Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

FLYOVER YA TAZARA YAKAMILIKA KWA ASILIMIA 98-MAJALIWA

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesemaujenzi wa barabara ya juu katika eneo la Tazara umekamilika kwa asilimia 98 na itafunguliwa Oktoba mwaka huu na Rais Dkt. John Magufuli.


Mradi wa barabara ya juu (Mfugale flyover) chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani, unalengo la kupunguza msongamano wa magari katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere.Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 29 ,2018) baada ya kukagua ujenzi wa mradi huowa barabara ya juu katika eneo la Tazara jijini Dar Es Salaam. 

Waziri Mkuu amesema ameridhishwa kazi ya umaliziaji wa mradi huo inayoendelea kwenye hilo.“Mradi utapunguza muda wa usafiri katika barabara ya Nyerere hususani kwa wananchi wanaotoka katikati ya jiji kwenda uwanja wa ndege na wanaotoka Buguruni, Temeke.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi Mkoa wa Dar Es Salaam watafute eneo kwa ajili ya wafanyabiashara ndogondogo ili waweze kuondoka kandokando ya barabara hizo za juu zinazojengwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Isack Kamwelwe kuhusu barabara ya juu ya TAZARA wakati alipokagua hatua za mwisho za ujenzi wa barabara hiyo jijini Dar es salaam Agosti 29, 2018. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua hatua za mwisho za ujenzi wa barabara ya juu ya eneo la TAZARA wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo jijini Dar es salaam Agosti 29, 2018. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale kuhusu ujenzi wa barabara ya juu ya eneo la TAZARA wakati alipokagua hatua za mwisho za ujenzi wa barabara hiyo jijini Dar es salaam Agosti 29, 2018. Watatu kushoto ni Waziri wa Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Isack Kamwelwe na watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaaam, Paul Makonda.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kukagua hatua za mwisho za ujenzi wa barabara ya juu katika eneo la TAZARA jijini Dar es salaam Agosti 29, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alikagua ujenzi wa barabara za juu katika eneo la Ubungo jijini Dar es salaam Agosti 29, 2018. Watatu kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Isack Kamwelwe na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.

Mzee Mwinyi amuombea dua na kumjulia hali Dkt. Kigwangalla MOI

0
0
RAIS Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi leo Agosti 29,2018 amemtembea na kumuombea dua maalum Dkt Hamisi Kigwangalla ambaye anapata matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI akiuguza majeraha ya mkono aliyopata katika ajali iliyotokea Agosti 4, mwaka huu Mkoani Manyara.

Mzee Mwinyi aliambatana na Mkewe Bi. Siti Mwinyi ambapo wamemjulia hali pamoja na kufanya dua hiyo ili aweze kupona haraka kurejea kwenye majukumu yake ya kitaifa.“Nimefika leo kukujulia hali na upokee dua hii upone haraka. Sisi tunaendelea kukuombea muda wote kwa muumba” alieleza Mzee Mwinyi.

Kwa upande wake Dkt. Hamis Kigwangalla amemshukuru Mzee Mwinyi na Mama Mwinyi kufika kumjulia hali ambapo awali alimuelezea kuwa anaendelea vizuri na muda wowote ataruhusiwa.“Nashukuru kufika kwenu na sasa naendelea na mzoezi vizuri huku kubwa nikisubiria ruhusa ya Madaktari wanaoendelea kunipatia matibabu” alieleza Dkt. Kigwangalla.

Katika hatua nyingine kwa sasa Dkt. Kigwangalla afya yake imeendelea kuimarika zaidi ambapo jana jioni ya Agosti 28, ameweza kutembea umbali wa zaidi ya Kilometa Nane ambapo hii ni hatua nzuri kwani kila siku amekuwa akiongeza umbali wa kutembea kwa lengo la kufanya mazoezi ya viungo vyake.

Dkt Kigwangalla alihamishiwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI tarehe 12/08/2018 baada ya kupata matibabu ya awali katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na kwa sasa bado anaendelea na tiba kuuguza mkono wake wa kushoto.
Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamuhuli ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi akiteta jambo alipomtembelea kumjulia hali Dkt Hamisi Kigwangalla ambaye anapata matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI akiuguza majeraha ya mkono. Kushoto ni Mke wa Mzee Mwinyi, Bi. Siti Mwinyi.

Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyeketi (katikati) akiongoza dua maalum kumuombea Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamisi Kigwangalla (kulia)ambaye anapata matibabu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI akiuguza majeraha ya mkono. Aliyekaa kushoto ni Mke wa Mzee Mwinyi, Bi. Siti Mwinyi.

VIONGOZI WA DINI WAWE SEHEMU MUHIMU KATIKA MIKAKATI YA KUJIKINGA NA EBOLA.

0
0
Na Editha Karlo,wa blog ya jamii Kigoma

VIONGOZI wa dini zote wametakiwa kushirikishwa kwenye maandalizi ya mapambano ya ugonjwa wa ebola ambao umetaatifiwa upo nchi jirani ya Jamhuri ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo endapo itatokea utaingia nchini Tanzania ili kuweza kuutokomeza kabisa.

Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi wakati alipotembelea Mkoa wa Kigoma akiongozana na timu yake ya wataalam kwa ajili ya ukaguzi wa nyenzo na afua mbalimbali zilizowekwa ili kupambana na ugonjwa wa ebola leo Mkoani humo.

"Afua muhimu ya mkoa wowote katika kupambana na ugonjwa huu ni kuwashirikisha vizuri viongozi wa dini zetu pamoja na viongozi wa kimila na jamii kwani ndio wanaokutana na wanajamii kwa muda mwingi zaidi hivyo kuwashirikisha kwao elimu juu ya kujikinga na Ebola itakuwa kubwa zaidi na hatimae tutafanikiwa kujikinga na ugonjwa huu" alisema Prof. Bakari.

Aidha Prof. Bakari Kambi amesema kuwa Mkoa wa Kigoma upo kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa wa Ebola kwa kuwa kuna mipaka mingi iliyo wazi ambayo inaingiza wageni kutoka Burundi na Congo ambapo ugonjwa huo umetaarifa upo maeneo ya nchi ya Congo.

Mbali na hayo Prof. Bakari Kambi ameuoingeza uongozi wa Mkoa wa Kigoma kwa jitihada na mikakati waliyoiweka na kuifanyia kazi ili kuweza kudhibiti ugonjwa wa Ebola endapo utaingia Mkoani humo. Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chaote amesema kuwa Kigoma amesema kuwa hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyeripotiwa kuwa na dalili za ugonjwa wa Ebola katika maeneo yote ya Mkoa huo.

"Utambuzi wa joto la Mwili kwa wageni kutoka nchi jirani ya Congo wanaoingia kupitia bandari ya Kigoma, Manyovu, Kibirizi, Mabamba , Uwanja wa Ndege , Kituo cha Gari Moshi bado unaendea kufanyika kwa uhakika kwa kutumia Thermo scanner ili kudhibiti ugonjwa huo" alisema Dkt. Chaote.

Aidha Dkt. Chaote amesema kuwa bado wanaendelea kutoa elimu kwa jamii, watumishi wa Afya, madereva wa magari ya kubebea wagonjwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kujikinga na ugonjwa huo endapo utaingia nchini. "Tumetoa mafunzo kwa timu za kitaalam mbalimbali za Mkoa pamoja na kuhakikisha madawa, vifaa tiba na PPE vipo vya kutosha wakati wote katika vituo vyote vilivyoanishwa kupokea na kutoa huduma kwa wagonjwa wa Ebola" alisema Dkt. Chaote.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Kambi ameambatana na jopo la wataalam ikiwemo idara ya uhakiki ubora wa huduma za afya , Kitengo cha Dharura na Maafa,Elimu ya Afya kwa Umma , Kitengo Cha mawasiliano Wizara ya Afya zote kutoka Wizara ya Afya pamoja na Wawakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) ili kukagua na kujiridhisha mikakati ya kujikinga na Ebola endapo itaingia nchini.



Mganga Mkuu wa serekali Prof.Mohammed Bakari akitoka kukagua moja ya mabanda yaliyopo katika bandari ya Kigoma ambayo yatatumika kumpumzisha mgonjwa mwenye dalili ya ugonjwa wa Ebola mara baada ya kushuka katika bandari ya Kigoma.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt.Paul Chawote akitoa taarifa ya ugonjwa wa ebola kwa Mganga Mkuu wa Serekali prof.Bakari Kambi kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkoa wa Kigoma

Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaombwa kuondoa kero ya kukosekana kwa vifaranga wa kuku bora nchini

0
0

Waziri Mkuu Mstaafu MIZENGO PINDA ameiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuondoa adha ya kukosekana kwa vifaranga wa kuku bora nchini, sambamba na uhaba wa upatikanaji wa chakula bora cha kuku.

PINDA ambaye pia ni Mlezi wa Chama cha Wafugaji Kuku Bora Mkoani DODOMA -CHAWAKUBODO amesema hayo leo Jijini DODOMA wakati chama hicho kikipokea msaada wa vifaranga vya kuku bora kutoka Kampuni AKM GLITTERS, ambapo amebainisha kuwa ukosefu wa vifaranga na chakula bora cha kuku imepelekea wafugaji kukosa ari ya kuendelea kufuga.

