Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

MV MAGOGONI KUSIMAMA KUTOA HUDUMA MAPEMA LEO ASUBUHI


KWANDIKWA AAGIZA DARAJA LA RUHUHU KUKAMILIKA

$
0
0
Muonekano wa Daraja la Ruhuhu linalojengwa wilayani Nyasa na mkandarasi wa kampuni ya Lukolo kwa gharama ya shilingi bilioni 6. Daraja hilo litaunganisha Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukifanyia ukarabati kivuko cha MV Ruhuhu kinachotoa huduma kati ya wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe ili kiweze kutoa huduma kipindi chote wakati ujenzi wa Daraja la Ruhuhu ukiendelea.
Muonekano wa Kivuko cha MV. Ruhuhu kinachotoa huduma kati ya wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma na Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe. Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba magari 6 na watu 100.
Mhandisi Mkazi anayesimamia ujenzi wa Daraja la Ruhuhu, Mhandisi Napegwa Kiseko, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa daraja hilo linalounganisha Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe na wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa daraja hilo kwa upande wa mkoa wa Ruvuma.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Lazeck Alinanuswe (katikati), akitoa taarifa ya mradi wa ujenzi wa Daraja la Ruhuhu lililopo wilayani Nyasa, mkoani humo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, wakati alipokagua daraja hilo kuona maendeleo ya ujenzi wake.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Lazeck Alinanuswe (katikati), wakati alipokagua ujenzi wa Daraja la Ruhuhu linalojengwa wilayani Nyasa na mkandarasi wa kampuni ya Lukolo kwa gharama ya shilingi bilioni 6.
 

Muonekano wa barabara ya Kitai-Lituhi yenye urefu wa KM 89 inayojengwa kwa kiwango cha changarawe mkoani Ruvuma.


Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa, amemtaka mkandarasi anayejenga daraja la Ruhuhu wilayani Nyasa, mkoani Ruvuma kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha anamaliza daraja hilo kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Agizo hilo amelitoa leo Wilayani Nyasa, mkoani Ruvuma alipokuwa akikagua ujenzi wa daraja hilo ambapo ameusisitiza Uongozi wa Wakala wa Barabara (TANROADS), Makao makuu kuhakikisha kuwa utaratibu wa zoezi zima la ununuzi wa vyuma vitakavyowekwa juu ya daraja hilo linaenda sambamba na makadirio ya muda wa mradi ili kupelekea kazi hiyo kukamilika kwa muda uliopangwa.

"Nafikiri sasa jipangeni vizuri ili masika yakiiisha mhakikishe mnafanya kazi kwa bidii ya hali ya juu, nataka kufikia mwezi Juni daraja liwe limekamilika, pia TANROADS Makao makuu hakikisheni mchakato wa manunuzi ya vyuma vya daraja mnauanza mapema ili kuweza kukamilika mapema, msisubiri hadi daraja hili kukamilika", amesema Naibu Waziri Kwandikwa.

Ameongeza kuwa daraja hilo likikamilika litakuwa ni kiungo kwa watu wa Nyasa mkoani Ruvuma na Ludewa mkoani Njombe kwani wamekuwa wakilisubiri daraja hilo kwa ajili ya kujiendeleza katika shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Aidha, amemwagiza Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), mkoani humo, Mhandisi Elisha Mgira, kuhakikisha anarekebisha kasoro zilizopo kwenye kivuko cha Ruhuhu ili kuweza kufanya kazi katika kipindi hiki ambacho wananchi wanasubiri ujenzi wa daraja kukamilika.

Kwa upande wake, Mhandisi Mkazi wa daraja hilo, Mhandisi Napegwa Kiseko, amesema kuwa Ujenzi wa mradi huo umefika asilimia 50 ambapo kazi zinazofanyika sasa ni kujaza matabaka ya barabara zinazoingia darajani hapo ili kunyanyua tuta la barabara.

Amefafanua kuwa kazi hiyo inaendelea pande zote mbili yaani mkoa wa Ruvuma na Njombe ingawa kwa kipindi hiki cha mvua kazi hiyo imekuwa na vikwazo vingi."Ujenzi wa misingi ya daraja kwa upande wa mkoa wa Ruvuma upo kwenye hatua za mwisho na kwa upande wa Njombe ujenzi wa misingi ulianza mwishoni mwa mwezi Disemba na unaendelea", amesisitiza Mhandisi Kiseko.

Mradi wa ujenzi wa daraja la mto Ruhuhu ambao upo mpakani mwa mkoa wa Ruvuma na Njombe unatarajiwa kugharimu takribani kiasi cha shilingi Bilioni 6 ambazo ni fedha za Serikali kwa asilimia mia moja na unatarajiwa kukamilka mwezi Juni mwaka huu.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

SERIKALI YAJA NA MUONGOZO WA KUPAMBANA NA USUGU WA VIMELEA VYA DAWA.

$
0
0
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi Muongozo wa Matibabu na Orodha ya dawa muhimu wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali prof. Mohammed Bakari Kambi na kushoto ni Mwakilishi wa WHO.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akikata utepe kuashiria kuzindua rasmi Muongozo wa Matibabu na Orodha ya dawa muhimu wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam, wa kwanza kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali prof. Mohammed Bakari Kambi na kushoto ni Mwakilishi wa WHO.
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiongea na wadau mbalimbali wa sekta ya afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa matibabu na orodha ya dawa zote muhimu leo jijini Dar es salaam.

 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto mwenye kilemba akiwakabidhi baadhi ya wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Afya nchini Muongozo wa Matibabu na orodha ya dawa wakati wa uzinduzi wa Muongozo huo leo jijini Dar es salaam.


NA WAMJW-DAR ES SALAAM

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeandaa Muongozo wa matibabu nchini na orodha ya dawa zote muhimu ili kuepukana na tatizo la usugu wa vimelea vya dawa. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa Muongozo wa matibabu na orodha ya dawa zote muhimu uliofanyika leo jijini Dar es salaam. 

"Ni muhimu kila kituo cha afya kuwa na dawa za kutosha, vifaa na vifaa tiba lakini ni lazima tuzingatie muongozo wa matibabu na orodha ya dawa kulingana na ugonjwa fulani ili kuepuka tatizo hili" alisema Waziri  Ummy 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Muongozo huo umezingatia vigezo vyote vya kuweka dawa ambazo zilikuwa hazipo katika ngazi ya  zahanati na  vituo vya afya ambazo zimepata uthibitisho kutoka Shirika la Afya la Dunia (WHO). 

Aidha Waziri Ummy amewapiga marufuku Bohari Kuu ya dawa ya Taifa MSD na Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifa (NHIF) kuagiza na kuandika dawa zilizo nje ya muongozo uliozinduliwa leo ili kuondoa matumizi ya dawa yasiyo sahihi. 

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa kila kituo cha afya ni lazima kiongozwe na Tabibu na sio vinginevyo ili kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana katika kituo cha afya husika. 

Kwa mujibu wa Waziri Ummy amesema kuwa itafika kipindi vituo vya afya ambavyo havikizi vigezo vitafungiwa ili kuepuka usababishwaji wa vifo visivyo vya lazima kwa watanzania. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi amesema kuwa muongozo wa kutibu magonjwa mbambali 
umezingatia Orodha ya dawa ambazo zitakuwa zinatumika nchini kwetu kama dawa muhimu za kutibu magonjwa hayo. 

WADAU WAJADILI MTAALA WA MAFUNZO KWA VYUO VYA USTAWI

$
0
0
Kamishna Msaidizi Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawke na Watoto Simon Panga akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku moja wa wadau wa Ustawi wa Jamii kutengeneza mtaala wa Ustawi wa jamii kwa vyuo vinavyofundisha masuala ya Ustawi katika ngazi ya Cheti na Diploma jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Paulo Mwangozi akitoa ufafanuzi wakati wa wa mkutano wa siku moja wa wadau wa Ustawi wa Jamii kutengeneza mtaala wa Ustawi wa jamii kwa vyuo vinavyofundisha masuala ya Ustawi katika ngazi ya Cheti na Diploma jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya washiriki wa mkutano wa wadau wa Ustawi wa Jamii kutengeneza mtaala wa Ustawi wa jamii kwa vyuo vinavyofundisha masuala ya Ustawi katika ngazi ya Cheti na Diploma jijini Dar es Salaam.

……………….

Kamishna Msaidizi Ustawi wa Jamii (Mafunzo) kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Bw. Simon Panga amesema utengenezaji mitaala ya taaluma ya Ustawi wa Jamii katika ngazi ya cheti na astashahada itasaidia kuboresha elimu ya ustawi wa jamii nchini.

