Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live

BONGO MOVIE KUIBUA VIPAJI VIPYA NA KUHUBIRI AMANI, UPENDO NA UZALENDO TANZANIA

0
0

Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza ambaye ni Mratibu wa Tamasha la Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi, Steve Nyerere akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuelezea Tamasha la ‘Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi,’ Pembeni (kushoto) ni Msanii Shamsa Ford na kulia ni Msanii Wolper.
Wasanii waliohudhuria utambulisho wa Tamasha la ‘Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi.
Msanii wa maigizo na filamu nchini, Single Mtambalike maarufu kwa jina la Richie akifafanua machache.

Na Mwandishi Wetu.
Kundi la Wasanii wa Muziki, Bongo Fleva, Mziki wa Singeli na Filamu nchini wanataraji kutoa elimu ya kujikwamua kiuchumi vijana wa Iringa katika Viwanja vya Mwembe Togwa mkoani Iringa.
Akizungumza wakati wa utambulisho wa Mwenyekiti wa Uzalendo Kwanza ambaye ni Mratibu wa Tamasha la Iringa ya Kwetu, Kijana Amka tufanye kazi, Steve Nyerere amesema kuwa Tamasha hilo lenye kauli mbiu ya ‘Kijana wa Iringa inuka tukafanye kazi,’.
“Tunataka tuwaonyeshe vijana kuwa huyu Wolper, JB au Steve Nyerere awakuwa wasanii maarufu moja kwa moja bali kuna maisha walipitia mpaka kufikia hapo hivyo wanatakiwa kufanya kazi ili waweze kufikia mafanikio kutoka kijiweni na kuwa wajasilimali kama walivyo hawa wasanii wakubwa” amesema Steve.
Kwa upande wake Msanii mkongwe kwenye tasnia ya filamu nchini, Msanii maarufu wa Bongo Movies Jacob Steven ‘JB amesema wanafika Iringa kwa lengo moja tu la kuhakikisha wanaonana na wasanii na vikundi vya Iringa kwa lengo la kutaka kuwainua kitaaluma kwa kuwapa uzoefu ambao wameupata kwa zaidi ya miaka 20.
Amesema tunajua kuna wasanii wengi sana huku mikoani lakini je ni muda gani wanapata nafasi hivyo wanakwenda Iringa na wataacha mabalozi ambao ndio watakuwa maharufu katika kizazi kijacho cha filamu.Kwa upande wake Msanii maharufu wa kike wa filamu nchini, Jackline Wolper amesema umaharufu hauzuii kufanya mambo ya msingi kama ujasiliamali ili aweze kujiongezea kipato.
Amesema kuwa licha ya kuwa maarufu bado amekuwa akijihusisha na ufundi cherehani kama sehemu ya kujiongezea kipato katikamaisha yake ya kila siku.
Msanii Jackline Wolper akifafanua machache.
Mwenyekiti Steve akitoa ya Moyoni.


TASAF YAENDELEA KUWANUFAISHA WANANCHI MKOANI SIMIYU

0
0

Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu wakikagua shamba la pamba la mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini(TASAF), Bibi . Rebecca Masunga (mwenye kitambaa cheupe kichwani) wa Mtaa wa Nyakabindi wilayani Bariadi wakati wa Ziara ya Kamati hiyo ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA B
Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu wakiangalia mifugo ya mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini(TASAF), Bibi . Rebecca Masunga wa Mtaa wa Nyakabindi wilayani Bariadi wakati wa Ziara ya Kamati hiyo ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA C
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akimpongeza mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini(TASAF), Bibi . Rebecca Masunga wa Mtaa wa Nyakabindi wilayani Bariadi kwa kununua jembe la kukokotwa na ng’ombe (plau) kwa ajili ya kulimia, wakati wa Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA D
Baadhi ya Viongozi wa Serikali na Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu walipotembelea na kuona nyumba ya mnufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini(TASAF), Bibi . Stella Masamaki  wa Mtaa wa Old Maswa wilayani Bariadi, wakati wa Ziara ya Kamati hiyo ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA E
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akitoa maelezo ya awali juu wanafaika wa TASAF III wilayani humo wakati wa Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA F
Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi  akitoa maelezo ya awali juu mradi wa Maji ulioibuliwa na wanafaika wa TASAF III katika Kijiji cha Nkoma wilayani humo wakati wa Ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa  wa Simiyu kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA G
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt.Joseph Chilongani (kulia) akiwaongoza Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Simiyu na baadhi ya viongozi wa Serikali kuelekea kwenye ukaguzi wa Jengo la Wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, wakati wa ziara ya viongozi hao ya kukagua Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA H
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Ndg..Fabian Manoza akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Simiyu na baadhi ya viongozi wa Serikali kuhusu Jengo la Wodi ya Wazazi linalojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Meatu, wakati wa ziara ya viongozi hao ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.
PICHA I
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Dkt. Seif Shekalaghe akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Simiyu na baadhi ya viongozi wa Serikali kuhusu Jengo la Zahanati ya Kijiji cha Mwandete inayojengwa kwa ushirikiano wa Serikali na wananchi, wakati wa ziara ya viongozi hao ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM wilayani humo.

…………………..
Na Stella Kalinga, Simiyu
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Awamu ya tatu umeendelea kunufaisha wananchi  wakiwemo wakazi wa kijiji cha  Nkoma wilaya ya Itilima  na  Nyakabindi    wilaya ya  Bariadi  mkoaniSimiyu.

 Hayo yamebainishwa na baadhi ya Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya maskini katika Kijiji cha Nkoma wilayani Itilima, Mtaa wa Nyakabindi na Mtaa wa Old Maswa wilayani Bariadi wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Simiyu ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Mmoja wa wanufaika wa Mpango huo, Bibi. Rebecca Masunga kutoka Mtaa wa Nyakabindi wilayani Bariadi, amesema TASAF imemsaidia kutoka katika umaskini sasa anapata kipato kinachomwezesha kujikimu, kwa kuwa amelima ekari tatu za pamba, ekari moja ya mahindi, ana ng’ombe 14 na mbuzi wanne na amenunua plau kwa ajili ya kulimia.  

“Nilikuwa maskini wa kutupwa , nilipoingia TASAF na kuanza kupokea zile elfu 36 nilikopa fedha nikalima nyanya ekari moja nikauza, nilipata shilingi laki sita nikanunua ng’ombe watatu wakakua;  baadaye nikawauza nikapata milioni moja na laki tano nilinunua ng’ombe 14 ndiyo hao mnaowaona tunawachunga sasa” alisema Rebecca Masunga

“Tuna kikundi chetu ambacho tunaweka fedha zetu baadaye tunagawana, tukisha gawana tunaenda kuzalisha, tunalima nyanya, kabeji, pamba halafu tunauza; mpango wangu wa baadaye niwe na mtaji mkubwa na nijenge nyumba bora ” alisisitiza Bibi.Masunga.

Nae Bibi. Stella Masamaki mkazi wa Old Maswa wilayani amesema kupitia mpango wa Kunusuru kaya maskini aliweza kukodi mashamba nakulima pamba, baada ya kuuza pamba akajenga nyumba bora ya vyumba vitatu na akatoka kwenye nyumba ya udongo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo amewapongeza wanufaika wa TASAF ambao wamezitumia fedha hizo kwa manufaa na akawashauri kuanzisha miradi midogo midogo na kuwatumia wataalamu wa kilimo pamoja na mifugo kuwasaidia katika uendelezaji wa miradi yao ya kilimo na mifugo.

