Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46370 articles
Browse latest View live

RAIS WA SHIRIKISHO BARAZA LA TAIFA FALME ZA KIARABU (UAE) AFUNGUA MKUTANO WA PILI WA BUNGE LA AFRIKA

$
0
0

Rais wa Shirikisho la Baraza la Taifa la Falme za Kiarabu (United Arab Emirates – UAE),Dr. Amal Abdullah Al Qubaisi akifungua Mkutano wa Bunge la Afrika leo nchini Afrika Kusini

Rais wa Shirikisho la Baraza la Taifa la Falme za Kiarabu (United Arab Emirates – UAE),Dr. Amal Abdullah Al Qubaisi amefungua Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika ulioanza leo Mei 6,2019 jijini Johannesburg,Afrika Kusini kwa kukutanisha wabunge kutoka nchi 54 barani Afrika.

Akitoa hotuba yake, Dr. Amal Abdullah Al Qubaisi alisema Bunge la Nchi za Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE) zimekubaliana kushirikiana na Bunge la Afrika katika kumaliza changamoto zinazowakabili wananchi barani Afrika.

“Uhusiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu na Bara la Afrika umekuwa mkubwa,tumekuwa tukisaidia mambo kadha wa kadha barani Afrika,tunataka kuona usalama unazidi kuimarika Afrika,kwani bila usalama katika nchi zetu hakuna maendeleo yanayoweza kufikiwa”,alisema Dr. Amal.

“Masuala ya vitendo vya kigaidi yana athari kubwa,tunatakiwa kwa pamoja kushirikiana kuyatafutia ufumbuzi ili wananchi wetu wawe salama lakini pia kuwa na suluhisho la kudumu juu ya wakimbizi wanaorejea nyumbani na wakimbizi wa ndani,tunafurahi kuona wakimbizi wakirudi kwenye nchi zao kwa amani”,alisema.

Kwa upande wake,Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang alisema ili ushirikiano na umoja madhubuti unahitajika ili kufikia suluhu za kudumu juu ya masuala ya amani na usalama barani Afrika.Ufunguzi wa Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika litakalofungwa Mei 17,2019 umekwenda sanjari na wabunge 26 wapya wa bunge la Afrika kutoka nchi mbalimbali kuapishwa.

Kauli mbiu ya Bunge la Afrika mwaka huu ni "2019 mwaka wa Wakimbizi,wanaorejea nyumbani na wakimbizi wa ndani : Kuelekea kupata masuluhisho ya kudumu katika kulazimishwa kuhama makazi katika Afrika".Mwandishi wetu,Kadama Malunde ametuletea picha za matukio mbalimbali yaliyojiri wakati wa Bunge la Afrika likifunguliwa leo..Tazama hapa chini

Rais wa Shirikisho la Baraza la Taifa la Falme za Kiarabu (United Arab Emirates – UAE),Dr. Amal Abdullah Al Qubaisi akitoa hotuba yake wakati akifungua Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika leo Mei 6,2019 Midrand, jijini Johannesburg,Afrika Kusini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang akitoa hotuba yake Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika leo Mei 6,2019.

Rais wa Shirikisho la Baraza la Taifa la Falme za Kiarabu (United Arab Emirates – UAE),Dr. Amal Abdullah Al Qubaisi (katikati),Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang na washiriki wa Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika wakiwa wamesimama kuimba wimbo wa Umoja wa Afrika.
Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa wakiimba wimbo wa Umoja wa Afrika.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele (kulia) na viongozi mbalimbali wa bunge la Afrika wakiwa katika ukumbi wa bunge la Afrika leo Jijini Johannesburg.
Wabunge wa Bunge la Afrika wakiwa ukumbini.
Bunge linaendelea.
Wabunge wakiwa ukumbini.
Aliyekuwa Mjumbe wa Uongozi wa Bunge la Afrika Dr. Bernadette Lahai kutoka Sierra Leone akitoa tamko na ujumbe wa mshikamano barani Afrika.


Wabunge wakiwa ukumbini.

Wabunge wapya wa bunge la Afrika kutoka Swaziland wakila kiapo bungeni leo. Hao ni miongoni mwa wabunge 26 kutoka nchi mbalimbali walioapishwa leo.
Wabunge wapya wa bunge la Afrika wakiendelea kiapo Wageni mbalimbali wakiwa ukumbini.
Wageni mbalimbali wakiwa ukumbini.

Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Mkutano wa pili wa kawaida wa Bunge la Afrika.

MAKAMU WA RAIS AZINDUA RIPOTI YA MAZINGIRA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia ripoti ya Mazingira Tanzania iliyoandaliwa na Benki ya Dunia pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira mara baada ya kuizindua katika hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird (kushoto) mara baada ya kuzindua ripoti ya Mazingira Tanzania iliyoandaliwa na Benki ya Dunia pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira uliofanyika katika hotel ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Mazingira Tanzania iliyoandaliwa na Benki ya Dunia pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bi. Bella Bird akihutubia wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Mazingira Tanzania iliyoandaliwa na Benki ya Dunia pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam na Mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akihutubia wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Mazingira Tanzania iliyoandaliwa na Benki ya Dunia pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
…………………. 




Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
MAKAMU wa Rais Samia Suluhu Hassan amezindua ripoti ya hali ya Hali ya Mazingira nchini Tanzania ambapo ripoti hiyo imetaja sababu mbalimbali ikiwemo ya kasi ya ongezeko la watu na ukuaji wa maendeleo unachangia kwa sehemu kubwa uharibifu wa mazingira.

Akizungumza leo Mei 6,2019 wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam, Mama Samia amesema ripoti hiyo imefanywa kati ya Serikali ya Tazania na Benki ya Dunia na lengo ni kuangalia kwa kina kuhusu hali ya mazingira nchini na hatua za kuchukua katika kutafuta ufumbuzi wake. 

Amefafanua ripoti ioanesha kuwa kasi ya ongezeko la watu na kasi ya ukuaji wa uchumi nchini unachangia uharibifu wa mazingira, hivyo ni jukumu la Watanzania pamoja na watalaam wa kada mbalimbali na wadau wa maendeleo kuangalia namna bora itakayowezesha idadi ya watu inayoongezeka na ukuaji wa uchumi hauwi sehemu ya kuharibi mazingira nchini. 

“Ripoti inaposema ukuaji wa uchumi na kasi ya ongezeko la watu ndio sababu za uharibifu wa mazingira, lazima watanzania na watalaamu kwa ujumla kutusaidia kutafuta ufumbuzi wake.Kama kasi ya ongezeko la watu ni sababu sasa tufanyeje ?Inaana nusu ya watu ipungue, au kasi ya ukuaji wa uchumi ambayo nayo inatajwa kama sehemu ya chanzo cha kuharibu mazingira inachangia. 

“Ni lazima Watanzania tuangalie namna bora itakayofanikisha mazingira yanatunzwa na shughuli za maendeleo na kasi ya ukuaji wa watu inaendelea.Ndani ya ripoti imeonesha namna ambavyo rasilimali za Tanzania namna ambavyo zinaharibiwa. 

“Imeonekana kuwa matumizi mabaya ya maji, uharibifu wa hali ya hewa, kilimo na mambo mengine kadhaa yanachangia kuharibu mazingira.Watalaamu wanayo nafasi ya kushauri na kutoa mapendekezo ya nini kifanyike ili kulinda mazingira yetu,”amesema Makamu wa Rais. 

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Januari Makamba amesema kuwa “Leo ni siku muhimu kwa watu tunaohusika na mazingira kwasababu tumezindua ripoti ya hali ya mazingira ambayo imefanywa na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.Ripoti hii inaeleza hali ya uchambuzi nchini Tanzania. 

“Chimbuko la ripoti hii ni mazungumzo ambayo tumekuwa nayo muda mrefu na wenzetu wa Benki ya Dunia pamoja na wadau wa maendeleo kuhusu namna gani nchi yetu inapata maendeleo kwa namna endelevu zaidi. Tunaposema maendeleo endelevu maana yake ni mchakato mzima wa kutafuta maendeleo ambayo yatadumu. Tutafute maendeleo huku tukitunza mazingira. 

“Ripoti inaonesha hali halisi ya uharibifu wa mazingira na bahati nzuri inaelekeza namna bora na nzuri ya kuhakikisha tunalinda mazingira yetu.Tumeona kuna changamoto kubwa ya uharibifu wa mazingira na wakati huo huo tunayo matumaini makubwa kwani kuna hatua ambazo zimependekezwa ndani ya ripoti hiyo ili kuhakikisha tunabaki salama katika eneo la mazingira. 

Amefafanua katika ripoti hiyo kuna sababu nyingi ambazo zimetajwa kama sehemu ya kuchangia uharibifu wa mazingira na sababu kubwa inatajwa kasi ya ongezeko la ukuaji wa watu na kasi ya ukuaji wa uchumi.Pia amesema kilimo cha umwagiliaji maji nacho kimetajwa moja ya sababu ya kuharibifu wa mazingira. 

Kuhusu mapendekezo ambayo yametajwa ndani ya ripoti hiyo , Waziri Makamba kuna mapendekezo manne ambayo yametolewa na pendekezo namba moja ni kuhakikisha taasisi za uharibifu wa mazingira na uchafuzi wa hali ya hewa zinaimarishwa kuongeza udhibiti. 

Makamba amefafanua katika ripoti inaonesha watu 26000 wanafariki dunia ka mwaka kutokana na uharibifu wa hali ya hewa huku akieleza kuwa kila dakika misitu inayoharibiwa ni urefu wa kiwanja cha mpira, hivyo kuna kila sababu ya kuendeleakuchukua hatua ili mazingira yabaki salama. 

