Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

TATU MZUKA YAWATUNUKU WASHINDI WA WAWILI WA SH. MILIONI 10

$
0
0
Mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka umetoa  washindi wa wawili wa sh. Milioni  10  katika droo maalumu ya mwisho wa mwaka ili kuwapa wachezaji wa droo hiyo kufurahia sikukuu za mwisho wa mwaka .

Akizungumza na waandishi habari wakati wa kukabidhi hundi hizo  kwa washindi hao , Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba amesema droo hiyo inachezwa majira ya saa tatu na nusu usiku ambayo inakwenda hadi mwishoni wa mwaka.

Kemi amesema  kuwa washindi wote waliopewa hundi ni kutokana na kushinda mchezo huo kwa kufuata taratibu zilizowekwa za  mchezo,Amesema Watanzania waendelee kuchangamkia fursa ya mchezo huo na kuibuka washindi na kufurahi  msimu wa sikukuuu na ziku zinazoendelea.

Kemi amesema kuwa droo ya walioshinda ni maalumu na wakiona umuhimu wataweza kuitumia na droo zingine zikiendelea.Mshindi wa Tatu Mzuka wa Sh.milioni 10, Samson Mwamwenda amesema  hakuamini kama ameshinda kutokana na kusikia watu wanashinda.

Amesema kuwa amecheza kwa wiki mbili akipata sh.2000  na mara ya mwisho akapata sh.10,000 lakini ameweza kushinda milioni 10.
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Samson Mwamwenda,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
 Afisa Habari wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Godfrey Madeje,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .


RC MBEYA MHE. AMOS MAKALA AFUNGUA MAFUNZO YA MADAKTARI WA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI YANAYORATIBIWA NA WCF

$
0
0



NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mbeya

TAKRIBAN madaktari na watoa huduma za afya 100 kutoka mikoa saba ya Kanada ya Nyanda za Juu Kusini, wameanza kupatiwa mafunzo jijini Mbeya yanayoratibiwa na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF).

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa mafunzo hayo ya siku tano yaliyofunguliwa rasmi Desemba 12, 2017 (jana) NA Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makala kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa jijini Mbeya, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw.Masha Mshomba, alisema, mafunzo hayo ni muendelezo wa mafunzo kwa madaktari na watoa huduma za afya ili kuwajengea uwezo wa kufanya tathmini ya ulemavu maradhi anayopata mfanyakazi wakati akitekeleza majukumu yake mahala pa kazi ili hatimaye madaktari hao waweze kutoa mapendekezo kuwezesha mfuko kutoa mafao ya fidia stahiki.

Kwa mujibu wa mratibu wa mafunzo hayo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar, mafunzo hayo yamewaleta pamoja madaktari na watoa huduma za afya kutoka mikoa ya Mbeya, Songwe, Katavi, Rukwa, Iringa, Njombe na Ruvuma.

Katika hatua ya kuimarisha Hifadhi ya Jamii, Tanzania, Serikali ilianzisha Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi kwa mujibu wa kifungu namba 5 cha sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, kipengele cha 263 kilichofanyiwa marejeo mwaka 2015 ili kuhakikisha kila mfanyakazi Tanzania Bara kutoka sekta ya umma na binafsi anapata fursa ya kuwekewa bima na mwajiri wake ili anapopata majeraha au magonjwa awapo kazini basi aweze kufidiwa kwa mujibu wa sheria, alisema Bw. Mshomba.

“Lengo kuu la kuanzishwa kwa Mfuko huu ni kutoa fidia stahiki kwa mfanyakazi aliyepatwa na majeraha, maradhi kutokana na kutekeleza wajibu wake awapo kazini, lakini pia kuwalipa fidia wategemezi wake anapofariki katika mazingira hayo.” Alifafanua Bw. Mshomba na kuongeza, WCF ilianza kutekeleza majukumu yake Julai Mosi, 2015 na mwaka uliofuata Mfuko ulianza rasmi kupokea madai ya fidia na kulipa mafao kwa waathirika.

Wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Wadau wa WCF jijini Arusha mwishoni mwa mwezi uliopita, kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Vijana, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, aliitaka WCF kuendelea kutoa elimu kwa wadau, ili waweze kuelewa vema shughuli za Mfuko na nia njema ya serikali ya kuanzisha mfuko huo ili mfanyakazi wa Tanzania aweze kupata fidia stahiki anapopata madhara sehemu ya kazi.

Bw, Mshomba aliishukuru Serikali na Wizara zake kwa kuunga mkono na kusaidia juhudi za WCF katika kuimarisha mifumo yake ili kutoa huduma bora kwa wadau wake.“Pia napenda nizishukuru taasisi za Hospitali ya Taifa Muhimbili, MOI, Ocea Road Hospital, MUHAS, na OSHA kwa kuwaruhusu wataalamu wake ili tuwatumie katika kutoa mafunzo haya.” Alisema.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Amos Makala ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo, alisema, juhudi za ushirikiano wa pamoja miongoni mwa wadau yaani Serikali, Wafanyakazi, Waajiri unahitajika sana kuhakikisha tathmini endelevu ili kuimarisha mfuko. 

“Nimeambiwa mafunzo haya yataongeza uelewa katika kufanya tathmini na uchunguzi wa majeraha au maradhi anayoyapata mfanyakazi mahala pa kazi na kutoa mapendekezo stahiki kwa uamuzi wa mwisho.” Mkuu wa Mkoa pia alipongeza juhudi za WCF kwa kuendesha mafunzo hayo ambayo yatawezesha kupanua wigo wa mtandao wa watoa huduma za afya na hospitali 

“Katika mwaka wa fedha wa 2015/2016 naambiwa mlianza kutoa mafunzo kwa madaktari na watoa huduma za afya wapatao 359, katika wailaya zote za Tanzania Bara mafunzo mliyoyaendesha katika kanda nne za Pwani, kanda ya Ziwa, kanda ya Kaskazini, na Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na mwaka uliofuata mkatoa mafunzo kwa madaktari wapatao 145 katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza na kufanya idadi ya jumla hadi sasa ya madaktari na watoa huduma za afya ambao mmewapatia mafunzo kufikia 504, napenda kuipongeza Bodi ya Wadhamini na uongozi wa Mfuko kwa kazi nzuri mnayofanya.” Alimaliza Mkuu wa Mkoa Bw. Amos Makala. 

