Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live

MHE MWANJELWA AMUAGIZA MKURUGENZI KUMSIMAMISHA KAZI MSIMAMIZI WA ZAO LA PARETO KUPISHA UCHUNGUZI

0
0
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017. Picha zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mhe Oran Njeza akizungumza katika mkutano huo kufikisha kilio cha wananchi mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwwa kuhusu zao la Pareto na matatizo la wafanyabiashara kujaza Lumbesa kwenye uuzaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la viazi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Jojo Kata ya Santilya, Jana Novemba 29, 2017.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana Novemba 29, 2017 amemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kumsimamisha kazi Afisa Kilimo Wilaya ya Mbeya anayesimamia zao la Pareto Ndg Emmanuel Halinga ili kupisha uchunguzi.

Mhe Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania mara baada ya Mhe Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Oran Njeza na Wananchi wote waliokuwepo kwenye mkutano huo wa hadhara kumrushia shutuma nzito na kumkataa mtaalamu huyo wa kilimo mbele ya Naibu Waziri.

Alisema kuwa pamoja na zao hilo la Pareto kuwa la kwanza kwa uzalishaji katika nchi za Afrika huku likiwa zao la pili kwa uzalishaji Duniani lakini bado halijamkomboa Mkulima nchini jambo ambalo linaonyesha namna ambavyo baadhi ya wataalamu Wa Kilimo wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema kuwa wataalamu wa kilimo walipaswa kusimamia kwa kiasi kikubwa zao hilo kwani Pato lake ni wastani wa tani 2000 kwa mwaka sawa na Bilioni 12 mpaka 14 ambapo katika kipindi hili bei ya kuanzia Mkulima analipwa shilingi 2300 kwa kilo lakini inapanda mpaka shilingi 3300 kulingana na ubora wa zao hilo ambalo mkulima amelima.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli inaamini katika kazi ambazo matokeo yake yanapaswa kuonekana hivyo Mkulima kushindwa kunufaika na mazao ya Kilimo ni uzembe wa baadhi ya wataalamu Wa Kilimo unaosababishwa na kufanya kazi kwa mazoea.

Aidha, Mhe Mwanjelwa ametoa siku saba kwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto nchini Ndg Lucas Ayo kutoa sababu za kwanini mnunuzi ni mmoja wa zao hilo jambo ambalo linaonyesha kuwa na harufu ya rushwa au kupelekea kudumaza solo la zao hilo kwa kuwa na mnunuzi mmoja asiyekuwa na ushindani.

Ili kuongeza ufanisi wa zao hilo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameelekeza wakulima Kuanzisha vikundi vya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitakuwa na usajili serikalini kwani vitasaidia kuwa na mjadala wa jinsi ya kuwa na ubora wa zao la pareto jambo litakalopekea kuanzisha viwanda vidogo ambavyo ni ishara ya kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuwa na Tanzania ya Viwanda.

"Mkishaanzisha tu vikundi vya vyama vya ushirika mtoe taarifa mapema iwezekanavyo na serikali kupitia mrajisi itatoa Elimu ya ushirika" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Ameagiza zao la Pareto kuwa huru ili mkulima awe huru kuuza kwa mnunuzi anayemtaka kwani kwa sasa kuna mnunuzi mmoja tu ambaye anajipangia mwenyewe namna ya kununua zao hilo kwa gharama atakazo pasina kupingwa.

Pia alielekeza wakulima Kuingia kwenye Kilimo cha mkataba kati yao na Chama cha msingi (AMCOS) jambo litakalorahisisha kupata mikopo ya Kilimo kupitia Benki ya Kilimo nchini (TADB).

Kuhusu Lumbesa, aliwataka wafanyabiashara wa wanaojaza Lumbesa badala ya kujazwa kilo 100 kwa gunia lakini linajazwa mpaka kilo 120 kuacha haraka tabia hiyo kwani wanakwenda kinyume na sheria hivyo kwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua Kali za kisheria.