Panga alisema hayo leo wakati akifungua mkutano wa siku moja wa wadau wa Ustawi wa Jamii kutengeneza mtaala wa Ustawi wa jamii kwa vyuo vinavyofundisha masuala ya Ustawi katika ngazi ya Cheti na astashahada leo jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kamishna Msaidizi Ustawi wa Jamii (Mafunzo), mtaala utakaopendekezwa na wadau utatumika na vyuo vyote Nchini tofauti na sasa ambapo kila chuo kinajitengenezea mtaala na utakuwa umepunguza majukumu na gharama kwa vyuo katika kutengeneza na kuandaa mitaala yao.

Alisema, mtaala pendekezwa unaonzia ngazi ya cheti na astashahada utasaidia kuzalisha maafisa ustawi wa jamii wenye sifa stahiki zitakazowawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi hasa ikizingatiwa kumekuwa na changamoto nyingi katika masuala ya kiuchumi na kijamii hasa katika masuala ya utumiaji dawa za kulevya, unyanyasaji wa kijinsia na kadhalika.

Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Paulo Mwangosi alisema lengo la kuwashirikisha wadau katika mkutano wa kukutengeneza mtaala kwa vyuo vinavyotoa elimu ya Ustawi wa jamii ni kuja na mtaala shirikishi utakaotumika na vyuo vyote vya Tanzania ambapo kwa sasa kumekuwa na vyuo vingi na kila chuo kina mtaala wake.

Kwa mujibu wa Mwangosi, kutokuwepo mtaala mmoja unaotumika na vyuo vinavyotoa elimu ya Ustawi wa jamii kunaleta mkanganyiko katika dhana nzima ya utoaji elimu hiyo kwa wanafunzi na kusisitiza kuwa elimu ya ustawi inayotolewa ni lazima ilingane na masuala ya ustawi wa jamii tofauti na ilivyo sasa ambapo baadhi ya vyuo hutoa elimu hiyo na kuchanganya na mafunzo mengine.

Kwa sasa nchini Tanzania kuna vyuo kumi na saba vinavyotoa mafunzo ya Ustawi wa Jamii na kati ya vyuo hivyo vyuo kumi na tano viko Tanzania bara na vyuo viwili viko Zanzibar.

KAMISHNA GASTON SANGA AMWAKILISHA KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA KUFUNGUA MAFUNZO YA MAAFISA VIUNGANISHI WA UTUNZAJI WA TAKWIMU

$
0
0
Afisa Mradi wa Envirocare , ndugu Antony Mlelwa (Mwenye shati jeupe) akifungua na kumkabidhi kompyuta Afande Kamishna Gaston Sanga huku Mkurugenzi na Meneja Mradi wakishuhudia. Kompyuta hizo zitatumika kuhifadhia Taarifa na Takwimu kwa wataalam wapya wa katika Mradi wa Msaada wa Kisheria Magerezani.
Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Afande Gaston Sanga (aliyevaa suti) akiingia Makao Makuu ya Envirocare na kupokewa na Mgurugenzi wa kituo hicho Bi Loyce Lema (wa pili toka kushoto). Wa kwanza kulia ni Meneja mradi bi Catherine Jerome na wa kwanza kushoto ni mwanasheria wa Jeshi la Magereza Makao Makuu, Mkaguzi Msaidizi Hobokela Mwansumbule.
Kamishna Gaston Sanga akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkurugenzi wa Envirocare huku Mkurugenzi Bi Loyce Lema akishuhudia.
Mkurugenzi wa Envirocare Bi Loyce Lema akitoa maelezo mafupi ya historia ya Envirocare kabla ya kumkaribisha Afande Kamishna Gaston Sanga kutoa hotuba ya Kamishna Jenerali wa Magereza na kufungua rasmi mafunzo ya siku tatu kwa wataalamu wapya wa Utunzaji wa Takwimu katika Mradi wa Msaada wa Kisheria Magerezani


Kamishna Sanga akitoa Nasaha za Kamishna Jenerali wa Magereza kabla ya kufungua rasmi mafunzo ya wataalam wapya Utunzaji wa Takwimu ambayo yanafanyika Makongo juu jijini Dar es Salaam kwenye ofisi Envirocare
Meneja Ufuatiliaji na Tathmini wa Envirocare Bi Salome Kisenge akiwa darasani akiwafundisha wataalamu wapya wa Utunzaji wa Takwimu katika Mradi wa Msaada wa Kisheria Magerezani
Meneja Mradi wa Envirocare, Bi Catherine Jerome (aliyesimama) akitoa maelezo mafupi kuhusu mradi wa Envirocare na changamoto zake kwa Kamishna Gaston Sanga.
Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza Afande Gaston Sanga( wa pili kulia), Mkurugenzi wa Envirocare Bi Loyce Lema (wa pili kushoto) ,Meneja Mradi Bi Catherine Jerome( wa kwanza kulia) na Mwanasheria wa Jeshi la Magereza Makao Makuu, Mkaguzi Msaidizi Hobokela Mwansumbule(wa kwanza kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Utunzaji wa Taarifa na Takwimu.


Picha zote na Makao Makuu ya Magereza kitengo cha Habari

RC NDIKILO AWAPA ONYO WARATIBU WA ELIMU KATA /AWATAKA KUJIKITA KWENYE AJIRA YAO ILI KUINUA TAALUMA MKOANI PWANI

$
0
0
Kaimu afisa elimu sekondari halmashauri ya Chalinze ,Irene Lubega akimkabidhi ripoti ya taarifa ya mahudhurio ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mashuleni hadi sasa ,mkuu Wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo,ambapo mahudhurio hayaridhishi kimkoa bado yakiwa chini ya asilimia 50
Kaimu afisa elimu sekondari halmashauri ya Bagamoyo ,Juma Yusuph akisoma ripoti ya taarifa ya mahudhurio ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mashuleni hadi sasa mbele ya mkuu Wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo,ambapo mahudhurio hayaridhishi kimkoa bado yakiwa chini ya asilimia 50
Mbunge wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete akizungumzia masuala ya kielimu mara baada ya mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,kupitia shule ya sekondari Mboga ,Chalinze kuzungumzia hali ya mahudhurio ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu ambapo hali ya mahudhurio mashuleni hayaridhishi kimkoa bado yakiwa chini ya asilimia 50
Mkuu Wa Mkoa Wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo(aliyesimama) akizungumzia masuala ya kielimu mara baada ya kupitia shule ya sekondari Mboga ,Chalinze kuzungumzia hali ya mahudhurio ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu ambapo hali ya mahudhurio mashuleni hayaridhishi kimkoa bado yakiwa chini ya asilimia 50.Picha na Mwamvua Mwinyi


Na Mwamvua Mwinyi,Chalinze

MKUU wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo,amewaasa waratibu wa elimu kata,kusimamia masuala ya elimu ili kuinua kiwango cha taaluma,na atakaebainika kwenda kinyume na majukumu yake ajihesabu amejifukuzisha kazi.

Aidha hajafurahishwa na hali ya mahudhurio ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu ambapo mahudhurio yapo chini ya asilimia 50 kimkoa.Pamoja na hayo,ametoa rai kukamatwa na kufikishwa mahakamani , wazazi na walezi wote ambao watashindwa kuwapeleka watoto wao kuripoti shule kwa wakati.

Ndikilo,aliyasema hayo ,wakati akizungumza na baadhi ya waratibu wa kata, maafisa elimu wa Chalinze na Bagamoyo,walimu na wajumbe wa bodi ya shule ya sekondari Mboga,iliyopo Chalinze .Alisema mratibu wa elimu kata atakayefanya uzembe na kubainika kujishughulisha na masuala tofauti na kazi yake atamvua kazi.

Ndikilo ,aliwapa siku saba kuhakikisha hali ya mahudhurio ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mashuleni inakuwa nzuri tofauti na sasa.Alisema hali ya mahudhurio hairidhishi ,kwani wanafunzi waliotakiwa kuripoti shule ya sekondari Mboga hadi sasa ni asilimia 51 pekee.

Alisema tathmini iliyofanyika kwa halmashauri ya Bagamoyo wanafunzi walioripoti shule ni asilimia 43.4,Chalinze ni asilimia 50.63.Halmashauri nyingine ni Rufiji ambayo hali ya mahudhurio ni asilimia 75, Mafia wanafunzi walioripoti ni asilimia 86.73 hivyo ni lazima kulivalia njuga suala hilo.

Ndikilo alieleza ,hii ni wiki ya pili lakini inashangaza kuona mahudhurio hayaridhishi katika shule walizopangiwa watoto hao huku elimu ikiwa ni bure.Hata hivyo,alikemea tabia inayofanywa na baadhi ya wakuu wa shule na bodi za shule kuwapa masharti ya kuchangia michango wazazi wakati wakiwapeleka watoto wao kuripoti shuleni.

