Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

Elimu ya fedha, taarifa za mikopo ni muhimu-Gavana Luoga

$
0
0
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Florens Luoga, amesema elimu kuhusu masuala ya fedha ni muhimu katika mfumo mzima wa taarifa za mikopo ili kuwawezesha Watanzania kupanga matumizi bora ya mikopo.

Prof Luoga alitoa kauli hiyo katika uzinduzi wa kampeni ya uelimishaji umma kuhusu taarifa za mikopo na fedha iliyoratibiwa na BOT kwa kushirikiana na taasisi ya International Finance Corporation ambayo ni mwanachama wa Kundi la Benki ya Dunia.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mpango, Dk. Philip Mpango, Prof Luoga alisema taarifa za mikopo na elimu ya fedha ni muhimu ili kuhakikisha Watanzania wanaondokana na matumizi ya anasa ya mikopo.

“Kampeni hii ya elimu kwa umma inalenga kuwaelimisha watumiaji wa huduma za fedha na wadau wengine kukuza uelewa wao kuhusu taarifa za mikopo ili kuongeza ushiriki katika matumizi ya taarifa za mikopo hapa nchini,” alisema.

Aidha, Meneja Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa Magina alisema kampeni hiyo ya miezi mitatu inalenga kuongeza uelewa, mwamko kuhusu taarifa za mikopo na kukuza upatikanaji wa mikopo.

”Kauli mbiu katika kampeni hiyo ni: “Pata Taarifa Yako ya Mikopo Leo. Angalia hali yako ya kifedha ili kupanga mustakabali wako bora wa kesho” inaungwa mkono na wadau mbalimbali katika sekta ya huduma za fedha.

“Wadau hao wameahidi kusaidia kusambaza ujumbe kuhusu umuhimu wa upatikanaji wa mikopo na jinsi Watanzania wanavyoweza kuishi maisha bora kwa kuweza kupata taarifa za mikopo yao na kujua historia ya mikopo yao,” alisema.

Alisema usimamizi mzuri wa mikopo na historia nzuri ya mikopo ni muhimu katika kuwezesha kupata mkopo nafuu."Kuhakiki taarifa yako ya mikopo mara moja kwa mwaka ni huduma inayopatikana bila malipo, tena itakuletea mafanikio kwa kukuandaa vema utakapoenda kuomba mkopo. 

"Historia nzuri ya mikopo inaweza kusaidia kustahili viwango vya chini vya riba na ada, hivyo kuondokana na kutenga fedha kwa ajili ya dharura na gharama zisizotarajiwa," alisema. 

Alisema mikopo inasaidia kupata mahitaji ya sasa, kama vile nyumba au ada ya shule ya mtoto wako, kwa kuzingatia ahadi yako ya kulipa kwa awamu na kwa muda uliopangwa.Aidha, Meneja wa IFC - Tanzania, Manuel Moses alisema taarifa ya mikopo inaonesha taarifa binafsi; utambulisho na taarifa ya mawasiliano na ikiwezekana historia ya ajira; idadi na aina za akaunti za mikopo.

Naye Meneja Maendeleo ya Biashara kutoka Dun & Bradstreet, Josephine Temu alisema kwa sasa, kuna taasisi mbili zilizopatiwa leseni na Benki Kuu ya Tanzania kuandaa na kutoa taarifa za mikopo hapa Tanzania ambazo ni Creditinfo Tanzania Limited na Dun & Bradstreet.Alisema taasisi hizo zinakusanya na kutunza taarifa za mikopo na kutoa taarifa za mikopo kwa kampuni au watu wanaozihitaji kama vile benki. 

Alisema ripoti hiyo ya mikopo inaweza kutolewa na taasisi hizo (Creditinfo na Dun & Bradstreet) mara moja kwa mwaka bila malipo.“Ili kupata taarifa ya mikopo unatakiwa kuwasilisha nakala ya kitambulisho chako cha taifa au kingine kama leseni ya udereva, hati ya kusafiria. Jaza na wasilisha fomu ya maombi ya taarifa yako ya mikopo katika taasisi zinazoandaa taarifa za mikopo ambazo kwa sasa ni Creditinfo au Dun & Bradstreet," alisema.

Akifafanua kuhusu mambo muhimu ya kuangalia kwenye taarifa ya mikopo, Meneja Maendeleo ya Biashara kutoka Creditinfo, Tonny Missokia alisema muhimu ni taarifa binafsi kama vile jina, hadhi ya ndoa, anwani, taarifa za ajira na namba za mawasiliano ni sahihi.
 Meneja Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa Magina akizungumza katika warsha ya kuhusu elimu ya taarifa za fedha na ripoti za mikopo kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma.
 Meneja Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa Magina akizungumza katika warsha ya kuhusu elimu ya taarifa za fedha na ripoti za mikopo kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma.
 Wataalam wa Benki Kuu ya Tanzania, Creditinfo na Dun & Bradsheet wakitoa elimu kuhusu umuhimu wa taarifa za mikopo kwa mwananchi eneo la Nyerere Square mchana huu. Kampeni hiyo inaendeshwa kwa pamoja na Benki Kuu ikishirikiana na International Finance Corporation ambayo ni sehemu ya kundi la Benki ya Dunia

WATEJA WA TIGO MIKOA YA MBEYA NA IRINGA KUFANYA MALIPO KWA KUTUMIA MFUMO WA KIELETRONIKI WA MALIPO SERIKALINI (GePG)

$
0
0
Mkuu wa Mauzo wa Tigo kwa mikoa ya Mbeya na Rukwa Ladislaus Karlo (wa kwanza kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi wa Mfumo wa Kielekroniki wa Malipo Serikalini (GePG) kwa mkoa wa Mbeya namna mteja anavyoweza kutumia simu yake kufanya malipo. Wa kwanza kulia ni Meneja wa Malipo ya Biashara kwa Tigo Pesa wa Tigo Dennis Sakia na anayefuatia ni Afisa Uhusiano Msaidizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa mazingira Mbeya, Kadri Makongwa.
Afisa Uhusiano Msaidizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa mazingira Mbeya, Kadri Makongwa (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Mfumo wa Kielekroniki wa Malipo Serikalini (GePG) kwa mkoa wa Mbeya. Kulia ni Meneja wa Malipo ya Biashara kwa Tigo Pesa wa Tigo Dennis Sakia na kushoto ni . Mkuu wa Mauzo wa Tigo kwa mikoa ya Mbeya na Rukwa Ladislaus Karlo.
Waandishi wa habari wakimskiliza Mkuu wa Mauzo wa Tigo kwa mikoa ya Mbeya na Rukwa Ladislaus Karlo (wa kwanza kushoto) wakati wa uzinduzi wa Mfumo wa Kielekroniki wa Malipo Serikalini (GePG) jijini Mbeya. Wa kwanza kulia ni . Meneja wa Malipo ya Biashara kwa Tigo Pesa wa Tigo Dennis Sakia na anayefuatia ni Afisa Uhusiano Msaidizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya, Kadri Makongwa,



Fanya malipo ya haraka, urahisi na kwa usalama kwa zaidi ya idara 300 za Serikali, mawakala na mamlaka mbali mbali kupitia Tigo Pesa

Wateja wa Kampuni ya Tigo wa mikoa ya Mbeya na Iringa sasa wanaweza kufanya malipo kutumia mfumo wa Kielektroniki wa Malipo Serikalini (GePG) baada ya kampuni hiyo kuongeza malipo ya Serikalini kwenye App yake ya Tigo Pesa.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira jijini Mbeya (WSSA) Afisa Uhusiano Msaidizi wa WSSA Mbeya Kadri Makongwa, alisema mfumo wa GePG umerahisisha upatikanaji wa ankara na kufanya malipo kwa wananchi na kuongeza kuwa umeleta faida nyingi ikiwa ni pamoja na kuboresha uwekaji wa kumbukumbu, utoaji wa taarifa, kupunguza ubadhirifu na kuongeza mapato kwa idara mbali mbali na taasisi za Serikali 

“Mfumo wa GePG, pia imeongeza wigo wa upatikanaji wa huduma kwa wananchi na kuongeza fursa za biashara kwa kampuni zinazotoa huduma za malipo kama Tigo. Wananchi wanaweza kupokea ankara zao moja kwa moja kutoka ofisi na mashirika ya Serikali ikiwa ni pamoja na za kutoka (WSSA) 

Malipo pia yanaweza kufanyika kwa njia mbali mbali za kimtandao, na kufurahisi na mahali popote kwa njia ya simu za kiganjani, benki au kwa njia ya mtandao.,” alisema 

“Kufanya kazi kwa karibu na Serikali ili kufikisha huduma za kifedha kwa wananchi wengi ni moja kati ya malengo mkakati yetu,” alisema Makongwa 

Kwa upande wake Mkuu wa Mauzo wa Tigo kwa Mbeya na Rukwa Ladislaus Karlo alisema “Zaidi ya wateja milioni 7 wanaotumia huduma yetu ya Tigo Pesa sasa wana uwezo zaidi wa kufanya malipo kwa haraka kwenda kwa taasisi, Wizara na wakala wa Serikali zaidi ya 300 kupitia Tigo Pesa USSD, Tigo Pesa App na QR Code,” 

Baadhi ya taasisi za Serikali ambazo malipo yanaweza kufanywa kwa Tigo Pesa ni pamoja na Wizara ya Ardhi, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka za Miji, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Mamlaka ya Misitu (TFS), Wizara ya Utalii, Bodi ya Utalii, Idara ya Uhamiaji, Mamlaka za Maji katika miji ya Mwanza (MWAUWASA), Tanga (Tanga UWASA), Dar es Salaam (DAWASA), Dodoma (DUWASA), Hospitali mbali mbali kama vile Muhimbili, Mwananyamala na idara nyingine zaidi ya 300. 

