Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

MAJALIWA AKUTANA NA WAZIRI WA KILIMO WA CHINA

0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Changfu wakati alipotembelea Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo iliyopo Beijing Septemba 3, 2018. Majaliwa yupo nchini China kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya Afrika na China – FOCAC



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Changfu (kushoto) wakati alipotembelea Wizara hiyo iliyopo Beijing, Septemba 3, 2018.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Chanfu wakishuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Ushirikiano katika masuala ya Uvuvi kati ya China na Tanzania kwenye ukumbi wa Wizara ya Kilimo ya China katika jiji la Beijing, Septemba 3, 2018. Wanaotia Saini ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Zanzibar, Rashid Ali Juma (kushoto) na Naibu Waziri wa Kilimo wa China, Qu Dongyu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Chanfu (wanne kulia) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) baada ya mazungumzo yao kwenye ukumbi wa wizara hiyo jijini Beijing, Septemba 3, 2018. Wengine pichani ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Zanzibar, Rashid Ali Juma. (wapili kushoto), Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (watatu kushoto), Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki na Naiba Waziri wa Kilimo wa China, Qu Dongyu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na ujumbe wake wakiagana na viongozi wa Wizara ya Kilimo ya China baada ya mazungumzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Wizara hiyo, Beijing nchini China, Septemba 3, 2018. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



UWEKEZAJI KUTOKA CHINA KUTUFIKISHA UCHUMI WA KATI-MAJALIWA


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Jimbo la Jiangsu nchini China katika sekta ya kilimo na viwanda utaiwezesha nchi kufikia malengo yake ya kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2020 na ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Amesema jimbo la Jiangsu ni miongoni mwa majimbo yaliyopiga hatua kubwa ya maendeleo kwenye teknolojia na viwanda duniani na Tanzania inahitaji wawekezaji wa uhakika katika sekta ya kilimo hususani watakaowekeza kwenye viwanda vya kuchakata mazao ya kilimo, kuongeza thamani na kutafuta masoko.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumatatu, Septemba 03, 2018) wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Gavana wa Jimbo la Jiangsu nchini China, Bw. Guo Yuan Qiung kwenye ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini China.

“Tunathamini mchango wa Jimbo la Jiangsu katika uchumi wa Tanzania, ambapo sasa wawekezaji kutoka jimboni humo, waliowekeza kwenye viwanda mbalimbali kama cha kuchambua pamba, kutengeneza nyuzi na kukamua mafuta ya kula kwa kutumia mbegu za pamba cha Jielong kilichopo wilayani Shinyanga na kiwanda cha nguo cha Urafiki cha jijini Dar es Salaam.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alisema bado mchango wa jimbo hilo unahitajika katika uendelezaji viwanda hususan katika masuala ya teknolojia ya viwanda, kuimarisha utafiti kwenye sekta ya kilimo na kuisaidia Tanzania kupata masoko ya mazao kama mbaazi, muhogo na soya. “Tunaomba uendelee kuhamasisha kampuni nyingi zaidi kutoka jimboni kwako kuja kuwekeza nchini.

Kuhusu kiwanda cha nguo cha Urafiki cha jijini Dar es salaam, Waziri Mkuu na Naibu Gavana huyo walikubaliana kuangalia uwezekano wa kufanya mapitio ya changamoto za uendeshaji wa kiwanda hicho ili kutafuta suluhisho la mapungufu yanayojitokeza katika kiwanda hicho.

Kwa upande wake, Bw. Qiung alimhakikishia Waziri Mkuu ushirikiano wa hali ya juu hasa katika uwekezaji wa viwanda na kwamba anaamini kuwa mkutano wa FOCAC utatoa dira ya maendeleo kwa Tanzania na Bara zima la Afrika.

Aliongeza kuwa jimbo lake lipo tayari kushirikiana na Tanzania katika masuala ya elimu kwani lina vyuo vingi vinavyotoa kozi mbalimbali na aliwakaribisha wanafunzi kutoka Tanzania kwenda jimboni humo kusoma.



IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, SEPTEMBA 04, 2018.


RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA BARABARA YA NYAMUSWA-BUNDA-KISORYA-NANSIO , AHUTUBIA WANANCHI WA NANSIO UKEREWE

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe kuashiria uzinduzi wa Barabara ya Nyamuswa-Bunda-Kisorya-Nansio km 121 katika sehemu ya Barabara ya Bulamba Kisorya km 51 katika sherehe zilizofanyika Kisorya Bunda mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika mkasi na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isaack Kamwelwe wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa Mitambo itakayotumika katika ujenzi wa barabara Barabara ya Nyamuswa-Bunda-Kisorya-Nansio km 121 katika sehemu ya Barabara ya Bulamba Kisorya km 51 katika sherehe zilizofanyika Kisorya Bunda mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kisorya kabla ya kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Barabara ya Nyamuswa-Bunda-Kisorya-Nansio km 121 katika sehemu ya Barabara ya Bulamba Kisorya km 51 katika sherehe zilizofanyika Kisorya Bunda mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako ili kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Chuo cha Ualimu Murutunguru kilichopo Nansio Ukerewe mkoani Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa wakati akipokuwa akisikiliza maelezo ya mradi wa maji wa Nansio Ukerewe mkoani Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Ukerewe mara baada ya kuwasili akitokea Kisorya mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima kabla ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa barabara Barabara ya Nyamuswa-Bunda-Kisorya-Nansio km 121 katika sehemu ya Barabara ya Bulamba Kisorya km 51 katika sherehe zilizofanyika Kisorya Bunda mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa wakati akitoka kukagua pampu za kusukuma maji katika mradi wa maji uliopo Nansio Ukerewe mkoani Mwanza.PICHA NA IKULU



WAZIRI LUGOLA ATEMBELEA ENEO LA AJALI YA MAGARI MANNE YALIYOGONGANA YAKIWA KATIKA MSAFARA KUELEKEA MKUTANO WA RAIS MAGUFULI, KISORYA, BUNDA

