Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46200 articles
Browse latest View live

NEWS ALERT: MBUNGE ZITTO KABWE APANDISHWA KIZIMBANI LEO,AACHIWA KWA DHAMANA

0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

MBUNGE wa Kigoma mjini Zitto Kabwe, leo Novemba 2, 2018 amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi.

Mashtakia Zitto amesomewa mashtaka yake na wakili wa serikali Mwandamizi, Tumain Kweka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shahidi.

Wakili Kweka amedai Oktoba 28, 2018 akiwa katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya ofisi ya chama cha ACT Wazalendo mshtakiwa Zitto akiwa katika  mkutano huo kwa nia ya kuleta chuki kwa wananchi wa Tanzania dhidi ya Jeshi la polisi alitoa Maneno ya uchochezi yenye kuleta hisia ya hofu na chuki.

Katika shtaka la pili, Kweka alidai kuwa siku na mahali hapo, Zitto Kijitonyama alitoa Maneno ya uchochezi ambayo y yalikuwa na lengo lenye  kuleta hofu.Aidha Zitto anadaiwa Kutoa walaka kwa umma ukiwa na Maneno ya kichochezi kwa nia ya kuleta chuki kwa watanzania dhidi ya polisi.Hata hivyo, mshtakiwa amekana mashtaka hayo amachiwa huru kwa dhamana na upande wa mashtaka umedai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hata hivyo Wakili Kweka amewasilisha hati ya kiapo iliyoapwa na mkuu wa Upelelezi wa Kipolisi Mkoa wa Kinondoni SSP John Malulu ya kupinga dhamana dhidi ya Zitto.Katika hati hiyo ya kiapo wanaiomba mahamakama isitoe dhamana kwa mshtakiwa kwa sababu za kiusalama,  na kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika, Amedai iwapo mshtakiwa huyo ataachiwa kwa dhamana ataweza kuingilia upelelezi.

Wakili Peter Kibatala anayemtetea Zitto ameiomba mahakama impatie dhamana mteja wak na kwamba hati ya kiapo iliyowasilishwa na upande wa mashtaka mahakamani hapo inamapungufu ya kisheria ikiwamo kuwa hati ya kiapo haitakiwi kutajwa vifungu  vya sheria.Kibatala alieleza kuwa hata kama kuna  hati ya kiapo mahakamani, hakuna sababu za msingi zilizotolewa kuishawishi mahakama kumnyima dhamana Kabwe.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Shahidi amesema katika hati ya kiapo iliyowasilishwa na upande wa mashtaka ni lazima iwepo na sababu za kutosha na za msingi kupinga dhamana.Amesema ni jukumu la polisi kulinda raia na Mali zao kwa hilo nashangaa polisi kuhofia usalama wa Zitto wakati ni jukumu lao kuhakikisha kila RAIA kuwa salama."Ni kweli hati ya kiapo imebeba vifungu vya sheria wakati siyo matakwa ya sheria kwa namna hiyo sowezi kumnyima dhamana.

Hivyo Hakimu Shahidi amemtaka Zitto kuwa na mdhamini mmoja Mwenyekiti kitambulisho atakayesaini bondi ya Sh 10 milioni.

Zitto amefanikiwa kutimiza masharti ya dhamana na kuachiwa huru na kesi imeahirishwa hadi Novemba 26, mwaka huu.
 Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe akifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kushikiliwa katika kituo cha Polisi kwa siku kadhaa. Mh. Zitto ameachiwa kwa dhamana ya mdhamini mmoja na bondi ya sh. Milioni kumi
 Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, akiwa katika ukumbi wa wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri kusomewa mashtaka yake yanayomkabili. Zitto anakabiliwa na mashtaka matatu ya uchochezi.
Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, akiteta jambo na wakili wake Steven Mwakibolwa, kabla ya kwanza kusomewa kwa kesi hiyo katika ukumbi wa wazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Watendaji Wakuu na Wenyeviti wa Bodi Waaswa Kuzingatia Sheria Kanuni na Taratibu

0
0








Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania Bw. Edwin Rutageruka akizungumza wakati wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka (katikati)akiwa kwenye picha ya pamoja na sehemu ya watendaji wakuu wa mashirika ya umma walioshiriki katika semina kwa Watendaji hao, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) Dkt. Respicius Boniface (kulia) akifuatilia hotuba ya Msajili wa Hazina Bw. Athumani Mbuttuka wakati wa ufunguzi wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya MOI Prof. Charles Anael Mkonyi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Prof. Humphrey Moshi akizungumza wakati wa wa semina kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na wajumbe wa Bodi kuhusu usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Sehemu ya Watendaji wakuu na Wenyeviti na wajumbe wa Bodi wakifuatilia semina ya usimamizi wa Taasisi na mashirika ya Umma ili kuyawezesha kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake, Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina. Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO



Na: Frank Mvungi- MAELEZO

Msajili wa Hazina Bw. Athumani Selemani Mbuttuka amewata Watendaji wakuu , Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi za Taasisi na mashirika ya umma kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na miongozo inayotolewa na Serikali .

Akizungumza katika Semina ya kuwajengea uwezo Viongozi hao, Bw. Athumani amesem,a kuwa lengo la Serikali ni kuona dhamira ya kuazishwa kwa Taasisi na Mashirika ya Umma inafikiwa kwa wakati.

“Kwa mujibu wa vifungu Na.10 (2) (e) na 10 (5) vya Sheria ya Msajili wa Hazina ina mamlaka ya Kusimamia Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma hivyo, tuna wajibu wa kuhakikisha kuwa Bodi na Viongozi wote wanaelewa majukumu yao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu”; Alisisitiza Mbutuka.

Akifafanua amesema kuwa Bodi na Watendaji wakuu wanapaswa kuwa makini, wabunifu na kufanya maamuzi sahihi na kwa wakati ili kuhakikisha kuwa Taasisi zinajiwekea mikakati ya kupunguza gharama za uendeshaji zinazotokana na matumizi yasiyo ya lazima hususani safari za Bodi na viongozi zisizokuwa na manufaa kwa Taasisi husika.

Alibainisha kuwa Taasisi zinapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kukusanya mapato ili kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, sambamba na kuhakikisha kuwa matumizi yote yanafanyika kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali ya Serikali.

“Taasisi zenye utendaji usioridhisha na zile zinazopata hasara kila mwaka, kuweni wabunifu na kuweka mikakati ya kuboresha utendaji na pia kuhakikisha kuwa, hoja za ukaguzi ( CAG,IAG, TR na PPRA) na maagizo ya kamati za Bunge yawekewa mkakati thabiti na zinatekelezwa ipasavyo na kwa wakati;” Amebainisha Mbutta.

Akizungumzia Taasisi zinazopaswa kuchangia asilimia 15 ya mapato ghafi katika mfuko mkuu wa Serikali zinatekeleza wajibu huo kwa mujibu wa sheria kila robo mwaka,Bodi inatakiwa kuhakkisha kuwa, mchango unaowasilishwa ni sahihi na unaendana na kiwango cha mapato ghafi ya Taasisi husika au shirika.

