Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

MADEREVA WAZEMBE JESHI LA POLISI HALITAWAFUMBIA MACHO

0
0
Na. Vero Ignatus, Arusha 

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini Fortunatus Musilimu amewaomba abiria kulisadia jeshi la polisi kwa kutoa taarifa pale wanapoona dereva amekaidi sheria ya usalama barabarani, wasisubirie hadi ajali itokee ndipo waanze kutoa malalamiko

Hayo ameyasema leo Jijini alipokuwa akifanya ukaguzi wa magari pamoja na askari wa usalama barabarani na wadau wengine wa usalama katika stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani ambapo aliwataka abiria kutokufumbia macho uzembe wowote atakaoufanya dereva wa kuhatarisha maisha ya abiria awapo safarini.

Aidha ameeaagiza abiria hao punde wanapomuona dereva anaotaka kulipita gari lingine kimakosa, mwendo kasi, lugha chafu kwa abiria, kuongea na simu sambamba na viashiria vyote vinavyoweza kupelekea kutokea ajali watoe taarifa kwa namba 0656111444

'' Piga simu muda wowote tunapambana sisi tunapambana na madereva wazembe hadi kuhakikisha tunakuwa salama barabarani "'' Tunapozungumzia maisha ya watu hatuna mchezo wacheni uzembe na mambo ya kitotokitoto muwapo barabarani dereva unakimbia kwenda wapi gari limejaa udereva ni taaluma, zingatia sheria uwapo barabarani"alisema Muslimu

Muslim ametahadharisha madereva ambao hawatazingatia na kutii sheria za usalama barabarani kuwa jeshi la polisi halitawafumbia macho sheria itafuata mkondo wake. Pia amesisitiza kuwa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani lipo tayari kwaajili ya waananchi na kuhakikisha usalama wa maisha yao wawapo safarini. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa usalama barabarani mkoa wa Arusha Baraka Msangi amesema zoezi la Abiria paza sauti sambamba na ile ya Nyakua ya jeshi la polisi imesababisha ajali zimepungua katika Jiji la Arusha
Amewataka Madereva kuendelea kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani kwasababu abiria wanawategemea wao wawapo safarini 

'' Abiria fungeni mikanda yenu mnapokuwa kwenye vyombo vya moto, usikae kimya pale dereva anapokiuka sheria za usalama barabarani toa taarifa kwa askari yeyote atakapolisimamisha gari kwa ukaguzi '' alisema Bakari

Hamza Kasongo ni mjumbe kutoka Baraza la usalama barabarani Taifa katika kamati ya Elimu, mafunzo na uenezi amesema wao kazi yao kubwa ni kupanga mikakati na kushirikiana na jeshi la polisi ili kupunguza ajali na kila mwisho wa mwaka wanashirikiana nao kufanya ukaguzi nchi nzima

Amesema hadi sasa wameshatoa elimu hiyo na kufanya ukaguzi zaidi ya mikoa zaidi ya 11na lengo kuu ni kuepusha ajali za kizembe kwani mwisho wa mwaka ajali huwa zinaongezeka na wanafanya yote hayo kwa kishirikiana na Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani

Msafiri Mussa Afisa Msafiri Mussa ni Afisa kutoka Sumatra yeye amesema kazi yao kubwa haswa katika sikukuu za mwisho wa mwaka nikuhakikisha kuwa abiria wanalipa nauli stahiki, tiketi, na wanasafiri salama

Aidha amesema kwa mwaka huu malalamiko haswa katika jiji la Arusha yamepungua kwani mwanzoni kulikuwa na mkanganyiko wa magari. 

Awali ilikuwa mbili kwa tatu (three by two) lakini kwa sasa ni mbili kwa mbili(two by two) ambapo nauli kwa sasa zipo sawa, wamiliki wanatoza shilingi elfu 30,000-35,000 kwa msimu huu wa sikukuu ni shilingi 38,000 ambacho ni kiwango cha kawaida.
Wa Pili kutoka kulia ni Kamanda wa kikosi cha uslama. Barabarani SACP Fortunatus Musilim, akifuatiwa na Mrakibu msaidizi Joseph Bukombe mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Mkoani Arusha, Mjumbe wa Baraza la usalama barabarani Taifa Hamza Kasongo na wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa mabalozi wa usalama barabarani mkoa wa Arusha Bakari Msangi wakiwa stendi kuu leo asubuhi. Picha na Vero Ignatus.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama barabarani nchi SACP Fortunatus Musilimu akizungumza na abiria leo asubuhi katika stendi ya mabasi Jijini Arusha kabla hawajaanza safari. Picha na Vero Ignatus
Magari yakiwa yanatoka stendi kuu ya mabasi Arusha. Picha na Vero Ignatus 
Baadhi ya mabalozi wa usalama barabarani wakiwa tayari kwa kupaza sauti stendi kuu ya mabasi jijini Arusha. 
Kutoka kulia ni Kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani SACP Fortunatus Musilim ni mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Jijini Arusha Joseph Bukombe, Mwenyekiti wa mabalozi wa usalama barabarani Bakari Msangi. Picha na Vero Ignatus

Askofu Mkuu Kanisa la AICT Dayosisi ya Mwanza awekwa wakfu

0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano (pichani) hii leo Disemba 23, 2018 amewekwa wakfu na kusimikwa kazini katika ibada maalum iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa kanisa hilo nchini, Askofu Mussa Magwesela katika kanisa la AICT Makongoro Jijini Mwanza.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano (kushoto), akila kiapo cha uaminifu.
Jopo la Maaskofu wa Kanisa la AICT wakimweka wakfu na kumsimika kazini Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano.
Jopo la Maaskofu wa Kanisa la AICT wakimweka wakfu na kumsimika kazini Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano.
Jopo la Maaskofu wa Kanisa la AICT wakiongozwa na Askofu Mkuu nchini, Askofu Mussa Magwesela, wakimweka wakfu na kumsimika kazini Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano.
Jopo la Maaskofu wa Kanisa la AICT wakimweka wakfu na kumsimika kazini Askofu Mkuu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) Dayosisi ya Mwanza, Askofu Philipo Magwano.
Mama Askofu Mkuu Kanisa la AICT Dayosisi ya Mwanza (kushot), akitoa salamu zake.
Mgeni rasmi kwenye ibada hii maalum ya kumweka wakfu na kumsimika kazini Askofu Mkuu Kanisa la AICT Dayosisi ya Mwanza alikuwa Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella (wa pili kushoto).Tazama BMG Online TV hapa chini
#PamojaDaimaBMG

WADAU WA ELIMU WACHANGIA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 250 UJENZI WA MADARASA BUSEGA SIMIYU

0
0
Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu wakichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu wakichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkuu wa Wilayaya Busega Mhe. Tano Mwera (kushoto) na Mbunge wa Busega,Mhe. Dkt. Raphael Chegeni wakiteta jambo katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ambaye alialikwa kama Mgeni rasmi wa Harambee hiyo, Luteni Kanali Josephat Mshashi, Mkuu wa Kikosi cha 27 Makoko Musoma akizungumza na wadau wa elimu, katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo. 

Mdau wa Maendeleo katika Wilaya ya Busega, Bw. Deo Kumalija akichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa Wilaya ya Maswa, mhe. Dkt. Seif Shekalaghe na Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni wakiteta jambo, katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

………………………….

Na Stella Kalinga, Simiyu

Wadau mbalimbali wa elimu wamechangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega mkoani Simiyu katika Harambee iliyofanyika Mjini Nyashimo, ambapo zimepatikana jumla ya shilingi 254, 969,000/= fedha taslimu zikiwa ni shilingi 15,360,000/= ahadi shilingi 241,809,000/= na mifuko ya saruji 127.

Akiongea na wadau hao Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ambaye alialikwa kama Mgeni rasmi wa Harambee hiyo, Luteni Kanali Josephat Mshashi, Mkuu wa Kikosi cha 27 Makoko Musoma amesema upo umuhimu wa kuhakikisha watoto wanapata elimu kwa kuwa elimu ni urithi hivyo kila mmoja awe na uchungu wa kuona watoto wanasoma. 

