Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA NCHI WA MAMBO YA NJE WA JAPAN, IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Nchi  wa Mambo ya Nje wa Japan Masahisa Sato mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Waziri wa Nchi  wa Mambo ya Nje wa Japan Masahisa Sato zawadi ya Kinyago pamoja na Picha ya Mlima Kilimanjaro mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Nchi  wa Mambo ya Nje wa Japan Masahisa Sato mara baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

RAIS MAGUFULI AAPISHA WAKUU WA MIKOA, MAKATIBU WAKUU, MAKATIBU TAWALA WA MIKOA NA MANAIBU KATIBU WAKUU IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Brigedia Jenerali Nicodemus Elias Mwangela kuwa mkuu wa mkoa wa Songwe  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli   akimuapisha Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018 .
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha Ally Salum Hapi kuwa mkuu wa mkoa wa Iringa  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha  Andrew Wilson Massawe kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha Jilly Elibariki maleko kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara wenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha Kalolina Albert Mthapula kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimuapisha  Dkt. Jim james Yonazi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mawasiliano)  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018
 Viongozi wa dini wakiomba dua kwenye hafla ya kuapisha wateule mbalimbali iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea baada ya kuapisha viongozi wateule  kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
Picha na IKULU
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na Jaji Kiongozi Dkt. Fereshi wakiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Wakuu, Naibu makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Katibu wa Mikoa walioapishwa kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na Jaji Kiongozi Dkt. Fereshi wakiwa katika picha ya pamoja Wakuu wa Mikoa wa Zamani na   walioapishwa kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 1, 2018.


TAWLA yazungumzia vikwazo vinavyozuia ongezeko la ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika uongozi na shughuli za siasa

$
0
0

Josephine Arnold Wakili wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA akifungua semina ya matekelezo ya Mradi wenye lengo la kuchangia ongezeko la ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika ngazi mbalimbali za uongozi na shughuli za kisiasa kwa ujumla wake 

Moja ya Shughuli ndani ya mradi huo ni pamoja na kumiarisha uwezo wa vikundi / Majukwaa ya wanawake katika ngazi ya wilaya za mkoa wa Dar es salaam ili waweze kuongelea changamoto zinazowazuia kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kisiasa, Walioshiriki katika semina hiyo ni vikundi na majukwaa ya wanawake katika ngazi za kata na wilaya za mkoa wa dar es salaam. Semina hiyo imefanyika kwenye hoteli ya New Africa leo.
Isabella Nchimbi Mwanasheria wa Chama cha Wawanasheria Wanawake akitoa mada katika semina hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Josephine Arnold Wakili wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA na Bi. Sara Kinyaga wakifurahia jambo kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
Mwezeshaji wa Semina hiyo Sara Kinyaga akitoa mada katika semiha hiyo
Picha mbalimbali zikionyesha baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa leo.
 

     

NSSF KUSHIRIKI MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE MKOANI SIMIYU

$
0
0
Shirika la la Taifa la Hifadhi ya jamii NSSF linashiriki kwenye maonesho ya wakulima NANE NANE yaliyoanza tarehe moja mwezi wa nane katika viwanja vya Nyakabunda mkoani Simiyu. 

Kaimu meneja Uhusiano na Masoko wa NSSF Salim Khalfan amesema kuwa mwaka huu wameshiriki tena ambapo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye banda lao kwa ajili ya kujua masuala mbali mbali. 

“Tumejipanga vyema kwenye maonesho ya mwaka huu, tunaomba wananchi wajitokeze kwa wingi katika banda letu kujionea mambo mbali mbali tynayoyafanya ” Khalfan amesema kuwa katika banda la NSSF wananchi wataweza kupata elimu juu ya mafao yanayotolewa na Shirika kama vile mafao ya matibabu ambayo kwa kiasi kikubwa yamesaidia sana kuimarisha sekta ya afya hapa nchini. 

Pia amesema kuwa kutakuwepo na zoezi la uandikishaji kwa wananchi ambao wako kwenye sekta isiyo rasmi na wataweza kujiunga na NSSF kufaidika na mafao yanayotolewa. “Kutakuwepo na zoezi la kuandikisha wanachama wapya kwenye maonesho hayo ya nanenane hivyo ni wakati pekee kuja kujiandikisha “Alisema Khalfan. 

Tunapoazimisha sikukuu ya wakulima nchini ,NSSF inatoa fursa mbali mbali kwa wakulima zikiwemo mkulima kuweza kujiandikisha na kuchangia kwa kiasi cha shilingi elfu ishirini tu kila wmezi na kufaidika na mafao yanayotolewa baada ya kukidhi sifa stahili za kuwa mwananchama wa Hiari. 

Huu ni muendelezo wa Shirika la NSSF kushiriki katika maonesho ya wakulima ya nane nane ambayo kwa namna moja ama nyingine yanasaidia kutangaza fursa mbali mbali kwa wakulima nchini. 


Imetolewa na Kitengo cha Uhusiano na Masoko 
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii NSSF

Dkt. Shein akutana na kufanya mazungumzo na Meya wa Jimbo la Gorontalo na Kiongozi wa Kampuni ya gesi nchini Indonesia

$
0
0
Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar 
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amefanya mazungumzo na Makamo wa Rais wa Indonesia Muhammad Jusuf Kalla ambapo katika mazungumzo hayo viongozi hao walisisitiza haja ya kuzidisha ushirikiano katika sekta za maendeleo.

 Viongozi hao walifanya mazungumzo katika Ofisi ya Makamo wa Rais wa Indonesia Muhammad Jusuf Kalla iliyopo mjini Jakarta Indonesia, ambapo mkutano huo pia ulihudhuriwa na Mawaziri wa pande zote mbili. 

 Katika mazungumzo hayo Rais Dk. Shein alimpongeza Makamo wa Rais wa nchi hiyo kwa muwaliko wake huo muhimu ambao unaimarisha uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya Indonesia na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jumla na makhsusi kwa Zanzibar. 

 Dk. Shein alimueleza Makamo huyo wa Rais wa Indonesia kuwa Tanzania inajivunia kwa kiasi kikubwa uhusiano na ushirikiano wa kihistoria uliopo baina ya pande mbili hizo ambao umeasisiwa na viongozi wakuu wa nchi hizo tokea miaka ya sitini na kuahidi kuwa utaendelezwa. 


