Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

DKT TIZEBA AZINDUA MKUTANO WA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA KILIMO JIJINI DODOMA

$
0
0
Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba akizungumza wakati akifungua mkutano na kuzindua Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo kwenye ukumbi Wa Wakala Wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Mjini Dodoma, Leo 28 Juni 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, WK)
Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba (Kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe (Katikati) na Katibu wa Baraza la wafanyakazi Wizara ya kilimo Bi Agnes Hugo wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa ufunguzi wa mkutano na uzinduzi wa Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo kwenye ukumbi Wa Wakala Wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Mjini Dodoma, Leo 28 Juni 2018.
Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano na kuzindua Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo kwenye ukumbi Wa Wakala Wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Mjini Dodoma, Leo 28 Juni 2018.
Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati akifungua mkutano na kuzindua Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo kwenye ukumbi Wa Wakala Wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Mjini Dodoma, Leo 28 Juni 2018.
Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati akifungua mkutano na kuzindua Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo kwenye ukumbi Wa Wakala Wa Taifa wa hifadhi ya chakula (NFRA) Mjini Dodoma, Leo 28 Juni 2018.



Na Mathias Canal, WK-Dodoma

Waziri wa kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba leo 28 Juni 2018 amefungua mkutano na kuzindua Baraza la wafanyakazi wa wizara ya kilimo, mkutano utakaotuama kwa siku mbili kuanzia leo mpaka kesho 29 Juni 2018 katika ukumbi wa Wakala wa Taifa wa hifadhi ya Chakula (NFRA) Jijini Dodoma.

Akizungumza katika mkutano huo Dkt Tizeba aliwasisitiza wajumbe wa baraza hilo kwa umoja wao kujadili kwa muktadha wa kutatua changamoto na kuboresha sekta ya kilimo kupitia mada mbalimbali zitakazowasilishwa ikiwa ni pamoja na kuhusu elimu ya majukumu ya wajumbe wa Baraza la wafanyakazi, Elimu juu ya watumishi wa Umma na hoja kutoka vyama vya wafanyakazi sambamba na wajumbe kupitishwa katika bajeti ya wizara kwa mwaka 2018/2019.

Alisema kuwa Baraza la wafanyakazi ni chombo muhimu ambacho kimepewa nguvu kisheria ili kuwapa watumishi nafasi ya kushiriki katika maamuzi ya utekelezaji wa masuala mbalimbali yanayohusu utendaji na ufanisi wa Taasisi ili kuongeza tija mahali pa kazi hivyo wajumbe hao wanapaswa kujadili mada hizo kwa ufanisi na tija.

Alisisitiza kuwa Baraza hilo linapaswa kuzaa matokeo mazuri ikiwemo uboreshaji wa mazingira ya kazi huku akisema kuwa serikali imekuwa ikisisitiza kila taasisi ya umma kuunda mabaraza ya wafanyakazi ili kuongeza ufanisi na tija katika mchango wa mapinduzi ya uchumi wa viwanda.

Alisema, serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli inatambua ushirikiano wa pande hizo mbili katika maamuzi hivyo ni vigumu kutekeleza majukumu endapo pande moja haitashirikishwa kwani umuhimu huo umetiliwa mkazo na kupitia sera, sheria na kanuni zinazosimamia uendeshaji wa taasisi za umma.

Katika hatua nyingine Mhe tizeba aliwakumbusha wajumbe hao kuwa miongoni mwa majukumu muhimu ya sekta ya kilimo ni pamoja na kutambua kuwa katika maendeleo ya nchi asilimi 66.5 ya watanzania wanategemea sekta ya kilimo pamoja na kuhakikisha usalama wa chakula nchini hivyo ni vyema katika mkutano huo kujadili mada hizo na kuwa na mategemeo ya kuwanufaisha zaidi wakulima kote nchini.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe akizungumza kabla ya kumkaribisha waziri wa kalimo kufungua kikao hicho cha Baraza la wafanyakazi alisema kuwa Baraza hilo jipya limeundwa kufuatia Baraza la awali kufikia muda wa ukomo wake baada ya maridhiano baina ya Menejimenti ya wizara ya kilimo na vyama vya wafanyakazi vya TUGHE na RAAWU kufikiwa.

Mhandisi Mtigumwe aliongeza kuwa Mkutano wa Baraza la wafanyakazi ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya ajira na mahusiano kazini Na 6 ya mwaka 2004 na sheria ya majadiliano ya pamoja katika utumishi wa umma Na 19 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2005. Ambapo kwa mujibu wa sheria hizo lengo la kuanzishwa mabaraza ya wafanyakazi ni kuwa na chombo cha ushauri na majadiliano ya pamoja kati ya wafanyakazi na waajiri ili kuwa na ushirikishwaji mpana wa wafanyakazi mahala pa kazi.

Alisema, kufuatia mabadiliko ya muundo wa Wizara ya kilimo hususani baada ya idara ya utafiti kuwa Taasisi inayojitegemea imelazimu muundo wa Baraza hilo kufanyiwa mabadiliko na kupelekea kupungua kwa idadi ya wajumbe kutoka 98 hadi kufikia 57, Aidha, mkataba mpya wa kuunda Baraza la wafanyakazi umezingatia mabadiliko hayo.

TPW YATOA SH MILIONI 40 KWA WANAWAKE 250 WILAYANI MONDULI KUFANIKISHA UFUGAJI WA NYUKI

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Monduli Iddi Kimanta akipokea mfano wa Hundi ya zaidi ya Sh milioni 40 kutoka kwa Msimamizi wa Miradi wa Asasi ya Watu na Wanyama (TPW),Revocatus Magayane kwa ajili ya mtaji wa mradi wa ufugaji nyuki kwa wanawake 250.
Mkuu wa wilaya ya Monduli Iddi Kimanta akibadilishana mawazo na Msimamizi wa Miradi wa TPW Revocatus Magayane mara baada ya kukabidhi mradi wa ufugaji nyuki kwa wanawake 250 wa Kata ya Lemooti na Mswakini.
Mratibu wa Miradi kutoka BAWAKIMO Angela Kagashe akizungumza na baadhi ya wanawake wanachama wa baraza hilo juu ya kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo mpya wa uhifadhi mazingira na ufugaji wa nyuki wilayani Monduli.



Msimamizi wa miradi wa Asasi ya Watu na Wanyama ya (TPW), iliyopo Simanjiro mkoani Manyara akizungumza wakati wa kukabidhi mradi mpya wa uhifadhi mazingira na ufugaji nyuki kwa Baraza la Wanawake wa Kikufugaji Monduli (BAWAKIMO), Asasi hiyo imewapa Sh milioni 40 kama mtaji.
Mkurugenzi wa Baraza la Wanawake wa Kifugaji Monduli (BAWAKIMO), Mary Morindat akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa uhifadhi mazingira na ufugaji nyuki kwa wanawake wa 250 kutoka Kata ya Lemooti na Mswakini wilayani humo.

Msimamizi wa miradi wa Asasi ya Watu na Wanyama ya (TPW), iliyopo Simanjiro mkoani Manyara akizungumza wakati wa kukabidhi mradi mpya wa uhifadhi mazingira na ufugaji nyuki kwa Baraza la Wanawake wa Kikufugaji Monduli (BAWAKIMO), Asasi hiyo imewapa Sh milioni 40 kama mtaji.
Mkuu wa wilaya ya Monduli Iddi Kimanta akizungumza wakati wa ufunguzi wa mradi wa uhifadhi mazingira na ufugaji wa nyuki wilayani humo.

Na Ripota Wetu, Arusha

MAISHA ya wanawake 250 waliopo Kata ya Lemooti na Mswakini Monduli mkoani Arusha yanataraji kubadilika baada ya Asasi ya Watu na wanyama(TPW) kuwapatia Sh.milioni 40 za mradi wa uhifadhi mazingira na ufugaji nyuki.

Kupitia mradi huo wanawake hao kutoka kwenye vijiji sita vya Mswakini Juu, Mswakini chini, Lengolwa, Lemooti, Oldonyo na Naitolia watapatiwa mizinga 475 itakayofungwa kwenye maeneo ya vikundi 25 vya watu 10. Akizungumza wakati wa kukabidhi mradi huo leo, Msimamizi wa miradi Asasi ya TPW Revocatus Magayane amesema mradi huo wanautekeleza kwa ushirikiano na Baraza la Wanawake wa Kifugaji Monduli (BAWAKIMO).

Magayane amewataka wanawake hao kutoa taarifa za maendeleo ya mradi kila wakati hatua itakayowawezesha kuwa na mwanzo mzuri wa utekelezaji. Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Monduli Iddi Kimanta aliwataka wanawake hao kutoingiza siasa kwenye shughuli zinazohusiana na maendeleo kwani kufanya hivyo kutawafanya wakwame kufikia ndoto zao.

