Jumia imewakabidhi wakazi wa jijini Dar es Salaam, Bw. Johnson Kiama na Dismas Kamalamo zawadi za pikipiki na luninga mpya ya kisasa walizojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’
Shindano hilo lilikuwa likifanyika kila siku ya Ijumaa kupitia kampeni kubwa ya mauzo ya mwaka ya Jumia inayokwenda kwa Black Friday. Kampeni hiyo ambayo ilianza Novemba 16 na kufikia ukomo Ijumaa iliyopita ya Desemba 7, imewawezesha wateja kufanya manunuzi yao ya msimu huu wa sikukuu kwa ofa na punguzo kubwa la bei mpaka 70%!
Zawadi zote mbili za pikipiki na luninga zilifichwa kwenye mtandao wa Jumia ambapo wateja walitakiwa kuzisaka na kukabidhiwa kwa punguzo la asilimia 99 mara baada ya kuzipata. Zoezi hilo lilifanyika kupitia njia ya App ya Jumia inayopatikana kwenye simu zote za iPhone (Apple Store) na Android (Google Play Store). Dhumuni lilikuwa ni kuwawezesha wateja wengi zaidi, ambao wanamiliki simu za kisasa za mkononi, kushiriki mahali popote na muda wowote walipo.
Pikipiki hiyo aliyokabidhiwa mshindi, aina ya Skymark, inauzwa kwa shilingi 1,850,000 katika mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 18,500 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!Huku naye mshindi wa luninga mpya na ya kisasa aina ya Bruhm yenye ukubwa wa inchi 32 yenyewe inauzwa kwa shilingi 570,000 kwenye mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 5,700 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!
Akielezea namna atakavyoitumia zawadi yake ya pikipiki mara baada ya kukabidhiwa, Bw. Johnson Kiama, amesema kuwa, “siamini kama leo hii nimekabidhiwa hii pikipiki maana ilinichukua muda mrefu kuipata.
Shindano hilo lilikuwa likifanyika kila siku ya Ijumaa kupitia kampeni kubwa ya mauzo ya mwaka ya Jumia inayokwenda kwa Black Friday. Kampeni hiyo ambayo ilianza Novemba 16 na kufikia ukomo Ijumaa iliyopita ya Desemba 7, imewawezesha wateja kufanya manunuzi yao ya msimu huu wa sikukuu kwa ofa na punguzo kubwa la bei mpaka 70%!
Zawadi zote mbili za pikipiki na luninga zilifichwa kwenye mtandao wa Jumia ambapo wateja walitakiwa kuzisaka na kukabidhiwa kwa punguzo la asilimia 99 mara baada ya kuzipata. Zoezi hilo lilifanyika kupitia njia ya App ya Jumia inayopatikana kwenye simu zote za iPhone (Apple Store) na Android (Google Play Store). Dhumuni lilikuwa ni kuwawezesha wateja wengi zaidi, ambao wanamiliki simu za kisasa za mkononi, kushiriki mahali popote na muda wowote walipo.
Pikipiki hiyo aliyokabidhiwa mshindi, aina ya Skymark, inauzwa kwa shilingi 1,850,000 katika mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 18,500 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!Huku naye mshindi wa luninga mpya na ya kisasa aina ya Bruhm yenye ukubwa wa inchi 32 yenyewe inauzwa kwa shilingi 570,000 kwenye mtandao wa Jumia. Lakini mshindi amekabidhiwa kwa kulipia shilingi 5,700 tu ambayo ni sawa na punguzo la asilimia 99!
Akielezea namna atakavyoitumia zawadi yake ya pikipiki mara baada ya kukabidhiwa, Bw. Johnson Kiama, amesema kuwa, “siamini kama leo hii nimekabidhiwa hii pikipiki maana ilinichukua muda mrefu kuipata.
Mimi ni mteja wa muda mrefu wa Jumia tangu kipindi cha nyuma ikiwa inajulikana kama Kaymu. Huwa naitumia kununua bidhaa kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya nyumbani na siku hiyo mpaka nafanikiwa kuipata pikipiki hii nilikuwa naweka oda mtandaoni,” alisema na kumalizia, “naitumia kwa shughuli zangu za kiofisi kwa sababu tunajihusisha na huduma za kuchapisha vifaa mbalimbali kwa ajili ya shughuli za kimasoko na matangazo za makampuni mbalimbali.”
