Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46200 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU AAGIZA VIONGOZI NCHINI WATOE TAARIFA

0
0
*Ni kuanzia Mawaziri hadi Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Mawaziri wote, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na Wilaya na Wakurugenzi watoe taarifa za fedha za miradi ya maendeleo kwa wananchi badala ya kusubiri ziara za viongozi wakuu.

Ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Januari 6, 2018) wakati akizungumza na watumishi na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa kwenye kikao kilichofanyika hoteli ya Mt. Vicent, mjini Mbamba Bay, wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.

“Kuanzia sasa ninaagiza, viongozi wote wa ngazi za juu wakiwemo Mawaziri hadi Wakurugenzi na hata ninyi wakuu wa idara mnawajibika kutoa taarifa za fedha tunazopeleka kwenye miradi kwa sababu wananchi wana haki ya kujua utekelezaji wa ahadi za Serikali,” alisema.

Alisema kila wanapoenda kwenye ziara ya kikazi vijijini, waelezee thamani za kazi zilizofanyika na waeleze ni lini miradi hiyo itakamilika.

“Mnapopata fursa ya kupanda jukwaani, tumieni wasaa huo kueleza kazi kubwa ambazo zimefanywa na Serikali. Elezeni Serikali imeleta fedha kiasi gani, kwa ajili ya kitu gani na kwa kufanya hivyo, mtasaidia kutoa taarifa za utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa kampeni,” alisema.

Alisema wananchi wana haki ya kupatiwa taarifa za utendaji wa Serikali yao na akawataka viongozi hao wasisubiri ziara za viongozi wa kitaifa. “Nendeni mkaongee na wananchi, msiwaachie Wakuu wa Wilaya au Wabunge peke yao ndiyo waseme na wananchi,” alisema.

Waziri Mkuu leo anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Ruvuma kwa kukagua kituo cha kufua umeme kilichopo Unangwa, kuweka jiwe la msingi la ofisi ya TANESCO, kuzungumza na wananchi na kisha kuzungumza na watumishi wa Halmashauri ya Songea.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMAPILI, JANUARI 7, 2018.

TANZIA:BEKI WA ZAMANI WA YANGA,PAMBA NA TIMU YA TAIFA ATHUMANI JUMA ‘CHAMA JOGOO’ AFARIKI DUNIA

0
0
 BEKI wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Athumani Juma ‘Chama’ aliyeweika klabu za Pamba FC ya Mwanza na Yanga ya Dar es Salaam amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya ugonjwa wa Kiharusi. 

Chama ni jina la utani ambalo marehemu Athumani Juma alipewa kutokana na beki wa zamani wa kimataifa wa Zambia, Dick Chama ambaye naye ni marehemu aliyecheza kwa mafanikio timu ya taifa ya kwao kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia 1967 hadi 1976 na klabu za za Mufulira Wanderers, Green Buffaloes na Bancroft Blades.

Athumani alipewa jina hilo baada ya kujiunga na Yanga SC mwaka 1981 akitokea Pamba ya Mwanza na mashabiki wa timu hiyo ya Jangwani walimbatiza Juma jina hilo baada ya beki wao mwingine, Rashid Idd aliyekuwa akiitwa Chama pia kuhamia Pan Africans baada ya kudumu tangu Jangwani tangu 1979.

Na umaarufu wake zaidi Jangwani ukaja kutokana na alivyoweza kumdhibiti mshambuliaji hatari wa mahasimu enzi hizo, Simba SC, Zamoyoni Mogela ‘Golden Boy’.

Kisoka, Chama aliibukia Pamba FC ya Mwanza alikozaliwa na kukulia kabla ya kujiunga na Yanga SC na aliocheza nao wakati huo ni akina Joseph Fungo, Yussuf Ismail Bana, Ahmed Amasha ‘Mathematician’, Isihaka Hassan Chukwu, Juma Mukambi ‘Jenerali’, Hussein Iddi, Charles Boniface Mkwasa, Abeid Mziba ‘JJ Masiga’, Elisha John, Ali Mchumila, Makumbi Juma ‘Homa ya jiji’, Omar Hussein ‘Keegan’, Juma Kampala na wengineo.

Chama pia alikuwa akijulikana kwa jina lingine la utani, Jogoo ambalo alipewa mwaka 1981 kwenye michuano ya CECAFA Challenge nchini Kenya kutokana na mchezaji mmoja wa Harambee Stars, Sammy Onyango ‘Jogoo’. 
Chama alistaafu soka mwaka 1990 na kujikita kwenye biashara zake ndogo ndogo kabla ya kuanza kusumbuliwa na maradhi mwaka 2014 na kujikuta anashindwa kufanya shughuli yake hadi umauti wake.

Mungu ampumzishe kwa amani marehemu Chama. Amin.

AMISI TAMBWE AREJEA JIJINI DAR KWA MATIBABU

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BAADA ya kushindwa kucheza katika michuano ya kombe la Mapinduzi kutokana na kuwa na Malaria, mshambuliaji wa kimataifa kutoka Burundi Amisi Tambwe  amereja Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu zaidi.

Tambwe  amepanda boti mchana huu visiwani Zanzibar kurejea Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.Daktari wa Yanga SC, Edward Bavu amesema Tambwe amelazimika kuondoka kambini mjini Zanzibar kurejea Dar es Salaam kwa  ajili ya matibabu zaidi ya Malaria.

“Ana Malaria, kwa siku zaidi ya nne sasa amekuwa na wakati mgumu, tumelazimika kumrejesha Dar es Salaam ili apatiwe matibabu zaidi,” amesema Dk. Bavu.Tambwe anaondoka wakati Yanga leo inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar kuvaana  na Singida United  katika mchezo wa mwisho wa kundi B utakaoanza Saa 2:15 usiku.

Mrundi huyo amekuwa katika msimu mgumu, akianza kukaa nje tangu Agosti kutokana na maumivu ya goti kabla ya kurejea Desemba, lakini mapema Januari hii tena anaondolewa kambini kwa sababu ya Malaria.

Na hii inazidi kuipunguzia nguvu safu ya ushambuliaji ya Yanga kipindi hiki ambacho inawakosa wakali wake wengine wazoefu, Mzimbabwe Donald Ngoma na Mzambia, Obrey Chirwa. 

Yanga sasa itaendelea kumtegemea Ibrahim Ajib, Mateo Antony,Juma Mahadhi na Yohana Mkomola.

RAIS DK.SHEIN AZUNGUMZA NA GAVANA WA BENKI YA TANZANIA ( BOT) ANAYEMALIZA MUDA WAKE PROFESA NDULU IKULU ZANZIBAR

0
0
RAIS wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Gavana wa Benki ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu, alipofika Ikulu Zanzibar kumuaga rasmin kwa kumaliza muda wake wa Kazi BOT, hafla hiyo imefanyika leo IkuluZanzibar 8-1-2018 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na mgeni wake Gavana wa Benki ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu, wakitoka katika ukumbi baada ya mazungumzo yao alipofika Ikulu Zanzibar kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa Kazi BOT
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na Gavana wa Benki ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu na maofisa wa BOT aliofuatana nao .

Picha na Ikulu

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAUNDA TIMU YA WATAALAMU 15 KUFUATILIA UTEKELEZAJI ZOEZI LA UPIGAJI CHAPA KATIKA MIKOA 26 TANZANIA BARA

0
0
NA MWANAHAMISI MSANGI, WMVU 

WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imeunda timu ya wataalamu 15 iliyopo katika mikoa 26 ya Tanzania bara ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Mifugo) Dk. Maria Mashingo kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa zoezi la upigaji chapa mifugo yote nchini kabla ya kufika tarehe ya mwisho ya muda wa nyongeza wa Januari 31 mwaka huu. 

Timu hiyo ya wataalamu imeanza kutekeleza majukumu yake Januari 4 mwaka huu ambapo kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk Maria Mashingo wilaya 30 ambazo bado hazijaanza zoezi la chapa na zimetiliwa mkazo katika ufuatiliaji ikiwemo Monduli, Kilwa, Liwale, Ruangwa, Mafia. 

Aidha, Wilaya nyingine ni Sikonge, Tabora, Urambo, Mwanza, Ilemela Manispaa, Magu, Ukerewe, Buchosa, Tarime, Kyerwa, Ngara, Newala, Newala Mjini, Tandahimba, Nanyamba, Mtwara, Mikindani Manispaa, Masasi, Masasi Mjini, Nanyumbu, Moshi DC, Hai, Same, Rombo, na Kigamboni. 

Dk. Mashingo amesema suala la upigaji chapa mifugo lipo kwa mujibu wa Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa mifugo Namba 12 ya Mwaka 2010 ili kudhibiti magonjwa ya mifugo pamoja na wizi wa mifugo, kuimarisha usalama wa afya na mazao ya mifugo pamoja na kudhibiti usafirishaji na uhamaji holela wa mifugo. 