Hata hivyo amesema baada ya kuzinduliwa kwa ripoti hiyo, kinachofuata ni mjadala katika kuichambua na kisha kuwekwa mikakati mbalimbali ambayo itaifanya nchi yetu iendelee kutunza mazingira yake hasa kwa kuzingatia kuna hatua nyingi zinachukuliwa kuhakikisha mazingira yabanaki salama.

TAFITI NI MOYO WA TAALUMA KATIKA KULETA MAENDELEO NCHINI-PINDA

$
0
0

"Atembelea na kujifunza utekendaji wa kazi katika baadhi ya Ndaki na Shule Kuu"


Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda amesema tafiti ni duru inayotanua mawanda ya taarifa na kuchangia katika kuleta maendeleo nchini na kwenye jamii kwa ujumla. 

Amesema hayo wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Tano ya Tafiti akiwa mgeni rasmi wa wiki hiyo iliyoanza leo katika Chuo Kikuu Dar es Salaam tarehe 6 Mei,2019. 

"Wiki hii itachochea ushirikiano kati ya Chuo Kikuu na serikali na kusaidia kuhabarisha umma kuhusu tafiti zitakazo oneshwa na kuzisikia na jinsi zitakavyosaidia kuleta maendeleo katika jamii", alisema Pinda. 

Maendeleo ya jamii yanahusiana moja kwa moja na maendeleo ya tafiti kwani ukuaji jumuishi wa uchumi katika masuala ya maendeleo huenda sambamba na matumizi bora ya rasilimali, alisema. 

Pinda amepongeza uongozi wa chuo kikuu kwa jitihada ya maboresho katika upande wa elimu kwa kuchagua njia mbadala ya ufundishaji kwa vitendo, amekitaka chuo kutumia vema mfumo huo mpya wa ufundishaji ili kuondoa changamoto zilizopo pale wanafunzi wanapohitimu mafunzo yao kuweza kufikiria kujiajiri wenyewe. 

MAPEMA: Makamu Mkuu Chuo Kikuu Dar es Salaam Prof. William Anangisye alisema, tafiti hizi huleta maendeleo na ukuaji wa misingi muhimu sana inayochochea katika kuhamasisha uchumi wa viwanda, kwani tafiti nyingi zinatusaidia katika kuongeza thamani za shughuli chuo kikuu kwa ujumla kwakuwa tunazingatia mihimili mitatu ufundishaji, tafiti na elimu, alisema. 

Maonesho ya Wiki ya tafiti ya Chuo Kikuu Dar es Salaam yatafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Jumatatu tarehe 6 hadi Jumatano tarehe 8 Mei 2019 yenye kauli mbiu isemayo "Utafiti kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu" . 

Imetolewa na Afisha Habari na Uhusiano 

Imetolewa na Afisa Uhusiano 
Kitengo cha Huduma kwa Umma 
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam 









RC Wangabo awasihi wafanyabiashara kutoongeza bei za bidhaa mwezi mtukufu wa Ramadhani

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wafanyabiashara wa vyakula katika masoko ya Mkoa huo kuwa na moyo wa huruma kwa wale watakaofunga mwezi mtukufu wa Ramadhani kwani ni mwezi wa toba ambao waumini hujinyima kwaajili ya watu wengine.

Amesema kuwa mwezi wa ramadhani ni kipindi ambacho waumini humrudia Mwenyezi Mungu kwa nguvu zote, hivyo sio kipindi cha wafanyabiashara hao kujinufaisha kwa watu wanaofunga, kwani waumini wamekuwa wakijidunduliza ili kusaidia wasiojiweza lakini wafanyabiashara hao wanaona ni fursa ya kujinufaisha.

“Hiki ni Kipindi ambacho wanawasaidia watu mbalimbali kwa nguvu zao zote, sasa akamsaidie mtu mwingine na wakati huo huo akusaidie wewe ambaye unataka kujinufaisha kwa manufaa yako mwenyewe ukijua kabisa kwamba hiki ni kipindi maalum cha kumrudia Mwenyezi Mungu niwasihi sana wafanyabiashara wote msiongeze bei ya vyakula mbalimbali ten asana sana mshushe bei za vyakula, nisinikie bei zimepanda sijui ongezeko la bei ya sukari sijui ya unga, maharage sitaki kusikia nataka kusikia bei zimeshuka, “ Alisisitiza.

Aidha, amewatakia mfungo mwema wa mwezi wa Ramadhani Waislamu wote Tanzania pamoja na wale waumini wa dini mbalimbali watakaosindikiza mwezi huo na kumuomba Mwenyezi Mungu atupe baraka kutokana na mwezi huo ndani ya Mkoa wa rukwa na Tanzania kwa ujumla.

Waislamu wote wa Tanzania wanatarajia kuungana na waislamu wengine duniani kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani huku waumini wa Tanzania wakianza kufunga kuanzia tarehe 7.5.2019.

Waganga Wakuu wa Mikoa wapewa mwezi mmoja kutathmini utendaji wa Kamati za afya za Mikoa na Wilaya zao

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Dkt Dorothy Gwajima akizungumza na Kamati ya uendeshaji ya huduma za afya ya mkoa wa Ruvuma mjini Songea jana
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia afya Dkt Dorothy Gwajima akizungumza na baadhi ya wananchi waliokuja kupata huduma za afya katika kituo cha afya cha Mjimwema kilichopo Manispaa ya Songea
baadhi ya wajumbe wa kamati ya uendeshaji ya huduma za afya wa mkoa wa ruvuma wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia afya Dkt Dorothy Gwajima jana mjini Songea.


Na Mathew Kwembe, songea 

Waganga wakuu wa Mikoa Tanzania Bara wamepewa mwezi mmoja kuhakikisha kuwa wanazifanyia tathmini ya kina Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya za Mikoa na Wilaya zao kuona kama zinaendana na kasi ya mabadiliko yanayokusudiwa na Serikali ya Awamu ya Tano. 

Agizo hilo limetolewa jana mjini Songea na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI anayeshughulikia Afya Dkt. Dorothy Gwajima wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya kutoka Halmashauri ya Namtumbo, Halmashauri ya Wilaya ya Songea pamoja na Manispaa ya Songea. 

Amesema anawapa siku 30 Waganga Wakuu wa Mikoa yote kuhakikisha kuwa wanafanya tathmini ya Wajumbe waliopo katika ofisi zao kama wanatosha kuendelea na nyadhifa zao za kusimamia jukumu la uendeshaji huduma za afya katika mikoa na halmashauri zao. 

Dkt Gwajima ameongeza kuwa endapo itabainika kuwa baadhi ya Wajumbe wa Kamati hizo hawana sifa zinazowafanya kushindwa kutekeleza majukumu yao ya usimamizi na uendeshaji huduma za afya katika maeneo yao, Waganga Wakuu wa Mikoa watalazimika kuwaweka pembeni Wajumbe hao na kuunda upya Kamati ambazo zitaweza kuiendeleza agenda ya mabadiliko katika sekta ya afya. 

“Kinyume na hapo katika ziara hizi ninazoendelea kuzifanya mikoani nikikuta yupo Mganga Mkuu wa Mkoa ambaye ametulia tu, mapungufu katika vituo bado yapo na amewezeshwa na Serikali, ajue wazi kuwa wa kutokutosha wa kwanza atakuwa yeye,” amesema Dkt Gwajima na kuongeza: 

“Haiwezekani tukute mapungufu madogo kabisa katika vituo, ambayo yangeweza kuonwa na wao walioko huko eti hayaonekani hadi tuje sisi kutoka Tamisemi ndiyo mapungufu hao yafanyiwe kazi,”amesisitiza Dkt Gwajima. 

Naibu Katibu Mkuu huyo ameonya tabia iliyojengeka miongoni mwa Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma ya Afya kukimbilia kuomba msamaha pindi zinaposhindwa kutekeleza majukumu yake kwa makusudi. 

Amesema huu ni wakati wa kuboresha sekta ya afya katika vituo vya afya na zahanati kwa kuhakikisha kuwa mazingira ya utoaji huduma yanaboreshwa ili yaweze kuwavutia wananchi wengi kukimbilia kupata huduma katika zahanati na vituo vya afya vinavyomilikiwa na serikali ikiwemo hospitali za halmashauri. 

Dkt Gwajima amesema kuwa kamwe hatawapa nafasi Wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya wa Mikoa na Wilaya ambao siku zote wamekuwa ni watu wa visingizio vya kuomba kusamehewa ama kupewa muda kuwa wamefahamu mapungufu yao wakati mapungufu husika ni yale yale ambayo kila siku Serikali inatoa maelekezo kuwa yafanyiwe kazi. 

Amesema angependa kuona Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya katika Mikoa na Halmashauri zikijikita katika kuongelea mambo ya ubora wa huduma kwa mteja “’quality care” na kuwa, mteja ni mfalme na si vinginevyo. Serikali imeshirikisha Wananchi na kutuwezesha miundombinu safi na dawa za kutosha, bajeti ya kufuatilia huduma inatolewa, semina za uongozi zinafanyika, maelekezo yanatolewa je, tatizo huwa linatokea wapi? 

“Hivi vitu vidogo vidogo vya kitaalamu tubebe sisi wenyewe, Wananchi wametuunga mkono, tumeweza kushirikiana nao kujenga zahanati na vituo vya afya katika mikoa na halmashauri zetu hivyo ni jukumu letu sasa kuhakikisha kuwa tunatoa huduma bora za afya kwa Wananchi na kuondoa hii tabia ya kuwepo kwa malalamiko yanayosababishwa na uzembe katika kufuatilia na kusimamia,” amesema. 

Kwa mujibu wa Dkt.Gwajima, katika ziara zake alizokwisha zifanya katika mikoa ya Morogoro, Dodoma, Njombe na Songea amejionea mapungufu mbalimbali ya utoaji wa huduma bora za afya katika vituo vya afya na zahanati ambayo yapo ndani ya uwezo wa Kamati za Usimamizi na Uendeshaji Huduma za Afya katika mikoa na halmashauri husika. 

