Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

Miradi inayotekelezwa sio kikwazo cha mishahara kupanda kwa watumishi wa umma- Naibu Katibu Mkuu Dkt Francis

$
0
0

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

SERIKALI imesema miradi inayoendelea hivi sasa nchini si kikwazo kinachosababisha mishahara ya watumishi kutopanda.

Pia imesema tayari bodi ya watumishi imeshafanya tafiti zake za kuangalia  viwango vya mishahara kwa kila mtumishi na kuondoa utofauti uliopo kwa baada ya kupanda kila mtumishi atafufurahi.

Imesema kinachosubiriwa hivi sasa ni vikao vya pamoja kwa ajili yakujadili kuhusiana na ripoti hiyo na baadae iweze kupelekwa kwa Rais ili iweze kufanyiwa utekelezaji.Hayo yalisemwa jana na Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais Menegimenti ya Utumishi wa Umma Dkt.Francis Michael katika mkutano wa 25 wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA lililofanyika Mjini Bagamoyo mkoani Pwani.

Amesema Serikali ina lengo zuri la kutekeleza miradi ya maebdeleo ambayo inatija kubwa katika Taifa.Michael amesema miradi hiyo inatekelezwa na fedha za watanzania na miradi hiyo ni faida kwa watanzania ambao fedha zao zinatumika hivi sasa.

"Faida ya miradi ya maendeleo haiwezi kuonekana leo,lakini baada ya miaka kadhaa tutaona faida ya miradi hiyo,ijapokuwa miradi ya barabara tayari ishaanza kuleta faida na wananchi kuweza kufaidika.Katika mkutano huo,Dk.Michael aliupongeza  uongozi wa TPA kwa ufanyaji wake wa kazi kwa kuwa imekuwa ndio chanzo kikuu cha kuongeza mapato nchini.

Amesema shehena ndio kigezo kikuu cha uendelezaji wa Bandari ya Tanzania ambapo hivi sasa imeongezeka kutoka milioni 14hadi milioni 15.Dk Michael alilitaka Baraza hilo kushirikuana na uongozi wa TPA ili kuweza kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Baraza hilo .Mhandisi Deusdedit Kakoko amesema,TPA inaendelea kujiwekea malengo ambayo yatakuwa endelevu katika kulisaidia taifa na kukuza uchumi wake.Hata hivo Mhandisi Kakoko amesema dhumuni lao kubwa ni kuongeza shehena nyingi zaidi ili kuweza kuongeza mapato kwa taifa.

,,Uboreshaji wa bandari zetu nchini zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza shehena nyingi zaidi kutoka katika nchi mbalimbali kutokana na kupakana na nchi nyingi ambazo zinategemea bandari zetu"amesema Mhandisi Kakoko.

"Kila nchi inayopakana na bandari zetu za hapa nchini tutafanya nao mazungumzo ili mizigo yao wawe wanaipitisha katika bandari hizo na hilo linawezekana kutokana na mikakati waliojiwekea.
 Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) Mhandisi Deusdedit Kakoko akitoa utendaji wa mamlaka hiyo katika Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka hiyo uliofanyika Mjini Bagamoyo mkoani Pwani.
 Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari(TPA) Abraham Lukumay akitoa maazimio ya baraza hilo katika mkutano wa 25 uliofanyika mjini Bagamoyo mkoani Pwani.
 Naibu Katibu Mkuu Ofisi Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt Francis Michael akifungua mkutano wa 25 wa baraza la wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari uliofanyika Mjini Bagamoyo mkoani Pwani.
 Mgeni rasmi katika picha pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi Makao Mkuu
 Mgeni Rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi la TPA katika Mkutano wa 25 uliofanyika Mjini Bagamoyo mkoani Pwani.
 Baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi la TPA wakisikiliza taarifa mbalimbali za baraza


CHAMA CHA ADC CHAFANYA MKUTANO MKUU ZANZIBAR

$
0
0

-Mwenyekiti Taifa wa Chama cha lliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Hamad Rashid akisisitiza jambo alipokua akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Mwenyekiti Taifa wa Chama cha lliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Hamad Rashid akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Baadhi ya Wageni Waalikwa wavyama mbalimbali waliohudhuria katika Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha ADC uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)waliohudhuria katika Mkutano huo uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change (Dira ya Mabadiliko-ADC)Queen Althbat Sendiga akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Democratic Change(Diara ya Mabadiliko-ADC)Doyo Hassan Doyo akitoa hotuba ya makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho uliofanyika Hoteli ya Madinatul Bahri Chukwani Zanzibar.
….

NA Rahma Khamis Maelezo Zanzibar

Mwenyekiti wa Chama cha ADC Taifa Hamad Rashid Mohammed amewataka wanachama wa chama hicho kufuata ilani yao kwa vitendo ili kupambana na vitendo viovu ikiwemo rushwa na wizi uliyomo katika jamii.

Ameyasema hayo huko Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar katika Ukumbi wa Madinat Al Bahri wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama hicho.

Amesema msingi wa Mkutano huo unatokana na matakwa ya katiba ya ADC ambao ndio dira ya maendeleo ya wananchi katika kufikia malengo ya kuchagua viongozi ambao wanaweza na hatimae kushika dola.

Aidha amesema kuwa mkutano huo utawezesha kutambua changamoto zinazowakabili wanachama na kutoa mafunzo ya mara kwa mara ili kutatua changamoto hizo zinazowakabili. Mwenyekiti huyo amefahamisha kuwa umakini wa uongozi wa chama ndio msingi unaohitajika kwani ndio unaoleta maendeleo na kuweza kupata wanachama wapya ambao ndio watakaofikisha chama hicho kule wanakokuhitaji.

Akizungumzia suala la kisiasa amesema kuwa Duniani kote wanazingati a hali ya usalama na amani hivyo anazipongeza Serikali zote mbili kwa kudumisha amani na utulivu uliopo Nchini. Pia amefafanua kuwa ADC ina uwezo wa kusimamia hali ya usalama na amani na ndio mana imefanikiwa hadi leo kufikia Mkutano Mkuu wa chama Taifa na kuchagua Viongozi watakaoweza kusimamia na kuleta maendeleo.

Amesema kuwa suala la Bima ya Afya lazima lifanyiwe kazi ili kuwapunguzia wananchi gharama za matibabu sambamba na kufanikiSha afya bora kwa kila mwananchi. Hata hivyo Hamad Rashid anaunga mkono Serikali suala la elimu bure hadi kufikia chuo kikuu lakini kwa upande wao wamsema kuwa ni hatua kawa hatua hadi kufikia lengo hilo.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa chama ADC Queen Alithbert Sendiga amesema kuwa katika uchaguzi mkuu ujao 2020 anatarajia kugombea nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia ADC ili kuweza kuwainua wanawake kimaendeleo.

Aidha amefahamishakuwa wanawake wengi ndio wanaokuwa mbele katika kushiriki mambo mbalimbali laikini wanarudi nyuma kutokana na changamoto zinazowakabili ikiwemo mila na taratibu zinazowazuwia kugombea nafasi hizo.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRIL 15,2019.

CREDIT SUISSE BANK: TUTAENDELEA KUIKOPESHA TANZANIA KWA KUWA INAKOPESHEKA NA MAHILI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI

$
0
0
Na Benny Mwaipaja, WFM, Washington DC

Benki ya Credit Suisse ya Uingereza imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuikopesha Tanzania ili kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo baada kuridhishwa na uaminifu wa urejeshaji mikopo kwa wakati pamoja na ubora wa viwango vya miradi inayotekelezwa nchini.

Ahadi hiyo imetolewa Mjini Washington D.C nchini Marekani na Mkurugenzi wa Masoko ya Kimataifa wa Benki hiyo Bi. Elizabeth Muchemi, alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, katika mikutano ya kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha na Kimataifa inayoendelea Mjini, Washington D.C.

Bi. Elizabeth Muchemi amesema uzoefu unaonesha kuwa baadhi ya nchi zinazochukua mikopo hazitekelezi ipasavyo miradi iliyoombewa fedha jambo ambalo ni tofauti kwa Tanzania ambayo miradi iliyoombewa mkopo inatekelezwa vizuri na kwa viwango.

