Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

MWENYEKITI WA CHADEMA ALIYEHUKUMIWA MIEZI 9 JELA AACHIWA HURU BAADA YA KUSHINDA RUFAA

$
0
0

Na James Festo.Makete

Jeshi la polisi nchini limeaswa kutenda kazi kwa haki bila kushurutishwa na mtu yeyote kwani lisipofanya hivyo haki haitatendeka kwa kila raia kama katiba inavyosema kusababisha maafa mbalimbali yatakopelekea kuvinjika kwa amani

Rai hiyo imetolewa  na mwenyekiti wa CHADEMA wilaya ya Makete Shaaban Mkakanze wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Ivalalila wilayani hapa waliojitokeza kumpokea mwenyekiti wa CHADEMA kijijini hapa aliyekuwa gerezani mara baada ya kuachiwa huru.

"jeshi la polisi ni zuri sana pale litakaposimamia haki, lakini wanapokwenda kinyume kwa kweli wanageuka mwiba mchungu kwa wananchi" alisema Mkakanze. 

Mkakanze amesema hukumu iliyotolewa na mahakama ya mwanzo makete mjini Juni 28 mwaka huu dhidi ya mwenyekiti huyo imeonekana kuwa na mapungufu mengi ambayo amesema atayataja katika mkutano wa hadhara utakaofanyika muda wowote kuanzia sasa, hivyo ndiyo maana wameibuka kidedea katika rufaa waliyokata.

Amesema wao kama chama hawatakatishwa tamaa na mambo kama hayo na badala yake wataendelea kupigania haki za wananchi pale wanapoonewa na ikibidi hata kupoteza maisha wakati wakipigania haki zao

"Chadema sisi si watu wa vurugu, lakini sisi tunasimamia haki na maendeleo ya wananchi bila kujali  itikadi za vyama, hata yeyote tupo pamoja nae kama anatenda haki na kile anachotakiwa kuwafanyia wananchi lakini anapokwenda kinyume sisi hatutakubali na badala yake tutapambana mpaka kieleweke" alisema Mkakanze

Naye mwenyekiti wa CHADEMA kijiji cha Ivalalila ambaye alikuwa gerezani Bw Godfrey Mahenge amesema hana cha kusema zaidi ya kumshukuru Mungu na wananchi wa kijiji hicho ambao walikuwa naye pamoja tangu wakati wa kesi hadi gerezani na kusema kwa sasa ametoka na wembe ni ule ule wa kupigania haki za wananchi wake

Amesema kwa sasa hana mengi ya kuongea zaidi atakuja kuzungumza kwenye mkutano wa hadhara ambao utaandaliwa kwa ajili ya wananchi hao ambapo anatarajia kueleza yote yaliyomkuta ili wananchi wake wajue, huku akitoa rai kwa waandishi wa habari kuutangazia umma kuwa hivi sasa yuko huru na kesi zote ameshinda kama ilivyokuwa wakati akitiwa nguvuni.

"Nawaomba waandishi wa habari kama mlivyotangaza wakati nafungwa naomba mtangaze pia na jinsi nilivyoshinda rufaa na kuwa huru" alisema Mahenge

Mnamo Juni 28 mwaka huu mahakama ya mwanzo makete mjini ilimtia hatiani kwa kosa la kutukana polisi hivyo kuhukumiwa kifungo cha miezi 9 gerezani hali iliyomlazimu kukata rufaa na kushinda rufaa hiyo na alikaa jela zaidi ya miezi miwili

kumekucha miss TPSC mkoani Tabora

Tanzania yaingiza timu mbili robo fainali Airtel Rising Stars

$
0
0

=========  ========  =====
Tanzania yaingiza timu mbili robo fainali Airtel Rising Stars

Timu zote za wavulana na wasichana zimeingia robo fainali katika michuano ya kimataifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars yanayofanyika Lagos , nchini Nigeria na mshindi atapata medali , kombe pamoja na dola za marekani 10,000.

