania, wakiwa na dhamira ya kupanua wigo wa ushindi kwa Watanzania wote, hususan wanaotumia Mpesa.

"Kwa kuendeshwa mchezo huu, sasa wigo wa ushindi umepanuka kutoka mara mbili hadi tatu, kama vile zawadi za papo kwa hapo, zawadi kubwa ya wiki ya Jumatano au jumapili, bila kusahau droo kubwa ya wachezaji pekee wa Mpesa ambao wao pekee watatafutwa mara baada ya kupata washindi wetu wa kawaida kutoka Biko.

"Tunadhani sasa kushinda Biko ni rahisi zaidi, ukizingatia kuwa droo zetu zote zinachagizwa na tumaini letu la kugawa zawadi za juu kwa Watanzania wetu, hivyo ukiacha wigo wa droo zetu za kawaida, bado upo ukumbi muhimu wa watumiaji wa Mpesa ambao wote watacheza kwa mfumo wa kawaida wa kutumia namba yetu ya Kampuni ya 505050 na kumbukumbu namba 2456,"alisema Mgeta.

Naye Mkuu wa Kitengo Cha Uzalishaji Cha wateja wakubwa, Ali Z Ali, aliishukuru Biko kwa kuanzisha droo mahususi kwa ajili ya wateja wao wa Mpesa, akisema kuwa itaonyesha ni namna gani wametambua huduma nzuri kutoka Vodacom Tanzania.

"Vodacom kupitia Mpesa na wenzetu Biko tupo kwa ajili ya wateja wetu wote ambao sasa fursa za ushindi kwao ni pana zaidi, hivyo tunawaasa watumie fursa hii ili wajishindie zawadi kutoka Biko kila siku,"Alisema Ali.

Mbali na droo hiyo maalum ya Biko kwa wateja wa Mpesa, zawadi za papo kwa hapo zinaendelea kutoka kwa wachezaji wa Biko wa mitandao yote ya Tigopesa, Airtel Money, Halopesa na Mpesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku zawadi za papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi milioni moja, bila kusahau droo kubwa za wiki za Jumatano na Jumapili.

TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA (TAEC) KUSHIRIKI MAONESHO YA NANE NANE KITAIFA MKOANI SIMIYU

$
0
0


Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), inatarajia kushiriki kwenye maadhimisho ya sherehe za kitaifa za Nane Nane kanda ya ziwa mashariki yatakayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu kuanzia tarehe 28 Julai hadi 10 mwezi Agosti, 2019. 

Katika maadhimisho hayo, TAEC itaweza kuonesha shughuli mbali mbali zinazofanyika katika Tume ikiwemo utoaji wa elimu kwa wananchi na wadau mbali mbali juu ya udhibiti na matumizi salama ya mionzi hapa nchini. 

Elimu kwa wananchi kuhusu matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia kwenye sekta za afya, kilimo, viwanda, mifugo, maji, lishe pamoja na ujenzi inatolewa. 

Wananchi wote wanakaribishwa ili kuweza kujipatia elimu bure kwa njia za maelezo, video fupi, vipeperushi na majarida ili kujiongezea uelewa juu ya majukumu yanayotekelezwa kisheria na TAEC katika Nyanja za udhibiti wa mionzi na uhamasishaji wa matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia. 

Imetolewa na , 

Peter Ngamilo 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano 
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania

Benki Ya NBC Yaahidi Ushirikiano Zaidi Na Mamlaka Za Serikali Za Mtaa.

$
0
0

Benki ya NBC imeahaidi kuendelea kutoa huduma bora zenye ubunifu kwa Mamlaka za serikali ya mtaa hapa nchini ili kuongeza tija na ufanisi zaidi kwa mamlaka hizo.

Ahadi hiyo imetolewa na Meneja Mahusiano ya Kiserikali wa NBC, Bw William Kallaghe wakati akizungumza kwenye kwenye Mkutano wa Mkutano Mkuu wa 35 wa Mwaka wa Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika hivi karibuni jijini Mwanza hivi karibuni.

Alisema katika kipindi cha miaka 50 ya uwepo wa benki hiyo hapa nchini, imewekeza katika huduma mbalimbali za kifedha ambazo zimeleta tija kubwa kwa mamlaka hizo na taifa kwa ujumla.

“Katika kipindi chote hicho NBC tumefanikiwa kutoa suluhisho ya kiubunifu kupitia huduma za kielectroniki kwa Halmashauri za Wilaya na Manispaa katika ukusanyaji wa mapato sambamba na huduma za malipo zinazoboresha usahihi katika uendeshaji akaunti’’ alisema.

