Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

WAHASIBU WATATU SHIRIKA LA MAWASILIANO WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA TUHUMA ZA WIZI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Wahasibu watatu wa shirika la Mawasiliano Tanzania, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za wizi wakiwa watumishi na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya sh milioni 57

Akisoma hati ya mashtaka, wakili wa serikali Mwandamizi, Patrick Mwita, amewataja washtakiwa hao kuwa ni, Mercy Semwenda (49) Flora Bwahawa (54) na Hawa Tabuyanja(54).

Mbele Hakimu Mkazi, Augustine Rwizile imedaiwa, mshtakiwa Semwenda peke yake anadaiwa, kati ya Januari Mosi mwaka 2017 na Septemba 21 mwaka 2017 jijini Dar es Salaam, aliiba vocha za muda wa maongezi za TTCl zenye thamani ya sh 44,393,000/ pamoja na fedha za mauzo ya Vocha zenye thamani ya sh milioni 5,914000/

Imedaiwa kuwa, mshtakiwa alifanya uwizi huo kutokana na kamba alikuwa mfanyakazi wa TTCL kama Mhasibu.Katika shtaka la pili imedaiwa, siku na mahali hapo, washtakiwa wote, waliisababishia Shirika la Mawasiliano Tanzaniq, (TTCL), hasara ya sh. Milioni 57,773,122.

Hata hivyo, washtakiwa hao hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kwa kuwa mahakamani hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi hadi Mahakamani kuu au kwa kupata kibali kutoka kwa DPP

Kufuatia hivyo, kesi imeahirishwa hadi Julai 24.2018 kwa ajili ya kuja kutajwa, kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika, watuhumiwa wote wamerudishwa rumande.

Wakili anayewatetea washtakiwa hao amedai, ingawa mashtaka dhidi ya washtakiwa hao yanadhamana lakini wameshtakiwa kwa sheria ya uhujumu uchumi, basi atafuata taratibu zote za kisheria kuomba dhaman Mahakama kuu.

MKUTANO WA MAREJESHO WA MAAMUZI NA MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU WA 71 WA AFYA ULIMWENGUNI YAFANA ZANZIBAR

$
0
0
Na Mwashungi Tahir
NAIBU  Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman  alisema  matarajio ya kuwapatia  wananchi huduma zilizo bora za afya  popote walipo ndio dhamira kuu ya Wizara zote za afya za Tanzania Bara na Zanzibar.

Hayo aliyasema  leo huko katika  ukumbi wa  Ngalawa Beach Resort wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mrejesho wa maamuzi  na maazimio ya mkutano  mkuu wa 71 wa Afya Ulimwenguni  .

Alisema Huduma za afya zinahitajika  kuwafikia wananchi  hivyo ili kufikia jitihada hizi Serikali zetu mbili hizi zimepiga hatua kubwa kuhakikisha kila sehemu zinawafikia walengwa bila matatizo yeyote na kwa urahisi.

Aidha alisema baada ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 nchi yetu imekuwa ikichukuwa kila jitihada ili kufikia malengo yaliyotarajiwa , hivyo nchi yetu imekuwa ni moja kati ya nchi chache Barani Afrika , zenye mtandao mzuri wa miundo mbinu ya Afya.

Amewahakikishia wananchi kuwa sasa huduma za Afya   za msingi zinapatikana katika masafa  yasiozidi kilomita nne hadi tano  hili ni jambo jema na tunapaswa kujipongeza.
 Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Harus Said Suleiman akifungua Mkutano wa Marejesho wa Maamuzi na maazimio ya Mkutano Mkuu wa (71) wa Afya Ulimwenguni katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngalawa Mjini Zanzibar.
 Mwakilishi wa Shirika la Afya Ulimwenguni Tanzania (WHO) Dkt. Adiele Onyeze akizungumza katika Mkutano wa Marejesho wa Maamuzi na Maazimio ya Mkutano Mkuu wa (71) wa Afya Ulimwenguni katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngalawa Mjini Zanzibar.
 Naibu Waziri wa Afya Tanzania faustine Ndugulile, akionesha kipeperushi cha  Mpango kazi kilichoandaliwa na Wizara ya Afya Tanzania katika Mkutano wa Marejesho wa Maamuzi na Maazimio ya Mkutano Mkuu wa (71) wa Afya Ulimwenguni katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngalawa Mjini Zanzibar.
  Baadhi ya Washiriki wa Mkutano wa Marejesho wa Maamuzi na Maazimio ya Mkutano Mkuu wa (71) wa Afya Ulimwenguni katika Ukumbi wa Hoteli ya Ngalawa Mjini Zanzibar.
Picha ya pamoja.Picha na Abdalla Omar  Maelezo - Zanzibar.


WANANCHI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA VIKUNDI VYA ULINZI SHIRIKISHI

$
0
0
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi akimpa kitambulisho mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Polisi Jamii wa Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini Arusha.
Meya wa Jiji la Arusha Bw. Kalist Lazaro akiongea na wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kabla Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha kufunga rasmi mafunzo ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi pamoja na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na askari wa kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kilichopo jijini Arusha. (Picha na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha).

Na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha

Wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini hapa, wametakiwa kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao na kikundi cha ulinzi shirikishi ili kuweza kuimarisha usalama katika eneo lao.

Wito huo ulitolewa jana jioni na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi wakati alipokuwa anafunga mafunzo ya wiki mbili ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo pamoja na kuwapa vitambulisho askari 16 waliopewa mafunzo hayo.

Kamanda Ng’anzi alisema mbali na askari wa kikundi hicho kufanya doria katika eneo hilo pia watahitaji kupata taarifa za uhalifu toka kwa wananchi ili waweze kubaini maeneo korofi ambapo kama zitakuwa juu ya uwezo wao watashirikiana na Jeshi la Polisi.

Aidha aliwataka askari hao kufanya kazi kwa kufuata taratibu kama jinsi walivyoelekezwa katika mafunzo yao na kutomuonea mtu yoyote hali ambayo itasidia kuimarisha mahusiano bora baina yao na wananchi.

Hata hivyoKamanda Ng’anzi  aliwataka wananchi hao nao pia wawe mstari wa mbele katika jukumu la ulinzi badala ya kutegemea baadhi ya vyombo vya ulinzi pekee kwani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewapa dhamana.

Naye Meya wa jiji la Arusha ambaye pia ni Diwani wa kata ya Sokoni One Bw. Kalist Lazaro aliahidi kuendeleza ushirikiano kati ya halmashauri ya jiji na Jeshi hilo katika masuala ya usalama.

