Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

Rasimu ya Katiba Mchezo wa Ngumi ya kabidhiwa kwa Waziri Mwakyembe

$
0
0

Na Anitha Jonas – WHUSM-Dar es Salaam

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ameipongeza Kamati iliyoandaa rasimu ya katiba ya mchezo wa ngumi nchini kwa kumaliza kazi hiyo kwa wakati.

Mheshimiwa Mwakyembe ametoa kauli hiyo alipokuwa akikabidhiwa rasimu ya katiba hiyo jana jijini Dar es Salaam mara baada kukamilika kwa kuandaliwa kwake na kamati maalum iliyokuwa na wajumbe 13 wakuteuliwa ambao walifanya kazi ya kuzunguka kwa wadau wa ngumi na kukusanya maoni.

“Nitateuwa watu wasaba kutoka katika kamati hii iliyounda rasimu watakao uungana na Baraza la Michezo la Taifa kuboresha rasimu hii ili tuweze kuitisha kikao kikubwa cha wadau wote wa mchezo wa ngumi na tuweze kuipitisha rasimu hii,”Dkt.Mwakyembe.

Akiendelea kuzungumza katika makabidhiano hayo Waziri Mwakyembe alieleza kuwa ataendelea kupokea maoni ya wadau hao ndani ya miezi mitatu kwa kuzingatia sheria ili kufanikisha kikao cha kupitisha rasimu hiyo ambacho kitaitishwa kwa mujibu wa sheria ili kufanikisha lengo la kuboresha sekta ya mchezo wa ngumi nchini.

Pamoja na hayo waziri huyo alisisitiza kuwa na mapema wiki ijayo atamuagiza Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw.Mohamed Kiganja kutangaza wajumbe atakao kuwa amewateuwa kuungana na BMT katika kuboresha rasimu hiyo.

Akizungumza katika sherehe za makabidhiano ya rasimu hiyo ya katiba ya kusimamia mchezo wa ngumi nchini Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bw.Emmanuel Salehe alieleza kuwa pamoja na kukamilisha rasimu hiyo kamati hiyo iliunda pia kanuni za kusimamia mchezo wa ngumi kwa lengo la kuhakikisha misingi imara inawekwa katika kuboresha sekta ya mchezo huo.

Kwa Upande wa Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw. Mohamed Kiganja alisema kuwa ofisi yake iko tayari kuungana na wajumbe watakaoteuliwa na Mheshimiwa Waziri kukamilisha mchakato wa kuboresha rasimu hiyo kabla ya kupitishwa.

Pamoja na hayo naye bondia wa zamani aliyekwisha kushinda katika mikanda ya kimataifa Bw.Rashid Matumla alitoa maoni yake pamoja na kuipongeza serikali kwa kufanya maamuzi ya kuunda chombo imara kitakacho simamia mchezo wa ngumi kwa kuzingatia sheria tofauti na awali huku akiwasihi wadau wangumi kuacha tofauti zao na kuangalia suala la msingi kuboresha mazingira ya mchezo huo na kuufanya uwe na tija kwa zaidi pamoja na kuondoa mazingira yenye utata katika uendeshaji wa mchezo huo.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na wadau wa ngumi (hawapo pichani) kuhusu mchakato wa kukamilisha rasimu ya katiba ya kusimamia mchezo wa ngumi nchini maara baada ya kukabidhiwa jana jijini Dar es Salaam,kulia kwake ni Msajili wa Vyama vya Michezo Nchini kutoka Baraza la Michezo la Taifa Bw. Ibrahim Mkwawa.
Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw.Mohamed Kiganja (kulia) akitoa taarifa kuhusu mchakato wa kuundwa kwa rasimu ya katiba ya mchezo wa ngumi kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) kabla ya makabidhiano ya rasimu hiyo jana jijini Dar es Salaam,wapili kulia ni Msajili wa Vyama vya Michezo Nchini kutoka Baraza la Michezo la Taifa Bw Ibrahim Mkwawa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunda rasimu ya Katiba ya kusimamia mchezo wa Ngumi nchini Bw.Emmanuel Salehe akikabidhi rasimu ya katiba hiyo kwa Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe () jana jijini Dar es Salaam katikati ni Katibu Mtendaji  Baraza la Michezo la Taifa Bw.Mohamed Kiganja.
Mmoja wa wanakamati waliyoandaa rasimu ya Katiba ya kusimamia mchezo wa ngumi Bw.Ally Champion akitoa maoni yake na kuwasihi wadau wangumi kuacha tofauti zao za vikundi vyao waungane kwa lengo la kuimarisha mchezo wangumi kwa taifa jana katika mkutano wa kukabidhi rasimu hiyo kwa Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (hayupo pichani).
Baadhi ya wajumbe waliyoandaa rasimu ya Katiba ya kusimamia mchezo ngumi wakiwa katika picha ya pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (wanne kulia)mara baada ya kumkabidhi rasimu hiyo jana jijini Dar es Salaam,watatu kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunda rasimu hiyo Bw.Emmanuel Salehe na watatu kulia ni Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa Bw.Mohamed Kiganja.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza bondia wa kike Bi.Feriche Mashauri (kulia) alipokuwa akimweleza changamoto za mchezo wa ngumi nchini jana jijini Dar es Salaam baada ya Waziri kukabidhiwa rasimu ya mchezo wa ngumi .

WANA CCM MUHEZA WAADHIMISHA MIAKA 41 KUSHRIKI MSARAGAMBO UJENZI WA HOSPITALI

$
0
0
 Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza,Like Gugu kulia akiwa na Katibu Tawala wa wilaya hiyo,Desderia Haule kushoto wakishirikiana na wananchi na wanachama wa chama hicho kushiriki msaragambo wa ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo 
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza,Like Gugu kulia akiwa na Katibu Tawala wa wilaya hiyo,Desderia Haule kushoto wakiwa na mashepe wakishirikiana na wananchi na wanachama wa chama hicho kubeba kukoto kwa ajili ya ujenzi ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo 
Sehemu ya wananchi wakishriki kwenye zoezi la kubeba maji kwa ajili ya kushiriki Msaragambo wa Ujeniz wa Hospitali ya wilaya ya Muheza 
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza,Like Gugu kushoto akishusha ndoo iliyokuwa na zege kwa ajili ya kusambazwa kwenye msingi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ambapo Mwenyekiti huyo aliwaongoza wanachama wa chama hicho kushiriki kwenye msaragambo huo
Sehemu ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM wakishiriki kwenye kuchanganya zege
Sehemu ya wana CCM na wananchi wakishirikiana kubeba zege tayari kuimwaga kwenye msingi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Muheza wakati waliposhiriki Msaragambo ambao uliongozwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza,Like Gugu (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

WANANCHI BOMBABILI WAPEWA SOMO UPIMAJI WA ARDHI

$
0
0
Na David John

WANANCHI wa mtaa wa Bombambili Kata ya Kivule wamepewa somo kuhusu suala zima la upimaji wa ardhi, huku wakielezwa umuhimu wa kurasimisha ardhi yao kwa lengo la kuzifikia huduma mbalimbali za kiserikali

Akizungumza katika mkutano wa wananchi wa mtaa huo ambao uliitishwa na ofisi ya Serikali hiyo. Adolph Milunga ambaye ni mtalaamu mpimaji kutoka chuo cha ardhi mkoani Morogoro aliwaeleza wananchi hao umuhimu wa kupima ardhi na faida Zake.

Amesema hata kuchagua watalaamu kutoka chuo cha Ardhi Morogoro hawajafanya Makosa Kwani ni uhakika kwamba serikali ndio inasimamia ambapo kupimwa kwa ardhi kunakufanya kuondoka kwenye umasikini.

Ameongeza kuwa kupimwa kwa ardhi kunakuwezesha kupata dhamana Mahakamani na mambo mengine kama mirathi. Lakini pia mikopo kwa urahisi tofauti na kuwa na ardhi ambayo haijapimwa.