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makala, akihutubia wakati akifungua rasmi mafunzo ya siku tano kwa madaktari wanaofikia 100 kutoka mikoa saba ya kanda ya nyanda za juu Kusini, kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa, jijini humo Desemba 12, 2017. Mafunzo hayo yanayoratibiwa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), yanalenga kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kufanya tahmini ya mfanyakazi aliyepata ulemavu au ugonjwa mahali pa kazi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfukom wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akitoa hotuba ya ukaribisho kweye ufunguzi rasmi wa mafunzo ya siku tano kwa madaktari wanaofikia 100 kutoka mikoa saba ya kanda ya nyanda za juu Kusini, kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa, jijini humo Desemba 12, 2017. Mafunzo hayo yanayoratibiwa na WCF, yanalenga kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kufanya tahmini ya mfanyakazi aliyepata ulemavu au ugonjwa mahali pa kazi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makala, na Mkurugenzi wa Tiba na Tathmini wa Mfuko huo, Dkt. Abdulsalaam Omar.
Washiriki wakifuatilia hotuba kwa umakini.
Washiriki wakifuatilia hotuba kwa umakini.
Washiriki wakifuatilia hotuba kwa umakini.
Mshiriki akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Mshiriki akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Dkt. Ali Mtulia(kushoto) kutoka WCF, na wawezeshaji wakifuatilia hotuba hiyo.
Washiriki wakifuatilia hotuba kwa umakini.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano WCF, Bi. Laura Kungenge, akiwa makini kufuatilia hotuba.
Sekretariat ya WCF ikiwa kwenye majadiliano ili kuhakikisha mafunzo yanakwenda kwa ufasaha. Kutoka kushoto ni Dkt. Pascal Magesa, Bw.Vincent Steven, Bi. Laura Kunenge, na Bi.Innocencia William.
Afisa Kazi Mkoa wa Mbeya, Bi. Mary Patrick Mwansisya (kulia na maafisa wengine wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa Mkoa.
Bw. Mshomba akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala wakati akihutubia madaktari.
Mhe. Makala, akionyesha kitu, akiwa Bw. Mshomba
Picha ya pamoja kundi la kwanza
Picha ya pamoja kundi la kwanza
Picha ya pamoja kundi la kwanza
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Amos Makala, (kushoto), akipongezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, (kushoto) mara baada ya kutoa hotuba yake ya ufunguzi rasmi wa mafunzo ya siku tano kwa madaktari wanaofikia 100 kutoka mikoa saba ya kanda ya nyanda za juu Kusini, kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa, jijini humo jana (Desemba 12, 2017). Mafunzo hayo yanayoratibiwa na WCF yanalenga kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kufanya tahmini ya mfanyakazi aliyepata ulemavu au ugonjwa mahali npa kazi. Mafunzo hayo yanafanyika jijini Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Amos Makala, (kulia), akiongozana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, 9WCF), Bw. Masha Mshomba, baada ya ufunguzi rasmoi wa mafunzo ya siku tano kwa madaktari wanaofikia 100 kutka mikoa saba ya kanda ya nyanda za juu Kusini, kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa, jijini humo. Mafunzo hayo yanayoratibiwa na WCF yanalenga kuwajengea uwezo madaktari na watoa huduma za afya kufanya tahmini ya mfanyakazi aliyepata ulemavu unaotokana na ajali au magonjwa mahala pa kazi

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHUDHURIA MKUTANO MKUU WA TISA WA UMOJA WA WAZAZI TANZANIA - MJINI DODOMA

$
0
0
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM, Phillip Mangula wakati alipohudhuria katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Wazazi Tanzania kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma Desemba 12, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo wakati alipohudhuria katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Wazazi Tanzania kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma Desemba 12, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana wakati alipohudhuria katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Wazazi Tanzania kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma Desemba 12, 2017. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, Rodrick Mpogolo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MKUU WA JESHI LA POLISI IGP SIRRO AAGANA NA MAAFISA NA ASKARI MKOANI TABORA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE.

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro akiaga vingozi wa Jeshi la Polisi mkoani Tabora baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani humo.  Picha na Jeshi la Polisi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (katikati) kushoto kwake ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora SACP, Willprod Mtafugwa wakiwa katika  picha ya pamoja na kikosi cha kupambana wahalifu Mkoa wa Tabora.  Picha na Jeshi la Polisi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro katikati akiwa katika picha ya pamoja na Askari wa kike wa Jeshi la Polisi kikosi cha kupambana na uhalifu Mkoa  wa Tabora.  Picha na Jeshi la Polisi.

KIKAO CHA KUJADILI HALI YA USALAMA BARABARANI NCHINI CHAFANA MJINI DODOMA

$
0
0
Na WAMJW - Dodoma 

Madereva nchini wamepongezwa kwa kuanza kubadilika na kutii sheria bila shuruti katika kukabiliana na ajali za barabarani na hivyo kupungua kwa ajali pamoja na vifo vitokanavyo na ajali kwa uendeshaji unaofuata taratibu na sheria za barabarani.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kikosi cha Barabarani Tanzania  Fotunatus Mselemu –Kamishana Msaidizi Mwandamizi wa Polisi(SACP) wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa kupokea maoni ya sheria kuhusu ajali za barabarani  unaojumlisha mashirika yasiyo ya Kiserikali 
Kamanda Mselemu alisema tatizo la ajali barabarani bado ni kubwa kwani watu wengi wanafariki na kujeruhiwa kutokana na ajali barabarani”sisi sote  ni wahanga wa usalama barabarani hivyo hatuna budi  wadau wote kushirikiana katika kukabiliana na suala hili  na kila mmoja anayo nafasi ya kuchangia ili usalama wa barabarani uimarike  na kuboreka zaidi”Alisema.

Alisema hivi sasa watu wengi wameanza kubadilika hususan madereva wengi ambapo kuna wakati inabidi jeshi la polisi kutumia nguvu nyingi ili kuweza kuepuka ajali zinazoweza kuepukika na nguvu hizi zimetumika kwa nia nzuri ili watanzania kuwa salama wanapotumia vyombo vya moto
Akitolea mfano kwa hali ya usalama barabarani kwa siku ya jana (juzi) nchi nzima kulikua na ajali nne ambazo zimesababisha vifi viwili na majeruhi nne,hivyo ni hatua nzuri.

Hata hivyo aliwataka wadau hao kuhakikisha wanatoa maoni mazuri ambayo yatasaidia kupata sheria ambayo haitamkandamiza mwananchi na ambayo itakua salanma na kupunguza ajali za barabarani nchini na kuwa na sheria inayotekeklezeka kwa kupunguza ajali kwa asilimia 50 kama
“Serikali ya awamu ya tano inapenda kulinda maisha ya watanzania,serikali inatengeneza uchumi wa kati  na viwanda kwa kuboresha miundombinu ikiwemo barabasha hivyo jukumu letu kushirikiana na serikali kuilinda  miundombinu yote inayotengenezwa”

Aidha,Kamanda Mselemu aliwataka wananchi waondoe dhana kwamba ajali zinatokana na nmapenzi ya Mungu “hii siyo kweli ila matatizo yote ya ajali ni sisi wenyewe tunasababisha kutokana na mwendo kasi na kutotii sheria za barabarani.

