Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

KESI YA TUHUMA ZA MAUAJI YA KUKUSUDIA YAKWAMA MAHAKAMANI

$
0
0
*Ni baada ya gari ya kubeba mahabusu kuharibika

Na Dixon Busagaga, Moshi

KESI ya tuhuma za mauaji ya kukusudia linalomkabili mmilikiwa wa Shule ya Sekondari ya Scolastica Edward Shayo na wenzake wawili limehairishwa kwa mara ya tatu sasa na sababu ya kuahirishwa ikitajwa imetokana na kuharibika kwa gari la kubebea mahabusu.

Kwa jana kesi hiyo ilipangwa kuendelea kwa hatua ya usomaji wa maelezo ya mashahidi kwa ajili ya kufunga ushahidi kabla ya shauri hilo kuhamishiwa Mahakama Kuu. Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Sophia Masati alieleza kuwa shauri hiyo itatajwa kwa ajili ya usomaji wa maelezo ya mashahidi Agosti 3,mwaka huu.

“Kesi hii imeahirishwa hadi Agosti 3 mwaka huu kwa ajili ya kuja kusoma maelezo ya mashahidi wa kesi hii,"amesema Hakimu huyo.Kabla ya kutajwa kwa mara nyingine kwa shauri jana, Julai 6 mwaka huu Hakimu mkazi wa mahakama ya hakimi mkazi ,Moshi ,Julieth Mawole aliieleza maelezo ya ushahidi wa shauri hilo utatolewa .

Kwa mara ya kwanza usomaji wa maelezo ya kufunga ushahidi uliahirishwa baada ya washtakiwa kushindwa kufikishwa mahakamani.Sababu za kutofika kwa washtakiwa mahakamani hapo zilitajwa kuwa ni mkanganyiko wa tarehe iliyopangwa na mahakama hiyo ambayo ilikua ni June 29 mwaka huu kutofautiana na ile iliyowasilishwa Mahabausu Gereza la Karanga ambayo ilitajwa kuwa ni Julai 29 ,mwaka huu.

Maelezo hayo yaliwasilishwa mahakamani hapo na Wakili wa Serikali,Agatha Pima alipoomba kupangwa kwa tarehe nyingine kwa ajili ya kuendelea kwa hatua ya Kufunga Ushahidi kwenda Mahakama kuu.Ombi hilo lilipingwa na Wakili wa upande wa utetezi anaye mtetea Mshtakiwa wa Pili katika shauri hilo ,Edward Shayo,Elikunda Kipoko akieleza kutoridhishwa na maelezo ya upande wa Jamhuri .

Hata hivyo Hakimu,Mawole aliarisha Shauri hilo na kuoanga Julai 6 mwaka huu huku akieleza kusikitishwa na kitendo hicho kwa Washtakiwa kushindwa kufikishwa mahakamani hapo kutokana na mkanganyiko huo wa tarehe .Julai 6 mwaka huu Mahakama ya Hakimu Mkazi ,Moshi ilihairisha kuendelea na shauri kwa mara nyingine safari hii sababu zikitajwa ni kuugua ghafla kwa wakili wa upande wa Jamhuri ,Agatha Pima muda mfupi kabla ya kuanza kwa shauri hilo.

June 27,mwaka huu Mahakama ya Hakimu Mkazi ,Moshi ilielezwa kukamilika kwa upelelezi wa shauri hilo linalomkabili mmiliki wa shule ya sekondari ya Scolastica,Edward Shayo na wenzake ,Laban Nabiswa(Mwalimu) na Hamisi Chacha,mlini wa shule hiyo.

Wakili wa serikali Agatha Pima aliieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo la mauaji ya kukusudia ya mwanafunzi Humphrey Makundi umekamilika kwa asilimia 100.

Novemba 6,mwaka jana Mwanafunzi huyo ,mwili wake ulikutwa umetupwa mto Ghona mita 300 kutoka eneo la shule hiyo ambapo mwili huo ulizikwa katika makaburi ya Manispaa ya Moshi Novemba 12,mwaka jana.

CCM YAZINDUA KAMPENI KATA YA MAWENZI, YAAHIDI KUSIMAMIA, KUTOA FURSA ZA MAENDELEO KWA WANANCHI

$
0
0
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimezindua rasmi kampeni za uchaguzi mdogo Kata ya Mawenzi ilipo Moshi Mjini huku kikitumia nafasi hiyo kuahidi kuenddelea kusimamia na kutoa fursa nyingi zaidi za maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo wa kampeni hizo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole amesisitiza CCM kuendelea kusimamia na kutoa fursa nyingi zaidi za kimaendeleo kwa wananchi wa Moshi Mjini katika Kata ya Mawenzi.

Polepole amewaomba wananchi wa Kata ya Mawenzi kumpatia kura za ushindi mgombea wa CCM Apaikunda Ayo Naburi kuwa Diwani wa Kata hiyo ili awe kiungo cha fursa zitokanazo na Serikali ya CCM kwa wananchi wake.

Akifafanua kuhusu fursa hizo za wananchi Polepole amesema CCM imejipanga kuhakikisha wananchi wanapata mikopo ya Halmashauri bila usumbufu, mizengwe wala riba.

Pia wafanyabiashara wadogo wadogo waendelee kufanya shughuli zao kwa utaratibu mzuri pasina usumbufu na Vijana wa bodaboda na bajaji watazamwe katika jicho la utu, usawa na haki katika shughuli zao za usafirishaji wa abiria katikati ya mji wa Moshi.

"Naomba mtupatie Apaikunda awe jicho letu, mtu tunaye muamini, ndio kiungo akisema nasi tunatoa maelekezo kwa manufaa ya wananchi," amesema Polepole.

Uzinduzi huo wa kampeni, ni muendelezo wa mikutano ya kampeni ya uchaguzi Mdogo katika kata na majimbo ambapo CCM inaendelea kunadi Sera zake bora kwa wananchi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole  akiwahutubia Wananchi na wafuasi wa chama hicho wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo,
amesisitiza CCM kuendelea kusimamia na kutoa fursa nyingi zaidi za kimaendeleo kwa wananchi wa Moshi Mjini katika Kata ya Mawenzi.

CHILIGATI AKABIDHI MKURABITA KWA NJOOLAY.

$
0
0
JOSEPH MPANGALA

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania MKURABITA,Balozi Daniel Ole Njoolai ameiomba Halmashauri kote nChini Kuhakikisha zinasaidia Mpango wa kurasimisha ardhi ili wananchii waweze kupatiwa hati zitakazowawezesha kujikwamua kiuchumi.

Hayo yameyasema katika makabidhiano ya uongozi wa Kamati Hiyo ambayo ilikuwa ikiongozwa na Kaptein Mstaafu John Chiligati katika kipindi cha Miaka Mitatu Jijini Dodoma.

Balozi Njoolay amesema katikakipindi chake cha uongozi kama mkuu wa mkoa kwa miaka 16 tayari anazifaham Halmashauri hivyo kuziomba kushirikiana ili kuwezesha Wananchi kuweza kurasimisha ardhi na Biashara.