Ili kufanya malipo kwa kutumia Tigo Pesa App na QR Code, wateja wa Tigo wanahitaji kupakua App ya Tigo Pesa na kuscan QR code kisha kuingiza namba ya siri ili kufanikisha muamala.

Ili kufanya malipo kwa kutumia menu ya Tigo Pesa, mteja anatakiwa kufuata hatua zifuatazo;. 

1) Kupiga *150*01# kisha kuchagua Lipa Bili
2) Kuchagua namba 5 (Malipo ya Serikali)
3) Kuingiza tarakimu 12 za mamlaka au taasisi anayotaka ipokee malipo 
4) Kuingiza kiasi cha fedha anachotaka kulipa
5) Kuingiza namba ya siri kwa ajili ya kuruhusu malipo

Kwa upande mwingine, wateja wanaweza kutumia App ya Tigo Pesa ambayo inarahisisha ufanyaji wa malipo kwa kiasi kikubwa.

Baada ya kukamilisha malipo, wateja wa Tigo watapokea risiti ya kielektoniki kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi unaothibitisha kuwa muamala umefanyika kikamilifu. Risiti hiyo ya kielektroniki inakubalika kama uthibitisho tosha wa malipo na inaweza kusaidia kurahisisha kufuatilia malipo kwa kuwa ni rahisi kuhifadhi na kuipata pale inapohitajika ukilinganisha na risiti za karatasi ambazo ni rahisi kupotea au kuharibika.

Tigo inawakaribisha wateja wake kuanza kutumia huduma hii ya Malipo ya Kieletroniki Serikalini (GepG) sasa.

Jumia rasmi yaorodheshwa kwenye Soko la Hisa la New York, Marekani

$
0
0
  Pichani kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumia Tanzania, Bw. Zadock Prescott aakifafanua jambo leo mbele ya Waandishi wa Habari namna walivyojiunga na Soko la Hisa la New York na kuwa kampuni ya kwanza kabisa ya kiteknolojia kuanzishwa Afrika kufanya hivyo, akaongeza na kubainisha kuwa wanataka kuonyesha Dunia ubunifu wa kidigitali unaotokea Afrika na fursa kutoka Afrika kwa upande wa teknolojia na biashara ya mtandaoni,pichani kushoto ni  Meneja Uhusiano wa Umma na Masoko, Jumia Travel Tanzania, Geofrey Kijanga
kampuni inayoongoza kwa utoaji wa huduma za uuzaji na manunuzi kwa njia ya mtandao, imetangaza rasmi kuwa imeorodheshwa katika Soko la Hisa la New York nchini Marekani. Kuorodheshwa huku ni matokeo ya mafanikio ya timu nzima, wafanyakazi wote wa Jumia Afrika nzima. Tukio hili lilisherehekewa kwa ishara ya kupiga kengele kwenye kila nchi ambapo Jumia inafanya shughuli zake muda sawa sawa na jijini New York.

Ikiwa imeanzishwa mwaka 2012, Jumia ilianza mkakati wa kuboresha maisha ya kila siku barani Afrika, kwa kutumia teknolojia kuleta ubunifu, urahisi na unafuu wa upatikanaji wa huduma kwa wateja. Jumia pia inaziwezesha biashara kukua, kwa kutumia jukwaa ililonalo kuwafikia na kuwahudumia wateja barani kote Afrika. 

Kwa sasa, Jumia inafanya shughuli zake katika nchi 14 ikiwa na wauzaji takribani 81,000 wakiwa wanafanya biashara na mamilioni ya wateja. Jukwaa la biashara kwa mfumo wa mtandaoni limetoa ajira za moja kwa moja kwa wafanyakazi takribani 5,000 Afrika.

“Mafanikio haya kwa kiasi kikubwa yamefanikishwa na bidii ya timu yetu, imani ya wateja wetu, pamoja na kujitolea kwa wauzaji na washirika wetu. Wadau wetu wote wanastahili pongezi kwa hatua hii muhimu, na ndiyo kwanza tuko mwanzoni mwa safari ndefu na kubwa. 

Tutaendelea kujikita zaidi kwenye azma yetu na kufanya kazi kwa bidii zaidi kuwasaidia wanunuzi, wauzaji, washirika na wadau wote wanaofaidika na mapinduzi ya kiteknolojia,” walisema Sacha Poignonnec na Jeremy Hodara ambao ni waanzilishi na Wakurugenzi Wakuu ambao walikuwepo jijini New York, nchini Marekani wakati wa kufanyika kwa tukio hilo.
Akielezea sababu zilizopelekea mpaka Jumia kujiunga na Soko la Hisa kubwa zaidi duniani, Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumia Tanzania, Bw. Zadock Prescott amebainisha kuwa, “kwa kujiunga na Soko la Hisa la New York na kuwa kampuni ya kwanza kabisa ya kiteknolojia kuanzishwa Afrika kufanya hivyo, tunataka kuonyesha dunia ubunifu wa kidigitali unaotokea Afrika na fursa kutoka Afrika kwa upande wa teknolojia na biashara ya mtandaoni.”

“Jumia kuorodheshwa rasmi kwenye Soko la Hisa la New York ni ishara kwamba kuna ubunifu unatokea barani Afrika - inaionyesha Afrika kuwa ni bunifu, inabadilika na kuwa ya kisasa zaidi. Hatua hii muhimu itatusaidia kuwavutia wauzaji wengi zaidi kwenye mtandao wa Jumia. 

Kwa sababu wauzaji na washirika wengi bado hawajatufahamu vizuri, na pindi wakitujua, tunaamini kuwa watatamani kufanya kazi na sisi,” alisema Bw. Prescott na kuhitimisha kuwa, “Tunaamini pia hii itatusaidia kujenga uaminifu zaini na wauzaji wetu, hususani kwa wale ambao bado hawajaanza kuzoea mfumo wa mtandaoni, wengi sasa watatuona kama kampuni imara na, tunaamini itatusaidia kwenye ukuaji na wateja kukubali huduma zetu. Hivyo basi, ningependa kuchukua fursa hii kuishukuru timu nzima kwa kufanya kazi kwa bidii, kujitolea kwa wauzaji na washirika pamoja na imani kutoka kwa wateja wetu.” 

JAPAN KUIPIGA JEKI TANZANIASHILINGI BILIONI 794 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) kushoto, akiwa pamoja na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japani-JICA, Bw. Hiroshi Kato, walipokutana na kufanya mazungumzo kwenye Ofisi za ubalozi wa Tanzania mjini Washington DC-Marekani, kando ya Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la KImataifa-IMF
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) kushoto, akiwa pamoja na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Japani-JICA, Bw. Hiroshi Kato, walipokutana na kufanya mazungumzo kwenye Ofisi za ubalozi wa Tanzania mjini Washington DC-Marekani, kando ya Mikutano ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, ambapo JICA imeahidi kutoa ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania.

Na Benny Mwaipaja, WFM, Washington D.C

 Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo la Kimataifa-JICA inakusudia kuipatia Tanzania mkopo nafuu pamoja na ruzuku wenye thamani ya zaidi ya dola milioni 345 za Marekani, sawa na takriban shilingi bilioni 794, kwa ajili ya kutekeleza miradi mitatu ya maendeleo ikiwemo ukarabati wa barabara ya Arusha hadi Holili, ukarabati wa Bandari ya Kigoma na Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Visiwani Zanzibar.

Ahadi hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Shirika la Maendeleo la JICA anayesimamia Ukanda wa Kusini mwa Jangwa la Sahara Bw. Hiroshi Kato, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Mjini Washington D.C nchini Marekani.

Ameitaja miradi hiyo iliyoko mezani kwao inayosubiri kupatiwa fedha wakati wowote kuanzia sasa kuwa ni mradi wa ukarabati wa barabara ya Arusha-Holili utakaopatiwa mkopo wa dola milioni 221, Mradi wa maji safi na usafi wa mazingira Zanzibar utakaopatiwa fedha kupitia mkopo wa dola milioni 99 na mradi wa upanuzi wa Bandari ya Kigoma ambao Japan itatoa ruzuku ya dola za Marekani milioni 25.

Bw. Kato amesema kuwa Japan inajivunia ushrikiano wa muda mrefu kati yake na Tanzania na kwamba iko tayari kusaidia juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano za kuwaletea wananchi wake maendeleo na kuitaka Serikali kuwasilisha miradi yake ya kimkakati ambayo Japan itafadhili kupitia mikopo yenye riba nafuu pamoja na ruzuku.

