Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46327 articles
Browse latest View live

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA ZIARA YA GHAFLA BANDARINI DAR ES SALAAM KUKAGUA MATANKI YA MAFUTA YA KULA

$
0
0
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo na kuulia maswali alipowasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo na kuulia maswali alipowasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo na kuulia maswali alipowasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo na kuulia maswali alipowasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018. Wa pili kushoto ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage, kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Mhe. Doto James, mwenye kofia ngumu ya njano ni Mkurugenzi wa kampuni ya uingizaji mafuta nchini TLS & VOT Bw. Claudio Ghirardi, Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Profesa Olesante ole Gabriel anayefuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Kuchunguza mafuta ya Kula na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Joseph R. Buchweishaija.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa maelekezo na kuulia maswali alipowasili eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018, Nyuma yake ni Mkurugenzi wa kampuni ya uingizaji mafuta nchini TLS & VOT Bw. Claudio Ghirardi,
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akitoa pongezi kwa Bw. Ben Usage Asubisye baada ya kumpandisha cheo kuwa kamishna kamili kutoka Kaimu Kamishna wa Forodha na Bidhaa za Ndani katika Mamlaka ya Mapato (TRA) alipotembelea  eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiondoka eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiondoka eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018. Hapa akiagana na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Profesa Olesante ole Gabriel na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Kuchunguza mafuta ya Kula na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Joseph R. Buchweishaija.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akinunua mapapai na ndizi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akigawa mapapai na ndizi kwa wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akigawa mapapai na ndizi kwa wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akigawa mapapai na ndizi kwa wananchi nje ya eneo lenye matanki ya kuhifadhia mafuta ya kula baada ya kushushwa melini alipofanya safari ya ghafla kukagua uingizwaji na ugawaji wa ulipiaji wa ushuru  bidhaa hiyo kwenye bandari ya Dar es salaam leo Mei 15, 2018. Picha na IKULU


TBC, KWESE FREE SPORTS (TV1) KURUSHA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA (FIFA) BURE KWA KISWAHILI

$
0
0
Na Leandra Gabriel, blogu ya jamii

KITUO cha Televisheni ya Taifa (TBC), TBC Taifa na Kwese Free Sports (TV1)  wameingia makubaliano ya kurusha matangazo ya moja kwa moja ya michuano ya kombe la Dunia (FIFA World cup 2018) bure kabisa kwa lugha adhimu ya Kiswahili yatakayoanza 14 Juni hadi 15 Julai mwaka huu huko Moscow Urusi.

Akizungumza katika hafla ya makubaliano hayo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa TBC Dk.Ayoub Rioba amesema huu ni wakati wa wananchi kufurahia michuano hiyo kupitia televisheni ya taifa bure kabisa na kwa lugha ya Kiswahili.

Ameeleza kuwa watanzania wategemee mambo mazuri kupitia Kwese Free Sports wakiwa sambamba na TBC1 na TBC Taifa.Kwa upande wa Mkurugenzi wa Kwese Free Sports (TV1) Joseph Sayi amesema wameamua kuwaletea watanzania uhuru wa kufurahia bure kabisa kwa kuangalia michuano hiyo na kusikiliza kupitia TBC Taifa kwa lugha ya Kiswahili.

Meneja Masoko TBC Dafrosa Kimbory ameeleza kuwa licha ya watanzania kupata burudani hii pia ni fursa kwa wafanyabiashara kwa kutangaza bidhaa zao na wanaamini watawafikia watanzania wengi zaidi.

Aidha Mkurugenzi Kitengo cha Mawasiliano TBC amewashukuru Kwese kwa ushirikiano na kueleza kuwa hii ni fursa kwao katika kubadilishana uzoefu wa kiteknolojia na maudhui na matangazo hayo yataanza hivi punde na kuendelea hadi mashindano yatakapoisha.

Aidha Walter Kimaro mbunifu kutoka TV1 ameeleza kuwa wamejipanga na hadi sasa studio kabambe imeandaliwa kwa shughuli hiyo hivyo watanzania watarajie mambo mazuri kutoka kwao.

Akizungumza kuhusu Kwese Free Sports Mkurugenzi mtendaji wa Kwese Free Sports Mgope Kiwanga ameeleza kuwa Kwese Free Sports ilianzishwa mwaka 2014 ikijulikana kama TV1 na baadaye kuwa Kwese Free Sports na Chaneli hii imelenga kuwaburudisha waafrika na ipo kwenye nchi zaidi ya 10 Afrika.
Mkurugenzi mtendaji TBC Ayoub Rioba (katikati) na Mkurugenzi wa Kwese Free sports wakionesha hati ya makubaliano baina ya vituo hivyo yalilenga kurusha michuano ya kombe la dunia mwaka 2018.
Mkurugenzi mtendaji wa Kwese Free Sports (TV1) Joseph Swai akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kusaini makubaliano hayo.

SADC WATOA MAFUNZO KWA MAAFISA WA SERIKALI

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Innocent E. Shiyo akifungua Warsha ya Mafunzo ya Mfumo wa Ufuatialiaji na Tathmini wa SADC (SADC Results Based Online Monitoring and Evaluation System) kwa niaba ya Katibu Mkuu Prof. Aldof Mkenda, kulia kwake ni Meneja Mradi kutoka GIZ Bw. Robson Chakwama na wa mwisho ni mmoja wa Wakufunzi wa Warsha hiyo kutoka SADC Bi. Lerato Moleko 

Mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Wizara kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani chini ya Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), yametolewa kwa Maafisa wa Serikali na Taasisi za Umma, tarehe 15 - 17 Mei,2018 katika ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya Washiriki wakifuatilia mafunzo hayo.
Sehemu ya Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia mafunzo hayo.
Mkutano ukiendelea
Picha ya pamoja baada ya mkutano

TAARIFA KUHUSU WARSHA YA MAFUNZO JUU YA MFUMO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI WA SADC KWA MAAFISA WA SERIKALI NA TAASISI ZA UMMA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani chini ya Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) na Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) imeandaa Warsha ya Mafunzo ya Mfumo wa Ufuatialiaji na Tathmini wa SADC (SADC Results Based Online Monitoring and Evaluation System) kwa maafisa wa Serikali na taasisi za umma. Warsha hii inafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam kuanzia tarehe 15 hadi 17 Mei, 2018.

