Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

maadhimisho siku ya Malaria Duniani,Kitaifa kufanyika Kasulu mkoani Kigoma

$
0
0
Tanzania inatarajia kuungana na nchi zingine duniani kwenye kuadhimisha siku ya Malaria Duniani ambayo ufanyika April 25 kila mwaka.

Maadhimisho hayo ya kitaifa yatafanyika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma huku Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii akitarajiwa kuzindua ripoti ya hali ya Malaria nchini.

Akiongea jijini Dar es Salaam leo, Waziri Nyoni ambaye ni Mkurugenzi wa Miradi kutoka VectorWorks alisema kutakuwa na shamra shamra mbali mbali kuanzia tarehe 22 April kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo.

VectorWorks ni mradi wa miaka mitano wa kupamba na malaria hapa nchini umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria na kuratibiwa na John Hopkins Center for Communications.

‘Sisi kazi yetu ni kuhakikisha hali ya ugonjwa wa malaria inapungua. Kwa sababu hiyo, tumekuwa na zoezi endelevu la kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa kila kaya hapa nchini. Vile vile, tunatumia vituo vya afya kuwafikia walengwa wakuu ambao ni akinamama waoenda kliniki na watoto wenye umri chini ya mwaka mmoja, alisema Nyoni.

Akina mama wanaonza kliniki ni lazima wapatiwe chandarua chenye dawa ya muda mrefu bure. Hii njia bora ya kujikinga na mbu waenezao malaria. Vile vile tunafanya kazi kwa kushirikiani na Serikali kupitia Wizara ya Afya kitengo cha kupamba na Malaria nchini ambao wamekuwa wakipuliza dawa yenye viatilifu kwenye maeneo yenye masalia ya mbu. 

Tumepiga hatua kubwa kupunguza malaria hapa Tanzania kwa hivyo natoa wito wangu kwa kila Mtanzania kuhakikisha analala kwenye chandarua kwenye dawa ya muda mrefu, aliongeza Nyoni.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni mimi natokomeza malaria, wewe je?

WIZARA YAAMSHA ARI YA WANANCHI KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO

$
0
0
Wizara ya Afya, Mandeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imedhamiria kuendelea na kampeni ya kuamsha ari ya Wananchi kushiriki katika Miradi ya Maendeleo na katika kipindi cha Julai 2017 hadi Machi 2018, Wizara imefanya uhamasishaji katika Mikoa 11 ya Iringa, Dodoma, Mwanza, Pwani, Kigoma, Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Kagera na Shinyanga.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2017/2018 na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Bungeni Mjini Dodoma.

Waziri Ummy ameeleza kuwa uhamasishaji huu umewezesha ujenzi wa majengo ya Kituo cha Afya Mondo, Wilaya ya Misungwi (Mwanza); ujenzi wa bwawa la maji Maghangu Mpwapwa (Dodoma); ujenzi wa Zahanati Ufyambe (Iringa); ujenzi wa shule ya sekondari na kituo cha afya – Uvinza (Kigoma); ujenzi wa shule ya sekondari na kituo cha afya – Mpanda (Katavi); ujenzi wa kituo cha afya –  Sumbawanga (Rukwa); ujenzi wa kituo cha afya – Mbozi (Songwe); ujenzi wa shule ya sekondari – Manispaa ya Mbeya (Mbeya).

Pia amesema kuwa Kampeni hii ya Kuamsha Ari ya Wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo imesaidia  kuchangia fedha na vifaa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya mtumishi wa Makazi ya wazee (Kagera); kuzindua Kituo cha Mkono kwa Mkono (One Stop Centre) cha wahanga wa ukatili wa kijinsia na ukatili wa watoto Wilaya ya Kahama (Shinyanga) na ujenzi wa madarasa mawili katika Kijiji cha Chambasi, Kisarawe (Pwani).

Aidha Mhe. Ummy Mwalimu ameongeza kuwa Wizara imeendelea kushirikiana na Mashirika yasiyo ya Kiserikali katika kutekelza miradi mbalimbali ya maendeleo na kutoa Huduma kwa jamii na kwa kipindi cha kwa kipindi cha Julai 2017 hadi Machi, 2018, jumla ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali192 yalisajiliwa.

Mhe.Ummy Mwalimu alisema pia imeongeza Ustawi wa watoto wazee na jamii nchini kwa kushirikiana na wadau imeendelea kutekeleza Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18 – 2021/22). Katika mwaka 2017/18, Kazi zilizofanyika chini ya mpango huu ni kutoa elimu kuhusu athari za mila na desturi zenye madhara kwa jamii ikiwemo ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni kwa makundi mbalimbali katika jamii.

Kwa upande wao baadhi ya wabunge waliochangia Hotuba wameipongeza Wizara kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo na kutoa huduma kwa wananchi.

Naye Mwanyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Mandeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba ameiomba Wizara kuajiri Maafisa Maendeleo ya Jamii nchini ili kuondokana na upungufu uliopo kwani Maafisa hawa ni watu muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum Zanzibar Mhe. Najma Giga amesema kuwa Wizara inatakiwa kukaa na wadau ili kupata namna bora ya kutokomeza tatizo la ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto kwani limekuwa ni tatizo linalosumbua katika sehemu nyingi hapa nchini.

“Naomba suala hili la Ukatili wa kijinsia dhidi ya Wanawake na Watoto tuondokane nalo maana tatizo hilo linalowakumba na kuwasababishia ukatili mkubwa watoto na wanawake wenzetu” alisisitiza Mhe. Najma.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwasilisha Utekelezaji wa Bajeti ya kwa Mwakawa fedha  2017/2018 na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa fedha 2018/2019 Bungeni Mjini Dodoma.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI UMOJA,AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inatekeleza Mpango wa Miaka Mitano (2017- 2021), wa kusogeza huduma karibu na wateja kwa kuanzisha ofisi za Kikanda katika Kanda ya Kaskazini, Kusini, Kati, Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Zanzibar kwa awamu. 

