Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

Dkt.Zainab Chaula aripoti wizara ya afya

0
0
Picha ya pamoja ya Viongozi wa Wizara na baadhi ya watumishi waliopo ofisi ndogo ya wizara hiyo
Waziri wa Afya,Maendekeo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akimsikiliza Katibu Mkuu mpua wa Wizara yake Dkt.Zainab Chaula(picha na Wizara ya Afya).
Dkt.Zainab Chaula akitoa salamu baada ya kukaribishwa Ofisi ndogo za Wizara hiyo,kushoto ni aliyekua Katibu Mkuu Dkt.Mpoki Ulisubisya 

Naibu Waziri Dkt.Faustine Ndugulile akitoa neno la ukaribisho wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto-Idara Kuu Afya (hayupo pichani)
Aliyekua Katibu Mkuu-Idara Kuu Afya Dkt.Mpoki Ulisubisya akimkabidhi baadhi ya vitendea kazi Katibu Mkuu Mpya Dkt.Zainab Chaula kwenye ukumbi wa ofisi ndogo ya Wizara jihini Dar es Salaam
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akimkaribisha Katibu Mkuu Mpya wa Idara Kuu Afya Dkt.Zainab Chaula kwenye ofisi ndogo za wizara zilizopo jijini Dar es Salaam mara baada ya kuapishwa

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK,ALI MOHAMED SHEIN ATUNUKU NISHANI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI WA SERIKALI YA ZANZIBAR

0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein akimtunuku Nishani ya Mapinduzi Bw.Said Bakari Jecha katika Hafla ya Kutunuku Nishani iliofanyika katika Viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.Ikiwa ni shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein akimtunuku Nishani ya Utumishi uliotukuka Bi Fatma Mohamed Said katika Hafla ya Kutunuku Nishani iliofanyika katika Viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.Ikiwa ni shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi waliohudhuria katika Hafla ya Kutunuku Nishani iliofanyika katika Viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.Ikiwa ni shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk,Ali Mohamed Shein akiwa katika Picha ya pamoja na Viongozi na watunukiwa wa Nishani katika Hafla ya Kutunuku Nishani iliofanyika katika Viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.Ikiwa ni shamra shamra za miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

TANESCO YAWAHIMIZA WAWEKEZAJI KUWEKEZA KWENYE VIWANDA, UMEME BORA NA WA UHAKIKA UPO WA KUTOSHA

0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Nchini TANESCO limewahimiza wananchi kuwekeza kwenye viwanda kwani hivi sasa umeme bora na wa uhakika upo, Meneja Miradi wa Shirika hilo, anayeshughulikia uzalishaji (Generation) Mhandisi Stephene S. A. Manda (pichani juu) amesema leo Januari 9, 2019. 

Amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akielezea utekelezaji wa miradi ya umeme Kinyerezi II wa Megawati 240 na ule wa upanuzi wa Kinyerezi I wa Megawati 185. “Mradi wa Kinyerezi namba II wa Megawati 240 umekamilika, kwa hivyo ombi letu kwa wote ambao wanaweza kuwekeza kwenye viwanda wawekeze kwani umeme wa uhakika na wa kutosha upo.” Alisema na kuongeza. 

Licha ya mradi huo wa Kinyerezi II Mradi mwingine ni wa upanuzi wa Kinyerezi I unaozalisha megawati 150 ili ufikie Megawati 335 kwa kuongeza Megawati 185.“Itakapofika Agosti 2019 jumla ya umeme utakaokuwa unatoka Kinyerezi pekee ni Megawati 575 kwa hivyo ni umeme wa kutosha, kama ni kulisha Dar es Salaam, basi Dar es Salaam nzima Kinayerezi inaweza kuibeba.” Alitoa hakikisho. 

Kwa hivyo uwezo wa kuhakikisha viwanda vinapata kile vinavyopasa kupata kuhusiana na umeme TANESCO imejipanga vizuri na tunaomba sana wawekezaji wawekeze, kiwanda si lazima kiwe kikubwa sana, hata cha kukoboa na kusaga nafaka na vile vya kukamua matunda ya kutoka Tanga na kwingineko. Alisema Mhandisi Manda. Alitoa wito kwa watanzania kuuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Rais Dkt. John Pombe Magufuli wa kujenga uchumi wa kati na wa viwanda kwani inawezekana kwa vile umeme upo, ulio bora na wa uhakika.
 Picha ya dron ikionyesha muonekano wa sasa wa mitambo ya kufua umeme wa gesi Kinyerezi II jijini Dar es Salaam. Mradi huo umekamilika na unafua umeme wa Megawati 240.






Meneja Miradi wa Shirika hilo, anayeshughulikia uzalishaji (Generation) Mhandisi Stephene S. A. Manda, akiwa kwenye chumba cha udhibiti mitambo (control room) cha kituo cha kufua umeme wa gesi Kinyerezi II leo Januari 9, 2019.

Mhandisi Stephene S. A. Manda (katikati), akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Miradi wa kampuni ya Jacobsen Elektro Ingar Tollum Andersen (kulia) na Mtaalamu wa kusimika mitambo kutoka kampuni hiyo, Markku Siren wakati alipotembelea kuona maendeleo ya mradi wa upanuzi wa Kinyerezi I leo Januari 9, 2019.

Picha ya dron ikionyesha muonekano wa sasa wa mitambo ya kufua umeme wa gesi Kinyerezi II jijini Dar es Salaam. Mradi huo umekamilika na unafua umeme wa Megawati 240.

Picha ya dron ikionyesha muonekano wa sasa wa mitambo ya kufua umeme wa gesi Kinyerezi II jijini Dar es Salaam. Mradi huo umekamilika na unafua umeme wa Megawati 240.

Mhandisi Manda akiwa juu kabisa ya jengo la utawala la Kinyerezi II, akifafanua kukamilika kwa mradi huo ambapo amesema kazi iliyobaki ni kuimarisha bustani na kusafisha njia.

Jengo la utawala Kinyerezi II kama linavyoonekana leo Januari 9, 2019.

Jengo la karakana na ghala la vifaa.

Mhandisi Manda akionyesha moja ya mashine mpya zilizoko kwenye karakana ya Kinyerezi II.

Meneja wa Kituo cha kufua umeme wa gesi cha Kinyerezi II, Mhandisi Ambakisye Mbangula, akiwa kwenye karakana ya kituo hicho leo Januari 9, 2019.

Meneja wa Kituo cha kufua umeme wa gesi cha Kinyerezi II, Mhandisi Ambakisye Mbangula, akiwa na mwangalizi wa karakana hiyo.

Mhandisi Manda akifafanua jambo kwenye chumba cha udhibiti mitambo (Control room) cha Kituo hicho.

MWANRI AAGIZA UCHUNGUZI KWENYE UJENZI WA TENKI LA MAJI KATIKA KIJIJI CHA IBELAMILUND WILAYANI UYUI

0
0
Na Tiganya Vincent, Tabora
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amesitisha kwa muda siku mbili kuendelea na ujenzi wa tenki ya ujazo wa lita laki tatu uliokuwa ukiendelea katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui baada ya kuzuka utata wa idadi ya nondo zilizokuwa zikitakiwa katika mzuko wake ambao unasababisha uduni wa ubora.