“Mimi nimefanyakazi kama mkuu wa Mkoakwa Miaka 16 Nazifaham Halmashauri,Nitumia nafasi hii kuziomba Halmashauri Zitusaidie sana,ziwe positive kwa swala hili watu wao ndio Tunawasaidia kwa sababu Bila halmashauri hakuna Kitu”amesema Balozi Njoolay

Naye Mwenyekiti Mstaafu wa kamati hiyo Kaptein Mstaafu John Chiligati amesema wananchii wa Vijijini ambao wanakadiriwa kufikia asilimia 80 hawana uwelewa wa Urasimishaji ingawa wanamashamba Makubwa lakini hayana hati ya Umiliki hivyo kuendelea kubaki kuwa masikini.

“Wananchii wetu wa Vijijini karibu asilimia 80%mtu ambaye anamigomba yake mihogo yake kila kitu anacho halafu anasema masikini wakati Duniani kote Mtu ambaye anamiliki Ardhi anaitwa LandLord yaan ni mtu ambaye yuko vizuri lakini siri yake ni kwamba hii mali aliyonayo bado haitambuliki na yeyote”Amesema Chiligati Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania MKURABITA Ulianzishwa mwaka 2004 na tayari umefika katika mikoa 27,23 mikoa ya Tanzania Bara na mikoa 4 ya Zanzibar na tayari hati hati elf 71 na 51 na zimewawezesha kukopa shilingi Billlion 5.5 kutoka katika taasisi mbalimbali za kifedha
Mwenyekiti Mstaafu wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA), Kapteni Mstaafu John Chiligati akimkabidhi kitabu cha mwongozo, Mwenyekiti mpya wa Kamati hiyo, Balozi Daniel Ole Njoolay mbele ya wajumbe na watendaji wa kamati hiyo jijini Dodoma.

Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njoolay akizunguza mbele ya watendaji na jumbe wapya MKURABITA katika kikao elekezi kilichofanyika jijini Dodoma.

CHADEMA SIRARI WAMFUTIA UANACHAMA KIONGOZI BAADA YA KUMTUHUMU KUTAFUNA FEDHA ZA KUNUNUA JENEZA

$
0
0
Na Frankius Cleophace, Tarime

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo( Chadema)Kata ya Sirari wilayani Tarime mkoani Mara kimemvua uongozi na kumfutia uanachama aliyekuwa Mwenezi wa kata hiyo Samwel Kijiji Mwita kutokana na tuhuma za upotevu wa fedha Sh.80,000 zilizochangwa kwa ajili ya kununua jeneza katika msiba wa aliyekuwamwanachama wa chama hicho marehemu Chacha Makuri.

Mwita Isansi ni Mwenyekiti wa Chadema Kata ya Sirari amesema wameamua kumfutia uanachama Mwita kutokana na tuhuma hizo za upotevu wa fedha.Mwita amesema kuwa zilichangwa ni Sh.320,000 kwa lengo la kununu jeneza nchini Kenya lakini baadae zilipungua Sh.80,000.

“Baada ya upotevu wa fedha hizo sisi kama viongozi tulijichanga ili kununua jeneza baada ya msiba tumemuita kamati ya maadili takribani mara mbili lakini hajaweza kuitikia na maamuzi yetu ni kumfuta uanachama na kumvua uongozi kwahiyo mpaka sasa siyo kiongozi,” amesema Mwita.

Mwenyekiti huyo ametoa mwito kwa viongozi wengine kuendelea kuzingatia maadili ya uongozi na sikufanya ubadhilifu wowote na kusema kuwa chama kitaendelea kuchukua hatua kali kwa viongozi ambao wanaenda kinyume na maadili ya uongozi.

Aidha Mwenyekiti wa kijiji cha Sokoni Denson Makanya amesema kuwa licha ya kutafuna fedha hizo bado Mwenezi huyo amekuwa akituhumiwa kwa makosa mbalimbali na tayari alishaandikiwa barua ya onyo juu ya vitendo vyake alivyokuwa akifanya akiwa kiongozi ndani ya jamii.

WAZIRI KIGWANGALLA AWATAKA WAVAMIZI MAENEO YALIYOHIFADHIWA KUONDOKA

$
0
0
Na Pamela Mollel,Arusha

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla amewataka wananchi waliovamia maeneo ya hifadhi nchini, kujiandaa kuondoka ndani ya miezi mitatu kabla ya operesheni kuanza.

Akizungumza na waandishi wa habari,Julai 19 katika eneo la hifadhi ya Jamii ya wanyamapori(WMA) ya makao, wilayani Meatu, Dk Kigwangalla alisema wavamizi wa maeneo ya hifadhi wengi wamekuwa wakijihusisha na matukio ya ujangili.

"utakula kijiji kina ardhi kubwa, lakini wengine wanajenga hadi katika ndani ya eneo la mita 500 kutoka mpaka wa hifadhi na hao mara nyingi ndio wanaingiza mifugo hifadhini usiku na kufanya ujangili"alisema.Alisema maeneo mengi ya hifadhi na mapori ya akiba nchini yamevamia na wananchi jambo ambalo serikali haiwezi kukubali yaharibiwe ama kutumika kwa ujangili.Waziri huyo, pia alitembelea kambi ya kitalii ya TGTS na hoteli ya Mwiba na kushuhudia vikosi vya kupambana na ujangili katika maeneo hayo ambavyo vipo yapo chini ya taasisi Friedkin Conservation Fund na kueleza kuridhishwa na uwekezaji wa taasisi hiyo.

Mkurugenzi wa Mwiba Holding, Abdukaril Mohamed, alisema katika eneo la Mwiba wamewekeza sh 2.2 bilion na hivi sasa wanaendelea na shughuli za uhifadhi na utalii."mheshimiwa Waziri katika eneo hili, kampuni yetu inafanya utalii wa picha na kuna hoteli,tunafanyakazi kwa amani na utulivu na vijijini vinavyotuzunguka"alisema

Mwenyekiti wa kijiji cha makao, Anthony Philip, alimweleza Waziri Dk Kigwangalla kuwa, katika eneo hilo kuna mahusiano mazuri baina ya vijiji na wawekezaji na vijiji vinapata mgao wa fedha.Alisema kijiji cha makao kimekuwa kikipata zaidi ya sh 147 milioni kwa mwaka kutoka kwa mwekezaji na vijiji vingine sita vimekuwa vikipata zaidi ya milioni 80,000 kila mwaka"alisema.

Akiwa katika pori la akiba la Maswa,Meneja wa pori hilo, Lusato Masinde alisema pia wanauhusiano mzuri na wawekezaji ambao licha ya kulipia ada za vitalu pia wamekuwa wakitoa msaada wa huduma mbali mbali ikiwepo maji.Hata hivyo, alisema katika pori hilo changamoto kubwa ni uvamizi wa mifugo, uchache wa watumishi na upungufu wa vitendea kazi.