Alisema kuwa upande wa matumizi hasa katika malipo ya posho, marupurupu, na maslahi mbalimbali ya Bodi, Viongozi wa Taasisi na Watumishi yanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya Serikali.

Aliongeza kuwa malipo ya posho za nyumba, posho za simu na umeme yanapaswa kulipwa kwa watumishi wenye stahili hizo kisheria tofauti na ilivyo sasa ambapo baadhi ya Taasisi zinaendakinyume na utaraibu huo.

Pia aliwata Watendaji wakuu na Bodi kutofanya malipo kwa kutumia nyaraka ambazo hazijaidhinishwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina.

Ofisi ya Msajili wa Hazina inafanya kazi kwa ushirikiano ili kujenga Taasisi zinazoendana na Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ambazo ni madhubuti, Bora na endelevu kwa maslahi ya wananchi wote na Taifa kwa ujumla.

Ofisi ya Msajili wa Hazina imeratibu mafunzo hayo kwa Watendaji Wakuu, Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi za Taasisi na Mashirika ya Umma 17 kwa lengo la kuwajengea uwezo katika utendaji wao wa kusimamia taasisi hizo ili kuongeza ufanisi.

WAGONJWA 23 WAPATIWA HUDUMA YA TIBA YA RADIOLOJIA MUHIMBILI

0
0
Mkuu wa Idara ya Radiolojia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Flora Lwakatare akizungumza na waandishi wa habari juu ya wataalam kuzibua njia ya nyongo ya mgonjwa kupitia huduma ya kibingwa ya tiba radiolojia kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) na Chuo Kikuu cha Yale na Emory nchini Marekani. Kutoka Kushoto ni daktari bingwa wa upasuaji wa Muhimbili, Dkt Godfrey Mchele na mtaalam wa tiba ya radiolojia, Profesa Frank Minja kutoka Chuo Kikuu cha Yale nchini Marekani.
Baadhi ya wataalam wa tiba hiyo pamoja na waandishi wa habari wakimsikiliza Dkt. Flora Lwakatare.
Wataalam wa radiolojia wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) pamoja na wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Yale na Emory nchini Marekani wakishirikiana kuzibua njia ya nyongo ya mgonjwa kupitia huduma ya kibingwa ya tiba radiolojia.
Mtaalam wa tiba radiolojia, Profesa Frank Minja kutoka Chuo Kikuu cha Yale nchini Marekani akizungumza na waandishi wa habari kuhusu jinsi wataalam wa Muhimbili, MUHAS na MOI walivyofanya maandalizi ya kufanikisha huduma ya tiba radiolojia. Kushoto ni Dkt. Lwakatare na kulia ni mtaalam wa huduma za radiolojia kutoka Chuo Kikuu cha Emory nchini Marekani.
Baadhi ya wataalam wa huduma za tiba radiolojia wakifuatilia mkutano huo leo. 
Dkt Lwakatare akifafanua jambo kwenye mkutano huo leo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Muhimbili, Dkt. Praxeda Ogweo, Dkt. Mchele wa Muhimbili, Prof. Minja kutoka Chuo Kikuu cha Yale, Dkt. Prologo kutoka Chuo Kikuu cha Emory na Dkt. Mechiris Mango wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI).



Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS), Taasisi ya Tiba Mifupa (MOI), Chuo Kikuu cha Yale na Emory nchini Marekani wameendesha kambi maalum ya kutoa huduma za kibingwa kupitia tiba Radiolojia ambapo wagonjwa 23 wamenufaika na tiba hiyo.

Tiba hiyo inahusisha utaalam wa kutumia vifaa vya Radiolojia kama X-Ray, MRI, CT-Scan na Ultra- Sound kutibu moja kwa moja ugonjwa au kuchukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Radiolojia MNH, Dkt. Flora Lwakatare amesema huduma hiyo ya kibingwa ilianza kwa mara ya kwanza nchini Novemba mwaka jana ambapo kabla ya uanzishwaji wake wagonjwa waliokuwa wanahitaji huduma hizi walikuwa wakienda nje ya nchi.

Akielezea kuhusu huduma zilizitolewa katika kambi hiyo amesema ni utoaji wa sampuli kutoka kwenye vivimbe katika sehemu mbalimbali za mwili ambazo si rahisi kufikiwa bila upasuaji mkubwa, kuzibua mirija ya nyongo, kuweka mirija kwenye figo ambazo mirija ya mkojo imeziba na unyonyaji wa vivimbe vyenye maji au usaha.‘‘Kambi hii imehusisha wakufunzi ambao ni madaktari bingwa, mafundi sanifu Radiolojia, wauguzi Radiolojia kutoka vyuo vikuu vya Yale na Emory. Pia, watalaam kutoka Hospitali ya Benjamini Mkapa na CCBRT nao wananufaika na mafunzo hayo.’’

Akielezea faida ya tiba hiyo amesema inamuwezesha mgonjwa kuepuka upasuaji mkubwa ambao ni hatarishi, kuepuka ukaaji wa muda mrefu hospitalini na kupunguza gharama.Tangu kunzishwa kwa tiba Radiolojia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wagonjwa takribani 100 wamenufaika na huduma hiyo.Naye Dkt. Mchele amesema kuwa ujio wa wataalam hao kutoka Chuo Kikuu cha Yale na Emory umekua msaada mkubwa kwa wataalam wa Muhimbili, MUHAS na MOI kwa kuwa wamejifunza mambo mengi ya kitaalam.

“Tumejifunza mambo mengi ambayo yatatuwezesha kuendelea sisi wenyewe baada ya timu hii kurejea Marekani. Hii imetusaidia sana kwani kuna baadhi ya wagonjwa wana usaa kwenye ini, hivyo wametuwezesha kugundua tatizo mapema na kuweza kufanya upasuaji kwa mgonjwa bila kuacha jeraha kubwa,” amesema Dkt. Mchele.

Amesema kuanza kwa huduma ya tiba radiolojia ni hatua nzuri na muhimu kwani mwaka 2022, Muhimbili inatarajia kuanza kupandikiza ini na kwamba tiba radiolojia ni moja ya maandalizi ya kuelekea kupandikiza ini.

RC MAKONDA AKABIDHI MABASI 4 KWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA, NI YALE YALIYOKUWA "UKWECHE".

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo amekabidhi Mabasi 4 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ na Jeshi la Magereza kwaajili ya kuongezea ufanisi katika utendaji wa Kazi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Mabasi 4 aliyoyakabidhi RC Makonda Leo ni Kati ya Mabasi 11 yaliyokuwa yamekufa (ukweche) ambapo baada ya RC Makonda kuyaona na kubaini uhaba wa magari kwa vyombo vya ulinzi na usalama aliwatafuta wafadhili wa Kampuni ya Dar Coach Ltd waliojitolea kuyarejeshea uhai magari hayo na hatimae leo yanatembea Barabarani yakiwa mazima.