Katika hatua nyingine Mratibu wa TASAF Wilaya  Itilima Bw. John Rajabu amesema wanufaika wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini wameibua mradi wa maji ambao pia utawanufaisha na wananchi wengine, ambapo mpaka kukamilika kwake utatumia takribani milioni 15.

Wakati huo huo Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Simiyu wamefanya ziara katika Wilaya ya Meatu, Itilima na Maswa na kukagua miradi ya Maji, Afya na Elimu nakuwataka viongozi na watendaji katika maeneo husika kutimiza wajibu wao na kuhakikisha kuwa miradi yote inatekelezwa kwa viwango na kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma wanazostahili.

Sanjali na hilo wajumbe hao wamewataka viongozi kutambua fedha zinazochangwa na wananchi na kusimamia vizuri kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo,  ili zitumike kama ilivyokusudiwa.

KICHUYA KUMKABIDHI MSHINDI WA BAJAJI MAFINGA

0
0
Mkazi wa Iringa, Mafinga Ndugu Mathias Edward (25) ambaye pia ni mshindi wa bajaji kupitia promosheni inayoendeshwa na kampuni ya michezo ya kubashiri SportPesa wakishirikiana na kampuni ya mtandao wa simu na wadhamini ya ligikuu Tanzania Vodacom wamemkabidhi bajaji hiyo mnano tarehe tisa mwezi huu. 

Alizungumza wakati wa makabidhiano yaliyoongozwa na mchezaji wa klabuya Simba Siza KichuyaNdugu Mathias alisema “Niliunganishwa na mjomba wangu ambaye makazi yake hasa ni mkoani Dodoma yeye ni mchezaji mzuri kwahiyo alinishawishi ili na mimi niweze kujiunga nakucheza. 
 
Kupitia bajaji hii itanisaidia kubadili maisha yangu na kuanza rasmi kujitegemea kimaisha nikiwa kama kijana nayekaribia umri wa miaka 28. Nikiwa kama kijana msomi mwenye stashahada ya ukutubi nilihangaika sana kutafuta ajira na mwisho ya siku nikaamua kujiingiza kwenye maswala ya kilimo ili kuinuaki patochangu. 
 
Nilikuwa nachezana SportPesa kwanjiaya USSD ambayo napiga*150*87#, urahisi ambao upo kwenye SportPesa na ndio unaotofautisha na kampuni nyingine za michezo ya kubashirini kwamba viwango vya kampuni nyingine za kubashirini vya juu sana lakini kwa kampuni kama SportPesa viwango vyao ni vizuri, rahisi sana kushindana kila kitu kiko wazi. 
 
Akizungumza wakati wa makabidhiano ya bajaji mchezaji mahiri watimu ya Simba Shiza Ramadhani Kichuya alisema “Kwanza kabisa napenda kukupongeze kwa zawadi hii uliyoishinda kwa kupitia ubunifu wako mwenyewe, ninaimani kuna watu wengi ambao wanatamani siku moja washinde kama wewe ulivyobahatika na inakubidi uwe mfano kwao kwa kuwaelekeza ili nao waweze kubahatika” “Mimi nikiwa kama mchezaji wa timu kubwa inayoshiriki ligi kuu Taanza rasmi kuchezana SportPesa iliniwezekuibuka mshindi siku moja” alimaliza Kichuya

BUSTANI YA KISASA MANISPAA YA SONGEA KUNZA KUTUMIKA MWEZI MEI MWAKA HU

0
0
MRADI wa bustani ya kisasa ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma umekamilika ,unatarajia kuanza kufanyakazi mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu.

Akizungumza na Ruvuma TV Afisa habari wa Manispaa Albano Midelo, amesema Mkandarasi tayari amekabidhi mradi huo kwa Manispaa. Bustani hiyo itakuwa na sehemuya Mgahawa,Maegesho ya Magari,kituo cha Utalii,sehemunya michezo ya watoto na huduma za choo, Kwa undani wa habari hii tizama video yake.

BUNIFU: MAKEKE KUJA NA VAZI LA UNGO LIJULIKANALO KAMA "LUPAHERO".

0
0
BUNIFU: MAKEKE KUJA NA VAZI LA UNGO LIJULIKANALO KAMA "LUPAHERO".  Jinsi wazo lilivyopatikana.

Katika maandalizi yaonyesho la kwanza kufanywa chini ya MAKEKE INTERNATIONAL lililofahamika kama I AM MAKEKE ndipo wazo hili la lupahero lilipozaliwa. Kwamujibuwa MAKEKE INTERNATIONAL ilimchukua muda mrefu kupata wazo la kufanya katika onyesho hilo licha ya kua na bidhaa nyingi za kubuni nguo mbalimbali ofisini kwake.

Baada ya kuwaza kwa muda mrefu ndani ya ofisi, alitoka nje na kurudi baada ya kutuliza akilila na wakati akirudi aliuona ungo kupitia dirisha uliokua umetundikwa ukutani kama pambo la ofisia mbapo aliamua kuuchukua na kukaa nao huku kichwa kikiendelea kuwaza na kuwazua ni wazo gani ataonyesha kwenye onesho lililokua mbeleyake.

Baada ya kuwaza kwa masaa kadhaa wazo lilimjia na kutaka kutoboa ungo aliokua nao  kwakiasi cha kuweza kuvaa shingoni ambapo alifanya hivyo na kupata ladha ya mapambo ya shingoni ya kimasaii la katika mwonekano wa ungo na ndipo alipoanza kufikiria mikato mingine ambayo   ungo unaweza kuingia na kudhihirisha ubunifu wa ungo kama vazi.

Baada ya kupata yote hayo Makeke alichukua daftari na kuanza kuchora kila alichokua amekiwaza kwa ufanisi zaidi kufanyia kazi kwa muda aliokua nao hali iliyofanya ubunifu wa ungo kutumika kwamara ya kwanza katikatamasha la I AM MAKEKE mpaka hivisasa.

Mikato ya Lupahero


MAKEKE INTERNATIONAL 
imelenga zaidi kujenga dhana ya ushujaa na asili ya kiafrika ili kujenga mazingira ya kuweza kujiamini na kujua kuwa wewe ni bora zaidi kutoka na jinsi ulivyo kama mwafrika na shujaa akiwa katika kila jambo.
Follow us on Facebook  @makeke international Instagram@makekeinternational  
On Apr 6, 2018 8:11 PM, "Mr. Lulela" wrote:

LUPAHERO
Baadayauzoefumkubwakatikamatumiziyamapishijikoni, ungoumejizoleaumaarufumkubwabaadayakuingizwarasmikatikatasniayasanaahususanikatikaubunifuwamavazinakupewajina la LUPAHERO naJocktanMakeke.

Maanaya LUPAHERO

Ubunifu huu wa mavazi umepewa jina la LUPAHERO ambalo nimchanganyiko wamajina mawili ambayo ni LUPAPIKE, neno la kinyakyusa lenye maana ya ungo na neno la pilini LUHELO, ambalo ni neno la kihehe lenye maana ya ungo.