“Uchumi hauna itikadi ya kisiasa, mkiingiza siasa kwenye masuala haya mtahawanyika na kushindwa kufikia mnachokihitaji kama kuwa na maisha mazuri kusomesha watoto na kujenga nyumba bora na kisasa,” alisema Kimanta. Naye Katibu wa BAWAKIMO Nai Zakayo ameishukuru TPW kwa kuwawezesha kupata na kuanzisha mradi huo wa nyuki kwenye kata mbili za wilaya hiyo.

Aidha ameiomba TPW kuwafikia wanawake wengi zaidi kwani bado wanayo maeneo mengi katika Kata nyingine ambazo zinaweza kufanya miradi ya uhifadhi wa mazingira na ufugaji wa nyuki.

TANZANIA NI KIMBILIO KWA WALIOKOSA AMANI-MAJALIWA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipewa tuzo ya Balozi wa Amani na Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge Wapenda Amani, Dk Thomas Walsh katika hafla ya kuzindua tawi la Tanzania la Wabunge wapenda amani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, jijini Dodoma Juni 28, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia katika hafla ya kuzindua tawi la Tanzania la Wabunge wapenda amani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, jijini Dodoma Juni 28, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipeana mkono na Mbunge wa Tabora Mussa Ntimizi katika hafla ya kuzindua tawi la Tanzania la Wabunge wapenda amani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, jijini Dodoma Juni 28, 2018 katikati ni Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge Wapenda Amani, Dk Thomas Walsh. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Umoja wa Kimataifa wa Wabunge Wapenda Amani, Dk Thomas Walsh, katika hafla ya kuzindua tawi la Tanzania la Wabunge wapenda amani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa, jijini Dodoma Juni 28, 2018.



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuvumiliana na kustahamiliana ndiko kunakolifanya Taifa la Tanzania kuwa mfano wa kuigwa na kimbilio la wale waliovurugikiwa na amani katika nchi zao. 

Kadhalika, uwepo wa amani nchini si tu unatoa fursa ya kutekeleza majukumu ya kiuchumi na kijamii bila hofu bali pia ni sababu muhimu ya wenzetu wengine kutoka nje kuona fursa ya kuwekeza na kushirikiana nasi katika kujenga maendeleo ya nchini. 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Alhamisi, Juni 28, 2018) wakati akizindua Umoja wa Kimataifa wa Wabunge Wapenda Amani tawi la Tanzania (IAPP), kwenye mkutano uliyofanyika katika ukumbi wa Msekwa Bungeni, jijini Dodoma.

Amesema amani na utulivu ni tunu kubwa sana katika jamii yoyote ile Duniani na Tanzania muda wote imeendelea kuenzi tunu hiyo iliyojengwa kwenye misingi imara kupitia waasisi wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.Kadhalika, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu Shirikisho la Amani kwa Wote (Universal Peace Federation (UPF), ambalo lilianzishwa kwa lengo la kumkomboa binadamu kutoka katika udhalili wa kukosa mahitaji muhimu. 

“Hili linadhihirika kupitia mipango ya shirikisho hilo ya kushirikiana na jamii nyingine katika kuimarisha sekta zenye kugusa maisha ya watu wengi kama vile kilimo, mazingira, afya, elimu, miundombinu na nyinginezo,” amesema.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema utekelezaji wa mipango hiyo utategemea kwa kiasi kikubwa uwepo wa amani na utulivu katika jamii husika, ambapo amewahakikishia kwamba Serikali ipo tayari na itaendelea kushirikiana nao katika nyanja hizo za kijamii na maeneo mengine kwa ajili ya kulinda maslahi ya pande zote mbili na kuwaletea maendeleo wananchi.

“Nitoe rai kwa Waheshimiwa Mawaziri wa sekta husika kwamba hakikisheni mnaanzisha mazungumzo na wawakilishi wa UFP nchini kwa lengo la kuona namna nzuri ya kuchangamkia fursa zinazopatikana kupitia shirikisho hilo hususan katika sekta za kilimo, elimu, afya, mazingira na miundombinu,” amesema. 

Awali, Mwenyekiti Mwanzilishi wa IAPP, Bw. Mussa Ntimizi amesema Shirikisho la Amani kwa Wote litasaidia nchi kuboresha miradi mbalimbali ya maendeleo kama ya kilimo, afya kwa sababu hakuwezi kuwa na amani bila maendeleo.

Naye, Makamu Mwenyekiti wa umoja huo, Bw. William Ngeleja amesema Shirikisho la Amani kwa wote limetenga dola bilioni tatu kwa ajili ya kusaidia sekta ya afya katika nchi 10 za Bara la Afrika na Tanzania ikiwemo.

Katika hafla hiyo Waziri Mkuu amepewa tuzo ya Balozi wa Amani na Mwenyekiti wa Shirikisho la Amani kwa Wote (UPF), Dkt. Thomas Walsh. Viongozi wengine walipewa tuzo hiyo ni pamoja na Spika wa Bunge, Job Ndugai, Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson, Makamu Mwenyekiti wa umoja huo,Bw. William Ngeleja Katibu Msaidizi wa umoja huo Bibi Anna Lupembe, Mweka hazina Bibi Ritta Kabati.

Baada ya kukabidhi tuzo hizo, Dkt. Walsh shirikisho lao linahitaji kufanya kazi nna Serikali, sekta binafsi, asasi za kiraia kwa ajili ya kuboresha maendeleo na amani. Amesema katika Taifa kukiwa na maendeleo amani lazima itakuwepo.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson, Mwenyekiti wa Shirikisho la Amani kwa Wote (UPF), Dkt. Thomas Walsh, Katibu wa Shirikisho la Amani kwa Wote Kanda ya Afrika (UPF_Afrika), Bw. Adama Doumbia, Katibu wa Shirikisho la Amani kwa Wote Tanzania (UPF_Tanzania), Bw Stylos Simbamwene, 


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
ALHAMISI, JUNI 28, 2018.

Zimbabwe Kuendelea kuimarisha uhusiano na Tanzania

$
0
0
Na. Immaculate Makilika –MAELEZO

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Emmerson Mnangangwa amesema serikali yake itaendelea kushirikiana na kuimarisha uhusiano wake na Tanzania  ili kuimarisha uchumi wa nchi hizo mbili.

Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam leo, Rais Mnangagwa amesema kuwa Tanzania imesaidia kwa kiasi kikubwa katika harakati za ukombozi wa nchi za Zimbabwe, Afrika Kusini, Namibia na Msumbiji na hivyo ni jukumu lao kuimarisha uhusiano huo mzuri.

“Sisi kizazi cha zamani ni jukumu letu kuhakikisha kuwa tunakieleza kizazi cha sasa kuhusu jitihada za Tanzania katika harakati za ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika”

“Tulikuwa tunakuja hapa, jengo hili na Mwalimu Nyerere alikuwa Rais wakati huo, ambapo aliweza kusuluhisha migogoro iliyokuwepo kati ya chama cha ZANU na ZAPU” aliongeza Rais Mnangangwa.

Rais Mnangagwa alisema kuwa serikali yake iko tayari kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali yatakayosaidia kukuza uchumi wake na kuahidi kuwa baada ya Uchaguzi Mkuu kuisha utaotarajiwa kufanyika Julai 30 mwaka huu, Tume ya Ushirikiano itakutana kuzungumzia masuala mbalimbali ikiwemo ya kibiashara.

Kwa upande wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli alisema Tanzania na Zimbabwe ni nchi marafiki tangu harakati za uhuru mwaka 1960.Ambapo mwaka 1982 ilianzishwa Tume ya pamoja ya ushirikiano kati ya Tanzania na Zimbabwe kupitia taasisi mbalimbli za kimataifa ikiwemo SADC.

Aidha, Rais Magufuli ametaja mikakati ya kukuza na kuimarisha ushirikiano wa uchumi katika maeneo ya sita ambayo ni biashara ambapo nchi hizo zimedhamiria kutumia fursa za SADC za kulegeza masharti ya biashara.Maeneo mengine ni la kukuza uwekezaji , utalii, usafiri wa anga na barabara, kushirikiana kupitia SADC kwa maana ya fursa za wanachama. Pamoja na eneo la ulinzi, usalama, afya, utamaduni, sanaa na michezo.

Vilevile, Rais Magufuli amesema wanawakaribisha Wazimbabwe kuja kuwekeza nchini Tanzania hasa ukizingatia kwamba kuna kiwango kidogo cha uwekezaji baina ya nchi mbili ambazo ni marafiki wa muda mrefu.

“Mwaka 2006 kiwango cha uwekezaji cha Zimbabwe nchini kilikuwa na thamani ya biashara ya sh. bilioni 18.3, huku mwaka 2017 ikiwa sh. bilioni 21.1, hivyo tumekubaliana kuimarisha baadhi ya maeneo ili kuleta mkakati wa kuimarisha uchumi wa nchi hizi mbili” alisema Rais Magufuli.

