Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Property International Tanzania Leila Maingu akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari wakati akizungumza kuhusu uuzaji wa viwanja katika miradi mbalimbali hapa nchini kutoka Kampuni hiyo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Property International Tanzania Bw. Masoud Alawi akizungumza jambo na Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu katika banda la kampuni hiyo lililoko kwenye viwanja vya TANTRADE Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam ambapo maonyesho ya biashara ya Sabasaba yanaendelea Mkurugenzi wa Kampuni ya Property International Tanzania Bw. Masoud Alawi akizungumza jambo na Julius Charles ambaye yuko katika banda hilo ili kuwahamasisha watanzania kujipatia viwanja kwa bei rahisi kutoka kampuni hiyo.
Wananchi mbalimbali wakimiminika kuingia katika banda hilo.
Mmoja wa wafanyakazi akiwahudumia wananchi waliotembelea katika banda hilo.
Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu paoja na wafanyakazi wenzake wakiwahudumia wananchi mbalimbali waliofika kwenye banda hilo.
.....................................................................................
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
PROPARTY International Limited imewahimiza watumishi wa umma na hasa walimu na wauguzi katika Mkoa wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya kujipatia viwanja kwa bei nafuu.
Tayari Proparty International Limted imesema kuanzia Julai mwaka jana wameuza viwanja kwa watumishi wa kada hizo wapatao 2000 lakini imeendelea kuwahimiza kuchangamkia fursa hiyo kupitia mradi maalumu wa viwanja ambao umetengwa kwa ajili yao.
Hayo yamesemwa na Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu wakati anazungumzia kuhusu miradi mbalimbali ya viwanja ambayo wanayo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata nafasi ya kumiliki kiwanja ambacho kimepimwa na kilicho maeneo sahihi kwa makazi.
Akizungumza akiwa kwenye banda lao katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea Viwanja vya Sabasaba barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam Maingu amesema kuwa wanayo miradi mingi ya “Tunawashauri walimu na wauguzi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya unafuu wa bei ya viwanja vyetu.Watapa viwanja kwa gharama nafuu kwani kuna punguzo la bei kwa ajili yao.
“Tangu tuanze kuuza viwanja kwa ajili ya watumishi hao kwa mkoa wa Dar es Salaam muamko umekuwa mkubwa kwani wengi wamenunua.
“Hata hivyo tunaendelea kuwasisitiza walimu na wauguzi ambao bado hawajununua viwanja waje na tutazungumza nao, lengo letu ni kuona watumishi wetu wanakuwa kwenye makazi salama,”amefafanua.
Akifafanua zaidi kuwa wameingia mikataba na benki ya Amana , Tpb Bank, CRDB , PBZ na DC Bank ambapo wateja wanaonunua kiwanja kwa mkopo watalipa katika moja ya akanti za benki hizo.
“Kwa wanaonunua kiwanja kwa mkopo kupitia benk ya PBZ mteja atatakiwa kugungua akaunti na kulipa asilimia 20 ya thamani ya kiwanja na kasha benki itampa asilimia 80 na marejesho ni miaka mitano,”amesema.
Wakati kwa Amana Bank malipo ya awali ni asilimia 20 na baada ya hapo mteja atapewa asilimia 80 na marejesho yake ni mwaka mmoja au mwaka mmoja na nusu.
Pia Tpb Bank mteja baada ya kufungua akaunti na kulipa malipo ya awali ya asilimia tano ya thamani ya kiwanja na benki ndipo itampa mkopo wa asilimia 95 na marejesho hadi miaka mitatu.
Amesema kwa benki ya CRDB mteja atalipa malipo ya awali asilimia 20 ya thamani ya kiwanja na baada ya hapo benki itamuwezesha kupata asilimia 80 na marejesho ni hadi miaka mitatu.
Amewaomba Watanzania kununua viwanja kutoka kwenye moja ya miradi yao kwani gharama yake ni nafuu na kubwa zaidi maeneo yao yamepimwa na wameweka utaratibu maalumu ambao unawafanya kuwa karibu na wateja wao.
