Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU AKABIDHI KADI ZA MATIBABU KWA WAZEE 280

$
0
0





Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kadi ya matibabu ya bure kwa wazee, Johaness Chacha, moja wa wazee 280waliopatiwa vitambulishbo hivyo vitakavyowawezesha kutibiwa bure popote wilayani Serengeti katika makabidhiano yaliyofanyika kwenye viwanja vya hospitali ya wilaya ya Mugumu Januari 18, 2018. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu


AZIRI MKUU Kassim Majaliwa amegawa kadi za matibabu kwa wazee 280 wa wilaya ya Serengeti mkoani Mara, kadi hizo zitawawezesha wazee hao kutibiwa bure.

Amesema Serikali imedhamiria kuboresha huduma za afya kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kutoa matibabu bure kwa wazee walio na umri wa kuanzia miaka 60.

Waziri Mkuu alikabidhi kadi hizo jana (Alhamisi, Januari 18, 2018) alipotembelea mradi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Serengeti, inayojengwa katika mji wa Mugumu.Alisema Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Serengeti itakamilisha ujenzi wa hospitali hiyo, itakayokuwa na uwezo wa kuwahudumia wakazi wa wilaya hiyo na wageni.

Waziri Mkuu alisema ujenzi wa hospitali hiyo ni muhimu kwa kuwa mbali na kuwanufaisha wananchi, pia watalii wanaotembelea mbuga ya Serengeti nao wataweza kutibiwa hapo.Awali, Mkuu wa wilaya hiyo Bw. Nurdin Babu alisema tangu mwaka 1974 wilaya hiyo ilipoanzishwa hadi sasa haina hospitali ya wilaya na wakazi wake wanatibiwa katika hospitali teule ya Nyerere inayomilikiwa na kanisa la Mennonite Tanzania.

Alisema kutokana na kuongeka kwa idadi ya wakazi hao pamoja na idadi kubwa ya wageni wanaotembelea Serengeti, hususan watalii hospitali hiyo haina tena uwezo wa kutoa huduma kwa kiwango kinachostahili.Bw. Babu alisema mara nyingi wageni wanaotembelea mbuga ya Serengeti hulazimika kufuata huduma za afya mjini Arusha au Nairobi nchini Kenya pale wanapougua au kupata ajali katika shughuli zao za kitalii.

Alisema kwa upande wa wakazi wa wilaya ya Serengeti wao hulazimika kufuata huduma za afya katika hospitali ya Mkoa au hospitali ya Rufaa ya Bugando, hivyo kukamilika kwa mradi huo wa ujenzi wa hospitali utawapunguzia kutembea umbali mrefu kufuata huduma hizo.

Pia Mkuu huyo wa wilaya alisema alianzisha kampeni ya changia sh. 1,000 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo ya wilaya, kwa lengo la kuwafanya wakazi hao wajisikie kuwa wameshiriki katika ujenzi huo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
IJUMAA, JANUARI 19, 2018.

Ukitaka kufanya biashara ya mkaa ama kusafirisha,lazima ufuate masharti haya

$
0
0

Haya sio matenga ya samaki la hasa ni mbinu mpya iliyobuniwa na wahalifu wanaosafirisha mkaa kinyume na taratibu kama yalivyokutwa na maafisa Misitu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania Kanda ya Mashariki walipokuwa wakifanya doria eneo la Dumila barabara ya Domoma - Morogoro jana.
kulia ni Herman Awet Afisa Misitu kanda ya mashariki akiwa na  henry malya ambaye anasimamia safu ya Dumila wakimueleza Mama mfanya biashara (aligoma kutaja jina lake) taratibu za bishara na usafirishaji wa mkaa mara baada ya kumkamata kwa kosa la kukiuka taratibu za usafirishaji mkaa kwa kuweka mkaa huo kwenye matenga na kusafirisha kama matenga ya samaki ili kukwepa maduhuli ya Serikali. Mama huyo alikamatwa Barabara ya Dumila.

Wakala unapenda kuujulisha umma kuwa Serikali ya Tanzania haijapiga marufuku biashara na matumizi ya mkaa, isipokuwa inachotaka ni kuona uvunaji misitu unafanywa kwa kuzingatia sheria na kanuni zilizotungwa. Serikali inataka watu wafanye biashara hiyo kwa njia halali na walipe ushuru na kodi kwa mujibu wa sheria.

Wafanyabiashara wa mazao ya misitu wanatakiwa kutimiza masharti yafuatayo:

(i) Awe na hati ya usajili;
(ii) Awe na hati ya usafirishaji wa mazao ya misitu (Transit Pass);
(iii) Awe na leseni ya kuvuna mazao ya misitu;
(iv) Awe na leseni ya biashara ikiwa ni pamoja na TIN namba;
(v) Alipie ushuru wa Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kama ilivyobainishwa kisheria;
(vi) Awe na daftari la kumbukumbu ya kupokea na kuuza mazao ya misitu.
Kutokana na Kanuni za usafirishaji wa mazao ya misitu za mwaka 1999 hairuhusiwi mtu yeyote kusafirisha mazao ya misitu (kwa njia ya barabara au maji) kati ya saa kumi na mbili jioni na saa kumi na mbili asubuhi.
Atakayevunja masharti hayo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mkaa.