“Hakuna urithi tunaoweza kuwapa watoto wetu zaidi ya elimu tusipowapa elimu rasilimali zote ambazo tunazipigania leo hii, tunavyopambana kulikomboa Taifa letu kiuchumi itakuwa kazi bure kwa sababu tutabaki na Taifa la watu ambao ni watumwa wa watu wenye elimu” alisema Mshashi

Awali akitoa taarifa ya hali ya vyumba vya madarasa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njinginya amesema halmashauri hiyo ina upungufu wa vyumba vya madarasa 107.

Mmoja wa Wadau wa elimu katika Wilaya ya Busega, Bw. Deo Kumalija ambaye alichangia katika harambee hiyo ametoa wito wadau wa maendeleo na wananchi kuchangia shughuli za maendeleo katika maeneo waliyopo, ikiwemo ujenzi wa shule kwa kuwa maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameupongeza uongozi wa wilaya ya Busega kuandaa harambee hiyo huku akiwataka kusimamia fedha zilizopatikana, ili zifanye kazi iliyokusudiwa, na kuwasisitiza wazazi, walezi na jamii yote kwa ujumla kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kwenda kidato cha kwanza wanaenda shule.

“Nawapongeza sana viongozi wa wilaya ya Busega wakiongozwa na Mhe. DC kwa kuandaa harambee hii, fedha hizi mhakikishe zinasimamiwa vizuri na zifanye kazi iliyokusudiwa, lakini pia mhakikishe watoto wote waliochaguliwa wanaenda shule, haiwezekani juhudi kubwa namna hii ifanyike kuchangia halafu watoto wasiende shule” alisema Mtaka.

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka kuwa Viongozi watasimamia fedha yote iliyopatikana na kuhakikisha inafanya kazi itakayokuwa na thamani halisi ya fedha hiyo(value for money).

Akitoa shukrani kwa viongozi na wadau mbalimbali wa elimu waliochangia katika harambee hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Busega, Mhe. Vumi Magoti ametoa wito kwa madiwani kuwahamasisha wananchi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika kata zao, ili fedha zilizopatikana ziweze kuwasaidia katika ukamilishaji.

Pamoja na kutafuta wadua wa elimu waliochangia zaidi ya shilingi milioni 70 katika harambee hiyo Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni amesema kwa kushirikiana na wadau ameshatoa vifaa vya ujenzi ikiwemo mabati 1700 na mifuko ya saruji 640 ambavyo vimeshasambazwa na kusaidia katika ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani humo

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 24,2018.

0
0














SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR, ZAKUBALIANA KUONGEZA KASI USIMAMIZI WA SEKTA YA UVUVI

0
0
Na. Edward Kondela

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amekutana na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma, Mjini Unguja na kumweleza kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inahakikisha miradi inayohusu wavuvi inawanufaisha moja kwa moja.

Katika mazungumzo hayo ambayo pia yamehudhuriwa na Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Makame Ali Ussi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Bw. Islam Seif Salum pamoja na watendaji wengine wizara, Mhe. Ulega amesema lengo kuu la ziara yake ya siku moja kisiwani Zanzibar ni kutazama shughuli za Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu Zanzibar kupitia mradi wa Usimamizi wa Uvuvi Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH).

“Tunahitaji tuone rasilimali za bahari zinatunufaisha, mchango wake bado ni mdogo sana mradi wa SWIOFISH una pesa nyingi lakini bado hatujaona mafanikio ya moja kwa moja kuwasaidia wananchi tulikubaliana kuna mambo ya kurekebisha.” Alisema Mhe. Ulega

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma amesema uchafuzi wa bahari, uwepo wa maharamia na uvuvi haramu ni mambo ambayo Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea kukabiliana nayo ili kuhifadhi bahari na kufanya sekta ya uvuvi kuwa yenye tija kwa wananchi.

Mhe. Juma pia amesema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendelea kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika masuala yanayohusu uvuvi ili kubadilishana uzoefu hasa baada ya hivi karibuni kuhudhuria mkutano wa “Blue Economy” nchini Kenya ambapo nchi washiriki wa mkutano huo walikubaliana kusimamia mambo mbalimbali ili kulinda rasilimali za Bahari ya Hindi.

Mara baada ya mazungumzo hayo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega alipata fursa ya kukutana na watendaji wa wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi pamoja na watendaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu Zanzibar ambapo amewataka kujenga mazingira ambayo yatawanufaisha wavuvi hususan kwa kubuni teknolojia za kisasa kwa ajili ya shughuli za uvuvi.

“Unajua viongozi wetu wanataka kuona tunakuja na vitu gani vipya, mapinduzi gani mapya, tusikae na sisi tukaendelea kufanya vile vile kwa maana shughuli za uvuvi za kurithishana, jukumu letu viongozi ni kuwasaidia wavuvi hawa kupata teknolojia ili kuwarahisishia shughuli zao badala ya sasa wakiendelea kuvua kwa kubahatisha.” Alisema Mhe. Ulega

Aidha Mhe. Ulega ametoa wito kwa watendaji hao kutumia vizuri fedha zilizotolewa na Benki ya Dunia Shilingi Bilioni Tano kwa ajili ya mradi wa SWIOFISH ili kuleta mapinduzi ya kweli katika sekta ya uvuvi na kuhakikisha wanafanyakazi kwa kasi kulingana na matarajio ya serikali zote mbili kwa wananchi wake.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amemaliza ziara hiyo kwa kutembelea na kujionea namna teknolojia mbalimbali zinazotumiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu Zanzibar katika uhifadhi wa Bahari ya Hindi pamoja na kupata taarifa sahihi za shughuli za uvuvi zinazofanywa baharini katika eneo la Tanzania. 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (kushoto) akiwa na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma

SPORTPESA WAMKABIDHI JOSHUA MBISSE WA KING’ORI ARUSHA BAJAJI YAKE,

0
0
Promosheni ya Shinda Zaidi na SportPesa  imeendelea kuzunguka huku na kule na kipindi hiki ni zamu ya Jiji la Arusha.Hapa anakabidhiwa mshindi wa droo ya Joshua Mbisse wa King’ori Arusha ikiwa ni kutokana na mafanikio ya ubashiri aliouweka kupitia SportPesa Kwa njia ya USSD yani *150*87#

Akipokea bajaj yake Mbisse aliishukuru SportPesa kwa kumuwezesha kushinda bajaj na hiyo imempa nguvu kubwa na matumaini ni kubadili maisha na kufungua wigo mpya atakaomuwezesha kuinuka kiuchumi.Sasa nimeamini mchezo huu wa ubashiri kutoka SportPesa ni wa uhakika na hauna longolongo kama nilivyokuwa nikifikiri, Ghafra ushindi wangu umenifanya nibadili fikra tofauti na mtazamo wa hapo awali, mambo ni mengi ya kufanya kupitia bajaj hii nachokiona kikubwa ni kutengeneza maisha yangu Na kuyaboresha Kabisa sina budi kushukuru kwa hili"
Mkakati mwingine mkubwa ni kumalizia ujenzi wa nyumba yake ambayo mpaka hivi sasa ujenzi ulikuwa haujamalizika.Ushindi wa Mbisse ulipokelewa kwa Furaha kubwa na wanakijiji wenzake Wengi wao wakiamini kuwa mafanikio ya Mshindi huyo ni ya kwako pia maana bajaj hiyo inaweza kuwa msaada hata kwa upande wao kwenye masuala ya usafiri .
Mbali ya kushinda bajaj SportPesa inakukumbusha kucheza jackpot ambayo imesimamia kwenye zaidi ya sh. Milioni 420 hii inampa mtu nafasi ya kubashiri Mechi 13 na akifanikiwa kuzibashiri mechi zote kwa usahihi ataondoka nazo zote lakini yule anayefanikiwa kubashiri Mechi 10, 11, na 12 kwa ufasaha anaondoka na bonus ambayo ni ya utofauti na wala haigawanyiki.
Katika msimu huu wa sikukuu wateja wa mitandao yote ya simu wanaweza kujishindia zawadi mbalimbali kutoka SportPesa kama Bajaji, Jezi za Simba na Yanga, Smartphone(simu janja) pamoja na safari ya kwenda kushuhudia ligi kubwa mbili suniani yaani Hispania na Uingereza.

