Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live

GAVANA LUOGA ATOA PONGEZI MAALUM KWA WAFANYAKAZI BOT KUANDAA MIFUMO YA KUKUSANYA MALIPO YA SERIKALI

0
0

Kushoto: Gavana wa BoT Prof. Florens Luoga akimpongeza Bi. Mota Cecilia Mlama kwa kazi nzuri. Kulia Prof. Luoga (waliokaa katikati) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa BoT walioshirikiana na wataalam kutoka taasisi zingine za serikali kutengeneza mifumo ya kulipa watumishi wa umma mishahara kupitia Benki Kuu na kukusanya malipo ya serikali kielektroniki. Waliokaa wengine kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Kened Nyoni na kulia ni Bi. Flora Mwaigomole, Meneja wa Rasilimali Watu.


Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, amewapongeza wafanyakazi nane wa Benki Kuu upande wa teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kwa mchango na uzalendo wa hali ya juu uliowezesha kusimikwa kwa mifumo ya kielektroniki ya kulipa mishahara na kukusanyia mapato ya serikali nchini.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam katika hafla fupi ya kuwapongeza wafanyakazi hao kwa kushirikiana na wataalam kutoka taasisi zingine za serikali katika kubuni, kutengeneza na kusimika mifumo ya kukusanya malipo ya serikali kielektroniki ya GePG na kulipa mishahara kupitia Benki Kuu ya Tanzania (GSPP) kati ya mwaka 2015 na 2018.

“Siku zote, Benki Kuu imekuwa ikihamasisha wafanyakazi wake kujituma katika kazi kwa weledi na ubunifu wa hali ya juu ili kuongeza tija na kuachana na kufanya kazi kwa mazoea. Katika hili, tunawapongeza kwa kuwa mmetekeleza kwa vitendo falsafa hii kutokana na utendaji wenu uliotukuka. Hongereni sana!,” amesema Prof. Luoga.

Gavana Luoga alisema kwa kutumia wataalam wa ndani kusimika mifumo hiyo, sio tu kumeiwezesha serikali kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi na kuimarisha ukusanyaji wa mapato, bali pia kumeliwezesha taifa kuokoa fedha nyingi ambazo zingetumika kununua mifumo kama hiyo kutoka nje ya nchi.

Pamoja na pongezi hizo, Gavana Luoga amewakabidhi wafanyakazi hao barua ya pongezi kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Ofisi ya Rais, Balozi John Kijazi, aliyoitoa kwao kutokana na kazi yao kutambuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakati taarifa ya kazi hiyo ilipowasilishwa kwake na Wizara ya Fedha na Mipango. Waliopongezwa ni Kiongozi wa Timu ya BoT, Bw. Joel Ngussa, Bw. Eric Lwambura, Bw. Mutashobya Mushumbusi, Bw. Jeremiah Tunutu, Bi. Mota Cecilia Mlama, Bw. Emmanuel Millinga, Bw. Anthony Lyaruu na Bw. George Sije.

“Aidha, napenda kutoa rai kwa wafanyakazi wote wa Benki Kuu kuchukulia mafanikio ya wenzetu hawa wachache kama chachu katika utendaji wenu wa kazi. Heshima ya Taasisi hii katika taifa na hata kimataifa itatokana na jinsi kila mmoja wetu anavyofanya kazi kwa kujituma, kwa weledi na kwa kuleta matokeo chanya ambayo yatasaidia maendeleo ya taasisi na taifa kwa ujumla,” Gavana amesema.

Prof. Luoga amesema Benki Kuu itaendelea kufanya kazi kwa kutumia wataalam wa ndani kwa manufaa ya taifa na kuongeza kuwa “ni wajibu wa taasisi hii na taifa kwa ujumla kutambua mchango mkubwa unaotolewa na wataalam wa ndani kwa kuhakikisha wanatumika kikamilifu.”

Katika maelezo ya awali, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Kened Nyoni, alisema utekelezaji wa miradi hiyo umeiwezesha serikali kuanza kulipa mishahara ya watumishi wake kupitia Benki Kuu ya Tanzania, kuokoa fedha zilizokuwa zinalipwa kwa mawakala katika mchakato wa ulipaji mishahara pamoja na kuharakisha mchakato mzima wa ulipaji.

Pia, mfumo wa GePG) umeiwezesha serikali kukusanya mapato ya taasisi zake kikamilifu, kuwa na uwezo wa kujua kila wakati kiwango cha makusanyo (maduhuri) yake na pia kupunguza upotevu. Akitoa shukrani kwa niaba ya wenzake, Bw. Joel Ngussa alisema kwamba pongezi walizopata ni “chachu ya kuongeza juhudi ya utendaji katika kazi na miradi mingine yenye tija kwa taasisi na taifa kwa ujumla.” Aidha, Bw. Ngussa ameeleza kutambua ushiriki na kazi kubwa ya watumishi wenzao katika kutekeleza miradi hiyo kutoka Benki Kuu pamoja na taasisi zingine nchini.

“Kwa niaba ya timu nzima iliyoshiriki katika kazi hizo, napenda kuchukua fursa hii kuweka katika kumbukumbu mchango wa wafanyakazi wengine wa Benki Kuu ambao waliwezesha kufanikisha kazi hiyo. Wafanyakazi hao ni Bi. Peragia Nsabi, Bw. Stephano Mwendo, Bw. Justice Faustine, Bw. Mathew Massoy na Bw. Luphingo Mwasalujonja,” alisema Bw. Ngussa

Hafla hiyo ya ilihudhuriwa pia na wafanyakazi na menejimenti Benki Kuu ya Tanzania.

LUGOLA ASEMA POLISI WACHACHE WANAOLICHAFUA JESHI KWA KULA RUSHWA DAWA YAO IPO JIKONI

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kushoto), akifurahi jambo wakati alipokua anasalimana na Diwani wa Kata ya Nyamihyolo, Mgendi Patrick, wakati Waziri huyo alipopokelewa na mabango na wananchi wa Kijiji cha Mahyolo, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, leo, ambayo yalikua yana ujumbe mbalimbali. Lugola aliwataka wananchi wa Kijiji hicho wafanye shughuli za maendeleo bila kuvunja sheria za nchi. Pia alitoa onyo kwa baadhi ya askari kuiacha tabia hiyo haraka iwezekanavyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola (kulia), akimsikiliza Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahyolo, Clifford Bwire, alipokua anajibu maswali kuhusu ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Mahyolo iliyopo Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, kutokuendelea licha ya kua wananchi wa kijiji hicho walichanga fedha. Pia Lugola aliwataka wananchi wa Kijiji hicho wafanye shughuli za maendeleo bila kuvunja sheria za nchi. Pia alitoa onyo kwa baadhi ya askari ambao wanaomba rushwa kwa wananchi kuiacha tabia hiyo haraka iwezekanavyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola, akiwasalimia wanafunzi wa Shule ya Msingi Muungano iliyopo Kijiji cha Namibu, Kata ya Neluma, Jimbo la Mwibara, Bunda, Mkoani Mara, wakati Waziri huyo alipofanya ziara shuleni hapo kwa ajili ya kuwasalimia wanafunzi hao pamoja na uongozi wa shule hiyo. Lugola yupo katika ziara ya kuhamasisha maendeleo na pia kuwapa elimu ya ulinzi na usalama jimboni kwake. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola maesema licha ya kuwa Jeshi la Polisi linapambana usiku na mchana kuwaondoa askari wala rushwa lakini ana taarifa ya baadhi yao wanaendeleza tabia hiyo, hivyo dawa yao ipo jikoni inachemka.