Hivi karibuni benki hiyo iliikopesha Tanzania mkopo wa dola za Marekani milioni 200 kwa ajili ya kutekeleza miradi mabalimbali ya maendeleo ikiwemo sekta miundombinu ya barabara na reli.

"Tuko tayari kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania kwa kadri Serikali itakavyoona kwa sababu ya mipango mizuri ya Serikali pamoja na kulipa madeni kwa wakati. Benki ya Credit Suisse haijawahi kuwa na tatizo na Tanzania katika urejeshaji wa mikopo jambo linaloongeza imani kwa Tanzania" alisema Bi. Elizabth Muchemi.

Akizungumza na Mwakilishi huyo wa Benki ya Credit Suisse katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, katika kikao kilichohudhuriwa pia na Gavana wa Benki Kuu Prof. Florens Luoga, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa utayari wake wa kuendelee kushirikiana na Serikali katika ugharamiaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema kuwa Taifa limejipanga kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo reli, barabara, umeme, maji, elimu, afya, mradi wa gesi kimiminika (LNG), usafiri wa anga na majini, bandari, elimu, ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanzania, mradi ambayo inahitaji uwekezaji mkubwa wa rasilimali fedha.

Dkt. Mpango amesema Tanzania inataka kutumia uwepo wa nchi zisizopakana na bahari kama vile Burundi, Uganda, Rwanda, na Jamhuri ya Congo kujenga mtandao wa reli ya kisasa na barabara utakao saidia kuchochea biashara na kukuza uchumi wa nchi na ukanda huo kwa ujumla.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens Luoga (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Masoko ya Kimataifa wa Benki ya Credit Suisse ya Uingereza Bi. Elizabeth Muchemi, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika Ubalozi wa Tanzania Mjini Washington ambapo Credit Suisse Bank imeahidi kuongeza mikopo kwa Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya kimkakati ya Serikali.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akiwa na Mkurugenzi wa Masoko ya Kimataifa wa Benki ya Credit Suisse ya Uingereza Bi. Elizabeth Muchemi, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika Ubalozi wa Tanzania Mjini Washington ambapo Credit Suisse Bank imeahidi kuongeza mikopo kwa Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya kimkakati ya Serikali.

DC KASESELA AWATAKA KKKT KUWA NA UMOJA ILI KUOKOA VYUO VYAO

$
0
0
MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiongea na wanafunzi na viongozi wa chuo kikuu cha Iringa waliokuwa kwenye mkesha wa kuabudu na kuomba na kuwataka waamini wote kujiandaa kabla hawajaanza kusali ili kuweza kuyafikisha maombi yao vilivyo kwa mwenyezi mungu. 
MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa kwenye picha ya pamoja na moja ya kwaya iliyota burudani siku hiyo ya mkesha wa kuabudu na kuomba
Baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuku cha Iringa wakiwa kwenye mkesha huo.


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MKUU wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela amewataka waamini wote kujiandaa kabla hawajaanza kusali ili kuweza kuyafikisha maombi yao vilivyo kwa mwenyezi mungu.

Akizunguza wakatika wa mkesha na kuambudu kwa wanafunzi wa chu kikuu cha Iringa mkoani Iringa Kasesela alisema kuwa wa kila jambo ambalo unatarajia kulifanya ni lazima ujiandae kwanza.

“Mimi katika maisha yangu kabla sijafanya jambo huwa natafuta muda wa kulifikiria jambo hilo ndio nalifanyia kazi ndio maana mara nyingi nimekuwa na maamuzi sahihi katika kufanya kazi zangu kila wakati” alisema Kasesela

Kasesela aliwataka wanafunzi hao kufanya maombi ya kukiombea chuo hicho ili kuendelea kuwa chuo bora hapa nchini na nje ya nchi na kuendelea kuutangaza mkoa wa Iringa kwa kuwa jina la chuo hicho limebeba jina la mkoa wa Iringa.

“Chuo hiki kilitaka kufungwa kwa ajili ya mambo ambayo hayana miguu wa kichwa hivyo naowaomba mkiombee chuo hiki ili kisije kikafungwa au kufikiriwa kufungwa tena maana kimekuwa kikitoa elimu iliyo bora sana” alisema Kasesela

Aidh Kasesela alisema kwanini kanisa la KKKT limekuwa kanisa ambalo limegawanyika katika kanda mbalimbali ambapo kila ukanda unafanya mambo bila kuwa na ushirikiano wowote ule na dayosisi nyingine.“Ukiangalia maisha ya viongozi wanaofanya kwenye kanda mbalimbali wanatofautiana kuanzia mishahara na maisha yao yamekuwa yanatofauti kubwa sana sasa nawaomba leo hii mliombee pia hili ili kanisa liwe na umoja” alisema Kasesela

Kasesela alisema kuwa mgawanyiko huo utasabisha vyou vingi vya KKKT kufa kutokana na kutokuwa na ushirikiano kama ilivyokuwa na vyuo vingine hapa.Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa,Blaston Gavile aliwataka wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa kukesha na kukiombea chuo hicho mara kwa mara.Ombeni nanyi mtapewa kwa kuwa mnaomna kwa nia njemba na mungu nimoto ambao unaweza kuwabariki kila mmoja wetu hapa hivyo nawaomba tena kuendelea kuomba” alisema Askofu Gavile

Askofu Gavile alimushukuru na kumpongeza mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela kwa utendaji wake wa kazi kwa wananchi wote kwa kuwa anaitendea haki nafasi hiyo anayoteuliwa na Rais.

SPIKA MSTAAFU ANNE MAKINDA AWAFUNDA TAWCA,AKUMBUSHA UTHUBUTU ,KUJIAMINI

$
0
0
 Spika wa Bunge mstaafu Anne Makinda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanawake Wahasibu nchini baada ya kufunga Mkutano wa Pili wa Taasisi ya Wanawake Wahasibu(TAWCA)
Spika wa Bunge Mstaafu Anne Makinda akikabidhiwa vipeperushi vya Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) baada ya kufunga mkutano wa Taasisi ya Wanawake Wahasibu nchini(TAWCA) uliofanyika jijini Dar es Salaam.TANESCO ndio waliofanikisha kufanyika kwa mkutano huo kwa kuamini utaleta tija katika maendeleo ya nchi hasa kwa kuzingatia ulilenga kuwajengea uwezo wanawake wahasibu
 
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SPIKA wa Bunge mstaafu Anne Makinda amewataka Taasisi ya Wanawake Wahasibu nchini( TAWCA)kujiamini,kuthubutu na kuwa na mtandao katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika shughuli za kimaendelo nchini.

Pia amewakumbusha TAWCA wahakikishe wanawajali wanawake wa hali chini kwa kuwajali na kuwasaidia kufanikisha ndoto zao pamoja na kuwaonesha upendo.

Makinda ameyasema hayo wakati anafunga Mkutano wa Pili wa TAWCA ambapo mkutano huo umefanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam .Wahasibu wanawake wa TAWCA wameshiriki mkutano huo.

"Niwapongeze sana TAWCA kwa namna ambavyo mmejadili mambo yenu na kutafuta ufumbuzi wa changamoto zilizopo mlipokuwa kwenye mkutano wenu kupitia mada ambazo zimetolewa.Kwa namna ambavyo mmejipanga na kwa mikakati yenu mtafika mbali sana.Ni wanawake wenye utalaam wenu ambao mnapanga mambo yenu na yanapangika.Hongereni sana," amesema.

Makinda ametumia nafasi hiyo kueleza wanachama wa TAWCA wana kilasababu ya kujiamini katika kufanya mambo ya maendeleo katika jamii yetu na kwamba pamoja na mambo mengine watambue kupanga muda katika kufanya jambo lolote ni jambo la msingi na lenya maana.

"Hakikisheni suala la muda mnalipa kipaumbele kinyume na hapo mambo hayatakwenda sawasawa.Muda ni muhimu katika kupanga maendeleo,pia tengenezeni mtandao ambao nao ni muhimu kwani huwezi kufanya maendeleo peke yako," amesema Makinda.