Rais Mnangagwa ambaye yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili, kesho juni 29 anatarajiwa kutembelea Chuo cha Sanaa cha Kaole Bagamoyo ambacho awali kilitumika kutoa mafunzo kwa wapigania uhuru kutoka nchi za Kusini mwa Bara la Afrika. Ambapo Rais Mnangagwa ni miongoni mwa waliopata mafunzo katika chuo hicho.

NIDA KUTOA VITAMBULISHO VYA URAIA MSIMU WA SABASABA

$
0
0

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MAMLAKA ya vitambulisho vya taifa (NIDA) itatua muda wa wiki mbili za msimu wa sabasaba kuanzia June 28 hadi Julai 2 kutoa vitambulisho vya uraia kwa wakazi wa Dar es salaam.

Akizungumza na Michuzi blog Mkuu wa kitengo cha mawasiliano (NIDA) Rose Joseph ameeleza kuwa kama mamlaka wamejipanga kuhudumia wananchi wote watakaojitokeza katika viwanja vya sabasaba kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho hivyo.

Akieleza taratibu za kupata kitambulisho cha utaifa bi. Rose ameeleza kuwa lazima mwombaji ajaze fomu ya maombi inayotolewa na mamlaka hiyo sambamba na kuambatanisha na vyeti vya elimu, pasipoti, leseni, kitambulisho cha mkazi Zanzibar au kati ya vilivyoorodheshwa na nakala hizo zitakazoambatanishwa zisipungue tatu.

Pia amesema kuwa vyeti vya kuzaliwa na muhimu na lazima kwa waliozaliwa kuanzia miaka ya 1980 kushuka chini, na nakala za vivuli zitakazoambatanishwa ni muhimu mwombaji kwenda na nakala halisi ili waweze kujiridhisha.
 Jaji Mkuu kiongozi Dkt. Eliezer Mbili Feleshi akisalimia na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano (NIDA) Rose Joseph alipo tembelea banda la Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa mapema leo .(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa(NIDA)Rose Joseph  akizungumza Globu ya jamii  leo jijini Dar as Salaam
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa (NIDA) Rose Joseph akimueleza jambo Jaji mkuu kiongozi Dkt. Eliezer Feleshi namna walivyojipanga kuwahudumia wananchi katika maonesho hayo ya saba saba.picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii.
 Baadhi ya Wananchi walio fika kwenye banda la (NIDA) wakijaza fom ili kupata vitambulisho vya Taifa

Sanlam yasherehekea miaka 100 tangu kuanzishwa kwake

$
0
0

*Kamishna wa Bima nchini atoa ufafanuzi , aipongeza kampuni ya Sanlam kwa kutimiza miaka 100


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMISHNA wa Bima nchini Dk.Baghayo Saqware amesema kuanzia Agosti mwaka huu kampuni za bima nchini yataanza kusajili mawakala wa bima wao wenyewe kadri wanavyoweza huku mchakato wa ununuzi wa bima kwa njia ya kibenki ukiendelea.

Ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa sherehe ya kutimiza miaka ya 100 ya kampuni ya bima ya Sanlam tangu kuanzishwa kwake.

Hivyo mbali ya kuipongeza Sanlam kwa kutimiza miaka 100 akatumia nafasi hiyo kutoa majibu ya changamoto ambazo ziliwasilishwa kwake na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Sanlam Ibrahim Kduma.

Kaduma pamoja na kuzungumzia mafanikio ya kampuni hiyo kwenye masuala ya bima ametaja changamoto tatu ambazo zinakwamisha sekta ya bima nchini.Changamoto hizo ni masharti magumu ya kusajili wakala wa bima, kuchelewa kwa mchakato wa benki kutumika kununua bima pamoja na kodi kubwa.

Hivyo Dk.Saqware amewahakikisha watoa huduma za bima nchini kuwa tayari yameandaliwa mabadiliko ya sheria na hivyo kampuni ya bima itakuwa na uwezo wa kusajili mawakala wengi kadri ya uwezo wao.

Kuhusu benki kufanya shughuli za bima Dk.Saqware amefafanua changamoto hiyo nayo itapata ufumbuzi hivi karibuni kwani hivi sasa wanaandaa kanuni na Agosti mwaka huu watazipeleka kwa wadau ili wazipitie na kisha kuanza kutumika bada ya kupata baraza za Waziri.

"Kuhusu benki kufanya shughuli za bima hili lilichekelewa kwasababu Benki Kuu Tanzania(BoT) ilikuwa inataka kujiridhisha na sas imekubali , hivyo ni changamoto ambayo kimsingi imepata ufumbuzi wake na kilichobaki ni kuandaliwa kwa kanuni ili benki nazo zitumike kwenye masuala haya ya bima"amesema.

Akijibu kuhusu chagamoto ya kodi katika bima ya maisha, amejibu ni vema wadau wa bima wakafanya utafiti na kisha kuuwasilisha kwa Kamishna wa Bima.Amesema kuwa baada ya utafiti huo na maombi ya wadau wataangalia kama kuna uwezekano wa kutoa unafuu wa kodi au laa lakini akawahakikishia ni jambo ambalo linazungumzika kwani lengo la Serikali ni kuona suala la bima linapewa kipaumbele ili wananchi wengi wawe a bima mbalimbali.

Kuhusu kampunni ya Sanlam kutimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake Juni 8 1918, Dk.Saqware amesema wanastahili pongezi kwani ni wazi wapo imara na wameweza kukabiliana na kila aina ya changomoto na kuzivuka wakiwa salama na bora katika kutoa huduma ya bima na hasa bima ya maisha.

Amesema bila kuwa na menejementi imara na yenye kupanga mipango ya uhakika ni ngumu kampuni kufika miaka 100 na kutoa mifano ya kampuni nyingi ambazo zimenzishwa na hazikufika miaka kama hiyo.Hivyo amewataka kuendelea kujiimarisha na kuendelea kutoa huduma bora za bima nchini.

Awali Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Sanlam mbali ya kutaja changamoto hizo amesema sekta ya bima nchini bado haijapewa kipaumbele na hivyo kati ya watanzania milion 54 waliopo katika soko la bima ni asilimia 1.3.

"Ni vema kukawa na mikakati ya kuhakikisha idadi ya wanaonufaika na bima inaongezeka na moja ya kuhakikisha changamoto zilizopo zinaondelewa ili kupanua wigo wa masuala ya bima nchini.Kenya wamepiga hatua kwenye soko la bima ukingalinganisha na sisi,"amesema Kaduma.

Wakati huohuo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Khamis Suleiman amesema pamoja na kujikita kwenye bima ya maisha bado wamekuwa wakijihusisha na shughuli za kijamii katika maeneo mbalimbali nchini.

Amesema kupitia Sanlam Foundation wametengea Sh.milioni 413 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miundombinu kwenye sekta elimu nchini kwa kufanya mambo mbalimbali yakiwamo ya ujenzi wa madarasa.

Amefafanua kila mwaka kwenye mfuko huo watatumia Sh.milioni 136 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu na mradi huo ni wa kipindi cha miaka mitatu na kwamba watatekeleza ujenzi huo kwenye mikoa ambayo katika sekta ya elimu bado changamoto ziko nyingi.


Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Insurance, Khamis Suleiman (wapili kushoto), akizungumza na baadhi ya wateja wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 100 ya kampuni hiyo.Hafla hiyo iliyofanyika jana usiku jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Insurance Ibrahim  Kaduma (kulia) pamoja na viongozi wengine akigonganisha glasi pamoja na wateja wa kampuni hiyo wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 100 ya Sanlam tangu kuanzishwa kwake. Wa tatu kushoto ni Kamishna wa Bima Dk Baghoyo Sakwale ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wateja waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya miaka 100 ya Kampuni ya Bima ya Sanlam Life Insurance ambayo imefanyika jijini Dar es Salaam ambapo pia wadau mbalimbali wa masuala ya bima walihudhuria.

SERIKALI YAUTAKA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA KUONGEZA KASI YA KUBUNI MIKAKATI NA MABORESHO

$
0
0

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

SERIKALI imeutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuongeza kasi katika kubuni mikakati na maboresho ikiwemo taratibu za kujiunga ambazo zitawawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma zake.

Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa NHIF mjini Morogoro ambapo amesema kuwa mwelekeo wa Serikali kwa sasa ni kuhakikisha watu wote wanakuwa na bima ya afya.

"Serikali ya Awamu ya Tano imeweka nguvu kubwa katika utoaji wa huduma bora za matibabu kwa wananchi hivyo ninawaagiza muongeze kasi katika ubunifu na maboresho mbalimbali ambayo yatakwenda sambamba na matarajio ya Serikali yanayolenga wananchi wengi zaidi kuwa katika mfumo wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya,” amesema Dk. Ndugulile.