Timu ya wasichana imetinga robo fainali baada ya ya kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Malawi jana  na kumaliza na  pointi nne katika kundi ambapo timu ya Uganda ikishika uskani kwa point sita. Wakicheza kwa kujiami timu ya wasichana ya Tanzania ilipata goli katika dakika ya 17 kupitia kwa mshambuliaji hatari Shelda Boniface , kabla ya Malawi kuzawazisha dakika ya saba katika kipindi cha pili.

Mshambuliaji mwenye uwezo wa hari ya juu  Athanas Mdam alionyesha makeke yake  jana baada ya kufunga magoli matatu (hat-trick) katika mechi dhidi ya Sierra-Leon ambapo Tanzania ilishinda 4-2 na kukata tiketi ya kushiriki hatua inayofata ya michuano ya Mwaka ya kimataifa inayoandaliwa na Airtel. 

Mdamu ambaye amedhiliisha kwamba yeye ni liungo muhimu katika michuano hii , alifunga magoli katika dakika ya  6, 48, 56 , Omari Hamisi ndiye aliitimisha goli la nne la Tanzania  katika dakika ya 60. Sierra-Leone walipata magoli yao kupitia kwa Mohamed Mustapha katika dakika ya 8 na Alimamy katika dakika ya 14.

Timu ya wavulana ya Tanzania itacheza mechi ya robo fainali na Madagascar leo wakati wasichana watacheza na Democratic Republic of Congo. Timu ya wavulana itakosa huduma ya mpikaji mabao Athanas Mdamu ambaye yupo majeruhi.Mshambuliaji hatari Athanas Mdamu ametoa mchango mkubwa sana  katika timu mpka kufikia hatua ya mtoano . Amefunga goli kwa kila mechi , dhidi ya Ghana na Zambia. “ Tutamkosa ila tutapigana mpaka mwisho kuakikisha tuanshinda mechi zote.”Alisema naodha wa timu Thomas Chndeka .

Timu nyingine zilizofanikiwa kutinga katika hatua ya robo fainali kwa upande wa wavulana ni mabingwa watetezi Niger  ,wenyeji Nigeria , Chad, Malawi, Madagascar, Zambia, na Congo. Na kwa upande wa wasichana ni mabingwa watetezi Ghana , Nigeria , Chad, Kenya , Uganda , Malawi and DRC. Mashindano ya kimataifa ya Airtel Rising Stars ni mpango wenye lengo la kuchangia maendeleo ya  mpira wa miguu barani Afrika. Pia vijana wanapata fulsa ya kuonyesha uwezo na vipaji vyao katika medani ya soka.

Mh. Lowassa aongoza Kikao cha Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden leo

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya BUNGE, Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Mhe. Edward Lowassa akimsikiliza mmoja wa wajumbe wa kikao alichokiongoza wakati alipokutana na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania jijini Stockholm,Sweeden.Waliohudhuria kwenye kikao hicho ni Balozi Muhammed Mzale,Mhe. Juma Nkamia,Mhe. Suzanne Lyimo,Bw. Jacob Msekwa,Bw. Athuman Brambath,Bw. Yusuf Mndolwa,Bw. Arthur Mwambene na Bi Apronia Rutaihwa.Kikao hicho kimefanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Ubalozi huo.

RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU YA CHUO KIKUU CHA GUELPH JIMBONI ONTARIO, CANADA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Dkt. Shukuru Kawambwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe kuelekea ukumbini kutunukiwa Shahada Ijumaa Septemba 20, 2013.
Nyimbo za taifa zikipigwa wakati wa sherehe za kumtunuku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aki Shahada ya Uzamivu katika Chuo Kikuu Guelph jimboni Ontario, Canada, Ijumaa Septemba 20, 2013.
Sehemu ya umati ulioshuhudia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kutunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Chuo Kikuu cha Guelph jimboni Ontario Ijumaa Septemba 20, 2013.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akitunukiwa Shahada ya Uzamivu na Provost na Makamu wa Rais wa Chuo Kikuu cha Guelph jimboni Ontario, Dkt Maureen Mancuso , Ijumaa Septemba 20, 2013.
BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Banki ya Barclays Tanzania yazindua wa udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha nchini.