Amesema licha ya kutoa taarifa mara kwa mara kuwataka askari hao kufanya kazi kiuhadilifu kwa kuacha tabia ya kuomba rushwa lakini baadhi ya askari hao hawajamuelewa hivyo atapambana nao mpaka Jeshi hilo litakapokuwa safi.

Lugola amesema anapokea taarifa mbalimbali kutoka kwa wananchi kuwalalamikia baadhi ya Polisi kufanya matukio hayo ambayo hayakubaliki lakini anawataka askari polisi hao wajue kuwa kati ya maagizo aliyopewa na Rais Dk. John Pombe Magufuli ni kupambana na rushwa ndani ya Wizara hiyo, hivyo hawezi kumuangusha hata siku moja.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kijiji cha Namibu, Kata ya Neruma, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, Lugola alisema baadhi ya polisi wanalichafua Jeshi hilo kutokana na tamaa zao, hivyo ameendelea kusisitiza kuwa, Serikali ya Magufuli ya awamu ya tano siyo ya kuchezewa.

“Jeshi la Polisi linalinda usalama wa raia na mali zao, linapambana na rushwa katika mambo mbalimbali yakiwemo ya ardhi hapa kijijini, hivyo ndugu wananchi mnapopata migogoro mbalimbali ikiwemo ya ardhi na mengineyo akikisheni mnatoa taarifa polisi ili muweze kusaidiwa,” alisema Lugola.

Hata hivyo, Lugola aliongeza kuwa, anapofanya ziara sehemu mbalimbali nchini anapokea maswali na pia anatumiwa meseji zikilalamikia tabia ya baadhi ya askari polisi ambao wanaomba rushwa hasa askari wa usalama barabarani.

Lugola aliongeza kuwa, licha ya kuwa Polisi inaendelea kupambana na rushwa lakini nchi ipo salama hivyo wananchi popote nchini wanapaswa kuwa na amani na kuendelea kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo pamoja za kilimo kijijini hapo. “Mimi sitakubali kuona mwananchi anateseka, mwananchi anaonewa, nasema hivi hao askari ambao ni wachache sana nitahakikisha ninapambana nao bila huruma, kwanini mnaonea wananchi ambao wengi wao ni maskini kwa kuwaomba rushwa, hii haijakaa sawa,” alisema Lugola.

Lugola ambaye mwezi Septemba alitangaza kuwa vituo vya polisi vifanye kazi saa 24 kwa kutoa dhamana kwa mwananchi yeyote mwenye sifa atakayekuja siku ya Jumamosi au Jumapili, akiwa na maana kuwa ataondoa rushwa katika vituo, na pia alitangaza kupambana na askari wala rushwa pamoja na watumishi wote waliopo wizarani kwake na Serikali kwa ujumla.

Aidha, Lugola aliwataka wananchi wa Kata hiyo waendelee kufanya shughuli za kimaendeleo katika vijiji vyao na pia waanze maandalizi ya kilimo, naye atahakikisha anatoa misaada mbalimbali ikiwemo mbegu ili wananchi hao waweze kupata mazao yaliyo bora kwa hapo baadaye.

ZAIDI YA WANANCHI 500 BUTIAMA WAJITOKEZA KUPATA HUDUMA YA KINYWA CHA MENO.

0
0
Na Frankius Cleophace Mara.

Zaidi ya wananchi wanao kadiliwa kufikia miatano wamejitokeza kupata huduma ya kinywa na meno katika wilaya ya Butiama mkoani Mara kupitia huduma ya Madkatari Bingwa wa Afya ya Kinywa na meno.

Imelezwa kuwa zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wemekuwa Wakiungua ugonjwa wa kinywa na meno jambo ambalo linahatarisha maisha yao ambapo pia Tatizo Sugu la fizi hupelekea kutokea kwa Magonjwa mengine ikiwemo Magonjwa ya moyo na sukari.

Hayo yamebainishwa na Rais wa chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na meno Tanzania Daktari Ambege Jack Mwakatobe wakati wa utoaji huduma hiyo kwa wananchi wa Wilaya ya Butiama ,Mwitongo mkoani Mara

Daktari Mwakatobe amesema kuwa uwepo watatizo hilo ndio chanzo kikubwa cha kupelekea kutoa huduma hiyo ambapo waliamua kufanyia wilayani Butiama ikiwa lengo nikumuenzi Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na uwepo wa changamoto ya ukosefu wa watalamu wa Tatizo hilo katika hospitali za wilalaya.

“Tulishwahi kuja awali tukagundua kuwa kuna uhitaji mkubwa sana wa kutoa hudma ya matatizo ya Fizi ndio maana tumeamua kuja kutoa huduma hii ambapo novemba 28 tunamkutano wetu wa madaktari Bingwa.” Alisema Mwakatobe.

Pia alisema kwa Mujibu wa Utafiti wa uliofanywa na hospitali ya muhimbili ni mika 10 mfululizo Asilimia 80 ya watu wazima wamekuwa na matatizo ya kinywa na meno huku watoto kuanzia miaka 12 nao wakikumbwa na matatizo hayo ya kinywa na meno hivyo kuepelekea kushindwa kutimiza ndoto zao za masomo.

Serikali ya wilaya ya Butiama kupitia mkuu wake Wawilaya Bi.Annarose Nyamubi Alipongeza ujio wa madkatari hao huku akiwataka wananchi kutumia Fursa zinazojitokeza kutoka kwa madaktr Bingwa ,ambapo alisema wanauhitaji mkubwa wa watoa huduma kutokana na wingi wawananchi wenye matatizo hayo.

Costanzia Malyabibi nimmmoja ya wananchi walipata nafasi ya kuhudumiwa ambapo wanaipongeza serikali kwa kuwajali wananchi wake kwa kuwasogezea huduma huku wakiomba zinapotokea fursa kama hizo basi zitoke kwa mda mrefu ili kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa na upatikanaji wa huduma hiyo ambayo imekuwa ikileta matatizo mengi.

Chama cha Madkatari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania kinatarajiwa kufanya mkutano wake katika manispaa ya Musoma Novemba 28 huku Mgeni Rasimi wa Ufunguzi wa mkutano huo akitarajiwa kuwa waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu.
Mkuu wa wilaya ya Butiama Anarose Nyamubi akiongea na baadhi ya waginjwa wa maeneo katika eneo la madaktari bingwa wa Kinywa na meno wanapotoa huduma.
Madaktari bingwa wa kinywa na Meno wakiendelea na matibabu ikiwemo kungoa Meno katika eneo la Mwitongo Wilayani Butiama Mkoani Mara.
Baadhi ya wananchi wakipatiwa elimu jinsia ya kutunza vinywa na Meno.
Wanafunzi wa Sekondari wa Sekondari wakipatiwa elimu ya kutunza Kinywa na Meno.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MJI WA GEITA.

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamewaagiza Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wahakikishe wanasimamia vizuri uwajibikaji na utowaji wa huduma kwa wananchi katika maeneo yao bila ya woga. 

Kadhalika, Waziri Mkuu amemtaka kila mtumishi wa umma nchini awajibike katika kufanya kazi kwa bidii na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano haitowavumilia watumishi ambao ni wezi, wabadhilifu, wavivu na haitosita kuwachukulia hatua.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na watumishi, viongozi wa mkoa, wilaya ya Geita na taasisi za umma katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Mamlaka ya Mji Geita.“Watumishi fanyeni kazi kwa bidii na msitarajie kuundiwa tume pale mnapofanya vibaya, ukiharibu kazi tunakushughulikia hapo hapo na huu ndio msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli.”