RC Makonda amesema ukarabati wa mabasi hayo ulihusisha Kubadilisha Bodi, kupaka Rangi, kubadili Viti, kuweka Mfumo wa kuchaji simu, AC, TV, Taa,Madirisha, Matairi pamoja na kuongeza na kupunguza idadi ya viti.

Aidha RC Makonda amesema mkakati wa kuendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa vyombo vya ulinzi na usalama utaendelea ikiwa ni pamoja na kugusa maisha ya mtumishi mmojammoja kwa kuwapatia mikopo ya viwanja vya bei nafuu.

Hata hivyo RC Makonda ameshukuru Kampuni ya Dar Coach Tanzania Ltd kwa uzalendo walioonyeaha kukarabati magari hayo pasipo kutumia pesa ya serikali.

Kwa upande wake Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Luteni Jenerali Yacoub Mohamed amempongeza RC Makonda kwa ubunifu wa kufufua magari yaliyokuwa yamekufa ambapo ameeleza kuwa yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaongezea ufanisi katika kazi kwa kupunguza changamoto ya usafiri.

Mabasi 4 yaliyokabidhiwa leo ni Ashok Leyland 01, Iveco 2 na Toyota Coaster moja huku magari mengine 7 yakiwa hatua ya mwisho kukamilika.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akisalimiana na baadhi ya Maofisa wa jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),wakati alipokwenda leo kukabidhi Mabasi 4 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ na Jeshi la Magereza kwa ajili ya kuongezea ufanisi katika utendaji wa Kazi wa vyombo vya ulinzi na usalama.
 Baadhi ya magari yaliyokabidhi wa kwa JWTZ na Jeshi la Magereza
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiagana na mmoja wa Maoisa wa JWTZ,mara baada ya kukabidhi Mabasi 4 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ na Jeshi la Magereza kwaajili ya kuongezea ufanisi katika utendaji wa Kazi wa vyombo vya ulinzi na usalama.
 Picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano hayo
 

MPINA ATEKETEZA ZANA HARAMU ZA UVUVI KIGOMA

0
0

Na Editha Karlo wa blog ya jamii,Kigoma

KUFUATIA operesheni ya kutokomeza uvuvi haramu ndani ya Ziwa Tanganyika inayoendelea Waziri wa mifugo na uvuvi Luhaga Mpina ameteketeza zana mbalimbali za uvuvi haramu zenye zaidi ya shilingi bilioni tatu zilizokuwa zikitumika katika ziwa Tanganyika.

Akiongea na wananchi baada ya zoezi la kuteketeza zana hizo haramuza uvuvi katika eneo la Businde nje kidogo ya Manispaa ya Kigoma Ujiji Mpina amewataka wananchi kushirikiana na serekali kwa kuwafichua wahalifu wanaotumia zana haramu ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kupigwa faini na kwenda jela.

Alisema serekali haitomuonea mtu yoyote huruma ambayeatakamatwa anafanya uvuvi haramu au kuwa na zana za uvuvi haramu awe kiongozi au raia wa kawaida sheria lazima ichukue mkondo wake.''Sisi lengo letu ni kuona samaki wanaongezeka katika ziwa Tanganyika,na watu wavue kwa kufuata sheria ili Taiafa lipate mapato na watu wapate ajira"alisema

Alisema oparesheni inayofanyika katika ziwa Tanganyika ni oparesheni ya Kitaifa ya kupambana na uvuvi haramu ambayo itaendelea katika maeneo yote ya ziwa Tanganyika lengo likiwa ni kuondoa uvuvi haramu na mitandao ya wafanyabiashara wa zana haramu za kuvulia samaki wachanga na utoroshwaji wa samaki na mazao yake kwenda nje ya nchi kinyume cha sheria.

Alisema takwimu zinaonyesha utoroshwaji wa samaki na dagaa kwenda nje katika ZIwa Tanganyika ilikuwa ni mkubwa kwenda nje ya nchi bila kulipa chochote na wageni nao kutoka nchi za jirani wanakuja kwenye maji yetu wanavua na kuondoka.

''Kwa muda mfupi wa siku 15 ambao oparesheni hii imefanyika toka ianze tayari nyavu haramu 3250 thenye thamani ya bilioni tatu haramu zimekamatwa na tumeziteketeza leo hapo ni mitaji imetekea'alisema

Alisema pamoja na nyavu hizo haramu pia wamekamata mitumbwi 93,magari 32,pikipiki 16 na samaki tani kilo elf tano vyote vimekamatwa katika maeneo mbalimbali.Aliongeza kwa kusema kuwa oparesheni hiyo ameizindua ila itaendelea mpaka pale biashara ya uvuvi haramu itakapo koma na kubakia historia.

Kiongozi wa oparesheni hiyo kwa kanda ya Kigoma Nchama Marwa alisema kuwa katika oparesheni hiyo ambayo mpaka sasa ina siku 15 toka ianze kuna baadhi ya wananchi wasiowaaminifu wamekuwa wakiwapa hifadhi raia wa kigeni wanaofanya shughuli za uvuvi huku wakiwa hawana vibali na kuisababishia serekali hasara ikiwemo kukosa mapato.

Marwa alisema changamoto nyingine ni baadhi ya wanasiasa kujaribu kuingilia zoezi hilo,kutokuwepo kwa ushirikiano kwa taasisi za serikali wakati wa kutekeleza oparesheni hadi maelekezo yatolewe toka ngazi za juu.Alisema oparesheni hiyo imeanza kutoa matokeo ambapo baadhi ya wavuvi wameanza kujisalimisha kwa kutii sheria na kukata leseni katika baadhi ya maeneo.

Aliiomba serekali itenge bajeti ya kutosha katika kuendesha oparesheni hiyo ili washiriki wa opareshini hiyo wawe wa kutosha.Naye Mkuu wa Wilaya ya Kigoma mjini Samson Hanga amewatahadharisha watendaji ambao wanashirikiana na wavuvi haramu yeyote ataksayebainika katika kitendo hicho serekali itamchukulia hatua .

''Mhe.Waziri nikuhakikishie tutaendelea kushirikiana na kuwakamata wale wote wanaofanya uvuvi haramu nia yetu ni kuwa na uvuvi endelevu,serekali tupo macho tutawakamata tutawapiga faini ikibidi tutawapeleka mahakamani na tutachoma zana haramu ambazo hazifai kutumika katika uvuvi''alisema
 Waziri wa Mifugo na Uvivu Luhaga Mpina akiteketeza nyavu 352 haramu za uvuvi katika eneo la Businde nje kidogo ya Manispaa ya Kigoma Ujiji zilizokamatwa kwenye oparesheni maalum ya kuzuia uvuvi haramu ndani ya ziwa Tanganyika.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akiongea na wavuvi pamoja na wafanyabiashara wa mazao ya dagaa na samaki katika mwalo wa Kibirizi kabla ya kuteketeza zana haramu za Uvuvi zilizopatikana kufuatia oparesheni ya kuzuia uvuvi haramu inayoendelea katika Ziwa Tanganyika