Muunganikowamaneno haya mawili yamelenga kuletadhana yaushujaa kutokan ana ladha ya mavazi hayo kuwa na dhima hiyo, huku neno Luhelo likitamkwa herufi zamwisho kama Hero, herufi L ikibadilishwa kuwa R ilikupataneno hero la kingereza lenyemaana ya shujaa nakukamilisha maana halisi yaubunifu huo kuwashujaa wa ungo.  

Jinsiwazolilivyopatikana.

Katika maandalizi yaonyesho la kwanza kufanywa chini ya MAKEKE INTERNATIONAL lililofahamika kama I AM MAKEKE ndipo wazo hili la lupahero lilipozaliwa. Kwamujibuwa MAKEKE INTERNATIONAL ilimchukua muda mrefu kupata wazo la kufanya katika onyesho hilo licha ya kua na bidhaa nyingi za kubuni nguo mbalimbali ofisini kwake.

Baada ya kuwaza kwa muda mrefu ndani ya ofisi alitoka nje na kurudi baada ya kutuliza akilila na wakati akirudia aliuona ungo kupitia dirisha uliokua umetundikwa ukutani kamapambo la ofisia mbapo aliamua kuuchukua na kukaa nao huku kichwa kikiendelea kuwaza na kuwazua ni wazo gani ataonyesha kwenye onesho lililokua mbeleyake.

Baada ya kuwaza kwa masaa kadhaa wazo lilimjia na kutaka kutoboa ungo aliokua nao  kwakiasi cha kuweza kuvaa shingoni ambapo alifanya hivyo na kupata ladha ya mapambo ya shingoni ya kimasaii la katika mwonekano wa ungo na ndipo alipoanza kufikiria mikato mingine ambayo   ungo unaweza kuingia na kudhihirisha ubunifu wa ungo kama vazi.

Baada ya kupata yote hayo Makeke alichukua daftari na kuanza kuchora kilaalichokua amekiwaza kwa ufanisi zaidi kufanyia kazi kwa muda aliokua nao hali iliyofanya ubunifu wa ungo kutumika kwamara ya kwanza katikatamasha la I AM MAKEKE mpaka hivisasa.

Mikato ya Lupahero


MAKEKE INTERNATIONAL 
imelenga zaidi kujenga dhana ya ushujaa na asili ya kiafrika ili kujenga mazingira ya kuweza kujiamini na kujua kuwa wewe ni bora zaidi kutoka na jinsi ulivyo kama mwafrika na shuja akiwa katika kila jambo.
Follow us on Facebook  @makeke international Instagram@makekeinternational  

WATAKAOBAINIKA KWA KUJIHUSISHA BIASHARA YA MAGENDO HAWATABAKI SALAMA

0
0



















MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo kulia ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim
Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama akizungumza wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo kulia Afisa Mtekelezaji Mkuu wa Bandari ya Tanga Donald Ngaire kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
PRO wa Bandari ya Tanga Moni Jarufu akizungumza wakati akiwakaribisha wageni kwenye sherehe hizo zilizofanyika kwenye viwanja v ya Bandari Jijini Tanga
Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama katikati akifuatilia matukio mbalimbali kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kulia ni Afisa Mtekelezaji Mkuu wa Bandari ya Tanga Donald Ngaire
Afisa Tehama wa Bandari ya Tanga Ally Isaka akimueleza kitu Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo katikati ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama
Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama kushoto akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Bandari leo akiwa ameambatana na Mkuu wa Polisi wilaya ya Tanga (OCD) Jumanne Abdallah na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim
Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akisalimiana na wafanyakazi wa Bandari ya Tanga 
Sehemu ya wafanyakazi wa Bandari ya Tanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Sehemu ya wafanyakazi wa Bandari ya Tanga wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Zoezi la utoaji wa damu likiendelea kwenye sherehe hizo 


SERIKALI mkoani Tanga imesema kuwa haitakuwa na simile na wananchi watakaokamatwa kujihusisha na kuingiza bidhaa za magendo kupitia bandari bubu kwani wanachangia kuikosesha mapato serikali. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa wakati wa ufunguzi wa sherehe za wiki ya bandari pamoja na maadhimishi miaka 13 ya Mamlaka hiyo.

Alisema kuwa kumekuwepo na wimbi kubwa la wafanyabiashara wasio waaminifu kutumia bandari bubu kupitishia bidhaa za magendo ambazo sio salama kwa matumizi ya binadamu. “Katika hili hatutakiwa na msamaha wala kumuonea mtu haya tukikukamata chombo tutakitaifisha pamoja na mali zake huku muhusika atachukuliwa hatua kali za kisheri nilazima wananchi wajifunzi kuona umuhimu wa kutumia bandari rasmi”alisema DC Mwilapwa. 

Aidha aliitaka Mamlaka ya usimamizi wa bandari Mkoani Tanga kuhakikisha utendaji kazi wao unaendana na kasi ya maboresho ya bandari hiyo unaofanywa na serikali kwa sasa. Awali Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama alisema kuwa maboresho ya vifaa na vitendea kazi katika bandari hiyo yameweza kusaidia kuongeza ufanisi wa kuhudumia shehena za mizigo kutoka siku kumi hadi nne. 

Alisema kuwa kuhudumia shehena za mizigo katika kipindi kifupi kumesaidia kupunguza gharama kwa wateja wanaohudumiwa na bandari hiyo . “Licha ya kuhudumia mizigo kwa awamu mbili lakini uwepo wa vifaa umesaidia kuboresha uwezo wa bandari yetu ya kuhudumia mizigo kwa ufanisi zaidi”alibainisha Mkuu huyo.

Sherehe hizo zinakwenda sambamba na kauli mbiu Bandari za TPA ni chachu ya uchumi Viwanda na Ustawi nchini Tanzania (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

WWF YAZINDUA MRADI WA KUHIFADHI MAZINGIRA-MTWARA

0
0
Na Joseph Mpangala-mtwara

Shirika la Kuhifadhi mazingira duniani WWF imezindua Mradi wa Kuleta mabadiliko katika usimamizi na Uendelezaji wa Maliasiri za misitu,wanyapori na bahari kwa kushirikisha Asasi za Kiraia pamoja na Wananchi katika mikoa ya Kusini.

Mradi huo wa miaka mitano unagharimu zaidi ya shilingi Billion10 fedha ambazo ni msaada kutoka shirika la maendeleo la SIDA kutoka Nchini Sweden kwa lengo la kusaidia Serikali na wananchii katika Kuboresha Usimamizi wa maliasili.

Akiongea katika Uzinduzi wa Mradi huo Mkurugenzi wa shirika la WWF hapa Nchini Dk.Amani Ngusaru amesema katika Mradi Utawezesha akina mama na Vijana ili kuhakikisha wanachochea mabadiliko katika katika usimamizi wa maliasili kwa ajili ya matumizi ya Vizazi vya sasa na Vijavyo.

Dr.Amani ameongeza kuwa Bado Maliasiri zetu zinakabiliwa na Changamoto ya Uharibifu unaochangiwa na Ongezeko la Shughuli za kibinadamu.

“katika hivi karibuni kumekuwepo na uvamizi mkubwa wa maeneo yaliyohifadhiwa kwa ajili ya shughuli za Kilimo,Malisho ya Mifugo,Uchimbaji wa madini,ukataji wa miti mjanga ya moto pamoja na uvunaji wa misitu ya asili kwa ajili ya ujenzi”amesema Dk.Amani.