Hayo yameelezwa Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakati akijibu maswali ya msingi ya Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Jacqueline Msongozi (CCM), aliyetaka kujua lini Serikali itapeleka Benki ya Kilimo katika Mkoa wa Ruvuma ili wananchi waweze kukopeshwa.

Aidha, Mhe. Msongozi alitaka kufahamu utayari wa Serikali kupunguza riba ya mikopo wanayokopeshwa Wakulima katika Benki hiyo.

Akijibu maswali hayo, Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa hadi kufikia Juni 30, 2018 Ofisi ya Kanda ya Kati, Dodoma, itakuwa imefunguliwa ambayo pia itakuwa ni Makao Mkauu ya Benki hiyo.

“Baada ya ufunguzi wa ofisi ya Kanda ya Kati kukamilika Benki Itafanya uchambuzi wa fursa zilizopo Kikanda na hivyo kuchukua hatua na taratibu za kufungua ofisi nyingine kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa Benki hiyo inatoa mikopo kwa kutumia mfumo wa makundi, kundi la kwanza wakulima wadogo wadogo kwa riba ya asilimia 8- 12, kundi la pili la miradi mikubwa ya kilimo kwa asilimia 12 – 16 kwa mwaka na kundi la mwisho ni mikopo ya ushirika ambapo riba yake inaendana na hali ya soko la matumizi ya mkopo.

Kuhusu kupunguza riba kwa wakopaji, Dkt. Kijaji alibainisha kuwa majadiliano ya kiwango cha riba yanaweza kufanyika kulingana na historia ya mkopaji.

SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI HOJA YA CAG KUHUSU TRILIONI 1.5

NEWZ ALERT AGNESS MASOGANGE AFARIKI DUNIA JIONI YA LEO

$
0
0
Msanii Video Queen Agness Gerald (Masogange)  amefariki Dunia jioni ya leo  katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo jijini Dar Es Salaam baada ya jana kuzidiwa na kukimbizwa hospitalini hapo.

Taarifa kutoka kwa vyanzo vya uhakika vimeeleza kuwa Agness alizidiwa jana mapema na kukimbizwa katika hospitali hiyo kwa matibabu ya haraka,lakini kwa bahati mbaya mapema leo jioni  alifariki Dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo,ambapo mpaka sasa haijainishwa wazi Ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.

Aidha Michuzi Blog imeshuhudia Mwili wa Marehemu Agness Masogange ukiondolewa kituo cha Afya cha Dkt Ngoma  na kupelekwa kuhifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili jioni hii. 

Tutazidi kuwaleta taarifa zaidi kuhusiana na msiba huu,

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi-Amen 

OBC yatoa magari 15 kwa wizara ya maliasili

$
0
0
Magari 15 yaliyokabidhiwa na Kampuni ya OBC ya Loliondo.
Mkurugenzi idara ya wanyamapori, Nebbo Mwina akikata utepe kuashiria uzinduzi wa magari 15 aina ya Toyota Land cruiser yenye thamani ya shilingi Billion 1.5 yaliyotolewa na kampuni ya uwindaji ya OBC,ya Loliondo kwa ajili ya shughuli za kuzuia ujangili na uhifadhi. Hafla hiyo ilifanyika jana jiji Dar es Salaam.
Mkurugenzi idara ya wanyamapori, Nebbo Mwina akijaribu kuendesha moja ya magari 15 aina ya Toyota Land cruiser yenye thamani ya shilingi Billion 1.5 yaliyokabidhiwa na kampuni ya uwindaji OBC,ya Loliondo kwa ajili ya shughuli za kuzuia ujangili na uhifadhi. Hafla hiyo ilifanyika jana jiji Dar es Salaam


KAMPUNI ya uwindaji ya Otterlo Business Corporation Limited (OBC) imekabidhi magari 15 kwa wizara ya maliasili na Utalii kwa ajili ya kusaidia kulinda rasilimali ya wanyamapori nchini.

Magari hayo aina ya Toyota Landcruiser yalikabidhiwa jana kwa Mkurugenzi wa idara ya wanyamapori, Nebbo Mwina,katika ofisi za Wizara ya Maliasili, jijini Dar es Salaam.

Akikabidhi magari hayo yenye thamani ya Zaidi ya sh. Bilioni 1.5, Mkurugenzi msaidizi wa OBC, Molloimet Yohana, alisema kuwa msaada huo ni mahususi kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye mapambano dhidi ya ujangili na ulinzi wa wanyamapori.

“Huu ni mwendelezo wa azma ya serikali ya UAE na OBC katika kuunga mkono mapambano hayo kwani tumekuwa tukifanya hivyo mara kwa mara,”alisema.Alisema ushiriki wao katika uhifadhi wanyamapori utaendelea kwani ni mpango endelevu na kamwe hawatasita kusaidia pale itakapobidi.Akipokea msaada huo, Mwina alisema serikali inatambua mchango mkubwa wa OBC ambao imekuwa ikitoa katika sekta hiyo,na kuwataka kuendeleza mahusiano na kutokatishwa tamaa na maneno yanayozungumzwa juu ya kampuni hiyo.

“Napenda kusema kwamba OBC tumekuwa na mahusiano na nyinyi ya muda mrefu tumepata misaada yenu kwa muda mrefu kwa hiyo mahusiano yenu na sisi ni ya muda mrefu na ni mazuri hivyo tunawaomba kwamba muendeze hayo mahusiano yenu msikate tamaa tunajua kuna maneno yanasemwahuku na kule yakijaribu kuwakatisha tamaa juhudi zenu naomba msikate tamaa kwa hayo maneno ambayo yanasemwa Chini chini “Alisema

Alisema ni vyema OBC ikawapuuza watu ambao wamekuwa wakisema kampuni hiyo hafanyi kazi yake inavyotakiwa lakini wao kama wizara tunatambua kwamba wamekuwa ni msaada msaada mkubwa kwa serikali na uhifadhi.