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Meya wa Jimbo la Gorontalo Prof.Nelson Pamalingo wakati wa mkutano na Meya huyo yaliyogusia zaidi katika ushikiano wa kilimo cha Minazi. Mazungumzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Borobudur Mjini Jakarta, Indonesia katika ziara ya kikazi kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohammed Jusuf Kalla. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) na Ujumbe wake katika mazungumzo na Meya wa Jimbo la Gorontalo Prof. Nelson Pamalingo (kulia) wakati wa mkutano na Meya huyo yaliyogusia zaidi katika ushikiano wa kilimo cha Minazi hafla ya mazungumzo hayo ilifanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Borobudur Mjini Jakarta,Indonesia katika ziara ya kikazi kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohammed Jusuf Kalla
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Meya wa Jimbo la Gorontalo Prof.Nelson Pamalingo(katikati) na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi katika Ujumbe wake Rais (kushoto) na Viongozi waliuongama na Mstahiki Meya wakiwa katika Picha ya pamoja mara baada ya mazungungumzo ya pamoja yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Borobudur Mjini Jakarta,Indonesia katika ziara ya kikazi kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mohammed Jusuf Kalla.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Kiongozi wa Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Pertamina ya Jakarta Nchini Indonesia Bw.Daniel S.Purba akiwa na ujumbe wa kampuni hiyo walipofika kwa mazungumzo katika ukumbi wa Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara na Wenyeviwanda ya Indonesia (KADIN) Mjini Jakarta Indonesia Rais akiwa katika ziara ya kikazi ya siku saba kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mhe.Mohammed Jusuf Kalla
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimsikiliza Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malaysia pia akiwakilisha Tanzania Nchini Indonesia Mhe.Dkt Ramadhani Kitwana Dau (wa pili kulia)wakati wa mazungumzo na Uongozi wa Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Pertamina ya Jakarta Nchini Indonesia,(hawapo pichani ) katika Ukumbi wa Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara na Wenyeviwanda ya Indonesia (KADIN) Mjini Jakarta Indonesia ,katika ziara ya kikazi ya siku saba kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mhe.Mohammed Jusuf Kalla
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akiwa na ujumbe wake katika mazungumzo na Uongozi wa Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Pertamina ya Jakarta Nchini Indonesia,unaoongozwa na Kiongozi Daniel S.Purba (wa pili kulia) mazungumzo hayo yalifanyika jana katika ukumbi wa Ofisi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara na Wenyeviwanda ya Indonesia (KADIN) Mjini Jakarta Indonesia ,katika ziara ya kikazi ya siku saba kwa mualiko wa Makamo wa Rais wa Nchi hiyo Mhe.Mohammed Jusuf Kalla. Picha na Ikulu. 

CHANGAMOTO YA SOKO YAPELEKEA WAKULIMA WA ZAO LA KOROSHO MKINGA KUUZA NCHINI KENYA

$
0
0
Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga, Joseph Sura akizungumza namna walivyojipanga kuimarisha ulinzi mipakani kupitia vyombo vya ulinzi na usalama huku wakisisitiza hakuna ulazima wa kuvusha korosho nje ya nchi kwani athari zake ni kubwa
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana kulia akisistiza jambo kwa Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga (DAS) Joseph Sura kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi na salama viwatilifu vinavyosambazwa na serikali kupitia na bodi ya korosho Tanzania lililoanza mikoa ya Mtwara na Lindi,Ruvuma na sasa Tanga watakwenda Pwani na mikoainayolima korosho
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana kushoto akisisitiza jambo na Nzaro Kijo ambaye ni Mratibu wa zao la Korosho Halmashauri ya wilaya ya Mkinga Abdallah Omari mwanakikundi akizungumza wamepata wafadhili kutoka Woldvision wamepata vifaa hivyo kwa ajili ya kubangulia korosho Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga Joseph Sura kushoto akiagana na Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana mara baada ya mazungumzo
Mkazi wa Kijiji cha Gezani Kata ya Mkinga Hafidhi Mamboleo akiwa anapulizia dawa mikorosho
Sehemu ya viwatilifu vilivypo kwenye ghala la Mkinga
Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana kulia akitoa elimu kwa wakulima wa zao la Korosho Kijiji cha Horohoro wilayani Mkinga kuhusu umuhimu wa matumizi sahihi nasalama viwatilifu vinavyosambazwa na serikali kupitia na bodi ya korosho Tanzania lililoanza mikoa ya Mtwara na Lindi,Ruvuma na sasa Tanga watakwenda Pwani na mikoa inayolima korosho,


KUTOKUWEPO kwa soko la uhakika wa zao la Korosho wilayani Mkinga mkoani Tanga kumepelekea baadhi ya wakulima kulazimika kuyasafirisha nchini Kenya kwa njia za panya kwa ajili ya kuuza ili waweze kupata fedha papo kwa papo badala ya kuuza kwa mfumo wa stakabadhi ghalani ambako wakati mwengine malipo yanachelewa kuwafikia.

Hayo yalibainishwa na Katibu wa Kikundi Kinachojushughulisha na Uzalishaji wa miche ya Korosho kilichopo Kijiji cha Horohoro kilichopo mpakani mwa Tanzania na Kenya (Kikohoki) Khalfan Mang’ana wakati wa zoezi la kutoa elimu kwa wakulima wa Korosho mkoa wa Tanga,juu ya matumizi sahihi na salama ya viwatilifu vya Mikorosho vinavyosambazwa na serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania.

Alisema hali hiyo inatokana na wakati mwengine soko la kutokuwa zuri na kutokana na kuwa mpakani wanalazimika kuzisafirisha korosho zao tani kwa tani kwenda nchini Kenya ili kuweza kupata bei nzuri na soko ambalo linawawezesha kunufaika na kilimo hicho.

“Korosho nyingi tani kwa tani zinasafirishwa kwenda nchini Kenya kwasababu tupo mpakani ukienda ghalani unaambiwa kilo ni sh.2000 lakini kule nchini Kenya wananunua kilo 150 hadi 170 na ndio maana Korosho nyingi zinakwenda huko na hilo linatokana na kutokuwa kwa uzibiti wa bei hauridhishi “Alisema.

Naye kwa upande wake mkulima wa kukindi hicho Moni Rashidi alisema sababu kubwa ni kwamba wanapopeleka zao hilo nchini Kenya kuuza wanapata fedha papo kwa papo kuliko mfumo wa kupeleka ghalani ambapo wakati mwengine unaambiwa fedha zimechelewa jambo ambalo linekuwa likiwarudisha nyuma kimaendeleo.

Alisema licha ya hivyo wakati mwengine wanalazimika kuambiwa wachukue mizigo yao lakini iwapo bei hiyo itaboreshwa hawatakuwa na mpango wa kuzisafirisha kwani hata wenzao wa nchi hiyo wataileta nchini ili waweze kupata manufaa kupitia zao hilo.

Awali akizungumzia suala hilo la korosho kuvushwa nje ya nchi, Katibu Tawala wa wilaya ya Mkinga, Joseph Sura alisema kwanza wamejipanga kuwaelimisha wananchi kwamba bei iliyopo kutokana na soko letu ni nzuri na hakuna haja ya kuivusha nje ya nchi pasipo na ulazima.