Ameongeza kuwa mapungufu hayo ambayo ameyashuhudia kwenye vituo vya afya na zahanati zinazomilikiwa na umma yametokana na watoa huduma waliopo katika vituo hivyo kutopata usimamizi unaostahili kutoka kwa Kamati za Usimamizi na Uendeshaji wa Huduma za Afya za Mikoa na Halmashauri husika. 

Dkt Gwajima anaamini kuwa, kushindwa kwa Kamati za Uendeshaji na Usimamizi wa utoaji huduma za afya katika ngazi za mikoa na halmashauri kutekeleza majukumu yao, ndiko kulikopelekea kukithiri kwa uchafu katika majengo ya vituo vya afya na zahanati, kushindwa kufanyiwa matengenezo muhimu ya kuboresha mazingira ya zahanati na vituo hivyo licha ya vituo hivyo kuwa na fedha za uendeshaji wake. 

“Unakuta kituo kina fedha za kutosha kwenye akaunti lakini mapungufu madogo madogo ya kukera yamejaa,” ameeleza Naibu Katibu Mkuu. 

Amesema hali hiyo imesababishwa na kushindwa kwa Kamati za Uendeshaji Huduma za Afya za Mkoa (RHMT) na zile za Halmashauri (CHMT) kwa kutofanya kazi ya ufuatiliaji wa utoaji huduma bora na utaalam kwenye vituo vya afya nchini licha ya kuwezeshwa na Serikali. 

Sambamba na kuwataka Waganga Wakuu wa Mikoa kuzitathmini Kamati hizo, Dkt Gwajima pia amewataka wajumbe wa Kamati hizo kutambua kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli ipo na agenda moja tu ya kuleta mabadiliko katika sekta ya afya na kuwagusa watumiaji wa huduma hizo kwa huduma zenye ubora unaostahili. 

“Hatutapimwa kwa idadi ya semina au uwepo wa kituo cha afya tu karibu na Wananchi bali kwa ubora huduma zinazotoleewa katika vituo hivi, vinginevyo Wananchi watakuwa karibu na vituo husika lakini hawavitumii,” amesema. 

Dkt Gwajima amebainisha mapungufu kadhaa aliyoyaona kwenye ziara yake kuwa ni pamoja na Kamati za Uendeshaji Huduma ya Afya kushindwa kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zinazojitokeza kwenye vituo vyao vya afya na zahanati, kuwepo kwa malalamiko toka kwa wagonjwa, kukosekana kwa takwimu sahihi za utendaji kazi na Wajumbe wa Kamati za uendeshaji huduma za Afya kushindwa kuandika vizuri kumbukumbu za taarifa za kazi za ikiwemo mihutasari ya vikao na wengine kutokaa kabisa vikao muhimu. 

Akiwa katika kituo cha afya Mjimwema Manispaa ya Songea Naibu Katibu Mkuu Dkt.Gwajima alipokea kero za wagonjwa kuhusu uwepo wa kauli mbaya toka kwa baadhi ya watumishi wakiwemo wauguzi na matabibu, tatizo la ukosefu dawa na vifaa tiba muhimu hususan vya akina mama wajawazito. 

“Hapa Mjimwema nimebaini kasoro nyingi mojawapo kauli mbaya za watumishi na tatizo la dawa na vifaa tiba kwa wagonjwa ” ameonya Dkt .Gwajima. 

Aidha, alimpongeza tabibu msaidizi mmoja aliyeibuliwa na mteja kwamba, anatamani watoa huduma wote wangekuwa kama tabibu huyo anayeitwa Lidya Mwakyusa Hii ni mara ya pili kwa wateja kuwataja hadharani watumishi watoa huduma wenye huduma inayojali mteja akiwemo Edward Mapunda wa Kituo cha Afya cha Halmashauri ya Njombe. 

Dkt. Gwajima amewapongeza watoa huduma wanaotambua wajibu wao kuwa, mteja ni mfalme na amewataka kutovunjwa moyo na baadhi ya watumishi wasiozingatia maadili ya kazi na kuleta kero kwa wateja. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Jairy Khanga ameahidi kuchukua hatua za mapema kufanya mabadiliko ya utendaji kazi wa Kamati za Usimamizi wa Huduma za Afya katika Mkoa wa Ruvuma

MERU KUONDOKANA NA TATIZO LA CHUMBA CHA KUHIFADHIA MAITI

$
0
0
Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha

Wananchi Wa Wilaya ya Arumeru wapo mbioni kuondokana na adha ya ukosefu wa chumba chakuhifadhia maiti (mochwari) baada ya kujengewa mochwari Mpya ya kisasa.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya mkuu wawilaya hiyo
mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Meru Cosmas Kalasala alisemakuwa
chumba hicho chakuhofadhia maiti mpaka kiishe kitagarimu kiasi cha shilingi
milioni 160.

Alisema kuwa mpaka sasa ujenzi umekamilika kwa asilimia 80%na wanatarajia
kukamilisha ujenzi huo hivi karibuni ili wananchi waweze kutumia jengo hilo
waondokane na usumbufu wa kwenda kuhifadhi miili ya marehemu nje ya Wilaya.

Kwa upande wake mkuu wawilaya hiyo Jerry Muro alisema serikali ya awamu ya
tano imeona tatizo hili la ukosefu wa chumba cha kuhifadhia maiti hivyo
wakaamua watoe fedha za mfuko wa jimbo na kijengea chumba hichi katika
hospital ya wilaya ya Arumeru

"unajua fedha hizi za maendeleo ya mfuko wa jimbo ni zamaendeleo ya
wananchi wa meru hivyo tumefata utaratibu wa kushirikisha wananchi
tukachukua fedha hizi kwaajili ya kuwajengea wananchi wa meru chumba cha
kuhifadhia mihili ya marehemu ndugu zao"alisema Muro.

Alisema kuwa wananchi hao walikuwa wanapata tabu sana pindi ndugu zao
wanapofariki kwani hospital ya wilaya ilikuwa haina huduma hiyo kwakipindi
kirefu hivyo walikuwa wanalazimika kwenda kuhofadhi miili ya marehemu ndugu
zao katika hospital ya mkoa ya Arusha(mounti meru hospital ) ambapo ni
zaidi ya kilometa 20kutoka hospital ya Wilaya.

Muro alisema jengo hilo linalojengwa nikubwa nalinaeza kuhifadhi miili 45
hadi 50 ya marehemu nawanatarajia kulizindua rasmi na mwenge wa uhuru
mapema Mwezi June.
Mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Meru Cosmas Kalasala akimuonyesha Mkuu wa wilaya ya Arumeru jinsi chumba hicho cha kuhifadhia maiti kilivyofikia .
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema jengo hilo la kuhifadhia maiti litasadia sana wananchi wa wilaya yake, kwani walikuwa wanapata tabu sana ya kusafirisha miilii pindi ndugu zao wanapofariki dunia

HIVI NDIVO MAELFU YA WANANCHI DAR WALIVYOJITOKEZA BARABARANI KUUPOKEA MWILI WA MENGI

$
0
0
Jeneza lenye Mwili wa marehemu Dk. Reginald Mengi ukiingizwa kwenye gari maalumu baada ya kuwasili nchini nchini ukitoa Dubai, tayari kwa safari ya kuelekea Hospitali ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es salaam kwa kuhifadhiwa.

*Ni baada ya mwili wake kuwasili nchini ukitokea Dubai 
 *Wengine waamua kukimbilia gari ili kugusa jeneza lake


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MAELFU ya wananchi wa Jiji la Dar es Salaam leo Mei 6,2019 wamejitokeza kwa wingi kuupokea na kuulaki mwili wa aliyekuwa mfanyabishara maarufu nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dk. Reginald Mengi ambaye amefariki dunia Mei 2 mwaka huu akiwa Dubai.

Mwili wa marehemu Dk.Mengi umewasili nchini saa nane mchana ambapo viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wastaafu na wananchi wa kada mbalimbali walijitokeza Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam kuupokea.

Pia Mke wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete alikuwa miongoni mwa waliofika uwanjani hapo kuupokea mwili huo wa Dk.Mengi. Baada ya kuwasili na kupokelewa na kufanyika maombo kabla ya kuanza safari ya kuelekea Hospitali ya Lugalo.
Mjane wa Marehemu Dkt. Mengi, Bi. Jacquenine akiwana wa waombolezaji wengine pamoja na Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete waliofika kwenye uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere kumlaki.

Maelfu ya wananchi waliamua kuweka kambi katika barabara ambazo mwili wa Mengi umepitishwa ambapo wapo baadhi ya wananchi walionekana wakigusa jeneza ambalo limebeba mwili kama ishara ya kuonesha upendo.

Wakati mwili unapitishwa katika barabara ya Nyerere, Buguruni, Ilala,Kigogo, Magomeni, Kinondoni na  Morroco wakati ukielekea Mwenge na kisha Lugalo idadi ya watu ilizidi kuongezeka kuusubiri mwili wa Dk.Mengi.

Simanzi na majonzi yalikuwa yametawala katika nyuso za wananchi walioamua kwenda kuulaki mwili wa Dk.Mengi huku wengi wao wakionekana kukimbilia gari iliyobeba mwili huo kwa lengo la kulishika. Mengi enzi za uhai alijipambanua kuwa karibu na jamii ya Watanzania ambapo alitumia sehemu ya fedha zake kutoa misaada.
Kutokana na idadi ya watu waliokuwa wamejipanga barabarani, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda aliyekuwa kwenye msafara huo alionekana akihakikisha msafara huo unakwenda katika mazingira yaliyotulivu huku akisaidiwa na Jeshi la Polisi kupita Kikosi cha Usalama barabarani.