“Kama bado kuna mwalimu ama shule inatoza wazazi ama wanafunzi fedha za michango,la sivyo vifaa kama madawati na mambo mengine atafukuzwa kazi,’;kwa hili halina mchezo tutafukuzana kazi ,haiwezekani mh.Rais anasisitiza elimu bure nyie huku mnakandamiza wazazi”

Ndikilo,aliwataka waratibu wa elimu,watendaji,maafisa Tarafa,wakuu wa shule kushirikiana kusimamia watoto waliopo majumbani kuhakikisha wanakwenda shule ,kwani sio jambo la mzaha hata kidogo.

“Pia mzazi,mlezi ambae ana mtoto aliyechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ,haumwi ukigundulika ni kukamatwa na kufikishwa mahakamani,ili wapate cha mtema kuni,Serikali inatoa mabilioni ya fedha ,lakini walengwa hakuna wanachokifanya,inasikitisha sana”;:

Kwa upande wao kaimu afisa elimu sekondari Bagamoyo,Juma Yusuph na kaimu afisa elimu sekondari Chalinze,Irene Lubega walipokea maagizo yaliyotolewa na kusema watayafanyia kazi.Nae ,mkuu wa wilaya ya Bagamoyo alhaj Majid Mwanga,alisema alichogundua waratibu wa elimu kata wanahangaika na masuala ya TASAF badala ya kushughulika na elimu.

Aliwakemea waratibu hao kujishughulisha na mambo nje ya majukumu ya elimu,ambayo yanatia doa elimu ,inashusha taaluma wilayani humo na kuwa wa mwisho.Alhaj Mwanga,aliwaeleza kazi za TASAF wawaachie watendaji wa kata,wa vijiji ,maafisa Tarafa ili kuongeza hali ya taaluma wilayani Bagamoyo.

Mbunge wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete alisema mwaka uliopita wa masomo wanafunzi wamefaulu wengi lakini changamoto iliyopo Chalinze ni kuchelewa wanafunzi kuripoti shule kutokana na maeneo waliyopangiwa ni ya mbali.

Alisema jiografia iliyopo inasababisha wanafunzi kushindwa kufikia maeneo ya shule walizopangiwa kuwa mbali.Ridhiwani alisema wapo wanafunzi waliochaguliwa kutoka shule za Chalnze na Bwilingu lakini wamepangiwa shule za Kibindu na Matipwili ambako ni umbali mrefu hali ambayo wazazi hawana uwezo wa kumudu gharama zinazotakiwa.

Alitoa wito huo na kutoa changamoto hiyo ili halmashauri zianze kujipanga na kuweka mkakati hasa wa kuongeza madarasa kwenye shule za sekondari hadi ifikapo 2020.

WAZIRI MWIGULU AKUTANA NA VIONGOZI KUJADILI MASUALA YA JESHI LA MAGEREZA

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa kikao cha kujadili masuala mbalimbali ya Jeshi la Magereza baada ya kukutana na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Meja Jenerali Mstaafu Projest Rwegasira (kushoto) na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Dk . Juma Malewa.Kikao hicho kimefanyika leo ofisi ya wizara,jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
 Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu Projest Rwegasira (kushoto) na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dk. Juma Malewa(kulia), wakimsikiliza Waziri wa wizara hiyo,Dk. Mwigulu Nchemba walipokutana kujadili masuala  ya jeshi hilo. Kikao hicho kimefanyika leo ofisi ya wizara,jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu Projest Rwegasira, akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Mwigulu Nchemba na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Dk. Juma Malewa (kulia), wakati wa kikao cha kujadili masuala mbalimbali ya jeshi hilo.Kikao hicho kimefanyika leo ofisi ya wizara,jijini Dar es Salaam.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

MAAZIMIO YA MKUTANO KATI YA SMZ NA SMT KUSHUGHULIKIA MELI ZINAZOPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA KWA TUHUMA ZA KUSAFIRISHA SILAHA NA MADAWA YA KULEVYA, TAREHE 17 JANUARI 2018

$
0
0
Ndugu Waandishi wa Habari, nimewaita hapa kuzungumza nanyi na kupitia kwenu kuzungumza na wananchi wenzangu kuhusu taaarifa ya kukamatwa kwa meli zilizokuwa zimepakia shehena za dawa za kulevya na silaha zikiwa zinapeperusha bendera ya nchi yetu.


Meli hizo ni: 

Kaluba yenye usajili namba IMO 6828753 iliyokamatwa tarehe 27 Desemba 2017 ikiwa na wastani wa kilo 1,600 za dawa za kulevya huko katika maeneo ya Jamhuri ya Dominican Republic; na 

Andromeda yenye namba za usajili IMO 7614666 iliyokamatwa kwa kusafirisha silaha kinyume na Sheria za kimataifa. 

Meli zote mbili zimesajiliwa Tanzania kupitia taasisi yetu ya Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar ambayo ndiyo imepewa mamlaka ya kusajili meli za nje.

Hapa kwetu Tanzania tuna aina mbili za kusajili Meli; usajili wa Meli zenye asili ya Tanzania na zile zenye asili ya Nje. kwa kuzingatia kuwa Tanzania ni nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa na mashirika yake mbalimbali, siku zote tumekuwa tunaheshimu na kutekeleza kikamilifu majukumu yetu ya kimataifa yaliyowekwa kupitia mikataba na maazimio mbalimbali ya vyombo hivyo

Ndugu Waandishi wa Habari, kwa mujibu wa mkataba wa UNCLOS 1982 kila nchi imepewa haki ya kufanya usajili wa meli kwa kuzingatia mikataba ya kimataifa na sheria za nchi husika.Kwa upande wa Tanzania, usajili wa meli za kimataifa unasimamiwa na Sheria Na 5 ya mwaka 2006,


(Kwa upande wa SUMATRA ina Merchant Shipping Act ya mwaka 2003. Sheria hi inaruhusu usajili wa meli inayomilikiwa na Mtanzania, au meli inayomilikiwa kwa ubia kati ya Mtanzania na raia wa nchi nyingine. Kwa sheria hii ili meli ipate usajili wa SUMATRA na kuruhusiwa kupeperusha bendera ya Tanzania ni lazima umiliki wa meli uhusishwe na raia wa Tanzania kwa umiliki wote au kwa ubia lakini ni lazima Mtanzania awe na hisa nyingi. Vilevile kampuni hiyo ya umiliki lazima iwe ya Kitanzania kwa maana ya kusajiliwa na kujiendesha kutokea Tanzania hata kama kampuni hiyo inamilikiwa na watu wasio Watanzania. Na kwa upande wa Zanzibar kupitia ZMA wana Maritime Transport Act ya mwaka 2006).

Sheria hii inaruhusu usajili wa meli yoyote hata kama mmiliki wake sio Mtanzania wala kampuni kuwa ya Kitanzania hivyo basi kutoa fursa kwa meli ambayo haina umiliki wa aina yeyote wa Tanzania kwa maana umiliki na ukazi kupewa usajili wa kupeperusha bendera yetu nje ya Tanzania. Aidha, Sheria hizi huendeshwa sambamba pamoja na Sheria na Kanuni za Kimataifa.

Ni vyema tukafahamu kuwa Sheria na Kanuni hizo humlazimu mwenye Meli, kujaza fomu maalumu ya maombi pamoja na Fomu za “DECLARATION OF VESSELS NON INVOLVEMENT WITH CRIMINAL ACTS OR OMISSIONS”; na ndipo hatua nyingine za kufanya uchunguzi wa historia ya meli kupitia International Maritime websites na vyanzo vingine, tangu Meli ilipotengenezwa hadi muda inapoomba usajili.

Uhakiki hufanywa pia kupitia mitandao mingine mikubwa mitatu inayotumika duniani kote kupata historia ya meli, Mitandao hiyo ni:

Fleet Moon; 
Maritime Traffic; na 

iii. Maritime-connector.

Baada ya ZMA ambayo ndio kisheria imeruhusiwa kusajili meli nje ya Tanzania, kujiridhisha na maelezo na taarifa zilizopatikana, maamuzi ya kusajili au kutosajili yanatolewa kupitia Idara ya Usajili.

Ndugu Waandishi wa Habari, kwa mujibu wa taratibu za Mkataba wa Kimataifa wa Kupambana na Usafirishaji wa Dawa za Kulevya, 1988 na Azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa 1970 (2011).

nchi zilizosajili Meli zinazokamatwa hutakiwa kutoa kibali kwa Walinzi wa Mwambao wa Bahari wa nchi husika, na kwa Meli hizi, tulitoa kibali kwa Jeshi la Mwambao wa Marekani na Jeshi la Mwambao wa Ugiriki kuzikamata na kuzipekua meli hizo.

Baada ya kupata taarifa za upekuzi hatua za haraka zilizochukuliwa upande wetu ni kufuta Usajili wa Meli hizo.

