Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU AZINDUA MAABARA YA NYUKLIA

$
0
0

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama vifaa vya kisasa katika maabara ya nyuklia
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama vifaa vya kisasa katika maabara ya nyuklia
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema Akizungumza
Mbunge wa Viti Maalumu Catherine Magige akizungumza

Wananchi wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa maabara
Picha ya pamoja ya Mgeni rasmi na kamati ya maandalizi
picha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa pamoja na Wafanyakazi wa Tume ya mionzi.
picha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa pamoja naViongozi wa Mkoa wa Arusha

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama maabara ya Nyulia iliyozinduliwa katika tume ya Mionzi jijini Arusha.



Na Vero Ignatus, Arusha.

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amezindua maabara ya kisasa ya nyuklia iliko katika Time ya Mionzi Tanzania jijini Arusha ambapo maabara hiyo itasaidia kutumia nyuklia kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa.

Majaliwa amesema kuwa maabara hiyo ni muhimu katika kuhakikisha kuwa hakuna madhara yanayotokana na matumizi ya mionzi kwa kuwa na vifaa na wataalamu waliobobea katika mionzi.

Aidha amesema kuwa Tanzania ina hazina ya tank 58.2 za nyuklia katika maeneo mbalimbali ikiwemo Namtumbo,Nachingwea,Minjingu na Songea Vijijini."Maabara hii ya kisasa itasaidia kuongeza mchango wa nyuklia kwenye ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa" Alisema Majaliwa

Naibu Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Dr.Faustine Ndugulile ambaye alimuwakilisha Waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia amesema kuwa maabara hiyo ya kisasa barani Afrika imejengwa kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Umoja wa nchi za Ulaya na serikali ya Tanzania .

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema maabara hiyo itawawezesha Wataalu kudhibiti mionzi katika maeneo mbalimbali hususan viwanja vya ndege.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Atomiki Najat Mohammed ametaja majina ya Wafanyakazi bora ambao wamedhibiti vyanzo vya mionzi katika bidhaa na maeneo ya mipakani licha ya kushawishiwa na rushwa

RAIS DKT. MAGUFULI AENDELEA NA ZIARA YAKE RUNGWE NA KYELA MKOANI MBEYA

$
0
0

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimia wananchi wa Busokelo wilayani Rungwe katika mkoa  wa Mbeya wakati sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya

lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa Kilometa 81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika. Pamoja naye ni Mbunge na Waziri Mstaafu Profesa Mark Mwandosya na mkewe Mama Lucy Mwandosya.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Busokelo wilayani Rungwe katika mkoa wa Mbeya wakati sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya

lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa Kilometa 81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika. Pamoja naye ni Mbunge na Waziri Mstaafu Profesa Mark Mwandosya na mkewe Mama Lucy Mwandosya na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Albert Chalamila (kulia).
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisindikizwa na Mbunge na Waziri Mstaafu Profesa Mark Mwandosya na mkewe Mama Lucy Mwandosy baada ya sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa Kilometa 81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika.
.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa Kilometa
81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaga wananchi  baada ya sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa Kilometa
81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi  eneo la Suma wakati akielekea kuuweka jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Katumba-Busokelo-Tukuyu yenye urefu wa

Kilometa 81.3 ambapo kilometa 10 kati yake ujenzi umeshakamilika.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifunua pazia akisaidiana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Albert Chalamila  kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya lami ya
Kikusya-Ipinda-Matema yenye urefu wa Kilometa 39.1 ambayo itagharimu shilingi Bilioni 65
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Albert Chalamila  baada ya kuweka jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Kikusya-Ipinda-Matema
yenye urefu wa Kilometa 39.1 ambayo itagharimu shilingi Bilioni 65
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi wengine akikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Kikusya-Ipinda-Matema yenye urefu wa Kilometa 39.1 ambayo itagharimu shilingi Bilioni 65.
.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na  wananchi na kusikiliza kero zao eneo la Tenende, Kyela, baada ya kuweka jiwe la msingi wa barabara ya lami ya Kikusya-Ipinda-Matema yenye urefu wa Kilometa 39.1 ambayo itagharimu shilingi Bilioni 65.


Vodacom Tanzania yazindua duka jipya kwa wateja wake ndani ya Aura mall jijini Dar

$
0
0
 Mkuu wa Mauzo Kanda ya Dar na Pwani, George Lugata  (kushoto) na bwana  Mirza Ngoshani (mwenye Tshirt ya blue)   wakikata utepe kuzindua duka jipya la Vodacom katika jengo la Aura mall hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Mpaka sasa, kampuni ya Vodacom ina maduka 100 na inaendelea kupanua upatikanaji wa huduma ili kuwawezesha wateja wake kupata huduma kirahisi zaidi. Wengine pichani ni watoa huduma wa duka hilo duka hilo jipya litakalotoa huduma kila siku kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa tatu usiku. 
Mkuu wa Mauzo wa Vodacom Kanda ya Dar na Pwani, George Lugata (wa pili kulia) akizungumza na wageni na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania baada ya uzinduzi wa duka jipya la kampuni hiyo lililopo katika jengo la Aura mall jijini Dar es Salaam. Kampuni ya Vodacom ina maduka 100 na inaendelea kupanua upatikanaji wa huduma ili kuwawezesha wateja wake kupata huduma kirahisi zaidi. Wengine pichani ni watoa huduma wa duka hilo duka hilo jipya litakalotoa huduma kila siku kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa tatu usiku.    