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Banki ya Barclays Tanzania Kihara Maina akitoa hotuba ya kumkaribisha  Mgeni Rasmi Waziri wa Wizara ya Fedha na Uchumi  Dkt. William Mgimwa katika hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika  usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions).Uzinduzi huo uliyofanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.

 Mgeni Rasmi Waziri wa Wizara ya Fedha na Uchumi Dkt. William Mgimwa akiongea na viongozi, wawezeshaji na wateja wa  Benki ya Barclays Tanzania  wakati wa  hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika  usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions)  iliyofanyika leo kwenye  hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.

 . Mjumbe wa bodi ya benki ya Barclays Tanzania Fatma Karume (kulia) akisisitiza na kufurahia jambo alipokuwa anaongea na Mgeni Rasmi (hayupo kwenye picha) wakati wa hafla ya uzinduzi wa udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions) iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam. Kushoto ni mjumbe wa bodi ya benki hiyo Suleiman Mohamed.

 Baadhi ya washiriki wa semina ya udhibiti wa vihatarishi katika usimamizi wa fedha (Risk Management Solutions) wa Benki ya Barclays wakihudhuria  hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye  hoteli ya Hyatt Kilimanjaro jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Eleuteri Mangi-Maelezo).

Hafla ya kumuaga aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda.

$
0
0
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Siaba Nkinga akimkabidhi zawadi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Seth Kamuhanda. 
 Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (aliyesimama katikati) akiifurahia zawadi aliyopewa na Katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo katika hafla iliyoandaliwa na Wizara hiyo. Kushoto ni Katibu Mkuu mpya wa Wizara hiyo Bi. Siaba Nkinga na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel. Hafla hiyo imefanyika leo jijini Dar es Salaam. 
 Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (kushoto) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel wakiangalia kwa furaha zawadi aliyokabidhiwa Bw. Kamuhanda kwenye hafla ya kuagwa kwake. 
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel akikabidhiwa zawadi.

 Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (wa tatu toka kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (wa nne toka kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Wizara na Wakurugenzi.  

PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO, DAR ES SALAAM.


 Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (katikati) akiwasili Uwanja wa Taifa kuhudhuria hafla ya kumuaga. Kushoto ni Naibu Katibu mpya wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel na kulia ni Katibu Mkuu wa mpya wa Wizara hiyo Bi. Siaba Nkinga. 
 Viongozi hao wakielekea ukumbi  mdogo kusubiri hafla kuanza .

 Katibu Mkuu wa mpya wa Wizara hiyo Bi. Siaba Nkinga (kushoto) akiwa pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (kulia).

 Viongozi hao wakiwa wakielekea kwenye ukumbi kwa ajili ya kushiriki hafla ya kumuaga aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda (katikati). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Siaba Nkinga na kushoto ni Naibu wake Profesa Elisante Ole Gabriel.

 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi wa hafla hiyo Bw. Seth Kamuhanda iliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
 Aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda akihutubia wakati wa hafla ya kuagwa kwake iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.



Nairobi mall shooting: 20 dead in Westgate shopping mall attack

$
0
0


An injured man is treated outside an upmarket shopping mall, seen background, in Nairobi, Kenya, 21 September 2013.
Emergency medical staff treated some of the wounded near the building's entrance
A soldier moves to take up a position outside an upscale shopping mall, seen background, in Nairobi, Kenya Saturday 21 September 2013.
Security forces have surrounded the shopping centre
Shoppers are helped to evacuate the area of an upmarket shopping mall, seen background, in Nairobi, Kenya Saturday 21 September 2013.
Dozens of shoppers were given assistance in evacuating the area
Two women hug outside an upscale shopping mall, seen background left , in Nairobi, Kenya Saturday 21 September 2013.
Children and families were taken to safety after the shootings began. More Story Click Here.