0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akiliangalia gari la CCM Mkoa wa Mwanza lenye namba ya usajili T223 CHN Toyota Land Cruiser, lililopata ajali Kijiji cha Kasuguti Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda Mkoa wa Mara, leo. Magari manne likiwemo moja walilopanda waandishi wa habari, yalikua katika msafara yakielekea katika Mkutano wa Rais Dkt John Pombe Magufuli, wa uzinduzi wa barabara ya kiwacho cha lami katika Kijiji cha Kisorya, wilayani humo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akizungumza na baadhi ya majeruhi wa ajali iliyojumuisha magari manne yaliyokuwa yanaenda katika Mkutano wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, kwa ajili ya uzinduzi wa barabara ya kiwacho cha lami katika Kijiji cha Kisorya, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Mkoa wa Mara.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli (wapili kulia), akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) alipokua anampongeza kwa kuja jimboni kwake Mwibara, pamoja na kumpa changamoto wanazokabiliwa nazo jimboni humo, Wilaya ya Bunda, Mkoani wa Mara, leo. Rais Magufuli alizindua barabara yenye kiwango cha lami inayojengwa kutoka Kisorya mpaka Mramba katika jimbo hilo.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli (wapili kushoto), akikata utepe kuashiria barabara ya kiwango cha lami iliyoanza kujengwa kutoka Kijiji cha Kisorya mpaka Mramba yenye kilomita 51kuzinduliwa. Kulia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, Kangi Lugola akishuhudia tukio hilo lililofanyika katika Kijiji cha Kisorya, Wilaya ya Bunda, Mkoani wa Mara, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

WANAHABARI WATAKA RAIS MAGUFULI AKOMESHE WATU WANAOSABABISHA MANYANYASO KWA WAANDISHI

0
0
Jopo la majaji wa Tuzo ya Daudi Mwangosi mwaka 2018 limemtangaza Mwandishi wa habari I wa gazeti la Mwananchi Azory Gwanda kuwa mshindi wa tuzo hiyo mwaka 2018.

Tuzo hiyo imetangazwa leo Jumanne Septemba 4,2018 wakati wa mkutano mkuu wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania UTPC unaofanyika katika ukumbi wa Lush Garden Hotel jijini Arusha.
Kushoto ni Absalom Kibanda Mhariri mkuu kutoka gazeti la. Mtanzania akikabidhi tuzo ya Daudi Mwangosi 2018 kwa mke wa Azory Gwanda.Katikati ni rais wa UTPC,Deogratius Nsokolo
Kushoto ni Absalom Kibanda akikabidhi cheti cha utambuzi kwa mke wa Azory Gwanda
Mwenyekiti wa Jopo la Majaji wa Tuzo ya Mwangosi Mwaka 2018, Ndimara Tegambwage akitangaza mshindi wa tuzo ya Mwangosi 2018.
Mbali na kukabidhiwa tuzo hiyo,pia amekabidhiwa cheti cha utambuzi pamoja na shilingi milioni 10.
Jopo la Majaji wa Tuzo ya Mwangosi Mwaka 2018, wakwanza kulia ni mwenyekiti wa jopo hiloNdimara Tegambwage, Katikati ni mama Edda Sanga, na wengine wawili. 

Na Vero Ignatus. Arusha

Mwanahabari Mkongwe nchini Absolom Kibanda  ambaye pia ni Mhariri Mtendaji wa gazeti la Mtanzania amemuomba Raisi Magufuli achukue hatua juu ya matukio ya kupotea  kwa Wanahabari akiwemo  Azory Gwanda wa gazeti la Mwananchi ambaye alipotea miezi 9 iliyopita katika mazingira ya kutatanisha.
Kibanda amesema kwa Rais Magufuli amekua akisifia juhudi za Wanahabari hivyo asiishie  katika kusifia bali achukue hatua ili kuponya majeraha ya Wanahabari ambao wanakamatwa na kuteswa huku wengine wakipotea kwenye mazingira ya utata
Absolom Kibanda amevitaka vyombo vya dola kubaini alipo Azorry Gwanda ambaye ametoweka kwenye mazingira ya kutatanisha kwa takribani miezi 9 sasa na hajulikani alipo.Kibanda ambaye ni Mgeni rasmi aliyekabidhi Tuzo ya Daudi Mwangosi kwa Mke wa Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Azory  ambaye amepotea kwa takribani miezi tisa katika mazingira ya kutatanisha.
Aidha ameitaka Wizara husika kuchukua hatua na kufanya uchunguzi na kubaini ili Azory aweze kupatikana na kuendelea na majukumu yake ya Kitasnia.“Vyombo vya dola vikate mzizi wa fitina kwa kuwakamata wanaohusika na vitendo vya kikatili kwa wanahabari ikiwemo Kupotea kwa Azory ,kuteswa kwa Kibanda ,kumwagiwa tindi kali Kubenea” Alisema Kibanda
Amesema katika mitandao kuna Taarifa 17500 Zinazoelezea tukio la Azory  kwenye mitandao ya kijamii  hivyo suala hilo bado linagonga vichwa katika vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa.Mke wa Azory ,Anna Pinuni  amepokea tuzo hiyo huku akigubikwa na machozi ,pia ameshukuru kwa tuzo hiyo na kuishukuru kampuni ya Mwananchi kwa kumjali na kumtunza tangu siku ya kwanza mume alipopotea.
Anna ambaye kwa sasa ana mtoto mchanga wa miezi 6 ,mume wake alipopotea alikua na ujauzito wa miezi 6 .Raisi wa Muungano wa Vilabu vya Wanahabari nchini UTPC Deudatus Nsokolo  amesema kuwa vyombo vya habari vinapaswa uwajali wanahabari hasa wanapoingia katika matatizo pia kuiga mfano wa Kampuni ya Mwananchi.

RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU DR. GODFREY MBARUKU

0
0






Familia ya Marehemu Mzee Thomas Mbaruku wa Dar es salaam imetoa ratiba ya mazishi ya kumzika ndugu yao marehemu Dr Godfrey Michael Dafa Thomas Mbaruku aliekua mtafiti Mkuu wa Miradi mbalimbali wa Ifakara Health Institute alietwaliwa usiku wa kuamkia Jumapili Nyumbani kwake Mbezi Jogoo Dar es salaam.

Msiba upo nyumbani kwake Mbezi Jogoo nyuma ya Art Gallery .

Bwana Ametoa Bwana ametwaa Jina lake lihimidiwe, Apumzike kwa Aman

TADB NA ESRF ZAINGIA MAKUBALIANO YA KUWAJENGEA UWEZO WAKULIMA NCHINI

0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakitiliana saini mkataba wa makubaliano ya kufanya tafiti za maendeleo ya kilimo hasa katika kuwajengea uwezo wakulima wadogo nchini jana jijini Dar es salaam
Baadhi ya wakuu wa vitengo na maofisa wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) wakiwa katika kikao hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakibadilisha na hati za mikataba mara baada ya kutiliana saini makubaliano ya kufanya tafiti za maendeleo ya kilimo hasa katika kuwajengea uwezo wakulima wadogo nchini jana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakionyesha mikataba mara baada ya kutiliana saini makubaliano ya kufanya tafiti za maendeleo ya kilimo hasa katika kuwajengea uwezo wakulima wadogo nchini jana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa pande zote mbili baada ya kutiliana saini mkataba wa makubaliano ya kufanya tafiti za maendeleo ya kilimo hasa katika kuwajengea uwezo wakulima wadogo nchini jana jijini Dar es salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakiwa katika mazungumzo
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine kulia akiongoza ujumbe kutoka benki ya kilimo.
Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine na Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) , Dk. Tausi Kida wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF)

....................................................................................