Waziri wa Maliasili na utalii,Dk Hamis Kigwangalla akipata maelezo juu ya hoteli ya kitalii ya Mwiba kutoka kwa meneja wa hoteli hiyo,Alina Redka jana baada ya kutembelea hoteli hiyo iliyopo hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Makao

Waziri wa Maliasili na utalii,Dk Hamis Kigwangalla akipata maelezo juu ya mipaka baina ya kijiji cha Makao na eneo la hifadhi kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Mwiba holding's Abdulkadir Mohammed jana eneo la Makao

Waziri wa Maliasili na utalii,Dk Hamis Kigwangalla alipotembelea hoteli ya kitalii ya Mwiba iliyopo ndani ya hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Makao

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA

$
0
0

Na Kumbuka Ndatta,Arusha

NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega ametembele taasisi za Serikali zilizopo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau wengine wa sekta ya mifugo na uvuvi.

Akitoa taarifa fupi kwa Naibu waziri,Mkurugenzi wa Wakala wa vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Tengeru Joseph Msemwa amemweleza Ulega kuwa kazi kubwa ya LITA ni kutoa mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi,kufanya utafiti na ushauri elekezi na uzalishaji Mali.

Pia mafunzo hayo yamejikita katika fani ya afya ya mifugo na uzalishaji.Aidha mafunzo hayo yanalenga kutoa watalaam wenye ujuzi wa hali ya juu katika fani za ufugaji.Amesema lengo ni kuwa na mtazamo wa Kujiajiri na kuendesha miradi mbalimbali ya kibiashara.

Msemwa amemwambia Naibu Waziri baadhi ya changamoto zinazoikabili Kampasi hiyo kuwa ni uchakavu wa majengo,huduma duni za maji,upungu wa watumishi na Muundo wa Wakala.Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa LITA (CEO)Magreth Pallangyo pamoja na kupokea maagizo kutoka kwa Naibu Waziri,ameahidi kuyatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na kuyashughukia ipasavyo.

Akihutubia watumishi waliofika katika ukumbi wa Kampasi ya Tengeru Ulega amesema kuwa vyuo hivi vya mafunzo ya mifugo ndio nguzo mama katika kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa letu."Wakufunzi wa Vyuo hivi vya Mifugo jitahidi sana kuhusianisha kile mnachokifundisha darasani na mazingira halisi ya itanzania.

"Toeni elimu bora ili muweze kuwasaidia vijana hawa na taifa kwa ujumla.Vijana hawa wakitoka hapa tunataka waone kuwa wamezungukwa na fursa za kiuchumi," amesema Ulega.

Pia Ulega amesema kuwa ni jukumu la vyuo hivyo kuhakikisha vinatoa vijana walioiva kitaaluma ili wakitoka hapo waweze kutoa elimu bora ya namna ya uchakataji wa nyama, maziwa,vyakula vya mifugo na namna bora ya uchunaji wa ngozi, kwani ngozi hizo ni malighafi ya Viwanda vyetu na itasaidia kuendana na soko la ndani ya nchi yetu na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine Ulega amepata fursa ya kutembelea Kituo cha Uzalishaji Mifugo Kwa Chupa (National Artificial Insermination Centre) na kushuhudia baadhi ya madume ya ng'ombe yaliyopo kituoni hapo.

Mkurugenzi wa Kituo hicho Dk.Mollel amesema kituo hicho kwa sasa kinazalisha mbegu bora za ng'ombe na hewa baridi aina ya (Liquid Nitrogen) kwaajili ya kuhifadhia mbegu na kutoa vifaa vyote vya uhimilishaji ambayo ni mitungi ya kuhifadhia na Kusafirisha Mbegu.

Vilevile Dkt. Mollel amemueleza Naibu Waziri kuwa kwa mwaka 2018/2019 kituo hicho kimejipanga kuhimilisha ng'ombe takribani milioni tatu hivyo katika kipindi cha miaka mitano ng'ombe takribani milioni 10 watakuwa wameshahimilishwa.Amesema na hiyo ni kutokana na juhudi za Serikali katika kuboresha Sekta ya Mifugo hapa nchini.

Pia kituo cha NAIC kinatoa wataalam wa uhimirishaji ikiwa ni pamoja na watu binafsi wanaoteuliwa na vikundi vya wafugaji na vilele kukusanya na kutunza takwimu muhimu za himulishaji.

Awali Naibu Waziri Ulega alipata fursa ya kutembelea wadau mbali mbali wa mifugo na uvuvi mkoani Arusha ikiwa ni pamoja na kiwanda cha ngozi cha Salex LTD,Shamba la Ufugaji samaki la Shazain na Ezekiel Mhina.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiangalia ng`ombe wa uhimilishaji katika kituo cha Taifa cha(NAIC) kilichpo Usa River jijini Arusha.
 Mkufunzi mwandamizi wa kitengo cha teknolojia ya maziwa,Theresia Teti  akimwelezea  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega namna ya usindikaji wa maziwa jijini Arusha.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiangalia namna ya uhimilishaji unavyofanyoka katika kituo cha Taifa cha(NAIC) kilichopo Usa River jijini Arusha.Picha na Emmanuel Massaka,MMG Arusha)
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akitembelea shamba la samaki Shazan lililopo jijini Arusha.

RAIS DKT MAGUFULI ATOA POLE KWA RAIS MSTAAFU DKT KIKWETE KWA KUFIWA NA BABA MZAZI WA MKEWE MAMA SALMA KIKWETE

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
 Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Mama salma Kikwete, kwa kufiwa na baba yake mzazi Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete na wanafamilia wakiomba dua walipofika kutoa pole kwa kufiwa na baba mzazi wa mkewe Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mama Janeth Magufuli wakiagana na mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete Mama Salma Kikwete baada da ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na ndugu wa  Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete baada da ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  wa Mama Salma, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mama Janeth Magufuli wakisindikizwa na Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete baada ya kutoa pole kwa kufiwa na baba yake mzazi  Mama Salma, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu, nyumbani kwa wafiwa Msasani jijini Dar es salaam leo Julai 21, 2018. Picha na IKULU

MAKAMU WA RAIS AWASILI MKOANI SONGWE KWA ZIARA YA KIKAZI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Songwe tayari kwa ziara ya siku 5.

Makamu wa Rais amepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Japhet Hasunga na Viongozi wengine wa Chama na Serikali.

Akiwa mkoani Songwe, Makamu wa Rais atakagua na kuhamasisha shughuli mbalimbali za maendeleo ambapo atatembelea Wilaya Tatu za Mkoa huo ambazo ni Mbozi, Momba na Ileje. Makamu wa Rais ataanzia ziara yake katika Wilaya ya Mbozi ambapo miongoni mwa shughuli atakazofanya ni pamoja na kukagua na kufungua kituo cha Afya Nanyala, kusalimia wananchi katika eneo la mradi la Nanyala, kuweka jiwe la Msingi katika Mradi wa maji Iyula na kufanya Mkutano wa hadhara katika kijiji cha Iyula.

Makamu wa Rais pia atatembelea Wilaya ya Momba ambapo atakagua na kuzindua kituo cha Afya Tunduma, atakagua shughuli za vikundi vya wajasiriamali Tunduma na kufanya mkutano wa hadhara kuzungumza na wananchi wa Wilaya ya Momba.

