Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2018, Charles Kabeho akizindua mradi wa vyumba vitatu vya madarasa Shule ya msingi Wishiteleja wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabaganga Taraba.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Charles Kabeho akiwa ndani ya chumba cha darasa cha Shule ya sekondari Maganzo ambao ni mradi wenye thamani ya sh. miloni 141 uliogharamiwa na fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Charles Kabeho akikagua moja ya vyumba vya madarasa Shule ya msingi Wishiteleja wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani humo
Mwenge wa Uhuru ukikimbizwa katika maeneo mbalimbali wilayani Kishapu ambako ulikagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani sh. bilioni 2.2.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Charles Kabeho akipata maelezo kuhusu uandaaji wa chakula cha kulisha ng’ombe alipofika katika mradi wa unenepeshaji wa mifugo hiyo eneo la Ukenyenge ambao unamilikiwa na mjasiliamali Eliud Urasa ukiwa na thamani ya sh. milioni 285.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabaganga Taraba (kulia) akimuongoza Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa, Charles Kabeho (kulia kwake) kwenda kukagua mradi wa utengenezaji wa madawati unaondelea katika ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo wenye thamani ya sh. milioni 289.3.
Mhandisi wa Maji Wilaya ya Kishapu, Lucas Said (kushoto) akitoa maelezo kwa Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Charles Kabeho kuhusu mradi wa maji kijiji cha Unyanyembe wakati Mwenge wa Uhuru ulipofika na kuweka jiwe la msingi ambapo una thamani ya sh. milioni 453.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Charles Kabeho akikagua mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Songwa wenye thamani ya sh. milioni 400. Wengine pichani kushoto ni diwani wa Kata ya Songwa, Mhe. Abdul Ngolomole na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kishapu. Dkt. Josephat Shani.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Charles Kabeho akizungumza na wananchi waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa nyumba za walimu shule ya sekondari Maganzo wenye thamani y ash. milioni 141. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabaganga Taraba.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Nyabaganga Taraba (kushoto) na mwenzake wa Wilaya ya Kishapu, Mhe. Hyasinta Mboneko wakikabidhiana Mwenge wa Uhuru katika eneo la Wame mara baada ya kumaliza mbio zake wilayani Kishapu.
………………….
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2018, Charles Kabeho ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwa kutekeleza miradi ya maendeleo yenye ubora na kwa gharama nafuu.
Pia ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutoa fedha kwa ajili ya uimarishaji wa vituo mbalimbali vya afya pamoja na sekta ya elimu.Kabeho ametoa pongezi hizo jana kwa nyakati tofauti wakati akikagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi mbalimbali ya mendeleo wilayani humo ambako Mwenge wa Uhuru ulikimbizwa.
Sanjari na hilo Kiongozi huyo alipongeza wilaya hiyo kwa kuishirikisha jamii katika kutekeleza miradi hiyo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya elimu na afya jambo ambalo linachangia uboreshaji wa sekta hizo.“Kishapu mna kitu cha pekee tofauti na huko kwengine nilikopita, hapa ninyi katika miradi yenu mlipopewa fedha ndani ya gharama mmebakiza chenji na mnaongeza miradi mingine kwa fedha hizo hizo hivyo mnafanya kitu cha kuigwa,” alisema.
Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge aliongeza kuwa kwa kuishirikisha jamii katika utekelezaji wa miradi hali inayoifanya nayo ifanye uwekezaji wa maendeleo katika senkta mbalimbali.Mwenge wa Uhuru wenye ujumbe “Elimu ni Ufunguo wa Maisha, Wekeza Sasa kwa maendeleo ya Taifa letu” ulikabibidhiwa mkoani Shinyanga wilayani Kishapu ukitokea wilayani Maswa mkoani Shinyanga umepitia miradi ya sh.bilioni 2.2.