Amewataka watumishi wa Mfuko hususan Mameneja wa Mikoa kutokaa maofisini mwao na badala yake watoke nje kwa ajili ya kuhamasisha wananchi, kuangalia huduma wanazopata katika vituo vya kutolea huduma pamoja na kushughulikia changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.

Akizungumzia utendaji kazi wa Baraza, amewataka wajumbe wa baraza hilo kutambua wajibu wao ndani ya baraza kwa kuwa ni chombo muhimu katika kubuni na kuweka mipango thabiti ya kuendesha taasisi ambayo ina dhamana kubwa ya kuangalia ama kushughulikia huduma za matibabu kwa wanachama.

Amesema kwa sasa Serikali iko katika mchakato wa kuwasilisha muswada wa sheria ambao utawezesha wananchi wote kuwa katika utaratibu wa kupata huduma za matibabu kwa mfumo wa bima ya afya.

Akitoa salaam za NHIF, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo Bernard Konga amemhakikishia Naibu Waziri kuwa, Mfuko unaendelea kutekeleza na kuunda mipango ya kuongeza wigo wa wananchi kunufaika na huduma zake.

Amesema Julai mwaka huu, Mfuko unatarajia kuzindua ‘Ushirika Afya’ ili kuwezesha wakulima katika vyama vyao vya ushirika kunufaika na bima ya afya huku uundaji wa vifurushi mbalimbali ukiendelea.

"Mathalan, Mpango wa kulipa michango ya bima kidogo kidogo kwa kudunduliza kwa lengo la kuwawezesha wananchi wengi zaidi kunufaika na huduma za Mfuko. “Tumejipanga na hivi karibuni tutazindua huduma mbalimbali na hii yote ni mikakati ya kuelekea bima ya afya kwa wote kwa lengo la kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma za matibabu wakati wowote,” alisema Konga.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akimkabidhi nyaraka za kuongoza Baraza hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Baraza hilo.
Wajumbe wa Baraza la Pili la NHIF, wakionyesha ishara ya mshikamano baada ya kuzinduliwa rasmi kwa Baraza hilo.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga.
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza wakionyesha ishara ya mshikamano
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Faustine Ndugulile katika picha ya pamoja na Mameneja wa NHIF Mikoani.
 

WAZIRI PROFESA NDALICHAKO MGENI RASMI KONGAMANO LA MUHAS JULAI 2

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako anataraji kuwa mgeni rasmi katika kongamano la sita la kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) litakalofanyka Julia 2 hadi Julai 3 mwaka huu katika ukumbi wa LAPF Millenium Tower, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Makamu Mkuu wa chuo hicho, Prof. Andrea Pembe amesema jukumu mojawapo la MUHAS ni kutoa mafunzo ili kujenga rasilimali watu ya fazi za afya, kufanya tafiti na kushiriki kikamilifu utoaji huduma za afya kwa umma.

Amesema ili matokeo ya tafiti zinazofanywa yaweze kutumiwa na watekelezaji, wadau, wafanyakazi wa huduma za afya na wengine wanaofanya kazi katika maeneo husika ya kitaalamu, matokeo ya tafiti hizi hayana budi yasambazwe kwa ufanisi. “Hivyo basi, madhumuni ya kongamano hili la sita ni kushirikiana, kuelezana, kujifunza na kubadilishana ujuzi unaotokana na matokeo ya tafiti kati ya watafiti mbali mbali.

"Watoa huduma wa afya, watekelezaji wa mikakati na sera mbalimbali na wadau wengine wote ndani na nje ya Tanzania ikiwa ni pamoja na kushirikisha jamii kwa ujumla kupitia vyombo mbalimbali vya habari,"amesema. Pia katika Kongamano hili, Chuo kitaeleza mafanikio ya tafiti na athari zake kwa upande wa kijamii na maendeleo ya uchumi wa nchi. Katika Kongamano la sita la kisayansi, Chuo kitaonesha matokeo ya tafiti za hivi karibuni ya kisayansi kutoka miradi mbali mbali ya tafiti zinazotoka ndani na nje ya nchi katika kipindi cha miaka ya nyuma.

" Kitu cha muhimu zaidi katika jamii ya wanataaluma wa MUHAS ni kuwa watapata fursa ya kushiriki matokeo yao na kubadilishana mawazo na wataalamu pamoja na wadau kutoka sehemu mbalimbali za nchi na duniani kote ikiwa lengo kuu ni kuboresha afya kupitia tafiti," amesema Prof. Pembe. Amesema kauli mbiu ya Kongamano hili ni “Uimarishaji wa Uchumi wa Viwanda kupitia Tafiti za Afya kwenye nchi zenye kipato cha chini”.

Kauli mbiu hiyo imechaguliwa mahususi kusisitiza umuhimu wa matumizi ya matokeo ya tafiti za kisayansi za afya katika kuchangia uimarishaji wa uchumi wa viwanda hapa Tanzania na chi nyingine zenye uchumi wa kipato cha chini. Amesema hiyo ni kutokana na ukweli kuwa ili kuimarisha uchumi wenye viwanda Taifa linatakiwa kuwa na majibu ya changamoto zinazokabili sekta ya afya na kuboresha ukuaji wa uchumi. Ametaja kuwa katika kongamano hilo makala za kisayansi 164 zitawasilishwa kwa njia ya maongezi (Oral Presentations).

Amesema makala zitakazowakilishwa zimeangukia katika mada ndogo ndogo zifuatazo: Tafiti za Afya ya Uzazi,Tafiti wa Magonjwa yasiyoambukiza, Tafiti wa Magonjwa yanayoambukiza,Utafiti wa Msingi katika Maswala ya Afya, Tafiti za Sera na Mifumo ya Afya, Tafiti za Teknolojia ya Habari mawasiliano pamoja na Afya, Tafiti za Afya ya Kinywa, Tafiti za Tiba Asili na Tiba Mbadala, Huduma za Dawa za Tiba,Tafiti za Maswala ya Jinsia na Afya.

Amesema jumla ya washiriki na wajumbe zaidi ya 400 kutoka nchini na nje ya nchi kutoka nchi za Rwanda, Uingreza, Japan, Uturuki, Itali na Marekani. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Prof Andrea Pembe akizungumza na Waandishi wa habarai kuhusu Kongamano lake la sita la Kisayansi tarehe 2 na 3 Julai 2018. Kongamano hili litafanyika katika ukumbi wa LAPF Millenium Tower, jijini Dar es Salaam. Ofisa Uhusiano wa Muhas akizungumza na Waandishi wa habari juu ya Mkutano huo utakaoanza jumatatu.



TRC YAZINDUA TRENI YA MIZIGO,YABEBA TANI 2,400 KUPELEKA NCHINI UGANDA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limezindua treni ya mizigo kuelekea nchini Uganda ikiwa imebeba shehena ya mzigo wa tani 2,400 wa Shirika la Chakula Duniani (WFP).

Kubebwa kwa shehena hiyo ya mizigo kwenye treni kumenusuru takribani dola 96,000 sawa na Sh.211,200,000 za gharama ya usafirishaji.

Treni hiyo iliyoanza safari leo imezinduliwa na Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji Focus Makoye Sahani na kueleza utekelezaji huo ni maagizo ya Rais wa  Dkt John Magufuli kwa Wakurugenzi wa Shirika la Reli na mamlaka ya bandari kuhakikisha treni ya mizigo inafanya kazi akiwa katika ziara ya kikazi nchini Uganda.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Sahani amesema kuwa treni hii ya mizigo ilisimama toka Agosti mwaka 2009 wakiwa chini ya mwekezaji ila kwa juhudi zilizofanywa na mamlaka ya bandari na shirika la Reli limefanikisha kurejea kwa usafiri huo kuelekea nchini Uganda.

Sahani amesema kuwa, kwa mara ya hii ya kwanza wamepata ofa ya tani 2,400 toka kwa WFP utakuwa ni kwa treni tatu pia wanashukuru  kwani njia ya reli ni usafiri mzuri na wenye uhakika na wameweza kushirikiana na Shirika la Reli nchini Uganda na kufanikiwa kukarabati eneo la kilometa 9 kuelekea Kampala lililokuwa linasumbua.

"Tumeshirikiana na Shirika la Reli Uganda kufungua njia inayoelekea Kampala kwa kuwapatia vifaa vya kufungulia njia hiyo,"amesema Sahani.
Ameongeza  amesema anaishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuweza kupata vichwa vya treni vipya na vifaa vingine ambavyo vitaboresha huduma zao za usafirshaji kuanzia sasa.

Mkuu wa Usafirishaji wa WFP Muhamad Mabuyu amesema kuwa wameokoa dola 40 kwa kila tani ambapo thamani yake ni zaidi ya milioni 211 za kitanzania kama wangetumia usafiri wa njia ya barabara, na hiyo hela kwa sasa itatumika kununulia mahitaji mengine kwa ajili ya wahanga mbalimbali.
Mabuyu amesema, treni hiyo ya mizigo itatoka kuanzia katika hifadhi yao ya chakula bandarini Dar es Salaam na itafika moja kwa moja katika hifadhi yao ya nchini Uganda katika Jiji la Kampala.