" wao kama watalaamu wa serikali wanafanya kazi hiyo kwa uadilifu mkubwa mno na kwenye mtaa huu tumetoa ofa ya 160,000 na ofa hii itadumu kwa wiki moja. "alisema . Pia amesema baada ya kumalizika kwa wiki moja hakutakuwa tena kwa maana ahadi tena ya ofa hata hivyo watakwenda kuchungulia na kuona kuna nini kipo huko Benki.

"kuhusu hati baada ya mchakato wa upimaji kumalizika zitakuja kukabidhiwa katika mtaa huo tena ikiongozwa na Waziri husika wa ardhi. Nakusisitiza kuwa watakuwa tayari kwenda nawale ambao wako Tayari kufanya nao kazi. "amesema Milunga.

Hata hivyo Mwenyekiti wa mtaa huo. Moses Malela aliomba watalaam had wa upimaji kuongeza ofa hiyo angalau iwe ya wiki mbili . Kwaupande mwingine Mtalaamu huyo alikubaliana na Mwenyekiti huyo wa serikali nakusisitiza kwamba atatoa majibu halisi ijumaa ya wiki inayoaza kesho.

Pia mtalamu huyo alitoa ofa nyingine kwa taasisi za dini kwa kuchangia shilingi 100000 ili nao waweze kupimiwa huku akitangaza ofa nyingine kwa watu wasiojiweza kabisa. Wakati huohuo mwenyekiti aliwahamasisha wananchi wake kupima ardhi nakusisitiza kwamba faida hiyo sio ya serikali bali ni ya kwao.

Amesema kupima ardhi nikufungua vichocheo vya maendeleo ikiwa pamoja na kukaa katika maeneo ambayo yamepimwa na hayo pia ilikuwa nimoja ya ahadi zao wao kama viongozi kwamba watahakikisha wakiingia watapambana ili kuona ardhi yao inapimwa.

Selemani Kimeya alishukuru mchakato huo wa upimaji lakini alidai kiwango cha pesa iliyotajwa kulipa kwa mara moja ningumu nakuhoji kwanini wasilipe mara mbili. Salimin Issa naye alisema hadi wanakwenda kwenye mkutano kero kubwa ilikuwa ni shilingi 310,000/= hawana na hiyo pesa badala yake wangepunguza zaidi.

Aidha wananchi hao pamoja na mambo mengine lakini walikuwa wanahitaji kamati yao ili iweze kusimamia mchakato huo nakudai kamati hiyo iliyokuwepo ni ya zamani ambayo ilikuwa kivule na sasa bombambili hata hivyo walifafanuliwa juu ya hilo na mwisho kukubaliana na kamati iliyopo.

POLEPOLE AMNADI MTULIA KWA KISHINDO KATA YA MUZIMUNI, MAGOMENI JIJINI DAR ES SALAAM, LEO

$
0
0
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akitema cheche wakati akimnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.

 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akiingia kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Wananchi na wana CCM wakitimua vumbi kumlaki Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole , alipowasili kwenye viwanja vya Mtambani, kumnadi mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Kinondoni  Maulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimsalimia Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni baada ya kuwasili kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia (wa pili kushoto) katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni katibu wa CCm mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akimsalimia mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Kamba baada ya kuwasili kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole na viongozi wengine wa meza kuu wakishangilia baada ya kuwasili, kumnadi Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.
 Katibu wa Halmashauri Kuu ya taida (NEC) ya CCM Humphrety Polepole akisaini kitabu cha wageni baada ya kuketi
 Mwenyekiti wa zamani wa Wilaya ya Kinondoni Ndugu Londa akizungumza baada ya kukaribishwa jukwaani kusalimia
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Kate kamba akimkaribisha Ndugu Polepole jukwaani baada ya kuhutubia
 Ndugu Polepole akitamba jukwaani kabla ya kumwita jukwaani Ndugu Mtulia kumnadi
 Polepole akimnadi Mtulia kwa wananchi
 Mtulia na Polepole wakionyesha furaha jukwaani wakati wakishangiliwa na wananchi
 "Ukishachaguliwa hawa wananchi wasaidie sana kutatua matatizo yao, maana wanakuamini na wanaaiamini CCM ndiyo maana watakuchagua" akasema Polepole kumwambia Mtulia (kushoto)
 " Na utatutuzi wa matatizo ya wanancho kwako utakuwa rahisi ukitumia Ilani hii ya CCM, maana kila kitu kimo humu" akaongeza Ndugu Polepole kumwambia Ndugu Mtulia kabla ya kumkabidhi kitabu hicho cha Ilani ya CCM ya 2015-2020
 Wananchi na wana CCM wakilipuka kwa nderemo wakati Ndugu Polepole akimnadi Mtulia
 Ndugu Polepole akimpongeza Mtulia baada ya kumkabidhi Ilani hiyo
 Kisha akamuasa zaidi
 Wananchi wakizidi kushangilia kwa vifijo
 Mgombea Ubunge katika uchaguzi mdogo Jimbo la Kinondoni Said Mulid Mtulia akiomba kura katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanayika leo katika Viwanja vya Mtambani, Kata ya Muzimuni, Magomeni jijini Dar es Salaam, leo.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

WAZIRI MAHIGA AHITIMISHA ZIARA YAKE KOREA KUSINI

$
0
0
Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa kwenye mazungumzo na Bw. Chang Yaong Hun, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim ya Korea Kusini. Viongozi hao wawili walikutana kwenye ofisi za Benki hiyo Jijini Seoul Korea Kusini wakati wa ziara ya kikazi ya siku tatu ya Waziri Mahiga nchini humo.
:Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na ujumbe wake kwenye mazungumzo na Bw. Chang Yaong Hun, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim ya Korea Kusini. Viongozi hao wawili walikutana kwenye ofisi za Benki hiyo Jijini Seoul Korea Kusini.
Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa kwenye picha ya pamoja na Bw. Jundong Kim, Makamu Mwenyekiti wa Korea Chamber of Commerce and Industries (KCCI). Mwingine pichani ni Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea Mheshimiwa Matilda Masuka. 
Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa na ujumbe wake kwenye mazungumzo na Bw. Jundong Kim, Makamu Mwenyekiti wa Korea Chamber of Commerce and Industries (KCCI). 
Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akimkabidhi zawadi ya majani ya chain a kahawa za Tanzania Bw. Choi Jong-won, Makamu Mwenyekiti wa Kampuni ya Dong Myeong ya Korea Kusini.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga ameahidi kusimamia uimarishwaji wa uhusiano wa kiuchumi na biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini ili wananchi wa pande zote mbili wapate manufaa. 

Waziri Mahiga ameyasema hayo alipokuwa anahitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu ambapo siku ya mwisho aliitumia kikamilifu kukutana na taasisi za umma za biashara na viwanda, Benki ya Exim ya Korea pamoja na makampuni binafsi yanayojipanga kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania. 

Amesema kuwa miaka 25 ya kwanza ya uhusiano wetu na Jamhuri ya Korea ilijikita kwenye kuweka misingi imara ya uhusiano wa kidiplomasia ambapo nchi zetu zilikuwa zinajiimarisha kama mataifa huru. “Sasa ni wakati wa kushamiri kiuchumi tuone sekta binafsi zinavyoshiriki katika kukuza uchumi, wananchi wa Tanzania waje kwa wingi nchini Korea kujifunza masuala ya teknolojia, uhandisi na hata usanifu na ubunifu. Huu ndio uhusiano wenye tija kwa mataifa yetu”. Mheshimiwa Waziri alisema.

Akizungumza na Bw. Chang Yaong Hun, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim ya Korea, Mheshimiwa Mahiga mbali na kuishukuru taasisi hiyo kwa kuendelea kutoa mikopo na misaada nchini Tanzania, Waziri Mahiga alieleza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli sasa imejikita kwenye mapambano dhidi ya rushwa na ujenzi wa viwanda ili kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wetu. Kwasasa Benki hiyo inatekeleza miradi ya ujenzi wa miundombinu ya umeme na maji mikoa mbalimbali ya Tanzania ukiwemo Mkoa wa Dar es Salaam. 

Mheshimiwa Mahiga alifafanua kuwa ajenda ya Mheshimiwa Magufuli ya viwanda, haiwezi kukamilika bila kuwa na miundombinu ya msingi kama vile uzalishaji wa umeme wa kutosha na ukuaji wa sekta ya uchukuzi na mawasiliano ambapo Korea Kusini ni wabobezi kwenye masuala hayo. 