Ndugu Waandishi wa Habari, Tanzania vilevile ni mwanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Kupiga Vita Usafirishaji Haramu wa Dawa za Kulevya (United Nations Convention Against Illicit Traffic of Narcotic Drugs and Psychotropic Substance, 1988) na pia ni Mwanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa Kupiga Vita

Usafirishaji Haramu wa Silaha (United Nations Protocol Against Illicit Manufacturing of and Trafficking in Arms, their Parts and Components and Ammunition, Supplementing the United Nations Convention Against Transnational Organized Crime, 2001).

Kwa mnasaba huu, tunapenda kutoa taarifa kuwa Tanzania imejidhatiti na imedhamiria kutekeleza majukumu yake yaliyoelezwa katika mikataba hiyo ya kimataifa, ikiwemo kushirikiana na mataifa mengine pamoja na mashirika ya kimataifa katika kupiga vita usafirishaji wa dawa za kulevya na silaha. Nyote ni mashahidi kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Awamu ya Tano imetangaza vita dhidi ya watu wote wanaojihusisha na dawa za kulevya na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vimekuwa vikifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha vinatokomeza kabisa uhalifu huo.

Hivyo basi, taarifa ya kukamatwa kwa meli zenye bendera ya Tanzania zikisafirisha dawa za kulevya na silaha ni kinyume na Sheria za nchi yetu na zile za kimataifa. Taarifa hizi zimeleta mshtuko mkubwa ndani ya nchi yetu. hasa kwa kuwa Tanzania imejipambanua kupambana na maovu hayo kwa kutumia nguvu zote.

Ndugu Waandishi wa Habari, kufuatia taarifa hizo, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliniagiza kuitisha kikao cha dharura baina ya viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wale wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuzungumzia kadhia hiyo.
Jana Jumatano, tarehe 17 Januari 2018, Viongozi na Wataalamu wa pande zote mbili wakiongozwa na mimi mwenyewe na Mhe. Balozi Seif Ali Idi, Makamo wa Pili wa Rais, Zanzibar tulifanya kikao kilichojadili masuala haya kwa kina huko Zanzibar.

Ndugu Waandishi wa Habari, baada ya majadiliano ya kina kuhusu masuala haya, kikao kilibaini yafuatayo: 
Suala la Usajili wa Meli za Nje linafanywa na Nchi nyingiduniani; Kwa mfano katika Bara la Afrika 

nchi zinazofanya usajili wa kimataifa ni pamoja na Liberia, Komoro na Sierra Leone. Aidha, kwa Bara la Asia, kuna nchi za China na Singapore na kwa Amerika ya Kusini ni pamoja na Panama.

Ilibainika kwamba Wenye Meli hupendelea kusajili meli zao nje ya nchi zao kwa kukimbia uzito wa kodi na sheria zinazobana shughuli zao. 

Wakala aliyekuwa akifanya kazi hii kwa niaba ya ZMA na ambaye ameshavunjiwa Mkataba bado anaendelea kufanya usajili kwa kuiba Bendera ya Tanzania. 

Kutokana na hayo kikao kiliazimia yafuatayo: 
Kutoa taarifa na ufafanuzi wa kina kuhusu kadhia ya meli hizo kukamatwa na dawa za kulevya na silaha kwa umma wa Watanzania na dunia kwa ujumla ili kuondoa upotoshaji wa aina yoyote kwa kupitia vyanzo visivyo rasmi. Kwa sasa ndio natekeleza azimio hili; 

Kwa kuwa uendeshaji wa biashara hii unaonekana kuleta utata na kutia dosari kubwa kwa Taifa letu na kuharibu sifa njema za Nchi yetu, imeonekana haja ya kuunda kamati ya pamoja ya wataalam wa SMZ na SMT itakayoshirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kwa ajili ya kupitiwa upya usajili uliokwishafanyika na kuzihakiki taarifa za meli zote zilizosajiliwa nchini mwetu, kuangalia mwenendo mzima wa usajili, na hatimaye kutoa mapendekezo na ushauri kwa Serikali; 

Kuanzisha utaratibu wa kuzifanyia uchunguzi wa kina (due diligence) meli zote mpya zitakazoomba usajili pamoja na wamiliki wake kwa kushirikisha vyombo mbalimbali vya Serikali vikiwemo vile vya ulinzi na usalama; 

iii. Kufanya mapitio ya sheria zetu, ili kuzipa nguvu zaidi taasisi zinazosimamia usajili wa meli. Wakati wa mapitio ya sheria, timu ya wataalam itaangalia kwa makini kodi zinazotozwa na mchango wake nchini ili zisiwe kivutio kwa meli zisizokidhi viwango kuomba usajili Tanzania;

Kuendelea kushirikiana na nchi nyengine kwa kuzipa ruhusa kukamata na kuzipekua meli zinazopeperusha bendera yetu wakati wote zinapohisiwa kuwa zinafanya uhalifu, au masuala ambayo haziruhusiwi kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni zinazokubalika kimataifa na wakati wa usajili. 


Asanteni kwa kunisikiliza.

WATOTO WENYE SHIDA WAFAIDIKA NA BIMA YA AFYA

$
0
0
 Wageni wa Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wakiangalia moja ya mradi wa ufugaji unaofadhiliwa na na Mfuko wa Abbot Tanzania katika Makao ya Taifa Dar es Salaam  aliye katikati ni Makamu wa Rais wa Mfuko wa Abbot  Bi. Jenna Daugherty.
 Baadhi ya watoto wa Makao ya Taifa ya Watoto wakiimba mbele ya wageni kutoka wafadhili wa Makao yao Abbot Tanzania pamoja na uongozi wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto jijini Dar es Salaam.
 Baaadhi ya Maafisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  pamoja na Wafanyakazi wa Makao ya Watoto  wakifuatilia kwa makini maigizo ya Watoto wanalelewa kituoni hapo pichani ni Bi. Ferediana Kiromo kushoto na kulia kwake ni Beatrice Mwatujobe wote kutoka Wazira ya Afya.
Mlezi wa Makao ya Taifa ya Watoto Bi. Beatrice Mugubilo akiongoza wageni wa Makao yake kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Abbot Tanzania.
Na Anthony Ishengoma.

Watoto wanaoishi katika Makao ya Taifa ya Watoto Kurasini wamefaidika na huduma ya Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu yao baada ya shirika la Abbot Tanzania kuwezesha ufadhili wa huduma hiyo muhimu pamoja kuwafungulia akaunti za benki ili waweze kumudu kulipia upya wakati bima zao zinapofikia mwisho wa muda wake.

Shirika hili limekuwa mfadhili mkuu wa Makao ya Taifa ya watoto tangu mwaka 2001na limewezasha watoto wa kituo hiki kuhakikisha wanapata huduma mbalimbali ikiwemo ustawi wa watoto kiafya na huduma nyinginezo kama vyeti vya kuzaliwa, ujenzi wa mabweni pamoja na huduma za miundombinu ya kituo hicho.
Makao ya Taifa ya watoto wenye shida Kurasini yametembelewa na ujumbe maalum katoka Shirika linalofadhili kituo hiki la Abbot Tanzania ili kujionea Maendeleo ya shughuli za kituo hicho zinazofadhiliwa na shirika hilo.
Akiongea wakati wa kuwakaribisha wageni hao kituoni hapo, Kaimu  Kamishina wa Ustawi wa Jamii Simon Panga amesema Shirika la Abbot Tanzania limekuwa likitoa ifadhili wake kwa kituo hiki tangu mwaka 2001 na kufanikiwa kuleta mageuzi makubwa kwa Maendeleo ya kituo hiki.
Kamishina Panga ameongeza kuwa pamoja na ufadhili was shirika la Abbot Tanzania, serikali imehakikisha huduma muhimu kama vile chakula, malazi, mavazi, matibabu na elimu vinapatikana kwa watoto wote wanaoishi katika Makao ya Watoto Kulasini.
“Watoto huletwa katika kituo hiki kupitia Maofisa wa Ustawi wa Jamii kutoka Hamashauri zote nchini wakiwa na taarifa zilizokamilika kulingana na mazingira waliyotoka na kuanza maisha kituoni hapa kwa ufadhili wa wasamalia na wafadhili kwa kushirikiana na serikali amesema Kamishina Panga.,”
Historia ya kituo inaanza mwaka 1966 pale Wamissionari walipokianzisha kwa lengo la kulea Watoto yatima. Kituo kilianza na  idadi ya Watoto watatu na baadaye kukabidhiwa rasmi kwa serikali ya Tanzania mwaka 1968 na tangu wakati huo serikali ilibadili mfumo wake na kuanza kutoa huduma ya malezi kwa watoto wote wenye shida.