Waziri Mkuu aliwaeleza watumishi hao kuwa wanatakiwa wafanye kazi kwa kuzingatia sheria na kanuni za kazi na pia watambue dhamana kubwa waliyonayo, ambayo ni kuwahudumia wananchi wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza watumishi wa umma hususani Wakuu wa Idara wahakikishe wanakuwa na kitabu cha Ilani ya Uchanguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili wapate muelekeo wa utekelezaji washughuli zao.

Waziri Mkuu amesema kitabu cha Ilani ya uchanguzi cha CCM 2015/2020 kina maelekezo ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo kila idara inatakiwa kuangalia maelekezo yaliyotolewa kuhusu idara husika na kuyafanyia kazi.Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alimuhakikishia Waziri Mkuu kwamba yeye kwa kushirikiana na viongozi wenzake watayafanyia kazi maelekezo yote ambayo ameyatoa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Geita kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Novemba 27, 2018. Kulia ni Mbunge wa Chato na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Geita wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Novemba 27, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

VIONGOZI WAANDAMIZI WA JUMUIYA ZA CCM WASHIRIKI MKUTANO NCHINI NAMIBIA

0
0
 Katibu Mkuu UWT Queen Mlozi akiwasilisha mada kwenye moja ya mkutano wa siku tatu uliofanyika hivi karibuni  Nchini Namibia
Nikiwa na picha ya pamja na Makatibu Wakuu wa Jumuia za Chama Cha Mapinduzi Ndg. Erasto Sima( Wazazi) na Ndg. Raymond Mwangwala (UVCCM) kabla ya kuanza kushiriki mkutano huo hivi karibuni nchini Namibia.

MZAZI AFURAHI KUUAWA KWA MWANAE.

0
0
JOSEPH MPANGALA,MTWARA.

Mwanamke Mmoja aliyejulikana kwa Jina la Ndilikuli Matupa Mkazi wa kijiji cha Mkangaula Kata ya Namalenga wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara ameshukuru wananchii wenye hasira Kali kwa Kumchoma Moto Kijana wake Abdallah Hussein Mahona kwa Tuhuma za Kuhusika na matukio Kadhaa ya Ukabaji,Unyang'anyi na Mauaji.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 12 asubuh mwanzoni mwa wiki hii ambapo marehemu alihusishwa na kuwajeruhi watu wawili ndipo wananchi wenye hasira wakamtafuta na kumchoma moto mpaka kifo chake.

Akiongea katika eneo la Tukio ambalo Marehem Abdallah Hussein amechomwa mama yake Mzazi Bi Ndilikuli Matupa anasema alilazimika kulala nyumba za stareh {Disco}ili kuepuka kuuawa na Mwanae ambapo mara kadhaa amekuwa akimtishia Kumuua.

“Sina Masikitiko yoyoyote Mzazi Mimi,Nimepona kwa chukuchuku kila siku Mwenye disko mtu mkubwa kama Mimi nilikuwa nawaacha wajukuu wangu Mmoja wa Marehem Mmoja wa kaka yake mimi nakwenda kwenye disco ilihali mimi sio mtu wa disco yaan kukimbia Kifo”alisema Bi Ndilikuli Matupa ambaye ni Mama wa marehem.

Hata Hivyo Bi Ndilikuli ameongeza kuwa sio mara ya kwanza kwa Marehem mwanae Kumtishia kumuua kwa kumtuhumu kuwa ni Mchawi kutokana na Mtoto wa Marehemu Kuumwa kwa kipindi cha Muda Mfupi.

“Kwanza kifo Cha kwanza kabisa nilitaka kuuwawa kutokana na Mtoto wake Yupo hapa Mohamed Kuumwa tu Mudy nikataka kuuwawa nikasema huyu anaumwa tu sio kwa kumroga mimi nimroge mimi kwa sababu gani”Alisema Mama wa Mzazi wa Marehem.

Mnape Mohamed Mnape ni Mmoja wa ndugu wa Marehem wanaoishi kijijini hapo anasema ndugu yake alikuwa akizulumu watu na mara nyingi alikuwa akimpiga mama yake Mzazi na mara nyingi alikuwa akitembea na Panga mkononi.

“Huyu mimi ni ndugu yangu na matukio yake nayafaham tokea siku za nyuma na hata juzi nilikuwa naye kwanza alifikia kuwa katili kuwazulumu watu mpaka imefikia hatua ya kumpiga mama wakati akitoka kwenye sherehe”amesema Mnape ambaye ni Ndugu wa Marehem.

Lakini naye Mtendaji wa kata ya Namalenga ambapo ndipo marehema alikuwa akiishi Sijaona Binamu anasema pindi aliporipoti kazini mwezi wa saba mwaka 2016 taarifa ya kwanza ya kiuhalifu ilimtuhumu marehema Abdallah kwa kuua mwanzafunzi wa kudato cha kwanza mwaka 2010.

“Niliporipoti mwaka 2006 taarifa ya kwanza niliyopewa ilikuwa ni Marehem Kutuhumiwa kumuua mwanafunzi wa kidato cha kwanza mwaka 2010 na akatoweka hapa kijijini kwa muda wa miaka mitatu lakini baada ya miaka mitatu akaanza kujionesha kidogo kidogo mpaka mazingira alipoona ni rafiki kwake ndio akaendelea na matukio Mengine”alisema Sijaona Binamu.

Hata Hivyo jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara bado linaendelea na Uchunguzi ili kubaini sababu halisi ya Kifo hicho.


Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Mkangaula kata ya Namalenga tarafa ya Lulindi wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara wamekusanyika kutazama mwili wa marehem Abdallah Hussein Mahona aliyechomwa Moto kwa Tuhuma za Ukabaji na Unyang’anyi.
Mabaki ya mwili wa marehem Abdallah Hussein mahona ambaye ameuwawa kwa kuchomwa moto na wananchii wenye hasira kali baada ya kutuhumiwa kuwa kibaka ambapo wananchii wa kijiji hicho walikusanyika kwa ajili ya Kuutazama.
 
Mwanamke Mmoja aliyejulikana kwa Jina la Ndilikuli Matupa Mkazi wa kijiji cha Mkangaula Kata ya Namalenga wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara ameshukuru wananchii wenye hasira Kali kwa Kumchoma Moto Kijana wake Abdallah Hussein Mahona kwa Tuhuma za Kuhusika na matukio Kadhaa ya Ukabaji,Unyang'anyi na Mauaji.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 12 asubuh mwanzoni mwa wiki hii ambapo marehemu alihusishwa na kuwajeruhi watu wawili ndipo wananchi wenye hasira wakamtafuta na kumchoma moto mpaka kifo chake.

Akiongea katika eneo la Tukio ambalo Marehem Abdallah Hussein amechomwa mama yake Mzazi Bi Ndilikuli Matupa anasema alilazimika kulala nyumba za stareh {Disco}ili kuepuka kuuawa na Mwanae ambapo mara kadhaa amekuwa akimtishia Kumuua.

“Sina Masikitiko yoyoyote Mzazi Mimi,Nimepona kwa chukuchuku kila siku Mwenye disko mtu mkubwa kama Mimi nilikuwa nawaacha wajukuu wangu Mmoja wa Marehem Mmoja wa kaka yake mimi nakwenda kwenye disco ilihali mimi sio mtu wa disco yaan kukimbia Kifo”alisema Bi Ndilikuli Matupa ambaye ni Mama wa marehem.

Hata Hivyo Bi Ndilikuli ameongeza kuwa sio mara ya kwanza kwa Marehem mwanae Kumtishia kumuua kwa kumtuhumu kuwa ni Mchawi kutokana na Mtoto wa Marehemu Kuumwa kwa kipindi cha Muda Mfupi. 