Na Mwandishi wetu, Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na (ESRF) zimeingia makubaliano ya kufanya tafiti za maendeleo ya kilimo hasa katika kuwajengea uwezo wakulima wadogo nchini.

Akizungumza wakati wa utiaji saini makubaliano hayo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine amesema kuwa ushirikiano huo unalenga kuchagiza katika kuendeleza maeneo ya utafiti, uchambuzi wa sera na kuwajengea uwezo wakulima nchini ili kuweza kuharakisha mapinduzi ya kilimo Tanzania.

Akizungumzia malengo ya ushirikiano huo, Bw, Justine amesema pande zote zinalenga katika taasisi hizo zinalenga katika upatikanaji na uhamasishaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya utafiti wa kilimo na maendeleo, uchambuzi wa sera, utetezi, na kujenga uwezo wa wakulima wadogo wadogo, wakulima wa kati na wakulima nchini Tanzania.

Ameongeza kuwa ushirikiano huo utalenga katika kuandaa kanzi-data ya maarifa kwa ajili ya kujenga mtandao wa taarifa za kutosha kuhusu sekta ya kilimo ili kuwezesha maamuzi sahihi katika sera na utekelezaji wa masuala mbalimbali yanayohusiana na kilimo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa ESRF, Dk. Tausi Kida, amesema kuwa kuwa ushirikiano kati ya Benki ya Kilimo na Taasisi yake unalenga kufanya utafiti juu ya minyororo ya thamani ya kilimo pamoja na kuendeleza na kutekeleza mipango ya utetezi ili kusaidia katika utoaji wa maamuzi katika ngazi ya sera.

YALIYOJIRI BUNGENI LEO SEPTEMBA 4, 2018

0
0


Mbunge wa Jimbo la Buyungu Mhe. Mhandisi Christopher Chiza akiapa mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job NdugaiS leo Jijini Dodoma mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
2 (2)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimpongeza mbunge wa Buyungu Mhe. Mhandisi Christopher Chiza mara baada ya kula kiapo mbele ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job  Ndugai leo Bungeni Jijini Dodoma.
5
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.  Dkt. Mary Mwanjelwa akieleza mikakati ya Serikali katika kuinua sekta ya kilimo hapa nchini wakati wa kipindi cha maswali na majibu leo Bungeni Jijini Dodoma.
4 (2)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani   Jafo akiwasilisha Bungeni maelezo ya Serikali kuhusu muswaada wa sheria ya kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa makao makuu ya nchi wa mwaka 2018( The Dodoma Capital City ( Declaration) Bill, 2018.
3 (2)
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akijibu swali Bungeni Kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuwezesha mikoa kutekeleza miradi ya kimkakati ya maendeleo ili kuinua uchumi wa mikoa hiyo.
8
Mbunge wa Kibakwe Mhe. George Simbachawene akisisitiza kuhusu faida za Dodoma kuwa makao makuu ya nchi yetu leo Bungeni  Jijini Dodoma.
6 (1)
Sehemu ya wabunge wakifuatilia  mkutano wa  12 kikao cha kwanza cha Bunge leo Jijini Dodoma.

Rais Shein awataka Wafanyakazi wa Wakala wa matukio ya Kijamii Zanzibar kutoa huduma zinazostahiki kwa Wananchi

0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Muhammed Shein akizungumza na wananchi na Wafanyakazi wa Wakala wa Usaji wa Matukio ya Kijamii Zanzibar baada ya Uzinduzi huo (kuli) Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Haji Omar Kheir na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala Matukio ya Kijamii Zanzibar Dkt. Hussein Khamis .
Wafanyakazi wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ( hayupo pichani) baada ya Uzinduzi wa Ofisi yao katika Kijiji cha Dunga Mkoa wa Kusini Unguja.
Wananchi wa Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein ( hayupo pichani) baada ya Uzinduzi wa Ofisi ya Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar .

Na Maryam Kidiko / Fatma Makame – Maelezo. 4/9/2018.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraa la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amewataka Wafanyakazi wa Wakala wa matukio ya Kijamii Zanzibar kutoa huduma zinazostahiki kwa Wananchi ili kupata taarifa sahihi katika kazi zao.

Hayo aliyasema huko Dunga Mkoa wa kusini Unguja wakati akizindua Ofisi ya Wakala wa Usajili wa Matukiuo ya Kijamii Zanzibar. Alisema ili kupata taarifa sahihi na kujua idadi ya watu lazima kujenga masharikiano makubwa baina yao na Wananchi.

Alisitiza Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inahitaji takwimu sahihi hivyo Wafanyakazi nilazima kufanya kazi kwa kuzingatia misingi ya sheria, kanuni na uadilifu. Aidha aliwataka wafanyakazi hao kuelimisha jamii juu ya suala zima la kujisajili katika matukio ya kijamii na kupambana na changamoto zitazojitokeza ili ziweze kuleta maendeleo.

“Katika kazi hii changamoto mbali mbali zitajitokeza hivyo ni muhimu kupambana na changamoto hizo kwa kuzifanya ziweze kuleta mafanikio” alisema Rais Shein. Hata hivyo Rais wa Zanzibar alitoa wito kwa wananchi na wageni kutumia vizuri fursa hiyo na kila mmoja awe tayari kutoa taarifa sahihi zinazomuhusu.

Amewaomba Wafanyakazi wanaohusika na usajili wa matukio ya kijaamii Zanzibar kuwa majukumu yao yanagusa sehemu mbali mbali hivyo waandae mikakati sahihi na taarifa ili waweze kufanikisha malengo waliyokusudia. Akielezea zaidi alisema kuwa ili kupatikana maendele na kuimarisha Sekta mbali mbali ni muhimu kushirikiana na kuendeleza jukumu la kulinda amani iliopo katika Nchi.

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Haji Omar Kheir alisema kuwa sheria iliyowekwa inataka matukio yote ya kijamii ni lazima yasajiliwe . Alisema kuwa kila kitu kimekamilika na tayari kuanza rasmin kwa kufanya usajili kwa Wakaazi wa Zanzibar pamoja na wageni waliokuwepo Zanzibar.

Alilisisitiza kuwa upo umuhimu mkubwa kwa wageni kwa upande wao kusajiliwa kwani wanasehemu yao tofauti na wenyeji wa Zanzibar.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

ZAIDI YA WANAFUNZI 6000 KUFANYA MTIHANI WA KUHITIMU DARASA LA SABA MKURANGA

0
0

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga,Mhadisi Mshamu Munde akizungumza na Michuzi Blog leo kuhusu wasimamizi wa mitihani ya darasa la saba unaoanza kesho Jumatano 5-6 Septemba wasimamiee kwa weledi na wanafuzi wafanye kwa waminifu.