Kuhusu TAWCA kuwajali wanawake wengine na hasa wale wanaonekana wa hali chini,Mama Makinda amesema ni muhimu wanawake wa chini wakaoneshwa upendo kwani humsaidia kumpa faraja na kubwa zaidi kuhakikisha wanabeba ndoto zao na kuzifanyia kazi.

Wakati anazungumzia wanawake wa hali ya chini,ametoa mfano kwa wadada wanaofanya kazi za ndani ambapo amesema ni muhimu wakathaminiwa badala ya kuzarauliwa na wenye nyumba kisa tu anafanyakazi katika nyumba yako.

"Tuishi vizuri na hawa wanawake(wadada wa kazi) ambao tunaishi nao majumbani.Kwangu mimi huwa nashindwa kumuita dada wa kazi maana naona sitatenda haki.Hivyo Wanawake wahasibu na wanawake wengine kwa ujumla tambue thamani ya hao wadada.

" Wapendeni na kubwa zaidi hakikisheni mnatimiza ndoto zao kwani pamoja na kuwa wanafanya kazi za ndani nao kuna ndoto wanazo.Ukipenda dada wa kazi na kumjali hata ulinzi wa nyumbani mnaongezeka.Unaporudi nyumbani rudi na zawadi ya dada ,atakupenda na atafanya kazi zake kwa bidii,"amesema Makinda.

Kuhusu TAWCA ,Makinda amewema amefurahishwa na namna ambavyo wanawake wahasibu ambavyo wamejipanga kuhakikisha wanatimiza malengo yao na kwa mtazamo wake watafika mbali kikubwa ni kuyasimamia yale ambayo wanakubaliana na kuyaamua kupitia vikao vyao.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake Wahasibu Tanzania(TAWCA) Neema Kiure-Mssusa amesema kikao chao cha siku mbili kimekuwa na mafanikio nakubwa,hivyo kikubwa ni kuyatekeleza kwa vitendo yote ambayo wamekubaliana kama maazimio.

"Kikao chetu kimepata mafanikio makubwa,ndugu washiriki tukayafanyie kazi ambayo tumekubaliana.Pia tuwahakikishie tutaandaa notisi na kisha kuzisambaza kwa wanachama wetu kwa lengo la kukumbusha ambayo tumejadiliana.

" Niwahakikishie yale ambayo yanahitajika kutekelezwa lazima yatekelezwe kwa wakati. Na niwaombe huu ni wakati wa kuendelea kusoma,lazima tusome kwa bidii ili kuongeza maarifa.Kwa kuwa hatusomi hata watoto wetu wakiulizwa wanasema mama hasomi ila afanya kazi.Anajibu hivyo kwasababu hawatuoni tukisoma,hivyo tusome,"amesema.

Ameongeza wanatambua TAWCA wana maono yao mengi lakini moja ya maoni ni kuwa na benki ambayo itakuwa inatokana na Wanawake Wahasibu nchini na hilo watalitimiza.

WANAWAKE WAHASIBU NCHINI TANZANIA SASA WAJIPANGA KUANZISHA BENKI YAO

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

TAASISI ya Wanawake Wahasibu nchini( TAWCA)imesema moja ya malengo yao makuu ni kuhakikisha wanaanzisha benki yao siku za karibuni na wanaamini hakuna kitakachowakwamisha katika kufanikisha lengo hilo.

Akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa Pili wa TAWCA uliofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa TAWCA Neema Kiure-Mssusa amewaeleza washiriki zaidi ya 300 waliohudhuria mkutano huo kuwa lengo la kuanzishwa kwa benki litafanikiwa na mikakati waliyoiweka inakwenda vizuri.

"Kutokana na wingi wetu, tuliamua kuanzisha VICOBA na baada ya kuona mafanikio ni makubwa , tukahamia kwenye SACOSS na kwa namna tunavyokwenda ndoto yetu ni kwenda kuanzisha benki. Kikubwa ni kuendelea kushirikiana na kuhakikisha wote tunajiunga kwenye SACOSS ili kufikia lengo la kufungua benki,"amesema.

Kwa upande wake Katibu wa TAWCA Prisca Ndali amefafanua waliamua kuanzisha VICOBA ikiwa ni sehemu ya kuwawezesha wanachama wao kuwa na sehemu ya kutunza fedha na baada ya kuona ni nyingi walamua kuanzisha SACCOS na ndani ya miezi sita wakajikuta wamepata Sh.milioni 70.

"Kutokana na mafanikio ambayo tumeyapata, tukaamua sasa muelekeo wetu ni kuwa na benki yetu ya Wanawake Wahasibu.Kama tulianza na VICOBA na ndani ya muda mfupi tukawa na SACCOS, hivyo hivyo katika muda mfupi ujao unakwenda kuanzisha benki yetu na tukianzisha benki kuna faida nyingi ikiwemo ya kutoa ajira kwa wanawake wengine, katika mkutano wetu wa siku mbili tumezungumza namna ya kuwainua wanawake wengine, hivyo benki hii itasaidia kuwainua wengine,"amesema Ndali.

Amesisitiza kinachowapa matumaini ya kufanikisha lengo la kuwa na benki ni kwamba wamejipanga na wana kila kitu na hata benki itakapoanza hawatakuwa na tatizo katika kuiendesha na kuisimamia kwani wanao watalaamu waliobobea kwenye mambo ya fedha na uhasibu.

Ametumia nafasi hiyo kuendelea kuwahamasisha wana-TAWCA ambao hawajajiunga na SACCOS yao kujiunga kwani kadri wanavyoendelea kujitafakari ndivyo ambavyo wanajichelewesha kunufaika."Katika benki tunaamini haitapita miaka miwili tutakuwa na benki tayari, hivyo ambao hamjajiunga na SACCOS huu ni wakati wenu , jazeni fomu."
 Mmoja wa washiriki wa Mkutano wa Pili wa Taasisi ya Wanawake Wahasibu nchini(TAWCA) akifuatilia kwa makini hotuba ya Spika wa Bunge mstaafu Anne Makinda aliyekuwa amealiakwa kufunga mkutano huo uliofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam
Washiriki wa Mkutano wa Pili wa Taasisi ya Wanawake Wahasibu nchini(TAWCA)wakiwa katika mkutano wao ambapo pamoja na mambo mengine wamezungumzia kuanzishwa kwa benki ya wanawake wahasibu

TUCTA IWASHUGHULIKIE VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI WANAOKIUKA KATIBA- DKT FRANCIS MICHAEL

$
0
0


Na Hussein Stambuli, Morogoro..


Naibu katibu mkuu ofisi ya rais utumishi na utawala bora dr francis Michel amewataka viongozi wa umoja wa shirikisho la vyama vya huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) kuhakikisha wanawaondoa viongozi wa vyama mbalimbali vya wafanyakazi ambao wanakiuka katiba, miongozo na kanuni za vyama vyao badala yake wanaweka vipaumbele katika marumbano na migongano huku wakiacha kujadili mambo ya msingi kwaajili ya maendeleo ya wafanyakazi..

Akizungumza na kamati tendaji ya baraza kuu la shirikisho hilo katika kikao kilichokuwa na lengo la kujadili na kuchambua jinsi ya kuboresha shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini tucta, dr francis amesema viongozi wa vyama vya wafanyakazi wanatakiwa kutambua wanajukumu la kutetea maslahi ya wafanyakazi ambao wamewachagua na si masuala binafsi jambo ambalo litawafanya kupoteza wanachama wa vyama hivyo.

“ili kuachana na maslahi binafsi hakuna budi kwa viongozi kufuata katiba, miongozo na kanuni, sasa viko vyama ambavyo viongozi wao wanafanya vitu kwa maamuzi yao binafsi wakilala wakiamka anasema chama kitafanya hivi mara hii katiba haifai tubadili, mfumo huu unavuruga vyama watu wataondoka na chama kikikosa watu hakiendi na nikuombe rais na katibu mkuu tucta mnakazi kubwa si kuongoza tucta tu na kuongoza vyama kama kuna viongozi hawafai muwaondoe” amesema dr francis.