Amesema jumla ya ng’ombe millioni 19, 219,487 sawa na theluthi mbili ya ng’ombe wote milioni 28, 829,231 walioko nchini ambapo mpaka sasa jumla ya ng’ombe milioni 7, 701,661 sawa na asilimia 38.5 ndio wamepigwa chapa ambapo wamechangia kiasi cha shs. Bilioni 3, 700,830,500 kwa malipo ya Tsh 500 kwa kila ng’ombe. 

Hivyo, Tathmini iliyofanyika kutokana na taarifa zilizokusanywa kutoka halmashauri zinaonesha kwamba, kati ya malengo waliojiwekea, Halmashauri 62 wamepiga chapa zaidi ya asilimia 50; Halmashauri 43 zimepiga kati ya asilimia 10 hadi 50; Halmashauri 23 zimepiga chini ya asilimia 10 na Halmashauri 30 hazijaanza lakini ziko kwenye maandalizi. 

Ametaja baadhi ya changamoto zilizochangia kuathiri utekelezaji wa zoezi la chapa ni wafugaji kukataliwa kupiga chapa mifugo yao kwa kisingizio kuwa ni wavamizi na wahamiaji haramu katika Wilaya za Kibiti, Rufiji, Sumbawanga, Tanganyika, Kibondo. 

Pia kutofautiana kwa gharama za uchangiaji ambapo baadhi ya wafugaji waliogomea kiwango cha sh 1000/= ambacho ni kinyume na kiwango elekezi cha sh 500/= kwa kila ng’ombe mfano katika Wilaya za Chunya na Tanganyika. Vilevile fedha zilizochangwa kugharamia zoezi la chapa kutotolewa kwa wakati katika baadhi ya Halmshauri ikiwemo Mbarali na Misungwi hivyo kukwamisha utekelezaji wa kazi hiyo. 

Timu hiyo ya watalaamu imegawanyika katika makundi saba kwenye mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Singida, Dodoma, Morogoro, Pwani, Dar es Salaam. 

Mikoa mingine ni Tabora, Katavi,Rukwa, Kigoma, Shinyanga, Simiyu, Mara,Mwanza, Geita, Kagera, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe, Ruvuma, Lindi na Mtwara.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Maria Mashingo akipiga chapa ng’ombe katika Kijiji cha Igalula Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi ikiwa ni sehemu ya timu ya wataalamu 15 ya Wizara hiyo walioko katika mikoa 26 ya Tanzania bara kufuatilia na kusimamia kikamilifu zoezi la upigaji chapa ambapo Dk Mashingo alisema mifugo itakayokuwa haijapigwa chapa hadi kufikia Januari 31 mwaka huu haijulikani Serikali nini kuhusu mifugo hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Mifugo) Dk. Maria Mashingo akiwaonesha wafugaji sehemu sahihi ambayo ng’ombe anatakiwa kupigwa chapa ili kuepuka kuharibu ngozi baada ya kushiriki zoezi la upigaji chapa katika Kijiji cha Igalula wilayani Tanganyika mkoani Katavi ikiwa ni sehemu ya timu ya wataalamu 15 iliyoundwa na Wizara hiyo kufuatiliaji na kusimamia upigaji chapa kabla ya Januari 30 mwaka huu 

NIDHAMU YA KUAHIDI NA KUTEKELEZA, MATUMIZI SAHIHI VYAONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI MIRADI

0
0
Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo wakati alipotoa taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kutolea ufafanuzi wa masuala kadhaa, Pichani kushoto  Mkurugenzi Msaidizi upande wa usajiri wa Magazeti Ndugu Patric Kipangula  na Kulia Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari Maelezo, Rodney Thadeus 
Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari mapema leo katika ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO,alipokuwa akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli. Pichani kushoto ni  Mkurugenzi Msaidizi upande wa usajiri wa Magazeti Ndugu Patric Kipangula  na Kulia Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari Maelezo, Rodney Thadeus .PICHA NA MICHUZI JR


NIDHAMU mpya katika ukusanyaji na matumizi ya fedha za umma na dhamira ya dhati ya kutekeleza ahadi kubwa kwa faida ya wananchi vimesaidia Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuendelea kutekeleza kwa mafanikio miradi mbalimbali mikubwa ya kitaifa. Baadhi ya mambo yaliyotekelezwa na kufafanuliwa leo kwa wanahabari ni kama ifuatavyo: 

Hali ya Uchumi

Kama alivyoeleza Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango siku chache zilizopita, tunawahakikishia watanzania kuwa hali ya uchumi wa nchi yetu inaendelea kuwa imara kwa kiasi cha kuziridhisha taasisi mbalimbali za kimataifa.

Ripoti za Shirika la Fedha Duniani (IMF), Benki ya Dunia (WB) na Taasisi ya Goldman Sachs ya Marekani zimetabiri kuwa wakati uchumi wa dunia utakua kwa wastani wa asilimia 3.0 hadi 4.0, ukuaji wa uchumi wa Tanzania unatajwa kuendelea kuwa kati ya nchi tano bora za Afrika ukitarajiwa kukua kwa asilimia 6.5 hadi 7.0 katika mwaka 2018.

Ahadi ya Kuhamia Dodoma

Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuonesha nidhamu ya kuahidi na kutekeleza ahadi ya kuhamia makao makuu, Dodoma. Kufikia mwishoni mwa Desemba, 2017, viongozi waandamizi wa Serikali wameshahamia Dodoma. Rais mwenyewe akitarajiwa mwaka huu.

Mbali na viongozi, jumla ya wafanyakazi 3,671 kutoka wizara na taasisi mbalimbali za umma wameshahamia makao makuu Dodoma. Awamu inayofuata baadaye mwaka huu itahusisha wafanyakazi wengine 2,460. Sekta binafsi ichangamkie fursa za Dodoma.

Viwanda Vyashamirisha Uchumi Mpya 

Moja ya ajenda kuu za Serikali ya Awamu ya Tano ni kujenga uchumi mpya wa viwanda. Kufikia mwaka jana viwanda zaidi ya 3,300 vilisajiliwa kupitia Msajili wa Makampuni (250), Kituo cha Uwekezaji (361), Mamlaka ya Usimamizi wa Maeneo Maalum ya Kiuchumi (41) na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO lililosajili viwanda vidogo vya kati ya mtu mmoja hadi 9 takribani 2,721). Ujenzi na uzalishaji katika viwanda hivi uko katika hatua mbalimbali.

Kati ya miradi hiyo iliyosajiliwa, viwanda vikubwa ni 652. Viwanda hivi vina jumla ya mtaji wa zaidi ya TZS trilioni 5 utakaowekezwa nchini na vitaajiri watu 50,625. Katika taarifa ya mwezi ujao tutaainisha baadhi ya viwanda vilivyokamilika na uzalishaji unavyoendelea.

Miradi Mikubwa ya Umeme

Katika sekta ya nishati, Serikali inaendelea kutekeleza miradi zaidi ya 20 ya kuhakikisha nchi ina umeme wa uhakika. Miongoni mwa miradi ya kimageuzi ni usimikaji wa mitambo ya umeme wa gesi Kinyerezi I (mtambo wa nyongeza wa megawati 185) na Kinyerezi II wa megawati 240. Mitambo hii kwa pamoja itaongeza megawati 425.

Mtambo wa Kinyerezi 1-nyongeza umefikia asilimia 50. Mtambo wa Kinyerezi II umekamilika kwa asilimia 87 ambapo Desemba, 2017, mtambo huo wa kisasa umeingiza megawati 55.94 katika gridi ya Taifa. Kiasi kingine cha megawati 27.94 kinatarajiwa kuingia kwenye gridi mwezi huu. Mitambo yote miwili itakamilika mwaka huu. 

Ujenzi Reli ya Kisasa “Standard Gauge”

Aidha, Serikali imeendelea kutekeleza mradi wa kihistoria wa ujenzi wa reli ya kisasa kwa kiwango cha kimataifa (Standard Gauge) kwa kuanzia na kipande cha kilometa 300 (Dar-Moro) kitakachogharimu TZS trilioni 2.7.

Kazi ya kusanifu njia yote itakayopita reli imeshakamilika na kwa sasa uandaaji wa tuta, ujenzi wa madaraja kabla ya kutandika reli yenyewe umeanza kwa kasi. Aidha, ujenzi wa kipande cha pili cha kilometa 442 (Morogoro-Makutupora, Dodoma) kitakachogharimu TZS TZS trilioni 4.3, mkandarasi ameshaanza maandalizi.

Ununuzi Mabehewa, Vichwa Waanza

Wakati ujenzi wa reli ukiendelea, Serikali kupitia Kampuni Hodhi ya Raslimali za Reli (RAHCO) imeshatangaza zabuni kwa ajili ya kupata makampuni yatakayotengeneza vichwa na mabehewa ya kisasa ya treni ya umeme na mafuta. Zabuni zitafunguliwa mwezi huu.