Alitaja takwimu za ajali barabarani kwa Tanzania kwa mwezi Julai hadi Septemba mwaka 2016 ilikua 639, vifo 923 na majeruhi 2,469 na kwa mwaka 2017 kuanzia Julai hadi Septemba ajali za barabarani zilikuwa 1,376, vifo 655 pamoja na majeruhi 1,469.

Naye  Mwakilishi toka shirika la Afya Dunia  Mery Kessy alisema zaidi ya asilimia 90 za ajali zinazotokea katika nchi zinazoendelea ingawa ni asilimia 10 tu nchi hizo  zinamiliki vyombo vya moto na hiyo ni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo miundombinu,mazingira pamoja na tabia.

Alisema wahanga wakubwa wanaopata ajali na vifo ni  vijana kati ya miaka miaka 15 mpaka 29 kwani umri huu wanakuwa kwenye hatari kubwa ya kusababisha ajali na hivyo ajali hizo kuchukua zaidi ya asilimia 3 za pato la Taifa kwani serikali inaingia gharama kubwa kutibu majeruhi katika sekta ya afya.
 Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu aliyesimama akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.
 Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Bi. Mary Kessy akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.
 ASP Deus Sokoni wa kwanza kulia akiongea na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma, wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Wizara ya Mambo ya Ndani  Bi. Marlin Komba  anayefuata ni Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu.
 Katibu Mkuu wa Shirikishi wa vyama vya Walemu nchini Bw. Felicina Mkude aliyesimama akiongea na baadhi ya wadau mbalimbali wa usalama barabarani  hawapo pichani wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.
 Baadhi  ya wadau mbalimbali wa usalama barabarani  wakimsikiliza kwa makini Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu hayupo pichani  wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.
Kamanda wa Kikosi Cha Usalama Barabarani Nchini SACP Fortunatus Musilimu katikati waliokaa akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa usalama barabarani  wakati wa kikao cha kujadili hali ya usalama barabarani nchini kilichofanyika leo mjini Dodoma.

Mohammed Enterprises yashinda tuzo nne za ATE 2017

$
0
0
Kampuni ya Mohammed Enterprises (MeTL Group) imeshinda tuzo nne za Mwajiri Bora wa Mwaka 2017 (EYA) zinazotolewa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), katika hafla ya iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam. MeTL imeshinda tuzo hizo kupitia kampuni zake tanzu ambazo ni Mo Assurance Limited iliyoshinda kipengele cha Tuzo ya Kampuni Ndogo, 21st Century Holding Limited imeshinda nafasi ya pili ya Tuzo ya Mwajiri Bora wa Ndani na Star Oil Tanzania Limited imeshinda tuzo mbili, Tuzo ya Kampuni ya Kati na nafasi ya tatu ya Tuzo ya Mwajiri Bora wa Ndani. Ushindi huo wa tuzo nne, umeiwezesha MeTL Group kuwa moja ya kampuni nne ambazo zimeshinda tuzo nyingi za ATE 2017, na kuwa kampuni ya kizalendo ambayo imeshinda tuzo nyingi kuliko kampuni zingine ambazo zimeshiriki katika tuzo hizo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya Royal Soap, Jackline Mbaga, Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya Star Oil Tanzania Limited , Ester Dotto, Meneja Mkuu wa Mo Assurance Limited, Kura Bonniface, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Mohammed Enterprises, Hassan Dewji, Meneja Mauzo na Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya 21st Century Holding Limited, David Mziray, Ofisa wa kitengo cha Rasilimali Watu wa Mohammed Enterprises, Jessica Julius, Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya 21st Century Textiles, Godfrey Ndimbo na Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu wa kampuni ya 21st Century Food and Packaging, Anna Zongo wakiwa na tuzo nne ambazo wameshinda kwenye tuzo za ATE 2017.

Akizungumza kuhusu ushindi huo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa MeTL Group, Hassan Dewji, alisema wamefurahishwa na ushindi huo, lakini pia unaonyesha jinsi gani kampuni inafanya vizuri katika soko la hapa nchini. "Tuna furaha kushiriki kwenye tuzo za ATE 2017 na tuna furaha kushinda tuzo nne, naamini tumekuwa moja ya kampuni tano ambazo zimeshinda tuzo nyingi. Nafikiri sisi ni moja ya kampuni kubwa nchini na tunaendelea kukua na kugusa maisha ya watu wengi kila siku, ushindi kama huu utuwezesha kuongeza juhudi zaidi," alisema Dewji.

NEC yawajibu UKAWA

$
0
0
Na Mwandishi Maalum
MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Kailima Ramadhani alisema chama cha siasa kutangaza kugomea kushiriki uchaguzi hakuwezi kuifanya tume ihahirishe uchaguzi kwani tume haiko kumshawishi mtu au chama kushiriki uchaguzi.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Ramadhani alisema chama kushiriki uchaguzi ni jambo la hiyari na tume ya uchaguzi iko pale kwa ajili  ya kuweka na kutengeza mazingira yatakayofanya vyama vya siasa kushirki uchaguzi.

Alisema iwapo kuna chama kitaamua kutoshiriki uchaguzi, chama kitakachoshiriki hata kama ni mmoja mgombea wake atapita bila kupingwa.  Alisistiza kuwa hakuna sehemu yoyote ya katiba na sheria ya uchaguzi inayotamka kwamba chama kisiposhiriki uchaguzi basi uchaguzi unaahirishwa. 

“Ila ikitokea vyama vikasusa vyote kushiriki kwenye uchaguzi hapo ndipo unaweza kuahirishwa kwa kuwa hakutakuwa na mgombea,”alifafanua mkurugenzi wakati alipokuwa anazungumza na baadhi ya waandishi wa habari ambao walitaka kupata ufafanuzi wa tume kuhusu tamko lililotolewea na mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe.

Hivyo ameviasa vyama vya siasa vinavyotishia kutoshiriki kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika majimbo matatu na kata sita kufuata mifumo ya kisheria ya kushughulikia malalamiko ya uchaguzi.

Aliitaja mifumo hiyo kuwa ni kuwasilisha malalamiko kwenye kamati ya maadili wakati wa kampeni,  wakati wa kuanza kupiga kura wakala akiwa na malalamiko anajaza fomu namba 14 na fomu namba 16 wakati upigaji kura unapoeendelea  na kama mgombea hakuridhikai anaruhusiwa kwenda mahakamani.

Juzi Mbowe  alitishia kuwa vyama vinavyounda umoja wa katiba (UKAWA) havitashiriki uchaguzi iwapo changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 zisipofanyiwa kazi na NEC.

