Mkurugenzi wa NMB – Bi. Ineke Bussemaker akichangia kwenye mdahalo ulioandaliwa na KPMG juu ya nafasi ya Tekinolojia kwenye ukuaji wa Biashara Nchini uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkurugenzi wa Tehama, Wizara ya Kazi, Usafirishaji na Mawasiliano – Melembwa Munaku, Mkurugenzi wa Selcom – Sameer Hiurji na Mkurugenzi wa Tehama kutoka KPMG – Anthon Nzamu.
Mkurugenzi wa NMB – Bi. Ineke Bussemaker akichangia kwenye mdahalo ulioandaliwa na KPMG juu ya nafasi ya Tekinolojia kwenye ukuaji wa Biashara Nchini uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkurugenzi wa Tehama, Wizara ya Kazi, Usafirishaji na Mawasiliano – Melembwa Munaku, Mkurugenzi wa Selcom – Sameer Hiurji na Mkurugenzi wa Tehama kutoka KPMG – Anthon Nzamu.
Mkurugenzi wa NMB – Bi. Ineke Bussemaker akichangia kwenye mdahalo ulioandaliwa na KPMG juu ya nafasi ya Tekinolojia kwenye ukuaji wa Biashara Nchini uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkurugenzi wa Tehama, Wizara ya Kazi, Usafirishaji na Mawasiliano – Melembwa Munaku, Mkurugenzi wa Selcom – Sameer Hiurji na Mkurugenzi wa Tehama kutoka KPMG – Anthon Nzamu.
BENKI ya NMB imesema itaongeza kiwango cha mikopo inayoitoa kwa kampuni ndogo na za kati mara mbili zaidi na kufikia Shilingi trilioni tatu kwa miaka mitatu ijayo. Hayo yalisemwa na Mkurugenzi Mtengaji wa benki hiyo Bi – Ineke Bussemaker wakati akizungumzia udhamini wa NMB kwa hafla ya Kampuni Bora 100 zamwaka 2018/2019 (Top100 Mid-sized Companies' Survey).
Kwa miaka mitatu iliyopita, NMB imetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi trilioni 1.5 kwa kampuni ndogo na za kati. Akizungumza katika uzinduzi wa utafiti wa Kampuni Bora 100 za mwaka 2018/2019 jijini Dar es Salaam jana, Bi. Bussemaker alisema kampuni zinazowekeza katika kufanya biashara kidigitali zipo katika nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri kibiashara.
"Hatima ya uchumi wa nchi upo katika kufanya biashara kidijitali ili kuhakikisha mifumo ya utendaji inakwenda kwa kasi,” alisema na kuongeza kuwa kampuni zilizoweza kuweka mifumo sawa ya dijitali zipo katika nafasi bora zaidi ya kupata mikopo kutoka katika benki yake.
Alisema Benki ya NMB inazidi kuwekeza katika mifumo ya utoaji huduma kwa njia za kidijitali ili kuwafikia wananchi wengi zaidi wanaohitaji huduma zake nchini kote. Kampuni Bora 100 Tanzania ni shindano linaloendeshwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited kwa kushirikiana na KPMG.
Mbali na NMB, wadhamini wengine wa Kampuni Bora 100 za mwaka 2018/2019 ni pamoja na Soko la Hisa la Dar es Salaam na Azam Media na Hoteli ya Hyatt Regency.
Akitoa matokeo ya utafiti wa Kampuni Bora 100 za mwaka 2018/2019, Mtafiti kiongozi wa kampuni ya AZ Advisory, Dk. Remidius Ruhinduka, alisema asilimia 23 ya Kampuni za kati nchini zinaona mwenendo wa uchumi nchini kwa kipindi cha miezi sita iliyopita sio mzuri huku asilimia 62 ya kundi hilo iko na kuimarika kwa uchumi kwa kipindi cha miezi sita ijayo.
Mkutano huo wa utafiti umefanyika ikiwa imesalia siku moja kufikia fainali za shindano la Top100 ambayo itafanyika Oktoba 25, katika fainali hizo kampuni bora 100 za kati zitatangazwa. Dk. Ruhinduka alisema asilimia kubwa ya wafanyabiashara wanamatumaini ya kuimarika kwa uchumi licha ya changamoto walizonazo katika biashara zao.
"Mtazamo wa wafanyabiashara kwa kipindi cha miezi 6 iliyopita asilimia 55 wanasema biashara inaimarika, asilimia 22 wanasema iko sawa na asilimia 23 wanasema mwenendo sio mzuri. Hata hivyo kwa kipindi cha miezi sita ijayo Asilimia 60 wanasema uchumi utaimarika, asilimia 28 itakuwa sawa na asilimia 12 itakuwa mbaya," amesema Dk. Ruhinduka.
Pia utafiti huo ulihoji mtazamo wa wafanyabiashara hao kuhusu mwenendo wa sekta ya wafanyabiashara wakati nchini ambapo kwa kipindi cha miezi sita iliyopita aslimia 62 walisema hali imeimarika asilimia 20 walisema iko sawa na asilimia 18 walisema hali ni mbaya.
Mwenendo wasekta kwa kipindi cha miezi sita ijayo utafiti huo ulibainisha kuwa asilimia 66 ya wafanyabiashara walisema mwenendo utaimarika asilimia 20 walisema itakuwa sawa na asilimia 14 walisema utakuwa sawa.