Akizungumza na Mwakilishi huyo wa Japan katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, ameishukuru Japan kwa uhusiano wake mzuri na Tanzania na namna inavyo isaidia nchi kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo akitaja mmoja wa miradi hiyo kuwa ni barabara ya juu ya kwanza nchini Tanzania  katika makutano ya Tazara Jijini Dar es Salaam, maarufu kama Daraja la Mfugale.

Dkt. Mpango ameiomba Japan kupitia Shirika lake la JICA kutoa ruzuku na mikopo nafuu ili kutekeleza miradi ya kimkakati ya ujenzi wa reli ya kisasa kwa kiwango cha kimataifa - SGR, Mradi wa kufua umeme wa Rufiji, Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato mkoani Dodoma, ujenzi wa barabara za mzunguko jijini Dodoma, ujenzi wa mtandao wa barabara, upanuzi wa bandari na miradi mingine ya kijamii.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango anaongoza ujumbe wa Tanzania katika mikutano ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF, inayofanyika mjini Washington DC nchini Marekani, ambapo ametumia fursa hiyo kukutana na wadau wa maendeleo kupenyeza ajenda za maendeleo ya kiuchumi ya Tanzania.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 17,2019

Waziri Kairuki Akutana na Mabalozi wa Nchi Tatu Kuzungumzia Uwekezaji.

$
0
0
Na.Paschal Dotto-MAELEZO.

Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki ameanza kukutana na wawekezaji kutoka balozi za Ufaransa, Uholonzi, Norway na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Marekani, USAID, mazungumzo mafupi baina wao yamefanyika leo kwa wakati tafaouti, huku Waziri Kairuki akisema kuwa mazungumzo hayo yalilenga kuongeza ushirikiano katika sekta ya uwekezaji nchini.

Katika mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini, Frederic Clavier, Waziri Kairuki alisema kuwa nchi ya ufaransa na Tanzania zina ushirikiano wa muda mrefu katika sekta mbalimbali ikiwemo ya uwekezaji pamoja na biashara.

“tulikuwa na mazungumzo na Balozi wa Ufaransa ambaye tumejadili mambo mbalimbali katika ushirikiano wetu, ili kuwaita wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Ufaransa waje nchini kama ilivyokuwa mwaka jana,” alisema Waziri

Akitoa mfano Waziri Kairuki alisema kulikuwa na ugeni wa wawekezaji na wafanyabiashara kutoka huko Ufaransa na walifanya majadiliano na Tasisi ya uwekezaji nchini, TPSF, akasema, “kwa hiyo na mwaka huu tumekubaliana watawaalika tena TPSF na TIC (Kituo cha uwekezaji) ili kuweza kujadili mambo ya uwekezaji”.

Kukutana na wawekezaji hao kutoka nchi mbalimbali Waziri Kairuki amesema kutabainisha fursa kadhaa na kufuatilia changamoto ili uwekezaji mkubwa uweze kufanyika nchini, pia Waziri Kairuki alieleza kuwa wamekubaliana na Balozi wa Ufaransa kuwa na ugeni mkubwa wa wawekezaji kati ya mwezi Mei na Septemba ambao watakuja kuwekeza katika sekta ya kilimo.

Aidha, Waziri Kairuki alimhakikishia Balozi wa Ufaransa kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji kwa kuendelea kuwajengea mazingira na hivyo kuhimiza wawekezaji kutoka Ufaransa kuongezaka nchini kutoka 40 waliowekeza kwa sasa.

“Uwekezaji unaongeza pato letu, unaongeza fedha za kigeni, ajira pamoja na masuala mengine katika uchumi, katika hili Ufaransa wamesema wako tayari kuanzisha jukwaa la biashara kwa wafanyabiashara kutoka Tanzania na Ufaransa ili kuweza kuvutia zaidi wawekezaji”, Waziri Kairuki.

Aidha, Balozi Clavier aliongeza kuwa Serikali ya Ufaransa inaridhishwa na jitihada za Rais Magufuli na kuwa nchi yake ilikuwa inachangia maendeleo ya nchi Euro milioni 50 kwa mwaka na imeongeza mpaka kufika Euro milioni 100, ambazo zitatumika katika uwekezaji mbalimbali hapa nchini ikiwemo Sekta ya mafuta, Viwanda vya Dawa na kilimo.

Katika mazungumzo mengine na Mabalozi wa Uholanzi, Jeroen Verheul, Norway, Elisabeth Jacobsen pamoja na Mkurugenzi Mkazi USAID, Andy Karas, Waziri Kairuki amewahakikishia kuwa atakutana na wawekezaji kutoka nchi hizo, kuwasikiliza changamoto zao na kuzitatua ili kuimarisha sekta ya uwekezaji nchini.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.

Dkt. Ndumbaro afanya mazungumzo na balozi wa Italia nchini

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Damas Daniel Ndumbaro(Mb.), amefanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini, Mheshimiwa Roberto Mengoni katika ofisi za wizara Dodoma. Katika mazungumzo hayo, miongoni mwa mambo mengine, Tanzania na Italia zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika sekta za uwekezaji, utalii pamoja na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia. 
Mazungumzo yakiendelea. 
Msaidizi wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Charles Faini (wa kwanza na kulia) na Afisa wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Kisa Mwaseba (wa mwisho kushoto), wakifuatilia mazungumzo baina ya Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro(Mb.) na Balozi wa Italia nchini, Mhe Roberto Mengoni. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (Mb.) na Balozi wa Italia nchini, Mhe Roberto Mengoni, wakiagana mara baada ya mazugumzo.

WAZIRI KALEMANI ASISITIZA TAASISI ZA UMMA VIJIJINI ZIWEKEWE UMEME

$
0
0
Na Veronica Simba – Dodoma

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amewaagiza wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), kuwasimamia wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini nchi nzima, kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha kuunganisha umeme kwa taasisi zote za umma zilizo katika maeneo yao.

Alitoa maagizo hayo kwa nyakati tofauti jana, Aprili 16, 2019 akiwa katika ziara ya kazi wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma, ambapo aliviwashia umeme vijiji vya Buigiri na Mwigamwile.

Akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Buigiri pamoja na wananchi, Waziri alisisitiza kwamba, kitendo cha kuwasha umeme katika shule hiyo kinalenga kutoa hamasa katika utekelezaji wa maagizo ya serikali kuwa taasisi zote za umma ni lazima zipelekewe umeme.

“Niwaombe viongozi wa Halmashauri za Vijiji na Wilaya nchini kote, kuhakikisha taasisi za umma katika maeneo yenu zinalipia gharama ya kuunganishiwa umeme ambayo ni shilingi 27,000 tu kwa ninyi mlioko vijijini, ili taasisi hizo zote ziunganishiwe umeme,” alisisitiza.

Aidha, kuhusu suala hilo la kulipia gharama za kuunganishiwa umeme, Waziri alilazimika kutoa msisitizo kwa viongozi na wananchi kwani alisema kumekuwepo na tabia ya baadhi ya watu kulalamika kuwa hawajaunganishiwa umeme lakini baada ya kufuatilia sababu iliyobainika ni kuwa wanakuwa hawajalipia huduma hiyo.

“Lipieni umeme. Msibaki kulalamika tu. Mlalamike mkiwa mmelipia.”

Katika hatua nyingine, Waziri Kalemani aliwataka wanafunzi wa Shule hiyo ya Buigiri kuongeza jitihada katika masomo kwani tayari wamepelekewa umeme ili kuongeza kiwango cha ufaulu shuleni hapo.

Awali, akizungumza wakati wa tukio hilo la uwashaji umeme, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Vumilia Nyamoga alimweleza Waziri kuwa, Shule husika imekuwa na kiwango duni cha ufaulu kutokana na sababu mbalimbali, mojawapo ikiwa ni ukosefu wa umeme tangu ilipoanzishwa mwaka 2007.

Akiwa katika kijiji cha Mwigamwile, Waziri Kalemani aliwasha umeme katika Ofisi mpya ya Serikali ya Kijiji, ili kuendelea kutoa msisitizo wa azma ya serikali kuhakikisha taasisi za umma zinaunganishiwa umeme.

Aidha, ili kuonesha msisitizo zaidi, Waziri Kalemani, alilazimika kulipa yeyé mwenyewe shilingi 27,000 ikiwa ni gharama za kuunganisha umeme katika kisima cha maji kilichoko kijijini Ikoa, Kata ya Ikoa ambacho pamoja na kuwa kimekamilika kwa muda mrefu hakijaanza kufanya kazi kutokana na kutokuwa na umeme.

Waziri aliwaagiza wataalamu wa TANESCO kuunganishia kisima hicho umeme kabla ya Jumanne ijayo, Aprili 23 mwaka huu.

Katika maeneo yote ya Wilaya hiyo ambayo Waziri alipita kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, alimsisitiza Mkandarasi kuongeza kasi ya kuunganisha umeme ambapo alimtaka kufikia Desemba mwaka huu, awe amekamilisha kazi ya kuviunganishia umeme vijiji na vitongoji vyote vya Jimbo la Chilonwa.

Mbunge wa Jimbo hilo, ambaye alifuatana na Waziri katika ziara hiyo, Joel Mwaka, alimwambia kuwa vijiji 20 vya jimbo hilo kati ya 47 vilivyopo, havijafikiwa na umeme.