CHAMA CHA NGUMI MKOA WA DAR ES SALAAM 'DABA' WAPATA VIONGOZI WAO

$
0
0

Baadhi ya viongozi waliochaguluwa kuendesha chama cha mchezo wa masumbwi Mkoa wa Dar es salaam DABA wakiwa katika picha ya pamoja na mwenyekiti wa uchaguzi huo Zuwena Kipingu  katikati pamoja na mwangalizi mkuu wa uchaguzi Remmy Ngabo kulia
Mwenyekiti wa Mkutano wa Uchaguzi wa viongozi wa mchezo wa Masumbwi Mkoa wa Dar es salaam Zuwena Kibena katikati akizungumza baada ya kumalizika uchaguzi huo na kupatikana viongozi wake Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Baadhi ya wajumbe kutoka klabu ya Ashanti ya Ilala wakifatilia uchaguzi huo kutoka kushoto ni Emanuel Mgaya, Hamisi Manyota na Juma Mwalimu  wakifatilia uchaguzi mkuu wa chama cha mchezo wa ngumi mkoa wa Dar es salaam 'DABA' ULIOFANYIKA SIKU YA JUMAMOSI KATIKA UKUMBI WA ddc mLIMANI

BONIA KALAMA NYILAWILA AKIFATILIA UCHAGUZI HUO

Mweka hazina wa klabu ya Ashanti ya Ilala Emanuel Mgaya akitumbukiza kula yake
Mngombea wa nafasi ya makamu Mwenyekiti Timithi Kingu akijinadi wakati wa kuomba kula
Baadhi ya viongozi wakipiga kula za kuchagua viongozi watakaokiongoza chama cha mchezo wa ngumi Mkoa wa ar es salaam DABA
MMOJA YA MJUMBE ALIYEOMBA  NAFASI YA KATIBU MKUU WAMBOI MANGORE AKIJINADI KWA WAPIGA KULA
MMOJA YA WAJUMBE JAFARI NDAME AKIOMBA KULA ZA KUWA MJUMBE WA KAMATI YA  UHUSIANO HABARI NA MASOKO
Juma Uwesu akiomba kuchaguliwa kwa wapiga kula  ujumbe wa maendeleo ya vijana
Arnord Ngumbi akiomba nafasi ya ujumbe wa vilabu,wilaya na taasisi za umma
Mazimbo Ali akiomba kuwa mjumbe ili awaletee maendereo ya mchezo wa masumbwi kwa upande wa wanawake wanaojiunga na mchezo huo kuhakikisha wanashiriki kama wengine

TANZANIA YAZINDUA RASMI SIKU YA TEMBO KITAIFA LEO.

$
0
0

 Gari la Maliasili likiwa limebeba Meno ya Tembo, wakati wa kujiandaa na Maandamano kuelekea Mlimani city kwa ajili ya maadhimisho hayo
 Msanii wa Muziki wa Kitanzania Mrisho Mpoto akianza kuongoza maandamano kutoka Chuo kikuu cha Dar es salaam Kuelekea Ukumbi wa Mlimani City leo.

 Maandamano ya Siku ya Tembo yakiwa yanaendelea kuelekea ukumbi wa Mlimani City kwa ajili ya Kongamano hilo


 Wasanii wa Mrisho Mpoto wakiwa wamebeba chatu katika maadhimisho ya Siku ya Tembo Kitaifa leo
Mkurugenzi wa wanyamapori  Wizara ya maliasili na utalii Prof. Alexander Songorwa akisoma Hotuba kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na utalii.


 Wadau mbalimbali wa utalii na kupinga mauaji dhidi ya Tembo wakiwa wanafuatilia kwa umakini maadhimisho ya Siku ya Tembo kitaifa.
 Wanafunzi kutoka Shule ya Jitegemee wakiwa wanafuatilia kwa umakini Maadhimisho hayo
Mrisho Mpoto akiwa anatumbuiza katika Maadhimisho hayo ya siku ya Tembo
Mmoja ya waratibu wa Shuguli za Siku ya Tembo kitaifa Issa Isihaka kushoto akifuatilia kwa umakini siku ya Tembo kitaifa


 Picha ya Pamoja ya Viongozi Mbalimbali wa Serikali na wadau.