MAAMUZI YA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI KUHUSU RUFAA MOJA YA UCHAGUZI MDOGO KATA YA MAGOMENI JIMBO LA KINONDONI

0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipokea Rufaa moja (1) kutoka kwa Mgombea Udiwani wa Kata ya Magomeni katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni. Tume imepokea rufaa hiyo kwa kuzingatia kifungu cha 44(5) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, kikisomwa pamoja na kanuni ya 28(1) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani) za mwaka 2015,Rufaa hiyo iliwasilishwa na mgombea Udiwani wa Chama cha Wananchi (CUF) Ndg. Ngude Athumani Yusuph akitaka arejeshwe kuwa mgombea udiwani katika Kata ya Magomeni kupitia chama hicho.

Kuenguliwa kwake kulitokana na pingamizi lililowekwa na mgombea mwenzake kwa madai kuwa Sio Raia wa Tanzania, hakudhaminiwa na chama chake cha siasa kugombea udiwani na fomu yake ya uteuzi haikujazwa kikamilifu. Msimamizi wa Uchaguzi alikubaliana na pingamizi hilo, hivyo kumuengua mgombea.

Tume katika kikao chake cha tarehe 24 Disemba 2018, ilipitia vielelezo vilivyowasilishwa na kujiridhisha kuwa mrufani ni Raia wa Tanzania na kwamba alidhaminiwa na chama chake cha siasa na kwamba fomu yake ya uteuzi ilijazwa kwa ukamilifu na hivyo, kuelekeza arejeshwe kuendelea kuwa mgombea udiwani katika Kata ya Magomeni, Halmashauri ya Manispaa ya kinondoni

Aidha, Tume ilipokea malalamiko kutoka kwa Ndg. Ngulangwa Eng Mohamed Mshamu wa Chama cha Wananchi (CUF) akipinga uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Temeke kumuondoa kwenye orodha ya wagombea Ubunge na kumtangaza Mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Abdallah Ally Mtolea kuwa amepita bila kupingwa.

Kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Mgombea akitangazwa kuwa amepita bila kupigwa Tume haina mamlaka juu ya uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi. Hivyo, malalamiko hayo yaliyowasilishwa na Ndg. Ngulangwa Eng. Mohamed Mshamu na pia hayana sifa ya kuwa rufaa.

Taarifa za maamuzi ya rufaa na malalamiko, zimetumwa kwa wahusika kupitia kwa Wasimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri husika.

Imetolewa leo tarehe 24 Disemba, 2018 na:

Giveness Aswile

MKURUGENZI WA HABARI NA ELIMU YA MPIGA KURA

Umoja wa vijana waunga mkono juhudi za maendeleo za Rais Dk. John Magufuli

0
0

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) umesema kuwa katika kipindi cha miaka mitatu cha Rais Dkt.John Magufuli kumekuwa maendeleo ya kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati kwa miundombinu mbalimbali.

Akizungumza na waandishi Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama hicho Raymond Mwangwala amesema tunakwenda katika uchumi wa kujitegemea zaidi.

Amesema kwa sasa ndege tano ambapo ni faida kwa watanzania kupata maendeleo kwa kuingia katika biashara ya usafiri wa anga.Mwangwala amesema sasa ni mapigano ya uchumi hivyo Umoja utamlinda katika kwenda na uchumi huo kwa kasi.

Amesema ndege iliokuja ni ya kwanza kwa nchi za Afrika hivyo kila mtanzania anatakiwa kupongeza Rais Dkt.John Pombe Magufuli.Ametaja miradi mikubwa ambayo inafanywa na serikali ya awamu ya tano ikiwa mradi mmoja umeshakamilika na miradi mingine ni Ubungo, Salender na Mradi wa Reli ya Kisasa SGR.

Amesema kuwa Demokrsia iliyopo lazima kuwa na mipaka hivyo kila mtu lazima kufuata sheria katika kuitumia Demokrsia hiyo pamoja na kumsaidia Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Aidha amesema baadhi ya vijana wanatumika na mataifa ya nje na kusahau uzalendo wa nchi."Vijana wa CCM tutakuwa wa kwanza kumlinda Rais Wetu ili kuweza kufikia uchumi wa kati"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Raymond Mwangwala akizungumza na waandishi habari kuhusiana na kupongeza Rais Dkt.John Pombe Magufuli katika maendeleo mbalimbali yaliyotokea katika kipindi cha miaka mitatu, leo jijini Dar es Salaam.

MAHAKAMA YAMWACHIA HURU MFANYABIASHARA KILUWA,

0
0
*Mahakama yaagiza fedha zake Milioni 90/- arudishiwe
*Ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa umejaa hisia

Na Ripota Wetu, Globu ya jamii

MKURUGENZI wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone Mohamed Kiluwa (50) aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kutoa rushwa ya Sh.milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameshinda kesi baada ya upande wa mashtaka
kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake.

Hivyo Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam leo Desemba 24,2018 imemuchia imeamuru Kiluwa ambaye pia ni mfanyabiashara na kuagiza arudishuwe fedha zake Sh.milioni 90 anazodaiwa kutaka kutoa rushwa kwa Waziri Lukuvi.

Hukumu  ya kesi hiyo imetolewa na hiyo Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Samweli Obas ambapo amesema katika kifungu cha sheria namba 15(1)B(2) Cha Sheria  ya Kuzuia na Kupambana na rushwa ili mtu atiwe hatiani lazima vitu viwili vithibitike ikiwemo nia ovu ya kutoa fedha na kutoa fedha hizo ili
afanye au aache kufanya  jambo fulani.

Pia amesema katika mashahidi wa upande wa mashitaka, Shahidi wa watu watano na vielelezo saba vilivyowalishwa mahakamani hapo  vilikuwa vya hisia, hivyo Mahakama haiwezi kumtia hatiani mshitakiwa kwa ushahidi huo.Amefafanua ushahidi wote wa upande wa mashitaka umekaa kihisia, mlalamikaji alikuwa anahisi kupewa rushwa, hivyo hata kama hisia inanguvu kiasi gani Mahakama haiwezi kumtia hatiani mshitakiwa kwa hisia tu.

 "Katika ushahidi wao,  upande wa mashtaka ulidai kuwa kwa nia ovu mshtakiwa alimpatia Waziri kiasi hicho cha fedha, , hivyo miongoni mwa maswali aliyojiuliza ni kama mshtakiwa alikuwa na nia ovu ya kumpatia Waziri fedha hizo kama kishawishi ama zawadi au malipo ya kufanya jambo fulani,"amesema.

Aidha alijiuliza swali jingine kuwa ni kweli mshtakiwa alitoa fedha hizo kwa Waziri kwa sababu akiachia mlalamikaji mashahidi wengine wa upande wa mashitaka walitoa ushahidi wao walioambiwa na mlalamikaji au kusikiliza audio CD iliyowasilishwa mahakamani hapo.

Amesema ukiondoa mashahidi wote, ushahidi wa msingi ni wa mlalamikaji mwenyewe ambao ni lazima uchukuliwe kwa tahadhari lakini katika ushahidi wake mlalamikaji aliieleza mahakama kuwa hati za Kiluwa zimepatikana kihalali, hivyo anakiri zilitolewa kihalali. Ameongeza  pia msiri wake alimwambia mshtakiwa atamletea Dola za Marekani 50,000  ila zilizokamatwa ni Dola 40,000, hivyo Mahakama ina
mashaka.