Hatua hiyo inalenga kutuma timu ya wataalamu ambao watakaochunguza kama ujenzi wake umezingatia maagizo yaliyopo kwenye ramani ya ujenzi na uko katika ubora unaotakiwa.

Mwanri ametoa kauli hiyo wilayani Uyui baada ya kauli za wataalamu kutofautiana na idadi ya nondo ambazo zimeshawekwa katika tenki hilo zikisubiri umwagaji wa zege

Alisema katika maelezo ya mkandarasi na takwimu zilizopo katika ramani zilionyesha kuwa tenki hilo lingechukua nondo 170 kukamilisha mzunguko lakini baada ya kuziheshabu zilikutwa 125.

Mwanri alisema ili kuepuka kujengewa tenki lililo chini ya kiwango ni vema wataalamu wapitie na kudhiirisha kuwa idadi ya nondo zilizosukwa katika tenki hilo zitatoa tenki bora.

Alisema likijengwa tenki chini ya kiwango cha matakwa ya michoro ya kihandisi linaweza kusababisha Serikali kupata hasara na kuwa na uwezekano kutokea maafa kama likipasuka kutokana na kutokuwa na ubora uliokusudiwa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alimtaka Mhandisi Mshauri wa mradi huo akiwa kama msimamizi Mkuu wa Serikali katika ujenzi wa mradi huo  kuhakikisha kazi inayofanyika inakuwa na ubora unaotakiwa na inalingana na fedha zilizolipwa.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema timu hiyo halitachukua muda mrefu ili kuhakikisha ujenzi wa mradi huo unaendelea na  kukamilika kwa muda ulipangwa.

Katika hatua nyingine Mwanri aliwataka wakazi wa maeneo yote ambayo mradi hiyo ya kuleta maji kutoka ziwa Victoria inatekelezwa kuhakikisha wanalinda vifaa vya Wakandarasi kwa kuwafichua watu wachache wenye tabia mbaya za wizi ili kutokuwa kikwazo cha kukamilisha mradi kwa wakati.

Alitoa kauli hiyo kufuatia malalamiko ya uwepo wa wizi wa nondo na saruji katika mradi wa  ujenzi wa tanki la Nzega mjini.

Mwanri aliwaagiza Polisi kuhakikisha wanaimarisha ulinzi na kuwachukulia hatua wale wote watakaobainika kuhusika na kuhujumu mradi kwa kuiba vifaa vya wakandarasi,

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Said Ntahodi alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kwa kuwapelekea mradi wa maji katika Wilaya ya Uyui kutoka ziwa Victoria.

Alisema hatua hiyo itasaidia kuwapunguzia adha ya kutafuta maji kwa watumishi na wananchi wa  maeneo ambayo mradi huo utapita na hivyo kuwapunguzia gharama za kutumia fedha nyingi kutafuta maji.

Ntahodi alimuomba Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuwafikishia shukurani zao kwa Rais Magufuli kwa kutekeleza ahadi yake ya kuwaondolea shida ya maji wakazi wa Isikizya na maeneo mengine ya Uyui.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi Tabora(TUWASA) Mukama Bwire alisema kuwa jumla ya vijiji 33 vilivyopo kando kando ya barabara kutoka Nzega hadi Tabora watanufaika na huduma ya maji safi na salama mara baada ya kukamilika mradi huo.
  Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (aliyechumaa) akipima upana wa nondo zilizotandazwa chini ya mradi wa ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui wakati wa ziara yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama kutembelea mradi wa maji wa ziwa Victoria.
  Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (katikati) akiwa ameshika nondo zilizoleta utata kabla ya kuanza zoezi za kuzihesabu ili kuona kama idadi yake inawiana na ile iliyopo katika mchoro wa ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui wakati wa ziara yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama kutembelea mradi wa maji wa ziwa Victoria.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (katikati) akipima upana wa nondo zilizosukwa kwenye  mradi wa ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui wakati wa ziara yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama kutembelea mradi wa maji wa ziwa Victoria.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (katikati) akiwa katika zoezi la kuhesabu nondo nyembamba zilizosukwa kwenye mradi wa ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui wakati wa ziara yake na Kamati ya Ulinzi na Usalama kutembelea mradi wa maji wa ziwa Victoria. Picha na Tiganya Vincent
 Nondo za ujenzi wa tenki la maji katika Kijiji cha Ibelamilundi wilayani Uyui ambazo zimesababisha mashaka na kumfanya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kusitisha kwa muda wa siku mbili kuendelea ya ujenzi hadi hapo timu ya wataalamu kutoka Mkoani watakaidhinisha kuwa idadi yake inalingana na zile zilizopo katika michoro.

Serikali Yashinda Kesi Dhidi ya Wanaharakati Kuhusu Kanuni za Maudhui Mitandaoni

0
0
Na: Beatrice Lyimo, MAELEZO

Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara imehukumu kwamba Waziri wa Habari, Utamaduni, sanaa na Michezo hakukosea wala kukiuka Katiba kwa kutunga Kanuni za Maudhui Mitandaoni za mwaka 2018.

Hayo yamejidhihirisha baada ya Mahakama hiyo kusikiliza na hatimaye kuitupilia mbali kesi iliyofunguliwa na Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu, Bodi ya Wadhamini wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Mtandao wa Watetea Haki za Binadamu Tanzania (Human Rights Defenders Coalition) dhidi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Katika shauri hilo walalamikaji wameshindwa kuthibitisha jinsi gani Kanuni hizo zitakavyo athiri haki za msingi za Walalamikaji katika masuala ya uhuru wa habari na mawasiliano ya mitandaoni.

Katika hukumu hiyo iliyotolewa leo Januari 9, 2019 Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara, imekubaliana na hoja za Mawakili wa Serikali kuwa Kanuni za Maudhui Mtandaoni zimetungwa kwa mujibu wa sheria na kupelekea Mahakama hiyo kutupilia mbali shauri hilo.

Shauri hilo liliendeshwa na mawakili kutoka Ofisi Mpya ya Wakili Mkuu wa Serikali ambao ni Bibi Alesia Mbuya, Bw. Ladislaus Komanya, Bw. Sylvester Mwakitalu, Bw. Johanes Kalungura, Bw. Killey Mwitasi, Bw. Abubakar Mrisha na Bibi Neisha Shao ambapo upande wa walalamikaji waliwakilishwa na mawakili Fulgence Masawe, James Marenga na Jeremia Mtobyesa.

Kwa hukumu ya kesi hiyo iliyofunguliwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Mtwara Septemba 4, 2018, sasa ni rasmi madai ya kwamba Kanuni hizo zinabana uhuru wa habari na kwamba zilitungwa kimakosa yaaanguka rasmi.