Mradi huu unaafanyakazi katika mikoa ya Lindi,Rumuma pamoja na mtwara.

Mkurugenzi wa WWF hapa nchini Dr.Amani Ngusaru akiongea na wawakilishi wa asasi mbalimbambali za kiraia wakati wa uzinduzi wa Mradi wa uendelezaji Maliasili Mkoani Mtwara. 
.Kaim Mkurugenzi wa Tunduru Jonathan A Haule wakatikati akionesha Kitabu cha WWF mara baada ya kufanya Uzinduzi wa Mradi wa Uendelezaji wa maliasi katika mikoa ya kuzini

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA BALOZI WA UGANDA NCHINI TANZANIA.

0
0
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na mgeni wake Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Mabonero (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza mgeni wake Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Mabonero (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Mabonero (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.

 (PICHA NA OFISI YA BUNGE)

MATUKIO YA OFISI YA WAZIRI MKUU BAADA YA BUNGE KUPITISHA BAJETI YA OFISI HIYO

0
0
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akipongezana na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Rogers Sianga mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Ofisi hiyo Aprili 10, 2018.
 Makatibu Wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia hoja za Wabunge zinazohusu ofisi hao wakati wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya fedha za Ofisi yake kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Bungeni Dodoma, wa kwanza ni Bw.Erick Shitindi anayeshungulikia Kazi,Ajira, Vijana na wenye ulemavu, kulia kwake ni Prof.Faustin Kamuzora (Sera na Uratibu) kulia kwake ni Bi.Maimuna Tarishi (Bunge na Waziri Mkuu).
 Baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia hoja za wabunge kuhusu ofisi yao wakati wa kujadili na kupitisha Bajeti hiyo kwa mwaka wa Fedha 2018/2019.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde akipongezana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Dkt.Irene Isaka mara baada ya Bunge kupitisha bajeti Ofisi hiyo.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Bunge na Siasa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Yona Mwakilembe Bungeni Dodoma.

MPINA AWABANA WANAOTOROSHA PUNDA KWENDA NJE YA NCHI

0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (katika) akizungumza na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchinjia Punda Fang Hua, Lifang Yu, kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Assimwe Lovince. Picha na John Mapepele.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akiangalia zizi la Punda na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kuchinjia Punda Fang Hua, Lifang Yu aliye kushoto kwake. Picha na John Mapepele.

Punda kwenye zizi la Kiwanda cha kuchinjia Punda Fang Hua mjini Shinyanga. Picha na John Mapepele.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (mwenye miwani) katika picha ya pamoja na watumishi wa Kiwanda cha kuchinjia Punda Fang Hua. Picha na John Mapepele.


Na John Mapepele, Shinyanga

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewahakikishia wenye viwanda nchini kuwa hakuna mali ya mifugo ya Tanzania itakayotoroshwa tena kwenda nje ya nchi kimagendo kwani Tanzania haiwezi kukubali kugeuzwa kuwa machungio ya mifugo hiyo.

Waziri Mpina ametoa kauli hiyo jana mjini Shinyanga baada ya kutembelea Kiwanda cha Fang Hua kinachojishughulisha na uchinjaji wa Punda ambapo alielezea kuridhishwa kwake na juhudi kubwa zilizofanywa na mwekezaji huyo kuwezesha kuwepo soko la uhakika la mifugo hiyo.

Mkurugenzi wa Kiwanda cha Fang Hua, Lifang Yu alimweleza Waziri Mpina kwamba kiwanda chake kimeshaingia ubia na wafugaji wadogo wapatao 27 ili kuongeza uzalishaji ambapo kinatarajia kuwashilikisha wafugaji wengi zaidi katika mikoa mbalimbali nchini

Waziri Mpina aliwahakikishia wawekezaji wenye viwanda katika sekta ya mifugo kuwa malighafi hiyo itakuwepo ya kutosha kwani Serikali ya awamu ya tano chini ya Dk. John Pombe Magufuli haitakubali tena mifugo hiyo kuendelea kutoroshwa nje ya nchi na kunufaisha viwanda vya nchi hizo.

Hivyo Waziri Mpina alisema uwekezaji wa aina hiyo wa kuongeza thamani ya mazao ya mifugo ni moja ya vipaumbele vya wizara yake kwa sasa ili kuchochea kwa kasi kufanikisha azma ya Tanzania ya viwanda.

Alisema kiwanda hicho mbali na kuongeza soko la punda pia kimechangia kuchochea uchumi wa Mkoa wa Shinyanga pamoja na kutatua changamoto ya ajira ambapo hadi sasa kimeajiri wafanyakazi 100 hivyo alimhakikishia mwekezaji huyo kuwa changamoto ya punda wengi kutoroshwa nchini Kenya haitakuwepo tena.

Alisema kwa sasa kuna viwanda viwili vya kuchakata nyama ya punda na kuuza nchini China, ambapo wastani wa mauzo ya nyama hiyo nje ya nchi yalifikia tani 2000 mwaka 216/17

Mpina aliwahimiza wawekezaji hao kuhakikisha wanawasaidia wafugaji katika kuongeza uzalishaji, kupambana na maradhi, upatikanaji wa maji na malisho kwa mifugo.Aliwataka kuanzisha ranchi ya mifugo na maeneo yakupumzishia mifugo hiyo kabla ya kuchinjwa.

Alisema idadi ya punda waliopo nchini ni 520,000 tu hivyo juhudi za makusudi zinahitajika kuongeza uzalishaji.Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Lovince Assimwe aliwataka wafugaji kuongeza soko la uhakika.

Alipongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kubuni mbinu za kuwasaidia wafugaji kwa kuwapatia shilingi elfu tano kila mwezi kwa ajili ya matibabu ya punda.

Rais Magufuli ateua Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA

0
0

RC MAKONDA KUTOA KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WATOTO WALIOTELEKEZWA.

0
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema kinamama wote waliofika ofisini kwake wakiwa na watoto kwa ajili ya kupatiwa msaada wa kisheria baada ya kutelekezwa atawapatia kadi za Bima ya Afya (Toto Afya Card) Bure kwa ajili ya matibabu ya watoto wao.

RC Makonda amesema kadi hizo zitatolewa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 17 kwa kila mama aliefika ofisini kwake pasipokujali idadi ya watoto alionao.

Uamuzi huo umekuja baada ya RC Makonda kujionea mateso wanayopata kinamama hao ikiwemo watoto kuugua Magonjwa yanayohitaji gharama kubwa za matibabu na kwakuwa wengi wa kinamama hao wana hali ngumu kimaisha wanashindwa kumudu gharama na kusababisha maumivu na mateso kwa mtoto.

Aidha RC Makonda amesema hadi kufikia mchana wa leo zaidi ya kinamama 1,030 walikuwa tayari wamesikilizwa na Kati ya hao watu mashuhuri 107 wakiwemo wanasiasa na viongozi wa dini wametuhumiwa kutelekeza watoto.

Hata hivyo RC Makonda amesema kuanzia wiki ijayo kinababa waliotelekeza watoto wataitwa ofisini kwake kwaajili ya kutoa ufafanuzi na atakaekaidi kufika atachukuliwa hatua kaliza kisheria.