Katika zabuni hiyo Serikali inatarajia kununua vichwa 25 (23 vya umeme na 2 vya dizeli), mitambo 25 ya ukarabati wa reli na mabehewa 1,590 (kati ya hayo 1,530 yakiwa ni ya aina mbalimbali za mizigo kama vile kubeba makontena, nafaka, mafuta n.k), mabehewa 60 ni ya abiria (15 yakiwa ni daraja la kwanza na 45 daraja la kawaida).

Meli Mpya Zaleta Matumaini Maziwa Makuu 

Serikali iliahidi na sasa inatekeleza. Katika Ziwa Nyasa mwishoni mwa wiki iliyopita meli mbili mpya za mizigo za MV Njombe na MV Ruvuma zinazobeba mizigo tani 1,000 kila moja zimeanza safari kwenda bandari mbalimbali zikiwemo za nchi jirani. Serikali imetumia TZS Bilioni 11.252 na meli nyingine mpya ya abiria itakamilika Juni mwaka huu.

Katika Ziwa Victoria, kupitia kampuni ya Serikali ya Huduma za Usafiri Katika Maziwa, Marine Services Company LTD, mkandarasi wa kutengeneza meli mbili kubwa, mpya na za kisasa ameshapatikana. Aidha, tayari meli ya abiria ya MV Clarios na ya mizigo MV Umoja zilizofanyiwa ukarabati na kuwa za kisasa zimeshaanza kazi.

Katika taarifa zijazo tutaendelea kutoa maendeleo ya miradi hii mikubwa na kuainisha utekelezaji katika sekta na miradi mingine kwa wananchi. Kwa maelezo zaidi kuhusu taarifa ya leo ikiwemo picha za miradi zinazoambatana na taarifa hii tafadhali tembelea:

Twitter: TZ_Msemaji Mkuu

Imetolewa na:
Dkt. Hassan Abbasi,

Mkurugenzi, Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali.

DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA KIJIJI CHA NYANGANGA KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUCHANGIA SHUGHULI ZA MAENDELEO MKOANI KIGOMA

0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akishirikiana na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga kuchanganya zege kwa ajili ya kuweka ‘rental’ kwa ajili ya madarasa manne ya Shule ya Kijiji hicho katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kujitolea katika kufanya shughuli za maendeleo.
Mtendaji wa Kjjiji cha Nyanganga Bw.Erick Ruhomola akitoa taarifa ya Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji chao kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) ambao uliibuliwa, kubainishwa na kutekelezwa wananchi wenyewe na wananchi kwa takribani.
Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mhe. Mwanamvua Mrindiko akimshukuru Naibu Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) kwa kuja kuonesha mfano wa kuamsha ari ya wananchi wa Uvinza kujitolea katika shughuli za maendeleo yao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga mara baada ya kushiriki zoezi la kuamsha ari katika ujenzi wa Shule ya Kijiji hicho.
Wananchi wa Kijiji cha Nyanganga wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) mara baaada ya kushirikiana naye katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kufanya kazi katika ujenzi wa vyumba vine vya madarasa ya shule ya Sekondari ya Kijiji chao.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akikabidhi mifuko 37 ya Saruji kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kijiji cha Nyanganga wa kujitolea kwa nguvu zao kujenga shule ya Sekondari ya Kijiji chao.
Baadhi ya wananchi wakifanya kazi ya kumwaga ‘rental’ katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji cha Nyanganga kilichopo Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akitia saini katika kitabu cha wageni mara alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya Ziara ya siku mbili ya kikazi Mkoani hapo.




Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Dkt. Paul Chaote akitoa taarifa ya Mkoa kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) katika Ziara ya siku mbili ya kikazi ya Naibu Waziri huyo Mkoani hapo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) akisalimiana na wananchi wa Kijiji cha Nyanganga mara baada ya kuwasili katika kushiriki ujenzi wa madarasa manne ya Shule ya Kijiji hicho katika kuamsha ari ya wananchi kujitolea katika kufanya shughuli za maendeleo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Uvinza Bw. Lutabola Weja akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi kujishughulisha katika shughuli za maendeleo ambapo wanachi wa Kijiji cha Nyanganga wamejitolea na kujenga vyumba vinne vya madarasa kwa ajili ya shule ya Kijiji chao.


Na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile(Mb) ameshiriki ujenzi wa Shule ya Kijiji cha Nyanganga iliyoko kata ya Kazuramimba, wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma ikiwa ni jitihada za wananchi wa kijiji hicho kuharakisha upatikanaji wa huduma ya elimu kijijini hapo.

Akiwa katika Kijiji hicho Naibu Waziri Dkt. Ndugulile ameshiriki zoezi la kumimina zege kwa ajili ya kufunga ‘rental’ ya vyumba vya madarasa ya shule hiyo.

Dkt. Ndugulile amesema lengo la kuwepo ziara hiyo ni kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii (1996), na Sera nyingine za Wizara amabzo zinasisitiza ushiriki wa jamii katika kuibua mahitaji, kupanga, kuamua, kutekeleza, kufuatilia na utathmini shughuli za miradi ya maendeleo ikiwemo uboreshaji wa huduma ya miundo mbinu ya kufundishia na kujifunzia katika maeneo ya mijini na vijijini.

Mhe. Ndugulile ameongeza kuwa Ili kurejesha ari ya wananchi kushiriki katika maendeleo yao kuelekea uchumi wa kati na wa viwanda, Wizara imeamua kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Jamii katika ngazi za Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kuhamasisha jamii kushiriki na kuchangia shughuli za maendeleo yao kwa kufanya kazi za bega kwa bega, kuchangia nguvu zao, rasilimali fedha, rasilimali vifaa na ufundi kwenye utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa miundo ya elimu, afya, kilimo, mifugo, barabara na viwanda vidogo vidogo. 

“Nimeambiwa kuwa mradi wenu wa ujenzi wa shule ya sekondari katika kijiji cha Nyanganga utasaidia kusogeza huduma ya elimu jirani na wananchi, na nimevutiwa na hamasa mliyonayo katika maendeleo name nimekuja kushirikiana nanyi kuendeleza ujenzi wa madarasa ya shule kazi amabyo ni kigezo thabiti cha cha dhamira ya dhati yawananachi wa kijiji hiki katika kutoa haki ya msingi ya kumwendeleza Mtoto katika ngazi ya kijiji na jamii kwa ujumla” alisisitiza Mhe. Dkt. Ndugulile.

Kwa upande wake Mtendaji wa Kjjiji cha Nyanganga Bw.Erick Ruhomola amesema kuwa Mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya kijiji uliibuliwa na kubainishwa na wananchi wenyewe na kutekelezwa na wananchi kwa takribani asilimia mia moja hadi kufikia hatua ya kumwaga zege kwa ajili ya ‘rental’.

“Tunaishukuru Serikali kwa kutuona na kuja kutuunga mkono katika jitihada zetu za kujiletea maendeleo katika kijiji chetu” alisisitiza Bw. Ruhomola.Naye Mkuu wa Wilaya yaUvinza Mhe. Mwanamvua Mrindiko amemshukuru Naibu Waziri kwa kuja kuonesha mfano wa kuamsha ari ya wananchi wa Uvinza kujitolea katika shughuli za maendeleo yao.

“ Hili ni Jambo la kipekee kwa Mhe. Naibu Waziri kutembelea na kushiriki na wananchi katika ujenzi wa shule hii” alisisitiza Mhe.Mwnanamvua

Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kijiji cha Nyanganga kilichopo Wilaya ya Uvinza Mkoa wa Kigoma itawasaidia watoto wa jamii hiyo kuwa na shule karibu na makazi yao ambapo hapo awali watoto hao walikuwa wanatembea umbali wa kilometa 14 kwenda shule ya jirani.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile yupo katika Mkoa wa Kigoma kwa ziara ya siku mbili ya kikazi kufuatilia utekelezaji wa Sera mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara yake.

WAZIRI NCHI OFISI YA RAIS KATIBA SHERIA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA HAROUN ALI SULEIMAN AFUNGUA KITUO CHA AFYA UKONGORONI

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala bora Haroun Ali Suleiman akikunjuwa kitambaa kuashiria Ufunguzi wa Kituo cha Afya Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar`
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala bora Haroun Ali Suleiman wakwanza kushoto akipata maelezo kutoka kwa Afisa uendeshaji Timu ya Afya Halmashauri Wilaya ya Kati Salma Bakari Mohammed wakati akitembelea kituo cha Afya baada ya kukifungua Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar
Naibu katibu Mkuu Wizara ya Afya Halima Maulid Salum akitoa maelezo kuhusiana na Kituo cha Afya cha Ukongoroni pamoja na kuahidi kutatua baadhi ya changamoto zilizopo baada ya kufunguliwa kituo hicho Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mkuu wa Mkoa wa Kusini Hassan Khatib Hassan akizungumza machache kuhusiana na Kituo cha Afya cha Ukongoroni pamoja na kuahidi kutatua baadhi ya changamoto zilizopo katika Mkoa huo katika ufunguzi wa Kituo cha Afya cha Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Kituo cha Afya cha Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala bora Haroun Ali Suleiman akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Kituo kipya cha Afya Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.kushoto yake ni Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Hassan Khatib Hassan

Baadhi ya waalikwa pamoja na wananchi waliohudhuria katika Ufunguzi wa Kituo cha Afya Ukongoroni Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.Ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

DC GAIRO AAMURU KUKAMATWA VIONGOZI WALIOKULA FEDHA ZA UJENZI WA SEKONDARI YA KATA IDIBO

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Shaidi Mchembe ameagiza kukamatwa kwa viongozi wote waliofuja shilingi milioni 32 za ujenzi wa shule ya sekondari ya Kata ya Idibo.