TANESCO: HITILAFU KWENYE GRIDI YA TAIFA ASUBUHI HII

0
0
MAJIRA ya saa 7:20 leo hii Alhamisi Novemba 30, imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha umeme kukatika takriban kwenye mikoa yote iliyounganishwa kwenye Gridi hiyo.


Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, mafundi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO wameanza kufuatilia kujua chanzo chake hasa ni nini na taarifa Zaidi zitatolewa kila baada ya muda ili kuufahamisha umma na watuamiaji wa umeme.

Wananchi Jijini Mwanza wapatiwa Tiba ya Viungo na Ushauri Bure

0
0
Ni katika viunga vya Hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza ambapo Chama cha Watoa Tiba kwa Vitendo Tanzania TOTA, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kimetoa fursa kwa wanchi kupata huduma ya tiba ya viungo na ushauri bure. Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza, Dkt.Leonard Subi akifungua kongamano hilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella. Rais wa Chama cha Watoa Tiba kwa Vitendo Tanzania TOTA, bI.Neophita Lukiringi akizungumza kweny uzinduzi huo

DAWA ZA SARATANI ZAPATIKANA KWA ASILIMIA 80 % KUTOKA ASILIMIA 4%

0
0
  Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (kulia), akizungumza na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja Dar es Salaam leo ya kujua changamoto za upatikanaji wa dawa katika hospitali hiyo na kuzitafutia ufumbuzi. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Meshack Shimwela.
 Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Meshack Shimwela, akisisitiza jambo katika mkutano huo.
 Maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa MSD,Laurean Bwanakunu.
 Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam , Celestine Haule akichangia jambo wakaz8i akizungumza na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana.
 Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Anna Kajiru (kulia), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (wa sita kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana. 
 Mkutano ukiendelea.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage akizungumza katika mkutano huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu akisisitiza jambo wakati akizungumza na maofisa wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road katika ziara hiyo ya siku moja.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage ( kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (wa tano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Taasisi ya Saratani Ocean. 

Na Dotto Mwaibale

TAASISI ya Saratani ya Ocean Road wameipongeza Bohari ya Dawa (MSD), kwa usambazaji wa dawa katika taasisi hiyo na maeneo mengine nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage wakati akizungumza na watendaji wa MSD ambao walifanya ziara ya kikazi ya kujua changamoto mbalimbali za usambazaji dawa katika taasisi hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu.

Katika hatua nyingine  upatikanaji wa dawa za saratani,vifaa tiba na vitendanishi  vya maabara katika taasisi hiyo ni asilimia 80  kutoka asilimia nne mwaka 2015.

Kutokana na hatua hiyo taasisi hiyo imesema ipo haja jamii kutambua mchango mkubwa unaotolewa na Bohari ya Dawa MSD katika kupunguza changamoto za huduma za saratani ambapo ilikuwa kero miaka miwili iliyopita.

 Mwaiselage alisema hapo awali  upatikanaji wa dawa vifaa tiba na vitendanishi ilikuwa ni changamoto kubwa katika utendaji.

"2015 taasisi hiyo ilikuwa ikipata dawa,vifaa tiba na vitendanishi asilimia nne sasa ni asilimia 80 haya ni matokeo mazuri ya utendaji wa kazi wa MSD," alisema.

Alisema bajeti ya taasisi hiyo mwaka 2015 ilikuwa ni sh.milioni 790 na sasa ni sh.bilioni saba jambo ambalo linatia faraja.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu alisema taasisi hiyo inatambua kuwa dawa za kansa ni gharama lakini atahakikisha zinaendelea kupatikana kwa wakati ili kuokoa maisha ya watanzania.

Alisema suala la vifaa vya maabara ni tatizo linalohitaji mpango wa kitaifa wa manunuzi."Nawahakikishia Ocean Road ni mteja muhimu hivyo nipo tayari muda wote kuwahudumia leteni orodha ya mahitaji ya dharura hata leo," alisema.

Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Anna Kajiru alisema katika Hospitali hiyo upatikanaji wa dawa kutoka MSD ni asilimia 80 na kuwa hali hiyo imetokana na ushirikiano mzuri baina yao.

"Hivi sasa hali ya upatikanaji wa dawa ambazo zinahitajika sana na wananchi ni mkubwa mkubwa tofauti na zamani na hii inatokana na kazi nzuri inayofanywa na ninyi MSD" alisema Kajiru.

Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu na maofisa wake yupo katika ziara ya kikazi ya kutembelea Hospitali za Mkoa wa Dar es Salaam ambapo leo alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Amana na Saratani ya Ocean Road na kesho atazitembelea Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili, Vijibweni na Temeke.


MAMBO 10 UNAYOTAKIWA KUYAFAHAMU KUHUSU UKIMWI

0
0

Na Jumia Travel Tanzania
Wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya UKIMWI kila ifikapo Desemba mosi ya kila mwaka, bado Virusi Vya UKIMWI (VVU) na ugonjwa huo unabaki kuwa ni changamoto muhimu ya kiafya ndani ya jamii hususani kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati.

Kutokana na maendeleo yaliyofikiwa sasa katika upatikanaji wa tiba ya mchanganyiko wa dawa zinazotumika kuzuia VVU kuongezeka mwilini (antiretroviral therapy - ART), watu waliogundulika kuwa na VVU wanaishi kwa muda mrefu na maisha yenye afya. Kwa kuongezea, imethibitishwa kwamba dawa hizo zinazuia kuendelea kuongezeka kwa VVU.

Katika kukupatia elimu zaidi juu ya ugonjwa huu, Jumia Travel ingependa kukufahamisha juu ya mambo yafuatayo ambayo yamebainishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), ambalo huunga mkono nchi mbalimbali katika kuunda na kutekeleza sera na programu ili kuboresha na kuongeza jitihada za kuzuia VVU, matibabu, huduma na kutoa msaada kwa watu wote wanaohitaji msaada.

Taafirifa hizi zinatoa takwimu zilizopo sasa kuhusu ugonjwa huu pamoja na njia za kuuzia na kuutibu:

VVU huambukiza seli za kwenye mfumo wa kinga za mwili. Maambukizi husababisha kuendelea kuzorota kwa mfumo wa kinga ya mwili, huvunja uwezo wa mwili kuweza kuepuka baadhi ya maambukizi na magonjwa. UKIMWI hujulikana kuwa ni hatua ya juu kabisa ya VVU ambapo hujipambanua kwa kujitokeza kwa maambukizi kati ya zaidi ya 20 au saratani zinahusiana na virusi hivyo.   