Sura alisema pia wataimarisha ulinzi mipakani kupitia vyombo vya ulinzi na usalama huku wakisisitiza hakuna ulazima wa kuvusha korosho nje ya nchi kwani athari zake ni kubwa ikiwemo kuikosesha halmashauri mapato lakini pia fedha inayokwenda serikali kuu moja kwa moja kupitia bodi ya korosho inakosekana.

Hata hivyo alisema serikali imeweza kuagiza pembejeo na viwatilifu ambavyo vitapatikana kwenye wilaya hiyo hivyo ni fursa ikiwemo kwa wilaya nyengine kwa mkoa wa Tanga ili kuweza kupata mazao bora na kasi ya serikali kuhimiza korosho zao la biashara zinaloweza kuwakwamua kiuchumi.

Naye kwa upande wak,Afisa Uhusiano wa Bodi ya Korosho Tanzania,Bryson Mshana alisema zoezihilo linalofanyika kwa mkoa wa Tanga lina lengo la kutoa elimu ya matumizi sahihi na salama viwatilifu vinavyosambazwa na serikali kupitia na bodi ya korosho Tanzania lililoanza mikoa ya Mtwara na Lindi,Ruvuma na sasa Tanga watakwenda Pwani na mikoa inayolima korosho.

Alisema lengo ni wakulima kutambua viwatilifu vinavyosambazwa na serikali na vipo kwenye maeneo yao hivyo wanapaswa kufahamu namna gani wanaweza kuvipata kwa ajili ya kuvitumia.

MAMA WA SHIGONGO AZIKWA BUCHOSA SENGEREMA

$
0
0
MAZISHI ya mama wa Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo, marehemu Asteria Kapela, yamefanyika jana Agosti 1, 2018 katika kijiji cha Bupandwamhela Wilayani Sengerema yakihudhuriwa na maelfu ya wakazi wa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mwanza.   

 Katika usia wake, Shigongo amesema kuwa hakika ni pigo kwake na kwa familia kwa ujumla kwani ameondokewa na mtu muhimu katika maisha yake na Mwenyezi Mungu ampumzishe katika nyumba yake ya milele daima kwani atamkumbuka siku zote za maisha yake na ataendelea kutenda yale yote aliyojifunza kutoka kwake. Paroko wa Kanisa Katoliki Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja, akiongoza ibada fupi ya kumuombea marehemu.[/caption] Katika mazishi hayo viongozi mbalimbali wa vyama na serikali wamejitokeza kuungana na familia hiyo katika msiba huo, ambao ni pamoja na Waziri wa Kilimo na Mbunge wa Buchosa (CCM) Dkt. Charles Tizeba, mbunge wa zamani wa Nyamagana na aliyekuwa waziri wa zamani wa mambo ya ndani, Lawrence Marsha. Pia miongoni mwao ni Mbunge wa Mtama (CCM) Nape Nauye, na mchekeshaji Masanja 'Mkandamizaji'. Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo (wa kwanza kulia) akiwaongoza ndugu zake kuweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu. Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto), Mhasibu Mkuu wa Global Group, Laurence Kabende , akifuatiwa na Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally, wakiwaongoza wafanyakazi wa Global Group kuweka shada la maua kwenye kaburi. Watoto wa kike wa marehemu wakiweka shada la maua kwenye kaburi. Dada wa marehemu wakiweka shada la maua. Hawa ni ndugu wa familia. Wajukuu wa kike wa marehemu Dkt. Charles Tezeba akiweka shada la maua. Baadhi ya wajukuu wa kiume wa marehemu.[/caption] [caption id="attachment_231650" align="alignnone" width="1024"] Laurence Masha. Paroko wa Kanisa Katolikia Mwangika Parokia ya Mt. Yakobo Mkuu, Padri Hilary Faraja.

MAOFISA WA JESHI LA MAGEREZA WAASWA KUZINGATIA MAADILI YA KAZI

$
0
0
Na Lucas Mboje, Magereza;

KAMISHNA Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike amewataka Maofisa na askari wa Jeshi hilo kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume na maadili ya kazi yao, badala yake wazingatie kanuni, miiko na maadili ya uendeshaji wa Jeshi la Magereza.

Kamishna Jenerali Kasike ametoa rai hiyo jana Agosti 1, 2018 wakati akiongea na Maofisa na askari wa Jeshi la Magereza Mkoani Arusha alipofanya ziara ya kikazi Mkoani humo.Alisema kuna upungufu katika uzingatiaji wa maadili kwa baadhi ya Maofisa na askari hususani mahusiano mabaya ya askari na wafungwa ikiwemo tabia za askari kuingiza simu magerezani.

Amesema hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa kwa maofisa na askari watakaobainika kufanya vitendo hivyo ikiwemo kuwajibishwa na kufukuzwa kazi."Mnajua kabsaa gharama za kujihusisha na tabia hizi za mahusiano mabaya na wafungwa nawaasa mzingatie maadili mnapotekeleza majukumu yenu ya kazi". Alisisitiza Kamishna Jenerali Kasike. 

Kuhusu agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa Kamishna Jenerali Kasike amesena kwa sasa Jeshi hilo linakamilisha mpango kazi wake utakaowezesha utekelezaji wa agizo hilo.Amewataka askari wote nchini kujiandaa kisaikolojia kutekeleza agizo hilo bila kisingizio chochote kwani Jeshi la Magereza linazo rasilimali za kutosha kutekeleza agizo hilo.

"Tunayo ardhi yakutosha, nguvu kazi ya wafungwa ipo hivyo agizo la Rais na Amiri Jeshi Mkuu lazima litekelezwe bila kisingizio chochote". Alisema Jenerali Kasike.Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani Arusha ambapo lengo la ziara hiyo ni kukagua utendaji kazi pamoja na kuzungumza na Maofisa na askari wa Jeshi hilo.

TAWLA yazungumzia vikwazo vinavyozuia ongezeko la ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika uongozi na shughuli za siasa

$
0
0

Josephine Arnold Wakili wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA akifungua semina ya matekelezo ya Mradi wenye lengo la kuchangia ongezeko la ushiriki na uwakilishi wa wanawake katika ngazi mbalimbali za uongozi na shughuli za kisiasa kwa ujumla wake 

Moja ya Shughuli ndani ya mradi huo ni pamoja na kumiarisha uwezo wa vikundi / Majukwaa ya wanawake katika ngazi ya wilaya za mkoa wa Dar es salaam ili waweze kuongelea changamoto zinazowazuia kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za kisiasa, Walioshiriki katika semina hiyo ni vikundi na majukwaa ya wanawake katika ngazi za kata na wilaya za mkoa wa dar es salaam. Semina hiyo imefanyika kwenye hoteli ya New Africa leo.
Isabella Nchimbi Mwanasheria wa Chama cha Wawanasheria Wanawake akitoa mada katika semina hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Josephine Arnold Wakili wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA na Bi. Sara Kinyaga wakifurahia jambo kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
Mwezeshaji wa Semina hiyo Sara Kinyaga akitoa mada katika semiha hiyo
Picha mbalimbali zikionyesha baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika semina hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa leo.
 