KINANA AMTEMBELEA MKUU WA MAJESHI MSTAAFU,GENERALI DAVID MSUGULI

$
0
0
1aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Jenerali David Msuguli Mkuu wa Majeshi Mstaafu wakati alipomtembelea na kumjulia hali Mjini Butiama leo, wakati akiondoka wilayani humo kuelekea Mugumu Wilaya ya Serengeti kuendelea na ziara yake ya kuimarisha chama na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho, Jenerali Musuguli alionekana kuwa na bashasha wakati alipomuona Abdulrahman Kinana pengine ni kutokana na utendaji kazi wa katibu mkuu huyo wa CCM, ambapo alisikika akisema huyu ni kijana wangu huku wakiwa wameshikana mikono wakiingia ndani kwa mazungumzo ya faragha.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-MUGUMU SERENGETI2aJenerali David Msuguli Mkuu wa Majeshi Mstaafu akisalimiana na Nimrod Mkono Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa Itikadi Siasa na Uenezi CCM.3aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali David Msuguli nyumbani kwake Butiama.4aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo huku Mkuu wa Wilaya ya Butiama Angelina Mabula akisikiliza kwa  makini.Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana na Jenerali David Msuguli wakiingia ndani huku wakiwa wameshikana mikono.7aJenerali David Msuguli akipiga picha ya kumbukumbu na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana, na maofisa kadhaa ambao ameongozana nao katika msafara huo, kushoto ni Mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini Nimrod Mkono. 

8aJenerali David Musuguli akipiga picha ya kumbukumbu na waandishi wa habari, kushoto ni Nimrod Mkono Mbunge wa Musoma vijijini.9aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na Jenerali David Musuguli wakati alipomtembelea nyumbani kwake leo.11aJenerali David Musuguli akiagana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi Siasa na Uenezi huku wakionekana kufurahia jambo. 15aAkisalimiana na na wana CCM walipokuwa wakimlaki leo16aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia kikundi cha ngoma wakati kikitumbuiza. 18Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nata wilayani Serengeti leo.19aWimbo wa taifa 20aWanafunzi wa Shule ya sekondari Nata wakiimba wimbo wa taifa.21aMwalimu Mwema Machage wa Darasa la Kompyuta katika shule ya sekondari ya Nata akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakati alipokagua shule hiyo22Mwalimu Peter Simon wa shule ya Sekondari ya Nata wilayani Serengeti akielezea Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana jinsi wanavyowafundisha wanafunzi wake somo la sayansi wakati alipotembelea maabara ya shule hiyo.katikati ni mwanafunzi wa kidato cha nne Silvesta Joseph23a mwanafunzi wa kidato cha nne Silvesta Joseph akitoa maelezo mbele ya Katibu Mkuu wa CCM kuhusu wanafunzi hao wanavyojifunza jinsi ya kutengeneza sabuni katika maabara hiyo ya shule.24aWananchi wakimpungia mkono Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana25Kinana akizungumza na wananchi katika kata ya Isenye29aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mgorole na Mzee Nyangarisi Kumari kuwa mmoja wa wazee wa heshima wa kimila wa kabila la Kiikoma tukio hilo limefanyika katika kata ya Bukore.30aKatibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana baada ya kutawazwa mzee wa heshima wa kabila la Kiikoma katika kijiji cha Bukore wilayani Serengeti

Rais Kikwete awasili New York kuhudhuria Kikao cha 68 cha Umoja wa Mataifa

$
0
0
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa kazi na Utumishi wa Umma wa Zanzibar, Mhe. Haroun A. Suleiman.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Naibu Mwakilishi wa Kudumu katika Ubalozi wa Tanzania, New York, Mhe. Balozi Ramadhan Mwinyi.
Mhe. Rais Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Iadara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KINANA ATINGA SERENGETI, ASISITIZA BARABARA SERENGETI-ARUSHA ITAJENGWA