Alibainisha kuwa uwezo huo umeimarishwa zaidi kufuata mfumo wa Malipo ya Serikali Kielektroniki (GePG),Mtandao wa NBC Wakala, Mfumo wa makusanyo wa POS pamoja na makusanyo kupitia simu za mikononi.

Kwa mujibu wa Bw Kallaghe, huduma za kielektroniki za malipo na ukusanyaji wa mapato zinazotolewa na benki ya NBC kwa mamlaka hizo zimeongeza ufanisi katika malipo na ukusanyaji wa mapato kwa mamlaka hizo na hivyo kurahisisha usahihi katika uendeshaji wa akaunti zao.

“Matawi ya NBC yamewezeshwa kwa nyanja zote katika kufanikisha mahitaji yote ya kifedha kwa Halmashauri na Mamlaka zote za serikali ya mitaa,’’ alibainisha huku akiongeza kuwa lengo kuu ni kuhakikisha mamlaka hizo zinatoa huduma bora na za kisasa sambamba na kujiongezea mapato.
Mkuu wa Kitengo cha Kibenki cha Taasisi za Sekta ya Umma kutoka Benki ya NBC, Bi. Noelina Kivaria akipokea cheti cha utambuzi kutoka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa ikiwa ni utambuzi wa mchango wa benki hiyo katika kufanikisha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika hivi karibuni jijini Mwanza. Anaeshudia ni Mwenyekiti wa Alat Taifa, Gulamhafeez Mukadam (kushoto). Benki hiyo ilikuwa ni moja ya wadhamini wa mkutano huo.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akipata maelezo ya huduma za kibenki kutoka kwa Meneja Mahusiano ya Kiserikali wa NBC, Bw William Kallaghe alipotembelea kwenye banda la benki hiyo kwenye Mkutano wa Mkutano Mkuu wa 35 wa Mwaka wa Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika hivi karibuni jijini Mwanza. Wengine ni Mkuu wa Kitengo cha Kibenki cha Taasisi za Sekta ya Umma, Bi. Noelina Kivaria. Benki hiyo ilikuwa ni moja ya wadhamini wa mkutano huo.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa akisoma moja ya machapisho ya huduma za kibenki ya Benki ya NBC alipotembelea kwenye banda la benki hiyo kwenye Mkutano wa Mkuu wa 35 wa Mwaka wa Jumuiya za Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika hivi karibuni jijini Mwanza. Kushoto ni Meneja Mahusiano ya Kiserikali wa Benki ya NBC, Bw William Kallaghe pamoja na maofisa wengine wa benki hiyo. Benki hiyo ilikuwa ni moja ya wadhamini wa mkutano huo.

DC Ikungi aapishwa, aahidi kushirikiana na wananchi wake

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akimuapisha Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Mh Edward Mpogolo leo Ofisini kwake,mara baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli kufuatia .Mh Edward alikuwa Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma. 
 Mkuu wa mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Mh Edward Mpogolo vitendea kazi leo Ofisini kwake,mara baada ya kuteuliwa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli.Mh Edward alikuwa Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma. 
 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,Mh Edward Mpogolo akitia saini kiapo chake mara baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singinda Mh Dkt.Rehema Nchimbi.



Na Charles James, MICHUZI TV

MKUU mpya wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida, Bw Edward Mpogolo ameapishwa leo rasmi kuanza majukumu yake kama Mkuu wa Wilaya hiyo, kuchukua nafasi ya iliyoachwa wazi na Miraji Mtaturu ambaye kwa sasa ni Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ikulu jana, uteuzi wa Bwana Mpogolo ulianza rasmi jana Julai 24, 2019, kuwa mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Baada ya kuapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Bi Rehema Nchimbi, Mpogolo ameahidi kushirikiana na uongozi wa Halmashauri ya  Wilaya katika  kuhakikisha inakuwa na maendeleo sambamba na kusimamia kikamilifu  makusanyo  ili kuinua uchumi wa eneo hilo.

“Ninamskuru Rais Dk,John Magufuli kwa kuniteua,ninaahidi kuwa sitamwangusha ,nitahakikisha ninashirikiana na Uongozi wa Mkoa na Halmashauri yangu ya Ikungi ili kuhakikisha tunafikia malengo ya makusanyo katia Wilaya yetu”amesema Mpogolo.

Ameahidi kushirikiana na uongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ili kuhakikisha wanatumikia wananchi wa Wilaya hiyo ikiwa wao ndio wawakilishi wa Rais katika eneo hilo.