Kwa upande wake Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi ABDALLAH ULEGA amekiri kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa chakula bora cha kuku nchini na kusema kuwa suala hilo ni lazima lishughulikiwe ili kumaliza tatizo hilo kwa wafugaji wa kuku .Pia Naibu Waziri ULEGA amebainisha kuwa kukosekana kwa vifaranga bora nchini kumetokana na udhibiti wa uingizwaji holela wa vifaranga vya kuku na kubainisha kuwa hivi sasa tatizo hilo lipo katika hatua za utatuzi na kwamba hali ya upatikanaji wa vifaranga itarejea kama zamani.

"Tumekubaliana lazima kuwe na udhibiti wa utotoleshaji wa vifaranga kiholela na utengenezaji wa vyakula vya mifugo jambo litakalosaidia kuondoa tatizo la kuwa na vifaranga na vyakula visivyo na ubora" alisema Waziri Ulega.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjinj PATROBAS KATAMBI amewapongeza wafugaji hao na kusema kuwa kwa sasa sekta ya ufugaji inakua hivyo ni lazima changamoto zilizopo ziweze kutatauliwa. Chama cha Ushirika wa Wafugaji Kuku Mkoa wa DODOMA kimepokea msaada wa vifaranga elfu nne ikiwa ni awamu ya kwanza ya msaada huo.



Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi ABDALLAH ULEGA akimkabidhi Vifaranga bora mmoja wa wachama chama cha Wafugaji Kuku Bora Mkoani DODOMA -CHAWAKUBODO mapema leo mjini Dodoma,kuku hao wametolewa na kampuni ya AKM GLITTERS,huku Mlezi wa Chama hicho CHAWAKUBODO Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda akishuhudia
Makabidhiano ya Vifaranga bora kwa Chama cha Wafugaji Kuku Bora Mkoani DODOMA -CHAWAKUBODO,yakifanyika kwa baadhi ya wanachama wa chama hicho kutoka kwa viongozi wa mkoa wa Dodoma akiwemo mkuu wa wilaya ya Dodoma Mh.Patrobas Katambi.
Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi (MB) Abdallah Ulega akizungumza mapema leo kwenye hafla fupi ya kukabidhi Vifaranga bora kwa wachama wa chama cha Wafugaji Kuku Bora Mkoani DODOMA -CHAWAKUBODO mapema leo mjini Dodoma,kuku hao wametolewa na kampuni ya AKM GLITTERS
Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi ABDALLAH ULEGA,Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mh.Patrobas Katambi pamoja na Mlezi wa chama cha Wafugaji Kuku Bora Mkoani DODOMA -CHAWAKUBODO wakionesha vifaranga bora kwa wanachama wa CHAWAKUBODO,vifaranga hivyo vimetolewa na kampuni ya AKM GLITTERS

TCRA YASHIRIKI VYEMA WIKI YA ZIMAMOTO DODOMA

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kulia) na Kamishna Jerenali wa Zimamoto, Thobias Andengenye wakisikiliza maelezo kutoka kwa ofisa Mwamdamizi wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mabel Masasi juu ya huduma za anuani za makazi zinavyoweza kusaidia utoaji haraka wa huduma za zima moto na uokoaji nchuni. Waziri Lugola alikuwa akitembelea mabanda ya maonesho ya wiki ya Zimamoto Nchini, iliyozinduliwa Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ni miongoni mwa taasisi za serikali zilizoshiriki katika maonesho ya Wiki ya Zimamoto na Uokoaji kitaifa ambayo inafanyika jijini Dodoma kwa mara ya kwanza nchini.

Lengo kuu la maadhimisho hayo ni kutoa elimu juu ya namna bora ya kuepuka majanga ya moto na kuwawezesha wananchi kuzifahamu vyema shughuli nyiongi zinazofanywa na jeshi hilo ambazo si tu kuzima moto kama inavyofahamika na wananchi wengi lakini ni pamoja na kusaidia katika majanga mbalimbali na ajali.

TCRA kama mdau mkubwa wa zimamoto mbali na kusaidia katika mawasiliano baina ya wananchi na Jeshi la Zimamoto kuwa rahisi na ya bure kwa mujibu wa sheria lakini pia kupitia mradi wao wa anuani za makazi unasaidia Jeshi hilo na wananchi kuweza kufikiwa kirahisi.

Ofisa Mwandamizi Mkuu wa Mawasiliano, Mabekl Masasi alimwambia Waziri Kangi lugola kuwa kupitia anuania za makazi zimeweza kurahisisha jeshi hilo kufika katika maeneo mengi kirahisi kwa kutaja jina la mtaa na namba ya nyumba la eneo husika. 
 Waziri wa Mambi ya Ndani, Kangi Lugola akiuliza jambo katika banda hilo la TCRA 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (wapili kulia) na Kamishna Jerenali wa Zimamoto, Thobias Ndengenye wakisikiliza maelezo kutoka kwa maofisa wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) juu ya huduma za anuani za makazi zinavyoweza kusaidia utoaji haraka wa huduma za zima moto na uokoaji nchuni. Waziri Lugola alikuwa akitembelea mabanda ya maonesho ya Siku ya Zimamoto Nchini, Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma jana.
Wananchi na maofisa mbalimbali wa Jeshi la Zimamoto wakiwa katika Banda la TCRA kupata vipeperushi na maelezo mbalimbali ya kazi za taasisi hiyo.

AFISA MIRADI UMOJA WA ULAYA AFANYA ZIARA SHINYANGA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUTOKOMEZA MILA NA DESTURI KANDAMIZI KWA WATOTO

0
0
Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union - EU) John Villier amefanya ziara ya kutembelea na kujionea maendeleo ya mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni mkoani Shinyanga unaotekelezwa na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto la Save The Children.

Ziara hiyo imeanza Jumatano Agosti 29,2018 kwa Afisa Miradi huyo kukutana na wadau wanaoshiriki katika kutekeleza mradi huo wakiwemo viongozi wa serikali ya mkoa wa Shinyanga, Shirika la Save The Children na Shirika la Agape Aids Control Programme (AACP) ambao kwa pamoja wanaendelea kushirikiana katika kufanikisha mradi huo.

Akiwa katika ziara yake, John Villier pia amekutana na wanafunzi wa shule ya Msingi Mwamashele iliyopo kata ya Mwamashele kupitia “Tuseme Club” pamoja na kikundi cha watu wazima katika kijiji cha Itilima kata ya Itilima halmashauri ya wilaya ya Kishapu ambao hukutana na kujadili namna ya kukabiliana na mila na desturi kandamizi.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo,Villier alieleza kufurahishwa na jinsi mradi huo wa kutokomeza mila na desturi kandamizi unavyotekelezwa kwani umesaidia kupunguza mimba na ndoa za utotoni mkoani Shinyanga.

“Nimefurahi kuona kazi kubwa inayofanywa na Save The Children na AGAPE kwa kuwa na ushirikiano wa karibu na serikali pamoja na jamii katika kupiga vita mila na desturi kandamizi ambazo zinasababisha watoto wakose haki zao na kushindwa kutimiza ndoto zao,naomba tuendelee kushirikiana zaidi ili kuwakomboa watoto wanaopewa mimba na kuolewa katika umri usiotakiwa”,aliongeza Villier.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew aliushukuru Umoja wa Ulaya kwa kufadhili mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Save The Children na kueleza kuwa kumekuwepo mafanikio makubwa akibainisha kuwa sasa jamii imebadilika na imeanza kuachana na mila na desturi kandamizi.

“Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na sekta binafsi,Umoja wa Ulaya na Save The Children tunatambua mchango wenu,kwa kweli sasa mila na desturi potofu zimeanza kupungua katika baadhi ya maeneo,mafanikio haya yanatokana na nyinyi kuwa karibu na serikali na wadau wengine”,alieleza

Aidha alisema mradi huo umekuwa chachu kwa maafisa maendeleo ya jamii kuwajibika zaidi kwa kuyafikia maeneo ya pembezoni ambayo haikuwa rahisi kuyafikia na kuwapa elimu wananchi.

Naye Naibu Mkurugenzi Uendeshaji Miradi Kutoka Shirika la Save The Children nchini Tanzania, Jesse Orgenes alisema shirika hilo litaendelea kushirikiana na serikali na wadau wote wa maendeleo katika kupiga vita mila na desturi potofu katika jamii.
Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akifanya mazungumzo na viongozi wa Shirika la Save The Children katika ofisi za Shirika hilo Mjini Shinyanga leo Jumatano Agosti 29,2018 - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde
Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akizungumza na viongozi wa Shirika la Save The Children na kuhoji masuala mbalimbali kuhusu Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni unaotekelezwa na Shirika la Save The Children kwa kushirikiana na Shirika la Agape Aids Control Programme (AACP) la Mjini Shinyanga wilaya ya Kishapu na Kahama mkoani Shinyanga.
Naibu Mkurugenzi Uendeshaji Miradi Kutoka Shirika la Save The Children nchini Tanzania, Jesse Orgenes akifafanua namna wanavyotekeleza mradi wa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi katika mkoa wa Shinyanga.
Kushoto ni Naibu Mkurugenzi Uendeshaji Miradi Kutoka Shirika la Save The Children nchini Tanzania, Jesse Orgenes akielezea namna jamii inavyoshirikishwa katika mradi huo ili kuufanya uonekane ni wa jamii na siyo wa shirika.
Katikati ni Meneja wa Shirika la Save The Children Mkoa wa Shinyanga Benety Malima akielezea namna wanavyoshirikiana na shirika la AGAPE katika kutekeleza mradi wa Mila na Desturi Kandamizi katika mkoa wa Shinyanga. 
Meneja wa Shirika la Save The Children Mkoa wa Shinyanga Benety Malima akizungumza katika kikao hicho na kubainisha kuwa serikali ya mkoa wa Shinyanga imekuwa ikitoa ushirikiano mkubwa katika kufanikisha mradi wa kutokomeza mila na desturi kandamizi mkoani Shinyanga.
Wa pili Kulia ni Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni ,Mary Zabron akisisitiza jambo katika kikao hicho.
Hapa ni katika Ofisi ya Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga : Kulia ni Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew.
Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akifurahia jambo wakati akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew.
Wa pili kushoto ni Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akielezea lengo la ziara yake mkoani Shinyanga kwa Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew (katikati).
Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew akielezea mchango unaotolewa na Umoja wa Ulaya na Shirika la Save The Children katika kutetea haki za watoto ikiwa ni pamoja na kupiga vita mila na desturi kandamizi zinazochangia kuwepo kwa ndoa na mimba za utotoni.
Kaimu Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga George Andrew akiwaomba wadau wa maendeleo kuendelea kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya ndoa na mimba za utotoni.
Hapa ni katika Ofisi za Shirika la AGAPE Mjini Shinyanga : Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE John Myola akimwelezea Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier jinsi wanavyoshirikiana na shirika la Save The Children katika kutekeleza mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni mkoani Shinyanga.


Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akisaini kitabu cha wageni katika ofisi za shirika la AGAPE.




Hapa ni katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Kishapu : Kushoto ni Meneja wa Shirika la Save The Children Mkoa wa Shinyanga Benety Malima akimtambulisha Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier. Katikati ni Mkurungezi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Mang'era Mang'era.




Wa pili kushoto ni Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akieleza malengo ya ziara yake katika wilaya ya Kishapu.




Mkurungezi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu, Mang'era Mang'era akiushukuru Umoja wa Ulaya kwa kufadhili mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni ambao unatekelezwa na shirika la Save The Children kwa kushirikiana na shirika la AGAPE.




Ndani ya Ofisi ya Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Mwamashele wilayani Kishapu : Kushoto ni Afisa Miradi 'Afisa Programu' kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akiuliza swali kwa Mwalimu mku wa shule hiyo Justin Claud (wa kwanza kushoto) kuhusu changamoto zinazojitokeza kwenye 'Tuseme Club' ya wanafunzi wa shule hiyo. Jumla ya Tuseme Club 12 zipo katika shule 12 wilayani Kishapu. Klabu hizo zinasimamiwa na shirika la AGAPE kwa kushirikiana na Shirika la Save The Children.




Wanafunzi katika shule ya Msingi Mwamashele ambao wanaunda 'Tuseme Club' wakicheza mchezo ikiwa ni sehemu ni ya kupeana elimu juu ya madhara ya mimba na ndoa za utotoni.




Afisa Miradi kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier na viongozi wa shirika la Save The Children wakishuhudia elimu iliyokuwa inatolewa na walimu wa shule ya msingi Mwamashele kwa Klabu ya wanafunzi 'Tuseme Club'.




Kushoto ni Mwalimu Kalunde Majid akiendelea na kipindi kwa wanafunzi wa 'Tuseme Club'.




Afisa Miradi kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akifuatilia kwa makini kilichokuwa kinaendelea darasani.




Wanafunzi wakionesha kwa vitendo kazi ya kuosha vyombo kuwa inafanywa na watu wa jinsi zote zote yaani kiume na kike na siyo kazi ya wanawake/wasichana tu.




Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni nchini ,Mary Zabron akiuliza swali kwa wanafunzi wa shule ya msingi Mwamashele.




Mwanafunzi akinyoosha mkono ili ajibu swali kuhusu madhara ya ndoa na mimba za utotoni.




Hapa ni katika kijiji cha Itilima kata ya Itilima wilayani Kishapu : Afisa Miradi kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier akijitambulisha kwa kikundi cha wananchi wa rika mbalimbali katika kijiji cha Itilima waliokuwa wanaendelea na mdahalo kujadili namna ya kuondokana na mila na desturi kandamizi ili kupiga vita ndoa na mimba za utotoni. 




Afisa Miradi kutoka Umoja wa Ulaya (European Union) John Villier alisema alifarijika kuona namna wananchi wa kata ya Itilima walivyohamasika kujitoa kupiga vita mila na desturi kandamizi kwa watoto.




Wakazi wa Itilima wakiendelea na mdahalo kuhusu mila na desturi kandamizi.




Mdahalo unaendelea.




Mkazi wa Itilima akichangia hoja wakati wa mdahalo huo.




Wa pili kulia ni Mratibu wa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni nchini ,Mary Zabron akiwaomba wananchi kuacha kufumbia macho mila na desturi zinazomkandamiza mtoto na kusababisha akose haki zake.




Mkazi wa Itilima Peter Mulwano 'Mzee Goma' akilishukuru shirika la Save The Children na AGAPE kuwafikia wananchi wa Kishapu kupitia mradi huo.




Afisa Mradi wa Kutokomeza Mila na Desturi Kandamizi zinachochangia ndoa na mimba za utotoni kutoka shirika la AGAPE, Peter Amani akizungumza wakati wa mdahalo huo.




Naibu Mkurugenzi Uendeshaji Miradi Kutoka Shirika la Save The Children nchini Tanzania, Jesse Orgenes akiwataka wananchi kubadilika na kuachana na mila na desturi potofu zinachochangia kuwepo kwa mimba na ndoa za utotoni.


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

MAKALA: WAFANYABIASHARA CHANGAMKIENI MSAMAHA WA RIBA NA ADHABU YA KODI

0
0
Na Veronica Kazimoto ,Dar es Salaam 

Hivi karibuni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) ilitoa msamaha maalum wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100 tofauti na asilimia 50 ya hapo awali. 

Msamaha huu umetokana na malalamiko ya wafanyabiashara waliyoyatoa kwa Mhe. Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli ya kuwepo kwa malimbikizo makubwa ya madeni ya kodi za nyuma yakijumuisha riba na adhabu wakati wa Mkutano wa 11 wa Baraza la Taifa la Biashara (TNBC) uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam mnamo tarehe 19 Machi, 2018. 

Kufuatia malalamiko hayo, Rais aliwaambia wafanyabiashara hao kuzungumza na Wizara ya Fedha na Mipango ili waweze kupunguziwa riba na adhabu za madeni yao ya kodi. 

"Suala la kodi ni very sensitive (nyeti sana) hata Rais unaweza kushtakiwa kwa kukwepa kodi, mimi niwaombe wale mnaodaiwa kwa miaka ya nyuma nendeni mka-negotiate (mkajadiliane) na Wizara ya Fedha, ninajua kuna kipengele ambacho kinaweza kuwapunguzia", alisema Rais Magufuli. 

Dk. Magufuli alitumia baraza hilo pia kuwasisiza wafanyabiashara kulipa kodi ambapo alisema "Tunahitaji kodi kwa ajili ya survival (kudumu) ya nchi hii, mtu ajue kwamba kulipa kodi ni wajibu wake na kukwepa kodi is a big crime (kosa kubwa). Hivyo ninawaomba wafanyabiashara msikwepe kulipa kodi, mjitahidi kulipa kwa maana kodi hizi ndio zinatusaidia kuijenga nchi yetu". 

Baada ya mkutano huo wa baraza la biashara, Bunge la Tanzania katika kikao chake cha bajeti cha Mwaka wa Fedha 2018/19 cha mwezi Juni, 2018 lilipitisha marekebisho ya Kifungu cha 70 cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 ili kumpa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya Fedha ya kutunga kanuni maalum za kutoa msamaha wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi ya nyuma. 

Kupitia marekebisho hayo, Waziri wa Fedha na Mipango, alimpa Mamlaka Kamishna Mkuu wa TRA kutoa msamaha maalum wa riba na adhabu kwenye malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100 tofauti na asilimia 50 ya awali. 

Ni kufuatia mamlaka hayo, Kamishna Mkuu wa TRA Charles Kichere alitangaza msamaha huo maalum mnamo tarehe 11 Julai, 2018 kwa lengo la kutoa unafuu kwa walipakodi wenye malimbikizo ya madeni ya riba na adhabu kwa kuwapa fursa ya kulipa kodi ya msingi (principal tax) mara moja au kwa awamu ndani ya mwaka wa fedha wa 2018/19. 

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu Kichere alisema kuwa msamaha wa riba na adhabu unahusu kodi zote zinazotozwa kwa mujibu wa Sheria zinazosimamiwa na TRA ambazo ni Sheria ya Kodi ya Mapato sura. 332, Kodi ya Uendelezaji Ufundi Stadi sura 82, Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani sura 148; Sheria ya Ushuru wa Stempu sura 189, Sheria ya Ushuru wa Bidhaa sura 147, Sheria ya Ada ya Huduma za Bandari sura 264 pamoja na Sheria ya Ada ya Huduma ya Viwanja vya Ndege sura 365. 

Hivyo basi, mapato yasiyo husika na utaratibu huu ni yale yasiyo ya kodi ambayo TRA imepewa jukumu la kisheria la kukusanya kwa niaba ya Serikali za Mitaa, Wakala na Taasisi za Serikali. Mapato hayo ni kama vile Kodi katika Michezo ya Kubahatisha, Kodi za Majengo, Tozo ya kuendeleza utalii, Tozo ya kuendeleza Reli na Ada za Matangazo. 