Aidha Rais wa umoja wa shirikisho la vyama vya huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Tumaini Nyamuhoka amesema licha ya serikali kuwa sikivu juu ya masuala mbalimbali ya wafanyakazi bado kuna wafanyakazi wa darasa la saba walioajiriwa tarehe 20 mei mwaka 2004 kwa baadhi ya maeneo wanakabiliwa na changamoto ya kutokurejeshwa kazini licha ya serikali kutoa tamko la kurejeshwa..

“baadhi ya maeneo watumishi hawa hawajarudi kazini na inatokana na tofauti kubwa iliyopo kati ya muajiri mmoja hadi mwingine, maeneo ambayo kunawatumishi waliojaza form za opras na wakajaza wamemaliza kidato cha nne na hawakujaza kwa mapenzi yao walijaza kwa kuelekezwa na maafisa utumishi kwasababu usipojaza kidato cha nne mfumo unakukataa kwasababu mfumo wa ajira serikalini unamtambua mtu mwenye elimu ya kidato cha nne na kukendelea kwahiyo baada ya kujaza fom hizo zimekuja kuwageuka leo wanaambiwa walidanganya baadhi ya halmashauri wamewakubali na baadhi wamewakataa” amesema rais tucta nyamuhoka.

Mwenekiti kamati ya wanawake tucta rehema ludanga amesema wanaishukuru serikali kwa kuwa sikivu hasa kwenye suala la vikokotoo na kuwaomba wafanyakazi nchini wanatakiwa kutambua shirikisho la tucta lipo kwa sababu yao na linafanyakazi kuwawakilisha wao.

“ningependa kuwaomba wafanyakazi nchini kutambua kuwa shirikisho linafanya kazi kwaajili yao na tunawaomba watuamini na tunaendelea kuwatendea kazi na tunashukuru kwa ushirikiano tunaoupata kutoka serikalini inaturahisishia kufanyakazi hasa mfano katika suala la kikokotoo ninaamini na mambo mengine yote yatakwenda vizuri” amesema rehema.
 Naibu katibu mkuu ofisi ya Rais utumishi na utawala bora Dkt Francis Michael akizungumza jambo kwenye mkutano huo
 Rais wa umoja wa shirikisho la vyama  huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Tumaini Nyamuhoka akizungumza na kamati tendaji ya baraza kuu la shirikisho hilo
 Umoja wa shirikisho la vyama vya huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika kikao kilichokuwa na lengo la kujadili na kuchambua jinsi ya kuboresha shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini tucta,
Umoja wa shirikisho la vyama vya huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) katika kikao kilichokuwa na lengo la kujadili na kuchambua jinsi ya kuboresha shirikisho la vyama vya wafanyakazi nchini tucta,_1

UIMARISHAJI MPAKA WA TANZANIA NA KENYA WAENDELEA KWA KASI

$
0
0





Na Munir Shemweta, NGORONGORO

Kazi ya uimarishaji mpaka wa Tanzania na Kenya kuanzia eneo la Ziwa Natroni katika wilaya ya Ngorongoro hadi Namanga wilaya ya Longido mkoani Arusha inaendelea kwa kasi kubwa na sasa ukaguzi kwa ajili ya kuimarisha mpaka huo umekamilika.

Ukaguzi wa mpaka katika eneo hilo unafuatia kukamilika zoezi la uimarishaji mpaka kwa kuweka alama za mipaka ya nchi hizo mbili kuanzia Ziwa Victoria mkoani Mara hadi Natron wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha kwa umbali wa kilomita 238.

Tayari timu za wataalamu kutoka nchi za Tanzania na Kenya zimefanya ukaguzi eneo la mpaka kuanzia eneo la Natroni wilaya ya Ngorongoro hadi Namanga wilaya ya Longido ambapo timu hizo zimeainisha mahitaji ya uimarishaji mpaka huo na kilichobaki ni uwasilishaji ripoti.

Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi mwishoni mwa wiki alitembelea mpaka wa nchi za Tanzania na Kenya kijiji cha Engoserosambu, eneo karibu na Ziwa Natron la cha Nani katika wilaya ya Ngorongoro pamoja na Namanga wilaya ya Longido mkoani Arusha kwa ajili ya kujionea kazi ya ukaguzi iliyofanyika ikiwa ni maandalizi ya uimarishaji mpaka.

Katika ziara hiyo Katambi alijionea jinsi wataalamu wa nchi mbili za Tanzania na Kenya walivyoshiriki katika kazi ya ukaguzi kwa nia ya kuanisha mahitaji ya uimarishaji mpaka kwa kuwekaji alama kwenye maeneo ambayo vigingi vya mipaka vimeharibika ili kupata picha halisi kwa ajili ya kuhuisha mpaka huo.

Kwa mujibu wa Katambi, ukaguzi wa mpaka wa Tanzania na Kenya katika eneo la kuanzia Natroni hadi Namanga ni matokeo ya mkutano wa Narok uliofanyika nchini Kenya ambapo nchi husika zilikubalina kabla ya kuanza kazi ya kuimarisha mpaka zifanye ukaguzi ili kujua mahitaji halisi wakati wa kuimarisha mpaka.

‘’Ukaguzi ni muhimu sana ili kuwa na bajeti halisi ya kazi, kufahamu ni vigingi vingapi vinahitajika kuongezwa na umbali wa kuweka vigingi hivyo sambamba na njia za kupitisha vifaa wakati wa ujenzi wake’’ alisema Katambi

Kaimu Mkurugenzi huyo wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi alisema, zoezi hilo la uimarishaji mpaka wa Tanzania na Kenya litakapokamilika litaendelea maeneo mengine kutoka Namanga kuelekea mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Tarakea mkoani Kilimanjaro, Hororo hadi kijiji cha Jasini kilichopo wilaya ya Mkinga mkoa wa Tanga na hivyo kukamilisha uimarishaji mpaka huo wenye urefu wa kilomita 760 kutoka Ziwa Victoria hadi Jasini.

Mkuu wa Kikosi Kazi cha Ukaguzi Uimarishaji Mpaka wa Tanzania na Kenya kwa upande wa Tanzania Joseph Ikorongo kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alisema, zoezi la ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo mbili eneo la Ziwa Natron hadi Namanga limeenda vizuri na jumla ya kilomita 128 zimeshakaguliwa na lengo la ukaguzi huo ni kuandaa taarifa ya kina itakayowezesha kuwa na mpango kazi halisi.

Kwa mujibu wa Ikorongo, ukaguzi huo umehusisha kipande cha eneo ambalo halijawahi kuwekewa alama tangu enzi za ukoloni la Ziwa Natroni kati ya kijiji cha Nani na Jema lenye urefu wa kilomita 20 na eneo la kilomita 110 lilokuwa na alama kati ya kilomita moja hadi mbili.