Akizungumzia hoja hiyo Ramadhani alisema kwamba katika orodha ya vyama vilivyopo NEC, Ukawa sio moja ya vyama vya siasa na akaongeza kuwa kushiriki kwenye uchaguzi ni hiyari ya chama cha siasa.

“Niwasihi vyama vya siasa watumie mifumo iliyopo ya kawaida ya kuwasilisha malalamiko yao, kwenye kamati za maadili, kujaza fomu namba 14 kabla ya kura kuanza kupigwa, fomu 16 wakati kura zinapigwa na kuwasilisha malalamiko mahakamani baada ya kura kuhesabiwa,”alisema Kailima.

Aliseima hiyo ndio mifumo iliyowekwa kisheria katika kushughulikia changamoto za  uchaguzi zinapojitokeza, “Je hiyo mifumo wanayotaka wao ni ipi?  Kama kama kuna mgombea hakuridhika mahakama zipo aende maana wamepewa siku 30 za kufungua kesi.”

Alisema NEC haiwezi kuahirisha uchaguzi kwani sheria inatamka kuwa uchaguzi unaweza kuahirishwa iwapo tu kuna mgombea amefariki, kutokuwepo mgombea, zikitokea ghasia na fujo au wagombea wakifungana kwa kura.

“Je kuna mgombea amefariki? Haya mambo yote manne hayajatokea, sasa tutaahirishaje uchaguzi? Alihoji Ramadhani na akavitaka vyama vya siasa kutumia mifumo iliyopo kuwasilisha malalamiko yao

Akizungumzia kuhusu jimbo la Longido ambalo Mbowe alidai kuwa shauri la uchaguzi bado liko mahakamani na kwamba wameiandikia NEC kuhusu suala hilo na hawajajibiwa barua yao, Ramadhani alisema madai hayo sio ya kweli kwani barua zote walizoandikiwa wamezijibu.

Alisema jimbo hilo liko wazi kwa kuwa mahakama ndio imeiandikia NEC kuitaarifu kumalizika kwa kesi iliyokuwepo mahakamani. Alisema kwamba NEC itasimamisha uchaguzi wa jimbo hilo iwapo tu wataambiwa na mahakama kusimamisha mchakato huo.

“Nimesikitishwa na kauli kwamba eti wametuandikia barua sisi tume ya kusimamisha uchaguzi wa Longido eti hatujawajibu, tulipata barua kutoka kwa ole Nangole (Onesmo) tukamjibu, tukapata barua kwa wakili wa Ole Nangole nikamjibu, tukapata barua kutoka kwa katibu wa Chadema tukamjibu na nikaongea naye kwenye simu, sasa aleo wanaposema kwamba hatujawajibu kwa kweli kauli hiyo imenisikitisha sana,”alisema Ramadhani.

MWENYEKITI WA CCM RAIS DKT MAGUFUGULI AFUNGUA MKUTANO WA JUMUIYA YA WAZAZI MJINI DODOMA LEO

$
0
0

 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017. 
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mhe. Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Mhe. Maalim Seif wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
 Wajumbe wakimshangilia Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
  Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mama Maria Nyerere na Mama Fatma Karume wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na  Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Brigedia Generali John Julius Mbungo wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa kaongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi aliyemaliza muda wake Alhaj Abdallah Majura Bulembo (kushoto) na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na viongozi wengine baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Ndg. Kheri James baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
Wake wa viongozi kutoka kushoto Mama Janeth Magufuli, Mama Maria Nyerere, Mama Mary Majaliwa na Mama Bulembo wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017. 
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahmana Kinana akiwa na Mama Maria Nyerere muda mfupi kabla ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tisa wa Jumuiya ya Wazazi katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.
 Mwenyekiti wa CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimpatia zawadi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi aliyemaliza muda wake Alhaj Abdallah Majura Bulembo wakati wa ufunguzi wa  Mkutano Mkuu wa Jumuiya hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma leo Desemba 12, 2017.

PICHA NA IKULU

NAISINYAI YANYAKUA UBINGWA WA TAKUKURU SIMANJIRO

$
0
0
Na Woinde Shizza,Simanjiro.

Timu ya jamii ya wafugaji wa Naisinyai S. C ya Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, imeshinda ngao ya maadili iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa kuifunga Mirerani SC kwa penalti 6-5.

Katika mchezo huo wa fainali uliochezwa juzi kwenye uwanja wa barafu mji mdogo wa Mirerani, mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Zuwena Omary. Hadi dakika 90 ya mchezo ulipomalizika timu hizo zilikuwa hazijafungana na walipopigiana penalti tano kwa tano hakukuwa na mshindi ndipo wakapigiana penalti moja kwa moja na Naisinyai ikashinda. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi ngao hiyo ya maadili kwa timu ya Naisinyai,Katibu Tawala Omary alisema jamii inapaswa kupiga vita matumizi ya vitendo vya rushwa kwa kila sehemu. Alisema jamii inapaswa kuzingatia hilo kupitia kauli mbiu ya wajibika, piga vita rushwa, zingatia maadili, haki za binadamu na utawala bora kuelekea uchumi wa kati. 

"Tupige vita rushwa kila mahali, kuanzia michezo ni, makazini, polisi, hospitalini, mahakamani na kila eneo ukiona rushwa inatumika toeni taarifa," alisema Omary. Mkuu wa Takukuru wilaya ya Simanjiro Mashauri Elisante alisema mashindano hayo yalishirikisha timu nne za Naisinyai SC, Mirerani SC, Veterani Mirerani za Simanjiro na Tanzanite FC ya wilaya ya Arumeru mkoani Arusha. 

Alisema lengo la mashindano hayo ni maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu kitaifa na kupiga vita vitendo vya rushwa. Mwenyekiti wa Kijiji cha Naisinyai, Taiko Laizer alisema hii ni mara ya pili kwa mwaka huu timu hiyo kubeba ubingwa wa soka kwani awali walishinda kombe la mbunge wa jimbo la Simanjiro James Ole Millya. 
Laizer alisema siri ya ushindi mara mbili kwa mwaka mmoja kwenye timu hiyo ni kuzingatia mazoezi, nidhamu na ushirikiano wa uongozi na wananchi kwa ujumla. 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Naisinyai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Taiko Laizer akimbeba golikipa wa Naisinyai SC Joseph John baada ya kunyakua ngao ya Takukuru kwa kuifunga Mirerani SC kwa penalti 6-5
Mwenyekiti wa Kijiji cha Naisinyai Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Taiko Laizer akimbeba golikipa wa Naisinyai SC Joseph John baada ya kunyakua ngao ya Takukuru kwa kuifunga Mirerani SC kwa penalti 6-5

MAKAMU WA CHUO CHA IJA ASHINDA KUKU LUSHOTO KATIKA BONANZA

$
0
0
Nazael Mkumbo Mshindi wa kuku

Makamu Mkuu wa Chuo cha uongozi wa mahakama IJA, Fahamu Mutlya mwishoni mwa wiki alionesha uhodari wa kukimbia baada ya kufanukiwa kumkamata kuku katika bonanza kuadhimisha siku ya uhuru na kufunga mwaka wa 2017lililofanyika katika uwanja wa chuoni hapo.

