Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live

REGIONAL FARMERS FEDERATION MEET EALA SPEAKER, PUSH FOR INCREASED FUNDING FOR SECTOR

0
0

EALA Speaker admires a memento as Ms Rachel Muyoboke representing ESAFF, Rwanda and Hon Mathias Kasamba, Chair of the EALA Agriculture, Tourism and Natural Resources (ATNR) look on.

The ESAFF delegation in talks with the EALA Speaker, Rt Hon Ngoga Karoli Martin earlier today.

Mr Alfayo Kurunah, ESAFF Board Member, Kenya (left) addresses as Hakim Baliraine, ESAFF, Uganda and Richard Kipara from Muungano wa Vikundi vya Wakulima Wadogo (MVIWATA), Tanzania look on. ESAFF Board officials today paid a courtesy call on the EALA Speaker, Rt hon Ngoga Karoli Martin.

EALA Speaker, Rt Hon Ngoga Karoli Martin (centre) in dark suit with representatives of the East Africa Small Scale farmers Forum who paid him a courtesy call this morning in Arusha


East African Legislative Assembly, Arusha, Tanzania: 30thOctober, 2018: Small scale farmers under the aegis of the East and Southern Africa Small Scale Farmers Forum (ESAFF) are set to petition the EAC Heads of State to galvanize for increased financing for agricultural sector in the EAC region to ensure food security, reduce poverty and increase public awareness on the Comprehensive Africa Agriculture Development Programme (CAADP). This morning, officials of the ESAFF paid a courtesy call on Rt Hon Ngoga Karoli Martin, Speaker of EALA, in Arusha and made a plea for the petition, when ready, to be forwarded for the attention of the Summit of EAC Heads of State.

Rt Hon Ngoga assured the ESAFF officials of the Assembly’s support towards initiatives that leverage agriculture to ensure food security and raise the region’s GDP. He pledged to work closely with the EAC Council of Ministers and the EAC Secretary General to ensure the petition, once done by ESAFF is given attention and channeled appropriately to the EAC Heads of State. Rt Hon Ngoga further said time was ripe for the establishment of an institution dealing specifically with matters of agriculture and food security. The Speaker noted that the Assembly would champion Partner States to set aside public spending for agriculture at 10% as envisaged under the Malabo Declaration.

Speaking on behalf of the Forum, Mr Alfayo Kurunah, a farmer from Kenya and board Member of ESAFF reiterated his organization was keen to collaborate with EALA in organizing a high-level meeting to deliberate on the status of commitment by Partner States in achieving the commitments under the Malabo Declaration. According to Mr Kurunah, the meeting which is expected to bring together Ministers for Agriculture and Ministers for Finance from the Partner States, as well as legislators from the National Legislatures and EALA would lead to a regional position on the progressive implementation of the Malabo goals reflected to national budgets

“We hope that this meeting would take place in the coming sitting of EALA in November or December 2018 and that the review will be done during the next agriculture summit in May 2019”, Mr Kurunah said.

The Malabo declaration of June 2014, hopes to accelerate agricultural growth and transformation. It among other things calls for commitment to ending hunger by 2025 by at least double productivity while focusing on inputs, irrigation and mechanization. 
 
The Malabo Declaration further anticipates commitment towards enhancing resilience in livelihoods and production systems to climate variability and other shocks and to boosting intra-African trade in agricultural commodities and services by tripling intra-Africa trade in agricultural commodities and fast-track of the continental free trade area. Further envisaged is a commitment to halve poverty, strengthen inclusive Public-Private Partnerships on agricultural commodity value chains and creation of job opportunities for at least 30% of the youth in agricultural value chains.

According to the ESAFF, the EAC region is doing quite well, but has fallen short on budgetary allocation in the agriculture sector to reach the 10% target, ending hunger including malnutrition and stunting among children under 5 years whose statistics was deemed as shocking.

The Farmers organization thus put a strong case and emphasis for the region to focus its (EAC) industrialization on agriculture.

In attendance was the Chairperson of the EALA Committee on Agriculture Tourism and Natural Resources, Hon Mathias Kasamba and officials from ESAFF Members in the Partner States; Ms. Rachel Muyoboke, Apui Petit Peysant et Envirnement (APEE), Rwanda, Hakim Baliraine –ESAFF, Uganda, Obeid Girukwayo, ESAFF, Burundi, Justus Lavi Mwololo, Kenya Small Scale Farmers Forum (KESSFF) andRichard Kipara, Mtandao wa Vikundi Vya Wakulima Tanzania (MVIWATA). Others were Martha Makenge, EACSOF and three officials from the ESAFF Secretariat, Joe Mzinga, Stella Henry and Irene Ngao.

KILUWA AFANIKIWA KUWAHAMASISHA WACHINA KUJA NCHINI TANZANIA KUJENGA VIWANDA VITATU MLANDIZI

0
0
*Dola za Marekani milioni 100 kutumika katika ujenzi 
*Ahimiza Watanzania kuwa wazalendo kwa nchi yao


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MWENYEKITI wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd Mohammed Kiluwa amesema katika kuhakikisha anaunga mkono jitihada za Rais Dk.John Magufuli za ujenzi wa Tanzania ya viwanda amefanikiwa kuwashawishi wawekezaji kutoka nchini China kuja kujenga viwanda kuwekeza nchini.

Kiluwa amesema kupitia ushawishi wake na kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) wawekezaji hao kutoka China wamekubali kujenga kiwanda cha kuongeza thamani ya bidhaa za ngozi, Kiwanda cha Saa pamoja na Kiwanda cha Simu na kwamba awamu ya kwanza ya uwekezaji huo jumla ya dola za Marekani milioni 100 zitatumika.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu ujio wa wawekezaji hao Kiluwa amesema viwanda hivyo vitajengwa Mlandizi mkoani Pwani na wakati wowote kuanzia sasa baada ya kukamilisha taratibu zote ikiwemo za vibali ujenzi wa viwanda hivyo utaanza mara moja.Pia amesema mbali ya kujengwa kwa viwanda hivyo wawakezaji hao wameonesha nia ya kujenga kiwanda cha kubangua korosho mkoani 

Mtwara na kinachoendelea sasa ni mazungumzo ambayo yanakwenda vizuri na hakuna kitakachoshindikana."Wawekezaji hawa wameonesha nia kujenga kiwanda cha korosho na walikuwa tayari kwenda mkoani Mtwara kuona mazingira." 

Kiluwa amefafanua kwenye mazungumzo yake na wawekezaji hao aliwagusia kuhusu zao la korosho nchini na hivyo wamekubali kujenga kiwanda cha korosho.Amezungmzia umuhimu wa wananchi kuwa na uzalendo kwa nchi yao katika kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kwenye ujenzi wa uchumi wa nchi na hasa kuelekea ujenzi waTanzania ya viwanda.

