Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

WASANII JISAJILINI MPATE HAKI ZENU ZA MSINGI-BASATA

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Arusha. 

Wito umetolewa kwa wasanii nchini kujisajili katika Baraza na sanaa nchini ili waweze kutambulika, kupata haki zao msingi, na wawe na uhuru wa kufanya kazi

Hayo yamesemwa jijini Arusha na Katibu wa Shughuli za Sanaa Kanda ya Kaskazini Flora Mgonja ambapo amewataka wasanii kufahamu kuwa sanaa ni kazi kama zilivyo kazi nyingine na wanatakiwa kuithamini, kuipenda na kuilinda

Amesema sheria namba 23 ya mwaka 1984 iliyoanzishwa kwa mujibu wa Bunge na kanuni mpya ya Februari 2018 inamtambua msanii, inaelezea sababu ya msanii kusajiliwa, pia zimeweka wazi kwamba hakuna msanii yeyote ambae anaweza kufanya kazi zake bila kusajiliwa Basata

Kwa mujibu wa Kanuni za Baraza la sanaa la Taifa, 23-(1)Mtu yeyote hatoruhusiwa kufanya kazi ya sanaa ya aina yeyote kwa mujibu wa sheria inayohusika na sanaa, kufanya biashara ya kazi za sanaa bila kusajiliwa na Baraza

Amesema kuwa Baraza la sanaa la Taifa lipo tayari kuwasaidia pele watakapokuwa wamesajiliwa na kutambuliwa ili kuweza kuwapa huduma kwa mujibu wa sheria na taratibu.'' Tuna dawati la sheria pale ofisini kwetu hawalijui wasanij wengi, wanadhukumiwa mikataba, wanashindwa kupata fidia zao kwasababu hawajasajiliwa, leo unakuja kusema kazi yangu imechukuliwa wakati hujasajiliwa''

Amesema kwa sasa wameanza kutoa elimu kwanza kwa wasanii mbalimbali katika kanda zote sita nchini ambapo kila mmoja wapo anatakiwa kutambua kwamba anatakiwa ajisajili kwenye Baraza la sanaa la Taifa.''Hatuwezi kuwabana tukakimbikia kwenye sheria, tunamuda ambao tumejiwekea kuhakikisha kwamba msanii ajitambue kwamba ni lazima nisa jiliwe kwenye Baraza la sanaa la Taifa"Alisema

Amesema wanapoelekea itafikia mahala ambapo washehereshaji (MC) wote,Dj, kufanya kazi bila kuwa na cheti kutoka Basata kwani wasanii wote wanatakiwa wawepo kwenye Data base.Amewataka kufahamu kuwa kujisajili kwao ni fursa, kwani baraza hilo linanafasi ya kumsaidia msanii pale anapopata mialiko mbalimbali ya kwenda nje ya nchi kufanya matamasha nchi za nje 

Amesema kwa sasa msanii hawezi kupita uwanja wa ndege bila barua kutoka Basata kama anakwenda nje ya nchi kwa mujibu wa kanuni na sheria za Baraza la sanaa la Taifa

'' Lazima msanii apate barua na ada yake ni shilingi 50,000Msanii anapoondoka nchini kwenda nje ya nchi anatakiwa aondoke na kibali kutoka basata ambacho ni shilingi 50,000 akiwa na tatizo lolote nchi husika zinawasikiana lakini akiondoka. Kiholela hawezi kusaidika''alisisitiza

Ameainisha garama za kujisajili kwa msanii ni shilingi 45,000, mchanganuo wake fomu 5000, usajili 20,000, kibali cha mwaka 20,000 ambapo jumla yake ni 45,000 .Sambamba na hayo amesisitiza kuwa usajili kwa msanii binafsi ni mara moja kwa mwaka, ila kibali cha mwaka kinalipiwa kila mwaka mpya unapoaanza.
Mratibu wa shughuli za sanaa Kanda ya Kaskazini Flora Mgonja akiwa katika ofisi ya Utamaduni Jijini Arusha. Picha na Vero Ignatus
Kutoka kulia ni Mratibu wa shughuli za Sanaa Kanda ya Kaskazini (BAATA) Flora Mgonja, akiwa na Msimamizi wa maendeleo ya sanaa Kanda ya Kaskazini - BASATA. Picha na Vero Ignatus
Kutoka kulia ni Afisa michezo na Utamaduni Jiji la Arusha Benson B. Maneno, Mratibu wa shughuli za sanaa Kanda ya Kaskazini (BASATA) Flora Mgonja na Msimamizi wa maendeleo ya sanaa Kanda ya Kaskazini -BASATA

MGUNDUZI WA MADINI YA TANZANITE MZEE NGOMA AFARIKI DUNIA

$
0
0
Mvumbuzi wa madini ya Tanzanite, Jummane Ngoma amefariki dunia leo Jumatano Januari 30, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mtoto wa marehemu, Hassan Ngoma amesema, “Ni kweli Mzee amefariki leo jioni hii hapa Muhimbili,” amesema Ngoma Hassan amesema kinachofanyika kwa sasa ni kuuhifadhi mwili wa baba yake kisha baadaye watatoa taarifa rasmi ikiwamo utaratibu wa msiba utakuwa wapi na mazishi yatafanyika wapi baada ya kikao cha familia.

Aprili 6 mwaka jana, Rais John Magufuli akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini hayo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wenginme wakimsikiliza Mzee Jumanne Ngoma akitoa shukurani zake kwa kutambuliwa na serikali na kupewa shilingi milioni 1000 na Rais kama ahsante yake wakati wa sherehe za kuzindua rasmi ukuta kuzunguka migodi ya Tanzanite eno la Mirelani wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara  Aprili 6, 2018. Picha na Maktaba 

CCM Z’BAR YATOA VIFAA TIBA KWA HOSPITALI YA KIVUNGE

$
0
0
MWENYEKITI wa Kikundi cha Hamasa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman (kushoto) akimkabidhi Daktari dhamana Tamim Hamad Said(kulia) Friji mbili za kuhifadhi dawa za hospitali zilizotolewa na kikundi cha hamasa cha vijana wa Afisi Kuu CCM Zanzibar.

MWENYEKITI wa Kikundi cha Hamasa Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman (wa pili kushoto) akizungumza mara baada ya kuwasili katika Hospitali ya Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja, Daktari dhamana Tamim Hamad Said (wa kwanza kushoto) pamoja na Katibu wa CCM Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Haji Machano Juma(wa kwanza kulia) wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya vifaa tiba vilivyotolewa na kikundi cha hamasa.


BAADHI ya vijana wa kikundi cha hamasa cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar wakisikiliza kwa makini nasaha za viongozi mbali mbali wa CCM, UVCCM na Hospitali ya Wilaya Kivunge katika hafla ya makabidhiano ya Vifaa Tiba iliyofanyika leo Tarehe 30/01/2019.(PICHA NA IS-HAKA OMAR


………………………….

NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

VIJANA mbali mbali nchini wameshauriwa kuendeleza utamaduni wa kujitolea katika kuisaidia jamii katika masuala mbali mbali ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kimaendeleo.

Rai hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Kikundi cha Hamasa cha Afisi Kuu ya CCM Zanzibar Ndugu Shaaban Ali Othman wakati akikabidhi Friji(Jokofu) mbili zilizotolewa na kikundi hicho na kukabidhi Uongozi wa Hospitali ya Kivunge ya Wilaya Kaskazini ‘A’ Unguja.

Amesema vifaa hivyo vimetolewa kwa ajili ya kusaidia uhifadhi wa vifaa tiba vya hospitali hiyo hasa dawa za matumizi ya binadamu zinazohitaji hali ya baridi muda wote.

Ameutaka uongozi wa Hospitali hiyo kuvitunza na kuvitumia katika matumizi yaliyokusudiwa ili vitoe huduma endelevu kwa wananchi mbali mbali wanaofika hopitalini hapo kwa ajili ya matibabu.

Pamoja na hayo amebainisha kuwa vifaa hivyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi zinazofanywa na viongozi wa CCM ambao ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Dkt.John Pombe Magufuli pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein wanaotekeleza kwa kasi mipango ya maendeleo kwa maslahi ya wananchi wote.