MAADHIMISHO SIKU YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA JIJINI DAR

0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza na watoto na wageni waalikwa waliohudhuria katika sherehe ya siku ya watoto duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez akizungumza katika maadhimisho ya siku ya watoto duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Bi. Maniza Zaman akizungumza na watoto na wageni waalikwa waliohudhuria katika sherehe ya siku ya watoto duniani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Wageni waalikwa wakifuatilia.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez akiteta jambo na mgeni mwalikwa.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu ambaye alikuwa mgeni rasmi akisalimiana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Ally Mwalimu ambaye alikuwa mgeni rasmi (kushoto) na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez (kulia) wakifuatilia mijadala.
Miongoni mwa vijana waliotoa ushuhuda wao ni mtangazaji wa kituo cha radio Clouds FM, Millard Ayo (pichani), ambaye amesema yeye alisimamia ndoto yake hadi dakika ya mwisho licha ya vikwazo kadhaa alivyopambana navyo.



Miongoni mwa vijana waliotoa ushuhuda wao ni aliyewahi kuwa Miss Tanzania 2012 Briggitte Alfred Lyimo (pichani), ambaye kwa sasa anajishughulisha na kusaidia watuu wenye ulemavu wa ngozi.

Mwenyekiti wa Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mtoto Joel Festo akitoa shukrani zake za pekee kwa wageni walioweza kufika katika sherehe yao.


SHIRIKA la Kuhudumia Watoto Duniani (Ofisi ya Tanzania), leo Novemba 27, 2018 imeungana na watoto wote duniani kusherehekea siku ya kimataifa ya watoto iliyofanyika jijini Dar es Salaam.





Hafla hiyo ambayo mheni rasmi alikuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto, Mhe. Ummy Mwalimu, ilishuhudia mamia ya watoto wakisikiliza ushuhuda kutoka kwa watoto na vijana ambao walieleza namna ya kusimamia ndoto aliyonayo my ili kuifikia.

Miongoni mwa vijana waliotoa ushuhuda wao ni mtangazaji wa kituo cha radio Clouds FM, Millard Ayo, ambaye amesema yeye alisimamia ndoto yake hadi dakika ya mwisho licha ya vikwazo kadhaa alivyopambana navyo.

Amesema darasani hakuwa "mzuri" sana, na hivyo hakuwa na hamu ya kuendelea na masomo kwani hakuwa akifanya vizuri, lakini kichwani mwake alikuwa na ndoto ya kuwa mtangazaji siku moja.

Millard Ayo ambaye pia ni mmiliki wa mtandao wa kijamii wa Millard Ayo.com, amesema, jitihada zake za kufikia ndoto hiyo zilitimia lakini jambo la muhimu ambalo amewaasa watoto kulizingatia ni kutokuwa na tamaa, na kufanya kazi kwa bidi na kwa uaminifu na kumtanguliza Mungu mbele.

BENKI YA ABC YAWEKEZA KWENYE MAENDELEO YA JAMII

0
0
Na Vero Ignatus, Arusha.

Benki ya ABC tawi la Arusha imeendelea na juhudi za kuwekeza kwenye maendeleo ya jamii kwa kutoa mikopo kwa wajasiriamali ,kusaidia jamii kupata bima za afya ili kuharakisha maendeleo ya jamii ya Kitanzania.

Meneja wa Benji hiyo tawi la Arusha Magabe Nyambuche amesema kuwa kwa mwaka 2019 Benji hiyo imejipanga kutoa mikopo kwa Vikundi maalumu ikiwemo Vicoba na Sacco's ambao wamekua wakipewa mafunzo na Maafisa Wa Ustawi wa jamii ili waweze kunufaika na mikopo kwa kufanya shughuli za uzalishaji Mali.

Magabe alisema kuwa benki hiyo limekua karibu na jamii na kuwafikia wananchi walioko vijijini kupitia ubunifu wa kutoa huduma za kifedha kwa njia ya mtandao ambapo benki hiyo ilipewa tuzo ya Ubunifu.

"Kwa sasa tuna mawakala 250 ambao wanahakikisha kuwa wateja wetu wanafikiwa na huduma za kifedha popote pale walipo" Anaeleza Meneja hiyo

Hata hivyo benki hiyo imedhamini mkutano mkuu wa Wadau wa maendeleo ya jamii unaondelea jijini Arusha ikiwa ni juhudi mojawapo ya kuisaidia jamii ambayo hunufaika na Utaalamu wa Maafisa wa Maendeleo katika Vijiji na Mjini.

Pia wamejizatiti katika kuendelea kushirikiana na serikali kuharakisha maendeleo ya jamii kwa kutuma dhana ya uwezeshaji wa mikopo yenye masharti nafuu.


Meneja wa Benji ABC tawi la Arusha Magabe Nyambuche

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA BALOZI WA PALESTINA PAMOJA NA BALOZI WA JAPAN JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli (kushoto) aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli (kushoto) aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Japan nchini Mhe. Shinichi Goto (kushoto) aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuonyesha viungo vya chai kutoka Zanzibar Balozi wa Japan nchini Mhe. Shinichi Goto (kushoto) wakati wa kumkabidhi kama zawadi, Mheshimiwa Balozi wa Japan alifika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Japan nchini Mhe. Shinichi Goto (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Rais)

KITUO CHA UWEZESHAJI SEKTA YA USAFIRI WA KATI WAKUTANA KUJADILI SERA MBALIMBALI

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mkutano wa Kituo cha Uwezeshaji wa Usafiri wa Kati (CCTTFA), kimekutana na wadau kutoka nchi tofauti katika Ukanda wa Jangwa la Sahara kujadili sera mbalimbali.

Mkutano huo utakaofanyika kwa siku tatu kuanzia Novemba 28- 30 mwaka huu utazungumzia  mpango wa sera za usafiri wa Afrika eneo la kiuchumi jamii ya ushirikiano wa kamati ya usafiri.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Mtendaji wa CCTTFA, Capt Dieudonne Dukundane amesema mkutano huu unalenga kujadili masuala mbalimbali ya Kiuchumi kwa nchi washirika na kuhakikisha mafanikio yanafikiwa.

Amesema, CCTTFA ni kituo kinachokutanisha nchi ya Tanzania, Kenya, Uganda, Zambia, Jamhutri ya Kidemokrasia  Congo, Rwanda na Burundi na kukutana pamoja ni kwa ajili ya kufahamu Tanzania wanafanikiwaje kwenye sekta ya usafiri hususani Reli na barabara na hata sisi pia tunajifunza baadhi ya vitu kutoka kwao.

"Tumekutana katika mkutano huu wa siku tatu lengo letu likiwa ni kujadiliana na masuala mbalimbali pia wao wanakuja pia kujifunza Tanzania imefanikiwa kwa namna ipi kwenye sekta ya usafiri hasa kwenye reli na barabara ikiwemo na sisi wenyewe kujifunza baadhi ya vitu kutoka kwao,"amesema Dukundane.

Aidha, ameeleza kuwa kila kanda zinakuwa na kazi maalumu katika kuhakikisha mafanikio yanafikiwa ili wakuze uchumi wa mataifa yao,"tukiangalia kwa upande wa Afrika Mashariki hakuna kulipia visa (Kibali) kwa ajili ya kwenda katika nchi za Uganda, Kenya na zingine kitu kinachochochea kukua kwa uchumi wakati nchi zingine za Afrika hakuna hicho kitu.