WCF YASHINDA TUZO KATIKA MASWALA YA AFYA NA USALAMA MAHALA PA KAZI, KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI DUNIANI, JIJINI MBEYA

$
0
0

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi Tuzo na Cheti Bw. Masha Mshomba Mkurugenzi Mkuu wa WCF. Mfuko umekuwa Mshindi katika masuala ya afya na usalama kazini baina ya Taasisi za Bima na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Tuzo hiyo imetolewa katika Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani, 2019.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi Cheti cha ushiriki wa Siku ya Afya na Usalama Duniani Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini Dkt. Abdulssalaam Omary jijini Mbeya.
  Tuzo na Cheti katika masuala ya afya na usalama kazini baina ya Taasisi za Bima na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
Tuzo hiyo imetolewa katika Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani, 2019.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama(wa kwanza kushoto) akipata maelezo ya Mfuko kutoka kwa Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulssalaam Omary (wa pili kulia) alipo tembelea banda hilo. Wa tatu kushoto ni Mwakilishi wa ILO Afrika  Bw. Jealous G. Chirove na Naibu  waziri  Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Anthony Mavunde (katikati kulia)
Mkurugenzi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Masha Mshomba (katikati) akifurahia pamoja na wafanyakazi wa Mfuko baada ya Mfuko kuwa Mshindi katika masuala ya afya na usalama kazini baina ya Taasisi za Bima na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii
Mkurugenzi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Masha Mshomba (wa pili kushoto) pamoja na wafanyakazi wengine wa WCF mara baada ya kupata Tuzo na Cheti cha ushindi wa huduma bora za Bima.
Wafanyakazi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) wakifurahia baada ya kupata wakifurahia pamoja na wafanyakazi wa Mfuko baada ya Mfuko kuwa Mshindi katika masuala ya afya na usalama kazini baina ya Taasisi za Bima na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu Wenye Ulemavu), Stella Ikupa (aliyeketi) akipata maelezo ya mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kutoka kwa Mkurugenzi wa huduma za Tiba na Tathmini Dkt. Abdulssalaam Omary (wa pili kulia) walipo tembelea banda hilo
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini Dkt. Abdulssalaam Omary akimpa maelekezo Dkt. Kiva Mvungi kutoka Geita Gold Mine kuhusiana na viwango vya ulemavu kwa mujibu wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi
Afisa Matekelezo Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Amina Likungwala akitoa zawadi kwa wadau mbali mbali waliotembelea banda la WCF wakati wa maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Duniani, 2019 yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya
Wadau mbalimbali waliotembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) wakipata maelezo juu ya mafao na shughuli za Mfuko wakati wa maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Duniani, 2019 yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya
Afisa afya na usalama mahali pa kazi  kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Bw. Robert  Duguza akitoa maelezo juu ya huduma na mafao yatolewayo na WCF kwa mdau aliyetembelea banda la Mfuko huo
Watu mbalimbali wakiendelea kutembela katika Banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)  wakati wa maadhimisho ya siku ya usalama na afya Duniani ambapo kitaifa imefanyia mkoani Mbeya.
Afisa Mwandamizi, Afya na Usalama Mahali pa Kazi  kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Bi. Tumaini Kyando akitoa maelezo ya Mafao yanayotolewa na WCF kwa wageni na wadau waliotembelea banda la Mfuko huo
Meneja Tathmini, Vihatarishi  wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bi. Naanjela Msangi akifafanua umuhimu wa kufanya tathimini ya vihatarishi  katika maeneo ya kazi kwa wadau waliotembelea banda la Mfuko wakati wa maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Duniani, 2019 yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya
Afisa Mwandamizi wa Mahusiano kwa Umma kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Sebera Fulgence akimkabidhi Kava la Gurudumu  mdau aliyetembelea Banda la WCF
 Afisa Matekelezo Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Amina Likungwala akitoa zawadi kwa wadau mbali mbali waliotembelea banda la WCF
Baadhi  wa WCF wakiwa katika banda lao 
Kikundi cha ngoma kikitumbuiza mbele ya Banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Duniani, 2019 yaliyofanyika kitaifa jijini Mbeya



Prof. Kabudi ashiriki maadhimisho ya siku ya Taifa la Uholanzi

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akihutubia kwenye kuadhimisha siku ya Taifa la Uholanzi, kulia ni Balozi wa Uholanzi nchini Mhe. Jeroen Verheul. 

Prof. Palamagamba ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alitumia fursa hiyo kuelezea mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Uholanzi katika sekta mbalimbali zikiwemo Kilimo, Elimu, Biashara na Ujenzi wa Miundombinu. Pia alilipongeza taifa hilo kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania kwenye kuleta maendeleo nchini.

Aidha, Prof. Kabudi alieleza kuwa Tanzania inaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia wawekezaji wa Uholanzi kuja kuwekeza nchini kwa wingi, ambapo alieleza kuwa mpaka sasa Uholanzi ni miongoni mwa nchi 10 zinazoongza kwa uwekezaji nchni, ambapo imewekeza jumla ya miradi 159 Tanzania.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Makamu wa Rais Mstaafu Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Mabalozi mbalimbali wanao ziwakilisha nchi zao hapa pamoja na wawakilishi wa mashirika ya Kimataifa. 
Prof. Palamagamba John Kabudi akiendelea kuhutubia kwenye maadhimisho hayo. 
Sehemu ya Mabalozi wanaoziwakilisha nchni zao hapa pamoja na wageni mbalimbali wakimsikiliza kwa makini Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani) alipokuwa akihutubia. 
Juu na chini ni sehemu nyingine ya wageni waalikwa aliohudhuria maadhimisho hayo wakisikiliza hotuba hiyo ya Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Hayupo pichani). 
Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb.) akigonganisha glasi na Mhe. Balozi Jeroen Verheul kwa kuwatakia viongozi wa Tanzania na Uholanzi Nguvu na Afya Njema. 
Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb.) akigonganisha glasi na Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal. 
Prof. Palamagamba John Kabudi akizungumza na Mabalozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo. 
Sehemu Nyingine ya wageni waalikwa wakisalimiana na kubadilishana mawazo wakati wa maadhimisho hayo yakiendelea. 
Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo.

Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje washiriki maadhimisho ya Mei Mosi kwa kishindo jijini Dodoma

$
0
0
Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (katikati) na viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (kushoto) wakiwa wamesimama kuwasalimu Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) walipopita mbele ya jukwaa kuu wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma tarehe 1 Mei 2019. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka 2019 ni "Tanzania ya uchumi wa Kati inawezekana, wakati wa mishahara na maslahi bora ya wafanyakazi ni sasa".
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakipita mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) kwa shangwe na furaha huku wakiwa wameinua juu bango lao wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (Mei Mosi) 
Sehemu ya wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho hayo 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na bango la Wizara wakati wa maadhimisho ya mei Mosi jijini Dodoma. 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho ya Mei Mosi jijini Dodoma 
Ilikuwa ni shangwe na furaha kwa Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuadhimisha siku yao ya wafanyakazi inayoadhimishwa duniani kote tarehe 1 Mei kila mwaka 
Wafanyakazi waWizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa na ari katika kuadhimisha siku yao 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakijumuika na wenzao duniani kote kuadhimisha Mei Mosi 
Sehemu nyingine ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 
Juu na chini ni umati wa Wafanyakazi kutoka Wizara, Sekta na Taasisi mbalimbali wakiadhimisha siku ya wafanyakazi duniani 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mabo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa jukwaani wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 
Sehemu nyingine ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa uwanjani wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walishiriki kwa wingi kuadhimisha siku yao 
Sehemu nyingine ya wafanyakazi hao wakiwa kwenye maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma 
Ni nyuso za tabasamu kama zinavyoonekana kwa Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki waliposhiriki kikamilifu maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 
Watoto hawakuachwa nyuma na wazazi wao ambao ni Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuja kuadhimisha siku ya mfanyakazi duniani kama inavyoonekana pichani 
Juu na chini ni sehemu ya Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiungana na wafanyakazi wengine kuimba wimbo wa mshikamano "Solidarity Forever" kama wanavyoonekana pichani 
Picha ya pamoja

WANANCHI WA BUSI, MAUNO AMBAO HAWAJAJENGA MAENEO YAO KUPATA UMEME

$
0
0
Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani,akizungumza na baraza la madiwani wa Kondoa kabla ya kuanza ziara ya kuwasha umeme katika kijiji cha Mauno pamoja kituo cha Afya cha Busi mkoani Dodoma
 
Sehemu ya madiwani wakimsikiliza Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani (hayupo pichani) wakati akizungumza nao katika kikao hicho

Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani,akizungumza na wananchi wa Kinyasi alipfanya ziara ya kuwasha umeme kijiji cha Mauno pamoja na Kituo cha Afya cha Busi wilayani Kondoa
Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani,akiwaonyseha wananchi kifaa cha kuunganishia umeme
Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani akiwakabidhi wananchi kifaa cha kuunganishiwa umeme katika kitongoji cha Kinyasi.
Waziri wa Nishati,Merdard Kalemani,akimueleza jambo mbunge wa Kondoa ambaye pia ni Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji kabla ya kuwasha umeme katika kituo cha Afya cha Busi
Waziri wa Nishati,Dk.Merdard Kalemani,akisisitiza jambo kwa wananchi wa kijiji cha Busi kabla ya kuwasha umeme katika kituo cha Afya
Baadhi ya wananchi wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nishati,Dk.Merdard Kalemani alipokuwa anazungumza nao kabla ya kuwawashia umeme katika kituo cha Afya cha Busi.
Waziri wa Nishati,Dk.Merdard Kalemani,akiwasha umeme katika kituo cha Afya cha Busi wilaya ya Kondoa.Picha Zote na Alex Sonna-Fullshangwe blog



Na.Alex Sonna,Kondoa

WAZIRI wa Nishati Dk. Medard Kalemani amewataka wakazi wa vijiji vya Mauno na Busi wilayani Kondoa ambao bado hawajajenga kwenye maeneo yao kuweke miti ili wasogezewe huduma ya umeme kwa haraka.

Pamoja na hayo, amemwagiza Meneja wa shirika la umeme (Tanesco) pamoja na mkandarasi kuhakikisha wanamaliza kusambaza huduma ya umeme katika vijiji vyote vilivyosalia wilayani Kondoa ndani ya wiki moja.

Waziri Kalemani ametoa agizo hilo baada ya kufanya ziara ya kuwasha umeme katika Kijiji cha Mauno pamoja na kituo cha Afya cha Busi huku akiwa ameongozana na Mbunge wa jimbo la Kondoa ambaye ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji. 

Waziri Kalemani amewataka wananchi hao kuwa, kuanzia sasa uunganishwaji wa umeme ni sh. 27,000 tu, uwe wa Tanesco au Rea huku akiahidi kupiga mnada wa kuku wa mkazi ambaye atashindwa kulipia kiasi hicho kwa ajili ya kuunganishiwa huduma hiyo.

Kalemani amefafanua kuwa Tanesco kupitia mkandarasi hawana sababu ya kusuasua kuwasha umeme katika maeneo hayo kwa kuwa nguzo na nyaya wanazo za kutosha,Aidha Waziri Kalemani ameahidi kurejea kwenye kata hiyo mwezi ujao kufuatilia agizo lake.

Mbunge wa Kondoa,Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji,aliwataka wananchi kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za serikali za kuwapelekea huduma ya umeme kwa kutumia fursa hiyo kuingiza umeme katika nyumba zao.

Pia ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano kwa jitihada kubwa inazozifanya kupeleka maendeleo kwa wananchi na kujali wananchi wanyonge na wenye hali ya chini.

Mmoja wa wakazi kijijini cha Busi Bw.Nuru Bi Mdanga akizungumza baada ya kuwashiwa umeme ameelezea furaha yake ya kupunguzwa kwa gharama ya uunganishwaji wa huduma hiyo pasipokujali unatokea Rea au Tanesco.