Aidha, katika mkutano huo wa waandishi wa habari, Kamishna Mkuu Kichere aliwataja walengwa wa msamaha huu ambapo alisema "Walengwa wa msamaha huu ni makampuni, taasisi na watu binafsi ambao wamewasilisha ritani ya kodi lakini bado wanadaiwa kodi yote au sehemu ya kodi zitokanazo na ritani hizo, hawajawasilisha ritani za kodi, hawajasajiliwa na kupatiwa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) au Namba ya Usajili wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na wale walio wasilisha pingamizi au rufaa za kodi ambazo bado zinashughulikiwa katika ofisi za TRA, Bodi ya Rufaa na Mahakama ya Rufani za kodi". 

Pia, alitaja makampuni, taasisi na watu binafsi ambao hawahusiki na msamaha huu kuwa ni wale ambao wangestahili kupata msamaha lakini tayari wameshalipa madeni yao, masuala yao ya kikodi yapo katika hatua ya ukaguzi au uchunguzi, wana madeni ya nyuma ya kodi ambayo yanatokana na kesi za jinai za kodi, utakatishaji fedha, usafirishaji wa binadamu au shughuli nyingine haramu kama ilivyothibitika kisheria, wenye madeni ya nyuma ya kodi yanayotokana na adhabu zilizoamuliwa tayari au adhabu za makosa yatokanayo na uzembe wa kukusudia uliobainika kisheria pamoja na wenye riba au faini zilizotokana na kutoa au kutumia risiti za kielektroniki za kughushi. 

"Mlipakodi atastahili kupata msamaha wa riba na adhabu endapo yeye binafsi au mwakilishi wake aliyeidhinishwa kisheria atawasilisha maombi ya msamaha kwa kutumia fomu maalum zinazojulikana kama ITX207.01.E zinazopatikana katika Ofisi za TRA mikoa yote au katika Tovuti ya TRA www.tra.go.tz na maombi yawasilishwe kwa Meneja wa Mkoa TRA au kwa Kamishna wa Walipakodi Wakubwa sambamba na kujaza Dodoso maalum la msamaha na ritani ya taarifa za mlipakodi,” alieleza Kichere. 

Kichere aliongeza kuwa, mwisho wa kuwasilisha maombi hayo ni tarehe 30 Novemba, 2018 ambapo Ofisi ya Kamishna Mkuu wa TRA itajibu kwa maandishi maombi ya msamaha huo ndani ya siku thelathini (30) tangu siku ya kupokea maombi. 

Lakini malipo ya kodi ya msingi baada ya kuondoa malimbikizo ya riba na adhabu yanaweza kufanyika mara moja au kwa awamu ndani ya mwaka wa fedha 2018/19 na mwisho wa malipo hayo ni tarehe 30 Juni, 2019. 

"Msamaha huu maalum umetolewa kwa walipakodi kwa kipindi cha miezi 6 kuanzia tarehe 1 Julai 2018 mpaka tarehe 31 Desemba 2018 na madeni yanayohusiana na msamaha huu ni yale yote yaliyolimbikizwa hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2018 isipokuwa madeni ya wafanyabiashara wapya ambao hawajasajiliwa kama walipakodi,” alifafanua Kichere. 

Ikumbukwe kwamba, mnufaika wa msamaha huu anapaswa kuwasilisha ritani zote ambazo hazikuwahi kuwasilishwa, kuingia mkataba wa makubaliano maalum na Kamishna Mkuu wa TRA utakaoanisha deni lote la kodi, riba na adhabu inayosamehewa na jinsi ya ulipaji wa kodi ya msingi kabla ya tarehe 30 Juni, 2019. Kodi ya msingi italipwa kwa mujibu wa masharti na taratibu za mkataba wa malipo na kwa mtu binafsi au taasisi ambayo ilikuwa ikifanya biashara au shughuli za uwekezaji lakini haijasajiliwa kama mlipakodi, itabidi isajiliwe kabla ya tarehe 30 Novemba, 2018. 

Hata hivyo, msamaha utatolewa kwa maombi yatakayokidhi vigezo vya masharti na kukubaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania ambapo Kamishna Mkuu wa TRA na Mlipakodi husika watasaini mkataba wa makubaliano utakaoainisha deni lote la kodi, riba na adhabu inayosamehewa, pamoja na kodi isiyo na riba wala adhabu itakayopaswa kulipwa kabla ya tarehe 30 Juni, 2019. 

Kutokana na umuhimu wa msamaha huu, Mamlaka ya Mapato Tanzania inaendelea na zoezi la kutoa semina elekezi kwa wafanyabiashara, washauri wa wafanyabishara (tax consultants) na wadau mbalimbali kote nchini ili waweze kuwasilisha maombi yao kwa usahihi na hatimaye kunufaika na msamaha husika. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa semina hizo uliofanyika katikati ya mwezi Agosti, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna wa Walipakodi Wakubwa wa Mamlaka hiyo Alfred Mregi alisema kwamba TRA ina jukumu la kuhakikisha kuwa, wafanyabiashara wengi wanajitokeza kwa wingi kuomba msamaha wa riba na adhabu ili waweze kunufaika na msamaha huo maana wamekuwa wakilalamikia suala hili kwa muda mrefu. 

"Mtakumbuka kwamba, wafanyabiashara wengi wamekuwa wakiomba kupunguziwa riba na adhabu ya malimbikizo ya kodi kwa muda mrefu. Malalamiko haya yalifikishwa hadi kwa Mhe. Rais ambaye alitoa maelekezo ya kutoa msamaha huu. Hivyo, sisi kama TRA tuna jukumu la kupeleka habari hii njema kwa wafanyabiashara wote ili wajue kwamba maombi yao yalipokelewa na sasa wanaweza kupata msamaha wa riba na adhabu kwa asilimia 100," alisema Mregi. 

Uzinduzi wa semina hizi elekezi ulihudhuriwa na wafanyabiashara wapatao 500 ambapo mmoja wa wafanyabiashara wakubwa kutoka kampuni ya Super Group of Companies inayozalisha Sukari ya Mtibwa na Kagera Ibrahim Ali alimshukuru Rais Magufuli kwa kupokea na kufanyia kazi malalamiko yao ya muda mrefu lakini pia hakusita kuishukuru TRA kwa kutoa semina elekezi ambayo imewasaidia kuelewa mambo mengi kuhusiana na msamaha huo. 

Akizungumza mara baada ya uzinduzi huo, Ali alisema "Kwa kweli mimi napenda kumshukuru Rais Magufuli kwa kusikia kilio chetu sisi wafanyabiashara na napenda pia kuishukuru TRA kwa kuanzisha programu hizi za kutoa elimu kwa wafanyabiashara ili kuongeza uelewa na namna bora ya kuwasilisha maombi ya msamaha wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya kodi, alieleza Ali. 

Mpaka sasa, semina hizi elekezi zinaelendelea kufanyika katika mikoa mbalimbali nchini na licha ya kutoa elimu hii kupitia semina, TRA inajitahidi kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari, mitandao ya kijamii pamoja na kukutana na wafanyabiashara, washauri wa wafanyabiashara na wadau mbalimbali katika majukwaa na mikutano ya mabaraza ya biashara ngazi ya mkoa na wilaya. 

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo ambaye ndiye anayeongoza gurudumu hili la kutoa elimu hii kuhusu msamaha wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya kodi pamoja na elimu ya kodi kwa ujumla, amekuwa akiwahimiza walipakodi kutumia fursa hii adhimu ili waweze kuondokana na malimbikizo ya madeni na hatimaye waweze kulipa kodi ya msingi pekee. 

Akizungumza wakati wa Jukwaa la Fursa za Biashara lililofanyika mwezi Agosti, 2018 mkoani Geita, Mkurugenzi Kayombo alisema "Nachukua fursa hii kutoa wito kwa wafanyabiashara wote wenye malimbikizo ya madeni ya kodi na wote waliokuwa wakifanya biashara bila kusajiliwa kuwasilisha maombi yao TRA ili waweze kupata msamaha huu wa riba na adhabu kwa asilimia 100 ambapo mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 30 Novemba, 2018." 

Aidha, Kayombo aliwaambia washiriki wa jukwaa hilo kuwa wasisite kuwasiliana na Mamlaka pale watakapohitaji msaada zaidi juu ya zoezi hili kwa kutembelea Ofisi za TRA zilizopo nchi nzima, kutembelea tovuti ya TRA www.tra.go.tz au Kituo cha Huduma kwa Mlipakodi kinachopatikana kwa namba za simu za bure 0800 750 075 au 0800 780 078 au kutuma barua pepe huduma@tra.go.tz

Kazi kwenu walipakodi, kile mlichokuwa mkikililia kwa muda mrefu mpaka kufikisha malalamiko yenu kwa Mhe. Rais kimefanyiwa kazi, hii inaonyesha kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano ni sikivu na inatekeleza ahadi zake kwa vitendo. Chamgamkieni fursa hii mapema kabla muda uliopangwa wa kutuma maombi haujaisha ili muweze kunufaika na msamaha huu wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100. 
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitangaza msamaha maalum wa riba na adhabu ya malimbikizo ya madeni ya kodi kwa asilimia 100 jijini Dar es Salaam Julai, 2018. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa Mamlaka hiyo Richard Kayombo.

RAIS DKT MAGUFULIA KUFANYA ZIARA MIKOA MITATU

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli, atafanya ziara ya kikazi katika mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu kati ya tarehe 3 na 10  Septemba, 2018.


ZIARA YA DC NEWALA KATIKA MIRADI YA KILIMO BIASHARA INAYOFADHILIWA NA SHIRIKA LA AGAKHAN FOUNDATION

0
0

Mkuu wa Wilaya ya Newala Aziza Mangosongo (mwenye pama), akishiriki utoaji chanjo ya ugonjwa wa kideri kwa kuku alipozindua uchanjaji huo katika kijiji cha Chihangu Wilayni Newala.