"Tutakutana hapa kwa siku tatu tutajadili masuala muhimu kwenye sekta ya usafiri na ukuaji wa uchumi, hata hivyo ukiangalia kwa nchi za Afrika Mashariki watu wanaigia bila kulipia Visa kitu ambacho kinasaidia kwa kiasi kikubwa kuleta maendeleo na ukiangalia nchi zingine za Afrika hakuna,"amesema.

Dukundane amesema, kushirikiana kwenye masuala ya usafiri yamekuwa kichochea kikubwa cha uchumi kukua, kuangalia kipi kinaweza kusababisha mzigo kuchelewa.

Hata hivyo, mkutano huo umewakutanisha wadau hao na watajadiliana ushirikiano uliopo katika nchi hizo kwenye sekta ya usafirishaji na masuala mbalimbali ya kimaendeleo kwenye sekta za biashara.
Katibu Mtendaji wa   Kituo cha Uwezeshaji wa Usafiri wa Kati (CCTTFA),  Capt Dieudonundne Dukane akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa mkutano huo utakaofanyika kuanzia Novemba 28- 30 mwaka ukiwa na lengo la  kujadili masuala mbalimbali ya Kiuchumi kwa nchi washirika na kuhakikisha mafanikio yanafikiwa.
Washiriki wa mkutano wa mwaka wa  kituo cha Uwezeshaji wa Usafiri wa Kati (CCTTFA) wakiwa katika picha ya pamoja.

UNICEF identifies youth role in SDG

0
0
By Our Reporter

Young citizens in Tanzania can play a significant role to enable the country realize its Vision 2025, the global Sustainable Development Goals and Agenda 2063.

Speaking in Dar es Salaam on Tuesday during World Children's Day celebrations , United Nation Children's Fund (UNICEF) Representative Ms. Maniza Zaman said youth of Tanzania should be encouraged and engaged in realizing of the country’s development objectives.

Ms. Maniza who was addressing over 100 young men and women from different schools and higher learning institutions from all over the country at an event organized at the Bank of Tanzania Conference Facilities said that Tanzania’s children under the age of 18 have their hopes and dreams in life, just like adults and, that these aspirations should not only be encouraged to blossom but also to benefit the country’s development agenda.

The Oxford University educated Ms. Maniza said that if every boy and girl is given a fair chance and the opportunity to be heard in life as well as supported accordingly, then chances are that they will be successful and make significant contribution to the country’s struggle for development.

“Let us encourage them to make the right choices and pursue the paths to make those choices a reality in their lives. This will surely help them achieve their goals in life as well as significantly contributing to the country’s major development goals,” said Ms Maniza.

During the event five young Tanzanians shared their aspirations, dreams, and narrated their stories on how they chose their path in life, bringing them to some encouraging achievements.

The five included Brigitte Lyimo, Miss Tanzania 2012 and now an activists for the rights of young people with albinism in Tanzania, an activist for youth rights from Arusha Raphael Dennis and an IT and engineering student at the University of Dar Es Salaam Witness Mtui.

Other were a popular radio presenter and online influencer Millard Ayo as well as Vanessa Innocent, a form two student at Chang’ombe Secondary School in Dar Es Salaam, who received a standing ovation for her articulate presentation on her hopes and aspirations in life, where she told participants that she wants to be a motivational speaker in life.

The aim of these talks was to draw attention to the issues and challenges being faced by children and young people in Tanzania, as well as encouraging them to believe in themselves, knowing that hopes and dreams cultivated at young age in life and driven by self confidence can turn them into successful citizens of their country.

The United Nations Children Fund (UNICEF) was first set up on December 11th in 1946 in New York, and for more than 70 years the Fund has worked to promote children’s survival, protection and development in key life support areas such as health and nutrition, clean and safe water provision and sanitation, basic quality education and protection from violence, exploitation and recently, from HIV/AIDS.

The work of UNICEF which has now operations in more than 170 globally with more than 13,000 staff, 85 percent of which is in filed activities was significantly enhanced by the adoption of the Declaration of the Rights of the Child in 1959 which was followed, twenty nine years ago, in 1989, by the global adoption of the Convention of the Rights of the Child (UNCRC), which then became the most rapidly and widely ratified international human rights treaty in the history of mankind.

The Convention changed the way children are viewed and treated.

They came to be seen as human beings with a distinct set of rights – and not just passive objects in need of care and charity.

Twenty-seven years ago, Tanzania ratified the UNCRC, and. today, the country has much to celebrate – from less children under-five dying, less babies getting HIV, a steady decline in malnutrition over the years, more children accessing schooling to name a few.

Maniza says that Tanzania’s commitment and efforts in support of children’s rights have to be recognized and appreciated.

"Tanzania’s growing child population (set to double by 2030), socio-economic and cultural diversity, and its regional, gender and social disparities, still pose challenges to the realization of all that is in the Convention on the Rights of the Child" she said.

She added that there are children still dying too soon, who are not growing up healthy and well nourished, who don’t manage to go to school and learn, who live in fear and experience all forms of violence, which do not have clean water and proper toilets to use.

Maniza added that there are children whose voices are not heard – never heard, insisting that these children must be the focus of everybody's collective attention – “leave no one behind” as world leaders said when they signed the Sustainable Development Goals.

She insisted that UNICEF has a special role in supporting the Convention.

"Article 45 assigns UNICEF a legal obligation to promote and protect child rights by supporting the work of the Committee on the Rights of the Child. Guided by the provision and principles of the CRC, child rights are at the heart of UNICEF’s work" she said.

Rais Magufuli akutana na Rais Mstaafu Thabo Mbeki na Waziri wa Maendeleo wa Norway, Ikulu Dsm

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais mstaafu wa Afrika Kusini Mhe.Thabo Mbeki Mwenyekiti wa jopo la Umoja wa Afrika linalohusu Udhibiti na Utakatishaji wa Fedha haramu kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu Jijini Dar es salaam.Novemba 28,2018
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza  na Rais mstaafu wa Afrika Kusini Mhe.Thabo Mbeki Mwenyekiti wa jopo la Umoja wa Afrika linalohusu Udhibiti na Utakatishaji wa Fedha haramu kabla ya kuagana nae Ikulu Jijini Dar es salaam.Novemba 28,2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Rais mstaafu wa Afrika Kusini Mhe.Thabo Mbeki Mwenyekiti wa jopo la Umoja wa Afrika linalohusu Udhibiti na Utakatishaji wa Fedha haramu(watatu kutoka kushoto) kutoka kulia kwa mhe.Rais Magufuli ni  Bw.Barrister Akere Muna,Naibu Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Dkt.Damas Ndumbaro,Bi Mojanko Gumbi (Wapili kutoka kulia )Wakili wa Mhe.Thabo Mbeki, na Balozi Zuhura Bundala (wakwanza kutoka kushoto) Ikulu Jijini Dar es salaam.Novemba 28, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya kumaliza mazungumzo na Rais mstaafu wa Afrika Kusini Mhe.Thabo Mbeki Mwenyekiti wa jopo la Umoja wa Afrika linalohusu Udhibiti na Utakatishaji wa Fedha haramu .Ikulu Jijini Dar es salaam.Novemba 28,2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway Nicolai Astrup kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.Novemba 28,2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway Nicolai Astrup alipomtembelea Ikulu jijini Dar es Salaam Novemba 28, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi  Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway Nicolai Astrup kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.Mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya nje na Afrika mashariki Dkt.Damasi Ndumbaro,Naibu waziri wa Kilimo Omary Mgumba pamoja na Balozi wa Norway nchini Elisaberth Jacobsen Novemba 28, 2018.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway Nicolai Astrup , Naibu Waziri wa Mambo ya nje na Afrika mashariki Dkt.Damasi Ndumbaro,Naibu waziri wa Kilimo Omary Mgumba pamoja na Balozi wa Norway nchini Elisaberth Jacobsen Novemba 28, 2018. PICHA NA IKULU