Pia ameahidi kwenda kuisimamia  Katiba ya Nchi pamoja na Ilani ya Chama Tawala, Chama Cha Mapinduzi  katika  kuwatumikia   wananchi atakaowaongoza.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Rehema Nchimbi amesema  Mkuu wa Wilaya ndio msimamizi mkuu wa Kamati ya ulinzi na usalama na ndio msimamizi mkuu wa shughuli za maendeleo katika eneo husika na kumtaka kwenda kusimamia  vyema miradi ya Serikali inayotekelezwa Wilayani humo.

“Mkuu wa Wilaya yeye ni msimamizi mkuu na muwakilishi wa Rais katika Wilaya na ndio mkuu wa kamati ya ulinzi na usalama na ukasimamie miradi yote inayotekelezwa Wilayani humo” amesema Dtk Rehema.

Hata hivyo amemwambia kuwa Wilaya ya Ikungi inamiradi mbalimbali ya maendeleo iliyokusudiwa kwenye malengo ikiwemo miradi ya visima 28 vilivyokusudiwa kukamilishwa .

Aidha Dk.Nchimbi amesema upande wa Singida magharibi wana miradi ya visima 13 na Singida mashariki visima 15 .

Amebanisha malengo mengine yaliyowekwa kwa Wilaya hiyo kuwa ni kilimo cha zao la michikichi ekari 200 pamoja na kilimo cha zao la korosho.

RC MAKONDA AENDELEA KUTIMIZA AHADI YA UFADHILI WA MATIBABU YA UPASUAJI WA MOYO KWA WATOTO 60 KUTOKA FAMILIA DUNI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo Juni 25 amepokea zaidi ya Shilingi Milioni 23 kutoka kwa wadau ambao wameguswa na kampeni aliyoanzisha ya ufadhili wa matibabu ya upasuaji moyo kwa watoto 60 kutoka familia zenye hali duni.

Miongoni mwa Wadau waliomuunga Mkono RC Makonda ni Mbunge wa Kibaha Mjini Mhe. Sylvester Koka ambae amekabidhi hundi ya Shilingi milioni 10 kwaajili ya matibabu ya watoto 5 huku Mkurugenzi wa Dorka Catering Bi. Dorothy Kansolele akichangia milioni 6 na mkurugenzi wa kampuni ya Abe Professional Sound Bw. Abraham Ngomko akichangia Milioni 6 kwaajili ya matibabu ya watoto 3.

Akipokea fedha hizo RC Makonda amezikabidhi kwa uongozi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete na kueleza kuwa zitasaidia kugharamia zaidi ya Watoto10 kwenye upasuaji wa awamu ya pili.

Aidha RC Makonda amewashukuru wadau wote wanaondelea kumuunga mkono kwenye kampeni hiyo inayolenga kuokoa maisha ya watoto ambao wangeweza kupoteza maisha kutokana na wazazi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Kwa upande wao wadau waliokabidhi fedha hizo wameeleza kuwa wataendelea kuunga mkono zoezi hilo kwa kuongeza fedha nyingine kwakuwa wanaamini kampeni aliyoanzisha RC Makonda ni njema na linapaswa kuungwa mkono na wadau mbalimbali ili kuokoa maisha ya watoto.

Itakumbukwa kuwa RC Makonda alitoa ahadi ya kufadhili matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto 60 kwa muda wa miezi sita ambapo kila mwezi watatibiwa watoto10 na hadi sasa tayari amefanikisha matibabu ya watoto 30 kati ya 60 alioahidi.

PUMA ENERGY TANZANIA YAENDELEA KUTOA ELIMU YA MAFUNZO USALAMA BARABARANI NCHINI KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI

$
0
0
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde (wa pili kushoto), akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni nne kwa mshindi wa kwanza wa shindano la michoro ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi mwaka 2019, Alphonce Philipo wa shule ya msingi Jenerali Musuguri, katika hafla iliyofanyika jijini Dodoma jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde,akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah,akisoma taarifa katika utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah,akifurahia jambo na wanafunzi (hawapo pichani) wakati akisoma taarifa inayohusu utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mratibu wa mafunzo ya Elimu ya usalama barabarani kutoka Amend Bi.Neema Swai,akiongea wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mwalimu wa shule ya Msingi ya General Musuguri,Beatrice Chidumizi,akitoa pongeza kwa Puma Energy wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Afisa Elimu Msingi jiji la Dodoma,Joseph Mabeyo,akitoa shukrani kwa Kampuni ya Mafuta ya Puma Energy Tanzania wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .

Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde (wa pili kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, waandaaji wa shindano, Dominic Dhanah, wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mwalimu wa shule ya msingi Kaloleni Bi.Edina Kagulumbega,akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Sehemu ya Wanafunzi kutoka shule za msingi wakifuatilia hafla ya utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Baadhi ya walimu wakifuatilia utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Wanafunzi wakiimba wimbo maalumu wa unaoelezea umuhimu wa kuzingatia sheria za usalama barabarani wakati wa utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Mmoja wa wanafunzi waliopata elimu ya mafunzo ya usalama barabarani akionesha mfano wa mwanafunzi aliyepata ajali kwa kutozingatia sheria za usalama barabarani wakati wa utoaji zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi walioshinda shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Wakiangalia michoro ya usalama barabarani iliyochorwa na wanafunzi kutoka shule tano za msingi katika jiji la Dodoma kabla ya kumtangaza mshindi wa shindano la Michoro ya Usalama Barabarani kwa mwaka 2019 yaliyoandaliwa na Puma Energy Tanzania hafla hiyo imefanyika katika shule ya msingi Kaloleni jijini Dodoma .
Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde,akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa shindano la michoro ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi mwaka 2019, hafla ambayo imefanyika jijini Dodoma.

......................

*Ni katika mkakati wake wa kukomesha ajali nchini, wanafunzi Dodoma wanufaika

*Naibu Waziri Mavunde awapongeza, asema ni kampuni ya mfano...atoa maombi maalum

Na Said Mwishehe,Michuzi TV -Dodoma

KAMPUNI ya Puma Energy Tanzania imesema itaendelea kutoa elimu ya mafunzo ya usalama barabarani kwa shule za msingi mbalimbali nchini ikiwa ni mkakati wake wa kupunguza ajali nchini.

Pamoja na ahadi hiyo kampuni hiyo imetoa mafunzo ya usalama barabarani kwa wanafunzi zaidi ya 4500 katika shule tano za msingi katika Jiji la Dodoma kwa mwaka huu wa 2019 huku ikiahidi kuendelea kutoa elimu hiyo na kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kuhakikisha elimu hiyo inawafikia wanafunzi wengi zaidi ambao watakuwa mabalozi kwa wengine.

Akizungumza leo Julai 25 jijini Dodoma mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Vijana Athony Mavunde, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania Dominic Dhanah amesema programu hiyo ya mwezi mmoja kwa Dodoma ilihusisha mafunzo ya usalama barabarani kwa walimu 15 na wanafunzi 4500, katika shule tano.

Amefafanua kulikuwa na shindano la uchoraji wa michoro inayo hamsisha usalama barabarani ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni iliyozinduliwa rasmi mwaka 2013 ambapo zaidi ya shule 80 zimefikiwa huku wanafunzi 100,000 wakiwa wamepatiwa mafunzo katika mikoa ya Dar-es-salaam, Geita, Ruvuma na Dodoma.

“Puma Energy Tanzania imeamua kuja jijini Dodoma kwa sababu ya ukuaji wa haraka wa jiji hili ambapo shughuli za kijamii na ongezeko la watu na magari ambayo yanahatarisha usalama wa watoto wanapokwenda shuleni na kurudi nyumbani,",amesema Dhanah na kuongeza “Hadi sasa tumeweza kufundisha wanafunzi zaidi ya 4500 wa shule tano za msingi zilizopo jiji la Dodoma".

Dhahana amesema mafunzo hayo ya usalama barabarani na uchoraji alama za barabarani ni kipaumbele kwa lengo la kuwapa uelewa watoto hususani wa shule za msingi juu ya namna bora ya matumizi ya barabara.Alibainisha lengo ni kuwafanya watoto kuwa na uelewa wa matumizi ya barabara ili kuongeza uelewa kuhusu dhima nzima ya usalama barabarani kwa Watanzania.

“Lengo letu kama kampuni ni kuongeza wigo ili kufikia shule nyingi zaidi nchi nzima. Puma Energy Tanzania itaendelea kuwekeza katika kampeni ya usalama barabarani ikishirikiana na serikali kupitia jeshi la Polisi ili kuokoa maisha ya watanzania,” amebainisha.Akieleza zaidi amesema unzo hayo yametolewa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kupitia Shirika lisilo la kiserikali la Amend ambapo elimu hiyo pia imetolewa kwa walimu 15 wa shule hizo.

Awa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi ,Ajira na Vijana Anthony Mavunde amesema Puma Energy Tanzania ni kampuni iliyoamua kutoa elimu ya usalama barabara nchini huku akitoa ombi kwa kampuni hiyo kufundisha walimu hizo ili wakifundisha masomo ya kawaida wawe pia wanataka na elimu ya usalama.