NEWALA, MTWARA
Mkuu wa Wilaya ya Newala mkoani Mtwara Aziza Mangosongo amelipongeza shirika la Agakhan  Foundation kwa kuwajengea uwezo wakulima  katika Wilaya hiyo.

Pamoja na pongezi hizo Mkuu huyo wa Wilya amesema Programu zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuinua hali ya kiuchumi kwa mtu mmoja mmoja, vikundi na jamii ya wananchi wa Newala kwa jumla.

Mkuu huyo wa wilaya alisema hayo mapema wiki hii, akiwa katika ziara ya mafunzo, Agosti 27, 2018, ambapo aliongozana  na timu ya Viongozi  na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya Newala ili kujionea  miradi ya vikundi vya wananchi katika Halmashauri hivyo.

Katika ziara hiyo, Mkuu huyo wa wilaya aliongozana na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Rashidi Ndembo , Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Mussa Chimae, Madiwani wawili wa Halmashauri ya Wilaya pamoja na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya.

Mkuu huyo wa Wilaya pamoja na ujumbe wake walitembelea Shirika lisilo la Kiserikali la Aghakani Foundation (ARF) linaloendesha Program ya Ajira  na Ujuzi (Employment and Skills)  inayolenga kuwawezesha Kaya  zipatazo 5000 za wakulima wadogowadogo  kujiongezea kipato, kujipatia chakula na kuongeza uzalishaji mali na kuongeza thamani ya mazao yao kwa Mikoa ya Lindi na Mtwara.

Programu hiyo inayo miradi ijulikanayo kama Kilimo ni Biashara  unaotekelezwa katika Wilaya ya Newala kuanzia April 2016 hadi Machi 2018, chini ya ufadhili  wa shirika la Kijerumani lisilo la Kiserikali la GTZ.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Newala alitembelea Vijiji vya Chihanga, Idamnole, Tengulengu na Kitangari, mbapo akiwa katika Kijiji cha  Chihangu yeye na msafara wake walikutana na vikundi  vya wakulima wanaofadhiliwa na Aghakhan Foundation  katika miradi ya kuongeza kipato kwa kufuga kuku wa kienyeji kisasa,  akashiriki kuzindua  chanjo ya ugojwa wa kideri  wa kuku unaoelezwa na wataalamu kuwa ndiyo  ugonjwa hatari wa kuambukiza unaorudisha nyuma usalishaji wa kuku katika Wilaya ya Newala.

Akiwa katika Kijiji  cha Idamnole  Kata ya Chihangu alikagua shughuli ya ukamuaji wa mafuta  ya Alizeti unaofanywa na wakulima  katika vikundi vilivyo chini ya mradi wa kilimo Biashara unaofadhiliwa pia na Aghakan Foundation, ambko aliona ujenzi wa nyumba bora ya mkulima unaotokana na uzalishaji  na bei nzuri ya mauzo ya zao la korosho katika Mkoa wa Mtwara, hususani Wilaya ya Newala. 

Tangu Serikali ya awamu ya tano chini ya Eais Dk. Jonh  Magufuli iingie madarakani bei ya zao la korosho imepanda na kuimarika hivyo kuwezesha wananchi kadhaa wa Wilaya ya Newala kujenga nyumba nzuri na za kisasa, Vijijini.

Baadae msafara ulielekea katika Kata ya Kitangari Kijiji cha Kitangari Tarafa ya Kitangari ambapo ulifika  kwa Wafugaji wawili wa kuku wanaofadhiliwa na Agakhan Foundation, wakulima hao wameweza kuongeza uzalishaji wa kuku kiasi cha kufuga hadi kuku 800 wa chotara ambao kwa wastani mmoja huuzwa Sh.20,000 hadi Sh. 25,000 baada ya kuhudumiwa kwa  miezi minne tu.

Agosti 28, 2018, Mkuu huyo wa Wilaya Newala alitembelea miradi ya kilimo cha Mbogamboga katika bonde la Chiunjila katika Kijiji cha Chihanga Kata ya Mkunya na kisha kwenda Kijiji cha Mapili ambako alikutana na mkulima wa nyanya na mfugaji wa kuku wa kienyeji ambaye anafuga kisasa baada ya kupata mafunzo kutoka shirika  lisilo la Kiserikali la Agakhan Foundation. 

Mkuu wa Wilaya alihitimisha ziara yake katika Kijiji cha Nanguruwe.
Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea Aziza Mangosongo akiwa na ujumbe aliokuwa nao katika ziara hiyo.

MAHAKAMA JUMUISHI MBEYA KUSOGEZA HUDUMA ZA KIBENKI NDANI YA MAHAKAMA HIYO

0
0

Viongozi wa Mahakama Kanda ya Mbeya (kushoto) wakiwa katika majadiliano na Viongozi wa Benki ya NMB, majadiliano juu ya uanzishwaji wa huduma za kibenki ili kuwarahishia wateja wanaofika katika Mahakama hiyo.Mjumbe kutoka NMB akichangia jambo katika majadiliano.
Picha ya pamoja baada ya majadiliano, (wa pili kushoto) ni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Kanda ya Mbeya. (Picha na Rajabu Singana, Mahakama Kuu, Mbeya)


Na Rajabu Singana. Mahakama Kuu Mbeya

Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, Mhe. Robert Makaramba amekutana na uongozi wa benki ya NMB na kufanya mazungumzo juu ya uanzishwaji wa huduma za Kibenki katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya linalotoa huduma kwa Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya.

Mhe. Makaramba alikutana na uongozi huo mapema Agosti 28, aliwaeleza viongozi wa NMB kwamba Mahakama ipo katika maboresho makubwa ya huduma zake kupitia mpango mkakati wa miaka mitano (2015-2020) unaolenga kumsogezea mwananchi huduma.

Kutokana na changamoto ya kufanya malipo ambayo wamekuwa wakiipata wananchi Mhe. Makaramba aliwaomba NMB kusogeza huduma zao katika jengo la Mahakama Kuu Mbeya. Akichangia katika mazungumzo hayo, Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Straton Chilongola alisema kwa sasa Benki ya NMB imekuwa ikifanya kazi kwa kushirikiana na Mawakala ambao hufanya kazi za Kibenki.

Bw. Chilongola aliongeza kwa kusema kwamba watafanya utaratibu wa kuanzisha ‘Cash Collection Point’ kwa ajili ya wananchi kufanya malipo ya Huduma za Mahakama. Meneja wa Wakala wa Benki wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bw. Respicious Denis aliongeza kuwa kwa sasa benki ya NMB imekuwa ikifanya vizuri kwa kutumia Mawakala kwenye malipo na makusanyo mbalimbali ambapo tayari baadhi ya taasisi za serikali zinatumia huduma hiyo. Alizitaja taasisi hizo ni paoja na TRA, Idara ya Maji Mbeya na walitumia mfumo huo katika makusanyo ya NaneNane mwaka huu.

Ifahamike kwamba baada ya ukarabati mkubwa wa jengo la Mahakama Kuu Mbeya, Uongozi wa Mahakama ya Tanzania ulifikia maamuzi ya kulifanya jengo hii kuwa Kituo Jumuishi cha kutoa huduma za Mahakama. Wadau muhimu wa Mahakama walipatiwa ofisi za kuendeshea shughuli zao ikiwa ni njia mojawapo ya kumsogezea mwananchi huduma na kuondoa usumbufu kwa wananchi. Wadau walipotiwa ofisi ni pamoja na Mawakili wa Kujitegemea, Mawakili wa Serikali, Polisi na Huduma kwa Jamii.

Pamoja na mambo mengine viongozi hawa wameafikiana kuanzisha Huduma za Kibenki wiki ijayo kwa kumtumia Wakala wa Benki.

DC MPYA BAGAMOYO AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE

0
0
VICTOR MASANGU,  CHALINZE.

MKUU mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa amewataka vijana ambao wanahitimu  mafunzo ya jeshi la akiba  kuhakikisha wanakuwa wazalendo na nchi yao na kuachana kabisa na vitendo vya kujiingiza katika matukio ya kihalifu na badala yake wahakikishe wanazingatia sheria na taratibu zote zilizowekwa  kwa lengo la kuweza kulinda hali ya ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao.

Kauli hiyo aliitoa wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa mafunzo  ya awali ya  jeshi la akiba ambayo yamefanyika katika kata ya Bwilingu  na kuwajumusiha vipana wapatao 183 kutoka  katika halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.

Mkuu huyo pia aliwahimiza vijana hao kuhakikisha wanakuwa na nidhamu ya hali ya juu katika kipindi chote cha mafunzo hayo ya kijeshi na kuzingatia maelekezo ambayo wanapatiwa na walimu wao kwa lengo la kuweza kujifunza   mbinu mbali mbali ambazo zitaweza kuwa ni mkombozi mkubwa katika kulilinda Taifa la Tanzania na kuweza kukabiliana na wimbi la matukio ya uhalifu.