"Tuwe wazalendo kwa nchi yetu kwa kuhakikisha tunaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli katika kujenga Tanzania yenye uchumi imara kupitia viwanda.Ni jukumu letu Watanzania kusimama imara kufanikisha dhamira ya Rais wetu mpendwa,"amesema Kiluwa na kuongeza kwa kutambua malengo ya Rais ameamua kushiriki kwa vitendo kuhamasisha wawekezaji kuja kuwekeza nchini.

"Kushawishi wawekezaji ni kazi ngumu lakini naifanya kwa moyo wangu wote huku nikitanguliza uzalendo kwa taifa langu.Nitoe rai kwa wanaohusika na utoaji wa vibali kuhakikisha wanatoa kwa wakati ili wawekezaji ambao wanakuja kuwekeza waanze shughuli za uwekezaji nchi kwetu,"amesema Kiluwa na kuongeza kuwa anafurahishwa pia na ushirikiano uliopo kati yake na TIC.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kukuza Uwekezaji kutoka TIC John Mnali amesema moja ya mikakati yao ni kuendelea kuhamasisha wawekezaji kuja kuwekeza nchini Tanzania ambako kuna mazingira mazuri ya uwekezaji.Pia amefafanua pamoja na kuandaa mazingira mazuri ya uwekezaji nchini wamekuwa wakisaidia kuhakikisha wawakezaji wanapata vibali vyote muhimu vinavyotakiwa katika uwekezaji."Moja ya jukumu letu ni kuwasaidia wawekezaji waweze kupata vibali kwa haraka ili waendelee na uwekezaji."

Wakati huo huo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yinengda New Material Techonology Mayi Hong ambaye amesema wamefurashiwa na mazingira mazuri ya uwekezaji ya nchini Tanzania na kutokana na mazingira mazuri yamewavutia kuwekeza kwa kujenga viwanda hivyo katika eneo la Mlandizi mkoani Pwani.

"Tutajenga kiwanda cha kuongeza thamani ya ngozi na kisha kutengeneza bidhaa zitokanazo na ngozi.Pia tutajenga kiwanda cha saa na kiwanda cha simu.Tumetenga Dola za Marekani milioni 100 kwa ajili ya viwanda hivyo.Pia katika mazungumzo yetu na Kiluwa tumejadiliana kuhusu ujenzi wa kiwanda cha korosho na tunaamini tutajenga,"amesema Hong.

Mkurugenzi wa Kukuza Uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. John Mathew Mnali akizungumza jambo mbele ya waandishi wa Habari leo jijini Dar kuhusu masuala mbalimbali ya uwekezaji wa viwanda,ikiwemo na kuwapokea wageni wa uwekezaji wa viwanda kutoka nchini China na wenyeji wao kutoka kampuni ya Kiluwa Group Ltd.



MWENYEKITI wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd Mohammed Kiluwa (pichani kushoto) akifafanua jambo mbele ya Waandishi wa habari leo alipokwenda kuwatambulisha Wadau wake wa Uwekezaji katika masuala ya Viwanda kutoka nchini China,kwa kituo cha Uwekezaji nchini (TIC),na kueleza mikakati yao mbalimbali waliyonayo kuhusiana na uwekezaji wa viwanda nchini Tanzania,kulia ni Mkurugenzi wa Kukuza Uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Bw. John Mathew Mnali. 

Wawekezaji wa Kampuni ya Yinengda New Material Techonology kutoka nchini China,wakiwa wameambatana na Mkurugenzi wao Mayi Hong wakisikiliza mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa kwenye mkutano huo,uliofanyika katika kituo cha Uwekezaji (TIC),jijini Dar

Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji (TIC),Geofrey Mwambe akisalimia na Mkurugenzi wa kampuni ya Kiluwa Group,Naima Mohamed Kiluwa,walipokwenda kwenye ofisi za kituo hicho kuwatambulisha wadau wao wa uwekezaji katika mambo ya Uwekezaji wa Viwanda,anaeshuhudia pichani kati Mwenyekiti wa Kampuni ya Kiluwa Group,Mohamed Kiluwa (pichani kati) na kuwasilisha mikakati yao mbalimbali ya uwekezaji wa viwanda.
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji (TIC),Geofrey Mwambe akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yinengda New Material Techonology Mayi Hong alipokuwa akifafanua jambo kuhusiana na mambo ya uwekezaji wa viwanda hapa nchini Tanzania,maara aada kuzungumza na waandishi wa habara katika ofisi za kituo hicho .
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Yinengda New Material Techonology Mayi Hong akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji (TIC),Geofrey Mwambe walipowasili leo kwenda kutambulishwa na Mdau wake Mkubwa kwenye mambo ya Uwekezaji wa Viwanda,Mwenyekiti wa Kampuni ya Kiluwa Group,Mohamed Kiluwa (pichani kati) na kuwasilisha mikakati yao mbalimbali ya uwekezaji wa viwanda.

Wakiwa katika picha ya pamoja

RAIS DKT. MAGUFULI AHUTUBIA KONGAMANO LA HALI YA UCHUMI NA SIASA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITATU YA UONGOZI WAKE

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa Mshiriki Maalum, akizungumza na Wageni mbalimbali wakiwemo Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Viongozi wa Kiserikali, Mabalozi kutoka nchi mbalimbali, pamoja na wananchi   waliohudhuria katika Kongamano la Hali ya Uchumi na Siasa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano lililofanyika katika ukumbi wa Nkuruma uliopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Sehemu ya Watoa Mada wakiwa Wanasikiliza michango mbalimbali iliyokuwa ikitolewa katika Ukumbi wa Nkuruma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Wakwanza kushoto ni Profesa Humphrey Moshi, Profesa Kitila Mkumbo, Makamu Mkuu wa Chuo Profesa William Anagisye, Profesa Rwekaza Mukandala, Profesa Martha Qorro pamoja na Profesa Hudson Nkotagu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa mshiriki Maalum katika Kongamano hilo akiandika baadhi ya Hoja katika Kongamano hilo.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa Mshiriki Maalum akiwa pamoja na washiriki wengine wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na Watoa Mada katika Kongamano la Hali ya Uchumi na Siasa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano lililofanyika katika ukumbi wa Nkuruma uliopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Baadhi ya Washiriki wa Kongamano la Hali ya Uchumi na Siasa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano wakisikiliza kwa makini wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa mshiriki Maalum alipokuwa akizungumza katika ukumbi wa Nkuruma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
  Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwa nje ya Ukumbi wa Nkuruma wakifatilia Kongamano la Hali ya Uchumi na Siasa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano kwa njia ya Luninga wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa mshiriki Maalum alipokuwa akizungumza katika ukumbi wa Nkuruma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alikuwa mshiriki Maalum katika Kongamano hilo akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Wasichana ya Kisutu mara baada ya kutoka katika Ukumbi wa Nkuruma katika Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
PICHA NA IKULU

KILUWA AFANIKIWA KUWAHAMASISHA WACHINA KUJA NCHINI TANZANIA KUJENGA VIWANDA VITATU MLANDIZI

0
0

SERIKALI YAMALIZA MGOGORO WA KIWANDA CHAI MPONDE

0
0
*Yaagiza mashine zichunguzwe, mitambo yenye hitilafu ikarabatiwe kazi ianze
SERIKALI imemaliza mgogoro uliodumu kwa miaka mingi kati ya wakulima wa chai wa wilaya za Lushoto na Korogwe na kampuni ya Mponde Tea Estate uliosababisha kufungwa kwa kiwanda cha chai cha Mponde baada ya kuagiza kiwanda hicho kianze kazi.