MAJALIWA AKUTANA NA MWALIMU WAKE WA SHULE YA MSINGI

0
0

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Mwalimu wake, Bibi Notburga Ivo Mbepera wakati walipokutana na kuzungumza mjini Songea hivi karibuni. Mwalimu huyo alimfundisha Waziri Mkuu katika Shule ya Msingi ya Mnacho wilayani Ruangwa 1973 – 1980.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MAADHIMISHO YA MIAKA 55 YA MAPINDUZI YAENDA SAMBAMBA NA UZINDUZI WA JENGO JIPYA LA KISASA LA OFISI YA NIDA

0
0

Afisa Usajili Msaidizi NIDA Bw. Makame Khamis Makame akitoa ufafanuzi kwa mgeni rasmi namna hatua za awali za Usajili wa Vitambulisho vya Taifa zinavyofanywa.
Kaimu Mkurugenzi NIDA Zanzibar Bw. Hassan H. Hassan akielezea jambo kwa mgeni rasmi na ujumbe wake wakati wa sherehe za uzinduzi wa jengo la ofisi za NIDA. Kulia ni Mh. Dkt. Khalid Salum Mohamed (Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi), wa pili kushoto ni Mh. Mohamed Aboud (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais) na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Dkt. Arnold M. Kihaule.

Baadhi ya watumishi wa NIDA Visiwani Zanzibar wakiwa wenye nyuso za furaha wakati wa sherehe za uzinduzi wa Jengo la Ofisi za NIDA wilaya ya Kati Dunga.



Mkurugenzi Mkuu NIDA, Dkt Arnold M. Kihaule akiiwasilisha taarifa ya ujenzi wakati wa sherehe ya Uzinduzi wa Jengo la NIDA Wilaya ya Kati Dunga.



Mh. Dkt. Khalid Salum Mohamed akizungumza mbele ya wageni waliohudhuria sherehe ya uzinduzi wa Jengo la NIDA wilaya ya Kati Dunga.



Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi, Mh. Dkt. Khalid Salum Mohamed(katikati mstari wa mbele) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na watumishi wa NIDA wakati wa Sherehe ya uzinduzi wa Jengo jipya la NIDA wilaya ya Kati Dunga.

………………………..

Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe Dkt Khalid Salum Mohamed amezindua jengo la ofisi ya Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wanaoishi Wilaya ya Kati Dunga – Tanzania Zanzibar.

Uzinduzi huo ulifanyika na kushirikisha wadau mbalimbali wa ndani na nje ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zikiwemo Taasisi za Muungano.

Akihutubia kwenye sherehe hizo Waziri Dkt. Khalid Salum Mohamed amewataka wananchi na wadau muhimu katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kutoa ushirikiano kwa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA); kuhifadhi na kutunza miundombinu ya Mfumo wa Taifa na Utambuzi kwani taarifa zinazopatikana katika mfumo huo zitasaidia kupata takwimu sahihi ambazo zitaimarisha uchumi wa Nchi.

Aidha amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwa juhudi zake za kuboresha mradi wa Vitambulisho vya Taifa unaosimamiwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa kujenga Ofisi za Usajili katika Wilaya mbalimbali nchini, na kusisitiza umuhimu wa Vitambulisho hivyo kwa wananchi, Kiuchumi, Kijamii na Kiusalama.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Vitambulisho vya Taifa, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Dkt. Anold Mathias Kihaule amesema, zaidi ya asilimia 96.5 ya wananchi wa Zanzibar wameshaandikishwa na zaidi ya asilimia 90 tayari wameshazalishiwa vitambulisho vyao.

Dkt Kihaule amesema kukamilika kwa jengo la ofisi ya usajili wilaya ya Kati Dunga limegharimu zaidi ya Shilingi za Kitanzania Bil. 1.9 na kufanya mpaka sasa jumla ya kiasi cha Shilingi Bil 32 kuwa zimetumika katika kujenga majengo 13 nchi nzima ambapo kwa upande wa Zanzibar jengo hilo linakuwa ni la kwanza kukamilika katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa majengo ya ofisi za usajili.

Pia ameishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mchango wake mkubwa ilioutoa ikiwamo upatikanaji wa viwanja na kupatiwa msamaha wa kodi mbalimbali (exemption) ambazo zimesaidia kukamilika kwa jengo hilo linalotarajiwa kuhudumia zaidi ya wakazi 47,000.

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa imeahidi kuendeleza mikakati ya ujenzi wa majengo ya Ofisi ili kusogeza karibu zaidi huduma kwa Wananchi, ambapo katika awamu ya pili ya Ujenzi itakayoanza hivi karibuni itakuwa na ujenzi wa ofisi zingine tatu kwa Unguja na Pemba.

Awamu ya kwanza ya ujenzi mbali na Tanzania Zanzibar; maeneo mengine yaliyopata majengo ya Ofisi ni mikoa ya Mwanza, Morogoro, Dar-es-salaam, Kibaha na Arusha.

Ujenzi wa Ofisi hizo umetokana na mkopo wa masharti nafuu kutoka Serikali ya Korea Kusini kupitia Benki ya Exim Korea.

WIZARA YA YA KILIMO IPO KATIKA MAPITIO YA SIFA ZA VIONGOZI WA VYAMA VYA USHIRIKA – MHANDISI MTIGUMWE

0
0

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Rukwa


Wizara ya Kilimo ipo katika mapitio ya sifa za viongozi wa Vyama vya Ushirika nchini ili kupata viongozi watakao ongoza kwa weledi sekta ya Ushirika.

Dhana ya kuchagua viongozi wa ushirika wenye sifa ya kujua kusoma na kuandika imepitwa na wakati hivyo kuna kila sababu ya kuchagua viongozi wenye weledi na utashi katika utendaji.

Hayo yameelezwa jana tarehe 8 Januari 2019 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe wakati akizungumza kwenye kikao kazi na maafisa wa Kilimo wa Wilaya za Mkoa wa Rukwa, Wadau mbalimbali wa Kilimo wakiwemo mawakala wa pembejeo, wasindikaji, wawakilishi wa vyama vya msingi vya ushirika na wakulima, kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.

Alisema kuwa mfumo wa ushirika ni nyenzo muhimu ambayo ukitumika vizuri itasaidia kuondoa umaskini wa wakulima hapa nchini na utaimarisha uanzishwaji wa viwanda kuleta tija katika kilimo hivyo ni lazima kuwa na juhudi za makusudi kuwa na viongozi wenye weledi.

Katibu Mkuu huyo katika ziara yake mkoani Rukwa alitembelea maduka na maghala ya mbolea yanayomilikiwa na kampuni za ETG, YARA na PREMIER na kujionea hali halisi ya upatikanaji wa mbolea ambapo amepongeza utoshelevu wa mbolea uliopo mkoani humo.

Akizungumzia swala la masoko ya mazao ya wakulima Mhandisi Mtigumwe alisisitiza kuwa ubora wa mazao ya wakulima ni suala la msingi kulizingatia ili kuweza kusaidia wakulima kupata masoko ya uhakika na kujiongezea kipato, kwani mazao bora yana ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kuhusu Milipuko ya visumbufu vya mimea, Mhandisi Mtigumwe alisisitiza kuwa ili kunusuru mazao ya wakulima nchini, hatua madhubuti zinaendelea kuchukuliwa ili kuweza kudhibiti wadudu wanaothiri mazao akiwemo Kiwavijeshi Vamizi (FAW). 