Hakimu Obasi ameongeza kielelezo cha CD kina mashaka kwa sababu kina mapungufu ambapo ukiisikiliza mwanzo hadi mwisho wa CD hakuna kauli ambayo ameitoa mshtakiwa akisema anatoa Dola 40,000 pia katika CD hiyo ilisikika sauti ya mshitakiwa akisema "Ninachokifanya kama ndugu sitoi hongo wala nini nakupatia hichi kidogo kama mafuta ila sitoi hongo kama nakwenda tofauti mimi ni ndugu yako niambie,"

Hakimu alisema katika maneno hayo na kwamba Hakuna mahali ambapo mshitakiwa alisema anatoa hongo au anampatia Waziri dola 40,000 hivyo maelezo  hayo ya CD hayatoshelezi kusema alikuwa anatoa rushwa.
Hakimu Obasi akiendelea kusoma Hukumu hiyo kwa kuuchambua  uliowasilishwa mahakamani hapo Amesema, kilichopelekwa mahakamani hapo ni CD na si kifaa kilichorekodi hivyo mahakama hawezi
kujiridhisha kuwa sauti iliyopo kwenye CD hiyo ndio ya mshitakiwa.

Kwa mantiki hiyo basi, ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka haukuitosheleza mahakama na kuweza kumtia hatiani mshtakiwa, hivyo Mahakama inamuachia huru na fedha alizokuwa nazo Milioni 90 arudishiwe.
Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam leo Desemba 24,2018 imemuachia huru mfanyabiashara Mohamed Kiluwa (50)  (Pichani kushoto) ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone aliyekuwa akikabiliwa na shtaka la kutoa rushwa ya Sh. Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi baaada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha shtaka hilo la rushwa dhidi yake.
Mfanyabiashara Mohamed Kiluwa (50)  (Pichani kulia)  ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Steal Group. Co.ltd na Kiluwa Free Processing Zone akiwa na Wakili wake Imani Madega wakitoka Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru katika kesi iliyokuwa ikimkabili ya kudaiwa kutoa rushwa ya Sh. Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi,ambapo upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha shtaka hilo la rushwa dhidi yake.
 Mfanyabiashara Mohamed Kiluwa (50) akiwa na Mkewe wakipeana mikono kutoka kwa ndugu na jamaa,mara baada ya kutoka Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam baada ya kuachiwa huru katika kesi iliyokuwa ikimkabili ya kudaiwa kutoa rushwa ya Sh. Milioni 90 kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi,ambapo upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha shtaka hilo la rushwa dhidi yake.

BASATA YAWARUHUSU DIAMOND NA RAYVAN KUFANYA SHOO NJE YA NCHI

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

BARAZA la Sanaa la Taifa ( BASATA) limewaruhusu wasanii Nasib Abdul 'Diamond Platnumz' na Raymond Mwakyusa 'Rayvan' kufanya maonesho nje ya nchi.

Wakitoa taarifa hiyo leo, BASATA wamesema kuwa wasanii hao walikuwa wameshaingia mikataba inayofahamika katika nchi mbili za jirani kabla ya adhabu ya BASATA kutolewa.

Wamesema kuwa, kwa kuzingatia mahusiano mazuri kati ya nchi yetu na nchi nyingine lakini pia kwa upande wa mashabiki tayari walikuwa wameshakata tiketi za maonesho hayo.

Kupitia taarifa hiyo BASATA limewaondolea katazo la maonesho hayo tajwa tu na kubakiza katazo la ndani ya nchi mpaka pale Diamond na wenzake watakapoonesha mabadiliko chanya kitabia.

Mbali na hiyo, BASATA limeonekana kutokuridhishwa na baadhi ya waheshimiwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kuuim ana kucheza wimbo huo kwa bashasha na nderemo ukiwa tayari umeshafungiwa bila kujali athari zake kwa vijana na watanzania kwa ujumla.

BASATA wanawasiliana na vyombo vya ulinzi na usalama kuwa nyimbo zote zilizofungiwa haziruhusiwi kwa namna yoyote kutumiwa na jamii.

MATUKIO KATIKA PICHA TIGO FIESTA 2018 ILIVYOFUNIKA DAR

0
0

Mkali wa muziki wa Bongo Fleva Ali Kiba aka King Kiba, akiwa stejini pamoja na madensa wake wakati wa Tamasha la Tigo Fiesta 2018 lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.
Mwanadada anayefanya vizuri katika tasnia ya muziki wa Bongo Flava Vanessa Mdee (katikati) akitoa burudani ya kufunga mwaka pamoja na madensa wake katika hitimisho la tamasha la Tigo Fiesta 2018 lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya mashabiki wa muziki wa kizazi kipya wakishangilia kundi la Weusi( hawapo pichani) wakati walipopanda jukwaani kutumbuiza katika Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.
Msanii Chege Chigunda (kushoto) akitoa burudani ya kufunga mwaka kwenye hitimisho la tamasha la Tigo Fiesta 2018 lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Chid Benz, akiwapagawisha mamia ya mashabiki waliofika kushuhudia hitimisho la Tamasha la Tigo Fiesta ‘Champion’ lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.
Kundi la muziki wa kufoka foka (Hip Hop) la Weusi likitoa burudani ya kufunga mwaka katika hitimisho la tamasha la Tigo Fiesta 2018 lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.

Msanii Dogo Janja akitoa burudani ya kufunga mwaka kwenye hitimisho la tamasha la Tigo Fiesta 2018 lililofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam.

TTB NA CHINA KUSHIRIKIANA KUUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII VYA NCHINI

0
0

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

SERIKALIya Nchini China imedhamiria kuisaidia Bodi ya Utalii nchini (TTB) katika kutangaza vivutio mbalimbali nchini na kukuza biashara kati ya nch hizo mbili Tanzania na China. 

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya TTB Jaji Mstaafu Thomas Mihayo amesema kuwa lengo kuu la ziara iliyofanyika nchini China katika Jiji la Shanghai, Guangzhou, Hong Kong, Chengdu na Beijing Novemba 12-20 ilikuwa ni kwa ajili ya kutangaza utalii. 

Amesema, wametumuia fursa hiyo kuhakikisha Tanzania inaongeza sehemu ya umiliki wa soko kwenye soko la utalii kwa kutangaza vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji zikizopo nchini ikiwamo na safari za ndege za ATCL kwenda China.

Jaji Mihayo ameeleza kuwa, katika safari hiyo ya nchini China wameweza kusaini mkataba na kampuni ya Touchroad Group na TTB na wamekubaliana kuwa kampuni hiyo italeta watalii elfu kumi (10,000) kutoka China hadi kufikia mwaka 2019."Kundi la kwanza la watalii wanatarajiwa kuwasili nchini mwezi Januari na Februari 2019, watakuwa nchini kwa muda wa siku tatu na Touchroad wameonesha nia ya kuwekeza katika huduma ya malazi zenye hadhi ya nyota tano na tayari wanazo hoteli nne,"amesema Mihayo. 

Katika ziara waliyoifanya ya jiji la Beijing, wawakilishi wa Shirika la Utangazaji la China (CCTV) walikutana na maafisa wa MNRT na wakatoa mapendekezo ya kutengeneza makala za dakika 30 za Zamadam kisha kutoa Filamu kama ya Jurassic Park ili kurushwa kwebye televisheni yao. 

"Pia, CCTV4 wameafiki kushiriikiana na Bodi ya misitu nchini (TFS) kupiga picha katika hifadhi za asili za misitu wakati wa sherehe za maadhimisho ya mwaka mpya wa China mnamo mwezi Februari 2019,"amesema Jaji Mihayo. 
Aidha, amesema kuwa kwa takwimu inaonesha Tanzania kwa mwaka 2017 imeweza kupokea watalii 29,224 kutoka nchini China wakitembelea vivutio tofauti nchini. 

Kwa upande wake, Meneja Mauzo na Usambazaji wa ATCL, Edward Nkwabi alisema kuwa katika ziara hiyo walipokea maombi kutoka kwa viongozi wa miji ya Hong Kong, Beijig, Chengdu na Shanghai kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi kwenye miji hiyo. Alisema, jambo hilo liliwafanya kuingia makubaliano na kampuni moja ya uwakala ambayo itatangaza na kuuza tiketi za safari za ndege za ATCL. 

