Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46206 articles
Browse latest View live

Ziara ya Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Mkoa wa Kusini Pemba

0
0

Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Hassan A. Ramadhan (kulia) akifafanua jambo kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (wa pili kulia) kuhusu mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano inavyosaidia kurahisisha mawasiliano na utendajikazi katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba. Kamishna Sururu akiendelea na ziara ya kikazi, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 – 19 Disemba, 2017.
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Juma A. Khamis (aliesimama) akichangia hoja kwenye kikao cha Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (hayupo pichani) na Watumishi wa Idara ya Uhamiaji walioko Mkoa wa Kusini Pemba leo tarehe 19 Disemba, 2017. Alisema “Ongezeko la Bandari Bubu ndani ya Wilaya ya Mkoani ni changamoto kubwa katika utekelezaji wa majukumu yetu. Tunazo takriban Bandari bubu 103, tunaomba Idara itupatie gari la kufanyia doria katika maeneo hayo”. Kwa upande wake Kamishna Sururu katika ziara yake hiyo ya kikazi Mkoani humo, aliahidi kulifanyia kazi ombi mapema iwezekanavyo.
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (kushoto) akikagua baadhi ya magari chakavu yaliyopo katika Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba, yanayosubiri kupigwa mnada baada ya kukamilika kwa taratibu za uuzaji wa Mali za Serikali. Wakati wa ziara ya kikazi Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 – 19 Disemba, 2017. Pamoja na kutembelea maeneo mbali mbali ya utendaji kazi Mkoani humo ikiwemo Bandari ya Mkoani, Bandari ya Wesha iliyopo Chake Chake na Bandari bubu kadhaa. Kulia kwake ni Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abdi Bulushi. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akikagua kitabu cha utoaji wa Hati za Dharura za Kusafiria “ETD” katika Ofisi ya Uhamiaji Wilaya ya Mkoani, zinazotolewa kwa Watanzania wanaohitaji kusafiri nje ya Nchi. Huku akiwasisitiza Maofisa Uhamiaji katika utoaji wa Hati hizo wazingatie vyema Sheria na Taratibu zilizopo ili kuepusha matumizi yasiyo sahihi. Aliyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kikazi Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 – 19 Disemba, 2017. Hati za Kusafiria za Dharura ni miongoni mwa Hati mbali mbali za Kusafiria zinazotelewa na Idara ya Uhamiaji Nchini
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akiambatana na Maofisa waandamizi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar kukagua baadhi ya bandari Bubu zinazotumiwa na wakaazi wa Shehia za Kengeja na Muwambe, Kusini Magharibi mwa kisiwa cha Pemba, kwa shughuli mbali mbali za kiuchumi na kijamii, ambazo hutumika kama vipenyo kwa watu kuingia na kutoka visiwani humo kinyume na taratibu za Uhamiaji. Wakati alipofanya ziara ya kikazi maeneo mbali mbali ndani ya Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 Disemba, 2017. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akitoa nasaha zake kwa Maafisa, Askari na watumishi Raia wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba, wakati akihitimisha ziara ya kikazi Mkoani humo Leo tarehe 19 Disemba, 2017. Aidha, Kamishna Sururu aliwataka watumishi wote kuzingatia maadili ya kazi, pamoja na kutilia mkazo matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii. “Naelewa tupo kwenye utandawazi, lakini narudia kuwasihi matumizi ya Mitandao ya kijamii itumike kwa kuzingatia Kanuni na Miongozo ya Serikali, pia mjiepushe na utoaji wa Siri na Taarifa za serikali, ni mwiko kutoa taarifa yoyote. fuateni Sheria na Taratibu tulizowekewa”. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akiambatana na Maofisa waandamizi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar kukagua baadhi ya bandari Bubu zinazotumiwa na wakaazi wa Shehia za Kengeja na Muwambe, Kusini Magharibi mwa kisiwa cha Pemba, kwa shughuli mbali mbali za kiuchumi na kijamii, ambazo hutumika kama vipenyo kwa watu kuingia na kutoka visiwani humo kinyume na taratibu za Uhamiaji. Wakati alipofanya ziara ya kikazi maeneo mbali mbali ndani ya Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 Disemba, 2017. 
Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu akiambatana na Maofisa waandamizi wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar kukagua baadhi ya bandari Bubu zinazotumiwa na wakaazi wa Shehia za Kengeja na Muwambe, Kusini Magharibi mwa kisiwa cha Pemba, kwa shughuli mbali mbali za kiuchumi na kijamii, ambazo hutumika kama vipenyo kwa watu kuingia na kutoka visiwani humo kinyume na taratibu za Uhamiaji. Wakati alipofanya ziara ya kikazi maeneo mbali mbali ndani ya Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba tarehe 18 Disemba, 2017. 
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Kusini Pemba, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abdi Bulushi akimuonesha Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari M. Sururu (wa pili kulia) na Maafisa Uhamiaji aliombatana nao, matunzo na usafi wa mazingira katika nyumba za Makaazi ya Askari wa Uhamiaji, zilizoko eneo la Ndugukitu, Wilaya ya Chake chake, Mkoa wa Kusini Pemba. Kamishna Sururu yupo Mkoa wa Kusini Pemba kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 18 – 19 Disemba, 2018. Aidha, Nyumba hizo zilifunguliwa rasmi na Mhe. Makamo wa Pili wa Rais, Balozi Seif Iddi mapema mwezi Januari, 2017.
Mojawapo ya nyumba za Makaazi ya Askari wa Uhamiaji, zilizoko eneo la Ndugukitu, Wilaya ya Chake chake, Mkoa wa Kusini Pemba. Kamishna Sururu yupo Mkoa wa Kusini Pemba kwa ziara ya kikazi kuanzia tarehe 18 – 19 Disemba, 2018. Aidha, Nyumba hizo zilifunguliwa rasmi na Mhe. Makamo wa Pili wa Rais, Balozi Seif Iddi mapema mwezi Januari, 2017.

QNET YATOA MSAADA KWA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA KHAYRAAT ORPHANS CENTRE KILICHOPO KIGOGO KATI

0
0
Mwakilishi wa QNET Tanzania, Benjamin Mariki akikabidhi mashine ya kusafishia maji ya kunywa (water purifier) kwa mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Khayraat Orphans Centre kilichopo Kigogo Kati, Bi. Khadija Hussein jana.
Mwakilishi wa QNET Tanzania, Benjamin Mariki akikabidhi vyakula kwa mlezi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Khayraat Orphans Centre kilichopo Kigogo Kati, Bi. Khadija Hussein jana.

………….