     

FOMU YA KUOMBA HATI MPYA PALE YA ZAMANI INAPOPOTEA.

$
0
0

Na Bashir Yakub.

Ni fomu namba 3 katika kanuni za Sheria ya usajili wa ardhi .Inatokana na kifungu cha 38 cha Sheria ya Usajili wa Ardhi Sura ya 334. Fomu hii kazi yake ni kuombea hati mpya ya ardhi baada ya ile uliyokuwa nayo mwanzoni kupotea. Hati, sawa ilivyo kwa vitu vingine vyote inaweza kupotea, kuibiwa au kuharibiwa. Mazingira ya matukio haya yote yameandaliwa majibu na sheria za ardhi. Fomu hii namba 3 ni rasmi kwa waliopoteza hati na hivyo kutaka kupata hati mpya.

Fomu hii hutakiwa kujazwa na mhusika yaani yule ambaye jina lilikuwa linasomeka kwenye hati iliyopotea. Kama lilikuwa likisomeka jina la kampuni basi wale waliokuwa wamesaini ile hati iliyopotea awali ndio wasaini na kujaza fomu hii. Anaweza kuwa mkurugenzi wa kampuni ama katibu wa kampuni.

Msimamizi wa mirathi pia anaweza kujaza na kusaini fomu hii ikiwa jina lililo kwenye hati iliyopotea ni la mtu ambaye sasa ni marehemu. Isipokuwa sasa kwa msimamizi wa mirathi ni lazima awe na fomu za kuthibitisha kuteuliwa na kuthibitishwa na mahakama kuwa msimamizi wa mirathi. Ikiwa msimamizi wa mirathi ni zaidi ya mmoja basi wote watajaza fomu hii ya kuomba hati mpya na watasaini .

KUSOMA ZAIDI sheriayakub.blogspot.com

GAVANA WA BoT ATANGAZA BANK M SASA IKO CHINI YA USIMAMIZI WAO

$
0
0

*Ni baada ya mtaji wake kutetereka, yapewa siku 90 kujitathimini

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

BENKI Kuu ya Tanzania(BOT) imeamua kuchukua usimamizi wa Bank M kuanzia leo na uamuzi huo unachukuliwa baada ya kubainika benki hiyo ina upungufu mkubwa wa ukwasi.

Akizungumza leo Dar es Salaam Gavana BoT Profesa  Florens Luoga amesema kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha Sheria namba 56 (1)(g)(III)cha sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2006 ameamua kuchukua uamuzi huo kwa Benk M na sasa itakuwa chini ya usimamizi wa BoT.

"Upungufu huu wa ukwasi unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na pia kuendelea kutoa huduma za kibenki kwa Bank M kutahatarisha usalama wa amana za wateja wake,"amesema Profesa Luwoga.

Amefafanua kutokana na uamuzi huo ,Benki Kuu imeisimamisha Bodi ya Wakurugenzi na uongozi wa Bank M kuanzia leo(Agosti 2) mwaka huu na kutokana na uamuzi huo BoT imemteua Meneja Msimamizi atakayesimamia shughuli za benki hiyo kwa kipindi ambacho itakuwa chini ya usimamizi.

Ameongeza Watanzania wafahamu kuwa katika kipindi kisichozidi siku 90 kuanzia leo , shughuli zote za utoaji wa huduma za kibenki za Bank M zitasimamiwa ili kuipa nafasi BoT kutathmini hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa suala hilo.

P ia kuwa BoT itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu katika sekta ya fedha.

Jumia yasisitiza kuuza bidhaa bora na halisi mtandaoni

$
0
0
 Katika kuwajengea Watanzania mazingira salama na rahisi ya kufanya manunuzi kwa njia ya mtandao, Jumia imesisitiza kuwa bidhaa zote zinazopatikana kwenye mtandao wake ni halisi na zenye bora wa hali ya juu kutoka kwa kampuni na wafanyabiashara wanaoaminika Tanzania na duniani kote.

Kwa watanzania wengi dhana ya kufanya manunuzi kwa njia ya mtandao bado ni ngeni na haijazoeleka. Miongoni mwa sababu zinazopelekea hali hiyo ni; uaminifu kwa sababu hakuna mawasiliano ya moja kwa moja baina ya muuzaji na mnunuzi, hofu ya wizi wa mitandaoni kutokana na upya wa huduma hii pamoja na changamoto ya maendeleo ya kiteknolojia ambayo watu wengi bado hawajafikiwa nayo.

Watanzania wengi wamezoea kwenda maduka moja kwa moja pale wanapohitaji kununua bidhaa kwa sababu hupata wasaa wa kuziona, kuzishika, kuzijaribisha, kufanya makubaliano ya bei ili kujiridhisha zaidi kabla ya kukata shauri la kununua.

Akizungumzia juu ya faida ambazo zimeletwa na mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao kwa wafanyabiashara na wateja wa Kitanzania, Mkuu wa Masoko wa Jumia Tanzania, kampuni inayoongoza kwa huduma za manunuzi mtandaoni Afrika, Bw. Albany James amebainisha kuwa mfumo huu upo kwa ajili ya kuwarahisishia wateja huduma za kufanya manunuzi pamoja na kuongeza thamani kwa wafanyabiashara.

“Kuna baadhi ya wafanyabiashara wanahofia pengine mfumo huu umekuja kuua biashara zao, la hasha! Maendeleo yoyote ya teknolojia duniani huja kwa lengo la kurahisisha maisha ya kila siku ya binadamu. Mfumo wa manunuzi ya mtandaoni una faida kubwa ya kuwa ni rahisi, kuokoa muda na gharama kwa mteja kwenda na kurudi dukani. Badala yake, mteja mahali popote na muda wowote alipo anaweza kuperuzi bidhaa, kununua na kisha kuletewa mpaka alipo,” alielezea Bw. James.

Kwa nchi kama Tananzania na nyinginezo zinazoendelea Afrika ambapo ufahamu na mwamko wa matumizi ya huduma za kiteknolojia bado ni mdogo, kunakuwa na ugumu katika kuyapokea mabadiliko kama ya manunuzi ya mtandaoni kwa haraka.