Akishukuru kwa msaada huo mkurugenzi wa mamlaka ya usimamizi wanyamapori nchini (TAWA )Dk. James Wakibara alishukuru OBC kwa msaada huo ambao alisema utarahisisha utendaji kazi wa mamlaka hiyo ambayo inakabiliwa na changamoto ya rasilimali fedha,watu na vifaa.

“Lazima tutoe shukrani zetu za dhati kwa uongozi wa OBC kwanza kwa kufikiria hili wazo lakini pia kwa kujitoa,nguvu waliyoifanya,jitihada walizozifanya,matumizi waliofanya hadi leo tunapata hivi vifaa ambavyo vitatusaidia mtufikishie salam zetu kwa mkurugenzi ambae hakuweza kufika lakini Mwambie tunashukuru na Tunaheshimu kwa msaada huu uliotolewa.”alisema 

Amesema gari ni kitu mihimu sana katika shughuli ya uhifadhi kwa sababu inawezesha kufika mahali popote kwa kuwa ni vigumu sana kulinda mapori kwa kutembea kwa miguu.

“Ni vizuri kwamba mtu anapokusaidia lazima atakuwa amewaza hapa kuna tatizo kwa hiyo katika tatizo hili na mimi nisaidie,kwa hiyo ule moyo tu wa kusema kwamba niwasaidie wenzangu Ndio hazina kubwa kuliko hata kile kilichotolewa”,alisema Dk.Wakibara.

VETA MOSHI WAJIVUNIA AJIRA ZA MOJA KWA MOJA WANAZOPATA WANAOSOMA KATIKA CHUONI HAPO

$
0
0

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii, MOSHI

CHUO cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Moshi kimeaanzisha na kuendeleza mafunzo ya kozi ya Uzalishaji mvuke yenye fursa kubwa katika soko pamoja na kozi ya mitambo katika uchimbaji wa madini ambao umetoa ndani na nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi habari waliotembelea katika Chuo cha VETA Moshi, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Douglas Mlulla amesema moja ya mafanikio yao ni kwamba vijana wanaosoma hapo wana uhakika wa ajira za moja kwa moja kutokana na ushirikiano na kampuni za uchimbaji madini.

Amesema VETA Moshi ni chuo kina kozi ambazo zina wigo mkubwa wa ajira katika uchimbaji wa madini, pamoja kozi uzalishaji mvuke ambapo sehehu ya viwanda vya vinywaji ni lazima kuwepo kwa wataalam wa kozi hiyo.

Hata hivyo amesema mwitikio wa vijana ni mdogo kutokana na kutofahamu umuhimu wa ufundi stadi ambao ndio unaajiri watu kwa sehemu kubwa, hivyo ameashauri vijana kuchangamkia fursa hata kama anashahada ni vema akaongeza na mafunzo ya ufundi stadi.

Pia amesemakozi ya Uendeshaji wa mitambomikubwa imeonekana kuvutia vijana wengi wakiwemo wasichana.Mmoja wanafunzi wa kozi hiyo, Happiness Steven amesema yeye anashahada ya kwanza rasilimali watu na baada ya kuona changamoto ya ajira ameamua kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi na kufanikiwa kupata kazi katika kiwanda na kuwa afisa uajiri katika kiwanda hicho.

Amesema kozi ya uchomeleaji na uchongaji wa vyuma alivutiwa na kuamua kujiunga nayo licha ya mtazamo uliokuwepo kwa muda mrefu kuwa hiyo ni kozi kwa ajili ya wanaume.Amesema waliohitimu Shahada wajiongeze katika ufundi stadi na hatimaye changamoto ya ajira watakuwa wameimaliza kwani hakuna kazi isipokuwa ni watu kuchagua kazi za kufanya kwa taaluma waliozonazo.

Kwa upande wa Mratibu wa Mradi wa IMTT Chuo hicho,Theresia Mosha amesema ushirikiano kati yao na kampuni za uchimbaji madini umetoa fursa vijana wengi waliopita katika mradi huo pamoja na waliosomea kozi ya uzalishaji mvuke kupata ajira.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Moshi , Douglas Mlulla akizungumza na waandishi habari walipotembelea chuo hicho kuhusiana na fursa ambazo zinapatikana katika chuo.
.Afisa Rasilimali Watu wa Kiwanda cha Press , Forge & Metal Works (PFM2000) na Munufaika mafunzo ya ufundi Stadi VETA Moshi, Happiness Steven akizungumza wa kuhusiana na vijana kuchangamkia kozi ya ufundi stadi licha ya kuwa na shahada walizozipata.
Munufaika mafunzo ya ufundi Stadi VETA Moshi Happiness Steven akionesha  umahiri alioupata katika mafunzo ya ufundi Stadi katika chuo cha VETA Moshi.
Mwanafunzi wa kozi ya Mitambo Mikubwa,Happiness Rwechungura akioneha jinsi wanavypata mafunzo ufundi stadi katika chuo cha VETA Moshi.
Mkufunzi wa Kozi ya Mtambo wa kuzalishaji Mvuke , Mosana Marcus akionesha jinsi mtambo unavyoweza kuzalisha mvuke

Rais Magufuli amteua Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Tabora

MATUKIO KATIKA PICHA BALOZI WA ITALIA NCHINI TANZANIA AMTEMBELEA SPIKA OFISINI MJINI DODOMA

$
0
0
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akisalimiana na Balozi wa Italia nchini Tanzania Mheshimiwa Roberto Mengoni wakati Balozi huyo alipomtembelea ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma 
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akimsikiliza Balozi wa Italia nchini Tanzania Mheshimiwa Roberto Mengoni wakati alipomtembelea ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma 
Naibu Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akimsikiliza Balozi wa Italia nchini Tanzania Mheshimiwa Roberto Mengoni wakati Balozi huyo alipotembelea Ofisi za Bunge Mjini Dodoma

UCHIMBAJI WA MCHANGA KWENYE MITO DAR ES SALAAM WAPIGWA MARUFUKU.