Mitihani ya taifa ya darasa la saba inatarajiwa kuanza kesho nchini kote hivyo walimu wameombwa kusimamia mitihani hiyo vizuri na wale watakaokiuka sheria za usimamizi wa mitihani hatua Kali zitachukuliwa dhidi yao huku zaidi wanafunzi 6000 watafanya mtihani huo.

Akizungumza Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Juma Abeid amesema kesho wanafunzi wa darasa la saba nchi  nzima wanafanya mtihani wao wa mwisho kwahiyo amewaomba walimu wanaosimamia mitihani hii wafanye kazi yao kwa uadilifu na kufuata sheria muache udanganyifu.

Aidha amewataka wanafunzi kuwa watulivu katika pindi chote cha mitihani ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao hiyo nakuiletea sifa wilaya ya Mkuranga."Mwaka Jana Mkuranga tulishika nafasi ya kwanza katika mkoa wa Pwani naamini tunaweza pia kuwa wa kwanza kitaifa kama wanafunza watatumia nafasi ya kesho kufanya mitihani vizuri"alisema Abeid

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga Mhandisi Mshamu Munde amesema kuwa halmashauri hiyo imejiandaa vizuri kwani mpaka sasa vifaa vyote vinavyohusiana na mitihani vimeshakamilika."mandalizi ya mitihani yanahusisha vifaa vya mitihani,na mafunzo kwa wasimamizi wote wa mitihani vyote vimakailika ikiwemo masurufu,usambazaji wa mitihani na magari"alisema

Alisema kuwa zoezi hilo ni la kitaifa na serikali imewekeza fedha nyigi kwahiyo anawasihi wasimamizi wawe waadilifu wasijihusishe na vitendo vya udanganyifu wataitia serikali hasara kwa sababu imetumia pesa nyingi na kutoa rai kwao wafanye kazi kwa weledi.

Aidha alitoa wito kwa wanafunzi kufanya mitihani yao kwa uaminifu mkubwa wadifanye udanganyifu wa aina yeyote ile kwani utawaletea hasara kubwa

Hata hivyo zaidi ya wanafunzi 6000 wilayani mkuranga wanatarajiwa kuanzà mitihani wao wa mwisho wa kumaliza Elimu ya msingi hapo kesho

MKUU WA MKOA MJINI MAGHARIBI AGAWA KOMPYUTA 96 KWA WAHITIMU KIDATO CHA 6

0
0
Na Agness Francis,Glogu ya jamii

MKUU wa Mkoa wa mjini Magharibi Zanzibar Ayoub Mahmoud amekabidhi kompyuta mpakato kwa wanafunzi 96 waliohitimu kidato cha 6 ambao wana ufaulu wa  alama ya daraja la kwanza (devision 1) kwa kila mmoja.

Kompyuta hizo zimetolewa na taasisi ya Mimi na wewe foundation ili kusawasaidia wanafunzi hao kurahisisha kazi katika masomo yao ya elimu ya juu na kuleta hamasa kwa wale waliobaki mashule kufanya vizuri zaidi.

Mahmoud ameyasema hayo wakati wa ugawaji wa kupyuta hizo  kuwa kiwango cha Elimu kwa mwaka huu kimepanda kulinganisha na kipindi kilichopita.

"hali ya kiwango cha ufaulu katika mkoa wetu haikuwa ya kuridhisha kipindi cha nyuma ambapo tumechukua hatua za dharula na haraka ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa kushirikiana na wizara ya elimu,mwaka huu kumekuwa na ongezeko la ufaulu wanafunzi 96 daraja la 1"amesema mkuu wa mkoa huyo.

Katika ugawaji wa zawadi hizo walikuwepo wanamuziki wa aina ya kizazi kipya  waliamsha dude visiwani humo katika viwanja vya mapinduzi square.

Hamsha hamsha hizo zilipamba moto baada ya Mkuu wa Mkoa kumaliza kugawaji wa vifaa  mjini hapo.
 Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Ayoub Mahmoud kushoto pamoja na makamu wa  Rais wa Zanzibar balozi seif Iddy Kati kati, wakikabidhi kompyuta mpakato kwa mmoja wa wanafunzi waliofaulu kwa alama ya daraja   la kwanza (devision 1) kidato cha 6 katika viwanja vya mapinduzi square visiwani Zanzibar.
 Msanii wa kizazi kipya  Amba lulu akitoa burudani viwanjani hapo katika kuhitimisha  sherehe za ugawaji wa zawadi za  kompyuta kwa wanafunzi waliohitimu kidato cha 6  waliofaulu alama ya daraja la kwanza.
Msanii wa muziki wa dansi Papy Kocha akitoa shoo visiwani Zanzibar wakati wa hafla ya ugawaji wa zawadi kwa wanafunzi hao ambapo mkuu wa Mkoa Wa mjini magharibi Ayoub Mahmoud ndie aliyekabidhi katika viwanja vya Mapinduzi Square.

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA BUNDA WAKATI AKIWA NJIANI KUELEKEA MUSOMA MKOANI MARA

0
0


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Bunda mjini wakati akiwa njiani kuelekea Musoma mkoani Mara.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Bunda wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliposimama kuwasalimia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kwa njia ya Simu kuhusu mgogoro wa ardhi uliopelekea Bibi Nyasasi Masige mwenye kilemba aliyekaa kudai kunyang’anywa Kiwanja chake Wilayani Bunda. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Bibi Nyasasi Masige kiasi cha Shilingi laki tano ili zimsaidie mara baada ya kusikiliza kero yake ya madai ya kunyanga’nywa kiwanja chake. Rais Dkt. Magufuli ameagiza uchunguzi ufanyike haraka ili haki ya bibi huyo iweze kupatikana. PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MEYA WA SHENZHEN, ATEMBELEA OFISI KUU YA KAMPUNI YA HUAWEI TECHNOLOGIES ILIYOPO SHENZHEN NCHINI CHINA