“Waziri Mwijage na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilomo Prof. Siza Tumbo hakikisheni kazi ya kukagua kiwanda na mitambo inafanyika haraka na kubaini mitambo ipi ni mizima na ipi ina hitilafu ili ukarabati ufanyike na kiwanda kianze kazi mara moja.”

Uamuzi huo wa Serikali umetangazwa leo (Alhamisi, Novemba 1, 2018) na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Kweminyasa kata ya Mponde, wilayani Lushoto baada ya kutembelea kiwanda hicho .

Waziri Mkuu amesema mwaka 1999 Serikali iliamua kuwapa wakulima wa chai na kiwanda hicho  kwa ajili kuwawezesha kuwa na sehemu ya kuchakata chai yao lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kiuchumi. Imeamua kukirudisha Serikali baada ya kuwepo migogoro iliyoathiri uzalishaji kiwandani hapo.

Kuhusu suala la madeni ya watumishi, ameagiza watafutwe na madai yaorodheshwe kwa ajili ya malipo, amewahakikisha wananchi hao kuwa suala la ajira ambazo zilipotea baada ya kiwanda kufungwa zitarudi kwa sababu Serikali inataka kuona kiwanda kikifanya kazi.

“Serikali imeamua kukichukua kiwanda hiki ambacho awali ilikikabidhi wakulima wa chai na kwamba itahakikisha lengo lake la kuboresh kilimo linafanikiwa na  wakulima wanaendelea kulima zao la chai. Hatutaki kusikia masuala ya Utega wala Mponde hapa si mahali pake.”
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mitambo ya kiwanda cha Chai cha Mponde wilayani Lushoto Novemba 1, 2018.  Kushoto kwake ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mitambo ya kiwanda cha Chai cha Mponde wilayani Lushoto akiwa katika ziara ya Mkoa wa Tanga, Novemba 1, 2018. Alikuwa katika ziara ya Mkoa wa Tanga.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kiwanda cha Chai cha Mponde wilayani Lushoto, Novemba 1, 2018. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, January Makamba, watatu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela na wanne kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Henry Shekifu.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa Bumbuli wilayani Lushoto akiwa katika ziara ya Mkoa wa Tanga, Novemba 1, 2018. 
 Wananchi wakimpungia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati  alipowasili kwenye kijiji cha Mponde wilayani Lushoto kukagua kiwanda cha chai cha Mponde na kuzungumza na wananchi, Novemba 1, 2018.



MISS TANZANIA AKABIDHIWA BENDERA KUIWAKILISHA NCHI MASHINDANO YA DUNIA

0
0

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amemkabidhi bendera ya taifa Miss Tanzania (2018) Queen Elizabeth Makune  atayewakilisha taifa katika mashindano ya urembo ya dunia "Miss World" yatayofanyika nchini China.

Akizungumza na vyombo vya habari Mwakyembe amesema kuwa mlimbwende huyo analiwakilisha taifa na amemtaka akawe balozi bora hasa katika kuitangaza lugha adhimu ya Kiswahili pamoja na maadili ya kiafrika.

Aidha Mwakyembe amemshukuru na kumpongeza mkurugenzi wa "The Look" na mwandaaji wa mashindano hayo Basila Mwanukuzi kwa kurudisha heshima ya mashindano hayo na ametenda haki katika katika tasnia hiyo ya ulimwende.Vilevile amewashukuru wadhamini wa mashindano hayo na kusema kuwa wao kama Wizara kwa kushirikiana na waandaaji wa mashindano hayo watahakikisha kuwa tasnia hiyo inaendelea kusimama imara, na kwa washindi na washiriki wa mashindano hayo watachukuliwa na shirika la ndege nchini ili wawe mabalozi wa kulitangaza taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi na muandaaji wa mashindano hayo Basila Mwanukuzi amesema kuwa tarehe 8 mwezi huu mrembo huyo ataondoka nchini  kuelekea  China ambako mashindano hayo yatafanyika na amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili Tanzania ing'are katika mashindano hayo.Mlimbwende anayewakilisha nchi katika mashindano hayo ambaye ni miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth Makune amesema kuwa anakwenda China kuwakilisha nchi na amejiandaa vya kutosha na amehaidi kuleta ushindi nyumbani.

Queen Elizabeth ameeleza kuwa atakuwa balozi katika kuitangaza lugha ya Kiswahili akiwa huko pamoja na utamaduni na maadili ya Kitanzania.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akikabidhi Bendera ya Taifa kwa Mshindi wa Miss Tanzania 2018,Queen Elizabeth Makune ambaye anataraji kwenda nchini Uchina katika Mashindano ya Urembo ya Dunia kuiwakilisha Tanzania katika Masuala ya Urimbwende
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, akizungumza na Waandishi wa habari kabla ya kukabidhi Bendera kwa Miss Tanzania 2018 , Queen Elizabeth Makune
 Miss Tanzania 2018 , Queen Elizabeth Makune akiongea na Waandishi wa Habari na kutoa Tumaini kwa Watanzania kuwa atatwaa taji la Urembo la Dunia
 Mkurugenzi wa Shindano la New Miss Tanzania , Basila Mwanukuzi akizungumza na Waandishi juu ya Safri ya Miss Tanzania Uchina na Fursa walizopata Warembo walioshiriki shindano hilo Mwaka huu.
Afisa Uhusiano wa Baraza la Sanaa nchini, (BASATA), Agness Kimwanga akizungumza jambo kwa niaba ya katibu Mkuu wa BASATA wakati wa makabidhiano ya Bendera kwa Miss Tanzania 2018

BBC DIRA YA DUNIA ALHAMISI 01.11.2018

0
0

MAHAKAMA YAAMBIWA FREEMAN MBOWE MGONJWA, APELEKWA AFRIKA KUSINI KWA MATIBABU YA MOYO

0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya Jamii

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), Freeman Mbowe anayekabiliwa na kesi ya Uchochezi namba 112 ya mwaka huu amesafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini akiwa mahututi kwa ajili ya matibabu ya moyo na shinikizo la damu.

Hayo yameelezwe leo Novemba Mosi mwaka huu na Wakili Peter Kibatala mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Wilbard Mashauri wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya awali, (PH).

Wakili Kibatala ameieleza Mahakama kuwa alimuhoji mdhamini wa Mbowe, Grays Celestine na akamueleza kuwa Mbowe amesafirishwa jana jioni akiwa mahututi kuelekea Afrika Kusini na nyaraka za usafiri na matibabu zitawasilishwa kwa barua mahakamani.