“Pamoja na kuwa mkataba unaonesha kazi hii ya kuunganisha umeme kupitia mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Kwanza (REA III, Phase I) inatakiwa ifikie tamati Juni mwakani, lakini nakuagiza wewe mkandarasi ukamilishe kazi hii ifikapo Desemba,” alisisitiza Waziri.

Mbali na kuwasha umeme katika vijiji vya Buigiri na Mwegamile, Waziri pia alikagua utekelezaji wa miradi ya umeme katika vijiji vya Ikoa (Kata ya Ikoa), Nguga (Kata ya Msamalo) na Mlebe (Kata ya Msamalo).

Viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo ni pamoja na Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga, Kaimu Meneja wa TANESCO, Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Tumaini Nyari, pamoja na wahandisi wasimamizi wa miradi ya umeme vijijini kutoka wizarani na REA.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akiwasha umeme katika ofisi mpya ya Serikali ya Kijiji cha Mwigamwile, wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma, alipokuwa katika ziara ya kazi, Aprili 16, 2019.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (mwenye shati la bluu), akilipia shilingi 27,000 ikiwa ni gharama ya kuunganisha umeme katika kisima cha maji kijijini Ikoa, Kata ya Ikoa, wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma, akiwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, Aprili 16, 2019.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (mwenye shati ya bluu-katikati), akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mlebe, Kata ya Msamalo, wilayani Chamwino, Mkoa wa Dodoma, akiwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, Aprili 16, 2019.
Kaimu Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga (kushoto) na viongozi wengine kutoka wizarani, TANESCO, REA na wilayani, wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Buigiri pamoja na wananchi wa maeneo jirani, katika tukio la kuwawashia rasmi umeme, Aprili 16, 2019.
Sehemu ya umati wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Buigiri iliyopo Chamwino, Dodoma, wakionesha furaha yao mbele ya Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani), alipofika kuwawashia rasmi umeme akiwa katika ziara ya kazi, Aprili 16, 2019.
Taswira ya jengo jipya la ofisi ya serikali ya kijiji cha Mwigamwile, wilayani Chunya, Mkoa wa Dodoma, kama ilivyonaswa wakati Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani) alipofika kuwasha rasmi umeme akiwa katika ziara ya kazi, Aprili 16, 2019. Waziri alisisitiza dhamira ya serikali kuunganisha umeme katika taasisi zote za umma.
Sehemu ya umati wa wanawake na watoto wa Kijiji cha Mwigamwile kilichopo Chamwino, Dodoma, wakionesha furaha yao mbele ya Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (hayupo pichani), alipofika kuwawashia rasmi umeme akiwa katika ziara ya kazi, Aprili 16, 2019.

MIGOGORO YA NDOA YATAJWA KUCHANGIA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

$
0
0

Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Elizabeth Mweyo akizungumza kwenye kikao cha mrejesho wa kazi za viongozi wa jamii kata ya Usanda katika kutokomeza mila na desturi kandamizi katika jamii.

Imeelezwa kuwa migogoro ya wanandoa imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa watoto kukosa haki zao matokeo yake wanafanyiwa vitendo vya kikatili. 

Hayo yamesemwa leo Jumanne Aprili 16,2019 na Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Elizabeth Mweyo kwenye kikao cha mrejesho wa majukumu ya viongozi wa jamii kata ya Usanda katika kutokomeza mila na desturi kandamizi zinazochangia ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 

Kikao hicho kimeandaliwa na Shirika la Agape ACP ambalo linalenga kutokomeza mila na desturi kandamizi zinazochangia ukatili dhidi ya wanawake na watoto ili kupunguza mimba na ndoa za utotoni na maambukizi ya VVU na UKIMWI. 

Afisa ustawi huyo wa jamii aliwataka wanandoa kuvumiliana panapotokea migongano kwani hakuna ndoa takatifu huku akibainisha kuwa pale wanandoa wanapoachana wanaoteseka zaidi huwa ni watoto. 

“Wanaume mmekuwa na kasumba na kuuza mazao na kuamua kuoa wanawake wengine matokeo yake mnaacha watoto wakiteseka,mnasahau hadi majukumu ya kuwalea na kuwasomesha matokeo yake watoto hawa wanaanza kuiga tabia za makundi mabaya”,alisema Mweyo. 

“Mtoto anahitaji mapenzi ya baba na mama,ndoa inaposambaratika watoto wanakosa pa kwenda,wengine wanaamua kuacha hata kwenda shule na kujiunga kwenye makundi yasiyofaa,mbaya zaidi wanaume wakipata mke mpya wa kwanza anamsahau,anasahau hadi kuwapatia haki watoto wake”,alieleza Mweyo. 

Aidha aliwashauri wananchi kuwa mstari wa mbele kubadilisha mila na desturi zisizofaa katika jamii ikiwemo kurithi wajane, kuozesha watoto na kutopeleka watoto shule akieleza kuwa mabadiliko yataletwa na wao wenyewe. 

Afisa mradi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana kutoka Shirika la Agape unaofadhiliwa na shirika la Sida la nchini Sweden, Lucy Maganga aliwaomba viongozi wa jamii kufanya kazi ya kutokomeza mila na desturi kandamizi kwa weledi ili kuondoa ukatili dhidi ya watoto na wanawake. 

Kwa upande wao,viongozi hao wa jamii walilishukuru shirika la Agape kwa kuwafikia na kuwapatia elimu ya kukabiliana mila na desturi kandamizi huku wakisema hivi sasa jamii ya Usanda imebadilika na matukio ya mimba na ndoa za utotoni yamepungua. 

“Tumeendelea kutoa elimu kwa jamii,kwa kweli mwitikio umekuwa mzuri ,na sasa ile kasumba ya kwamba baba ndiyo kila kitu katika familia imeisha”,alisema Juma Katabuka kutoka Shabuluba. 

“Hivi sasa jamii imeanza kuacha tabia ya kurithi wajane kwani imeshatambua madhara yake kwani huko ni kumfanyia ukatili mwanamke lakini pia ni chanzo cha maambukizi ya magonjwa ya zinaa ukiwemo UKIMWI,kwani huwezi kujua marehemu alifariki kwa ugonjwa gani”,alisema Ramadhan Kulwa ambaye ni mwenyekiti wa Kitongoji cha Mwagala. 

Naye Singu Njegi kutoka kitongoji cha Munge alisema kutokana na elimu waliyopata wataendelea kuzifikia kaya na makundi mbalimbali ili kila mtu atambue mila na desturi kandamizi zinachangia ukatili dhidi ya wanawake na watoto. 
Afisa Mtendaji wa kata Usanda Emmanuel Maduhu akizungumza wakati wa kikao cha mrejesho wa kazi zilizofanywa na viongozi wa jamii kata ya Usanda kilichofanyika leo katika shule ya msingi Shingida. Maduhu alisema Shirika la Agape limesaidia kwa kiasi kikubwa kupungua mimba na ndoa za utotoni katika eneo hilo- Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Afisa mradi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana kutoka Shirika la Agape Lucy Maganga akiwahamasisha viongozi wa jamii kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za watoto na wanawake ambao wamekuwa waathirika wakubwa wa mila na desturi kandamizi katika jamii.
Viongozi wa jamii wakiwemo viongozi wa kimila na Wazee maarufu kata ya Usanda wakimsikiliza afisa mradi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana kutoka Shirika la Agape Lucy Maganga.
Afisa mradi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana kutoka Shirika la Agape Lucy Maganga akizungumza wakati wa kikao hicho. 
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Elizabeth Mweyo akiwataka viongozi wa jamii kuwakumbusha wanandoa kuvumiliana ili familia zisitawi vizuri kwa maslahi ya kulinda haki za watoto kwani ndoa zinaposambaratika watoto wengi hukosa mwelekeo wa maisha matokeo yake wanajiingiza kwenye makundi yasiyofaa.
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Elizabeth Mweyo akizungumza katika kikao hicho.
Mzee Singu Njegi kutoka kitongoji cha Munge akitoa mrejesho wa kazi anazofanya kutokomeza mila na desturi kandamizi katika jamii.
Kikao kinaendelea.
Kaimu Mwenyekiti wa kitongoji cha Kanyenye,Daudi Michael akielezea namna anavyohamasisha wazazi kupeleka watoto shule.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Nzega kijiji cha Shigita,Mwinyi Albinus akielezea namna anavyoendelea kuielimisha jamii kuachana na mila na desturi kandamizi zinazochangia ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Kikao kinaendelea.
Mwakilishi wa kundi la watu wenye ulemavu Mayunga Mayunga akielezea jinsi anavyotoa elimu kwa jamii kuachana na ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Washiriki wa kikao hicho wakiwa ukumbini.
Mwakilishi wa kundi la vijana,Suzana Amos kutoka kitongoji cha Munge akielezea jinsi anavyotoa elimu kwenye kaya mbalimbali kuhusu madhara ya mila na desturi kandamizi.
Simon Makenza kutoka Nzagaluba akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
Muelimisha rika kata ya Usanda,Hamis Malundi akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mwagala, Ramadhan Kulwa akizungumza wakati wa kikao hicho.
Ng'wanzalima Malimi kutoka kitongoji cha Buchamike akizungumza wakati wa kikao hicho cha viongozi wa jamii.
Afisa Ustawi wa Jamii kata ya Usanda, Halima Tendeja akifunga kikao cha mrejesho wa kazi za viongozi wa jamii katika kutokomeza mila na desturi kandamizi. Tendeja alitumia fursa hiyo kuwakumbusha wanaume kushauriana na wenza wao kupanga uzazi kwani bado baadhi ya wanawake wamekuwa wakiogopa kupanga uzazi kwa kuogopa waume zao.