HALI ZA MAJERUHI WALIOPATA AJALI YA TRENI JIJINI DAR ES SALAAM

0
0

MAJALIWA ATEMBELEA VIWANDA JIJINI TANGA

0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu uzalishaji wa saruji  kutoka kwa Bw. Pradeep Punlana  (katikati) ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha saruji cha  Rhino kilichopo eneo la Maweni jijini Tanga  wakati alipotembelea kiwanda hicho  Novemba 1, 2018. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu uzalishaji wa saruji  kutoka kwa Bw. Pradeep Punlana  (katikati) ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha saruji cha  Rhino kilichopo eneo la Maweni jijini Tanga  wakati alipotembelea kiwanda hicho  Novemba 1, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama usindikaji wa maziwa wakati alipotembelea kwanda cha Maziwa cha Tanga Fresh cha jijini Tanga, Novemba 1, 2018.  Kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage, watatu kushoto ni Meneja Ufundi wa kiwanda hicho, Adam Gamba na wanne kukhoto ni Meneja Mkuu wa kiwanda, Michael Karata. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Soni wilayani  Lushoto akiwa katika ziara ya mkoa wa Tanga, Novemba 1, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE ASHIRIKI MKUTANO WA MAWAZIRI WA NCHI ZA MWAMBAO WA BAHARI YA HINDI

0
0


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) anaongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya nchi za mwambao wa Bahari ya Hindi unaofanyika Durban, Afrika Kusini leo tarehe 2 Novemba, 2018. 

Mkutano huu umetanguliwa na Kikao cha 20 cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi tarehe 31 Oktoba hadi tarehe 01 Novemba, 2018 ambapo ujumbe huo uliongozwa na Balozi Ramadhan M. Mwinyi, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Jumuiya ya nchi za mwambao wa Bahari ya Hindi (Indian Ocean Rim Association – IORA) ilianzishwa mwaka 1997 awali, ikijulikana kama Indian Ocean Rim Association for Regional Cooperation IORA-AC kabla ya kubadilishwa kuwa IORA mwaka 2013. Jumuiya hii inaundwa na nchi wanachama 21 ambazo ni Afrika Kusini, Australia, Bangladesh, Comoro, India, Indonesia, Jamhuri ya Kiislam ya Iran, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kenya, Malaysia, Madagascar, Mauritius, Msumbiji, Shelisheli, Singapore, Somalia, Sri Lanka, Sultani ya Oman, Thailand, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na Yemen. Tanzania ni moja kati ya nchi waanzilishi wa Jumuiya hii.

Katika muundo wake, IORA pia ina washirika wa mazungumzo (Dialogue Partners) saba (7) ambao ni Jamhuri ya Watu wa China, Japan, Marekani, Misri, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ambao hushiriki katika utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Jumuiya.

Katika uongozi, Afrika Kusini ndie Mwenyekiti wa sasa wa IORA akisaidiana na Umoja wa Falme za Kiarabu kama Makamu Mwenyekiti. Hivyo, Mheshimiwa Lindiwe Sisulu (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Kusini aliongoza mkutano huu.

Lengo kuu la IORA ni kuimarisha ushirikiano miongoni mwa nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi. Ikumbukwe kwamba Bahari ya Hindi ni eneo muhimu sana kiuchumi, kirasilimali, kiusalama pamoja na maendeleo kwa ujumla.

Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania ya mwaka 2001 inaelekeza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ishirikiane na nchi jirani, za mbali na zenye malengo mema katika sura za kikanda, kimataifa na pande mbili kwa manufaa yetu. Huu ndio msingi wa Tanzania kuendelea kushiriki katika IORA kwani inatusaidia kujenga mahusiano yanayolenga kukuza uchumi; tunapata fursa ya kutangaza na kuvutia uwekezaji katika uchumi bahari (blue economy); na tunashiriki katika kuandaa na kutekeleza mikakati ya kikanda ya usimamizi wa rasilimali za uvuvi. Vilevile, kupitia IORA tunashiriki katika mfumo wa kupeana taarifa za kibiashara (IORA Trade Repository); kuimarisha ushirikiano wa kikanda katika kukuza biashara ndogo na za kati (SMEs); pamoja na kushirikiana kwenye kulinda usalama katika Bahari ya Hindi.

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huu wa 18 wa Mawaziri umeridhia maombi ya nchi za Maldives na Myanmar kujiunga uanachama wa IORA. Vilevile, Mawaziri wamekubali maombi ya nchi za Uturuki na Jamhuri ya Korea (Korea Kusini) kuwa Washirika wa Mazungumzo

Aidha, nchi mbalimbali wanachama ikiwemo Tanzania wameahidi kuendelea kushirikiana katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyo chini ya maeneo tisa vipaumbele kwa IORA ambayo ni usalama na ulinzi wa bahari; biashara na uwekezaji; usafiri wa bahari; uvuvi; menejimenti ya udhibiti wa majanga; taaluma, sayansi na teknolojia; utalii na utamaduni; uchumi bahari; na uwezeshaji wanawake.

Jumuiya hii ni fursa nyingine muhimu sana kwa Tanzania kwa kuwa ina malengo mazuri yenye maslahi kwa nchi na Ukanda kwa ujumla. 

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dodoma.
02 Novemba, 2018

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiwa kwenye Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya nchi za mwambao wa Bahari ya Hindi (IORA) unaofanyika Durban, Afrika Kusini kuanzia tarehe 2 Novemba, 2018. Mhe. Dkt. Ndumbaro anaongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo ambao pamoja na mambo mengine nchi hizo zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyo chini ya maeneo tisa vipaumbele kwa IORA ambayo ni usalama na ulinzi wa bahari; biashara na uwekezaji; usafiri wa bahari; uvuvi; menejimenti ya udhibiti wa majanga; taaluma, sayansi na teknolojia; utalii na utamaduni; uchumi bahari; na uwezeshaji wanawake. Mwingine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi
Mkutano ukiendelea
Picha ya pamoja ya Mawaziri
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi (kushoto) akijadiliana jambo na mmoja wa wajumbe wakati wa Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya nchi za mwambao wa Bahari ya Hindi (IORA). Balozi Mwinyi aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenye kikao cha 20 cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi kilichofanyika tarehe 31 Oktoba na tarehe 01 Novemba, 2018.

KAMATI YA BAJETI YAKUTANA NA WIZARA YA FEDHA

0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti Mheshimiwa George Simbachawene akielezea jambo mbele ya Kamati hiyo ilipokuwa ikijadili Taarifa za Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/2020 na Mwongozo wa maandalizi ya Mpango wa Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2019/20 – 2021/22 katika kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma. Kulia kwake ni Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.
Waumbe wa Kamati ya Bajeti wakijadili Taarifa za Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2019/2020 na Mwongozo wa maandalizi ya Mpango wa Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2019/20 – 2021/22 kataika Kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma.

BancABC yaja na ofa kwa wateja wa akaunti za amana.

0
0
· Wateja wanaoufungua akaunti za amana kupata riba hadi asilimia 14 papo hapo.