Ukiachana na maendeleo ya teknolojia, Watanzania wengi bado hawana ufahamu wa kutosha juu ya mifumo salama ya kufanya manunuzi mtandaoni hivyo kupelekea kuwa wagumu kuwaamini wafanyabiashara wanayojihusisha nayo.

“Jumia ni tofauti na mitandao mingine inayodai inafanya huduma za manunuzi ya mtandaoni. Utofauti ni mkubwa kwa sababu sisi tunatoa huduma zetu kwa kushirikiana moja kwa moja na makampuni na wafanyabiashara wakubwa na wanaoaminiwa nchini na duniani kwa ujumla. 
 
Hivyo hofu ya wateja kununua bidhaa feki, sio halisi na zilizo chini ya kiwango halipo kwa upande wetu. Kwa mfano; Tigo, Tecno, Samsung, Apple, Sony, Philips, Hp, Delly, Lenovo, LG, Hitachi, Tronic, Kenwood, Bruhm, Revlon, Epson, Hisense, Panasonic, kampuni hizi zote yaliyopo kwenye mtandao wetu yanasifika kwa ubora na uhalisi wa bidhaa zao duniani,” aliongezea Mkuu wa Masoko wa Jumia Tanzania.

Ikiwa inaadhimisha miaka sita ya kuleta mapinduzi ya huduma za manunuzi ya mtandaoni Afrika, Jumia imefanikiwa kuwashawishi wafanyabiashara na wateja wengi kuamini na kuhamia kwenye mfumo huu mpya.

“Tunafahamu sio kazi rahisi kuwaaminisha watanzania wote kuwa manunuzi ya mtandaoni ni salama na rahisi kama wanavyokwenda dukani. Katika kuhakikisha tunafanikiwa kuwashawishi na kuwazoesha taratibu, Jumia inafanya shughuli zake kulingana na matakwa ya wateja,” alisema na kumalizia Bw. James kuwa, “Kupitia mtandao wetu pekee mteja anaweza kuagiza huduma kwa gharama nafuu, akapelekewa mpaka mahali alipo, akaikagua bidhaa baada ya kujiridhisha ndipo hufanya malipo. Kama hiyo haitoshi, tunayo sera ya kurudisha bidhaa bure bila ya malipo yoyote endapo mteja ameletewa bidhaa ambayo hajaridhika nayo, kitu ambacho hutokea mara chache sana kutokana na umakini wa timu yetu.”

WATOROSHAJI TANZANITE KIAMA KINAKUJA- WAZIRI KAIRUKI

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Simanjiro

Waziri wa Madini Angellah Kairuki amesema Serikali itaaendelea kusimamia ulinzi na kudhibiti utoroshaji wa madini ya Tanzanite na watakaokwenda kinyume na matakwa ya Sheria, kiama chao kinakuja.
Waziri Kairuki aliyasema hayo tarehe 1 Agosti wakati wa ziara yake mkoani Manyara wakati alipotembelea migodi mbalimbali ya madini ya tanzanite ndani ya ukuta wa Mirerani.

Alisema ziara hiyo ililenga kuangalia suala zima la ulinzi katika ukuta unaozunguka migodi ya tanzanite, shughuli za uchimbaji madini mengine zinavyofanyika na kuangalia namna uzalishaji wa madini ya tanzanite unavyoendelea katika migodi husika. 

Kairuki aliongeza kuwa, ziara hiyo ililenga kuangalia namna Sheria ya Madini inavyotekelezwa, masuala ya Mikataba ya watumishi katika migodi na namna migodi husika inavyolipa kodi mbalimbali za Serikali yakiwemo masuala ya usalama sehemu za kazi na wafanyakazi kwa ujumla.

“Utoroshaji madini hausaidii, fedha ni za haraka lakini zinawaadhibu watanzania walio wengi kwa kuwa, fedha hizo hizo zingeweza kutumika katika miradi mingine ya maendeleo. Hivyo, kila mtanzania awe mlizi wa mwenzake,” alisema Kairuki.

Awali, akizungumza katika eneo Lemshuku kunakofanyika shughuli za uchimbaji wa madini ya Green Garnet, waziri Kairuki alisema kuwa, serikali inatambua mchango wa wachimbaji wadogo katika kuchangia pato la taifa kupitia shughuli za uchimbaji, hivyo akawaasa wachimbaji nchini kufuata Sheria, kanuni na taratibu ili kufanya shughuli halali ikiwemo kulipa kodi stahiki.
Waziri wa Madini Angellah Kairuki akiangalia moja ya seal inayotumika kufunga madini ya tanzanite baada ya kuzalishwa na kufanyiwa tathmini kwa lengo la kuhakikisha serikali inapata mapato yake stahiki.
Waziri wa Madini Angellaha Kairuki akipima ubora wa madini ya Tanzanite katika kifaa maalum baada ya kuzalishwa kutoka katika mgodi wa moja ya wachimbaji madini ya tanzanite.
Waziri wa Madini Angellah Kairuki akiangalia madini ya Green Garnet alipotembelea moja ya migodi inayochimba madini hayo katika eneo la Lemshuku Wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara wakati wa zira yake.
Waziri wa Madini Angellah Kairuki akieleza jambo wakati akipata ufafanuzi kutoka kwa mchimbaji (aliye ndani ya shimo) wakati alipotembelea moja ya migodi ya madini ya Green Garnet katika eneo la Lemshuku wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara.
Sehemu ya wachimbaji katika eneo la Lemshuku Wilayani Simanjiro kunakofanyika shughuli za uchimbaji madini ya Green Garnet wakimsikiliza Waziri wa Madini Angellah Kairuki hayupo pichani wakati wa ziara yake katika eneo hilo.


NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA AWAASA WATUMISHI WA TFS KANDA YA KUSINI

$
0
0
Watumishi wa Wakala wa Huduma Tanzania (TFS) wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia kanuni na sheria za utumishi wa Umma ili kuleta ufanisi wakati wanapotekeleza majukumu yao ya uhifadhi.

Rai hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga wakati alipowatembelea jana watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) kanda ya Kusini kwa ajili ya kuzungumza nao ikiwa ni muendelezo ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Mtwara kwa ajili ya kushughulikia changamoto za Maliasili, Malikale na Uendelezaji Utalii.

Amewataka kufanya kazi kwa uadilifu wa hali ya juu na yeyote atakayetuhumiwa kupokea rushwa hata kama hajapokea rushwa hiyo kutoka wafugaji kwa makubaliano ya kuingiza mifugo hifadhini kwa makubaliano ya malipo atashughulikiwa ipasavyo.Aliongeza kuwa endapo watumishi hao wataweza kutekeleza majukumu yao ipasavyo hakuna kiongozi yeyote watakayesumbuana nao.