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Selemani Jafo (Mb) amepiga marufuku uchimbaji wa mchanga unaoendelea katika mito mbalimbali Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Jafo ametoa katazo hilo wakati wa ziara yake ya kuangalia athari zilizotokana na mafuriko katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala leo 20 Aprili 2018. Akiwa katika kata ya Gongolamboto eneo la Ulongoni A na Ulongoni B, amejionea jinsi ambavyo mafuriko yaliyotokana na wingi wa mvua zilizonyesha yalivyoharibu madaraja na kuacha athari kubwa kwa wananchi. 

“Nimejionea mwenyewe jinsi ambavyo mvua hizi zimeleta athari kubwa hapa na kusababisha mawasiliano kukatika baina yenu nyinyi na wenzenu wa upande wa pili. Lakini niwaambie kuwa kwa sehemu kubwa baadhi ya wananchi wanachangia uharibifu wa maeneo haya kutokana na uchimbaji wa mchanga unaoendelea na kusababisha uharibufu katika kingo za mito pamoja na miundombinu hii iliyojengwa,” alieleza Mhe. Jafo

Waziri ameeleza kuwa miundombinu inajengwa kwa gharama kubwa na Serikali lakini wapo watu ambao wanaiharibu kwa makusudi kutokana na uchimbaji wa mchanga, hivyo akaeleza kuwa Serikali haitavumilia swala hilo.“Hatuwezi kuzizuia mvua zisinyeshe lakini hatuwezi kuvumilia kuwaacha watu wanaoharibu miundombinu na kingo za mto kwa kuchimba mchanga. Hivyo kuanzia leo napiga marufuku uchimbaji wa mchanga katika maeneo yote ya mito ya Dar es Salaam,” ameagiza Waziri Jafo.

Amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Sofia Mjema aliyeambatana naye katika ziara hiyo kusimamia agizo hilo pamoja Mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla wake, na kuwakamata wale wote watakaokaidi agizo hilo.Aidha Mhe. Jafo ameeleza kuwa Serikali inajitahidi kurejesha mawasiliano katika maeneo hayo yaliyoathirika kwa kujenga madaraja ya muda wakati wakisubiri ukarabati mkubwa kufanyika.

Ameeleza kuwa amewasiliana na waziri wa Ulinzi Mhe. Hussein Mwinyi ili Jeshi la Ulinzi lisaidie katika kutengeneza madaraja hayo. “Waziri wa Ulinzi ameniahidi kuwa anatuma wataalamu wa Jeshi kufanya tathmini ya uharifu ili kutengeneza madaraja hayo ya muda,” amesema Jafo.Awali, katika ziara hiyo Mhe. Jafo ametembelea Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi “DART” katika kituo cha Jangwani na kuangalia athari zilizoltokana na mafuriko.

Akiwa katika kituo hicho cha Jangwani amepongeza uongozi wa UDART kwa kuzingatia agizo lake alilolitoa awali la kuyahamisha mabasi katika kituo hicho na kuyalaza Kimara pamoja na Gerezani hivyo kufanikiwa kuokoa mabasi hayo.“Mmeniambia kuwa yale mabasi niliyoyaona hapa wakati wa mafuriko ni yale ambayo yalikuwa hayatembei kabisa na hata hivyo mmetoa vifaa amabavyo vingeharibika katika mabasi hayo na mengine yote mliyatoa hapa. Nawapongeza kwa hilo,” ameeleza Jafo.

Mhe.Jafo amesema kuwa mafuriko hutoke duniani kote marekani, china na kwingineko na hatuwezi kuyazuia, lakini ni akasema kuwa ni lazima wadau na wananchi wote wazingatie tahadhari zinazotolewa ikiwa ni pamoja na kuhama mabondeni ili kupunguza athari.Pia ameeleza kuwa Serikali inampango mkubwa wa kuutengeneza Mto Msimbazi kupitia Mradi wa DMDP, ambapo takribani dola za kimarekani 20 milioni zimetengwa ili kupata suluhisho la kudumu. Alieleza kuwa kazi hiyo inatarajiwa kuanza mwezi Septemba, 2018 mara baada ya kumalizika kwa usanifu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo akiwa na viongozi wengine akiwemo Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema wakionyeshana  maeneo ya daraja yalivyo haribika na mafuriko.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Selemani Jafo akiwa na viongozi wengine katika ukaguzi wa athari za mvua.
 Maeneo yaliyoharibiwa na Mvua
 Maeneo yaliyoharibiwa na mvua
 Maeneo yaliyoharibiwa na mvua
 Maeneo yaliyoharibiwa na mvua
Athari za mafuriko

RC TABORA: VIONGOZI WA DINI TUASAIDIENI KUWAHIMIZA WATOTO WAKIKE WAJE KWENYE CHANJO YA HPV VACCINE JUMATATU

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akifungua jana semina ya siku moja ya Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi ya Mkoa huo ikiwa ni maandalizi ya chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi itakayoanza tarehe 23 Mwezi huu mkoani kote.

Viongozi wa dini mbalimbali na wageni waalikwa wakiwa katika semina ya siku moja ya Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi ya Mkoa huo ikiwa ni maandalizi ya chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi itakayoanza tarehe 23 Mwezi huu mkoani kote.Picha na Tiganya Vincent


NA TIGANYA VINCENT,RS TABORA

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imewaomba viongozi wa dini mbalimbali kusaidia kuwaelimisha waumini wao juu ya umuhimu wa watoto wenye umri wa miaka 14 kupatiwa chanjo ya kuwakinga na saratani ya mlango wa kizazi ili wajitokeza kwa wingi kupatiwa huduma hiyo kuanzia wiki ijayo.