Lengo la warsha hii ni kuwezesha wizara na taasisi mbalimbali za Serikali kufahamu utendaji kazi wa mfumo huu wa SADC ambao unalenga kukusanya taarifa za utekelezaji wa itifaki na programu mbalimbali za maendeleo za SADC ambazo zinatekelezwa ndani ya nchi na kikanda kwa ujumla. 

Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa SADC uliridhiwa na Kikao cha Baraza la Mawaziri wa SADC kilichofanyika katika Falme ya Eswatini (Swaziland) mwezi Machi, 2017. Pamoja na mambo mengine, mfumo huu utawezesha pia nchi wanachama kufanya tathmini ya kina ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Kanda uliofanyiwa maboresho wa mwaka 2015-2020 (Revised Regional Indicative Strategic Plan, 2005 – 2020). Mpango huu ndio mkakati mkuu (blueprint) unaosimamia programu zote za kisiasa, kiuchumi na kijamii zinazotekelezwa SADC. 

Warsha hii itatuwezesha kufuatilia kwa karibu zaidi maendeleo ya utekelezaji wa itifaki na programu mbalimbali za SADC katika sekta zao na kutoa tathmini, na kubainisha fursa zinazopatikana kupitia uanachama wetu. Hadi sasa nchi za Lesotho, Mauritius, Falme ya Eswatini (Swaziland), Zambia na Zimbabwe tayari wameshapata mafunzo ya mfumo huu. Tanzania itakuwa ni nchi ya sita. 

Tanzania kama mwanachama hai na mwanzilishi wa Jumuiya hii, hadi kufikia Machi, 2018 imesaini jumla ya Itifaki 28 kati ya itifaki 31. Kati ya Itifaki zilizowekwa saini, jumla ya Itifaki 23 zimesharidhiwa na itifaki 5 ziko katika hatua mbalimbali za kuridhiwa. 

Aidha, kuna Itifaki nyingine tatu ambazo Tanzania bado haijaweka saini ambazo ni itifaki ya Ajira na Kazi 2014; Itifaki ya Utunzaji wa Mazingira kwa Maendeleo Endelevu 2014 na itifaki ya kulinda aina Mpya ya Mimea, 2017. Itafaki hizi zinatarajiwa kusainiwa wakati wa Mkutano wa 38 wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika mwezi Agosti, 2018 Windhoek, Namibia.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 15 Mei ,2018.

MFANYA BIASHARA MKOANI RUVUMA AKUTWA AMEHIFADHI BIDHAA CHOONI

$
0
0
Wafanyabiashara Watatu katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma,Wanashikiliwa na Jeshi la polisi kwa tuhuma za kutunza bidhaa katika maghala yasiyotambulika na serikali, huku mwingine akihifadhi bidhaa katika mazingira hatarishi kwa afya ya mwanadamu.( Chooni).

WAMACHINGA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA YA KUJISAJILI NA KUPATIWA VITAMBULISHO MAALUM

$
0
0
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akizindua usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi wakati wa hafla fupi ya uzinduzi huo iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Wa pili kushoto ni Meneja wa TRA Mkoa wa Arusha Bw. Faustine Mdessa.
Kiongozi wa Kikundi cha Levolosi Machinga Group Bw. Hassan Shayo maarufu kama G akikabidhiwa kitambulisho wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitabulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (wa tatu kulia) akiwa ameketi meza kuu wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Baadhi ya wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Fabian Daqqaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi baada ya uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao ulioandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika leo jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara wadogo.(PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO



Na Veronica Kazimoto,Arusha,

Wito umetolewa kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi hususani wamachinga kujisajili na hatimaye kupatiwa vitambulisho maalum kwa lengo la kusaidia biashara zao kutambulika, kukopesheka na kurahisisha mawasiliano ya usimamizi wa biashara hizo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo uliofanyika leo mkoani Arusha, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Fabian Daqqaro amesema ni muhimu wafanyabiashara kutumia fursa hii ya kujisajili ili kurasimisha biashara zao.

“Ni matumaini yangu kuwa, wafanyabiashara wengi wadogo wadogo mkoani hapa, mtatumia fursa hii kujisajili kwa sababu ninafahamu wengi wenu malengo yenu siyo kuwa wafanyabiashara wadogo muda wote, bali mtakuza biashara zenu na kuwa wafanyabiashara wakubwa na hii itawezesha kuchangia mapato ya Serikali,” alisema Daqqaro.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Kodi za Ndani kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Abdul Zuberi ameeleza kuwa, zoezi hili la kuwasajili na kuwapatia vitambulisho wafanyabiashara wadogo limetokana na juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

“Ni ukweli usiopingika kwamba, Rais wetu kwa nyakati tofauti amekuwa akiwapigania na kutaka wafanyabiashara wadogo wadogo kutambulika rasmi na kupatiwa vitambulisho ikiwa ni pamoja na kutafutiwa maeneo rafiki ya kufanyia biashara zao,” alisema Zuberi.

Ameongeza kuwa, kutokana na juhudi hizo za Rais Magufuli, Serikali kupitia Kikao cha Bunge la Bajeti la Mwaka wa Fedha 2017/2018, ilifanya marekebisho mbalimbali ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 ambapo moja ya marekebisho hayo ni kuwatambua na kuwapatia vitambulisho maalum wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi na jukumu hili limekasimiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Zuberi alisema kuwa, zoezi hili limeshafanyika katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mwanza na sasa limefanyika mkoani Arusha ambapo jumla ya vikundi 125 vya wafanyabiashara wadogo vinatarajiwa kusajiliwa na hadi sasa vikundi 25 vimeshatambuliwa vikiwa na jumla ya wafanyabiashara wadogo takribani 3,600 na kwa uwakilishi wafanyabiashara 100 wamepatiwa vitambulisho jijini hapa.