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Meya wa Manispaa ya Shenzhen, Bw. Wang Wanzhong kwenye ukumbi wa Hoteli ya Wuzhou nchini China, Septemba 5, 2018. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Meya wa Manispaa ya Shenzhen kwenye hoteli ya Wuzhou nchini China, Septemba 5, 2018. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyeshwa piano ya Kichina na msan , Xing Man baada ya mazungumzo kati yake na Meya wa Manispaa ya Shenzhen nchini China. Bw. Wang Wanzhong, Septemba 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea maua wakati alipowasili kwenye makao mkuu ya kampuni ya Huawei Technologies yaliyopo Shenzhen nchini China, Septemba 5, 2018. Kulia ni Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo duniani, Li Da Feng. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama vifaa vya elektroniki wakati alipotembelea makao makuu ya kampuni ya Huawei Technologiies yaliyopo, Shenzhen nchini China, Septemba 5, 2018. Kulia ni Makamu wa Rais wa Kampuni hiyo Duniani, Li Da Feng . Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Augustine Mahiga.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoka ndani ya jengo la Makao Makuu ya Kampuni ya Huawei Techinologies yaliyopo Shenzhen nchini China baada ya kutembelea Ofisi hizo na kuzungumza na viongozi wa Kampuni hiyo, Septemba 5, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA SPIKA MSTAAFU PIUS MSEKWA

0
0
Rais Dkt John Pombe Magufuli akiagana na wenyeji wake spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Pius Msekwa kulia,Ikulu ndogo,Nansio Ukerewe,Mkoani Mwanza. Septemba 5,2018. 
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akiagana na wenyeji wake Mke wa Spika msaafu Pius Msekwa Mama Anna Abdallah Msekwa,Ikulu ndogo,Nansio Ukerewe,Mkoani Mwanza. Septemba 5,2018. Kushoto ni spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Pius Msekwa.
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa amewashika mikono wenyeji wake spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Pius Msekwa na Mkewe Mama Anna Abdallah Msekwa,Ikulu ndogo,Nansio Ukerewe,Mkoani Mwanza. Septemba 5,2018. 
  Rais Dkt John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mwenyeji wake spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Pius Msekwa Ikulu ndogo,Nansio Ukerewe,Mkoani Mwanza. Septemba 5,2018.

DC TANGA AZINDUA KAMPENI JUMUISHI YA UPIMAJI WA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI MKOANI TANGA

0
0

MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa katika akizundua mpango wa Furaha Yangu uliokuwa na lengo la Pima,Jitambue,ishi ambapo kwa mkoa wa Tanga imezinduliwa leo kwenye viwanja vya Tangamano kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango wa Furaha Yangu uliokuwa na lengo la Pima,Jitambue ambapo kwa mkoa wa Tanga imezinduliwa leo kwenye viwanja vya Tangamano kushoto ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita na kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florance Temu Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita akizungumza katika uzinduzi huo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florance TemuMKURUGENZI wa Mpango wa Furaha Yangu kutoka Shirika la Benjamini Mkapa Rahel Sheiza akizungumza katika uzinduzi huo

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florence Temu akizungumza katika uzinduzi huo

Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim akizungumza katika uzinduzi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella anayefuata ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha Mahita Mwakilishi wa JWTZ akizungumza katika uziunduzi huoMkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akiwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha mahita wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye uzinduzi huo

Sehemu ya wageni mbalimbali wakifuatilia uzinduzi huo kulia ni Suleimani Zumo Afisa Tarafa,nyuma waliokaa aliyevaa miwani ni Afisa Mradi wa Mkoa wa Tanga wa Kifua Kikuu na Ukimwi Dkt Anastazia Masanja

Mgenii rasmi kwenye uzunduzi huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati mwenye koti la suti akikagua mabanda mara baada ya kufanya uzinduzi huo

Mgenii rasmi kwenye uzunduzi huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wengine kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita

Wasanii wa kundi la Tanga Kwanza wakitumbuiza kwenye uzinduzi huo




NA MWANDISHI WETU,TANGA.




KATIKA kuendeleza kuchangia juhudi za Serikali kuimarisha huduma za Afya ikiwemo huduma za Ukimwi,Shirika la Benjamini Mkapa kupitia Shirika lisilo la Kiserikali la Amref chini ya ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) inatekeleza mradi wa miaka mitatu 2018-2020 Desemba.




Mradi huo wenye kufanya upimaji Jumuishi wa Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi katika Jamii na Kuhamasisha Jamii kubadili tabia hatarishi ili kuweza kusaidia kupunguza maambukizi hayo kwa jamii .




Hayo yalisemwa na Afisa Mradi wa Mkoa wa Tanga wa Kifua Kikuu na Ukimwi Dkt Anastazia Masanja wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo iliyofanywa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kwenye viwanja vya Tangamano mjini hapa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita,Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florence Temu na Mkurugenzi wa Mpango wa Furaha Yangu kutoka Shirika la Benjamini Mkapa Foundation Rahel Sheiza akizungumza katika uzinduzi huo




Alisema kupitia mradi huo wa kupambana na kifua kikuu na Ukimwi ambao utekelezaji wake umeanza mwezi Juni 2018,Taasisi imepewa wilaya mbili ambazo ni Kilindi na Pangani kwa Mkoa wa Tanga .




"Kwa kipindi hiki Shirika la Benjamini Mkapa linatarajia kufikia kata zote 35 ambapo kati ya hizo 21 ni za wilaya ya Kilindi na 14 ni za wilaya ya Pangani lengo la upamaji kwa kila kati ni kuweza kupima watu 2081(Jumla 72,839 kwa kata 35).




Huduma ambazo zimekuwa zikitolewa ni pamoja na uchunguzi wa awali wa kifua kikuu ambapo watu wote 7082 waliohudhuria waliweza kuchunguzwa ambao watu 220 walikutwa na dalili za kifua kikuu na kupewa rufaa kwenda Hospitali ya wilaya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.




"Kwa upande wa shinikizo la damu ambapo jumla ya watu 5269 walipimwa kati yao 182 walikutwa na shinikizo la damu lisilokuwa la kawaida "Alisema.




Afisa Mradi huyo alisema pia huduma za uzazi wa mpango zilitolewa ikiwamo vipandikizi,sindano,vidonge ambapo jumla ya wakina mama waliopata huduma hiyo walifikia 188 na ugawaji wa kondomu ambapo jumla ya kondomu 5000 zimegawiwa.