"Tumeweza kutumia usafiri wa njia ya reli kwani ni rahisi na wenye uhakika kwakuwa mwaka 2017 tulisafirisha tani 16,000 kuelekea Mkoani Dodoma na haikupotea hata kiroba kimoja cha kilo 50,"amesema. 
Mabuyu amesema,mbali na tani hizo zinazoelekea Kampala, kuna tani zingine 15,000 zinaanza kuingia kesho ambazo pia tutatumia usafiri wa njia ya reli kuzisafirisha na iwapo wangetumia magari ya tani 30 wangeingia gharama kubwa sana ya magari 500 ila watatumia treni 19 kufikisha mzigo huo .

WFP wamesifia huduma za TRC na kueleza yeye kama mdau wa usafirishaji anaupongeza  uongozi wa TRC na Serikali kwa ujumla kwa kufanikisha huduma hiyo ya njia ya reli kurudi ikiwa ni baada ya miaka 10.
Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji Focus Makoye Sahani akizindua treni ya mizigo na kuashiria kuanza kwa huduma hiyo baada ya kusimama kwa kipindi cha miaka 10.
Kaimu Mkurugenzi Uendeshaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Focus Makoye Sahani akizungumza na waandishi wa habari kabla kuzindua treni ya mzigo kuelekea nchini Uganda ikiwa ni baada ya miaka 10 toka kusitishwa kwa huduma hiyo ya usafirishaji.
Mkuu wa Usafirishaji wa Shirika la Chakula Duniani Nchini Tanzania (WFP) Muhamad Mabuyu akizungumza na waandishi wa habari na kuelezea ubora na ufanisi mzuri wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) katika ufanisi wa usafishaji mizigo wakati wa uzinduzi wa treni ya mizigo kuelekea Nchini Uganda.

Unesco wakabidhi kijiji digitali cha Ololosokwan kwa serikali

$
0
0
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) wamekabidhi rasmi kijiji cha digitali cha Ololosokwan katika sherehe kubwa iliyofanyika kijijini hapo na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali na mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Katika kukabidhiana huko Unesco imesema kwamba itaendelea kutoa msaada katika mtandao wa intaneti kwa miezi sita ijayo.
Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba na Dk. Abdul Rahman Lamin, Ofisa msimamizi wa ofisi ya Unesco, Ann Therese Ndong-Jatta alisema kwamba wakati wanakabidhi facility hizo wamefurahishwa na ushirikiano mkubwa waliopewa katika mradi huo.

Kijiji cha digitali cha Ololosokwan ni moja ya vijiji vinne ambavyo vimefadhiliwa huku vikitoa huduma muhimu za elimu, afya na biashara kuendeshwa kidigitali.Kijiji hicho cha digitali ambacho ni matokeo ya ushirikiano kati ya UNESCO na kampuni ya Samsung imelenga kutoa elimu kwa kutumia njia ya mtandao, kufaniklisha tiba mtandao na pia kutumia mtandao wa kompyuta katika kuwezesha biashara.

Ofisa huyo alisema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano uliopo ili mradi uweze kuendelea kuchangia maendeleo ya wakazi wa eneo hilo.
Aidha aliitaka serikali kuhakikisha kwamba inaendeleza ushawishi kwa wananchi wa eneo hilo la Ngorongoro kutumia vyema teknolojia ya kisasa katika kufanikisha maisha endelevu ya zana zilizopo.

“UNESCO inajisikia furaha kwa kutambua kwamba kupitia mradi wa kijiji cha digiti, wilaya ya Ngorongoro imekuwa miongoni mwa waanzizilishi wa matumizi ya Tehama katika kufanikisha elimu na afya nchini Tanzania. “ alisema Ndong-Jatta .Alisisitiza kuwa kuwapo kwa kijiji hicho kunaambatana na mamchakato wa sasa wa serikali ya awamu ya tano ya kuwa na taifa lenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

“Nataka kuhakikishia wilaya ya Ngorongoro, kijiji cha Ololosokwan na serikali ya Tanzania kwamba UNESCO itaendelea kutoa msaada wa kiufundi na kuhakikisha kwamba kunakuwa na maendeleo endelevu kwa kijiji hichi” alisema Ndong-Jatta.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo akizungumza na wananachi wa kijiji cha Ololosokwan pamoja na wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Abdul Rahman Lamin akizungumza kwa niaba ya Ann Therese Ndong-Jatta wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Avemaria Semakafu akitoa salamu za Wizara ya Elimu pamoja na za Mbunge  wa Jimbo la Ngorongoro ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo,Ufugaji na Maendeleo ya Uvuvi, Mh. William Ole Nasha wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Mkurugenzi wa Tehama MUHAS na Mratibu wa huduma ya tiba mtandao, Dkt. Felix Sukums akitoa salamu za MUHAS wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Diwani wa kata ya Ololoskwan, Mh. Yannick Ndoinyo akitoa neno la shukran kwa niaba ya wananchi wake kwa mgeni rasmi na Unesco kwa ushiriki wao wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Abudl Rahman Lamin (wa tatu kushoto) akimwakilisha Ann Therese Ndong’ Jatta, Mkurugenzi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki akimkabidhi rasmi ripoti ya mradi wa kijiji cha kidigitali (Unesco-Samsung Digital Village) kwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mh. Rashid Mfaume Taka (wa tatu kulia) kwa ajili ya uendelezaji baada ya majaribio wakati wa hafla iliyofanyika katika kituo cha mafunzo ya kazi za mikono na utamaduni cha jamii ya wamasai (Community Arts Space-CAS) kilichojengwa na Umoja wa Ulaya (EU) kwa ushirikiano wa Unesco kwenye kijiji cha Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha. Wengine wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Avemaria Semakafu (waliosimama kwa nyuma), Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo (kushoto), Kaimu Katibu Mkuu wa Tume ya Taifa wa UNESCO nchini Tanzania, Dkt. Moshi Kimizi (wa pili kushoto), Diwani wa kata ya Ololosokwan, Mh. Yannick Ndoinyo (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa  Kitongoji cha Ololosokwan, John Pyando (kulia).
 Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akiteta jambo na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Abdul Rahman Lamin wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali wilayani Ngorongoro mkoani Arusha. Wengine meza kuu kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro, Emmanuel Sukums pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mh. Rashid Mfaume Taka.
 Baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan waliohudhuria hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Baadhi ya wazee wa kijiji cha Ololosokwan waliohudhuria hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo katika picha ya pamoja na wananchi, viongozi wa serikali na mashirika ya Umoja wa Mataifa walioshiriki mara baada ya hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.

KATIBU MKUU WA CCM BASHIRU ALLY AMTAKA MFANYABIASHARA JIJINI DODOMA KUREJESHA ENEO LA CCM ANALODAIWA KULIHODHI KWA MIAKA MINGI

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dk. Bashiru Ally amemtaka mfanyabiasha aliyetajwa kwa jina moja la Deogratius wa jijini hapa, kurejesha kwa hiari yake eneo la CCM ambalo anadaiwa kulihodhi kwa miaka kadhaa sasa katika Kata  ya Makutupola wilaya ya Dodoma Mjini ambalo amekujenga ukumbi na fremu kadhaa za maduka.
Dk. Bashiru ametoa agizo hilo kwa mfanya biashara huyo leo alipokuwa akizungumza na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake katika Kata ya Nakutupola jijini hapa.Amesema amefikia uamuzi huo kwa sababu mfanyabiashara huyo ameonekana kutokuwa na uaminifu wa kutosha kwa kuwa hivi karibuni alizungumza nae ofisini kwake na kuahidi kukutana ili kufanya makabidhiano ya eneo hilo kwa sherehe na nderemo kwenye kikao hicho.

"Cha kushangaza juzi akikuja mwenyewe ofisini kwangu tukaxungumza kwa muda wa saa mbili tukakubaliana leo aje kwenye kikao hiki kukabidhi eneo letu kwa sherehe na ndelemo lakini leo nimempigia hadi simu akasema eti ameenda Dar es Salaam kushughulika na masuala ya mwanae, sasa  endeleeni na mazungumzo  na utaratibu wa makabidhiano akabidhi kwa hiari eneo letu", alisema Dk Bashiru

Dk. Bashiru aliwataka wanachama na viongozi wa CCM kutofanya vurugu za aina yoyote kwa Mfanya biashara huyo na kusema Mchakato uliotumika kurejesha ukumbi ndio utakaotumika kurejesha eneo lote la  Chama na mali yote iliyopo kwenye eneo la hilo ni mali ya CCM.