Alisema askari wa Jeshi la Polisi hawawezi kuenea kila mtaa bali wananchi wanatakiwa watoe michango yao kwa kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi kama wa mtaa wa Kanisani walivyofanya na kuongeza kwamba endapo kila mtaa utaanzisha vikundi hivi basi hali ya usalama jijini hapa itazidi kuimarika zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Polisi Jamii mkoa wa Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Edith Makweli alisema kwamba, mpaka hivi sasa mkoa wa Arusha una jumla ya vikundi vya Ulinzi Shirikishi 147 ambavyo vimeweza kushirikiana na Jeshi la Polisi na kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa ambapo mwaka 2016 uhalifu ulipungua kwa asilimia 6.8 na mwaka 2017 uhalifu ulipungua kwa asilimia 17.9 ikilinganishwa na mwaka 2016.

Uwepo wa kikundi hicho chenye zaidi ya miaka 11 katika mtaa huo umeleta amani kwa wakazi hao kwani awali matukio ya uhalifu yalikuwa yanatokea mara kwa mara katika barabara kuu ya mtaa huo tofauti na sasa hali iliyomlazimu Paroko Reginald Kimati wa Kanisa ya Parokia ya Vicent Paroti apendekeze iitwe Amani road.

WANANCHI WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA VIKUNDI VYA ULINZI SHIRIKISHI

$
0
0
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi akimpa kitambulisho mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Polisi Jamii wa Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini Arusha.
Meya wa Jiji la Arusha Bw. Kalist Lazaro akiongea na wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kabla Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha kufunga rasmi mafunzo ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi pamoja na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na askari wa kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kilichopo jijini Arusha. (Picha na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha).

Na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha

Wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini hapa, wametakiwa kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao na kikundi cha ulinzi shirikishi ili kuweza kuimarisha usalama katika eneo lao.

Wito huo ulitolewa jana jioni na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi wakati alipokuwa anafunga mafunzo ya wiki mbili ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo pamoja na kuwapa vitambulisho askari 16 waliopewa mafunzo hayo.

Kamanda Ng’anzi alisema mbali na askari wa kikundi hicho kufanya doria katika eneo hilo pia watahitaji kupata taarifa za uhalifu toka kwa wananchi ili waweze kubaini maeneo korofi ambapo kama zitakuwa juu ya uwezo wao watashirikiana na Jeshi la Polisi.

Aidha aliwataka askari hao kufanya kazi kwa kufuata taratibu kama jinsi walivyoelekezwa katika mafunzo yao na kutomuonea mtu yoyote hali ambayo itasidia kuimarisha mahusiano bora baina yao na wananchi.

Hata hivyoKamanda Ng’anzi  aliwataka wananchi hao nao pia wawe mstari wa mbele katika jukumu la ulinzi badala ya kutegemea baadhi ya vyombo vya ulinzi pekee kwani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewapa dhamana.

Naye Meya wa jiji la Arusha ambaye pia ni Diwani wa kata ya Sokoni One Bw. Kalist Lazaro aliahidi kuendeleza ushirikiano kati ya halmashauri ya jiji na Jeshi hilo katika masuala ya usalama.

Alisema askari wa Jeshi la Polisi hawawezi kuenea kila mtaa bali wananchi wanatakiwa watoe michango yao kwa kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi kama wa mtaa wa Kanisani walivyofanya na kuongeza kwamba endapo kila mtaa utaanzisha vikundi hivi basi hali ya usalama jijini hapa itazidi kuimarika zaidi.

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha Polisi Jamii mkoa wa Arusha Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Edith Makweli alisema kwamba, mpaka hivi sasa mkoa wa Arusha una jumla ya vikundi vya Ulinzi Shirikishi 147 ambavyo vimeweza kushirikiana na Jeshi la Polisi na kupunguza uhalifu kwa kiasi kikubwa ambapo mwaka 2016 uhalifu ulipungua kwa asilimia 6.8 na mwaka 2017 uhalifu ulipungua kwa asilimia 17.9 ikilinganishwa na mwaka 2016.

Uwepo wa kikundi hicho chenye zaidi ya miaka 11 katika mtaa huo umeleta amani kwa wakazi hao kwani awali matukio ya uhalifu yalikuwa yanatokea mara kwa mara katika barabara kuu ya mtaa huo tofauti na sasa hali iliyomlazimu Paroko Reginald Kimati wa Kanisa ya Parokia ya Vicent Paroti apendekeze iitwe Amani road.

Uhusiano kati ya sekta ya usafiri wa Anga na Utalii

$
0
0

Na Jumia Travel Tanzania

Kuna uhusiano mkubwa baina ya usafiri wa anga na utalii wa kimataifa. Usafiri wa anga ni nyenzo muhimu katika mchakato wa sasa wa dunia ya utandawazi ambapo mataifa mbalimbali hutegemeana.
Mchango mkubwa katika ukuaji wa idadi ya watalii wa kimataifa unatakiwa kuonyeshwa na nchi husika, hususani kwenye maendeleo ya sekta ya anga ambayo inaweza kuongeza nguvu ya uchumi na maeneo mengi zaidi.

Lazima tukubali kwamba zaidi ya nusu ya watalii wote duniani hutumia usafiri wa anga kama njia yao kuu ya usafiri. Hii ni sawa na kusema kwamba utalii kwa namna moja ama nyingine unategemea kwa kiasi kikubwa njia tofauti za usafiri.

Hivi karibuni serikali ya Tanzania imepokea ndege mpya aina ya Boeing 787-8 Dreamliner. Ndege hiyo ni ya 4 kununuliwa na serikali ikiwa ni jitihada za kuliimarisha Shirika la Ndege la Taifa (ATCL). Ndege hii ya kisasa kabisa ina uwezo wa kubeba abiria takribani 262 ukilinganisha na uwezo wa ndege aina ya Bomberdier Q400 wa kubeba abiria 132. Hii itasaidia kubeba abiria wengi zaidi kwa wakati mmoja pamoja na kutanua huduma zake katika mikoa mbalimbali nchini.
Tangu kufanyika jitihada za kufufua usafiri wa anga Tanzania, ATCL imeongeza kiwango cha kusafirisha abiria kutoka 4,000 mpaka 21,000 kwa mwezi na kuvifikia vituo 12. Takwimu hizi ni ishara nzuri kwa ukuaji wa shughuli tofauti za kiuchumi ikiwemo sekta ya utalii ambayo huingizia taifa fedha nyingi za kigeni.