"Lakini pia tuliotoa elimu ya mfuko wa Afya ya Jamii ikiwemo ya mabadiliko ya tabia kupitia sinema na vikundi vya ngoma "Alisema

MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa katika akizundua mpango wa Furaha Yangu uliokuwa na lengo la Pima,Jitambue,ishi ambapo kwa mkoa wa Tanga imezinduliwa leo kwenye viwanja vya Tangamano kulia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita

MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa mpango wa Furaha Yangu uliokuwa na lengo la Pima,Jitambue ambapo kwa mkoa wa Tanga imezinduliwa leo kwenye viwanja vya Tangamano kushoto ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita na kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florance Temu

Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita akizungumza katika uzinduzi huo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florance Temu

MKURUGENZI wa Mpango wa Furaha Yangu kutoka Shirika la Benjamini Mkapa Rahel Sheiza akizungumza katika uzinduzi huo

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florence Temu akizungumza katika uzinduzi huo

Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim akizungumza katika uzinduzi huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella anayefuata ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha Mahita

Mwakilishi wa JWTZ akizungumza katika uziunduzi huoMkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akiwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga (RMO) Dkt Asha mahita wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye uzinduzi huo

Sehemu ya wageni mbalimbali wakifuatilia uzinduzi huo kulia ni Suleimani Zumo Afisa Tarafa,nyuma waliokaa aliyevaa miwani ni Afisa Mradi wa Mkoa wa Tanga wa Kifua Kikuu na Ukimwi Dkt Anastazia Masanja

Mgenii rasmi kwenye uzunduzi huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati mwenye koti la suti akikagua mabanda mara baada ya kufanya uzinduzi huo

Mgenii rasmi kwenye uzunduzi huo Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tanga Martine Shigella katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wengine kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita

Wasanii wa kundi la Tanga Kwanza wakitumbuiza kwenye uzinduzi huo


NA MWANDISHI WETU,TANGA.

KATIKA kuendeleza kuchangia juhudi za Serikali kuimarisha huduma za Afya ikiwemo huduma za Ukimwi,Shirika la Benjamini Mkapa kupitia Shirika lisilo la Kiserikali la Amref chini ya ufadhili wa Mfuko wa Dunia wa Kupambana na Ukimwi Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund) inatekeleza mradi wa miaka mitatu 2018-2020 Desemba.

Mradi huo wenye kufanya upimaji Jumuishi wa Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi katika Jamii na Kuhamasisha Jamii kubadili tabia hatarishi ili kuweza kusaidia kupunguza maambukizi hayo kwa jamii .

Hayo yalisemwa na Afisa Mradi wa Mkoa wa Tanga wa Kifua Kikuu na Ukimwi Dkt Anastazia Masanja wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo iliyofanywa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kwenye viwanja vya Tangamano mjini hapa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt Asha Mahita,Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim,Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Amref Tanzania Florence Temu na Mkurugenzi wa Mpango wa Furaha Yangu kutoka Shirika la Benjamini Mkapa Foundation Rahel Sheiza akizungumza katika uzinduzi huo

Alisema kupitia mradi huo wa kupambana na kifua kikuu na Ukimwi ambao utekelezaji wake umeanza mwezi Juni 2018,Taasisi imepewa wilaya mbili ambazo ni Kilindi na Pangani kwa Mkoa wa Tanga ."Kwa kipindi hiki Shirika la Benjamini Mkapa linatarajia kufikia kata zote 35 ambapo kati ya hizo 21 ni za wilaya ya Kilindi na 14 ni za wilaya ya Pangani lengo la upamaji kwa kila kati ni kuweza kupima watu 2081(Jumla 72,839 kwa kata 35).

Huduma ambazo zimekuwa zikitolewa ni pamoja na uchunguzi wa awali wa kifua kikuu ambapo watu wote 7082 waliohudhuria waliweza kuchunguzwa ambao watu 220 walikutwa na dalili za kifua kikuu na kupewa rufaa kwenda Hospitali ya wilaya kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

"Kwa upande wa shinikizo la damu ambapo jumla ya watu 5269 walipimwa kati yao 182 walikutwa na shinikizo la damu lisilokuwa la kawaida "Alisema.fisa Mradi huyo alisema pia huduma za uzazi wa mpango zilitolewa ikiwamo vipandikizi,sindano,vidonge ambapo jumla ya wakina mama waliopata huduma hiyo walifikia 188 na ugawaji wa kondomu ambapo jumla ya kondomu 5000 zimegawiwa.

"Lakini pia tuliotoa elimu ya mfuko wa Afya ya Jamii ikiwemo ya mabadiliko ya tabia kupitia sinema na vikundi vya ngoma "Alisema

MWALIMU MLOZI AITAKA UWT KUYASEMEA MATATIZO YA WANYONGE ILI KUWAKOMBOA KIMAISHA

0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

KATIBU Mkuu UWT Taifa, Mwalimu Queen Mlozi ,ameutaka umoja huo wilaya na mikoa ,kujiwekea mikakati ya kumkomboa mwanamke kisiasa ,kiuchumi na kijamii pamoja na kuwasemea wanyonge ili kujiinua kimaisha.

Aidha, amewataka wanawake ,washikamane kwa kujenga mahusiano mema kwa lengo la kuimarisha umoja huo .Pamoja na hayo ,wajitume kwa kuanzisha miradi ya kujikwamua kiuchumi ili waweze kujitegemea na kuondokana na hali ya kuwa ombaomba kwenye familia .

Alitoa rai hiyo ,wakati akizungumza na kamati ya utekelezaji na wanachama wa UWT Mkoa wa Pwani ,katika ofisi za CCM Mkoani humo .Aliwasihi ,viongozi wa umoja huo ,kurudi katika katiba ya UWT ambavyo inaelekeza kuwajengea uwezo wanawake katika kuwakomboa kimaisha.

"Ninawaomba wanawake tupendane ,wanasema adui ya mwanamke ni mwanamke lakini mimi siamini hilo,tushauriane tusonge mbele wanawake ni jeshi kubwa ,kwanza kwa kumsemea mh .Rais Dk.John Magufuli kwa kueleza mazuri yanayofanywa na serikali yetu "

"Pili tuwasemee na wanawake wenzetu walio wanyonge,wanapokuwa na shida tuseme sisi tukemee ili tusonge mbele " Mwalimu Queen alieleza ,hakuna kitu kikubwa dunia kama mtaji wa mahusiano mazuri na wengine ,hivyo ni lazima wapendane.

"Weka pembeni mali, weka pembeni pesa lakini tujenge mahusiano baina yetu" alisema Mwalimu Queen.Mwalimu Queen aliwaomba ,kuendelea kuongeza idadi ya wanachama ndani ya jumuiya kuanzia ngazi za chini na kulipia kadi kwani ndio mtaji wa kisiasa .Nae mwenyekiti wa UWT Mkoani Pwani ,Farida Mgomi aliwasihi wanawake kujishughulisha na kujiunga vikundi ili kujikomboa kimaisha na kuondokana na utegemezi .

Alisema kuwa ,kwasasa wanajenga Pwani mpya ,CCM mpya na UWT mpya hivyo umoja na mshikamano ndio nguzo pekee kwao.Farida aliahidi kwa niaba ya UWT mkoani hapo, kuyafanyia kazi maagizo waliyopatiwa kwa hali na mali kwa kuzingatia kwamba umoja huo ni chachu ya maendeleo kwa Taifa .