BancABC Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara na ambao imeorodhesha kwenye soko la hisa la London, imepiga hatua nyingine kwenye soko baada ya kutangaza ofa kabambe kwa wateja wakati huu wa kuelekea msimu wa Krismasi na sikukuu za mwisho wa mwaka.

Ofa hiyo ni maalum kwa wateja wote wanaofungua akaunti za amana ambapo Watapata riba ya hadi asilimia 14 papo hapo, Ofa hiyo imeanza leo na wateja wote watanza kufaidika nayo kuanzia leo Novemba mosi mpaka Disemba 31 mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza hatua ya benki hiyo kutoa ofa hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Wateja binafsi BancABC Joyce Malai alisema kuwa benki yake imeamua kutoa ofa hadi asilimia 14 ya papo kwa papo kwa wateja wote ambao wanafungua akaunti za amana.

Hata hivyo, Malai alisema wateja watakuwa na uhuru wa kuchangua kuchukua riba papo hapo au kwa kila mwezi au mwishoni mwa amana. Vile vile, mteja atakuwa na uwezo wa kuchukua mkopo wa hadi asilimia 80 ya amana yake, Malai aliongeza. Hii ni ofa bora kwenye soko kwa sasa na hivyo tutoa wito kwa wateja wetu na hata wale wasiokuwa na akaunti kwetu kutumia fursa ya ofa hii ya msimu huu wa sikukuu kwa manufaa yao,” alisema alisema Malai.

Malai alisema kuwa BancABC imejidhatiti kufikia mahitaji ya wateja na kuhakikisha kwamba wanakua pamoja na benki hiyo. “Tunathamini jinsi wateja wetu wanavyotuunga mkono na hiyo ndio sababu sisi kama benki tumeamua kuwazawadia ofa hii kabambe katika msimu huu wa sikukuu,”.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Hazina wa benki hiyo Barton Mwasamengo “Kinachotakiwa kufanywa na mteja yeyote ili aweze kujipatia ofa hii nikufika kwenye matawi yetu nchini kote na kufungua akaunti ya amana ya muda maalumu ambapo riba hiyo italipwa papo hapo, lengo ni kukupa uhuru wa kuitumia kwa ajili ya kufanya manunuzi binafsi kama upendavyo ikiwemo kununua zawadi kwa familia au marafiki ili kuwaongezea furaha katika msimu huu wa sikukuu,” aliongeza Malai.

Mwasamengo aliongeza kuwa ofa hiyo itawahusu wateja watakaofungua akaunti za amana za muda maalumu BancABC na ofa hii inaanza leo Novemba mosi mpaka Disemba 31 mwaka huu. “Tunataka msimu huu wa sikukuu kuwa mzuri zaidi kwa wateja wetu kwa kuwa tunafahamu kwamba watu wengi hutumia kiasi kikubwa cha fedha wakati wa Krismasi. Kupitia riba hii watakayopata awali, wataweza kupata mahitaji yao kirahisi,” alisema.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja binafsi BancABC Joyce Malai (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Hazina wa benki hiyo Barton Mwasamengo wakionyesha bango baada ya benki hiyo kutangaza kutoa ofa maalum kwa wateja wote wanaofungua akaunti za amana ambapo Watapata riba ya asilimia 14 papo na inaanza leo Novemba mosi mpaka Disemba 31 mwaka huu.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja binafsi BancABC Joyce Malai (kushoto) kutangaza hatua ya benki hiyo kutoa ofa maalum kwa wateja wote wanaofungua akaunti za amana ambapo Watapata riba ya asilimia 14 papo na inaanza leo Novemba mosi mpaka Disemba 31 mwaka huu. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Hazina wa benki hiyo Barton Mwasamengo.

DC MURO AIBUA UFISADI WAKUTISHA KANISANI,VIGOGO KUBURUZWA

0
0

DC MURO AKABIDHIWA MIFUKO 75 YA SARUJI NA MIL. 5 KWA AJILI YA UJENZI WA VYOO

0
0
Na, Imma Msumba Arumeru

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh. Jerry Muro Amepokea misaada ya saruji mifuko 75, shilingi milioni 5 pamoja na vyoo 20 vya kisasa kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya Shule ya Msingi Seliani kilichotitia wiki iliyopita.

Akizungumza mara baada ya kupokea misaada hiyo Dc Muro amesema kuwa misaada hiyo itasaidia kufanikisha ujenzi wa vyoo hivyo kwa muda mfupi, Pia amewashukuru sana wadau wa kampuni ya Usafiri ya Dar Lux kwa msaada wa Milioni Tano ( 5 ).

kwa upande wake Ndg. Nangu amesema wamejitolea Saruji hiyo kwa ajili ya vyoo vya kisasa kabisa yenye thamani ya sh.milioni Moja na Laki moja na ishirini na tano kwa ajili ya kuunga mkono jitihada za Dc Muro baada ya kupata Taarifa za janga la kutitia kwa choo hicho.

“Tunatambua changamoto wanazopata wanafunzi hasa kwa mtoto wa kike kutokana na maumbile yake, hivyo ujenzi wa vyoo hivi utasaidia kuwafanya wanafunzi hao kufurahia mazingira yatakayokuwamo wakiwa shuleni,” alisema Nangu.

Alisema wanafahamu matatizo wanayoyapata watoto wa kike wakiwa shuleni hasa wanapofkia hatua ya kuvunja ungo, kutokana na mabadiliko yanayoanza kutokea na wanapokuwa kwenye tarehe zao ambapo wengine hulazimika kutokwenda shule kutokana na mabadiliko yao ya kimwili, hivyo kwa kushirikiana na Dc Muro wanaamini ujenzi wa vyoo hivyo utawaondolea mabinti wasiwasi.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro Akikabidhiwa mifuko ya Saruji kutoka kwa mdau wa maendeleo Ndg. Ramadhani Nangu mwakilishi wa Bwana Manglan anayeishi nchini Marekani kwa ajili ya ujenzi wa choo cha shule ya Seliani kilicho titia wiki iliyopita.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro,sambamba na Katibu Tawala wa Arumeru Mwl. James Michembe pamoja na Mkurugenzi Halmashauri ya Arusha wakipokea msaada wa Fedha Tsh. Milioni Tano kutoka kwa Ndg. Joel Nathaniel Sasali ambaye ni Operesheni Meneja wa Kampuni ya Usafirishaji ya Dar Lux akiwa ameambatana na baadhi ya watumishi wa kampuni hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Akipokea Vyoo Ishirini kutoka kwa Mdau wa maendeleo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa choo cha wananfuzni wa shule ya msingi Seliani kilichotitia .
Mwakilishi wa Chama cha Mapinduzi akikabidhi mchango wa ujenzi wa choo kilichotitia kwa Mkuu wa wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro.

Shirika la SBFIC kuwajengea uwezo watanzania kuhusu huduma za kifedha

0
0

Na George Binagi-GB Pazzo

Shirika la “Savings Banks Foundation for International Coorperation- SBFIC” lenye makao yake makuu nchini Ujerumani, limefungua rasmi ofisi yake nchini Tanzania lengo likiwa ni kufikisha karibu huduma zake  kwa watanzania.