Profesa Mbarawa awataka TPA kukamilisha na kuhamia jengo jipya

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko (kulia)akitoa ufafanuzi kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Mbarawa (kushoto) alipokagua jengo jipya 'One Stop Centre' la TPA leo.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo  kwa Naibu Mkurugenzi wa TPA (Miundombinu), Eng. Karim Mattaka (kushoto) alipotembelea na kukagua jengo jipya 'One Stop Centre' la TPA leo.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati) akitoa maelekezo katika ziara ya kukagua ujenzi wa jengo jipya 'One Stop Centre' la Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) lililopo bandarini leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Eng. Deusdedit Kakoko na Naibu Mkurugenzi wa TPA (Miundombinu), Eng. Karim Mattaka wakimsikiliza.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati) akimsikiliza kwa makini mmoja wa abiria wa Kivuko cha Magogoni alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati) akiwasikiliza baadhi ya abiria wa Kivuko cha Magogoni alipofanya ukaguzi wa kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (katikati) akiwa na baadhi ya abiria wa Kivuko cha Magogoni mara baada ya ukaguzi wa kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto) akisalimiana na Naibu Mkurugenzi wa TPA (Miundombinu), Eng. Karim Mattaka (kulia) mara baada ya kuwasili kukagua ujenzi wa jengo jipya 'One Stop Centre' la Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Kakoko.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisisitiza jambo katika ziara ya kukagua ujenzi wa jengo jipya 'One Stop Centre' la Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) lililopo bandarini leo jijini Dar es Salaam. 

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameitaka Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), kuhakikisha kazi ya kukamilisha ujenzi wa jengo jipya 'One Stop Centre' inakamilika haraka na kuanza kutoa huduma kwa mamlaka hiyo na wadau wake wote.

Akizungumza mara baada ya kukagua jengo hilo leo jijini Dar es Salaam, Prof. Mbarawa  amesema ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam utafikiwa pale wadau wote wa bandari hiyo watakapofanya kazi saa 24 na katika eneo moja ili kumrahisishia mteja kupata huduma kwa haraka na katika kiwango kinachokubalika kimataifa.

"Natoa miezi sita kuanzia leo kwa TPA msimamieni mkandarasi  kikamilifu ili ikifika Juni muwe mmehamia ninyi na wadau wenu wote katika jengo hili," alisititiza Prof. Mbarawa katika ziara hiyo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko amemhakikishia Prof. Mbarawa kuwa katika kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati tayari yeye amehamia kwenye jengo hilo, ili kuongeza hamasa kwa mkandarasi kukamilisha ujenzi wake.

"Tumejipanga ifikapo mwezi wa nne ofisi zote zitakazotumiwa na wadau wa bandari ziwe zimekamilika ili kuruhusu baadhi ya ofisi kuanza kuhamia katika jengo hili," amesema Eng. Kakoko.

Jengo hilo la kisasa lenye ghorofa 36 ambalo litawaweka wadau wote wa bandari mahali pamoja ili kurahisisha huduma kwa wateja litagharimu takribani shilingi bilioni 143 litakapokamilika mwezi Juni mwaka huu na kutoa fursa kubwa ya uwekezaji kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine Prof. Mbarawa amekagua huduma za Kivuko cha Magogoni na kuwataka wasimamizi wa kivuko hicho kuondoa wafanyabiashara na ombaomba ndani ya eneo la kivuko ili kuboresha usalama na kupunguza kero kwa abiria na madereva, na kuwataka abiria kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira waingiapo na watokapo katika eneo la kivuko.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

SERIKALI KUMALIZA MGOGORO WA NYAMONGO-MAJALIWA

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kumaliza mgogoro ulipo kati ya wananchi wa Kata ya Nyamongo na muwekezaji wa mgodi wa North Mara.

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi pamoja na mwekezaji wa mgodi huo wanaishi na kuendesha shughuli zao za kimaendeleo kwa kufuata sheria za nchi.Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Januari 18, 2018) wakati akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kata ya Nyamongo, wilayani Tarime.

Waziri Mkuu amesema Serikali haiwezi kuvumilia kuona wananchi na wawekezaji wakigombana, inataka kumaliza mgogoro huo ili pande zote zifanye kazi zake kwa amani.Katika kuhakikisha mgogoro huo unakuwa historia Waziri Mkuu ameitisha kikao kitakachowakutanisha wawakilishi wa wananchi , viongozi wa mgodi na mbunge wa jimbo la Tarime Bw. John Heche.

Amesema katika hicho kitakachofanyika Januari 28, 2018 Ofisini kwa Waziri Mkuu mjini Dodoma, ambapo aliwakikishia wananchi hao kwamba Serikali italinda maslahi yao.Awali, Waziri Mkuu alitembelea kata ya Nyamwaga na kukagua kituo cha afya cha Nyamwaga, ambapo amesema kinatosha kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya.

Hivyo amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Francis Mwanisi aanze mchakato wa kupeleka vifaa katika kituo hicho ili wananchi wa Halmashauri ya Tarime waanze kutibiwa.

Waziri Mkuu amesema Rais Dkt. John Magufuli ameongeza bajeti ya ununuzi wa dawa na kufikia sh. bilioni 269 ili kuhakikisha hakuna mgonjwa anayekwenda hospitali na kukosa dawa.

Amesema mbali na kuongeza bajeti katika ununuzi wa dawa, pia ameziagiza halmashauri zote kuhakikisha suala la utoaji wa vitambulisho kwa wazee ili watibiwe bure linatekelezwa

WATEJA AIRTEL MONEY WAPATA GAWIO LA BILIONI 1.7/-

$
0
0

Na Agness Francis, Globu ya Jamii

KAMPUNI ya simu za mkononi Airtel imetangaza rasmi kugawa gawio la Sh.bilioni 1.7 kwa kila robo ya mwaka kwa wateja wake wote wanaotumia Airtel Money  ikiwa ni mara ya tano kufanyika tangu ianzishwe huduma hiyo mwaka 2015.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Masomo Airtel  Money Isack Nchunda, amesema kuwa leo wametoa rasmi Sh, bilioni 1.7 ambayo ni riba ya robo ya mwaka iliyopita  ikiwa zoezi hilo litakuwa endelevu badala ya ule utaratibu wa mwanzowa kila  miezi sita ambapo gawio hilo la faida litawafikia moja kwa moja  walengwa ambao ni wateja pamoja na mawakala wote wanaotumia huduma hiyo ya Airtel Money hapa nchini. 

Amefafanua Nchunda amesema Mr. Money atarudisha gawio kulingana na salio linalosalia katika akaunti kila siku kwa anayetumia huduma hiyo ambayo mteja atakuwa huru kufanya matumizi yake binafsi kama kununua bando, luku, na mahitaji mengine kupitia riba hiyo bila kupangiwa na Mr. Money  huyo.

Kwa upande wake Meneja wa Huduma za Airtel Money Ibrahim Malando, amewataka mawakala hao kuendelea kufanya huduma bora kwa wateja wao kwani ni hatua nzuri ya kujiongezea zaidi faida kwa gawio lijalo.
 Meneja huduma za Airtel money Ibrahim Malando akiongea Jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutangaza gawio kwa wateja na mawakala wa Airtel money ambapo jumla y sh bilioni 1.7 zitatilewa kwa robo ya mwaka iliyoisha Disemba 2017 katika ni Mkurugenzi wa masoko Airtel money Tanzania Isack Nchunda  na Meneja  uhusiano wa Airtel  Tanzania Jackson  Mmbando
Mkurugenzi wa masomo Airtel Tanzania Isack Nchunda akiongea Jijini Dar es Salaam leo wakati wa gawio kwa wateja na mawakala wa Airtel money ambapo jumla Sh bilioni 1.7 zitatolewa kwa robo ya mwaka iliyoisha Disemba 2017.kushoto ni Meneja huduma za Airtel money  Ibrahim Malando na Meneja uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA DARAJA MTO MARA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nyamongo wilayani Tarime Januari 18, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la mto Mara linalounganisha wilaya za Tarime na Serengeti akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara Januari 18, 2018. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikata utepe kuweka jiwe la msingi la daraja la mto Mara linalounganisha wilaya za Serengeti na Tarime Januari 18, 2018. Wengine kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Josephat Kandege , Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mara, Samweli Kiboyi, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima na Mkuu wa wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimwagilia mti alioupanda baada ya kuweka jiwe la musing la ujenzi wa daraja la mto Mara linalounganisha wilaya za Tarime na Serengeti akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara, Januari 18, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizunguma na wananchi wa Kijiji cha Nyamwaga wilayani Tarime akiwa katika ziara ya mkoa wa Mara , Januari 18, 2018. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wateja sita wa Benki ya NBC wajinyakulia Suzuki Carry ‘kirikuu’ kampeni ya Malengo