“Napenda kuchukua fursa hii  kuwapongeza vijana ambao mmeweza kujitokeza katika mafunzo haya ya jeshi la akiba,lakini kitu kikukbwa ninawaomba muwe wazalendo na nchi yenu kwa kuhakikisha mnazingatia sheria na taratibu za nchi ikiwa ni sambamba na kuyatumia vizuri mafunzo mliyopatiwa kwa maslahi ya nchi na sio vinginevyo,”alisema
Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Rashid Kawawa kulia akiwa na  Mshauri wa jeshi la akiba wilayani humo wa kushoto Maj Chinguku wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa mafunzo wa jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183  ambayo yamefanyika katika  kata ya Bwilingu halmashauri ya Chalinze.
  Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa wa kati kati akirukaruka mara baada ya kufungua mafunzo rasmi ya jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183 hawapo pichani  kutoka kata ya  Bwilingu katika halmashauri ya Chalinze pembeni yake kulia ni Mshauri wa jeshi la akiba Wilayani Bagamoyo Maj Chinguku.
Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa wa kati kati akirukaruka mara baada ya kufungua mafunzo rasmi ya jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183 hawapo pichani  kutoka kata ya  Bwilingu katika halmashauri ya Chalinze pembeni yake kulia ni Mshauri wa jeshi la akiba Wilayani Bagamoyo Maj Chinguku.

RC TABORA AWAONYA WAVAMIZI WA ARDHI MAENEO YA SERIKALI

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja baina ya wananchi na watendaji wa Serikali mkoa wa Tabora jana.
Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Erick Kitwala akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja baina ya wananchi na watendaji wa Serikali mkoa wa Tabora jana.
Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Kizigo Kata ya Ng’ambo mkoani Tabora, Bw. Said Thabit Mnwagi akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja baina ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia),wananchi na watendaji wa Serikali mkoa wa Tabora jana.Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Komanya Erick Kitwala na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Joseph Kashushura.
Baadhi ya washiriki wa mkutano wa pamoja baina ya wananchi na watendaji wa Serikali mkoa wa Tabora wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri wakati wa mkutano huo uliofanyika katika ukubi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo jana.(Picha na Frank Shija – MAELEZO, Tabora)

Maafisa Habari Wasisitizwa Mawasiliano Kupitia Mitandao ya Kijamii

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri akizungumza katika kikao baina yake na viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Seriikalini (TAGCO) na Idara ya Habari –MAELEZO wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kutoka kulia ni Mjumbe wa Kamati Tendaji wa TAGCO, Inocent Byarugaba, Afisa Tehama wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema, Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika na Mweka Hazina Msaidizi wa TAGCO, Gerald Chami. Kutoka kulia ni Mjumbe wa TAGCO, Innocent Byarugaba,Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa, Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika, Mweka Hazina Msaidizi wa TAGCO, Gerald Chami na Kaimu Mkuuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Mkoa wa Tabora, Frank Lema. Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO,Bi. Zamaradi Kawawa akielezea jambo walipokutana na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema katika ziara ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kutoka kulia ni Mjumbe wa Kamati Tendaji wa TAGCO, Inocent Byarugaba, Kaimu Mkuuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Mkoa wa Tabora, Frank Lema, Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika na Mweka Hazina Msaidizi wa TAGCO, Gerald Chami. Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO), Bi. Sarah Kibonde Msika akifafanua jambo katika kikao baina ya viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari – MAELEZO na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kutoka kulia ni Mjumbe Afisa Tehama wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa(katikati). Mweka Hazina Msaidizi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO), Gerald Chami akielezea jambo katika kikao baina ya viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO), Idara ya Habari – MAELEZO na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema(wapili kulia) wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kutoka kulia ni Mjumbe wa TAGCO, Innocent Byarugaba,Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa, na Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika . Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Ignas Mjwahuzi(kulia)akielezea jambo mara baada ya kikao baina yake na viongozi wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) na Idara ya Habari – MAELEZO wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya TAGCO, Innocent Byarugaba,Mweka Hazina Msaidizi wa TAGCO, Gerald Chami, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema na Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika . Mjumbe wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO), Innocent Byarugaba akisisitiza jambo katika kikao baina ya viongozi wa Chama hicho, Idara ya Habari – MAELEZO na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Frank Lema (katikati) wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri za Kanda ya Kati leo Mkoani Tabora. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari –MAELEZO, Bi. Zamaradi Kawawa, na Makamu Mwenyekiti wa TAGCO, Bi. Sarah Kibonde Msika . Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO) na Idara ya Habari – MAELEZO, wakati wa ziara ya kutembelea Maafisa Habari na Mawasiliano katika mikoa ya Kanda ya Kati jana mkoaniTabora. (Picha zote na: Frank Shija- MAELEZO, Tabora)

FM ACADEMIA KUWAVURUGA KWA BURUDANI WAKAZI WA WAMOSHI

0
0
Na woinde shizza, Kilimanjaro

Bendi ya FM Academia ya jiji Dar es Salam imeahidi kuangusha burudani ya nguvu septemba mosi Katika ukumbi wa filomena klabu, uliopo wilayani Hai mkoani kilimanjaro.

Akizungumza na waandishi wa habari kiongozi wa bendi hiyo Pacho Mwamba alisema kuwa bendi hiyo ikiwa chini yake itaangusha burudani ya nguvu katika usiku wa  kuazimisha miaka minne  ya tangu kuanzishwa kwa Bendi ya Filomena Pamoja na ukumbi wa sherehe na klabu ya Filomena tangu ianzishwe. 

Alisema kuwa wamejipanga vizuri kwa ajili ya kuwapa burudani wakazi wa moshi Pamoja na vitongoji vyao huku wakibainisha kuwa siku hiyo watatumia pia kuwatambulisha wimbo wao wa Rivasi nakuwaonyesha wakazi wa kilimanjaro na vitongoji vyake jinsi unavyochezwa. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa filomena band na klabu Swaumu Kileo kuwaambia waandishi wa habari kuwa onyesho hilo liyafanyika september 1 na pia mbali na FM academia kuaindikiza siku hiyo pia kutakuwa na burudani zingine Za aina mbalmbali zitakazo tangulia kabla ya bendi ya nyumbani Pamoja na Fm Academia kupanda jukwaani majira ya sa a mbili usiku. 

Alisema kuwa kama ilivyo kawaida ya filomena kuwapa burudani watu wa mkoani kilimanjaro hivyo hivyo wataendelea kuwapa burudani wananchi wote ikiwa ni desturi yao

Saumu alitaja viingilio vya siku hiyo kuwa kwa viti maalumu(V.I.P)nishilingi efu 10000 na kawaida huku kawaida ikiwa ni shilingi 7000 tu, alimalizia kwakuwakaribisha wananchi wote kuweza kuhuziria katika sikukuu hii ya kuazimisha miaka mince ya tangu kuanzoshwa kwa Filomena bendi Pamoja na klabu. 
Baadhi ya Wacheza shoo wa bendi hiyo

ALAT TABORA YAIPONGEZA UYUI KWA MATUMIZI MAZURI KWENYE UJENZI WA VYUMBA VYA SHULE YA LOLANGULU

0
0

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Lolangulu Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora Mary Zacharia akisoma taarifa jana ya ujenzi wa mradi wa vyumba vitatu vya madarasa na uwekaji wa samani kwa gharama ya milioni 38 kwa wajumbe
Jengo lenye vyumba vitatu vya madarasa na samani zake lilipo katika Shule ya Msingi Lolalungu wilayani Uyui Mkoani Tabora ambalo limegharimu milioni 38 hadi kukamilika.
Wajumbe wa Jumuiya ya Serikali za mitaa Tanzania ( ALAT) Mkoani Tabora wakikagua na kupata taarifa jana ya mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa matatu katika Halmashauri ya Wilaya ya Tabora -Uyui kwenye Shule ya Msingi Lolangulu vilivyogharimu milioni 38.



NA TIGANYA VINCENT-TABORA

Jumuiya ya Serikali za mitaa Tanzania ( ALAT) Mkoani Tabora imeipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Tabora -Uyui kufanikisha ukamishaji wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika Shule ya Msingi Lolangulu kwa kiasi cha shilingi milioni 38.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Tabora Adam Malunkwi wakati wajumbe wa Jumuiya hiyo wakiwa katika kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.

Alisema juhudi za Kamati ya Shule hiyo kwa kushirikiana na wananchi zimewapa fundisho kuwa miradi mingi inaweza kutekelezwa kwa fedha kidogo na kwa ubora wa hali ya juu.

Mbunge wa Jimbo la Manonga Seif Gulamali alisema Vyumba vipya vya madarasa katika Shule hiyo vinapaswa kutumika kama funzo kwa watu wanaosimamia miradi ya ujenzi katika Mkoa wa Tabora.

Alisema hali hiyo imeonyesha kuwa wakipewa na Serikali shilingi milioni 64 wanaweza kujenga vyumba zaidi ya vinne vikiwa vimekamilika na samani zake kama walivyoona katika Shule ya Lolangulu.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Kiwele Bundala alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wake kuhakikisha anatuma wataalamu wake wa ujenzi ili waweze kujifunza mbinu walizotumia wakazi wa pale na Kamati yao kufanikisha mradi huo kwa kiwango cha juu.

Alisema hatua ya wao kuweza kujenga vyumba vitatu vikiwa na samani kwa fedha hizo kimeonyesha jinsi miradi mingi ya maendeleo ya wananchi inaweza kufanyika kwa kiwango kidogo cha fedha.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Urambo Margaret Nakainga alisema wataalamu wa ujenzi katika Halmashauri za Mkoa wa Tabora watakiwa waige mfano wa ujenzi wa vyumba vingi vya madarasa kama vya shule ya Lolangulu ambapo vimewekewa na makinga maji.

Alisema hatua itasaidia kupunguza tatizo la maji katika shule kwa ajili ya shule mbalimbali mkoani Tabora.