Alitumia fursa hiyo kumkaribisha Bw. Chang na timu yake kwenda Tanzania kufanya tathmini ya miradi tunayoshirikiana nao, lakini pia miradi mipya kwenye sekta ya uchukuzi kama ujenzi wa Standard Railway Gauge “SRG” kutoka Isaka hadi Kigali, n.k. ambayo ni miradi ya kipaumbele kwa sasa kwa taifa letu. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Chang alisifu utendaji kazi wa Rais John Pombe Magufuli, na Serikali ya awamu ya tano ya Tanzania na kusema kuwa utendaji kazi wa aina hii ni wa kupigiwa mfano barani Afrika, na umekuja wakati muafaka tunapoingia kwenye hatua nyingine ya uhusiano wa kiuchumi baina ya nchi zetu mbili. Aidha aliongeza kuwa, wakati umefika sasa wa kufanya kazi, nay eye yuko tayari kufanya kazi na Tanzania kwani Serikali yake, imetoa kipaumbele kwa nchi hii. 

Korea Exim Bank ni taasisi ya Serikali inayosimamia mikopo na misaada ya Jamhuri ya Korea inayotoa kwa nchi nyingine. Katika kipindi cha miaka minne (tangu 2016 hadi 2020), Korea Kusini kupitia taasisi hiyo, imeongeza mikopo ya maendeleo kwa bara la Afrika kwa asilimia 20. Uamuzi wa Serikali iliyokuwa madarakani mwaka 2016 wa kuichagua Tanzania kupokea kiasi kikubwa cha msaada huo kuliko nchi nyingine ya Afrika, umeendelezwa na Serikali iliyopo sasa madarakani ya Mheshimiwa Moon Jae-in, Rais wa Jamhuri ya Korea. 

Ujumbe wa Mheshimiwa Augustine Mahiga pia ulikutana na kufanya mazungumzo na Bw. Judong Kim, Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara na Viwanda ya Korea (Korea Chamber of Commerce and Industries KCCI), ambapo Waziri Mahiga aliwasisitiza kuja Dar es salaam kuangalia fursa zilizopo ili kuwashawishi wanachama wao kutafuta bidhaa na masoko nchini Tanzania. 

Akielezea umuhimu wa KCCI kuzuru Tanzania na kujifunza soko la biashara, Bw. Edwin Rutageruka Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE aliyeongozana na ujumbe wa Mheshimiwa Waziri Mahiga, alisema njia nzuri ya kupata picha halisi ni kupitia Maonesho ya Biashara ya Saba Saba. Hivyo alitumia fursa hiyo kualika ujumbe wa KCCI kushiriki kwenye maonesho ya 42 yanayotarajiwa kuanza tarehe 28 Juni – 10 Julai, 2018. 

Kabla ya kuhitimisha ziara yake, Mheshimiwa Mahiga pia alikutana na kufanya mazungumzo na watendaji wakuu wa makampuni ya DOHWA, ambao wamejikita kwenye ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya reli n.k. Makampuni mengine ni KORAIL, STX Engine, KTMI & STX Offshore pamoja na GS E&C, ambao wote wameonesha nia ya kuwekeza au kufanya biashara nchini Tanzania. Ujumbe mkuu kwa taasisi na makampuni hayo ulikua ni kupanua fursa za ushirikiano wa biaashara na uwekezaji, ubadilishanaji wa ujuzi na ujengaji uwezo wa wafanyakazi ambao ndio nguvu kazi ya taifa letu.

Pamoja na kuzungumza na makampuni ya umma na sekta binafsi yaliyoorodheshwa hapo juu, ziara ya Mheshimiwa Augustine Mahiga, ilimuwezesha kuwa mgeni rasmi kwenye Kongamano la Kwanza la Biashara kati ya Tanzania na Korea Kusini ambapo alihutubia mamia ya wafanyabiashara wa Korea kuhusu utayari wa Tanzania kushirikiana na nchi hiyo kibiashara. 

Mkutano huo uliopewa kauli mbiu ya “Eplore Tanzania” ulifuatiwa na mikutano midogo midogo iliyowakutanisha baadhi ya wafanyabiashara wa Tanzania na Korea Kusini ili kuangalia kwa ukaribu maeneo ya ushirikiano. Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini na mwenzake wa Korea Kusini nchini Tanzania wameazimia kuendeleza makongamano hayo ya kila mwaka ili kuwa na ushirikiano wa karikiano wa karibu wa kibiashara kwa mataifa hayo mawili kwa maendeleo ya wananchi wote. 

Wajumbe wengine walioongozana na Mheshimiwa Waziri Mahiga nao walipata fursa ya kuhutubia hadhara hiyo kuhusu Tanzania ambapo Bw. Geoffrey Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Investment Centre alitoa utangulizi kuhusu uwekezaji Tanzania; Kanali (mstaafu) Joseph Simbakalia, Mkurugenzi Mkuu wa EPZA alizungumzia maeneo ya kipaumbele kwenye maeneo maalum ya uwekezaji nchini Tanzania. Naye Bi. Nasriya Nassor, Mkurugenzi wa Biashara wa Taasisi ya Uwekezaji Zanzibar alitoa taarifa fupi kuhusu Zanzibar kama kivutio cha utalii ndani ya Tanzania na eneo linalopendelewa na watalii wengi duniani.

Jamhuri ya Korea, kama inavyojulikana rasmi na Umoja wa Mataifa, ni mojawapo ya nchi zinazofanya vizuri zaidi duniani kiuchumi kwa sasa. Viashiria vya uchumi vinaonyesha uchumi wa nchi hiyo utaendelea kukua kwa viwango kutokana na jitihada za dhati za viongozi wa nchi hiyo za kufuta kabisa umaskini kwa wananchi wao. Kwa sasa wastani wa pato kwa mtu “per capital income” inakadiriwa kuwa zaidi ya US$ 34,000, ukilinganisha na US$ 22,670 mwaka 2012. Baada ya vita ya Korea kwenye miaka ya mwanzo ya 1950, nchi ya Korea Kusini ilikua maskini kuliko nchi nyingi barani Afrika ikiwemo Tanzania ambapo wastani wa pato kwa mtu ilikua na US$67.

Mheshimiwa Mahiga anatarajiwa kurejea nyumbani baada yakuhitimisha ziara hiyo aliyosema italeta faida sio tu kwa wafanyabiashara, ila kwa jamii kwa ujumla. “Nchi hii ni tajiri sana kiuchumi; lakini utajiri wake mkubwa pia uko kwenye taaluma ya rasilimali watu, hivyo kwa Tanzania kufanikiwa kufungua ubalozi hapa, sasa tumefungua milango ya ushirikiano wa karibu, kuliko ilivyokuwa mwanzo. Tuchangamke tuige mfano wa uchapa kazi wao, na sisi tutaondoka kwenye umasikini” Waziri Mahiga alisema kwa umaliza, kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Incheon, uliopo mjini Seoul, Jamhuri ya Korea.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Seoul, Korea Kusini, 
3 Februari 2018.

TATUMZUKA YACHANGIA VIFAA VYA SHULE NA MATANKI YA MAJI WILAYA YA UBUNGO.