Kauli hiyo ameitoa leo wakati alipofanya ukaguzi wa ujenzi wa shule hiyo lililokwenda sambamba na ugawaji wa mabati na vifaa mbali mbali kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Idibo.Mhe. Mchembe aliwaomba TAKUKURU kuwakamata viongozi wote wanaosimamia ujenzi wa shule ili waweze kuhojiwa matumizi ya pesa na wizi uliotokea tokea kuanza kwa ujenzi huo.

"Nimepokea taarifa ya Kamati ya Ujenzi ambayo imebaini wizi wa shilingi milioni 12 na matumizi ya utata yenye thamani ya shilingi milioni 20, hivyo ninawaagiza TAKUKURU na OCD ndani ya siku saba kuwakamata wale wote wanaohusika na sheria ichukue mkondo wake," alisema Mhe. Mchembe.

Aidha mpaka sasa japo kuna dosari Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata Idibo umemaliza madarasa 3, vyoo na jengo la utawala.Wakati huo huo Mhe. Mchembe alikabidhi msaada wa mabati 120 na vifaa mbalimbali kwa ajili ya kupanua kituo cha Polisi Idibo kilichojengwa kwa nguvu za wananchi.

Katika hafla hiyo, Mhe. Mchembe aliyepokelewa na mwenyeji wake OCD - Gairo, Mratibu Mwandamizi Jeshi la Polisi, Ramadhani Kitantu, alitoa pongezi kwa Diwani Kata ya Idibo Mhe. Rajabu Mguhi na viongozi wake wote na wananchi wa Idibo kwa michango yao hadi boma kukamilika.

Mhe. Mchenbe aliwaomba wananchi washiriki kuchangia awamu ya pili ya umaliziaji bila kusahau nyumba za Polisi. Pia anakaribisha Wadau wengine wa maendeleo wenye Mapenzi mema na Gairo TUSHIRIKIANE.

Katibu Tawala Wilaya Bw. Adam John wakati wa ziara hizo alisisitiza wananchi kushirikiana na Serikali ili kujiletea Maendeleo yao. Pale ambapo kuna matatizo atahakikisha anayashughulikia ipasavyo kwa mujibu wa Sheria, Taratibu na Kanuni (STK). Ndani ya mwaka mmoja tumefanikiwa kufungua Sekondari za Kata mbili ambazo ni Chagongwe na Chanjale. Kote huko watoto walikuwa wanatembea zaidi ya km 20 kwenda shule na maabara sita.

Miradi yote ni nguvu za wananchi kwa zaidi ya asilimia 45 na fedha kutoka Serikali. Pongezi kwa Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwajali watoto wa masikini huku pembezoni vijijini kabisa ambapo nao wanajisikia vizuri na wanajenga Uzalendo wa kuipenda nchi yao tangu wadogo.

Gairo ina kituo kimoja tu cha Polisi hivyo hiki kitakuwa cha pili. Kituo hiki kitahudumia Kata tano za Gairo na Kata jirani zaidi ya sita kutoka Wilaya ya Kilindi, Kiteto na Mvomero kwani kipo mpakani mwa Wilaya hizo.

Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Siriel Shaidi Mchembe (kushoto) akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita na OCD - Gairo, Mratibu Mwandamizi Jeshi la Polisi, Ramadhani Kitantu (kulia) wakati alipofanya ukaguzi wa ujenzi wa Kituo cha Polisi Idibo, shule ya sekondari ya kata ya Idibo sambamba na ugawaji wa mabati na vifaa mbali mbali kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Idibo. 
 Ukaguzi wa Ujenzi shule ya Sekondari Kata ya Idibo. 
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Shaidi Mchembe (wa kwanza kulia) akabidhi msaada wa mabati 120 na vifaa mbalimbali kwa Jeshi la Polisi na uongozi wa kata ya Idibo kwa ajili ya kupaua kituo cha Polisi Idibo kilichojengwa kwa nguvu za wananchi. 
Wananchi na Wazee Maarufu wakifatilia mkutano na makabidhiano.

UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA SONGEA MJINI WAZIDI KUIMALIZA KAMBI YA UPINZANI

0
0
Moses Machali akimnadi Dkt Damas Ndumbaro
Wakati kampeni za kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma zikiendelea katika kata mbalimbali za manisipaa ya Songea mkoani Ruvuma kwa ajili ya kumpata mbunge wa jimbo hilo ambaye chama cha mapinduzi kimemteua Dkt Damas Ndumbaro kupeperusha bendera ya chama hicho waliokuwa viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani nchini wamezidi kujitokeza kwenye kampeni hizo na kutangaza kuachana na vyama vyao vya awali.

Miongoni mwa viongozi hao wa vyama vya upinzani ni pamoja na waliokuwa wajumbe watatu wa serikali ya mtaa wa Majengo mjini Songea kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo ambao walitangaza uamuzi huo wa kukihama chao hicho na kujiunga na chama cha Mapinduzi baada ya hotuba ya siku mbili mfululizo kwenye kampeni hizo za kumnadi mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama cha mapinduzi iliyotolewa na aliyewahi kuwa mwanachama wa chama na kingozi pia cha Demokrasia na maendeleo Moses Machali.

Katika hotuba yake ya kumnhadi mgombea huyo Machali alieleza sifa alizo nazo mgombea Dkt Damas Ndumbaro ambazo alizifahamu muda mrefu tangu akiwa kwenye kambi ya upinzani ambazo alisema hazina mashaka yoyote ya kumfanya asichaguliwe kuwa mwakilishi wa wananchi wa jimbo hilo na kuwataka wananchi wa jimbo la Songea mjini kwa ujumla kuitokeza kwa wingi siku ya Januari 13 mwaka huu kumpigia kura mgombea huyo na kuacha kuendelea kusikiliza na kufuata propaganda za wagombea wa vyama vya upinzani ambao walio wengi hawajui kilichoko kwenye vyama hivyo vya upinzani kwa sababu yeye alikuwepo huko na anajua kulivyo.

Viongozi wengine wa kambi ya upinzani waliopanda jukwaani katika viwanja vya mikutano vya Majengo na kutangaza kujiunga na chama cha mapinduzi ni pamoja na aliyekuwa katibu wa chama cha ACT Wazalendo mkoa wa Kigoma Sharon Msanya ambaye kabla ya kutangaza kujiunga na chama cha mapinduzi aliwataka wapiga kura wa jimbno la Songea mjini kutokuthubutu kulifanya jimbo hilo kuwa kambiya upinzani kwa sababu kufanya ni kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuwaletea wananchi maendeleo ambayo wameyahityaji kwa muda mrefu kurtoka serikalini na serikali ya awamu ya tano inaendelea kuonesha dhamira ya dhati kuwafikishia wananchi maendeleo hayo.

Alisema yeye amekuwa kiongozi mkubwa wa chama cha ACT Wazalendo katika ngazi ya mkoa lwa Kigoma akini amefikia uamuzi huo wa kusafiri kutoka mkoani Kigoma mpaka mjini Songea ili aweze kupata fursa ya kuwaeleza wananchi wa Songea umuhimu wa kukiunga mkono chama cha mapinduzi na mgombea wake Dkt Dams Ndumbaro kwa ajili ya maendeleo yao na taifa kwa ujumla kwa sababu mgombea huyo amekuwa mpigania maendeleo ya taifa kwa muda mrefu hata kabla hajafikia uamuzi huo wa kugombea nafasi hiyo ya kuwawakilisha wananchi wa jimbo lake.

Huku naye Edna Sunga aliyekuwa katibu wa kamati ya maendeleo ya jamii taifa na mjumbe wa kamati kuu na halmashauri kuu taifa wa chama cha ACT Wazalendo akizungumza baada ya kukihama chama hico na kujijnga na chama cha mapinduzi amesema kwa sababu yeye ni muumini wa kuzingatia miiko na vita dhidi ya rushwa na kuwaletea maendeleo wananchi ameona hana sababu ya kuendelea kuwa kwenye upinzani badala ya kuongeza na kujnganisha nguvu ya kuwajhudumia wananchi walio wengi.

Amesema kiongozi au mwananchi yeyote mwenye dhamira ya dhati ya maendeleo ambayo wananchi walio wengi wanayahitajihana budi kukiunga mkopno chama cha mapinduzi na mgombea wake ambaye amevaa taswira ya chama hicho na taifa kwa ujumla huku naye mgombea wa jimbo hilo kwenye uchaguzi huo akiendelea kuwaomba wananchi wa mji wa Songea kujiktokeza kwa wingi siku hiyo ya uchaguzi kwa ajili ya kupiga kura kwa chama cha mapinduzi.