Vilevile, Makamu wa Rais atatembelea Wilaya ya Ileje ambapo atapokea taarifa ya shughuli za uhifadhi wa mazingira na upandaji miti na kukagua shughuli za uhifadhi na shamba la miti la Wakala wa Misitu Tanzania lilopo Katengele na baadae kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Isoko ambapo atapata fursa ya kuzungumza na wananchi wa Ileje.

Mhe. Makamu wa Rais atahitimisha ziara yake Mkoani Songwe tarehe 25, Julai 2018.

Imetolewa na;
Ofisi ya Makamu wa Rais
Julai 21, 2018
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Songwe na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala na Viongozi wengine wa Chama na Serikali katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia baadhi ya viongozi wa Chama cha CCM,mara baada ya kuwasili mkoani Songwe na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa Songwe Mhe. Lt. Mstaafu Chiku Galawa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala na Viongozi wengine wa Chama na Serikali katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Songwe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).


 

LUGUMI AITWA OFISINI KWA LUGOLA SAA MBILI ASUBUHI

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ameliagiza Jeshi la Polisi nchini kuhakikisha linampeleka mmiliki wa Kampuni ya Lugumi, Said Lugumi ofisni kwake Dodoma Julai 31 mwaka huu.

Lugola ametoa maagizo hay oleo ofisni kwake jijini Dar es Salaam wakati anazungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.

Ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa anamhitaji Lugumi ofisini kwake saa mbili asubuhi ya Julai 31 na kufafanua kuwa Lugumi alikuwa amepewa mkataba wa kufunga vifaa vya utambuzi wa alama za vidole baina ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na kampuni yake.

“Najua Lugumi ni mtanzania mwenzetu na hivyo ninapomuhitaji najua atafika kwa wakati.Nitafurahi zaidi siku hiyo kama nikisikia mlango unagongwa na kasha baada ya kuufungua nikamuona Lugumi,”amesema Lugola.Alipoulizwa anamuitwa kwa ajili ya kitu gani akajibu ni vema ikafahamika kampuni yake ilikuwa imeingia mkataba na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, hivyo anataka kuzungumza naye.


MTAMBO WA KUTENGENEZA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Wakati huo huo Lugola amesema ili kukamilisha mchakato wa usajili na utoaji wa vitambulisho vya Taifa ambapo amemuagiza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamalaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA) kuwalisha taarifa kamili kuhusu ununuzi wa mtambo wa kutengeneza kadi ghafi ambao bado haujaletwa.

“Katika hili namhitaji ofisni kwangu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA aje pamoja na mmiliki wa kampuni iliyopewa zabuni ya kuleta mtambo huo kwani alishapewa fedha dola milioni 14 ambazo ni sawa na Sh.bilioni 32.

“Hivyo siku hiyo nachohitaji ni kuuona mtambo au fedha zetu ambazo tutazipeleka benki tukiwa na ulinzi,”amesema.

CHUO CHA MAJI WAHIMIZA VIJANA WALIOSOMA MASOMO YA SAYANSI KUJIUNGA KATIKA CHUO HICHO

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii.

CHUO cha Maji kimesema changamoto kubwa iliyopo katika sekta ya maji nchini ni uhaba wa watalaamu ,hivyo jukumu la chuo hicho kuendelea kuandaa watalaamu  ambao watakuwa watakuwa wamebobea katika eneo sekta ya maji ili kuondoa changamoto hiyo.

Katika kuhakikisha changamoto hiyo inamalizwa Chuo hicho kimetoa rai kwa Watanzania na hasa vijana ambao wamesoma masomo ya sayansi na kufaulu vizuri wakajiunga na chuo hicho kwani tayari wameanza kupokea maombi ya wanaotaka kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo unaonza 2018.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam katika Maonyesho ya 13 ya Vyuo Vikuu ya Elimu ya Juu Tanzania (TCU) na Ofisa Masoko wa Chuo cha Maji Ghanima Chanzi.

Amesema kuwa chuo hicho kimedhamiria kuondoa changamoto hiyo kuwa kuhakikisha wanapatikana wahitimu waliohitimu masomo yanayotolewa na chuo hicho kwa ajili ya kulitumikia taifa kaika eneo la sekta ya maji.

"Wapo watalaam ambao wanatoa huduma katika eneo hilo lakini bado kuna changamoto kubwa , hivyo jukumu letu ni kuwapika watalaam ambao ndio wenye kujua vema eneo la maji.

"Hivyo kadri ambavyo wahitimu wataendelea kumaliza chuoni hapo watakwenda kuondoa changamoto maana tutakuwa tunaongeza watalaam mwaka hadi mwaka.Hivyo kikubwa tunaomba Watanzania kujiunga kwenye chuo chetu  ili waje kuwa wahandisi wa maji,"amesema.

Hivyo amesisitiza wanafunzi wasome masomo ya sayansi ili wawe wataalam wa maji na kufafanua wameanza kupokea maombi kupitia tovuti ya www.waterinstitute.ac.tz.

Amefafanua wanafunzi wanaosoma masuala ya maji katika chuo cha maji wengi wao wanapata ajira kwani wanahitajika zaidi na kueleza waliohitimu mwaka jana hakuna ambaye amebaki mtaani.

Kuhusu mafunzo yanayotolewa chuoni hapo amesema yapo katika ngazi ya Stashahada na Shahada na baadhi ya kozi zinazotolewa ni Uhandisi wa usambazaji maji na usafi wa mazingira,Uhandisi na umwagiliaji, Ubora wa maji (maabara),Maji na hali ya hewa na Uchimbaji visima.
Moja wa Maofisa wa chuo cha maji akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea katika banda lao katika maonesho ya vyuo vikuu yanayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.

CHUO CHA KODI WAANZISHA KLABU MPYA SHULE ZA SEKONDARI NA VYUO KUJENGEA UWELEWA KUHUSU KODI

$
0
0
Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

CHUO Cha Kodi (ITA)kimeanzisha klabu mpya katika shule za sekondari na vyuo ili kuanza kuwajenga na kuwaandaa  wanafunzi kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu kodi na umuhimu wake kwa Taifa.

Akizungumza katika Maonyesho ya 13 ya Vyuo Vikuu ya Elimu ya Juu Tanzania (TCU)yanayofanyika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Ofisa Udahili wa ITA Pascal Gomba amesema kila mwanannchi anahitajika kujua elimu ya kodi ili awe analipa kodi kwa wakati.

"Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)iliamua kuanzisha klabu za wanafunzi mashuleni kwa ajili ya kueneza elimu kwa watu wengi zaidi.Tunaamini utararibu huu utaongeza chachu ya wananchi kulipa kodi kwa maslahi ya Taifa letu,"amesema.Gomba amefafanua klabu hizo zimeanzia kwa shule za sekondari zilizopo Mkoa wa Dar es Salaam na ametaja baadhi ya shule hizo ni Jangwani,Zanaki,Kibasila,Kisutu,Loyora na Makongo.