Kibatala alieleza kuwa Mbowe amekuwa akifika mahakamani mara kadhaa bila kukosa, hivyo adhabu kwamba kueleza anaidharau mahakama kwani hata kitendo cha kumtuma mdhamini wake si jambo la dharau.Kutokana na taarifa hiyo, Wakili wa Serikali Mkuu Faraja Nchimbi ameiomba Mahakama itoe amri ya kumkamata mara moja Mbowe ili ajieleze kwani dhamana aliyopewa na mahakama isifutwe kwa kushindwa kuiheshimu.

Baada ya mdhamini huyo kueleza hayo, Hakimu Mashauri alimuuliza kama ana nyaraka ya kuithibitishia mahakama kuwa Mbowe amesafiri nje ya nchi kwa Matibabu lakini mdhamini huyo alidai kuwa hana na kwamba mshtakiwa akirejea atawasilisha nyaraka za safari na Matibabu kwa mahakama na upande wa mashtaka. 

Pia anaendelea kufanya mawasiliano ili aweze kutumia kwa Fax.Hata hivyo wakili Nchimbi alidai, kutokana na taarifa hizo bado analazimika kueleza mdhamini hajaonesha uzito wowote kwa kuwa tunata kujua ameenda nje kwa matibabu, lini, katika taasisi gani na nchi gani.Ameongeza labda aliondoka akiwa mahututi lakini waliomsindikiza wangeweza mdhamini, hivyo hao wao upande wa mashtaka hayo wanaona ni muendelezo wa dharau ya mshtakiwa kwa kuwa alikwisha pewa onyo mara mbili.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mashauri amekubaliana na hoja hizo za upande wa mashtaka na kwamba mshtakiwa huyo anapaswa kuja mahakamani kueleza kwa nini dhamana yake isifutwe.Hata hivyo Hakimu Mashauri amesema iwapo mshtakiwa hatopeleka vielelezo atatoa amri ya kukamatwa ili ajieleze kwani ni asifutiwe dhamana kwa kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa na mahakama.

Mbali na Mbowe, Washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo, wanatetewa na wakili Peter Kibatala ni Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika, mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee, mbunge wa bunda, Esther Bulaya, Mbunge wa 

Tarime Mjini, Esther Matiko na katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Vincent Mashinji. Huku Peter Msigwa anatetewa na wakili Jamuhuri 
Johnson.Washtakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13, ikiwemo kula njama, kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari 1 na 16, 2018, Dar es Salaam.

TCRA YATANGAZA KUWACHUKULIA HATUA WAVUNJIFU WA MAADILI KATIKA MITANDAO

0
0
Na Khadija Seif,Globu ya jamii

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) imesema haitasita kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote wanaopotosha jamii na vitendo vya uvunjifu wa maadili ya kitanzania kwa kujirekodi na kisha kusambaza picha za video za utupu mtandaoni.

Akizungumza leo Dar es salaam Mkurugenzi wa TCRA Joannes Karungura amesema kutokana na video inayosambaa kwa sasa nchini ikimuhisha msanii wa filamu nchini Wema Sepetu imeamua kumfikisha mahakamani ili asomewe shtaka linalomkabili na kwamba huo ni mwanzo tu kwani wote ambao wanaokiuka maadili mitandaoni watachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha Karungura amebainisha kuwa sheria zitaendelea kufuatwa na kwa yoyote atakayekiuka maadili ya kitanzania kama alivofanya Wema 
Sepetu na wengine ambao kesi zao ziko Kwenye taratibu kufikishwa 
mahakamani basi watatumikia kifungo cha miaka Saba au kutoa faini 
ya Sh.millioni saba.

Ametoa mwito kwa Watanzania kuwa ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha jamii yetu inakua na maadili,tabia njema pamoja na desturi nzuri ili kukijenga kikazi cha kesho na vinavokuwa maadili mazuri na hofu ya kutokufanya vitendo viovu.

Pia amewataka watu wenye picha pamoja na video chafu kufuta mara 
moja kwani TCRA wana mikakati mizito kwa watu ambao wanahifadhi 
pamoja na wanaosambaza picha hizo kuwafikisha Kwenye sheria 
ichukue mkondo wake.

DC Katambi atinga Stesheni ya Dodoma, Atishia Kuwatumbua

0
0
Charles James

MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobas Katambi ametishia kuwatumbua watumishi wa Stesheni ya Treni endapo hawatotekeleza maagizo maagizo yake.

DC Katambi ametoa kauli hiyo leo alipofika katika stesheni hiyo baada ya kupigiwa simu na abiria waliokua wamekwama tangu jana kufuatia treni mbili kukutana.

Mkuu huyo wa Wilaya pamoja na kuzungumza na abiria hao ambao aliwaomba kutulia huku akiuagiza uongozi wa Reli kuwatafutia usafiri mwingine wa kuwapeleka jijini Dar es Salaam pia alikagua mazingira ya stesheni hiyo kutokana na kulalamikiwa na wasafiri hao.

“ Nimepita kukagua mazingira ya stesheni yetu, nimekutana na mambo mengi ya hovyo ambayo yanaweza kutatulika ili kuondoa kero za abiria wetu ambao kimsingi ni Watanzania wenzetu ambao wanalipa kodi ya Nchi yao kwa kulipa nauli.

“ Stesheni kubwa kama hii haina vyoo vya kutosha na vilivyopo vimeziba kutokana na wingi wa vinyesi, maji hakuna pia kwa sababu stesheni inadaiwa na nimewaagiza kulipa deni wanalodaiwa. Na wasipotekeleza basi wajue nitawatumbua,” amesema DC Katambi.
MKUU wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobas Katambi

WALIOMALIZA CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI WAHAMASISHWA KUCHANGIA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA CHUO HICO

0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Anna Mghwira akizungumza wakati wa uzinduzi wa Harambee ya kuchangia ujenzi wa miundombinu katika Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) .
 Baadhi ya Watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Anna Mghwira wakati wa uzinduzi ya kuchanga ujenzi wa Miundombinu ikiwemo Hosteli katika chuo hicho. 
 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika,Moshi (MoCU) Prof,Faustine Bee akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katik aukumbi wa mikutano wa Ushirika . 
 Baadhi ya Viongozi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) wakiwa katika mkutano huo wa uzinduzi . 
 Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee ya kuchangia ujenzi wa Miundombinu katika Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Noel Nko ambaye pia ni mhitimu wa chuo hicho akizungumza juu ya wazo la kuwashirikisha Wahitimu wote wa Chuo hicho tangu mwaka 1963 katika kuchangia ujenzi wa miundombinu Chuoni hapo. 
 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Prof ,Faustine Bee akimueleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira alipotembelea baadhi ya maeneo katika Chuo hicho. 
 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi wa Harambee ya kuchangia ujenzi wa miundombinu katika chuo hicho.




Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini 

WANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) wanaoishi katika hosteli za nje ya chuo hicho wako kwenye mazingira hatarishi kutokana na baadhi yao kufanyiwa vitendo vya kinyama huku ikidaiwa wengine tayari wamepoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha.