Hivyo, alitoa rai kwa Katibu Tawala wa mkoa wa Rukwa na Makatibu Tawala wote nchini, kuwaagiza Maafisa Kilimo kufanya tathmini ya awali na kubaini maeneo ambayo kiwavijeshi vamizi ameanza kuonekana ili Wizara kwa kushirikiana na halmashauri ziweze kuchukua hatua za kudhibiti milipuko ya kiwavijeshi vamizi kabla hajasambaa zaidi na kuleta athari kubwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe

MAGAZETI YA LEO AL HAMISI JANUARI 10,2019

0
0











UZALISHAJI SUKARI WAONGEZEKA TPC

0
0

Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda (kulia) na Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumba wakiwa ameshika sukari inayozalishwa katika kiwanda cha TPC kufuatia ziara waliyoifanya katika kiwanda hicho jana.
Picha ya Pamoja ya Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda (kulia) na Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumba wakiwa na uongozi nwa TPC,Bodi ya Sukari na Wataalamu wa Halmashauri.



Na Vero Ignatus,Kilimanjaro.

Kiwanda cha Sukari TPC kimeongeza uzalishaji wa sukari kutoka tani 36,000 ambayo ilikua ikizalishwa mwanzoni kabla ya ubinafsishaji na kufikia tani 110,000 ikiwa ni juhudi za kutatua changamoto ya upungufu wa sukari ya majumbani nchini ambayo ni tani 100,005.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Utawala kiwanda cha TPC ,Jaffari Ally alisema hayo katika ziara ya Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mgumba pamoja na Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda katika kiwanda hicho ambapo alisema kuwa bado wanaendelea na upanuzi wa mashamba na wanatarajia kuzalisha tani 120,000 .

Jaffari aliipongeza serikali kwa kuziba mianya ya biashara magendo ya sukari ambapo sukari zisizokidhi viwango zilizua zikiingizwa nchini na kushindanishwa katika masoko ya ndani hivyo kuathiri viwanda vya ndani.

“Wazalishaji wa sukari tunapenda kuipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuzibiti mianya ya uingizwaji holela wa sukari ,miaka ya nyuma soko lilichafuliwa na sukari iliyokua ikiingizwa nchini isiyokua na viwango na iliingizwa kwa njia ya magendo bila kulipiwa kodi wala ushuru ,sukari ambayo ilikua ikiathiri afya za watanzania tunaishukuru serikali kwa kuziba mianya” alisema Jaffari

Naibu Waziri wa Kilimo Omari Mghumba baada ya kutembelea kiwanda cha sukari cha tpc yakiwemo mashamba mapya ya miwa ,aliwataka wawekezaji hao kupanua wigo wa kilimo cha miwa ili kuongeza uzalishaji wa sukari .

Omari alisema kuwa kuna fursa kubwa ya uwekezaji katika mashamba ambayo yanastawi miwa yaliyopo katika mikoa ya Pwani,Kigoma,Musoma ambapo kuna maeneo makubwa ya uwekezaji.

Waziri wa Viwanda ,Biashara na Uwekezaji Joseph Kakunda alisema kuwa bado kuna fursa kubwa ya uwekezaji katika sukari ya viwandani ambayo ina soko kubwa ili kupunguza wimbi la kuagiza sukari ya viwandani kutoka nje ya nchi

NGOMA AFRICA BAND NA CD YAO MPYA AWAMU YA TANO HAPA KAZI

0
0
Si wengine ni ile bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya Ngoma Africa Band aka FFU-Ughaibuni ,inayoongozwa na mwanamuziki Kamanda Ras makunja wenye makao yao nchini Ujerumani,bendi hiyo iliyojizolea umarufu kila kona barani ulaya na kufanikiwa kuteka washabiki kwa kutumia muziki wao wa dansi wa bongo.

Ngoma Africa band ukipenda waite FFU ughaibuni au viumbe wa ajabu "Anunnaki Aliens" mara hii wamepakua CD yao "Awamu Ya Tano Uwanjani" yenye nyimbo
mbili za "Amkeni Kumekucha"  na "Awamu ya Tano Sasa Kazi"  nyimbo hizo ni utunzi na uimbaji wake Kamanda Ras Makunja akimshirikisha Chris-B  Bakotesa ambaye pia ni  solo gitaa na kundi zima la FFU wa Ngoma Africa band wakisindikiza kwa mdundo mzima wa Hapa Kazi Kumpigia Saluti na  kumuunga mkono Rais Magufuli


Felix Tshisekedi: Mgombea wa upinzani ashinda uchaguzi wa urais DRC

0
0
Wafuasi wa Felix Tshisekedi awali walikusanyika nje ya makao makuu ya chama chake Limete, Kinshasa Jumatano

Felix Tshisekedi ameshinda uchaguzi wa urais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, tume ya uchaguzi imesema.

Matokeo ya awali yanaonyesha mgombea huyo wa upinzani amemshinda mgombea mwingine wa upinzani Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali Emmanuel Shadary.

Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, alisema mapema Alhamisi kwamba Bw Tshisekedi alipata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na "anatangazwa mshindi wa urais mteule."

Tshisekedi alipata zaidi ya kura 7 milioni naye bw Fayulu akapata kura takriban 6.4 milioni, huku mgombea wa serikali Emmanuel Ramazani Shadary akipata takriban kura 4.4 milioni.

Iwapo matokeo hayo yatathibitishwa, Bw Tshisekedi atakuwa mgombea wa kwanza kabisa wa upinzani kushinda uchaguzi wa urais tangu DRC ilipojipatia uhuru.

Bw Tshisekedi yuko kwenye muungano wa kisiasa aliyekuwa mgombea wa chama cha UNC (Union for the Congolese Nation) Vital Kamerhe UNC ambapo walikuwa wamekubaliana kwamba Tshiskedi atagombea wadhifa wa rais naye Kamerhe awe waziri mkuu iwapo muungano wao utashinda urais.

Rais Joseph Kabila anatarajiwa kuondoka madarakani baada ya kuongoza kwa miaka 18.Mgombea wake aliyemteua kuwakilisha muungano tawala Emmanuel Ramazani Shadary amemaliza wa tatu.

Martin Fayulu ambaye awali alikuwa mgombea wa pamoja wa muungano wa upinzani kabla ya Tshisekedi na mgombea wa chama cha UNC (Union for the Congolese Nation) Vital Kamerhe kujiondoa kutoka kwenye muungano huo na kuunda muungano wao wawili, alimaliza akiwa nafasi ya pili.
 
CHANZO BBC Swahili.

TIMU YA MAAFISA HABARI WIZARA YA AFYA WASHUHUDIA UWEKEZAJI MKUBWA ULIOFANYIKA SEKTA YA AFYA,WAIPONGEZA SERIKALI

0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Timu ya Maafisa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto pamoja na Taasisi zake iko katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya kwa kuangalia uwekezaji katika Sekta ya Afya katika kipindi cha miaka mitatu ya serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Akizungumza  kwenye Kampeni hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mwakilishi wa Wizara ya Afya na Meneja wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma Gaudensia Simwanza amesema ziara hiyo katika Hospitali na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya ni kuangalia uwekezaji katika utoaji huduma bora za Afya kwa wananchi,kuhakikisha kuna nguvu kazi imara ya uzalishaji katika Sekta ya viwanda.