RC Makonda aliongeza hayo wakati wa zoezi la kubaini Wazazi waliokimbia Watoto wao linaloendelea katika ofisi zake,amesema kuwa idadi hiyo imebainika jana na juzi wakati wa zoezi hilo, pia amesema kuwa si kundi hilo tu la watu mashughuli pia kuna kundi la Watu ambao wanaona aibu kufika katika eneo hilo.

"Hawa Watu wanaona aibu kufika ofisini ofisini hapa, hakuna kukutana na mimi chemba, habari yakupigiana simu kuniambia Mheshimiwa naomba nije peke yangu hakuna", amesisitiza Makonda

"Watu Mashughuli, watu wenye heshima tukikupima DNA nakugundua mtoto ni wako, basi utalipa fidia zote za huyo mtoto".Amesema wale wanaokaidi wito kufika ofisini hapo, kuanzia kesho watapelekewa barua pamoja na kupigiwa simu.

Zoezi hilo lakubaini Wazazi waliokimbia watoto wao lilianza siku ya Jumatatu ya April 9, 2018 na linatarajiwa kumalizika siku ya Ijumaa April 13 mwaka huu.
 Baadhi ya Akina Mama waliojitokeza katika Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kudai fidia za Watoto wao kwa Wazazi wenzao waliokimbia watoto hao.
 Mmoja wa Maafisa wa Ustawi wa Jamii akiwasikiliza Wazazi wa Kiume walioitikia wito kufika Ofisni kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
 Baadhi ya akina Baba waliotikia wito kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kusikiliza malalamiko kwa wake zao. (PICHA NA EMMANUEL MASSAKA)

Serikali Yapunguza Idadi Ya Hati Chafu

0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Prof. Mussa Juma Assad amesema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli inaendelea vizuri na uwekaji wa mahesabu uliopelekea kupungua kwa hati chafu katika Taasisi na miradi mbalimbali ya Serikali. 

Prof. Assad ameyasema hayo leo Mjini Dodoma alipokuwa akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu ripoti za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2017.

"Katika ukaguzi wa hesabu nilioufanya katika Serikali Kuu na Taasisi zake, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Mashirika ya Umma kwa mwaka wa fedha 2016/17 nimetoa jumla ya Hati 561 za ukaguzi. Kati ya hati hizo, Hati zinazoridhisha ni 502 sawa na asilimia 90, Hati zenye shaka ni 45 sawa na asilimia 90, Hati zenye shaka ni 45 sawa na asilimia 8, Hati zisizoridhisha ni Saba sawa na asilimia Moja na Hati Mbaya ni Saba sawa na asilimia Moja," alisema Prof. Assad. 

Amesema, katika ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na Taasisi mbalimbali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ametoa jumla ya Hati za Ukaguzi 742 ambapo Hati zinazoridhisha ni 697 sawa na asilimia 94, Hati zenye shaka ni 44 sawa na asilimia 5.9 na Hati isiyoridhisha ni moja, Hati hii imetolewa kwa mradi wa maji (WSDP) unaotekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ya Wilaya ya Makete. 

Naye, Mjumbe wa Kamati ya LAAC Mhe. Abdallah Mtolea amezipongeza Halmashauri zilizofanya vizuri kwa kuonekana kupunguza idadi ya hati chafu na kushamiri kwa hati safi.

Aidha Mhe. Mtolea amesema kuwa kamati hiyo itaziita Halmaushari na kufanya nazo mahojiano bila kuujali matokeo ya ukaguzi kama zilifanya vizuri au vibaya ili kuhakikisha kuna kuwa matumizi mazuri ya fedha za umma.
 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Juma Assad akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Dodoma kuhusu  ripoti za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia June 30, 2017.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya PAC, Naghenjwa Kaboyoka akizungumza kuhusu hatua zitakazochukuliwa na Serikali baada ya CAG kuwasilisha ripoti za Hesabu za Serikali  kwa mwaka wa fedha ulioishia June 30, 2017.
 Sehemu ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Juma Assad  leo mjini Dodoma kuhusu ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia June 30, 2017.
Mbunge wa Temeke, Abdalah Mtolea akizungumza kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya LAAC mara baada ya  Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Juma Assad kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti za Mdhibiti na  Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha ulioishia June 30, 2017.Katikati ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Prof. Juma Assad na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya PAC mhe. Naghenjwa Kaboyoka.(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO)

MADE IN TANZANIA WEEK IN KENYA

0
0

MADE IN TANZANIA WEEK IN KENYA

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation through its Embassy in Nairobi, Kenya and in collaboration with the Ministry of Industry, Trade and Investment (Tanzania Mainland); Ministry of Trade, Industry and Marketing (Zanzibar); Tanzania Trade Development Authority (TanTrade) and Tanzania Private Sectors has organized “Made in Tanzania Week” seeking to pursue wider and broader markets opportunities for country’s industrial products and tourism potentials in the East African Community which will take place between 25th to 28th April 2018 in Kenya.

 This comes as an effort in the implementation of the country’s Foreign Policy which focuses on Economic Diplomacy with much emphasis on the development of sectors like trade, investment and tourism. The event will fall within the National Day (54th Union Day celebration) on 26th April 2018 and will feature industrial products, services in particular tourism, technology, agribusiness, culture, arts and craft.

It should be recalled that, in 2010 the East African Community Partner States signed an agreement on the Common Market Protocol; hence “Made in Tanzania Week in Kenya” will be amongst Government initiatives to promote the forging relationship that has been existing among the Partner States in the Community and spearhead economic development. 

‘’Made in Tanzania week in Kenya’’ which will take place at the Kenyatta International Convention Center (KICC) is scheduled as follows; on the 25th– 28th April 2018 "Made in Tanzania” Exhibitions to showcase Tanzanian products will take place followed by Tanzania - Kenya Business to Business (B2B) meeting on 25th April 2018. Again, on 26th April 2018 a reception for the 54th Union Anniversary will be held at the High Commissioner’s residence in Nairobi. The 54th Union celebrations will be concluded by two major events; the Tanzania - Kenya Business Forum that will take place on 27th April 2018 and Made in Tanzania Business Gala Dinner.

On behalf of the Organizing Committee Co-Chaired by Tanzania Trade Development Authority (TanTrade) and Tanzania Private Sector Foundation (TPSF), the Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation would like to invite the key stakeholders particularly the business community to take advantage of this opportunity and participate in the event.
 For more information on Made in Tanzania Week in Kenya, kindly call +255767123055 or +255687368443 or register ONLINE via www.tanzaniakenya.com.
Issued by;

Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dar es Salaam.
11th April 2018.