Naye Kiongozi wa Wamachinga mkoani Arusha Fredson Athumani, ameishukuru Serikali kwa kuwatambua rasmi na kusisitiza kuwa, atahakikisha anashirikiana na viongozi wenzake pamoja na Serikali kuwahamasisha wafanyabiashara wote wadogo kusajiliwa na kupata vitambulisho maalumu.

Zoezi la usajili na utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo walio kwenye sekta isiyo rasmi linafanyika chini ya Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Serikali za Mitaa, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) pamoja na Idara ya Uhamiaji.

MSANII DIAMOND AZINDUA WIMBO WA COLOURS KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA 2018 NCHINI URUSI

$
0
0
Msanii Diamond akipagawisha mashabiki wa Soka waliohudhuria katika Uzinduzi wa wimbo wa Colours maalum kwa ajili ya kombe la dunia 2018 linalofanyika nchini Urusi.
Mkurugenzi wa Coca-Cola Kwanza, Basil Gadzios akiongea machache kuhusu hafla hiyo,(kushoto) ni Meneja wa Coca-Cola nchini, David Karamagi.
Mkurugenzi wa Coca-Cola Kwanza, Basil Gadzios akikata keki wakati wa hafla hiyo. Msanii Diamond akisalimiana na Mameneja Waandamizi wa Coca-Cola. Msanii Peter Msechu na bendi yake wakipagawisha mashabiki wa soka waliohudhuria katika uzinduzi wa wimbo maalum alioshirikishwa msanii Diamond utakaosheresha Kombe la Dunia 2018.

MSANII wa Bongo fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewapagawisha vilivyo mashabiki wake wakati akiimba wimbo maalum utakaosherehesha Kombe la Dunia 2018 wimbo uitwao Colours nyimbo aliyoshirikiana na Jason Derulo, katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam. 

 Meneja wa Chapa ya Coca-Cola nchini, Sialouise Shayo, alisema kampuni ya Coca-Cola Tanzania ni moja ya mdhamini wa mashindano hayo makubwa ya soka duniani na inayofuraha kwa msanii kutoka Tanzania kushiriki kuimba wimbo maalum wa mashindano hayo na kwamba anaimani watanzania watapata mzuka wa soka dimbani na kujisikia sehemu ya mashindano.

Elimu ya Mlipa Kodi Kutolewa Mashuleni

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Serikali imeona umuhimu wa kuingiza elimu ya mlipa kodi kwenye mitaala ya elimu nchini ili kwajengea Watanzania tabia, mwenendo na mazoea ya kulipa kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Kauli hiyo imetolewa leo, Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Lupembe Mhe. Joram Ismael Hongoli juu ya kwa nini Serikali isiingize kwenye mitaala ya elimu somo la umuhimu wa kulipa kodi ili lifundishwe kuanzia shule ya msingi ili wananchi wapate uelewa wa kodi na waweze kulipa kodi kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea.

"Serikali inatambua umuhimu wa elimu ya mlipa kodi katika kumjengea mwananchi tabia ya kulipa kodi. Katika somo la Uraia na Maadili kuanzia darasa la III na kuendelea, mtaala umelenga kumjengea na kumuandaa mwanafunzi kuwa mwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya kila siku," alisema Mhe. Ole Nasha.

Vile vile mtaala umelenga kumjengea mwanafunzi kuiheshimu na kuithamini jamii yake kwa kuwa mwadilifu na mzalendo ikiwa ni pamoja na kutekeleza majukumu ya kitaifa ikiwemo kulipa kodi.

Aidha amesema, kutokana na umuhimu wa kuwajengea vijana utamaduni wa kulipa kodi, elimu ya mlipa kodi ni jambo muhimu, Serikali kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa kushirikisha Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) itaendelea kuboresha elimu hiyo ili isisitizwe na kuwekewa mkazo katika mitaala ya elimu kuanzia elimu ya Msingi.

Wakati huo huo, Mhe. Ole Nasha amesema Serikali ilifuta ada na michango ya lazima katika shule za umma ngazi ya elimu ya msingi (elimu ya awali hadi kidato cha Nne) na mpango huo hakuhusisha kidato cha tano na sita pamoja na shule binafsi.

Ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Seter Alexander Mahawe juu ya lini, Serikali itafuta ada kwa wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi.

"Ada na michango iliyokuwa inalipwa na wazazi/walezi kwa sasa hugharamiwa na Serikali. Mpango huu haukuzihusu shule binafsi pamoja na shule za Umma ngazi ya kidato cha Tano na Sita. Hivyo shule hizo zitaendelea na utaratibu wa wazazi/walezi kuchangia gharama za uendeshaji wa elimu ikiwemo kulipa ada za mitihani.

Hata hivyo amesema, Ili kuhakikisha mazingira rafiki katika utoaji wa elimu, Serikali imekuwa ikifanya majadiliano na sekta binafsi kwa lengo la kuondoa changamoto zinazowakabili ambapo hadi sasa Serikali imeweza kuondoa baadhi ya kodi na tozo mbalimbali ambazo awali walikuwa wakitozwa wamiliki wa shule binafsi.

Ametoa mfano wa kodi hizo kuwa ni kodi za mabango, kodi ya kuendeleza ufundi standi stadi (Skills Developmentt Levy), tozo ya Afya na Usalama mahala pa kazi (Occupational Safety and Health Administration - OSHA) na tozo ya zimamoto.

MAKAMU WA RAIS APOKEA VIFAA VYA UPASUAJI KUTOKA UBALOZI WA KUWAIT

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema uboreshaji wa huduma katika hospitali zetu za kibingwa kama MOI, zitaipunguzia Serikali mzigo wa kupeleka wagonjwa nje ya nchi na hivyo kutekeleza azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuboresha huduma za afya kwa wananchi.

Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa kupokea vifaa vya Chumba Cha Upasuaji wa Watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI) leo tarehe 15 Mei, 2018.“ Aidha kwa namna ya kipekee nakushukuru Mheshimiwa Balozi wewe binafsi na Serikali ya Kuwait kwa ushirikiano ambao mnaendelea kuipatia Serikali yetu ya awamu ya Tano katika Sekta mbalimbali za maendeleo lakini hasa hasa katika sekta ya afya” alishukuru Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais amesema kuwa Balozi wa Kuwait Mhe. Jasem Al Najem amekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza sekta ya Afya hapa nchini ambapo leo wamesaidia vifaa vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 258 ambavyo vitaiwezesha Taasisi kuimarisha utoaji wa huduma ya upasuaji hasa kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi.