Amesema kwua safari za moja kwa moja kuelekea nchini China zitaanza mapema mwakani kwa ajili ya kuimarisha sekta ya utalii nchini na lengo kuu ni kuwapa fursa ya kuja moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania. 
Mwakilishi kutoka ubalozi wa China, Gao Wei alisema kuwa kupitia ziara waliyoifanya TTB, ATCL, Wizara ya utalii pamoja na wadau wengine wakiwemi wamiliki wa Hoteli, Serikali ya China imeendelea kukuza na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania nchini China. 

Amesema, Tanzania wana vivutio vingi sana na wao kama serikali ya China wanaona hii ni fursa kwao ila wametoa pendekezo moja kwa TTB kuweza kuondoa Viza ili watalii wengi waweze kuja na suala hilo tayari wameshawaeleza na wanaamini watalifanyia kazi.
MWENYEKITI wa Bodi ya Utalii (TTB), Jaji mstaafu Thomas Mihayo, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo , kuhusu mafanikio ya ziara kutangaza utalii katika soko la utalii la China. Kushoto ni Mkurugenzi Mwendeshaji wa TTB, Devota Mdachi na kulia ni Ofisa wa Ubalozi wa China nchini Tanzania, Gao Wei.
Meneja Mauzo na Usambazaji wa ATCL, Edward Nkwabi akizungumzia maombi kutoka kwa viongozi wa miji ya Hong Kong, Beijig, Chengdu na Shanghai kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi kwenye miji hiyo.

DROO YA MAKUNDI KLABU BINGWA AFRIKA KUPANGWA IJUMAA HII

0
0


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

DROO ya upangwaji wa Makundi hatua ya 16 bora ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika (CAF) inatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa Disema 28 ili kupata makundi manne yatakayoanza kuchuana Januari 16 mwaka huu makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) mjini Cairo, Misri.

Timu hizo zimefanikiwa kuingia hatua ya 16 baada ya kufanikiwa kushinda mechi zao za mzunguko wa pili na kutoka Afrika Mashariki na kati timu pekee kutoka Tanzania Simba wamefanikiwa kuingia hatua hiyo baada ya kuwafungwa Nkana 'Red Devil' goli 3-1 baada ya mchezo wa kwanza kufungwa 2-1 wakiwa ugenini.

Katika uchezeshaji wa droo hiyo timu ya Simba imewekwa katika kundi cha nne kutokana na nafasi ya kisoka kwa klabu za Afrika na watasubiri timu zitakazoanza kupangwa kutoka kundi la kwanza hadi la tatu.Mbali na Simba SC, timu nyingine zilizofuzu Ligi ya Mabingwa Afrika ni mabingwa watetezi, Esperance na Club Africain zote za Tunisia, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Ismailia, Al Ahly za Misri.

Timu zingine TP Mazembe na AS Vita za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Wydad Casablanca ya Morocco, JS Saoura, CS Constantine za Algeria, Horoya FC ya Guinea, Lobi Stars ya Nigeria, FC Platinums ya Zimbabwe na ASEC Mimosa ya Ivory Coast.

Mara ya mwisho Tanzania kuingiza timu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika ilikuwa mwaka 2003 na walikuwa hao hao Simba SC waliofika hatua hiyo, wakifuata nyayo za wapinzani wao wa jadi, Yanga SC waliokuwa timu ya kwanza nchini kufikia mafanikio hayo mwaka 1998.

BINTI FILAMU WAANDAA TAMASHA LA KATAA MIHADARATI DESEMBA 28

0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

BINTI Filamu Foundation imeandaa tamasha maalum liitwalo 'Kataa Mihadarati Festival' litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya.

Katika kuhakikisha tamasha hilo linafanikiwa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini limetangaza kuungana na Binti Filamu kufanikisha lengo hilo na huku likifafanua jukumu la kupiga vita biashara ya matumizi ya dawa hizo ni la kila mmoja wetu.

Akizungumzia tamasha hilo leo jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea amesema wanatarajia kuwepo kwa makundi ya watu mbalimbali siku hiyo wakiwamo wasanii maarufu.Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi na Vijana Anthony Mavunde.Pia Naibu Waziri katika ofisi hiyo anayeshughulikia walemavu Stella Ikupua atahudhuria tamasha hilo.

"Tamasha litaanza saa tatu kamili asubuhi ya Desemba 28 mwaka huu wa 2018, wasanii mbalimbali wa Bongo Movie na Bongo Fleva watakuwepo ili kufanikisha tamasha hilo.Pia waliokuwa wanatumia dawa hizo na sasa wameacha watatoa ushahidi wa athari za dawa za kulevya,"amesema Thea.Thea amesema Binti Filamu inayo dhamana ya kuhakikisha inashiriki kutoa elimu kuhusu athari za dawa za kulevya huku akifafanua kuwa wapo baadhi ya wasanii wamekuwa wakihusishwa na matumizi ya dawa za kulevya.

Kauli mbiu ya tamasha hilo inasema Nguvu yako, afya yako, jiokoe uokoe Tanzania.Kwa upande wake Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi amesema mamlaka inaunga mkono juhudi hizo na kwamba wote wanajua matumizi ya dawa za kulevya yamepoteza ndoto za vijana wengi hapa nchini wakiwamo wasanii."Vijana wengi hujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya bila kujua madhara yake na baadae wanapata madhara makubwa yakiwemo maambukizi ya magonjwa , kupoteza umaarufu wao na hata kupoteza maisha.".

Dk.Mfisi amesema mamlaka inaamini tamasha hilo litakuwa ni jukwaa muhimu kwa vijana wa Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla kupata elimu kuhusu madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya ili wasijaribu kabisa kujiingiza katika matumizi ya dawa hizo.Pia amesema kutakuwa na watalaam mbalimbali watakaoshiriki kikamilifu katika kutoa elimu kuhusu madhara yatokanayo na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.Watalaam wa afya kutoka Hospitali ya Mwananyamala watatoa huduma ya upimaji wa afya kwa ujumla ikiwemo VVU.Pia wananchi watapata fursa kuchangia damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wahitaji.
Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu tamasha maalum liitwalo ‘Kataa Mihadarati Festival’ litakalofanyika Desemba 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii ya Watanzania kuhsu athari za dawa za kulevya katikati ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon Mwakifwamba akizungumza machache katika mkutano huo katikati ni Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi na kulia ni Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi Joyce Fisoo akifafanua jambo kuhus tamasha hilo la kupiga vita matumizi ya madawa ya kulevya katika mkutamo huo.
Mkurugenzi wa Binti Filamu Foundation Ndumbagwe Misayo a.k.a Thea akieleze malengo ya kuandaa tamasha hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo kushoto ni Rais wa Shirikisho la Filamu nchini Tanzania TAF Bw Simon Mwakifwamba na katikati ni Kamishna wa Kitengo cha Tiba na Kinga kutoka Mamalaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Dk.Peter Mfisi

WAZIRI JAFO KUONGOZA UZINDUZI JUKWAA LA WAKULIMA,KUKABIDHI HATI ZA ARDHI ZA KIMILA WILAYANI KISARAWE`

0
0
Ofisa Ardhi wa Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association (TWCHA) , Ivy Mwansepe, akimkabidhi taarifa ya kazi ya shirika hilo ya mwezi Novemba na Desemba mwaka 2017, Mgeni rasmi, Ofisa Kilimo wa Kata ya Kurui, Baraka Budangi, wakati wa mkutano wa Madiwani na wadau wa kilimo uliofanyika juzi wilayani Kisarawe mkoani Pwani juzi. Kulia ni Mratibu wa kilimo wa shirika hilo, Saidi Simkonda.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Zegero, Abdallah Binda akifungua mkutano huo.
Katibu wa shirika hilo, Richard Ng'wandu, akizungumza kwenye mkutano huo. Kulia ni Mwenyekiti wa shirika hilo, Isabela Luoga na Ofisa Ardhi Ivy Mwansepe.
Mkazi wa Kijiji cha Zegero Marcelina Mziray, akichangia jambo kwenye mkutano huo. Kutoka kulia ni Zulfa Tarazo na Mwenyekiti wa Kikundi cha Wakulima wa Kijiji cha Zegero, Fatuma Ali.
Mwenyekiti wa Kikundi cha Wakulima wa Kijiji cha Zegero, Fatuma Ali, akizungumza.
Mratibu wa Mradi wa Kilimo kutoka Taasisi hiyo, Saidi Simkonda, akizungumza.
Mwenyekiti wa shirika hilo, Isabela Luoga, akizungumza.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kilimo Joint, Linda Byaba, akichangia jambo kwenye mkutano huo. Kushoto ni mdau wa kilimo, Salama Somboka



Na Dotto Mwaibale, Kisarawe

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Suleiman Jafo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya uzinduzi wa Jukwaa la Kilimo utakaofanyika Kata ya Kurui wilayani Kisarawe mkoani Pwani.