Kauli hiyo imetolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati anafungua semina ya siku moja ya Kamati ya Huduma ya Afya ya Msingi ya Mkoa huo.Alisema viongozi hao wanayo nguvu kubwa na wafuasi wengi wakitumia fursa hiyo watasaidia kufikisha ujumbe sahihi na kwa wakati na hivyo kuokoa maisha ya wanawake hapa baadaye.

Mwanri alisema ugunduzi wa Chanjo hiyo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) ni habari njema ambayo inapaswa kuwafikia wananchi wengi ili waweze kuwapeleka watoto wao wa kike kwa ajili ya kuwakinga na ugonjwa wa saratani ya mlango ambao umekuwa ukisababisha upotevu wa maisha ya wanawake wengi.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa watoto wa kike kutojihusisha na vitendo vya ngono katika umri mdogo kwa sababu vinaweza kuharatisha maisha yao na kujikuta wakipata saratani yamlango wa kizazi.Aliongeza kwa watu wazima ni vema wakawa na mpenzi mmoja kwa ajili ya kuwakinga wakinamama kupata tatizo hilo.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ametoa wito kwa wananchi kujenga tabia ya kwenda mara kwa mara kupima afya zao ili kuweza kujikinga mapema kabla ya tatizo halijawa kubwa.Alisema mara nyingi watu wamekuwa na tabia ya kwenda Hospitali wanapokuwa wanauma na ndio wanapokuta tatizo limeshakuwa kubwa zaidi .

Naye Sheikh wa Mkoa wa Tabora Ibrahim Mavumbi ameipongeza Srikali ya Mkoa wa Tabora kwa kuwashirikisha katika utoaji elimu juu ya umuhimu wa kuwahimiza waumini wao kuhakikisha wanawapewa watoto wanatakiwa kupatiwa chanzo ili waweze kuchanjwa kwa ajili ya kuwakinga na saratani ya mlango wa kizazi.

Aidha aliitaka jamii kuendelea kutii maagizo ya Mwenyezi Mungu ambayo yanakataza zinaa kwa njia na umri wowote ikiwa ni hatua ya awali nay a msingi ya kuwakinga watoto wa kike kupata maambukizi ambaye yanaweza kuwapelekea kupata tatizo hilo.

Kwa upande wa Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tabora Askofu Elias Chakupewa alisema kuwa wao wakiwa viongozi wa Kiroho watajitahidi kutumia nafasi yangu katika kuungana na Serikali katika kuhakikisha wanaelimisha juu ya wananchi kuwapeleka watoto wenye umri kupatiwa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi ili kuokoa maisha yao ya baadaye.

Alisema wao kama kanisa pamoja na jukumu lao la kufundisha mafundisho ya kiroho pia wanalo jukumu la kuangalia maendeleo ya waumini wao na wananchi wengine ya kielimu na kiafya kwa maendeleo ya Taifa.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora(RMO) Gunin Patrick Kamba alisema katika uzinduzi wa chanjo unaonza mapema wiki ijayo mkoani kote zaidi wasichana elfu 30 wenye umri wa miaka ( 14 ) wanatarajiwa kupata chanjo ya kinga ya Saratani ya mlango wa kizazi .

Alisema kuwa chanjo hiyo maalumu kwa watoto wa kike wenye umri wa miaka 14 itazinduliwa Aprili 23 mwaka huu katika Manispaa ya Tabora na Mkuu wa Mkoa kwa niaba ya maeneo mengine mkoani humo.

Chanjo hiyo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) hapa nchini ilizinduliwa hivi karibuni na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.

RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA MAJAJI 10, Naibu MWanasheria Mkuu, Wakili Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka

$
0
0
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Simu: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Tovuti : www.ikulu.go.tz              