$
0
0
 Katibu Tawala wilaya ya Ubungo ,James Mkumbo akizungumza na Waandishi wa habari mwishoni mwa wiki kuhusu wilaya hiyo kupokea msaada wa baadhi ya vifaa Vya shule,kama vile Madawati 25,Vitabu 131 pamoja Matanki makubwa mawili  ya kuhifadhia maji kutoka kwa wachezeshaji wa Mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka.Kulia ni Mwakilishi wa TatuMzuka,Bi Patronela. Mkumbo alisema kuwa wamepewa msaada wa vifaa hivyo kutokana na mkazi wa wilaya hiyo ya Ubungo,aitwaye Catherine Tryphone kushinda kitita cha Milioni 60 kupitia mchezo huo wa TatuMzuka.
 Mwakilishi wa mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka,Bi.Patronela akikabidhi Vitabu 131 kwa ajili ya shule za Wilaya hiyo kwa  Katibu Tawala wilaya ya Ubungo ,James Mkumbo,kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya  hiyo,Ally Juma Ally akishuhudia tukio hilo.
 Mwakilishi wa mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka,Bi.Patronela akikabidhi madawati 25 kwa Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya hiyo,Ally Juma Ally,pichani kati anaeshuhudia ni Katibu Tawala wilaya ya Ubungo ,James Mkumbo.Pichani nyuma kulia ni moja ya tanki lililokabidhiwa kwa viongozi hao wa Serikali.

taarifa ya maadhimisho ya 19 kumbukizi ya prof Kairuki

$
0
0
  

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Herbert Kairuki Memorial, Prof. Chales Mgone akiongea na waandishi wa habari kwenye mkutano nao uliohusu maadhimisho ya Kumbukizi ya Mwasisi na Mmiliki wa Shirika la Elimu Kairuki (KHEN), Chuo Kikuu cha Kumbukumbuku ya Hubert Kairuki (HKMU), Hospitali ya Kairuki (KH)  na Shule ya Uuguzi Kairuki (KSN). Mkutano huo umefanyika Dar es Salaam leo Februari 4 2018. Kushoto ni Makamu Mkuu wa HKMU (Taaluma), Prof. Ntabaye Moshi na Mkurugenzi wa chuo hicho, Dkt. Asser Mchomvu. (Na Robert Okanda Blogs)
Mkurugenzi wa chuo hicho, Dkt. Asser Mchomvu, akiongea na waandishi wa habari kwenye mkutano uliohusu maadhimisho ya Kumbukizi ya Mwasisi na Mmiliki wa Shirika la Elimu Kairuki (KHEN), Chuo Kikuu cha Kumbukumbuku ya Hubert Kairuki (HKMU), Hospitali ya Kairuki (KH)  na Shule ya Uuguzi Kairuki (KSN). Mkutano huo umefanyika Dar es Salaam leo Februari 4 2018. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Herbert Kairuki Memorial, Prof. Charles Mgone na Makamu Mkuu wa HKMU (Taaluma), Prof. Ntabaye Moshi. 

HUBERT KAIRUKI KUJENGA KITUO KUSAIDIA WENYE MATATIZO YA UJAUZITO

$
0
0
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), Professa Charles Mgone akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano iliohusu maadhimisho ya Kumbukizi ya muasisi na Mmiliki wa Shirika la Elimu Kairuki (KHEN), Chuo Kikuu cha Kumbukumbuku ya Hubert Kairuki (HKMU), Hospitali ya Kairuki (KH) na Shule ya Uuguzi Kairuki (KSN). Mkutano huo umefanyika Dar es Salaam leo Februari 4, 2018. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo HKMU (Taaluma), Prof. Ntabaye Moshi na Mkurugenzi wa Hospitali ya Hubert Kairuki, Dkt. Assey Mchomvu. 

Na Cathbert Kajuna- Kajunason/MMG.

 Katika kuadhimisha miaka 19 ya kumbukizi ya Marehemu Profesa Hubert Kairuki, Shirika la afya na elimu la Kairuki limejipanga kujenga kituo cha kusaidia watu wenye matatizo ya kupata ujauzito kwa njia ya kawaida. Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), Professa Charles Mgone amesema kuwa maadhimisho hayo yaliyoanza tokea Februari 1-6, 2018 jambo kubwa wamejipanga kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha kusaidia watu wenye matatizo ya kupata ujauzito kwa njia ya kawaida huko Bunju jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi atakuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Ali Hapi. 

"Kumekuwa na matatizo hasa ya ukosefu wa vituo vya kuwasaidia watu wenye matatizo ya uzazi jambo linalotupa msukumo wa kuanza ujenzi huu, kwa sasa tupo katika hatua za mwisho tupate kibali tuanza ujenzi maana sisi tumeshajipanga na tumeshazalisha wataalamu wa kutosha," alisema Prof. Mgone. Professa Mgone amesema kukamilika kwa kituo hicho kitakuwa msaada mkubwa maana mpaka sasa hospitali ya Hubert Kairuki imekuwa chachu katika utoaji wa huduma ya afya ambapo kwa siku wanapokea zaidi ya wagonjwa 700. 

Aliongeza kuwa mbali na ujenzi wa kituo hicho wanatarajia kuanzisha kliniki ya mama, baba na mtoto huko Bunju ili kuendeleza kuokoa vifo vya akinamama na watoto hasa waliombali na huduma. Jambo lingine ambalo wanalifanya katika maadhimisho hayo ni kutoa huduma za afya bure kwa kipindi cha kuanzia Februari 1-6, 2018  kwenye Hospitali ya Kairuki, pia wanajitolea damu kwa hiari ili kuokoa vifo vitokanavyo na ukosefu wa damu. 

 Vile vile wanafunzi wa Chuo cha Kumbukumbu cha Hubert Kairuki watashiriki katika shindano la kujipima ujuzi juu ya mambo mbalimbali katika taaluma ya afya, maswali ya ufahamu kuhusu Tanzania, maisha ya mhasisi Marehemu Prof. Kairuki, Jiografia na jamii kiujumla. Mwisho wa kilele cha maadhimisho hayo kutafanyika mhadhara wa kitaaluma utakaoendeshwa na Professa Malise Kaisi juu ya mada 'Maono ya Prof. Hubert Kairuki yanayodumu': Umuhimu wake katika utoaji wa huduma za afya barani Afrika. 

 Shirika la Afya na Elimu la Kairuki (KHEN) limasimamia Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), Hospitali ya Kairuki (KH) na Shule ya Uuguzi Kairuki (KSN) ambapo muasisi wake ni marehemu Hubert Clement Mwombeki Kairuki aliyezaliwa Juni 24, 1940 Bukoba mkoani Kagera. Mnamo Machi 17, 1987 muasisi huyo alianzisha hospitali ya TAG Mikocheni na mwaka 1992 aliibadilisha jina na kuitwa Mission Mikocheni hospitali ambayo kwa sasa inaitwa Kairuki Hospitali. Mwaka 1997, Prof. Kairuki alianzisha Mikocheni International University na baadae miaka 2 kupita alifariki dunia Februari 6, 1999 na chuo kikabadilishwa kuwa Hubert Kairuki Memorial Univesity. 

 Wakati hospitali inaanzishwa ilikuwa walikuwa na uwezo wa kupokea wagonjwa wa nje 200 na wagonjwa wa ndani 30 kwa siku na kwasasa hospitali inauwezo wa kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje 700 kwa siku na wagonjwa 150 wa ndani ambapo wakati muasisi anafariki chuo kilikuwa na wanafunzi 30 katika fani ya udaktari na uuguzi kwasasa chuo kinatakribani wanafunzi 1509.

NAIBU GAVANA BENKI KUU TANZANIA (BOT) AFUNGUA SEMINA YA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UCHUMI NA FEDHA MKOANI MTWARA

$
0
0
ki01
Bw. Julian Raphael Banzi Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC) akifungua semina ya siku tano ya waandishi wa habari kuhusu masuala ya Uchumi inayofanyika katika ukumbi wa BOT Mtwara., Waandishi wa habari watapata ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu masuala ya uchumi, Kama vile Mabadiliko ya Mfumo mpya wa Kuandaa sera ya Fedha, Mapitio ya Maendeleo ya Uchumi nchini, Kikanda na Kimataifa BDuniani, Mifuko ya Dhamana kwa wajasiliamali na mengine mengi.