Na Nathan Mtega, Jamvi la habari - Songea

MHASIBU HALMASHAURI YA NAMTUMBO MKOANI RUVUMA AJISHINDIA KITITA CHA SHILINGI MILIONI 50 ZA TATUMZUKA

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Mh.Luckiness Amlima akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 50 Mkazi wa wilaya ya namtumbo mwenye umri wa miaka 31,ambaye ni Mhasibu msaidizi wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoa wa Ruvuma,ndugu Jacob Ndee aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 50 .
 
Akielezea kwa furaha za kushinda kitita cha milioni 50 za mchezo huo wa kubahatisha wa TatuMzuka,Jacob alisema kuwa ndoto yake kubwa siku akipata fedha za kutosha atazitumia kwa Kilimo,Anasema kwa sasa anaona ndoto yake imetimia baada kupata fedha hizo,hivyo atazitumia katika kilimo.
 Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Mh.Luckiness Amlima akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa Kitita cha Milioni 50 cha TatuMzuka Ndugu Jacob Ndee pamoja na baadhi ya Wadau wengine,ambapo pia walionekana kuuufurahia ushindi wa Jacob,ambaye ni Mhasibu msaidizi wa halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoa wa Ruvuma.

DALILI KWAMBA BADO UNA UCHOVU WA LIKIZO NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO

0
0

Na Jumia Travel Tanzania

Ni hali ya kawaida kujisikia hali ya uchovu mahala pako pa kazi hususani baada ya kurudi kutoka likizo au mapumziko. Na inawezekana bado miongoni mwa wafanyakazi wenzako hawajarudi kutoka mapumzikoni. Achilia mbali bado kusikia salamu za, “likizo yako ilikuaje?” Au “Natumaini ulikuwa na mapumziko mema,” zikitawala kila unapokutana na watu.

Endapo unajisikia mwili na akili ni vizito kuanza na majukumu ya mwaka huu mpya basi kuna uwezekano mkubwa  hizo ni dalili za uchovu wa likizo. Na ukweli ni kwamba haupo peke yako, ni hali ya kawaida ambayo watu wengi hupitia kipindi kama hiki sehemu tofauti duniani.


Changamoto ni kwamba watu wengi huwa hawajijui kama bado wana uchovu wa likizo au mpaka waje kugundua inakuwa ni muda mrefu umepita. Jumia Travel ingependa kukushirikisha mambo yafuatayo ambayo ni dhahiri kwamba bado una uchovu wa likizo na namna yakukabiliana nao.

Akili yako. Endapo kumbukumbu za matukio uliyoyafanya kipindi cha mapumziko bado zinajirudia mara kwa mara basi ujue ni dalili upo kwenye uchovu wa likizo.


Nguvu yako. Endapo mwili bado unajisikia uchovu, kwa maneno mengine tunaweza kusema kwamba kila unachotaka kukifanya unakuwa ni mzito kufanya hivyo, basi ujue una uchovu wa likizo.

Hali yako. Kuna wakati unakuwa na ari ya kufanya kazi iliyopo mbele yako lakini kila ukijitahidi kuanza inakuwa ni vigumu akili yako kuwa makini. Hii ni dalili nyingine kwamba bado una uchovu wa likizo.


Usingizi wako. Kipindi cha mapumziko ilikuwa ni vigumu kulala kwa wakati kwani haukuwa na hofu ya kuwa na majukumu siku inayofuatia. Hivyo ulikuwa unalala muda wowote unaotaka na kwa kiwango chochote ulichokitaka. Lakini sasa itabidi kulala kwa wakati na kuamka muda ambao utakufanya uwahi kwenye shughuli zako ipasavyo. Kama unajisikia usingizi unaupata kwa tabu au haupati usingizi ndani ya muda muafaka basi hiyo ni dalili nyingine ya uchovu wa likizo.

Hamu yako ya kula. Kipindi cha likizo watu wengi huwa hawazingatii ratiba ya kula au aina ya vyakula wanavyokula. Kwa sababu huwa ni kipindi ambacho tunaupumzisha mwili na akili kutokana na pilikapilika za mwaka mzima, suala la kuzingatia vyakula vya kula huwa halipo. Endapo bado haujisikii kula chochote au aina fulani ya vyakula basi ujue hali ya kujisikia bado upo mapumzikoni haijatoka mwilini na akilini mwako.   


Dalili zote hizo hapo juu ni kwamba bado unakabiliana na uchovu wa likizo ambao ni vigumu kuondoka mwilini na akilini mwako kwa haraka kama unavyotarajia. Umefikia wakati sasa wa kuondokana na hali hiyo ili uendelee na majukumu yako kama kawaida kwani kipindi cha mapumziko kimekwishapita.

Namna ya kurudia hali yako ya kawaida.


Fuatilia kwa karibu mienendo yako ya sasa. Inawezekana kwamba ulikuwa na wakati mzuri kipindi cha likizo, moyo na akili yako bado unakukumbusha namna ilivyokuwa. Suluhu ni kubadili ratiba ya shughuli ulizozifanya ili kuendana na shughuli ulizonazo kwa sasa.  

Fanya mazoezi. Mbinu nyingine itakayokusaidia zaidi ni kwa kufanya mazoezi mepesi aidha ya viungo au hata kutembea jioni mara baada ya kazi. Mazoezi huufanya mwili na akili kuondokana na uchovu na kuupatia ari na nguvu mpya ya kufanya mambo mengi kwa ufanisi zaidi.

Hakikisha unazingatia mlo wenye afya na usingizi wa kutosha. Ni wakati sasa wa kurudi kwenye ratiba ya mlo wenye afya kama ilivyokuwa awali. Kwani inaaminika kwamba namna pekee ya kuufanya mwili na akili yako kujisikia vizuri ni kupitia mlo wenye afya na usingizi wa kutosha. Kujinyima usingizi wa kutosha ni ni sawa na kujipatia mateso bila ya kujijua. Kwa hiyo, acha kujitesa!  

Mshirikishe rafiki au mtu wako wa karibu namna unavyojisikia. Hii hali haikutokei wewe peke yako bali ni watu wengi. Hivyo basi, kwa kumshirikisha mtu wako wa karibu inaweza kuwa ni tiba mbadala. Huwezi kufahamu atakuwa na ushauri wa aina gani ili kukusaidia kuishinda hiyo hali. Jumia Travel inaamini kwamba lazima utakuwa na mtu wako wa karibu ambaye unaelewana naye, anakufahamu vya kutosha na kamwe hatosita kukusaidia pale unapohitaji msaada katika kujinasua na hali kama hii. Kushindwa kufanya hivyo kunaweza kukuhatarishia shughuli zako kutoenda sawa na kukupoteza fursa mbele yako bila ya kujijua.   

WAZIRI MPINA AKAMATA KILO 65,600 ZA SAMAKI ZENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI MIA TATU

0
0
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina (katikati )akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Bi Mwanaidi Mlolwa akitoa maelezo baada ya kushuhudia shehena ya samaki wachanga aina ya Sangara kilo 65600 mjini Bukoba waliokamatwa katika kisiwa cha Lubili wilayani Muleba leo.Mwenye koti ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustapha Kijuu.
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina (aliyenyanyua mikono ) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustapha Kijuu (mwenye koti) leo, nje ya ghala la kuhifadhia samaki katika ofisi ya Uvuvi mjini Bukoba mara baada ya kushuhudia shehena ya samaki wachanga aina ya Sangara kilo 65600 waliokamatwa katika kisiwa cha Lubili wilayani Muleba.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustapha Kijuu (aliyesimama) akisoma taarifa ya mkoa kuhusu sekta ya mifugo na Uvuvi kwa Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina (alikaa kulia kwake) leo, mara baada ya kufanya ziara ya ghafla leo ili kushuhudia shehena ya samaki wachanga aina ya Sangara kilo 65600 waliokamatwa katika kisiwa cha Lubili wilayani Muleba. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi nchini, Mwanaidi Mlolwa.
Sehemu ya shehena ya samaki wachanga waliokaushwa kwa chumvi aina ya Sangara kilo 65600 waliokamatwa katika kisiwa cha Lubili wilayani Muleba, wakiwa wamehifadhiwa katika ghala kwenye ofisi ya Uvuvi jijini Bukoba. Samaki hao walikaatwa kufuatia raia mwema kutoa taarifa kwa Waziri Luhaga Mpina hivi karibuni.

Mwandishi Maalum,Bukoba
…………………………………………………………………………………………………………………
Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Luhaga Joelson Mpina amekamata kilo 65600 za samaki wachanga aina ya Sangara waliokaushwa kwa chumvi wenye thamani ya shilingi milioni mia tatu katika Kisiwa cha Lubili wilayani Muleba kwenye Mkoa wa Kagera baada ya wamiliki wa samaki hao kukimbia.