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAIKABIDHI TBA NYUMBA ZILIZOREJESHWA NA UMOJA WA ULAYA NCHINI

0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa pamoja na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Roeland van de Geer wakisaini Hati ya Makabidhiano ya nyumba nne (4) kutoka Umoja wa Ulaya zilizopo katika maeneo tofauti ya Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam. Nyumba hizo zimekabidhiwa kwa Wizara na EU baada ya kutumiwa na Umoja huo tokea miaka ya 1975. Baada ya makabiadhiano hayo, Wizara ilizikabidhi nyumba hizo kwa Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA). Makabidhiano hayo yalifanyika Wizarani tarehe 11 Aprili, 2018. 
Balozi Mushy kwa pamoja na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Mhandisi. Elius Mwakalinga wakisaini hati ya makabidhiano kama ishara kwa Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuzikabidhi kwa TBA nyumba nne (4) zilizopokelewa na Wizara kutoka EU. 
Balozi Mushy na Balozi Roeland van de Geer wakibadilishana hati hiyo baada ya kusaini 
Balozi Mushy na Balozi van de Geer wakionesha hati hiyo 
Balozi Mushy na Mhandisi Mwakalinga wakibadilishana hati hiyo mara baada ya kusaini 
Wakionesha hati hiyo 
Mhandisi Mwakalinga na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Grace Martin wakishuhudia Balozi Mushy na Balozi Roeland (hawapo pichani) wakisaini hati ya makabidhiano ya nyumba kutoka EU 
Ujumbe uliofuatana na Balozi Roeland kutoka Ofisi za EU nchini nao wakishuhudia tukio hilo 
Balozi Mushy na Balozi Roeland wakiteta jambo
Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje katika Idara ya Itifaki akitoa maelezo na utaratibu kwa Mabalozi kabla ya kuanza kusainiwa kwa hati hizo za makabidhiano 
Picha ya pamoja

DK. KIGWANGALLA AITAKA KAMATI INAYOCHUNGUZA TUHUMA ZA MAUAJI YA TEMBO IKOLOJIA YA RUGWA-RUAHA KUTENDA HAKI

0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Kamanda wa Polisi Mstaafu wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova ambaye ni Mwenyekiti wa kamati inayochunguza tuhuma za mauaji ya tembo katika Ikolojia ya Rugwa-Ruaha ambazo zilitolewa hivi karibuni na kituo cha habari cha ITV LONDON cha nchini Uingereza, alipokutana na kamati hiyo leo ofisini kwake mjini Dodoma. Wengine pichani ni wajumbe wa kamati hiyo.

Na Hamza Temba-Dodoma
........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla ameitaka kamati inayochunguza tuhuma za mauaji ya tembo katika Ikolojia ya Rugwa-Ruaha ambazo zilitolewa mwishoni mwa mwaka jana na kituo cha habari cha ITV London cha Uingereza kufanya kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu mkubwa bila kumuonea mtu ili ukweli ubainike na Serikali iweze kuchukua hatua stahiki.

Dkt. Kigwangalla ametoa rai hiyo leo mjini Dodoma alipokutana na wajumbe wa kamati hiyo ambayo imewasilisha taarifa za awali za kazi ilizoanza kuzifanya za kupitia taarifa mbalimbali kuhusu tuhuma hizo kabla ya kwenda kuzifanyia uchunguzi maeneo husika.


Amewataka wajumbe hao kuchunguza ukweli wa tuhuma hizo ili kubaini kama kweli kuna watumishi wa Wizara waliohusika katika mauaji hayo pamoja na tuhuma kuwa mauaji ya tembo yalikuwa ni makubwa kama ilivyoripotiwa na chombo hicho cha habari.


Dkt. Kigwangalla pia ameitaka kamati hiyo kuchunguza ukweli wa tuhuma kuwa fedha za ufadhili wa mradi wa SPANEST zilizotolewa na Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) zilitumika vibaya kufadhili mauaji hayo kama ilivyoripotiwa na chombo hicho cha habari.


“Msimtafute mtu, wala msimuonee mtu, fanyeni kazi hii kwa uadilifu na uaminifu mkubwa ukweli ujulikane ili sisi kama Serikali tuweze kuchukua uamuzi unaostahili” alisema Dkt. Kigwangalla.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mstaafu wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amesema kamati yake itafanya kazi kwa uaminifu na weledi wa hali ya juu na kuleta taarifa za ukweli na mapendekezo yatakayoisaidia Serikali kufanya maamuzi sahihi kuhusu tuhuma hizo.


Mapema mwezi Januari mwaka huu, Waziri Kigwangalla na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Natalie Boucly wakiwa katika ofisi ndogo ya wizara hiyo jijini Dar es Salaam walikubaliana kuunda kamati ya pamoja kuchunguza tuhuma hizo.


Kamati hiyo iliyoundwa mapema mwezi januari mwaka huu inajumuisha wajumbe tisa wakiwemo wawili kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na wajumbe wengine kutoka taasisi mbalimbali za Serikali.Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Ndugu Robert Mande ambaye ni mjumbe wa Kamati hiyo kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Bi. Getrude Lyatuu ambaye ni mjumbe wa Kamati hiyo kutoka Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wajumbe wa kamati inayochunguza tuhuma za mauaji ya tembo katika Ikolojia ya Rugwa-Ruaha ambazo zilitolewa hivi karibuni na kituo cha habari cha ITV LONDON cha nchini Uingereza, alipokutana na kamati hiyo leo ofisini kwake mjini Dodoma.

MZEE KIKWETE WATANZANIA TUNAKUKUMBUKA - RAIS MAGUFULI

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya Nchi kabla ya kuzindua rasmi Taasisi hiyo isiyo ya Kiserikali ya Jakaya Mrisho Kikwete(JMKF) Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipigiwa makofi mara baada ya kumaliza kusoma hotuba yake na kuizindua rasmi Taasisi hiyo isiyo ya Kiserikali ya Jakaya Mrisho Kikwete(JMKF) Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya (JKMF) Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza kabla ya uzinduzi wa Taasisi hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya (JKMF) Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuizindua.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa Taasisi hiyo ya (JKMF) Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuizindua. PICHA NA IKULU

*Azungumzia mambo makubwa ambayo aliyafanya kwenye utawala wake ambayo yatakumbukwa
*Azindua rasmi Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation,aahdi Serikali kutoa ushirikiano mkubwa
*Aelezea Kikwete alivyosababisha awe Rais wa Awamu ya Tano, Kikwete azungumzia malengo ya taasisi

Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii.

RAIS Dk. John Magufuli amesema kwa kazi kubwa ambayo imefanywa na Rais mstaafu Jakaya Kikwete kwenye uongozi wake kuna mambo makubwa ya maendeleo katika nchi yetu huku akitanguliza uzalendo mkubwa Watanzania wanamkumbuka na wataendelea kukumbuka watake wasitake.

Pia ametumia nafasi hiyo kutoa shukrani zake za dhati kwa Rais mstaafu Kikwete kwani ndio amesababisha awe Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano huku akitumia nafasi hiyo kuahidi kuwa atahakikisha Serikali yake itashirikana na Taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete inayofahamika kwa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF)ambayo ameizindua rasmi leo Ikulu jijini Dar es Salaam.

"Mzee wangu Kikwete naomba niseme kutoka moyoni wakati wa uongozi wako umefanya mambo makubwa ya kuleta maendeleo kwa ajili ya nchi yetu ya Tanzanania.Kuna miradi mikubwa ya maendeleo ambayo ameifanya na imeacha alama ambayo itatufanya watanzania tumkumbuke.Kwa kazi ambayo umeifanya kwa uzalendo mkubwa ndani ya nchi yetu Watanzania tunakukumbuka na tutaendelea kukumbuka watake wasitake,"amesema Rais Dk.Magufuli.

Ametaja ipo mifano mingi hai ya mambo ambayo ameyafanya Rais mstaafu Kikwete kwenye Serikali ya Awamu ya nne na baadhi ya miradi hiyo lipo  la ujenzi wa bomba la gesi kutoka mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam, ujenzi wa miundombinu ya barabara nchi nzima, ujenzi wa miradi ya maji , umeme na kuimarisha sekta muhimu za afya, kilimo na vijana.