Akizungumza wakati akifungua semina hiy.Banzi  amewashukuru waandishi wa habari kwa kazi kubwa wanayofanya katika kuandika habari za Benki Kuu kuhusu masuala ya uchumi, na pia akawaasa kuandika habari zinazohusu utekelezaji wa miradi mikubwa mbalimbali inayoendelea nchini ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), Miradi ya Umeme , Bomba la Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda Mpaka Tanga nchini Tanzania na mingine mingi inayoendelea kutekelezwa.
ki5
Mkurugenzi wa BOT,Lucas Mwimo Tawi la Mtwara akimkaribisha  Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC),Julian Raphael Banzi ili kufungua semina hiyo.
ki1
 Meneja Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BOT),Bi Zalia Mbeo akitambulisha wageni mbalimbali katika semina hiyo.
ki3
Bw. Julian Raphael Banzi Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC) kulia, Bw. Lucas Mwimo Mkurugenzi wa BOT Tawi la Mtwara katikati na Jonson Myella Mkurugenzi Tafiti za Uchumi (BOT) wakiwa katika semina hiyo.
ki6
Bw. Julian Raphael Banzi Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC) na Bi Zalia Mbeo Meneja Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BOT) wakifuatilia hotuba ya Bw. Lucas Mwimo Mkurugenzi wa BOT Tawi la Mtwara hayupo pichani wakati wa ufunguzi wa semina hiyo.
13
Jonson Myella Mkurugenzi Tafiti za Uchumi (BOT) na maofisa wenzake wakiwa katika semina hiyo.
ki7
Vick Msima Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki akiwa pamoja na maofisa wenzake kutoka BOT wakifuatilia hutoba ya Bw. Julian Raphael Banzi Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC).
4
Vick Msima Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki akitoa ratiba kwa washiriki wa semina hiyo.
567
Mwenyekiti wa Semina hiyo Bw. Ezekiel Kamwaga akitoa maelezo mafupi kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
8
Katibu wa Semina hiyo Dorcas Mtenga kutoka Chanel Ten akizungumza machache kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
10
Mwenyekiti wa Semina hiyo Bw. Ezekiel Kamwaga akitoa maelezo mafupi kabla ya kuanza kwa semina hiyo.
12
Bw. Casmir Ndambalilo kutoka Idara ya Habari Maelezo akitaka ufafanuzi wa jambo katika semina hiyo kulia ni Goodluck Msola kutoka EFM.
ki2
Bw. Khalfan Said wa K-Vis Blog akifanya vitu vyake kwa ajili ya matukio ya semina hiyo.
IMG_1358
Bw. Julian Raphael Banzi Naibu Gavana wa Benki Kuu Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa semina hiyo mara baada ya kufanya ufunguzi rasmi.

WAZIRI MKUU KATIKA HAFLA YA CHAKULA CHA MCHANA NA WATU WENYE ULEMAVU

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi, katika hafla ya chakula cha mchana kwa ajili ya watu wenye ulemavu, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Februari 4, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na muimbaji wa muziki wa kizazi kipya, Saida Kalori, katika hafla ya chakula cha mchana kwa ajili ya watu wenye ulemavu, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Februari 4, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi walioshiriki katika hafla ya chakula cha mchana kwa ajili ya watu wenye ulemavu, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Februari 4, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpatia chakula mtoto Mwahija Hassan, katika hafla ya chakula cha mchana kwa ajili ya watu wenye ulemavu, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Februari 4, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpatia chakula mtoto Ibrahim Shaibu, katika hafla ya chakula cha mchana kwa ajili ya watu wenye ulemavu, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee. Februari 4, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

NAIBU GAVANA WA BoT DKT. BANZI AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUTANGAZA KWA KINA JITIHADA ZA SERIKALI ZA KUJENGA UCHUMI

$
0
0
 Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Julian Raphael Banzi, akitoa hotuba ya ufunguzi wa warsha kwa waandishi wa habafri za Uchumi, Biashara na Fedha, mkoani Mtwara leo Februari 5, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mtwara
WAANDISHI wa Habari za uchumi na Fedha, wameaswa kutumia kalamu zao vema ili kuongeza tija katika jitihada za serikali za kujenga uchumi wa viwanda nchini ifikapo mwaka 2025, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt.Julian Raphael Banzi amesema leo Februari 5, 2018 wakati akifungua semina ya waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha kwenye ukumbi wa BoT , mkoani Mtwara.
“Waandishi mnao wajibu wa kuamsha ari ya uelewa kwa wananchi kuwaelimisha nini serikali inafanya kwa ajili ya nini na kwa utaratibu upi.” Alisema Dkt. Banzi na kuwaasa badala ya waandishi kutumia muda mwingi kuandika maswala ambayo hayasaidii sana katika kusaidia ujenzi wa uchumi, ni vema sasa wakaangazia katika kuelimisha umma juu ya jitihada za serikali wakati huu ambapo kuna utekelezaji wa miradi mbali mbali ya kiuchumi kama vile jenzi wa reli ya kisasa, (SGR).
Naibu Gavana pia amewataka waandisjhi wa habari kuwafichua wale wanaokatisha tama au kukwamisha uwekezaji nchini kwani kwa kutofanya hivyo waandishi wa habari watakuwa hawawatendei haki wananchi na umma kwa ujumla.
Alisema kuwa BoT inaposema pato la taifa limeongezeka, haimaanishi kwamba wananchi wanajazwa pesa mfukoni lakini pia mwananchi inabidi ajiulize yeye mwenyewe anashiriki vipi katika ujenzi wa uchumi ili kuweza kufaidika na pato lenyewe.
“Kwa msingi huo elimu mtakayopata hapa katika kipindi cha siku tano, itawaongezea uwezo wa kufanya uchambuzi wa kina mnapoandika makala ze uchumi, biashara na fedha ili ziweze kuufikia umma kwa usahihi na kuepuka upotoshaji.” Alisema Dkt. Banzi.
Kwa upande wake, Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Itifaki cha BoT, Bi. Zalia Mbeo, alisema semina hii ni ya tano ambazo BoT imekuwa ikifanya kila mwaka, ili kujenga uelewa kwa waandishi kuweza kuandika kwa usahihi shughuli za BoT.
“Tumezidi kuona mafanikio makubwa tangu tuanze kutoa semina kwa waandishi wa habari kwa waandishi wamekuwa wakijitahidi kuandika kwa usahihi taarifa za BoT.” Alisema.
Bi Mbeo pia alisema katika semina ya mwaka huu, waandishi watapata fursa ya kuelimishwa mambo mbalimbali kutoka Kurugenzi ya sera na tafiti za uchumi, kurugenzi ya masoko ya fedha, kurugenzi ya usimamizi wa ,mabenki, kurugenzi ya huduma za kibenki na kurugenzi ya mifumo ya malipo, na pia kuna ushiriki kutoka kurugenzi ya bima ya amana.
“Mwaka huu tuna kurugenzi ya Katibu wa Boadi ambayo itaelezea dawati ambalo linashughulikia matatizo ya watu wanayoyapata katika huduma mbalimbali za kibenki, na kwa kupitia waandishi wa habari, tunategemea wataelimisha umma kuhusu dawati hili.” Alisema Bi. Mbeo.

 Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Julian Raphael Banzi, akitoa hotuba ya ufunguzi wa warsha kwa waandishi wa habafri za Uchumi, Biashara na Fedha, mkoani Mtwara leo Februari 5, 2018. Wengine pichani kutoka kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Itifaki, Benki Kuu ya Tanzania, Bi. Zalia Mbeo na Mwenyekiti w aSemina, Bw. Ezekiel Kamwaga,
 Baadhi ya waandishi wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi.
 Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia yaliyokuwa yakizungumzwa kwenye warshan hiyo
 Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Itifaki, BoT, Bi. Zalia Mbeo, akielezea maudhui ya semina hiyo ambayo itafanyika kwa siku tano kuanzia leo Februari 5, 2017.
 Meneja wa tawi la Benki Kuu ya Tanzania Mkoani Mtwara, Bw.Lucas Mwimo, akitoa hotuba ya ukaribisho

 Bi.Vicky Msina, kutoka Kitengo cha Uhusiano na Itifaki BoT. akizunguzma mapema wakati wa ufunbguzi wa warsha hiyo.
  Bi.Vicky Msina, kutoka Kitengo cha Uhusiano na Itifaki BoT. akizunguzma mapema wakati wa ufunbguzi wa warsha hiyo.
 Baadhi ya washiriki

 Mwenyekiti wa Warsha hiyo, Bw. Ezekiel Kamwaga akitoa hotuba yake.