Ameeleza kwamba vijana nchini wana wajibu wa kutekeleza kwa vitendo masuala mbali mbali ya kijamii kwa lengo la kuwasaidia wananchi wanaokabiliwa na changamoto katika mazingira wanayoishi.

Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo Shaaban,amesema endapo vijana wa Zanzibar wataweka mbele dhana ya uzalendo,umoja, mshikamano na kuelekezana mambo mema ya kuisaidia jamii, itasaidia Zanzibar kuwa nchi bora zaidi duniani iliyopiga hatua kubwa za kimaendeleo.

Awali Katibu wa Kikundi hicho cha Hamasa, Suleiman Mohamed Rashid amefafanua kuwa kikundi hicho kitaendelea kusaidia masuala mbali mbali ya kijamii katika maeneo mbali mbali yaliyopo katika Wilaya zote za Unguja na Pemba. Amesema Chama Cha Mapinduzi kipo mstari wa mbele kushughulikia changamoto zinazoikabili jamii katika maeneo ya mijini na vijijini.

Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo Daktari Dhamana wa Hospitali hiyo Tamim Hamad Said, amesema uongoizi wa hospitali hiyo umefurahi kupokea vifaa hivyo kwani vilikuwa ni miongoni mwa mahitaji muhimu ya taasisi hiyo.

Dr.Tamim ameahidi kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa hasa kuhifadhi dawa na vifaa mbalimbali vinavyotumika katika matibabu ili wananchi wapate huduma bora za Afya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Ndugu Pandu Salum Sungura amesema vijana wa mkoa huo wapo imara katika kuunga mkono juhudi za vijana wenzao wa kikundi cha hamasa kutoka Afisi Kuu ya CCM Zanzibar, kilichoonyesha mfano bora wa kutoa vifaa hivyo kwa hospitali ili viwasaidie wananchi wa Mkoa huo.

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Afisi Kuu ya CCM Zanzibar, Katibu Msaidizi wa Taasisi hiyo Ndugu Khamis Salum Abdi amesema Chama Cha Mapinduzi kinaendelea kusimamia na kutekeleza Ilani yake ya Mwaka 2015/2020 kwa ufanisi mkubwa kwa lengo la kumaliza kero zinazoikabili jamii.

Amesema suala la kuwapelekea wananchi maendeleo halina itikadi za kisiasa hivyo kila mwananchi, kikundi pamoja na taasisi yoyote wana wajibu wa kutatua changamoto za wananchi.

KNCV, Muhimbili waboresha huduma kwa wagonjwa wa kifua kikuu

$
0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imekabidhiwa jengo la wagonjwa wa Kifua Kikuu (TB) lililokarabatiwa na mradi wa TB unaofadhiliwa na USAID chini ya Shirika la KNCV ili kusaidia wagonjwa wengi kutibiwa kwa wakati mmoja katika hospitali hiyo tofauti na awali.

Awali, wataalam wa Muhimbili walikuwa wakitoa huduma kwa wagonjwa sita hadi 10 kwa siku na kwa wiki walikuwa wakitibiwa wagonjwa 30 hadi 40. Lakini hivi sasa baada ya ukarabati wa jengo hilo wagonjwa 10 watakuwa wakilazwa kwa wakati mmoja na wangine 50 wa nje watakuwa wakitibiwa kila siku.

 Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko huo, Dkt. Vishnu Mahamba amesema ukarabati wa jengo hilo umegharimu TSh. milioni 69 na kwamba wametoa msaada wa ukarabati ili kuhakikisha wagonjwa wa kifua kikuu wanapata huduma bora.

Akizungumzia msaada huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru alishukuru mfuko huo kwa kusaidia ukarabati wa jengo hilo  kwani litakuwa na manufaa kwa wagonjwa mbalimbali wanaotibiwa katika hospitali hiyo.

Pia, Prof. Museru aliagiza jengo hilo lianze kutumika mara moja baada ya kukabidhiwa kwa uongozi wa hospitali hiyo na kwamba wataalam wanapaswa kuweka mahitaji muhimu vikiwamo vitanda pamoja na vifaa vingine ili kuanza mara moja kwa huduma za matibabu.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani wa Muhimbili, Dkt. Amina Mgunya amesema kwamba jengo hilo watalitumia kutoa huduma za matibabu kwa wagonjwa wa ndani na nje wa kifua kikuu na wa kifua kikuu sugu.

Dkt. Mgunya amesema mbali na ukarabati wa jengo hilo, pia wagonjwa watakuwa wakipatiwa matibabu yote Muhimbili badala ya kupelekwa Hospitali ya Kibong’oto mkoani Kilamanjaro kwa ajili ya matibabu zaidi.

“Kuanzia sasa wagonjwa wa kifua kikuu watakuwa wakipatiwa matibabu yote Muhimbili badala ya kupelekwa Kibong’oto kwa ajili ya matibabu zaidi,” amesema Dkt. Mgunya.

Naye Mkuu wa Idara ya Huduma za Uuguzi Muhimbili, Yassin Munguatosha amesema wamepokea agizo la Prof. Museru na kwamba agizo hilo watalitekeleza maramoja ili kuhakikisha wagonjwa wa kifua kikuu wanapatiwa matibabu katika jengo hilo.

Mbali na ukarabati wa jengo hilo, pia, Muhimbili imekarabati jengo lingine ambalo wataalam wa ugonjwa wa kifua kikuu watakuwa wanalitumia kutoa huduma.

Wagonjwa wa kifua kikuu wamekuwa wakionwa na wataalam katika Kituo cha Magonjwa Yanayoambukiza kwa njia ya hewa (IDC) na baadaye kupelekwa Muhimbili kwa ajili ya matibabu zaidi.

 Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)
 Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru akikata utepe ikiwa ishara ya kufungua  jengo la wagonjwa wa kifua kikuu lililokarabatiwa na mradi wa TB unaofadhiliwa na USAID chini ya Shirika la KNCV. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Muhimbili, Dkt. Hedwiga Swai, katikati ni Ofisa Mradi wa Shirika la KNCV, Irene Mauya na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la KNCV, Dkt. Vishnu Mahamba.
  Ofisa Mradi wa Shirika la KNCV, Irene Mauya akitoa maelezo kuhusu mradi huo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Museru wa tatu kutoka kushoto. Wengine ni wataalam wa MNH wakimsikiliza ofisa huyo.
  Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ndani wa Muhimbili, Dkt. Amina Mgunya akitoa maelezo kwa Prof. Museru wa pili kushoto kuhusu matumizi ya jengo hilo.
 Mkuu wa Kitengo cha Majengo Muhimbili, Injinia Gama Kimoto akimweleza Prof. Museru kuhusu ukarabati wa jengo litakalotumiwa na wataalam wa kifua kikuu wakati wa kutoa tiba. Jengo hilo limekarabatiwa na Muhimbili.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Museru akizungumza na wataalam wa MNH  na maofisa mradi wa Shirika la KNCV kuhusu ukarabati na matumizi ya jengo hilo baada ya kukabidhiwa leo.
 Prof. Museru akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa MNH na maofisa mradi wa Shirika la KNCV. Nyuma ni jengo la wagonjwa wa kifua kikuu lililokarabatiwa na KNCV

KADETFU NA BUKOBA DC WAINGIA MAKUBALIANO RASMI YA KUFANYA KAZI PAMOJA

$
0
0
 
Anaandika Abdullatif Yunus - Kagera.

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Kagera Development and Credit Revolving Fund (KADETFU) lenye Makao Makuu yake Manispaa ya Bukoba, limeiingia makubaliano rasmi na Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ya kufanya pamoja Shughuli mbalimbali za Kimaendeleo kwa Kushirikiana pande zote mbili.

Hapo awali KADETFU wamekuwa wakifanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kwa ushirikiano mkubwa na Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba kwa Muda mrefu pasina kuwepo Mkataba wa Maelewano, licha ya kuwa shughuli hizo zikiwemo za Kijamii zimekuwa zikifanikiwa kwa kiwango Kikubwa kama yalivyo matarajio yao.