MAJALIWA ATEMBELEA MRADI WA MAJI WA NYAMTUKUZA WILAYANI NYANG’HWALE

0
0


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Kamuyaga Ibuga (kushoto) wakati alipotembelea Mradi wa Maji wa Nyamtukuza wilayani Nyang’hwale,  Novemba 28, 2018
PMO_0086-min
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea chanzo cha Maji katika  Mradi wa Maji wa Nyamtukuza wilayani Nyang’hwale, Novemba 28, 2018
PMO_0043-min
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitazama wingi wa Maji katika tangi  wakati alipotembelea Mradi wa Maji wa  Nyamtukuza wilayani Nyang’hwale Novemba 28, 2018.  Kulia ni Waziri wa Nisahati na Mbunge wa Chato, Medard Kalemani. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

UPELELEZI KESI YA UHUJUMU UCHUMI WAFANYAKAZI WA NEMC BADO HAUJAKAMILIKA

0
0
Na Karama Kenyunko blogu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa, upelelezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili wafanyakazi watano wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) bado haujakamilika. 

Wakili wa Serikali, Jenipher Massue aamedai hayo leo Novemba 28.2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando wakati kai hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa, 

"Mheshimiwa kesi leo imekuja kwa ajili ya kutajwa upelezi bado haujakamilika tu naomba tarehe ya kutajwa" amedai wakili Massue.
Hakimu Mmbando ameahirisha kesi hiyo hadi Desemba 12, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa. 

Katika kesi hiyo wafanyakazi hao wanakabiliwa na mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya Waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira,Januari Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa Mazingira.

Washtakiwa hao ni Ofisa wa Mazingira NEMC,Deusdith Katwale(38) na Mtaalam wa IT, Luciana Lawi(33) wote wakazi wa ubungo Msewe, Katibu Muhasi wa NEMC (Sekretari), Edna Lutanjuka (51) Mkazi wa Mbezi Beach St Gasper, Msaidizi wa ofisa Mwaruka Mwaruka (42) naOfisa mazingira Nemc, Lilian Laizer (27) wote Wa kazi wa Ukonga Mombasa na Ofisa mazingira wa Nemc, Magori Wambura (38) mkazi wa Bombambili. 

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka sita ikiwamo la kula njama, mawili ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kusababisha hasara ya Sh.Milioni 160

Kwa pamoja washtakiwa hao wanadaiwa kati ya Septemba 27, 2016 na April Mosi,2018 jijini Dar es Salaam walikula njama ya kutenda kosa la kughushi.

Katika shtaka la pili washtakiwa hao wanadaiwa kuwa Oktoba 17,2017 Dar es Salaam kwa udanganyifu walighushi cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3366 wakijaribu kuonesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati wakijua si kweli.

Washtakiwa hao, katika shtaka la tatu wanadaiwa kuwa Oktoba,2017 Dar es Salaam kwa nia ovu walighushi saini ya Januari Makamba ambaye ni Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira katika cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira chenye usajili namba EC/ EIA/3366 wakijaribu kuonesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati wakati wakijua si kweli.

Katika shtaka la nne, mshtakiwa Edna anadaiwa kuwa Oktoba 2017 katika ofisi za NEMC Makao Makuu Dar es Salaam kwa kujua alitoa cheti cha kughushi cha tathmini ya uharibifu wa mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3366 cha oktoba 17,2017 kwa Deogratius Chacha, akijaribu kuonyesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati akijua si kweli.

Katika shtaka la tano, washtakiwa hao wote wanadaiwa kuwa kati ya Septemba 27 na Aprili 6 ,2018 walijipatia kwa njia ya udanganyifu Sh. Milioni 160 toka kwa PMM Estate (2001) Ltd kwa madai kuwa wangeweza kufanya tathimini ya uharibifu wa mazingira na kumpatia cheti ambacho kinatolewa na NEMC kitendo ambacho si kweli.

Katika shtaka la sita washtakiwa hao wanadaiwa kuwa kati ya Septemba27, 2016 na Aprili 6,2018 Dar es Salaam waliisababishia NEMC hasara ya Sh.Milioni 160.

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA SOKO LA KALANGALALA

0
0
*Azitaka halmashauri zingine nchini ziige mfano wa Mji wa Geita
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaameweka jiwe la msingi mradi ujenzi wa soko kuu la  Kalangalala katika Mji wa Geita na kuzitaka halmashauri zingine nchini kuiga. Pia, amesema wajasiriamali waliokuwa wakifanya shughuli zao katika eneo hilo kabla ya  ujenzi watakuwa wa kwanza kupewa maeneo ya kufanyia biashara. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 28, 2018) baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa soko la Mji wa Geita.

Amesema ni vema halmashauri zote zikaiga mfano wa Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kujenga masoko ya kisasa ili wajasiriamali wapate maeneo ya kufanyia kazi zao. “Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwaondolea wananchi kwa kuboresha na kuimarisha huduma za jamii.” Hivyo, Waziri Mkuu amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel kwa kuwa mbunifu na msimamiaji mzuri wa miradi ya maendeleo. Waziri Mkuu amesema Serikali inahitaji viongozi wa aina yake, ambao si wabadhilifu bali wanajali thamani na maslahi ya wananchi katika maeneo yao ya kazi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi  Gabriel ameahidi kulinda heshima ya wananchi wa mkoa huo kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Amesema atasimamia kikamilifu ujenzi wa miradi ya maendeleo, ukiwemo ujenzi wa soko la kisasa ambalo litakapokamilika wajasiriamali watafanyakazi muda wote hadi usiku. Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mji wa Geita, Adolf Ritte amesema ujenzi wa mradi huo umegawanyika katika awamu mbili, ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa soko lenye majengo makubwa mawili yenye thamani ya sh. bilioni 1.9. 

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na wananchi watakaokuwa wanakwenda kununua bidhaa mbalimbali kwenye soko hilo. “Pia Halmashauri ya Mji nayo itanufaika kwa kuongezeka kwa mapato yake ya ndani. Ajira zitakazozalishwa sokoni hapo ni takribani 200. Faida nyingine ya mradi huu ni kumaliza mgogoro wa maeneo ya kufanyia biashara katika mji wetu.” Mapema leo Waziri Mkuu alikagua mradi wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Mji Geita kwenye eneo la Magogo na kisha alikwenda katika eneo la Bombambili kwa ajili ya kukagua na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa ofisi za CCM mkoa wa Geita.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la Msingi la Kiwanda cha Kuchenjua Dhahabu cha Nyamigogo wilayani Nyang'hwale Novemba 28, 2018. Wapili kulia ni mmiliki wa kiwanda hicho, Hussein Nassoro Amali ambaye pia ni Mbunge wa Nyang'hwale. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constatine Kanyasu, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mwita Waitara na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel. Watatu kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj Saidi Kalidushi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea kiwanda cha Kuchenjua Dhahabu cha Nyamigogo wilayani Nyang'hwale Novemba 28, 2018. Kushoto kwake ni mmiliki wa kiwanda hicho, Hussein Nassoro Amali ambaye pia ni Mbunge wa Nyang'hwale.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama eneo maalum la kuhifadhi na kusafisha Maji machafu wakati alipozindua Kiwanda cha Kuchenjua Dhahabu cha Nyamigogo wilayani Nyang'hwale Novemba 28, 2018. Wapili kushoto ni mmiliki wa kiwanda hicho, Hussein Nassoro Amali ambaye pia ni Mbunge wa Nyang'hwale. Kushoto ni Mke wa Mbunge huyo, Ashura Muhoja.