RC SHIGELLA AWAPIGA MARUFUKU TABIA YA WAKUU WA WILAYA ZA MKOA HUO KUWAWEKA NDANI WAFANYAKAZI

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani (MEI MOSI) ambapo kimkoa ilifanyika kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani mjini Tanga kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Mhandisi Zena Saidi 
MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) happines Sima akizungumza wakati wa maadhimisho hayo leo 
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akikabidhi zawadi ya TV kwa wafanyakazi mbalimbali
Sehemu ya watumishi wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa Martine Shigella 
Sehemu ya wafanyakazi na wananchi wakiwa kwenye maadhimisho hayo leo
Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kushoto ni Meneja wa Mfuko huo mkoa wa Tanga Happines Sima akiweka sawa mwamvuli wakipita mbele ya mgeni rasmi 


MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella amewapiga marufuku wakuu wa wilaya za mkoa huo kukamatwa kwa watumishi na kuwekwa ndani wafanyakazi kwa misingi isiyofuata sheria na taratibu zilizopo nchini. 

Shigella aliyasema hayo leo wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambapo kimkoa iliadhimishwa kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani mjini Tanga ambapo alisema kama sio kosa ambalo linaweza kuhatarisha amani, linalohusisha na wizi, mauaji. 

Alisema badala yake watumie taratibu za kisheria wawafikisha kwenye mamlaka za waajiri wao waweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu sheria zilizopo ili kuweza kuwarekebisha kitabia. 

“Mfanyakazi anaweza akawa amechelewa lakini anaweza kuwa na sababu za msingi lakini haumsikilizi wala haufanyi hivyo unamuaaguza Mkuu wa wilaya (ODC) amkamate amweke ndani hii sio sawa acheni kutumia madaraka yenu vibaya”Alisema .

Alisema wakifanya hivyo watakuwa wamejenga misingi ya utawala bora, haki za binadamu ikiwemo utamaduni na utaratribu wa kuheshimia jambo ambalo litasaidia kuwawezesha kupiga hatua ya kubwa za kimaendeleo kwao na jamii zinazowazunguka. 

“RPC wafikishie wakuu wa Polisi wilaya za mkoa huu kwamba kuanzia sasa wa wafanyakazi kwenye mkoa wa Tanga kama sio la kuhatarisha amani,wizi ,mauaji ni marufuku kuwekwa ndani wafanyakazi kwa misingi isiyofuata taratibu “Alisema . Hata hivyo aliwataka lazima waweze kuweka mazingira mazuri ya kuwajenga wafanyakazi wao ili waweze kuona kosa walilofanya waweze kujutia na kuweza kujirekebisha badala ya kutumia mamlaka waliyonayo vibaya.

WAFANYAKAZI SHIRIKA LA POSTA WALIVYOSHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI (MEI MOSI) KITAIFA MBEYA NA DAR ES SALAAM 2019

$
0
0

Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, akiwahutubia wafanyakazi katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda (wa pili kushoto), akiwa pamoja na Wakuu wa Wilaya (kulia) na viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), wakiimba wimbo wa mshikamano, katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam leo.
 Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania wakisakata rumba katika gari lao la matangazo kabla ya kuingia katika viwanja vya uhuru kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta wakiwa nje ya uwanja wa Uhuru tayari kuingia uwanjani kwa maandamano katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi, ndani ya Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta wakiwa wenye furaha huku wamebeba bango lenye ujumbe maalum wakipita mbele ya mgeni rasmi,Jijini Dar es salaam.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakipita mbele ya mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, na bango lao lenye ujumbe maalum.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakimpungia mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, wakati wakipita na bango lao.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakiwa na furaha huku wamebeba miavuli yao, wakipita kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakifurahi wakiwa kwenye jukwaa kumsikiliza mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda.
Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania wakipita na Pikipiki zao za kutolea huduma mbalimbali za Shirika mbele ya mgeni Rasmi.
Magari ya kusafirisha vifurushi na kutoa huduma zingine za Shirika la Posta Tanzania yakipita kwa msafara mbele ya mgeni katika viwanja vya Uhuru, jijini Dar es Salaam. 
Meneja Rasilimali watu, Miriam Mbaga kwa niaba ya Postamasta Mkuu, akimkabidhi cheti mfanyakazi hodari kitaifa wa Shirika la Posta, Madaraka Simba (kulia), katika maadhimisho ya Mei Dei, mkoani Mbeya.
Meneja Rasilimali watu, Miriam Mbaga kwa niaba ya Postamasta Mkuu, akimkabidhi cheti mfanyakazi hodari wa Mkoa wa Mbeya, Godwin Davis (kulia), katika maadhimisho ya Mei Dei, mkoani humo.
Mwenyekiti (TEWUTA) Makao Makuu Shirika la Posta, Aneth Mdamu, katika hafla fupi ya kumpongeza mfanyakazi bora kitaifa wa Shirika la Posta, Madaraka Simba.
Meneja wa Shirika la Posta mkoani Mbeya, Abdon Mahimbo (katikati mwenye koti), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi walioshiriki sherehe za Mei Dei, jijini humo.

BREAKING NEWZZZZ: Dkt Reginald Mengi afariki Dunia

$
0
0

Taaarifa iliyotufikia kwa masikitiko makubwa katika chumba chetu cha habari, Globu ya Jamii zinazeleza kuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP , Dkt Reginald Abraham Mengi amefarikia Dunia akiwa Dubai, U.A.E, usiku wa kuamkia leo. 

Kufuatia msiba huo Mkubwa kwa Taifa,tutaedeleea kuwaletea taarifa kamili kadiri ya zitakavyokuwa zikiingia. 

Michuzi Media Group inatoa pole kwa ndugu zetu wa IPP, Familia ya Marehemu na wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja nyingine.

Mungu ailaze roho ya Marehemu , mahali pema, peponi -AMEN

MAGAZETI YA LEO AL HAMIS APRIL 3,2019

WAAJIRI WAASWA KUTOWANYANYASA WAFANYAKAZI

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Monduli Idd Kimanta akihutubia siku ya wafanyakazi duniani mkoani Arusha,ambapo alimuwakilisha mkuu wa mkoa Mrisho Gambo.
Maandamano ya wafanyakazi kama yanavyoonekana pichani Jijiji Arusha.
Maandamano yakiendelea kuelekea katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid Karume Jijiji Arusha.