Faksi: 255-22-2113425


OFISI YA RAIS,
     IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,   
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 20 Aprili, 2018 amewaapisha Majaji 10 wa Mahakama Kuu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wakili Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka aliowateua tarehe 15 Aprili, 2018.
Majaji walioapishwa ni Mhe. Elvin Claud Mgeta, Mhe. Elinaza Benjamin Luvanda, Mhe. Yose Joseph Mlyambina, Mhe. Immaculata Kajetan Banzi, Mhe. Mustapher Mohamed Siyani, Mhe. Paul Joel Ngwembe, Mhe. Agnes Zephania Mgeyekwa, Mhe. Stephen Murimi Magoiga, Mhe. Thadeo Marco Mwenempazi na Mhe. Butamo Kasuka Philip.
Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Dkt. Evaristo Emmanuel Longopa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Edson Athanas Makallo kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Dkt. Julius Clement Mashamba kuwa Wakili Mkuu wa Serikali na Dkt. Ally Saleh Possi kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.
Baada ya kuapishwa kwao, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kufanya uteuzi wa Majaji hao na kwamba uteuzi huo utasaidia kupunguza mrundikano wa mashauri ya Mahakama Kuu ambapo sasa Jaji mmoja atakuwa akisikiliza wastani wa mashauri 460 kwa mwaka ikilinganishwa na Jaji mmoja kusikiliza mashauri 535 kabla ya uteuzi huo.
Mhe. Prof. Juma amewahusia Majaji wapya umuhimu wa kuzingatia majukumu yao, miiko na kuwa mfano bora wa kusimamia sheria na pia ametoa wito kwa wananchi kuwa makini wanapopata taarifa za mahakama kutoka vyanzo visivyo rasmi kwani kumekuwa na upotoshaji wa makusudi.
“Mhe. Rais Bajeti yetu ya mwaka 2017/18 ilikuwa Shilingi Bilioni 125, bajeti tuliyopangiwa sasa 2018/19 ni Shilingi Bilioni 141, sasa wanaosema bajeti imeshuka, imeshuka kwa namna gani? labda ni kushuka kwa kugeuza. Kwa upande wa bajeti ya maendeleo kwa mwaka 2017/18 ilikuwa Shilingi Bilioni 18, mwaka huu tumepangiwa Shilingi Bilioni 35” amesisitiza Mhe. Prof. Juma.
Akizungumza baada ya salamu za Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Majaji na viongozi wote walioapishwa na ametoa wito kwao kutekeleza majukumu yao kwa kumtanguliza Mwenyezi Mungu, kuweka mbele maslahi ya Taifa na kutenda haki hasa kwa Watanzania wanyonge wakiwemo wajane na watu masikini ambao hudhulumiwa katika vyombo vya kutolea haki.
Mhe. Rais Magufuli ameungana na Jaji Mkuu wa Tanzania kuwatahadharisha Watanzania dhidi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kufanya upotoshaji wa taarifa na kuleta madhara katika jamii na ametaka Majaji na mamlaka nyingine zichukue hatua za kisheria dhidi ya wanaofanya upotoshaji huo.
Mhe. Rais Magufuli ametaja upotoshaji mmojawapo kuwa ni madai kwamba Serikali imeiba Shilingi Trilioni 1.5, na akamuuliza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Mussa Juma Assad ambaye amejibu sio kweli kwamba fedha hizo zimeibwa.
“Nilikuwa nasoma mahali wanasema Serikali imeiba Shilingi Trilioni 1.5, siku moja nikampigia CAG, kwamba mbona kwenye ripoti yako uliyonisomea Ikulu hukunieleza huu wizi wa Trilioni 1.5? Kwa sababu ungenisomea siku hiyo hiyo ningefukuza watu, kama nimefukuza wakurugenzi watatu siku hiyo hiyo kwa sababu ya hati chafu, hawa wa Trilioni 1.5 uliwaficha wapi? Nimejaribu kupita kwenye ripoti siioni mahali palipoandikwa zimepotea Trilioni 1.5, Prof. Assad akaniambia hakuna kitu kama hicho, nikamuuliza Katibu Mkuu akasema hakuna kitu kama hicho” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Viongozi wote walioapishwa pia wamekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela, na hafla ya kuapishwa kwao imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, Makatibu Wakuu, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama na viongozi wa dini.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
20 Aprili, 2018
  Majaji 10 wa Mahakama Kuu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wakili Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuapishwa na Ikulu jijini Dar es salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 20 Aprili, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Elvin Claud Mgeta kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Aprili, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe.Thadeo Marco Mwenempazi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Aprili, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha  Dkt. Ally Saleh Possi kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Aprili, 2018
 Viongozi wote walioapishwa wakila kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kikiongozwa na Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji Mstaafu Harold Nsekela Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Aprili, 2018
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiongea machache baada ya kuwaapisha Majaji 10 wa Mahakama Kuu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Wakili Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Ikulu jijini Dar es salaam leo tarehe 20 Aprili, 2018

TUCTA MEI MOSI 2018 IRINGA ; HII NI HESHIMA KUBWA KWA MKOA WA IRINGA RC MASENZA

$
0
0
WAKATI maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani kwa nchini Tanzania yaliyoandaliwa na shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) yakitaraji kufanyika mkoani Iringa kitaifa mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza amesema mkoa wa Iringa kuwa mwenyeji wa mei mosi ni heshima kubwa katika Taifa .

Akizungumza na wanahabari leo ofisini kwake kuhusiana na maandalizi ya Mei Mosi Kitaifa alisema kuwa mkoa wa Iringa umeteuliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi atakuwa ni Rais Dkt John Magufuli .

Alisema kuwa katika maadhimisho hayo ya Mei Mosi kitaifa kauli mbiu ni Kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kulenge kuboresha mafao ya wafanyakazi na kuwa kupitia maadhimisho hayo wakazi wa mkoa wa Iringa na wafanyabiashara watapata fursa kubwa ya kujitangaza pamoja na kuonyesha shughuli zao.
Mkuu  wa mkoa wa  Iringa  Amina  Juma Masenza
Rais wa shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Tumaini Vyamhokya katikati akiongoza kuimba wimbo wa wafanyakazi wakati wa kikao na  wanahabari mjini  Iringa .
Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Juma Masenza akila kiapo mbele ya Rais Dkt Jonh Magufuli pindi alipoteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Iringa

Katika maadhimisho hayo ambayo kilele chake kitafanyika uwanja wa Samora mjini Iringa kabla ya kilele kutakuwa na michezo mbali mbali kama mpira wa miguu, kuvuta kamba ,bonanza la michezo tofauti ,mpira wa pete ambayo yote yameanza toka April 17 hadi April 30 mwaka huu .

Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa Iringa mwenyeji wa Mei mosi kitaifa mwaka 2018 Bi Amina Masenza alisema sherehe hizo zitahusisha maonyesho ya shughuli ,huduma na bidhaa mbali mbali za wafanyakazi ,taasisi za umma na binafsi ,wawekezaji na wajasiliamali zitakazofanyika uwanja wa Kichangani Kihesa mjini hapa .

Hata hivyo alisema kwa ajili ya kuufanya mkoa wa Iringa uzidi kuwa fursa kwa wageni kutembelea vivutio vya utalii kama hifadhi ya Ruaha na vingine serikali imekaa na wafanyabiashara wa nyumba za kulala wageni na Hoteli ili kuepuka kutumia mei mosi kupandisha gharama za vyumba kwa wageni .