Katika uzinduzi huo Waziri Jafo ambaye ni kiongozi wa juu wa serikali katika wilaya hiyo atakabidhi hati miliki za kimila za ardhi 315 ambazo zimeandaliwa na Shirika la The Winamwanga Cultural Heritage Association (TWCHA) katika maeneo ya vijiji vya Mafizi, Gwata, Kidugalo, Mtakayo, Zegero na Marui.

Akizungumza katika mkutano wa madiwani na wadau wa maendeleo ya kilimo wakati akitoa taarifa ya kazi zilizofanywa na shirika hilo kwa mwezi Novemba na Desemba 2017 Mratibu wa Mradi wa Kilimo kutoka Taasisi hiyo, Saidi Simkonda alisema waliona ni busara Waziri Jafo awe mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo kwa kuzingatia kuwa yeye ni mwenyeji wa eneo hilo.

"Tayari mchakato wa kumuomba Waziri Jafo kuwa mgeni rasmi tumeufanya tunachosubiri ni majibu yake kwani tunapenda kufanya tukio hilo mwanzoni mwa mwezi wa kwanza mwaka 2019" alisema Simkonda.Alisema mpaka sasa wana wanachama 750 kati ya hao 250 ni walemavu ambao wanamashamba katika kata hizo ambayo yanafanyiwa mchakato wa kupata hati miliki za kimila za ardhi huku 315 zikiwa tayari. 

Alisema katika kipindi hicho shirika hilo o kwa kushirikiana na Halmshauri ya `Wilaya ya Kisarawe limeweza kutoa ushauri mbalimbali kwa watu Wanaotaka `Kuendeleza maeneo yao, kufanya mikutano na wananchi juu ya kuwaelimisha namna ya kuipandisha ardhi thamani kwa kupima mashamba yao na `kupata hati ya hakimiliki ya kimila.

Alitaja baadhi ya changamoto kuwa ni wananchi wengi wa wilaya hiyo kutokuwa na elimu ya umiliki wa mashamba na umuhimu wa kumiliki haki ya hati miliki ya kimila na watendaji wa vijiji kutojua makusanyo ya fedha za kodi ya ardhi ya kijiji kuwa zinawakilishwa wapi.

Alisema katika makusanyo ya kodi za ardhi shirika lilishauri ni vyema kama Serikali za vijiji havina vitabu vya risiti ni vizuri wananchi wapewe akaunti za Serikali za vijiji kufanya malipo ya tozo za ardhi au makusanyo yoyote kwa maendeleo ya kijiji husika.

Katika mkutano huo madiwani hao waliwakilishwa na Ofisa Kilimo wa Kata ya Kurui Baraka Mudangi.


MBUNGE WA SIMANJIRO AIMWAGIA SIFA UJAMAA COMMUNITY RESOURCE TEAM(UCRT)

0
0
Mbunge wa jimbo la Simanjiro mkoa wa Manyara,James Ole Millya akizungumza kwenye mkutano wa kukabidhi Hati za Kimila kwaajili ya malisho ya mifugo katika kijiji cha Lerumo Kata ya Ruvuremit. 
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula(katikati) akifatilia mazungumzo ya mbunge wa jimbo hilo,James Ole Millya(kushoto) na Katibu Tawala wa wilaya ya Simanjiro,Zuwena Omary . 
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula(kushoto) akipokea zawadi ya Ndama kutoka kwa wananchi wa Kijiji cha Lerumo. 
Mbunge wa jimbo la Simanjiro,James Ole Millya (katikati) akipokea zawadi ya Ndama kutoka kwa wananchi wa Kijiji cha Lerumo. 
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula(kushoto) akifurahia zawadi ya fimbo aliyokabidhiwa na wananchi wa Kijiji cha Lerumo Kata ya Ruvuremit baada ya kukabidhi Hati za Kimila kwa vijiji Sita. 
Kwaya ya Lerumo ikitumbuiza wakati wa mkutano huo. 
Wananchi wakifurahia kwa shangwe baada ya Hati za kimila kukabidhiwa kwa viongozi wao. 
Mratibu wa taasisi ya Ujamaa Community Resouce Team wilaya ya Simanjiro.Edward Loure (wa pili kushoto) akipokea zawadi ya Ndama kutoka kwa wananchi wa Kijiji cha Lerumo. 
Mkuu wa wilaya ya Simanjiro,Mhandisi Zephania Chaula(wa pili kushoto) akikabidhi Hati ya Kimila za nyanda za malisho zilizoandaliwa na taasisi ya Ujamaa Community Resource Team(UCRT) katika mkutano uliofanyika Kijiji cha Lerumo Kata ya Ruvuremit,Hati za Kimila zilikabidhiwa kwa vijiji Sita. 
Furaha ya kukabidhiwa Hati ya Kimila . 
Kwaya ya Lerumo ikitumbuiza wakati wa mkutano huo.Imeandaliwa na Filbert Rweyemamu 


Prof. Msanjila awataka Stamico kujitangaza mtambo wa kuchoronga miamba

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila (Kushoto) akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Kanali Sylvester Ghuliku hati ya makabidhiano ya mtambo wa kuchoronga miamba unaojulikana kama Multi-Purpose Air Rotary Drill Rig.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila akisalimiana na mmoja kati ya wajumbe walioshiriki katika makabidhiano ya mtambo huo.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Kanali Sylvester Ghuliku wakisaini hati za makabidhiano ya mtambo wa kuchoronga miamba.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Kanali Sylvester Ghuliku wakionesha hati za makabidhiano mara baada ya kusaini.




Katibu Mkuu wa Madini, Prof. Simon Msanjila akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali na Utawala, Nsajigwa Kabigi mara baada ya kuwasili katika ofisi za STAMICO kwa ajili ya makabidhiano ya mtambo wa kuchoronga miamba. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Kanali Sylvester Ghuliku.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi, akieleza jambo kuhusu mtambo huo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila (mwenye tai) na wajumbe walioshiriki katika tukio hilo.
Kutoka Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO Kanali Sylvester Ghuliku pamoja na Msaidizi wa Katibu Mkuu Justin Mdamila kabla ya makabidhiano ya mtambo wa kuchoronga miamba baina ya wizara na Stamico.
Mtambo wa kuchoronga miamba uliogharimu kiasi cha dola za kimarekani milioni 1.3. Mtambo huu unajulikana kama Multi-Purpose Air Rotary drill Rig.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi, (Kulia) akieleza jambo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila (wa pili kulia) kabla ya makabidhiano rasmi.
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na RasilimaliWatu Nsajigwa Kabigi, akieleza jambo kuhusu mtambo huo mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila (mwenye tai) na wajumbe walioshiriki katika tukio hilo.
Mkurugenzi wa kampuni ya Geo fields Tanzania Ltd Denis Dillip akizungumzia juu ya uwezo wa mtambo huo. Wanaoshuhudia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila pamoja na ujumbe aliombatana nao.
……………………………………………………………………………

Na Nuru Mwasampeta, Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila amelitaka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kutumia mtambo wa kuchoronga miamba kwa ufanisi ili kuliletea tija Taifa pamoja na shirika hilo kutokana na kipato kitakachotokana na uwepo wa mtambo huo.

Prof. Msanjila ameyasema hayo leo Desemba 24, 2018 wakati wa hafla fupi ya kuukabidhi rasmi mtambo huo kwa STAMICO kwa ajili ya kuanza kuutumia rasmi. Mtambo huo unaitwa Multi-Purpose Air Rotary Drill Rig.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Prof. Msanjila amesema, ununuzi wa mtambo huo ni uwekezaji mkubwa ambao Serikali imeufanya kwa shirika la Stamico hivyo, halina budi kuutumia vyema ili uweze kuleta tija.