Makamu wa Rais amesema msaada huo utaiwezesha Taasisi kuwa na chumba cha upasuaji ambacho kitakuwa maalum kwa watoto tu, hivyo idadi ya wagonjwa watakaopata huduma ya upasuaji itaongezeka kutoka 500-700 kwa mwezi, kufikia zaidi ya wagonjwa 1000 kwa mwezi na watahudumiwa kwa haraka zaidi.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndugulile  amesema Tanzania iatendelea kuimarisha uhusiano na nchi ya Kuwait kwani wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa msaada haswa msaada inayohusu sekta ya afya.Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Al Najem amesema kuwa Wananchi wa Kuwait wana mapenzi makubwa na Watanzania na kuahidi wataendelea kutoa msaada.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI).
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsalimia mtoto Daniella Wilfred Pallangyo mwenye umri wa miaka 8 ambaye ana matatizo ya kichwa kikubwa wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa kuwait nchini Mhe. Jasem Al Najem wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya baadhi ya vifaa vya upasuaji kutoka kwa Dkt. Karima Khaled wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo ya baadhi ya vifaa vya kisasa vya upasuaji vinavyoweza kuona mishipa na kuisoma kutoka kwa Dkt. Karima Khaled wakati wa hafla ya kupokea vifaa vya chumba cha upasuaji wa watoto vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa Taasisi ya Mifupa (MOI). (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 


Mamia wajinyakulia simu janja kutoka Tigo.

$
0
0
 Meneja Masoko wa Tigo, Mkoa wa Tanga Lilian Mwalongo (kulia) akimkabidhi Jeremiah Mwamlenga (kushoto) zawadi ya simu janja yenye uwezo wa 4G aina ya Tecno R6 baada ya kuibuka kama moja wa washindi wa promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus inayoendeshwa na kampuni ya Tigo. Jumla ya washindi 996 wamepatikana katika prmosheni hiyo inayoendelea.
 Meneja Masoko wa Tigo, Mkoa wa Tanga Lilian Mwalongo (kulia) akimkabidhi Mwanaisha Bakari  (kushoto) zawadi ya simu janja yenye uwezo wa 4G aina ya Tecno R6 baada ya kuibuka kama moja wa washindi wa promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus inayoendeshwa na kampuni ya Tigo. Jumla ya washindi 996 wamepatikana katika prmosheni hiyo inayoendelea. 
 
 Meneja Masoko wa Tigo, Mkoa wa Tanga Lilian Mwalongo (kulia) akimkabidhi Nuhu Munhambo (kushoto) zawadi ya simu janja yenye uwezo wa 4G aina ya Tecno R6 baada ya kuibuka kama moja wa washindi wa promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus inayoendeshwa na kampuni ya Tigo. Jumla ya washindi 996 wamepatikana katika prmosheni hiyo inayoendelea.  


· Wateja 996 wajinyakulia simu janja za TECNO R6 na bonasi za data bure baada ya kununua bando za intaneti kupitia *147*00#


Tanga, Mei 15, 2018 – Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ya Tigo Tanzania, imewazawadia washindi 996 kutoka sehemu mbali mbali nchini simu za zenye uwezo wa 4G aina ya Tecno R6 katika promosheni yake inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus

Akikabidhi zawadi kwa washindi 11 jiijini Tanga leo, Meneja Masoko wa Tigo, Mkoa wa Tanga Lilian Mwalongo alibainisha kuwa kupitia promosheni ya Nyaka Nyaka Bonus, Tigo itaongeza idadi ya watumiaji wa simu za kisasa pamoja na matumizi ya data nchini.

‘Ofa hii kabambe ni sehemu ya ubunifu wa Tigo unaoendana na mahitaji ya wateja na utakaowezesha kila mtu kufurahia huduma bora za mtandao wa Tigo 4G wenye kasi zaidi na ulioenea zaidi nchini,’ alisema.

Katika promosheni hiyo murwa ya Nyaka Nyaka Bonus, wateja wote wa Tigo wanaonunua bando za data kuanzia TZS 1,000 kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*00# wanapokea bonasi ya hadi 1GB intaneti bure papo kwa hapo kwa matumizi ya Facebook, WhatsApp, Instagram ama Twitter. Pamoja na hayo, wateja pia wanapata nafasi ya kushinda mojawapo ya simu janja zenye uwezo wa 4G aina ya TECNO R6 ambazo zinatolewa bure na Tigo

MOI SASA KUFANYA UPASUAJI KWA WAGONJWA 1000 KWA MWEZI ASEMA MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN.

$
0
0
NA WAMJW-DAR ES SALAAM

TAASISI ya Mifupa nchini MOI sasa itafanya upasuaji wa mifupa kwa wagonjwa wapatao 1000 kwa mwezi kutoka wagonjwa 500 mpaka 700 baada ya kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake kutoka kwa Serikali ya Kuwait .

Hayo yamesemwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa kuzindua na kupokea msaada wa chumba cha upasuaji na vifaa vyake vyenye thamani ya shilinigi milioni 186 leo katika Taasisi ya mifupa MOI leo jijini Dar es salaam.

“Hii ni faraja kubwa sana kwa Serikali kwani uboreshwaji wa huduma katika hospitali zetu za kibingwa kubwa kama MOI itaweza kuhudumia wagonjwa wengi Zaidi kutoka wagonjwa 700 kwa mwezi mpaka kufikia 1000 kwa mwezi” alisema Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Aidha Makamu wa Rais Samia Suluhu amesema kuwa anaishukuru Serikali ya Kuwait kupitia Balozi wake Jasem Al Najem kwa msaada huo kwani utaisaidia kwa kiasi kikubwa MOI katika kuboresha utoaji huduma hasa katika fani ya upasuaji kwa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi hapa nchini.