Mtulya aliweza kuwashinda wengine waliokuwa kwenye kundi la wahadhiri baada ya kuchomoka kwa haraka na kisha kumdaka kuku huyo wakati kundi la uhasibu mshindi alikuwa Noel Njau wakati Barnaba john alishinda kundi la utawala.Mpira wa kikapu watumishi waliweza kuwafunga wanafunzi wa chuoni hapo magoli 12 -8 na mpira wa wavu watumishi walifungwa seti 3-2.

Mwenyekiti wa kamati ya Bonanza hilo,Daudi Hemba alisema lilifanyika kwa lengo la kuwaeka pamoja watumishi na wanafunzi katika kujenga afya zao huku wakitafakari kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo uhuru wa nchi hii.“Bonanza hili limefanyika kwa lengo la kuwaweka pamoja watumishi na wanafunzi lakini pia kujenga afya zao huku wakitafakari kuhusu uhuru”alisema Hemba.

Mkuu wa Chuo cha IJA,Paul Kihwelo aliwataka watumishi kujenga tabia ya kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili kuimarisha afya zao.

“Bila shaka mnafahamu kwamba anayeshiriki michezo si rahisi
kushambuliwa na magonjwa mbalimbali,na ndiyo maana tumeanzisha IJA joging club ambayo watumishi na wanafunzi wanashiriki kila jumamosi”alisema Kihwelo.Katika bonanza hilo pia lilifanyika zoezi la upimaji wa afya ambapo watu 25 waliojitokeza kupima virusi vya ukimiwi walionekana kutokuwa na maambukizi wakati waliopima kisukari (Blood Suger) walikuwa 30 ambao walionekana kuwa ya kawaida.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha
Mr. Fahamu Mtulya Mshindi wa kuku (Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma

Airtel Yaleta ‘SMATIKA Na Yatosha Intaneti’ SMATIKA NA 1GB Siku Tatu Kwa 2000 Tu

$
0
0
Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano – kulia akiongea jana wakati wa uzinduzi wa bando za ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ mpya ambapo mteja wa Airtel itamuwezesha mteja wa Airtel KUSMATIKA NA GB 1 ya Yatosha Intaneti kwa siku tatu mfululizo kwa shilingi elfu mbili. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isack Nchunda.
Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isack Nchunda – kushoto akiongea jana wakati wa uzinduzi wa bando za ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ mpya ambapo mteja wa Airtel itamuwezesha mteja wa Airtel KUSMATIKA NA 1GB ya Yatosha Intaneti kwa siku tatu mfululizo kwa shilingi elfu mbili. Kushoto ni Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano.
Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isack Nchunda na Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano wakionyesha bango baada ya kuzindua bando za ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ mpya ambapo mteja wa Airtel itamuwezesha mteja wa Airtel KUSMATIKA NA 1GB ya Yatosha Intaneti kwa siku tatu mfululizo kwa shilingi elfu mbili.

…………… 
‘SMATIKA NA 1GB Yatosha Intaneti inayokupa muda mrefu kwa gharama nafuu zaidi. 

Airtel Tananzania Mtandao bora kwa Smartphone yako imewapatia wateja wake uhuru zaidi kwa kuwaletea bando mpya za ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ maalum kwa watumiaji wa huduma za intaneti. Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Isack Nchuna wakati wa hafla ya kuzindua ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti, alisema “Airtel itaendelea kuleta huduma zenye ubora na ubunifu wa hali ya juu ili kuendelea kuwa sambamba na mahitaji ya wateja katika huduma za intaneti ambapo kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa Airtel imejiwekea mikakati endelevu mingi ili kukidhi uhitajika na wateja wote”

“Tuaendelea kudhihirisha dhamira yetu ya kutoa suluhisho la mawasiliano kupitia uzinduzi wa ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ kwa kutoa huduma nafuu ya Intaneti kwa watumiaji wote nchini huku tukiweka kipaumbele zaidi katika ubora wa mtandao pamoja na kuwapatia wateja uhuru zaidi” aliongeza Nchunda 

“SMATIKA na Yatosha Intaneti’ ni zawadi ya awali kabisa tunayowapatia watumiaji wa Airtel katika msimu huu wa sikukuu, tunaamini kuwa ndani ya msimu huu wa sikukuu wateja wanauhitaji mkubwa sana wa intaneti katika kukamilisha shamrasharna wakiwa wanawasiliana na ndugu, jamaa na marafiki wakati wote!”

Akifafanua zaidi Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Bi Beatrice Singano alisema Bando za ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ zinatoa uhuru kwa wateja wote wa airtel kujichagulia bando la intaneti KABAMBE wakati wowote.“Mteja wa Airtel ataweza kunufaika na SMATIKA na Yatosha Intaneti kwa gharama nafuu ya hadi shilingi 200 na kujipatia MB 40, vilevlie mteja ataweza KUSMATIKA NA 1GB ya Yatosha Intaneti kwa siku tatu mfululizo kwa shilingi elfu mbili tu” alieleza Bi Singano

“kujiunga na ‘SMATIKA na Yatosha Intaneti’ unatakiwa kupiga *149*99# kisha chagua 5 Yatosha Intanet vilevile unaweza kujiunga kupitia Airtel Money kwa kupiga *150*60# kisha chagua Yatosha Intanet”.

Airtel Tanzania imekuwa katika programu ya uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano yake ili kukamilisha lengo lake la kutoa mawasiliano bora na yenye uhakika kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya U900. Tayari Airtel imezindua maboresho ya mtandao wake kwa kutumia teknolojia hiyo ya U-900 kwenye mikoa ya Arusha, Dar es salaam, Dodoma, Morogoro na Mwanza huku ikiendelea kuwahakikishia wateja wake mawasiliano bora hasa katika maeneo ya nje na ndani ya majengo marefu au yenye uhitaji zaidi.