VVU vinaweza kuambukizwa kwa njia kadhaa. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia: kujihusisha na ngono isiyo salama; kuhamishiwa damu au bidhaa inayohusiana na damu au kufanyiwa upandikizaji ambao sio salama; kushirikiana kutumia vifaa vya kutobolea mwili (sindano) na vimiminika au vya kuchorea michoro mwilini (tattoo); kutumia vifaa vya upasuaji na vinginevyo vyenye ncha kali; na maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto mchanga wakati wa ujauzito, kujifungua na kunyonyesha.   
Zipo njia kadhaa za kuzuia maambukizi ya VVU. Njia muhimu za kuzuia maambukizi ya VVU ni: kufanya ngono salama kama vile kutumia kondomu; kupima na kupatiwa matibabu kwa magonjwa yaliyoambukizwa kupitia ngono, ikiwemo VVU ili kuzuia maambukizi kuendelea; hakikisha kwamba damu au bidhaa yoyote inayohusiana na damu unayotaka kuitumia imepimwa VVU; chagua njia salama ya kimatibabu wakati wa tohara endapo unatoka katika nchi ambazo huchangia vifaa; kama una VVU anza mara moja kutumia dawa za kusaidia kupunguza virusi kuongezeka mwilini kwa manufaa yako na pia kuzuia kuambukiza VVU kwa mwenza au mtoto wako (kama ni mjamzito au unanyonyesha).  
Watu milioni 36.7 duniani wanaishi na VVU. Duniani kote, inakadiriwa kuwa watu milioni 36.7 (milioni 34.0 - 39.8) walikuwa wanaishi na VVU mwaka 2015, na kati ya hawa milioni 1.8 (milioni 1.5 - 2.0) walikuwa ni watoto. Idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU wanapatikana kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Inakadiriwa watu milioni 2.1 (milioni 1.8 - 2.4) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015. Inakadiriwa watu milioni 35 mpaka sasa wamefariki kutokana na VVU, wakiwemo milioni 1.1 (940,000 mpaka milioni 1.3) mwaka 2015.    
Mchanganyiko wa dawa za ART huzuia virusi hivyo kuongezeka mwilini. Endapo kuzaliana kwa VVU kukikoma, basi seli za kinga za mwili zitaweza kuishi kwa muda mrefu na kuupatia mwili kinga dhidi ya maambukizi. Ufanisi wa dawa za ART hupelekea kupungua kwa virusi, kiasi cha virusi mwilini, kwa kiasi kikubwa hupunguza kuambukiza virusi kwa watu walio kwenye mahusiano ya kimapenzi. Endapo mmojawapo wa wapenzi kwenye mahusiano anatumia dawa za ART ipasavyo, kuna uwezekano wa maambukizi ya njia ya ngono kwa mwenza ambaye hana VVU kupungua kwa kiasi cha takribani 96%. Kupanua wigo wa matibabu ya VVU kunachangia katika jitihada za kuzuia VVU.   
Katikati ya mwaka 2016, watu milioni 18.2 duniani walipokea dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Kati ya hawa zaidi ya milioni 16 wanaishi kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Mwaka 2016, WHO ilitoa toleo la pili la “Miongozo juu ya matumizi ya dawa za kusaidia kuzuia kuongezeka VVU mwilini ili kutibu na kuzuia maambukizi ya VVU.” miongozo hii imetoa mapendekezo kadhaa, ikiwemo pendekezo la kutoa dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini kwa watoto kwa kipindi chote cha maisha yao, vijana na watu wazima, wakiwemo wanawake wajawazito na wanaonyonyesha waishio na VVU, licha ya idadi ya CD4 walizonazo mara baada tu baada ya kugundulika.          

Kupima VVU kunasaidia kuhakikisha matibabu kwa watu wenye uhitaji. Upatikanaji wa huduma ya kupima VVU na madawa unatakiwa kuongezeka kwa kasi ili kufikia lengo la kutokuwa na ugonjwa wa UKIMWI kufikia mwaka 2030. Upimaji wa VVU bado ni mdogo, ambapo inakadiriwa kwamba 40% ya watu wenye VVU au zaidi ya watu milioni 14 bado hawajatambulika na hawafahamu hali ya maambukizi yao. WHO inapendekeza ubunifu kwenye mbinu za kujipima wenyewe VVU na wenza wao ili kuongeza huduma za kupima VVU kwa watu ambao hawajagundulika.    
Inakadiriwa watoto milioni 1.8 duniani wanaishi na VVU. Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2015, wengi wa watoto hawa wanaishi katika nchi zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara na waliambukizwa kutoka kwa mama zao wenye VVU wakati wa ujauzito, wakati wa kuzaliwa au kunyonyeshwa. Karibu watoto 150,000 (110,000 - 190,000) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015.
Kuondoa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto inawezekana. Ufikiwaji wa hatua za kuzuia maambukizi ya VVU umekuwa ni mdogo kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Lakini jitihada zimeendelea kufanyika kwenye baadhi ya maeneo tofauti kama vile kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na kuokoa maisha ya akina mama. Mwaka 2015, karibu wajawazito 8 kati ya 10 wanaoishi na VVU au sawa na wanawake milioni 1.1 walipokea dawa za kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Mwaka 2015, Cuba ilikuwa ni nchi ya kwanza kutangazwa na WHO kufanikiwa kuzuia maambukizi ya VVU na Kaswende kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Mwaka 2016, nchi zingine tatu: Armenia, Belarus na Thailand nazo zilithibitishwa kulifanikisha hilo.        
VVU ni sababu kubwa inayopelekea kupata ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Katika mwaka 2015, inakadiriwa kuwa watu milioni 1.2 (11%) kati ya watu milioni 10.4 duniani waliopata TB walikuwa ni waathirika wa VVU pia. Mwaka huohuo takribani vifo 390,000 vilivyotokana na TB vilitokea miongoni mwa watu waliokuwa wanaishi na VVU. Nchi za Kiafrika ambazo zilizo chini ya WHO zilizidi karibu 75% ya idadi ya vifo vilivyokuwa vinahusiana kati ya TB na VVU.
UKIMWI ni janga ambalo linaikumba dunia nzima Tanzania ikiwemo, licha ya ugonjwa huu kutzungumziwa kwenye kampeni tunazozisikia lakini ukweli ni kwamba bado upo, ni tatizo, unaathiri na kuua nguvu kubwa ya taifa. Katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani, Jumia Travel ingependa kuikumbusha jamii inapaswa kutambua kwamba jukumu la kuupiga vita ugonjwa huo bila ya kutegemea taasisi binafsi au mashirika ya nje.   