$
0
0
Kinana  akishangiliwa baada ya kusimikwa kuwa mmoja wa wazee wa kimila wa kabila la wanata
Akina mama wa kabila la Nata wakimkabidhi zawadi ya mkekeka kwa ajili ya mke wake.
Katibu Mkuu wa  Umoja wa Wanawake T anzania (UWT/CCM) Amina Makilagi akigawa chakula kwa wageni na wenyeji wa Serengeti.
Kinana akiangalia ngoma ya asili.
Kianan akikagua  majengo ya shule ya awali ya Bokole wilayani Serengeti.
Nape akitangaza kuahirisha mkutano wa hadhara baada kunyesha mvua kubwa mjini Serengeti.Picha zote na kamanda wa matukio blog.
 Gari lililombeba Katibu Mkuu wa CCM KAbdulrahman Kinana likivuka kwenye maji eneo la Nyamswa Butiama, kwenda Wilaya ya Serengeti kuendelea na ziara ya kuimarisha uhai na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Nape akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Anjelina Mabula (kulia) na Katibu wa CCM wa wilaya hiyo.
Kinana akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Anjelina Mabula.


Kinana akiagana na Katibu wa CCM wilaya ya Butiama pamoja na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Nimrod Mkono.
Kijana wa Chipukizi wa CCM akifanya mabo wakati wa kumlaki Kinana katika Kijiji cha Isenye wilaya ya Sengeti, Mkoani Mara leo.
Kinana  akiangalia ngoma ya asili katika Kijiji cha Isenye baada ya kuwasili wilayani Serengeti
Kinana akivishwa skafu na wanafunzi wa Shule ya Sekondari na Nata wilayani Serengeti leo. Picha na kamanda wa matukio blog
Kinana akiwa kwa kutumia sabuni iliyotengenezwa na wanafunzi katika maabara ya shule ya Nata wilayani Serengeti.Kulia ni mwanafunzi Sylvester Joseph.
Wanafunzi wa shule hiyo wakiwa na baadhi ya waandishi wa habari walio kwenye msafara wa Kinana.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Nata Mbiso, Fortunatusi Sesela (kushoto) akimkabidhi Kinana usinga ikiwa ni ishara ya kumsimika kuwa mmoja wa wazee wa kimila wa kabila ya Nata wilayani Serengeti.

tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage mjini shinyanga.

$
0
0
 Anajiita Mzee wa Mahaba kutoka Manzabay,Cassim Mganga akiwaimbisha mashabiki wake kwa shangwe huku mayowe yakitawala kila kona ya uwanja wa Kambarage usiku huu ndani wakati tamasha la Serengeti fiesta likiendelea kurindima usiku huu.
 Mtoto wa Mama Said a.k.a Chege akiimba kwa hisia jukwaani.
Msanii wa Bongofleva Ney wa Mitego akiwaimbisha mashabiki wake.
 Msanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya,Rich Mavoko akiimba jukwaani usiku huu sambamba na madensa wake (hawapo pichani). 
Tamasha la Serengeti fiesta 2013 likiendelea usiku huu.

Mashabiki wake wanamuita Kinga Zilla kutoka Sala Sala,lakini pia jina la Godzilla limemuongeza umaarufu kwa mashabiki wake kutokana na umahiri wake wa kushusha mistari ya hip hop mikavu mikavu,kama aonekavyo jukwaani akiwaimbisha mashabiki wake ndani ya uwanja wa Kambarage usiku huu.
  Baadhi ya wakazi wa mji wa Shinyanga wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye uwanja wa Kambarage mkoani Shinyanga,ambapo tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea kufanyika.
Mwanadada Linah akiimba sambamba na shabiki wake jukwaani usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga usiku.
 Baadhi ya Wadau wakubwa na wadhamini wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2013,kutoka kampuni ya Serengeti Breweries,Octavian,Bahati pamoja na mdau wao,wakiwa katika picha ya pozi usiku huu ndani ya uwanja wa Kambarage,mkoani Shinyanga
 Mwanadada ambaye kwa sasa ameonekana akifanya vyema kwenye jukwaa la Serengeti fiesta 2013,Neylee akiwaimbisha mashaniki wake (hawapo pichani). 
 Anajiita Jita Man kutoka jijini Mwanza akitumbuiza jukwaani usiku huu.