Mkuu huyo wa Kikosi kazi cha Ukaguzi wa mpaka kwa upande wa Tanzania alibainisha kuwa, katika ukaguzi huo, kikosi kazi kimebaini jumla ya alama 47 zikiwa imara huku alama 11 zikihitaji kujengwa upya na alama 3 zikihitaji marekebisho. Ikorongo alisema, eneo la mpaka kuanzia Ziwa Victoria mkoani Mara hadi Jasini mkoa wa Tanga lenye urefu wa kilomita 760 ndiyo eneo refu la mpaka ukilinganisha maeneo mengine ya mipaka ya Tanzania na nchi jirani
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi akitoa maelekezo kwa timu ya ukaguzi wa Tanzania na Kenya katika eneo la Namanga mkoani Arusha kuhusiana na kigingi cha mpaka kilichoanguka eneo la Namanga baada ya kutembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya kuimarisha mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi akiangalia moja ya kigingi cha mpaka kilichowekwa katika mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la kijiji cha Engoserosambu wilaya ya Ngorongoro wakati alipotembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya kuimarisha mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi (Kulia) akielekea kuangalia moja ya alama za mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la kijiji cha Engoserosambu wilayani Ngorongoro wakati alipotembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo.
 Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi wa mpaka wa Tanzania na Kenya kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo akimuonesha Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi (Wa pili Kulia) muelekeo wa alama ya mpaka kati ya nchi hizo eneo la Namanga mkoani Arusha wakati alipotembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga.
 Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo (Wa pili Kulia) akimuonesha Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi (Wa pili Kushoto) muelekeo wa alama ya mpaka kati ya Tanzania na Kenya katika kijiji cha Engoserosambu Loliondo wilaya ya Ngorongoro mkoa wa Arusha wakati alipotembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga.
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi akioneshwa eneo unapopita mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Namanga mkoani Arusha na Afisa aliyeshiriki ukaguzi wa mpaka huo kutoka Wizara ya Ardhi John Solwa wakati alipotembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi akiangalia kigingi cha mpaka kati ya Tanzania na Kenya kilichoanguka katika eneo la Namanga mkoani Arusha baada ya kutembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Samuel Katambi (wa sita waliosimama) akiwa katika picha ya pamoja na kikosi kazi kilichoshiriki kazi ya ukaguzi mpaka wa Tanzania na Kenya baada ya kutembelea kuona ukaguzi kwa ajili ya maandalizi ya uimarishaji  mpaka wa nchi hizo kutoka eneo la Ziwa na Natron hadi Namanga. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Ukaguzi kwa upande wa Tanzania kutoka Wizara ya Ardhi Joseph Ikorongo. (PICHA ZOTE NA MUNIR SHEMWETA-WIZARA YA ARDHI)

WASANII WASHAURIWA KUHUSISHA MAWAKILI KWENYE MIKATABA YAO

$
0
0
Ay,Mwanafa wadaiwa  kudhulumiwa haki zao

WASANII  wote nchini wameombwa kujitathimini upya katika mikataba au makubaliano wanayoingia na makampuni, mashirika, wamiliki wa filamu kwenye kazi zao.

Akizungumza na wasanii wakili wa wasanii Alberto Msando  katika kongamano la waigizaji lililoandaliwa na  bodi ya filamu (TFB)  pamoja na chama cha waigizaji (TDFAA)  lililofanyika ukumbi wa Suma JKT Mwenge jijini Dar es salaam. amesema ni wakati wa Wasanii kujitathimini na kuingia makubaliano ya kikazi kwa njia ya maandishi ili kuepuka unyonywaji na utapeli kwenye malipo baada ya kazi na kabla ya kazi.

"Mikataba inasaidia wasanii kuwa na adabu na nidhamu ya kazi kutokana na kumtaka muda maalum kuwepo kwenye kazi na hata hivyo inamsaidia msanii kudai stahiki zake  haraka huku akiwa na vielelezo husika ," alisema Msando.

Msando amewataja baadi ya wadau wakiwemmo waandaaji wa filamu,watunzi wa filamu pamoja na watengenezaji wa matangazo ambao wanawatumia wasanii kwenye matangazo hayo, kuwa na leseni za kikazi ili kutambulika kisheria.

Halikadhalika amewatolea mfano wasanii kama Ambwene Yesya a.ka AY Khamisi Mwinjuma a.k.a MwanaFA,Wema Sepetu pamoja na Masanja Mkandamizaji ambao wameshapata matatizo kwenye kazi zao kutokana na mikataba wanayoingia na wakifika katika mikono sheria wanafanikiwa kupata haki zao ,Hivyo amewasihi wasanii kufika kwenye vyombo vya sheria au hata kusaini mikataba na kuhusisha Mawakili .

Pia ametoa rai kwa wasanii kujiandikisha kwenye vyama vya sanaa,bodi ya filamu pamoja baraza la sanaa ili kutambulika kama msanii mwenye kutambulika.

TRA YATANGAZA MAKUSANYO YAKE YA MIEZI TISA,YAKUSANYA TRILIONI 11.96

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi Trilioni 11.96 katika kipindi cha Miezi Tisa ya Mwaka wa Fedha 2018/19 ikiwa ni kuanzia Julai 2018 hadi Machi 2019. 

Katika robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2018/19 TRA, ilifanikiwa kukusanya Shilingi Trillioni 1.30 kwa mwezi wa Januari, Shilingi Trillioni 1.23 kwa mwezi wa Februari na kiasi cha Shilingi Trillioni 1.43 kwa mwezi wa Machi, 2019.  

Mamlaka ya Mapato Tanzania inawashukuru walipakodi wote waliochangia makusanyo hayo kwa  kulipa kodi zao kwa hiari na kwa wakati na kuhimiza wale ambao bado wanasuasua kujitokeza kulipa kodi hizo kwa wakati. TRA inaendelea kuhimiza wananchi wote ambao wana changamoto za kikodi kutembelea ofisi za TRA na kuonana na mameneja wa mikoa na wilaya kwa ufumbuzi wa changamoto hizo.

Aidha, katika kuongeza wigo wa kodi, TRA kwa sasa imeweka utaratibu wa kurahisisha upatikanaji wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) ambapo TIN inaweza kutolewa katika ofisi zote za TRA katika ngazi ya Mkoa na Wilaya baada ya mwombaji kuwasilisha kitambulisho cha taifa au kwa kupata namba ya kitambulisho wakati kitambulisho kikiendelea kushughulikiwa . Sambamba na hilo TRA inaendelea kuhamasisha, kutoa elimu ya kodi na kusajili walipakodi wapya katika mikoa, wilaya na vitongoji mbalimbali nchini kote. 

Wakati huo huo, Mamlaka inapenda kuwakumbusha wamiliki wote wa majengo nchini kujitokeza kulipia kodi za majengo haraka kuepuka usumbufu wa kulipa mwishoni kwani kwa sasa viwango ni rafiki na vinalipika. Viwango hivyo kwa mwaka ni Shilingi 10,000 kwa nyumba ya kawaida, Shilingi 50,000 kwa kila sakafu nyumba ya ghorofa katika majiji, Manispaa na halmashauri za miji na Shilingi 20,000 kwa jengo la ghorofa katika maeneo ya halmashauri za wilaya.

Vile vile, TRA inawaasa wale wote wanaojishughulisha na vitendo vya kughushi risiti za kielektroniki za EFD nchi nzima kuacha mara moja kwa sababu wakibainika watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani. Kila mwananchi na mfanyabiashara atambue wajibu wake wa kudai risiti kwa kila manunuzi na kutoa risiti kwa kila mauzo.


Tunaendelea kuwakaribisha wakazi wa Dar es Salaam kutembelea kituo cha ushauri kwa walipakodi kilichopo katika makutano ya mitaa ya Samora na Bridge katikati ya jiji, karibu na jengo TTCL. Pia wanaweza kupiga simu bure namba 0800 750075 au 0800 780078 na kwa upande wa barua pepe tafadhali tuandikie huduma@tra.go.tz. Vile vile, wanaweza kutuma ujumbe kupita namba ya Whatsapp 0744 233 333.
 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi TRA, Richard Kayombo akitangaza makusanyo ya yaliyopatikana kwa muda wa miezi 9 ambapo kiasi cha Trilioni 11.96 kimepatikana ikiwa ni makusanyo ya kodi mbalimbali nchini mkutano huo umefanyika leo kwenye makao makuu ta TRA Stesheni jijini Dar es salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG) 
 Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa kodi TRA, Richard Kayombo akifafanua jambo kwa wanahabari leo wakati akitangaza makusanyo  yaliyopatikana kwa muda wa miezi 9 ambapo kiasi cha Trilioni 11.96 kimepatikana.