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA HUDUMA MPYA YA WCF YA WAAJIRI KUJISAJILI KWENYE MTANDAO WA INTERNET

0
0
Mkuu wa kitengo cha Tehama cha WCF, Bw. Stephen Goyayi, akielezea jinsi huduma hiyo iyakavyofanya kazi.
 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID. ARUSHA
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama, amezindua huduma mpya itakayowawezesha waajiri kujisajili na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), kwa kutumia mtandao wa Internet.
Mhe. Mhagama amezindua huduma hiyo leo Novemba 29, 2017, wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Mwaka wa Wadau wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), kwenye ukumbi wa Simba wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC, Arusha.
“Huduma hii itawawezesha waajiri kujisajili na Mfuko kupitia mtandao wa internet na hawalazimiki kujaza fomu na kuja ofisini kwetu au kwa maafuisa kazi” Mkuu wa kitengo cha Tehama cha WCF, Bw. Stephen Goyayi, alisema wakati akitambulisha huduma hiyo kwa Mhe. Waziri.
Katika hatua nyingine, Benki ya NMB Bank plc  imenyakua tuzo baada ya kuwa mwajiri bora katika uwasilishaji michngo miongoni mwa waajiri wenye wafanyakazi wengi.
Kampuni zingine zilizonyakua tuzo kundi la waajiri ni Steel Master Ltd kwa kuwa mwajiri bora katika uwasilishaji nyaraka za madai ya fidia kwa wafanyakazi na kampuni nyingine ni KPMG  Advisory Ltd kwa kuwa mwajiri bora katika uwasilishaji michango miongoni mwa kundi la waajiri wenye wafanyakazi wengi.
WCF iliwatunukia tuzo wadau wa Mfuko huo ambapo Waziri Jenista kwa niaba ya Serikali alipokea tuzo hiyo, kwa kutambua mchango wa Serikali katika kuanzisha na kufanikisha utendaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
Wadau wengine ni Shirika la Vyama vya Wafanyakazi, (ATE), Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi, (TUCTA), Mamlaka ya Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii, (SSRA), kwa kutambua ushiriki wake katika uanzishwaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF)
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama, (wapili kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshjomba, wakishuhudia Mwenyekiyti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, (kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilinhi milioni 15, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo, ikiwa ni mchango wa Mfuko kusaidia mpango wa elimu mkoani humo. Makabidhiano haya yamekwenda sambamba na ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Wadau wa WCF jijini Arusha
 Waziri Mhagama (watatu kushoto) na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Eric Shitindi, (wakwanza kushoro), wakipokea hundi yenye thamani ya shilingi milioini 33.8 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, (wapili kushoto). Fedhab hizo ni kwa ajili ya kusaidia ununuzi wa komputa nundu (perkins Braille Machines) kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa kuona katika shule za umma.
 
 Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya WCF,. Wakwanza kushoto ni katibu wa Waziri Jenista Mhagama.
 Mheshimiwa Waziri Jenista Mhagama, akimkabidhi tuzo Bw. Richard L.Makungwa kutoka NMB Bank Plc tuzo ya mwajiri mwajiri bora katika uwasilishaji michngo miongoni mwa waajiri wenye wafanyakazi wengi. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo, na kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba.
 Mheshimiwa Waziri akimkabidhi tuzo Kaimu Mwenyekiti wa ATE, Bi. Janet Reuben Lekashingo tuzo ya ushiriki kama Mdau wa WCF. Anayeshuhudia ni Bw. Humba.
Mheshimiwa Waziri akimkabidhoi tuzo Kaimu Mwenyekiti wa ATE, Bw.Tumaini Peter Nyamhokya, Katibu Mkuu wa TUCTA, tuzo ya ushiriki kama mdau wa WCF. Anayeshuhudia ni Bw. Humba.
 Mheshimiwa Mhagama akimkabidhi tuzo, Bw. Hiroshi Yamobana kutoka ILO kwa ushiriki na kama mdau
 Waziri Jensita akipokea zawadi ya saa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba
 Mwenyekiti wa Boadi ya Wadhamini ya SSRA hadi Aprili 2017, Bw.Juma Muhimbi, (kulia), akiteta jambo na Bw. Masha Mshomba
 Waziri akipokea na Bw. Feddy Maro, wa AICC alipowasili mapema leo kufungua mkutano huo.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Bw. Mrisho Gambo, akizungumza
 Kamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge, na Mbunge wa Chemba, Mhe. Juma Nkamia
 Bi. Sara Kibonde Msika kutoka SSRA
 Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Dkt. Irine Isaka akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bw. Adam Mayingu, wakati wa mkutano Mkuu wa Kwanza wa mwaka wa Wadau wa WCF jijini Arusha Novemba 29, 2017

Mmoja wa watu wanaofaidika na Mafao ya WCF,

MKESHA WA THE WORSHIPPERS NIGHT 2017 KUFANYIKA IJUMAA HII KATIKA UKUMBI WA UPANGA CCC

0
0

WAKAZI WA DAR ES SALAAAM MKO TAYARI? The worshippers night 2017 - USIKU WA WAMUABUDUO ni usiku wa kusifu na kuabudu ambapo watu wote wa Dar es salaaam tutakutana katika ukumbi wa CCC UPANGA JIJINI DAR E SALAAAM, Ni siku ya ijumaaa hii tarehe 1.12.2017 kuanzia saa 2 kamili usiku.Mkesha huu unawaunganisha watu wote wa madhehebu yote. Mkesha huu utapambwa na choir na waimbaji mbalimbali kama vile
  1. Kwaya ya uinjilisti KIJITONYAMA
  2. AIC CHANG'OMBE
  3. MTBC PRAISE AND WORSHIP TEAM
  4. IFM TAFES
  5. MSASANI PRAISE AND WORSHIP TEAM
  6. ESSENCE OF WORSHIP
Bila kuwasahau wenyeji THE WORSHIPPERS NIGHT MASS CHOIRPamoja na waimbaji binafsi wakiwemo
  1. BEDA ANDREW
  2. SARAH NDOSI
  3. BOMBY JOHNSON
  4. NSAJIGWA MWODEKAI
  5. ROGATE KALENGO
KUMBUKA NI IJUMAA HII PALE UPANGA CCC BUREEEEE KABISAKWA MAWASILIANO ZAIDI0657266777 NA 0627111777THE WORSHIPPERS NIGHT---- KUSANYIKO LA WOTE WAMUABUDUO

Machinjio Ya kisasa Ya Ruvu Lazima Yakamilike Ifikapo 2018 – Mpina

0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luhaga J. Mpina ameagiza machinjio ya kisasa ya Ruvu yaliyotelekezwa kwa muda mrefu kujengwa na kukamillika ifikapo Desemba, 2018.