Kwa uapnde wake Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa kukamilika kwa vyumba hivi viwili vya upasuaji, kutaiwezesha Taasisi ya MOI kuwa na jumla ya vyumba vya upasuaji 8 kutoka 6 vilivyopo sasa na miongoni mwa vyumba hivi vya upasuaji kimoja kitakuwa maalumu kwa ajili ya watoto tu.

“MOI imeshatoa matibabu ya upasuaji kwa wagonjwa 1,670 ikiwemo upasuaji mifupa (wagonjwa 1,228), kubadilisha nyonga (wagonjwa 84), kubadilisha goti (wagonjwa 72), upasuaji wa uti wa mgongo (wagonjwa 109), ubongo (wagonjwa 64), na watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi (wagonjwa 113” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika kuimarisha na kuboresha afya za Watanzania jengo hilo pia litakuwa na vitanda 16 vya ICU (Intensive Care Unit) na 16 vya HDU (High Dependency Unit), hivyo kuimarisha huduma za tiba kwa wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.

Naye Balozi wa Kuwait Nchini Balozi Jasem Al Najem amesema kuwa Nchi ya Kuwait ipo mstari wa mbele katika kuhakikisha Hospitali na Vituo vya afya nchini Tanzania vinatoa huduma bora za Afya kwa kutumia Taaluma na ujuzi wa kisasa ikiwemo vifaa na vifaa tiba .

“Serikali ya Kuwait itakuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Tanzania katika kuimarisha afya za wananchi kwa kuendelea kutoa misaada mbalimbali ikiwemo vifaa,vifaa tiba na wataalamu wa afya na kutochoka katika hilo” alisema Balozi Najem.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MOI Bi. Zakia Mejhi amesema kuwa Taasisi yake imeokoa Bilioni 3 za kufanyia upasuaji kwani kwa sasa huduma hizo za kibingwa zinafanyika nchini kwa Shilingi Bilioni 12 kutoka Bilioni 15 za rufaa ya kwenda kutibiwa nje.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU VYETI VYA WAHITIMU PROGRAMU ZA UUGUZI UKUNGA NA SAYANSI SHIRIKISHI ZA AFYA

MKAZI DAR MBARONI KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA DAWA ZA BINADAMU ZILIZOISHA MUDA WAKE

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

JESHI la Polisi Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya kinamshikilia mkazi wa Tabata Segerea Chama jijini Dar es Salaam Joseph Jaumbe( 52) kwa tuhuma za  kukutwa na dawa za binadamu kinyume na sheria huku zingine zikiwa zimepita  muda wake wa matumizi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP), Alhaj Kabaleke Hassan amesema kupatikana kwa mtuhumiwa huyo kumetokana na taarifa kutoka kwa wananchi kuwa anahifadhi dawa za kulevya ndipo wakafanya uchunguzi na nyumbani kwake hakuwa na dawa za kulevya kama walivyopata taarifa.

Amesema baada ya uchunguzi ndipo wakakuta ana dawa za binadamu zikiwa katika mifuko mbambali huku zingine zikiwa katika mfuko wa sandarusi.

Kamanda Hassan amesema kuwa baada ya kuwasiliana na Mamlaka Chakula na Dawa (TFDA) walipata dawa makopo 12 yenye vidonge 1000 ambazo hazijasajiliwa na mamlaka hiyo, dawa za Serikali makopo mawili ya vidonge 1000 , dawa za zilizoisha matumizi yake uzito wa kilo 25, dawa bandia zilizoisha muda wake makopo saba yenye vidoge 1000 , dawa za mashirika ya msaada makopo 12 yenye dawa 1000 kila kopo pamoja na vingashio za dawa mbalimbali.

Kwa Meneja wa Kanda ya Mashariki ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Emmanuel Alphonce amesema Jeshi la Polisi liendelee kufanya uchunguzi kwa mtu huyo kujua dawa anakozipata ili kubaini mtandao huo.

Alphonce amesema dawa hizo ziingeingia mtaani zingeleta madhara kwa binadamu huku akishangaa kwa dawa hizo kufungwa mfuko wa kiroba pamoja na mifuko ya rambo. Amesema kuwa TFDA itaendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuweza kulinda watanzania katika matumizi ya dawa , vifaa tiba na vitendanishi.


Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP), Alhaj Kabaleke Hassan akizungumza na waandishi habari kuhusiana na kukamatwa kwa, Mkazi wa Tabata Segerea Chama Joseph Jaumbe( 52) kwa tuhuma kukutwa na dawa za binadamu kinyume na sheria huku zingine zikiwa zimepita muda wake wa matumizi , jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Kanda ya Mashariki ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Emmanuel Alphonce akizungumza kuhusiana na dawa zilizokamatwa na jeshi la Polisi Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya , jijini Dar es Salaam.
Dawa zilizokutwa kwa mtuhumiwa Joseph Jaumbe( 52) mkazi Mkazi wa Tabata Segerea Chama Joseph Jaumbe( 52)

DC SHINYANGA AZINDUA RASMI ZOEZI LA KUGAWA VITAMBULISHO VYA TAIFA KWA WANANCHI

$
0
0
Uzinduzi huo umefanyika leo Jumatano Mei 16,2018 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna uliopo katika ofisi za Manispaa ya Shinyanga. Mkuu huyo wa wilaya amekabidhi vitambulisho 12,918 kwa maafisa watendaji wa kata 17 za manispaa hiyo watakaokwenda kugawa vitambulisho hivyo kwa wananchi. 

“Hapa nchini, hili ni zoezi la kwanza la ugawaji vitambulisho kwa wananchi kwa kutumia ugawaji wa mkupuo,tunaanzia katika manispaa ya Shinyanga,nakabidhi rasmi vitambulisho hivi kwa maafisa watendaji wa kata ambao watagawa vitambulisho kwa wananchi”,alieleza Matiro. 

Aidha aliwataka maafisa watendaji kuwa makini na kugawa vitambulisho hivyo haraka huku akisisitiza kuwa vitambulisho hivyo havitolewi kwa ubaguzi bali kila mwananchi ana haki ya kupata. 