Amesema kuwa serikali imewekeza sehemu kubwa ya vifaa na mitambo katika hospitali na hali iliyofanya serikali kuokoa fedha nyingi kutibu wagonjwa nje ya nchi.

Simwanza amesema kuwa Hospitali ya MOI imekuwa na vifaa katika kila idara na kurahisisha utoaji huduma za Afya ambazo ni bora kutokana na Serikali kutilia mkazo uwekezaji wa vifaa tiba,mitambo, Dawa pamoja na vitendanishi.

Nae Afisa Habari wa MOI Patrick Mvungi amesema kuwa MOI itaendelea kutoa huduma bora kutokana na Serikali kuwekeza mashine mbalimbali zilizo kuwa changamoto,ambazo zilikuwa zinasababisha wagonjwa kupewa rufaa.

Mvungi ameipongeza serikali katika uwekezaji uliofanyika Hospitalini hapo pamoja na ujenzi wa majengo ya kisasa na kulaza wagonjwa kwenye 340 vitanda.Amesema katika ununuzi wa vifaa wamenunua Darubin ya kisasa ya sh.bilioni Moja.

Daktari Bingwa wa Upasuaji Moyo wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kissenge amesema serikali imenunua mtambo wa sh.Bilioni Tatu na kufanya Taasisi hiyo kuendelea kutoa huduma bora za Afya ndani na nje ya nchi.

Kissenge amesema kuwa Taasisi hiyo ni kati ya Taasisi 25 zinazotoa huduma za matibabu ya Moyo katika nchi za Afrika.Amesema magonwa ya Moyo yanatokana na wananchi kushindwa kufanya mazoezi pamoja hali ya ulaji wa vyakula.

Kissenge amesema kuwa nchi ya Thailand wananchi wake wanatumia baiskeli zaidi kuliko magari hali hiyo ni tofauti na hapa nchini ambao wanaona kutembea na magari ni ufahari. 
 Sehemu ya kufanyia  uangalizi wa magonjwa ya mwili wa binadamu kwa kutumia mitambo hiyo ambayo imenunuliwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt. John Magufuli katika Hospitali ya MOI. 
 Daktari wa Hospitali ya MOI Ngina Mitti Akizungumza na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
Daktari Bingwa wa Picha za MRI Rahma Hingora akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya katika Hospitali ya Mifupa (MOI) Jijini Dar es Salaam.

 Mgonjwa wa Figo Magesa Masigi akizungumza namna ya huduma za Afya zilizoboreshwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Muuguzi mwandamizi wa Kitengo cha Figo Moroa Nyamatara akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya jijini Dar es Salaam.
 Mratibu wa Maduka ya MSD Betia Kaema akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
 Duka la MSD lilopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambalo limejngwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.
 Afisa Habari wa MOI Patrick Mvungi akizungumza na waandishi habari kuhusiana na Mafanikio ya Miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uboreshaji wa upatikanaji wa vifaa katika Hospitali hiyo
 Jengo la MOI lilojengwa kwa udhamini wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
 Daktari Bingwa wa Hospitali ya MOI Hamis Shaban akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
 Meneja Uhusiano wa NHIF Akizungumza na wagojwa katika Hospitali ya MOI kuhusiana na utumiaji wa bima ya Afya katika Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam.
 Jengo la Watoto katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambapo limejengwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pembe Magufuli.
Moja ya mtambo wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI Ulionunuliwa kwa sh.bilioni tatu katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.

NAIBU WAZIRI MHE.KANYASU ATEMBELEWA NA BALOZI WA UINGEREZA NCHINI TANZANIA

0
0

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu (kulia) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke (katikati) mapema leo akiwa na ujumbe wake, wakati alipomtembelea ofisini kwake Mpingo House jijini Dar es Salaam
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu(katikati) mapema leo mara baada ya kufanya mazungumzo ofisini kwake Mpingo House jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu(katikati) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke (kulia) kabla ya kuagana naye wakati alipotembelewa ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania,Sarah Cooke (katikati) akizungumza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu(kulia) kuhusiana na mikakati mbalimbali ya kukabailiana na tatizo la ujangili wa tembo nchini mapema leo ofisini kwake Mpingo House jijini Dar es Salaam.(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT)

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke mapema leo Alhamisi Januari 10, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu katika ofisi ndogo ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Mpingo House jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamejadili namna ya kukabiliana na tatizo la ujangili wa tembo pamoja na mikakati ya kukuza utalii nchini.

Maafisa Kilimo na ugani watakiwa kuwafuata wakulima mashambani kutoa elimu ya viwavi jeshi vamizi

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo (wa pili toka kulia) akiwa pamoja na mwenye shamba hili Alenx Ndenge (kulia) pamoja na wataalamu mbalimbali wakiangalia namna viwavijeshi vamizi wanavyoanza kushambulia mimea ya mahindi wilayani Nkasi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo (wa pili toka kulia) akiwa pamoja na mwenye shamba hili Alenx Ndenge (kulia) pamoja na wataalamu mbalimbali wakiangalia namna viwavijeshi vamizi wanavyoanza kushambulia mimea ya mahindi wilayani Nkasi.



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza maafisa ugani wote wa mkoani humo kuhakikisha wanawafikia wakulima kwenye mashamba yao na kuwapa elimu ya kukabiliana na wadudu aina ya viwavijeshi vamizi ambao wanaonekana kuanza kuleta athari katika wilaya ya Nkasi.

Amesema kuwa wakulima wengi hawana elimu ya kukabiliana na wadudu hao hasa kujua aina ya dawa ya kutumia ili kuwaua na wasiendelee kuharibu mazao na kuongeza kuwa ni wakati wao sasa maafisa ugani kufanya kazi ya kuwasaidia wananchi kupata matokeo bora ya mavuno kwa kutoa elimu ya kukabiliana na wadudu waharibifu na magonjwa.

“Kitu cha kufanya ni maafisa ugani wote na maafisa kilimo wote washuke kwenda kwenye mashamba, wakague na kutoa ushauri wa moja kwa moja, dawa zipo zinapatikana wanaanzia dawa gani inayofuata ni ipi, ili tuweze kuwasaidia wakulima waweze kuokoa haya mahindi, DC hawa watu wasimamiwe washuke asibaki mtu kwenye ofisi zao,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo baada ya kuona athari ya viwavi jeshi alipotembelea shamba la mkulima wa mahindi Alex Ndenge katika ziara yake ya kuangalia maendeleo ya kilimo kwa wakulima na changamoto wanazokabiliana nazo ikiwemo upatikanaji wa pembejeo pamoja na mashambulizi ya wadudu na magonjwa ya mazao Wilayani Nkasi.

Kwa upande wake Afisa Kilimo wa Mkoa wa Rukwa Ocran Chengula alifafanua namna ya kupambana na wadudu hao na kutoa tahadhari kwa wakulima kuwa na tabia ya kupanda kwa kipindi kimoja na sio kupishana kwani hali hiyo hupelekea wadudu hao kuhama kutoka sehemu moja hadi nyingine ili kufuata mimea teke.