Hairuhusiwi mtu yeyote kusafirisha mkaa hadi atimize masharti yaliyoko hapo juuu. Vilevile, mkaa, hata kama ni mfuko mmoja kwa ajili ya biashara au matumizi ya nyumbani, sharti ulipiwe.Pamoja na kutimiza masharti yaliyoorodheshwa hapo juu, wafanyabiashara wa mkaa wanatakiwa kutimiza masharti yafuatayo:-

(i) Awe na leseni itakayotolewa na Afisa Misitu wa Wilaya au Wakala wa Huduma za Misitu;
(ii) Awe na hati ya kusafirisha mkaa (Transit Pass), ambayo itagongwa muhuri katika kila kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu.
(iii) Mkaa usafirishwe kupitia njia zilizoruhusiwa na Ofisi za Misitu.
(iv) Atatakiwa alipie ushuru wa Serikali kwa kila kilogramu moja Sh 250 au kilogramu 50 kwa Sh 12500.
Kwa mtu yeyote atakayesafirisha mkaa bila kutimiza masharti yaliyotajwa hapo juu, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Maelezo zaidi yanapatikana katika ofisi za Misitu za Wilaya na TFS.

watatu walamba mamilioni ya tatumzuka jumapili Jackpot

$
0
0
 Meneja Mawasiliano wa mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) hivi karibuni wakati wa kuwatambulisha na  kuwakabidhi hundi zao washindi watatu wa TatuMzuka (Jumapili Jackpot),mchezo huo ulifanyika mwishoni mwa wiki.Maganga amewaomba Watanzania kuendelea kujitokeza kwa wingi kuendelea kucheza mchezo huo,kwani umekuwa ukiwakwamua wengi waliobahatika na kuwa wafanyabiashara/wajasiliamali wazuri na vipato vyao vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku.
Pichani kati ni Lucas Swebe akitoa ushuhuda wa namna alivyojishindia fedha taslimi Milioni tano katika  mchezo wa TatuMzuka (Jumapili Jackpot),Pichani kulia ni mshindi mwingine aitwaye Mrisho Maganga aliyejinyakulia kitita cha shilingi Milioni 22 pamoja nae (kutosho) ni Daniel Mwachali ambaye naye alijinyakulia kitita cha shilingi Milioni 22.
 Meneja Mawasiliano wa mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi ya Milioni 22,Danie Mwachali aliyojishindia kwenye mchezo wa TatuMzuka (Jumapili Jackpot) uliofanyika mwishoni mwa wiki.

WAKULIMA WA USAGALI AMCOS WILAYANI NZEGA WAMUOMBA MKUU WA MKOA KUWASAIDIA ILI WALIPWE DENI LAO LA MILIONI 193

$
0
0
RS TABORA

WAKULIMA wa Tumbaku wa Chama cha Msingi cha Ushirika Usagali (AMCOS) wilayani Nzega wameiomba Serikali ya Mkoa wa Tabora kuwasaidia kusimamia madai yao ya fedha zao kiasi cha shilingi milioni 193 za mauzo ya tumbaku kwa msimu 2015/2016 ambayo watuhumu kuchukuliwa na viongozi waliokuwa madarakani wakati huo.

Wakulima hao walitoa kilio hicho jana katika Kijiji cha Usagali wilayani Nzega wakati Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey akiwa katika ziara ya kutembelea Vyama vya Ushirika kuhimiza upandaji miti kupitia ushirika kwa ajili ya kurudisha uoto wa asili na kukifanya kilimo cha tumambaku kiwe rafiki kwa mazingira.

Mmoja wa wakulima Peter Mashoto alisema kuwa waliokuwa Viongozi wa Usagali na wajumbe wa Bodi wanatuhumiwa kulipwa fedha na Kampuni ya Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) lakini wao walishindwa kuwalipa wakulima waliouza tumbaku yao na kuzichua wao kwa ajili ya matumizi binafsi.

Aliongeza kuwa wakulima waliodhulumiwa fedha hizo wameendelea kuishi maisha ya dhiki wakati watuhumiwa wanaendelea kuishi maisha mazuri na kujiendeleza wao binafsi huku wao wakishinda hata kuwaeneleza watoto wao kielimu.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa sasa wa Usagali AMCOS Alphonce Sylvester aliomba Mrajisi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuwasaidia kusimamia madai ya wakulima ili waweze kulipa fedha zao na kuwarudishia matumini.
Alisema kuwa baadhi ya wakulima wanaolima zao hilo yamekata tamaa baada ya kuona fedha za msimu msimu 2015/2016 hawajalipwa na kuona kuwa vitendo vya namna hiyo vinaweza kuendelea.

Sylvester aliongeza kuwa ili kurudisha matumaini kwa wakulima ni vema Serikali isaidie kusimamia ili haki itoewe na wakulima waweze kupata fedha zao.Kufuatia kilio hicho cha wakulima hao, Mkuu wa Tabora Mwanri aliwaagiza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega kwa kushirikiana na Ofisi ya Mrajisiri Mkoa kufuatilia suala hilo na kuoana limekwamia wapi ili wakulima waweze kupatiwa haki yao kama madai yao ni halali.

Aliongeza kuwa ni jukumu lao kuhakikisha wanawashika mkono wakulima walidhulumiwa ili hatua dhidi wahusika zichukuliwe kwa ajili ya kuhakikisha haki inatendeka.Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega Jacob Ntalitinya aliahaidi kushirikiana na viongozi wa Ushirika kushughulikia tatizo hilo lilikwamia wapi ili wakulima wapate fedha zao na wahusika wachukuliwe hatua zinazostahili.

WANANCHI NJOMBE WAKIRI KUKWAMA KATIKA BAADHI YA HUDUMA KWA KUKOSA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0
Wananchi wa mkoa wa Njombe wameonyesha mwamko mkubwa kujitikoza kwa wingi kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa wakielezea namna wanavyotegemea kuvitumia katika kupata huduma mbalimbali za kijamii.