MWENYEKITI WA CCM TAIFA RAIS DKT. MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM (NEC) IKULU CHAMWINO JIJINI DODOMA

$
0
0
 Mwenyekiti wa  Chama Cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli na MAkamu Mwenykiti wa CCM (VIsiwani) na Rais wa Zanzibar na Baraa la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein  wakitoka kwenye kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya  chama hicho (NEC)  kilichofanyika
Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo Jumatatu Aprili 15, 2019.
Wajumbe wa Kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya  Chama Cha Mapinduzi (NEC) wakitoka kwenye kikao chao kilichofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt. John Pombe Magufuli leo Jumatatu Aprili 15, 2019
Katibu Mkuu wa  Chama Cha Mapinduzi Dkt. Bashiru Ally akizungumza na Wajumbe wa Kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya  Chama hicho  (NEC) kabla ya kuanza kwa kikao chao kilichofanyika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo  chini ya Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dkt. John Pombe
Magufuli Jumatatu Aprili 15, 2019

Kamati ya Maudhui ya TCRA yatoa onyo kali kwa vituo vya Star TV na Magic FM

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) imeotoa onyo kwa Kampuni za vyombo vya habari vya Sahara Media Group na African Media Group kutokana na kutangaza habari za magazeti baadhi ya habari kiundani.

Akizungumza wakati wa kutoa maamuzi ya kamati ya maudhui TCRA Mwenyekiti wa Kamati hiyo Vallerie Msoka amesema kuwa kituo cha Magic FM ilitangaza habari za habari magazeti katika kiundani ambayo ni kinyume na sheria ya zuio la Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt Harison Mwakyembe.

Amesema kuwa habari iliosomwa na Megic FM katika moja ya magazeti kuhusiana na matumizi ya kondomu ambapo watangazaji walikuwa wanadisi juu ya matumizi hayo.

Msoka amesema kuwa African Media Group katika utetezi wake walidai kuwa wakati linafanyika kosa hilo Megic FM ilikuwa chini ya umiliki mwingine na kuomba msamaha huo katika kamati hiyo.

Aidha amesema kuwa utetezi wa Megic FM haufanyi umiliki wa mtu mwingine kuharalisha utangazaji uliofanyika huku wakijua ni zuio la Waziri Habari, Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harison Mwakyembe Kwa upande wa Star Tv walitangaza habari ya Waziri wa Madini Dotto Biteko kiundani zaidi huku wakijua ni kosa kwa zuio la Waziri wa Habari,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dk.Harison Mwakyembe.

Msoka amesema katika utetezi wake kampuni inayomiliki Star Tv ilisema kuwa wakati wanatangaza habari za magazeti aliyefanya hana uzoefu na kudai kuwa wale wazoefu wanaacha kazi.Amesema kuwa utetezi wa star tv haufanyi kuondoka kwa wafanyakazi ndio kutangaza habari za magazeti kiundani.
Amesema kuwa kwa vituo hivyo kama hawajalidhika wanaweza kukata rufaa ndani ya siku 21 pamoja kutaka kufuata sheria za utangazaji.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA) Vallerie Msoka akitoa maazimio ya ukiukaji maudhui ya Utangazaji kwa Vituo vya Star Tv na Magic FM leo jijini Dar es Salaam.

WANAWAKE WATAKIWA KUTUMIA FURSA KUJIONGEZEA MASOKO

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii


Wito umetolewa kwa Wanawake wanaofanya shughuli za uvuvi na kuchakata mazao ya uvuvi kutumia chama chao kuweza kupanua fursa ya masoko baina ya wao kwa wao kutokana na sehemu wanazotoka.

Hayo yamesemwa leo April 15 jijini Dar es Salaam 2019 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama alipokuwa akifungua kikao cha kwanza cha TAWFA Kilichofanyika katika Hotel ya Mbezi Garden Jijini Dar es Salaam.

“TAWFA ni mtandao au chombo kitakachotumika kuwaunganisha kwa pamoja Wanawake wote wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi hapa nchini ,pia kupitia TAWFA,nataraji kwamba wanawake watatoa changamoto na uzoefu wao kwa sauti moja katika shughuli za uvuvi na kuuza mazao ya uvuvi”amesema Dk . Rashid.

Amesema kuwa TAWFA Ndio chombo pekee kutoka Tanzania kitakachokuwa mwanachama katika mtandao wa Africa (Africa Women fish processors and Traders Association-AWFISHNET) Ambao umeunganisha wanawake wote Africa wanaojishughulisha na uchakataji na biashara ya samaki na mazao yake ili wawe na sauti moja katika kushiriki kwenye masuala mbalimbali.

Pia alitoa wito kwa wanawake wote wanaohusika katika mtandao wa TAWFA waweze kushirikiana,kupendana na kusaidiana katika shughuli zenu ili kuwa na uelewano wa kibiashara na kukuza kipato na uchumi kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Chama cha Wanawake wanaojishughulisha na kuchakata mazo ya uvuvi nchini.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanawake wanaojishughulisha kuchakata mazo ya Uvuvi nchini(TAWFA) Wakati wa hafala ya ufunguzi wa Chama hicho Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Emedo akizungumza mbele ya mgeni rasmi kumeuleza mchakato wa kuanzishwa kwa TAWFA
Sehemu ya Wanachama wa TAWFA Walioshiriki uzinduzi wa chama chao jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikagua baadhi ya mazo ya uvuvi yalionyeshwa na Wanawake hao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikagua baadhi ya mazo ya uvuvi yalionyeshwa na Wanawake hao.
Sehemu ya Wanachama wa TAWFA Walioshiriki uzinduzi wa chama chao jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akiwa katika picha ya pamoja na Wanachama wa TAWFA.

SERIKALI KUANDAA SHERIA,KANUNI KATAZO LA MIFUKO YA PLASTIKI

$
0
0
Na Karama Kenyunko,Globu ya jamii

WAZIRI wa  Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira),Januari Makamba amesema kwamba katazo la kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki nchini litakuwa la kisheria na kanuni zake zitakazokuwa na adhabu kwa wale watakaokiuka.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Makamba pia amesema katika kipindi hichi cha mpito,wizara yake itaweka utaratibu wa mahali pa kuiweka,sehemu ya kuisalimisha na kuiteketeza kwa walio na mifuko hiyo katika magodauni yao kabla haijawa kosa kisheria kwa muda uliowekwa na Serikali.

Kwa kukumbusha tu,mapema wiki iliyopita Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa bungeni Mjini Dododma,alisema kuanzia Juni Mosi mwaka huu, itakuwa ni marufuku kutengeneza, kuuza, kuingiza na kutumia mifuko ya plastiki kwa ajili ya kubebea bidhaa za aina yoyote.

Hivyo Waziri Makamba wakati anazungumza na wadau wa mifuko ya plasiki, kuhusu fursa za uwekezaji katika uzalishaji wa mifuko mbadala ya plastiki amefafanua katazo hilo litakuwa la kisheria na sio tamko.

Ameongeza kuwa katazo hilo  ni kuanzia uzalishaji, kuuza, kuingiza, kumiliki, kuhifadhi kutumia,yote hayo ni makosa.Kanuni hizo watakazoweka zitakuwa na adhabu kwa watakaokiuka hata atakayekutwa naye na kutakuwa na faini au vifungo kwa mujibu wa sheria,kanuni zitakapokamilika zitatangazwa"alisema Makamba

Pia amesema katazo hilo halitausisha vifungashio vya plastiki kwa bidhaa kama Korosho,maziwa, na nyinginezo bali litaanza kwa mifuko ya plastiki inayotumika kubebea bidhaa.

Wakati huo huo Makamba amesema uwamuzi wa katazo hilo si wa gafla kama inavyosemwa na baadhi ya wamiliki wa viwanda vya kutengeneza mifuko ya plastiki kwani inafahamika tangu Agosti mwaka 2016 kwa wadau kuandikiwa barua kujadili  kupiga marufuku mifuko hiyo.

Makamba amesema katazo hilo lina manufaa kwa taifa kàtika kutunza mazingira na kwamba kwa mwaka mifuko bilioni 3 inaishia katika fukwe za mito,bahari na kukaa muda mrefu ikichafua mazingira.
  
Kwaupande wake ,Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda amewataka watakaopewa mamlaka ya kusimakia katazo hilo kutolichukulia kama fursa ya kuomba na kupokea rushwa.

Kwa baadhi ya mawakala na wafanyabiashara wa mifuko ya plastiki kutoka Sokoni Kariakoo wameiomba serikali iwaongezee muda wa kuiuza hadi Januari mwakani, kwani bado ipo mingi na wanadaiwa na wafanyabiashara raia wa china waliowapa.