QNET imetoa Msaada wa mashine ya kusafishia maji (water purifier) na vyakula kwa watoto yatima wa kituo cha Khayraat, Dar es salaam

Tarehe 20th Desemba, Dar es salaam – Moja kati ya taasisi inayokua kwa kasi sana Tanzania ya masoko ya mtandao QNET, leo imetoa msaada wa mashine yenye mfumo wa kusafisha maji ya Water purifier na chakula chenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 2 kwa kituo cha watoto yatima cha Khayraat jijini Dar es salaam.

Msaada wa QNET ni sehemu ya juhudi za kampuni hiyo za kuwajibika katika jamii, ambazo zimeelekezwa katika kutoa msaada wa upatikanaji wa maji safi na salama kwa zaidi ya watoto 500 wenye uhitaji katika kituo cha kulelea watoto yatima na kuwapatia chakula kwaajili ya kuwawezesha kufurahia sikukuu za krimasi katika kipindi hiki cha sikukuu kama watoto wengine.

Kwa mujibu wa mwakilishi wa QNET Tanzania Benjamin Mariki, kampuni ya mauzo ya moja kwa moja ina sera bora ya uwajibikaji kwa jamii ambayo inatafuta kutoa kwa jamii inayoihudumia.

“Katika kampuni ya QNET, tunaamini kuwa zaidi ya kusambaza bidhaa zenye ubora wa kiwango cha juu kwa wateja wetu, tuna jukumu la kusaidia serikali na wadau wengine katika kutekeleza shughuli ambazo zina athari nzuri kwa jamii, hasa miongoni mwa wanajamii wenye uwezo mdogo,” alisema Mariki.

Mariki alisema kuwa msaada uliotolewa kwaajili ya kituo ni pamoja na ufungaji wa mashine ya kusafishia maji, kilo 100 za Mchele, kilo 100 za maharage, kilo 100 za unga, lita 60 za mafuta ya kupikia, kilo 100 za sukari, kilo 100 za sabuni ya kufulia pamoja na biskuti, pipi na juisi.

Akipokea msaada huo, Mwasisi wa kituo cha Khayraat Orphans Centre, Bi Khadija Khussein aliishukuru kampuni ya QNET kwa kutoa msaada akisema kuwa msaada huo utawasaidia kwa kiwango kikubwa watoto walioko kituoni.

“Tunashukuru kwa msaada huo tukiwa tunatambua kuwa mashine ya kusafishia maji ya water purifier itasaidia katika kurahisisha upatikanaji wa maji safi na salama kwaajili ya watoto, hivyo kutoa uhakika wa afya kwa watoto kwa kuzuia magonjwa yanayoambukizwa kwa maji kama vile typhoid na Kipindupindu wakati vyakula vitawapa watoto nafasi ya kufurahia sikukuu ya krimasi na mwaka mpya”. Alibainisha Bi Khussein

Kuhusu QNET

Ni kampuni maarufu ya mauzo ya moja kwa moja yenye asili ya Asia, QNET inatoa aina mbalimbali za bidhaa za kuboresha maisha ambazo zinatolewa kupitia mfumo wake wa biashara ya mtandao (e-commerce) kwa wateja na wasambazaji katika zaidi ya nchi 100. Kampuni hii pia ina baadhi ya ofisi zake na Mawakala katika nchi 25 duniani kote, na zaidi ya watayarishaji 50, nje ya waendeshaji wa ndani ya nchi au mawakala katika nchi kadhaa.

QNET ni mwanachama wa Chama cha wauzaji wa moja kwa moja (Direct Selling Association) cha Malayasia, Singapore, Ufilipino na Indonesia. QNET pia ni sehemu ya Chama cha Chakula Bora cha Hong Kong (Hong Kong Health Food Association) na Chama cha viwanda vya Virutubisho vya afya cha Singapore (Health Supplements Industry Association) miongoni wa vingine.

QNET pia inafanya vizuri katika kudhamini michezo dunia kote, ikijumuisha mpira wa miguu (Mshirika wa moja kwa moja wa mauzo wa Klabu ya Manchester City), Mashindano ya Magari ya fomula One, badminton na zaidi, kufuatia imani thabiti ya kampuni ya QNET kwamba msukumo, ari na kufanya kazi kwa pamoja katika michezo kunaendana na ule wa QNET

Kwa maelezo zaidi kuhusu QNET, Tafadhali tembelea Wavuti ya QNET, www.qnet.net

SSRA MWAJIRI BORA SEKTA YA UMMA

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu Mh Jenista Mhagama akikabidhi kwa SSRA Tuzo ya Mwajiri Bora kwa Mwaka 2017. Anayepokea ni Mkurugenzi wa SSRA Bi Lightness Mauki.

Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Ajira, Kazi, Vijana na Walemavu Bw. Eric Shitindi akikabidhi kikombe kwa SSRA baada ya kuibuka mwajiri bora wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za Mwajiri bora wa Mwaka 2017 zilizotolewa hivi karibuni na Chama cha Waajiri Nchini (ATE) jijini Dar es Salaam. Anayepokea ni Mkurugenzi wa SSRA Bi. Lightness Mauki

Watumishi wa SSRA wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuibuka mshindi wa jumla kwa Taasisi za Umma katika hafla ya utoaji Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka 2017 zilizotolewa na Chama cha Waajiri Nchini (ATE) Jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA Bi. Sarah Kibonde Msika akiwa kwenye Meza ya SSRA wakati wa hafla ya utoaji Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka 2017 zilizotolewa na Chama cha Waajiri Nchini (ATE) Jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Wafanyakazi wa SSRA wakiwa kwenye meza ya SSRA wakati hafla ya utoaji Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka 2017 zilizotolewa na Chama cha Waajiri Nchini (ATE) Jijini Dar es Salaam.

SHIRIKA LA POSTA NCHINI LAZINDUA NEMBO MPYA YA SHIRIKA HILO YENYE KAULI MBIU YA TWENZETU

0
0
 Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa  akizindua nembo mpya ya Shirika la Posta nchini ambayo imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam katika Kuboresha huduma za shirika hilo kuwa la kisasa.
 Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, akimpongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta nchini, Dr Haroun Kondo mara baada ya kuzindua nembo mpya ya shirika hilo jijini Dar es Salaam leo
 Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa akishuka katika mabasi mapya ya Shirika la Posta nchini mara baada ya kuzindua huduma ya mabasi ya shirika hilo ambayo yatakuwa yanabeba abiria na vifurushi
 Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa, akizungumza mara baada ya kuzindua Nembo mpya ya  Shirika la Posta nchini
 Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta nchini, Dr Haroun Kondo  akizungumza kabla yakumkaribisha mgeni rasmi kuzindua nembo mpya ya shirika la Posta nchini.
 Mjumbe wa bodi ya Shirika la Posta nchini, Khadija Khamis Shabani akitoa neno la shukrani mara baada ya kumalizika kwa uzinduzi wa nembo mpya ya shirika la Posta nchini
 Muongozaji wa shughuli ya uzinduzi wa nembo mpya ya Shirika la Posta nchini, Pascal Mayala akizungumza wakati sherehe hizo zikikiendelea.
 Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta nchini, Dr Haroun Kondo pamoja na Posta Mkuu Hassana Mwang'ombe wakiongozana kwenda kukagua magari
Sehemu ya wafanyakazi wa shirika la Posta nchini wakiwa katika hafala hiyo ya uzinduzi wa nembo mpya ya Shirika la Posta.