Tanzania imejaaliwa kuwa na vivutio vingi vya kitalii katika maeneo mbalimbali ambavyo kwa miaka mingi suala la kufikika kwa urahisi limekuwa ni changamoto. Lakini kwa jitihada hizi za serikali katika kuboresha usafiri wa ndege ambao ndiyo njia salama zaidi ya usafiri duniani, sehemu nyingi zitaweza kufikika kwa urahisi.

Mataifa tofauti duniani yanayotegemea sekta ya utalii katika uchumi wake yamewekeza kwa kiasi kikubwa katika usafiri wa anga. Kwa mfano, mnamo Agosti 2017 Rais wa Rwanda, Paul Kagame aliweka jiwe la msingi la uzinduzi wa kitovu kipya cha usafirishaji, uwanja wa ndege wa kimataifa wa Bugesera. Kikiwa kinatarajiwa kukamilika mwaka 2019, uwanja huo utaweza kuwahudumia abiria takribani milioni 1.8 kwa mwaka. Hatua hii itawaongeza fursa kubwa katika sekta ya utalii ya Rwanda.

Nini kifanyike ili kuboresha sekta ya usafiri wa anga?
Yapo mambo kadhaa ya kufanya ili kuufanya usafiri wa ndege ustawi nchini kama vile: Kuendeleza sekta nzima kwa ujumla ili kukuza fursa kwa wataalamu na ajira; kuboresho ubora wa huduma; kuongeza kiwango cha ulinzi; upanuzi na maboresho ya kisasa ya viwanja vya ndege ili kuendana na uhitaji wa sasa; endapo yote haya yakifanyika yatasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la ajira kwa kuongezeka kwa ajira katika makumpuni mbalimbali kwenye sekta ya anga.

Usafiri wa anga unaweza kuwa ndiyo njia pekee ya usafiri katika maeneo yasiyofikika kwa urahisi, hivyo kukuza muunganiko wa jamii kwa ujumla. Lakini pia hutoa mtandao pekee wa usafiri kwa kuyaunganisha mataifa mbalimbali, na kuufanya kuwa muhimu kwa biashara na utalii duniani. Una nafasi kubwa ya kuwezesha ukuaji wa uchumi, hususani katika nchi zinazoendelea.  

RAIS DKT MAGUFULI ATEUA KAMISHNA JENERALI MPYA WA MAGEREZA

Waziri wa Afya azindua mradi wa TUWATUMIE Itilima mkoani Simiyu

$
0
0
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu amezindua rasmi mradi wa TUWATUMIE unaotekelezwa katika wilaya za Itilima mkoani Simiyu na Misungwi mkoani Mwanza. 

 Uzinduzi wa mradi huo unaotekelezwa na shirika la Amref Health Africa Tanzania pamoja na taasisi ya Benjamin Mkapa umefanyika katika wilaya ya Itilima, ukilenga kuboresha huduma za afya hususani huduma za uzazi ili kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano. 

 Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Waziri Mwalimu amesema serikali itaendelea kuboresha huduma za afya ikiwemo kuongeza watumishi wa afya pamoja na kuwatumia wahudumu wa afya ngazi ya jamii ili wasaidia kutoa huduma za afya kwa wananchi. Naye Mkuu wa Miradi kutoka shirika la Amref Health Africa Tanzania, Dkt.Aisa Muya amesema utekelezaji wa mradi wa TUWATUMIE unaofadhiliwa na serikali ya Ireland kupitia shirika la Irish Aid, ulianza mwezi Disemba 2017 na unatarajiwa kufikia tamati mwezi Juni mwaka 2020 ambapo ametoa rai kwa serikali kuandaa mwongozo utakaowaajiri wasaidizi hao wa afya ngazi ya jamii baada ya kipindi cha mwaka mmoja ambacho shirika hilo litakuwa likiwalipa mishahara kukamilika.

 Amesema mradi huo ulibuniwa na shirika la Amref Health Africa Tanzania kwa kushirikiana na taasisi ya Benjamin Mkapa pamoja na Wizara ya Afya kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma (Health Promotion Unit) lengo likiwa ni kuajiri watumishi wapatao 215 wilaya za Itilima na Misungwi (Itilima wahudumu 102 na Misungwi wahudumu 113) ili wasaidie utoaji huduma za awali kwa wananchi. 

 “Asilimia 50 ya miradi yetu inatumia watoa huduma za afya ngazi ya jamii ambapo kwa mwaka huu tayari wahudumu 2,265 wamepatiwa mafunzo na majukumu yao makubwa yanaanza kwa kuwahamasisha wananchi kuzingatia usafi wa mazingira, utumiaji wa maji safi na salama, kuzuia ukatili wa kijinsia, kutoa elimu ya lishe bora, kutambua viashiria vya magonjwa hatarishi kwa akina mama”. 

Amesema Dr.Muya. Nao baadhi ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii wilayani Itilima wamesema wako tayari kufanya kazi kwa bidii na weledi hususani kuwahamasisha wananchi kuhudhuria kliniki, kujifungulia katika vituo vya afya ili lengo la kupunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano liweze kutimia.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto akiongea na Wananchi wa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu wakati wa ufunguzi wa mradi wa Tuwatumie ambao unawaajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii katika vijiji vyote vya halmashauri hiyo chini ya ufadhili wa AMREF
Waziri Ummy Mwalimu akifungua mradi huo
Wadau mbalimbali wa sekta ya afya walifuatilia hotuba ya mgeni rasmi(hayupo pichani) aliyekaa kushoto ni Niall Morris Mkuu wa Arish Aid,Dar.Aisa Muya -Kaimu Mkurugenzi Mkazi Amref Tanzania(katikati) na kulia ni Dkt.Helen Senkoro Mkurugenzi wa Benjamin Mkapa Foundation
wananchi waliojitokeza kushuhudia ufunguzi wa mradi huo ambapo watoa huduma hao watakua kiungo kati ya wananchi na vituo vya kutolea huduma

KAMISHNA MKUU WA TRA ATEMBELEA WAFANYABIASHARA JIJINI DODOMA

$
0
0
*TRA yawataka wafanyabiashara wenye changamoto za kikodi kufika ofisini

NA RACHEL MKUNDAI, DODOMA

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere, amewataka wafanyabiashara wote nchini ambao wanakutana na changamoto za kikodi kuwasiliana na ofisi za TRA zilizo karibu nao ili ziweze kupatiwa ufumbuzi wa haraka.

Kamishna Kichere ameyasema hayo alipotembelea kiwanda wa DI&PC kinachotengeneza vinywaji kilichopo jijini Dodoma na kuongeza kuwa TRA ipo tayari kusikiliza changamoto zozote za kikodi kutoka kwa wafanyabiashara na itazifanyia kazi kwa kushirikiana na wafanyabiashara hao ili kuhakikisha kuwa serikali inapata mapato na wafanyabiashara wanalipa kodi zao kwa wakati. 