“Zoezi kujiandikisha linaendelea katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga lakini kwa upande wa manispaa ya Shinyanga tumemaliza zoezi la uandikishaji kinachoendelea sasa ni kugawa vitambulisho,hili ni zoezi endelevu wale ambao hawajiandikisha wafike katika ofisi za NIDA kujiandikisha ili wapate vitambulisho”,aliongeza Matiro. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo,Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau alisema tangu waanze zoezi la uandikishaji mwezi Septemba 2017 katika manispaa ya Shinyanga wamezalisha jumla ya vitambulisho 17,780 na tayari wameshagawa vitambulisho 3651 kwa watumishi wa umma na leo vitambulisho 12,918 kwa wananchi na zoezi la uandikishaji na ugawaji vitambulisho linaendelea. 

Naye Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa aliwasisitiza wananchi ambao bado hawajisajili waendelee kujisajili katika ofisi za Uhamiaji huku akiwataka kutoa ushirikiano kuwafichua watu wasiostahili kupata vitambulisho hivyo. 

“Uzalishaji wa vitambulisho unaendelea na tunatarajia hadi mwezi Desemba mwaka huu kila mwanachi awe na kitambulisho,NIDA inaomba wananchi kufichua watu wasiotahili kupata vitambulisho hivi wakiwemo wahamiaji haramu”,aliongeza Kapesa. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi aliwataka maafisa watendaji kutoendekeza urasimu katika ugawaji wa vitambulisho na hatarajii kusikia kitambulisho cha mwananchi kimepotea. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga. Kushoto ni Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Agnes Machiya. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akiwasisitiza maafisa watendaji wa kata kuwa makini katika zoezi la ugawaji vitambulisho kwa wananchi ili kuepuka changamoto inayoweza kujitokeza ya kupotea kwa vitambulisho.
Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau akisoma taarifa ya zoezi la uandikishaji na utoaji vitambulisho vya taifa katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Kitengo cha Usimamizi wa Vihatarishi NIDA Makao makuu,Stephen Kapesa akizungumzia kuhusu zoezi la utoaji vitambulisho vya taifa.
Maafisa watendaji,madiwani na watumishi mbalimbali wa manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la ugawaji vitambulisho.
Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Agnes Machiya akimkaribisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro kuzindua rasmi zoezi la ugawaji wa vitambulisho vya taifa kwa wananchi wa manispaa ya Shinyanga.
Sehemu ya vitambulisho 12,918 vilivyokabidhiwa kwa maafisa watendaji wa kata 17 za manispaa ya Shinyanga watakaokwenda kugawa vitambulisho hivyo kwa wananchi. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Agnes Machiya wakati akizindua rasmi zoezi la kugawa vitambulisho vya taifa (NIDA) kwa wananchi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi akionesha kitambulisho chake cha taifa baada ya kukabidhiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa diwani wa kata ya Lubaga Mchungaji Obedi Jilala (CHADEMA).
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akimkabidhi Kitambulisho cha taifa diwani wa viti Maalum Manispaa ya Shinyanga Mariam Nyangaka (CCM).
Diwani wa kata ya Kizumbi,Reuben Kitinya akipokea kitambulisho cha taifa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akikabidhi Vitambulisho vya taifa kwa afisa mtendaji wa kata ya Mwawaza,Nhiga Nhiga ili akavigawe kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga mheshimiwa Josephine Matiro akikabidhi Vitambulisho vya taifa kwa afisa mtendaji wa kata ya Ndembezi,Felister Msemelwa ili akavigawe kwa wananchi wa kata hiyo.
Mratibu wa NIDA mkoa wa Shinyanga Nathanael Fredrick Njau akisisitiza jambo wakati wa zoezi la ugawaji vitambulisho vya taifa kwa maafisa watendaji wa kata za manispaa ya Shinyanga.
Maafisa watendaji na madiwani wakiwa ukumbini.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

JENGO LA BEIT EL AJAB KUFANYIWA MATENGENEZO MAKUBWA KUTOKA SEREKALI YA OMAN

$
0
0
  JENGO la kihistoria la Beit el ajab liliopo Forodhani Mjini Zanzibar linalotarajiwa kufanyiwa matengenezo makubwa na Serekali ya Oman baada ya kubomoka baadhi ya sehemu zake miaka michache iliyopita.
  WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza katika hafla ya kumuaga  Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk ( kushoto) iliyofanyika katika jengo la kihistoria la Beit el ajab Forodhani. Wa kwanza (kulia)  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Dkt. Amina  Ameir  na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Khadija Bakari Ali.
 KATIBU MKUU Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk akizungumza na Viongozi wa Wizara ya Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar kuhusu matengenezo makubwa ya Jengo la Beit el ajab ambalo lilibomoka miaka michache iliyopita, (kulia)  Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo.
 WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi zawadi mbalimbali Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk baada ya kumaliza ziara ya kutembelea Maeneo mbalimbali ya historia ya Zanzibar.
 WAZIRI wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akiagana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Kale wa Oman Salim Mohammed Almaharouk baada ya kumaliza ziara yake Zanzibar.
(Picha na Abdalla Omar Maelzo Zanzibar).

BENKI YA CRDB KUFANYA MKUTANO WA WANAHISA JIJINI ARUSHA

$
0
0
Na Pamela Mollel,Arusha


Benki ya CRDB inatarajia kufanya mkutano wake wa ishirini na tatu(23)wa wanahisa wa benki hiyo katika ukumbi wa Kimataifa wa AICC ulipo jijini Arusha na kuhudhuriwa na watu zaidi ya Elfu moja.


Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei alisema kuwa mkutano huo wa wanahisa unatarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu


Dkt.Kimei alisema kuwa Mkutano huo wa wanahisa wa benki ya CRDB utatanguliwa na semina maalumu kwa wanahisa wa benki hiyo utakaofanyika tarehe 18 mwenzi huu ambapo pamoja na mambo mengine wanahisa watapata fursa ya kufahamu mambo mbalimbali kibenki


Alisema kuwa agenda za mkutano huo ni kupokea na kupitisha taarifa za fedha na ripoti za wakurugenzi kwa mwaka uliopita tarehe 31 mwezi Disemba 2017,kuhidhinisha taarifa maalumu ya gawiyo wa mwaka ,kuchagua wajumbe wa bodi ,kuhidhinisha uchaguzi wa wakaguzi wa hesabu wanaokupalika kisheria


Dkt Kimei alitoa rai kwa wanahisa wa benki hiyo kuuhudhuria kwa wingi katika mkutano huo mkuu huku akiongeza kuwa kwa mwanahisa ambaye hataweza kuudhuria anahaki ya kuchagua mwakilishi au wawakilishi kuudhuria na kupiga kura kwa niaba yake.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha leo ,kuhusu mkutano mkuu wa ishirini na tatu wa Wanahisa unaotarajia kuanza rasmi tatehe 18 na 19 utakaohudhuriwa na wanahisa zaidi ya Elfu moja  katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC uliopo jijini Arusha(Habari Picha na Pamela Mollel,Arusha)
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei kushoto,kulia ni Mkurugenzi wa mikopo James Mabula  kulia 
Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa masoko wa CRDB Jadi Ngwale,kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt.Charles Kimei
Waandishi wa habari wakiwa wanafanya mahojiano ya kina kuhusu mkutano huo

KAMPUNI YA UCHIMBAJI MADINI YA TANZANITE ONE YAKUBALI KUILIPA SERIKALI FIDIA MARA BAADA YA KUFIKIA MAKUBALIANO

$
0
0
 Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande wa Serikali, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akitia saini pamoja na Mkurugenzi wa Tanzanite One Faisal Juma mara baada ya kufikia makubaliano na  Kampuni hiyo ya Uchimbaji wa Madini ambayo imekubali kulipa fidia kwa Serikali pamoja na mambo mengine ya Kimkataba.  
 Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande wa Serikali Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akibadilishana hati za Makubaliano na Mkurugenzi wa Tanzanite One Faisal Juma mara baada ya Kampuni hiyo ya Uchimbaji wa Madini kukubali kulipa fidia kwa Serikali.  
 Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande wa Serikali Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi  akiwa na watendaji wa Kampuni ya Uchimbaji madini ya Tanzanite One wakati akielekea kusaini hati za makubaliano baina ya kampuni hiyo na Serikali.
 Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande wa Serikali Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza mara baada ya kuhitimisha mazungumzo na kusaini hati ya Makubaliano yatakayoiwezesha Serikali kulipwa fidia na Kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzaniate.
 Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande Kampuni ya Tanzanite One Faisal Juma akizungumza mara baada ya kuhitimisha mazungumzo na kusaini hati ya Makubaliano yatakayoiwezesha Serikali kulipwa fidia na Kampuni ya uchimbaji madini ya Tanzaniate.
Kiongozi wa Kamati ya Majadiliano kwa upande wa Serikali Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akiagana na Mkurugenzi wa Tanzanite One Faisal Juma mara baada ya Kampuni hiyo ya Uchimbaji wa Madini kukubali kulipa fidia kwa Serikali pamoja na mambo mengine ya Kimkataba kama walivyokubaliana. PICHA NA IKULU



BALOZI KIDATA AMUAGA MAKAMU WA RAIS LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kuzungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada, Balozi Alphayo Kidata, ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Balozi Kidata ambaye aliapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada tarehe 10, Mei 2018 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Balozi Kidata alifika leo kuona Makamu wa Rais na kumuaga rasmi tayari kwa kwenda kulitumikia Taifa kwenye kituo chake kipya cha kazi nchini Canada. 

Makamu wa Rais, Mhe. Samia amempongeza na kumtakia kazi njema ambapo alimtaka kwenda kufanya yale nchi imeelekeza haswa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya Uchumi wa Viwanda.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Mhe. Alphayo Kidata aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Tanzania nchini Canada Mhe. Alphayo Kidata aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja  na Balozi wa Tanzania nchini Canada Mhe. Alphayo Kidata mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuaga kabla ya kwenda kwenye kituo chake kipya cha kazi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) ​\

UJENZI WA KIVUKO KIPYA CHA MV. MWANZA KUKAMILIKA MWEZI JUNI

$
0
0

Na. Theresia Mwami - TEMESA

Serikali kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), imeahidi kukamilika kwa ujenzi kivuko kipya cha Kigongo Busisi (MV. MWANZA) unaofanywa kampuni ya kizalendo ya Songoro Marine Transport Boatyard ifikapo mwezi Juni 2018. Kivuko hicho kitakuwa na uwezo wa kubeba tani 250, ambazo ni sawa na kubeba magari 36 na abiria 1,000 kwa wakati mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari, wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa kivuko hicho, uliofanywa na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya TEMESA mapema leo, Mtendaji Mkuu wa TEMESA Dkt. Mussa Iddi Mgwatu alisema ujenzi huo unagharimu jumla ya shilingi za kitanzania bilioni 8.9 na ulianza rasmi tarehe 28/08/2017 na kwamba tayari umekamilika kwa asilimia 95.

“Namuagiza Mkandarasi kuhakikisha kuwa ujenzi wa kivuko hiki unakamilika kwa aslimia 100 ifikapo mwezi Juni,2018 kama ilivyoainishwa kwenye mkataba ili kuweza kuboresha zaidi huduma ya uvushaji abiria na mizigo yao katika eneo Kigongo – Busisi”, aliongeza Dkt. Mgwatu.

Aliongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa kivuko cha MV. MWANZA kutafanya eneo la Kigongo Busisi kuboresha zaidi huduma za uvushaji kwani kwa sasa tayari kuna Kivuko cha MV. Misungwi ambacho pia kina tani 250, MV. Sengerema tani 170 na MV. Sabasaba tani 85.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya ushauri ya TEMESA Brigedia Jenerali Mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri alisema kuwa, serikali inalengo la kuboresha hali ya maisha ya wananchi, kwa kuwawekea miundombinu salama ya vivuko, ili kuhakikisha wanapata huduma bora na salama wakati wote. 

Aliongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi huo kutatoa nafasi ya ukarabati mkubwa wa vivuko vingine vinavyotoa huduma kati ya Kigongo na Busisi kufanyika kwa awamu. Aidha alitumia nafasi hiyo pia kuwapongeza TEMESA kwa kazi nzuri ya usimamizi wa ujenzi wa kivuko hicho, kwa kuhakikisha kuwa unakamilika kwa wakati kama ilivyo kwenye mkataba wa ujenzi wake.