MATUKIO YA ZIARA YA WAZIRI WA MAMBO YA NE NCHINI CHINA

0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea jambo wakati alipokuwa katika mazungumzo rasmi na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming jijini Beijing. 
Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming akisisitiza jambo alipokuwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt.Augustine Mahiga leo jijini Beijing. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa na ujumbe wake aliongozana nao katika ziara ya kikazi nchini China. Kutoka kushoto ni Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China, Kanali Remigius Ng'umbi anayefuata ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Thomas Kashililah na Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki. 
Wajumbe wa pande mbili za China na Tanzania wakiwa katika mazungumzo. 
Wajumbe wengine wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo. Kutoka kulia ni Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Malmeltha Mutagwaba, Naibu Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango kutoka Serikali ya Zanzibar, Bw. Khamis Omar 
Balozi Mahiga akitoa zawadi ya picha kwa Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming. 
Mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango ya China 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipngo ya China, Bw. Ning Jizhe alipowasili ofisini kwake kwa ajili ya kufanya mazungumzo. 
Ujumbe wa Tanzania na China wakijadiliana namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiano katika masuala ya uchumi, uwekezaji n biashara. 
Bw. Jing Jizhe akionesha utayari wa nchi yake wa kushirikiana na Tanzania katika masuala ya maendeleo ya kiuchumi. Mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi
Balozi Mahiga na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China. 
Balozi Mahiga akiwa na katika mazungumzo na mmoja wa wawekezaji aliyedhmiria kuwekeza Tanzania. 
Mwekezaji mwingine akisalimiana na Balozi Mahiga kabla ya kuanza kwa mazungumzo yao. 
Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na aliyekuwa Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt, Lu Youqing

TUME YA ARDHI KUANZISHA KANZIDATA YA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI

0
0
Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) ipo mbioni kuanzisha Kanzidata (Database) ya mipango ya matumizi ya ardhi iliyofanyika nchini na wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi.

Kwa kushirikiana na wadau wa upangaji, usimamizi na utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi wa taasisi za serikali pamoja na asasi za kiraia, Kanzidata hiyo itabeba taarifa zitakazoonyesha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali kama vile kilimo, malisho, huduma za jamiii, n.k itarahisisha utendaji kazi kwa Tume, mamlaka zingine za upangaji, wadau pamoja na wananchi kwa ujumla ambao watatumia teknolojia kujua maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali nchi nzima
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya mipango ya matumizi ya Ardhi(NLUPC) Dkt. Stephen Nindi akifungua mkutano wa kikosi kazi kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzidata ya mipango ya matumizi ya ardhi,Mjini Morogoro
Mwenyekiti wa Kikao Bw. Jamboi Baramayegu kutoka ujamaa Community akielezea utaratibu wa namna kazi itakavyofanyika
Afisa Tehama kutoka wakala wa Serikali Mtandao Bw. Thomas Malinga akitoa maelezo ya malengo ya wao kushiriki katika mchakato wa uanzishwaji wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango na matumizi ya ardhi.
Afisa Mipango wa Tume ya Taifa ya mipango ya matumizi ya Ardhi Bw. Gelard Mwakipesile, akielezea kwa kina kwa wajumbe wa mkutano kuhusu mipango ya matumizi ya ardhi,mchakato ulipo anzia hadi kuanza kwa mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi
Bw. Paulo Tarimo kutoka Wizara ya Kilimo akichangia jambo wakati wa kikao cha mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi.
Baadhi ya wanakikosi kazi kutoka sekta mbalimbali wakiendelea na majadiliano ya kutoa maoni yao juu ya kuandaa mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi.
Katibu Mkuu wa Chama cha wafugaji Tanzania Bw. Magembe Makoye akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la wafugaji
Bw. Godfrey Massay Meneja utetezi kutoka LANDESA akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Kilimo
Afisa Sheria kutoka NLUPC Bi. Devotha Selukele akichangia jambo wakati makundi mbalimbali wakiwasilisha maoni yao juu ya kanzi data
Afisa programu kutoka Haki Ardhi Bw. Joseph Kiombola akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Asasi za Kiraia.
Afisa wanyama pori (TAWA) Bw. Herman Nyanda akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Maliasili 
Afisa Mpelembaji kutoka TNRF Bw. Wilbard akiwasilisha mapendekezo yao kwa ajili ya mchakato wa uanzishwaji wa kanzi data ya mipango ya matumizi ya ardhi kutoka katika kundi la Utafiti
Wadau wakiendelea na mkutano huo.Picha na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa Tanzania 

RAIS DKT MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU MJINI DODOMA LEO

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Mhe. Bella Bird  wakifungua kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipeana mikono na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Mhe. Bella Bird  wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa  jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipeana mikono na Mwenyekiti wa Bodi ya  Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Andrew Wilson Massawe wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipeana mikono na Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Miles wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Kassima Majaliwa Majaliwa wakizungumza wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipokea kutoka kwa Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango ramani ya Tanzania yenye kuonesha takwimu ya hali ya  maambukizi ya VVU kimkoa wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia  wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi jengo la ofisi ya Taifa ya Takwimu mjini Dodoma leo Desemba 20, 2017.

PICHA NA IKULU

RC ATEMBELEA DAMPO LA KISASA MANISPAA YA DODOMA, ASEMA DODOMA LAZIMA IWE SAFI ZAIDI

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (katikati mbele) akiwa na Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida (kulia) na Meneja wa Dampo la Kisasa la Manispaa hiyo John Chiwanga (kushoto) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Moja ya magari maalum kwa ajili ya kubeba uchafu ya Manispaa ya Dodoma likipimwa uzito kabla ya kuingia kumwaga uchafu katika Dampo hili la kisasa lilipo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu katika Manispaa hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (kushoto) akiwa katika sehemu ya Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma iliyoanza kutumika huku akipata maelezo kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.