Wilaya ya Njombe Halmashauri ya Mji wa Makambako, ambako zoezi la usajili linaendelea hivi sasa, wananchi wengi wamekiri kupoteza muda wao mwingi kufuatilia kupata vitambulisho vya Taifa kutokana na Umuhimu mkubwa wa Vitambulisho hivyo katika huduma mbalimbali za kijamii.

Bwana Alphonce Mtengela mkazi wa Njombe akiwa anasubiri kupata huduma amesema “Sasa hivi kila mahali wanahitaji Kitambulisho cha Taifa ili waweze kukuhudumia, nimekwama kuchukua Mkopo baada ya kutokuwa na Kitambulisho cha Taifa hivyo kuna haja ya kuwa nacho ili iwe rahisi kutambulika katika huduma za Kijamii”

Wananchi wa Mkoa wa Njombe katika Wilaya za Njombe, Ludewa, Wanging’ombe, Makete na Makambako wanaendelea na zoezi la Usajili utakaomalizika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.
Ndugu Nicholaus Lugandu mkazi wa Kijiji cha Ikelu Kata ya Ikelu Wilaya Njombe akichukuliwa alama za Vidole wakati akipatiwa huduma ya usajili na Utambuzi uliohusisha uchukuaji wa alama za Kibaiologia, saini ya Kielektroniki pamoja na Picha, zoezi linaloendelea hivi sasa katika Wilaya ya Njombe Halmashauri ya Mji wa Makambako.
Wakazi wa Kijiji cha Lyamkena Halmashauri ya Mji Makambako wakiwa nje ya Moja ya kituo cha Usajili wilayani Njombe wakisubiri kupatiwa huduma ya Usajili na Utambuzi ili kupatiwa Vitambulisho vya Taifa.
  
Wanakijiji wa Kata ya Ikelu Kijiji cha Ikelu wakiwa kwenye foleni kusubiria huduma ya Usajili na Utambuzi katika moja ya vituo vya Usajili katika kata hiyo.
Bwana Alphonce Mtengela wa Kijiji cha Lyamkena Kata ya Lyamkena Wilaya Njombe akichukuliwa alama za Vidole wakati akipatiwa huduma ya usajili na Utambuzi uliohusisha uchukuaji wa alama za Kibaiologia, saini ya Kielektroniki pamoja na Picha, zoezi linaloendelea hivi sasa katika Wilaya ya Njombe Halmashauri ya Mji wa Makambako.
Bi. Anusiata Mwakalebela mwananchi mkazi wa wa Kijiji cha Lyamkena Kata ya Lyamkena Wilaya Njombe akichukuliwa alama za Vidole wakati akipatiwa huduma ya usajili na Utambuzi uliohusisha uchukuaji wa alama za Kibaiologia, saini ya Kielektroniki pamoja na Picha, zoezi linaloendelea hivi sasa katika Wilaya ya Njombe Halmashauri ya Mji wa Makambako.

KIWANDA CHA DANGOTE CHAAGIZWA KUWALIPA KWA WAKATI WACHIMBAJI WA JASI

$
0
0
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa pili kushoto) akisaini kitabu cha wageni katika ukumbi wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote wakati alipofanya ziara yake kiwandani hao. Wa kwanza kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mayigi Makolobela. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtwara Vijijini, na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mitambo ya Uzalishaji Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha.
Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mayigi Makolobela akimweleza Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (wa nne kulia) katika eneo la uzalishaji la Block 1 la Kiwanda cha Saruji cha Dangote. Wengine katika picha ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mitambo ya Uzalishaji, Hemendra Raithatha (mwenye suti nyeusi). Wa kwanza kulia ni Mwenyekiti wa Wachimbaji Wadogo wa Jasi, Peter Ludvick, Wafanyakazi wa Wizara ya Madini, Wafanyakazi wa Kiwanda cha Dangote na Uongozi wa Wachimbaji Wadogo.
Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko (mbele) akiongoza kikao baina yake na Uongozi na Wafanyakazi wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Wafanyakazi wa Wizara ya Madini, pamoja na Uongozi wa Wachimbaji wa Madini ya Jasi.

Eneo la uzalishaji Kitalu Na. 1 katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote.


Kampuni ya Saruji ya Dangote imetakiwa kuwalipa kwa wakati Wachimbaji wa Madini ya Jasi ili kuwawezesha kulipa kodi zao kwa Serikali kulingana na taratibu zilizopo.

Hayo yamesemwa tarehe 19/01/2018 na Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko alipotembelea kiwandani hapo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mikoa ya Lindi na Mtwara.Naibu Waziri amesema kuwa, lazima Wachimbaji Wadogo wapate malipo yao kwa wakati baada ya kuuza madini ili kuwawezesha kulipa kodi za Serikali pamoja na kurejesha mikopo yao kwa wakati katika Benki walizokopa.

Pia, Naibu Waziri Biteko ameutaka uongozi wa kiwanda hicho kuandaa rasimu ya Mkataba ndani ya kipindi cha wiki mbili na kueleza kuwa, kuwepo kwa mkataba huo ambao kutawawezesha Wachimbaji wadogo wa madini ya Jasi kutatua changamoto zilizopo baina yao na Kiwanda husika.