Hat hivyo,Waziri Mahakama akijibu hoja hiyo,alisisistiza kuwa katazo hilo ni msimamo  wa Serikali na halitarudi nyuma hivyo wakae na waliowauzia kuona kama watawalipa fidia ama la.

VIONGOZI WA DINI NA WAGANGA WA TIBA ASILI NI NGUZO MUHIMU KATIKA KUTOKOMEZA TB NCHINI

$
0
0

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na Wadau wa kupambana dhidi ya ugonjwa wa Kifua Kikuu katika ufunguzi wa Mkutano wakwanza wa wadau wenye lengo la ushirikiano katika kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu nchini leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.(Picha na Emmanuel Masska,MMG)
Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Muhammad Bakari Kambi akieleza jambo kuhusu mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu nchini baada ya kupewa fursa ya Kumkaribisha mgeni rasmi, Mhe. Ummy Mwalimu katika ufunguzi wa Mkutano wa kwanza wa wadau wenye lengo la ushirikiano katika kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu nchini ulio fanyika leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalim (katikati) akiwa na baadhi ya wadau wa masuala ya Kifua Kikuu wakijadi mambo mbalimbali katika ufunguzi wa Mkutano wakwanza wa Wadau wenye lengo la kuimarisha ushirikiano katika kutokomeza ugonjwa huo nchini leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Wadau wa masuala ya Kifua Kikuu wakifuatilia neno kutoka kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu (Hayupo kwenye picha) katika ufunguzi wa Mkutano wakwanza wa Wadau wenye lengo la kuimarisha ushirikiano katika kutokomeza ugonjwa huo nchini leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Moja ya kikundi ambacho kimekuwa kikishiriki katika kampeni ya kupiga vita ugonjwa wa kifua kikuu kikitumbuiza katika mkutano huo.


Na WAMJW – DSM 

Waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa viongozi wa madhehebu ya dini na Waganga wa tiba asili ni nguzo muhimu sana katika kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu(TB) nchini. 

Ameyasema hayo leo katika ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa wadau wenye lengo la ushirikiano katika kutokomeza ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB) nchini uliofanyika Jijini Dar es salaam 

Waziri Ummy amesema kuwa Waganga wa Jadi na Viongozi wa Dini ni Wadau muhimu sana katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa TB, huku akidai kutokana na utafiti uliofanywa 2018 na Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma unaonesha kuwa waganga wa jadi wamekuwa wahanga wakubwa wa ugonjwa wa kifua kikuu. 

Aliendelea kusema kuwa, viongozi wa dini ni kundi lingine muhimu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa kifua kikuu nchini, hii ni kutokana na idadi kubwa ya waumini wanaowaamini katika kufikisha ujumbe. 

“Waganga wa jadi, ni wadau muhimu sana katika mapambano ya kifua kikuu, utafiti wa 2018 uliofanywa na mpango wa taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma unaonesha kuwa Waganga wa jadi na wenyewe wamekuwa wahanga wa ugonjwa wa kifua kikuu, na viongozi wa dini tunawahitaji wanaposimama katika makanisa na katika misikiti yetu ili wawe wanawakumbusha waumini juu ya ugonjwa wa Kifua Kikuu” alisema Waziri Ummy 

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa 2017, Tanzania iligundua na kuwapatia matibabu takribani wagonjwa 75,000 ikiwa ni sawa na 44% tu ya wagonjwa wanaokadiriwa kuugua TB, hii ina maana ya kuwa wagojwa 85,000 (56%) hawagunduliwi na hivyo kukosa matibabu kila mwaka nchini. 

Pia, Waziri Ummy amesema kuwa TB huathiri takriban watu milioni 10.4 duniani kila mwaka na 25% ya wagonjwa wanatoka barani Afrika. Tanzania ni miongoni mwa nchi 13 barani Afrika zenye kiwango kikubwa cha wagonjwa wa TB na inakadiriwa kuwa na wagonjwa wapya wa TB 154,000 kila mwaka. 

Mbali na hayo, Waziri Ummy amesema kuwa, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, imeendelea kutoa huduma za uchunguzi na matibabu bila malipo katika vituo vya kutolea huduma vya serikali na binafsi, hali iliyoleta mafanikio ikiwamo kuvuka malengo ya mwaka 2018 ambapo tuliwafikia wagonjwa 75,845 ikiwa ni sawa ongezeko la asilimia 22 kutoka mwaka 2015. 

Naye, Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammad Bakari Kambi amesema kuwa Tanzania ina wastani wa jumla ya Wagonjwa 154,000 ambao wanatakiwa kuibuliwa na kuanzishiwa matibabu, licha ya changamoto ya kutowafikia wote ametoa wito juu ya umuhimu wa ushirikishwaji wa watu na taasisi mbali mbali ili kurahisisha mapambano haya dhidi ya ugonjwa wa TB. 

Kwa upande wake Meneja wa Mpango wa Taifa wa kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Dkt.Beatrice Mutayoba amesema kuwa kila mwaka watoto 1,000,000 wanaugua kifua kikuu Duniani, huku watoto 250,000 wanafariki. 

“Kwa bahati mbaya Kifua kikuu hakijaacha watoto, kila mwaka watoto 1,000,000 wanaugua kifua kikuu Duniani, huku watoto 250,000 wanafariki, huku nchini Tanzania 10% ya watu 68,000 wanaogundukila kuwa na Kifua kikuu huwa ni watoto” alisema Beatrice Mutayoba

KANISA MAARUFU DUNIANI LATEKETEA KWA MOTO UFARANSA

$
0
0


Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

KANISA la Notre Dame lililopo Paris nchini Ufaransa likiwa ni  kanisa kubwa na mashuhuri duniani limeteketea kwa moto huku chanzo chako kikiwa hakijafahamika.

Polisi wamewataka raia kutokupita kwenye maeneo ya karibu ili kurahisisha uokoaji unaofanywa na vyombo vya usalama.

Meya wa Parid Anne Hidalgo ameeleza kuwa moto huo ni mkubwa na kuhakikisha kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vipo kazini katika kuzima moto huo.

Rais wa nchi hiyo Macron Emmanuel kupitia mtandao wa twitter ameeleza pia kusikitishwa na ajali hiyo huku akikanusha kuwa tukio hilo lilipangwa.

Kanisa hilo lililojengwa  kuanzia karne ya 13 na kukamilika karne ya 15 na huchukua watu zaidi ya million 13 kwa mwaka na hutembelewa na zaidi ya watu 30000 kwa siku.

VANILA NI DHAHABU YA KIJANI MKAKATI WA KUKOMESHA WIZI MASHAMBANI WASUKWA WEZI NA WALANGUZI KUKIONA CHA MOTO – RC GAGUTI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti


Na: Sylvester Raphael

Dhahabu ya kijani (vanilla) Mkoani kagera sasa yawekewa mikakati imara ya kuwanufaisha wakulima na kuinua uchumi wa mkoa badala ya wananchi kutegemea mazao kama ndizi na kahawa tu ambayo yamekuwa yakilimwa kwa mazoea lakini bila kumnufaisha mkulima kulingana na anavyokuwa amewekeza hadi kuuza sokoni.

Mikakati hiyo imefikiwa baada ya Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti kuitikia wito wa wakulima wa mazao ya vanilla, kakao, na chia na kufanya kikao nao katika Shule ya Sekondari KADEA Kanyigo Wilayani Missenyi na kusikia kilio chao cha wizi wa vanilla changa pamoja na marando yake.

Mara baada ya kutembelea na kukagua shamba la vanilla la Mwalimu Jovin Mbanga Mkuu wa Mkoa Gaguti alikutana na wakulima na kusikiliza kilio chao cha wizi wa vanilla changa na marando katika mashamba yao ambapo wizi huo mara baada ya kufanyika vanilla hizo huuzwa nchi jirani ya Uganda.