WAZIRI KAIRUKI ATAKA KAGUZI ZA MARA KWA MARA MIGODIN

0
0

Waziri wa Madini Angellah Kairuki akiangalia ramani ya jengo la Kituo cha Umahiri Chunya litakavyokuwa mara baada ya kukamilika kwake. Jengo hilo linajengwa na Mkandarasi SUMAJKT.
Waziri wa Madini Angellah Kairuki akisikiliza jambo kutoka kwa Mkandarasi SUMAJKT alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Umahiri Chunya. Wengine ni Wataalam kutoka Ofisi za Madini Mbeya na Chunya, wataalam kutoka Wizara ya Madini, na uongozi wa Wilaya ya Chunya.
Sehemu ya jengo la Kituo cha Umahiri Chunya likiwa katika maendeleo ya ujenzi wake.
Sehemu ya viongozi wa Wilaya, viongozi wa Ofisi za Madini Mbeya na Chunya pamoja na wadau wa madini wilayani humo wakimsikiliza Waziri wa Madini Angellah Kairuki (hayupo pichani).

…………………………………………………………………….

Na Asteria Muhozya, Chunya

Waziri wa Madini Angellah Kairuki amewataka Maafisa Madini nchini kuhakikisha wanafanya kaguzi za mara kwa mara katika maeneo ya wachimbji wadogo ikiwemo kutoa elimu ya uchimbaji, masuala ya afya na usalama kazini ili kuongeza tija katika shughuli hizo.

Waziri Kairuki aliyasema hayo Novemba 27, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Umahiri Chunya kinachojengwa na Mkandarasi kampuni ya SUMAJKT.

Alisema, wachimbaji wadogo wanatakiwa kulelelewa ili watoke katika uchimbaji mdogo wa madini kwenda uchimbaji wa Kati na hatimaye kuwa wachimbaji wakubwa, na kueleza kuwa, ili kufikia azma hiyo elimu ya mara kwa mara kwa wachimbaji ni muhimu ikatolewa kwani itawezesha serikali kupata mapato kutokana na kufuata uchimbaji sahihi.

Pia, aliwataka Maafisa hao kuhakikisha kuwa wanatatua migogoro katika maeneo yao kwani suala hilo litawezesha uzalishaji zaidi na kupelekea serikali kunufaika na shughuli hizo, ikiwemo ongezeko la ajira na ustawi wa jamii.

Vilevile, Waziri Kairuki alieleza kuwa, pamoja na kwamba katika Mwaka wa Fedha 2018/19 wizara yake imepangiwa kukusanya shilingi bilioni 310, lakini kama anataka makusanyo hayo yafikie shilingi bilioni 500 na kuongeza kwamba, Maafisa madini watapimwa kutokana na ukusanyo huo wa maduhuli.

“ Sisi tumepangiwa kukusanya shilingi bilioni 310. Lakini na mimi nataka makusanyo hayo yafikie shilingi bilioni 500 na nitawapima maafisa madini kwa ukusanyaji wa maduhuli,” alisema Waziri Kairuki.

Katika hatua nyingine, amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha kwamba zinashaurina na Wizara ya madini katika masuala yote yanayohusu kodi za madini kabla ya kuyatolea maamuzi kwa kuwa, isipofanyika hivyo inachangia taasisi za serikali kukinzana katika utoaji wa maamuzi.

Alisema, wizara inaandaa utaratibu wa kukutana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kulijadili suala la kodi katika sekta ya madini.

Akizungumzia umuhimu wa Kituo cha Umahiri, alisema kuwa, kitawezesha wachimbaji kujua taratibu zinazotakiwa katika utekelezaji wa majukumu yao katika sekta ya madini na kwamba, wizara inaangalia uwekezano wa kuwa na vituo hivyo katika kila mikoa ikiwemo ofisi za kisasa na vituo vya mafunzo ili kuwezesha kuwepo na tija zaidi katika sekta ya madini.

“ Tumeanza na vituo vya mahiri lakini upo umuhimu wa maafisa wetu kuwa na nyumba za kuishi lakini pia kuhakikisha kwamba maafisa wetu hawakai katika eneo moja kwa kipindi kirefu,” alisema.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi Wilaya ya Chunya Athumani Kwariko alimweleza Waziri Kairuki kuwa, leseni nyingi wilayani humo hazifanyiwi kazi kutokana na wamiliki wake kukosa mitaji na uwepo wa migogoro. Hata hivyo amesema kuwa, tayari ofisi hiyo imewasiliana na wamiliki hao ili kuhakikisha kwamba wanaziendeleza leseni hizo.

Akizungumzia madini yanayopatikana wilayani humo hiyo aliyataja kuwa ni pamoja na ya dhdhabu, chuma, bati, ulanga, chokaa na kokoto na mchanga.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Cha Wachimbaji Mkoa wa Mbeya Leonard Manyesha akielezea umuhimu wa kituo hicho alisema kwamba kitawawezesha kupata maelekezo ya kitaalam kuhusu uchimbaji na hivyo kuwawezesha kupata mazao bora ya dhahabu na yenye tija.

Aidha, alipongeza kwa hatua ya serkali ya kutaka kuhamasisha Mikoa kutenga maeneo kwa ajili ya uanzishaji wa masoko ya madini na kueleza kuwa, uwepo wa masoko hayo utasaidia tatizo la wachimbaji kuficha mapato kuisha.

Palozi wa Palestina Atembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)

0
0
 Mkuu wa huduma za Sheria na Katibu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Maulid Kikondo akimwelezea Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli maendeleo ya ukarabati wa wodi ya watoto wenye magonjwa ya moyo alipofanya ziara katika taasisi hiyo na kutembelea ukarabati wa wodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam
  Baba wa mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa moyo wa kufungua kifua Hamis Daud akimwelezea Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli maendeleo ya mtoto wake baada ya kufanyiwa upasuaji huo alipofanya ziara katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kutembelea wagonjwa wodini leo Jijini Dar es Salaam
 Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Bashir Nyangasa akielezea namna wagonjwa wa moyo wanavyofanyiwa upasuaji wa kufungua kifua na kupatiwa matibabu ya karibu katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) kwa balozi wa Palestina nchini  Mhe. Hamdi Mansour AbuAli alipotembelea chumba cha ICU wakati wa ziara yake katika taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam 
 Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli akizungumza na menejimenti ya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ambavyo Palestina itashirikiana na taasisi hiyo katika masuala mbalimbali ya afya ya moyo baada ya kufanya ziara kuangalia huduma zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiagana na Balozi wa Palestina nchini Mhe. Hamdi Mansour AbuAli baada ya kufanya ziara kuangalia huduma zinazotolewa na taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Pcha na: Genofeva Matemu - JKCI

MTANZANIA GERALD BIGURUBE ATUNUKIWA TUZO UJERUMANI

0
0
Siku ya Jumanne, tarehe 24 Septemba 2018, Mtanzania Gerald Bigurube alitunukiwa tuzo ya mwaka 2018 ya Ujerumani na Afrika (2018 German Africa Award). Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwake na Dr. Wolfgang Schäuble, Rais wa Bunge la Ujerumani Bundestag. Mwaka huu tuzo hiyo ilitolewa kwa watu wawili, mwingine akiwa ni Bw.