“Kuna sumu nyingine ukipiga inakuwa kwenye mmea, kwasababu huyu (mdudu) anatoa kinyesi kwahiyo ile sumu inaingia kwenye mmea kwahiyo anapokula anapata madhara anakufa, kwahiyo katika hatua za kwanza tunashauri (dawa aina ya) Duduba na hatua ya pili tunashauri dawa inaitwa “systemic” japo zina majina tofauti tofauti ni amjina ya kibiashara ila itumike hiyo baada ya kuona kwamba wameshaanza kutoa huu uchafu” Alieleza.

Kwa mujibu wa Afisa kilimo wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi Emanuel Sekwao amesema kuwa viwavijeshi vamizi hao wameshaathiri kwa asilimia 2 mpaka 5 kutegemea eneo lakini bado haijafikia hatua ya wadudu hao kuharibu mimea kiasi cha kushindwa kuzaa.

Katika kipindi cha mwaka 2018/19 mkoa unalenga kulima jumla ya hekta 599,345.45 za mazao mbalimbali, kati ya hizo hekta 517,482.15 ni za mazao ya chakula na hekta 81,863.3 za mazao ya biashara. Kutokana na eneo hilo mkoa unategemea kuzalisha jumla ya tani 1,817,171.84 za mazao ya chakula na biashara. Katika kiasi hicho tani 1,680,701.6 ni za mazao ya chakula na tani 136,470.25 ni za mazao ya biashara.

Milioni 50m/-za Tigo Jigiftishe zaenda kwa mkulima Songea

0
0

Mshindi wa zawadi kubwa ya shilingi milioni 50 katika Promosheni iliyomalizika ya Tigo Jigiftishe Sadiki Zabroni Kilipamwambu, akiwa amebebwa na wafanyabiashara wenzake wa nyanya wakati akienda kupokea zawadi yake katika hafla ya kumkabidhi zawadi iliyofanyika katika soko la Manzese mjini Songea.
Mshindi wa zawadi kubwa ya shilingi milioni 50 katika Promosheni iliyomalizika ya Tigo Jigiftishe Sadick Zabron Kilipamwambu (wa tatu kushoto) akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Meneja wa Tigo Kanda ya Kusini Abbas Abrahaman (wa pili kushoto). Wanaoshuhudia ni wafanyakazi wa Tigo na mshereheshaji wa shughuli hiyo Okechi Okechi.
Mshindi wa zawadi kubwa ya shilingi milioni 50 katika Promosheni iliyomalizika ya Tigo Jigiftishe Sadick Zabron Kilipamwambu kutoka Songea, akionyesha nyumba anayoishi muda mfupi kabla ya kukabidhiwa zawadi yake mjini Songea.
Mshindi wa zawadi kubwa ya shilingi milioni 50 katika Promosheni iliyomalizika ya Tigo Jigiftishe Sadick Zabron Kilipamwambu kutoka Songea, akimuonyesha Meneja wa Tigo Kanda ya Kusini Abbas Abrahaman (wa kwanza kushoto) na Oliver Baltazar ambaye ni mratibu wa biashara na masoko wakwa kanda ya Kusini shamba lake la nyanya.




Mkulima na mfanyabiashara wa nyanya katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Sadick Zabron, amejishindia kitita cha shilingi milioni 50 baada ya kuibuka mshindi katika droo kubwa ya promosheni iliyomalizika ya Tigo Jigiftishe.

Zabron ndiyo mshindi wa zawadi kubwa katika Promosheni ya Jigiftishe. Washindi wengine katika droo kubwa ni Emma Kauka mkazi wa Dar es Salaam na Abdulrazak Abdallah mkazi wa Zanzibar alijishindia Sh 15m/-

Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhiwa zawadi iliyofanyika katika Soko Manzese mjini Songea, Zabroni alisema maisha yake yatabadilika kwa kiasi kikubwa kupitia fedha hizo.

“Sikuwahi kuwaza kumiliki kiasi kikubwa cha fedha kama hiki…, maisha yangu yatabadilika. Nitajenga nyumba nzuri na kuachana na kibanda cha nyasi nilichokuwa nikiishi na familia yangu. Naishuru Tigo kwa kubadilisha maisha yangu,” alisema

Mshindi huyo alisema atatumia fedha hizo pia kupanua shughuli zake za kilimo cha nyanya kwa kulima mashamba makubwa zaidi na kwa klimo cha kisasa na pia atatumia fedha hizo kuwaendeleza watoto wake kielimu.

Zabron alisema kushinda kwake kunatokana na kuingiza vocha za Tigo kwa ajili ya kufanya mawasiliano na wateja wake wa nyanya pamoja na kutuma au kutumiwa fedha mara kwa mara kupitia Tigo –Pesa.

Akiongea wakati akimkabidi zawadi kwa mshindi, Meneja wa Tigo kwa Kanda ya Kusini Abbas Abrahaman aliwataka wakazi wa maeneo Songea na jirani kuendelea kutumia mtandao wa Tigo ili kuweza kunufaika.

“Zipo faida nyingi za kutumia Tigo. Ni mtandao wa uhakika na gharama nafuu. Leo mmeshuhudia mwenzenu akiweza kujishindia Sh milioni 50m/-kwa kutumia tu mtandao wa Tigo na hii inaonyesha kuwa Tigo inawajaili wateja wake,”alisema

Wanafunzi watoro na wazazi wao kusakwa na kukamatwa huku hostel ikibadilishwa matumizi

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Leonard Wangabo.


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza mkuu wa Wilaya ya Nkasi kuhakikisha anawatumia watendaji wa kata na vijiji pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya kuhakikisha wanawasaka na kuwakamata wanafunzi watoro pamoja na wazazi waoili kuhakikisha wanafunzi wote wanafika shule.

Amesema kuwa kwa kufanya hivyo itakuwa fundisho kwa wazazi ambao kwa makusudi wanaacha watoto wao kutokwenda shule huku akipigia mfano faida ya elimu kwa kuwataja viongozi mbalimbali wa kiserikali akiwemo yeye mwenyewe pamoja na wataalamu waliozingatia elimu na matokeo yake wamefanikiwa kimaisha.

“Kuna wanafunzi 173 watoro, hawajafika shuleni, sasa Mkurugenzi fuatilia shule yako, mkuu wa wilaya tumia watendaji wa vijiji, wa kata, kamati yako ya ulinzi, sakeni wanafunzi wote kamateni wazazi wao mpaka walete watoto wao shule, hatubembelezani hapa,”Alibainisha.

Ameyasema hayo alipotembelea shule ya sekondari Korongwe Beach katika Kijiji cha korongwe, kata ya Korongwe Wilayani Nkasi ili kujionea mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza pamoja na ujenzi wa madarasa ambapo wanafunzi 50 wamepangiwa kuanza kidato cha kwanza huku 17 tu wakiwa wameripoti na shule ikiwa na jumla ya wanafunzi 383.

Awali akitoa taarifa ya shule hiyo Mwalimu Mkuu wa shule Nicomedi Ntepele amezitaja changamoto za shule hiyo ikiwemo utorowa rejareja na wa kudumu, ukosefu wa madarasa na nyumba za waalimu, ofisi za waalimu na maji.