Maagizo hayo ameyatoa jana katika ranchi ya Ruvu, alipokuwa katika ziara ya kutembelea baadhi ranchi za mifugo nchini, ambapo amesema ni muhimu machinjio hayo ya ya kisasa yakamilike ili Tanzania ianze kuuza mazao yatokanayo na mifugo katika masoko ya kimataifa.

Ametoa siku tatu kwa Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kumpelekea mpango kazi unaoainisha namna ya kukamilisha ujenzi wa machinjio hiyo ya kisasa ambayo baada ya kukamilika itakuwa machinjio kubwa kuliko zote nchini.

Amesema kuwa Tanzania ni nchi ya tatu katika bara la Afrika kwa kuwa na uwingi wa mifugo hivyo hakuna sababu ya kushindwa kuongoza katika soko la mazao ya mifugo katika masoko ya duniani.Aidha, Waziri Mpina amesema  kukamilika kwa machinjio hayo kutasaidia kupunguza usumbufu kwa wafanyabiashara wa mifugo ambao wote nawapeleka mifugo yao Dar es Salaam hali ambayo inaongeza uharibifu wa mazingira kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Waziri Mpina amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Ranchi za taifa kuhakikisha kuwa kunatafutwa fedha kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora za mifugo na kuongeza idadi ya mifugo kulingana na uwezo wa eneo la ranchi ya Ruvu lenye ukubwa wa hekta 44,000 ambapo hivi sasa eneo hilo la ranchi ya Ruvu lina mifugo ipatayo 1530 wakati uwezo wa ni kuwa na mifugo kuanzia 12000 hadi 22000.

Alisisitiza kwamba maboresho hayo lazima yafanyike ifikapo Desemba , 2018  ambapo ifikapo Juni 2018 tathimini ya awali itafanyika kuona ni kwa namna gani agizo hilo limetekelezwa.“Tunataka wananchi wapate sehemu ya kujifunza,ranchi ya Ruvu iwe sehemu ya kupata mbegu bora. Siwezi kuwa Waziri wa Mifugo wakati shamba langu halina mifugo” alisisitiza Mpina.

Waziri aliongeza kuwa na mfumo wa kisasa wa kufuga mifugo kitaalamu badala ya mfumo wa sasa ambapo mifugo inafugwa kwa muda mrefu.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye miwani) akijaribu kukata nyama kwa kutumia mashine ya kisasa alipotembelea ranchi ya Ruvu hivi karibuni.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye miwani) akiwa na viongozi wa ranchi ya mifugo nchini akionyeshwa mbuzi wanaofugwa katika ranchi ya Ruvu alipotembelea ranchi hiyo hivi karibuni.
Jengo la machinjio ya kisasa lililopo katika eneo la ranchi ya Ruvu ambalo Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina amewaagiza Watendaji kuhakikisha linakamilika ifikapo Desemba 2018.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye miwani) akihakiki taarifa za ununuzi wa dawa za mifugo alipotembelea ranchi ya mifugo ya Ruvu hivi karibuni.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina (mwenye miwani katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ranchi ya Ruvu na watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi alipotembelea ranchi hiyo jana.