Akizungumza leo na Waandishi wa Habari katika Ofisi ya Kitengo cha Doria na Udhibiti wa Uvuvi wa mpakani katika Mkoa wa Kagera, Mpina amesema tukio la kukamatwa kwa samaki hao lilifanikiwa baada ya yeye kupata taarifa kutoka kwa raia mwema ambapo aliagiza mamlaka za Wilaya ya Muleba kufuatilia kwa karibu hatimaye kuwakuta samaki hao wakiwa wameanikwa chini katika kisiwa hicho.

Waziri Mpina alisema Sheria ya Uvuvi namba 22 ya Mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka 2009 kifungu cha 90(1) inataka samaki
wanaovuliwa waandaliwe katika mazingira yanayokidhi vigezo vya usalama  kwa mlaji na kwamba ni kosa kisheria kuwavua au kuchakata samaki aina ya Sangara walio chini ya sentimeta 50 kwa kuwa ni wachanga na sentimita 25kwa Samaki aina ya Sato. Pia sentimita 85 kwa Sangara kwa kuwa ni wazazi wanaotakiwa kundelea kuzaa.

Aidha Waziri aliongeza kwamba Sheria hiyo imetoa mamlaka kwa watendaji wa Serikali kutaifisha mali zote zilitumika katika uvuvi haramu kupitia kifungu cha 37(a) (ii) na (iii) pamoja na Sheria ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu namba 29 ya mwaka 1994.

Waziri Mpina ameagiza watendaji kufuata taratibu zote za kisheria ili samaki hao wauzwe kwa njia ya mnada na mapato hayo yaingie Serikalini mara moja.Aidha aliwaonya wafanyabiashara na wavuvi kuachana na uvuvi haramu kwa kuwa ni kuhujumu raslimali za taifa ambazo zingetumika kwa kizazi cha sasa na baadaye.

“Mfanyabiashara yoyote wa samaki na mazao yake anayetaka kufilisika na kutafuta matatizo katika maisha yake aendelee na biashara ya uvuvi haramu”alisisitiza Mpina

Kufuatia tukio hili, Waziri Mpina amewapa wiki mbili wafanyabiashara na wasafirishaji wote wa samaki na mazao yake waliopewa
leseni ya ya kufanya biashara hiyo kwa mwaka 2018 kuleta cheti cha uthibitisho cha ulipaji kodi ambapo amesema kama watashindwa
kufanya hivyo hawataruhusiwa kufanya biashara hiyo.

Alisema kuanzia sasa wafanyabiashara wote wote wataruhusiwa kupata leseni hiyo baada ya kuwasilisha cheti cha uthibitisho wa ulipaji kodi, cheti cha usajili wa kampuni na mahesabu ya kibiashara yaliyohakikiwa ili kuepuka utaratibu wa sasa ambao unatoa mwanya kwa mawakala wa ndani na nje ya nchi kujiingiza katika biashara hiyo kinyemela na kuikosesha Serikali mapato kwa kukwepa kulipa kodi
mbalimbali.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustapha Kijuu alisema Serikali itahakikisha kwamba uvuvi haramu unakuwa historia katika Mkoa wa Kagera na kuwataka wananchi kuwafichua wavuvi haramu ili vyombo vya Serikali viwakamate na kuwafikisha katika mikondo ya sheria.

Alisema sekta ya uvuvi inaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua hali ya uchumi kwenye mkoa wake na taifa kwa ujumla kama wadau wote watashiriki kikamilifu katika vita dhidi ya uvuvi haramu ambapo alisema jumla ya wananchi 26,272 wameajiriwa kutokana na shughuli za uvuvi katika mkoa huo.

Alisema mkoa utaendelea na kupambana na uvuvi haramu ambapo kwa mwaka 2016/17 jumla ya doria 65 zilifanyika na kuwezesha kukamatwa kwa makokoro ya Sangara 422, nyavu ndogo za dagaa 57,nyavu za timba 3,231, nyavu za makila 14,141, ndoano 711, katuli 16,mitumbwi 133 samaki wachanga kilo 5,621 na watuhumiwa 86.

Hata hivyo Mkuu huyo alisema katika kuongeza uzalishaji wa samaki jumla ya mabwawa 584 yamechimbwa kwa mwaka 2016/2017 kutoka mabwawa 181 mwaka 2005/2006 sawa na ongezeko la mabwawa 403.

Kwa upande mwingine Mkuu wa Mkoa alisema hivi karibuni Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Ngara ilikamata gari lenye namba za uasajili T 614 CLQ aina ya Mitsubishi Canter likiwa limepakia samaki kilo 2,000 aina ya Sangara na kilo 530 wa aina ya Sato kwenye mpaka wa Murusagamba wilayani Ngara.

Alisema Afisa wa Kitengo cha Doria na Udhibiti wa Uvuvi wa mpakani katika Mkoa wa Kagera bwana Ayoub Ngoma na dereva wa gari hilo Ayoub Sanga walishikiliwa na polisi kwa hatua za kisheria kwa tuhuma za kushiriki
katika utoroshaji wa samaki wenye kilo 2530 kwenda nchini Burundi zenye thamani ya shilingi 20,850,000/= ambapo Ngoma ameshasimamishwa kazi kupisha uchunguzi.

Pia Mshauri wa Uvuvi wa Mkuu wa Mkoa, Efrazi Mkama na maafisa Uvuvi wa Halmashauri ya Muleba Wilfred Tibendelana na Maengo Nchimani na Afisa Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba vijijini Renus Ruhuzi wanaendelea kuripoti katika kituo cha polisi Bukoba kwa mahojiano ya kisheria juu ya utoroshwaji wa samaki hao.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Mwanaidi Mlolwa alisema Serikali ina mkono mrefu na kwamba hakuna mtu atakayebaki salama iwapo atajihusisha na uvuvi haramu.

Aidha alisema maafisa uvuvi wanawajibu wa kuhifadhi na kutunza takwimu mbalimbali za sekta ya uvuvi ili kutoa picha halisi ya jinsi sekta inavyochangia katika uchumi wa nchi kwa ujumla.

“Kimsingi sekta ya uvuvi ina mchango mkubwa katika uchumi wa
nchi yetu lakini tatizo kubwa ni ukosefu wa takwimu sahihi

Katibu Mkuu atembele Kiwanda Cha Matrekta Na Kiwanda Cha Viua Dudu

0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel akiendesha trekta la Kiwanda cha URSUS.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel atembelea kiwanda cha Viua dudu kilichopo Tamco – Kibaha na kukutana na balozi wa Cuba nchini Tanzania Mhe. Lucas Domingo Hernandez Polledo.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel, akiagana na na balozi wa Cuba nchini Tanzania Mhe. Lucas Domingo Hernandez Polledo.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa na balozi wa Cuba nchini Tanzania Mhe. Lucas Domingo Hernandez Polledo pamoja na uongozi wa Kiwanda cha Viua dudu Kibaha Mkoani Pwani.
 

CHAMA KUZIKWA LEO MAKABURI YA KISUTU DAR ES SALAAM

0
0
Mmiliki wa Ujijirahaa blog anaungana na ndugu jamaa, marafiki na wapenzi wote wa Mpira na familia ya Athuman Chama katika kumuombea Dua na kumsindikiza  mpendwa wetu Chama katika kumpumzisha kwenye nyuma ya milele, Mungu ampumzishe kwa amani ndugu yetu kipenzi chetu, pumzika kwa amani  Allah muondoshee madhila ya kaburini (Amiin). (PICHA KWA HISANI YA UJIJIRAHAA BLOG)

MBUNGE MGIMWA ATUMIA MAMILIONI UJENZI WA MADARASA YA SHULE ZA MSINGI, ZAHANATI NA NYUMBA ZA WAFANYAKAZI KATIKA KIJIJI KIBENGU

0
0
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akizungumza na wananchi katika moja ya shule ambayo inahitajika kujengewa vyumba viwili ya madarasa na kukarabati vyumba vingine vitatu kwa gharama za wananchi na mbunge mwenyewe akichangia kwa asilimia kubwa kuboresha maendeleo ya sekta ya elimu kwa wananchi na wanafunzi wa jimbo hilo
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akizungumza mmoja ya walimu pamoja viongozi kutoka kwenye ofisi yake ya mbunge ambao alikuwa ameongoza nao katika kukagua na kutatua changamoto za wananchi kwenye kata ya Kibengu
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akitoa mfano wa kufanya kazi kwenye ujenzi wa vyumba vitatu vya shule ya msingi Kibengu ambako nako wananchi wamechangia nguvu zao
Katibu wa vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM wilaya ya Mufindi akiwa na katibu wa mbunge idara ya uhamasishaji na michezo Lwimbo nao wakijumika na wananchi katika ujenzi wa shule ya msingi Kibengu
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akizungumza na viongozi katika eneo ambalo vyumba vitatu vya madarasa vinajengwa
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akizungumza kwenye eneo ambalo ofisi ya kijiji inajengwa ajili ya kurahisisha kutoa huduma kwa wananchi 
Mbunge wa jimbo la Mufindi KaskaziniMahamuod Mgimwa akiwa na diwani wa kata ya Kibengu Zakayo Kilyenyi sambamba na katibu wa mbunge idara ya uhamasishaji na michezo Lwimbo



Na Fredy Mgunda,Mufindi Kaskazini. 


Mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Kibengu wametumia jumla ya shilingi milioni mia moja kumi na tisa na laki mbili (119,200,000) katika ujenzi wa madarasa ya shule,zahanati na nyumba za wafanyakazi wa zahanati na walimu wa shule zilizopo katika kijiji hicho lengo likiwa katika kuboresha sekta ya elimu na afya kwa wananchi.

Akizungumza na wananchi katika kijiji hicho mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini Mahamuod Mgimwa alisema kuwa ameamua kuwekeza katika elimu na afya kwasababu wananchi wakifanikiwa kupata vitu hivyo viwili kwa wakati watafanya maendeleo kwa kasi kubwa kulingana na wakati uliopo na kuendana na mazingira wanayoishi.

“Hivi ndio vipaumbele vyangu kwa kijiji hiki kwa wakati huu maana nimegundua kuwa changamoto kubwa ni kuwa shule nyingi za msingi zilijengwa miaka mingi iliyopita sasa zimechakaa na sio rafiki kwa wanafunzi kuwasaidia kupata elimu bora hivyo nimeanza na hilo pamoja na kuchangia maendeleo kwa kuboresha sekta ya afya ili wananchi wakiugua waweze kutibia hapa hapa kijiji kwa kuwa nina uhakika huduma itakuwa inatolewa kwa ustadi mkubwa na yenye ubora unaotakiwa” alisema Mgimwa

Mgimwa alieleza kuwa pesa hiyo itatumika katika maeneo yafuatayo ujenzi wa ofisi ya kijiji cha Kibengu utatumia gharama ya shilingi milioni thelathini (30,000,000) hadi kukamilika kwake,kuingiza umeme zahanati na kwenye nyumba za waganga imegarimu kiasi cha shilingi 1,200,000/=,ujimbaji wa kisima shilingi 2,00,000/=,ujenzi wa nyumba za walimu mbili kwa moja itagharimu kiasi cha shilingi 25,000,000/= na shule ya msingi Kibengu kutafanyika ujenzi wa madarasa matatu ambayo yatagharimu kiasi cha shilingi 21,000,000/=.

“Hizi ni gharama katika kijijicha Kibengu ambazo nimechangia na wananchi wangu hivyo napenda kuwapa habari vijiji na vitongoji vingine kwenye jimbo langu kuiga mfano wa kijiji cha Kibengu na kitongoji cha Mitanzi kwa kujituma kuleta maendeleo” alisema Mgimwa

Aidha Mgimwa alisema kuwa wananchi wa kitongoji cha Mitanzi katika kijiji cha Kibengu nao wamekuwa wakitoa ushirikiano na kufanikisha kufanya maendeleo katika maeneo yafuatayo ujenzi wa nyumba za walimu na madarasa ya shule ya msingi Mitanzi utagarimu kiasi cha shilingi milioni kumi na saba (17,000,000) uchimbaji wa kisima shilingi 1,000,000/=, ukarabati wa madarasa mawili shilingi 17,000,000 kutona na yalivyo haribika, kuingiza umeme kwenye nyumba za walimu na madarasa shilingi 5,000,000/=

“Ukaingalia tumetumia nguvu kubwa na wananchi kufanikisha haya japo kuna maeneo bado hatujamalizia na ninauhakika tutamalizia lakini bado kunawatu wanasema eti sifanyi kazi sasa sijui wataka niwe ninawapa pesa mikononi mwao ili wajue maendeleo yapo” alisema Mgimwa

Mgimwa alimalizia kwa kuwaomba wananchi wa jimbo la Mufindi Kaskazini kuendelea kumuunga mkono katika kuleta maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo kwa kuwa wanajinea kazi anayoifanyia hivyo wasikubali kulishwa maneno na watu wasiopenda maendeleo.

Kwa upande wake mtendaji wa kijiji cha Kibengu Dominicus Nyaulingo alimshukuru mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini kwa jitihada zake za kuleta maendeleo kwa kushirikiana na wananchi na kahidi kuwa watandelea kuzitangaza kazi anazozifanya ili wananchi wote wajue anafanya kazi gani na kupunguza maneo ambayo yamekuwa yakisemwa bila kuwa na ushaidi juu ya utendaji wa mbunge huyo.

“Kweli kabisa mbunge wetu amekuwa akifanya kazi kubwa sana ila sisi tumekuwa hatuzisemi kazi za mbunge kwa wananchi hivyo kuchochea chuku baina ya wananchi na mbunge hivyo kuanzia leo nitakuwa ninazisemea kazi za mbunge kila kwenye mkutano wa kijiji” alisema Nyaulingo

WAZIRI JAFO APONGEZA JITIHADA ZA MBUNGE WA MAKAMBAKO

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo(Katikati) alipotembelea Hospital ya Mji wa Makambako.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akisalimia na Muuguzi wa Hospital ya Mji wa Makambako alipotembelea Hospital hiyo kukagua utoaji wa uduma za Afya
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe.Lucy Msafiri wakati wa ziara yake katika Hospital ya Mji wa Makambako.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo katika Picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya pamoja na watumishi wa Hospital ya Mji wa Makambako.
Huu ndio Muonekano wa Hospital ya Makambako unavyoonekana kwa hivi sasa



Nteghenjwa Hosseah,Makambako.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo amempongeza Mbunge wa Makambako Mhe. Deo Sanga kwa jitihada mbalimbali anazozifanya katika kuboresha Sekta ya Afya katika Jimbo hilo.

Jafo ameyasema hayo wakati alipotembelea Hospital ya Mji wa Makambako na kuona vyumba viwili vya Madaktari ambavyo vimejengwa na Mbunge Mhe. Sanga.

“Kwa dhati kabisa nimpongeze Mhe. Sanga kwa kujitoa kuboresha huduma za Jamiia hii inaonyesha nia yake njema katika kuwaletea wananchi maendeleo kwa sabababu wananchi wakiwa na Afya Njema wataweza kuendelea na shughuli zao kikamilifu za kujitaftia kipato kisha kupata maendeleo” Alisema Jafo

Kwa kutambua Idadi kubwa ya watu wanaopata huduma katika Hospital hiyo ambayo ina miundombinu Duni ikiwa ni pamoja na ukosefu wa Jengo la kisasa la Kuhifadhia Maiti pamoja na Ukosefu wa wodi mbalimbali.Waziri Jafo amesema Serikali itaangalia jinsi ya kuboresha miundombuni hiyo ili wakazi wa Makambako waweze kupata huduma bora za Afya kama Watanzania wanazopata wengine.

“Tutaweka Jitihada katika kutafuta Fedha kutoka kwenye vyanzo vyetu Ili kuongeza miundombinu ya Afya na hospital hii iweze kuwa na hadhi ya kuwa na Hospital ya Mji” Alisema Jafo.Hata hivyo Jafo amechukua kilio cha Hospital hiyo kuendelea kupata mgao wa Kituo cha Afya wakati imeshapandishwa hadhi kuwa Hospital ya Mji ana ameahidi kulishughulikia.

“Makambako ni eneo muhimu sana katika Kanda hii yenye wakazi wengi, shughuli nyingi za kiuchumi na muingiliano wa watu wengi kutoka ndani na nje ya Nchi hivyo inahitaji huduma bora zaidi za Afya kwa kwa kuzingatia umuhimu wa eneo na wananchi wake” alisema Jafo.

Waziri Jafo anaendelea na ziara yake katika Mikoa Mbalimbali lengo ni ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo iki chini ya Ofisi ya Rais Tamisemi.

WANANCHI MKOANI MBEYA WAZIDI KUJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA USAJILI LICHA YA MVUA KUNYESHA KATIKA MAENEO TOFAUTI

0
0
Afisa Usajili Mamlaka ya Vitambulsho vya Taifa Ndugu Lodrick Hawonga, akiwapatia wananchi wa Kata ya Ilemi huduma ya Usajili kwa kuwajazia fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa.