Bw. Gerald Bigurube ametumia kipindi cha miaka arobaini na nne katika Maisha yake kutunza wanyama pori na mazingira. Alipokuwa kiongozi wa TANAPA, Bw. Bigurube (miaka 66), alipambana dhidi ya ujangili, na alifanya juhudi za kuleta uwiano sawa baina ya utunzaji misitu na Wanyama pori kwa upande mmoja, na maisha ya wanadamu na maendeleo ya kiuchumi kw aupande mwingine. Bw. Bigurube ametoa mchango mkubwa kuonyesha jinsi utunzaji wa mazingira na maendeleo ya kiuchumi vinavyotegemeana.

Kwa sasa, Bw. Bigurube anafanya kazi kama mkurugenzi mkaazi wa Frankfurt Zoolocal Society, taasisi ya kimataifa inayojihusisha na utunzaji wa mazingira, yenye makao yake mjini Frankfurt Ujerumani. Taasisi hiyo inafanya kazi kwa karibu na mamlaka za hifadhi nchini Tanzania, hususan katika kupambana na ujangili.

Ushirikiano wa mamlaka za Serikali ya Tanzania na Frankfurt Zoolocal Society umeiwezesha Tanzania kupata mafanikia katika utunzaji wa mazingira na kukabiliana na ujangili. Mpaka sasa, Tanzania imeweza kutenga maeneo takriban asilimia 32 ya ardhi yote kama hifadhi za taifa, na kuifanya kuwa ndiyo nchi yenye eneo kubwa zaidi la hifadhi barani Afrika.

Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Dkt. Abdallah Possi, amempongeza Bw. Bigurube kwa moyo wa uzalendo aliokua nao. Dkt. Possi pia amewahimiza wadau wa mazingira kuzidi kufanya kazi kwa karibu na Tanzania, haswa ukizingatia kwamba kazi ya Utunzaji wa mazingira inayofanywa na Tanzania pia ina manufaa kwa ulimwengu mzima.

Dkt. Possi alifafanua, juhudi za kutunza mazingira Tanzania zitafanikiwa zaidi iwapo kutakuwa kuna ushirikiano utakaoiwezesha Tanzania kupata teknolojia bora itakayorahisisha matumizi bora ya ardhi katika shughuli za binadamu, na kwa maana hiyo, nchi zilizoendelea na Taasisi mbalimbali za kimataifa zinapaswa kuzingatia kwamba masuala kama vile kilimo cha kisasa na upatikanaji wa uhakika wa nishati ni muhimu katika utunzaji wa mazingira.

ZAIDI YA SH. BILIONI TATU ZAPOTEA WILAYANI NYANGW’ALE

0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa hadhara kwenye kiwanja cha Sabasaba kilichopo Karumwa wilayani Nyang'hwale, Novemba 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wakati alipowasili kwenye Kiwanja cha Sabasaba  kilichopo Karumwa wilayani Nyang'hwale kuhutubia mkutano wa hadhara, Novemba 28, 2018.  
 Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia Mkutano wa hadhara katika kiwanja cha Sabasaba  kilichopo Karumwa, Novemba 28, 2018.

*Waziri Mkuu aagiza kuchukuliwa hatua kwa watumishi wote waliohusika
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyangw’ale waliohusika na ubadhilifu wa zaidi ya sh. bilioni tatu fedha ambazo zilitolewa na Serikali kugharamia miradi ya maendeleo wachukuliwe hatua.

Pia ameagiza kukamatwa na kuchukuliwa hatua kwa Mkaguzi wa Ndani wa halmashauri hiyo, Gavana Matesa kwa sababu ameshindwa kutoa kwa mamlaka husika kuhusu taarifa za wizi wa fedha za maendeleo zilizotafunwa.

Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Jumatano, Novemba 28, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Geita.
Miongoni mwa miradi ambayo fedha zake zimepotea ni pamoja na sh. bilioni 1.2 za ujenzi ofisi ya halmashauri hiyo, sh. milioni 400 za ukarabati wa kituo cha afya Nyangw’ale, sh. milioni 611.230 za miradi ya maji.

Nyingine ni sh. milioni 536.119 za mpango wa malipo kulingana na huduma (EP4R), sh. milioni 125.914 za ushuru wa huduma, sh. milioni 31 za ujenzi wa ofisi ya mbunge na sh. milioni 109 za mfuko wa barabara.

“Wilaya ya Nyangw’ale ni mpya na Serikali imekuwa ikileta fedha nyingi lakini fedha zote zimetafunwa, Serikali ipo makini sana na moja kati ya vita kubwa ni dhidi ya mafisadi, wala rushwa ambayo ni endelevu hivyo tutashughulika na kila mmoja.

Tayari watu saba akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale, Carlos Gwamagobe na wenzake wamekamatwa. Wizi unatisha Nyangw’ale wilaya inatia aibu tutawaondoa watu wote waliohusika na tutaendelea kuwakamata.”

Hata hivyo Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa wilaya hiyo kwamba Serikali itahakikisha miradi yote iliyoahidiwa kujengwa kwenye wilaya hiyo ikiwemo ya maji itatekelezwa kama ilivyopangwa, waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

Kuhusua suala la watumishi, amesema wilaya hiyo lazima iwe na watumishi wasafi wenye weledi wa kufanya kazi na lazima wahakikishe fedha za miradi zinazotolewa katika halmashauri hiyo zinalingana na thamani halisi ya mradi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema atahakikisha watumishi wote wa umma waliohusika na wizi huo wanachukuliwa hatua stahili na kwamba tayari baadhi yao wameshafikishwa kwenye vyombo vya dola. 

Amesema halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale inaongoza kwa matumizi mabaya ya fedha za maendeleo kwa kuwa awali lilikuwa chaka kubwa la wizi, ambapo amesema ni bora watumishi wote wasiokuwa waadifu waondolewe na waletwe wengine.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Gabriel amesema tayari baadhi ya watumishi wanaotuhumiwa kuhusika katika ubadhilifu wa fedha za miradi mbalimbali wameshakabidhiwa kwa vyombo vya dola huku watumishi wengine wakiendelea kuchunguzwa.”Watumishi wote waliohusika na wizi huu watapata tabu sana”

MWENYEKITI MPYA BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'.

0
0

Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Dkt Sinare Yusuph Sinare akimkabidhi rasmi Uenyekiti wa Baraza hilo Bi Jacqueline Mkindi baada ya kuteuliwa na Bodi na kuthibitishwa na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania, Dkt Sinare amemaliza muda wake baada ya kushika nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka 5.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania baada kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti Mh Jitu Son na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania Bi Janeth Bitegeko, Mkutano huo umefanyika Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akimkabidhi tuzo ya heshima ya utendaji uliotukuka katika Sekta ya Kilimo, Mwenyeki wa Bodi ya Baraza la Kilimo aliyemaliza muda wake Dkt Sinare Yusuph Sinare , kati kati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Bi Janeth Bitegeko, tukio hilo limefanyika Dar es Salaam wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akimakabidhi tuzo ya heshima ya utendaji uliotukuka katika Sekta ya Kilimo, Mwenyeki wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya baraza la kilimo Bw Salum Shamte, tukio hilo limefanyika Dar es Salaam wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania

Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Mh Jitu son ambaye kwa sasa ni Makamo Mwenyekiti wa Baraza la Kilimo Tanzania, na Bw Julias Nyabicha wakifuatilia kwa makini kitabu cha mahesabu wakati wa Mkutano Mkuu wa wajumbe wa Baraza la Kilimo Tanzania uliofanyika Dar es Salaam, wengine kwenye picha ni sehemu ya wajumbe wa Mkutano huo.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi, kulia ni makamo wake Mh Jitu Son, kushoto ni mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Sinare Yusuph Sinare wakiwa kwenye picha na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania muda mfupi baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo uliofanyika Dar es Salaam.
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live




Latest Images