Katika mkutano huo Katibu Mkuu wa CCM Dk Bashiru Ally amewapokea Winston Edward Katibu Kata hiyo wa CUF na Baraka Tayara Katibu kata wa Chadema pamoja na wanachama 181 kutoka vyama hivyo.
 Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally akipokelewa na Viongozi mbali mbali alipowasili kata ya Makutupola wilaya ya Dodoma mjini leo.
 Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akiwapungia Mkono kikundi cha ngoma

 Mwenyekiti wa Kata ya Makutu pola akifungua kikao hicho
  Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Bi Jamila Yusuph  akizungumza wakati akimkaribisha  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Ndg.Godwin Mkanwa kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM kuzungumza na Viongozi na wanachama wa Kata ya Makutupola Wilaya ya Dodoma Mjini.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dodoma Ndg.Godwin Mkanwa akizungumza wakati akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM kuzungumza na Viongozi na wanachama wa Kata ya Makutupola Wilaya ya Dodoma Mjini
 Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akizungumza na Viongozi na wanachama wa CCM na Jumuiya zake wa Kata ya Makutupola leo
 Katibu kata wa Chadema ndg.Baraka M.Tayara akizungumza mara baada ya kukabidhi kadi yake ya uwanachama toka Chama cha Demokrasia na maendeleo alipoungana na Katibu wa kata hiyo toka CUF Ndg.Winston Edward pamoja na wanachama 181 wa Vyama hivyo Leo walipojiunga na CCM.
 Wanachama na Viongozi wa Chama cha Mpinduzi kata ya Makutupola wakiimba nyimbo ya chama mara baada ya kuwapokea viongozi hao.
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akizungumza na Mwanachama wa CCM mara baada ya mkutano kumalizika( Picha na Fahadi Siraji CCM Blog)

Serikali inatarajia kuzindua muongozo wa Uendeshaji Viwanda nchini Julai 2

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 

SERIKALI imesema katika kukuza biashara nchini imesema inatarajia kuzindua Muongozo wa Uendeshaji Viwanda nchini Julai 2, mwaka huu kupitia Serikali Mitaa ili kutekeleza lengo la ufufuaji na uendeshaji viwanda nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika VIwanja vya Maonyesho ya 42 Sabasaba, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Elisante Ole Gabriel, amesema tayari Serikali imeridhia uanzishwaji wa mchakato huo.

Alisema tayari mikakati mbalimbali inaandaliwa kuhakikisha mkakati huo unakua endelevu.Amesema Serikali imedhamiria kukuza uchumi wa viwanda na ili kufikia malengo tutazindua mpango huu,"alisema Gabriel.Profesa Ole Gabriel sema kauli mbiu ya Maonyesho ya Sabasaba mwaka huu ni ukuzaji Biashara kwa ajili ya maendeleo ya Viwanda.

Gabriel alisema, kauli mbiu hiyo imeteuliwa kwa lengo kukuza uchumi wa viwanda hapa nchini.Amesema unapoangalia uchumi wa viwanda ni lazima uangalie bidhaa zinazouzwa ndani ya nchi," alisema Gabriel.Alisema Serikali ya awamu ya Tano imejidhatiti kuweka uchumi wa viwanda hivyo ni wajibu kwa kila taasisi itengeneze bidhaa bora itakayoingia katika uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Nchini (Tantrade), Edwin Rutageruka, alisema wanakuza biashara ili kupata kodi, ajira na kukuza viwanda nchini.Amesema maonyesho ya mwaka huu, yatafunguliwa Julai 2, ambapo hadi hivi sasa tayari wageni 33 wametoka nje ya nchi na washiriki wa ndani ni 2,956 na taasisi za Serikali 127.

"Tunashukuru kwa mwaka huu washiriki wa nje wameongezeka kwa mwaka jana walikuwepo 30,"alisema Rutageruka 
katibu MkuuTIBU Mkuu Wizara ya Viwanda na Uwekezaji Profesa Olisante Ole Gabriel, akipata maelezo kutoka kwa maofisa wa Shirika Simu Tanzania (TTCL) Rachael Mremi kuhusu huduma ya 4G wakati alipotembelea banda la shirika hilo, katika Maonyesho ya 42 ya ya Kimataifa ya Biashara, viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, B, Dar es salaam.

WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; William Lukuvi amekutana na viongozi wakuu wa Kampuni ya kuwezesha upatikanaji wa nyumba za bei nafuu – Shelter Afrique jijini Dar es Salaam.

Waziri Lukuvi alikutana na viongozi hao kwa kikao maalum ofisini kwake – Dar es Salaam. Viongozi hao ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo; Bwn. Femi Adowele na Katibu wake; Francesca Kakooza.
Aidha, Suala mahususi lililowakutanisha viongozi hao lilikuwa ni kuhusu maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 37 wa Kampuni hiyo unaotegemewa kufanyika hivi karibuni nchini Kenya, ambapo Waziri Lukuvi ni Mwenyekiti wa Mkutano huo.

Kwa ujumla changamoto za nchi za kiafrika katika kuwapatia wananchi wa kawaida makazi nafuu zinafanana na kilio kikubwa katika nchi wanachama, ambazo ni kuwepo makazi holela hata baada ya nchi hizo kujikomboa kutoka ukoloni mkongwe. Shelter Afrique imedhamiria kuweka juhudi katika kuipa kipaumbele sekta ya Nyumba kwa kuwa ni sekta mtambuka katika kuharakisha ukuaji wa uchumi na maisha bora ya watu.

Mambo mbalimbali katika sekta ya Nyumba yanatarajiwa kuzungumziwa katika Mkutano huo wa 37, hususan katika jitihada za kupatikana kwa makazi bora na nafuu katika nchi wanachama, ambapo changamoto Kuu imekuwa ni Rasilimali fedha.Tanzania ni nchi mojawapo Mwanachama wa Shelter Afrique kati ya nchi 44 za barani Afrika .

Tanzania ilijiunga na Shelter Afrique mwaka 2003 na Mkutano wa 32 ambao ulifanyika N’djamena, Chad 2013, uliopitishwa na Azimio Namba GM/ 2013/005 la kuongeza Hisa kwa kila nchi mwanachama kwa lengo la kukuza mtaji wa Kampuni hiyo na kuiwezesha kuweka nguvu zaidi katika masuala ya uendelezaji nyumba barani Afrika. 

Mkutano wa mwaka huu wa 37, unategemewa kufanyika Nairobi, Julai 20, 2018.

Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

CERA yafika Tanzania

$
0
0
Dar es Salaam: CERA Sanitaryware, chapa inayokua kwa kasi imezinduliwa kwenye hoteli ya Ramada Encore jijini Dar es salaam hivi karibuni. CERA inashirikiana na Imports International(T)Ltd (IIL), wadau wao nchini kwa ajili ya usambazaji, huduma kwa wateja na kujenga chapa ya CERA nchini Tanzania. Imports International (T) Ltd –IIL – imebobea na inajulikana kwa kuleta mafanikio makubwa katika kuwakilisha bidhaa za kifahari za kimataifa hapa nchini kupitia maadili mazuri ya ufanyaji biashara na huduma bora kwa wateja.
Mkurugenzi Mkuu wa IIL Bw. Trushal Jethwa ni mtu mwenye maono mazuri na ana dhamira ya dhati ya kutoa mchango mkubwa kuboresha ufanisi katika sekta ya ujenzi kwa kuleta bidhaa bora zinazokidhi viwango vya kimataifa, nchini Tanzania. Tokea mwaka 2004, IIL imejikita katika usambazaji wa bidhaa bora zinazofaamika kimatafika kutoka Makampuni mbalimbali duniani kama Saint Gobain, Gyproc, Weber, ISOVER, Insutech n.k.

Cera Sanitaryware Limited, kampuniya vifaa vya bafuni inayokua kwa kasi India, imekuwa mstari wa mbele katika ubunifu tangu uanzilishi wake manmo mwaka 1980. CERA imeweza kunyakua tunzo mbalimbali kwenye sekta ya ujenzi. Pia, imefanikiwa kushinda tunzo ya “Bidhaa Bora Ya Mwaka” kwa miaka 4 mfululizo katika maudhui ya ubunifu. Sio hivyo tu, CERA imetunukiwa “Chapa Inayoaminika na wateja” katika utafiti uliofanywa na gazeti la Reader’s Digest. Katika soko la Indiam wateja wameitunuku CERA na tunzo ya “Power Brand” .

Kampuni ya CERA inahesabika kati ya chapa kubwa za bara la Asia. CERA pia ipo kati ya chapa 100 zenye tuzo ya “Architecture & Design”. Pamoja na hayo, CERA pia inajulikana kwa teknolojia ya “green”, ambayo inajali mazingira, katika utengenezaji wa bidhaa zao zote. Ina mkusanyiko kubwa ya bidhaa zinatomia matumizi madogo ya maji. Kampuni ya CERA ina uwepo katika nchi 38, ndani ya mabara 4, na hakika hii huifanya kuwa kampuni ya kimataifa inayofikia kila kiwango kilichwekwa kwa ajili ya vifaa vya bafuni.