Nae Mkurugenzi Kampuni ya Songoro Marine Transaport Boat Yard Ltd, Major Songoro, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kuiamini kampuni hiyo na kuahidi kuimaliza kazi hiyo kwa haraka na ustadi mkubwa.
Kivuko kipya cha MV. MWANZA chenye uwezo wa kubeba tani 250, ambazo ni sawa na kubeba magari 36 na abiria 1,000 kwa wakati mmoja, kinachojengwa na kampuni ya kizalendo ya Songoro Marine Transport Boatyard ambacho kinagharimu jumla ya shilingi za kitanzania bilioni 8.9 fedha kutoka serikali ya Tanzania. Kitatoa huduma kati kigongo na Busisi Mkoani Mwanza.
Kivuko kipya cha MV. MWANZA chenye uwezo wa kubeba tani 250, ambazo ni sawa na kubeba magari 36 na abiria 1,000 kwa wakati mmoja, kinachojengwa na kampuni ya kizalendo ya Songoro Marine Transport Boatyard ambacho kinagharimu jumla ya shilingi za kitanzania bilioni 8.9 fedha kutoka serikali ya Tanzania. Kitatoa huduma kati kigongo na Busisi Mkoani Mwanza.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TEMESA Brigedia Jenerali Mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri, akipanda ngazi kukagua ujenzi wa kivuko kipya cha MV. MWANZA, nyuma yake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro Marine Transaport Boat Yard Ltd (inayojenga kivuko hicho) Salehe Songoro, akifuatiwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme( TEMESA) Dkt. Mussa Iddi Mgwatu.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme( TEMESA) Dkt. Mussa Iddi Mgwatu (wa kwanza kulia) akiongea na waandishi wa habari baada ya ukaguzi wa kivuko kipya cha MV. MWANZA kulia kwake mwenye miwani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TEMESA Brigedia Jenerali Mstaafu Mhandisi Mabula Mashauri.Picha na Kitengo cha Habri na Mawasiliano TEMESA

Article 1

$
0
0
Na Veronica Kazimoto,Arusha

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imekamata malori mawili yenye bidhaa mbalimbali eneo la Loliondo Wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha kupitia njia ya magendo yakitokea nchini Kenya zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 20.

Akizungumza leo jijini Arusha, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Charles Kichere amesema kuwa, malori hayo yenye namba T 985 AJP na T 840 ABF yalikamatwa usiku wa Mei 10 2018 na kusisitiza kuwa wafanyabiashara wenye bidhaa hizo wamevunja sheria kwa kuwa hawakulipa kodi stahiki kama inavyotakiwa.

Kichere amefafanua kuwa, wafanyabiashara wenye bidhaa hizi zilizokamatwa, wamevunja kifungu cha sheria namba 82 na 200 cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi ya Mwaka 2015 na Sheria ya Forodha ya Afrika Mashariki ya Mwaka 2004. Hivyo kwa Sheria hizi, wafanyabiashara hawa wanatakiwa kulipa kodi pamoja na faini ya shilingi milioni 39 na magari yao kutaifishwa.

"Kwa ujumla bidhaa hizi zote zina thamani ya shilingi 20,037,330.15 ambayo kodi ya bidhaa hizi ni shillingi 28,524,758.11 na adhabu au faini ya bidhaa hizi ni shilingi 10,768,665.08. Hivyo jumla ya mapato yanayotakiwa kulipwa Serikalini ni shilingi 39,293,423.19," alieleza Kichere.

Amezitaja bidhaa zilizokamatwa kuwa ni pamoja na mifuko 362 ya sukari yenye uzito wa kilo 50 kila mmoja, maboksi 40 ya mafuta ya kula yanayoitwa Karibu, maboksi matatu ya mafuta ya kula yanayoitwa Daria, magaloni 100 ya mafuta ya kula yanayoitwa Nyata na maboksi matatu ya viungo vya mboga 

Kufuatia tukio hilo, Kamishna Mkuu Kichere amewakumbusha wafanyabiashara wote kuzingatia taratibu za uingizaji bidhaa nchini ili kuepuka hasara kwenye biashara zao na kuongeza kuwa, TRA haitavumilia ukiukwaji wowote utakaofanywa na wafanyabiashara kwa kutozingatia sheria na taratibu hizo.

KAMPUNI ZA UKANDARASI ZAIDI YA 70 WAJITOLEA KUJENGA MITARO YA BARABARA JIJINI DAR BURE

$
0
0
Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

KAMPUNI za ukandarasi zaidi ya 70 zimeamua kujitolea kujenga mitaro ya barabara mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam bure kama sehemu ya kuunga mkono jitihada za Mkuu wa mkoa huo Paul Makonda.

Hatua hiyo inakuja baada ya Makonda kufanya ziara usiku na mchana kwa lengo la kujionea uharibifu mkubwa wa barabara uliotokana na ukosefu wa mitaro ya maji na kuamua kuwashirikisha wakandarasi hao ambao walipokea kwa mikono miwili ombi hilo. 

Taarifa yake kwa vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam Makonda pia amewaagiza wenyeviti wa mitaa kuratibu idadi ya barabara zisizokuwa na mitaro kwenye mitaa yao kisha kupeleka kwa Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini(TARURA) Wilaya kwa ajili ya kupatiwa kampuni itakayojenga mitaro hiyo. 

Aidha Makonda amezishukuru kampuni zilizojitolea kujenga mitaro hiyo bure jambo litakalosaidia kuokoa mabilion ya fedha za Serikali.

Kwa upande wao wakandarasi wamesema wamejiandaa vizuri kuanzia vifaa na wataalamu kwaajili ya ujenzi huo huku baadhi yao wakiwa tayari wameanza ujenzi kwenye baadhi ya mitaa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wakandarasi wa kampuni mbalimbali zilizojitolea kujenga mitaro ya barabara mbalimbali katika Jiji la Dar es Salaam, bure kama sehemu ya kuunga mkono jitihada za Mkuu wa mkoa .
Viewing all 46327 articles
Browse latest View live




Latest Images