“Wafanyabiashara wale wenye changamoto za kikodi waje, tukae tuongee nao, na tuone namna ya kuzishughulikia na wafanyabiashara walipe kodi kwa wakati, tusonge mbele”, ameongeza Kamishna Mkuu wa TRA”, amesema Kamisha Kichere

Naye mmoja wa wakurugenzi wa kiwanda hicho Katherine Mwimbe, amesema ujio wa Kamishna Mkuu wa TRA katika kiwanda hicho umeleta faraja kwao kwa sababu wamepata fursa ya kuwasilisha kwake moja kwa moja changamoto za kikodi walizokuwa nazo na Kamishna amewahakikishia kuzifanyia kazi haraka.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akiwa katika kikao na uongozi wa Kiwanda cha kutengeneza vinywaji visivyo na kilevi cha DI & PC kilichopo Jijini Dodoma, wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kiwandani hapo kusikiliza changamoto zinazowakumba Wafanyabiashara.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akizungumza na mmoja wa Wakurugenzi wa Kiwanda cha kutengeneza vinywaji visivyo na kilevi cha DI & PC kilichopo Jijini Dodoma, Bibi. Catherine Mwimbe wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kiwandani hapo kusikiliza changamoto zinazowakumba Wafanyabiashara.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kushoto) akizungumza na Wakurugenzi wa Kiwanda cha kutengeneza vinywaji visivyo na kilevi cha DI & PC kilichopo Jijini Dodoma mara alipokamilisha ziara yake ya kikazi kiwandani hapo kusikiliza changamoto zinazowakumba Wafanyabiashara.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akiwa pamoja na viongozi wengine wa TRA wakitazama shamba la mizabibu ambalo ni mali ya Kiwanda cha kutengeneza vinywaji visivyo na kilevi cha DI & PC kilichopo Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kikazi kiwandani hapo kusikiliza changamoto zinazowakumba Wafanyabiashara.
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles Kichere (kulia) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kutengeneza vinywaji visivyo na kilevi cha DI & PC kilichopo Jijini Dodoma, Bibi. Catherine Mwimbe wakitazama miundimbinu ya kiwandani hapo wakati wa ziara yake ya kikazi kusikiliza changamoto zinazowakumba Wafanyabiashara.



KAIMU MTENDAJI KATA YA KENYAMANYORI ASIMAMISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA UPOTEVU WA FEDHA, MIFUKO YA SARUJI 39

$
0
0
Na Frankius Cleophace,Tarime

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara Elias Ntiruhungwa amemsimamisha kazi Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kenyamanyori  Laurent Marwa kwa upotevu wa fedha za Serikali pamoja na mifuko 39 ya saruji ambayo ilipaswa kujenga vyumba viwili katika Shule ya Sekondari Kenyamanyori.

Akizungumza leo, Mkurugenzi huyo amesema kuwa Kaimu huyo alienda kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkende na kusaini na kisha kukabidhiwa mifuko ya saruji huku akisubiliwa na wananchi waendelee na ujenzi katika Shule ya Sekondari Kenyamonyori.

Amefafanua lakini alitokemea kusikojulikna na mifuko hiyo.Pia  alipotea tena na sh.80,000 zilizochangwa katika mkutano wa hadhara na Diwani wa kata hiyo kwa ajili ya kuunga mkono wananchi katika ujenzi huo.Pia Mkurugenzi ameongeza kuwa viongozi wa Serikali ya kijiji walikaa na kupitisha mitasari ili Mtendaji huyo aweze kuchukua fedha benki Sh.590,000 lakini mpaka sasa hazijulikani fedha hizo zilipo baada ya kuzitoa benki.

Hivyo ameamua kumsimamisha kazi na kudai lazima afikishwe Polisi na baadae kufikishwa mahakamani ili  ajibu mashitaka yanayomkabili.“Nilimuita ofisini kwangu nikampa saa mbili ili arejeshe vitu hivyo mfano mifuko ya saruji na fedha hizo  lakini mpaka sasa hajarejesha chochote.Nimeamua kumsimamisha kazi na huyo akuna haja ya kuunda tume lazima kesho afikishwe Polisi na kufikishwa Mahakamani mara moja,"amesema Elias.

Mkurugenzi amesema kuwa nia ya Serikali ni kuweka mazingira bora ya wanafunzi ili wasome lakini baaadhi ya viongozi wasiokuwa na maadili wanazidi kufanya hujuma jambo ambalo hawatalifumbia macho.

Ameongeza watachukua hatua kali kwa wale wote ambao wanakiuka maadili.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Elias Ntiruhungwa akiongea na Vyombo vya habari ofisini kwake ambapo amesimamisha kazi Kaimu Afisa Mtendaji wa kata ya Kenyamanyori kwa sababu za ubadhilifu wa fedha za Serikali pamoja na Mifuko 39 ya saruji.

MWENGE WA UHURU UNATARAJIA KUPITIA MIRADI 67 YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BIL.162.440 MKOANI PWANI

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA

MKUU wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo amepokea mwenge wa uhuru ,ukitokea jijini Dar es salaam ,ambapo ukiwa mkoani hapo unatarajiwa kupitia miradi ya maendeleo 67 yenye thamani ya sh.bilioni 162.440.8 .

Kati ya miradi hiyo ,16 itawekwa mawe ya msingi ,miradi 13 itazinduliwa ,nane itafunguliwa na 21 itakaguliwa.Akikabidhiwa mwenge huo ,wilayani Mkuranga Ndikilo alisema ,mwenge wa uhuru ukiwa mkoani humo, pia utapitia wilaya 7 na halmashauri 9#.

Alisema mwenge wa uhuru utapokea taarifa ya miradi 9 katika maeneo mbalimbali ya mkoa na wamehakikisha miradi yote itakuwa na thamani ya fedha ili wasiangukie kwenye mtego ambao uliwakumba mkoa wa Dar es salaam.

Alieleza ,miradi hiyo imetekelezwa kwa ushirikiano baina ya wananchi,serikali kuu,halmashauri na wahisani wa kitaifa na kimataifa." Kaulimbiu ya mbio za mwenge kwa mwaka huu ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa letu.’

"Katika kutekeleza ujumbe huo tumejipanga kutekeleza kwa vitendo ambapo kwenye elimu tumevuka lengo kwa kuandikisha watoto wa darasa la kwanza." alisema Ndikilo.Mkuu huyo wa mkoa alieleza ,mwaka huu lengo ilikuwa 47,686 walioandikishwa ni 52,551 sawa na asilimia 110.