Meneja Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Property International Tanzania Leila Maingu akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari wakati akizungumza kuhusu uuzaji wa viwanja katika miradi mbalimbali hapa nchini kutoka Kampuni hiyo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Property International Tanzania Bw. Masoud Alawi akizungumza jambo na Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu katika banda la kampuni hiyo lililoko kwenye viwanja vya TANTRADE Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam ambapo maonyesho ya biashara ya Sabasaba yanaendelea Mkurugenzi wa Kampuni ya Property International Tanzania Bw. Masoud Alawi akizungumza jambo na Julius Charles ambaye yuko katika banda hilo ili kuwahamasisha watanzania kujipatia viwanja kwa bei rahisi kutoka kampuni hiyo.
Wananchi mbalimbali wakimiminika kuingia katika banda hilo.
Mmoja wa wafanyakazi akiwahudumia wananchi waliotembelea katika banda hilo.
Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu paoja na wafanyakazi wenzake wakiwahudumia wananchi mbalimbali waliofika kwenye banda hilo.
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
PROPARTY International Limited imewahimiza watumishi wa umma na hasa walimu na wauguzi katika Mkoa wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya kujipatia viwanja kwa bei nafuu.
Tayari Proparty International Limted imesema kuanzia Julai mwaka jana wameuza viwanja kwa watumishi wa kada hizo wapatao 2000 lakini imeendelea kuwahimiza kuchangamkia fursa hiyo kupitia mradi maalumu wa viwanja ambao umetengwa kwa ajili yao.
Hayo yamesemwa na Meneja Mauzo na Masoko Leila Maingu wakati anazungumzia kuhusu miradi mbalimbali ya viwanja ambayo wanayo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanapata nafasi ya kumiliki kiwanja ambacho kimepimwa na kilicho maeneo sahihi kwa makazi.
Akizungumza akiwa kwenye banda lao katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea Viwanja vya Sabasaba barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam Maingu amesema kuwa wanayo miradi mingi ya “Tunawashauri walimu na wauguzi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuchangamkia fursa ya unafuu wa bei ya viwanja vyetu.Watapa viwanja kwa gharama nafuu kwani kuna punguzo la bei kwa ajili yao.
“Tangu tuanze kuuza viwanja kwa ajili ya watumishi hao kwa mkoa wa Dar es Salaam muamko umekuwa mkubwa kwani wengi wamenunua.“Hata hivyo tunaendelea kuwasisitiza walimu na wauguzi ambao bado hawajununua viwanja waje na tutazungumza nao, lengo letu ni kuona watumishi wetu wanakuwa kwenye makazi salama,”amefafanua.Akifafanua zaidi kuwa wameingia mikataba na benki ya Amana , Tpb Bank, CRDB , PBZ na DC Bank ambapo wateja wanaonunua kiwanja kwa mkopo watalipa katika moja ya akanti za benki hizo.
“Kwa wanaonunua kiwanja kwa mkopo kupitia benk ya PBZ mteja atatakiwa kugungua akaunti na kulipa asilimia 20 ya thamani ya kiwanja na kasha benki itampa asilimia 80 na marejesho ni miaka mitano,”amesema.Wakati kwa Amana Bank malipo ya awali ni asilimia 20 na baada ya hapo mteja atapewa asilimia 80 na marejesho yake ni mwaka mmoja au mwaka mmoja na nusu.Pia Tpb Bank mteja baada ya kufungua akaunti na kulipa malipo ya awali ya asilimia tano ya thamani ya kiwanja na benki ndipo itampa mkopo wa asilimia 95 na marejesho hadi miaka mitatu.Amesema kwa benki ya CRDB mteja atalipa malipo ya awali asilimia 20 ya thamani ya kiwanja na baada ya hapo benki itamuwezesha kupata asilimia 80 na marejesho ni hadi miaka mitatu.
Amewaomba Watanzania kununua viwanja kutoka kwenye moja ya miradi yao kwani gharama yake ni nafuu na kubwa zaidi maeneo yao yamepimwa na wameweka utaratibu maalumu ambao unawafanya kuwa karibu na wateja wao.