Hafla ya uzinduzi wa ofisi hiyo ilifanyika Novemba Mosi 2018 katika eneo la Bwiru Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza, yalipo makao makuu ya shirika hilo hapa nchini huku makao makuu ya Afrika Mashariki yakiwa Kigali nchini Rwanda.

Mkurugenzi wa shirika hilo hapa nchini, Stephen Noel Safe alisema limejikita kuwajengea uwezo wananchi pamoja na watoa huduma za kifedha kutekeleza miradi endelevu ili kutambua umuhimu na matumizi sahihi ya mikopo pamoja na kujiwekea akiba hususani kwa taasisi ndogondogo ikiwemo Vicoba.

Mgeni rasmi, Mtendaji Mkuu shirika la SBFIC, Dkt. Christoph Gogler kutoka nchini Ujerumani alisema huduma za shirika hilo zimewafikia wanufaika zaidi ya 2000 kwa njia mbalimbali ikiwemo mafunzo lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kuendeleza miradi yao kupitia huduma za kifedha ikiwemo mikopo na kujiwekea akiba.


Mkurugenzi wa shirika la SBFIC hapa nchini, Stephen Noel Safe akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Mtendaji Mkuu shirika la SBFIC, Dkt. Christoph Gogler akizungumza kwenye hafla hiyo.

Mtendaji Mkuu shirika la SBFIC, Dkt. Christoph Gogler akizungumza kwenye hafla hiyo.
Steven Revelian amnaye ni Mtendaji Mkuu mradi wa KARUDECA kutoka mkoani Kagera akiwasilisha salamu zake kwenye hafla hiyo.
Mudita Cheyo kutoka taasisi ya kifedha ya Self Entrepreneur akizungumza kwenye hafla hiyo namna taasisi yake inavyoshirikiana na shirika la SBFIC.
Viongozi wa shirika la SBFIC.
Mkurugenzi wa shirika la SBFIC hapa nchini, Stephen Noel Safe akieleza njia mbalimbali zinazotumika kufikisha elimu/ mafunzo kwa wananchi/ wanafunzi.
Mtendaji Mkuu shirika la SBFIC, Dkt. Christoph Gogler akiangalia machapicho yayotumika kufundishia.

Ofisini
Mgeni rasmi akisaini kitabu cha wageni.
Baadhi ya wafanyakazi shirika la “Savings Banks Foundation for International Coorperation- SBFIC”
Wanafunzi kutoka shule ya Msingi Karagwe mkoani Kagera ni miongoni mwa wanufaika wa mafunzo kutoka shirika la SBFIC
Kula keki kuashiria uzinduzi wa ofisi yetu.
Tazama video hapa nchi

ARUSHA KUJA NA VITUO 4 MAALUMU VYA POLISI VILIVYOGHARIMU ZAIDI YA MIL. 80

0
0
Na Vero Ignatus, Arusha.

Kikao cha Sekta ya wadau wa Utalii kimefanyika Mkoani Arusha kikiwa na lengo la kuona namna wanatekeleza azimio la kusimika vituo vinne Maalum vya Polisi kwa ajili ya Ukaguzi wa magari yanayosafirisha watalii.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii ambapo Mkuu wa mkoa Mrisho Gambo amesisitiza azma yake katika kuhakikisha utalii unatengenezewa mazingira mazuri ya ukuaji.“Hakuna kitu kinatupa sifa mbaya kwa wageni kama kusimamishwa na askari kila baada ya kilomita moja''alisema Gambo

Amesema Vituo hivyo maalum vya ukaguzi vitasaidia kuondokana na changamoto hiyo kwakuwa sekta ya utalii inategemewa sana katika kuliingizia taifa pato ."Magari yote yatakua na vituo maalum vya ukaguzi, tunafanya yote haya kwakua sekta ya utalii tunaitegemea sana kama taifa kwa kutuingizia pato la taifa.” Alisema Gambo.

Vituo hivyo vinne vinavyogharimu zaidi ya shilingi Milioni 80 vimetengenezwa kwa michango ya wafanyabiashara ya Utalii TATO na vinatarajiwa kuwekwa katika maeneo ya Kikatiti, Ngaramtoni, Makuyuni na Karatu.

Kwa upande wa serikali kupitia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na TANAPA, Mkurugenzi mkuu wa hifadhi za Taifa Dr. Kijazi amesema wao kama wadau wa mkubwa wa sekta hii wanaunga mkono wazo hili na wako tayari kuhakikisha taasisi zao zinajenga vyoo katika vituo hivi.“Sisi kama hifadhi za Taifa ni wanufaika namba moja endapo sekta hii inaboreshewa mazingira, na kwa kuunga mkono jitihada hizi mimi na wenzangu wa mamlaka ya Ngorongoro tunaahidi kujenga vyoo katika vituo vyote vinne kwa kushirikiana na ofisi za wakuu wa wilaya” alisema Kijazi.

Kwa niaba ya wafanyabiashara ya utalii Bwana Sirili Nko ambaye ni Katibu wa TATO, ametoa pongezi kwa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kuonyesha juhudi za kUkuzaji na kUboresha sekta ya Utalii Mkoani Arusha.Toka kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha Gambo amefanya jitihada nyingi za kuboresha sekta ya utalii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.
Kutoka kushoto ni mhifadhi mkuu wa mamlaka ya Ngorongoro Dkt. Fredy Manongi akifuatiwa na Mkurugenzi wa TANAPA Dr. Alan Kijazi
Wamiliki wa makampuni ya Utalii wakifuatilia mjadala wa kuweka vituo maalumu vya polisi mkoani Arusha.
Mdau wa Sekta ya Utalii wakitoa maoni yao juu ya zoezi la uwekaji wa vituo maalum vya polisi.

KATIBU MKUU MEJA JENERALI KINGU AONGOZA KIKAO CHA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, KUJADILI HOJA ZA KAMATI ZA BUNGE ZA PAC NA NUU, JIJINI DAR ES SALAAM LEO

0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (kulia) akiongoza kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo.
PIX 2
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (kushoto) akitaka ufafanuzi kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, (CGP), Phaustine Kasike, katika kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo.
PIX 3
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu (katikati) akiongoza kikao cha Watendaji Wakuu wa Wizara yake, cha kujadili hoja zilizotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Kudumu ya Bunge Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ndogo za Wizara, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi.

NGARIBA WABADILI MBINU ZA UKEKETAJI

0
0

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa MKoa wa Mnyara Bw. Anza-Amen Ndossa wakionesha Wajumbe wa Kamati ya Dawati la Ulinzi wa Wanawake na Watoto Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MATAKUWA) mara baada ya kuzindua kamati ya hiyo ya Mkoa jana katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu Mkoa Manyara.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe kuzindua Kamati ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto jana katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu Mkoa Manyara pembeni yake ni KaimuKatibu Tawala wa Mkoa wa Manyara Bw. Anza-Amen .Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW



Na Mwandishi Wetu Manyara.