Ndikilo alisema ,katika upande wa viwanda wamefanya kazi nzuri kwani kwasasa wana viwanda zaidi ya 400 vikubwa ,vya kati na vidogo."Asilimia 20 ya ajira zote viwandani Pwani ni za wazawa wa mkoa na wanatarajia kufikia asilimia 50." alielezea Ndikilo.

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu Charles Kabeho, alihimiza elimu kwa watoto wote na kuwataka wazazi kuwa na mwamko wa kuwapeleka watoto shule.Mwenge huo umeanza mbio zake July 12 wilayani Mkuranga Mkoani Pwani na July 13 unatarajiwa kupokelewa wilayani Rufiji.
MKUU wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo akimpokea kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa mwaka huu ,Charles Kabeho ,wilayani Mkuranga mkoani hapo.(picha na Mwamvua Mwinyi).

KAIMU MTENDAJI KATA YA KENYAMANYORI ASIMAMISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA UPOTEVU WA FEDHA, MIFUKO YA SARUJI 39

$
0
0
Na Frankius Cleophace,Tarime

MKURUGENZI wa Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara Elias Ntiruhungwa amemsimamisha kazi Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kenyamanyori Laurent Marwa kwa upotevu wa fedha za Serikali pamoja na mifuko 39 ya saruji ambayo ilipaswa kujenga vyumba viwili katika Shule ya Sekondari Kenyamanyori.

Akizungumza leo, Mkurugenzi huyo amesema kuwa Kaimu huyo alienda kwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Nkende na kusaini na kisha kukabidhiwa mifuko ya saruji huku akisubiliwa na wananchi waendelee na ujenzi katika Shule ya Sekondari Kenyamonyori.

Amefafanua lakini alitokemea kusikojulikna na mifuko hiyo.Pia alipotea tena na sh.80,000 zilizochangwa katika mkutano wa hadhara na Diwani wa kata hiyo kwa ajili ya kuunga mkono wananchi katika ujenzi huo.Pia Mkurugenzi ameongeza kuwa viongozi wa Serikali ya kijiji walikaa na kupitisha mitasari ili Mtendaji huyo aweze kuchukua fedha benki Sh.590,000 lakini mpaka sasa hazijulikani fedha hizo zilipo baada ya kuzitoa benki.

Hivyo ameamua kumsimamisha kazi na kudai lazima afikishwe Polisi na baadae kufikishwa mahakamani ili ajibu mashitaka yanayomkabili.“Nilimuita ofisini kwangu nikampa saa mbili ili arejeshe vitu hivyo mfano mifuko ya saruji na fedha hizo lakini mpaka sasa hajarejesha chochote.Nimeamua kumsimamisha kazi na huyo akuna haja ya kuunda tume lazima kesho afikishwe Polisi na kufikishwa Mahakamani mara moja,"amesema Elias.

Mkurugenzi amesema kuwa nia ya Serikali ni kuweka mazingira bora ya wanafunzi ili wasome lakini baaadhi ya viongozi wasiokuwa na maadili wanazidi kufanya hujuma jambo ambalo hawatalifumbia macho.Ameongeza watachukua hatua kali kwa wale wote ambao wanakiuka maadili.

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Matongo Joyce Mbusi akiofafanua jinsi vikunndi vya kata ya Matongo vilivyonufaika na Mikopo katoka halmashauri ya wilaya ya Tarime Mkoani Mkoani Mara.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Matongo Yohana Maisa maarufu Kunguru akisoma baadhi ya vifungu katika ilani ya chama hicho.
Viongozi hao pamoja na kamati ya siasa kata ya Matongo wakikagua ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Mjini kati
Viongozi hao pamoja na kamati ya siasa kata ya Matongo wakikagua ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Mjini kati
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Matongo Yohana Maisa maarufu Kunguru akikagua Kompyuta zilizotolewa na Mfuko wa dhamana North Mara katika shule ya Msingi Nyabichune.

HALMASHAURI YA BUHIGWE, MBUNGE WAANDAA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

HALMASHAURI ya Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma kwa kushirikiana na ofisi ya mbunge wameandaa mafunzo kwa wajasiriamali wadogo wilayani humo.

Lengo ni kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kuongeza uelewa kwa wajasiriamali katika shughuli wanazofanya.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo jana wilayani Buhigwe, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Anosta Nyamoga amesema semina hiyo inamalengo matatu , moja ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ili kuwawezesha na kuwapa mafunzo wajasiriamali wadogo wadogo.

Pia kuongeza mapato kwa halmashauri kwakuwa wajasiriamali wakiongeza kipato hata pato la halmashauri linaongezeka kupitia ukusanyaji wa kodi na kuboresha maisha ya wananchi.

Amesema asilimia kubwa ya mapato ya Wilaya ya Buhigwe yanategemea ukusanyaji wa ushuru wa mazao na kodi kutoka kwa wajasiriamali wadogo , semina hiyo ya kuwajengea uwezo wajasiriamali na kufaungua masoko ya nje ya nchi kwa kuwajenga wananchi kutengeneza bidhaa zenye ubora na kutumia masoko ya ujirani mwema kuuza bidhaa zao na kuongeza kipato chao itasaidia uchumi kuongezeka.

Amesema kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2016/2017 walikusanya shilingi milioni 450 , na kwa mwaka wa fedha 2017/2018 wamekusanya milioni 550 na Malengo ya Wilaya hiyo ni kufikia kukusanya kiasi cha Sh bilioni moja ifikapo 2020 kutokana na Miundombinu ya biashara kuboresha na kukamilika kwa soko la ujirani mwa litakalo jengwa Manyovu, ambapo wanatarajia kukusanya zaidi ya milioni 100 kupitia soko hilo.

" Wilaya ya Buhigwe tumejipanga ipasavyo kuhakikisha Wananchi wetu wanatoka kwenye maisha waliyokuwa nayo ya kufanya biashara kwaajili ya kupata chakula kwa sasa tunataka waanze kufanya biashara kwa malengo zaidi kwakuwa fursa ni nyingi na Wananchi walikuwa hawazitumii tunaamini kupitia semina hii uchumi utaongezeka na manufaa watayaona", alisema mkurugenzi huyo.

Awali akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Brigedia Jenerali Marco Gaguti, aliwataka wafanyabiashara hao kutumia Mafunzo hayo kuongeza uwelewa na uzalishaji kwakuwa serikali imejipanga kumuwezesha kila mwananchi na Nchi kwa ujumla kufika uchumi wa kati.