Katika msafara huo waendesha bodaboda nao hawakuwa nyuma kwani nao walikuwa sehemu ya wananchi ambao walihakikisha wanakuwepo katika mapokezi ya mwili huo.

Wananchi mbalimbali ambao walikuwa barabarani na kupata fursa ya kumzungumzia Dk.Mengi wamesema kuwa na mambo mengi ya kujifunza kutoka katika maisha ya Mengi ambaye enzi za uhai wake alikuwa na upendo kwa kila mtu na kubwa zaidi alihakikisha utajiri wake unawanufaisha na wengine kwani hakuwa mchoyo.
Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamejitokeza kwa wiki maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam kuulaki mwili wa marehemu Dk. Reginald Mengi uliowasili nchini mchana wa leo. Picha kwa hisani ya CloudsFM
Mjane wa Marehemu Dkt. Mengi, Jacqueline Mengi akilia kwa uchungu.


WATU WENYE ULEMAVU WATAKIWA KUCHANGAMKIA MKOPO USIO NA RIBA

$
0
0
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Stellah Ikupa (kulia), akiwa meza kuu pamoja na Rais wa Umoja wa Wanamuzi Tanzania (TAMUFO), Dkt. Donald Kisanga (katikati) na Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Mollel kwenye Tamasha la Kitaifa la kupinga Unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia kwa Watuwenye Ulemavu lililoandaliwa na umoja  huo lililofanyika Jijijini Dodoma wiki iliyopita. 

Viongozi hao wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Tamasha hilo.
Mtoto Bilal Donald Nyawenga mwenye ulemavu anayedaiwa kufungiwa tangu 1997
Rais wa Umoja wa Wanamuzi Tanzania (TAMUFO), Dkt. Donald Kisanga, akijaribu kuzungumza na mtoto huyo.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

WATU Wenyeulemavu wametakiwa kuchangamkia fedha za mkopo bila riba walizotengewa na Serikali ambazo zipo katika Halmshauri ya miji nchini.

Wito huo umetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenyeulemavu, Stellah Ikupa wakati akihutubia kwenye Tamsha la Kitaifa la kupinga Unyanyasaji na Ukatili wa kijinsia kwa watu wenye ulemavu lililoandaliwa na Umoja wa Wanamuzi Tanzania (TAMUFO) lililofanyika Jijijini Dodoma wiki iliyopita. 

"Changamukieni fedha hizo ambazo ni asilimia mbili zipo kwenye halmshauri zetu tena mnakopa bila ya kuwa riba yoyote waambieni na wenzenu" alisema Ikupa.

Alisema awali wanawake na vijana kila kundi lilitengewa asilimia 5 ya fedha kwa ajili ya kukopeshwa lakini baada ya waziri huyo na wenzake kuomba kusaidiwa walemavu kila kundi lilitoa asilimia moja na kuwa mbili kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Ikupa alisema Serikali imekuwa ikiwajali sana watu wenyeulemavu ndio maana imetenga wizara hiyo ambayo inashughulikia masuala yote yanayo wahusu walemavu.

Rais wa TAMUFO, Dkt. Donald Kisanga aliiomba serikali kuendelea kusimamia sheria zote zinazowalinda walemavu ikiwa pamoja na kuwajengea miundombinu mizuri kama ngazi za kushukia na kupandia katika majengo makubwa.

"Kumekuwa na ukihukaji wa sheria za kuwalinda walemavu kama kuwaficha majumbani na kukosa haki zao za msingi kama kupata elimu na huduma zingine za kijamii tunaiomba serikali iendelee kusimamia sheria hizo na kuchukua hatua kali kwa watuhumiwa" alisema Dk.Kisanga.

Baada ya Tamasha hilo wananchi waliweza kuwaongoza viongozi wa TAMUFO kwenda kumshuhudia mtoto Bilal Donald Nyawenga mwenye ulemavu ambaye yupo Kijiji cha Chogola Kata ya Sama wilayani Mpwapwa ambaye inadaiwa anafungiwa ndani  tangu azaliwe mwaka 1997.

Mtoto huyo mwenye ulemavu wa baadhi ya viungo vyake na mwenye kichwa kikubwa amekosa haki ya kusoma lakini licha ya baadhi ya viongozi wa kijiji hicho kujua changamoto aliyonayo hakuna hatua yoyote iliyochukulia ya kuweza kumsaidia.

MKUU WA WILAYA YA BUHIGWE AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUTUMIA VIZURI KALAMU ZAO.

$
0
0
Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kigoma.

MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Michael Ngayalina amewataka wanahabari kutumia kalamu zao vizuri ili kuepuka kuleta migogoro na uchochezi katika jamii badala yake wazitumie katika kuleta mabadiliko hasa katika sekta ya uchumi.

Kanali Ndayalina ameyasema hayo kwenye ukumbi wa NSSF uliopo Manispaa ya Kigoma mjini  kwenye maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari.

Mkuu wa Wilaya huyo ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo alisema kuwa wanahabari wana nafasi kubwa ya kuchochea kukua kwa uchumi wa Taifa iwapo watatumia vizuri nafasi zao.

"Nyie wanahabari ni kiungo kizuri kati ya jamii na serikali yao endapo mtatumia vizuri kalamu kuelimisha jamii mambo mbalimbali ya kuchochea maendeleo uchumi wa Taifa letu utapanda"Alisema

Pia amewataka wanahabari kuandika habari zao kwa usahihi kama sheria inavyowaelekeza hasa katika kipindi hiki tunachoelekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika octoba mwaka huu.

Naye Rais wa umoja wa muungano wa vilabu vya waandishi Tanzania(UTPC)Deogratius Nsokolo lengo kubwa ni kuona waandishi wanafuata maadili ya kazi za uandishi na kuwataka waandishi wa habari nchini kuwa sehemu ya mabadiliko hasa kwenye kipindi hiki kinachoelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2020.

Baadhi ya wadau wa habari waliohudhuria katika maadhimisho hayo wamewataka wadau kutoa ushirikiano kwa waandishi ili habari ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
 Rais wa UTPC Deo Nsokolo akiongea wakati wa maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo  vya habari katika ukumbi as nssf manispaa ya Kigoma
 Wanahabari wa Mkoa wa Kigoma wakiwa katika picha ya pamoja
 Katibu Mkuu wa Chama cha waandishi wa habari Mkoa wa Kigoma(KGPC)Fadhil Abdallah akisoma hotuba kwa wadau waliohudhuria maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari.
 Mmoja wa Wadau aliyehudhuria maadhimisho hayo akichangia mada

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA BUNGE LA AFRIKA

$
0
0
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akimpokea Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete alipotembelea Makao Makuu ya Bunge la Afrika “Pan- African Parliament” yaliyopo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini leo Mei 7,2019.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akimkaribisha ofisini Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete. 
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza na Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang (katikati) na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele. 
Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Roger Nkodo Dang akizungumza jambo wakati wa majadiliano hayo.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa majadiliano yake na Viongozi wa Bunge la Afrika.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu hali ya uchaguzi Afrika Kusini.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete ambaye anaongoza Timu ya Waangalizi wa Umoja wa Afrika kwenye Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019 akiongoza kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi huo nchini Afrika Kusini.
Kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi mkuu nchini Afrika Kusini kati ya Viongozi wa Bunge la Afrika na timu ya waangalizi ya Umoja wa Afrika inayoongozwa na Dkt. Jakaya Kikwete kikiendelea.
Waheshimiwa Mabalozi kutoka Kenya,Nigeria wa kiongozwa na Balozi Naimi Aziz wa kwanza kulia anayeiwakilisha Tanzania nchini Ethiopia na Umoja wa Afrika ambao wameambatana na Mheshimiwa Kikwete.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele (wa tatu kulia) akizungumza wakati wa kikao cha kujadili maandalizi ya uchaguzi mkuu mwaka 2019 nchini Afrika Kusini.
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete akitembelea ukumbi wa Bunge la Afrika.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe. Stephen Masele akipiga picha ya kumbukumbu ofisini kwake na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika, Jijini Johannesburg, Afrika Kusini. 


****

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Jakaya Kikwete ametembelea Makao Makuu ya Bunge la Afrika “Pan- African Parliament” yaliyopo Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Dkt. Kikwete ambaye ni Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Umoja wa Afrika wa Uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019 amepokelewa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele leo Jumanne Mei 7,2019.

Amelipongeza Bunge la Afrika kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kusimamia Demokrasia, Utawala na Masuala ya Ulinzi na Usalama barani Afrika.

“Mimi nilikuwa miongoni mwa Mawaziri wa Mambo ya Nje ambao tulikutana kule Sirte Libya kuandaa kanuni za kuanzishwa kwa Bunge la Afrika,hivyo ninayo furaha kubwa kuona hatua kubwa ya maendeleo ya bunge,Nawapongeza sana Rais na Makamu wa Rais kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuendeleza bunge hili na Waafrika wote tunawatagemea”,amesema Dkt. Kikwete

“Leo na timu yangu ya uangalizi ambao tupo hapa Afrika Kusini kwa ajili ya uangalizi wa Uchaguzi mkuu wa mwaka huu,na ninashukuru miongoni mwa timu yangu wabunge wa bunge la Afrika ni miongoni mwa wajumbe wangu,nawapongeza sana Bunge la Afrika kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika kusimamia demokrasia”,ameongeza Dkt. Kikwete.

Kwa upande,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele amemshukuru na kumpongeza, Mheshimiwa Kikwete kwa mchango wake mkubwa kwa bara la Afrika kwenye nyanja za afya,elimu na demokrasia.

"Sisi viongozi vijana tuna mengi ya kujifunza kutokana na uzoefu wako mkubwa kwenye masuala ya uongozi na siasa za kimataifa, binafsi nakushukuru sana kwa malezi yako ambapo kwa uwezo wa mwenyezi Mungu nimeweza kufika hapa nilipo kiuongozi",amesema Mhe. Masele.