Mangariba nchini wamebuni njia mpya za kuendeleza vitendo vya ukeketaji nchini kwa kutofanya sherehe wakati wa ukeketaji lakini pia kukeketa watoto wachanga na kufanya vitendo ua ukeketaji nyakati za usiku.

Hayo yamesemwa Wilayani Babati Mkoani Manyara na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizindua Kamati za Ulinzi kwa Wanawanke na Watoto kwa mkoa wa Manyara.

Naibu Waziri Ndugulile amesema kuwa kuanzia Januari mpaka Septemba 2017 jumla ya vitendo 41,000 vya ukatili viliripotiwa na jeshi polisi nchini akifafanua kuwa kama takwimu hizi zingekuwa za ujambazi katika mkoa mmoja hali ya wananchi ingekuwa mbaya sana huku akiviita vitendo hivyo na ujambazi katika sura mpya. Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imejipanga kutokomeza vitendo vya Ukeketaji kwa kuanzisha Mpango Mkakati wa kutokomeza Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wa mwaka 2016/2017 utakaoisha mwaka 2021/2022.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa kwa mujibu wa Takwimu inaonyesha Mkoani wa Manyara una Asilimia 27 ya vitendo vya ukatili wa kijinsia hivyo nguvu inahitajika sana katika kupambana na vitendo hivyo akiitaka kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuweka suala hilo katika mipango yao ili kudhibiti ukatili huo.

Naibu Waziri Ndugulile amewataka wajumbe wa Kamati ya Ulinzi kwa Wanawake na Watoto aliyoizindua jana mkoani humo kusoma na kuelewa majukumu yao kama ilivyabainishwa katiaka mkakati wa MTAKUWA kuendeleza mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto Mkoani Manyara.

Akitoa taarifa ya Ukatili wa Kijinsia Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Manyara Bi. Anna Fisso amesema kuwa mila zisizofaa zimekuwa zikiongeza vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Babati kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Elizabeth Kitundu amaahidi kufuatilia utendaji kazi wa Kamati hiyo ili iweze kufanya kazi ili kuondokana ama kufuta kabisa vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.

Akizungumza mmoja wa Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto akimwakilisha Sheikh wa Mkoa wa Manyara Sheikh Abdallah Suleiman amesema kuwa wao kama viongozi wa kiroho wanatumia ushawishi wao kutoa elimu kwa wananchi kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ili kupunguza vitendo hivyo.

Naibu Waziri Dkt. Faustine Ndugulile yupo katika ziara ya Siku 3 Mkoani Manyara katika kukagua utoaji huduma katika Sekta ya Afya, Ustawi na Maendeleo ya Jamii.

WAZIRI MKUU AFUNGA MAONESHO YA WIKI YA VIWANDA MKOA WA PWANI

0
0
 WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, akisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi, Cyprian Luhemeja, wakati alipofika Uwanja wa Sabasaba Picha ya Ndege Mkoa wa Pwani jana kwa ajili ya kufunga maonesho ya Wiki ya Viwanda
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja Utawala wa kampuni ya Terra inayobangua Korosho, Peter Christopher, wakati alipofika Uwanja wa Sabasaba Picha ya Ndege Mkoa wa Pwani jana kwa ajili ya kufunga maonesho ya Wiki ya Viwanda. (Picha na Muhidin Sufiani)

 WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, akisikiliza maelezo kutoka kwa Ofisa Masoko wa kampuni ya Chumi 'Neel Salt', Vivian Stephan, wakati alipofika Uwanja wa Sabasaba Picha ya Ndege Mkoa wa Pwani jana kwa ajili ya kufunga maonesho ya Wiki ya Viwanda.

Mamia wajitokeza kupima tezi dume Muhimbili tawi la Mloganzila

0
0
Mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam leo wamejitokeza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kwa ajili ya zoezi la kupima bure tezi dume (prostate) na mfumo wa njia ya mkojo kwa kutumia ultrasound.

Zoezi hilo limeandaliwa na Hospitali ya Muhimbili tawi la Mloganzila kwa kushirikiana na Chama cha Wataalam wa Matumizi ya Mionzi katika uchunguzi na Tiba Tanzania (TARA) ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya wataalam wa mionzi tiba duniani.

Akizungumzia zoezi hilo mtaalam wa Radiolojia, Dkt. Lulu Sakafu amesema umri unavyozidi kwenda juu, wanaume wanakuwa katika hatari ya kupata matatizo ya tezi dume, hivyo wameshauriwa kujenga utamaduni kwa kupima afya zao mara kwa mara.Amesema watu wasiofanya mazoezi wako katika hatari ya kupata matatizo ya tezi dume, wanaume wanaopenda kula chakula chenye kiasi kikubwa cha mafuta na wengine wanaweza pata ugonjwa huo kutokana na historia ya familia zao.

“Katika maadhimisho ya mwaka huu tumeamua kupima tezi dume kwa wanaume wenye umri kuanzia miaka 45 ili kuangalia dalili na viashiria vya ugonjwa huu kwa sababu kansa ya tezi dume duniani inashika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo kwa wanaume kutokana na saratani ya tezi dume,” amesema Dkt. Sakafu.

Akizungumzia dalili za tezi dume, Dkt. Sakafu amesema kuwa kupata shida wakati wa haja ndogo, kutiririka kwa mkojo baada ya kumaliza haja ndogo, kujisaidia mkojo wenye mtiririko dhaifu, kukojoa mara kwa mara nyakati za usiku na kujikamua wakati wa kujisaidia na kushindwa kumali mkojo wote.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Muhimbili, Dkt. Praxeda Ogweyo amesema wanaume wasiogope kujitokeza kupima tezi dume kwa kuwa hivi sasa inatumika njia nyingine ya ultrasound badala ya ile ya zamani ya vidole.Naye Rais wa TARA, Stephen Mkoloma ambaye ni mtaalam wa radiolojia amesema wamechangua kupima tezi dume kwa kuwa takwimu za wagonjwa wanaoripotiwa hospitali kutokana na matatizo ya tezi dume imeongezeka.

“Nawashauri watu kupima afya zao mara kwa mara ili kujua afya zao mapema kwani ukigundua ugonjwa mapema gharama za matibabu zinakuwa chini kuliko kusubiri ugonjwa unapokuwa mkubwa au sugu,” amesema Mkoloma.
Mmoja wa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam akipima tezi dume katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. Kulia ni mtaalam wa radiolojia, Burhani Abdul akimpima tezi dume kwa kutumia Utrasound.
Baadhi ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wakisubiri kupima tezi dume katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo.
Rais wa Chama cha Wataalam wa Matumizi ya Mionzi katika uchunguzi na Tiba Tanzania (TARA), Stephen Mkoloma akitoa elimu kwa wanaume kuhusu tezi dume ikiwamo sababu, dalili na jinsi ya kujikinga.
Pichani ni Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila iliyopo Halmashauri ya Manispaa

NEWZ ALERT: WATU SABA WAPOTEZA MAISHA AJALI YA CHALINZE MKOANI DODOMA

0
0
Watu saba waliokuwa wakisafiri katika gari STL 6250 mali ya CAG wamekufa papo hapo na wengine watatu kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na gari SU 41173 mali ya PSSSF, katika eneo la Chalinze Mkoani Dodoma leo.
 