Matukio mengine yanayotajwa kuwafika Wanafunzi hao ni pamoja na kuvamiwa na kuporwa mali ,kujeruhiwa kwa kuchomwa visu na kupigwa hasa kwa wanafunzi wa jinsia ya Kike jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limechangia baadhi yao kuathirika kimasomo na hata kupunguza hali ya kuendelea na masomo.

Kutokana na hali hiyo, Wahitimu wa Chuo hicho kuanzia mwaka 1963 wameanza kampeni ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa hosteli yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1000 ili kupunguza changamoto zilizopo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Harambee hiyo Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Anna Mghwira amesema miundombinu ya Chuo kikuu cha Ushirika Moshi haikidhi mahitaji ya sasa na ya baadae kwa wanafunzi wa elimu ya juu na kwamba kwa kiasi kikubwa inahitaji kuboreshwa.

Dkt Mghwira amesema hosteli zilizopo sasa zilizojengwa miaka ya 60 na 70 , pamoja na kuwa katika hali ya uchakavu zinauwezo wa kuchukua wanafunzi 766 tu ikiwa ni sawa na asilimia 20 ya idadi ya wanafunzi waliopo na ambayo inaendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka .

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) Prof ,Faustine Bee alisema jambo ambalo limeibuliwa na wahitimu wa chuo hicho ni jema na kwamba Uongozi wa chuo utaendelea kuwaonga mkono katika jitihada hizo.

“Niwashukuru kwa kuja na wazo hili ,nimpongeze Noel Nko ambaye amejitolea kuwaongoza wenzake katika jambo hili,sisi kama viongozi na wadau tunawashukuru na tunawaunga mkono kaitka jitihada hizi,mchango wao ni mkubwa na unachangia katika kuunga mkono juhudi za rais Magufuli ya kuona taasisi za elimu zinakuwa na mundombinu iliyobora”alisema Prof Bee .

Alisema uwepo wa miundombinu bora kutatoa nafasi kwa wanafunzi kujifunza kwa bidii huku akiishukuru Serikali kwa kutoa kiasi cha Sh Bil 1.3 ambazo tayari zimesaidia katika kuboresha baadhi ya miundombinu ya chuo hicho.

“Hata hivyo bado hatujakamilisha ,tunamahitaji mengine makubwa kama barabara za ndani hazijakamilika,tumefanya tu sehemu ,lakini pia upande wa malazi kwa wanafunzi ni changamoto ,wanafunzi wetu kiasi cha silimia 70 wanakaa nje ya chuo na kati ya hao kuna vijana wa kike ambao wanahitaji uangalizi mkubwa”alisema Prof Bee.

Naye Mwenyekiti wa Harambee hiyo,Noel Nko alisema wakati huu chuo kikiendelea kukua tuliona ni vyema wanafunzi wote waliohitimu chuoni hapa tangu mwaka 1963 tuone ni kitu gani tunaweza tukafanya kwa chuo zikiwa ni moja wapo ya kuunga mkono serikali.

“Niombe kutoa hamasa kwa wahitimu wote wa Chuo Kikuu cha Ushirika zoezi hili tulifanye kwa moyo ,hamasa itakuwa kwa mwenye kiasi chochote cha fedha atachangia na harambee hii itakuwa endelevu ,tutaifanya wanaushirika nchi nzima na niwaombe wanaushirika kote nchini ,wakiwa ni warajisi wa mikoa,maafisa ushirika wa halmashauri,popote pale walipo wahamasihe zoezi hili kwa nguvu zote”alisema Nko. 

Kukamalika kwa harambee hii kwa kiasi kikubwa litasaidia kuboresha ulinzi na usalama kwa wanafunzi pamoja na mali zao sambamba na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kujisomea kwa wanafunzi na pia itasaidia wanafunzi wengi wa kike kupata elimu bora .

HII NDIO HUKUMU YA WEMA SEPETU ENDAPO ATAKUTWA NA HATIA

0
0

DC AJITOSA KUHAMASISHA UHIFADHI WA MAZINGIRA WILAYANI NAMTUMBO

0
0
MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo ameamua kufanya ziara katika Kata za Rwinga na Namtumbo kwa ajili ya kuhamasisha uhifadhi wa mazingira na kusikiliza kero za wananchi.

Kizigo amefanya ziara hiyo jana ambapo amepata nafasi ya kuelezwa baadhi ya kero za idara ya maji na mazingira ya mji wa Namtumbo (NAUWASA) kutoza flat rate ya Sh.7,000 kila mwezi kwa wananchi kulipia maji, wakati maji yanatoka mara moja kwa wiki inayosababisha maji kutoka mara nne kwa mwezi.

Taarifa ya ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya ambayo imetolewa kwa vyombo vya habari inaeleza kuwa Mkuu wa idara ya maji alitoa majibu kwamba wanatoza 7000 flat rate kwasababu hakuna mita za maji katika baadhi ya maeneo.

Hata hivyo Mkuu wa wilaya ameiagiza idara ya maji iwaandikie EWURA 
kuomba kupewa mita za maji haraka ili wananchi walipe kwa haki kutokana na maji wanayoyatumia kwani sio haki kuwalipisha Sh.7000 kwa kuchota maji mara nne tu kwa mwezi tena kwa uchache.

Pia wananchi walitoa malalamiko yao kwa Mkuu wa Wilaya huyo kuwa katika kituo cha afya Namtumbo kuna wakati dawa hawapati na 
wanaambiwa wakanunue kwenye maduka ya dawa. Pia hakuna huduma za haraka kwani watendaji wa kituo cha afya wanachukua muda mrefu kuingiza taarifa kwenye komputa badala ya kuhudumia mgonjwa.

Hivyo Kizigo amemuagiza Mganga Mkuu wa wilaya ahakikishe kabla dawa hazijaisha kabisa awe ameshaagiza zingine ili ziwepo wakati wote. Lakini pia ahakikishe anaagiza dawa zinazotosha kata mbili (Rwinga na Namtumbo) kwani ni dhahiri kituo kinazidiwa na idadi ya wagonjwa kwani kinahudumia kata mbili badala ya moja.

Kuhusu matumizi ya kompyuta amemuagiza Mganga Mkuu wa wilaya ahakikishe mafunzo kwa vitendo yanatolewa na kufanyika ili kuongeza kasi ya watumishi kuhudumia watu kwa kutumia kompyuta kwani bado hawajazizoea katika kufanya kazi zao. Pia wakati huohuo kama kuna 
mgonjwa amezidiwa waweke kipaumbele katika kumhudumia hata 
kama hawajamaliza kuingiza taarifa kwenye kompyuta.
MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo akizungumza na Wakazi wa Kata za Rwinga na Namtumbo,alipofanya ziara yake  kwa ajili ya kuhamasisha uhifadhi wa mazingira na kusikiliza kero za wananchi.Kizigo amefanya ziara hiyo jana ambapo amepata nafasi ya kuelezwa baadhi ya kero za idara ya maji na mazingira ya mji wa Namtumbo (NAUWASA) kutoza flat rate ya Sh.7,000 kila mwezi kwa wananchi kulipia maji, wakati maji yanatoka mara moja kwa wiki inayosababisha maji kutoka mara nne kwa mwezi.
 Wananchi wakimsikiliza MKUU wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Sophia Kizigo .