 Dkt. Banzi akipeana mikono na Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Uchumi BoT, Bw, Johnson Nyella

 Dkt. Banzi, (katikati), Bi Zalie, na Bw.Mwimo





  Maafisa waandamizi wa BoT.
 Mkurugenzi wa Uchumi BoT, Bw, Johnson Nyella, akitoa Mada ya Mabadiliko ya mfumo wa kuandaa sera ya fedha, ambapo pa,moja na mambo mengine alisema pato la taifa ni mjmuiko wa thamani ya vitu vyote vilivyozalishwa katika uchumi kwa kipindi husika.
Meza kuu

MWANAHABARI PATRICK MWILLONGO ANAHITAJI MSAADA WA MATIBABU

$
0
0
Ndugu wanahabari mwenzetu Patrick Mwillongo yupo hoi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke ambako amelazwa kwa matibabu.

Mwillongo anasumbuliwa na ugonjwa wa kujaa maji kwenye mapafu ambao umesababisha hashindwe kujimudu kufanya jambo lolote.

Kwa umoja wetu na tabia tuliojijengea kama wanahabari tujitokeze kumsaidia mwenzetu ambaye anapita katika kipindi kigumu.

Mwillongo ni Mwandishi wa Habari wa kujitegemea
 na anafanya shughuli zake wilayani Bagamoyo mkoani Pwani na awali alikuwa akiandikia magazeti mbalimbali likiwemo Jambo Leo na yale yanayomilikiwa na Kampuni ya New Habari.

Kwa atakayegusa kumsaidia anaweza kutoa mchango wake kupitia namba MPESA-0754362990, Tigo Pesa ni 0712727062.
Wanahabari Hellena Mwango, Careen , Kulwa Mwaibale na mke wa Patrick Mwillongo wakiwa wamekaa nje ya jengo la Hospitali ya Mkoa Temeke wakitafakari namna ya kumsaidia Mwillongo walipofika  kumjulia hali leo hii asubuhi.

WADAU HAKI JINAI WAHIMIZWA KUSHIRIKIANA KUTOA HAKI KWA WAKATI

$
0
0

Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akifunga Kongamano la Wadau wa Haki Jinai lililofanyika katika Kituo cha Mafunzo na Habari kilichopo eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, katika maneno yake ya kufunga, Mhe. Jaji Wambali amewataka Wadau kuendeleza ushirikiano ili kuiwezesha Mahakama kutoa haki kwa wakati.
Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama-Lushoto (IJA) (aliyesimama mwenye tai akitoa maelezo mafupi kwa Mgeni rasmi juu ya Mafunzohayo kabla ya kufunga rasmi Kongamano hilo.
Mgeni rasmi, Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akikabidhi cheti cha Ushiriki kwa mmoja wa Washiriki wa Kongamano hilo, Mhe. Jaji Firmin Nyanda Matogolo.
Mgeni rasmi, Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wahe. Majaji wa Mahakama Kuu na baadhi ya Watumishi wa Mahakama walioshiriki katika Kongamano.
Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Washiriki wa Kongamano. (Picha na Ibrahim Mdachi, IJA)

Na Mary Gwera, Mahakama

WADAU wa Haki Jinai nchini wameazimia kwa pamoja kukuza ushirikiano baina yao katika kushughulikia uhalifu wa makosa yanayovuka mipaka kuanzia eneo la Ukusanyaji wa taarifa, Upelelezi, Uendeshaji wa Mashtaka pamoja na Mashauri ya namna hiyo.

Hayo yalibainishwa mwishoni mwa wiki iliyopita Februari 02, 2018 na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA), Mhe. Jaji Dkt. Paul Kihwelo katika mahojiano maalum mara baada ya kuhitimishwa kwa Kongamano la Wadau wa Haki Jinai lililofanyika katika Kituo kipya cha kisasa cha Mafunzo na Habari kilichopo eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

“Katika Kongamalo hilo ambalo lilihusisha Wadau mbalimbali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkemia Mkuu wa Serikali, Jeshi la Magereza, Wizara ya Katiba na Sheria na wengineo tumeazimia pia mamlaka zinazofanya upelelezi ziwe na Maabara za kufanyia Upelelezi wa Kisayansi ‘Forensic Science’ ili kuharakisha uendeshaji wa kesi na hatimaye haki iweze kupatikana kwa wakati,” alisema Mkuu wa Chuo huo ambaye pia alikuwa Mwezeshaji katika Mafunzo hayo.

Mhe. Kihwelo anasema kuwa kwa sasa wenye Maabara hizo ni Polisi pamoja na TAKUKURU, lakini wengine wote wanategemea Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, na kuongeza kuwa Tume ya Kupambana na Madawa ya Kulevya ipo kwenye mchakato wa kuanzisha Maabara yao ya uchunguzi.

Aidha; Wadau wa Kongamano hilo waliazimia kwa pamoja kuwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali iendelee kutoa majibu kwa wakati ili kuharakakisha haki kupatikana kwa wakati.

Mafunzo hayo ya Siku tano yalifanyika kwa mara ya kwanza katika Kituo Kipya cha Mafunzo na Habari za Kimahakama yalijikita katika Mada ya ‘Sheria za Uhalifu wa Makosa yanayovuka Mipaka’ ambapo katika Mada hii Sheria zilizoangaliwa ni pamoja na Sheria ya Makosa ya Kimtandao ‘Cybercrime’, Makosa yanayohusu miamala ya fedha kwa njia ya Kimtandao pamoja na Sheria ya Madawa ya Kulevya na makosa yanayoundwa na Sheria hiyo.

Kongamano hili lililofunguliwa rasmi na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Juma Januari 29, 2018 lililenga kuwakutanisha Wadau wa Haki Jinai ili kujadili changamoto zilizopo katika sheria hizokatika maeneo ya upelelezi, uendeshaji mashtaka pamoja na ubadilishanaji wa Wahalifu na kuwakutanisha kwa lengo la kujenga Mtandao wa Wadau na kukuza ushirikiano.

Aidha; Mhe. Jaji Dkt. Kihwelo anaongeza kuwa Mafunzo hayo yaliyomalizika ni miongoni mwa mafunzo mengi zaidi yatakayofuatia huku yakishirikisha Wadau tofauti tofauti.

RAIA WAWILI WA UINGEREZA KORTINI WAKITUHUMIWA KWA MASHTAKA TISA,YAMO YA KUISHI NCHINI BILA VIBALI

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

RAIA wawili wa Uingereza na Mkurugenzi Mkuu wa Afri Transport, wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili kujibu mashitaka tisa yakiwamo ya kufanya Kazi, kuishi na kupata vibali mbali mbali kwa njia ya uongo.

Wamepandishwa kizimbani leo Mahakamani hapo ya Hakimu Mkazi Godfrey Mwambapa na majina ya washtakiwa hao ni Mohammed Mabeeenullah Kashmiri (72) na Saleem Kashmiri (50) ambao wanashtakiwa pamoja na Mtanzania Mohammed Ameenullah Kashmiri (82) .

Katika kesi hii Ammeenullah ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Afri Transport anashtakiwa kwa kosa la kuajiri raia hao wa Ungereza bila ya kibali na kuwasaidia kupata vibali baada ya kutoa vibali vya ufeki.

Akisoma hati ya mashtaka, Mwendesha Mashtaka kutoka  Uhamiaji, Gerald Mardai amedai, Oktoba 25 mwaka jana, katika Makao Makuu ya ofisi za Uhamiaji Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam mshtakiwa Ameenullah, alikamatwa akitoa taarifa za uongo kwa ajili ya kuwapatia vibali raia hao wa Uingereza kufanya kazi nchini.

Pia aliwasaidia kupata vibali vya kuishi nchini kinyume na sheria baada ya kutoa taarifa ya uongo dhidi yao. Mshtakiwa Ameenullah anashtakiwa kwa kuwaajiri raia hao wawili wa Uingereza huku akijua kuwa raia hao hawana kibali cha kuwaruhusu kufanya Kazi nchini na bila kuwa na kibali cha kuishi nchini.