Aidha amemuahidi Mheshimiwa Kikwete kuwa Bunge la Afrika litatoa ushirikiano wote unaohitajika ili kuweza kutimiza majukumu yake katika uangalizi wa uchaguzi Mkuu wa Afrika Kusini mwaka 2019.


Na Kadama Malunde - Johannesburg,Afrika Kusini

KAFULILA ASITISHA MKATABA NA TBA UJENZI WA NYUMBA ZA VIONGOZI

$
0
0

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila akizungumza na Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Songwe Mhandisi Fidelis Cosmas katika eneo la ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala Mkoa, Kafulila amevunja Mkataba na TBA wa ujenzi wa Nyumba hizo kutokana na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo.
Eneo likionyesha hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Mkoa na Katibu Tawala Mkoa ambapo kwa muda wa miezi miwili tangu wakabidhiwe eneo la ujenzi TBA wamefikia hatua hiyo huku wakibakiwa na miezi mingine miwili ya kukamilisha ujenzi huo, hali iliyopelekea Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila kuvunja mkataba na TBA kutokana na kutoridhishwa na kasi hiyo.

……………………..

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila amesitisha Mkataba wa ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Mkoa na ya Katibu Tawala Mkoa uliokuwa kati ya yake na Shirika la Ujenzi la Taifa (TBA), kutokana na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo.

Kafulila akiambatana na wakuu wa Sehemu wa Sekretarieti ya Mkoa wa Songwe amefikia uamuzi huo jana mara baada ya kutembelea eneo la ujenzi wa nyumba hizo na kukuta hatua ya ujenzi iliyofikiwa hairidhishi.

Kafulila amesema kasi ya ujenzi wa nyumba hizo inatia mashaka kutokana na kuwa kazi iliyokwisha fanyika kwa muda wa siku sitini ni ndogo ukilinganisha kazi na muda uliobakia kufikia tarehe ya makubaliano ya kukamilika ujenzi.

“Kazi iliyobaki kiuhalisia haiwezekani TBA wakaikamilisha kwa muda uliobakia, kwani tuliwakabidhi eneo la ujenzi tarehe 2-2-2019 na tulikubaliana ikifika tarehe 30-06-2019 nyumba hizo mbili ziwe zimekamilika lakini kwa kipindi cha miezi miwili hakuna kitu wamefanya na kuna dalili zote za kutokamilisha kwa muda”, ameeleza Kafulila.

Ameongeza kuwa TBA wamekuwa na tabia ya kutekeleza miradi ya ujenzi kwa kasi ndogo mkoani Songwe na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina kuu kutokana na kutozitumia kwa muda unaotakiwa yaani ndani ya mwaka wa fedha wa serikali ambapo fedha hizo zinakuwa zimetolewa.

“TBA mmekuwa na kawaida ya kutekeleza miradi yetu kwa kasi ndogo na hivyo kusababisha fedha kurudishwa hazina, mfano ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamesababisha takribani Bilioni 3.8 zirudishwe na sasa tunahangaika kuziomba tena, uzembe huu tunaona unelekea kujirudia tena na sisi kama Mkoa hatuko tayari kila mara tunapewa fedha za ujenzi halafu zinarudishwa kwa uzembe wa TBA”, ameongeza Kafulila.

Amesema kuwa Mkoa hauna matatizo na Wizara ya Ujenzi wala shirika hilo la TBA ila lazima hatua za kusitisha mkataba huo zichuliwe ili kunusuru fedha hizo kurudishwa hazina kuu kutokana na kuchelewa kuzitumia ndani yam waka wa fedha wa serikali pia ili nyumba hizo zikamilike kwa muda na kuwezesha makazi ya viongozi.

“Naomba ifahamike mimi na mkoa kwa ujumla hatuna matatizo na Wizara ya Ujenzi pamoja na TBA lakini tukilifumbia macho hili hata sisi tutapimwa utimamu wa akili zetu, nimetembelea eneo la ujenzi zaidi ya mara nne lakini hakuna maendeleo yoyote, kiuhalisia kwa kasi hii TBA Mtatuangusha, sisi tunapenda kufanya kazi kwa kuendana na kasi ya Rais wetu”, amesisitiza Kafulila.

Amesema gharama ya Ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa Mkoa ni shilingi milioni 499.9 na tayari TBA walipewa malipo ya awali ya shilingi milioni 74.9 huku nyumba ya Katibu Tawala Mkoa ikiwa na gharama ya shilingi milioni 499.7 na malipo ya awali yaliyotolewa ni shilingi milioni 74.9

Imeelezwa kuwa TBA hawajawahi kuwasilisha taarifa ya kazi iliyokwisha fanyika lakini pia hawajaomba fedha zozote tangu walipwe malipo ya awali huku muda uliobaki ukionyesha kuwa hataweza kukamilisha kazi iliyobaki.

RAIS DKT. SHEIN AZUNGUMZA BALOZI BRAZIL NCHINI TANZANIA

$
0
0

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Balozi wa Heshima wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Zanzibar Abdulsamad Abdulrahim, alipowasili katika ukumbi wa mkutano Ikulu Zanzibar, katikatika Balozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Nchini Tanzania Antonio Augusto Cesar.
IMG_5701
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Balozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Nchini Tanzania. Antonio Augusto Cesar, alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo na kujitambulisha leo,7-5-2019.(Picha na Ikulu)
IMG_5726
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wac Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akifurahia jambo wakati akizungumza na Balozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Nchini Tanzania  Antonio Augusto Cesar, alipofika Ikulu Zanzibar kwa kujitambulisha na mazungumzo leo 7-5-2019.
IMG_5748
IMG_05749
IMG_5763
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Mlango (Zanzibar Door) Balozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Nchini Tanzania Antonio Augusto Cesar, baada ya mazungumzo yao yaliofanyika Ikulu Zanzibar leo,7-5-2019.
IMG_5802
IMG_5817
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja kushoto Balozi wa Shirikisho la Jamuhuri ya Brazili Nchini Tanzania Antonio Augusto Cesar, Afisa wa Ubalozi wa Brazil Bi. Daniella Xavier na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu na kulia Balozi wa Heshima Shirikisho la Jamuhuri ya Brazil Zanzibar.Bwa. Abdulsamad Abdulrahim na Kaimu Mkurugenzi Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Zanzibar,Balozi Mohammed Hamza. wakiwa katika picha ya pamoja. 

SERIKALI KUENDELEA KUTOA ELIMU YA MATUMIZI YA MBOLEA YA ASILI-MHE MGUMBA

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu swali bungeni leo tarehe 8 Mei 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu swali bungeni leo tarehe 8 Mei 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma.



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Serikali kwa kushirikiana na taasisi za sekta binafsi imeendelea kutoa elimu ya kilimo bora inayojumuisha matumizi sahihi ya mbolea za asili, viuatilifu vya asili, mbegu bora na hifadhi ya mazingira ili kuzalisha mazao kwa tija na kuwa na kilimo endelevu.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 8 Mei 2019 wakati akijibu swali la Mbunge wa Chambani Mhe Yussuf Salim Hussein aliyetaka kufahamu Serikali imeweka mikakati gani ya kutoa elimu ya mbolea ya asili kwa wakulima na hatua Serikali inayoichukua ili kuona kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza kwa kuzalisha mazao yasiyotumia mbolea za viwandani. 

Alisema kuwa katika kutekeleza mpango wa muda mrefu wa matumizi sahihi ya virutubisho vya udongo, Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) inafanya utafiti wa afya ya udongo katika Kanda zote saba za kiikolojia za kilimo nchini. 

Utafiti huo unalenga kubaini aina za virutubisho na tabia za udongo katika maeneo mbalimbali nchini ili kuweza kutoa elimu kwa wakulima kuhusu kiasi, aina na matumizi sahihi ya mbolea za viwandani na asili. Utafiti huo umeanza kwa kuchukua sampuli za udongo katika Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini na sehemu ya Kanda ya Mashariki (Mkoa wa Morogoro) na utaendelea katika maeneo mengine nchini na kukamilika Juni 2020.

Alisema, kwa kutambua ongezeko la mahitaji ya mazao na bidhaa za kilimo zinazozalishwa kwa kutumia mbolea za asili na viuatilifu vya asili, Serikali imeboresha mtaala wa mafunzo katika vyuo vya kilimo ambapo mada za kilimo hai na hifadhi ya mazingira zimejumuishwa ili kuwawezesha maafisa ugani na wakulima kupata elimu hiyo. 

Mhe Mgumba aliongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na Tanzania Organic Agriculture Movemet (TOAM), Sustainable Agriculture Tanzania (SAT), Ecology Agriculture chini ya SWISSAID, Zanzibar Organic Producers (ZANOP), Tanzania Alliance for Biodiversity (TABIO) na TANCERT inatoa elimu ya kilimo hai kwa wakulima na kutoa vyeti vya ubora wa mazao kwa ajili ya masoko maalum. Baadhi ya mazao ambayo yanazalishwa katika mfumo wa kilimo hai hapa nchini ni pamoja na kakao, kahawa, pamba na viungo. 

Kadhalika, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe Easter Michael Mmasi aliyetaka kufahamu kuhusu ushiriki wa wanawake kwenye sekta ya kilimo, Mhe Mgumba alisema kuwa Sekta ya Kilimo inajumuisha sekta ndogo za kilimo mazao, mifugo, uvuvi na misitu. 

Bajeti za Wizara za Sekta ya Kilimo zinajumuisha bajeti za Wizara za sekta husika, Bodi za mazao na Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara za Kisekta. Utekelezaji wa bajeti hizo huwawezesha wanaume na wanawake katika shughuli za kilimo. Wanawake wanachangia asilimia 90.4 ya nguvukazi ya wanawake inayotumika katika shughuli za kilimo na kuchangia wastani wa asilimia 70 ya mahitaji ya chakula nchini. 