LUKUVI AONYA WENYEVITI WA MITAA MAUZIANO YA ARDHI

$
0
0
Na Munir Shemweta

Waziri wa Adhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William lukuvi amewaonya wenyeviti wa Serikali za Mitaa kutojihusisha na masuala ya uuzaji ardhi katika maeneo mbalimbali kwa kuwa hapaswi kisheria kufanya kazi hiyo.

Lukuvi alitoa onyo hilo jana wakati alipokwenda kusuluhisha mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa Kikwajuni Vijibweni maarufu kama kwa Mkorea wilayani Kigamboni mkoa wa Dar es Salaam na Mwekezaji ‘Registered Trustee of Korea Church Mission’ katika eneo hilo la ukubwa wa ekari 305.

Lukuvi alisema sheria ya ardhi haisemi kama wenyeviti wa mitaa wanaruhusiwa kusimamia uuzaji ardhi na kusisitiza kuwa wenyeviti hao hawana mamlaka ya kufanya hivyo na mwenye jukumu la kusimamia masuala ya ardhi katika miji ni halmashauri za mji au Manispaa.

Waziri wa Ardhi alisema mtu yeyote atakayeuziwa ardhi kupitia wenyeviti hao wa mitaa au mtu mwingine asiyetambuliwa kisheria basi atakuwa ameuziwa ‘bomu’ na kuwataka wananchi kuwa makini na suala hilo na kuwashauri kabla ya kununua eneo lolote ni vyema wakaiuliza mamlaka husika iwapo eneo husika limepangwa kwa matumizi ya aina gani ili kuepuka kubomolewa.

‘’Ukitaka kununua kiwanja kwanza kaulize Manispaa maana unaweza kununua eneo kumbe ni la kuzikia kwani manispaa ndiyo inayojua kama eneo hilo ni salama’’ alisema Lukuvi

Katika hatua nyingine, Waziri Lukuvi ametoa siku kumi kwa halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam kufanya uhakiki kwa wananchi wote wanaoishi eneo lenye mgogoro na Mwekezaji la Kikwajuni Vijibweni Kigamboni maarufu kwa Mkorea ili kupata taarifa sahihi za wananchi hao.

Aidha, amemtaka Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Dar es Salaam Methew Mhonge kupata nakala ya hukumu ya kesi ya wananchi hao dhidi ya Mwekezaji ‘Registered Trustees Korea Church Mission’ inayoonesha kuwa wananchi wa eneo hilo wameshindwa kesi na wanatakiwa kuondoka.

Maagizo hayo ya Lukuvi yanafuatia kuelezwa na wananchi 22 wa Kikwajuni kupitia mwakilishi wao Meja Mstaafu Peter Ismail kuwa haki haikutendeka wakati wa zoezi la ulipaji fidia kwa wananchi wa eneo hilo jambo lililosababisha kukataa kuchukua fidia na wengine 6 kudai nyongeza ya fidia huku wananchi 95 wakilalamika.

Meja Mstaafu Ismail alisema, wao walichukua uamuzi wa kutokubaliana na mwekezaji aliyetaka kuwafidia laki nne kwa ekari moja wakati wao walitaka kulipwa shilingi milioni moja kwa ekari moja na kufafanua kuwa kilichowashangaza ni Mwekezaji kulipa fidia mwaka 2015 wakati zoezi hilo lilitakiwa kufanyika miezi sita baada ya Agosti 2004.

Kwa upande wa wananchi sita wanaotaka kuongezewa fidia wananchi hao kupitia mwakilishi wao Hamza Rashid walidai kesi yao iliamuliwa kupatiwa taarifa halisi ya uthamni na siyo nakala kama walivyofanyiwa jambo walilolieleza kuwa halikufanyika.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Lukuvi aliagiza taarifa zote muhimu zipatikane kipindi cha siku kumi ikiwemo Mwekezaji kuwasilisha mpango wa jinsi atakavyolitumia eneo hilo la ekari 305 sambamba na chanzo cha mtaji wa uwekezaji huo.

Eneo la Kikwajuni Vijibweni maarufu kwa Mkorea kwa muda mrefu tangu mwaka 2004 limekuwa na mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa eneo hilo na Mwekezaji ‘Registered Trustees Korea Church Mission’ anayetaka kujenga chuo Kikuu.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na Wakazi wa Kikwajuni Vijibweni wilaya ya Kigamboni alipokwenda kutatua mgogoro kati ya Mwekezaji Registered Trustees Korea Church Mission  jijini Dar es Salaam jana.
 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi  akitembea kuelekea eneo lenye mgogoro kati ya Wananchi wa Mkwajuni Vijibweni wilaya ya Kigamboni maarufu kama kwa Mkorea na Mwekezaji wakati alipokwenda kutatua mgogoro katika eneo hilo jana.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akimsikiliza mwananchi wa Mkwajuni Vijibweni  Mariam Kange alipokwenda kuatatua mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa eneo hilo maarufu kwa Mkorea na Mwekezaji Registered Trustees Korea Church Mission (PICHA NA WIZARA YA ARDHI)

HALMASHAURI ZATAKIWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MASOKO NCHINI

$
0
0
Afisa Mradi wa kupinga ukatili wa Kijinsia katika masoko ya Mbagala Rangitatu na Kampochea ujulikanao kama Mpe Riziki si Matusi, Shabani Rulimbiye (kushoto), akitoa mada wakati akitoa mafunzo ya namna ya kujikinga na ukatili wa kijinsia kwa maofisa wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Mafunzo hayo ya siku moja yaliandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG).
Afisa Ustawi wa Jamii, Getruda Nyagabona (kushoto) kutoka Manispaa ya Temeke akizungumza katika semina ya siku moja ya namna ya kupinga ukatili wa kijinsia masokoni iliyoandaliwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Ustawi wa Jamii, Magrida Mumba.
Washiriki wa semina hiyo wakifuatilia mada kwa makini.
Mwenyekiti wa Soko la Kampochea, Hemed Said Njiwa akichangia jambo. 
Majadiliano katika makundi.
Majadiliano wa kazi za makundi.
Ofisa Mtendaji wa Mbagala Rangitatu, Morris Ssendi (kushoto), akichangia jambo wakati wa kazi za makundi.
Afisa Ustawi wa Jamii, Magrida Mumba, akichangia jambo.
Katibu wa Soko la Mbagala Rangitatu, Frank Mapolu akichangia jambo kwenye semina hiyo.


Na Dotto Mwaibale


HALMASHAURI za miji zimetakiwa kuboresha miundombinu ya masoko kwa kuwa yanachangia asilimia kubwa ya pato la Serikali za mitaa nchini.

Ombi hilo limetolewa na Afisa Mradi wa kupinga ukatili wa Kijinsia katika masoko ya Mbagala Rangitatu na Kampochea ujulikanao kama Mpe Riziki si Matusi, Shabani Rulimbiye unaoendeshwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) wakati akitoa mafunzo ya namna ya kujikinga na ukatili wa kijinsia kwa maofisa wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Maofisa walionufaika na mafunzo hayo ni maofisa ustawi wa jamii,maendeleo ya jamii, watendaji wa kata, askari polisi kutoka dawati la jinsia na viongozi `wa masoko. 

Alisema masoko mengi ambayo yanaendeshwa na sekta binafsi ambayo imetoa ajira mara tano ya ajira zilizo sekta rasmi na kuokoa wanawake wengi na watoto wao miundombinu yake ni mibovu na hayajawekewa sera na usimamizi wa kisheria kuanzia mazingira ya kazi, kipaumbele kwa makundi maalumu na zaidi ukatili wa `kijinsia `uliokithiri.

"Pamoja na kua ni kimbilio la wahanaga wa mfumo dume, sekta hii pia ni chachu kubwa sana ya maendeleo ya mwanannchi binafsi, serikali za mitaa na Taifa kwa ujumla ambapo takwimu zinaonesha kuwa Halmashauri zinategemea zaidi masoko kwa kuchangia kipato" alisema Rulimbiye.

Aliongeza kuwa pamoja na sekta hii isiyo rasmi kuwa ni chanzo kikubwa cha ajira na kuchangia asilimia kubwa ya pato la Taifa, mazingira yake yanafanywa kama chaka la utovu wa nidhamu na wahanga wakubwa ni wanawake, ambao ni wengi ambao pia wakati mwingine hujumuika na watoto wao.

Afisa Ustawi wa Jamii, Getruda Nyagabona alisema kesi nyingi za ukatili wa kijinsia zimekuwa zikitatuliwa kwa ushiriano baina yao na viongozi mbalimbali kuanzia ngazi ya chini jambo ambalo limesaidia kupunguza vitendo hivyo.

KAMPENI YA JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA IMEZINDULIWA MKOANI ARUSHA

$
0
0

Na.Vero Ignatus,Arusha.