Dj Zero kutoka Clouds FM akiburuza mangoma usiku huu.
 Mwanadada Shilole na madensa wake wakilishambulia jukwaa vilivyo usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Kambarage.mkoani Shinyanga. 
 Masbabiki kibao waliojitokeza kwenye tamasha la serengeti fiesta 2013,usiku wakifuatilia na kushangweka vilivyo mbele ya jukwaa la fiesta.
 mashabiki wakifuatilia
 Kutoka Wanaume TMK,wakiongozwa Mh Temba na Chege kwa pamoja wakilishambulia jukwaa la Serengeti fiesta usiku huu ndani ya uwanja wa kambarage mjini Shinyanga.
 Weusi wakitumbuiza jukwaani usiku huu.
 Shabiki akifurahi jamboo.
Kundi la Wanaume TMK-Halisi likiongozwa na Sir Juma Nature wakilishambulia jukwaa la Serengeti Fiesta ndani ya uwanja wa Kambaraje,mjini Shinyanga.



Article 18


KING ZILA A.K.A GODZILLA AKIKAMUA USIKU HUU UWANJA WA KAMBARAGE-SHINYANGA .

DAYNA NYANGE, IZZO B, PNC WANUSURIKA KUFA KWA AJALI MKOANI MWANZA.

$
0
0

 Gari iliyopata ajali.
  Wasanii wa  tasnia ya mziki wa bongo Fleva, Dayna Nyange, PNC, Izzo B na wasanii wengine, leo wamenusurika kufya kufwatia gari waliyokuwa wakisafilia kupata ajali maeneo ya Buhongwa Mwanza, kwa mujibu wa msanii Dayana Nyange amesema, walikuwa wakitojkea kwenye show Geita iliyoandaliwa na Radio Free Africa ndipo walipofika maeneo ya Buhongwa gari yao aina ya Coasta, kapata ajali na msanii Filbert Kabago, amejeruhiwa.

NBC MANAGING DIRECTOR MIZINGA MELU WINS BUSINESS WOMAN OF THE YEAR 2013 AWARD

$
0
0

The National Bank of Commerce (NBC) Managing Director Ms. Mizinga Melu was named Business Woman of the Year 2013 at the All Africa Business Leaders Awards (AABLA) which was held in Johannesburg, South Africa.

The All Africa Business Leaders Awards (AABLA) aims to identify and honour those leaders who are making a difference through innovation and inspiration in their industry sectors. It is organized and overseen by ABN Productions.

AABLA was successfully launched in South Africa in 2011 with the first awards ceremony which took place in October the same year. As one of the most prominent award ceremonies in Africa, the AABLA ceremony is televised across the African continent annually. The Business Leaders Awards was originally conceived by CNBC Worldwide.

There are four categories through which participants can be nominated namely Business Leader of the year 2013, Business Woman of the year 2013, Entrepreneur of the Year 2013 and Young Business Leader of the year 2013.

The winner of the Southern Africa Business Woman of the Year category exemplifies outstanding leadership in business. She showcases positive financial results, increased shareholder value, and provided sound management, proven corporate governance, and demonstrated innovation, best business practices and accountability, together with intangible qualities such as integrity and vision.

Ms. Melu was appointed to the role of Managing Director at NBC with effect from 20th May 2013. She is an exceptional banker having worked in 6 African countries and equipped with more than 20 years of experience in the Banking Industry. Mizinga is an expert in formulating, implementing and developing Business Strategies; one such example is the award winning USD500m Microfinance Bill Clinton pledge of banking the unbanked.