Sehemu ya pili ya Dampo la kisasa la Chidaya katika Manispaa ya Dodoma linalotumia Teknolojia ya kuzika taka ardhini ambayo bado haijaanza kutumika kwa sasa.






Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (kushoto) akipokea taarifa fupi kuhusu Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (wa pili kushoto) akipatiwa maelezo kuhusu mfumo wa upimaji uzito wa taka zinazoletwa katika Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma unavyofanya kazi kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (wa pili kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.PICHA ZOTE: RAMADHANI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI WA MANISPAA


NA RAMADHANI JUMA,OFISI YA MKURUGENZI

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge amesema Mji wa Dodoma hauna sababu ya kuwa mchafu kwa sababu Manispaa ya Dodoma imetekeleza mradi wa ujenzi wa dampo la kisasa na litakalodumu kwa miaka mingi ijayo.

Aliyasema hayo baada ya kutembelea dampo la kisasa la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma lililopo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu takribani umbali wa kilometa 12 kutoka katikati ya Mji wa Dodoma.

Katika ziara hiyo fupi, Mkuu huyo wa Mkoa alioongozana na Katibu Tawala wa Mkoa huo Rehema Madenge pamoja na Mkuu wa Idara ya Mazingira na Usafishaji wa Manispaa hiyo Dickson Kimaro aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi.

Awali mara baada ya kuwasili katika eneo la dampo, Mheshimiwa Mahenge alielezwa jinsi Dampo hilo la kisasa linavyofanya kazi na Mhandisi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida, aliyemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa, dampo hilo linatumia teknolojia ya kuzika taka ardhini (Sanitary Landfill) ambayo ni rafiki kwa mazingira na afya za wakazi wa maeneo ya karibu na dampo.

Mhandisi Faida alimjulisha Mheshimiwa Mahenge kuwa, dampo hilo tayari limeanza kufanya kazi mapema mwaka huu, na limejengwa kwa fedha za mradi wa Kuimarisha Miji ya Kimkakati Tanzania (TSCP) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na kuratibiwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

China Yaunga Mkono Juhudi Za Rais Magufuli

0
0
Na Mwandishi Maalum, Beijing

China imeahidi kushirikiana na Tanzania kikamilifu katika miradi ya kipaumbele ambayo Serikali ya AwamuyaTano imepanga kuitekeleza ili kufikia azma yake ya uchumi wa viwanda ifikapo 2020 na baadaye uchumi wa Kati ifikapo 2025.

Hayo yalibainishwa leo jijini Beijing na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming na baadaye kukaririwa tena na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango (NDRC), Bw. Ning Jizhe walipofanya mazungumzo kwa nyakati tofauti na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Mahiga aliainisha na kufafanua namna Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Maguful iilivyokusudia kuwashirikisha wadau mbalimbali kwenye utekelezaji wa miradi ya kipaumbele ambayo inalenga kuchochea agenda ya uchumi wa viwanda. 

Miradi hiyo ni pamoja na kuendeleza nishati ya umeme ambapo Serikali imedhamiria kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020 ili kuharakisha utekelezaji wa agenda ya uchumi wa viwanda ambayo haitaweza kufanikiwa kama hakutakuwa na umeme wa kutosha na wauhakika.

Kutokana na uhalisia huo, Serikali imepanga kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa megawatts 2100 kwenye mto Rufiji na kujenga njia za kusambaza umeme huo kutoka Rufiji, Chalinze hadi Dodoma na nyingine kutokaChalinze, Kilimanjaro hadi Arusha. 

Miradi mingine ni ujenzi wa mtandao wa usafiri wa reli na uboreshaji wa reli ya TAZARA, ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na viwanja vya ndege ikiwa ni pamoja na kujenga jengo la abiria katika Kiwanja cha ndege cha Mwanza. 

Waziri Mahiga alisisitiza umuhimu wa miundombinu hiyo kuunganishwa ili iweze kuleta tija iliyokusudiwa katika uchumi. Aliongeza kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa wastani wa asilimia 7 kwa mwaka na uchumi wa nchi za jirani ambazo zinategemea bandari za Tanzania pia unakua, hivyo kuendeleza na kuunganisha miundombinu ya usafiri ni muhimu kwa ustawi wa uchumi wa nchi hizo na uchumi wa Tanzania.

Aidha, Waziri Mahiga alieleza namna Serikali inavyoendelea na zoezi la kuhamisha makao makuu ya Serikali kwenda Dodoma na kukaribisha makampuni ya China kushiriki kwenye uwekezaji wa miundombinu mbalimbali kwenye mji huo mpya wa makao makuu.

Baadhi ya miundombinu muhimu inayohitajika Mjini Dodoma ni upatikanaji wa maji safi ya na ya uhakika na kuiomba China ishiriki katika ujenzi wa Bwawa la Kidunda mkoani Morogoro. Bwawa hilo likijengwa na kukamilika litasaidia sio tu kusambaza maji ya uhakika mkoani Dodoma bali hata mkoa wa Dar Es Salaam ambao matumizi ya maji yanaongezeka kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu kila siku.

Waziri Mahiga aliahidi kuwa Serikali yake itakamilisha taratibu zilizosalia ili mradi wa Mchuchuma na Liganga uweze kuanza kwa kuwa mradi huo ni muhimu sana katika sera ya uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Biashara aliahidi kuwa Serikali ya China itafanyia kazi kwa haraka miradi yote iliyowasilishwa ili Tanzania iweze kutimiza malengo yake ya kuwaletea maendeleo wanachi. 

Aliongeza kuwa Serikali yake itaharakisha kufanya upembuzi yakinifu wa miradi hiyo kwa madhumuni ya kutimiza masharti ya kampuni za uwekezaji na taasisi zinazotoa fedha nchini China.

Aidha, alipongeza hatua ya Serikali ya Tanzania ya kuweka mikakati ya kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020. Hivyo, aliahidi kuwa atazishawishi kampuni za China zinazozalisha umeme wa jua, upepo na joto ardhi zijek uwekeza nchini ili lengo hilo litimie kwa haraka.

Wakati huo huo, Waziri Mahiga alikutana na watendaji wa makampuni mbalimbali ya uwekezaji yaliyodhamiria kuwekeza nchini kwenye sekta mbalimbali. Makampuni hayo yanataka kuwekeza kwenye uzalishaji wa Sukari, ujenzi wa kiwanda cha kusindika mihogo, uagizaji wa mihogo mikavu toka Tanzania kwa wastani wa tani laki 3 hadi 5 kwa mwaka na huduma za kitalii kama ujenzi wa mahoteli yenye hadhi ya nyota tano. 

Kampuni hizo zote zimeomba kukutanishwa na wadau husika ili wkamilishe taratibu zinazotakiwa waanze uwekezaji haraka iwezekanavyo.