IGP SIRRO AONGEA NA WANANCHI ALIPOKUWA NJIANI AKITOKEA MKOANI TABORA KWENDA KIGOMA KATIKA ZIARA YAKE

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro akiwagawia mahindi wananchi baada ya kumaliza kusalimiana nao wakati akitokea mkoani Tabora kwenda mkoa wa Kigoma katika ziara ya kikazi.  Picha na Jeshi la Polisi.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro akisalimiana na wananchi wakati akitokea mkoani Tabora kuelekea mkoani kigoma katika ziara yake ya kikazi.  Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP, Simon Sirro akisalimiana na maafisa wa Jeshi la Polisi baada ya kuwasili mkoani Kigoma akitokea mkoani Tabora alipokuwa na ziara ya kikazi ya siku mbili.  Picha na Jeshi la Polisi.

Waziri Mahiga awaasa Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne (4) la Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Wazalendo na kusimamia maslahi ya Jumuiya

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga(katikati) akiongea katika kikao cha uongozi wa Wizara hiyo na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne (4) la Jumuiya ya Afrika Mashariki, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, tarehe 12 Disemba 2017. Pembeni yake kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba na kulia ni Mwenyekiti wa Wabunge wateule wa Bunge la Afika Mashariki, Mhe. Abdullah Makame. 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiongea katika kikao hicho ambapo aliwakaribisha Waheshimiwa Wabunge wateule pamoja na kuwaeleza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ipo tayari kuwapa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao. Pembeni yake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi. 
Mwenyekiti wa Wabunge Wateule wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Abdullah Makame akiushukuru uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kikao kizuri cha utangulizi kabla ya kuanza kwa Bunge hilo na pia akaahidi kuwa wataenda kuliwakilisha Taifa vizuri sambamba na kusimamia maslahi ya Jumuiya kwa maendeleo na ustawi wa wananchi wake. 
Sehemu ya Waheshimiwa Wabunge Wateule wa Bunge la Afrika Mashariki wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na Mhe. Waziri Mahiga (hayupo pichani) 
Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Wabunge wakifuatilia kikao hicho. 
Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao hicho. Kutoka kulia Bw. Eliabi Chodota, Bw. Bernard Haule na Bw.Joachim Otaru
Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Stephen Mbundi akitoa ufafanuzi kuhusiana na taratibu na miongozo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Waheshima Wabunge Wateule. 
Mhe. Waziri na Naibu Waziri wakiwa katika picha ya pamoja na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Picha ya pamoja uongozi wa Wizara na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kaimu Mkurugenzi TAA, Ataka Madereva Wa Magari Ya Zimamoto kuyatunza

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (aliyesimama mbele), akiongea na askari wa zimamoto na uokoaji wa kituo cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA). Mbele kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa JNIA, Bw. Johannes Munanka na (kulia) ni Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji wa Viwanja vya Ndege nchini, Kamishna Msaidizi, Christom Manyologa.DSC_3447
Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka  (aliyesimama mbele) akitoa maelezo mbalimbali kwa askari wa zimamoto na uokoaji katika kikao kilichoitishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela.
DSC_3450
Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji wa Viwanja vya Ndege Tanzania, Kamishna Msaidizi, Christom Manyologa (aliyesimama) akiongea na askari wa kituo cha zimamoto na uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, katika mkutano ulioitishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela.
DSC_3458
Askari Ramadhani Mgogo wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), aliyesimama akichangia masuala mbalimbali kwenye mkutano ulioitishwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (watatu kushoto) katika meza kuu.DSC_3477Kamanda wa Vikosi vya Zimamoto na Uokoaji wa Viwanja vya Ndege, Kamishna Msaidizi, Christom Manyologa (wa pili kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (wapili kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Johannes Munanka (kushoto), wakiwa na msimamizi wa chumba cha Habari na Mawasiliano cha kituo hicho, afande Joines Matucha.
……………..
Na Mwandishi Wetu
KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela  amewataka madereva wanaoendesha magari ya zimamoto na uokoaji kwenye viwanja vyote vya ndege Tanzania kuyathamini na kuyatunza magari hayo kwa kuwa wameaminiwa kufanya kazi hiyo.
Bw. Mayongela alitoa kauli hiyo kwenye Kituo cha Zimamoto na Uokoaji cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), alipokwenda kujitambulisha na kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili, ambapo alisema magari hayo yamenunuliwa kwa gharama kubwa, hivyo yanapaswa kutunzwa.
Alisema uthamini wao kwa magari hayo kutayafanya kudumu na kuyafanya kazi kwa muda mrefu bila kuharibika, jambo ambalo litachangia ufanisi wa kazi, ya uokoaji na usalama kwenye viwanja vya ndege, ambapo mbali na miundombinu pia lazima miundombinu ipewe kipaumbele.
“Najua wapo wenzenu wachache sio waaminifu wamekuwa wakitengeneza manunuzi hewa ya vifaa na hata mafuta kwa manufaa yao binafsi, lakini ninawaomba mujione nyie ndio wenye thamani kwa kuaminiwa kuendesha magari haya ya mamilioni ya fedha, kwani ni nyie tu mnayoweza kuyaendesha kutokana na kuwa na mitambo ya kisasa tofauti kidogo na mengine, hivyo basi tuyatunze ili tuisaidie serikali yetu isiingie gharama za mara kwa mara za kununua vifaa au magari mengine mapya,” alisisitiza Bw. Mayongela.
Hatahivyo, alisema zimamoto ni moja ya mambo ya msingi hivyo amewahakikishia kuwapeleka kozi za mara kwa mara za ndani na nje ya nchi, kutokana na mambo mbalimbali yanayobadilika duniani, na kwa kuanzia ataanza na askari wawili hadi wanne, kulingana na mafunzo wanayostahili kushiriki, na atahakikisha washiriki ndio wanaokwenda kufanyia kazi kwa vitendo katika utendaji wao na sio kupeleka mabosi ambao hawahusiki.
“Nia yangu ni nyie kufanya kazi kwa weledi na kufanyakazi kwa bidii, nisije kusikia hakuna fedha, lakini wakati huo huo mnamuona Mkurugenzi mkuu anapanda ndege kwenda Ulaya na kurudi hizo fedha zinatoka wapi, nasema kama kweli kuna mambo ya msingi basi zimamoto ni jambo la msingi, hivyo basi sisi wafanya maamuzi tunatakiwa kuangalia wanaostahili kupata mafunzo na waende, hivyo nitahakikikisha kwa kadri ya bajeti nitatenga mafungu ya kupeleka watu wangu hawa kwenye mafunzo, ili nao waende na wakati katika endeshaji kulingana na mabadiliko ya teknolojia na mashirika ya usafiri wa anga duniani yanavyoagiza,” alisema Bw. Mayongela.
Hatahivyo, ameahidi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 TAA itanunua magari sita ya zimamoto na uokoaji pamoja na redio zitakazotumika kwa mawasiliano katika chumba cha habari na mawasiliano, kinachowasiliana na mnara wa kuongoza ndege.
Kutokana  na kuharibika kwa mara kwa mara kwa magari ya zimamoto kwenye viwanja vya ndege Tanzania ameahidi kufufua karakana ya kutengeneza magari hayo iliyopo JNIA, ambapo tayari amewaita mafundi waliopo hapo kukutana naye ili kuwasilisha changamoto na vifaa vinavyohusiana na magari hayo, ili waanze kutengeneza kwa haraka baada ya kununuliwa vifaa hivyo.
Pia aliwataka kuwa na ushirikiano wa dhati na wafanyakazi wa TAA katika utendaji wao wa kazi na kuwa walinzi wa mali za serikali kutokana na wao wamekula kiapo.
Naye Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji wa Viwanja vya Ndege Tanzania, Kamishna Msaidizi Christom Manyologa alisema amefarijika kwa ujio wa Kaimu Mkurugenzi wa TAA, Bw. Mayongela,  ambaye ameonesha nia thabiti ya kushirikiana katika kazi.
Kamishna Manyologa alisema askari wa zimamoto na uokoaji , astahili kuheshimika zaidi kwani yeye ndio anayeweza kuingia ndani na kufika karibu ya ndege na pia anayewasiliana na waongoza ndege.
“Huyu askari anastahili kuheshimiwa kwanza anamamlaka makubwa ya kuwa karibu kabisa ya ndege, kupita ndani ya barabara ya kutua na kuruka kwa ndege hivyo anaweza kufanya lolote baya akiamua, hivyo watendewe vizuri,” alisema Kamishna Manyologa.