$
0
0

Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Fi​l​bert Mponzi (katikati), akizungumza wakati wa droo kubwa ya kampeni ya akaunti ya Malengo ya NBC jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja Kampeni, Mtenya Cheya na kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bakari Maggid. Washindi sita walijishindia kila mmoja gari jipya aina ya Suzuki Carry maarufu kama ‘Kirikuu’ lenye thamani ya shs milioni 30. Washindi hao ni Fatuma Ramadhani kutoka kanda ya Dar es Salaam, Saidi Chiwini wa Pwani, Lucina Massawe wa kanda ya kaskazini, Kelvin Machage wa kanda ya ziwa, Patrick Mgimwa wa kanda ya kati na Fridino Benito kutoka kanda ya kusini. Katika kampeni hiyo iliyochukua muda wa miezi mitatu washindi wengine 24 walijishinda zawadi ya pesa taslimu shs milioni 1 kila mmoja.
Meneja wa Amana za Wateja wa Benki ya NBC, Dorothea Mabonye (wa pili kushoto), akichezesha droo kubwa ya kampeni ya akaunti ya Malengo ya benki hiyo jijini Dar es Salaam leo. Washindi sita walijishindia kila mmoja gari jipya aina ya Suzuki Carry maarufu kama ‘Kirikuu’ lenye thamani ya shs milioni 30. Washindi hao ni Fatuma Ramadhani kutoka kanda ya Dar es Salaam, Saidi Chiwini wa Pwani, Lucina Massawe wa kanda ya kaskazini, Kelvin Machage wa kanda ya ziwa, Patrick Mgimwa wa kanda ya kati na Fridino Benito kutoka kanda ya kusini. Katika kampeni hiyo iliyochukua muda wa miezi mitatu washindi wengine 24 walijishinda zawadi ya pesa taslimu shs milioni 1 kila mmoja. Wengine kutoka kushoto ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bakari Maggid, Meneja Kampeni ya Malengo, Mtenya Cheya na Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi.
Meneja Kampeni wa NBC, Mtenya Cheya (kushoto), akizungumza kwa simu na mmoja wa washindi sita aliyejishindia zawadi ya Suzuki Carry maarufu ‘Kirikuu’ wakati wa droo kubwa ya kampeni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi.

Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Fi ​l​bert Mponzi (​wa pili kulia ), akizungumza wakati wa droo kubwa ya kampeni ya akaunti ya Malengo ya NBC jijini Dar es Salaam leo ​ ambapo NBC imetoa zawadi zawadi ya gari aina ya Suzuki Carry 'Kirikuu' kama inavyoonekana moja ya gari hilo (kushoto) likionyeshwa kwa waandishi wa habari wakati wa droo hiyo. ​



WATEJA sita wa Benki ya NBC wameibuka kidedea baada ya kila mmoja kujishindia gari jipya aina ya Suzuki Carry maarufu kama ‘Kirikuu’ katika droo kubwa ya Kampeni ya Akaunti ya Malengo ya benki hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Kampeni hiyo iliyodumu kwa miezi mitatu imeshuhudia wateja hao kutoka katika maeneo yaliyogawanywa katika kanda sita nchini wakitangazwa washindi wa magari hayo yenye thamani ya shs millioni 30 kila moja jumla yakiwa na thamani ya shs milino 180.

Akizungumza wakati wa droo hiyo, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa NBC, Filbert Mponzi alisema kampeni hiyo iliyovutia waterja wengi wapya kujiunga ilishuhudia washindi wengine 24 kupatikana katika droo mbili zilizofanyika katika miezi miwili ya nyuma ambapo kila mmoja alijishindia zawadi ya pesa taslimu shs milioni 1. “Kampeni hii ya Akaunti ya Malengo ya NBC imekuwa na mafanikio makubwa kwani tumeshuhudia zaidi ya akaunti mpya 6000 ziikifunguliwa na wateja wetu wakihamasika kujiwekea akiba kwa malengo yao ya baadae”, alisema.

Alisema kampeni hiyo ilizinduliwa mwaka jana kipindi ambacho NBC ilikuwa ikiadhimisha miaka 50 ya huduma bora kwa wateja tokea kuanzishwa kwake. Katika droo hiyo zawadi hizo za Suzuki Carry sita ‘kirikuu’ zilikwenda kwa Fatuma Ramadhani kutoka kanda ya Dar es Salaam, Saidi Chiwini wa Pwani, Lucina Massawe wa kanda ya kaskazini, Kelvin Machage wa kanda ya ziwa, Patrick Mgimwa wa kanda ya kati na Fridino Benito kutoka kanda ya kusini.

Hii ni mara ya tatu Benki ya NBC kuendesha kampeni ya akaunti ya Malengo mara hii ikitoa zawadi zenye thamani ya zaidi ya shs milioni 204 ambapo mwaka 2016 wateja wawili Aldo Nsuha mkazi wa Tabata Dar es Salaam na Lawrence Njozi kutoka Masasi mkoani Mtwara wakijishindia magari mapya aina ya Toyota Hilux double cabin.

Vyombo vya Habari Vyaaswa Kuwa na Watumishi Wakutosha Mkoani Dodoma

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akizungumza na watumishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Kanda ya Kati Dodoma wakati wa ziara ya kutembelea vyombo vya Habari Mkoani Dodoma mapema leo.kulia ni Mkuu wa TBC Kanda ya Kati Bw. Bakari Msulwa.

Mmoja wa Mafundi Mitambo wa TBC Kanda ya Kati Bw. Mbijimi Mzungu akitoa maelezo kwa. Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi kuhusu namna mitambo ya Shirika hilo inavyofanya kazi wakati wa ziara yake katika Ofisi za Shirika hilo mapema leo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akikagua vifaa vilivyopo ndani ya moja ya Studio za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Kanda ya Kati Dodoma wakati wa ziara yake mapema leo.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari -MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Kanda ya Kati Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akizungumza na watumishi wa redio na gazeti la Uhuru Mkoani Dodoma mapema leo wakati wa ziara ya kutembelea vyombo vya Habari.

………………….

Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA

Mkurugenzi wa Idara ya Habari Dkt. Hassan Abbas ametoa wito kwa vyombo vyote vya habari mkoani Dodoma na kwingine nchini kuhakikisha wanakuwa na wafanyakazi wa kutosha watakaokidhi mahitaji kutokana na Serikali kuhamia Dodoma.

Dkt. Abbas ametoa wito huo leo mjini Dodoma wakati wa muendelezo wa ziara yake kutembelea vyombo vya habari mkoani humo ambapo leo ametembelea ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Uhuru Redio pamoja na Uhuru gazeti.

“Lengo la ziara yangu ni kuona na kujua changamoto za kiutendaji mnazao kutana nazo pamoja na jinsi gani mmejipanga juu ya ujio wa Serikali kuhamia Dodoma kwani matukio mengi ya kiserikali yatafanyika Mkoani hapa” ameongeza Dkt. Abbas.

Aidha, Dkt. Abbas amevitaka vyombo vya Habari kufanya kazi kwa bidii, ushirikiano, ubunifu na kufuata maadili katika utendaji kazi hasa katika wakati huu wa mageuzi makubwa nchini.

“Katika mabadiliko au mageuzi yeyote hasa yanayoendelea sasa nchini kila mtu anapaswa kutimiza wajibu wake mahali pake pa kazi ili katika Tanzania ijayo ajivunie si kwa kuwa mlalamishi tu bali ajivunie kuwa naye alishiriki ipasavyo katika safari hii ya mabadiliko” amesisitiza Dkt. Abbas.

Dkt. Abbas ameongeza kuwa “Kwa upande wa habari mimi nimepewa jukumu la kusimamia maadili katika vyombo vya habari hivyo nasimamia na kufuata sheria na busara katika kila jambo linalohusu sekta ya habari ndio maana hatuchukui hatua tu bali tunashauriana na kuonyana kwanza pale wachache wanapokengeuka”.

Mbali na hayo Dkt. Abbas amesema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli anapambana na azma ya kupigania nchi kujitegemea na si kutegemea nchi za nje kwa maisha yetu yote hivyo vyombo vya habari vinajukumu la kupongeza pale Serikali inapotimiza kazi vyema na kukosoa pale ambapo Serikali inakosea lakini si kwa kukejeli, kutusi au chombo cha habari kuonekana kinafanya inda.

Ziara hiyo itaendelea kesho mkoani humo ambapo Dkt. Abbas atatembelea vituo vya Redio Alternative Fm (AFm) na Redio Nyemo Fm.

MAKAMU WA RAIS AKAGUA MIFEREJI YA MAJI KATIKA ENEO LA BUGURUNI MIVINJENI NA MTONI KWA AZIZI ALI

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua mradi wa ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua kuelekea Baharini katika maeneo ya Ilala Bungoni na Temeke kwa Aziz Ally Jijini Dar es Salaam leo. Mifereji hiyo inajengwa ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo lengo ni kunusuru hali ya mafuriko katika maeneo hayo. Kutoka kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando..
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelekezo kutoka kwa mmoja wa mafundi wa wanaojenga mfereji wa maji taka eneo la Ilala Bungoni alipotembelea mradi huo leo Jijini Dar es Salaam


Sehemu ya mfereji unaojengwa katika eneo la Ilala Bungoni kwa ajili ya kupeleka maji hadi katika bonde la mto msimbazi ili kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo mafuriko.
Sehemu ya mfereji unaojengwa katika eneo la Temeke kwa Aziz Ally kwa ajili ya kusafirisha maji ya ikiwa ni njia ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo mafuriko.
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiulizia jambo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa mfereji wa maji katika eneo la Ilala Bungoni leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Theresia Mmbando, Mbunge wa Segerea Bonnah Kaluwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba.
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiulizia jambo wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa mfereji wa maji kuelekea baharini katika eneo la Temeke kwa Aziz Ally leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba.