Awali akitoa taarifa ya mradi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Lolangulu Mary Zacharia alisema wakazi wa Kijiji cha Ilolangulu waliweza kufanya kazi hiyo baada ya kuunganisha nguvu zao na kuchangishana na kuweza kufikisha jumla ya milioni 11 ambazo ziliwawezesha kufikisha majengo yao katika lenta.

Alisema Serikali baada ya kuona juhudi zao iliwaunga mkono kwa kuwapatia milioni 24 ambazo zimewezesha kuwamalizia kazi zilizokuwa zimebaki na kuwafanikiwa kuwa na madarasa matatu.

Aidha Mary alisema Shule hiyo bado inakabiliwa upungufu mkubwa wa miundombinu ya matundu ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi ambapo mahitaji kwa wavulana ni matundu 23 yaliyopo ni manne na kwa upande wa wasichana ni matundu 31 yaliyopo ni nane. Alisema hali hiyo inasababisha adha kubwa kwa wananfunzi wa shule hiyo.

AfDB YARIDHISHWA NA MIRADI YA NISHATI MIUNDOMBINU MIBOVU NA CHAKAVU KUONDOLEWA DODOMA

0
0


Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika( AfDB) nchini Marekani,Steve Dowd(kulia), baada ya viongozi hao kufanya mazungumzo kuhusu miradi ya nishati inayofadhiliwa na AfDB katika ofisi ya Waziri wa Nishati jijini Dodoma.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ( wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika( AfDB) nchini Marekani, Steve Dowd (wa pili kulia), wakikagua kituo cha kusambaza umeme cha Zuzu jijini Dodoma, ikiwa ni moja ya miradi ya nishati inayofadhiliwa na AfDB kwa kushirikiana na Serikali.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ( katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Marekani,Steve Dowd (wa pili kulia), wakikagua kituo cha kusambaza umeme cha Zuzu jijini Dodoma.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Benki ya maendeleo ya Afrika ( AfDB), watendaji wa Wizara ya Nishati, pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) baada ya kufanya ziara katika kituo cha kusambaza umeme cha Zuzu jijini Dodoma.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ( wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika( AfDB) nchini Marekani,Steve Dowd (wa pili kulia), wakiwa katika picha ya pamoja katika moja ya Transfoma zilizopo katika kituo cha kusambaza umeme cha Zuzu jijini Dodoma.



AfDB yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya nishati ya umeme wanayoifadhili
Yaahidi kuendelea kutoa ufadhili utakaohusisha uondoaji wa miundombinu mibovu ya umeme jijini Dodoma

Na Zuena Msuya, Dodoma

Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), imeahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika kuimarisha miundombinu ya umeme nchini hususan katika Mkoa wa Dodoma ili kuboresha upatikanaji wa huduma ya umeme kutokana na kuongezeka kwa shughuli za uwekezaji.

Uboreshaji wa hali ya umeme mkoani Dodoma unahusisha uondoaji wa miundombinu mibovu na chakavu zikiwepo takribani transifoma 75, kujenga njia ya kusafirisha umeme yenye urefu wa kilometa 135 kuzunguka Jiji, pamoja na kujenga vituo viwili vya kupokea na kupoza umeme katika eneo la Msalato na Kikombo vitakavyokuwa na uwezo wa kufua umeme wa takribani Megawati 200.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani alisema hayo katika kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Zuzu jijini Dodoma,wakati wa ziara ya Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Marekani, Steve Dowd, aliyekuwa akikagua utekelezaji wa baadhi ya miradi ya nishati ya umeme inayofadhiliwa na Benki hiyo katika mikoa mbalimbali nchini. “Katika mazungumzo yangu na AfDB kabla ya kufanyika kwa ziara hii, pia wameonyesha nia ya kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa Jua wa megawati 100 katika eneo la Zuzu jijini Dodoma katika kipindi cha miaka miwili ili umeme huo uingizwe katika Gridi ya taifa,” alisema Dkt Kalemani.

Akizungumzia miradi ya nishati, Dkt. Kalemani aliutaja mradi mkubwa wa umeme na wa kwanza nchini wa megawati 400 (National Backbone), kuwa ni miongoni mwa miradi mikubwa iliyotekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali ikiwemo AfDB. Alifafanua kuwa, katika utekelezaji wa mradi huo, Serikali ya Tanzania ilitoa shilingi Bilioni 18, Benki ya Maendeleo Afrika ( AfDB) ilitoa Dola za Marekani milioni 64.5 kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Japan( JICA), Benki ya Uwekezaji Ulaya (EIB), Benki ya Dunia( WB) na Benki ya Korea.

Aliongeza kuwa mradi huo wa Backbone unahusisha ujenzi wa Kituo cha kupoza umeme cha Zuzu ambacho kitaongezwa uwezo wa kusambaza umeme kutoka Megawati 48 za sasa hadi kufikia Megawati 200. Alisema kuwa, baada ya kukamilika kwa miradi hiyo, mji wa Dodoma utakuwa mahitaji ya umeme wa megawati 70 kwa kipindi cha miaka 5 ijayo, na megawati 108 kwa miaka kumi ijayo, huku Mpango wa serikali kwa miaka kumi na mitano ijayo, ni kuwa na zaidi ya megawati 210, ili mkoa uweze kujitosheleza.

“Tunataka Mji wa Dodoma uwe ni mji wa mfano kwa kuwa na umeme mwingi na wa kutosha,na wa uhakika kwa kuwa viwanda vingi sasa vitaanzishwa katika Mkoa wa Dodoma, na uwekezaji mkubwa utafanyika kwa muda mfupi, kutokana na mkoa huo sasa kuwa na hadhi ya Jiji na Makao Makuu ya nchi, hivyo umeme ni lazima uwepo wa kutosha na wa uhakika, ” Alisisitiza Dkt. Kalemani.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) nchini Marekani, Steve Dowd alisema kuwa ameridhishwa na utekelezaji wa miundombinu ya umeme inayofadhiliwa na Benki hiyo hapa nchini baada ya kukagua na kuona namna ambavyo inavyotekelezwa. Down alisema kuwa, Benki hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kufadhili utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nishati ya umeme kwa kuwa, Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoendelea kiuchumi ambazo zinafanya vizuri katika utekelezaji wa nishati hiyo kulingana mahitaji na ubora unaotakiwa na kwa wakati.

“ Nimefurahi kutembelea baadhi ya miradi hii ya nishati inayofadhiliwa na AfDB ambayo inatumia fedha nyingi. Kwa kweli mnafanya vizuri, nimeridhishwa na kasi ya kuwaletea wananchi wenu maendeleo kupitia sekta ya nishati, AfDB itaendelea kuwaunga mkono katika hili, tuendelee kushirikiana”, alisisitiza Dowd.

Akizungumzia namna ambavyo AfDB inashirikiana na Tanzania, Dowd aliishauri serikali ya Tanzania, kuendelea kuomba fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo kutoka katika nyanja mbalimbali, kwa kuwa inatekeleza miradi hiyo kama ilivyotarajiwa.

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI AAGIZA WAFANYAKAZI WALIOJIGAWIA VIWANJA WANYANG'ANYWE

0
0

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii

NAIBU Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye, ameagiza wafanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ambao walijigawia viwanja katika viwanja vya fidia za wananchi wanyang'anywe na kufikishwa mahakamani ili sheria ifuate mkondo wake.

Ameyasema hayo wakati alipofanya kikao na wawakilishi wa mkuu wa mkoa pamoja na wawakilishi wa kampuni ya Tanzania Remic centre jijini Dar es Salaam leo Agosti 30,2018.ambapo alieleza wasiwasi wake kuwa kampuni iliyopewa kandarasi ya kuwatafutia viwanja wananchi hao haijatekeleza wajibu wake ipasavyo licha ya kuwa tayari imelipwa kiasi cha shilingi bilioni 3.7.

Nditiye pia ameagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, wakakague viwanja 537 vilivyotengwa maeneo ya Msongola, kwa ajili ya waliokuwa wakazi wa eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam Jumanne wiki ijayo ili kujiridhisha kama viwanja hivyo vipo na  vinafaa. 

“Nakuagiza Mkurugenzi wa TAA, kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Wilaya Jumanne ijayo muende mkakague eno hilo la viwanja 537 muone kama vipo kwa sababu kumekuwa na shida sana na hawa wenzetu wa Tanzania Remix Centre  nyinyi wenyewe mnajua, kuna shida ya miundombinu, sasa lazime mjue eneo hilo linafikika, na viwanja hivyo vinajengeka.” Amesema.

Amesema Wananchi wako tayari kushirikiana na serikali katika kuhakikisha upanuzi wa uwanja unakwenda vizuri. Kampuni ya Tanzania Remix Centre ilipendekezwa na Manispaa ya  Ilala na kupewa kandarasi ya kutafuta viwanja kwa ajili ya makazi mapya ya wananchi waliokuwa wakiishi eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo kulikuwepo na mivutano kati ya Mamlaka na Wananchi ambapo baadhi yao walipeleka shauri hilo mahakamani na hivyo kufanya zoezi hilo la kuwahamisha wananchi hao kwenye eneo hilo jipya kusuasua.

“Mradi huu ulihusisha upatikanaji wa viwanja 1,600 kwa mujibu wa mkataba wa awali ambapo fidia yake ilipaswa kufanywa kwa awamu mbili ya watu 800, hata hivyo kwa mujibu wa sheria kipinde kile ilitaka mwananchi apewe eneo lakini alipwe fidia pia.” Amefafanua.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kikao kati ya wawakilishi wa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na Kampuni ya Tanzania Remix Centre katika ukumbi wa VIP terminal II uliopo Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.
 Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye akiteta jambo na  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA),Richard Mayongela. 
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA),Richard Mayongela akizungmza wakati wa kikao na  Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye kulia leo jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa kampuni ya Tanzania Remix centre akizungumza wakati wa kikao kilichofanyika leo katika ukumbi wa VIP terminal II uliopo katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kulia ni  Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye.