MSAMA AMSHUKURU RAIS DKT. MAGUFULI KWA UAMUZI WA KUWASAMEHE WASANII BABU SEYA NA PAPII KOCHA

$
0
0
Na Kajunason/MMG. 
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Action Mart, Alex Msama amshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kitendo cha kutoa msamaha kwa wanamuziki maarufu nchini, Papii Nguza (Papii Kocha) na baba yake mzazi, Nguza Viking (Babu Seya) aliyekuwa akitumikia kifungo cha maisha katika gereza la Keko jijini Dar es Salaam.
 
 Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaama, Msama ambaye ni alikuwa ni mjumbe wa Bodi wa BASATA na mpigania haki zawasanii na vile vile ni mlezi wa wasanii mbali mbali amesema jambo alilolifanya ni jema sana na ametekeleza maagizo ya Mungu ambayo anatushauri tusamehe.
 
 "Ukisoma hata kwenye vitabu vya biblia suala la kusamehe alishalisema, katika Mathayo 18:21-22... Ndipo Petro akamjia Yesu na kumwuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?” Yesu akamjibu, ''Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.' alisema Msama. 
 
Msama aliongeza kuwa jambo hilo ni kubwa na halina kipingamizi chochote maana kila kona ya Tanzania maamuzi hayo yamepokelewa kwa mikono miwili. Aliongeza kuwa wafanyabiashara wote wanaofanya kazi za sanaa ni vyema wakafuata taratibu kwa kuuza kazi halali zilizo na stika za TRA ambazo zitawanufaisha wasanii na serikali kwa ujumla. 
 
Hata hivyo, zoezi laukamataji Kazi feki za sanaa litaendelea katika Mkoa wa Morogoro, ikiwa ni zoezi la nchi nzima.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO DECEMBER 13,2017

KUMBE UNGA WA MUHOGO HUTENGENEZEA KIWASHIO MOTO CHA KIBIRITI?!!

$
0
0
Na Richard Mwaikenda, Mkuranga 

UNGA wa muhogo unatumika kutengenezea kishungi cha kuwashia moto katika vibiriti.

Jambo hilo lilithibitishwa na Mkurugenzi wa Kiwanda cha kusaga muhogo cha Ukaya, Mkuranga, Ibrahim mbele ya uongozi wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita) uliotembelea kiwanda hicho.

Alisema kuwa miongoni mwa wateja wakubwa wa unga wao ni Kiwanda cha kutengenezea vibiriti cha Kasuku kinachoutumia kwa kutengenezea kishungi cheusi cha njiti ya kibiriti kinachotumika kuwasha moto.

Uongozi wa Mkikita ulioongozwa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Kissui S. Kissui na Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao huo, Adam Ngamange ulitembelea kiwanda hicho kwa lengo la kuingia nao mkataba wa makubaliano ya kukitumia kusaga mihogo ya wanachama wao kupata unga utakaouzwa na katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Ibrahim alisema unga pia hutumika kutengenezea dawa ya kuzuia kuhara, pombe, mafuta, chakula cha wanyama na binadamu.meandaliwa na Richard Mwaikenda;Kamanda wa Matukio Blog 0715-264202
Uongozi wa Mkikita ukiwa na uongozi wa kiwanda cha Unga cha Ukaya, Mkuranga, Pwani, ulipotembelea kiwanda hicho ambacho wako mbioni kuingia mkataba wa kusaga mihogo ya wanachama wao kupata unga wa kuuza katika masoko ya ndani na nje ya nchi.Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kissui S. Kissui, Mkurugenzi wa Kiwanda, Ibrahim, Meneja wa Kiwanda, Matanga na Mkurugenzi wa Mkikita, Adam Ngamange.

WACHIMBAJI WA JASI WALILIA SOKO LA UHAKIKA

$
0
0
Wachimbaji wa Madini ya Jasi Mkoani Singida wametakiwa kufanya shughuli zao kwa uaminifu ili kujihakikishia soko la uhakika.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo ametoa wito huo Desemba 11, 2017 Wilayani Itigi mara baada ya kuzungumza na Wachimbaji wa madini hayo wakati wa ziara yake kwenye maeneo yenye uchimbaji wa madini ya Jasi Mkoani Singida. 

Wachimbaji wa Madini hayo walimueleza Naibu Waziri Nyongo changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa soko la uhakika.
Mara baada ya wachimbaji hao kuelezea changamoto zinazowakabili, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Itigi, Ali Minja alimueleza Naibu Waziri Nyongo kwamba tatizo la soko la Madini ya Jasi yanayochimbwa Singida linasababishwa na wachimbaji wenyewe kwa kuchanganya madini hayo na udongo.

Alisema wakati mwingine wachimbaji wenyewe wanasababisha kupotea kwa soko, kwani mnunuzi akinunua Madini ya Jasi yaliyochanganywa na udongo hawezi kurudi tena kununua.“Baadhi ya wachimbaji wa Jasi Mkoani hapa sio waaminifu kwani wanachanganya madini na takataka ikiwemo udongo, na hii inakimbiza wanunuzi,” alisema.

Kufuatia hali hiyo, Naibu Waziri Nyongo aliwaasa wachimbaji hao kuwa wakweli kwa kufanya shughuli zao kwa uadilifu na ubunifu mkubwa wa utafutaji wa masoko ili kuvutia wanunuzi wengi zaidi na hivyo kujiongezea kipato. 