“Andaeni rasimu ya mkataba ili kila moja auze madini yake kwa bei inayoeleweka bila kuoneana na kila moja apate faida anayostahili,” amesema Biteko.Ameongeza kuwa zipo changamoto za Wachimbaji wadogo kutokuwa na umoja na hivyo kuwataka kuwa na umoja ili waweze kufanikiwa katika shughuli zao ikiwemo kuwepo na bei moja ya madini yao.

Aidha, Naibu Waziri Biteko amewataka wananchi na Wachimbaji wadogo kuacha tabia ya wizi ambayo imelalamikiwa na uongozi wa Kiwanda hicho. Kwa upande wake, Mkurugezi Mtendaji wa Mitambo ya uzalishaji wa katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha amesema kuwa kulikuwepo na tatizo la malipo isipokuwa hivi sasa tatizo limeshughulikiwa, na kuahidi kuwa wachimbaji wa madini watalipwa kwa wakati.

Pia, Raithatha ameongeza kuwa, kiwanda hicho kipo tayari kufanya kazi na Wachimbaji wa Jasi kwa kuwa mali ghafi nyingi za kutengeneza Saruji zinatoka kwa wachimbaji hao jambo ambalo linaimarisha mahusiano kati ya pande husika.Aidha, ameishukuru Serikali kwa Mahusiano mazuri kati yake na Kiwanda hicho na pia amemshukuru Naibu Waziri kwa kutembelea kiwanda hicho. 

Mbali na Naibu Waziri, ziara hiyo imehudhuriwa pia na Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mayigi Makolobela, Watumishi wa Wizara ya Madini, Uongozi wa Halmashauri ya Mtwara, Uongozi wa Wachimbaji Wadogo wa Madini ya Jasi na Kamati ya Ulinzi na Usalama.

Naibu Waziri amefanya ziara yake ya siku tatu katika Mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo ililenga kukutana na wadau wa sekta hiyo na kukagua shughuli zinazofanyika ikiwemo kufahamu changamoto wanazokabiliana nazo.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA WATUMISHI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, na Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Karume,
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisikiliza hoja zikitolewa na Balozi Celestine Mushi wakati alipoongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji  wa Zanzibar Balozi Ali Karume, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama a Taifa Dkt. Modestus Kipilimba na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisikiliza hoja wakati alipoongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Karume, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama a Taifa Dkt. Modestus Kipilimba na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James wakati alipoongea na watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba. Kushoto kwake ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar Balozi Ali Karume, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama a Taifa Dkt. Modestus Kipilimba.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga wakifurahia jambo baada ya Mhe. Rais kuongea na watumishi wa Wizara hiyo kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius nyerere jijini Dar es salaam leo Januari 19, 2018. Picha na IKULU

UTEUZI WA KATIBU MTENDAJI TCU


SERIKALI YAKATAZA KULIMA PAMBA KWA MKATABA-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imekataza kilimo cha pamba cha mkataba kwa sababu kinawanyonya wakulima.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Januari 19, 2018) wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua zahanati ya Hunyari wilayani Bunda, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mara.

“Ni marufuku kwa wanunuzi wa pamba kulima pamoja na wakulima kwa sababu wakulima wanakosa uamuzi wa kupanga bei. Kuanzia sasa zao hilo litauzwa kwa njia ya mnada.”Amesema Serikali imeweka mkakati wa kuimarisha mazao makuu ya biashara ambayo uzalishaji wake umeanza kupungua likiwemo na zao la pamba.Waziri Mkuu amesema Serikali imeamua kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa kilimo cha zao la pamba kuanzia hatua za maandalizi ya shamba, pembejeo hadi masoko.

Pia Waziri Mkuu amewaagiza Maofisa Kilimo katika wilaya hiyo wawafuate wakulima vijijini kwa ajili ya kutoa elimu itakayowawezesha wakulima kulima kwa kufuata njia bora za kisasa.Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wafugaji kuhakikisha wanakuwa na idadi ya mifugo kulingana na uwezo wa eneo lao.“Marufuku kulisha mifugo katika mashamba ya watu.”

Amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa mfugaji yeyote atakayelisha mifugo yake katika mashamba ya wakulima kwani tabia hiyo huchangia migogo baina yao.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
IJUMAA, JANUARI 19, 2018.

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA WADAU WA MAZINGIRA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameongoza kikao cha Wadau wa Mazingira kuhusu Changamoto ya Mafuriko na Hifadhi ya Mazingira katika mkoa wa Dar es Salaam, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa mikutano uliopo kwenye ofisi ya Makamu wa Rais mtaa wa Luthuli.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam kuchukua hatua za haraka katika kukabiliana na mafuriko katika jiji la Dar es Salaam.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa mkutano na Wadau wa Mazingira kuhusu changamoto ya mafuriko na hifadhi ya mazingira katika mkoa wa Dar es Salaam.Makamu wa Rais alisema kulikosekana umakini katika kusimamia mazingira na miundo mbinu katika jiji la Dar es Salaam.

Makamu wa Rais alizungumzia changamoto za kuwepo kwa taka ngumu ambazo zingeweza kuzalisha umeme na gesi, “kuna miradi watu wanaomba kuzalisha umeme kwa taka, anazungushwa mtu miaka mitano, sita , saba, haambiwi ndio wala haambiwi hapana “Makamu wa Rais amesema kuna uhitaji sana wa elimu ya mazingira kwa jamii na kupeana taarifa mbali mbali zinazohusiana na mazingira .

Makamu wa Rais alisema moja ya tatizo kubwa ni kuchukua nyezo za uthibiti kufanya nyenzo za mapato “Vibali, leseni hivi ni vitu vinavyotolewa kwa ajili ya uthibiti lakini tumevigeuza kuwa vyombo vya mapato” kutokana na hali hiyo vibali vimeendelea kutolewa hovyo bila kuzingatia taratibu.