Bw. Dilip Thakkar, Meneja Mkuu (Export) wa Cera Sanitaryware Limited alikuwepo kwenye uzinduzi huo kukutana na wasanifu, washauri, wadau wa ujenzi. Alielieza kuhusu maono yake ya chapa ya CERA barani Africa – hasa nchini Tanzania. Aliongelea pia kuhusu kufungua showroom ya CERA katika jengo kuu la IIL iliyopo barabara ya Nelson Mandela karibu na Wiazara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambayo itakua suluhisho la wateja wote na kuongeza matarajio ya watanzania kujipatia mabafu yenye ubora zaidi.

Bidhaa zote za CERA, yaani vyoo na bafu, mabomba, vigae, mabeseni ya kunawia n.k. vitakuwepo kwenye showroom ambayo itafunguliwa saa 3 asubuhi hadi saa 11 na nusu jioni kutoka Jumatatu hadi Ijumaa and saa 3 na nusu asubuhi hadi saa 8 na nusu mchana kwa siku ya Jumamosi.
Kwenye tukio hili, Bw. Zaheer ambaye ni meneja wa CERA Tanzania na soko la Afrika, alishukuru wageni wote waliokuwepo na kuahidi kwamba yeye na timu yake watahakikisha wateja wote wataridhika kwa 100% na bidhaa zote za CERA.

BENKI YA CRDB YADHAMINI MKUTANO WA MAKANDARASI JIJINI DODOMA

$
0
0

Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Jane Ikira, akimkaribisha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la benki hiyo. Katikati ni Meneja Mahusiano wa benki hiyo anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford.
Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford (katikati), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa.
Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford, akizungumza na waandishi wa habari.
Jane Ikira, akimkabidhi zawadi Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika banda lao wakati wa mkutano wa mashauriano na wadau na maonyesho ya bidhaa na huduma za ujenzi yanayofanyika mkoani Dodoma.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la LAPF-Dodoma, Martha Ngwenya, akipeana mkono na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la benki hiyo.
Ofisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Nasibu Kalamba (kushoto), akielezea juu ya huduma na bidhaa zinazotolewa na Benki ya CRDB kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (kulia).

Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Shima Danford (katikati), akielezea juu ya dhamana ya mikopo ya makandarasi inayotolewa na Benki ya CRDB kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika mkutano wa mwaka wa makandarasi jijini Dodoma, ulioandaliwa na Bodi ya Makandarasi (CRB) na kudhaminiwa na benki hiyo. Kushoto ni Meneja Mahusiano wa hiyo anayeshughulikia wateja wakubwa na taasisi, Jane Ikira.
Baadhi ya wateja wakiwa katika banda la Benki ya CRDB wakipata huduma mbalimbali ikiwemo ya kufungua akaunti.
Mteja wa Benki ya CRDB akielezwa kuhusu Kampeni ya Shuhudia Kombe la Dunia la Fifa 2018 na TemboCardVisa baada ya kufungua akaunti katika banda la benki hiyo.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakiwa kwenye ukumbi wa mkutano.
Meneja Mwandamizi Huduma za Kibiashara wa Benki ya CRDB, Baraka Eusebio, akitoa ufafanuzi juu ya huduma mbalimbali za kibenki wanazotoa.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa wamepozi kwa picha ndani ya banda lao kutoka kushoto ni Lucy Kiondo kutoka tawi la Dodoma, Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory, Veronica Komba na Wakala wa Benki hiyo, Upendo Moses.
Ofisa wa Benki ya CRDB, Veronica Komba (kushoto), pamoja na Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory, wakimuhudumia mteja.
Wakala wa Benki ya CRDB tawi la Chamwino, Upendo Moses, akitoa huduma kwa wateja waliokuja kuweka fedha zao kupitia banda la CRDB.
Maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa wamepozi kwa picha ndani ya banda lao, kutoka kushoto ni Lucy Kiondo kutoka Dodoma Branch, Veronica Komba na Ofisa Maendeleo ya Biashara tawi la Chamwino, Ingrid Nestory.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (katikati aliyekaa), akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa mkutano wa mwaka wa makandarasi unaofanyika jijini Dodoma ambapo Benki ya CRDB ni miongoni mwa wadhamini wa mkutano huo.

SUMATRA YAANZA KUTEKELEZA AGIZO LA NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASILIANO

$
0
0
Na EmanuelMadafa,Mbeya.

MAMLAKA ya Udhibiti na Usafirishaji wa Nchi Kavu na Reli, (SUMATRA),imeanza kutekeleza agizo la Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi . Atashasta Nditiye,ambalo lilielekeza kuanza kutoa elimu kwa wadau na watumiaji usafiri njia ya reli ili kupunguza vitendo vya uhujumu uchumi vinavyofanywa na watu ambao si waadilifu.

Akizungumza Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya Mdhibiti na Mkaguzi wa Usalama wa Reli, kutoka Mamlaka ya Udhibiti SUMATRA, Mhandisi . Hanya Mbawala,amesema tayari Mamlaka hiyo imenza kutekeleza agizo la Waziri ambapo wameanza kutoa elimu hiyo kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa reli hiyo katika stesheni ya Chimala.

Amesema, kazi ya kitengo cha reli ndani ya SUMATRA ni kuhakikisha usafiri wa reli unakua salama na uhakika na jambo hilo linafanyika kwa kitengo kuendesha kaguzi za mara kwa mara ikiwa na kuishauri serikali na TAZARA kwa ujumla ya nini kifanyike.

Amefafanua kuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mwezi Mei mwaka huu akiwa Ifakara, alitoa maagizo ambayo tayari mamlaka imeanza kuyafanyia kazi, hivyo hatua iliyopo kwa sasa ni kutoa elimu kwa wadau na watumiaji wa reli kuanzia eneo la Makambako hadi Tunduma.

Amesema, eneo la Makambako/ Tumduma ambako reli hiyo inapita , limekuwa likihujumiwa sana kwa watu kuiba vifaa na kuharibu miundombinu ya reli hivyo mamlaka hiyo inakusudia kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kupitia viongozi wa serikali ambao ndio walengwa wakubwa wa elimu hiyo.

Mhandisi Hanya ameeleza kuwa usafiri wa reli ni salama na usioleta madhara kwa barabara, nani usafiri wa haraka na bei nafuu kwa usafirishaji hivyo serikali imeona umuhimu huo na ndio maana sasa maboresho yanafanyika na reli kurejea kwenye ubora wake, kwani usafiri wa reli ndio usafiri pekee unaoaminika na ndio unaokuza uchumi wa nchi.

Akizungumzia hali ya Usalama wa Reli hiyo ya Tazara Ndugu Sadiki Athony ,ambaye ni meneja usalama Tazara amesema eneo korofi kwa sasa ambalo limekuwa likihujumiwa mara kwa mara ni eneo la Inyala hadi Mbeya ambapo matukio ya kutoa vyama ndani ya daraja hali ambayo imekuwa ikihatarisha usalama wa abiria wanaotumia usafari wa reli hiyo ya Tazara.

Amesema wizi wa vyuma vya madaraja stesheni ya Ilongo na Mbeya Mjini, unaendelea kuitia hasara serikali kwani hivi karibuni daraja namba 248 kuna vyuma vimeibiwa na hii si mara ya kwanza, hivyo elimu hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza madahara hayo.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya mbarali Ndugu Rubeni Mfune amesema atahakikisha elimu hiyo inawafikia zaidi wananchi walio wengi pamoja na kuwataka watendaji wa vijiji kuingiza agenda ya ulinzi wa reli kwenye vikao vyao .
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Ndugu Rubeni Mfune akizungumza na Viongozi wa vijiji na wananchi (hawapo pichani)ambao wana ishi maeneo ya jirani na njia ya Reli ya Tazara katika Stesheni ya Chimala Wilayani humo .
Mdhibiti na Mkaguzi wa Uslama wa Reli, kutoka Mamlaka ya Udhibiti SUMATRA, Eng. Hanya Mbawala akisisitiza jambo katika mkutano na wananchi na watendaji wa vijiji (hawapo pichani) ambao wanaishi pembezoni na njia ya reli ya Tazara katika stesheni ya Chimala wilayani Mbarali Mkoani Mbeya June 29 ,2018.
Wananchi na Viongozi wanaoishi pembezoni mwa Reli ya Tazara katika Stesheni ya Chimala Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya wakisikiliza kwa makini maelezo yanayotolewa katika mkutano uliotishwa na viongozi wa Sumatra na Tazara katika kutoa elimu ya ulinzi wa Reli hiyo.
Meneja Usalama wa Reli ya Tazara Ndugu Sadick Anthony akizungumza na wananchi na Viongozi wa vijiji wanaoishi pembezoni mwa reli ya Tazara (hawapo pichani)katika mkutano ulioitishwa na Mamlaka ya Sumatra kwa lengo la kutoa elimu juu ya ulinzi wa reli ya Tazara .
Afisa mtendaji kijiji cha Iliumfilo kata ya Chimala Wilaya Mbarali Ndugu Adel Mwalioteti akitoa maoni yake katika mkutano huo katika ukumbi wa stesheni ya Chimala .
Afisa Mtendaji kijiji cha Matamba kata ya Mapogolo Wilayani Mbarali Anyagile Adam ,akichangia jambo katika mkutano uliotishwa na Sumatra pamoja na Tazara kwa lengo la kutoa elimu ya Ulinzi wa Reli ya Tazara katika ukumbi wa stesheni ya Chimala Mbarali

RITA KUTOA VYETI VYA KUZALIWA NA MSAADA WA KISHERIA SABASABA

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii.

