Na Emmanuel Massaka, Blogu ya jamii
NAIBU Waziri wa Nishati Subira Mgalu ameendelea na ziara yake Mkoani Mtwara kukagua miradi na kuangalia utekelezaji wa huduma ya umeme kwa wananchi mkoani huo.
Katika ziara yake Mgalu ameeleza kuwa kwa mwaka huu wananchi wa kata ya Chipuputa wataunganishiwa huduma ya umeme kwa bei ya shilingi elfu 99 ,gharama ambayo Tanesco iliwatangazia Wananchi tangu hapo awali.
Aidha Waziri Mgalu ameagiza kuwa bei hiyo ya elfu 99 walizoahidiwa na shirika hilo kipindi cha nyuma, ndizo zitakazotumika kuwaunganishia huduma ya umeme kwa wananchi wa kata ya Chipuputa kijiji cha Kagera.
"Takribani bilioni 1 zimetumika kwenye mradi huo, hivyo wananchi watakaokosa nafasi mwaka huu,waondoe hofu kwani kuna nafasi zitaongezwa ambazo zitawafikia wakazi wa Mtwara'',alisema Waziri Mgalu na kuongeza kuwa amemwagiza Meneja wa Tanesco kuandaa orodha ya wananchi waliojiandikisha kupata huduma hiyo ili wapatiwe huduma ya kwa wakati kama ilivyopangwa.
Mgalu amesema kuwa kwa mwaka huu wananchi wa kata ya Chipuputa wajiandae kupokea umeme ,kwani ujio wa huduma hiyo itawasaidia katika shughuli za kukuza uchumi wao.Aidha wakazi wa Chipuputa wameshukuru kwa ujio wa Naibu Waziri na kueleza kuwa changamoto iliyodumu kwa muda mrefu sasa imetatuliwa.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa kata ya Chipuputa kijiji cha Kagera mkoa wa Mtwara , ambapo alimuagiza Meneja wa Tanesco kuhakikisha wananchi wanaunganishwa umeme kwa bei ya zamani ya shilingi 99,000.
Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mtwara wakikagua maendeleo ya mradi wa mashine mbili mpya za kuzalisha umeme katika Halmashauri ya Mtwara.
Muonekano wa mashine mbili mpya za kuzalisha umeme zinazoendelea kufungwa katika Halmashauri ya Mtwara.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa kata ya Chipuputa kijiji cha Kagera mkoa wa Mtwara , ambapo alimuagiza Meneja wa Tanesco kuhakikisha wananchi wanaunganishwa umeme kwa bei ya zamani ya shilingi 99,000.
Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Mtwara wakikagua maendeleo ya mradi wa mashine mbili mpya za kuzalisha umeme katika Halmashauri ya Mtwara.
Muonekano wa mashine mbili mpya za kuzalisha umeme zinazoendelea kufungwa katika Halmashauri ya Mtwara.
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu akimsikiliza msimamzi wa mradi wa ujenzi wa mashine mbili mpya za kuzalisha umeme, Mhadisi Mkulugwa Chinumba namna mradi huo unavyofanya kazi.