Amesema kwa kufanya hivyo inasaidia kupunguza ama kumaliza kabisa ajali za barabarani huku akifafanua Serikali itaendelea kuweka alama za usalama barabarani ili kuondoa changamoto za ajali.Amesema kuwa kutokea kwa elimu hiyo kwa Jiji la Dodoma kunakwenda kutengeneza jamii yenye mabalozi wazuri katika kutoa elimu ya usalama barabarani huku akieleza Dodoma ni ya pili kwa mtandao wa barabara za lamo,hivyo ni muhimu elimu hiyo kuendelea kutolewa.

"Nimesikia ombi la walimu na wanafunzi la kuhitaji alama za barabarani, hivyo Serikali itaendelea kuweka alama hizo.Pia nimezungumza na wenzetu wa Puma wamekubali kupaka rangi za usalama barabarani na wataanza na shule tano ambazo zimepatiwa elimu hii ya usalama barabarani,"amesema Mavunde

Wakati huo huo walimu wakuu katika shule za msingi katika Jiji la Dodoma wametoa ombi la kuweka alama za barabarani na hasa alama za pundamilia au matuta ili kuhakikisha wanafunzi wanapovuka wanakuwa salama kwani barabara nyingi hazina alama hizo.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi General Musuguri Beatrice Chidumizi amesema changamoto iliyopo kwenye eneo la shule yao ni kukosekana kwa matuta au alama za barabarani, hivyo wanalazimika kumuweka mtu wa kuvusha wanafunzi ambaye analipwa fedha.

"Changamoto kubwa iliyopo katika shule yetu ni barabara yetu kutokuwa na matuta na alama za pundamilia,hivyo tunaomba tuwekewe alama za barabarani kwa ajili ya usalama wa wanafunzi wetu.Tunaishukuru Puma kwani imetusaidia sana kuwajengea uelewa wanafunzi wetu na sasa wanafahamu cha kufanya wanaoutaka kuvuka barabara.

"Tunaamini kupitia mafunzo haya tutapunguza ajali kwa watoto wetu na watumiaji wengine wa barabara zetu,"alisema Mwalimu Chidumizi na kuongeza kuwa umefika wakati kwa elimu hiyo kuendelea kutokea kwa Jiji la Dodoma hasa kwa kuzingatia Dodoma inakuwa kwa kasi kutokana na Serikali kuhamia Dodoma.

TAHA WATAKIWA KUFANYA TAFITI ZA KUWAKOMBOA WAKULIMA NCHINI TANZANIA

$
0
0
 Mgeni rasmi Afisa Kilimo wa mkoa wa Morogoro Isabela Chilumba akipewa maelezo juu ya kilimo cha kisasa cha nyanya kutoka kwa Meneja mradi huo Naimana. 
 Afisa Kilimo wa mkoa wa Morogoro Isabela Chilumba akiongea na wakulima na wageni waalikwa wakati wa sharehe za wakulima wa mazao ya mboga mboga yaliyoandaliwa Taasisi ya Tanzania Horticultural Association SASI (TAHA) iliyofanyika katika mjini Morogoro. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG, Morogoro. Meneja miradi Taasisi ya Tanzania Horticultural Association SASI (TAHA) Bi. Elianchea Shanga akiongea na wakulima na wageni waalikwa wakati wa sharehe za wakulima wa mazao ya mboga mboga yaliyoandaliwa taasisi ya TAHA iliyofanyika katika mjini humo. Wakulima wa Mboga Mboga akinyoosha mikono kujitambulisha.
 Meneja mradi Naimana akizungumza wakati akitambulisha mradi huo huku wakulima na wageni waalikwa wakifuatilia.
 Mmiliki wa shamba la nyanya la kisasa akiongea machache.
Meneja miradi TAHA Bi. Elianchea Shanga akiwatambulisha mabwana shamba wanaosaidia kufundisha wakulima.
 Wafanyakazi wa TAHA wakitoa elimu kwa wakulima.
 Kilima cha kisasa cha nyanya.

 Vingozi wa kijiji wakiwa na Mgeni rasmi.
Wakulima wakiwa na mgeni rasmi. 

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG, Morogoro.

 Watafiti wa mazao ya kilimo nchini wametakiwa kuhakikisha tafiti zao zinawafikia wakulima wadogo wadogo hasa waliopo vijiji ili wakulima hao waweze kulima kilimo chenye tija ikiwa ni katika kubabiliana na changamoto ya ushindani wa masoko kitaifa na kimataifa. 