Uzinduzi wa kampeni ya jiongeze tuwavushe salama umefanyika mkoani Arusha ikiwa na lengo la ''Kupunguza vifo vitokananvyo na uzazi'' na kuhakikisha mama na mtoto wanakuwa salama kabla na baada ya kujifungua.

Akizungumza katika uzinduzi huo mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa watendaji wote wa wizara ya afya ngazi ya mkoa watende kazi kwa weledi ili waweze kupunguza vifo vya wakina mama wakati wa kujifungua ambapo kwa ngazi ya mkoa ni 40%na Kitaifa ni 28%

Kampeni hiyo iliyobeba Kauli mbiu isemayo''Jiongeze Tuwavushe Salama''na Maudhui yasemayo '' Kila mmoja wetu anao wajibu wa kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi, maneno basi, sasa vitendo''

Amesema kuwa kampeni hiyo ni ya muhimu kwani inakwenda sambamba na lishe kwa mama mjamzito ili aweze kujifungua salama na mtoto atakayezaliwa awe mwenye afya njema,''Mwanaume ni wajibu wako kutambua kuwa mwanamke anapokuwa mjamzito ndio wakati wako wa kuwa karibu na mkeo, msindikize Kliniki, pimeni afya pamoja leeni mimba pamoja na mtoto akizaliwa mtamfurahia''. Alisema Gambo.

Ameainisha sababu kuu ambazo zinasababisha vifo kwa akina mama wajawazito ni pamoja na mama kutohudhuria kliniki mapema,kutokwa damu nyingi wakati wa kujifungua na baada ,shinikizo la damu.Amesema lishe duni imekuwa sababu kubwa ya wakina mama kujifungua watoto njiti ambapo pia vifo vya watoto hao ni 25 kati ya kila vizazi hai 1000husababishwa na kushindwa kupumua na wengine kuzaliwa kabla ya wakati.

Kwa upande wake Daktari mkuu wa mkoa Wedson Sichalwe amesema Tafiti zilizofanyika mwaka 2015/2016 zinaonyesha kiwango cha vifo vitokanavyo na uzazi ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 ambayo ni sawa na vifo 11,000 kila mwaka,sawa na wanawake 30 hufariki kila siku, kutokana na matatizo yatokanayo na uzazi.

Dkt. Sichalwe ameainisha kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni ukosefu wa dawa lishe,ukosefu wa virutubisho ambavyo hupelekea matatizo kwa mtoto akiwa tumboni hata kuzaliwa njiti au akiwa amefariki.Dkt amesema hiyo changamoto ya lishe katika mkoa imesababisha watoto wengine kuzaliwa wakiwa na udumavu halo inayopelekewa kuja kuwa na taifa lenye watoto wengi wenye tatizo hilo endapo hatua za haraka hazitachikiliwa.

Baadhi ya washiriki na wadau wa afya akiwemo Dkt. Emmanuel Maeda amesema swala la elimu kwa jamii ni changamoto hivyo wao wamekuja na kitu kiitwacho Vunja ukimya kwaajili ya kumkumbusha mwanaume kutambua wajibu wake pale mke anapokuwa mjamzito.

'' Mwanamke anapokuwa mjamzito inamuhitaji mwanaume kuelewa, anapaswa atambue mama mjamzito anahitaji lishe bora ili ajifungue salama, ikiwa kwenda pamoja kliniki na kutambua changamoto anazopitia na siyo wao kukaa pembeni na kusema kwani mimi ndo nimebeba mimba''alisema Dkt. Maeda.

Nae Munga kutoka Japayco nae alishauri kuwa kuwepo na siku ya afya vijijini ina lazima juhudi ziongezwe kuhakikisha kuangalia zaidi mama na kichanga anavuka salama na kila mjamzito lazima aende kliniki na hospitali kujifungua.

Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama ilizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan 6Novemba 2018 mkoani Dodoma. ampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama inatekelezwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Mashirika yasiyo ya kiserikali ikiwemo UNICEF.
 Baadhi ya washiriki na wadau wa Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama wakiwa katika uzinduzi huo
Katibu Tawala wa Jiji la Arusha Richard Kwitega akizungumza katika Uzinduzi wa Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa Jijini Arusha.
  Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, akibadilishana jambo na Mganga Mkuu wa mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe kwenye Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama

MWENYEKITI TUGHE PWANI AFANYA ZIARA BAGAMOYO KUSIKILIZA NA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYAKAZI AMBAO NI WANACHAMA WA CHAMA HICHO.

$
0
0
NA ELISA SHUNDA,BAGAMOYO.

MWENYEKITI wa Chama Cha wafanyakazi wa Serikali na Afya (Tughe) wa Mkoa wa Pwani Ameanza Ziara ya Kutembelea Taasisi Mbalimbali za Wilaya ya Bagamoyo ambapo Kuna Wafanyakazi Ambao ni Wanachama Wao kwenye Chama Hicho kwa Ajili ya Kuwasikiliza,Kupokea Changamoto zao na Kuzitatua Pale Inapobidi kwa Haraka Zaidi.

Akizungumza na wafanyakazi wa taasisi ya sanaa Bagamoyo (Tasuba) baada ya kuwatembelea Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Pwani,Catherine Katele alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kutoa semina fupi juu ya mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) jinsi unavyofanya kazi zake katika kuwahudumia watumishi wa umma lakini pia kusikiliza kero na changamoto za wafanyakazi hao na kuzichukua kuzifikisha sehemu husika pamoja na kuwashukuru kwa kumchagua kuwa kiongozi wao kwa kipindi cha miaka mitano.

“Tangu nimechaguliwa nafasi hii sikuwahi kuja kuwatembelea ndugu zangu watumishi wenzangu wa serikali japo kuwashukuru kwa kunichagua kwa kura za kishindo lakini pia sikuja bure nimeongozana na wenzangu kutoka ngazi ya mkoa ambapo leo hii mtanufaika kwa kupata semina fupi juu ya mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) jinsi unavyofanya kazi katika kumsaidia mtumishi wa umma pindi anapopatwa na matatizo akiwa kazini pamoja na kusikiliza kero na changamoto zenu tuzibebe na tuzifikishe sehemu husika zishughulkikiwe;

“Kwa sasa katika taasisi nyingi kumekuwa na hali ya sintofahamu ambayo inaleta mkanganyiko katika kipindi cha kutoa mfanyakazi bora mfano katika taasisi yenu hii kuna wafanyakazi ambao wapo katika vyama vingine vya wafanyakazi ukiachia chama chetu cha tughe sasa muda ukifika badala ya kuangalia mfanyakazi gani ameiletea taasisi mafanikio kinachoangaliwa kila watumishi na vyama vyao wanavutia upande wao,mimi niseme hatuendi hivyo niwasihi tumchague mfanyakazi kwa manufaa aliyoiletea taasisi yake na ubora wa utendaji kazi wake” Alisema Mwenyekiti Katele.

Aidha Mwenyekiti Katele amewaambia uongozi wa tawi la Tughe katika taasisi ya Tasuba kuwa Viongozi wamehakikisha wanasimamia haki za wanachama wao kwa kuhakikisha asilimia 20% zao za matawi zinaanza kutolewa na madeni Yote ya Nyuma  yanalipwa.

 Hata Hivyo Katibu wa Tughe wa Mkoa wa Pwani,Shadrack Mkodo wakati akitoa semina kuhusu mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) kwa watumishi hao wa Tasuba aliwaambia kuwa kazi inaanzia unapotoka mlangoni kwako au getini unaanza kuhesabika upo kazini hadi unafika ofisini unasaini hadi muda wa kuondoka hadi unafika nyumbani kwako lolote litakalokutokea utahesabika umepatwa na tatizo hilo ukiwa kazini ila endapo utakutwa na tatizo ukiwa umekwenda sehemu nyingine tofauti na maelekezo ya kazi yako inavyosema utakuwa umepatwa na matatizo hayo nje ya kazi akatolea mfano kama ukiumia bar na kumbi za starehe.

Naye mmoja kati ya wafanyakazi wa Tasuba ambaye ni mwanachama wa tughe,Mkufunzi,Haji Maeda aliwashukuru uongozi wa chama cha wafanyakazi kwa mkoa wa pwani kufanya ziara hiyo ambayo kwa namna moja itasaidia kutatua kero na changamoto zao walau kwa kiasi na kuwaomba kuwatembelea mara kwa mara ili kuzidi kuwasaidia katika kutatua matatizo yanayowakabili pamoja na kuwapatie elimu juu ya stahiki na haki zao kama wafanyakazi.

Katika msafara wa Uongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (Tughe) Mkoa wa Pwani ambao ulikuwa ukiongozwa na Mwenyekiti wake,Catherine Katele na Katibu wake,Shadrack Mkodo pia uliambatana na Mwakilishi wa Vijana Mkoa wa Pwani Tughe,Dk.Christian Benedict,Katibu wa Tughe Mkoa wa Dar es Salaam,Litson Magawa,Mratibu Tughe Wilaya ya Bagamoyo,Timothy George Twalib,Mratibu Tughe Wilaya ya Kibaha,Dk.Baraka Makayo.








NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO MHE. ATASHASTA NDITIYE AFUNGUA BARAZA JIPYA LA WAFANYAKAZI LA SHIRIKA LA RELI TANZANIA - TRC.