‘’Tunataka mfanye kazi zenu za uhifadhi kwa weledi wa hali ya juu na mkifanya vizuri basi nakuwa nimefanya mimi na mkifanya vibaya mnakuwa mnaniangusha mimi hivyo sitokubali’’ alisisitiza Naibu Waziri Hasunga.
Aidha, Amewata wafanye kazi kwa kushirikiana na jamii kwa vile hakuna shughuli yeyote itakayofanikiwa endapo wananchi wataachwa nyuma.

‘’Tunataka jamii ione faida ya moja kwa moja kwa kupata elimu kuhusu uhifadhi pamoja na kushirikishwa kwenye masuala yote ya misitu ili waweze kutoa ushirikiano wakati ukataji miti unapofanyika popote pale’’
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) wa kanda ya Kusini, Ebramtino Mgiye mara baada ya kuwasili jana kwenye ofisi za TFS kanda ya Kusini kwa ajili ya kuzungumza nao ikiwa ni muendelezo ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Mtwara kwa ajili ya kushughulikia changamoto za Maliasili, Malikale na Uendelezaji Utalii.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzani (TFS) wakati alipowatembelea jana kwenye ofisi za TFS kanda ya Kusini ikiwa ni muendelezo ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Mtwara kwa ajili ya kushughulikia changamoto za Maliasili, Malikale na Uendelezaji Utalii.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga(katikakati) akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuzungumza na Watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwenye ofisi za TFS kanda ya Kusini ikiwa ni muendelezo ya ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Mtwara kwa ajili ya kushughulikia changamoto za Maliasili, Malikale na Uendelezaji Utalii.

ZAO LA MCHIKICHI KUMALIZA UHABA WA MAFUTA NCHINI

$
0
0
SEKTA ya kilimo ni mhimili wa uchumi wa Taifa na inategemewa katika kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo 2025, kupitia viwanda kwa sababu kilimo ndicho kitawezesha viwanda kwa kuvipatia malighafi.

Kutokana na umuhimu wa sekta hiyo katika kukuza uchumi wa nchini, serikali imekuwa ikifanya juhudi kubwa kuhakikisha inaiboresha ili iweze kuwa na tija na kufikia malengo iliyojiwekea.
Sekta hiyo mbali na kuwa mhimili wa uchumi wa Taifa, pia imekuwa ikichangia pato la mkulima mmoja mmoja, kaya na pia ni tegemeo la mapato ya fedha za ndani na za kigeni.Kufuatia hali hiyo, Serikali imeweka msisitizo katika kusimamia mazao makuu matato ya biashara ambayo ni pamba, chai, kahawa, korosho na tumbaku ambayo uzalishaji wake umeonyesha tija.

Baada ya kupata mafanikio katika mazao hayo Serikali kwa sasa inaboresha kilimo cha mazao ya alizeti, ufuta, michikichi ili kuzalisha mafuta ya kula ya kutosha kwa kutumia mazao hayo na mbegu za pamba.Itakumbukwa kwamba kila mwaka, Serikali inatumia sh. bilioni 600 kwa ajili ya kuagiza mafuta ghafi ya kula kutoka nje ili kukidhi mahitaji kwa kuwa kiwango kinachozalishwa nchini hakitoshi.


Katika kuhakikisha kuwa jambo hilo linafanikiwa Serikali ya awamu tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli imeamua kuanzisha kampeni ya kufufua zao la michikichi ili kuweza kuzalisha mafuta ya kutosha.

Akizindua kampeni hiyo mkoani Kigoma hivi karibuni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji wa mafuta ya kula nchini kwa kufanya mageuzi makubwa katika zao la michikichi.

Uamuzi huo sasa umelifanya zao hilo kuwa la sita la biashara ambalo katika miaka ya l960 hadi 1970, mkoa wa Kigoma ulijipatia umaarufu kwa uzalishaji wa zao hilo.

Waziri Mkuu anasema kampeni ya kufufua zao la michikichi mkoani Kigoma inaenda sambamba na kuanzishwa kwa kituo cha utafiti wa zao hilo katika chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Kihinga kilichopo wilayani Kigoma kwa kuwa ndiko zao la Michikichi linalimwa kwa wingi.

Anasema zao la mchikichiki ni muhimu katika ukuzaji wa uchumi wa nchini, hivyo ufufuaji wa zao hilo ni kichocheo cha viwanda kwa kuwa kutakuwa na uhakika wa upatikanaji wa malighafi na kuvutia wawekezaji.

Waziri Mkuu anabainisha kuwa licha ya kuwepo kwa michikichi mingi nchini lakini uzalishaji wake unafanyika kwa njia za kienyeji, hivyo Serikali imedhamiria kuboresha kilimo hicho kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili liweze kuleta manufaa makubwa kwa Taifa na wakulima.


JENGENI DARAJA USIKU NA MCHANA- KWANDIKWA

$
0
0
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa amemtaka Mkandarasi anayejenga Daraja la Magara linalounganisha Wilaya ya Babati na Mbulu kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa haraka na ubora unaotakiwa ili kuwaondolea wananchi kero ya usafiri inayowakabili.

Akizungumza mara baada ya kukagua daraja hilo, Kwandikwa amesema tayari kiasi cha shilingi bilioni 1.4 kimelipwa kama malipo ya awali hivyo Mkandarasi aongeze kasi na kulimaliza daraja hilo pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa Kilomita 4.9 katika kipindi cha miezi 24.

“Daraja hili likikamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa litahamasisha shughuli za biashara na uzalishaji kati ya Mbulu na Babati na hivyo kuchochea uchumi wa wilaya hizo” amesema Kwandikwa.Aidha amemtaka Mkandarasi China Railway Seventh Group (CRSG) anaejenga daraja hilo kutoa fursa za ajira kwa wakazi wa Wilaya za Mbulu na Babati katika kuharakisha ujenzi wake.

Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Manyara, Mhandisi Bashiri Rwesingisa amemhakikishia Naibu Waziri Kwandikwa kuwa ujenzi wa Daraja la Magala ni Sehemu ya Mkakati wa Serikali wa kuijenga barabara ya Kutoka Mbuyu wa Mjerumani hadi Mbulu kwa Lami ambapo tayari upembuzi yakinifu kwa ajil ya ujenzi huo umekamilika.
Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Manyara, Mhandisi Bashiri Rwesingisa akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa (aliyevaa kofia) kuhusu hatua iliyofikia ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Mizani ya kudumu katika eneo la Mwada-Mbuyu wa Mjerumani, Wilayani Babati. Mkoani Manyara.
Muonekano wa mto Manyara ambapo linajengwa daraja la Magara lenye urefu wa mita 84, wilayani Babati Mkoani Manyara. Daraja hilo linatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 24.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa akitoa maelekezo kwa Uongozi wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Mkoa wa Manyara kuhusu kuzingatia viwango katika ukarabati wa barabara sehemu ya mlima Magara kwa kiwango cha zege mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Mkoani Manyara.
Mafundi wakindelea na ujenzi wa barabara sehemu ya Magara kwa kiwango cha zege, Mkoani Manyara.
Muonekano wa barabara Magara-Mbulu ambayo inafanyiwa ukarabati na Wakala wa Barabara Nchini (TNAROADS) kwa kiwango cha zege,Mkoani Manyara.