Miongoni mwa shughuli zilizotekelezwa na KADETFU kwa kushirikiana na Halmashauri ya Bukoba ni pamoja na Kujengeana uwezo Kati ya Wataalamu wa pande zote mbili (KADETFU na Halmashauri), kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali, kusaidiana katika shughuli za Kazi, Kuwajengea wananchi uwezo katika masuala ya mipango na bajeti, Masuala ya Upashanaji Habari, Ununuzi wa mashine ya Kusaga iliyopo katika Kata ya Rubale, ununuzi wa Injini ya gari la Halmashauri, kuibua miradi n.k

Hata hivyo kwa Mkataba waliokabidhiana Januari 30, 2019 mbele ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani, mara baada ya kumalizika kwa Kikao cha Madiwani, una lenga kuendelea kushirikiana kwa pande zote mbili katika Miradi ya Utawala Bora na Uwajibikaji, kujenga uwezo kwa Kamati za Kata kwa kutafuta Wafadhili wa Kuendesha semina kwa Wafanyakazi na watumishi, lakini pia kuanzisha Mradi wa pamoja wa Kulinda haki za watoto wa kike katika masuala ya mimba za utotoni, ubakaji, unyanyasaji wa kijinsia n.k ambapo mradi huu unatarajiwa pia kulishirikisha Jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la jinsia.

Itakumbukwa pia KADETFU chini ya ufadhili wa Shirika la The Foundation for Civil Society (FCS), wametekeleza Mradi wa Ufuatiliaji wa uwajibikaji kwa Jamii (UUJ) katika sekta ya Elimu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba, lengo hasa likiwa ni kuwawezesha Wananchi kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya maendeleo ya Elimu katika maeneo yao, mradi ulioanza Julai hadi Desemba 2018.
 Mkurugenzi wa Shirika la KADETFU  Bwana. Yusto Muchuruza na Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Bukoba Mheshimiwa Murshidi Ngeze, wakikabidhiana Mkataba wa makubaliano ya kufanya kazi pamoja kati ya Kadetfu na Halmashauri hiyo Januari 30, 2018 katika Ukumbi wa Chemba.
 Bwana Yusto Mchuruza Mkurugenzi wa KADETFU akitoa maelezo machache kabla ya Kukabidhiana mkataba kati ya KADETFU na Halmashauri ya Bukoba wa kushirikiana kufanya Shughuli mbalimbali kwenye Halmashauri hiyo.
 Wajumbe wa Kamati ya Ufatiliaji wa uwajibikaji  wa watumishi wa umma, wakizungumza na Mkuu wa shule ya Msingi ya Ntoma iliyopo Kata Kanyangereko Wilayani Bukoba, juu ya Matumizi ya fedha za Shule hiyo.
 Afsa Mipango wa Wilaya ya Bukoba Bwana Julian Tarimo akitoa semina elekezi kwa wafanyakazi wa KADETFU katika maana ya ushirikiano uliopo kati ya pande zote mbili.

WAZIRI UMMY ATOA MABATI 200 KUSAIDIA UJENZI WA SHULE TANO ZA SEKONDARI JIJINI TANGA

$
0
0

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa halfa ya kukabidhi mabati 200 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano Jijini Tanga kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Hamis Mkoba
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kulia akimkabidhi Mabati 200 Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu baada ya kumkabidhi Mkurugenzi wa Jiji hilo Daudi Mayeji





WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu ametoa mabati 200 yenye thamani yash.milioni 4.2 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa shule tano za Sekondari Jijini Tanga.

Halfa ya makabidhiano hayo yalifanyika mjini Tanga kwenye shule ya Msingi Mwakidila ambapo Mkurugenzi wa Jiji hilo alipokea mabati hayo ikiwa ni mkakati wa Waziri huyo ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga kusaidia kuondosha changamoto ya uhaba wa madarasa.


Akizungumza mara baada ya kukabidhi mabati hayo, Waziri Ummy aliwashauriwa wazazi na walezi kuhakikisha wanafuatilia maendeleo ya watoto wao jambo ambalo linaweza kuwasaidia kufanya vizuri kwenye masomo yao.

“Ndugu zangu wazazi na walezi hakikisheni mnafuatilia maendeleo ya watoto wenu wanapokuwa shuleni kwani nyie pia mnaweza kuchangia ufaulu wa mtoto wako “Alisema. idha pia Waziri Ummy amehaidi kuchangia ujenzi wa madarasa kwenye shule ya Sekondari Kange ili kuchochea ukuaji wa sekta ya elimu kwa mkoa wa Tanga .

“Lakini pia niwashukuru watendaji wa Shirika la Tawode kwa kujitoa katika kuchangia maendeleo ya Jamii ya Tanga kwa kutafuta wafadhili mbalimbali wa ndani na nje ya mkoa huu”Alisema

WANANCHI,SERIKALI WAONDOA CHANGAMOTO WANAFUNZI WA SEKONDARI KUTEMBEA UMBALI MREFU KATA YA OLDONYOWASI

$
0
0
Na Woinde Shizza ,Globu ya jamii Arusha

WANAFUNZI ambao wamemaliza masomo elimu ya darasa la saba mwaka 2018 na kufanikiwa kujiunga na elimu ya sekondari wanaoishi Kata ya Odonyowasi katika Halmashauri ya Arusha, wameepukana na adha ya kutembea umbali mrefu baada ya Serikali  kuwapangia Sekondari ya Oldonyowasi ambayo ni
mpya na ipo ndani ya kata hiyo.

 Kabla ya kukamilika kwa sekondari hiyo wanafunzi wanaosoma masomo ya sekondari kutoka ndani ya kata hiyo walikuwa wakitembea umbali wa kilometa 16 kwenda na kurudi shuleni katika Shule ya Sekondari ya Oldonyosambu.Umbali huo ulikuwa changamoto kubwa kwa wanafunzi ikiwemo ya wengi wao kutofanya vizuri kwenye masomo na wengine kuacha shule.

Hivyo wazazi, walezi na wananchi wa Kata hiyo waliweka mkakati kuhakikisha wanaondoa changamoto hiyo ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.Waliamua kuchangishana fedha pamoja na kuomba msaada wa wadau wa maendeleo wakiwamo TANAPA na Serikali kupitia mradi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Akizungumza leo Januari 30, 2019, Mwenyekiti wa Kijiji cha Oldonyowas Geophray Ayoa amesema ujenzi wa sekondari hiyo mpya ya Oldonyowas, ulianza mwaka 2018 baada ya wazazi kukerwa na changamoto  zinazowakabili watoto wao, hasa ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata elimu ya sekondari. "Ujenzi ulianza kwa nguvu za wananchi kwa kushirikiana na TANAPA kwa kujenga vyumba viwili vya madarasa, ofisi ya walimu na vyoo pamoja na samani za ofisi na za madarasa kwa gharama ya Sh.milioni 70 huku TANAPA wakitoa Sh.milioni 50 na wananchi Sh.milioni 15,"amesema.

Aidha ameipongeza Serikali kupitia mradi wa TASAF awamu ya III,  kwa kuunga mkono juhudi za wananchi wa Oldonyowas,  kwa kuongezea nguvu na  kufanikiwa kujenga vyumba viwili vya madarasa na ofisi ndogo ya walimu, nyumba ya walimu yenye sehemu mbili (2 in 1), vyoo na jengo la utwala pamoja
na kununua  samani za ofisi na madarasa.Jumla ya Sh.milioni 229.4 zimetumika."Tayari imeanza kupokea wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza."

Pia amesema wananchi wa Oldonyowas wamekwenda mbali zaidi na kukusanya nguvu na kujenga jengo la  maabara za masomo ya Sayansi, jengo lililogharimu Sh.milioni 45 ambapo wananchi wamechangia Sh.100,000 kwa kila familia na kwamba jengo lipo hatua za umaliziaji.

Papmoja na kuishukuru Serikali kupitia TANAPA na mradi wa TASAF kwa kusaidia ujenzi sambamba na kukamilisha usajili, amewashukuru  wananchi wa Oldonyowas kwa kuchangia maendeleo ndani ya kata yao,  pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano ya kutoa elimu bila malipo mpaka
kidato cha nne, fursa inayowawezesha watoto wengi kuendelea na shule pindi wanapomaliza elimu ya msingi. 
Sehemu ya picha ikionesha Vyumba viwili vya madarasa na ofisi ndogo ya walimu, jengo linalojengwa na wananchi kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi ya Taifa - TANAPA.
 Picha ikionesha wanafunzi wa shule ya Oldonyowas wakiwa darasani

TAFITI ZABAINI ASILIMIA 72 VIFO VYA MIFUGO HUSABABISHWA NA MAGONJWA MBALIMBALI

$
0
0
Woinde Shizza Globu  ya jamii Arusha

TAFITI zinaonesha kuwa asilimia 72 ya vifo vya mifugo nchini, hutokana na magonjwa mbalimbali yakiwamo magonjwa yanayotokana na kupe na ndorobo, na kulisababishia taifa hasara ya Sh.bilioni 63 kwa mwaka huku takribani asilimia 70 ya ndama wanaozaliwa hufa kila mwaka kutokana na wafugaji walio wengi kutokuwa na muamko wa kuogesha mifugo yao.

Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Arusha , Dk.Wilson Mahera  wakati wa kukabidhi za viuatilifu vya kuua wadudu na  dawa ya kuogeshea mifugo.Baadhi ya viuatilifu ni vya kuulia wadudu aina ya kupe, mgao huo ni kutokana na mpango wa Serikali ya Awamu ya tano wenye lengo la kuhamasisha wafugaji kuogesha mifugo yao ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Amesema neema hiyo kwa wafugaji imetokana na  Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoa jumla ya lita 75 za viuatilifu aina ya 'Paranex' yenye kiini cha 'Alphacypermethtrin yenye uwezo wa kuua wadudu ya kupe kwa ajiki ya wafugaji wa vijiji vitano vya halmashauri ya Arusha."Inaonekana wafugaji hawana mwamko wa kuosha mifugo yao, kupitia Serikali ya Kijiji na  wajumbe wa kamati za uendeshaji majosho, ni vema kukafanyika uhamasishaji ili na usimamizi mzuri ili kila mfugaji anufaike na huduma hii,"amesema Dk.Mahera.

Ili kuzuia vifo hivyo na hasara kubwa inayoligharimu Taifa, Serikali imeanza kuwawezesha wafugaji kwa kutoa dawa za kuogeshea mifugo ili  kuzuia magonjwa yanayoenezwa na kupe, hivyo ni lazima  kuhamasisha wafugaji kuogesja  ng'ombe kupitia majosho yaliyo katika maeneo yao.

Aidha Dk.Mahera amewataka wajumbe wa kamati  hizo kushirikiana na Serikali ya kijiji chini ya usimamizi wa maofisa mifugo wa ngazi zote, kusimamia vema utoaji wa huduma hiyo kwa wafugaji kwa kuhamasisha na kuwahimiza wafugaji kuogesha mifugo yao,  pamoja na kusimamia fedha za mapato na matumizi ili
mradi huo uwe endelevu.

Amefafanua Serikali inatoa dawa hizo kama mtaji wa kuanzia kutoa huduma ya kuogesha mifugo na mapato yatakayopatikana, yatumike kuendeleza huduma hiyo kwa wafugaji katika maeneo yao huku akiwahimiza kushirikiana na Serikali ya Kijiji pamoja na maofisa mifugo katika maeneo yao.

Kwa upande wake Daktari wa mifugo katika Halmashauri ya Arusha Dkt. Linus Prosper ametaja  bei elekezi iliyotolewa na Serikali  ya kuendesha huduma hiyo ya kuogesha mifugo kwa kufafanua bei ya ng'ombe mmoja kwa muosho mmoja ni Sh.50 na kwa mbuzi na kondoo Sh.10 kwa mbuzi na kondoo kwa muosho mmoja.

Pia Serikali Serikali imefafanua gharama hizo zinaweza kubadilika, kulingana na gharama halisi za uendeshaji wa josho katika eneo husika kutegemea uamuzi Kamati ya Uendeshaji wa Josho husika.Aidha Dk. Linus amezitaja kamati nne za majosho, zilizokabidhiwa dawa  za kuogesha mifugo  ambazo ni Kamati ya Josho la Engutukoit kata ya Oldonyowas, Oloitushula kata ya Musa, kidali na Engalaoni kata ya Mwandet huku kila Josho likipata lita 10 za dawa.

Hata hivyo wajumbe wa kamati hizo wameishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuwakumbuka wafugaji, kwani kwa miaka mingi sasa, Serikali ilikua kama imewasahau na kuahidi kwenda kuhamasisha wafugaji kujitokeza kuogesha mifugo yao,  kwa gharama nafuu ambazo hapo awali wafugaji wengi walikua
wanashindwa kuzimudu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Josho la Oloitushula kata ya Musa, Manase Meoki, licha ya kuishuru Serikali kwa kuwakumbuka wafugaji, amesema kuwa uwepo wa dawa hizo, zilizotolewa na Serikali utawasaidia kupunguza gharama kubwa walizokuwa wakizitumia pamoja na kuepuka kuuziwa dawa zisizofaa na kuwataka wananchi wenzake kuunga mkono jitihada hizi za Serikali.

Halmashauri ya Arusha ina jumla ya majosho 18, majosho  nane  kati ya hayo ndio yanatoa huduma, majosho matano hayatoi huduma kutokana na uhalisia wa maeneo yalipo  tayari kumeshakuwa miji na kuwa katika makazi ya watu hivyo hayatumiki kwa sasa, huku majosho matano yakihitaji ukarabati
kutokana na uchakavu uliotokana na kujengwa muda mrefu.
 Picha ikionesha Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Arusha Dkt. Wilson Mahera akimkabidhi mmoja wa mjumbe wa kamati ya uendeshaji josho (jina halikuweza kupatikana) box lenye lita kumi za dawa.
Picha baadhi ya wajumbe wa Kamati za Uendeshaji Majosho, wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa dawa za kuogeshea mifugo.

WATUMISHI WA TASAF WAOANISHA MAFANIKIO YA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI NA USIMAMIZI THABITI WA SERIKALI.

$
0
0


Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw.Ladislaus Mwamanga(aliyesimama)akitia nasaha za ufunguzi wa Kikao kazi cha watumishi wa taasisi hiyo jijini DSM.

Mkurugenzi wa Programu za TASAF,Bw. Amadeus Kamagenge (aliyeshika kipaza sauti) akitoa mada kwenye kikao kazi cha Watumishi wa Taasisi hiyo juu kukamilika kwa awamu ya kwanza na maandalizi ya awamu ya pili ya Mpango wa kunusuru kaya maskini-PSSN.

Mmoja wa Maafisa Ufuatiliaji wa TASAF akisoma taarifa ya pamoja ya utekelezaji wa maafisa hao kwenye kikao kazi kilichoanza hapo jana jijini DSM.

Baadhi ya Watumishi wa TASAF akiwa kwenye ukumbi wa Mikutano wa taasisi hiyo wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji Bw. Ladislaus Mwamanga (hayupo pichani kwenye kikao kazi ambacho hufanyika kila mwaka kujadili utekelezaji wa shughuli za taasisi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF, Bw. Ladislaus Mwamanga(aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa taasisi hiyo wanaohudhuria kikao kazi kinachojadili utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo jijini DSM.
 
 
Na Estom Sanga- DSM.

Wafanyakazi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF wamekiri kuwa usimamizi na miongozo thabiti inayotolewa na Serikali imechangia kwa kiwango kikubwa kufanikiwa kutekelezwa kwa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wenye lengo la kuboresha maisha ya wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na Umaskini.

Akifungua kikao kazi cha Wafanyakazi wa Mfuko huo, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw.Ladislaus Mwamanga amesema mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo yamechangia jitihada za Serikali za kukuza na kuboresha maisha ya wananchi hususani wale ambao wamekuwa wakiishi katika dimbwi la umaskini na kuamsha ari ya wao kujiletea maendeleo.

Bwana Mwamanga amewaasa Watumishi hao wa TASAF kutobweteka na mafanikio yaliyopatikana katika kuwahudumia Walengwa wa Mpango huo wa Kunusuru Kaya Maskini badala yake waongeze jitihada zaidi ili lengo la Serikali la kupambana na adui umaskini liwe la mafanikio endelevu na makubwa zaidi kupitia Mpango huo.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amebainisha kuwa maelekezo ya Serikali katika kusimamia na kuboresha utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kwa awamu ya pili yakiwemo ya kuwashirikisha Walengwa Kufanya kazi yatazingatiwa ili kukuza kipato cha Walengwa hao na kuwawezesha kuchangia kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuboresha huduma za kijamii kwenye maeneo yao.