 Taarifa za awali zinaeleza kuwa waliofariki katika ajali hiyo mkoani Dodoma leo katika gari la Ofisi ya CAG ni dereva wa ofisi hiyo na wengine 6 ni ndugu wa Naibu CAG waliokuwa wakitoka katika msiba huko Chato mkoani Geita. 

Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma Giles Muroto, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba watu saba wamefariki katika ajali iliyohusisha magari mawili ya serikali ikiwemo, STL 6250 Toyota Land Cruiser kutoka ofisi ya CAG, baada ya kugongana uso kwa uso na gari yenye nambari SU 41173.

Milioni 302 zakusanywa mashindano ya baiskeli

0
0
ZAIDI ya Sh milioni 302.6 zimekusanywa katika kilele cha mashindano ya baiskeli ya ACACIA Imara Pamoja Cycle Challenge, ambayo lengo kuu ni kuchangisha fedha kutekeleza miradi itakayoboresha upatikanaji wa elimu kwa jamii zinazozunguka migodi kampuni Acacia kanda ya ziwa. 

Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya Uchimbaji Madini –ACACIA kwa kushirikiana na Taasisi binafsi kutoka nchini Canada (CanEducate), yameshirikisha wanaume katika mbio za Kilomita 140 na wanawake km 87. 

Mzunguko wa mashindano hayo yaliyofanyika leo jijini Mwanza ulianza na kumalizikia katika Hoteli ya Malaika Resort kwa kupitia maeneo ya Kibandani, Igombe, Sangabuye, Kayenze, Nyanguge na Usagara, Buhongwa. 

Akizungumza katika kilele cha mashindano hayo, Meneja Uboreshaji tija wa kampuni hiyo, Janet Reuben alisema jumla ya washiriki 211 wameshiriki katika mbio hizo. Alisema kila mwaka ACACIA imekua ikidhamini mashindano ya baiskeli ya kanda ya ziwa chini ya jina la Acacia Tufanikiwe Pamoja Cycle Challenge. 

“Hata hivyo, mwaka huu mashindano hayo yamepewa jina Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge ili kuakisi dira mpya ya kampuni inayolenga kujenga mahusiano imara zaidi na jamii na wadau wetu. “Pia uamuzi huu wa kubadili jina unatokana na kuongezeka kwa kipengele cha uchangishaji fedha katika mashindano ya mwaka huu kwa ajili ya kusaidia sekta ya elimu. 

“Kwa niaba ya uongozi wa Acacia kwa kupitia migodi yetu ya dhahabu ya Bulyanhulu, Buzwagi na North Mara, wadau wetu CanEducate na kamati ya maandalizi, nipende kuwashukuru kwa uwepo wenu leo, pia nawapongeza washindi na washiriki wote kwa kumaliza mbio hizi salama,” alisema. 

Alisema uamuzi wa kuendelea kujihusisha na mbio za baiskeli umechangiwa na mapenzi makubwa ambayo watu wa kanda ya ziwa wanayo juu ya mchezo huo. 

“Mpango huo pia unatoa kipaumbele katika kuhakikisha jamii zetu – hasa watoto wa kike - wanapata elimu bora kama njia moja wapo ya kujikwamua na umaskini na kufanikisha dhamira ya Serikali ya kuinua uchumi na hali za maisha ya watanzania kama ilivyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo 2025. 

“Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Acacia imeelekeza zaidi ya asilimia 38 ya bajeti yake ya kutelekeza miradi ya kijamii, katika miradi ya elimu. Baadhi ya miradi ya elimu ni pamoja na ujenzi wa madarasa, nyumba za waalimu, mabweni ya kisasa kwa ajili ya wanafunzi wa kike na ukarabati wa maktaba sita kwenye shule zinazozunguka migodi yetu,” alisema. 

Aidha, aliongeza kuwa fedha hizo zitaelekezwa katika udhamini wa wanafunzi unaofanyika kati ya Acacia na CanEducate. 

“Baadhi ya matumizi yaliyopangwa kwa ajili ya fedha hizo ni kama ifuatavyo; Fedha hizo zitasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia zisizojiweza na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapatia sare na vifaa vingine vya shule ikiwemo vitabu na vifaa mbalimbali. 

“Fedha hizo pia zitaelekezwa katika kusaidia wanafunzi wa kidato cha tano na sita wanaotoka kwenye maeneo yanayozunguka migodi yetu kwa kuwalipia ada za mitihani, gharama za malazi na usafiri,” alisema. 

Aidha, Rais wa Chama Waendesha Baiskeli nchini, Godfrey Mhagama alimtangaza mshindi wa kwanza katika mbio hizo kwa upande wa wanaume kuwa ni Masunga Duba aliyejinyakulia Sh milioni 1.2, wapili Gerald Konnda (sh 900,000) na watatu Mungu Ataleta (Sh 500,000). 

“Kwa upande wa wanawake mshindi ni Laurencia Luzuba (Sh milioni moja) na wa pili Tatu Malulu (Sh 800,000),” alisema. 

   Meneja Uboreshaji Tija kutoka ACACIA, Janet Reuben akizungumza katika mashindano mbio za baiskeli yaliyopewa jina la Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge. Jumla ya Sh milioni 302.6 zimekusanywa katika mashindano hayo yaliyofanyika leo jijini Mwanza.



   Meneja Uboreshaji Tija kutoka ACACIA, Janet Reuben akiwa na baadhi ya washiriki wa mashindano mbio za baiskeli yaliyopewa jina Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge. Jumla ya Sh milioni 302.6 zimekusanywa katika mashindano hayo yaliyofanyika leo jijini Mwanza.

   Baadhi ya washiriki wa mashindano mbio za baiskeli yaliyopewa jina Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge wakiwakata upepo katika mashindano hayo yaliyofanyika jijini Mwanza. Jumla ya washiriki 211 wametimua mbio katika mashindano hayo.



  Mshindi wa mashindano ya mbio za baiskeli yaliyopewa jina Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge, Masunga Duba akishangilia kuibuka mshindi na kujinyakulia Sh milioni 1.2, wa pili Gerald Konda (sh 900,000) na watatu Mungu Ataleta (Sh 500,000).

    Baadhi ya washiriki wa mashindano wakikata utepe kuanza mashindano hayo yaliyofanyika leo jijini Mwanza. Jumla ya washiriki 211 wametimua mbio katika mashindano hayo.


  Baadhi ya washiriki wa mashindano wakianza kutimua mbio katika mashindano hayo yaliyofanyika leo jijini Mwanza. Jumla ya Sh milioni 302.6 zimekusanywa katika mashindano hayo kwa lengo la kusaidia huduma za elimu kwa jamii zinazozunguka migodi ya Acacia.


Viewing all 46200 articles
Browse latest View live




Latest Images