$
0
0
                                

Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe, Mhandisi Atashasta Nditiye afungua rasmi Baraza jipya la wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania - TRC katika ukumbi wa Bandari jijini Dar es Salaam hivi karibuni Aprili 2019.                                                       

Hafla hiyo ya ufunguzi wa Baraza la  wafanyakazi TRC kwa mara ya kwanza 
tangu kuunganishwa kwa iliyokuwa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli – RAHCO na kuanzishwa TRC.

Baraza jipya la wafanyakazi lina jukumu la kusimamia na kutetea maslahi ya wafanyakazi kupitia wawakilishi kutoka idara na vitengo vya taasisi pamoja na wajumbe wa kamati tendaji wanaotokana na wajumbe wa baraza.

kulingana na katiba ya baraza na taratibu za kisheria Baraza lina kazi ya kupitia na kutoa maoni na kuboresha utendaji wa Shirika,pia baraza ni chombo cha kuleta upendo na umoja baina ya wafanyakazi.

Mgeni rasmi wa ufunguzi wa Baraza hilo naibu waziri Mhe. Atashasta Nditiye amelipongeza Shirika la Reli Tanzania kwa kufanya uamuzi huo wa kuundwa Baraza jipya na kuwataka wajumbe kulifanya Baraza kama sehemu wa kuwawakilisha wafanyakazi kwa lengo la kutatua matatizo changamoto  na kuleta tija katika Shirika.    
      
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania - TRC alisema kuwa serikali inafuatilia Mali za Shirika ambazo zinamilikiwa na watu binafsi wamejibinafisha kwa njia zisizo halali na kuomba wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania kushirikiana katika kutoa taarifa sahihi ili rasilimali hizo zirudi kuongeza mapato kusaidia kuendesha Shirika ikiwemo kuinua maslahi ya wafanyakazi.


Naibu waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe, Mhandisi Atashasta Nditiye akifungua rasmi Baraza jipya la wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania - TRC katika ukumbi wa Bandari jijini Dar es Salaam hivi karibuni Aprili 2019.


Picha tofauti za matukio katika Hafla ya ufunguzi wa Baraza la kwanza la wafanyakazi TRC tangu kuunganishwa kwa kampuni mbili zilizokua TRC,yaani Kampuni ya Reli Tanzania(TRL) na kampuni hodhi ya Reli (RAHC
O)

ILALA YATOA MKOPO KWA BILIONI 1.7/-, DC MJEMA AWATAKA WALIOPEWA KUREJESHA KWA WAKATI

$
0
0

*Pia kuna mikopo ya Bajaji, bodaboda ili kuinua maisha ya wananchi

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

HALMASHAURI ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam imetoa mkopo wa Sh.bilioni 1.7 kwa vikundi 295 kwa lengo la kuwajengea uwezo kiuchumi, huku Mkuu wa Wilaya hiyo Sophia Mjema akiwataka waliopewa mkopo huo kurejesha kwa wakati ili wengine nao wakopeshwe.

Kwa mujibu wa Ilala utolewaji wa mkopo huo wa fedha kwa wananchi uliokwenda sambamba na utoaji wa mikopo ya bajaji 30 na bodaboda 29, ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ambayo inazungumzia kuwawezesha wananchi kiuchumi .

Pia imeelezwa ni mkakati wa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli iliyodhamiria kuinua maisha ya wananchi wanyonge kwa kuwajengea uwezo wa kiuchumi.

Akizugumza leo Aprili 17, 2019 wakati wa kukabidhi mkopo huo kwa vikundi 295, Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema amesema waliopewa mkopo huo wanapaswa kurejesha kwa wakati ili wengine nao wakope na kwa kufanya hivyo wananchi wengi watakuwa wameinuka kiuchumi.

"Leo hii Wilaya ya Ilala tumetoa mkopo wa fedha wenye thamani ya Sh.bilioni 1.7 kwa alili ya kukopesha vikundi mbalimbali ndani ya Wilaya yetu.Hata hivyo lengo letu ni kutoa mkopo zaidi na kati ya Mei na Juni mwaka huu tutatoa tena mkopo wenye thamani ya Sh.bilioni mbili na lengo letu ni kutoa Sh.bilioni nne.

"Mbali ya kutoa mkopo wa fedha, tumetoa mkopo wa bajaji, pikipiki na mkopo wa vifaa vya kilimo kulingana na mahitaji ya vikundi ambavyo vimepwa mkopo huu.Kazi yetu kubwa wasaidizi wa Rais wetu mpendwa ni kutimiza ndoto zake ambazo anataka kuona wananchi wa hali ya chini wanakuwa na maisha mazuri.

"Hivyo kitendo cha kutoa mkopo huu Ilala tunakwenda kuinua maisha ya wananchi wetu, tunaamini wapo ambao wamepata mkopo huu na baada ya kipindi kifupi watakuwa matajiri wakubwa,"amesema Mjema.

Ametoa rai kwa wananchi kuendelea kumuombea Rais Magufuli awe na maisha marefu na hatimaye aweze kutimiza ndoto zake za kuwaletea maendeleo Watanzania wote na kwamba Ilala itaendelea kuweka mikakati ya kuendelea kuinua maisha ya wananchi.

Mjema amesema viongozi wa Chama na Serikali wameungana na wataendelea kufanya kazi kwa bidii. "Kila jambo ambalo linafanyika katika taifa hili yamo kwenye Ilani ya uchaguzi. Kutoa bajaji, boda boda ,kutoa mikopo ya fedha ni utekelezaji wa Ilani".

Wakati huo huo Mjema amesema Rais Magufuli anawapenda Watanzania na kwamba alianza kutoa vitambulisho vya wajasirimali na sasa wanatamba na kuwataka waendelee kutamba na kwamba mikopo iliyotolewa haina riba. 

Awali Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam amesema kuwa jumla vikundi 295 vimenufaika na mkopo huo na kwamba wataendelea kutoa na kwamba wamejipanga kutoa Sh.bilioni nne licha ya kwamba leo tayari wametoa Sh.bilioni 1.7.

"Hadi sasa jumla ya 3, 209 wanafuika na mkopo ambao umetolewa na kati ya hao wanawake ni 2, 744 na kwa upande wa vijana ambao wamenufaika hadi sasa ni 332.Hata hivyo tunaamini waliokopeshwa bajaji na pikipiki watarudisha fedha kwa wakati,"amesema.

Ameongeza mikopo inalenga kupunguza umasikini wa kipato kwa wananchi wa Manispaa ya Ilala na kufafanua kuna vikundi ambavyo vimeomba mikopo ya vifaa vya kilimo.Pia kutokana na mkopo huo wapo ambao wamekopa kwa ajili ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo , hivyo matarajio ni kuanzishwa viwanda vidogo 150 ndani ya Wilaya hiyo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema akijiandaa kukabidhi bodaboda ambazo zimetolewa na wilaya hiyo ili kukopesha wananchi.Mikopo hiyo ya bodaboda imetolewa leo viwanja vya Mashujaa Mnazi Mmoja
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema(wa pili kushoto) akifurahia jambo baada ya kutoa hutuba kwa vikundi mbalimbali ambavyo vimekabidhiwa mkopo wa bajaji,bodaboda na fedha
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akiwa amepakizwa kwenye pikipiki baada ya kukabidhiwa kwa vikundi ambavyo vimepewa mkopo wa bodaboda
 Viongozi wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Sophia Mjema wakicheza muziki kabla ya tukio la kukbidhi mkopo kwa wananchi ambao wamejiunga kwenye vikundi mbalimbali
 Bajaji ya mkopo iliyotolewa na Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam ikiwa na ujumbe maalum kuhusu bajaji hizo ambazo ni za mkopo
 Sehemu ya wananchi wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakicheza muziki wakati wa utolewaji wa mikopo ambapo baadhi ya wamepata mkopo wa fedha, bajaji na bodaboda
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam wakiwa katika moja ya bajaji ambayo ni ya mkopo iliyotolewa na wilaya hiyo

MGONJWA MARIAM RAJAB WA SINGIDA AWASILI MUHIMBILI KWA MATIBABU.

$
0
0
Mariam Rajab (25), mkazi wa Singida ambaye video yake imesambaa kwenye mitandao ya kijamii akiomba msaada wa matibabu, amewasili saa 6:00 usiku huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Hivi sasa Mariam amepokelewa katika Idara ya Magonjwa ya Dharura ambapo anaendelea kufanyiwa vipimo vya awali na kisha atalazwa ili aweze kuonana na jopo la madaktari bingwa wa upasuaji kwa ajili ya kupatiwa matatibu Zaidi siku ya Alhamisi.

“Mimi naitwa Mariam Rajabu naishi katika Mkoa wa Singida, Mtaa wa Mnung’una naishi katika familia ya kimasikini, wazazi wangu hawana uwezo wa kunisaidia tatizo langu, tatizo ambalo ninalo, tatizo lenyewe ambalo ninalo ni kidonda ambacho kipo hapa mgongoni, naombeni Watanzania wenzangu muweze kunisaidia niweze kwenda Hospitali ya Muhimbili ili niweze kupata matibabu. Sina cha kuwalipa bali Mungu atawalipa, asanteni” hayo ni maelezo aliyotoa Mariam kupitia picha ya video iliyoanza kusambaa katika mitandao ya kijamii mwanzoni mwa wiki hii.