 Rai hiyo imetolewa na Afisa Kilimo wa mkoa wa Morogoro Isabela Chilumba, wakati wa sharehe za wakulima wa mazao ya mboga mboga yaliyoandaliwa Taasisi ya Tanzania Horticultural Association SASI (TAHA) iliyofanyika katika mjini Morogoro. Bi. Chumba amesema kuwa watafiti hao endapo watafanya zao vyema zinaweza kumkomboa mkulima na akaweza kupata soko bora la mazao yao na itawakwambua kiuchumi. 

"Niwashukuru wataalamu maana nyie mmekuja wakomboa wakulima wadogo ambao mara nyingi huwa ni  ngumu kufikiwa matokeo yake wamekuwa wakilima kilima cha mazoea ambacho hakina manufaa kwao," amesema. Nae Meneja Miradi ya Taasisi ya TAHA, Bi. Elianchea Shanga amesema kuwa kwa sasa wamesambaa mikoa mbali mbali ya Tanzania na lengo lao kubwa ni kumkomboa mkulima kutoka katika kilimo cha mazoea na kulima kilimo cha tija.

 "Sisi lengo kubwa mkulima aone dhamani ya kile anachokilima maana tunasimamia kuanzia kuandaa shamba, madawa na mbolea huku tukimpa ushauri na kumtafutia soko," amesema. Kwa upande wao wakulima Mwajuma Abdala wamefurahishwa na ujio wa Taasisi ya TAHA huku wakielezea kuwa changamoto kubwa ambayo imekuwa mwiba kwao kwa sasa ni mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yamepelekea ukosefu wa mvua huku wakiiomba serikali kuongezea nguvu katika kusaidia kilimo cha umwagiliaji.

SIKU YA UREMBO WA ASILI TANZANIA KURINDIMA KESHO VIWANJA VYA LIFE PARK-MWENGE JIJINI DAR

$
0
0

Tamasha la Urembo wa Asili Tanzania kufanyika kesho Jumamosi na keshokutwa jumapili Viwanja vya life park mwenge ilipo Maisha club ,zamani Sinema mwenge. 

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mh Naibu waziri wa Habari , Utamaduni, sanaa na michezo Bi Juliana shonza .

Tamasha hili litakua na faida kwa kila atakefika bila gharama yoyote itatolewa huduma ya vipimo vya kansa ya Titi pamoja elimu ya kansa na magonjwa ya ngozi bure kutoka kwa wataalam Ocean Road

Vile vile kutakua na mafunzo ya ujasiriamali utengezaji wa sabuni za maji za kuogea ( shampoo ) bure kutoka kwa mjasiriamali na mwalimu Bi. Ester Mgonja bure siku ya jumapili .

Burudani itaongozwa na Malkia wa Taarabu Khadija Kopa pamoja na Aneth kushaba, mtangazaji na mjasiriamali Dina Marious na Sakina Lyoka watakuwepo , wasanii mwasiti, Grace matata, mchekeshaji jaymond watakuwepo na Rose Ndauka atakuwepo, kutakua Fashion show na burudani ya muziki ya kutosha. 

Sherehe za Urembo wa asili zitaambatana na kutoa zawadi kwa wanawake 300 watakaofika wa kwanza viwanja ni hapo kujipatia zawadi ya pakti moja ya Pedi ya kutoka Belle Bure.

Njoo ukutane na Wajasiriamali wa bidhaa za Urembo wa ngozi na nywele na bidhaa zingine kuanzia asubuhi saa 2 hadi saa 12 jioni. Vyakula na vinywaji vitapatikana pia. 

Urembo wa Asili sio ushamba .
@tanzanianaturalbeautyday
@missmandoza

Vodacom wazindua simu janja kuwasaidia wateja kuingia ulimwengu wa kidigitali

$
0
0



Mkuu wa Matukio wa Kampuni ya TECNO, Anuj Khosla, akimkabidhi zawadi ya simu mwandishi wa habari Austin Beyadi, Mwandishi huyo alishinda simu katika hafla fupi ya uzinduzi wa simu aina ya TECNO Yente na Itel Bamba zilizozinduliwa kwa ushirikiano kati ya Vodacom na TECNO kwenye Duka la Vodacom Mlimani City Dar es Salaam jana. Kampuni ya Vodacom imewaletea wateja wao simu hizo kwa lengo la kuwawezesha kuwa na maisha ya kidijitali kupitia simu janja bora zinazouzwa kwa bei nafuu.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Vodacom Tanzania Plc, Nandi Mwiyombella akionyesha simu mpya aina ya TECNO Yente iliyozinduliwa kwa ushirikiano kati ya Vodacom na TECNO katika hafla fupi iliyofanyika Duka la Vodacom Mlimani City Dar es Salaam, jana. Kampuni ya Vodacom imewaletea wateja wao simu hizo kwa lengo la kuwawezesha kuwa na maisha ya kidijitali kupitia simu janja bora zinazouzwa kwa bei nafuu. Kushoto ni Mkuu wa Matukio wa Kampuni ya TECNO, Anuj Khosla.