Aidha Mtanzania huyo anadaiwa kuwasaidia raia hao kutenda kosa kinyume na sheria za uhamiaji.Kwa upande wa raia wa Ungereza wao wanakabiliwa na shtaka la kujipatia nyaraka kwa kutoa taarifa za uongo, kutengeneza taarifa za uongo ili wajipatie vibali vya kuishi nchini.

Pia wanadaiwa kujiingiza katika ajira bila ya kuwa na vibali vya kufanya kazi na kujiingiza katika ajira bila ya kuwa na vibali vya kuishi nchini.
Washtakiwa wamekana kutenda makosa hayo na wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

 Mahakama  imemtaka kila mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh.milioni 20.Pia wametakiwa kuwasilisha hati zao za kusafiria mahakamani na wasisafiri nje ya nchi bila ya kibali cha Mahakama.

Kesi imeahirishwa Februari 19, mwaka huu.

MATUKIO YA WAZIRI MKUU MAJALIWA BUNGENI LEO MJINI DODOMA

$
0
0
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Mji Mkongwe, Ali Saleh kwenye viwanja via Bunge Mini Dodoma Februari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Ileje, Janet Mbene kwenye viwanja vya Bunge Mini Dodoma Februari 5, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mbunge wa Kiteto, Emmanuel Papian, Bungeni mjini Dodoma Februari 5, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene, Bungeni mjini Dodoma Februari 5, 2017.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Ismani na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Bungeni mjini Dodoma Februari 5, 2018.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Wawekezaji Watakiwa Kuchangamkia Fursa Mkoani Manyara

$
0
0
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo akielezea jambo mbele ya mwenyeji wake ambaye ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Missaile Raymond Musa (katikati) mara baada ya kuwasilia katika Ofisi za Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, mjini Babati Leo. Mama Fissoo yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ili kuwajengea uwezo wajumbe wa Bodi za Filamu za Mikoa na Wilaya kuhusu Kanuni na Sheria ya Filamu. Kutoa kulia ni Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Manyara ambaye pia ndiye Katibu wa Bodi ya Filamu Mkoa Bi. Frida Nkarage na Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa wa Mkoa Kennedy Kaganda.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Mkoa, Missaile Raymond Musa akizungumza jambo alipokutana na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) leo Ofisini kwake mjini Babati, Mkoani Manyara. KBF yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ili kuwajengea uwezo wajumbe wa Bodi za Filamu za Mikoa na Wilaya kuhusu Kanuni na Sheria ya Filamu.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Mkoa, Missaile Raymond Musa akisoma kwa makini nakala za Sheria ya Filamu na Kanuni zake mara baada ya kukabidhiwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) Ofisini kwake leo mjini Babati. KBF yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ili kuwajengea uwezo wajumbe wa Bodi za Filamu za Mikoa na Wilaya kuhusu Kanuni na Sheria ya Filamu.




Kutoka Kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa WA Mkoa wa Manyara Kennedy Kaganda na Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Manyara ambaye pia ndiye Katibu wa Bodi ya Filamu Mkoa Bi. Frida Nkarage wakifuatilia mazungumzo baina ya Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Filamu Mkoa, Missaile Raymond Musa (hawapo pichani) walipokutana ofisi kwa RAS –Manyara, mjini Babati leo.Picha na: Frank Shija – MAELEZO, Babati
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi za Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, mjini Babati Leo. Katibu huyo yupo mkoani Manyara kwa ziara ya kikazi ili kuwajengea uwezo wajumbe wa Bodi za Filamu za Mikoa na Wilaya kuhusu Kanuni na Sheria ya Filamu katika mkoa huo. Kulia ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Missaile Raymond Musa.


Na: Frank Shija – MAELEZO, Babati,


Wawekezaji wametakiwa kuchangamkia fursa mbalimbali zinazopatikana katika Mkoa wa Manyara badala ya kukimbilia katika maeneo ambayo yamezoeleka na wadau wengi wa maendeleo.

Rai hiyo imetolewa leo Mjini Babati na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara alipokuta na ujumbe kutoka Bodi ya Filamu Tanzania ukiongozwa na Katibu Mtendaji wa Bodi hiyo Bibi. Joyce Fissoo mape hii leo.

Kaimu Katibu Tawala huyo ameema kuwa Mkoa wa Manyara unazo fursa nyingi za uwekezaji hivyo ni vyema sasa wawekezaji wakatumia fursa hizo na kuja kuwekeza katika Nyanja tofautitofauti za uwekezaji ikiwemo kilimo, viwanda na ufugaji.

“ Mkoa wetu wa Manyara unazo fursa nyingi ambazo kama wawekezaji wakijitokeza watanufaika nazo, hivyo ni wito wangu kwao kuwa waje mkoani Manyara watumie fursa hizo, tunayo maeneo yakutosha kwa shughuli za uwekezaji”, alisema Kaimu Katibu Tawala huyo.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Tanzania (KBF), Bibi. Joyce Fissoo amesema kuwa Mkoa wa Manyara ni miongoni mwa maeneo ambayo yamekuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya Filamu nchini hasa zinazohusisha wageni kutoka nje ya nchi.

Aliongeza kuwa kitu kikubwa kinachoubeba mkoa huo ni mandhara na jiografia ya ambayo imekuwa kivutio kikubwa katika uwekezaji hasa katika eneo la utalii na filamu hapa nchini.

“ Ni jambo muhimu Mkoa wa Manyara mkajivunia kuwa na mandhari inayovutia wawekezaji, katika tasnia ya filamu wageni wengi kutoka nchi mbalimbali wamekuwa wanakuja na kuhitaji kutumia mandhari ya Wilaya ya Mbuli katika uandaaji wa filamu zao hiyo ni moja ya fursa muhimu ambayo pia itatumika kuutangaza zaidi mkoa wenu”, alisema Bibi. Fissoo.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania yupo mkoani Manyara kwa ziara ya kikazi kwa ajili ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Bodi za Filamu za Mikoa na Wilaya kuhusu majukumu ya Bodi hizo na zinazoongozwa na Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya.

MAKAMU WA RAIS AONGOZA MAMIA YA WATANZANIA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MZEE KINGUNGE

$
0
0
 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha kumbukumbu cha maombolezo ya msiba  wa Kingunge Ngombale Mwiru kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam muda mfupi kabla ya kutoa heshima za mwisho. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)  
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa heshima ya mwisho mbele ya jeneza lililobeba mwili wa mwanasiasa mkongwe na kiongozi wa muda mrefu marehemu Kingunge Ngombale Mwiru kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa mkono wa pole mtoto wa kiume wa marehemu Kingunge anayefahamika kwa jina la Kinjekitile mara baada ya kutoa heshima za mwisho katika viwanja vya Karimjee.