KATIBU MKUU WA CCM DKT BASHIRU ALLY AFUNGUA KIKAO CHA BARAZA KUU LA UVCCM LEO.

0
0
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally Kakurwa akivalishwa mara baada ya kuwasili katika Ukumbi wa CCM White House Dodoma

Meza kuu ikiimba pamoja na Wajumbe wa Baraza kuu 

Wajumbe wa Baraza kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi wakiimba Nyimbo mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally Kakurwa 
 ambae pia ni Mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Kikao Cha Baraza kuu ala UVCCM Taifa 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala akizungumza Kuwakaribissha wajumbe wa kikao cha Baraza kuu Kilicho fanyika jjini Dodoma Leo


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Ndg.Kheri D James Akizungumza wakati wa Kumkaribisha Mgeni Rasmi Kufungua kikao Cha Baraza kuu la UVCCM Kilichofanyika JIJINI Dodoma Leo

Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally Kakurwa akifungua kikao  Cha Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM Kilichofanyika Jijini Dodoma Leo.



Wajumbe wa Baraza kuu wakifuatilia Mkutano 

Wabunge na wawakilishi wa nao tokana na Umoja wa Vijana



Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Bi Tabia Mwita akitoa neno la Shukran Kwa Mgeni rasmi Mara baada ya kikao cha Kufunguliwa na Katibu Mkuu wa CCM

 Mbunge wa Nzega Mhe Hussein Bashe akizungumza kwa Niaba ya Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi katika kikao cha Baraza kuu la Uvccm Taifa.

Naibu waziri wa Kazi Vijana na Ajira na Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini akizungumza kwa niaba ya Serikali katika kikao cha Baraza kuu la UVCCM leo jijini dodoma.(Picha zote na Fahadi Siraji UVCCM)

BENKI YA BIASHARA YA DCB YAZINDUA HUDUMA YA KIDIJITALI IJULIKANAYO KAMA DCB DIGITAL BANKING JIJINI DODOMA.

0
0


  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (wa tatu kushoto), akibonyezxa kitufe cha kompyuta kuashiria uzinduzi rasmi wa huduma za kibenki katika mfumo wa kidigitali za Benki ya Biashara ya DCB jijini Dodoma juzi. Wanaoangalia kutoka kushoto (mstari wa mbele ni; Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa, Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Prof. Lucian Msambichaka, Mbunge wa Viti Maalumu, Mama Janeth Masaburi, Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Peter Pinda na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Patrobas Katambi. Huduma hizo ni pamoja na DCB Akaunti Kidigitali, Kibubu Kidigitali, Nusu Mshahara Kidigitali na huduma ya kutoa pesa katika ATM bila kadi.
02 (1)
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji akizungumza katika uzinduzi huo.
03 (2)
Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akizungumza katika hafla hiyo mjini Dodoma juzi.
05 (1)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa akikaribisha wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi huo mjini Dodoma juzi.
06.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Peter Pinda (katikati), akishikana mikono na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashaitu huku Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Prof. Lucian Msambichaka akiangaalia mara baada ya uzinduzi huo.
07.
 Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Prof. Lucian Msambichaka (kulia), akikabidhi tuzo kwa Naibu Waziri wa Fedha, Dk. Ashatu Kijaji aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.
08.
 Mwenyekiti wa Bodi ya DCB, Prof. Lucian Msambichaka (kulia), akikabidhi tuzo kwa Naibu Waziri wa Fedha, Dk. Ashatu Kijaji aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.

Dodoma, Agosti 29, 2018, Benki ya Biashara ya DCB  imezindua huduma maalum ijulikanayo kama DCB DIGITAL BANKING ambayo ni huduma za kibenki zinazopatikana kwa njia ya simu.

Akiongea wakati wa uzinduzi huo Jijini Dodoma Naibu Waziri wa  Fedha na Mipango Dk Ashatu Kijaji alisema sote tumesikia DCB walikua wakwanza kuorodheshwa kwenye soko la hisa na leo DCB inakwenda kidijitali na ni ya kwanza kuzindua bidhaa zake nne muhimu hili ni jambo zuri sana kwa Benki ya DCB na Taifa letu hongereni sana.
Alisema ‘’Napenda pia niwashukuru sana uongozi wa benki hii kwa kutupatia nafasi sisi Wizara ya Fedha na Mipango kuja kua sehemu ya kihistoria katika sekta yetu ya fedha”.

Nikiwa kama kiongozi wa kusimamia maswala ya fedha nimefarijika sana kuwa pamoja nanyi lakini pia nimefarijika zaidi baada ya kuisikia historia ya DCB ikielezwa hapa mbele yetu na viongozi wa benki hio. Kwakweli ni tukio muhimu sana kwetu sekta ya fedha kwasababu kwa kauli mbiu hii ya SIMU YAKO,TAWI LETU inamaana Benki inawafikia watanzania kule walipo.

Kutokana na Ripoti ya Finscope ya mwaka 2017 ilionyesha idadi ya watanzania waliojiunga  na mfumo rasmi wa kifedha imeongezeka kwa asilimia 14 kutoka mwaka 2013 chachu ya ongezeko hili ni pamoja na urahisi wa upatikanaji wa huduma za kifedha kupitia simu zetu za mkononi na mashine za kutolea fedha. Lakini kutokana na uzinduzi huu wa leo naamini tutaongeza zaidi ya asilimia 70 kwasababu tutawafikia kule waliko.

Nawaelekeza DCB kuwatembelea wakulima wetu kwa sababu moja ya mpango wa serikali wa maendeleo wa miaka mitano  ulioanza kutekelezwa  tangu 2016 hadi 2021 umejikita zaidi katika kujenga uchumi wa viwanda, hivyo hakuna Viwanda bila taasisi za kifedha hususan benki zetu na hakuna uchumi wa Viwanda bila wakulima ambao  ndio wazalishaji wa malighafi za viwanda. Kupitia huduma kama hizi za kibenki nawahakikishia tutaifikisha Tanzania yetu ya uchumi wa kati wa viwanda kabla ya mwaka 2015. Ninachoomba elimu ya kifedha ambayo mmeitoa kwa wajasiriamali wa Dar es salaam nendeni mkaitoe kwa wakulima na wafugaji wa Tanzania kwani serikali inakwenda kuhakikisha Mkulima anapata soko la mazao yake.

Aliongeza Serikali yetu ya awamu ya tano ambayo ipo chini ya Muheshimiwa Rais John Pombe Magufuli inatambua wazi mchango wa sekta ya fedha hususan benki zetu  katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na kufikia malengo ya Taifa letu hivyo endeleeni kuwekeza lakini pia kubuni bidhaa na huduma zinazo lingana na mazingira ya watanzania na serikali kwa upande wetu tutaendela kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanaendelea kuwa bora.
Kuendelea kuboresha huduma za kibenki, mwezi huu wa nane mwaka 2018 Serikali imechukua hatua madhubuti za kiutawala na kisera  ambazo ningependa kuisema leo hapa kwa mara ya kwanza ni kushusha riba kutoka asilimia 16 hadi asilimia 8. Hivyo upatikanaji wa fedha utakua ni rahisi kwa mabenki yetu.Hii yote ni kuhakikisha watanzania wanapata mitaji kwa gharama nafuu, wito wangu kwa mabenki yote ikiwemo Benki yetu ya DCB kuakisi jitihada hizi za serikali yenu ya awamu ya tano.

Dk Kijaji  aliongeza “Nimefarijika sana kusikia kuwa DCB ni moja ya benki chache zilizojiunga na mfumo wa serikali ujulikanao kama  Government e Payment Gateaway (GePG ) ambao ni mfumo wa serikali unaotumika kufanya malipo mbalimbali hivyo  kupanua wigo wa malipo ya serikali”.

Mwenyekiti wa Bodi ya DCB Profesa Lucian Msambichaka aliongeza ‘’ Benki imeendelea kuimarika na Mwezi uliopita  Benki imetangaza kupata faida katika kipindi cha nusu ya kwaka kilichoishia mwezi Juni mwaka 2018, mafanikio haya yametokana na ubunifu wa bidhaa zinazokidhi mahitaji ya wateja wetu, uweledi  na huduma bora alisema.

Mkurugenzi Mkuu wa DCB Ndugu Godfrey Ndalahwa nae alisema DCB itaendelea kutoa huduma bora na za ubunifu ili kuweza kushindana kwenye soko. Bidhaa zetu ni nzuri sana na zenye ubunifu mkubwa. Kupitia DCB Digital mteja  sasa ataweza kufungua akaunti ya muda maalum (Digital FDR) , Akaunti ya malengo (Kibubu Digital Account) ,Digital Salary advance na vilevile  sasa anaweza kupata huduma za kutoa pesa kwenye ATM za umoja switch zilizoenea nchi nzima bila kutumia kadi ya benki (Cardless ATM).

MAKAMU WA RAIS AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI JIJINI DODOMA LEO TAREHE 31 AGOSTI 2018

0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri , kushoto ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa TAMISEMI, Mkapa House leo jijini Dodoma.
Kikao kikiendelea
Kikao kikiendelea
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kabla ya kuanza kwa kikao cha Baraza la Mwaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri katika ukumbi wa TAMISEMI jijini Dodoma.
(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images