Makamu wa Rais alitoa maagizo ya kuundwa kwa Kamati ya Mazingira ya mkoa wa Dar es Salaam ambayo itaundwa na  Waziri wa Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba na kuratibiwa  na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda.Makamu wa Rais aliwashukuru wadau wa maendeleo wakiongozwa na Benki ya Dunia katika kusaidia kupambana na tatizo la uharibifu wa mazingira na mafuriko jijini Dar es Salaam.

Awali Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba alisema ni wakati wa kutafakari na kupata jawabu la kudumu la suala la mafuriko yanayotokea katika jiji la Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Wadau wa Mazingira kuhusu Changamoto ya Mafuriko na Hifadhi ya Mazingira katika mkoa wa Dar es Salaam (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Ajipanga Kutembea Hadi Magogoni Kuunga Mkono Juhudi za Rais Magufuli

$
0
0
Kijana Mzarendo,Omary Kombe akizungumzana na waandishi wa hawapo pichani juu ya kutembea kutoka Kimara hadi Kivukoni siku ya Jumamosi, Januari 20,mwaka huu ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika kuliletea Taifa maendeleo, Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Kutoa Elimu ya Unyonyaji kwa Watu Wenye Ualbino, Maiko Lugendo.
Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Kutoa Elimu ya Unyonyaji kwa Watu Wenye Ualbino,Maiko Lugendo akimkabdhi Kijana Mzarendo,Omary Kombe t-shirt atakayo vaakesho kwaajili ya matembezi hayo.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Kijana mzalendo, Omary Kombe amejipanga kutembea kutoka Kimara hadi Kivukoni siku ya Jumamosi, Januari 20, 2018 ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika kuliletea Taifa maendeleo.

Kombe ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya nia ya matembezi yake pamoja na mpango wake wa kutoa tuzo kwa Rais Magufuli itakayojulikana kama ‘Tuzo ya Kiongozi Mzalendo’.

Kombe amesema kuwa Rais Magufuli amekuwa ni kiongozi makini, mwenye uthubutu, mwenye msimamo thabiti na mzalendo wa kweli kwani amefanya mambo mbalimbali yakiwemo ya kuimarisha mfumo wa ulipaji kodi, kubadilisha sheri kandamizi za madini, kukomesha vitendo vya ujangili katika mbuga za wanyama, rushwa na dawa za kulevya pia kurejesha nidhamu kwa watumishi wa umma.

“Kubwa kuliko yote, Serikali ya Awamu wa Tano kwa ujumla imekuwa ikihamasisha kwa vitendo kuhusu ujenzi wa Tanzania ya Viwanda na kupelekea nchi kuwa na uchumi wa kati hivyo kwa niaba ya vijana wazalendo napenda kumpongeza kwa kufanya matembezi, kumpa tuzo ya kiongozi mzalendo pamoja na kutoa msaada katika hospitali ya Ocean Road iliyopo jijini hapa,” alieleza Kombe.

Aidha, kijana huyo ametoa baadhi ya mapendekezo ambayo yataisaidia Serikali yakiwemo ya kuanzishwa kwa program ya kuunganisha wafanyabiashara wa zana za kilimo, Taasisi za kifedha, vikundi vya wakulima na Vyama vya Ushirika ili wakulima waweze kukopeshwa zana hizo kwa urahisi.

Ametoa rai kwa viongozi wa dini na wananchi kuzidi kumuombea Rais Magufuli ili aendelee kuwa na moyo wa uzalendo utakaoifanya Tanzania kuwa nchi yenye maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Kutoa Elimu ya Unyonyaji kwa Watu Wenye Ualbino, Maiko Lugendo amesema kuwa Tanzania ni nchi yenye utajiri mkubwa lakini watu wachache walikuwa wakiipeleka pabaya hivyo anamshkuru Rais Magufuli kwa kuonyesha uzalendo katika kuipeleka nchi mbele.

“Uzalendo ni kitu muhimu sana katika nchi kwani mjenga nchi na mbomoa nchi ni mwananchi mwenyewe hivyo nampongeza sana Kombe kwa nia yake, tukiamua kuwa wazalendo tukishirikiana na Rais Magufuli hakika nchi itakuwa bora,”alisema Lugendo. 

Kijana huyo amekuwa akishiriki katika mambo mbalimbali ya kijamii yakiwemo ya kuanzisha kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha New Hope Family Group, Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya Zahanati ya Mjimwema, Mjumbe wa Bodi ya Hospitali ya Vijibweni, Mwanzilishi wa Kombe la Amani na Upendo pamoja na kuanzisha stika yenye ujumbe maalum wa kutokomeza mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

UZINDUZI WA MBIO ZA 21KM TIGO KILIMANJARO MARATHONI MOSHI MJINI

$
0
0
​Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya simu za Mkononi ya Tigo kanda ya Kaskazini ,Henry Kinabo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro Premium Lager Marathon 2018,Uzinduzi uliofanyika katika Hoteli ya Kibo Palace Homes mjini Moshi,Mashindano ambayo Kampuni ya Tigo inadhamini Mbio za Nusu Marathon ,Km 21.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo ,wakijadiliana jambo wakati wa uzinduzi wa Mbio hizo ambazo hufanyika kila mwaka mjini Moshi,Mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya wageni waliofika wakati wa uzinduzi wa Mbio hizo ambazo hufanyika kila mwaka mjini Moshi,Mkoani Kilimanjaro.

Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro  Premium Lager Marathon 2018 ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira (Mwenye kofia) akiwa ameketi na Wawakilishi wa Kampuni zinazodhamini Mbio hizo ,Tigo na TBL pamoja na viongozi wa Chama cha riadha mkoa wa Kilimanjaro,Jeshi la Polisi na Chuo Kikuu cha Ushirika -Moshi.

Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro  Premium Lager Marathon 2018 ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira (Mwenye kofia) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mbio hizo huku Wadhamini wa Mbio hizo Kampuni ya Tigo (Km 21) na TBL (km 42 ) wakishuhudia.​

​Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Msimu wa 16 wa Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro  Premium Lager Marathon 2018 ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira (Mwenye kofia) akiwa katika picha ya pamoja na waandaaji wa Mbio hizo pamoja na Wadhamini wakuu ,Kampuni ya Tigo na TBL.​

Athman Kambi aomba Radhi Wadau wa Soka-Mtwara.

$
0
0
Kutokana  na Kamati ya Maadili Kuwakuta na Hatia Viongozi wawili Wa Shirikisho la Soka TFF akiwemo Msimamizi wa  Mchezo Mkoa wa Mtwara Dastan Mkundi pamoja na katibu Mku wa Chama Hicho Mkoa wa Mtwara Kizito Mbano Mwenyekiti wa soko Mkoa wa Mtwara Athman Kambi amewaomba radhi Mashabiki wa soka Mkoa wa Mtwara kwa Kashfa Hiyo.

Kwa Mujibu wa kamati ya Maadili Aliyekuwa Msimamizi wa Mchezo wa Ndanda FC dhidi ya Simba  tarehe 30 amehukumiwa  kifungo cha  Maisha Kutojihusisha na Soka kutoka na kosa LA Kughushi na Udanganyifu wa Mapato ya Mchezo huo ikiwa ni kinyume cha Kanuni ya Kifungu 32(2) na ile ya 32(4) pamoja na Katibu mkuu wa chama hicho Mkoa wa Mtwara  Kizito Mbano kwa Mujibu wa Kanuni za Maadili za TFF kifungu 73( 7) na amehukumiwa Miaka mitano Kutojihusisha na Soka huku Suleiman Kachele Kupewa Onyo

Akiongea mara baada ya Taarifa hizo Athman Kambi amesema swala la soka linahitaji uaminifu ili kuweza kusaidiwa na wadau wa soka.Lakini nao baadhi ya wadau wa soka wamesema bado kuna mapato yanapotea hasa katika mechi kubwa ambazo zinachezwa Mkoa wa Mtwara.

 Kwa mujibu wa kanuni za Chama cha Soka Nchini TFF Baada ya kamati ya Maadili kutoa Hukumu watuhumiwa wanaweza kukata Rufaa katika kamati ya Rufaa ya maadili na wanaweza wakasikilizwa Upya.
 

SHONZA:HATUTA MUANGALIA USONI MTU YEYOTE ATAKAYE KIUKA MAADILI YA MTANZANIA

JKCI yakabidhiwa wodi ndani ya jengo la wodi ya watoto

$
0
0
 
 Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili  (MNH) ) Agnes Mtawa akimkabidhi Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi  wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Mallya funguzo za baadhi ya wodi zilizopo ndani ya  jengo la wodi ya watoto  ambazo Hospitali hiyo imezitoa kwa JKCI ili wazitumie kutokana na   uhaba wa wodi ya watoto walionao.
 Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili  (MNH) ) Agnes Mtawa akitoa maelezo kwa viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kuhusu wodi zilizopo ndani ya jengo la watoto ambazo  Hospitali hiyo imezitoa kwa Taasisi hiyo  ili wazitumie kutokana na uhaba wa wodi ya watoto walionao.
 Viongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Mkurugenzi wa Idara ya Uuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili  (MNH) ) Agnes Mtawa kuangalia wodi zilizopo ndani ya jengo la wodi ya watoto ambazo  Hospitali hiyo imezitoa kwa Taasisi hiyo  ili waweze kuzitumia kutokana na uhaba wa wodi ya watoto walionao.
 Wodi zilizopo ndani ya jengo la wodi za watoto ambazo  Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imezitoa kwa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  ili wazitumie kutokana na uhaba wa wodi ya watoto walionao.

Picha na JKCI


USAJILI NDANI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU

$
0
0
Usajili katika kata za Uhuru, Ayamohe, Ayamami, Imboru, Silaloda umemalizika wilayani Mbulu huku wananchi wakimininika kuendelea na Usajili kwenye Kata za Daudi, Marang, Gidamba, Gehandu na Titiwi huhu vijana wakijitokeza kwa wingi baada ya kutambua umuhimu wake katika masuala ya Elimu.

Ndg. Prosper Alfred Marmo mkazi wa Kata ya Daudi Kijiji cha Moringa, Kitongoji cha Magasi amesema ameona ni vyema akatii agizo la Serikali ili apate Kitambulisho kitakachomtambulisha kupata huduma mbalimbali ikiwemo mikopo ya elimu ya juu pindi wakati utakapofika.