Na Vero Ignatus,Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Kimanta amekenea vikali tabia ya baadhi ya Waajiri wakorofi wanaowanyanyasa Wafanyakazi wao na kuwataka Viongozi wa vyama vya Wafanyakazi kuwachukulia hatua mapema pale watakapobainika.

Amesema hayo wakati akitubia katika Siku ya Wafanyakazi mkoani Arusha akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambapo Mrisho Gambo ambapo amewataka waajiri wajiepushe na vitendo vya unyanyasaji kwani sheria itafuata mkondo wake.

"Hatutamfumbia macho baadhi ya waajiri wakorofi wanaowanyanyasa wafanyakazi wao vyama vyavwafanyakazi fanyeni jitihada kuwabaini ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.alisema Kimanta.''

Mhe.Kimanta amewataka Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutatua kero za wafanyakazi badala ya kusubiri siku ya wafanyakazi na kutoa kero zao.

Nae Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya Wafanyakazi mkoani Arusha (TUCTA) Lota Laizer ameiomba serikali itoe nyongeza ya mishahara pamoja na ongezeko la asilimia la 1 la kila mwaka kama ilivyo matakwa ya sheria.

Aidha Laizer amewataka Wafanyakazi kuwa viongozi wa kisiasa wanatekeleza majukumu yao bila kukiuka sheria za wafanyakazi na kutumia lugha za kuwadhalilisha wafanyakazi.

Dkt. Ndumbaro akutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), nchini leo tarehe 1 Mei, 2019, katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es salaam. Mazungumzo hayo yamejikita katika kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na EU hususan katika nyanja za elimu na udhibiti wa biashara haramu ya dawa za kulevya. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.), akifafanua jambo wakati wa mazungumzo hayo. 
Kaimu Balozi Stuart akielezea jambo wakati wa mazungumzo hayo. 
Afisa Mambo ya Nje wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Albert Philipo akifuatilia mazungumzo hayo. 
Juu na chini mazungumzo yakiendelea. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb.) akiagana na Kaimu Balozi Charles Stuart mara baada ya mazungumzo.

NHIF TANGA YATUMIA MAADHIMISHO YA MEI MOSI KUWAKUMBUSHA WAAJIRI KUTOA MICHANGO YA WATUMISHI WAO

$
0
0

 MENEJA wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Happines Sima akizungumza wakati wa maadhimisho hayo leo
 Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kushoto ni Meneja wa Mfuko huo mkoa wa Tanga Happines Sima akiweka sawa mwamvuli wakipita mbele ya mgeni rasmi
 Watumishi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF)

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoani Tanga umetumia maadhimisho ya siku ya wafanyakazi dunia (Mei Mosi) kuwakumbusha waajiri kuhakikisha wanatoa michango kwa ajili ya watumishi wao.

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo yaliyofanyika kimkoa kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani mjini Tanga Meneja wa Mfuko huo Mkoani Tanga Happines Sima ambapo aliwataka waajiri kuzingatia suala hilo.

Alisema pia wametumia fursa hiyo kuweza kuhamasisha waajiri ambao watumishi wao ambao hawajajiunga na mfuko huo wajiunge ili waweze kunufaika na fursa zilizopo ndani ya mfuko huo.

“Lakini pia katika maadhimisho haya tumeweka banda letu ili kuweza kuwasikiliza wafanyakazi na kutatua kero zao mbalimbali zinazowakabili “Alisema Meneja huyo.

Hata hiyo aliwataka wazazi na walezi kuwaandikisha watoto wao kwenye mpango wa Toto Afya Kadi ili waweze kunufaika na huduma ya matibabu pindi wanapougua .

RC Mongella agoma kufungua mradi, rungu lamuangukia Mhandisi

$
0
0
Ukaguzi wa mradi wa maji wa kisima kirefu katika Kijiji cha Matela, Kata ya Isangijo wilayani Magu.
Ukaguzi wa mradi wa uzalishaji mali wa kikundi cha ESM Kangara ambapo kinajihusisha na ufugaji wa kuku, bata, njiwa, mbwa na paka.
 Ukaguzi wa Zahanati ya Bundilya wilayani Magu.
Jiwe la Msingi la Kituo cha Afya cha kwanza kujengwa wilayani Magu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella kwenye ukaguzi wa Kituo cha Afya Nyerere kilichopo Kata ya Kangara wilayani Magu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya anaendelea na ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Mwanza. Hapa Mongella akiwasili kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Lumnve iliyopo Kata ya Bujora wilayani Magu.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella kwenye ukaguzi wa kisima kirefu cha maji Isangijo ikiwa ni moja ya visima 16 vinavyochimbwa wilayani Magu ili kuondoa adha ya maji kwa wananchi.
Ukaguzi wa shamba la miti la Bahati Kwangu ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Busekwa, Kata ya Bujashi wilayani Magu lenye miti zaidi ya elfu 10 likiwa na ukubwa wa Hekali saba, lengo likiwa ni kuhifadhi mazingira pamoja na kitega uchumi kwa baadae.
Ukaguzi wa Zahanati ya Isangijo wilayani Magu.

Ukaguzi wa shughuli za kikundi cha wazalishaji mali cha "Meremeta Leather Group" wilayani Magu kinachojihusisha na utengenezaji wa bidhaa za ngozi ikiwemo viatu.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alitembelea Shule ya Musabi wilayani Magu ambapo kuna klabu ya TAKUKURU kwa wanafunzi wa shule ya msingi.
Wanafunzi wakafurahi kukutana na viongozi wao.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akaweka jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari Maligisu wilayani Kwimba.
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella alipotembelea Shule ya Sekondari Maligisu wilayani Kwimba.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella aligoma kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Kadashi wilayani Kwimba ambao ulianza mwaka 2013 ambapo aliagiza mradi huo ukamilike na kutoa maji katika magati yote 21 ifikapo Juni Mosi 2019.
Tazama BMG Online TV hapa chini

Kampuni ya Vodacom Tanzania yatoa mafunzo ya huduma ya kwanza kwa wafanyakazi wake

$
0
0
 Mkuu wa mauzo wa kanda ya Dar na Pwani wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, George Lugata (aliyelala chini) na Msimamizi wa mifumo ya kompyuta Emmanuel Lenduyayi (aliyesimama) akitoa mfano wa namna ya kumhudumia mtu aliyeanguka ghafla katika semina ya mafunzo ya huduma ya kwanza, yaliyofanyika makao makuu ya kampuni jijini Dar es Salaam karibuni jijini Dar es Salaam. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya uokoaji kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili kuwawezesha kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni hiyo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Aliyesimama kulia ni mwalimu wa mafunzo hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support Company.