Picha na: Frank Shija – MAELEZO


………………..


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wanaoishi kwenye mpaka kati ya Buguruni Mivinjeni na Sharifu Shamba pamoja na Mtoni kwa Azizi Ali kuwa watunzaji wazuri wa mitaro ya maji kwani ni mali yao wenyewe na si ya serikali.

Makamu wa Rais aliyasema hayo wakati wa kuhitimisha ziara yake ya siku mbili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kuta za bahari na mitaro ya maji jijini Dar es Salaam.Makamu wa Rais aliwaeleza wananchi hao kuwa mabadiliko ya tabia nchi yameathiri shughuli za kiuchumi , kijamii na kimazingira.

Makamu wa Rais Makamu wa Rais alisema kila mmoja anapaswa kujishughulisha katika suala la kusafisha na kuhifadhi mazingira .“ubaya wa mazingira ukiyaharibu yanakuadhibu” alisisitiza Makamu wa Rais.Mtaro wa Buguruni Mivinjeni una urefu wa mita 475 na ule wa kwa Azizi Ali una urefu wa mita 550.

Makamu wa Rais alisema nchi inapozungumzia uchumi wa viwanda ni mazingira “tukiharibu mazingira hamna uchumi wa viwanda” hata viwanda vitakavyojengwa vinahitaji kutunza mazingira, visafishe maji yake kabla ya kutiririsha.

Makamu wa Rais alitoa rai kwa yeyote atakayebainika kuharibu miundo mbinu wanachukuliwa hatua za haraka.Makamu wa Rais alimalizia kwa kusema kuwa Usalama wa Nchi, Amani, afya, mazingira bora hayana chama hivyo ni jukumu la kila mmoja kuwajibika ili maendeleo yaweze kupatikana.

Wakati huo huo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba amesema kuongezeka kwa watu katika jiji la Dar es Salaam na mabadiliko ya tabia nchi kutaendelea kutoa changamoto za miundo mbinu hivyo Ofisi ya Makamu wa Rais itaendelea kujenga miundo mbinu itakayowezesha wananchi kuendelea na shughuli zao kwa kushirikiana na wadau wa Maendeleo.

MWANAMITINDO WA KIMATAIFA FLAVIANA MATATA AZINDUA JENGO LA MADARASA MAWILI ALIYOYAJENGA YA SHULE YA MSINGI MKOANI PWANI

$
0
0
 Mwanamitindo wa Kimataifa afanyae kazi zake nchini Marekani, Flaviana Matata (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo alilojenga la madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu wa shule ya msingi kwa shule ya msingi Msinune, iliyopo kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani jana.
Mwanamitindo wa Kimataifa afanyae kazi zake nchini Marekani, Flaviana Matata kushoto akikabidhi mipira kwa wanaafunzi wa shule hiyo, Flaviana ni mlezi wa shule hiyo.
Mwanamitindo Flaviana akionesha cheti cha heshima alichotunukiwa na uongozi wa kata ya Chiwangwa baada ya kuwajengea majengo ya shule.
Flaviana akipokea zawadi ya mbuzi kutokea kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Msinune, Ramadhan Mtokeni (kushoto) huku Diwana wa kata ya Chiwangwa (kulia) Malota Kwagga na Afisa elimu wa kata hiyo Blasius Alphonce kulia kwa diwani na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Msinune, Alex Lugaigalila wakiangalia.
Flaviana akiwahoji wanafunzi hao maendeleo yao ya masomo shuleni hapo.
Flaviana akiwa amekalia moja kati madawati 45 ambayo aliyatoa kwa shule hiyo mwaka jana, kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Msinune, Alex Lugaigalila na kushoto ni Afisa elimu wa kata hiyo Blasius Alphonce.
Flaviana akipokea cheti cha heshima kutokea kwa Mtendaji wa Kijiji cha Msinune, Memory Mbangwa cha kutambua mchango wake huo.
Flaviana akiwa na watendaji wa kijiji hicho na kata pamoja na wanakijiji waliojitokeza siku hiyo.


Alipata wasaha wa kupiga picha na wanafunzi pia siku hiyo ambao walimpongeza kwa msaada wake huo



Na Evance Ng’ingo

MWANAMITINDO wa kimataifa afanyaye shughuli zake nchini Marekani, Flaviana Matata madarasa mawili ya shule za msingi iliyopo katika kijiji cha Msinune kilichopo kata ya Kiwangwa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

Flaviana alipewa jukumu la ulezi wa shule hiyo na wanakijiji wa Msinune mwaka 2014 wakati alipoenda kuwasaidia wanafunzi mabegi ya shule, walimpatia jukumu la kuwatengenezea vyoo, ofisi na nyumba za walimu pamoja na kumalizia ujenzi wa darasa.

Tangia alipopewa majukumu hayo alianza kwa ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi, na juzi alienda kukabidhi jengo la madarasa, darasa la saba na la sita pamoja na ofisi ya Mkuu wa Shule.Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Flaviana alisema, tangia alipopewa jukumu la ulezi wa shule hiyo amekuwa akihangaika huku na kule kupata fedha za kutatua kero za shule hiyo.

Alisema, kwa kufanikiwa kukabidhi jengo hio la madarasa anaona kuwa ameshiriki kikamilifu katika kutekeleza jukumu lake kama mwanajamii la kusaidia maendeleo ya elimu kwa jamii iliyokuwa na uhitaji mkubwa.

Alisema” sisi kama vijana kama watanzania tunalo jukumu la kujitokeza na kusaidia maendeleo ya elimu na sekta nyingine muhimu nchini kwa kuwa hili sio jukumu la serikali peke yake, sasa nimeshatengeneza vyoo vya walimu na wanafunzi na leo nakabidhi darasa”

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Alex Lugaigalila alisema ujenzi wa darasa huo utawaongezea ufanisi wanafunzi katika masomo yao huku akibainisha wazi ushiriki wa Flaviana kwenye maendeleo ya shule hiyo umeongeza hamasa ya wanafunzi kusoma.

Kwa upande wake Afisa wa elimu wa Kata hiyo,Blasius Alphonce alisema kwa ujenzi wa jengo hilo, Flaviana amesaidia jitihada za serikali katika kuendeleza elimu kwenye kata hiyo yenye vijiji vitano.

Jengo hilo la darasa lililojengwa lina vyumba viwili vikubwa vilivyoezekwa kwa bati huku likuwa na madirisha makubwa yanayowezesha kupitisha hewa na chumba cha mwalimu mkuu.

SHUKURANI toka kwa familia ya MAREHEMU BADRIYA RAMADHAN KIONDO

$
0
0
Sisi, Familia ya Mrs Bdariya Ramadhan Kiondo (Aliekuwa Afisa waMambo ya Nje Mkuu na Mkuu wa Utawala na Fedha katika Ubalozi wa Tanzania New Delhi, India, tunamshukuru Mungu kwa zawadi aliotupa kwetu kama Mke,Mama,Bibi, Shangazi ,Ndugu na kwa mwili wa kumcha Mungu.
Tunashukuru kwa upendo mkuu,kwa kushiriki nasi katika kumsindikiza mpendwa wetu katika nyumba yake ya milele tarehe 15 Desemba  2017.Tunapenda kuwashukuru marafiki,ndugu, Wafanyakazi wa Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Watumishi wenzake katika Ubalozi wa Tanzania Nchini New Delhi,India, marafiki na Ndugu wote kutoka Nchi mbali  mbali Duniani,(hasa India,,Uingereza, Uholanzi, Canada, Oman UAE na USA).
Shukran za pekee pia ziwafikie Madaktari wake wote katika Hospitali ya Apollo New Delhi,Mwambata Tiba katika Ubalozi wetu New Delhi kwa juhudi kubwa waliofanya katika matibabu yake, Viongozi Wakuu mbali mbali Serikalini,Balozi na Wafanyakazi wa Ubalozi wetu New Delhi India,Uongozi na wafanyakazi wa Wizara ya mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika mashariki,Majirani wa Kiondoni Ada Estate flats, ndugu na jamaa wote kutoka Zanzibar,Tanga na Msikiti wa Al Maamur ,Upanga Dar es salaam. Asanteni Sana.
Kisomo cha 40 ya Marehemu kitakuwa  tarehe 27 January 2018 huko Mkwajuni, Kivunge Kijijini, kwa Foum Kimara, Zanzibar baada ya Swala ya Adhuhuri (Saa saba mchana). Wote mnakaribishwa kushiriki nasi.
Ni vigumu kumshukuru kila mmoja kwa majina tunaomba mlioshiriki kwa namna moja au nyingine mpokee shukrani  zetu hizi za upendo kwa kuwa nasi katika kipindi hiki kigumu.
Tunaendelea kuomba Roho ya mpendwa wetu “B”ipumzike kwa Amani na utakuwa nasi daima milele Amen.