========   ========   ===========
Vodacom Tanzania Plc, kampuni nambari moja ya mawasiliano ya simu nchini imeungana na kampuni ya TECNO kuwaletea wateja wao toleo jipya la simu aina mbili za TECNO Yente na Itel Bamba, leo jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huu ni harakati ya Vodacom kuhakikisha jitihada zake za kuwezesha maisha ya kidijitali kwa wateja wao, kwa kupitia simu janja zinafanikiwa.

Akizungumza na waandishi wakati wa uzinduzi wa simu hizo, Mkuu wa matukio wa kampuni ya TECNO, Anuj Khosla alisema, “Tumedhamiria kuhakikisha kila Mtanzania anamiliki simu janja na kwa pamoja tunalifanya taifa la Tanzania kuwa la kidijitali”.

Simu hizi zitapatikana kwa bei ya shilingi 75,000 kwa Itel Bamba - 3G na Shilingi 195,000 kwa TECNO Yente ambayo ni - 4G, simu zote mbili zinakuja na ofa, ambapo kwa simu ya Itel Bamba wateja wetu watapata GB 3 kila mwezi kwa miezi minne na kwa simu ya TECNO Yente watapata GB 2 kila mwezi kwa mwaka mzima.

“Tunafuraha kushirikiana na TECNO kuendelea kuimarisha zaidi azimio letu la kuzidi kuwawezesha wateja wetu kuwa katika ulimwengu wa kidijitali. Uzinduzi huu umekuja katika kipindi muafaka, hasa kwa kuwa Watanzania wengi zaidi wanatumia huduma za simu janja” alisema Nandi Mwiyombella, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania.

Katika zama hizi za kidijitali, kupata taarifa, kununua na kulipia vitu, na kupata burudani za muziki na sinema, vinawezekana kwa kutumia simu janja, na matoleo haya mapya ya TECNO Yente na ITEL Bamba yatawezesha hayo yote na zaidi. “Uzinduzi huu umekuja sambamba na msimu wa sikukuu ya nanenane ili kuhakikisha wateja wetu, ambao ndiyo kipaumbele chetu wanasherehekea sikukuu ya nanenane msimu huu kidijitali zaidi” aliongeza Bi. Mwiyombella.

Simu hizi zitapatikana katika maduka yote ya Vodacom Tanzania Plc na pia katika madawati ya huduma kwa mteja (Service Desks) yanayotoa huduma kwa wateja wa kampuni hiyo maeneo mbalimbali nchini huku pia zikipatikana katika maduka ya TECNO.


RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MRADI WA KUFUA UMEME WA MAJI KATIKA MTO RUFIJI

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker mara baada ya kuweka Jiwe la Msingi mradi wa Ujenzi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji katikati ya Morogoro na Pwani.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia pamoja na viongozi wengine mara baada ya tukio hilo la uwekaji wa Jiwe la Msingi.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker, Waziri wa Nishati Medard Kalemani pamoja na viongozi wengine akisikiliza namna mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji utakavyokuwa ukifanya kazi mara baada ya kukamilika.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia michoro ya ujenzi huo mkubwa wa kufua umeme.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Kuzalisha umeme Megawati 2115 katika eneo la mto Rufiji.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Nishati wa Misri Dkt. Mohamed Shaker wakati wakielekea kwenda kuweka jiwe hilo la msingi.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mitambo itakayotumika katika mradi huo mkubwa wa kufua umeme.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia eneo la bonde katika mto Rufiji mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo wa umeme.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la Mradi.
Eneo la mto Rufiji ambalo litatumika katika ujenzi huo wa kufua umeme kama linavyoonekana. PICHA NA IKULU

Plasco expands operations - launches the first state of the art pipe factory in East and Central Africa using ‘Weholite’ technology

$
0
0
Plasco Limited in Tanzania is the largest manufacturer of plastic pipes for water supply and sanitation in the country has launched a USD 4 million factory expansion using ‘Weholite’ technology, the first of its kind in East and Central Africa used to produce Structured Wall High Density Polyethylene (HDPE) pipes for Sewerage and Drainage, Manholes and Tanks for storm water retention and drinking/potable water. 