Kutokana na taarifa hiyo, Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (MB) aliuagiza Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kumtafuta Mariam ili apelekwe Hospitalini hapa kwa ajili uchunguzi na matibabu.

Mariam ameletwa na gari la wagonjwa (ambulance) kutoka Singida lililoanza safari yake saa 8:00 mchana jana. Tutaendelea kuwapa taarifa juu ya mwenendo wa matibabu yake.

Betri la kuongoza Taa barabarani latia hasara serikali kiasi cha shilingi Milioni Tatu

$
0
0
Na Editha Edward- Tabora

Zaidi ya shilingi Milioni Tatu zimetumika  kununua betri la kuongozea taa za barabarani lililoibiwa katika makutano ya barabara la isevya wilaya ya Tabora mjini mkoani Tabora, Jambo ambalo limesababisha hasara kwa serikali ili hali fedha hiyo ingetumika kwa maendeleo mengine

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kitengo cha barabarani TANROADS Raphael Mlimaji amesema wizi wa betri hiyo imesababisha kusimama kwa kutumika Taa katika eneo husika,jambo ambalo limesababisha  ongezeko la ajali za barabarani

"Hii hasara imesababishwa na mtu mmoja lakini pia imeaathiri wananchi, Kati yetu wanamfahamu na nchi inataka kusonga mbele mnarudisha nyuma ni kinyume cha Sheria"Amesema Mlimaji

Naye kamanda wa jeshi la polisi wilaya ya Tabora John Mfinanga amesema kila mwananchi awe mlinzi wa mwenzake ili kuweza kuwafikisha wahalifu kwenye vyombo husika ili  kuweza kuimarisha usalama katika jamii

"Unapo iba vifaa vya barabarani si kwa kuikomoa serikali bali unakomoa wananchi wote ni vyema tushirikiane kuwafichua wezi hawa kwani wanarudisha nyuma maendeleo ya mkoa wetu"Amesema Mfinanga

Aidha Kamanda wa usalama barabarani Ame     Malawi,amewataka wananchi mkoani Tabora kufuata Sheria za barabarani ili kuweza kusaidia kuondokana na ajali za Mara kwa Mara.


Kamanda wa Jeshi la polisi wilaya ya Tabora, John Mfinanga
 

MAGAZETI YA LEO AL HAMISI ,APRIL 18,2019

WATUMISHI WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO WATAKIWA KUBORESHA ZAIDI MIFUMO YA UKUSANYAJI MAPATO YA SERIKALI

$
0
0
Na Farida Ramadhani & Josephine Majura. WFM, Dodoma
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji , amewataka  Watumishi wa Wizara hiyo kuendelea kuboresha mifumo ya ukusanyaji mapato ya ndani na kupanua wigo wa walipakodi pamoja na kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato kutoka vyanzo mbalimbali. 
Dkt. Kijaji ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika katika Ukumbi wa Kambarage, wizarani hapo.
Alisema Wizara ya Fedha na Mipango imebeba majukumu ya  kuhakikisha kuwa mapato ya Serikali na matumizi ya rasilimali fedha yanasimamiwa kikamilifu.
 “Watendaji na watumishi wote wa Wizara wanawajibu wa kuimarisha mifumo ya usimamizi wa fedha na ufuatiliaji wa matumizi ili kuhakikisha rasilimali fedha zilizopo zinatumika kwa ufanisi” ,alisema Dkt. Kijaji.
Alisema ni jukumu la Watumishi wa Wizara kugawa rasilimali fedha kwa kuzingatia vipaumbele vilivyoainishwa kwenye Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016-2021)  wenye dhima ya kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na maendeleo ya watu.
Aliwataka Watumishi  kufanyakazi kwa ushirikiano, umoja , mshikamano, ufanisi  na uadilifu kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali iliyopo.
“Ni wajibu wetu pia kutumia busara na hekima, hususan pale tunaposhughulikia maslahi ya watumishi na wananchi kwa ujumla”, alisisitiza Dkt. Kijaji.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo ambaye pia ni  Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi, Bw. Doto James, amemhakikishia Dkt. Kijaji kuwa watatekeleza maelekezo yote aliyoyatoa kwa haraka na ukamilifu kwa maendeleo ya nchi kwa kuwa Wizara hiyo ni nguzo ya kusimamia uchumi wa nchi.
Alisema uzoefu unaonesha kwamba vikao vya Baraza la wafanyakazi vimekua na umuhimu mkubwa mahala pa kazi na kwa kuzingatia umuhimu huo Wizara ya Fedha na Mipango imehakikisha kuwa vikao vya Baraza vinafanyika kila mwaka kulingana na Mkataba kati ya Wizara na Chama cha Wafanyakazi cha Serikali na Afya (TUGHE).
Alisema kupitia Baraza la wafanyakazi Wizara imefanikiwa kuongeza mshikamano kati ya Wafanyakazi hivyo kuamsha ari kwa watumishi kufanya kazi kwa kushirikiana na Viongozi wa Serikali.

Aliongeza kuwa hoja mbalimbali zilizowasilishwa kwenye Baraza zimeboresha huduma kwa watumishi, kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ikiwemo kuwapatia watumishi vitendea kazi pamoja na kuwelimisha watumishi kuhusu magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu (BP), Kifua kikuu, HIV na UKIMWI.
Meza Kuu (waliyokaa) ikiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb),(watatu kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara hiyo wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo lililofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Bw. Doto James akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) kabla ya kuanza Baraza la Wafanyakazi wa Wazara hiyo lililofanyika katika ukumbi wa Kambarage Jijini Dodoma .
Meza Kuu ikiongozwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), (watatu kushoto) wakiimba wimbo wa kudumisha umoja kabla ya kuanza Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, Jijini Dodoma .
Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Fedha na Mipango wakiimba wimbo wa kudumisha umoja na mshikamano "solidarity forever" kabla ya kuanza Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo Jijini Dodoma .
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kushoto) akimtambulisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo aliyeteuliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kuapishwa hivi karibuni , Bw. Adolf Ndunguru, katika Baraza la Wafanyakazi wa Wazara hiyo , Dodoma.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi na Katibu Mkuu wa Waziri wa Fedha na Mipango, Bw.Doto James akitoa salam za utangulizi kwa mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani), wakati wa ufunguzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo lililofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Jijini Dodoma.
Sehemu ya Wajumbe walioshiriki Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani), katika ukumbi wa Kambarage Dodoma ambapo Watendaji wa Wizara walitakiwa kutekeleza jukumu la kugawa rasilimali fedha kwa kuzingatia vipaumbele vilivyoainishwa kwenye Mpango wa Pili wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akizungumza wakati wa kufungua Baraza la Wafanyakazi, Jijini Dodoma, ambapo aliagiza Watendaji wa Wizara hiyo kuendelea kuboresha mifumo ya kukusanya mapato ya ndani ikiwa ni pamoja na kupanua wigo wa walipa kodi.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akipongezwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw.Doto James, baada ya kumaliza hotuba yake alipofungua Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo lililofanyika katika ukumbi wa Kambarage, Jijini Dodoma.

TIGO YAWAMWAGIA FEDHA TASLIMU MAWAKAWALA WAKE NCHI NZIMA

$
0
0

Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Mashariki Abbas Abdulrahman (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni moja Wakala wa huduma ya Tigo Pesa Shine Murtazah wa Iringa ambaye ni mmoja kati washindi wawili wa kanda hiyo waliojishindia zawadi za fedha taslimu kwenye promosheni ya ‘Cash In’ iliyomalizika mwishoni mwa mwezi Machi. Tigo imetoa zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya Tshs 1m/- kwa Mawakala wa Tigo Pesa nchi nzima
Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Mashariki Abbas Abdulrahman (kulia) akiteta jambo na Wakala wa huduma ya Tigo Pesa Shine Murtazah wa Iringa ambaye ni mmoja kati washindi wawili wa kanda hiyo waliojishindia zawadi za fedha taslimu kwenye promosheni ya ‘Cash In’ iliyomalizika mwishoni mwa mwezi Machi. Tigo imetoa zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya Tshs 1m/- kwa Mawakala wa Tigo Pesa nchi nzima

Baadhi ya wafanyakazi wa Tigo Mkoa wa Iringa wakiwa katika picha ya pamoja na Wakala wa huduma ya Tigo Pesa Shine Murtazah ambaye ni mmoja kati washindi wawili wa kanda hiyo waliojishindia zawadi za fedha taslimu kwenye promosheni ya ‘Cash In’ iliyomalizika mwishoni mwa mwezi Machi. Tigo imetoa zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya Tshs 1m/- kwa Mawakala wa Tigo Pesa nchi nzima.
Meneja wa Tigo kanda ya Kusini Mashariki Abbas Abdulrahman akiagana na na Wakala wa huduma ya Tigo Pesa Shine Murtazah wa Iringa ambaye ni mmoja kati washindi wawili wa kanda hiyo waliojishindia zawadi za fedha taslimu kwenye promosheni ya ‘Cash In’ iliyomalizika mwishoni mwa mwezi Machi. Tigo imetoa zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya Tshs 1m/- kwa Mawakala wa Tigo Pesa nchi nzima
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images