Mhe Mgumba alisema kuwa katika kutatua changamoto hizo Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004 kupitia mifuko ya uwezeshaji ikiwemo Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake (Women Development Fund - WDF) ambao huchangiwa asilimia 4 ya mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kila mwaka. Katika mwaka 2017/2018, jumla ya Shilingi 15,633,312,764.91 zimetolewa kwa vikundi 2,919 vya wanawake na vijana vyenye jumla ya wanawake wajasiriamali 29,190 katika Halmashauri mbalimbali nchini. 

Aidha, alisema kutokana na umuhimu wa wanawake katika kilimo Serikali imeielekeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo (Tanzania Agricultural Development Bank – TADB) katika mikopo inayotoa asilimia 20 ya mikopo itolewe kwa vikundi vya wanawake. Hadi Januari 2019, asilimia 33 ya mikopo imetolewa katika vikundi vya wanawake kupitia Benki ya TADB. Vilevile, benki za NMB na Azania zimeanzisha dirisha maalumu la kutoa mikopo kwa vikundi vinavyo jishughulisha na kilimo na miradi mbalimbali. Pia Serikali imehamasisha wanawake kujiunga kwenye vikundi vya ushirika wa akiba na mikopo kama SACCOS, VICOBA ili kupata huduma za kifedha na mikopo kwa urahisi ili kuongeza mitaji yao katika kilimo.

Mhe Mgumba aliongeza kuwa, Serikali imeuelekeza Mfuko wa Pembejeo za Kilimo (Agricultural Input Trust Fund - AGITF) kutoa kipaumbele kwa vikundi vya wanawake vinavyoomba mikopo ya kuendeleza kilimo. Vile vile, Serikali imeendelea kutoa hati miliki za ardhi za kimila na hati miliki za ardhi kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kumiliki ardhi na kuzitumia kama dhamana kukopa katika taasisi mbalimbali za kifedha ili waweze kupata mitaji ya kununua pembejeo na zana bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji, tija na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya usindikaji wa mazao ya kilimo.

MILIONI 700 ZA RAIS MAGUFULI ZAANZA KUTOA MATOKEO POLISI

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akipita kukagua ujenzi wa majengo mapya na ya kisasa yanayojengwa katika Chuo cha Maofisa wa Polisi kilichopo Kurasini jijini Dar es salaam, ujenzi unaotokana na fedha iliyotolewa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, kiasi cha shilingi milioni 700 kwa ajili ya ukarabati wa Chuo hicho cha Maofisa. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro akifurahia jambo huku akiwa amembeba mtoto aliyefika katika hospitali Kuu ya Polisi iliyopo Kurasini jijini Dar es salaam leo, akiwa na mzazi wake kwa ajili ya kupata huduma za matibabu hospitalini hapo, IGP Sirro amefanya ziara ya ghafla ya ukaguzi yenye lengo la kuona namna huduma za matibabu zinavyotolewa pamoja na kujua changamoto wanazokutananazo. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kulia) akizungumza na Maofisa wa Polisi wanaofanyakazi katika hospitali Kuu ya Polisi iliyopo Kurasini Dar es salaam leo, wakati alipofanya ziara ya ghafla ya ukaguzi yenye lengo la kuona namna huduma za matibabu zinavyotolewa pamoja na changamoto wanazokutananazo ambapo IGP Sirro amewataka viongozi hao kutoa huduma bora kwa wateja. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu Dkt. C. Msenga wa hospitali ya Jeshi hilo iliyopo Kurasini Jijini Dar es salaam wakati alipofanya ziara ya ghafla ya ukaguzi hospitalini hapo. Picha na Jeshi la Polisi.

DC KASESELA: MARUFUKU KUFANYA BIASHARA IRINGA KAMA HULIPI KODI AU HUNA KITAMBULISHO CHA MACHINGA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizunguza na wafanyabiashara wa bidha za kusindika walikuwa wamekusanyika katika Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Iringa kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya ujasiliamali 
Wafanyabiashara wa bidha za kusindika wakiwa wamekusanyika katika Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Iringa kwa ajili ya kupatiwa mafunzo ya ujasiliamali na wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wa bidhaa za kusindika



NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Wafanyabiashara wa wilaya ya Iringa wametakiwa kufanya biashara wakiwa wamelipa kodi au wanatakiwa kuwa na kitambulisho cha wafanyabishara wadogo wadogo maarufu kama kitambulisho cha machinga.

Akizungumza na wajasiliamali waliokuwa wamekusanyika katika Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) Iringa,mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alisema ni marufuku kwa sasa kufanya biashara yoyote wilaya ya Iringa bila kulipa kodi na zile ambazo hazijafikia hatua kodi zitalipa tozo

“Sasa tunaanza kufanya mchakato wa kuchunguza kujua wafanyabiashara wangapi wanafanya kazi hizo bila kulipa kodi na tutawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria za nchi zinavyosema” alisema Kasesela

Kasesela aliwataka wafanyabiashara wadogowadogo wote wa wilaya ya Iringa kuhakikisha wanapata kitambulisho cha kwa shilling elfu ishirini ambacho kinatamruhusu kufanya biashara sehemu yoyote hapa nchini kwa mujibu wa Rais.“Jamani ili ufanye biashara kwa uhuru katika wilaya ya Iringa ni lazima uwe na kitambusho cha wafanyabisahara wadogo au uwe umelipia leseni kutoka katika mamlaka husika la sivyo huwezi kufanya biashara hiyo wilaya ya Iringa” alisema Kasesela

Kasesela aliwataka wananchi wote wanaopenda kufanya biashara kuhakikisha wanafanyabiashara kwa kufuata taratibu zilizowekwa na nchi ili wasipate usumbufu wowote ule kutoka kwa mamlaka za wilaya ya Iringa.

“Jamani wananchi wa Iringa changamkieni kuchukua vitambulisho vya wafanyabishara wadogo wadogo ili kufanya biashara zenu mkiwa na uhuru wa kutosha ila mkikahidi mkono wa sheria utawahusu” alisema Kasesela

Aidha Kasesela aliwashauri wafanyabishara ya bidhaa za kusindika kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa kufuata kanuni za kisheria kwa kuhakikisha wanalipa kodi kama inavyostahili.Nao baadhi ya wafanyabiashara wadogo wadogo walimuadi mkuu wa wilaya hiyo kuwa watahamasishana kuhakikisha wote wanakuwa na vitambulisho hivyo ili wafanye biashara kwa uhuru na haki.

“Mkuu tunakuhakikishia kuwa tutafanyabiashara huku tukiwa tumevaa vitambulisho hivi kwa kuwa Rais wetu katupa uhuru wa kufanya biashara zetu mahali popote pale bora mradi tuwe na vitambulisho hivyo” walisema wafanyabiashara hao.

Benki Ya Exim Yamtangaza Rasmi Mtendaji Mkuu Mpya

$
0
0

Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki ya Exim Tanzania anaemaliza muda wake Bw Said Mwema (Kulia) akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Exim Tanzania pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakati wa hafla hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya Exim Tanzania Bw Jaffari Matundu (Kulia) kizungumza na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Exim Tanzania pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakati wa hafla hiyo. 

Baadhi ya wajumbe ya Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Exim Tanzania wakimpongeza Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo Bw Jaffari Matundu (Kulia) wakati wa hafla maalumu ya kumpongeza Mkurugenzi huyo pamoja na wafanyakazi wengine iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam jana.


Mwenyekiti mstaafu wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki ya Exim Tanzania Bw Yogesh Manek (Kulia) akiwapongeza Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki hiyo Bw Jaffari Matundu (katikati) pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Benki hiyo anaemaliza muda wake Bw Said Mwema wakati wa hafla hiyo.
 

MAHAKAMA INAYOTEMBEA KURAHISISHA UPATIKANAJI WA HAKI

$
0
0
Katika kuboresha huduma zake kwa wananchi, Mahakama ya Tanzania imeamua kuanzisha Mahakama inayotembea (Mobile Court) ili kuendelea kusogeza huduma za kimahakama karibu zaidi na wananachi. Lengo la kuanzishwa kwa kwa huduma hii muhimu pia ni kuwapunguzia wananchi gharama za kufuata huduma za Mahakama na Kuongeza imani ya wananchi kwa Mahakama.

Mahakama inayotembea ni kitendo cha Mahakama kuhamisha huduma zake na kuzitolea katika sehemu mbalimbali ndani ya mamlaka husika. Dhana hii pia inamaanisha kuwa Mahakama inaweza kuhamisha huduma zake na kuzitolea sehemu mbalimbali kwa kutumia gari maalumu lenye chumba kilichotengenezwa mithili ya ofisi ya Hakimu, kinachoweza kutumika katika kusikiliza mashauri na kuyatolea maamuzi.

Gari litakalotumika kutoa huduma za Mahakama lina nyenzo zote za kimahakama kama vile sehemu ya kusikilizia mashauri, vitendea kazi vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya kisasa ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kama vile kamera, mfumo wa matangazo (PA system) na mwavuli kwa ajili ya kivuli na viti vya kupumzikia wateja. Aidha, mahakama hii ni gari maalumu lenye sehemu mbili (2) Chumba cha hakimu ambacho kitakuwa na meza ya hakimu, meza ya wadaawa, meza ya karani/mpiga chapa, Televisheni, Kompyuta “Printer”, Kabati la kutunzia majalada, Vyombo vya kurekodi mashauri na vifaa vya kutangazia (vipaza sauti) pamoja na chumba cha faragha.