Akizungumzia zoezi la Usajili linaloendelea kwa sasa Wilayani Mbulu; Afisa Usajili Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Bi. Amina Farijala amesema pamoja na kwamba msimu huu ni wakilimo na wananchi wengi wako kwenye shughuli za kilimo mwitikio wao umekuwa mkubwa hasa nyakati za mchana na hivyo kuwaasa kupanga vizuri shughuli zao ili kujitokeza kwa wingi nakwa wakati kusajiliwa.“ Mwitiko hawa wa kundi la wazee umekuwa mkubwa na kutumia moyo hasa tunapoona wazee wanafika kwenye vituo kusajiliwa” alisema

Kwa sasa NIDA inandelea na zoezi la Usajili kwa mikao 19 ya Tanzania Ikiwemo Manyara na inakusudia kufikia Desemba 2018 zoezi hili kuwa limemalizika nchi nzima na wananchi kuanza kutumia Utambulisho wao kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi na kimaendeleo.

Mzee Tarmo Naita wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu mkoani Manyara akiweka vidole katika mashine ya Usajili BVR ikiwa ni sehemu ya hatua ya pili ya Mwombaji kuchukuliwa alama za kibaiolojia.
Mzee Nayhan Hhando mwenye miaka 79 mkazi wa Kitongoji cha Ampe akipigwa picha kwa kutumia Mashine za Usajili Vitambulisho vya Taifa na Afisa Msajili Msaidizi wa NIDA Ndg. Pastori Silo.
Afisa Msajili Halmashauri ya Mji wa Mbulu Ndg. Amina Farijala akitoa maelekezo

Wananchi Kijiji cha Moringa Halmashauri ya Mji ya Mbulu wajitokeza Kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa.
Wananchi Kata ya Daudi Halmashauri ya Mji ya Mbulu wakiwa wamepanga foleni tayari kusajiliwa Vitambulisho vya Taifa.
Ndg. Emmanuel Safari Amnaay mkazi wa Kitongoji cha Malasi (kulia) akiwa na Ndg. Josephati Faustini Masay mkazi wa Malasi kwa pamoja wakijaza fomu ya maombi ya Kitambulisho cha Taifa wakati wa zoezi la Usajili linaloendelea.

WAZIRI MKUCHIKA AWAFUNDA WALENGWA WA TASAF

$
0
0
NA ESTOM SANGA-MBEYA

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mheshimiwa George Mkuchika amewatembelea Walengwa wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF katika halmashauri ya Jiji la Mbeya na kuwataka kuongeza jitihada zaidi za kujitegemea kwa kutumia ruzuku wanayoipata kwa kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili kukuza kipato chao.

Mheshimiwa Mkuchika amesema jitihada za serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF za kuhamasisha wananchi kuuchukia umasikini haziwezi kuwa endelevu ikiwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya masikini hawatatumia fedha wanazozipata kubuni miradi ya uzalishaji mali.

“hiki mnachokipata kutoka serikalini kupitia TASAF kiwe chachu ya kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili hatimaye muweze kujitegemea” amesisitiza Waziri Mkuchika.
Akiwa katika eneo la Shule ya Sekondari ya Lupeta katika jiji la Mbeya , shule ambayo TASAF imejenga jengo la Utawala na Maabara,Waziri Mkuchika ameeleza kuridhishwa na matokeo ya ujenzi wa majengo hayo na kupunguza kero iliyokuwa inawakabili walimu na wanafunzi shuleni hapo.

Aidha Mheshimiwa Mkuchika amekutana na vikundi vya uzalishaji mali vilivyoanzishwa na Walengwa wa TASAF kwa kutumia ruzuku ya fedha kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambapo walengwa hao wamekuwa wakikopeshana fedha zinazotokana na uzalishaji wa bidhaa zikiwemo mikeka,na hivyo kuwaongezea uwezo wa kuhudumia kaya zao.

Hata hivyo Waziri huyo ametoa maagizo kwa uongozi wa mkoa wa  Mbeya kuhakikisha kuwa watu wanaonufaika na fedha za ruzuku kutoka TASAF ni wale wanaokidhi vigezo vya umasikini na kutaka fedha zilizolipwa kwa watu wasiostahiki zirejeshwe mara moja.

“rejesheni fedha za serikali ili ziwanufaishe walengwa wanaostahiki kupata ruzuku hiyo kama ilivyokusudiwa na serikali” ameonya Waziri Mkuchika.Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Bi. Mercy Mandawa ameishukuru serikali kwa kuendelea kuusimamia kikamilifu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ili uendelee kusaidia jitihada za kuwaondolea wananchi kero ya umaskini.

Amesema tangu kuanzishwa kwa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ,kumekuwa na mwitikio chanya kwa walengwa kutumia ruzuku hiyo kuboresha maisha yao huku mkazo ukiwekwa katika kuboresha elimu,afya na lishe kwa watoto wanaotoka  kwenye kaya za walengwa huku akisisitiza juu ya matumizi sahihi ya ruzuku inayotolewa kila baada ya miezi miwili.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  Mhe. George Mkuchika (aliyevaa suti nyeusi) akikagua bidhaa zilizotengenezwa na Walengwa wa TASAFkatika mtgaa wa Inyala katika jiji la Mbeya  kama njia mojawapo ya kujiongezea  kipato. 
 Waziri Mkuchika (aliyevaa tai) akimsikiliza mmoja wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Lupeta katika jiji la Mbeya alipotoa maelezo ya maabara iliyojengwa na TASAF shuleni hapo.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika akikagua jengo la maabara lililojengwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF katika shule ya Sekondari ya Lupeta katika halmashauri ya jiji la Mbeya.
 Picha ya juu na chini zinawaonyesha wanafunzi wanaotoka katika kaya za walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika Mtaa wa Inyala katika jiji la Mbeya wakitoa ushuhuda kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. George Mkuchika (watatu  kutoka kushoto) namna wanavyonufaika na ruzuku kutoka TASAF  
 Baadhi ya Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini katika mtaa wa Inyala katika jiji la Mbeya wakiimba nyimbo mbele ya Waziri George Mkuchika kushukuru hatua ya serikali kupitia TASAF kubuni Mpango huo ambao wamesema umeleta chachu ya maendeleo katika eneo hilo. 
 Waziri Mkuchika na viongozi wa mkoa na wilaya ya Mbeya pamoja na TASAF wakisikiliza risala ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini  katika Mtaa wa Inyala (hayupo pichani) wakati waziri huyo alipokutana na walengwa wa Mpango huo kuona namna wanavyonufaika na huduma za Mpango huo unaotekelezwa na Serikali kupitia TASAF.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, DK. HAMISI KIGWANGALLA ATEUA WAJUMBE WAPYA WA BODI YA MAMLAKA YA HIFADHI YA ENEO LA NGORONGORO