Akizungumzia gharama za mtambo huo, Prof. Msanjila amesema umegharimu kiasi cha Dola za Kimarekani milioni moja na laki tatu(USD 1.3) ambazo yeye kama Mtendaji Mkuu wa wizara anaona kuwa na deni kubwa kwake, na hivyo kuahidi kuusimamia ipasavyo ili kuhakikisha mtambo huo unazalisha faida na kuwa chachu ya kuweza kununua mitambo mingine kama hiyo ili kukuza sekta ya madini nchini.

Aidha, amelitaka Shirika hilo kujitangaza vema ili wananchi na hususn wadau wa madini wanaojihusisha na shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini kufahamu uwepo wa mtambo huo ili uweze kutumika hata kwa kampuni binafsi ili kujiongezea kipato lakini pia kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini. “Kwa zabuni nilizozisikia mpaka sasa mtambo huu utazalisha pesa za kutosha” amesema Msanjila.

Mbali na kukabidhi mtambo huo, Prof. Msanjila ameitaka Stamico kuwasilisha taarifa za mapato na matumizi ya mtambo huo kila robo ya mwaka ili kuweza kufanya tathmini endapo mtambo unatumika kwa faida.

Pia, ameliagiza shirika hilo kuhakikisha kuwa, mtambo huo unawezesha manunuzi ya mtambo mwingine mpya kila mwaka ili ndani ya miaka mitano shirika liweze kumiliki mitambo mitano na kurahisisha utekelezaji wa shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini.

Akizungumzia ubora wa mtambo huo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Geo field Tanzania Ltd Denis Dillip ambaye ndiye mnunuzi wa mtambo huo amesema, mtambo huo ni wa kisasa na unatumika katika kuchimba aina tatu za miamba lakini pia unaweza kutumika katika kuchimba visima vya maji.

Aidha, Denis ameishukuru Serikali kwa wazo la kununua mtambo huo na kukiri kuwa, utawasaidia wchimbaji wadogo katika kuendeleza kazi zao za uchimbaji na utafutaji wa madini.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Kanali Sylvester Ghuliku amekiri kuwa mtambo huo ni talanta waliyopewa na serikali na kuahidi kutoifukia na badala yake watahakikisha unatumika kwa faida na kuhakikisha unazalisha faida kwa serikali.

“Dola za kimarekani milioni 1.3 mlizotuamini na kutukabidhi ni pesa nyingi sana, na hamjatukabidhi ili zikae kwenye makabati, tutahakikisha tunautumia mtambo huu kwa weledi mkubwa ili uweze kuleta tija, ni imani yangu kuwa mtambo huu utanufaisha si Stamico pekee bali pia wachimbaji wadogo, wa kati, wakubwa na sekta nzima ya madini nchini,” amesema Ghuliku.

Ameongeza kuwa, mtambo huo unahitajika sana katika kufanikisha shughuli za utafutaji wa madini, hivyo atahakikisha katika kipindi cha mwaka mmoja stamico inazalisha ipasavyo kupitia mtambo huo na hivyo kuwezesha manunuzi ya mtambo mwingine wa aina hiyo.

UDHIBITI UCHAKUAJI MAFUTA WAVUTIA WAWEKEZAJI UINGEREZA

0
0

Na Seif Mangwangi ,Arusha

FURSA na mazingira mazuri ya biashara ya uuzaji mafuta nchini yametajwa kuanza kuvutia wawekezaji ambapo Kampuni ya Vivo Energy Plc ya Uingereza imepanga kuwekeza mtaji wa dola Milioni3 kwa mwaka ifikapo Machi mwakani.

Akizungumza jana mkoani hapa Mkurugenzi Mtendaji wa Engen Petroleum (Tanzania Ltd), Paul Muhato alisema, mazingira mazuri yameishawishi Vivo Energy Plc kujuna nchini na kuwekeza Dola za Marekani milioni 3 kila mwaka.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kituo cha kuuzia mafuta cha Engen kilichopo Tengeru wilayani Arumeru Muhato alisema, kumekuwa na udhibiti mkubwa wa njia za panya zilizokuwa zikiingiza mafuta nchini.

“Udhibiti huu umesaidia sana kuziba njia za panya ambapo mafuta mengi yaliingia nchini bila kulipiwa kodi na hivyo kusababisha kusiwepo uwiano wa kibiashara,” alisema Muhato na kuongeza:“Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), na Taasisi nyingine za Serikali kuweka kodi sawa kwa mafuta ya taa na dizeli,” alisema.

Alisema licha ya kodi kuwa sawa, baadhi ya kampuni zilikosa uaminifu na kuingiza mafuta ya taa kutoka Kenya kutokana na kodi ya mafuta hayo ilikuwa chini ikilinganishwa na Tanzania.Aidha kutokana na nchi ya Kenya kurekebisha kodi kwa mafuta ya dizeli na taa iliwezesha kuweka mizania sawa na hivyo Kampuni zilizoingiza mafuta kwa lengo la kuchakachua hazikuweza tena.

Akizungumzia uhifadhi wa mafuta, alisema, kampuni hiyo ina vituo vya kuhifadhia mafuta katika kwenye mikoa mitano.Muhato alivitaja vituo hivyo kuwa Dar es Salaam wanahifadhi Lita milioni 24, Moshi mkoani Kilimanjaro lita 4,000, Isaka mkoani Shinyanga lita 3,000, Mwanza lita 5,000 na Kigoma lita 4,000.

Alisema kituo cha kilichopo Tengeru kinakuwa cha pili kufunguliwa mkoani Arusha na cha nane nchini baada ya kufunguliwa vituo vingine Dar es Salaam, Segera mkoani Tanga, Visiga mkoani Pwani na Mazimbu mkoani Mogogoro.

Kwa upande wao baadhi ya madereva wa magari na vyombo vingine vya usafiri wakizungumzia biashara hiyo ya mafuta walisema, wafanyabiashara makini wa mafuta husaidia vyombo vyao visiharibike haraka.

“Unapoweka mafuta yasiyo chakachuliwa chombo cha usafiri kinakuwa na maisha marefu, kinakusaidia kuondokana na hasara ya unayoweza kuipata kwa kuweka mafuta machafu,” alisema Mollel
 .Mkurugenzi Mtendaji wa Engen Petroleum Paul Muhato wa sita kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja mbele ya kituo kipya cha mafuta cha engen alichokizindua jana jijini Arusha
 Mkurugenzi mtendaji wa Engen Petroleum ltd Paul Muhato akikata utepe kuashiria kuzindua kituo kipya cha mafuta cha Engen Tengeru Arusha jana.
 Mkazi wa Tengeru akihudumiwa mafuta katika kituo kipya cha mafuta cha Engen kilichozinduliwa jana

HIKI NDICHO WATOTO YATIMA WANAHITAJI KIPINDI CHA SIKUKUU

0
0

IMEKUWA kawaida kwa jamii ya kitanzania kushiriki na watoto wanaolelewa katika vituo vya watoto wenye uhitaji chakula na mahitaji mengine hususan katika msimu wa Sikukuu

Mwananchi mmoja mmoja , vikundi taasisi na ofisi mbalimbali za Serikali na binafsi zimekuwa zikitoa msaada wa chakula na mahitaji mengine kwa vituo vya watu wenye uhitaji lakini je umeshawahi jiuliza watoto hao wanahitaji nini zaidi?

“Mimi napenda sana mtu akipeleke kuogelea lakini, Sisi tunataka kutoka na kujumuika na  watu wengine tucheze nao na tufurahi badala ya wao kuja kutuachia chakula tuu nakuondoka “ alisema Mudy Mbeki mtoto anayelelewa katika kituo cha Yatima Group Trust Fund Chamazi ambaye alikuwa akisherehekea Sikukuu ya Krismass ikiwa ni maadhimisho ya Wakristo ulimwenguni kote  wakikumbuka kuzaliwa kwa masihi Yesu Kristu.