Historia ya Mahakama inayotembea Tanzania
Dhana hii ya Mahakama inayotembea ilikuwepo tangu miaka ya 1920 ambapo Mahakama Kuu kwa wakati huo ilitumia behewa la treni kutoa huduma za kimahakama kwenye ukanda ambao treni ilipita. Sababu za kuhamisha mahakama zilikuwa kumfuata shahidi kwa sababu ni mgonjwa au kuwapunguzia gharama mashahidi au iwapo kielelezo hakihamishiki kirahisi.

Huduma zitolewazo katika Mahakama inayotembea

Aidha, huduma zitakazotolewa na Mahakama inayotembea ni pamoja na kupokea, kusajili na kusikiliza mashauri, kutoa taarifa za mashauri, kutoa fomu za viapo na kuthibitisha nyaraka mbalimbali. Huduma nyingine zitakazotolewa ni kufanya usuluhishi kwa wadaawa na kutoa elimu kuhusiana na masuala mbalimbali ya Mahakama.


Aina za mashauri yanayosikilizwa katika Mahakama inayotembea

Kama ilivyo kwa Mahakama tulizozizoea, Mahakama inayotembea itasikiliza mashauri ya aina zote yanayosikilizwa na Mahakama za Mwanzo kama vile migogoro ya ndoa, madai, mirathi pamoja na jinai. Mahakama hii itasikiliza mashauri katika operesheni maalumu.


Ratiba ya utoaji huduma

Baada ya kuanzishwa kwa Mahakama inayotembea, Mahakama ya Tanzania inatarajia kutoa huduma kwa kufuata Kalenda na ratiba maalumu pamoja na taratibu zilizowekwa. Ratiba (causelist) zitatoa taarifa na maelekezo ya siku na muda ambao shauri litasikilizwa.


Utekelezaji Hukumu (kukaza hukumu)

Utekelezaji wa maamuzi ya Mahakama inayotembea utafanywa katika Mahakama za kawaida katika eneo/mamlaka husika. Mfano, hukumu iliyotolewa na mahakama inayotembea katika kituo cha Bunju utekelezaji wake utafanyikia kwenye Mahakama ya Mwanzo Kawe.

Haki ya Kukata Rufaa katika Mahakama inayotembea

Mhusika yeyote katika shauri asiyeridhika na uamuzi wa Mahakama inayotembea ana haki ya kukata rufaa katika Mahakama ya juu. Kwa upande wa Mahakama ya Mwanzo, mhusika anaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Wilaya kwa kufuata taratibu zilizopo. Kwa upande wa Mahakama ya Wilaya mhusika anaweza kukata rufaa katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Faida zitakazopatikana baada ya kuanzishwa kwa Mahakama inayotembea

Baadhi ya faida zitakazopatikana kutokana na Mahakama ya Tanzania kuanzisha Mahakama inayotembea ni pamoja na kusaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza au kuondoa kabisa mlundikano wa mashauri mahakamani. Mahakama inayotembea pia itasaidia kuwapunguzia gharama wananchi za kufika Mahakamani kufuatilia haki zao na kupitia Mahakama hii ustawi wa jamii utaimarika. Aidha, Mahakama hii itakuwa ni fursa pekee ya kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi kwa kuwa wananchi hawatatumia muda mrefu kufuatilia haki zao kwa kuwa Mahakama inayotembea uitarahisisha upatikanaji wa haki.

Maeneo yatakayohudumiwa na Mahakama inayotembea

Kwa kuanzia, huduma hii itatolewa katika mikoa ya Dar es salaam na Mwanza. Katika mkoa wa Dar es salaam, huduma ya Mahakama inayotembea itatolewa katika maeneo ya Bunju “A” (kwenye viwanja vya ofisi ya Serikali za mitaa), Kibamba (kwenye viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Wilaya Kinondoni), Chanika (pembeni ya kituo kipya cha Polisi Chanika) na Buza (eneo la kituo cha mabasi Buza).

Katika Mkoa wa Mwanza, huduma za Mahakama inayotembea zitatolewa katika maeneo ya Buhongwa (eneo la wazi karibu na kituo cha Polisi Buhongwa), Igoma (eneo la kuegesha Malori Igoma-Terminal Trucks ground) na Buswelu katika Viwanja vya Soko Buswelu.

Licha ya kuanzisha huduma ya Mahakama inayotembea kwa baadhi ya maeneo nchini, Mahakama ya Tanzania inao mpango la kutanua wigo wa utoaji wa huduma kwa njia ya magari maalum katika mikoa mingine hapo baadaye ili kuendelea kusogeza huduma za kimahakama karibu zaidi na wananchi na kurahisisha upatikanaji wa haki.


Rais azindua Mahakama inayotembea

Akizindua Mahakama inayotembea hivi karibuni, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli aliipongeza Mahakama ya Tanzania kwa kuanzisha huduma hii kwa kuwa itasaidia kutoa haki kwa wananchi wengi na kuitaka Mahakama kuongeza idadi ya magari hayo ili kufikia maeneo mengi zaidi nchini.

Akizungumza wakati wa sherehe za kilele cha wiki ya Sheria na Siku ya Sheria nchini, Mhe. Rais pia aliipongeza Benki ya Dunia kwa ufadhili wa ununuzi wa magari hayo ya Mahakama inayotembea.

“Nakupongeza sana Mhe. Jaji Mkuu pamoja na Watumishi wote wa Mahakama kwa ujumla kwa maboresho ya Mahakama yaliyofanyika na vilevile napongeza uanzishwaji wa huduma ya Mahakama inayotembea kwani itawasaidia wananchi kutatua migogoro mbalimbali” alisema Mhe. Dkt. Magufuli.

Hata hivyo, Mhe. Rais aliitaka Mahakama kuelekeza huduma hiyo katika kutatua matatizo ya wananchi hususani wanawake wajane ambao wanahangaika muda mrefu kufuatilia mirathi hatua ambayo wakati mwingine inawasababisha kukosa haki zao za msingi.

“Maombi yangu, huduma hii iwasaidie pia wanawake ambao wengi wanahangaika kwa muda mrefu kushughulikia mirathi, ikibidi liwepo gari maalum ambalo ikiwezekana awekwe Jaji/Hakimu mwanamke kwa ajili ya kuwasaidia wamama wajane kuhusu masuala ya mirathi,” alisisitiza Mhe. Rais.

Naye Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akizungumzia Mahakama inayotembea wakati wa siku ya Sheria nchini alisema Mahakama zinazotembea zitasaidia kusogeza huduma za mahakama karibu na wananchi hasa sehemu zisizo na Mahakama, kusikiliza kesi na kuzimaliza.

“Katika dhana hii mpya ya Mahakama inayotembea mahakama itahamishia shughuli zake katika chumba maalumu kilichotengenezwa ndani ya gari lakini kuna huduma zote muhimu kama ilivyo ofisi au “chambers” ya hakimu ambapo itasikiliza mashauri na kuyatolea maamuzi”, alisema Jaji Mkuu.

Alisema dhamira ya Mahakama baadaye ni kuwa na magari ya aina hii nchi nzima kwenye maeneo yasiyofikika kwa urahisi kwa mfano jamii za wafugaji na wavuvi ili kuwapunguzia wananchi wote kero. Mahakama hizi zitakuwa chini ya mamlaka ya Mahakama husika za Wilaya na Mwanzo na Mahakimu walioteuliwa kuzisimamia wamepatiwa mafunzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na namna ya kuhudumia wateja (customer care). Aliongeza kuwa Mahakama inayotembea inatarajiwa kuwa kimbilio la wananchi wengi kwa huduma nzuri zitakazotolewa katika mahakama hizo.
RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. JOHN MAGUFULI AKIZINDUA MAHAKAMA INAYOTEMBEA WAKATI WA KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI NA SIKU YA SHERIA. WA TATU KUSHOTO NI JAJI MKUU WA TANZANIA MHE. PROF. IBRAHIM HAMIS JUMA NA KULIA KWA RAIS NI SWPIKA WA BUNGE LA TANZANIA MHE. jOB nDUGAI AKIFUATIWA NA ALIYEKUWA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA MHE. PROF. PALAMAGAMBA KABUDI. KUTOKA KUSHOTO NI MWAKILISHI WA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AMBAYE NI MKUU WA WILAYA YA TEMEKE, SOPHIA MJEMA AKIFUATIWA NA MUWAKILISHI MKAZI WA BENKI YA DUNIA NCHINI BIBI BELLA BIRD.
 MUONEKANO WA NDANI GARI LITAKALOTOA HUDUMA ZA MAHAKAMA INAYOTEMBEA INAYOTARAJIWA KUANZA KUFANYA KAZI HIVI KARIBUNI.  

MILVIK, TIGO PAMOJA NA RESOLUTION INSURANCE KUWAPATIA WATANZANIA BIMA YA AFYA KWA BEI NAFUU

$
0
0
Wa kwanza kushoto ni Melchizedek Nyau - Meneja Uendeshaji Resolution Insurance, Hussein Sayed - Mkuu wa Huduma za Kifedha wa Tigo, Zamaradi Mketema - Balozi wa Milvik Tanzania 

Tigo kwa ushirikiano na Milvik Tanzania na Resolution Insurance tumeungana na mwanahabari mashuhuri na mama wa watoto watatu, Zamaradi Mketema, kuzindua Bima mkononi ya kulazwa na watoto kwa wateja wa Tigo pesa. Huduma hii inawapatia watumiaji wa Tigo Pesa bima nafuu inayowalinda wao na watoto hadi watano kwa sh.750 kwa mwezi kwa kila mtoto.

Wateja wa Tigo pesa wenye umri wa miaka 18 - 64 kwa sasa wanaweza kuongeza watoto wao wenye umri kuanzia Mwaka 1 hadi miaka 17, kwenye Bima Mkononi yao ya kulazwa na mtumiaji atapokea Sh. 40,000 kama fidia kwa kila usiku atakaolazwa hospitali.