Waziri Mahiga aliwahakikishia wawekezaji hao kuwa uamuzi wao wa kuwekeza Tanzania hawataujutia kwa kuwa Tanzania ni nchi tulivu na yenye amani, ina rasilimali nyingi na soko kubwa kutokana na kuwa mwanachama wa SADC na EAC.

NEC YATOA UFAFANUZI KUHUSU MGOMBEA WA CHADEMA SINGIDA KASKAZINI

0
0

WAHAMIAJI HARAMU 55 WAMAKATWA WILAYANI MKINGA

0
0

ZAIDI ya wahamiaji 50 raia kutoka nchini Ethiopia wameka matwa eneo la Duga wilayani Mkinga mkoani Tanga kwa kosa la kiungia nchini kinyume cha sheria.

Wahamiaji hao wamekamatwa ndani ya kipindi cha mwezi Desemba mwaka huu kutokana na operesheni ambazo zimekuwa zikiendeshwa na Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi ya kuhakikisha wanazibiti wimbi la uingiaji huo.

Hayo yalisemwa jana na Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Tanga DCI Crispian Ngonyani wakati akizungumza na gazeti hili ofisi kwake ambapo alisema wahamiaji hao hivi sasa wanaendelea na kesi zao zinazowakabili kutokana na kuingia nchini kinyume na utaratibu uliopo.

Alisema hatua ya kukamatwa kwa wahamiaji haramu hao inatokana na kuwepo kwa misako ya kushtukiza katika maeneo mbalimbali hasa ya mipakani mkoani hapa ambapo wahamiaji hao wamekuwa wakitumia kama njia ya kuingilia.

“Sisi kama Uhamiaji mkoani Tanga tumejipanga vizuri kuhakikisha wimbi la wahamiaji haramu hawaingii kutokana na doria ambazo tumekuwa tukizifanya mara kwa mara lakini kubwa zaidi ni kuwepo kwa vituo eneo la mipakani hususani Horohoro “Alisema.

Aidha alisema pia ili kuhakikisha suala hilo linazibitiwa kwa vitendo tayari wamekwisha kuweka kituo eneo la Vijinga wilayani Mkinga kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wanakagua magari ambayo yamekuwa yakitokea nchini Jirani ya Kenya ili kuweza kubaini iwapo wahamiaji haramu wamebebwa.

Hata hivyo alisema kuelekea sikukuu za krismasi na mwaka mpya wamejiandaa vizuri kuweza kukabiliana na wimbi la wahamiaji haramu wanaoweza kuingia mkoani hapa kwa kuendelea operesheni kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo nyumba za kulala wageni na kwenye hoteli.

“Licha ya kuendelea na operesheni hizo lakini nisema idadi ya wahamiaji haramu wanaoingia mkoani Tanga kwa sasa imepungua kwa sababu wakiwakamata wanawapeleka mahakamani pamoja na mawakala wao"Alisem.

Afisa Uhamiaji huyo alisema lakini bado tunaendelea kuhakikisha ina koma kabisa kwa kuwachukulia hatua kali na watanzania ambao watabainika wanashirikiana nao kuwaingia mkoani hapa(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

TANESCO YAHIMIZA MATUMIZI BORA NA ENDELEVU YA MTO PANGANI NA BWAWA LA NYUMBA YA MUNGU

0
0

  NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

MATUMIZI bora ya bonde la Mto Pangani, ndio njia pekee itakayosaidia kutunza vyanzo vya maji ambayo hutumika kuzalisha umeme kwenye vituo vya Pangani Hydro Systems, Meneja wa vituo hivyo, Mhandisi Mahenda S Mahenda amewaambia wahariri wa vyombo vya habari wanaotembelea bwawa la Nyumba ya Mungu lililoko mpakani mwa wilaya ya Mwanga na Simanjiro.
“Tanesco kama wadau wakubwa wa Mto huu, tumeona Mto umeingia mchanga na mchanga huo unatakiwa kuondolewa ili kuweza kuzalisha maji mengi zaidi kutoka bwawa la Nyumba ya Mungu na maji hayo yaweze kupatikana kwenye vituo na hatimaye kuzalisha umeme kama ambavyo inatakiwa.” Alisema Mhandisi Mahenda.
Pangani Hydro Systems ni mkusanyiko wa vituo vitatu vya kufua umeme vinavyofuatana ambavyo vimejengwa sehemu tofauti tofauti katika Mto Pangani.Vituo hivyo ni pamoja na Nyumba ya Mungu, kituo cha Hale na kituo cha New Pangani Falls na vyote kwa ujumla wake huzalisha umeme wa Megawati 97 ambazo huingizwa kwenye Gridi ya Taifa, alisema Mhandisi Mahenda.
Kituo cha Nyumba ya Mungu, kilizinduliwa mwaka 1964 na Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere, na kina mashine mbili za kufua umeme zilizofungwa tangu mwaka huo na kila moja inao uwezo wa kuzalisha Megawati 4 za Umeme na kufanya jumla ya Megawati 8
Hata hivyo changamoto kubwa inayokikabili kituo hicho na vituo vingine ambavyo vyote huendeshwa kwa kutumia nguvu za maji, ni mabadiliko ya tabia nchi na ongezeko la shughuli za kibinadamu kandokando ya Mto huo pamoja na kwenye bwawa lenyewe na hivyo kupelekea upungufu wa mara kwa mara wa maji ya kutosha kuendesha mitambo.
“Tunashirikiana na wenzetu wanaosimamia bonde la Mto Pangani, kwa kufanya doria za mara kwa mara ili kuwaelimisha wananchi matumizi bora na endelevu ya maji ya Mto huo ili kuleta manufaa kwa pande zote, amesema Mhandisi Mahenda.


Mhandisi Mahenda S. Mahenda(kulia), akifafanua mambo mbalimbali kwa wahariri kwenye bwawa la Nyumba ya Mungu Desemba 19, 2017

RITTA KABATI KUKARABATI SHULE YA MSINGI KIHESA

0
0
 Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mbunge wa viti maalam mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati amefanya ziara kwenye baadhi ya shule za msingi za manispaa ya Iringa kwa lengo la kubaini changamoto zilizopo na kuanza kuzitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuboresha mazingira ya wanafunzi kusomea.

Akizungumza mara baada ya kumaliza zira hiyo ya wiki moja Kabati alisema kuwa amefanya ziara katika shule ya msingi Kihesa,Igereke,Mtwira na shule ya Kibwabwa na kubaini changamoto nyingi ambazo anaanza kuzitafutia ufumbuzi hivi karibuni.