Awali Katibu Mkuu UWT Taifa na Naibu Katibu Mkuu UWT Taifa ,walichukua muda mchache wa kuzungumza na kamati hiyo kwa siri ikiwa ni sehemu ya kukumbushana majukumu yao katika utekelezaji wa ilani ya CCM na kusimamia kundi la wanawake .
Katibu wa UWT Taifa ,Mwalimu Queen Mlozi (katikati)akizungumza na wanawake na wanachama wa UWT Mkoani Pwani. (Picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa UWT Mkoani Pwani ,Farida Mgomi ( mwenye kipaza sauti) akizungumza na akinamama wa umoja huo nje ya ofisi ya CCM mkoa ,wakati katibu wa UWT Taifa ,Mwalimu Queen Mlozi (wa kulia )alipokwenda kuzungumza na kamati ya utekelezaji ya UWT Mkoani Pwani, 
Katibu wa UWT Taifa ,Mwalimu Queen Mlozi (wa kulia )akizungumza jambo baada ya kumsimamisha Mwenyekiti wa UWT Mkoani Pwani ,Farida Mgomi ( wa kushoto) katika kikao cha kamati ya utekelezaji ya UWT Mkoani Pwani, ambapo katibu huyo alipata nafasi ya kuwaelekeza na kuwakumbusha machache kuhusu utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya kikazi wakati tukielekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi Mkuu 2020.

RAIS DKT. SHEIN AZINDUA VITUO VYA MFUMO WA KIELEKTRONI WA KUSAJILI WAKAAZI WA ZANZIBAR (E-ID CARD)

0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Vituo vya Usajili wa Vitambulisho vya Mzanzibar na Uzinduzi wa Uimarishaji Mfumo wa Usajili kielektroniki, (kushoto_ Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Haji Omar Kheri, na (kushoto) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, wakishuhudia hafla hiyo iliofanyika katika viwanja vya Ofisi hiyo Dunga Wilaya ya Kati Unguja.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kuzindua jengo la Ofisi mpya za Wilaya -Dunga pamoja na uzinduzi wa Uimarishaji wa mfumo wa matukio ya kijamii uliofanyika katika Wilaya kati Mkoa wa Kusini Unguja. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akipata maelezo ya kifundi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar Dkt. Hussein Khamis Shaaban mara baada ya uzinduzi wa Uimarishaji wa mfumo wa matukio ya kijamii na Jengo la Ofisi mpya ya Wilaya Dunga uliofanyika leo katika Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, (kulia) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla hiyo ya Uzinduzi wa Ofisi za Wilaya za Usajili wa Vitambulisho vya Mzanzibar, katika viwanja vya Dunga Wilaya ya Kati Unguja. WANANCHI wa Mkoa wa Kusini Unguja wakifuatilia hafla ya Uzinduzi wa Mfumo wa Usajili wa Kieletroniki na Ofisi za Usajili wa Vitambulisho Wilaya ya Dunga wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, akihutubia hafla hiyo. RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa SMZ na Wafanyakazi wa Wakala wa Usajili, baada ya hafla ya uzinduzi huo, uliofanyika Dunga Wilaya ya Kati Unguja

YALIYOJIRI LEO TAREHE 5 SEPTEMBA, 2018 BUNGENI JIJINI DODOMA.

0
0


Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma, kwa Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge, Pia Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akizungumza na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma. Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge. Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (kushoto) akimsikiliza Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu (kulia) alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma. Katika mazungumzo hayo Mhe. Zungu alimuwakilisha Spika wa Bunge. Balozi huyo ambae ni mpya alikuja kwa lengo la kujitambulisha kwa Mhe. Spika na kumueleza nia ya kujenga jengo lao la Ubalozi wa Kenya hapa Jijini Dodoma katika vile viwanja walivyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli.
Mbunge wa Muleba Kusini, Mhe. Anna Tibaijuka (kushoto) akiteta jambo na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Dan Kazungu alipomtembelea leo Bungeni Mjini Dodoma.

CHAMA CHA USHIRIKA SIMIYU CHAFANYA UCHAGUZI KWA MARA YA KWANZA, VIONGOZI WAASWA KUENDESHA USHIRIKA KISASA

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wanachama wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa huo(SIMCU) katika Mkutano Mkuu wa kwanza, kwa lengo la kuchagua viongozi wa Chama uliofanyika Septemba 04, 2018 Mjini Bariadi, (wa tatu kushoto) Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Titus Kamani na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Simiyu(SIMCU), Bw. Charles Madata .
Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahim Kadudu (kulia) akipokea maelekezo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anthony Mtaka, katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu(SIMCU), uliofanyika Septemba 04, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kupata viongozi wa chama hicho.


Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Titus Kamani (kulia) akiteta jambo na Mrajisi Msaidizi wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahim Kadudu (katikati) mara baada ya Mkutano Mkuu wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu(SIMCU), uliofanyika Septemba 04, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kupata viongozi wa chama hicho.
Baadhi ya wanachama wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu(SIMCU) wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika Mkutano Mkuu wa kwanza wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu(SIMCU), uliofanyika Septemba 04, 2018 Mjini Bariadi kwa lengo la kupata viongozi wa chama hicho.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu- Simiyu Co-Operative Union (SIMCU) kimefanya Uchaguzi wa Viongozi wa Chama hicho, ikiwa ni kwa mara ya kwanza kwa Chama hicho kufanya Mkutano wake Mkuu, tangu kuanzishwa kwake baada ya Simiyu kujitoa Uanachama kwenye Vyama vya Ushirika vya NYANZA na SHIRECU.

Katika Mkutano huo uliofanyika Mjini Bariadi Septemba 04, 2018, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amewataka viongozi waliochaguliwa kuendesha ushirika wa kisasa ambao utakuwa wa tofauti huku akihimiza SIMCU kuwekeza katika maendeleo ya elimu, afya na ujenzi wa vitega uchumi.

“Viongozi vaeni mawazo ya kisasa muendeshe Ushirika kisasa, ningependa kuona Chama chetu cha Ushirika cha mkoa(SIMCU) kinajipambanua kwenye maendeleo hasa elimu na afya; wekezeni katika kujenga vitega uchumi, haiwezekani mkusanye zaidi ya bilioni moja kutokana pamba kwenye AMCOS halafu mkashindwa kujenga vitega uchumi” alisema Mtaka.

Naye Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Titus Kamani amewaasa viongozi wa SIMCU pamoja na vongozi wa Vyama vya Ushirika vya msingi (AMCOS) kusimamia ushirika mkoani humo kwa uadilifu na kuiacha historia ya zamani ambayo baadhi ya viongozi walichukulia ushirika kama mahali pa kupiga dili na mali isiyo na mwenyewe.