Huduma hii nafuu sana kwa Sh. 1,500 tu kwa mwezi kwa mteja mwenyewe na ongezeko la Sh 750 kwa kila mtoto. Malipo moja kwa moja kwenye akaunti ya Tigo pesa ya mtumiaji kila mwezi hivyo hii kumpunguzia mtuamiaji mzigo wa kufikiria kufanya malipo. Malipo ya fidia hutumwa moja kwa moja kwenye akaunti Tigo pesa ya mtumiaji.

Berengere Lavisse, Meneja Mkuu wa Milvik: "Toka tumezindua huduma ya kulazwa mwaka 2016, wateja wetu wamekuwa wakituomba kuboresha huduma zetu na kujumuishawatoto kwa bei nafuu; tumesikiliza mahitaji ya wateja wetu na kwa kushirikiana na wadau wetu pamoja na Mamlaka ya udhibiti wa bima Tanzania (TIRA), tumefanyia kazi kuleta huduma hii ya bima ya kulazwa kwa watoto. shirikiano wetu na Tigo unatuwezesha kuwafikia watu wengi zaidi hususani kwa watumiaji wa Tigo, ushirikiano huu ni muhimu kwetu katika kulinda hatima za familia nyingi zaidi. . Tuna furaha kubwa kuwa na ushirikiano na Zamaradi kama balozi wa huduma zetu.Kama mama mchapakazi anaelewa umuhimu na uhitaji wa kuwalinda uwapendao”.

Zamaradi Mketema, Balozi wa Bima Mkononi alikuwa na haya ya kusema, "Kama mama ninawajali watoto wangu, natamani kina mama na kina baba wote Tanzania wapata uwezo wa kutumia bima rahisi na nafuu zinazolinda familia zao na hiki ndicho Bima Mkononi ya kulazwa na watoto inachokitoa. Kuwa na watoto wadogo watatu inanifanya niwe na majukumu muda wote, kwahiyo kuwa na huduma rahisi kujisajili, rahisi kulipia na pia rahisi kufanya madai, ni fursa muhimu sana kwangu”.

Hussein Sayed, Afisa Mkuu - Huduma za Kifedha Tigo: "Kama sehemu ya jitihada zetu za dhati kabisa katika kuwaelewa wateja na kufanya maboresho yanayoendana na mahitaji yao kijamii, tumeungana na IDEO.org, katika utafiti wa jinsi tunavyoweza kuongeza ushiriki wa jamii katika huduma za kifedha na hususani kwa wanawake na kaya, matokeo ya utafiti huu yanaendana na mfumo ambao umeundwa na timu ya Milvik...Hivyo , ninafurahi kutangaza maboresho ya huduma za Bima Mkononi kwa wateja wetu wapendwa, inayotolewa kwa viwango nafuu na ambayo ni rahisi na ya haraka kujiunga. Tigo imejidhatiti katika mpango mkakati kuongeza ushiriki katika huduma za kifedha, ambapobima ni kiungo muhimu katika kufanikisha hilo. Tunajivunia kusema kuwa tumechukua hatua nyingine mbele zaidi, si tu kulinda maisha ya wateja wetu, bali pia maisha ya wale wawapendao”.

Melchizedek Nyau, Meneja uendeshaji Resolution Insurance: "Kama wadhamini wa bima hii, lengo letu ni kulinda kila chenye thamani kwa wateja wetu kwa kuhakikisha tunatoa huduma zenye tija, , za kuaminika, sahihi, na zenye uwazi. Toka kuanzishewa kwa bima ya kulazwa mwaka 2016 tumekuwa tukitimiza ahadi yetu ya kulipa madai kwa haraka ndani ya siku 3 hadi siku 5”.

Usambaaji wa bima nchini Tanzania ni mdogo ikiwa ni asilimia 1 tu ya Watanzania wenye huduma za bima, na bima ikichangia asilimia 0.9 tu kwenye kipato cha ndani cha taifa. Milvik, Tigo na Resolution Insurance tumejidhatiti katika kuchangia kwenye mfumo wa kuingiza fedha wa taifa (Tanzania National Financial Inclusion Framework (NFIF 2018-2022) ili kutoa huduma za kifedha zinazowajali wateja na kukidhi mahitaji yao ili kuboresha hali ya maisha yao ,pamoja na kuendelea kuwaelimisha watu wenye kipato cha chini jinsi bima inavyofanya kazi, sambamba na sera ya taifa ya elimu juu ya maswala ya bima (NATIONAL INSURANCE EDUCATION STRATEGY (2016 - 2020). Huduma za bima za Bima Mkononi ni rahisi - zinazokidhi mahitaji ya watu wenye kipato cha chini ambayo bima nyingine hazijaweza kukidhi mahitaji hayo, yaani kutoa huduma zenye vigezo na masharti rahisi ambayo ni rahisi kueleweka.

Kujiunga na Bima Mkononi ni rahisi. Wateja wanaweza kujisajili kupitia simu zao za mkononi kwa kutumia USSD kwenda nambari *148*15# au kupitia mawakala wa huduma kutoka Milvik kwa kupiga simu ya bure kwenda nambari 0659071001. Madai halali yanaweza kutumwakupitia whatsapp, barua pepe au kupelekwa kwenye tawi la Tigo kwa kutuma fomu ya taarifa fupi ya kuruhusiwa kutoka hospitalini na cheti cha kuzaliwa, na madai yatalipwa ndani ya siku tatu za kazi baada ya kupokea nyaraka halali.

MWENYEKITI UVCCM MKOA WA TANGA AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA KATIBU HAMASA KATA YA CHUMBAGENI JIJINI TANGA

$
0
0
 MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoani Tanga Omari Mwanga kulia akiwa kwenye msiba huo katikati ni Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo kushoto ni Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed
 MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoani Tanga Omari Mwanga kulia akiwa kwenye msiba huo katikati ni Katibu wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo kushoto ni Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed
 Sehemu ya Viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga wakiwa msibani leo
Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed akifuatilia matukio mbalimbali kwenye msiba ambapo aliyefariki alikuwa akifanya naye kazi

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoani Tanga Omari Mwanga leo amewaongoza viongozi mbalimbali wa jumuiya kwenye mazishi ya aliyekuwa Katibu wa Hamasa na Chipukizi (UVCCM) Kata ya Chumbageni Jijini Tanga Marry Dominic Dawa yaliyofanyika Bombani Muheza.

Kabla ya mwili huo kusafirishwa kuelekea wilayani Muheza aliagwa eneo la Kange Kasera Jijini Tanga ambapo Jumuiya ya Umoja wa Vijana mkoa wa Tanga walitoa salamu zao wakati wa halfa hiyo

Akizungumza wakati kuagwa mwili huo Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Tanga Mwanga aliwapa pole wafiwa na kuwataka kuwa wavumilivu kwenye kipindi hicho kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.

Alisema wao kama Jumuiya wapo pamoja na familia kwenye kipindi hicho kigumu huku wakimuelezea namna katibu huyo alivyokuwa mchapakazi na hodari katika utendaji wake.

Kwa kweli hapa tumepata pigo kubwa hasa ukizungatia Marry alikuwa kiongozi hodari na shupavu kwenye kuwajibika kwenye nafasi aliyokuwepo huku wakieleza mchango wake utaendelea kukumbukwa.

Hata hivyo aliwataka viongozi waliobakia kuiga mazuri yaliyofanywa na kiongozi huyo katika kuhakikisha Jumuiya hiyo inapata mafanikio makubwa .

Msiba huo ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga Zawadi Nyambo,Katibu wa (UVCCM) wilaya ya Tanga Fahad Siraji,Katibu Hamasa wilaya ya Tanga (UVCCM) Kipanga Juma,Mjumbe wa Baraza Taifa (UVCCM) Mbaruku Asilia.


Imetolewa na Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM Mkoa wa Tanga Katibu wa Hamasa na Chipukizi (UVCCM) Mkoa wa Tanga 

WAZIRI MKUU KUONGOZA MAZISHI YA DK. MENGI KESHO

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa anatarajiwa kuongoza mazishi ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Mengi yatakayofanyika kesho Mei 9, 2019 kijijini kwake, Kisereni, Machame, wilayani Hai, Kilimanjaro.

Waziri Mkuu anatarajiwa kuongoza mazishi hayo kwa niaba ya Serikali. Ibada ya mazishi itafanyika kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) la Kisereni, Machame.

Mwili wa Dkt. Mengi ambaye alifariki dunia alfajiri ya Mei 2, mwaka huu akiwa kwenye matibabu huko Dubai, Falme za Kiarabu, umewasili Moshi leo ukitokea Dar es Salaam na kupokekelewa na mamia ya wananchi waliojipanga barabarani.

Jana, (Jumanne, Mei 6, 2019) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa Serikali, waliongoza maelfu ya wananchi kutoa heshima za mwisho wakati wa shughuli za kuaga mwili huo katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.

Hadi mauti yanamfika, Dkt. Mengi alikuwa Mwenyekiti wa Wamiliki wa Vyombo Vya Habari Tanzania (Chairman of the Media Owners Association of Tanzania - MOAT). Pia aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (Tanzania Private Sector Foundation – TPSF).

Baadhi ya nyandhifa ambazo Dkt. Mengi aliwahi kushika ni pamoja na Kamishna wa kamati inayoshughulikia mishahara (Salary Review Commission); Mwenyekiti wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi Tanzania (NBAA); Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mazingira Tanzania (NEMC); Mwenyekiti wa vyombo vya habari vya Jumuia ya Madola Tanzania (Chairman of the Tanzania Chapter-Commonwealth Press Union-CPU); Kamishna wa TACAIDS na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Afrika Mashariki.

Viewing all 46370 articles
Browse latest View live




Latest Images