“Nimejionea mwenyewe changamoto zilizopo na naona kama changamoto kwa asilimia kubwa zinafanana hivyo ni kazi yangu kuanza kutafuta njia ya kuanza kuzitatua changamoto hizo”alisema Kabati.

ACACIA YAFANYA TAMASHA LA AJIRA KUWAPA FURSA WAFANYAKAZI WALIOACHISHWA KAZI MIGODI YA BUZWAGI NA BULYANHULU

0
0



Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Acacia kupitia migodi ya dhahabu ya Buzwagi na Bulyanhulu imefanya tamasha la ajira kwa kuwakutanisha waliokuwa wafanyakazi wa migodi hiyo na makampuni zaidi ya 20 kwa ajili kubalishana mawazo na kupeana mawasiliano na taarifa ili wafanyakazi hao wapate kazi.

Tamasha hilo limefanyika leo Jumatano Desemba 20,2017 katika ukumbi wa Umoja uliopo katika mgodi wa Buzwagi uliopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkufunzi katika Idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dk Chris Mauki.

Akizungumza wakati wa tamasha hilo,Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu alisema lengo la tamasha la ajira lilioandaliwa na Acacia ni kuwaonesha fursa za ajira waliokuwa wafanyakazi wa kampuni ya Acacia kwa kuwakutanisha na makampuni mbalimbali katika kipindi cha kuelekea kufunga migodi hiyo.

“Tumekutana hapa ili kuonesha fursa za ajira kwa wafanyakazi wetu waliobobea katika kazi za migodini, kuna maisha mengine baada ya mgodi,tumealika kampuni ambayo yanachukua mawasiliano na CV na kama kuna nafasi za ajira basi watapatia ili maisha yaendelee nje ya mgodi”,aliongeza Busunzu.

“Tulialika makampuni zaidi ya 40, 15 yalikubali kushiriki,na 11 leo yamehudhuria,lakini pia wafanyakazi zaidi ya 260 wamehudhuria kwa ajili ya kuonana na makampuni haya,Acacia inaamini tamasha hili litakuwa na mafanikio makubwa tuliyotarajia”,alieleza.

Aidha Busunzu alisema kupitia program yao ‘No Harm 2020’ yenye miradi 10,wamekuwa wakitoa elimu na mafunzo mbalimbali kwa wafanyakazi wao kuhusu namna ya kuishi baada ya kumaliza muda ajira mgodini ambapo wafanyakazi 800 katika mgodi wa Bulyanhulu na 600 katika mgodi wa Buzwagi wamepatiwa mafunzo ya ujasiriamali na ajira.

Kwa upande mgeni rasmi Dk Chris Mauki ambaye ni Mkufunzi katika Idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam aliipongeza Acacia kwa kuwaandaa wafanyakazi wake kwa kuwapatia mafunzo ya namna ya kuishi baada ya migodi kufungwa huku akiwataka kukubali mabadiliko na kuthubutu kufanya kazi nyingine badala ya kukata tamaa.

“Mnayo nafasi ya kufanya biashara,kuajiriwa,kujiajiri na kuajiri wengine, ,mnachotakiwa kufanya ni kujitambua,kukubali mabadiliko,kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha,muishi maisha ya kuokoa muda,kuweni na mahusiano mema na watu wanaowazunguka na hapo ndipo mtakubaliana nami kuwa kuna maisha baada ya mgodi”,aliongeza Dk. Mauki.

Nao washiriki wa tamasha hilo waliishukuru Acacia kuwakutanisha na makampuni hayo kwani wamewapa urahisi wa kutafuta kazi kwa kukutana na waajiri moja kwa moja na kuwapatia taarifa zao (CV).

Nayo makampuni hayo yalisema Acacia ina wafanyakazi wazoefu na waliobobea katika kazi za migodini hivyo yanaamini yatapata wafanyakazi wazuri watakaowatumia kwenye makampuni yao.

“Acacia ni kampuni kubwa ya kimataifa, hii ni sehemu nzuri ya kupata wataalamu wanaojua kazi vizuri”,alisema Kaimu Meneja rasilimali watu kutoka shirika la Madini la taifa- STAMICO Lameck Kabeho na Jolene Ngaluko Mtalo kutoka Wakala wa ajira. –CV People Africa.

Naye Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila alisema mpaka sasa wafanyakazi 3000 wameachishwa kazi katika migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu na zoezi la kupunguza wafanyakazi bado linaendelea katika mgodi wa Buzwagi hivyo idadi itaongezeka.

Kasitila aliyataja makampuni yaliyoshiriki katika tamasha hilo kuwa ni Twiga Cement,Mantrac Tanzania Ltd,Northern Engineering,SAO Hill,Shanta Gold mine,IMED,LINDAM,CV People,Junior Construction,Sandvick na STAMICO.

Mgeni rasmi Mkufunzi katika Idara ya Saikolojia ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Dk Chris Mauki akizungumza katika Tamasha la Ajira lililoandaliwa na Kampuni ya Uchimbaji madini ya dhahabu ya Acacia lililofanyika leo Jumatano Desemba 20,2017 katika mgodi wa Buzwagi na kukutanisha pamoja makampuni zaidi ya 10 na wafanyakazi zaidi ya 260 walioachishwa kazi katika mgodi wa Buzwagi na Bulyanhulu wakati Acacia ikielekea kufunga migodi hiyo.Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog



Dk Chris Mauki akizungumza katika Tamasha hilo la Ajira.Kulia ni Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu.
Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea lengo la kufanya tamasha la ajira lililokutanisha pamoja makampuni na wafanyakazi wa Acacia ili kupeana fursa za ajira. Kulia Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mganza,kushoto ni Dk. Chris Mauki.

Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akiwasisitiza waliokuwa wafanyakazi wa Acacia kutumia fursa ya tamasha hilo kutafuta maisha nje ya migodi.

Washiriki wa tamasha la ajira wakimsikiliza Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu

Meneja wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea namna Acacia inavyoendelea kutoa elimu ya ajira na ujasiriamali kwa wafanyakazi wake ili kujiandaa kuanza maisha mengine nje ya migodi.Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila. Wa kwanza kulia ni Meneja Msaidizi wa Ulinzi katika mgodi wa Buzwagi Allan Bunyan akifuatiwa na Meneja Ulinzi katika mgodi wa Buzwagi Gordon Surgeon

Washiriki wa tamasha la ajira wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea

Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila akielezea kuhusu tamasha la ajira ambapo alisema zaidi ya makampuni 40 yalialikwa kushiriki tamasha hilo, makampuni 15 yakakubali kushiriki na leo makampuni 11 yamekutana na wafanyakazi wa Acacia zaidi ya 260 walioachishwa kazi katika migodi hiyo.