Bi Masenza amewataka wananchi wa mkoa wa Iringa na wafanyakazi wote kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais wetu mpendwa wetu Dkt John Magufuli 


Na MatukiodaimaBlog 

CCM Z’BAR YAWATAKA WANANCHI KUFUATA MAELEKEZO YA SMZ

$
0
0
NYUMBA ya Farid Issa iliyoezuliwa na upepo na mvua katika shehiab ya Pwani mchangani.
KATIBU wa NEC, Idara ya organazesheni Bakari Hamad Khamis akionyeshwa nyumba za shehia ya sebleni zilizoathiriwa na mvua.

SHEHA wa shehia ya sebleni Khalfan Salum(wa kwanza kushoto) akitoa maelezo ya athari za nyumba zilizopata maafa katika eneo la shehia ya Kwa wazee.
NYUMBA zilizoingiliwa na maji katika shehia ya Kwa wazee Wilaya ya Mjini Unguja.

……………….

NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimewataka wananchi kufuata maelekezo na ushauri wa Serikali juu ya kujikinga na maafa yanayotokana na mvua za masika.

Rai hiyo imetolewa na Katibu wa Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Bakar Hamad Khamis, alipotembelea maeneo mbali mbali yaliyoathiriwa na mvua katika Mikoa ya Mjini na Kaskazini Unguja.

Alisema kila mwananchi anatakiwa kuchukua tahadhari kwa kufuata maelekezo ya Serikali hasa kuepuka kujenga katika maeneo hatarishi kwa lengo la kujikinga na madhara hayo yanayosababishwa na mvua za masika zinazonyesha kila mwaka nchini.

Bakari alisema lengo la ziara hiyo ni kuwafariji wananchi wote waliopata majanga sambamba na kuitaka serikali kupitia mfuko wa maafa iharakishe misaada kwa wananchi ambao nyumba zao zimebomolewa na mvua hizo.

Akizungumza Katibu wa Wilaya ya Mjini Fatma Shomari, alisema katika Wilaya hiyo jumla ya nyumba 68 zimeathiriwa na mvua hizo pamoja na kusababisha kifo cha mtoto Ramadhan Juma Khamis (4) katika shehiya ya Sebleni.

“Bado tunaendelea kukusanya taarifa za wananchi mbali mbali waliopata maafa katika Wilaya yetu ili tuziwasilishe kwa serikali kwa ajili ya hatua stahiki za misaada”, alisema Katibu huyo.

Kwa upande wake sheha wa shehia ya Kwa wazee Khalfan Salum alieleza kuwa jumla ya nyumba 130 zenye wakaazi wanaokisiwa kufikia 1300 zimeathiriwa na mvua hizo na wananchi wa maeneo hayo wamehama na kutafuta hifadhi kwa majirani waliopo katika maeneo salama.

Akizungumza mkaazi wa eneo hilo Haji Makame ‘London’ aliiomba serikali kupitia Manispaa ya mjini kuharakisha mradi wa ujenzi wa mtaro mkubwa utakaokuwa ukisafirisha maji yanayotwaama katika maeneo hayo ambayo kwa sasa ni makaazi ya kudumu kwa wananchi.

Aidha Katibu wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mulla Othaman Zubeir alisema zaidi ya nyumba 18 na boti sita za uvuvi aina ya mtando na ngwanda zimeharibiwa na mvua zilizonyesha katika maeneo mbali mbali ya mkoa huo na kuathiri mali za wananchi.

Mbali na maafa hayo Mulla alifafanua kuwa maafa hayo yamesababisha kifo cha mtoto wa mwaka mmoja aliyetumbukia katika shimo la takataka katika shehia ya Chaani kubwa Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja.

Akiwafariji wananchi wa Mkoa huo Katibu wa NEC, Idara ya Organazesheni CCM Zanzibar Bakari Hamad aliuagiza uongozi wa CCM Mkoa huo kusaidia shughuli za ujenzi wa nyumba ya Mkaazi wa shehia ya Mwange Mbaki Makame Ali (54), ambaye nyumba yake imeanguka kutokana na mvua zinazonyesha nchini.

Katibu huo wa Organazesheni Bakari aliwasihi wananchi waliopata maafa kuwa wavumilivu kwa kipindi hichi, huku Chama Cha Mapinduzi kikiendelea kuisimamia serikali iharakishe misaada kwa wananchi waliopata maafa hayo.

Naye mkaazi wa shehia ya Mkwajuni Kero Chumu Juma alikipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa kuendeleza utamaduni wa waasisi wa ASP waliokuwa wakiwatembelea wananchi mara kwa mara kwa lengo la kuratibu changamoto zao na hatimaye kuzitafutia ufumbuzi kupitia serikali.

“Nimefurahi sana kuona uongozi wa CCM umekuja kunifariji kwani utamaduni huu ulikuwa umepotea kwa muda mrefu na kwa sasa naona umerudi kwa kasi kubwa, hii inaonyesha wazi kuwa Chama kinarudi kwa wananchi wake”, alisema Mkaazi huyo ambaye ukuta wa nyumba yake ulianguka kutokana na mvua hizo.

Maeneo yaliyotembelewa katika ziara hiyo ni shehia ya Sebleni, Kwa wazee, eneo la Mtumwa jeni, Pwani mchangani, Chaani kubwa, shehia ya Kibeni, Shehia ya Mwange, shehia ya Mkwajuni na Mwanga pwani.

WAZIRI MWAKYEMBE ATUMA SALAMU ZA POLE KWA FAMILIA YA ALIYEKUWA MWANAMUZIKI WA BENDI YA KING KIKI

KIONGOZI MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA BUHIGWE KWA KUJENGA MAJENGO YENYE UBORA KWA GHARAMA NAFUU

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru jitaifa charles Kabeho ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma, kwa kuzingatia na kujenga majengo yenye ubora kwa kutumia gharama nafuu.