Among some of the recent recognitions awarded to Mizinga include, CEO of the year across all industries by the Zambia Institute Chartered Accountants in 2012 and Leaders and Achievers Outstanding CEO performance by PMR of South Africa in 2013. Mizinga is also one of the Frontier 100 CEO’s.

KINANA ASHUHUDIA MAABARA INAYOTEMBEA WILAYA YA SERENGETI

$
0
0
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza mwalimu wa masomo ya sayansi Ndugu Silvester Joseph , Katibu Mkuu alitembelea shule ya Natta Secondary na kushuhudia jinsi masomo ya sayansi yanavyopewa kipaumbele.
 Mwanafunzi wa Kidato cha Nne Peter Semion wa shule ya sekondari ya Natta iliyopo kata ya Natta wilaya ya Serengeti akimuelekeza namna ya kutengeneza sabuni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipotembelea shule hiyo ya Natta iliyopo wilaya ya Serengeti.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Wazee wa kata ya Isenya wilaya ya Serengeti waliokuja kumpokea.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na vijana wajasiriliamali wa kuendesha boda boda na ukulima wa mboga mboga mara baada ya kuzindua kikundi hicho ambapo aliwasihi lazima wapate elimu ya biashara wajue namna ya kuweka na kukopa na kulipa madeni kwa wakati.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka ndani ya ukumbi wa mkutano wa MUGUMU CCM ambapo alikutana na vijana wajasiriamali wa wilaya hiyo. 
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Natta mara baada ya kumaliza kikao na balozi wa shina namba 11 Tawi la Natta Majengo.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa shukrani kwa wazee wa Natta baada ya kumpa heshima ya kuwa Mzee wa Natta.

MKUU WA MKOA WA RUKWA INJINIA STELLA MANYANYA AFUNGUA KAMBI YA VIJANA WA CCM HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akishiriki kwa vitendo kufyatua matofali na vijana wa CCM walioweka kambi katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Mji mdogo wa laela tarehe 22 Septemba 2013. Lengo kuu la kambi hiyo ni kuwajenga vijana katika itikadi na sera za Chama cha Mapinduzi, Ukakamau na Uzalendo kwa chama na nchi yao kwa ujumla. Katika kambi hiyo wanajishughulisha pia na kazi za kijamii kama kufyatua matofali zaidi ya 6,000 yatakayosaidia katika kujenga kituo cha afya Laela. Katika kuwapa nguvu kuendeleza kambi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alitoa mchango wa laki mbili taslim. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa ambae pia ni Mbunge viti maalum CCM Mkoa wa Ruvuma akiwahamsisha vijana hao kukipenda chama chao kwa kuweka uzalendo mbele katika mkutano uliofanyika katika ofisi za Chama hicho katika mji mdogo wa Laela tarehe 22 Septemba 2013. Kutoka kushoto ni Matin Matete Mjumbe wa baraza kuu CCM taifa, C. Bakuli Katibu Mwenezi CCM Mkoa wa Rukwa, Injinia Manyanya RC Rukwa, Godwin Mzurikwao Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Rukwa, Ali Mgaya Katibu wa Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini na Persin Kalikule Mhamasishaji UVCCM Mkoa wa Rukwa. 
Sehemu ya vijana hao waliotoka katika maeneo tofauti ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga wakionekana kuhamasika vya kutosha katika kambi hiyo iliyopo katika mji mdgo wa Laela. 
Mwenyekiti wa umoja wa vijana wa CCM Mkoa wa Rukwa (UVCCM) Godwin Mzurikwao  akielezea mipango mbalimbali ya umoja huo ikiwemo uhamasishaji na upandaji miti ya mbao kwa ajili ya kuwainua vijana kiuchumi Mkoani Rukwa. Katikati akisikiliza kwa umakini ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkabidhi ndugu Ali Mgaya Katibu wa Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Vijijini miti na viriba vya kupandia miti ya mbao ambayo ni sehemu ya mpango wa UVCCM Mkoa wa Rukwa kuwawezesha na kuwahamasisha vijana katika zoezi la upandaji miti wa kibiashara.(Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa....rukwareview.blogspot.com)
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images