Kasitila alisema mpaka sasa wafanyakazi 3000 wameachishwa kazi katika migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu hivyo wanafanya jitihada za kuhakikisha wafanyakazi hao wanapata fursa za ajira sehemu zingine ili maisha yaendelee

Mtaalamu wa Mawasiliano Mgodi wa dhahabu wa Buzwagi Mary Lupamba akitoa maelekezo kwa washiriki wa tamasha hilo la ajira

Tamasha linaendelea

Washiriki wa tamasha hilo wakiwa eneo la tukio

Tamasha linaendelea

Washiriki wa tamasha wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea

Tamasha linaendelea



Tamasha linaendelea





Washiriki wa tamasha hilo wakiwa eneo la tukio





Waliokuwa wafanyakazi katika migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu wakiwa katika ukumbi wa Umoja katika mgodi wa Buzwagi kwa ajili ya kutembelea vibanda vya makampuni yaliyoshiriki katika tamasha la ajira kwa ajili ya kupata mawasiliano na kutoa taarifa zao (CV) kutafuta fursa za ajira





Waliokuwa wafanyakazi katika migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu wakiwa katika banda la shirika la Madini la taifa- STAMICO,wakisikiliza maelezo kutoka Kaimu Meneja rasilimali watu wa shirika hilo,Lameck Kabeho





Waliokuwa wafanyakazi wa Acacia wakiwa katika banda la Shanta Gold Mine kutafuta fursa za ajira





Hapa ni katika banda la kampuni ya Sandvik,kulia ni aliyekuwa mfanyakazi wa Acacia akiuliza jambo





Mfanyakazi wa Mantrac Tanzania Ltd akimsikiliza kwa makini mmoja wa waliokuwa wafanyakazi wa Acacia





Hapa ni katika banda la LINDAM huduma kwa waliokuwa wafanyakazi wa Acacia inaendelea


Ndani ya ukumbi wa Umoja washiriki wa Tamasha la ajira wakibadilishana mawazo





Kulia Mfanyakazi wa CV People,Jolene Ngaluko akimsikiliza kwa makini mmoja wa waliokuwa wafanyakazi wa Acacia aliyeamua kupeleka CV yake kwa ajili ya kutafuta fursa za ajira
Wafanyakazi wa CV Peole Africa wakiendelea kukusanya CV kwa kuziweka kwenye Laptop



Waliokuwa wafanyakazi wa Acacia wakiangalia CV walizokuja nazo kwenye tamasha la ajira kwa ajili ya kuzikabidhi kwenye makampuni



Waliokuwa wafanyakazi wa Acacia wakibadilishana mawazo



Meneja Msaidizi wa Ulinzi katika mgodi wa Buzwagi Allan Bunyan (kulia) na Meneja Ulinzi katika mgodi wa Buzwagi Gordon Surgeon wakifurahia jambo katika ukumbi wa Umoja wakati wa Tamasha la ajira



Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

SHONZA AFUNGA MASHINDANO YA MICHEZO YA VYUO VIKUU LEO UDOM MJINI DODOMA

0
0
 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana shonza akijiandaa kufunga kikapu wakati wa kufunga mashindano ya Michezo ya Vyuo Vikuu yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Dodoma mjini Dodoma leo.
.Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akikagua timu ya mpira wa pete ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) wakati wa fainali za Michezo ya Vyuo Vikuu Mjini Dodoma Leo..

SHIRIKA LA POSTA TANZANIA (TPC) LAZINDUA NEMBO YAKE MPYA JIJINI DAR ES SALAAM

0
0
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo (kulia) na Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe (kushoto), wakipiga makofi mara baada ya Naibu waziri kuizindua nembo hiyo (mbele yao), jijini Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (katikati), akimpongeza Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe (kushoto), baada ya kuizindua nembo hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa akilijaribu moja ya mabasi 3 wakati akiyazindua katika hafla hiyo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa, akipatiwa maelezo na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo, kuhusu magari madogo 5 ya usafirishaji wa mifuko ya barua na vifurushi, katika uzinduzi huo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakiburudika kwa kucheza ngoma za Mjomba Band, katika uzinduzi huo.
Baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari, wakiwa kazini kuchukua matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka katika uzinduzi huo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakifurahia jambo katika uzinduzi huo.
Miongoni mwa wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), waliokuwepo katika uzinduzi wa nembo mpya wakiionesha nembo hiyo, mara baada ya kuzinduliwa na Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa, jijini Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa, akitoa hotuba yake katika uzinduzi huo, leo jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Bi. Khadija Khamis Shaaban, akizungumza wakati akimshukuru Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa, kwa hotuba yake aliyoitoa.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (wa pili kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Haruni Kondo (kushoto), wakijumuika pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa shirika hilo katika kucheza wimbo maalum wa shirika katika uzinduzi huo. 
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa, akiwapungia wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakati akiwaaga, akiondoka katika hafla hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Haruni Kondo
Baadhi ya viongozi wa Idara za Shirika la Posta Tanzania, wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa Nembo mpya ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo, ambapo Mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo (kushoto) akiwa na Kaimu Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe, wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitendelea katika hafla ya uzinduzi wa Nembo mpya ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo.
Msanii Mrisho Mpoto (katikati), akiwa na baadhi ya wasanii wa bendi yake ya Mjomba Band wakitumbuiza katika hafla ya uzinduzi wa Nembo mpya ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), jijini Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), mh.Elias Kwandikwa (kushoto), akisalimiana na kukaribishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo, alipowasili tayari kwa uzinduzi wa Nembo mpya ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo, ambapo. Wa pili kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Elia Madulesi (katikati) na wa pili kushoto ni Afisa Uhusiano Mwandamizi wa TPC, Joseph Ngowi.
Baadhi ya magari mapya ya usafirishaji wa mifuko ya barua na vifurushi, yakiwa tayari kwa uzinduzi katika hafla hiyo.
Baadhi ya Malori ya kubebea mizigo na vifurushi yakiwa katika viwanja vya Posta tayari kwa uzinduzi katika hafla ya uzinduzi wa nembo mpya ya shirika hilo, jijini leo. Pia kulikuwepo na mabasi 3 mapya ya kubebea abiria, mifuko ya barua na vifurushi yatakayotumika kwenye njia ya Makambako-Songea na Masasi-Mtwara katika uzinduzi huo.
Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (kulia), akiteta na kufurahia jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo, katika uzinduzi wa Nembo mpya ya Shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo.
Kaimu Postamasta Mkuu wa TPC, Hassan Mwang'ombe, akizungumza mbele ya Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (kulia), wakati akitoa maelezo machache kuhusu Shirika hilo. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania, Dk. Haruni Kondo, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (kulia), kuzindua nembo mpya ya shirika na kutoa hotuba yake.