Alisema mafanikio hayawezi kupatikana kama wachimbaji watafanya shughuli zao kwa ulaghai na aliwataka kuacha kutafuta mafanikio kwa njia ya mkato ikiwemo hiyo ya kuchanganya Jasi na takataka ambayo alisema imewasababishia kukimbiwa na wanunuzi. 

“Tukitumia madini haya vizuri huku tukiongeza ubunifu, tutafanikiwa kufikia malengo tuliyojiwekea; vinginevyo tutaendelea kulalamika,” alisema.
Aliongeza kwamba Serikali itafanya jitihada za kutangaza Madini ya Jasi yanayochimbwa nchini na kuwataka wachimbaji wa madini hayo kuhakikisha wanazingatia suala la ubora unaotakiwa Kimataifa.
“Ninawahakikishia tutawatafutia soko mahala popote Duniani, ili kuhakikisha mnanufaika na madini haya mnayochimba ila mkumbuke uaminifu ni muhimu,” alisema Naibu Waziri Nyongo. 

Aidha, aliongeza kwamba Serikali inakaribisha wawekezaji wakubwa kuwekeza kwenye biashara ya Madini ya Jasi ikiwemo ujenzi wa viwanda vinavyotumia Madini ya Jasi kama malighafi ya kutengenezea saruji na bidhaa mbalimbali kama mapambo ya majumbani na chaki.

Naibu Waziri Nyongo yupo Mkoani Singida kwa ziara ya siku tatu ya kutembelea shughuli za uchimbaji wa Madini mkoani humo pamoja na kuzungumza na wachimbaji ili kubaini changamoto zinazowakabili kwa lengo la kutafutia ufumbuzi.
 Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Singida, Sosthenes Massola (kushoto) akizungumza na Wafanyakazi, Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini ya Jasi (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia aliyesimama) Mkoani Singida.
 Mkurugenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Mapambo ya majumbani cha RSR kilichopo Singida Mjini, Rashid Rashid (kushoto) akimuonesha Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) baadhi ya bidhaa zinazozalishwa kiwandani hapo zitokanazo na Madini ya Jasi yanayochimbwa Itigi mkoani humo.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (aliyesimama) akizungumza na Wafanyakazi, Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini ya Jasi (hawapo pichani) wakati wa ziara yake Itigi Mkoani Singida. Kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Pius Luhende.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akitembelea Kiwanda cha kutengeneza Chaki cha Furaha, kilichopo katika Kata ya Tambukareli, Itigi. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, Pius Luhende na kushoto ni Meneja wa Kiwanda hicho, Peter Nolasco.
 Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akimsikiliza Meneja wa kiwanda cha kuzalisha Chaki cha Furaha, Peter Nolasco (kushoto). Kutoka kulia ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kati Singida, Sosthenes Massola na Katibu Mkuu wa Chama cha Wachimbaji Madini wa Mkoa wa Singida (SIREMA), Farijala Kiunsi.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akizungumza jambo alipotembelea Kiwanda cha kuzalisha Chaki cha Dobercolor kilichopo katika Kijiji cha Majengo, Itigi. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda hicho.

HOTUBA YA RAIS DKT MAGUFULI UFUNGUZI WA MKUTANO WA 9 WA UMOJA WA WAZAZI WA CCM

OFISI NZIMA YA MKIKITA WAHAMIA SHAMBANI VIKINDU KUPANDA MCHAICHAI

$
0
0

Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kissui S. Kissui wakibeba miche ya mchaichai wakipeleka kupanda shambani Vikindu. Shmba hilo ni la wanachama wa Mkikita. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Adam Ngamange akiwa amebeba mbolea akipeleka shambani.

Na Richard Mwaikenda
OFISI nzima ya Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita/Livinggreen), umehamia shamba Vikindu kuanza kampeni ya kupanda mchaichai.

Katika kampeni hiyo ya aina yake iliwashirikisha wakurugenzi, maofisa na wafanyakazi wa mtandao huo ili kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Back to The Land.

Walipofika Block Farming hiyo ya mchaichai, waligawanyika katika makundi mbalimbali ambapo wengine kazi yao ilikuwa kubeba mbegu ya mchaichai, baadhi walisombelea mbolea, kufyeka majani, kuchanganya mbolea kwenye mashimo na wengine kupanda.

Kazi hiyo ilipamba moto hasa baada ya kuhamasishwa na viongozi wakuu ambao pia walishiriki bega kwa bega kubeba mbolea, mbegu na kupanda pia. Hakuna aliyeruhusiwa kukaa bila kazi akiwemo pia mwandishi wa habari hizi, Richard Mwaikenda.

Viongozi walioshiriki kwenye kampeni hiyo ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi,  Dk. Kissui S. Kissui, Mkurugenzi Mtendaji,  Adam Ngamange, Mkurugenzi wa Utawala na Mashamba, Catherina, Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth na Mhasibu Mkuu wa mtandao huo, Mshashu na msaidizi wake Samson.

Ofisi kwa siku nzima ilibidi zifungwe kwa siku nzima, ambapo walifanya kazi ya shamba kwa siku nzima ya jana hadi majira ya saa jioni saa 12.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kissui akishiriki kupanda mchaichai
Mkurugenzi wa Fedha wa Mkikita, Elizabeth akipanda mchaichai wakati wa kampeni hiyo
Wafanyakazi wa Mkikita wakiwa wamebeba mbolea ya kupandia mchaichai
Meneja Uhusiano wa Mkikita, Neema (kulia0 akiwa na Ofisa wa Mradi wa Kuku, Rose wakati wa shughuli ya kupanda mchaichai
Adam akibeba mbolea kupeleka shambani
Dk. Kissui akiwa amebeba miche akipeleka shambani
Eva akifanya usafi kwenye shamba tayari kupanda mchaichai
Wakichambua miche ya mchaichai
Catherina akishiriki vilivyo kwenye shamba hilo
Adam akichambua miche ya mchaichai
Meneja wa Kijaicos, Mishomari akisafisha shmba
Kazi ikiendelea
Mhasibu Mkuu, Mshahu akishiriki katika kampeni ya upandaji wa mchaichai
Ni kazi tu
Mkurugenzi wa Fedha, Elizabeth akisaidiana na Matrida
Mhasibu Mkuu msaidizi, Samson akishiriki kusafisha shamba
Hakuna kulala, Mkurugenzi wa mashamba, Catherina akiwa kazini
Sehemu ya shamba lililopandwa mchaichai
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mkikita, Dk Kissui (kulia) akiwapongeza wafanyakazi kwa moyo wao wao wa kujitolea kupanda mchaichai
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images