Bwana Mwamanga amesema kuwa kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini katika awamu yake ya kwanza , kumekuwa na mahitaji kutoka kwa baadhi ya wananchi ambao Mpango huo haujawafikia wakitaka wajumuishwe kwenye huduma za Mpango huo ambapo amesisitiza kuwa maelekezo ya Serikali ni kuhakikisha kuwa Wananchi wenye uhitaji na kuwa na vigezo vya kujumuishwa kwenye Mpango wapate huduma hiyo kazi ambayo amesema itatekelezwa katika awamu ijayo ya Mpango huo wa Kunusuru Kaya Maskini.

Katika awamu ya kwanza ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini takribani kaya Milioni Moja na Laki Moja zimeandikishwa na kuendelea kupata huduma za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF -ambayo ni sawa na asilimia 70 ya vijiji/shehia huku asilimia 30 ya vijiji/shehia ikisalia kutokana na ufinyu wa raslimali fedha.

Akitoa taarifa ya kukamilika kwa Awamu ya Kwanza ya Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini na Maandalizi ya Sehemu ya Pili ya Mpango huo inayotarajiwa kuanza hivi karibuni, Mkurugenzi wa Programu za Jamii wa TASAF, Bwana Amadeus Kamagenge ametaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana kwenye awamu ya kwanza kuwa ni pamoja na kuanzisha Masjala ya Walengwa zaidi ya Milioni Sita huku kazi ya kuhaulisha fedha ikitekelezwa kwa mafanikio makubwa kwa Walengwa tangu mwaka 2014.

Aidha amesema Serikali kupitia TASAF imefanikiwa kuhamasisha Wananchi ambao walikuwa wakiishi katika umaskini mkubwa kurejesha matumaini kwa kuanzisha miradi ya uzalishaji mali kwa kutumia sehemu ya ruzuku huku wakitekeleza masharti ya Mpango hususani yanayolenga katika sekta za Elimu na Afya na hivyo kujiongezea uwezo wa kukabiliana na kero ya umaskini.

KARIBUNI KWENYE MAONESHO YA AFYA BURE COLOSSSEUM HOTEL

$
0
0

Karibu katika Maonyesho ya Afya yatakayofanyika katika Hoteli ya Colosseum iliyopo Masaki siku ya Jumapili, tarehe 03/02/2019 kuanzia saa sita mchana hadi saa kumi jioni.

Pata nafasi ya kukutana na mabingwa katika kada zaidi ya 15 zikiwemo Lishe, Mazoezi, Ugonjwa wa Kisukari, Magonjwa ya Moyo, Afya ya Meno, Afya ya Akili, Msongo wa Mawazo, Matumizi ya Pombe na Ulevi, Madawa ya Kulevya, Afya ya Uzazi, Mahusiano, nk. Pia kutakuwa na walimu waliobobea katika malezi ya watoto watakaofundisha watoto Juu ya kutunza Afya zao!

Hakuna kiingilio! Karibu sana!

NMB yasaidia madawati Sekondari ya Magawa na vifaa vya ujenzi Zahanati ya Nganje, Mkuranga

$
0
0
Na Ripota wetu, Mkuranga

BENKI ya NMB imekabidhi msaada wa viti na madawati 50 kwa Shule ya Sekondari Magawa pamoja na baadhi ya vifaa vya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nganje Wilaya ya Mkuranga vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 10.

Vifaa hivyo vilikabidhiwa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo kwa Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Hamisi Mgalu (MB) katika hafla iliyofanyika kwenye Shule ya Sekondari Magawa wilayani Mkuranga.

Akifafanua zaidi juu ya msaada huo, Bi. Vicky Bishubo alisema viti na madawati 50 yaliyotolewa kwa Shule ya Sekondari Magawa vina thamani ya shilingi milioni 5, huku mbao 520 na misumari iliyotolewa kwenye ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Nganje inathamani ya shilingi milioni 5.

Aidha aliongeza kuwa Benki ya NMB inazipa kipaumbele changamoto za sekta ya elimu na afya nchini Tanzania kutokana na umuhimu wa sekta hizo, kwa kile kuwa kama nguzo kuu ya maendeleo kwa taifa na hata nchi yoyote duniani.

"..Tunatambua juhudi za Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ya kusimamia elimu na afya kwa nguvu zote kwa kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, na pia kuboresha utoaji wa huduma za afya mijini na vijijini; tunaipongeza Serikali kwa hilo."

Alisema Serikali inafanya mambo makubwa katika sekta hizo, lakini NMB kama wadau wanawajibu wa kuunga mkono juhudi hizi za maendeleo kwa kusaidia jamii kwani kupitia jamii ndio imeifanya benki kuendelea kufanya vizuri.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Hamisi Mgalu (MB) akipokea msaada huo aliishukuru Benki ya NMB kwa ukarimu wao wa kuijali jamii na kuziomba taasisi zingine zifuate nyayo za NMB katika kuisaidia jamii kwa mambo mbalimbali.

"...Nawashukuru, nawashukuru sana kwa kujitoa kwenu kwa jamii nimekuwa nikishuhudia mkisaidia jamii kupitia sekta mbalimbali, huu ni mfano wa kuigwa kwa kweli endeleeni kuisaidia jamii nasi tunaahidi kuunga mkono shughuli zenu," alisema Bi. Mgalu.


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Magawa wakiwa wamekalia madawati hayo mara baada ya kukabidhiwa na Benki ya NMB.
Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo akikabidhi sehemu ya madawati na viti 50 kwa Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Hamisi Mgalu (MB) kusaidia Shule ya Sekondari Magawa. Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 5. Wanaoshuhudia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga, Juma Abeid (kushoto) na Meneja wa Tawi la NMB Mkuranga, Joseph Iramba (kulia).

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Magawa wakibeba meza na viti mara baada ya kukabidhiwa na NMB.



Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo akikabidhi sehemu ya mbao 520 na misumari kwa Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Hamisi Mgalu (MB) ikiwa ni mchango wao katika ujenzi wa Zahanati ya Nganje iliyopo wilayani Mkuranga. Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 5. Wanaoshuhudia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga, Juma Abeid (kushoto) na Meneja wa Tawi la NMB Mkuranga, Joseph Iramba (kulia).
 

Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa NMB, Bi. Vicky Bishubo akizungumza katika hafla hiyo.

Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Hamisi Mgalu (MB) akiishukuru NMB kwa msaada wake.

Kesi ya uchochezi dhidi ya vigogo wa Chadema yapata Hakimu mpya

$
0
0
Na Karama Kenyunko, globu ya Jamii 

KESI ya uchochezi inayowakabili vigogo tisa wa Chadema akiwemo Mwenyekiti wa chama wao, Freeman Mbowe inayounguruma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imepangwa kuendelea kusikilizwa kwa Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina.

Hatua hiyo imekuja baada ya hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi Wilbard Mashauri kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Aidha, rufaa iliyokatwa na upande wa serikali kupinga uamuzi mdogo wa Mahakama Kuu wa kuendelea na usikilizwaji wa rufaa ya kufutiwa dhamana kwa Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko itaanza kusikilizwa katika Mahakama ya Rufani Februari 18, mwaka huu.

Mapema, wakili wa Serikali, Wankyo Simon ameeleza mahakamani hapo kuwa, kesi hiyo leo Januari 31.2019 imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba rufaa iliyopo Mahakama ya Rufani bado haijasikilizwa, hivyo aliomba Mahakama kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Profesa Abdallah Safari ameieleza mahakama kuwa rufaa imepangwa kusikilizwa Februari 18, 2019.Kufuatia taarifa hiyo, Hakimu Mhina ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 14, mwaka huu na kuwaeleza washitakiwa walio nje kwa dhamana kuwa dhamana zao zinaendelea Mbowe na Matiko wamerudishwa rumande.

Novemba 23, mwaka jana Jaji Mashauri akiwa Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, alifuta dhamana ya Mbowe na Matiko kwa sababu walikiuka masharti ya dhamana.Baada ya maamuzi hayo, washitakiwa wakiwakilishwa na Wakili wao Peter Kibatala walikata rufaa Mahakama Kuu kupinga maamuzi ya mahakama hiyo ya kufuta dhamana.