Aidha amewataka kutumia fursa ya somo la Nje kwakuwa vizuizi vilivyo kuwepo vimeondolewa na serikali inamkakati wa kuifungua Wilaya hiyo na mikoa mingine kwa kuboresha miundombinu ya usafirishaji, watumie fursa hiyo kuzalisha mazao ya kutosha na kuongeza thamani mazao yao iliuchumi wao uendele zaidi.

" Wilaya yetu tunependelewa zaidi tuko mpakani mwa nchi tatu Burundi, Congo na Rwanda ninaamini wananchi wakitumia fursa hii Vizuri ninahakika uchumi wa Wananchi wetu utaongezeka na tutaifungu Wilaya ya Buhigwe ambayo ilikuwa nyuma tumeanza kwa semina hii ninaamini Wafanya biashara hawatakuwa vile walivyo watainuka zaidi", amesema Brigedia Gaguti.

Kwa upande wa Mbunge wa Manyovu Albart Obama amesema changamoto aliyokuwa akiipata kwa wawekezaji waliokuwa wakitaka kuja kuwekeza katika Wilaya hiyo ni pamoja na kukosekana kwa Umeme.

Amesema kwa sasa umeme umefika na masoko ya ujirani mwema yanajengwa anewaomba wawekezaji kuanzisha viwanda vya juisi na usindikaji kwakuwa Wilaya hiyo inayozalisha matunda mengi, kahawa pamoja na ndizi.

Obama amesema mafunzo hayo yataleta msukumo mpya kwa wananchi wa Buhigwe kutumia fursa kwa kujua namna ya kuongeza ubora na thamani ya mazao wanayo zalisha na kuinua uchumi wao kwa namna bora ya uwekezaji na kutumia masoko ya ujirani mwema kama chachu ya maendeleo kwao.

Naye Mfanyabiashara Leonardi Kataga amesema biashara ya Kahawa ndio wanayoitegemea kama wafanya biashara zao hilo likipatiwa soko na kuongezewa uthamani wanahakika zao hilo linaweza kuinua uchumi wao haraka na kuomba Serikali kuwasaidia katika zao hilo iliwaweze kuzalisha kwa Wingi.

Amesema wananchi wamefurahia na hatua ya Serikali kuwapatia mafunzo na kuongeza kuwa mafunzo hayo ni chachu kwao kuwafanya waendelee mbele.Pia wataweza kuongeza thamani katika uzalishaji na kutumia fursa zilizopo kuongeza kipato chao.
Baadhi ya Wajasiriamali Wadogo wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa ukumbini humo mapema jana,mafunzo hayo yaliandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe kwa kushirikiana na Ofisi ya Mbunge wa Manyovu .Lengo la mafunzo hayo ikiwa ni kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri na kuongeza uelewa kwa wajasiriamali katika shughuli wanazofanya.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AANZA ZIARA YA WILAYA YA KISHAPU

$
0
0


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na mtoto Witness Castory wa Shule ya Awali ya Lubaga wilayani Kishapu baada ya mtoto huyo na wenzake kuimba wimbo wa kumkaribisha Waziri Mkuu kwenye viwanja vya Jengo la Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Julai 13, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PMO 3145 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na mbunge wa Kishapu, Mhe. Suleiman Nchambi wakati alipowasili kwenye viwanja vya Ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Julai 13, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.

MWENYEKITI WA CCM RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BARAZA JIPYA LA WADHAMINI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Ikulu jijini Dar es Salaam.Kutoka kulia mstari wa kwanza ni Dkt. Haruni Kondo, Anna Abdallah(Mwenyekiti wa Baraza) na Jaji Mstaafu Mark Bomani wa kwanza kushoto. Wengine mstari wa nyuma kuanzia kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally, Christopher Gachuma, John Chiligati, Balozi Mstaafu Daniel Ole Njoolay, Pandu Kificho pamoja na Hassan Mzee wa mwisho (kushoto) mstari wa nyuma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na baadhi ya Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mmoja wa wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Hassan Mzee ambaye ni mmoja kati ya watu waliochanganya udongo wakati Tanganyika ilipoungana na Zanzibar na kuunda nchi moja ya Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kwenye kikao pamoja na Wajumbe wa Baraza jipya la wadhamini wa Chama cha Mapinduzi CCM Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF IDDI ATEMBELEA BANDA LA (NSSF) LEO

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimsikiliza Kaimu meneja Uhusiano na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF) Salim Khalfan wakati akimpa maelezo alipotembelea kwenye banda la shirika hilo katika maonesho ya Sabasaba yaliyomalizika na kufungwa leo kwenye viwanja vya (TanTrade) Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam leo katikati ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara ya Nje (TanTrade) Bw. Edwin Rutageruka na kulia ni Afsa Uhusiano na masoko Bi Angela Michael.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa (NSSF) mara baada ya kuwasili katika banda hilo leo kwa lengo la kulitembelea.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Afisa Uhusiano wa (NSSF) Bi Angela Michael wakati alipowasili katika banda hilo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea zawadi kutoka kwa Afisa Uhusiano na Masoko wa (NSSF) Bi. Angella Michael baada ya kutembelea katika banda hilo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa (NSSF) mara baada ya kutembelea banda hilo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza jambo na Afisa Uhusiano na Masoko wa (NSSF) Bi. Angella Michael wakati akitembelea katika banda hilo.

WASIFU WA KAMISHNA JENERALI MTEULE WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI

$
0
0
KAMISHNA JENERALI MTEULE WA JESHI LA MAGEREZA, 
DCP PHAUSTINE  M. KASIKE,ndc

CGP Mteule DCP Phaustine M. Kasike, Alizaliwa mwaka 1965 na alipata Elimu ya Sekondari katika Shule ya Iyunga, Mbeya Mwaka 1984 na Elimu ya Kidato cha sita alihitimu katika Shule ya Sekondari Mzumbe, Morogoro Mwaka 1987.
Alijiunga na Jeshi la Magereza katika Chuo cha Magereza Kiwira, Mbeya mwezi Mei, 1989 na kuhitimu Januari, 1990 ambapo alipata mafunzo ya awali ya uaskari Magereza.

Mwaka 1992 alipata mafunzo ya Uhusiano wa Kimataifa kwa ngazi ya Stashahada katika Chuo cha Diplomasia Tanzania, Dare s salaam.  Mwaka 1999 alitunukiwa shahada ya kwanza ya Mahusiano ya Kimataifa na Utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Mwaka 2015 alitunukiwa shahada ya Uzamili katika masuala ya Usalama na Stratejia katika Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Tanzania (NDC) Aidha, amehudhuria pia kozi inayohusu Usimamizi wa Utekelezaji wa Sheria (Law Enforcement) nchini Ghana mwaka 2006.