Hivyo amezishauri Halmashauri zingine kuiga mfano huo ambapo amesema hayo wakati akikagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne na ofisi mbili katika Shule ya Msingi Kishanga, vilivyo gharimu zaidi ya Sh. milioni 100 pamoja na ujenzi wa Kituo cha Afya na Nyumba ya mganga Janda kilicho gharimu kiasi cha Sh. milioni 400, ikiwa ni fedha ya ndani.

Kiongozi huyo wakati akizindua na kuweka jiwe la msingi jana amesema amefurahishwa na viongozi wa Halmashauri hiyo kwa ubunifu walioufanya na uzalendo baada ya kupatiwa fedha za Serikali na kuamua kujenga ujenzi usio tumia gharama kubwa ili kuwasaidia wananchi kupata huduma mapema.

Aidha Kabeho ametoa mwito kwa makandarasi waliipewa zabuni za kujenga miradi katika Halmashauri mbalimbali nchini kufanya kazi kwa kuzingatia viwango vilivyo ainishwa kwenye mikataba yao na kuhakikisha miradi wanayoijenga inakuwa ni yenye ubora .Mwito huo aliutoa wilayani wakati akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kusisitiza kuwa kwa sasa serikali imetoa kipaumbele kwa makandarasi wazawa kufanya Kazi ili kuharakisha maendeleo ya nchi yao hivyo wafanye Kazi vizuri.

Hata hivyo aliwaagiza wananchi kuhakikisha wanailinda na kuitunza miradi yote ya maendeleo ili vizazi vijavyo navyo viendelee kunufaika na miradi hiyo kwani serikali imejipanga kutatua kero za wananchi kwa kuwawekea huduma za kijamii karibu ikiwa ni pamoja na hospitali, vituo vya afya na Shule ili wanafunzi wapate elimu karibu na maeneo wanayoishi.Wakizungumza mara baada ya uzinduzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi Kishanga, Bernadetha Samsoni alisema, wanaipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa kazi kubwa anayoifanya.Pia wanaiomba Serikali kuendelea kufanya miradi hiyo katika vijiji vingine ili kuondoa kero za upatikanaji huduma kwa Wananchi.

Jhoni Bhalagaye ni Mkazi wa Kijiji cha Janda amesema wanaipongeza Serikali kwa kuwajengea Kituo cha afya kwani mwanzoni walikuwa wakipata shida kupata huduma za afya katika Wilaya ya Kasulu."Lakini baada ya Kituo hicho kikikamilika tutakuwa na amani na tutapata huduma vizuri," amesema.

Kazi nyingine zilizofanywa na Mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Buhigwe ni kuweka jiwe la msingi Katika ujenzi wa Barabara ya Muzeze Kigogwe, inayotekelezwa na serikali kupitia wakala wa Barabara vijijini (TARURA )kuzindua jengo la kituo cha biashara katika kiiiji cha Buhigwe na kuzindua klabu ya wapinga rushwa katika shule ya msingi Biharu na uzinduzi wa Nyumba bora katika Kijiji cha Muyama .

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akutana na uongozi wa juu wa NBC jijini Dar

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (kushoto), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kulia), wakati alipotembelea ofisi za makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.  Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja BInafsi wa nbc, Filbert Mponzi.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (kushoto), akimsikiliza  Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi wakati alipotembelea ofisi za makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka (kulia), akimsikiliza  Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto), wakati Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa benki hiyo, Filbert Mponzi akiangalia  wakati alipotembelea ofisi za makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

SIKU YA MALARIA DUNIANI,KITAIFA KUFANYIKA KASULU MKOANI KIGOMA,WAZIRI UMMY MGENI RASMI

WAZIRI TIZEBA AAGIZA MKURUGENZI WA BODI YA KOROSHO KUSIMAMISHWA KAZI

$
0
0
Waziri wa wizara ya kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Dodoma, Jumamosi 21 Aprili 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-WK
Waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini taarifa ya Waziri wa wizara ya kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba ofisini kwake mjini Dodoma, Jumamosi 21 Aprili 2018.
Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe akisikiliza maagizo ya kusitisha mkatanba wa kazi wa Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania, Leo Jumamosi 21 Aprili 2018.

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo


Waziri wa wizara ya kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe kusitisha mkataba wa kazi wa Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania Ndg Hassan Jarufo.


Waziri Tizeba ametoa agizo hilo kwa katibu mkuu wa wizara hiyo leo Jumamosi 21 Aprili 2018 wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Dodoma ikiwa ni muda mchache mara baada ya kumalizika kwa dhifa ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa.


Akielezea sababu za kuagiza kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo, Mhe. Dkt Tizeba alisema kuwa hayo yamejili baada ya kuangalia mwenendo wa Ndg Jarufo na kutafakari jinsi zao la korosho linavyoendeshwa, ikiwa ni pamoja na kutoridhishwa na upatikanaji wa viuwatilifu kwa wakati.


Aidha, Mkataba huo umesitishwa kuanzia leo tarehe 21 Aprili 2018 hivyo Katibu Mkuu wa wizara hiyo atapaswa kufanya taratibu zote za kiutumishi ikiwa ni pamoja na kumpatia taarifa haraka muhusika na utekelezaji wake kuanza haraka.


Alisema ndani ya muda mfupi Wizara ya kilimo itamtangaza Kaimu Mkurugenzi wa Bodi hiyo ili kuchukua nafasi hiyo kuendeleza kusimamia sekta hiyo.


“Hizi hatua tunazochukua ni kuhakikisha kuwa wadau wakubwa wa korosho ambao ni wakulima wanaendelea kunufaika na zao lao, hivyo wakulima wasiwe na wasiwasi kwani pamoja na kuondolewa Mkurugenzi huyo lakini shughuli za serikali zitaendelea kama kawaida na maslahi yao yatasimamiwa ipasavyo” Alikaririwa Mhe. Dkt Tizeba
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images