Hata hivyo, baada ya mahakama Kuu chini ya Jaji Sam Rumanyika kusikiliza mapingamizi ya pande zote iliamua kuanza usikilizaji wa rufaa hiyo.Upande wa serikali ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi ulikata rufaa kupinga maamuzi yaliyotolewa na kuiomba mahakama hiyo kuacha kuendelea kusikiliza rufaa hiyo kwa sababu haina mamlaka.

Kufuatia hayo, Jaji Rumanyika alisema mahakama yake imefungwa mikono hivyo anasitisha usikilizwaji wa rufani hiyo hadi hapo itakapotolewa uamuzi katika Mahakama ya Rufani.

Mbali na Mbowe na Matiko washtakiwaa wengine katika kesi hiyo ni Mbunge wa Iringa mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Katibu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji, Mbunge wa Bunda, Ester Bulaya, Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalimu ambao wote walikuwepo mahakamani.

Katika kesi ya msingi, washitakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari Mosi na 16, mwaka 2018 maeneo ya Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa chama wao, Freeman Mbowe akizungumza jambo na Mh.Lazaro Nyarandu.
Baadhi ya viongozi waandamizi wa Chadema wakijadiliana jambo
Baada ya Hakimu kuahirisha kesi hiyo hadi Februari 14,

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MABALOZI WATATU WAPYA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 31 Januari, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi kutoka nchi 3 ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Balozi wa kwanza kukutana na Makamu wa Rais, alikuwa Mhe. Gaber Mohamed Abulwafa Balozi mpya wa Misri hapa nchini ambaye alifika kwa lengo la kujitambulisha na pia kuzungumzia mambo mbali mbali ya kuimarisha uhusiano baina ya nchini  mbili ambao ulianzishwa na waliokuwa marais wa nchi hizi, Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais Gamal Abdel Nasser Hussein wa Misri.

“Misri itaendelea kutoa ushirikiano katika masuala ya Elimu, Afya na masuala ya teknolojia ya ujenzi wa miundombinu yenye tija kwa mataifa haya mawili” alisema Balozi huyo.Mwisho Balozi huyo mpya wa Misri aliahidi kusimamia miradi yote ambayo ipo kwenye makubaliano baina ya Serikali hizi.

Kwa upande wake Makamu wa Rais alimpongeza na kumkaribisha Tanzania pamoja na kumhakikishia ushirikiano mzuri katika kazi zake akiwa hapa nchini na kumueleza kuwa kwa miaka mingi uhusiano kati ya Misri na Tanzania umezidi kuimarika.

Balozi wa Pili kukutana na kuzungumza na Makamu wa Rais alikuwa Mhe. Francisca Pedros, Balozi mpya wa Spain hapa nchini ambaye Makamu wa Rais alimpongeza kwa kuwa Balozi wa kwanza mwanamke kuteuliwa kuja kuitumikia nchi yake hapa nchini.

Balozi wa Tatu kukutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Makamu wa Rais ni Balozi wa Ethiopia nchini Mhe. Yonas Yosef Sanbe ambaye alimueleza Makamu wa Rais furaha yake ya kuwa hapa na kuona namna mahusiano ya nchi hizi mbili yameboreka ambapo alisema kuwa,“nafarijika kuona namna ambavyo wanawake wanapewa nafasi za juu katika uongozi katika nchi hizi mbili”

Makamu wa Rais pamoja na mambo mengine alimpongeza Balozi huyo wa Ethiopia kwa kuwa Balozi wa kwanza mwenye makazi yake hapa Tanzania.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe. Mohamed Gaber Mohamed Abulwafa (kushoto) aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kujitambulisha, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe. Mohamed Gaber Mohamed Abulwafa (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Spain nchini Mhe. Francisca (kushoto) aliyefika kujitambulisha ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi mpya wa Spain nchini Mhe. Francisca Pedros (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na Balozi mpya wa Spain nchini Mhe. Francisca Pedros(kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Ethiopia nchini Mhe. Yonas Yosef Sanbe aliyefika kujitambulisha leo Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi mpya wa Ethiopia nchini Mhe. Yonas Yosef Sanbe aliyefika kujitambulisha leo Ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

MKUU WA WILAYA KAKONKO KANALI NDAGALA AHAMASISHA WATOTO WENYE ULEMAVU KUPELEKWA SHULENI KUPATA ELIMU

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma

MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala amewataka wananchi wenye watoto walemavu kuacha kuwaficha ndani na badala yake wahakikishe wanapeleka shule ili wapate elimu kama watoto wengine.

Aidha amewataka wazazi wote waliowahifadhi watoto wao katika kituo cha Watoto wenye ulemavu Kakonko kuwatembelea na kuwapa huduma zinazo stahiki kwa kuwa na wao wanahaki ya kuthaminiwa kama watoto wengine.

Maagizo hayo aliyatoa jana wilayani Kakonko wakati akikabidhi baiskeli saba za watu wenye ulemavu zilitotolewa na Shirika lisilo la kiserikali Help age International linalosaidia wazee na makundi maalumu yenye uhitaji kwaajili ya kuwasaidia watoto wenye ulemavu waliokuwa wameshindwa kwenda shule.

Amesema wapo watu wengi wenye ulemavu lakini sasa hivi ni wasomi wakubwa na wanazisaidia familia zao na kulisaidia Taifa, kuwa mlemavu ni jambo la kawaida hivyo wazazi wanatakiwa kuwaibua watoto wengine waweze kupata elimu na sio kuwanyanyapaa.

" Ulemavu sio ugonjwa, leo unaweza kuwa mzima kesho ukapata ajali na bado ukawa mlemavu, hivyo tunatakiwa kuwajali na kuwalinda walemavu bila ubaguzi wowowte kwani hata wao wanahitaji huduma za muhimu kama watu wengine", amesema Kanali Ndagala.

Aidha aliyaomba mashirika mengine ya wakimbizi kuendelea kutoa misaada katika Wilaya hiyo, kwa kuwa wanauhitaji mkubwa wa vyumba vya madarasa na miundombinu mbali mbali ilikusaidia Wilaya hiyo inainuka na kusonga mbele.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Help age Kigoma Fredi Kianda alisema Baiskeli hizo walizozitoa zina thamani ya shilingi milioni tisa na laki nane na hiyo ni hatua ya awali wataendelea kufanya uchunguzi kwa makundi yanayo hitaji msaada ili waweze kuleta msaada.

Amesema awali walianza kwa kutoa magodoro 600 kwa wazee wasio jiweza na shirika hilo litaendelea kutoa misaada hoyo ilikuhakikisha makundi ya walemavu na wasiojiweza wanapata misaada na wanaishi vizuri.

Shirika la help age shirika linalo husika kusaidia wazee na watu wenye mahitaji mbalimbali pamoja na walemavu walifanya uchunguzi na kufanya tathimini na kubaini watoto saba wenye ulemavu wa viungo na kuamua kuleta vifaa kwaajili ya kuwasaidia watoto wanaaandikishwa Shuleni.

Zoezi lingine la kufanya uchunguzi kuendelea kuchunguza wazeee na Watu wenye ulemavu lomezinduliwa rasmi na wataendelea kupita vijijini kuwabaini wote pamoja na watoto wenye ulemavu waliofichwa.


 

WAZIRI MKUU AMUWAKILISHA RAIS MAZISHI YA MKE WA MUFTI

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika mazishi ya mke wa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakary Bin Zubeir yaliyofanyika Kwamndolwa, Korogwe mkoani Tanga.

Akitoa salam kwa niaba yake amesema “Rais Dkt. Magufuli aliweka nia ya dhati kushiriki mazishi haya ila kwa bahati mbaya leo ana mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Arusha ambapo yeye ni Mwenyekiti.” 

“Mheshimiwa Rais amenituma nije nikupe pole wewe, watoto, familia na wote walioguswa na msiba huu. Mheshimiwa Rais anawaombea kwa Mungu ili mpate utulivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na nguzo katika familia. Haya yote ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu.”

Waziri Mkuu ameshiriki mazishi hayo ya mke wa Mufti, Bibi Hidaya Omar leo (Alhamisi, Januari 31, 2019).

Kadhalika, Waziri Mkuu amewasihi wafiwa na waombolezaji wote waendelee kuwa watulivu na kumuombea marehemu kila mmoja kwa imani yake ili Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema.