Maamuzi ya taasisi lazima yashirikishe baraza la wafanyakazi –Profesa Msanjila

$
0
0
Na Chalila Kibuda.

Maamuzi yanapotakiwa kufanyika ni lazima uwepo ushirikishaji ili kuweza kuendesha taasisi na kupata mafanikio ya kimaendeleo na taifa kuona tija ya tasisi husika.

Hayo aliyasema Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila wakati akifungua Baraza la Pili la Shirika la Taifa la Madini (Stamico) amesema sheria ya mashauriano katika utumishi wa umma, serikali imebainisha nia yake thabiti ya kutaka kuona wafanyakazi wakishirikishwa katika kusimamia na kuendesha taasisi wanazozimamia.

Amesema kuwa baraza ni chombo muhimu katika taasisi hivyo lazima kitumike katika kujadili mambo mbalimbali yanayoyohusu masilahi na ustawi wa watumishi , mipango na malengo ya kazi ya kuishauri menejimenti ya Stamico.Profesa Msanjila amesema viongozi waliochaguliwa katika baraza la wafanyakazi wa stamico kunadhihirisha imani ya wafanyakazi kuwa kile wanachokitaka kitafanyika kutokana na maamuzi ya ushirikishwaji.

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Stamico Mhandisi Kanali Sylvester Ghuliku amesema baraza lilopita lilikuwa na changamoto nyingi ambazo zilikuwa zinatokana na shirika lenyewe kwa kutokuwa na fedha za kuitisha mkutano wa baraza na fedha ambazo zilikuwa zinapatikana katika shirika kidogo na hata kuendesha ofisi hazikutosha.

Amesema kuwa baraza litafanyaka kazi katika misingi iliyowekwa katika uanzishaji katika kufikia lengo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila akizungumza na baraza jipya la wafanyakazi la pili la Stamico lilofanyika Ofisi za Stamico jijini Dar es Salaam.
Watoa maada kutoka ofisi ya Kamishina wa madini, , Idara ya kazi na wawakilishi kutoa Chama cha wafanyakazi wa Migodi, Nishati , Ujenzi na Kazi Nyinginezo (Tamico)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Profesa Simon Msanjila wa sita kutoka kushoto mstari wa mbele akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la pili jipya la Wafanyakazi wa Stamico, kulia kwa katibu Mkuu ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Stamico Mhandisi Kanali Sylvester Ghuliku wane kutoka kushoto mstari wa mbele ni Katibu Mpya wa Baraza hilo Juma Mbawambo

BoT YAAMUA ZIUNGANISHA BENKI ZA BENKI ZA TWB , TPB BANK Plc

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imeridhia ombi la uunganishwaji wa benki za Benki ya Wanawake Tanzania(TWB) pamoja na TPB Bank Plc.

Kutokana na hatua hiyo sasa kutakuwa na benki moja kuanzia Agosti 3 mwaka huu itakayoendelea kuitwa benki ya TPB Bank Plc ambayo itaendelea kuwa na mtaji wa kutosha kama inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Profesa Florenc Luoga amesema wamefikia uamuzi huo kutokana na ombi la wanahisa la kutaka kuunganishwa kwa benki hizo. Amesema hivyo kuanzia sasa wateja, wafanyakazi , mali a madeni yote ya TWB yataunganishwa na yale ya benki ya TPB huku akifafanua muunganiko wa benki hizo unaifanya benki ya mpya ya TPB Bank Plc kuwa imara zaidi na itakuwa ina mtaji wa kutosha kama inavyotakiwa chini ya kifungu cha 17 cha sheria ya mabenki na taasisi za fedha.

"Benki Kuu inawaomba wateja wa benki ya TWB kuwa watulivu katika kipindi hiki cha mpito cha uunganishwaji wa benki hizi na watendelea kupata huduma za kibenki kwa utaratibu utakaotolewa na menejimenti ya uongozi wa benki ya TPB,"amesema Profesa Luoga. Wakati huo huo amesema Benki za TOBACO na KCBL kwa sasa zimeweza kuongeza mtaji na kukidhi kiwango kinachohitajika kisheria na hivyo zinaendelea na shughuli zake kama kawaida.

Amesema BoT inawagakikisha wananchi kuwa itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta uhimilivu katika sekta ya fedha. Awali Gavana Luoga amefafanua Januari 4 mwaka huu BoT iliongeza muda wa miezi sita kwa benki tatu ambazo ni Tandahimba Community Bank Limited (TOBACO), Tanzania Women's Bank Plc(TWB) na Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL).

Ambapo mpaka Juni 30 mwaka huu ili kufikisha kiwango cha mtaji kinachohitajika na sheria ya mabenki na taasisi za fedha ya mwaka 2007 na kanuni zake za kiwango cha chini cha mtaji cha Sh.bilioni mbili kwa benki za wananchi. Aidha benki hizo ziliongezewa muda wa mwezi mmoja hadi Julai 31 mwaka 2018 ili kukamilisha taratibu za kuongeza mtaji.

Kutokana na kutolewa kwa muda huo ndipo wanahisa wa TWB na TPB walipoamua kuunganisha benki hizo na BoT imeridhia.

BINTI THERESIA,MKAZI WA MBURU ANAHITAJI MSAADA WA MATIBABU

$
0
0

"Huyu binti anaitwa Theresia yupo hapa Mbulu, aliugua ghafla na kupooza upande wa kulia toka 2011,alikuwa hawezi kuongea kabisa kwa zaidi ya mwaka mmoja,baada ya matibabu kwa mwaka mmoja alianza kuongea kidogo na kukaa,

Lakini kutokana na hali kuwa ngumu ya kumuhudumia wazazi wake walishindwa kuendelea na matibabu,na kwa zaidi ya miaka sita amekuwa akilala ndani tu muda wote,na hawezi kufanya chochote japo kuwa kwa sasa anaweza kuongea kidogo saana na kwa mbali ananyanyua mkono wake,tumemtembelea na kumpatia kiti cha kumuwezesha hata kutoka nje. 