“miongoni mwa changamoto tulizonazo hapa shule ni pamoja na utoro wa wanafunzi wa reja reja na wa kudumu, ukosefu wa madarasa, pia wazazi kutokuwa na uelewa kuwaleta Watoto wao kuishi hostel, uhaba wa maji eneo la shule, ofisi za walimu kutokamilika hivyo tunaomba changamoto hizi kufanyiwa kazi ili tufanye kazi kwa ufanisi,” Alimalizia.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Missana Kwangula aliamua kubadilia matumizi ya hosteli ya wanafunzi wa kike kutumiwa na wanafunzi wa kiume baada ya Mh. Wangabo kumtaka ajibu maombi ya mwanafunzi Ibrahimu Musa ambaye pia ni kaka mkuu wa shule hiyo juu ya kujengewa hosteli baada ya Mkuu wa Mkoa kutoa nafasi kwa wanafunzi kuuliza maswali.

“Wanafunzi tunatembea umbali mrefu hasa Watoto wa jinsia ya kiume, sisi tulikuwa tunaomba ndugu Mkuu wa Mkoa uweze kutujengea sisi pia hosteli ili na sisi tuweze kukaa bweni nasi tuweze kufanya vizuri katika masomo yetu,”Alisema

Katika shule hiyo ya Korongwe Beach Sekondari kuna hosteli ya wanawake iliyojengwa kwa msaada wa watu wa Japan (JAICA) pamoja na serikali ya Tanzania, hosteli ambayo kwa mujibu wa taarifa ya mwalimu mkuu wa shule haijawahi kutumika tangu kumaliziwa kwake, ndipo Mkurugenzi aliposema.

“Hosteli ile ilipojengwa ilikuwa ni kwaajili ya kuawasaidia Watoto wa kike kwasababu ndio wanachangamoto zaidi, lakini kwasababu hosteli ile hawaingii walengwa ambao wako hapa, tuna uwezo tu wa kuibadilisha matumizi na uiandika hosteli ya wavulana kuliko kujenga hosteli nyingine, tutakapobadili matumizi ninyi Watoto wa kike msige kuidai tena wakati ipo sasa hamuingii,” Alimalizia.

Shule ya Sekondari Korongwe Beach ina wanafunzi 383 na kushika nafasi ya kwanza kiwilaya katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2018. Na wanafunzi 50 wamepangwa kuanza kidato cha kwanza huku 17 wakiwa wameripoti shuleni.

Tanzania Kutoa Taarifa Kuu ya Malengo Endelevu 2030, Julai Mwaka Huu

0
0
Mwandishi Wetu-MAELEZO.

Tanzania inatarajia kutoa taarifa ya takwimu ya malengo endelevu ya dunia 2030 Julai mwaka huu, huku suala la elimu likipewa kipaumbele katika taarifa hiyo.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam kwenye mkutano na wadau wa takwimu kutoka Sweden, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt Albina Chuwa amesema kuwa lengo kuu lililowakutanisha na wadau hao ni kutoa taarifa kuhusu taarifa kuu ya malengo endelevu ya dunia ya mwaka 2030.

“Huu mkutano lengo lake kuu ni kuwapa wananchi taarifa ya maendeleo ya utengenzaji wa kanzi data ya takwimu za kuripoti katika malengo endelevu ya dunia ya mwaka 2030 ambayo inatarajia kuwekwa hadharani Julai mwaka huu”, Alisema Dkt.Chuwa.

Dkt Chuwa alisema kuwa utengenezaji wa kanzi data hii umeanza muda mrafu kwa Ofisi ya Takwimu ikishirikiana na mtaalamu kutoka Sweden (Alexandra Silfverstolpe) ambaye anafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Ofisi ya Takwimu nchini humo.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu ilipata uzoefu wa kutengeneza kanzi data hii kutoka nchi mbalimbali duniani ikiwemo Colombia kwa kuwa kanzi data hizo zinaonyesha namna ya kutatua matatizo ili kutimiza malengo endelevu kwa taifa.

“Kanzi data hii inaonyesha viashiria kwenye malengo endelevu kwa mfano viashiria vya namna gani Tanzania itaondokana na umasikini ifikapo mwaka 2030, kwa hiyo ni rahisi kwa watu wanaotekeleza sera, wanasiasa na watawala wanaotoa maamuzi katika uchumi wa nchi kwani kanzi data hizi zitawasidia katika kazi zao”, Alisema Dkt. Chuwa.

Aidha aliongeza kuwa shabaha kubwa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu ni kushirikisha wadau wa maendeleo katika kuweka Takwimu sawa kwa hiyo mkutano wa Ofisi ya takwimu na wadau wa Takwimu kutoka Sweden wamejadili pamoja hatua ya utengeneza kanzi data na kutoa kipaumbele malengo enedelevu ya mwaka 2030 katika sekta ya elimu.

“kwa sasa kazi hii imefikia kwenye hatua nzuri ya kuingiza data kutoka kwenye kanzi data kuziweka kwenye Taarifa kuu inayotarajia kutolewa Julai mwaka huu, kwa hiyo tutafanya kazi hii karibu sana na hawa wenzetu ili kutoa taarifa yenye kiwango cha kimataifa”, Alisistiza Dkt.Chuwa.

Akizungumzia marekebisho ya sheria ya takwimu, Mkurugenzi huyo wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu aliwatoa wasiwasi wananchi kuwa hakuna mtu yeyote atakayefungwa kwa kufuata taratibu za utoaji takwimu kwa kutumia data kamili kwani nchi zote duniani zinahitaji data zenye kufuata utaratibu.

WADAU WAKUTANA TABORA KUANDAA JUMBE ZA KUTOKOMEZA UKATILI WA WANAWAKE NA WATOTO

0
0
WANANCHI wametakiwa kuunganisha nguvu pamoja kuhakikisha wanatokemeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto na mimba za utotoni hapa nchini kama ilivyoekelezwa katika Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokemeza Ukatili wa wanawake na watoto(MTAKUWWA). Tatizo hilo linasababisha athari nyingi ikiwemo vifo, ulemavu , kuwa na kundi kubwa la watoto kukimbilia mitaani na umaskini kwa watoto wanaokatishwa masomo na ndoto zao la baadae na hivyo kudhofisha juhudi za ujenzi wa uchumi wa kati na viwanda hapa nchini.

Kauli hiyo imetolewa  na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu Tawala Msaidizi Raphael Nyanda kwenye ufunguzi wa mafunzo ya kuandaa ujumbe wa kupinga ukatili dhidi ya wananwake na watoto na mimba za utotoni. Alisema suala hilo ni kubwa katika baadhi ya jamii na hivyo linahitaji kila mwanajamii kuwa mstari wa mbele kukemea na kutoa taarifa ambazo zitasaidia kukomesha ukatili kwa watoto , wanawake na kuondoa ndoa na mimba za utotoni hapa nchini na wahusika kufikishwa katika vyombo vya sheria.

 Nyanda alisema kuwa wakati mwingine vitendo vya ukatili vimekuwa vikifanyika katika jamii huku  wanajamii wanakaa kimya wakiwemo baadhi ya viongozi wa maeneo husika wakiwa wamefumba macho. Alisema ni lazima jamii itambue kuwa ukatili unafanyika kwa mtoto wa jirani kesho unaweza kufanyikwa kwa watoto wao na hivyo wanapaswa kuchukua hatua wanapoona vitendo vya namna hiyo vikifanyika.