NBS Wachukulieni Hatua Wanaotoa Takwimu za Uongo-Dkt Magufuli

0
0

MBULU WAMPONGEZA KAMOGA KWA KUFANIKISHA MAENDELEO

0
0
Wakazi wa Kata ya Masieda Wilaya yards Mbulu Mkoani Manyara, wamemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Hudson Kamoga kwa jitihada zake binafsi zilizofanikisha kupata ufadhili wa kumalizia madarasa ya shule ya msingi Umbur. 

Ofisa mtendaji wa Kijiji cha Masieda Yasenti Lazaro akizungumza wakati Kamoga akizindua madarasa matatu ya shule hiyo alisema wananchi wa eneo hilo wanashukuru kwa kuwezesha umaliziaji wa jengo la darasa la shule hiyo. 

Lazaro alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2014 na kusajiliwa mwaka 2015 ina wanafunzi 335 na vyumba vinne vya madarasa. Alisema bado wanakabiliwa na upungufu wa vyumba vitatu vya madarasa na nyumba za walimu kwani hivi sasa kuna nyumba moja pekee ya walimu wanne waliopo shuleni hapo. 

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Masieda, Nicomed Nada ameshukuru Rais John Magufuli kumteua Kamoga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwani anawatumikia wananchi kwa kuacha alama ya maendeleo. Nada alisema Kamoga ni mbunifu kwenye suala la maendeleo na amekuwa akipigania vipaumbele vya wananchi wa wilaya hiyo kwenye elimu, afya na maji. 

Alisema Kamoga ni mbunifu wa maendeleo kwani alifika kwenye shule hiyo na kubaini tatizo la ukosefu wa madarasa, akazungumza na wadau wa maendeleo waliowezesha jambo hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Hudson Kamoga alisema baada ya kutembelea shule hiyo na kubaini changamoto ya darasa, wakati Halmashauri haikuwa na fungu la kulimaliza, alizungumza na mdau wa maendeleo waliyejitoa sh10 milioni, kwa ajili ya kumalizia ujenzi huo. 

Kamoga alisema baada ya kuzungumza na wadau wa maendeleo, wakawezesha fedha hizo na kufanikisha ujenzi huo wa darasa, ambapo sh7 milioni zilimalizia ujenzi huo na sh3 milioni zikatumika kwenye utafiti wa maji wa Kijiji vya Mamagi na Genda. Aliwapongeza wananchi wa kijiji hicho kwa kufanikisha upatikanaji wa matofali 60 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa mengine ya shule hiyo. 

“Kuhusu changamoto ya upungufu wa madarasa mengine msiwe na shaka ninyi anzeni kisha tutawaunga mkono kama awali kwani kwenye hayo madarasa mengine mlitumia nguvu zenu kisha tutasaidiana pamoja,” alisema Kamoga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akipokea zawadi ya mbuzi baada ya wananchi wa Kijiji cha Masieda kumpatia kama shukrani ya kuwezesha umaliziaji wa jengo la darasa la shule ya msingi Umbur ambapo aliwapa shilingi milioni saba alizopata kwa wadau ambapo kati ya shilingi milioni 10 alizozipata saba alitoa kwa shule hiyo na nyingine milioni tatu zikapelekwa kwenye vijiji vya Mamagi na Genda ili kufanya utafiti wa upatikanaji wa maji. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga akizindua madarasa matatu ya shule ya msingi Umbur, ambapo moja kati ya madarasa hayo alimalizia ujenzi wake kwa kutumia fedha alizozipata kwa wadau wa maendeleo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuari ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Starnley Kamoga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Masieda.
Mzee wa jamii ya wairaq John Tluway wa Kijiji cha Masieda Wilayani Mbulu Mkoani Manyara akimpa zawadi ya majani, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Hudson Kamoga baada ya kuzindua madarasa matatu ya shule ya msingi Umbur.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Starnley Kamoga akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Masieda.

DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE

0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kuchanganya mchanga wa kutengeneza zege kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao katika wilaya ya Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kutengeneza tofali wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Bibi.Sihaba Nkinga akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akizungumza na wananchi wa kijiji cha wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Wananchi wa kijiji cha Chambasi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao wakati Naibu Waziri huyo aliposhiriki ujenzi wa madarasa ya shule ya Msingi Chambuso wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akifurahi pamoja na wananchi wa kijiji chaChambasi mara baada ya kushiriki ujenzi wa shule ya msingi Chambasi wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao wilayani Kisarawe.Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW



Na Kitengo cha Mawailiano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile ameshiriki kazi ya ujenzi wa shule ya msingi Chambasi Wilayani Kisarawe ikiwa ni zoezi la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo Dk. Ndugulile amesema kuwa kwa kipindi kirefu dhana ya wananchi kujitolea katika kufanya kazi za maendeleo imepungua kwa kiasi kikubwa na kuiachia Serikali ikitoa kila kitu kutekeleza miradi ya maendeleo hata kama inawezekana kazi hizo kutekelezwa na wananchi.

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa kwa kipindi cha sasa cha Serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa kazi tu wananchi hawana budi kujitoa katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneno hayo ili kuisaidia Serikali na kujisaidia wao wenyewe kujiletea maendeleo.

“Msisubiri kila kitu kifanywe na Serikali vingine mnaweza kufanya weneyewe hongereni sana ninyi ni mfano wa kuigwa kwa vijiji vingine katika hili” alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Chambasi Bi. Fodia Makebu Tungaraza amesema kuwa mradi huo wa ujenzi wa shule umeibuliwa na wananchi wenyewe mara baada ya watoto wao kutembea umbali mrefu kwenda kijiji cha jirani kuifata shule ya Msingi Msimbu takribani kilomita sita hivyo kuhatarisha maisha na usalama wa wanafunzi hao.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msimbu Bw. Hussein Mkambara ambae pia anayesimamia shule ya Chambasi hadi itakapopata usajili ameishukuru Serikali kwa kuona na kuwaunga mkono katika jiitihada za kujikwamua katika changamoto waliyokuwa nayo kwa kipindi kirefu.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile amefanya ziara ya siku moja mkoani Pwani wilaya ya Kisarawe kwa kushiriki ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Chambasi, kuvitembelea vikundi vya wanawake vinavyojishughulisha na biashara na viwanda vidogo vidogo vinaowezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na kutembelea Mahakama inayohusika na mashauri ya watoto wilayani Kisarawe.

NEC YATOA MAJIBU VYAMA VYA SIASA KUJITOA UCHAGUZI MDOGO

0
0
Viewing all 46206 articles
Browse latest View live




Latest Images