Naye kwa upande wake mshindi wa luninga, Bw. Dismas Kamalamo, ameelezea, “ilinichukua takribani lisaa limoja na dakika 40 mpaka kufanikiwa kuipata luninga hii. Kuna muda nilitaka kukata tamaa ukizingatia ni maelfu ya wateja wengine nao walikuwa wanashiriki. Kwa hakika hii ni zawadi bora kabisa katika msimu huu wa sikukuu. Nitaitumia luninga hii kwa matumizi yangu ya nyumbani ukizingatia ni ya kisasa kabisa. Bado siamini kama nimeweza kushinda na kuinunua kwa bei hii.”
Naye kwa upande wake mshindi wa luninga, Bw. Dismas Kamalamo, ameelezea, “ilinichukua takribani lisaa limoja na dakika 40 mpaka kufanikiwa kuipata luninga hii. Kuna muda nilitaka kukata tamaa ukizingatia ni maelfu ya wateja wengine nao walikuwa wanashiriki. Kwa hakika hii ni zawadi bora kabisa katika msimu huu wa sikukuu. Nitaitumia luninga hii kwa matumizi yangu ya nyumbani ukizingatia ni ya kisasa kabisa. Bado siamini kama nimeweza kushinda na kuinunua kwa bei hii.”
Akifafanua kuhusu zoezi zima la ‘Treasure Hunt’ na kampeni iliyomalizika ya Black Friday kwa ujumla, Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey ameeleza kuwa, “ni kawaida yetu Jumia kuja kitofauti kwenye kila kampeni tunayoifanya. Mwaka huu tulikuwa na Black Friday kwa Ijumaa nne mfululizo kuanzia Novemba 16 mpaka Desemba 7. Tofauti na mwaka jana ambapo ilikuwa ni kwa Ijumaa moja tu ya Novemba 23. Na kabla ya mwaka huu kuisha tungependa kufunga mwaka kwa kuwazawadia wateja wetu ”
“Tukiwa tumebakiza wiki chache kabla ya kuumaliza mwaka huu wa 2018, Jumia isingependa kuwaacha Watanzania hivi hivi. Siku ya kesho tarehe 12, mwezi wa 12 kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa moja usiku tutakuwa na kampeni ya mauzo ya siku moja tu au ‘Flash Sales’ ’itakayokwenda kwa jina la ‘ BOOM BAMIZA.’ Tutakuwa na mauzo ya bidhaa 24 tofuati kwenye ‘Flash Sales’ kwa siku nzima. Kila lisaa litakuwa na bidhaa mbili tofuati mtandaoni kwa punguzo la mpaka 70%,” alisema Bw. Geofrey
“Mauzo ya bidhaa haya yatafanyika kote kwenye mtandao wetu wa Jumia lakini pia kwa kupitia App yetu unayoweza kuipakua kwenye simu yako ya mkononi. Bidhaa zitakuwa ni tofauti ili kukidhi mahitaji ya watu wote kama vile: simu za mkononi kama vile Samsung S9, Nokia, Infinix Note 5 Stylus na matoleo mapya kabisa ya Tecno 11 na X Pro.
Vilevile kutakuwa na bidhaa za jikoni na nyumbani kwa ujumla kama vile vyombo vya kupikia, kufulia, friji, luninga na viyoyozi (Air Conditioner) Ningependa kuwasihi watanzania wote kukamilisha manunuzi yao ya sikukuu na ofa hii ya BOOM BAMIZA kabla hawajaenda mapumzikoni. Kama Jumia, tunawaahidi wateja wetu kuendelea kuwa wabunifu kwa kuja na ofa mbalimbali zenye manufaa kwao na kuleta mapinduzi ya manunuzi kwa njia ya mtandaoni nchini,” alihitimisha Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania.
Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari jijini Dar leo wakati wakikabidhi wakazi wawili wa jijini Dar es Salaam, Bw. Johnson Kiama na Dismas Kamalamo zawadi za pikipiki na luninga mpya ya kisasa walizojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’
Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akimkabidhi mbele ya Waandishi wa habari,Bw. Johnson Kiama luninga mpya ya kisasa aliyojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’Meneja Mahusiano ya Umma wa Jumia Tanzania, Kijanga Geofrey akimkabidhi ufunguo wa piki piki Dismas Kamalamo mbele ya Waandishi wa habari, aliyojishindia kupitia shindano la ‘Treasure Hunt.’