Mfanyakazi wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc Neema Mgombelo, akionyesha mfano wa jinsi ya kumtambua mgonjwa aliezimia katika semina ya mafunzo ya huduma ya kwanza, iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya uokoaji kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili kuwawezesha kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni hiyo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Kushoto ni Mwalimu wa mafunzo hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support Company.

Kongamano la QNET huko Malayasia lahudhuriwa na wajasiriamali 13 000 wakiwemo waAfrika 2600

$
0
0
Kampuni maarufu ya kimataifa ya mauzo ya moja kwa moja yenye asili ya Asia, QNET imeendesha kongamano la siku tano la kimataifa ambalo linaleta pamoja takribani wajasiriamali 13,000 kutoka maeneo mbalimbali duniani katika kisiwa cha Penang, Malaysia Takribani wajasiriamali wa kiafrika wenye shauku wapatao 2600  walishiriki katika kongamano la mwaka huu.

Kongamano ambalo hufanywa mara mbili kwa mwaka la (V-Convention) ni tukio la kipekee ambalo huleta pamoja wateja na wasambazaji wa QNET kutoka maeneo mbalimbali duniani, washirika wake wa kibiashara, na pia maofisa wa serikali kuja kujionea bidhaa na huduma za QNET na kuelewa vyema biashara yake. 

Kongamano la siku tano ilijumuisha mfululizo wa programu za mafunzo, hotuba za uhamasishaji, kutambulisha bidhaa mpya za mtindo wa maisha wa QNET na matukio ya burudani. Kivutio kikubwa mwaka huu ni QNET Carnival ambayo ilionyesha zaidi ya nembo au lebo 30 za bidhaa za QNET katika moja ya maonyesho makubwa kuwahi kufanywa na kampuni hiyo. Bidhaa mpya zilizozinduliwa mwaka huu ni pamoja na virutubisho vipya kwaajili ya afya ya wanaume vinavyoitwa QAlive, na toleo lenye ukomo la saa za kifahari kwaajili ya kumbukizi ya miaka mitano ya ushirikiano kati ya QNET na klabu ya mpira wa miguu ya jiji la Manchester  (Manchester City Football Club). Moja kati ya dondoo zilizoshika hisia za watu ni sherehe za mahafali ya wateja ambao wamekamilisha kozi zao kwa njia ya mtandao kupitia qLean, bidhaa ya elimu ya QNET, ambayo ni maarufu sana miongoni mwa wateja katika kanda ya Sahara ya Afrika. 

Washiriki vile vile walipewa fursa ya kusikiliza kutoka kwa wazungumzaji rasmi ambao wameshinda vikwazo vikubwa na kufanikisha ndoto zao.  Farouk Saad Hamad Al-Zuman, raia wa kwanza wa Saudi Arabia kupanda mlima Everest, na Sparsh Shah, mvulana mwenye umri wa miaka 15 raia wa marekani mwenye asili ya India aliyezaliwa na tatizo la mifupa dhaifu (brittle bones), ambaye alipewa siku 2 za kuishi na madaktari baada ya kuzaliwa, na sasa ni nyota katika mtandao wa Youtube kwa mtindo wake wa kipekee wa mziki ambao anaunganisha pamoja muziki wa classical na rap.  

Bwana Koné Doupin, Mwakilishi wa Kujitegemea anayeshiriki katika kongamano hilo la (V-Convention) kutokea Ivory Coast alisema:  "Nina furaha sana kuwa hapa mwaka huu.  Tangu nilipojiunga na QNET miaka kumi iliyopita, sijawahi kukosa kongamano la -V lolote kwa sababu ni fursa ya kipekee kukutana na viongozi wetu wa juu, kujifunza kutoka kwao, kukutana na watu kutoka sehemu mbalimbali na kugundua upekee wa bidhaa mpya.  Nina shauku kubwa ya kujaribu bidhaa mpya ya QAlive, kirutubisho kipya cha wanaume na kugundua ni jinsi gani kinaweza kuboresha maisha yangu."

Sherehe za ufunguzi ziliongozwa na watu mbalimbali maarufu kutoka Malayasia na Asia ya Kusini Mashariki.  Mgeni rasmi kutoka Afrika, Bwana Cissé Ibrahim Sory vile vile alikuwepo katika sherehe za ufunguzi, Bwana Cissé Ibrahim Sory ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri kutoka ofisi ya Rais katika Jamhuri ya Guinea-Conakry.

Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa QNET aliyeteuliwa, Bi. Malou Caluza alisema: "Matukio kama haya ya Kongamano (V-Convention) hutupa fursa ya kuwahudumia wasambazaji wetu na kuwapa fursa ya kuona na kushuhudia mtindo wa Kuishi Kikamilifu (Absolute Living) ambao inaongoza biashara yetu, Vile vile ni jukwaa bora la kusherehekea ari ya ujasiriamali ambayo kampuni ya mauzo ya moja kwa moja kama QNET inachochea kwa mamilioni ya watu duniani kote, kuwasaidia kuboresha maisha yao na kuchangia katika jamii."