Tunatamani binti huyu aweze kuanza kupatiwa matibabu tena na mazoezi! Watanzania wenzangu tumsaidie, Tutawajulisha pindi tutakapojua taratibu zote za matibabu na gharama kisha tutatoa mawasiliano ya wazazi wake! Ana umri wa miaka 27 na kabla alikuwa ni mfanyakazi katika mamlaka ya maji safi Mbulu". 

Mungu Ibariki Tanzania

Taarifa hii ni kwa Hisani ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndg. Hudson Kamoga

 Pichani ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndg. Hudson Kamoga akimsaidia  binti  Theresia mkazi wa Mbulu, kumtoa nje kwa njia ya baiskeli ya walemavu (Wheel Chair) ,Theresa aliugua ghafla na kupooza upande wa kulia tangu mwaka 2011,kufuatia hali hiyo bint huyo anahitaji msaada wa Matibabu

DKT TIZEBA AAGIZA WAKAGUZI WA VIUATILIFU KULINDA MASLAHI YA TAIFA

$
0
0

Mgeni rasmi-Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akizungumza wakati wa mkutano wa ufunguzi wa mafunzo ya wakaguzi wa viuatilifu kwenye hafla iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha kilimo (SUA) Mkoani Morogoro leo Tarehe 5 Agosti 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)

Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akisisitiza ufanisi kazini wakati akizungumza kwenye mkutano wa ufunguzi wa mafunzo ya wakaguzi wa viuatilifu kwenye hafla iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha kilimo (SUA) Mkoani Morogoro leo Tarehe 5 Agosti 2018.
Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (Tropical Pesticide Research Institute - TPRI) Dkt Margaret Mollel akitoa taarifa ya mafunzo ya wakaguzi wa viuatilifu mbele ya mgeni rasmi Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba kwenye hafla iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha kilimo (SUA) Mkoani Morogoro leo Tarehe 5 Agosti 2018.
Picha ya pamoja baada ya kumalizika mkutano wa ufunguzi wa mafunzo ya wakaguzi wa viuatilifu kwenye hafla iliyofanyika Chuo Kikuu cha kilimo (SUA) Mkoani Morogoro leo Tarehe 5 Agosti 2018.



Na Mathias Canal, WK-Morogoro

Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba leo tarehe 5 Agosti 2018 amefungua rasmi mafunzo ya wakaguzi wa viuatilifu yaani mimea na mazao katika hafla iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha kilimo (SUA) Mkoani Morogoro ambapo asilimia 99 ya washiriki wanatoka katika vituo vya ukaguzi wa mazao mipakani vikiwemo vya nchi kavu, bandarini na viwanja vya ndege.

Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (Tropical Pesticide Research Institute - TPRI), Waziri Dkt Tizeba ameagiza washiriki hao Kulinda maslahi ya wakulima, walaji na Taifa kwa ujumla dhidi ya wafanyabiashara wachache wa viuatilifu wanaotaka kutajirika kwa kutuletea viuatilifu vilivyo chini ya kiwango.

Waziri huyo anayeshughulikia sekta ya kilimo nchini ameyasema hayo kwa msisitizo mkubwa huku akiwataka kutekeleza wajibu wao wa ukaguzi wa viatilifu kwa umakini, uaminifu na uadilifu mkubwa kwa kutumia Sheria na Kanuni zilizopo.
Amesisitiza kuwa wataalamu hao wanapaswa kuitetea maslahi ya nchi pale inapohitajika kwa kutumia kwa umakini mkubwa kwa utashi wa Sheria na Kanuni zinazotakiwa ikiwa ni pamoja na taratibu nyingine za kisheria katika kuhusisha watumishi wengine wa Serikali kama waendesha mashtaka wa Serikali na askari.

Pia, aliwataka Wakaguzi kutoka Makao Makuu ya Wizara na Taasisi ya TPRI kuangalia namna ya kuunganisha shughuli zinazofanywa kati ya Kitengo cha afya ya mimea (PHS) na TPRI katika kuwasimamia na kuwaongoza wakaguzi kutoka katika vituo vyetu vya mipakani ili watekeleze majukumu yao kwa ufanisi na uadilifu kwa kuwapatia vitendea kazi pale fursa zinapopatikana kwa kuzingatia mahitaji.

Katika hatua nyingine Waziri Tizeba ameelekeza uongozi wa TPRI pamoja na PHS kuhakikisha katika mafunzo hayo wanawapatia taarifa muhimu za orodha ya viuatilifu vilivyosajiliwa kote nchini ili kurahisisha utendaji timilifu katika kutekeleza majukumu yao.

Amewasisitiza watumishi hao kushirikiana na watumishi wengine wa Serikali kutoka taasisi mbalimbali walio katika vituo vya ukaguzi mipakani ili kuongeza ufanisi wa kazi na kuwahudumia wadau kwa wakati kama ilivyoelekezwa katika mafunzo hayo.

Aidha, ameipongeza TPRI kwa juhudi wanazochukua za kuongeza idadi ya wakaguzi wa viuatilifu kupitia mafunzo ambapo ameeleza kuwa mafunzo hayo yatawezesha wakulima kuweza kudhibiti visumbufu vya mazao kwa kutumia viuatilifu sahihi na hivyo kulinda afya za walaji, viumbe wengine na mazingira, na kuiwezesha Tanzania kukidhi matakwa ya mikataba ya kimataifa ya udhibiti wa viuatilifu na visumbufu vya mimea na mazao.

Sambamba na hayo aliongeza kuwa kwa kutambua changamoto ya tija ndogo katika uzalishaji, Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 Ibara ya 22 inayosimamiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt John Pombe Joseph Magufuli, inaielekeza Serikali kufanya kilimo chenye tija kwa kuzingatia matumizi sahihi ya teknolojia (zikiwemo za udhibiti wa visumbufu vya mazao) ili kuongeza malighafi za viwanda vya kuongeza thamani ya mazao na ajira.

Alisema, Mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo ASDP II umeainisha umuhimu wa matumizi ya Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mazao (Integrated Pest Management - IPM) vikiwemo viuatilifu katika kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo.

“Hivyo, ni matumaini yangu kuwa usimamizi na udhibiti wa uingizaji na matumizi sahihi ya viuatilifu itawezesha kufikiwa kwa malengo ya nchi ya kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya kilimo na kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda” Alikaririwa Mhe Dkt Tizeba

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika Ukanda wa Kitropiki (Tropical Pesticide Research Institute - TPRI) ambaye pia ni makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Kilimo (SUA) Prof Raphael Chibunda amemshukuru Waziri huyo wa kilimo kwa kufungua mafunzo hayo ya siku 14 ambapo alisema kuhusu changamoto ya wakaguzi wa viutilifu na visumbufu vya mimea ni Chuo hicho cha kilimo kuanzisha Shahada ya Usimamizi na ulinzi wa mimea (Plant Protection Management).
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images