WAKALA wa usajili, ufilisi na udhamini (RITA) wanatoa  huduma za usajili kwa watoto chini ya miaka mitano na watu wazima kwa kutoa vyeti vya kuzaliwa.

Akizungumza na Michuzi blog Afisa habari wa RITA Jafari Malema ameeleza kuwa wamejipanga katika msimu huu wa sabasaba katika kuhakikisha watoto wanapata hati zao za utambulisho wa kuzaliwa na watu wazima ambao watasaidiwa kwa msaada maalumu.

Jafari ameeleza kuwa watakua wakiwahudumia wananchi wakati wote wa maonesho na amewaomba wazazi kutumia fursa hiyo kwa kuwapa watoto vyeti vya kuzaliwa vinavyotolewa na mamlaka hiyo.

Aidha ameeleza kuwa licha ya kutoa vyeti vya kuzaliwa RITA itatoa msaada wa kisheria hasa katika masuala ya talaka, ndoa, kuasili mtoto (child adoption), ushauri wa mirathi, wosia na namna ya kuandika na kuhifadhi wosia.

Ameeleza kwamba tangu waanze kutoa huduma hiyo changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni udanganyifu wa majina na mahali na amewataka wazazi kukubaliana majina ya watoto kabla ya kufanya usahili huo.

Jafari ameeleza kuwa ili mtoto aweze kupata cheti cha kuzaliwa mzazi awe na tangazo la kizazi kutoka kituo alichozaliwa mtoto, kadi ya kliniki, cheti cha ubatizo au falaki na kwa watu wazima wawe na tangazo la kizazi kama lipo, kadi ya kliniki, cheti cha shule (msingi/ sekondari) au cheti ya falaki au ubatizo.
 Mafisa mbalimbali wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) wakiendelea na kazi ya kuwahudumia wananchi waliotembelea mbanda hilo katika maonesho ya kimataifa yanayo fanyika Sabasaba jijini Dar as Salaam.
 Afisa habari Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Jafari Malema akiwaelekeza wananchi namna ya kujaza fom za cheti cha kuzaliwa leo jijini Dar as Salaam
 Mariam Ling'ande-Afisa msajili msaidizi akiwakabidhi vyeti vyakuzaliwa wananchi walio fika kwenye banda la RITA na kuhudumiwa.
 Afisa habari Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Jafari Malema akizungumza  leo jiji Dar as Salaam na  Michuzi Blog kuhusu kuwahudimia wananchi wakati ote wa maonesho ya sabasaba.
Wananchi wakiwa katika banda la Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kwenye

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA NAIBU KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed ambapo walikutana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mohammed V mjini Casablanca Morocco,Makamu wa Rais alikuwa njiani kuelekea nchini Mauritania ambako mkutano wa 31 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)​

BENKI YA WATU WA ZANZIBAR YATIMIZA MIAKA 52 TANGU KUANZISHWA KWAKE,YATOA NENO KWA WATANZANIA

$
0
0
Na Emmanuel Massaka, Globu ya jamii

BENKI ya Watu wa Zanzibar(PBZ),leo imefanya Sherehe ya kutimiza miaka 52 tangu kuanzishwa kwake ambapo uongozi wa benki hiyo umewaomba Watanzania kuhakikisha wanafungua akaunti kwao. 

Pia benki hiyo imewahakikishia Watanzania kuendelea kutoa huduma bora kutoka wa watumishi ambao wanaifanya kazi yao kwa weledi mkubwa.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam leo na Meneja Mkaguzi wa ndani wa Benk ya Watu  wa Zanzibar wa tawi la Tazara, Suleiman Ali Seleiman  baada ya kukata keki katika hafla ya kutimiza miaka hiyo 52 tangu kuazishwa kwake.

Akizungumza leo na Blogu ya jamii Suleiman  ametoa mwito kwa wananchi kujiunga na benki hiyo ili kurahisisha shughulizao na hasa zinazohusu huduma za kibenki.
 Picha ya pamoja
 Meneja wa mkaguzi wa ndani wa Benk ya watu wa Zanzibar tawi la Tazara Suleiman Ali Suleiman akimlisha keki mteja katika hafla ya miaka 52 tangu kuazishwa kwake.
 Meneja wa mkaguzi wa ndani wa Benk ya watu wa Zanzibar tawi la Tazara Suleiman Ali Suleiman akimlisha keki Meneja tawi ta Tazara,Fatma Khamis Mohad leo katika hafla ya kuazimisha miaka 52.
Meneja wa mkaguzi wa ndani wa Benk ya watu wa Zanzibar tawi la Tazara Suleiman Ali Suleiman akimlisha keki mteja katika hafla ya miaka 52 tangu kuazishwa kwake.

MAJALIWA AFUNGUA JENGO LA BIASHARA LA NHC SINGIDA,AITAKA KUWAFIKIA WATU WA CHINI

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lina jukumu kubwa la kuhakikisha sekta hiyo inakua na kuwafikia watu wa kipato cha chini.Amesema ya Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli inahimiza uchumi wa viwanda, hivyo sekta ya nyumba ina mchango mkubwa sana katika kuchochea ukuaji wa viwanda.

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Juni 30,2018) wakati akizindua mradi wa Singidani Commecial Complex, mjini Singida. Jengo hilo la biashara na ofisi limejengwa na NHC kwa ajili ya kupangisha wafanyabiashara na taasisi mbalimbali.

Waziri Mkuu amesema sekta ya nyumba ni mtambuka kwa kuwa huchochea ukuaji wa uchumi, kutoa ajira na kukuza uwekezaji wa viwanda vya vifaa vya ujenzi kama saruji, mabati, nondo, marumaru na vinginevyo, ambavyo vinafungua fursa kubwa ya ukuaji wa viwanda.Hivyo, Waziri Mkuu amesema wadau mbalimbali wanapaswa kuitazama sekta ya nyumba kama sekta mtambuka katika kuleta maendeleo endelevu ya uchumi na jamii kwa ujumla.

“Napenda kutoa pongezi kwa Shirika la Nyumba la Taifa kwa kujenga jengo hili zuri na la kisasa kabisa hapa mjini Singida. Vilevile, jengo hili limeboresha na kupendezesha mandhari ya mji wa Singida kwa kiwango kikubwa kabisa,” amesema. 

Waziri Mkuu amesema amefurahi kusikia jengo hilo limesanifiwa na ujenzi wake kusimamiwa na Watanzania wenyewe, wakandarasi washauri wakiwa ni NHC wenyewe na kwamba Watanzania zaidi ya 600 walipata ajira wakati wa ujenzi.Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Bw. Felix Maagi alisema mradi wa jengo hilo la ofisi na biashara la Singidani lililogharimu sh. bilioni 3.4 ulianza Januari 26, 2015 na kukamilika Februari 17, 2018 na linatarajia kuliingizia shirika pango ya sh. milioni 420 kwa mwaka. Tayari asilimia 50 ya jengo hilo limepangishwa.

Mkurugenzi huyo alisema mbali na mradi huo wa Singidani, pia shirika limeendelea kukua na kuimarika katika utendaji wake ambapo thamani ya mali zote imeongozeka kutoka sh. trilioni 1.7 mwaka 2011 mpaka kufikia sh. trilioni 4.8 mwaka 2018.

Bw. Maagi alisema mapato ya shirika yamekua kutoka sh. bilioni 40 kwa mwaka 2011 hadi kufikia sh. bilioni 154 mwaka 2018.” Pia shirika linalipa gawio la Serikali kila mwaka na gawio hilo limekua kutoka sh. milioni 250 mwaka 2011 hadi sh. bilioni 1.2 kwa mwaka 2018,”Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi, wabunge wa mkoa wa Singida, viongozi wa dini na maafisa wa Serikali.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
JUMAMOSI, JUNI 30, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (kushoto) wakifurahia baada ya Waziri Mkuu kufungua Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) mjini Singida Juni 30, 2018. Kulia ni Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima na wapili kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Singida, Juma Kilimba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images