Mudy ni mmoja kati ya watoto zaidi ya 250 kutoka vituo viwili vya watoto wenye uhitaji vya Yatima Group Trust Fund Chamazi na Kurasini Orphanage Center waliokutanishwa pamoja katika ukumbi wa kifarahi katika hoteli ya The Dar es salaam serena Hotel kusherehekea na wafanyakazi pamoja na wadau wa serena msimu huu wa sikukuu.

“Tumekodi zaidi ya magari matano  kwenda kuwafata watoto katika vituo vyak Kurasini na Chamanzi ili wawalete watoto hapa Serena Hotel tufurahi nao sikukuu hii, na huu ni utamaduni wetu wa miaka mingi baada ya kugundua watoto wanatakq sana kutoka nje ya makazi yao waliozoea kipindi hiki cha sikukuu” alisema Sophia Mketo Meneja Rasilimali watu wa Hoteli ya Serena.  

Aliongeza kuwa sherehe hiyo wameshirikiana na wadau wa serena kwa kuwanunulia zawadi watoto wote waliofika hapo kwenye sherehe na lengo kuu ni kuhakikisha watoto wanakuwa na furaha na kuona wanathaminiwa. 

Amesema hapo awali walikuwa wakipika chakula na kupeleka vituoni lakini watoto hao ndio walioonesha hamu ya kutaka kutoka nje ya vituo ndipo walipoanza utamaduni wa kuwatoa outing na imeendelea hivyo kwa miaka mitatu mfululizo sasa. 

Pamoja na kuwaandalia chakula cha mchana, zawadi na michezo mbalimbali serena Hoteli ilimualika Mchekeshaji maarufu Stan Bakora ambaye naye aliwaelezea watoto historia ya maisha yake kuwa akiwa mdogo pamoja na wadogo zake wawili walifiwa na wazazi wao na walilelewa na bibi yake ambaye baada ya miaka kadhaa naye alifariki na hivyo Bakora kuchukua jukumu la kuwalea wadogo zake kwakutumia kipato alichopata kupitia sanaa yake ya uchekeshaji. 

Mbali na kuwachelesha na kuimba na watoto hao waliokuwa na sura za furaha aliwakaribisha wanajamii wote kuwasiliana naye iwapo watataka ajumuike na watoto yenye uhitaji siku yeyote. “ mimi ni yatima kama nyinyi lakini nina ndoto kubwa na namshukuru Mungu kidogo naweza kujimudu na kusomesha wadogo zangu hivyo msikate tamaa na iwapo kuna yeyote atataka kunitumia kushiriki na watoto kama leo walivyofanya serena nawakaribisha tuwasiliane” . 

Naye Katibu Mtendaji wa kituo cha kulelea watoto cha Yatima group Trust Fund Chamazi, Fred Njegeja ameshukuru wanajamii kwa mchango wanaoutoa katika kituo hicho na kuwaomba kuzingatia hitaji la watoto kutoka nje ya kituo na kujichanganya na wanajamii katika kusherehekea sikukuu. 

“Hapa kituoni kwetu asilimia 95 ya msaada unatoka kwa wanajamiii na wanakuja sio tuuu kipindi cha sikukuu lkn na wakati mwingine tuu waki wiwwa kutoa msaada kwa watoto katika kituo chetu, lakini kipindi hichi cha likizo ni vyema hata mwenye uwezo wa kuchukua watoto 5 akatoka nao outing inawasaidia sana wanakuwa wanafurahi na kuona wanathaminiwa.” 

Amesema hali ya kutoka nao nje ya maeneo ya kituo ni kitendo kizuri kwakuwa watoto wengi katika kituo hicho ni wale ambao wamefukuzwa makwao au wazazi wao wamefariki hivyo wamejijenga katika fikra ya kuwa hawapendwi, hivyo kuwachukua kucheza nao na kushiriki nao chakula nje ya makazi yao kunaongeza sana morali na kuona yakuwa wanathaminiwa. 

Mbali na chakula pamoja na mahitaji mengine muhimu kwa Watoto Njegeja amesema wapo wanajamii ambao hujitolea kupeleka michezo mbalimbali na kuburudika na watoto pamoja lakini kama jamii itajitokeza kufanya kama kilichofanywa na serena Hoteli ni dhahiri itabadili kwa kiasi kikubwa mtazamano wa watoto hao wanaolelewa katika vituo vya watoto yatima.
 Watoto Yatima wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi wao walipokuwa Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam
Mwandishi na Mtangazaji maarufu Leaa Mushi (aliyebeba mtoto huku akiwa amebeba mkoba)akiwa kwenye picha ya pamoja na watoto yatima waliokuwa na viongozi wao wakifurahia msimu huu wa Sikukuu.

Waziri Mhagama; Serikali Imedhamiria Kuwezesha Vijana kushiriki kilimo Biashara

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akizindua Mradi wa Kuwawezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara, Manispaa ya Kigoma, Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Kuwawezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara, Manispaa ya Kigoma, Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akimsikiliza Mratibu wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Masuala ya Majadiliano ya Sekta ya Umma na Binafsi), Andrew Mhina juu ya ujenzi wa mabwawa ya Samaki kama sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuwawezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara, Manispaa ya Kigoma, Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akimsikiliza Mratibu wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Masuala ya Majadiliano ya Sekta ya Umma na Binafsi), Andrew Mhina juu ya ukarabati wa mabanda ya kuku kama sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuwawezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara, Manispaa ya Kigoma, Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Baraza la Taifa la Biashara mara baada ya kuzindua Mradi wa Kuwawezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara, Manispaa ya Kigoma, Mradi huo unalenga kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji. (PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)





Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amesema serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuwezesha vijana kiuchumi kupitia kilimo biashara ili kuchochea ongezeko la ajira na kipato chao.

Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Baraza la Taifa la Biashara, kupitia Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji, tayari wilayani Kigoma wameanza kutekeleza Mradi unaolenga kuwezesha vijana kushiriki katika shughuli za uchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.

Akiongea katika ziara yake mkoani Kigoma wakati wa kukagua shughuli za utekelezaji za Baraza la Taifa la Biashara, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama amefafanua kuwa Baraza la Taifa la Biashara kwa kushirikiana na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji, wameanza utekekezaji wa mradi huo kwa kushirikiana na chuo cha Maendeleo Kihinga.

“Nitoe wito watendaji wa Halmashauri na ngazi ya mkoa wa Kigoma waendelee kuwaunga mkono vijana hawa wanao shiriki katika Mradi huu wa Kilimo Biashara, na nawataka mtambue haya yote yanafanyika kwa sababu ya jitihada zinazofanywa na Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, hivyo ufadhili wa Mradi huu kutoka Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji, unaunga jitihada zake za kuwezesha vijana” Amesisitiza Mhagama.

Naye Mratibu wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (Masuala ya Majadiliano ya Sekta ya Umma na Binafsi), Andrew Mhina alibainisha kuwa katika kuhakikisha unawawezesha vijana kuwa na ujuzi wa Kilimo na ufugaji utakao wawezesha kujiajiri tayari wameanza ufadhili wa awali kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 53 ambazo zimetumika katika Ujenzi wa mabwawa ya samaki, ukarabati wa mabanda ya kufugia kuku na kuandaa shamba darasa.

Mradi wa Kuwezesha Vijana Kushiriki katika Kilimo Biashara wilayani Kigoma, Unaratibiwa na Baraza la Taifa la Biashara na ufadhiliwa na Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji chini ya wasimamizi na watekelezaji wa mradi huo amabao ni; Ofisi ya Rais TAMISEMI kupitia Manispaa ya Kigoma, Chuo cha Maendeleo Kihinga, Chuo cha Uvuvi Kigoma, Maradi wa LIC na Baraza la Biashara la Wilaya ya Kigoma.

Baraza la Taifa la Biashara lilianzishwa kwa Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2001 na kuchapishwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 39 la tarehe 28 Septemba 2001. Baraza la Taifa la Biashara ni jukwaa la majadiliano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Lengo kuu la Baraza ni kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa njia ya majadiliano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi. Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images