"Kujiunga katika klabu za kodi ni moja ya mikakati ya TRA kuhakikisha elimu ya kodi inafahamika kwa kila mwananchi kuanzia ngazi ya wanafunzi hadi watu wazima,"ameongeza  Gomba.Wakati huo huo amesema uchumi wa Tanzania unakuwa kwa sababu ya ukusanyaji mzuri wa kodi na wananchi wenyewe kujituma kulipa kodi kwa hiari.

Hata hivyo Gomba amewataka wanafunzi kujiunga katika chuo cha ITA kwani  Serikali inahitaji zaidi wataalamu wa ukusanyaji wa kodi kwa manufaa ya taifa.Kuhusu uwepo wao kwenye maonesho hayo, Gomba amesema lengo kuu ni kuwaonesha wanafunzi na wananchi kwa ujumla kozi zinazotolewa katika chuo chao.

Amesema taasisi za Serikali na za binafsi zinahitaji mtu mwenye ujuzi wa ukusanyaji wa kodi kwa ajili ya kufanya shughuli zao za uzalishaji.

"Kuna umuhimu mkubwa kwa vijana wa Tanzania na hata wale watu wazima kujiunga katika Chuo cha Kodi,"amesema na kuongeza kwa sasa wanaendelea kupokea wanafunzi kwa ajili ya mwaka wa masomo wa 2018.
Moja ya maofisa wa chuo cha kodi akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda hilo.

WAZIRI KAIRUKI NA UBALOZI WA KUWAIT WAWAFARIJI WAHANGA WA MAFURIKO SAME

$
0
0
Waziri wa Madini ,Angela Kairuki akisalimiana na wakazi wa kata ya Ruvu Kajiungeni alipowatembelea kutoa pole na msaada kufuatia Nyumba zao kuathirika na Mafuriko .
Waziri wa Madini ,Angela Kairuki akiwa ameongozana na Mkuu wa Wilaya ya Same,Rosemary Senyamule wakati akiwafariji wahanga wa mafuriko wilayani Same.
Waziri wa Madini ,Angela Kairuki akizungumza na wakazi katika eneo la Kombo alipofika kutoa pole na Msaada wa Blanketi na Mahemakwa ajili ya kujisitiri.
Baadhi ya Wananchi wakimsikiliza Waziri Kairuki.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania ,Jaseen Al Najem akizungumza wakati wa kukabidhi Msaada wa Chakula kwa wahanga wa Mafuriko katika Kata ya Ruvu Kajiungeni .
Mkuu wa Wilaya ya Same,Rosemery Senyamule akitoa taarifa kwa Waziri Kairuki namna ambavyo serikali ya wilaya na mkoa zilivyoshiriki katika kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko katika wilaya ya Same.
Waziri wa Madini,Angela Kairuki akiteta jambo na Balozi wa Kuwait nchini ,Jaseen Al Najem muda mfupi kabla ya kukabidhi msaada kwa wahanga wa Mafuriko.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kumsikiliza Waziri wa Madini ,Angela Kairuki aliyeongozana na Balozi wa Kuwait nchini ,Jaseen Al Najem kutoa msaada kwa Wahanga hao.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania ,Jaseen Al Najem akikabidhi msaada wa Chakula kwa wananchi wa eneo la Kombo wilayani Same.kushoto ni Waziri wa Madini,Angela Kairuki na Mkuu wa wilaya ya Same,Rosemery Senyamule.
Waziri wa Madini,Angela Kairuki akikabidhi msaada wa Blanketi na Maturubai kwa ajili ya kujengengea mahema ya muda kwa wahanga wa Mafuriko katika wilaya ya Same.
Baadhi ya wakazi wa eneo la Kombo wakiwa wamebeba Vifurushi vya Chakula baada ya kupata mgao kutoka kwa Ubalozi wa Kuwait nchini Tanzania zikiwa ni jitihada za Waziri wa Madini ,Angela Kairuki kwa wakazi wa eneo hilo.
Waziri wa Madini,Angela Kairuki akisalimiana na mmoja wa Wazee ambao kwa sasa wanahifadhiwa na Majirani baada ya nyumba yake kuzingirwa na Mafuriko .

 Na Dixon Busagaga,Same.

UBALOZI  wa Kuwait nchini Tanzania umetoa jumla ya tani saba za msaada wa Chakula kwa waathirika wa Mafuriko wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambao walilazimika kuyahama makazi yao katia Vijiji vya Kajiungeni na Ruvu Marwa na kuhamishiwa katika Makambi.

Msaada huyo uliowasilishwa na Balozi na Kuwait nchini ,Jaseen Al Najem unatokana na jitihada za Waziri wa Madini ,Angela Kairuki za kusaidia kaya zilizofikwa na athari ya mafuriko hayo ambapo yeye binafsi alitoa Blanketi 300 na Turubai 200 kwa ajili ya wahanga hao kujisitiri.

Akizungumza wakati wa kukabidhi Msaada huo ,Balozi wa Kuwait ,Al Najeem amesema mbali na msaada huo anataraji kuzungumza na Shirika la Huduma ya kwanza la nchini Kuwait kuona namna ambavyo watashirikiana na Shirikiana na Shirika la Msalaba mwekundu kusaidia wananchi hao.

Akitoa taarifa ya athari ya Mafuriko hayo Mkuu wa wilaya ya Same ,Rosemery Senyamule amesema wananchi wamekubalina kuhama kutoka eneo la Mafuriko ambalo wamekuwa wakifanya shughuli za Kilimo na kupewa maeneo ambayo sasa watafanya makazi ya kudumu.

Waziri wa Madini ,Angela Kairuki ambaye ni mwenyeji wa wilaya ya Same akatumia hadhara hiyo kuwasilisha Pole kwa waathirika wa Mafuriko huku akipongeza serikali ya mkoa na wilaya ya Same kupitia kamati za maafa kwa namna ambavyo wameweza kushughulikia changamoto hiyo.

Waziri Kairuki akawasilisha Ombi kwa wakazi wa kata ya Ruvu Marwa katika eneo la Kombo kutumia vizuri msaada huo kutoka kwa wafadhili mbalimbali likiwemo Kanisa la Kiinjili ka Kilutheli Tanzania (KKKT)
Zaidi ya watu wapatao7000 walilazimika kuyahama makazi yao baada ya kufikwa mafuriko kutokana na mvua kubwa za masika zilizonyesha huku eneo lililoathirika zaidi likiwa ni  ukanda wa tambarare wa wilaya ya Same unaopakana na Bwawa la Nyumba ya Mungu.

MTENDAJI MKUU WA TBS NA WATENDAJI WAKE WAPEWA AGIZO

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,PWANI

KIONGOZI wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu ,Charles Kabeho amemuagiza mtendaji mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na watendaji wake ,kwenda kufanya ukaguzi katika kiwanda cha Kuchi Jogoo kilichopo kata ya Visiga ,Kibaha mkoani Pwani ili kujiridhisha na kutoa kibali cha kuanza kuzalisha unga wa nafaka .

Amewataka wahakikishe wanatimiza agizo hilo mwisho July 26 mwaka huu na kupatiwa apatiwe majibu .Kabeho aliyasema hayo ,wakati mwenge wa Uhuru ulipokuwa ukikabidhiwa mkoani Morogoro ukitokea Mkoani Pwani .