"Rais mstaafu Kikwete alilitumikia Taifa la Tanzania kwa uadilifu mkubwa.Tabia ya binadamu wamekuwa na kawaida ya kumsifu mtu baada ya kufa na kusema pengo halitazibika wakati si kweli kwani kama ni nafasi ya uongozi inaweza kujazwa wakati huohuo.Kwa Rais mstaafu na mzee wangu Kikwete naomba nikusifu ukiwa hai tena upo mbele yangu unatabasamu.Umefanya kazi kubwa ya kizalendo kwa ajili ya nchi yetu ya Tanzania na unastahili sifa na shukrani kutokana na mchango wao wa kuleta maendeleo kwenye nafasi mbalimbali.

"Ulipokuwa Rais wa Tanzania umefanya mambo makubwa zaidi kwa ajili ya nchi yetu. Katika utawala wako umefanikisha ujenzi wa shule za sekondari za kata , ujenzi wa Hospitali ya Mloganzila na miradi mingine mikubwa ambayo umeifanya na sote ni mashahidi kwa yale ambayo umeyafanya,"amesisitiza Rais Dk.Magufuli na kuongeza mbali ya kuwa Rais mzee Kikwete ameshika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Bara la Afrika na nchi za ulaya na Dunia kwa ujumla na kote huko ametoa mchango mkubwa wa kuleta maendeleo.

Rais Magufuli amesema uzalendo wa mzee Kikwete kwa nchi yake umemfanya hata baada ya kustaafu kuamua kuanzisha taasisi ambayo leo amezindua rasmi na vipaumbele vya taasisi hiyo havina tofauti na vile ambavyo anavitekeleza kwenye Serikali yake , hivyo ameahidi kumpa ushirikiana mkubwa kufanikisha malengo hayo na kuomba wadau wengine wakiwamo mabalozi nao kuunga mkono kazi za taasisi hiyo.

DC ILALA AWATAKA WAJASIRIAMALI WANAWAKE KUJIUNGA NA JUKWAA LA WANAWAKE

0
0

Ofisa Tarafa wa Kata ya Kariakoo Christina Kalekezi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Kikundi cha Wajasiriamali cha Mshikamano Mchikichini Sokoni katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Ilala Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Katibu wa Kikundi hicho, Juliana Richard, Mwenyekiti, Anjela Mwamakula na aliyevaa miwani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Jane Magigita.
Wanachama wa Kikundi cha Mshikamano Mchikichini Sokoni wakiwa kwenye uzinduzi wa kikundi chao.
Hapa wakiserebuka.
Mwenyekiti wa Soko la Mchikichini-Ilala Jumanne Kongogo akizungumza kwenye uzinduzi huo.
Uzinduzi ukiendelea.
Wakiimba na kucheza katika uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Kikundi hicho, Anjela Mwamakula akisoma taarifa ya kikundi mbele ya mgeni rasmi.
Makofi yakipigwa.
Umakini katika uzinduzi huo.
Katibu wa Kikundi, Juliana Richard akimkabidhi mgeni rasmi risala yao.
Mkurugenzi wa Shirika la EfG, Jane Magigita akizungumza katika uzinduzi huo.
Ofisa Tarafa wa Kata ya Kariakoo Christina Kalekezi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akihutubia wakati akizindua kikundi hicho.
Mkurugenzi wa Shirika la EfG, Jane Magigita akionesha cheti cha kikundi hicho baada ya kuzinduliwa.
Mwenyekiti wa kikundi hicho, Anjela Mwamakula na Katibu wake Juliana Richard (kulia), wakionesha cheti.
Mwakilishi wa Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Ilala, Regina Ng'ongolo, akizungumza.
Ofisa Ushirika Manispaa ya Ilala, Donald Kibhuti akizungumza machache kwenye uzinduzi huo.
Ofisa kutoka ofisi ya Sheria na Msajili Msaidizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Geofrey Mlagala, akizungumza.
Mlezi wa Kikundi hicho, Betty Mtewele akizungumza.
Zawadi zikitolewa kwa mgeni rasmi.
Mjasiriamali Godliver Massawe (kulia), akimuonesha mgeni rasmi bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanawake hao.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi


Na Dotto Mwaibale

WANAWAKE Wajasiriamali wametakiwa kujiunga na Jukwaa la Wanawake ili kujiinua kiuchumi.

Mwito huo umetolewa na Ofisa Tarafa wa Kata ya Kariakoo Christina Kalekezi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema wakati akizindua kikundi cha wajasiriamali cha Mshikamano Mchikichini Sokoni katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Ilala Dar es Salaam jana.

Katika hatua nyingine Kalekezi amewataka wanawake hao kuacha unafiki na kupendana jambo litakalowasaidia kusonga mbele kwenye umoja wao huo.

Alisema Dunia imeanzisha Jukwaa la Wanawake ambapo wanawake watakuwa wakukutana kujadili changamoto walizo nazo na jinsi ya kuzikabili pamoja na kuangalia fursa mbalimbali za maendeleo."Jukwaa ili na sisi linatuhusu hivyo hatuna budi kujiunga nalo kwani huko tutapata wataalamu waliobobea katika masuala mbalimbali pamoja na biashara hivyo ni vizuri tukalichangamkia" alisema Kalekezi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Equality fo Growth (EfG) Jane Magigita alisema wakati huu si wakulala bali ni wakuangalia fursa nyingine ili kujikomboa kiuchumi.Alisema Serikali imeweka mazingira mazuri hivyo ni wajibu wa kila mmoja wetu kupambana vilivyo ili kujikwamua kiuchumi kupitia vikundi.

Mkurugenzi huyo ambaye kupitia shirika analoliongoza la EfG amekuwa chachu kubwa ya maendeleo kwa wanawake alisema hivi sasa kwa Dar es Salaam semina zimekwisha badala yake wanakwenda katika mikoa nane ambapo wataanzisha kampeni ya uhamasishaji kupinga ukatili wa kijinsia masokoni ambapo wasaidizi wa kisheria waliopata mafunzo kutoka shirika hilo ndio watakao kuwa wahamasishaji wakubwa.

"Sasa hatutakuwa tena na semina tunakwenda kufanya uhamasishaji mkubwa mkoani tutakuwa na basi letu maalumu katika kampeni hiyo" alisema Magigita.

Katibu wa kikundi hicho, Juliana Richard wakati akisoma risala kwa mgeni rasmi alisema changamoto yao kubwa ni miundombinu mibovu katika soko lao la mchikichini na mikopo wanayokopa kuwa na riba kubwa.Alisema kikundi hicho kwa sasa kinamtaji wa sh.milioni 11 lakini lengo lao kwa kiasi cha chini kuwa na sh.milioni 70.

Ofisa kutoka ofisi ya Sheria na Msajili Msaidizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Geofrey Mlagala alisema wanawake ambao wapo tayari kuanzisha vikundi vyao milango ipo wazi na watasaidiwa kuelekezwa namna ya kuvifungua.

NCAA YADHAMINI NGORONGORO MARATHON

0
0
Mashindano ya Ngorongoro Marathon 2017, ambayo kwa mara ya kwanza yalidhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Mamlaka hiyo inadhamini kwa mara ya pili mwaka huu. (Picha na Yusuph Mussa).