The company aims to provide modern water storage and sanitation solutions to the region through the use of this new technology that is now available in Tanzania and East Africa as a whole. The factory was inaugurated in Temeke, Dar es Salaam by the Minister of Industry and Trade, Innocent Bashungwa; other government official in attendance included the Deputy Permanent Minister of Water, Emmanuel Kolobelo. 

Speaking during the event, Hon. Bashungwa remarked on the company’s use of innovative technology to accelerate the progress of the pipe manufacturing industry in Tanzania. “The ministry applauds such innovations which directly contribute to catalysing industrial development and increases the competitiveness of our industries, locally and internationally. The factory expansion and its use of cutting-edge technology is a significant milestone in the revival of the industrial economy,” said Bashungwa. 

He added that the new technology will attract more investment and boost the economy of the country through exports. Bashungwa urged other industries to invest in innovative technology to boost the quality of their products to international standards. 

Speaking on behalf of the company, Alimiya Osman, the Chief Operating Officer, disclosed that the country will no longer need to import plastic pipes as the investment in new equipment meets the growing demand and aligns with local content policy. He added that the use of HDPE materials ensures that the pipes do not rust or corrode and adheres to international standards. 

“Since the start of the company’s operations in 1993, we remain committed to manufacturing and supplying quality, robust and leak proof plastic piping systems to our customers in Tanzania and neighbouring countries. The investment in new equipment supports the government’s efforts to develop critical infrastructure to improve water supply and sanitation systems that will improve the lives of Tanzanians throughout the country,” concluded Alimiya. 

As the country’s leading pipe manufacturer, Plasco Limited employs over 100 Tanzanians and supports the country’s industrialization drive and ambitions to become a middle-income economy by 2025. 

Minister of Industry and Trade Innocent Bashungwa launching Plasco Ltd extension factory that uses Weholite technology which is the first in Tanzania, East and Central Africa to produce plastic pipes. Dar es Salaam, today Third left is Plasco Ltd Chief Operating Officer, Alimiya Osman and Finland Ambassador for Tanzania, Ambassador Riitta Swan (Right).
Minister of Industry and Trade Innocent Bashungwa commending the technology and the quality of pipes produced by Plasco Ltd to during the launching ceremony of an extension factory that uses Weholite technology which is the first in Tanzania, East and Central Africa to produce plastic pipes, Dar es Salaam, today. Right is Plasco Ltd Chief Operating Officer, Alimiya Osman.


MAJALIWA APOKEA VIFAA VYA HOSPITALI NA SHULE KUTOKA TAASISI YA HELPING HAND NA BENKI YA NMB

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama vifaa mbalimbali vya hospitali vilivyotolewa na Taasisi ya Helping Hand na Taasisi ya Jamii Bora kwa ajili ya Hospitali, Zahanati na Vituo vya Afya wilayani Ruangwa, kwenye viwanja vya Zahanati ya Nandagala wilayani humo, Julai 28, 2019. Makabidhiano ya vifaa hivyo yalifanyika kwenye Zahanati ya Nandagala. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Jamii Bora, Yassir Salim. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Salum Tahir (kushoto) ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Helping Hand kuhusu vifaa mbalimbali vya hospitali alivyokabidhiw na Taasisi ya hiyo kwa ajili ya hospitali, zahanati na Vituo vya Afya wilayani Ruangwa. Mahakabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya zahanati ya Nandagala Julai 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Huduma za Serikali wa Benki ya NMB, Vicky Bishubo (wapili kulia) kuhusu kompyuta na madaftari kwa ajili ya shule wilayani Ruangwa pamoja na madirisha ya aluminium na milango kwa ajili zahanati ya Nandagala . Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Zahanati ya Nandagala Julai 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kupokea vifaa mbalimbali vya hospitali kutoka Taasisisi ya Helping Hand vyenye thamani ya sh. Milioni 250 pamoja na madirisha ya aluminium, milango kwa ajili ya zahahanati ya Nandagala wilayani Ruangwa pia kompyuta na madftari kwa ajili ya shule za wilaya hiyo vyanye thamani ya sh.milioni 25 vilivyotolewa na Benki ya NMB. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya zahanati ya Nandagala, julai 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya NMB baada ya kupokea madirisha ya aluminium na milango kwa ajili ya zahahanati ya Nandagala wilayani Ruangwa pia kompyuta na madftari kwa ajili ya shule za wilaya hiyo vyanye thamani ya sh.milioni 25 vilivyotolewa na NMB. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye viwanja vya zahanati ya Nandagala,Julai 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images