SERIKALI YATOA BILIONI 21 UJENZI MIUNDOMBINU MTWARA

0
0
Na Evaristy Masuha – Mtwara 

Serikali kupitia mradi wa uendelezaji miji Mkakati (Tanzania Strategic Cities Project) imetoa bilioni 21.7 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimblai ya maendeleo katika Manispaa ya Mtwara mikindani. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa barabara 4 za mitaa kwa kiwango cha lami, Ujenzi wa maeneo matatu ya kupumzikia (Recreation Center), mfereji mkubwa wa kuondoa maji ya mvua, ujenzi wa soko la kisasa pamoja na kituo cha daladala eneo la Mikindani. 

Akizungumza leo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo iliyofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda amesema fedha hizo zimetolewa kwa mkopo na Benki ya dunia na kwamba ujenzi wa miradi hiyo yote inatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2019. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutaufanya mji wa mtwara kuwa na muonekano mzuri na kwamba hiyo ndiyo hatua nzuri kuifanya Manispaa kuwa na sifa ya kuwa Jiji. “Naamini baada ya kukamilika miradi hii Mtwara itakuwa sehemu nyingine na pengine inaweza kupata sifa ya kuelekea kuwa jiji”. Amewataka vijana waliopata nafasi ya kuajiliwa katika ujenzi wa miundombinu hiyo kuwa waamifu ili kujijengea imani kwa waajiri. 
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (mwenye shati Jeupe) akikagua ujenzi wa mfereji wa maji kutoka Skoya, Nabwaba, Shakuru hadi Mtepwezi.
Mfereji wa kuondoa maji kutoka Skoya, Nabwada Shakuru hadi Mtepwezi

Ujenzi wa soko la Chuno 

 

CCM NYAMAGANA YAWATIMUA MAKATIBU WAWILI KWA UDHALILISHAJI

0
0
NA BALTAZAR MASHAKA, MWANZA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyamagana kimewavua uongozi Makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani wilayani humo kwa tuhuma na makosa ya kukidhalilisha na kukichafua kwenye jamii.
Pia kimelaani matukio hayo yaliyofanywa na viongozi hao wasio na hofu ya Mungu,katiba na sheria za nchi ambao wanakiangusha CCM kwa kufanya vitendo viovu na mambo ya ovyo yanayodhalilisha.

Akitoa tamko la kuwavua nyadhifa za uongozi makatibu hao wa Uenezi kwenye mkutano wa dharura wa Kamati ya Siasa ya Wilaya mbele ya vyombo vya habari Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kalli alisema viongozi wa namna hiyo hawatavulimiwa kwa sababu wanafedhehesha chama.

“CCM inalaani vikali mambo yaliyofanywa na viongozi hao kwenye jamii na hatua hii itakuwa fundisho kwa viongozi wenye tabia kama hizo,maana si utamaduni na maadili ya CCM kwani inawataka wawe waadilifu na waaminifu kwenye nafasi zao.Hivyo tutafuatilia tabia, mienendo na maadili ya kila kiongozi wa CCM aliyepo madarakani,”alisema.

Kalli alieleza kuwa Kamati ya Siasa ya Wilaya imechukua hatua hiyo na kutoa tamko hilo Watanzania wajue ili viongozi wenye tabia chafu zisizofaa kwenye jamii waache kwa kuwa CCM haitawavumilia.

Alifafanua kuwa Katibu wa Siasa na Uenezi wa Kata ya Buhongwa Hassani Bushagama, anadaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule moja ambayo haikutajwa ambapo alitoroka na kutokomea tangu Julai mwaka huu.

Kallia alisema Katibu wa Siasa na Uenezi wa Kata ya Mkolani Zephelin Maiko Shibugulu naye amekumbwa na panga hilo akidaiwa kukutwa akimlawiti kijana wa kiume mwenye umri kati ya miaka 16 na 19 , Oktoba 26 mwaka huu saa 11:00 jioni baada ya kumnunulia supu ya nyama sahani tatu kabla ya kumfanyia kitendo hicho, kinyume na katiba ya CCM toleo la 2017 na kanuni za uongozi na maadili.

Hata hivyo mtuhumiwa pamoja na kijana huyo walichoropoka na kukimbia na haijulikani walipo na kutokana na kitendo hicho Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ilimvua Bushagama uongozi Oktoba 23, mwaka huu na kutangaza nafasi hiyo ijazwe na kiongozi mwenye sifa Novemba 3, mwaka huu, huku halmashauri hiyo ikimvua Shibugulu wadhifa huo Oktoba 29.

Awali akifungua kikao kazi cha kamati ya siasa ya wilaya kabla ya tamko hilo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana Zebedayo Athuman alisema wamehangaika kukitoa chama kwenye hali mbaya lakini viongozi hao na wengine wenye tabia hizo wanachafua taswira na sura ya chama hicho.

Alidai kuwa viongozi wa aina hiyo ni zao la mchujo rahisi wakati wa kutafuta na kupata viongozi, mchujo ambao umesababisha CCM ipate viongozi wa ajabu wasio na nidhamu, wanaokiuka maadili na kufanya mambo ya ovyo kwenye jamii wanakati wanapaswa kuwa kioo.

Zebedayo alisema kuwa wanataka kujenga nidhamu kati ya watendaji wa chama maana nidhamu haipo na wengine wanafanya mambo yasiyofurahisha na kuwataka viongozi kuwa makini wanaposhughulikia tuhuma, wafuate taratibu bila kuathiri vyombo vya dola.

“ Zipo tuhuma mbaya zinakifedhehesha chama na zikithibitika tutakuomba uturejeshee uanachama wetu.Pia tukifanya maamuzi kwa mihemko, kesho utakuta Zebedayo kasingiziwa ni muhimu taratibu zifuatwe na ili kuepuka kupata viongozi wanaoharibu sifa ya CCM, tutaomba juu watupe nafasi ya kuchuja watu tupate wenye maadili na uadilifu uliotukuka,”alisema.

Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa kitendo cha viongozi hao kuchafua sura ya CCM lazima wakae pembeni na akaonya wasifanye mzaha na mambo ya chama kwani cheo ni dhamana na lazima wajue hivyo.


Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kallia akisoma tamko la kuwavua uongozi makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani, Hassani Bushagama na Zephelin Maiko Shibugulu, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu wilayani Nyamagana jana.
Katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Salum Kallia akisoma tamko la kuwavua uongozi makatibu wa Siasa na Uenezi wa kata za Buhongwa na Mkolani, Hassani Bushagama na Zephelin Maiko Shibugulu, mbele ya wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu wilayani Nyamagana jana.waliokaa mbele kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Zebedayo Athuman, Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire na wa kwanza kulia ni Katibu wa Siasa na Uenezi Musptapha Banigwa
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Zebedayo Athuman akifungua kikao kazi cha kamati ya siasa ya wilaya hiyo jana, kushoto ni Katibu wa Chama wilayani humo Salum Kalli na kutoka kulia wa kwanza ni Katibu wa Siasa na Uenezi Mustapha Banigwa na Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana, Zebedayo Athuman akifungua kikao kazi cha kamati ya siasa ya wilaya hiyo jana, kushoto ni Katibu wa Chama wilayani humo Salum Kalli na kutoka kulia wa kwanza ni Katibu wa Siasa na Uenezi Mustapha Banigwa na Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire. Picha na Baltazar Mashaka

LUGOLA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA VITUO VYA POLISI TABATA,BUGURUNI NA KUTOA MAAGIZO YA DHAMANA KUTOLEWE SAA 24

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiingia Kituo cha Polisi Tabata, jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha polisi hicho kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini. Pia Lugola alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha polisi Buguruni jijini humo leo
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiwaita majina watuhumiwa (hawapo pichani) waliopo katika mahabusu ya Kituo cha Polisi cha Tabata, jijini Dar es Salaam, leo, ili kujua aina ya makosa waliotuhumiwa pamoja na kujua muda waliokaa katika kituo hicho endapo imefika zaidi ya saa 24 bila kupewa dhamana. Pia Lugola alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha polisi Buguruni jijini humo leo. Lengo la ziara hiyo ni kuboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akimuhoji Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Tabata, jijini Dar es Salaam, Bakari Gothi (watatu kushoto) kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji kazi katika kituo chake, mara baada ya Waziri huyo kufanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho leo. Pia Lugola alifanya ziara kama hiyo katika Kituo cha Polisi Buguruni jijini humo. Lugola anafanya ziara ya kushtukiza katika vituo mbalimbali nchini kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akionyeshwa taarifa za watuhumiwa waliopo mahabusu ya Kituo cha Polisi cha Buguruni, jijini Dar es Salaam, leo, wakati Waziri huyo alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo hicho kwa lengo la kufuatilia utendaji kazi. Pia Lugola katika siku hiyo hiyo alifanya ziara ya aina hiyo katika kituo cha polisi Tabata, jijini humo. Kulia ni Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi Buguruni, Adam Maro.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimpa maelekezo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni, mara baada ya Waziri huyo kumaliza ziara yake ya kushtukiza katika Kituo cha Polisi cha Tabata na Buguruni jijini Dar es Salaam, leo. Lugola alisema lengo la ziara hiyo ni kuboresha utendaji kazi wa Jeshi la Polisi nchini. Kushoto ni Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi ya Buguruni, Adam Maro. 
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Na Felix Mwagara, MOHA

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha Polisi Tabata na Buguruni vya jijini Dar es Salaam ili kujua kama maagizo yake aliyoyatoa katika vituo mbalimbali kama yameanza kufanyiwa kazi.

Waziri Lugola alianza ziara yake saa 2:45 asubuhi kwa kuibukia katika kituo cha Tabata na moja kwa moja alianza kuulizia mahudhurio ya wafanyakazi wote wa kituo hicho na kujua nani yupo kazini na nani hayupo na kwanini hajafika ofisini hapo kwa muda huo wa asubuhi.

Wakati alipokua kituoni hapo, pia Lugola alikichukua kitabu cha taarifa za watuhumiwa wote waliopo mahabusu na baadaye kuelekea katika mahabusu hiyo akiwahoji watuhumiwa kwa kuwaita kwa majina kujua makosa yao yaliyoyafanya wawepo kituoni hapo.

Lugola baada ya kumaliza katika kituo hicho, saa 5:27 alielekea kimyakimya katika kituo cha Polisi cha Buguruni, na aliwahoji watuhumiwa waliopo mahabusu katika kituo hicho na kujua makosa mbalimbali yanayowakabili huku polisi wapepelezi wa tuhuma zao wakiwepo katika tukio hilo.

Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara yake, Lugola alisema, alitoa maagizo mbalimbali katika ziara zake nchini, hivyo anafuatilia kujua maagizo yake yameanza kufanyiwa kazi au bado baadhi ya vituo kama wameyapuuza.

“Lengo la hii ziara yangu ni kuboresha utendaji kazi wa vituo vya polisi nchini, sijaja kumuadhibu mtu mimi, hivyo msiwe na wasiwasi, bali kilichonifanya hapa nije nikufuatilia maagizo mbalimbali ambayo niliyatoa kama kweli mnayafanyia kazi,” alisema Lugola.

Maagizo aliyoyatoa mwezi miwili iliyopita katika ziara zake mikoa mbalimbali nchini ni kuhakikisha pikipiki zinaondolewa katika vituo vya polisi, dhamana zitolewe saa 24 ikiwemo Jumamosi na Jumapili, pamoja na polisi kutowabambikizia kesi wananchi.

Hata hivyo, Lugola alivipongeza vituo hivyo vya polisi vilivyopo wilayani Ilala na pia Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma alichokitembelea wiki iliyopita, kwa kuanza kuyafanyia kazi maagizo yake aliyoyatoa zikiwemo baadhi ya bodaboda, zimeondolewa vituoni na zilizobaki zina kesi mahakamani.

“Nilifanya ziara ya kushtukiza pale Kituo cha Polisi cha Tabata, na pia nimekuja hapa Buguruni, kwakweli wameaanza kuyafanyia kazi maagizo yangu, pikipiki zote nilizozikuta zinasababu yakuwepo hapo, na si vinginevyo kama walivyokua wanaziweka kiholela hapo awali,” alisema Lugola.

Pia lugola aliwataka Makamanda wa polisi nchini kuwafuatilia askari wao kwa umakini ili kujua utendaji kazi wao, na pia Waziri huyo alisema atakua anafanya ziara kama hizo mara kwa mara hivyo vituo vya polisi nchini viwe sawa muda wote.

“Hamjui siku wala saa ambapo nitakuja, tufanye kazi, tuwahudumie wananchi, tusiwaonee wananchi, tujitume kufanya kazi kwa weledi, sitamvumilia mtu ambaye atavunja utaratibu,” alisema Lugola.

MAWAKALA WA NMB WAPEWA SEMINA KUONGEZA UFANISI KATIKA KUTOA HUDUMA BORA

0
0

Meza kuu kwenye semina kwa mawakala wa Benki ya NMB wa jijini Dar es Salaam ikipiga picha ya pamoja na mawakala bora kwa mwaka 2018 wa Benki hiyo kwa kanda ya Dar es Salaam.