 Awali Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii ya Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Grace Mwangwa alisema mikoa ambayo ina vitendo vya juu vya ukatili wa wanawake na watoto ndio hiyo hiyo ipo juu katika tatizo la mimba na ndoa za utotoni. Aliitaja mikoa inayoongoza kwa mimba za utotoni kuwa ni Katavi kwa  asilimia 45, Tabora asilimia 43, Morogoro 39 na  Mara asilimia 39 na kwa upande wanajifungua kwa umri mdogo  ni Shinyanga kwa asilimia 59, Tabora 58, Mara 55, Dodoma 51 na Lindi 48.

 Mwangwa aliwaomba viongozi wa Dini hapa nchini kutumia ushwawishi wao wa kiroho kukemea ukatili wa wanawake na watoto kama vile upigaji wa wanawake na watoto, ukeketaji unaoendelea kwa siri katika baadhi ya maeneo, ndoa za utotoni na mimba za utotoni ambazo nyingine zinatokana na kubakwa.

 Aidha aliwataka wazazi au walezi wa watoto kuwa makini na kuwalaza watoto wao chumba kimoja na wageni kwa kuwa wakati unyanyasaji ikiwemo ubakaji na ulawiti unafanywa na watu hao ambao wamekaribishwa kama ndugu au marafiki. Alisema hatua hiyo inatokana na utafiti ambao umeonyesha asilimia 60 ya ukatili kwa watoto ufanyika nyumbani na 40 ndio unaofanywa katika maeneo ya Shule.

 Mkurugenzi Msaidizi huyo alisema ukatili kwa watoto ni pamoja na matusi, vipigo, kuchomwa moto wakifanya kosa, kunyimwa chakula, kubakwa, kulawitiwa na kuolewa katika umri mdogo. Aliitaka jamii kurudi katika mitazamo ya awali ambapo kila mtu mzima alimchukulia kila mtoto anayemuona mbele yake ni mwanae.
 Kaimu Katibu  Tawala Mkoa wa Tabora Raphael Nyanda (katikati) akifungua mafunzo ya kuandaa ujumbe wa kupinga ukatili dhidi ya wananwake na watoto na mimba za utotoni. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii ya Wizara ya Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Grace Mwangwa na kushoto niAfisa aneyeshughulikia Maendeleo ya Jamii kutoka Ofisi ya Rais , Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mwajina Ally.
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya  kuandaa ujumbe wa kupinga ukatili dhidi ya wananwake na watoto na mimba za utotoni  wakiwa katika mafunzo hayo mjini Tabora.
Kaimu Katibu  Tawala Mkoa wa Tabora Raphael Nyanda(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiri wa  mafunzo ya kuandaa ujumbe wa kupinga ukatili dhidi ya wananwake na watoto na mimba za utotoni. Picha na Tiganya Vincent

DR.MARY MWANJELWA AVUTIWA NA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI UNAOTEKELEZWA NA TASAF.

0
0
Na Estom Sanga-DSM

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ,Dr. Mary Mwanjelwa ameuagiza Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF kuendelea na Utaratibu bora zaidi wa kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa shughuli za Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ili Wananchi waweze kunufaika na Mpango huo ulioanzishwa na kutekelezwa na Serikali.

Dr. Mwanjelwa ametoa agizo hilo alipokutana na Menejimenti na Watumishi wa Mfuko huo akiwa katika ziara yake ya kikazi na kujitambulisha kufuatia uteuzi uliofanywa na Rais Dr. John Magufuli hivi karibuni ambapo Naibu Waziri huyo alihamishiwa katika Wizara hiyo.

Naibu Waziri huyo amesema pamoja na mafanikio makubwa ambayo Mfuko huo umeyapata katika kuhudumia takribani Kaya Milioni Moja na Laki Moja za Wananchi wanaoishi katika umaskini, haupaswi kubweteka kwani suala la kupambana na Umaskini ni agenda muhimu katika Mipango ya Serikali ambayo pia imeainishwa kupitia ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Aidha Dr.Mwanjelwa ameagiza Watumishi wa TASAF kuwa Wabunifu na kufanya kazi kwa karibu zaidi na Wananchi hususani walioko katika Mpango ili Matokeo ya utekelezaji wa Shughuli za miradi yawe endelevu na yanayopimika ili hatimaye kero ya umaskini miongoni mwa Wananchi iweze kupunguzwa kama siyo kumalizika kabisa.

Akizungumzia utekelezaji wa shughuli za Miradi ya Ajira ya Muda, Naibu Waziri huyo wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ameagiza TASAF kuhakikisha kuwa miradi inayotekelezwa kupitia utaratibu huo ni ile inayowanufaisha wananchi na malipo yafanywe kwa kuzingatia kanuni na taratibu za Serikali.

Wakati huo huo Dr. Mwanjelwa ametoa rai kwa halmashauri za wilaya kusimamia kwa karibu miradi inayotekelezwa na TASAF kwenye maeneo yao na kuonya kuwa pale ambapo itadhihirika kuwa halmashauri inakiuka taratibu wa miradi hiyo hatua zitachukuliwa haraka iwezekanavyo dhidi ya wahusika .

Akitoa taarifa ya Utekelezaji wa Shughuli, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga amesema Mfuko huo umeendelea kutekeleza Maagizo ya Serikali ya kusaidia jitihada za Serikali katika kupambana na Umaskini nchini kote .

Bwana Mwamanga amezitaja sekta za Elimu, Maji,Afya ,Barabara,hifadhi ya Mazingira, Mifugo, Kilimo na uzalishaji mali na ujenzi wa rasilimali watu kuwa miongoni mwa maeneo yaliyopewa kipaumbele tangu kuanzishwa kwa Mfuko huo takribani miaka 20 iliyopita miradi ambayo amesema imetekelezwa kwa mafanikio makubwa kwa kuwahusisha wananchi kwenye maeneo yao.


Mkurugenzi Mtendaji huyo wa TASAF amebainisha pia kuwa utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini licha ya changamoto kadhaa zilizotokana na ukubwa wa Mpango huo kumekuwa na mafanikio makubwa hususani katika kubadili fikra za Walengwa ambao kwa sasa wanaendelea kuboresha maisha yao kwa kutumia huduma za Mpango huo.Amesema maboresho muhimu yatafanywa kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali ili katika sehemu ya pili ya Mpango inayotarajiwa kuanza hivi karibuni kuwa na ufanisi zaidi ikiwa ni pamoja na kuyafikia maeneo ambayo hayakupata fursa hiyo katika awamu ya kwanza.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dr. Mary Mwanjelwa(aliyeshika kipaza sauti) akizungumza na Watumishi wa TASAF (hawapo pichani) kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bw. Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akitoa taarifa kwa Naibu Waziri Dr. Mary Mwanjelwa wakati alipofanya ziara ya utambulisho kwa watumishi wa taasisi hiyo.
Picha ya Juu na Chini baadhi ya Watumishi wa TASAF wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dr. Mary Mwanjelwa (hayupo pichani) ambaye alifanya ziara katika taasisi hiyo.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dr. Mary Mwanjelwa (aliyeketi katikati ) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watumishi wa TASAF alipofanya ziara ya kujitambulisha .
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images