Maafisa Usajili – NIDA wakiwafanyia usajili wananchi waliofika katika Vituo mbali mbali vya Usajili kata ya ilemi, usajili unaohusisha uchukuaji wa alama za Kibaiologia, Saini ya Kielektroniki, pamoja na Picha, nyuma yao ni foleni ya Wananchi wakisubiri kupatiwa huduma hiyo


Baadhi ya Wananchi wa Vijiji mbalimbali kata ya Ilemi wakikamilisha usajili wa awali kwa kujaza fomu za maombi kwa wale ambao hawakuwa wamekamilisha zoezi hilo, kushoto ni Mjumbe wa kata hiyo Ndugu Martini Mpwani akiwasaidia kujaza barua za Utambulisho kwa wale waliokosa Viambatisho.
Mtendaji wa kata ya Ilemi Ndugu Amiri Kassimu, akiwahakiki na kuwatambulisha Wananchi wake kwa kuwagongea Muhuri wa Serikali ya Mtaa ya Ilemi pamoja na kuwaandikia barua za utambulisho zitakazowawezesha kukamilisha hatua muhimu katika zoezi la usajili Vitambulisho vya Taifa ambalo linahusisha uchukuaji alama za Vidole, Picha na saini ya Kielktroniki

Wananchi wakiwa wamepanga foleni nje ya moja ya Kituo cha Usajili wakisuburi kupatiwa huduma hiyo licha ya Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali Mkoani Mbeya.
Mmoja wa Wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma ya Usajili katika kituo cha Usajili cha Mwamfute kata ya Ilemi akichukuliwa alama za Vidole katika zoezi la Usajili lililohusisha uchukuaji wa alama za kibailogia, saini ya Kielektroniki pamoja na Picha.

………………….

Licha ya Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Mbeya, Wananchi katika Kata na vijiji mbalimbali mkoani humo, wameendelea kuhamasika kujitokeza kwa wingi kusajili kupata Vitambulisho vya Taifa.

Katika Kata ya Ilemi amkusanyiko wa wananchi umekuwa mkubwa; ikidhihirisha ni kwa namna gani wananchi wamekuwa na uelewa mpana wa umuhimu wa Vitambulisho vya Taifa; hususani katika kipindi hiki ambacho zoezi kwa sasa linaendelea.

Afisa Usajili Wilaya ya Mbeya Bi. Alavuya Ntalima amesema katika Kata ya Ilemi zoezi limeanza Jumatano tarehe 3/01/2018 na linahusisha Kata za Iganzo, Isanga, Sisimba, Mabarini, Maendeleo pamoja na Forest.

Wakizungumzia zoezi la Usajili linaloendelea katika Kata zao Watendaji wa Serikali za vijiji wameahidi kuendelea kushrikiana kwa karibu na Mamlaka kuhakikisha wananchi wote wanaoishi kwenye vijiji vyao na wenye sifa wana sajiliwa na kupata Vitambulisho vya Taifa ndani ya muda uliopangwa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Wananchi wamepongeza juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) hususani hili la kuwatambua wananchi na kuwapatia Vitambulisho vya Taifa ambavyo vitawapa fursa ya kufanya mambo mengi na kutambulika katika shughuli mbalimbali za kijamii.

MWENYEKITI, WAJUMBE WA SERIKALI YA KIJIJI LAMADI WASIMAMISHWA KAZI KUPISHA UCHUNGUZI

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi katika mkutano wa Hadhara uliofanyika Lamadi wiayani Busega.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Lamadi Wilayani Busega, Mhe. Nzala Hezron akizungumza na wananchi katika Mkutano wa Hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka kwa lengo la kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzitolea ufumbuzi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Boniventure Mushongi akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Lamadi wilayani Busega.


Na StellaKalinga, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amemsimamisha kazi kwa muda wa mwezi mmoja Mwenyekiti wa Kijiji cha Lamadi Wilayani Busega Mhe.Nzala Hezron pamoja na Wajumbe wa Serikali ya Kijiji hicho, ili kupisha uchunguzi kufuatia tuhuma mbalimbali zinazowakabili.



Uamuzi huo umekuja kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wananchi wa Lamadi dhidi ya Mwenyeiti huyo kwa Mkuu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka katika Mkutano wa hadhara uliofanyika jana Lamadi, kuhusu tuhuma mbalimbali ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za michango ya wananchi katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari Lukungu pamoja na kutosoma mapato na matumizi ya fedha za michango mbalimbali ya wananchi.



“Ili tuweze kutenda haki ya uchunguzi na ukaguzi tumeona ni busara Mwenyekiti asiwe Ofisini na wajumbe wanaounda Serikali ya Kijiji wasiwe ofisini ili uchunguzi na ukaguzi wa akaunti uweze kufanyika kwa haki” alisema Mtaka.

Mtaka amesema Mkaguzi wa Ndani kutoka katika Ofisi yake atakayeshirikiana na Mkaguzi wa ndani wa Wilaya ya Busega kufanya ukaguzi katika Akaunti ya Shule kujua namna fedha zilizochangwa na wananchi na zilizotolewa na Halmashauri zilivyofanya kazi ya Ujenzi wa Vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo katika Shule ya Sekondari Lukungu.

Ameongeza kuwa kutokana na malalamilo ya baadhi ya wadau pamoja na wananchi uchunguzi na ukaguzi huo pia utahusisha pia Akaunti ya Kijiji cha Lamadi kwa kuwa Kijiji hicho kina hali nzuri kimapato na kimekuwa kikichangiwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, hivyo ni vema ikabainishwa wadau wanaokichangia, wanachangia kitu gani na namna michango hiyo inavyotumika.

Aidha, Mtaka amesema ukaguzi huo pia utafanywa kwenye kamati iliyohusika katika upimaji viwanja katika Mji Mdogo wa Lamadi kwa sababu nayo imekuwa ikilalamikiwa na baadhi ya wananchi kuwa haikuwatendea haki.

Mkuu wa Mkoa huyo amesema uchunguzi na ukaguzi katika maeneo hayo matatu utaanza tarehe 10/01/2018 na taarifa rasmi ya zoezi hilo itatolewa tarehe 10/02/2018 kwa wananchi kupitia Mkutano wa hadhara, itakapobainika kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi ya watu hao ni za kweli Serikali itachukua hatua.

Wakati huo huo Mtaka amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kumuondoa Afisa Mtendaji wa Kata ya Lamadi Bw.Furaha Magese Ng’onela na kuhakikisha kuwa ifikapo tarehe 10/01/2018 Kijiji cha Lamadi kinapata Mtendaji wa Kijiji kwa kuwa aliyepo sasa anakaimu na Kata ya Lamadi ipangiwe Afisa Mtendaji mwingine.

Vile vile Mtaka ameahidi kuchangia mifuko 100 ya saruji katika Ujenzi wa Shule ya Sekondari Lukungu ambayo sasa imepewe jina lake(Mtaka Sekondari) na wananchi hao, Mkuu wa Wilaya ya Busega,Mhe.Tano Mwera ameahidi kuchangia mifuko 40 na Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe.Dkt.Raphael Chegeni ameahidi kutoa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi milioni 10 kufanikisha ujenzi huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Lamadi, Mhe.Nzala Hezron amesema kuhusu suala la ujenzi wa Shule yeye pamoja na Serikali yake ya Kijiji haikushirikishwa kikamilifu na Kamati ya Maendeleo ya Kata(WADC).

Naye Mhe.Chegeni amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka kuwa michango ya viongozi, wadau wa mendeleo na wananchi wa Lamadi inayotolewa sasa itatumika kama ilivyokusudiwa na ikiwa kuna atakayebainika kutumia tofauti na utararibu atachukuliwa hatua.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano mwera ametoa wito kwa wananchi wa Lamadi kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuchangia shilingi 10,000 kwa kaya ili kufikia Februari 15, 2018 vyumba vinne vya madarasa viwe vimekamilika katika Shule ya Sekondari Lukungu(imebadilishiwa jina na wananchi na kuitwa Mtaka Sekondari), ambayo hadi sasa ina madarasa manne na matundu ya vyoo 16 yanayoendelea kukamilishwa ili wanafunzi waanze masomo.

Nao wananchi wa Vijiji vinavyounda Kata ya Lamadi wamesema wamejipanga kuhakikisha vyumba vya madarasa vinajengwa na kukamilika  katika shule hiyo kabla ya Februari 15, 2018 ambapo kila Kitongoji kimejipanga kuanza na ujenzi wa chumba kimoja cha darasa na vitongoji vyenye watu wachache vitaungana viwili kujenga chumba kimoja cha darasa, ambapo kamati za ujenzi zitachaguliwa na wananchi wenyewe.

SHAKA AWASILI SINGIDA LEO,KUMNADI MGOMBEA UBUNGE WA CCM SINGIDA KASKAZINI.

0
0
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka (Kulia) Akipeana mkono na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Singida Kaskazini Ndg:Peter Monko  Alipowasili katika Ofisi za CCM Mkoa wa Singida leo.
 Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka akisain kitabu cha wageni  katika Ofisi za CCM Mkoa wa Singida (kulia) Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Ndg Juma Kilimba.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi  dkt. Denis Nyiraha akimkaribisha  Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka alipowasili katika ofisi za CCM Mkoa wa Singida.
''Tutashinda na tutashinda kwa sababu mtaji wa ushindi tunao lengo ni lile lile kuhakikisha Singida kaskazini inaendelea kuwa ngome ya CCM''Alisema Shaka wakati akizungumza na Viongozi wa CCM Alipowasili katika ofisi za CCM Mkoa wa Singida leo.(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)
Viewing all 46200 articles
Browse latest View live




Latest Images