Meneja Mwandamizi NMB Wakala, Tito Mangesho (mbele) akiwasilisha mada kwenye semina kwa mawakala wa Benki ya NMB wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
Mmoja wa mawakala wa NMB akiuliza swali kwenye semina hiyo.
Meneja wa NMB Wakala Kanda ya Dar es Salaam, Kisamo Edwin akizungumza na mawakala wa NMB kwenye semina kwa mawakala wa Benki hiyo wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd akizungumza na mawakala wa NMB kwenye semina kwa mawakala wa Benki hiyo wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
Sehemu ya mawakala wa NMB waliohudhuria semina hiyo wakionesha vyeti vyao mara baada ya kukabidhiwa.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd (kulia) akimkabidhi cheti pamoja na zawaadi wakala bora kwa mwaka 2018 Kandaa yaa Dar es Salaam kwenye semina kwa mawakala wake wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam.
 
 
BENKI ya NMB imetoa semina kwa mawakala wake wanaotoa huduma za kifedha maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, lengo likiwa ni kuboresha huduma na ufanisi kwa wateja wa NMB wanaojipatia huduma za kibenki kwa mawakala hao.
Akizungumza katika semina hiyo, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd alisema semina hizo ni mwendelezo wa mafunzo kwa mawakala wa NMB nchi nzima ili kuboresha huduma, kukuza biashara zao na kuleta ufanisi katika kumuhudumia mteja.

Alisema NMB ndio benki pekee yenye idadi kubwa ya mawakala zaidi ya 6,000 ambao hutoa huduma nchi nzima huku ikiwa na matawi 228 na mashine za ATM zaidi 800 lengo likiwa kusogeza huduma kwa wateja wake.Mafunzo haya yanaenda sambamba na kuwapongeza mawakala waliofanya vizuri kwa mwaka huu katika kazi zao, ili kuleta chachu kwa wengine kufanya vizuri zaidi.

Akiwasilisha mada za mafunzo kwa mawakala, Meneja Mwandamizi NMB Wakala, Tito Mangesho alisema mikakati ya NMB ni kuongeza idadi ya wateja huku ikitumia njia rahisi na salama ya kuwahudumia watanzania. Alisema malengo mengine ni pamoja na kuongeza unafuu wa gharama zake na uharaka wa kuwahudumia wateja, kupunguza msongamano na kuboresha kamisheni kwa mawakala wake.

KEMI GOES NEXT LEVEL IN THE ART OF DESIGN

0
0
 Models shows the fashion work of Kemi
 Models shows the fashion work of Kemi
Models shows the fashion work of Kemi TANZANIA’s fashion designer, Kemi Kalikawe, has gone next level in fashion designing showbiz after her brilliant performance in many world class events. The just ended International Young Fashion Designers Tour at Hyatt Kilimanjaro Hotel in the city proved the designer is now a force to reckon as she parades her designs on the global arena. The feat earned the designer a huge international appeal, especially in Panama where her rare designs applied to the mixed Central American audience and has drawn a huge number of fans. The Tanzanian rose high above the huge names in designing during the International Young Fashion Designers Showcase Tour of Dar es Salaam that attracted many internationally acclaimed designers. 

 Kalikawe, who showcased her designs under Naledi Tanzania banner, has also participated in the previous fashion shows of Iceland and Panama prior to the Dar es Salaam fashion gala and will go to China for the last show. Her 2 central designs are made from Barkcloth also called 'The Cloth of Kings' a sustainable cloth made from a tree in her home town Bukoba. These center pieces of her collection have stood out in their architectural and yet feminine cuts, inspired by her interior design background. 

Others who paraded their designs alongside Kalikawe included Tony Vergara and Veronica Angel from Panama, Hildur Yeoman from Iceland. Others were Junne Liu and Jarel Zhang from China, Lina Yingzi and Yuzhu from Kanoe while Mary Yu, Kenny Li, Singchin Lo and Mountain Yam were from Hong Kong. Also attended the International Young Fashion Designers Showcase Tour of Dar es Salaam had government officials with the guest of honour being Hon. Mizengo P. Pinda, former Prime Minister of Tanzania. Other officials were Ambassador Ramadhani M. Mwinyi, Mr. Xu Chen, Charge d'affaires ad interim of the Embassy of China in Tanzania, Mr Godfrey Lebejo Mngerza, director of BASATA, Hon Rtd Judge Thomas Mihayo, Chairman of Tanzania Tourists Board (TTB), Mr Joseph Kahama, Secretary General of Tanzania China Friendship Promotion Association and various stakeholder of designing and modeling sectors from in and outside the country. Kalikawe used this rear international platform to give a chance to upcome designers to also showcase their work at the opening cocktail event. 

This opportunity helped to focus on talented youth who can later be promoted to the international level as well. Delighted with early success, Kalikawe said the international events have promoted her and her works very much and given her a confidence in her career. “The international level events have opened doors to showcase my designs to the world. I am getting calls from people in Hong Kong interested in buying my work. I feel honoured since I will be able to shine a light on the talent of Tanzania in the design sector. More over each trip has been a journey of sight seeing, cross culture friendship building with fellow designers and wonderful memories. 

One distinct memory of wander was attending a special dinner in celebration of us designers hosted by at the First Lady of Panama, at the presidential residents, what an honer is was. I look forward to the last stop in China coming soon,” she joyfully said. This series of the shows have been initiated by Dr. Annie Wu and supervised by an institution called Belt and Road International Young Artist Development Centre and organised by PR Network Hong Kong. The series of fashion designing events have been already staged in Reykjavik, Iceland ,Panama City and now in Dar es Salaam. The next event will be in Zhuhai (China).

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 2,2018

0
0

















BREAKING NEWZZZZ:AMBAR RUTY, JAMES DELICIOUS WAFIKISHWA KORTINI KWA TUHUMA ZA KUSAMBAZA PICHA ZA UTUPU MITANDAONI

0
0
Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

MCHEZA video Rutyfiya Abubakal a.k.a Amber Ruty , Said Bakari (kijana wake AmberRuty) na kijana  James Charles maarufu kama James Delicious anayedaiwa kuwa shoga wamefikishwa  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka yao kwa kupiga picha za utupu na kusimbaza mitandaoni.

Washitakiwa hao wamefikishwa mahakamani hapo leo ..endelea kufuatilia Michuzi Blog kupata habari kamili.

 MCHEZA video Rutyfiya Abubakal a.k.a Amber Ruty , Said Bakari (kijana wake AmberRuty) (hayupo pichani) wakiwa kwenye moja ya chumba cha Mahakama mara baada ya kufikishwa   Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka yao kwa kupiga picha za utupu na kusimbaza mitandaoni.
MCHEZA video Rutyfiya Abubakal a.k.a Amber Ruty , Said Bakari (kijana wake AmberRuty)  pamoja na James Charles maarufu kama James Delicious anayedaiwa kuwa shoga wakielekea kwenye moja ya chumba cha Mahakama mara baada ya kufikishwa   Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka yao kwa kupiga picha za utupu na kusimbaza mitandaoni.
 MCHEZA video Rutyfiya Abubakal a.k.a Amber Ruty , Said Bakari (kijana wake AmberRuty)  wakifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka yao kwa kupiga picha za utupu na kusimbaza mitandaoni.
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live




Latest Images