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Simiyu(SIMCU), Bw. Charles Madata, amesema atahakikisha SIMCU inafanya mambo ya maendeleo kama Mkuu wa Mkoa huo alivyosema, ikiwa ni pamoja na kuwekeza katika elimu, afya, kujenga vitega uchumi na kusimamia Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) ili vijiendeshe kibiashara.

Aidha, Madata amebainisha mikakati yake mingine kuwa ni kusimamia nidhamu ya matumizi ya fedha na mali za Ushirika, kutafuta soko la pamba ndani na nje, ili bei ya pamba iweze kupanda na kufikia zaidi ya shilingi 1500/= na kuwahamasisha wakulima kujiunga na ushirika ili kuboresha maisha yao.

Nao wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) ambavyo ndivyo vinavyounda Chama cha Ushirika cha Mkoa(SIMCU) wamesema, wana matumaini makubwa na Chama hicho na wanaamini kitawasaidia katika kuboresha bei ya zao la pamba, kama ilivyoanza kuonekana katika baadhi ya AMCOS wakati wa msimu wa mwaka 2018.

“Tunaimani SIMCU itatusaidia kuimarisha bei ya pamba , mwaka huu bei elekezi ilikuwa 1100/= lakini kupitia mpango wa wenye makampuni kununua kupitia AMCOS baadhi ya maeneo bei iliongezeka ikafikia 1250/=, tunajua viongozi watasimamia tutapata bei nzuri na wakulima tutanufaika kupitia ushirika” alisema Magima Mageme mwanachama kutoa Itilima

“Ushirika ukisimamiwa vizuri unawasaidia wakulima mambo mengi, mwaka huu wakulima walikuwa wanapewa hela zao cash(taslimu) na wanunuzi wa pamba wa makampuni maana hela zote zilikuwa zinaletwa kwenye AMCOS, viongozi wetu tuliowachagua leo watusaidie kusimamia ushirika vizuri” alisema Nkumbamboi Mchunga wa Budalabujiga.

Naye Mrajisi Msaidizi wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Ibrahim Kadudu, amesema Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Simiyu(SIMCU), kitakuwa na wanachama (Vyama vya Ushirika vya msingi (AMCOS) 379, huku akibainisha kuwa AMCOS hizo hadi sasa zimezalisha takribani kilo milioni 100.4 za zao la pamba.

Bw. Kadudu amesema kutokana na uzalishaji huo wa kilo milioni 100.4 za zao la pamba AMCOS zimepata bilioni 3.3 kutokana na ushuru ambao AMCOS inapata shilingi 33/= kwa kila kilo moja ya pamba na Chama cha Ushirika cha Mkoa (SIMCU) kitapokea shilingi Bilioni moja na milioni 40 kutokana na ushuru wa shilingi 10/= katika kila kilo moja ya pamba.

Viongozi wa SIMCU waliochaguliwa ni pamoja na Charles Madata(Mwenyekiti), wajumbe wngine ni Mabula Bwire, Emmanuel Mboi, Simon Magoma, Kulwa Bupuma, Filimoni Sambe na Tuma Magagi.

Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu amuwakilisha Spika Ndugai kupokea cheti kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA)

0
0


 Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala Mhe. Mussa Zungu (katikati) anaemuwakilisha Spika Ndugai akikabidhiwa cheti kutoka kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kushoto) ikiwa ni Shukrani kwa Kujitoa kwao katika Shughuli Mbali mbali zilizoratibiwa na Baraza hilo, moja ya tukio likiwa ni upimaji wa Virusi vya Ukimwi kwa hiari, baada ya kikao kilichofanyika leo Bungeni Jijini Dodoma. kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa
V25A6686
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu anaemuwakilisha Spika Ndugai, Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi wakimsikiliza Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kulia) wakati akiwashukuru Waheshimiwa kwa Kujitoa katika Shughuli Mbali mbali zinazohusiana na  Baraza hilo, moja wapo likiwa ni upimaji wa Virusi vya Ukimwi kwa hiari.
V25A6717
Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa (katikati) akizungumza na ugeni kutoka Ubalozi wa Marekani wanahusika na utekelezaji wa Miradi ya Ukimwi, Wajumbe wa kamati hiyo. Ugeni ulioongozwa na Mratibu Mkazi wa PEPFAR, Ndg. Brian Rettmann (kulia kwake) katika kikao kilichofanyika leo Bungenii Jijini Dodoma.
V25A6706
Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (mwenye tai nyeusi mbele), anaemuwakilisha Spika Ndugai akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi na Watendaji Wakuu kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), baada ya kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi, Mhe. Oscar Mukasa na kulia kwake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (NACOPHA), Ndg. Deogratius Rutatwa (Kulia)

Ujumbe Kutoka MCT Wakutana na Katibu Mkuu Wizara ya Habari Leo

0
0









Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Suzan Mlawi akizungumza wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) na Baraza la Habari Tanazania (MCT), walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo.[/caption]

Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi akizungumza wakati wa kikao baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Suzan Mlawi(wapili kushoto) na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) pamoja na Baraza la Habari Tanazania (MCT), walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Kiongozi wa MCT, James Marenga, na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William. Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akipokea nyaraka yenye mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kutoka kwa Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), Wallace Maugo(kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI)na MCT walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo hayo leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi, Rodney Thadeus, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William(katikati). Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akimsikiliza kwa makini kiongozi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), James Marenga (kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) na Baraza la Habari Tanazania (MCT), walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari –MAELEZO, Bibi. Zamaradi Kawawa, Mkurugenzi Msaidizi, Rodney Thadeus, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William na mjumbe wa bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo. Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari – MAELEZO, Rodney Thadeus akichangia mada wakati wa kikao baina ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(wanne kushoto) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa Jumuiya ya Watetezi wa Haki za Kupata Taarifa na Baraza la Habari Tanazania (MCT), walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 leo jijini Dodoma. Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akimsikiliza kwa makini Mjumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI), Dkt. Samwilu Mwafisi (kulia) wakati wa kikao baina yake na wajumbe wa muunganiko huo na Baraza la Habari Tanazania (MCT), walipofika wizarani hapo kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo ya maboresho ya Sheria ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William, Mjumbe wa Bodi ya Baraza la Habari Tanazania (MCT), Wallace Maugo na Kiongozi wa MCT, James Marenga. Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi.Suzan Mlawi(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Muungano wa Watetezi wa Haki ya kupata Taarifa (CORI) pamoja na Baraza la Habari Tanzania (MCT) mara baada ya kumaliza kikao leo Jijini Dodoma. Waliokaa kutoka kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya MCT, Wallace Maugo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi, Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Nicholaus William, na Mshauri wa Mradi wa Ufuatiliaji wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOM), Dkt. Samwilu Mwafisi. (Picha na: Idara ya Habari – MAELEZO).
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images