Alieleza endapo watachelea kufanya hivyo watawajibishwa kwa kuchukuliwa hatua .Alieleza wakati alipokwenda kuweka jiwe la msingi kiwandani hapo (july 19) alitoa siku saba kwa shirika hilo liwe tayari litimize agizo hilo .

Kabeho alisema ,haiwezekani kiwanda kikawa tayari kimekamilisha taratibu za uzalishaji na taratibu huku TBS ikawa kikwazo cha kushindwa kwenda kukagua na kutoa kibali baada ya ukaguzi.

"Mradi huo una gharama ya sh. milioni 812.7 ,ni mradi mkubwa na serikali inahimiza uwekezaji lakini ikitokea vikwazo ,inakwamisha adhma za serikali"Kiongozi huyo alisema kwamba ,kila mmoja atimize wajibu wake ili kuunga mkono juhudi za serikali pasipo kuweka vizuizi ambavyo vinaashiria suala la rushwa.

Hata hivyo Kabeho alisema ,viwanda vinasaidia kutoa ajira na kuinua pato la Taifa pamoja na uchumi .Aidha aliupongeza mkoa wa Pwani kwa kusheheni viwanda .
KIONGOZI wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu Charles Kabeho akimuaga mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo baada ya mwenge wa Uhuru kumaliza shughuli zake Mkoani Pwani na kuelekea Morogoro. 
MKUU wa wilaya ya Bagamoyo alhaj Majid Mwanga (kulia ) akimkabidhi mwenge wa Uhuru mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo baada ya kutoka halmashauri ya Chalinze kisha kwenda kuukabidhi mkoa wa Morogoro.
MKUU wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) akimkabidhi mwenge wa Uhuru mkuu wa mkoa wa Morogoro Kebwe Stephen Kebwe (kulia ) eneo la mpakani mwa mikoa hiyo Bwawani.(picha na Mwamvua Mwinyi)

KIGOMA YASHIKA NAFASI YA PILI KITAIFA KUWEZESHA WANANCHI KIUCHUMI

$
0
0
Na Editha Karlo,blog ya jamii,Kigoma

MKOA wa Kigoma wapiga hatua Katika kuwezesha wananchi wake kiuchumi

mkakati ulioanzishwa na Serikali wa kuwainua wananchi kiuchumi na kuboresha maisha ya wananchi kwa ujumla, umeonekana kuzaa matunda makubwa katika Mkoa wa Kigoma kwa kuinua pato la uchumi kibiashara na shuguli za ujasiliamali kwa wanaume, wanawake na vijana.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Brig. Jen. Mstaafu Emanuel Maganga ameyasema hayo leo wakati akikabidhiwa kombe na cheti cha ushindi kwa nafasi ya pili Kitaifa Katika kuwezesha wananchi kiuchumi katika ukumbi wa utamaduni Wilayani Kasulu.

Maganga alisema kuwa juhudi kubwa ambazo zimefanywa na Serikali ya Mkoa wa Kigoma ni kusimamia na kuwawezesha wananchi kiuchumi ikiwa pamoja na kutoa mikopo, kuwapa elimu na mafunzo ya Ujasiliamali wanachi kupita Mabaraza ya Biashara ya Wilaya.

Afisa wa Dawati la Uwezeshaji Kiuchumi la Mkoa wa Kigoma (RECO) Deogratias Sangu ameeleza mafanikio ya kushika nafasi ya pili yametokana na kukidhi vigezo Katika utekelezaji wa mambo yote yaliyopangwa kama msingi wa kuinua wananchi kiuchumi.Sangu ameongeza kwa kusema kuwa Mwaka jana (2017) Mkoa wa Kigoma ulishika nafasi ya mshindi wa tatu Kitaifa, na kwamba juhudi kubwa imefanyika katika kuwezesha wananchi na kutekeleza vigezo vilivyowekwa kiushindani na kufanikiwa kufikia nafasi ya pili kwa mwaka 2018.

" Ninaamini ushindi huu umetupa hamasa kimkoa ya kufanya vizuri zaidi ili mwakani tuweze kushika nafasi ya kwanza Kitaifa"alisema Sangu.Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti na mtandao huu wawakilishi wa wananchi kutoka katika vikundi, Asasi na jumuia za wafanyabiashara wameeleza kufurahishwa na juhudi zinazofanywa na Serikali ya Mkoa katika kuinua uchumi wa wananchi.

Serikali ya Mkoa wa Kigoma imeahidi kuendelea kuwawezesha wananchi katika shughuli za ujasiriamali na uanziashaji wa viwanda vidogo ili kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa Mkoani humo, ili kutoa tija zaidi katika biashar wanazofanya wajasiriamali hao.
Afisa wa dawati la uwezeshahi kiuchumi Mkoa wa Kigoma Deogratias Sangu akimkabidhi kombe la ushindi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga katika ukumbi wa utamaduni Wilayani Kasulu,kulia akishuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Brigedia Jenerali Marko Gaguti
Katibu tawala wa Mkoa wa Kigoma(RAS) Amos Charles Pallangyo akionyesha kombe ambalo Mkoa wa Kigoma umeshinda baada ya kushika nafasi ya pili Kitaifa katika kuwezesha wananchi kiuchumi

LUGOLA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA IDARA ZILIZO CHINI YAKE

$
0
0
*Pia akerwa na tabia ya wahalifu kupanga ratiba, ataka kazi zifanye saa 24 


Na Said Mwishehe, Globu ya jamii 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola ametoa maagizo kadhaa kwa idara mbalimba zilizopo chini yake kuhakikisha wanayatekeleza kwa maslahi ya nchi. 

Ametoa maagizo hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anatoa tathimini ya ziara yake aliyoifanya katika vyombo vya vyote vya ulinzi na usalama na idara zote za wizara hiyo. 

Amefafanua katika ziara yake aliyoianza Julai 11 mwaka huu yako mambo ambayo ameyabaini na hivyo ameona haja ya kuyaeleza kwa mustakabali wa ustawi wa Taifa kwa ujumla. “Miongoni mwa mambo ambayo nimeelekezwa na Rais Dk.John Magufuli ni kuhakikisha anasimamia suala la Magereza kujitosheleza kwa chakula. 

“Hivyo nimeagiza Jeshi la Magereza nchini kuwasilisha mkakati madhubuti na unaotekelezeka wa kujitosheleza kwa chakula ili kuipunguzia Serikali mzigo wa kulisha wafungwa,”amesema. 

Akifafanua katika hilo amesema kuwa kama mkakati huo kutakuwa na kipengele kinachoweka vikwazo kwa wafungwa kutofanya kazi za kuzalisha basi katika Bunge la Septemba wataanza kwa kuweka kipengele ambacho kinaelekeza wafungwa kufanya shughuli za uzalishaji chakula. 

“Mbona walioko majumbani wanalima kwa ajili ya kupata chakula kwanini waliko magerezani wasilime chakula kwa ajili yao na ikiwezekana kupata na ziada kwa ajili ya kulisha maeneo mengine,”amesema. 