KUMBILAMOTO APOKEA MIFUKO 90 YA VIROBA VYA NILU KUTOKA TOL

$
0
0

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kupokea Mifuko 90 ya Nilu kutoka kiwanda cha Tanzania Oxygen Limited ambapo Nilu hiyo itatumika kwa ajili ya kupaka katika shule mbalimbali zinazojengwa ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto akipokea viroba vya Nilu ambavyo vitatumika kupaka shule zilizopo katika Manispaa ya Ilala.
Karani kutoka kampuni ya Tanzania Oxygen Limited (TOL),Dorothy Katala akimuonesha Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, Idadi ya Viroba vya Nilu anavyotakiwa kuchukua .
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omary Kumbilamoto, akisimamia upakiaji wa Viroba vya Nilu kwenye gari hili iweze kufika panapo husika.

Sekta Ya Habari Ina Wajibu Wa Kupongeza Mafanikio Ya Serikali: Dkt. Abbas

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akifanya mahojiano katika Kituo cha redio A Fm cha mjini Dodoma wakati wa ziara yake yakutembelea vyombo vya Habari Mkoani humo .
Meneja wa Kituo cha redio cha A Fm cha mjini Dodoma Bw. Tatenda Nyawo (kushoto) akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi wakati wa ziara yake katika Ofisi za Kituo hicho mapema leo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akifurahia jambo nammoja wa wamiliki wa Kituo cha redio cha A fm Bw. Emmanuel Rutagonya wakati wa ziara yake katika Ofisi za Kituo hicho mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Kituo cha redio Afm cha mjini Dodoma mara baada ya ziara yake katika kituo hicho.
Meneja wa Kituo cha redio Nyemo Bw. Hezron Mwandambo (kushoto) ya mjini Dodoma akitoa maelezo kwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi wakati wa ziara yake katika kituo hicho mapema leo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi Dkt. Hassan Abbasi akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Kituo cha redio Nyemo ya mijini Dodoma.(Picha zote na Frank Mvungi



Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA

Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO Dkt. Hassan Abbas amesema Sekta ya habari inawajibu wa kupongeza mafanikio ya Serikali ikiwa ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa, elimu bila malipo, ununuzi wa dawa pamoja na ununuzi wa ndege kubwa za kisasa.


Dkt. Abbas ameyasema hayo leo Mjini Dodoma wakati wa ziara yake ya kutembelea vyombo vya habari vilivyopo Dodoma ambapo leo ametembelea Redio A.FM na Nyemo FM kwa lengo la kuona na kujua changamoto za kiutendaji wanazokutana nazo pamoja na jinsi gani wamejipanga juu ya ujio wa Serikali kuhamia Dodoma kutokana na matukio mengi ya Serikali kufanyika Mkoani humo.

“Serikali inapaswa kuungwa mkono, yapo mambo mengi ya kimaendeleo ambayo yanatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika sekta mbalimbali ila vyombo vyetu vya habari havitekelezi wajibu wake”

“Sisi kama vyombo vya habari tunawajibu wa kupongeza kwenye mafanikio, kama kuna watendaji wa Serikali wanakosea basi wakosolewe kwa kusema ukweli, hakina staha pale penye mapungufu na sio kwa kukejeli” amesisitiza Dkt. Abbas.

Aidha, Dkt. Abbas amevitaka vyombo vya habari mkoani humo kubadilika katika uandaaji wa vipindi wanavyo virusha kwa kuanza kuandaa vipindi vitakavyogusa mikoa yote na si Dodoma peke yake.“Dodoma sasa inawageni ambao ni watumishi wa Serikali zaidi ya 3000 kwa hiyo na wao wangependa kusikia habari na nyimbo za makabila yao kutoka kwenye redio zenu hivyo yawapasa kubadili utendaji kazi wenu” ameongeza Dkt. Abbas.

Vilevile amevitaka vyombo hivyo kuandaa vipindi vinavyohamasisha wananchi kufanya kazi, kulipa kodi pamoja na kuwaeleza wana thamani gani katika nchi.Kwa upande wake Meneja wa redio A.FM Tatenda Nyawo amesema kuwa redio Afm ipo katika harakati za kuongeza masafa ya redio hiyo kwa lengo la kupanua wigo wa matangazo yao kitaifa ili mikoa mingine iweze kupata habari mbalimbali kutoka Makao Makuu ya Nchi.

Mhariri wa A-fm Regina Mndeme ameongeza, “redio Afm tumejipanga vizuri kuhusu ujio wa Serikali kuhamia Dodoma kwa kufanya kazi kwa weledi na kutangaza rasimali zilizopo mkoani hapa”.
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images