Akiongeza katika hilo, Meneja Mkuu wa QNET wa kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Bwana Biram Fall, alisema: "V-Malayasia inafuata msimu wa kongamano la QNET Expo wa mwaka 2019 wenye mafanikio wenye jina la Kuisi Kikamilifu (Absolute Living), linaloenda sambamba na kanuni ya kampuni ya mauzo ya moja kwa moja QNET na falsafa yake ya  RYTHM - Jiinue Uweze Kuwasaidia Wanadamu (Raise Yourself to Help Mankind) Kongamano la mwaka 2019 lilianzia jijini Dar es salaam, Tanzania mwezi uliopita, kisha likahalia Kumasi, Ghana na sasa nchini Malayasia kwaajili ya kongamano la kiulimwengu la V-Convention.  Baadae nchi zingine za Afrika zitakuwa wenyeji wa kongamano la Kuishi Kikamilifu (Absolute living expo)."

QNET, inauza reja reja bidhaa mbalimbali za Afya na ustawi, huduma binafsi na urembo, sikukuu, utunzaji wa nyumba na kozi kwa njia ya mtandao miongoni mwa nyingi zingine ambazo zinaboresha maisha ya kila siku ya wateja wake duniani kote. QNET iliwekwa katika moja kati ya makampuni 100 makubwa na imara ya MLM  (Solid Top MLM Companies) kwa mwaka 2018 na Portal ya habari za mauzo ya moja kwa moja ya Business for Home.

Katika Afrika Magharibi, Chama cha Ghana cha CSR (GHACEA) mwaka 2018 kiliitunukia QNET kuwa Kampuni ya Mwaka ya Biashara ya Mtandao (E-Commerce Company of the Year.)
 Afisa Mtendaji Mkuu wa QNET,  Ms. Malou Calouza(wa kwanza kushoto)  na Maofisa wa serikali ya Malaysia wakikata  utepe kuzindua rasmi kongamano la V-Convetion lililofanyika mjini Penang, Malaysia hivi karibuni. Wengine ni wajumbe wa Bodi wa QNET.
Meneja wa QNET wa kusini mwa Afrika, Biram Fall (kushoto)akiwa amepozi na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri Ofisi ya Rais, Guinea-Conakry, Ndugu Cissé Ibrahim Sory wakati wa kongamano la QNET la V-Convetion lililofanyika mjini Penang, Malaysiahivi karibuni.

DAMPO LA ILEMBO LITACHAFUA MAJI- RC MWANGELA

$
0
0
Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imetakiwa kubadilisha mahali pa kutupa takataka (dampo) kutoka eneo la Ilembo lilipo sasa kwakuwa maji yanayotiririka kutoka katika eneo hilo yanaweza kuelekea katika chanzo cha maji cha Mantengu ambacho kinatarajiwa kuanza kutumika muda si mrefu.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji iliyopo Wilayani humo.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema zoezi la kubadilisha eneo lakutupa takataka lifanyike haraka kwakuwa mradi wa Maji wa Vwawa ambao unatumia chanzo cha Maji cha Mantengu umekamilika na hivi karibuni utaanza kuwafikia wananchi.

“Ile sehemu ya dampo ibadilishwe, maji yameshaanza kutoka na yatawafikia wananchi hivi karibuni, hivyo nawaagiza halmashauri utekelezaji wa hili ufanye haraka,”amesisitiza Brig. Jen. (Mst) Mwangela

Ameongeza kuwa licha ya kuwa eneo la kutupa takataka litabadilishwa lakini wahakikishe wanazoa takataka zilizopo kwakuwa zikibaki pale zitaendelea kuchafua maji.

“Ili chanzo cha Mantengu kibaki salama na maji yawe salama zile takataka zitolewe mara baada ya kuhamisha dampo, licha ya kuwa tunafahamu kuna utaratibu wa kuyachuja na kuyawekea dawa maji hayo bado kuna baadhi ya sumu haziwezi kumalizwa na madawa hayo”, amefafanu Brig. Jen. (Mst) Mwangela

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbozi John Palingo amesema kuwa halmashauri ya Wilaya ya Mbozi itatekeleza agizo hilo na sasa eneo la kutupa takataka litahamishiwa Mbozi Mission ili kulinda chanzo hicho cha maji cha Mantengu.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela akipanda katika tenki la maji litakalotumika katika mradi wa maji wa Vwawa-Mantengu wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maji iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi.

NI PIGO KWA TAIFA... VIONGOZI WA SERIKALI WABUNGE WAMLILIA DK. REGINALD MENGI....

$
0
0


*Wasema atakumbukwa kwa wema wake, kujitoa kwa kusaidia jamii ya Watanzania
*Wengine wasema ameacha somo...
Nape akumbuka kikao chao cha mwisho

 
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii


VIONGOZI wa ngazi mbalimbali nchini katika Serikali ya Awamu ya Tano pamoja na wabunge wamesema wamesikitisha na taarifa za kifo cha mfanyabiashara maarufu nchini Reginald Mengi.

Mengi aliyezaliwa mwaka 1944 mkoani Kilimanjaro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo(Mei 2,2019) akiwa Dubai katika moja ya nchi za Falme za Kiarabu.
Akizungumzia kuhusu taarifa za kifo cha Mengi, Rais Dk.John Magufuli amesema " Nimesikitishwa na taarifa za kifo cha Mzee na Rafiki yangu Dk. Reginald Mengi. 

"Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo ya Taifa letu na maono yake yaliyopo ktk kitabu chake cha I Can, I Will, I Must. Poleni wanafamilia, wafanyakazi wa IPP na Jumuiya ya Wafanyabiashara."
Wakati huo huo Makau wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema moja ya vitu alivyotuachia Mzee Mengi ni ule wepesi wake wa kusaidia masuala ya kijamii na kwamba Watanzania daima atakukumbuka.

Kwa upande wake Mbunge wa Mtama mkoani Lindi Nape Nnauye amesema kuwa Mengi ameacha alama kubwa."Nimejifunza mengi kwako, Rafiki, Mshikaji, Kiongozi na Mzazi! Ulinifundisha kuwa kukata tamaa ni dhambi! 