AGUSIA VITU HATARISHI GEREZANI 

Wakati huo huo Lugola amesema ili kukomesha vitendo vya kuingiza vitu hatarishi magerezani ikiwemo simu za mkononi tayari ametoa maagizo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza kusimamia kikamilifu nidhamu ya askari wake wenye wajibu mkubwa katika kukomesha vitendo hivyo vya kihalifu. 

“Katika kikao changu na maofisa wa Magereza , nimezungumza na CGP kuwa gereza lolote ambalo linapatikana na matukio hayo Mkuu wa Gereza awatajibika. 


UTATUZI AJALI ZA BARABARANI 

Pia Waziri Lugola amesema katika utatuzi wa ajali za barabarani ambazo zimekuwa tatizo kubwa kwa kupoteza maisha ya Watanzania na kuacha majeruhi amesema tayari amevunja baraza la Taifa la Usalama barabarani na kamati zake za mikoa na wilaya ili kuanza upya. 

“Kabla ya mwisho wa mwezi huu nitakuwa nimeshaunda baraza jipya.Aidha nimeagiza Jeshi la Polisi nchini kuongeza juhudi katika usimamizi wa Sheria ya usalama barabarani na ukaguzi wa magari ili kudhibiti ajali. 

“Hatua kali zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kutotii sheria za usalama barabarani na kuendesha magari mabovu yanayosababisha ajali na kusababisha vifo,”amesema. 

Aidha amesema amesema kumekuwepo na kero ya muda mrefu ya askari na watumishi raia kutobalishiwa mishahara baada ya kupandishwa vyeo. 

“Nimewaagiza wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama na idara zote ndani ya Wizara hii ifikapo mwisho wa Agosti kero zote ziwe zimetatuliwa na  asiwepo askari wala raia ambaye analipwa mshahara tofauti na cheo chake au kutolipwa mashahara kabisa,”amesema. 


KUHUSU WAKIMBIZI 

Wakati huohuo Waziri Lugola amesema ametoa maagizo kwa Idara ya Huduma za Wakimbizi kuongeza kasi ya kurejesha wakimbizi wa Burundi kwani hali ya amani kwenye nchi hiyo imerejea. 

Pia ametoa maagizo kuhakikisha wakimbizi wote wasioishi kambini warejeshwe kambini mara moja. 

HITAJI LA KUFANYA KAZI SAA 24 

Pia Waziri Lugola amesema kwa suala la usalama wa raia na mali zao ni jambo muhimu kwa Watanzania ambao wanahitaji kufanya kazi saa 24 ili kuendana na azma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati. 

Amesema tayari ametoa maelekezo kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini kuwalisha mkakati wa kuimarisha usalam ili watanzania waweze kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii kwa saa 24 wakiwa na uhakika na usalama wao na mali zao. 

“Hatuwezi kupewa amri , maelekezo na ratiba za kazi zetu na wahalifu.Gari inatoka Kagera na kasha inapita Mwanza eti ikifika Morogoro inaambiwa haitakiwi kusafiri usiku kwasababu ya kufohia usalama.Hii haiwezekani.Tutakaa na wadau wa usafiri ili nao utapate maoni yao na kasha tutaamua,”amesema.

NEC YATEUA MADIWANI NANE (8)WANAWAKE WA VITI MAALUM

$
0
0

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imefanya uteuzi madiwani nane (8) wanawake wa viti maalum kujaza nafasi wazi za madiwani katika halmashauri nane (8) za Tanzania bara.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage amesema kuwa uteuzi huo umefanyika baada ya NEC kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa kuitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi uwepo wa nafasi wazi za Madiwani wanawake wa Viti Maalum

Jaji Kaijage amesema kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Tume ilipokea taarifa ya uwepo wa nafasi wazi za Madiwani wanawake wa Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kufuatia walioteuliwa awali kufariki dunia au kujiuzulu.

Amewataja madiwani hao kuwa ni Ndugu Ajira Rajabu Kalinga(CCM-Halmashauri ya Wilaya ya Songea), Ndugu Mary Kazindogo Mbilinyi (CCM-Halmashauri ya Wilaya ya Makete), Ndugu Zainab Abdi Mabrouk (CCM-Halmashauri ya Manispaa ya Kongwa).

Wengine ni Ndugu Restuta Aloyce Gardian (CCM-Halmashauri ya Wilaya ya Muleba), Ndugu Siglinda Sylvesta Ngwega (CCM-Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro), Ndugu Zena Saadi Luzwilo (CCM-Halmashauri ya Mji Kahama), Ndugu Neema Michael Massawe (CHADEMA-Halmashauri ya Wilaya ya Monduli) na Ndugu Teodola Myula Kalungwana (CHADEMA-Halmashauri ya Manispaa ya Iringa).

SAKATA LA KUPOTEA 'MBWA ASKARI'LACHUKUA SURA MPYA, WAZIRI AAGIZA UCHUNGUZI UFANYIKE, IGP SIRRO APEWA JUKUMU

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amesma wamekubaliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchin IGP Simon Sirro kuanza uchunguzi wa kina kuhusu mbwa aliyepotea.

Amefafanua mbwa aliyepotea anayo mafunzo yote ya kukamata wahalifu na anao uwezo mkubwa wa kukabiliana na matukio ya kihalifu kama askari,hivyo kupotea kwa mbwa huyo lazima uchunguzi huo ufanyike.

Lugola ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine amesema tayari IGP Sirro amemueleza kuwa ameanza uchunguzi wa mbwa huyo na kwamba ni vema mjadala wa mbwa huyo ukasitishwa ili uchunguzi ufanyike.

Amefafanua katika ziara ambayo ameifanya hizo hivi karibuni katika vyombo vya ulinzi na usalama amepata nafasi ya kwenda katika kikosi cha mbwa na farasi."Mbwa na farasi walioko kwenye kikosi hicho 
wanatengewa fedha za chakuka na malazi.Mbwa na Farasi hao wanafanya kazi mbalimbali za ulinzi,"amesema Lugola.

Ameongeza maelezo ambayo aliyapata akiwa katika kikosi cha farasi na mbwa yanatofautiana na kila makabidhiano yanapofanyika kunakuwa na tofauti ya taarifa.Amesema katika kikosi hicho mbali ya farasi mbwa walikuwa sita lakini kwa sasa wamebaki watano na mmoja haieleweki yupo wapi.

"Nimekubaliana na IGP kufanya uchunguzi wa nini kimetokea hadi mbwa akapotea.Kwa kuwa jambo hilo linakwenda kuchunguzwa ni vema likaachwa sasa lifanyiwe uchunguzi," amesema Waziri Lugola.

Kwa siku kadhaa moja ya mjadala ni habari ya kupotea kwa mbwa mwenye mafunzo yote ya kipolisi na mbwa hao nao hujukana kama polisi na baada ya kubainika kupotea Lugola alitoa maagizo ya kutafutwa mbwa huyo.