Na Yusuph Mussa, Tanga

MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA) imedhamini mashindano ya Ngorongoro Marathon kama sehemu ya njia ya kukuza utalii kwenye eneo hilo lenye vivutio vya pekee duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo (Aprili 11) jijini Tanga, Naibu Mhifadhi wa NCAA Asangye Bangu, alisema mashindano hayo yatakuwa na faida kubwa kwenye nyanja za utalii na kuwezesha watu wengi ndani na nje ya nchi kuvutiwa na hifadhi hiyo.

"Tumeamua kudhamini mashindano haya ya Ngorongoro Marathon yanayofanyika Aprili 21, mwaka huu. Nia ya kudhamini mashindano haya, kwanza ni kufanikisha mashindano yenyewe na pili ni kuweza kutangaza utalii wetu.

"Tunaamini sisi Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro tuna dhima kubwa kuona watalii wa ndani na nje wanaongezeka. Lakini ili waongezeke ni lazima tutumie njia mbalimbali za kutangaza vivutio vya Hifadhi za Ngorongoro ambavyo ni vya kipekee duniani" alisema Bangu.

Bangu alisema Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, pia imekuwa na changamoto ya ujangili na uvamizi, hivyo kwa kutumia mashindano hayo, watawaeleza wananchi wajue umuhimu wa hifadhi hizo kwa maslahi ya nchi.

"Suala la kushirikisha jamii katika matukuo mbalimbali ni muhimu sana, ili wananchi waweze kujua Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inafanya kitu gani. Lakini pia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, imekuwa ikikabiliwa na masuala ya ujangili na uvamizi, hivyo tukikutana na wananchi tunawapa elimu ya kutosha juu ya hifadhi yetu" alisema Bangu.

Kaimu Meneja Mahusiano wa Hifadhi ya Ngorongoro Joyce Mgaya amewahamasisha wanawake na wasichana kushiriki mbio hizo, kwani ni fursa kwa wao, kwanza kuwa sehemu ya kushiriki mashindano ambapo watapata uzoefu mbalimbali, lakini pia wataweza kuijua Hifadhi ya Ngorongoro na shughuli zao, kama sio na wao kuweza kufanya utalii wa ndani.

"Tunataka kutumia mashindano haya kuwaeleza kuwa Watanzania, kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, tuna rasilimali nyingi ikiwemo miti na wanyama, bila jitihada za pamoja tunaweza kujikuta rasilimali hizo zinatoweka, hivyo ni muhimu kwetu kuweza kutunza hifadhi hiyo, kwa kutumia mashindano haya tunaamini ni sehemu ya mafanikio ya kulinda rasilimali hizo" alisema Mgaya.

Naye Meneja Huduma za Utalii Paul Fisso, alisema mashindano hayo yatahusisha kilomita 21, kilomita tano na kwa watoto kilomita mbili na nusu, ambapo itakuwa kwa pande zote wanawake na wanaume na washindi wote watapata zawadi.
Mashindano ya Ngorongoro Marathon 2017, ambayo kwa mara ya kwanza yalidhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Mamlaka hiyo inadhamini kwa mara ya pili mwaka huu. (Picha na Yusuph Mussa)

Mashindano ya Ngorongoro Marathon 2017, ambayo kwa mara ya kwanza yalidhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Mamlaka hiyo inadhamini kwa mara ya pili mwaka huu. (Picha na Yusuph Mussa).

Mashindano ya Ngorongoro Marathon 2017, ambayo kwa mara ya kwanza yalidhaminiwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA). Mamlaka hiyo inadhamini kwa mara ya pili mwaka huu. (Picha na Yusuph Mussa).

Rais Dkt. Magufuli azindua rasmi taasisi ya Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF)

0
0

 Msanii anayechipukia  Goodluck Gozbert akitumbuiza kwa wimbo wake maarufu wa "Hauwezi Kushindana" kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza msanii anayechipukia  Goodluck Gozbert baada ya kutumbuiza kwa wimbo wake maarufu wa "Hauwezi Kushindana" kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mshauri mwelekezi wa JMKF Bi. Aisha Sykes akiwa na mwezeshaji Aidan Eyakuze wakifanya mawasilisho ya mpango mkakati wa tasisi hiyo kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wajumbe wa Baraza la wadhamini wa JMKF wakiwa katika hafla hiyo
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa wakimpigia makofi  Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuongea  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuhutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiteta jambo na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2019
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Bw. Omari Issa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Sehemu ya mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
 Sehemu ya wageni waalikwa wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipigiwa makofi baada ya kuhutubia katika hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. wengine meza kuu kutoka kushoto ni Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Sehemu ya wageni waalikwa   kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
Meza kuu ikimsikilia mjumbe wa Baraza la Wadhamini wa taasisi hiyo Bw. William Mahalu akitoa neno la shukrani baada ya  ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Sehemu ya mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa taaisi hiyo - Profesa Rwekaza Mukandala na Balozi Ombeni Sefue - wakiwa  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa taaisi hiyo - Bw. Abubakar Bakhressa na Bi.Genevieve Sangudi  - wakiwa  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018

 Sehemu ya wageni waalikwa wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Sehemu ya wageni waalikwa wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakimsikiliza  mjumbe wa baraza la wadhamini wa JMKF Genevieve Sangudi  akitoa shukurani baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipeana mikono na  mjumbe wa baraza la wadhamini wa JMKF Genevieve Sangudi  baada ya kushukuru kwa uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi akipeana mikono na mjumbe wa baraza la wadhamini wa JMKF Genevieve Sangudi  baada ya kushukuru kwa uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Sehemu ya wageni waalikwa wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakisalimiana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Miraji Kikwete baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wanafamilia yake baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakiongea jambo na Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete na Miraji Kikwete  baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais wakiondoka ukumbini baada ya kuzindua rasmi taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwlimu katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la washamini wa taaisi baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018

 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwlimu katika picha ya pamoja na mabalozi baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwlimu katika picha ya pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwlimu katika picha ya pamoja na wanafamilia wa Kikwete  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Waziri wa MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwlimu katika picha ya pamoja na wake wa viongozi baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea CD toka kwa msanii Goodluck Gozbert  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakielekea kupata chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiongea na mjumbe wa baraza la wadhamini wa JMKF Genevieve Sangudi  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan wakiwakaribisha mabalozi kwa chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018

 Wanafamilia wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na  Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo Bw. Omari Issa
  Wanafamilia wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018

  Wanafamilia wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Wageni waalikwa wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018

  Wageni waalikwa  wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wageni waalikwa  wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Wake wa viongozi wakiwa katika chakula cha jioni  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
  Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mama Sitti Mwinyi  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
   Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi Ombeni Sefue  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
   Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mjumbe wa baraza la wadhamini Bw. Abubakar Bakhressa  baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
   Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Ofisa ubalozi wa Kuwait nchini Bw. Mohammad Rashidi Alamiri baada ya uzinduzi rasmi wa taasisi ya  Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
 Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na wake wa viongozi wakiongea na mjumbe wa baraza la wadhamini wa JMKF baada ya hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018
Mgeni rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akaigana  na Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  baada ya hafla ya uzinduzi wa Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam Jumatano Aprili 11, 2018. Picha na IKULU
Viewing all 46202 articles
Browse latest View live




Latest Images