POLEPOLE AZINDUA MUONEKANO MPYA WA GAZETI LA UHURU LEO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Idara ya Itikadi na Uendezi Humphrey Polepole (wapili kushoto) akifurahia nakala ya gazeti la Uhuru baada ya kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo katika hafla iliyofanyika kwenye Ofisi za Uhuru Publications Limited UPL), mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, leo. Kushoto ni Said Nguba aliyewahi kuwa Mhariri Mtendaji wa UPL, na Wengine kutoka watatu kushoto ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rhoda Kangero, Mhariri Mtendaji wa zamani wa UPL Jose[h Kulangwa na Kaim Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali
MWANZO
 Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rdhoda Kangero akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa UHURU FM Angel Akilimali (kulia) wakati akimsubiri Polepole kuwasili ofisi za UPL kuzindua muonekano mpya wa gazeti la Uhuru, leo
 Katibu wa NEC ya CCM Humphrey Polepole akisalimiana na baadhi ya maofisa wa UPL baada ya kuwasili. Kushoto ni Kaimu MJhariri Mterndaji wa UPL Rhoda Kangero na kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali.
 Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rhoda Kangero akimpeleka Ndugu Polepole ofisini
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili ofisini kwa Mhariri Mtendaji wa UPL. Kulia ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rhoda Kangero
 Ndugu Polepole akizungumza jambo na Kangero
 Baadhi ya waliowahi kuwa Wahariri Watendaji wa UPL wakiwa katika Ofisini ya |Mhariri Mtendaji wa UPL. Kutoka kushoto ni Jacquelin Liana, Joseph Kulangwa na Saidi Nguba. Kushoto ni Kamimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akizungumza na Viongozin wa UPL na wageni waalikwa katika Ofisi ya Mhariri Mtendaji wa UPL
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole akifungua mfuko wenye gazerti la Uhuru, kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo leo. Kulia ni kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rhoda Kangero na Kushoto ni Mhariri Mtendaji wa zamani saidi Nguba
Polepole akionyesha furaha yake baada ya kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo la Uhuru
Mhariri Mtendaji wa zamani Joseph Kulangwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM Angel Akilimali wakifurahia nakala ya Uhuru lenye muonekano mpya baada ya kuzinduliwa muonekano huo
 Polepole akilifurahia nakala ya Uhuru akiwa akiwa na viongozi kadhaa wa UPL na waalikwa baada ya kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo leo
  Polepole akilifurahia nakala ya Uhuru akiwa akiwa na viongozi kadhaa wa UPL na waalikwa baada ya kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo leo
 Polepole akilifurahia nakala ya Uhuru akiwa akiwa na viongozi kadhaa wa UPL na waalikwa baada ya kuzindua muonekano mpya wa gazeti hilo leo
 Baadhi ya wafanyakazi wa UPL wakiwa na nakala za gazeti la Uhuru lenye muonekano mpya. Wapili kushoto ni Mhariri wa habari wa Uhuru FM Pius Ntiga
 Polepole na wafanyakazi wa UPL na waalikwa wakiendelea kulitazama gazeti hilo la Uhuru lenye muonekano mpya.
 Polepole akimshukuru Kulangwa kwa kuhudhuria hafla hiyo. Kushoto ni Said Nguba
 Polepole na msafara mzima wakienda chumba cha habari kujadili muonekano mpya wa gazeti hilo
 Polepole na msafara mzima wakienda chumba cha habari kujadili muonekano mpya wa gazeti hilo
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Polepole akizungumza jambo na Kaimu Mhariri Mtendaji Ndugu Kangero wakati msafara ukienda katika chumba cha habari
 Kangero akiongoza msafara kuingia katika chumba cha habari cha UPL
Polepole,  Watumishi wa UPL na wageni waalikwa wakiwa wamesimama kufanya dua kabla ya kuanza kulijadili Uhuru 
 Kila mmoja akiwa makini kulisoma Uhuru wakati wa mjadala
  Kila mmoja akiwa makini kulisoma Uhuru wakati wa mjadala
  Kila mmoja akiwa makini kulisoma Uhuru wakati wa mjadala
 Mkutubi wa UPL Mussa Salmin akilipitia kwa makini gazeti la Uhuru
 Kaimu Naibu Mhariri Mtendaji wa UPL Rashid Zahor akilipia kwa makini gazeti la Uhuru. Kulia ni Kaimu Mhariri Mtendaji Roda Kangero
 Wahariri watendaji wa zamani wa UPL Said Nguba na Joseph Kulangwa wakipita gazeti hilo. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM angel Akilimali
 Kaimu Mhariri Mkurugenzi Mtendaji wa Uhuru FM Angel Akilimali akilisoma kiwa makini gazeti la Uhuru  Mhariri wa habari wa Uhuru FM Pius Ntiga akisoma kwa makini gazeti la Uhuru lenye muonekano mpya. Kushoto ni Jacqueline Liana
 "Unaona hiyo?" Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL Rhoda Kangero akimuonyesha moja ya habari picha Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole alipokuwa akipitia nakala ya gazeti loa kwanza la Uhuru lililoanza kuchapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1961
 Polepole akilitazama kwa makini nakala hiyo ya kwanza ya gazeti hilo la Uhuru
 "Ohhh... very nice" akasema Polepole wakati akitazama nakala ya gazeti hilo la uhuru la mwaka 1961
 "Safi sana,," akasema tena Polepole
 Polepole akionyesha nakala ya gazeti la kwanza la Uhuru la mwaka 1961. Kulia ni Kangero
 Mtangazaji wa Uhuru FM Ndugu Amina  akisoma gazeti la Uhuru kwa makini
 Mjadala wa gazeti ukiendelea
 Mhariri Mwandamizi wa UPL Jane Mihanji (kushoto) akifuatilia kwa makini mjadala wa gazeti sehemu ya mengineyo. Kulia ni kaimu Mhariri wa Makala Selina Wilson
 Ndani ya chumba cha habari cha UPL wakati mjadala ukiendelea
 Mhariri Mtendaji wa zamani Said Nguba akisoma kwa makini nakala ya Uhuru lenye muonekano mpya
 Mfanyakazi wa Idara ya |Matangazo UPL akiuliza jambo kuhusu uboreshwaji wa upande huo kwenye gazeti la UPL
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Polepole akizungumza kukamilisha mengineyo ya mjadala wa gazeti hilo la uhuru
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Polepole akizungumza kukamilisha mengineyo ya mjadala wa gazeti hilo la uhuru
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Polepole akizungumza kukamilisha mengineyo ya mjadala wa gazeti hilo la uhuru
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Polepole akizungumza kukamilisha mengineyo ya mjadala wa gazeti hilo la uhuru
 Ndugu Poloepole akiagana na Ndugu Masota wakati akiondoka. Kushoto ni Ndugu Rhoda
 Wafanyakazi wa UPL wakiwa katika picha ya kumbukumbu baada ya uzinduzi huo wa muonekano mpya wa gazeti la Uhuru. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

MHE.GABRIEL"NI WAJIBU WA KILA MWANANCHI KUTOA TAARIFA SAHIHI WAKATI WA UKUSANYAJI WA TAKWIMU ZA KAYA

AIRTEL YAZINDUA PROMOSHENI YA KUWAZAWADIA WATEJA WAO

$
0
0
Na Agness Francis -Globu ya jamii 

KAMPUNI ya Simu za mkononi Airtel Tanzania imeamua kuzindua promosheni ya Yatosha Intanenti kwa wale wanaonunua vifurushi vya bando la Yatosha SMATIKA Intanenti. 

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo,leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Masoka Airtel Tanzania Isack Nchunda, amesema kampuni hiyo imeamua kutoa zawadi kwa wateja wake wanaotumia bando la SMATIKA Intanenti.

Kwani wamekuwa waaminifu kwao na wanaendelea kutoa hamasa ili kuendelea kumtumia huduma zao. Nchunda amesema promosheni hiyo ya Yatosha Intanenti itakuwa ni ya muda wa siku 30, ambapo kutakuwa na droo 3 za kila wiki kati ya siku za Jumatatu, Jumatano na Ijumaa,

"Kwa ndroo ya kila siku wateja 1000 watajishindia bando ya Intanenti yenye 1 Gb kwa kila mmoja, wakati droo kubwa itakuwa na washindi 10,huku 5 wakijishindia simu za Smartphone na wengine 5 kujinyakulia modern,"amesema Nchunda. 

Aidha Meneja Uhusiano Airtel Tanzania,Jackson Mmbando amewataka wateja wao kutokuwa na hofu katika mchakato mzima wa uwendeshaji wa promosheni hiyo. "Itakuwa ni promosheni ya wazi sana itasimamiwa na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha hapa nchini.Kila mteja atakaeshiriki moja kwa moja ataingia kwenye droo ya bahati na kuambiwa kuwa ameshinda au hajashinda"amesema Mmbando.
 Kushoto Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando na kulia ni Mkurugenzi Masoko Airtel Isack Nchunda  katika zoezi la uzinduzi Wa Promosheni ya SMATIKA Intanenti leo makao makuu ya Airtel Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Masoko Wa Airtel Tanzania Isack Nchunda  akizungumza na waandishi Wa Habari leo katika Makao makuu ya Airtel Jijini Dar es Salaam  kuhusu promosheni hiyo itakavyokuwa ikifanyika ili Kuibuka mshindi Katiba Bahati nasibu hiyo.
Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando akizungumza na waandishi  Wa Habari  leo katika Makao makuu ya Airtel Jijini Dar es salaam kuhusu promosheni  hiyo iliyozinduliwa kama zawadi kwa wateja wake.
 
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images