PROF MBARAWA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI DAWASA

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange akizungumza baada ya bodi ya Wakurugenzi kuzinduliwa leo Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof Kitila Mkumbo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi  Jeneral Mstaafu Davis Mwamunyange, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ali Hapi na wajumbe wa bodi wakiwa katika picha ya pamoja.
 WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, ProfesaMakame Mbarawa, akikabidhi vitendea kazi kwa mmoja wa wajumbe wa bodi ya DAWASA,katika uzinduzi wa bodihiyo, Dar es Salaam, leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, ProfesaMakame Mbarawa, akizungumza wageni waliofika wakati wa uzinduzi wa bodi ya wakurugenzi ya DAWASA pamoja na kuwapatia vitendea kazi kwa kila mmoja wa wajumbe wa bodi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

*Awataka wasikae ofisi wawe wabunifu
*awaambia DAWASCO wasiridhike na mapato waongeze idadi ya watumiaji maji.

WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Prof Makame Mbarawa amezindua bodi ya wakurugenzi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji taka (DAWASA) iliyo chini ya Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli Julai 07 mwaka huu.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji amezindua bodi hiyo baada ya kukamilisha uteuzi wa wajumbe tisa wanaokamilisha Bodi ya DAWASA.

Akizungumza wakati wa kuzindua bodi hiyo, Prof Mbarawa amesema kuwa ana imani na bodi iliyoteuliwa kuwa itafanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuleta maslahi mapana kwa wananchi .

Prof Mbarawa amesema anahitaji taasisi kama DAWASA kuwa wabunifu na kuweza kufanikisha upatikanaji wa wateja wapya ili huduma za maji ziwafikie watu wote pamoja na kuongeza pato la nchi.

Amesema kuwa, bodi hii wanaamini watasimamia vizuri utendaji wa kazi wa mamlaka hizi kwakuwa kumekuwa na upotevu mkubwa wa maji na hilo linasababishwa na baadhi ya viwanda kuiba maji na kuitia hasara serikali.

" katika viwanda vya bia asilimia 75 ya uzalishaji maji ndiyo yanatumika ila kumekuwa na upotevu mkubwa  sana wa maji na pia kuna kiwanda sitakiweka wazi ambao kwa mwezi wanatumia lita Milioni 60 za maji ambazo ni Milioni 2 kwa siku lakini ukija katika malipo yao wanasema wanatumia Lita Milioni 17,"amesema Prof Mbarawa.

Ameeleza kuwa DAWASCO ambao ndiyo wasimamizi wa maji wamekuwa hawafanyi kazi zao inavyotakiwa kwa kutokuwafuata wateja kitu ambacho kinapunguza ufanisi wao wa kazi na kumtaka Afisa Mtendaji Mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja kubadilika na kuacha kukaa ofisini bali anatakiwa awafuate wateja na kufahamu mahitaji yao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Prof Kitila Mkumbo amesema kuaa mahitaji ya maji katika jiji la Dar es Salaam ni makubwa sana na kumekuwa hakuna upigaji wa hatua kwenye suala la upatikanaji wa maji.

Amesema kuwa hilo linatokana na mamlaka husika za maji kuridhika na mapato wanayoyapata kila mwezi katika ukusanyaji wa ankara ila ila kwa upande wa serikali wamekuwa wana malengo mengine zaidi.

" Mamlaka husika zimekuwa zinaridhika na mapato wanayoyapata hususani kutoka kwenye viwanda kama TBL na SBL ila sisi kama serikali ni kuona idadi ya watuw wangapi wameunganishwa na huduma za maji safi,"amesema Prof Mkumbo.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Bodi Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange amesema kuwa atafuata agizo la waziri na hawataishia katika makaratasi na watapambana kuhakikisha wanaiweka DAWASA katika sura mpya, pia kazi hiyo siyo ndogo bali kuna mengi yanahitajika kufanywa.

Bodi ya DAWASA inaongozwa na Jenerali Mstaafu akisaidiwa na wajumbe Mhandisi Nadhifa Kemikimba, Edward Mhede, Spora Liana,Dkt Fred Msemwa, Zuber Samataba, Mhandisi Gaudence Aksante,Rosemary Kasongo na Latson Msongole.

CCM YAKABIDHI GARI LA KUBEBA WAGONJWA KWA WANANCHI LENG'ATA

$
0
0
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimekabidhi gari la kubeba wagonjwa katika Kata ya Leng'ata wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Kukabidhiwa kwa gari hiyo ni moja ya mkakati wa CCM wa kuendelea kutekeleza ahadi ya kuboresha na kusogeza huduam za afya karibu na wananchi kwa kufanikisha kupatikana kwa gari hiyo.

Gari hiyo imekebidhiwa jana katika kituo cha afya cha Kagongo ambapo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole ndio aliyekabidhi kwa niaba ya Rais John Magufuli ambaye ndiye aliyetoa gari hilo baada ya kupokea kilio cha wananchi kupitia Mbunge wa Jimbo la Mwanga Proesa Jumanne Maghembe

Akizungumza baada ya kukabidhi gari Polepole amesema Rais Magufuli anawapenda wananchi wote bila kubagua vyama vyao."Na CCM nayo inahimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015 mpaka 2020 hata katika maeneo yanayoongozwa na upinzani ndio maana gari la kubebea wagonjwa limetolewa katika Kata yenye Diwani wa upinzani ili kuendeleza dhana ya CCM kuwa maendeleo yanayotolewa na Serikali ya CCM hayana chama,"amesema.

Wakati uo huo Polepole ametolea ufafanuzi wa masuala, changamoto na fursa za Serikali ya CCM kwa wananchi wa Wilaya ya Mwanga.Baadhi ya changamoto hizo ni upatikanaji wa mtandao wa simu, ambapo amesema Chama kimeahidi kufuatilia na kupatikana kwa mtandao wa simu katika maeneo ambayo yanayo changamoto hiyo ya mtandao wa simu ikiwepo Kata ya Lang’ata.

Katika masuala ya uvuvi katika Bwawa la Nyumba ya Mungu Polepole amesema napo Chama kimekemea vitendo vya baadhi ya kuwanyanyasa wananchi, kupokea rushwa na kutosimamia haki katika kudhibiti uvuvi haramu.

"Chama pia kimewataka wananchi nao kufuata utaratibu na kutii sheria katika matumizi ya Bwawa hilo kwa faida yao na vizazi vyao,"amefafanua Polepole.Aidha ameielekeza Halmashauri ya Mwanga kujenga maeneo maalumu ya kupokelea samaki ambapo Serikali itapata mapato na wananchi watafaida kibiashara na kiuchumi, Halmashauri itoe mikopo ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake na itumie ulinzi shirikishi katika kukabiliana na uvuvi haramu katika Bwawa la nyumba ya Mungu.

Polepole amesema Chama chao kinahimiza haki na usawa,hivyo Halmashauri haiwezei utaka kukusanya fedha kwa wananchi bila kuweka fedha."Jengeni maeneo maalumu ya kupokelea samaki, mtapata mapato, mtawawezesha wananchi kiuchumi na kibiashara na wekeni utaratibu mzuri wa ulinzi shirikishi katika kupambana na uvuvi haramu kwenye Bwawa la nyumba ya Mungu," amesema Polepole

Polepole yupo katika ziara za kukagua na kufuatilia utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM.

TTCL INAKULETEA FURSA

Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images