"Msalimie mzee Sitta, mkumbushe kile kikao chetu Cha mwisho nyumbani kwako.Pumzika kwa Amani Dk. R.A Mengi,"amesema Nape wakati anaelezea masikitiko yake kutokana na kifo cha mzee Mengi. 

Akizungumzia kifo cha Mengi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Januari Makamba amesema "Pole kwa Jacqueline na Regina, Abdiel and the twins - na familia nzima ya IPP Group. Mungu ailaze roho ya Mzee Reginald Mengi peponi."

Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema hivi " Pumzika kwa amani Dk.Reginald Mengi, asante kwa ushirikiano mzuri ulionipatia katika kutekeleza majukumu yangu lakini zaidi kwa kunihimiza mara kwa mara nitamani/kufanya mambo makubwa. 

"Pengo lako ni gumu kuzibika! Pole nyingi kwa Madam JNtuyabaliwe ,watoto, ndugu, jamaa na marafiki. Poleni sana,"amesema Waziri Mwalimu.
Naye aliyewahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akizungumzia kifo cha Mengi ametoa pole kwa wana familia, ndugu, jamii na marafiki wa Mengi kutokana na taarifa za kifo chake.

"Hakika, siku za maisha yetu zimehesabiwa na kuandikwa kitabuni. Ameimaliza safari yake hapa duniani. Iwe heri kwake huko ng'ambo ya mto. RIP baba yetu,"amesema Nyalandu.

Kwa upande wake Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa haijalishi tunaishi muda gani hapa duniani, cha msingi unatoa mchango gani hapa duniani kabla ya kifo. "Dk.Mengi si tu uliwavutia wengi ,bali uligusa sana maisha ya wengi , umetuonesha kuziacha jamii zetu bora zaidi kuliko tulivyo zikuta.Pumzika kwa Amani,"amesema.

Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amesema " Msiba mkubwa kwa Taifa na haswa kwa familia ya Mzee Reginald Mengi. Pole sana JNtuyabaliwe na Watoto, The twins. "Poleni sana Regina, Abdiel na familia nzima ya Makampuni ya IPP. Bwana ametoa na Bwana ametwaa. Mungu ailaze roho ya Mzee Reginald Mengi mahala pema anapostahili."

Mfanyabiashara maarufu Mohammed Dewji 'MO' ameandika hivi "Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un. Mwenyezi Mungu ampe pumziko na ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Ameen.RIP Mengi."

Kwa upande wa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amesema watu wanagopa kifo, kimsingi tunacho ogopa ni kuwahi kufa kwani kifo hakizuiliki.
"Katika maisha ni vyema kuishi maisha ya baraka na watu wote,ili utakapotangulia maisha yako yaweze kuwa na thamani. Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya maisha ya Dk. Mengi,kwani alijua thamani ya ubinadamu,"amesema Lema.

Mbunge wa Kawe Halima Mdee amesema amepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo cha ndugu Reginald Mengi.Ametoa pole kwa familia , ndugu, jamii na marafiki.

"Mwaka 2019 unaendelea kuwa wa majonzi kwetu kama Taita, tunapoteza watu makini waliokuwa na mchango mkubwa sana katika ujenzi wa nchi yetu.Upumzike kwa amani Mkuu,"amesema Mdee.
Katika Enzi za Uhai wake Dkt Reginald Abraham Mengi akiwa na familia yake.

UBA yaadhimisha miaka 70 ya utumishi

$
0
0
LAGOS, NIGERIA

BENKI ya United Bank of Africa (UBA) imeadhimisha miaka 70 tangu ianze kutoa huduma za kibenki kwa wateja wake wakati wa sherehe zilizoongozwa na Mwenyekiti wa kundi la kampuni Tony O. Elumelu.

Sherehe hizo zilizohudhuriwa na wateja, wafanyakazi na marafiki pia zilienda sambamba na hafla ya utoaji Tuzo za kila mwaka za Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO).

Tuzo hizo zilitolewa mbele ya maelfu ya wageni kwa wafanyakazi wa UBA kutoka nchi zote 23 ambako inaendesha shughuli zake kutokana na utendaji wao uliotukuka wa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Miongoni mwa watu mashuhuhuri katika usiku huo pamoja na makadhi, magavana wa zamani na sasa wa majimbo mbalimbali ya Nigeria.

Aidha marais wa zamani Olusegun Obasanjo na Ibrahim Babaginda, ambao walishindwa kuhudhuria kutokana na dharura walituma barua za kuipongeza benki hiyo kwa ufanisi na mafanikio makubwa yaliyopatikana.

Mwenyekiti wa UBA Plc, Tony Elumelu, ambaye aliambatana na mkewe Dk. Awele, alisema UBA imebakia kuwa taasisi ya kifedha inayoongoza barani Afrika na kutimiza kwake miaka 70 ni mafanikio makubwa.

Alisema, “Huu ni wakati wa kusherehekea urithi tajiri wa kipindi cha miaka mingi na kumwambia kila mtu aliyechangia kile kinachoifanya UBA isimame imara leo hii, kuwa tunashukuru kwa yote na jinsi walivyohakikisha uwekezaji uliowekwa katika benki kipindi cha miongo iliyopita unalipa.”

Shukrani kama hizo zilitolewa pia na CEO wa Kundi la Kampuni, Kennedy Uzoka huku Mwenyekiti wa Benki ya Zenith, Jim Ovia, akiisifu menejimeni na wafanyakazi wa UBA kwa kuifikisha hapo ilipo. Ovia alisema; “ UBA inabakia kuwa moja ya benki kubwa kabisa Kusini mwa Sahara Afrika. UBA imeanzishwa kwa ajili ya kudumu. Nawapongeza wafanyakazi wote na wanahisa. Najuta kutonunua hisa za UBA, lakini nadhani sijachelewa kufanya hivyo.



Mweyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya United Bank for Africa, Tony Elumelu, akifurahia jambo na washiriki wengine kwenye sherehe ya miaka 70 ya utoaji huduma kwa benki hiyo kwa nchi zaidi ya 50 za Afrika. Sherehe hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini Lagos nchini Nigeria
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images