Pumzika kwa Amanai Mpendwa wetu.                                    
Innalilah wainailah rajiun.

WANAOISHI MAENEO HATARISHI KUHAMISHWA CHEMBA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Chemba ,Simon Odunga akifafanuajamba wakati kamati ya maafa ya wilaya nakata ya Mrijo walipokutana na wataalamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajiliya tahmini ya athari zamaafa ya mafuriko katika katika wilaya hiyo.
Muonekano wa sehemu ya soko wilayani Chemba ambapo ni eneo mabalo wilaya hiyo imepanga kuweka kambi ya waathirika wa maafa ya mafuriko wakati wanapanga mikakati ya kuwapangia makazi salama waathirika hao.
Baadhi ya nyumba ambazo zimezungukwa na maji katika kata ya Mrijo wilayani Chemba kutokana na maafa ya mafuriko yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo.
Baadhi ya waathirika wa maafa ya mafuriko wakiwa katika kambi ya muda iliyo andaliwa na kamati ya maafaya wilaya ya Chemba kutokana na thari za maafa ya mafuriko wilayani humo.
Mratibu maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (shati jeupe), Eward Boniphace, akifuatilia majadiliano wakati kamati ya maafa ya wilaya na kata ya Mrijo walipokutana na wataalamu kutoka Ofisi hiyo kwa ajili ya tahmini ya athari za maafa ya mafuriko wilayani Chemba mkoani Dodoma.



SERIKALI wilayani Chemba mkoani Dodoma imesema kuwa imepanga kuwahamisha watu wanaoishi maeneo hatarishi ya kupata mafuriko kutokana zaidi ya kaya 2,000 zimezungukwa na maji katika kata ya Mrijo hadi hivi sasa.

Akiongea wakati akitoa taarifa kwa waratibu wa maafa kutoka ofisi ya waziri mkuu waliokwenda kufanya tathimini ya maafa yaliyotokana na mafuriko ya mvua zinazoendelea kunyesha wilayani humo, mkuu wa wilaya ya Chemba, Simon Odunga alibainisha kuwa mkakati wa muda mrefu walionao ni kuwatafutia wakazi hao maeneo salama. 

Odunga Alisema kuwa kwa sasa kamati za maafa zimechukua hatua ya kukabili maafa ya mafuriko kutokana na idadi ya nyumba zilizozungukwa na maji imekuwa ikiongezeka siku hadi siku kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha hivyo wameanzisha kambi maalum kwa watu ambao nyumba zao zimeanguka kutokana na maafa hayo.

Aliongeza kuwa msaada wa haraka unahitajika kutokana na waathirika hao wa mafuriko kutumia baadhi ya majengo ya madarasa ambayo yanapaswa kutumiwa na wanafunzi ambao wanajiunga na masomo mwaka huu.

“kwa sasa tunahitaji sana mahema, mataulo, mashuka , chakula pamoja na madawa kwajili ya kuwahudumia hawa watu ambao tunao hapa na tukipata vifaa hivyo basi tutaondoka hapa na kwenda kutengeza kambi sehemu nyingine ambayo tumeiandaa maaluum kwajili ya kuwahifadhi hawa watu na kuacha haya madarasa kwajili ya matumizi ya wanafunzi” alisema Odunga.

Mkuu huyo wa wilaya aliongeza kuwa tayari wilaya imeshaunda kamati mbalimbali ambazo zinahusika katika kusaidia wahanga hao kuwa salama kiafya kwa kuchukua tahadhari zinazoweza kuibuka kwa magonjwa ya mlipuko.

Naye mratibu wa maafa kutoka ofisi ya waziri mkuu Ally Mwatima, alisema kuwa mahitaji yote ambayo yameanishwa na mkuu huyo wa wilaya wameyachukua na watayawasilisha ili hatua ziweze kuchukuliwa mapema iwezekanavyo.

“Kwanza niwapongeze kwa kukabili maafa kwa mujibuwa sheria,kanuni namiongozo ya menejimentiya maafa, hali hii imesaidia kuokoa maisha ya hawa wenzetu na mahitaji yote mliyobainisha ni ya msingi sana hivyo tutakwenda kuonana pia na kamati ya maafa mkoa ili kuweza kuona na sisi tunaongeza nguvu katika vitu gani vya msingi ambavyo vitawasadia hawa wenzetu”alisema Mwatima.

KILWA YAJIPANGA KUBORESHA MIUNDOMBINI YA AFYA

$
0
0

Angela Msimbira- OR TAMISEMI KILWA

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Dr. Khalfanis Mbukwa amesema kituo cha afya cha Kilwa Msoko ni miongoni mwa vituo 44 vya afya vilivyopatiwa shilingi milioni 500 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) kwa ufadhili wa watu wa CANADA kwa ajili uanzishwaji wa huduma za upasuaji wa dharura kwa akina mama.

Akitoa taarifa kwa Wataalam kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwenye zoezi la ufuatiliaji wa utekelezaji wa ukarabati na ujenzi wa vituo vya afya nchini katika Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi Dr. Khalfanis Mbukwa amesema majengo yaliyojengwa ni chumba cha kuhifadhia maiti, nyumba ya Mtumishi, maabara, wodi ya akina mama, wodi ya watoto,, jengo la upasuaji na kichomea taka.

Dr.Mbukwa amesema jumla ya shilingi 356,988,598 zilikadiriwa kutumika katika ujenzi huo na mpaka sasa zimetumika shilingi 351,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa chumba cha kuhifadhia maiti, nyumba ya mtumishi, maabara, wodi ya akina mama, wodi ya watoto na jengo la upasuaji.

Amesema ujenzi huu utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto ya miundombinu ya afya kwa jamii kwa kuwa awali katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko hakukuwa na Majengo ya Upasuaji, Wodi ya akinamama, wodi ya watoto, maabara na jengo la kuifadhia Maiti kuwa chakavu .

Amesema kuwa Kamati ya Manunuzi, Kamati ya mapokezi ya vifaa na kamati ya ujenzi imejipanga vyema kuendelea kusimamia kwa makini ili kuhakikisha dhamani fedha zilizotolewa na serikali zinaenda sambamba na ujenzi uliokubalika.Aidha ameongeza kuwa kiasi cha fedha kitakachobaki kitatumika kwa ajili ya ujenzi wa uzio,ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD), ukarabati wa nyumba za watumishi na ujenzi wa jengo la kiliniki ya Mama, Baba na Mtoto.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi Maiko Makwayi ameipongeza Serikali kuboresha miundombinu ya afya katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko jambo ambalo litasaidia katika kuongeza huduma kwa jamii na kupunguza matatizo ya wananchi kutembea umbali mrefu kufuata huduma.

Amesema Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Masoko inachangamoto kubwa ya vituo vya afya ameiomba Serikali kuweka kipaombele katika kuboresha vituo vya afya, na Zahanati kwa kuweka miundombinu bora katika Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi ili kupunguza kero hiyo.

Wakati huohuo Katibu wa afya wa Halmashauri ya Wilaya Kilwa Bw.John Maongezi amesema wilaya hiyo inaupungufu mkubwa wa watumishi katika kada ya afya , hivyo ameiomba serikali kupanga watumishi kulingana na ukubwa wa eneo, idadi ya vituo vya afya na idadi ya watu ili kupunguza tatizo hilo kwa Wilaya ya Kilwa.

Aidha Kituo cha Afya cha Halmashauri Kilwa Masoko ni miongoni mwa vituo 5 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya Kilwa na kimezungukwa na zahanati 3 ambazo ni Kisiwani, Mpara Mali ambavyo ni vya Serikali na Zahanati ya Bakwa ambacho ni kituo binafsi na hutoa huduma kwa wakazi zaidi ya 20,000.
Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Dr. Khalfanis Mbukwa akitoa taarifa kwa wataalam kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kuhusu maendeleo ya ukarabati na ujenzi wa vituo vya afya katika Wilaya hiyo.
Moja ya jengo la Wodi ya akinamama lililojengwa katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi.
Moja ya jengo la upasuaji lililojengwa katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi
Baadhi ya Watumishi wa Kituo cha Afya cha Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Masoko wakimsikiliza Mkuu wa Msafara kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Mathew Mganga(Hayupo pichani) kwenye ufuatiliaji wa Ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya nchini katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images