Kwa upande wake, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum akizungumza kwa niaba ya familia amemshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kumtuma Waziri Mkuu amuwakilishe katika mazishi hayo. Pia amewashukuru watu wote waliojitokeza kwa ajili ya kuifariji familia kutokana na msiba walioupata.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo niWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo, Mhe. Salma Kikwete, Mhe. Hawa Ghasia, Mhe. Mary Chatanda ,Mhe. Mkuu wa Mkoa wa TangaMartine Shigelana Masheikh wa Mikoa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika mazishi ya Hidaya Omar, mke wa Mufti wa Tanzania, Abubakary Zubier  yaliyofanyika katika kijiji cha Kwamdolwa wilayani Korogwe, Januari 31, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akishiriki katika sala ya jeneza  wakati wa mazishi ya Hidaya Omar, Mke wa Mufti wa Tanzania, Abubakary Zubeir  (kushoto kwa Waziri Mkuu) yaliyofanyika katika kijiji cha Kwamdolwa wilayani Korogwe, Januari 31, 2019. Kulia kwa Waziri Mkuu ni Sheikh Mohammed Kigoda aliyeongoza sala hiyo na kushoto ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,  Alhad Mussa Salum. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mufti wa Tanzania, Abubakary Zubeir  baada ya kushiriki katika mazishi ya Hidaya Omar, mke wa Mufti ,yaliyofanyika  katika kijiji cha Kwamdolwa wilayani Korogwe, Januari 31, 2019. Katikati ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum.

KAMPUNI YA KENYA KUNUNUA TANI LAKI MOJA ZA KOROSHO GHAFI TANZANIA

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, Dkt. Hussein Mansoor (kushoto) kwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya INDO Power Solutions ya nchini Kenya, Bw. Brian Mutembei (kulia) wakisaini Mkataba wa mauziano ya korosho ghafi kiasi cha tani laki moja kwa malipo ya Shilingii bilioni 418. Wanaoshuhudia tukio hilo muhimu ni Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (wa pili kushoto), Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Joseph Kakunda (kushoto), Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Innocent Bashungwa (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Kilimo na Mhe. Dan Kazungu, Balozi wa Jamhuri ya Kenya nchini. Tukio hilo lilifanyika kwenye Ukumbi wa mikutano uliopo Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha tarehe 30 januari 2019. Mawaziri hao wapo jijini humo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Dkt. Mansoor na Bw. Mutembei wakibadilishana Mkataba huo mara baada ya kusaini
Mhe. Prof. Kabudi akizungumza kabla ya kuanza kwa tukio hilo la kihistoria la kusainiwa mkataba wa ununuzi wa tani laki moja za korosho ghafi
Mhe. Kakunda nae akizungumza

Mhe. Dkt. Bashungwa akizungumza mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani)
Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Kazungu akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi ya kusainiwa mkataba wa ununuzi wa tani laki moja za korosho kutoka Tanzania
Bw. Mutembei nae akieleza furaha yake katika kukamilisha ununuzi wa korosho kutoka Tanzania
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Joseph Buchweshaija akizungumza kwa ufupi kuhusu hafla hiyo ya uwekaji saini mkataba wa ununuzi wa korosho. Wengine katika picha ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Mhe. Prof. Florens Luoga ( kulia walioketi) akifuatiwa na Prof. Sifuni Mchome, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria na Dkt. Evaristo Longopa, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Mkutano ukiendelea. Kushoto ni Mkurugenzi wa TanTrade, Bw. Edwin Rutageruka
=============================================================================================


Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Taifa ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko imesaini mkataba wa mauzo ya korosho ghafi kiasi cha tani laki moja kwa Kampuni ya Kenya ya INDO Power Solutions kwa malipo ya Shilingi bilioni 418.


Mkataba huo umesainiwa jijini Arusha tarehe 30 Januari 2019 kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Dkt. Hussein Mansoor kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw. Brian Mutembei, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya INDO Power Solutions ya nchini Kenya.


Tukio hilo la kihistoria lilishuhudiwa na Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Joseph Kakunda, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Innocent Bashungwa, Naibu Waziri wa Kilimo, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga,  Dkt. Evaristo Longopa, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali,

Viongozi wengine walioshuhudia ni Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dan Kazungu, Prof. Sifuni Mchome, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Prof. Joseph Buchweshaija, Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Prof. Siza Tumbo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Edwin Rutaberuka, Mkurugenzi wa TanTrade, Maafisa Waandamizi kutoka Serikalini na Waandishi wa Habari.


Awali wakizungumza kabla ya kusainiwa kwa Mkataba huo Mawaziri hao wakiongozwa na Prof. Kabudi, kwa pamoja walipongeza kwa dhati uamuzi wa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Serikali kununua korosho kutoka kwa wakulima ili kuepusha wakulima hao kuuza korosho zao kwa bei ya chini kwa watu wasio kuwa na nia njema kwa wakulima. Itakumbukwa kuwa, mwezi Novemba 2018, Mhe. Rais Magufuli alitoa maelekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo waratibu zoezi  la ununuzi wa korosho kutoka kwa wakulima kwa shilingi 3,300 kwa kilo moja.


Kwa upande wake Prof. Kabudi alisema kuwa anampongeza  Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi huo wa Serikali kununua korosho yote ili wakulima wapate bei inayolingana na jasho lao ambao hatimaye umezaa matunda kwa faida na maendeleo ya nchi.


Naye Mhe. Kakunda alieleza kuwa Bw. Mutembei ni mnunuzi wa kwanza kati ya wengi ambao walikuwa kwenye mazungumzo na Serikali kuhusu ununuzi wa korosho hizo. Mhe. Kakunda alisema katika majadiliano Serikali iliangalia kufanya biashara ya faida ambayo itawezehsa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo gharama za upakiaji na upakuaji, malipo kwenye Serikali za Mtaa na michango mingine ya kijamii kwa mujibu wa makubaliano. Hivyo aliwataka watanzania na wenye viwanda kutokuwa na wasiwasi kwani Serikali ina nia njema ya kuwaletea maendeleo wananchi hususan kupitia sekta ya kilimo cha korosho.


“Wakulima wa Korosho wanatakiwa kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi wake ambao unalinda maslahi ya mkulima na umewawezesha kuuza korosho zao kwa faida. Nawakaribisha wafanyabiasha makini kuja nchini kwani Serikali ipo tayari kuwasikiliza watu wa aina hiyo na kufanya nao biashara” alisema Mhe. Kakunda.


Kwa upande wake, Mhe. Bashungwa alieleza kuwa katika msimu wa korosho wa mwaka 2018/2019 tayari zimekusanywa tani 213,159 ambazo kati ya hizo tani 126,194 zimehakikiwa na tayari  wakulima wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Pwani wamelipwa fedha zao kwa zaidi ya asilimia 95.5. Mhe. Bashungwa aliongeza kuwa, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha Wakulima wote kulipwa fedha zao hadi kufikia tarehe 05 Februari 2019.


Akizungumza wakati wa tukio hilo, Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Kazungu alisema kuwa kusainiwa kwa mkataba huo ni faraja kubwa kwake katika historia ya mahusiano kati ya Tanzania na Kenya ambayo yanaendelea kuimarika siku hadi siku. Aidha, alieleza kuwa mkataba huo ni mfano mzuri wa kuimarika kwa mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hususan katika masuala ya kilimo na biashara.


Kwa upande wake, mnunuzi wa korosho hizo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Indo Power Solutions, Bw. Mutembei alisema amekuja kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Magufuli za kumwinua mkulima wa Tanzania na kwamba anawataka wale wote wanaobeza jitihada hizo za Mhe. Rais Magufuli kuacha mara moja huku akilaani kitendo cha baadhi ya wafanyabiashara kuendelea kuwakandamiza wakulima kwa kununua mazao yao kwa bei ndogo wanazopanga wao huku wakijua wazi kuwa wakulima hao wametumia gharama kubwa katika uzalishaji wa mazao hayo.


Pia aliwataka wafanyabiashara kufuata taratibu na sheria katika kufanya biashara kama Serikali zinavyoelekeza na kuacha kuchanganya biashara na siasa.


Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka, Dkt. Mansoor alieleza kufurahishwa na tukio hilo ambalo limekuja wakati mwafaka wakati nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zikijiandaa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika jijini humo hivi karibuni. Aidha alisema kuwa, kwa kiasi kikubwa tukio hilo limeiinua Bodi yake na kwamba anatoa wito kwa wafanyabiasha wengine wa ndani na nje ya Tanzania kuja nchini na kushirikiana na Bodi hiyo ili kuwakomboa wakulima wengi Zaidi.


Mkataba huo umesainiwa wakati baadhi ya Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Tanzania wakiwa jijini Arusha kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 1 Februari 2019.




Waziri Mbarawa azindua Bodi ya Taifa ya Maji

$
0
0
 Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akimkabidhi nyenzo za kutendea kazi Mwenyekiti wa Bodi ya Maji Taifa Profesa Hudson Hamis Ngotagu.
Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa akiwa na Katibu Mkuu, Profesa Kitila Mkumbo pamoja na Wenyeviti wa Bodi za Maji Tanzania.

TAEC YAENDESHA MAFUNZO KWA WANAFUNZI WA CEDHA JIJINI ARUSHA

$
0
0

Wanafunzi 53 kutoka katika Kituo cha Elimu ya Maendeleo ya Afya ( CEDHA) cha Jijini Arusha, walimu na Baadhi ya Wafanyakazi wa Tume ya Nguvu za Atomiki wakiwa katika picha ya Pamoja wakati wa hitimisho la mafunzo ya udhibiti na matumizi salama ya vyanzo vya mionzi




Na. Vero Ignatus, Arusha

Tume ya Nguvu za Atomiki nchini imeendesha mafunzo kwa wanafunzi 53 wa kituo cha elimu ya maendeleo ya Afya CEDHA juu ya matumizi ya mionzi

Mafunzo hayo yamefanyika makao makuu ya ofisi ya TAEC iliyopo Jijini Arusha kwa siku tatu yakiwa na lengo la kujifunza maswala mbalimbali yahusuyo faida, matumizi udhibiti na madhara yatokanayo na mionzi mahala pa kazi pamoja na sheria zake

Mafunzo yameendeshwa na TAEC kupitia wataalamu wake wafuatao

Bw Eng. John Ben Ngatunga - Mtafiti
Bw Simon Mdoe- Mtafiti
Bw Jerome Mwimanzi- Mtafiti
Bw Siwidhani Ndovi- Mtafiti

Kwa mujibu wa TAEC lengo kuu la mafunzo hayo ni kutoa elimu ya matumizi salama ya vyanzo vya mionzi ili kujifunza maswala mbalimbali yahusuyo faida, matumizi, udhibiti na sheria zake ili kuwawezesha wanafunzi hao kuelewa matumizi salama ya teknoljia ya Nyuklia na kujilinda pindi watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kikazi hapo.

Peter Ngamilo ni Mkuu wa kitengo cha mawasiliano kutoka TAEC ameeleza Kutokana na ufuatiliaji wa Mara kwa mara ambao unaambatana na ukaguzi unaofanywa na TAEC ,mpaka hivi sasa hakuna athari zozote zilizojitokeza kwenye maeneo ya kazi isipokuwa tu kuna baadhi ya vituo vichache ambavyo vimekuwa vikikiuka utaratibu na tayari imeshavichukulia hatua za Kisheria.

Hatua mojawapo iliyochukuliwa na TAEC ni pamoja na kuvifungia ili visitoe huduma ambayo itapelekea kusababisha athari za madhara ya mionzi kwa Wafanyakazi na mazingira yanayozunguka

TAEC inapenda kuwakaribisha wananchi na wadau mbalimbali ili kupata elimu hiyo juu ya yanayohusu udhibiti usalama wa mionzi na matumizi sahihi ya teknolojia ya nyuklia hapa nchini

Mkataba Kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na MOI Kuwanufaisha Wananchi

$
0
0

NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR

WIZARA ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) leo Mjini Unguja, imesaini mkataba na Taasisi ya Mifupa MOI. Mkataba huo wa ambao umerasimisha SMZ kuleta wagonjwa wake kupata matibabu katika Taasisi hiyo badala ya kuwapeleka nje ya nchi kama ambavyo imekuwa ikifanyika.

Katika tukio hilo, Utiaji wa saini wa mkataba umefanywa na katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Bi. Asha Ali Abdulla pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface huku likishuhudiwa na Mwanasheria wa MOI, Suleiman Mgerwa pamoja na Mwanansheria wa Wizara ya Afya Zanzibar Bi Shufaa Nassoro Ali.

Akizungumza katika tukio hilo, Katibu Wizara ya Afya Zanzibar Bi Asha Abdula amesema Serikali ya Zanzibar imeamua kurasimisha ushirikiano na Taasisi ya MOI kwani imekuwa ikitumia gharama kubwa kupeleka wagonjwa nje ya nchi wakati huduma hizo zinapatikana hapa Tanzania.

"Tumekuwa tukipeleka wagonjwa wengi nje ya nchi kwa matibabu hususani hawa wa mifupa, sasa tunafahamu kwamba wenzetu hawa wa MOI wameboresha sana huduma zao hivyo tumeamua wagonjwa wetu waende MOI badala ya kwenda nje, naamnini Mashirikiano hayo haya yatakuwa yenye tija kwa wananchi wetu" alisema bi Asha.

Bi Asha ameongeza kwamba wagonjwa wamekuwa wakienda MOI kupata huduma kwa kipindi kirefu lakini mkataba huu unafanya ushirikiano uwe rasmi na wagonjwa wapokelewe na kupata huduma kwa namna bora zaidi.

" Hili sio jambo jipya, wagonjwa wetu wanakuja huko kupata huduma na tunashukuru kwamba mmekuwa mkiwahudumia vyema, mkataba huu utaboresha namna mnavyowapokea na hata kama kutakuwa na changamoto yoyote kwa mgonjwa tutajadiliana na kuangalia nini cha kufanya kwani mambo sasa yamekuwa rasmi" Alisema Bi Asha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface amesema ni heshma kubwa kwa MOI kuingia mkataba na Wizara ya Afya ya Zanzibar ikiwa ni ishara tosha kwamba Serikali ya Zanziba imetambua maboresho yaliyofanyika MOI pamoja na huduma za ubora wa hali ya juu zinazotolewa.

"Tunawashukuru sana kwa Kuona kwamba huu ni muda muafaka wa kuingia makubaliano nasi, tunawashukuru sana kwa kutambua ubora wa huduma zetu, tunawaahidi kwamba wagonjwa watakaofika kwetu tutahakikisha wanapata huduma bora na kwa wakati kama ambavyo mnatarajia" alisema Dkt Boniface

Dkt Boniface amesema kwamba huduma zinazopatikana MOI kwa sasa ni sawa na zile zinazotolewa katika mataifa yaliyoendelea hivyo wagonjwa kutoka Zanziba watapata huduma nzuri tena kwa wakati.

"Ndugu Katibu Mkuu tumeboresha sana huduma zetu, tuna kitengo cha kisasa cha radiolojia, maabara na wodi za kisasa (Executive ) hivyo tunaamini wagonjwa kutoka Zanziba na watanzania wataendelea kupata huduma bora" Alisema Dkt Boniface

Hatua hii ni itapelekea wagonjwa kutoka Visiwani Zanziba kupata huduma za kibingwa katika Taasisi ya MOI na hivyo kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho kimekuwa kikitumika kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa matibabu.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar Bi Asha Ali Abdulla akikabidhiana mkataba wa Matibabu kwa wagonjwa kutoka Zanzibar na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Bonifece katika Hafla iliyofanyika Zanzibar leo (Picha na MOI)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar Bi Asha Ali Abdulla akitia saini mtaba wa wagonjwa kutoka Zanziba kupata huduma za kibingwa MOI
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface akitia saini mtaba wa wagonjwa kutoka Zanziba kupata huduma za kibingwa MOI
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface akizungumza na waandishi wa habari (Hawapo pichani ) katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika Zanziba leo
Mwanasheria wa MOI Bwana Suleimani Mgerwa akitia saini Mkataba huo
Mwanasheria wa Wizara ya Afya Zanziba Bi Shufaa Nassoro Ali akitia sini Mkataba huo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanziba Bi Asha Ali Abdulla akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani ) katika hafla ya utiaji saini leo Zanziba

TAKUKURU TEMEKE YASHINDA KESI MBILI MAHAKAMA WILAYA YA TEMEKE

Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images