Katika utumishi wake ndani ya Jeshi la Magereza amepandishwa vyeo mbalimbali ikiwemo Sajini wa Magereza(1990), Sajini taji wa Magereza(1993), Mkaguzi Msaidizi wa Magereza (1996), Mkaguzi wa Magereza (2001), Mrakibu Msaidizi wa Magereza (2005), Mrakibu wa Magereza (2008), Mrakibu Mwandamizi wa Magereza (2010), Kamishna Msaidizi wa Magereza (2011), Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (2017), Naibu Kamishna wa Magereza ( 2018).

Amewahi kufanya kazi katika nafasi ya Afisa Mafunzo Msaidizi Kitengo cha Mafunzo Makao Makuu ya Magereza (1990- 1991 na 1993 – 1995), Afisa Msaidizi Kitengo cha Uhusiano wa Kimataifa Makao Makuu ya Magereza wakati huo huo Msaidizi Mkuu wa Jeshi la Magereza (1999 – 2007).

Aidha, Mwaka 2007 – 2012 alihudumu katika nafasi ya Afisa Msaidizi Kitengo cha Usalama Makao Makuu ya Magereza, Afisa Mwelekezi Mwandamizi Chuo cha Ulinzi cha Taifa, Tanzania (2013  -  2017),  Mkuu wa Kitengo cha Parole (2017) na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (2018).  

 Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano,
 Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dar es salaam.
13 Julai, 2018.

DKT TIZEBA AWAPIGA MSASA WATAFITI MARUKU-BUKOBA

$
0
0
Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akizungumza kwenye kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Maruku, Taasisi ya utafiti wa kahawa (TACRI) na Uongozi wa chuo cha mafunzo ya kilimo MARUKU katika kijiji cha Butairuka Kata ya Maruku Wilayani Bukoba vijijini, Leo 13 Julai 2018. (Picha zote Na Mathias Canal-WK)
Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba mbegu za maharege zinazofanyiwa utafiti na Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Maruku, wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika kijiji cha Butairuka Kata ya Maruku Wilayani Bukoba vijijini, Leo 13 Julai 2018.
Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba akizungumza kwenye kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Maruku, Taasisi ya utafiti wa kahawa (TACRI) na Uongozi wa chuo cha mafunzo ya kilimo MARUKU katika kijiji cha Butairuka Kata ya Maruku Wilayani Bukoba vijijini, Leo 13 Julai 2018. 
Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba mbegu za maharege zinazofanyiwa utafiti na Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Maruku, wakati akiwa katika ziara ya kikazi katika kijiji cha Butairuka Kata ya Maruku Wilayani Bukoba vijijini, Leo 13 Julai 2018.


Na Mathias Canal-WK, Bukoba-Kagera


UONGOZI wa Taasisi ya utafiti wa kilimo Tanzania (TARI) kituo cha Maruku, Taasisi ya utafiti wa kahawa (TACRI) umetakiwa kuongeza ufanisi katika utaalamu wao ili kuwanufaisha wakulima kote nchini kwani kwa sasa Benki ya Tafiti zilizopo hazijatumika ipasavyo.



Wataalamu wa utafiti wamepaswa kufanya vizuri pia katika eneo la kutangaza tafiti zao ikiwemo Kuongeza ujuzi katika Utafiti wa Mazao mbalimbali ikiwa ni pamoja na zao la kahawa ili kuongeza uwezo wa uzalishaji wa miche.


Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba ameyasema hayo wakati akizungumza kwenye kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa taasisi hizo za utafiti sambamba na uongozi wa chuo cha mafunzo ya Kilimo MARUKU katika kijiji cha Butairuka Kata ya Maruku Wilayani Bukoba vijijini.



Waziri huyo wa kilimo aliwasihi watafiti hao Kuendelea kufanya juhudi kubwa kuandika miradi mbalimbali (Reseach Proposals) kwa ajili ya kusaidia shughuli za uendelezaji wa utafiti kwani bajeti ya serikali pekee haiwezi kutosha kukamilisha kila changamoto zinazowakabili.


Alisema wataalamu hao wanapaswa kufanya tafiti kwa kuendana na matakwa ya sekta ya kilimo na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ili kuongeza tija katika uzalishaji wa Kahawa nchini sambamba na Mazao mengine.


Aliwasihi kuongeza ushirikiano ili kuendelea na utafiti kuhusu njia bora za uzalishaji mazao, urutubishaji udongo, mfumo wa usambazaji wa teknolojia, masoko yenye tija, tathmini ya uenezaji wa teknolojia na mchango wa matokeo ya utafiti katika kuboresha hali ya maisha ya wananchi na uchumi wa taifa kwa ujumla.


Alisema kuwa kituo cha utafiti wa kilimo kinapaswa kuendelea na juhudi za uzalishaji wa mbegu bora za mazao mbalimbali kama vile maharage, viazi vitamu, muhogo na mengineyo.


Kituo cha utafiti wa kilimo cha Maruku (TARI-MARUKU) ni kati ya vituo viwili vya utafiti wa kilimo katika Kanda ya ziwa ambapo makao makuu yake yapo Ukiriguru-Mwanza ambapo kinatoa mafunzo na ushauri kwa wakulima na wadau mbalimbali wa kilimo juu ya teknolojia mbalimbali za kilimo.


Katika hatua nyingine Waziri Tizeba amemuagiza Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kilimo Maruku Ndg Laurent Mathew Luhembe ndani ya mwaka mmoja kutatua changamoto ya ukosefu wa bweni la chakula.


Aliongeza kuwa chuo hicho kinapaswa kubuni mbinu mbadala za mapato ikiwa ni pamoja na kujenga kitalu nyumba (Green House) kwani itasaidia kuongeza kipato mahususi na hatimaye chuo kujiendesha badala ya kutaka changamoto zote zitatuliwe na serikali.


Aidha, Taasisi hizo za utafiti ikiwa ni pamoja na Chuo cha Maendeleo ya kilimo Maruku zimetakiwa kuhakikisha wanatunza ardhi yao ili kuondosha hofu ya uvamizi wa maeneo.