Wakimweleza Mkuu wa Mkoa wakulima wa vanilla walisema kuwa changamoto kubwa ni wizi wa vanilla ambapo wanalazimika kulala mashambani wakilinda kila siku zisiibiwe. Wizi huo hufanywa na baadhi ya Watanzania wasiokuwa wazalendo wakishirikiana na wafanyabiashara kutoka nje nchi kwa kupewa mitaji ya kununulia vanilla za wizi.

Pia wakulima hao mbale ya Mkuu wa Mkoa walitoa changamoto zao kuwa ni kutokuwa na masoko rasmi ya kuuza vanilla zao mara baada ya kukomaa aidha, wanunuzi wanaojishughulisha na ununuzi wa vanilla kutosajiliwa na kutambulika Kiserikali ili mwananchi akiwa na vanilla zake aweze kuziuza katika soko na kwa mnunuzi maalum.

Baada ya Mkuu wa Mkoa Gaguti kusikiliza kwa makini malalamiko ya wakulima hao alitoa maelekeza mahususi kuhusu zao la vanilla katika Mkoa wa Kagera Kwanza; Aliagiza kuanzia tarehe ya kikao Aprili 15,2019 vanila itakuwa na muda maalum wa kuvunwa mashambani na kutakuwa na vituo maalum kama masoko ya kununulia vanilla hizo ambapo wafanyabiashara ni marufuku kwenda moja kwa moja kwa wakulima.

Akitoa ufafanuzi zaidi Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kwa mwananchi yeyoyote atakayekamatwa na vanilla kabla ya tarehe ya kuvunwa kutangazwa atachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.

Pili; Wakulima wa Vanila wajiunge katika ushirika wa vyama vya msingi ambapo itakuwa rahisi katika kubainisha wezi, kuwa na soko la uhakika lakini pia kuuza vanilla ambazo tayari zimeongezwa thamani ili kupat bei nzuri zaidi na kuweka urahisi zaidi wa Serikali kuwasimamia kama ushirika kuliko mwananchi mmoja mmoja.

Tatu; Wafanyabiashara wote au makampuni yote yanayojihusisha na ununuaji wa vanilla wanatakiwa kujisajili na kupewa leseni ya kununua vanilla kuliko ilivyo sasa. Pia kwa Taasisi au Makampuni ambayo yanatoa ruzuku kwa wakulima wanunue vanilla kwa wakulima kulingana na bei ya soko na si kuwanyonya wakulima.

Aidha, Mkuu wa Mkoa alitoa rai kwa Watendaji wa Vijiji na Kata kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kikamilifu kama wanataka kuendelea kubaki kazini hasa jukumu la ulinzi na usalama kwa mfumo wa Nyumba Kumi Bora za Usalama ambapo wezi wa vanilla watabainika kirahisi kila eneo.

Mkuu wa Mkoa Gaguti pamoja na kufanya kikao na wakulima wa vanilla pia alichoma zana haramu katika mwalo wa Kabindi Kashenye Kanyigo Wilayani Missenyi na kutangaza rasmi kuwa mwaka huu wa 2019 atakikisha anatokomeza magendo yote iwe ya uvuvi, kahawa au vanilla na kuwataka wananchi wanaojishughulisha na biashara hiyo haramu kuacha mara moja.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Denice Mwila aliwataka wananchi wa Missenyi hasa Wakulima wa Vanila Kanyigio kubadilika kwani alisema kuwa wizi mwingine wa vanilla unatokea ndani ya familia na alitoa mfano kwa kusema kuwa unakuta shamba ni la baba na akitoka kwenda pengine Bukoba Mjini kufanya shughuli zake mama au mtoto anavuna vanilla haraha haraka na kuziuza lakini baba akirudi anaambiwa vanilla zimeibwa.

Katika kuchukua hatua kwa baadhi ya watuhumiwa ambao waliwahi kutajwa katika mikutano ya hadhara au kupigiwa kura Mkuu wa Mkoa alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Denice Mwila kuwa watu hao walipoti mara moja ofisini kwake na hatua zianze kuchuuliwa ambapo Mkuu huyo wa Wilaya alitekeleza agizo hilo mara moja kwa kuondoka na Mzee George Lubale aliwahi kutuhumiwa kujihusisha na wizi wa vanilla.

Vanila ni zao ambalo linaonekana kutaka kuukomboa mkoa wa Kagera, zao hili linalimwa katika sehemu yenye kivuli hasa kwenye migomba au kwenye miti na linahitaji mwanga sawa na kivuli asilimia 50% kwa 50%. Vanila inapandwa marando ambapo yanapandwa na kuwekewa mti aina ya jatrofa ili kukua kwa kupanda mti huo na mazao yake ni kama maharage. Bei kwa sasa sokoni tena kwa vanila changa ni kati ya shilingi 20,000/= hadi 30,000/= kwa kilo moja.

Mwaka 2017/18 bei ya vanilla mkoani kagera ilifikia kati ya shilingi 100,000/= hadi 150,000/= na siku za nyuma vanilla iliwahi kuzalishwa Mkoani Kagera hadi kufikia tani 103 lakini kwa sasa zinazalishwa tani 10 hadi 12 ambapo zao hili limekuwa likingiiza zaidi ya shilingi milioni 800,000/= Vanila inastawi au inalimwa na kukomaa kwa miezi tisa tu tayari unavuna na kuuaga umasikini milele badala ya kutegemea zao moja la kahawa.






 

MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRIL 16,2019

Ajiuwa kwa kujichinja chinja

$
0
0
Na Woinde Shizza globu ya jamii

MTU mmoja alietambulika kwa jina la Lazaro Keorori (53) mkazi mtaa Wa Simanjiro Kata ya Sombetini amefariki dunia Mara baada ya kujichinja chinja na kisu kikali.

Akizungumza na waandishi Wa habari kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana alisema kuwa tukio hilo limetokea aprili 15 majira Saa moja asubui . 

Alibainisha kuwa uchunguzi ulifanywa na jeshi la polisi umebaini kuwa marehemu amechukuwa uwamuzi huo kutokana na mgogoro Wa kifamilia uliokuwepo kati yake nawake zake wawili .

"Marehemu alikuwa na msongo Wa mawazo uliompelekea yeye kuamua kuchukuwa uamuzi Wa kujiuwa ,na kwamaelezo ya watu waliohojiwa walisema aliingia ndani usiku akachukuwa kisu kidogo chenye makali akaanza kujichinja sasa ,pamoja alikuwa chumbani watu waligundua Saa ile ambapo roho ilikuwa inataka kutoka akawa anapiga kelele ndio watu wakamjua ila haikuwezekana kumuokoa roho take" alisema kamanda

Aidha aliwaasa wananchi haswa wanafamilia wakiwemo wanaume kutochukuwa maamuzi ya haraka haraka na kuwasihi iwapo wakipata msongo Wa mawazo ni vizuri wakaenda kupewa ushauri katika nyumba za ibada au katika familia na sio kujichukulia sheria mkononi.

Wakati huo huo jeshi la polisi linawashikilia watu Tisa kwa makosa ya kuwatapeli watu Aridhi.Kamanda Wa polisi amesema kuwa sasa ivi mkoa Wa Arusha umegubikwa na wimbi la matapeli ambapo wanajidai wao ni maafisa ardhi ,huku wengine wakijifanya ni matajiri wanunuaji huku wengine wakijidai ni wenye mashamba .

Aisha alibainisha kuwa jeshi la polisi limefanya operation na kuwakamata watu Tisa ambapo kati yao wawili ni wafanyakazi Wa halmashauri ya jiji la Arusha ,huku wawili wakiwa ni wafanyakazi Wa ofisi ya Aridhi Kanda ya kaskazini na wengine sita waliobaki ni wananchi Wa kawaida.

Kamanda alisema kuwa watu hao watafikishwa mahakamani pindi tu upelelezi utakapo kamilika ,pia alitoa wito kwa wananchi kufuata sheria na kufanya uchunguzi kabla ya kununua au kuuza nyumba au kiwanja.

Picha kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana akionyesha waandishi Wa habari kisu ambacho marehemu Lazaro Keurori alitumia kuji chinjia chinjia .
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>