TFS NA WADAU WAANZA SAFARI YA KUTEMBELE A MSITU WA ASILI WA AMANI

$
0
0
Meneja Masoko na Uwekezaji wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),Mariam Kobelo  mapema leo asubuhi akigawa Vipeperushi kwa Wakazi wa Dar es Salaam ambao wanafanya safari ya kutembelea Msitu wa Asili wa Amani uliopo Muheza mkoani Tanga ,Safari hiyo ambayo imeratibiwa na TFS imewakutanisha wadau mbalimbali kwenda kujionea mazao ya Misitu
Baadhi ya Wadau waliopo katika safari hiyo wakipitia majarida yanayoelezea Msitu wa asili wa Amani na Vivutio vyake.
Baadhi ya Wanafunzi waliojumuika katika Safari hiyo wakisoma Makala mbalimbali zilizomo kwenye Jarida linalozungumzia Msitu wa asili wa Amani.
Baadhi ya Wadau waliopo katika safari hiyo wakipitia majarida yanayoelezea Msitu wa asili wa Amani na Vivutio vyake.
Wadau wakiw akatika basi tayari kwa ajili ya Safari kuelekea Tanga kutembelea msitu wa asili wa amani

WAZIRI MKUU AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KISHAPU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imelipa sh. bilioni 43 zikiwa ni madeni kwa watumishi wa umma na kati ya hizo sh. bilioni 16.25 zimelipwa kwa walimu.

“Hadi kufikia mwisho wa mwezi uliopita, jumla ya sh. bilioni 43 zimelipwa kwa watumishi 27,389 ambao kati yao watumishi 15,919 ni wa sekta ya elimu tu na madeni yao yanafikia sh. bilioni 16.25,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Julai 13, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga akiwa aktika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

“Mapema mwaka huu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kutoa sh. bilioni 200 za kulipa madeni ya watumishi na hadi sasa madeni ambayo yameshahakikiwa ni sh. bilioni 127 na mengine ni ya wazabuni,” amesema. 

Amesema hivi sasa Serikali inadhibiti uzalishaji wa madeni ya watumishi kwa kuzuia uhamisho kama hakuna fedha, kuzuia rufaa zisizokuwa za lazima na ambazo hazina ufuatiliaji wa waganga wakuu wa mikoa na wilaya, na kuhimiza matumizi ya Bima ya Afya kwa watumishi wa umma.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Julai 13, 2018. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack . 
 Baadhi ya Watumishi na Viongozi wa vyama vya Siasa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Julai 13, 2018. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo, Julai 13, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Rais TAMISEMI,  Joseph Kakunda na wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAKULIMA DAKAWA WANUFAIKA NA KILIMO CHA UMWAGILIAJI

$
0
0
  Mhandisi wa kanda ya Morogoro, kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Senzie Maeda, akiongea na waandishi wa habari katika skimu ya kilimo cha Umwagiliaji cha Dakawa, kilichopo katika Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro.
 Miundombinu inayopeleka maji katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji cha Dakawa iliyojengwa na Shirika la Kimataifa la misaada la Marekani (USAID) kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliji.

 Mwenyekiti Msaidizi wa cha Chama cha wakulima wa umwagiliaji Dakawa Bi.Bertha Chilosa akiongelea  Mafanikio na baadhi ya changamoto zinazowakabili wakulima katika kilimo hicho.
 Moja ya shamba la mpunga lililopo katika skimu ya kilimo cha umwagiliaji cha Dakawa mkoani, Morogoro.


Wakulima wakiweka katika magunia  mpunga uliyovunwa na kifaa maalum cha kuvunia zao hilo katika moja ya shamba lililopo katika skimu ya umwagiliaji ya Dakawa mkoani Morogoro.

Na Mwandishi Maalum - DAKAWA
Wakulima wa kilimo cha Mpunga katika skimu ya kilimo cha Umwagiliji ya Dakawa wamenufaika na kilimo hicho baada ya serikali kukarabati mindombinu ya umwagilijai ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, ofisi, ukarabati wa pump na  mifereji ya upili.
Hayo yameelezwa Mjini Dakawa na  Mhandisi wa Kanda ya Morogoro kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, Senzie Meeda, alipozungumza na waandishi wa habari  walipotembelea skimu ya umwagiliaji ya Dakawa.
Mhandisi Meeda, ameeleza kuwa Serikali kupitia shirika la kimaitaifa la misaada la Marekani USAID lmetumia takribani kiasi cha shilingi Bilioni 20, katika ujenzi wa skimu hiyo,  na mpaka sasa asilimia themanini (80%) ya kazi hiyo inaendelea vizuri na inategemea kukamilika mwezi December mwaka huu.
“Njia zote za kwenda mashambani zinapitika, maeneo ya pembezoni ambayo yalikuwa hayafikiki mwanzoni sasa yanafikika, Pump Mpya za kisasa zinazotumia umeme mdogo zimefungwa hivyo uzalishaji umeongezeka ambapo mkulima anaweza kuvuna hadi tani sita (6) kwa hekta hili limesaidia sana kuongeza kipato na kutengeneza ajira.” Alisema Mhandisi Meeda.
Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa chama cha wakulima wadogo wa umwagiliaji Dakawa Bi.  Bertha Chilosa, ametoa shukrani kwa serikali kwa niaba ya wakulima wa dakawa na kusema kuwa kilimo kimekuwa na uchumi mkubwa katika eneo hilo na kubadilisha maisha yao na kuiomba serikali kuwasaidia wakulima hao kutafuta masoko ya uhakika ili kuwe na bei ya uhakika.
“Naiomba serikali itusaidie katika jambo hili, maana kutokuwa na soko la uhakika kunasababisha madalali wanakuja hapa kununua mpunga kwa bei ya kulangua na kutasababishia sisi wakulima wadogo kupata hasara, Naiomba serikali ichukue jukumu hili, ili mkulima asinyanyasike, sambamba na hili, ninaiomba serikali iongee na Mabenki ili yaweze kutupunguzia riba katika mikopo tunayopewa.” Alisisitiza Bi. Bertha
Skimu ya kilimo cha umwagiliaji ya dakawa ambayo ipo chini ya mradi wa Irrigation and Rural  Roads, katika program ya Feed the Future ina ukubwa wa hekta 3225 ambapo hekta 2000 zina miundombinu ya umwagiliaji, hekta 1000 bado hazijaendelezwa na hekta 225 ni za makazi na huduma za kijamii.
Shamba hilo la Dakawa lilijengwa na kumilikiwa na serikali kwa kupitia NAFCO tangu mwaka 1981 hadi mwaka 2003, na mwaka 2008 katika kubinafsisha mashirika ya umma  likakabidhiwa kwa ushirika wa wakulima wadogo Dakawa.
Na imeelezwa chama cha wakulima wadogo wa kilimo cha umwagiliaji dakawa, kina jumla ya wanachama 850 ambapo 500 ni wanaume na 350 ni wanawake.

Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images