MADABA YAWA MFANO BORA KATIKA KUTATUA KERO YA MAJI KATIKA WILAYA YAO

0
0


Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akikagua mabomba yatakayotumika kusambazia maji kwa mradi wa Maweso akiwa na Mbunge wa Jimbo la Madaba, Joseph Mhagama katika Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akikagua ujenzi wa tenki la maji la mradi wa Lolindo na Mbunge wa Jimbo la Madaba, Joseph Mhagama ambao utekelezaji wake unaendelea katika Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma.
Mhandisi wa Mkoa wa Ruvuma, Jones Kimaro (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso katika kitekeo cha maji ikiwa ni sehemu ya mradi wa Lilondo katika Wilaya ya Madaba, mkoani Ruvuma.
Mradi wa mfano uliotekelezwa na wakazi wa Lilondo, ambao wametumia teknolojia ya kienyeji ya kukusanya maji kwa mabomba kutoka milimani na kuyahifadhi kwenye bwawa walilochimba na kuyasambaza kwa wananchi kupitia mitaro waliyochimba kwa gharama zao wenyewe ili kukabiliana na changamoto ya maji katika kijiji chao.

WAFUGAJI NA WAKULIMA BADO CHANGAMOTO, NAIBU WAZIRI ULEGA AAGIZA WAFUGAJI KUFUATA SHERIA

0
0

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mb) Abdalaah Ulega akimsikiliza moja ya wafugaji wa Kijiji cha Matanzi Kata ya Beta wakati wa ziara yake katika Jimbo la Mkuranga akisikiliza changamoto za wananchi wake.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Ili kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (mb) Abdalah Ulega amewataka wafugaji wote waliongia vijijini kinyume cha sheria kufuata sheria vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa zidi yao.

Hayo ameyasema Mkuranga mkoani pwani wakati alipofanya ziara ya kutembelea vijiji vya jimboni kwake kuangalia changamoto zinazowakabili wananchi wa jimbo hilo ambapo moja ya changamoto hizo ni tatizo la wakulima na wavugaji.

Aidha ulega amesema moja ya sababu ya migogoro ya wakulima na wafugaji ni kutokuwa na matumizi bora ya ardhi hivyo ameitaka jamii kuwa na matumizi bora ya ardhi ilikuweza kuepuka migogoro inayoweza kutokea.

"tatizo hakuna matumizi bora ya ardhi na ni lazima kuwe na matumizi bora ya ardhi pamoja na kupima maeneo ili maeneo ya wafugaji yaweze kujulikana",alisema

Amesema yeye kama Waziri atazungumza na watalaamu kutoka wizarani ili waweze kushirikiana na wataalamu wa halmashauri ya mkuranga kwa pamoja waweze kwenda katika kijiji cha Matanzi kutafuta ufumbuzi wa kudumu juu ya tatizo la wakulima na wafugaji.
Hata hivyo amemuagiza Afisa Mifugo wa kata ya Beta kuhakikisha ng'ombe wote wanapigwa chapa ili kuweza kujua idadi kamili ya ng'ombe na ametoa wito kwa wakulima na wafugaji kuhakikisha  anashirikiana,wanapenda,wavumiliane na waishi kwa amani. 

Awali wanachi wa kijiji cha Matanzi wakitoa malalamiko yao mbele ya Naibu Waziri huyo wamesema kijiji chao kilipokea kaya nne za wafugaji ambazo zina tambulika wakiwa na mifugo isiyozidi 300 lakini mpaka sasa kaya hizo zimeongezeka kinyume na utaratibu na idadi ya ng'ombe kuwa zaidi ya 900 hali inayopelekea mifugo kuwa mingi na kusambaa kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu mazao yao.

Mbali na changamoto hiyo, katika ziara ya Naibu Waziri amekutana na ukosefu wa walimu katika kata ya Mkwechembe na Matanzi na kumuagiza Afisa Elimu wa Wilaya kuhakikisha walimu wanaongezwa kwenye shule hizo, pia ameshukuru Bruda Marcos kwa hatua kubwa aliyoifanya ya kujenga madarasa manne ya Shule ya Msingi Mkwechembe.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mb) Abdallah Ulega akikagua shule ya Mkwechembe iliyojengwa na mfadhili Bruda Marcos katika Kijiji cha Mkwechembe.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mb) Abdallah Ulaga akipokea zawadi kutoka kwa wanakijiji cha Mkwechembe wakati wa ziara yake kwenye Jimbo lake la Mkuranga jana Mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mb) Abdallah Ulega akisalimiana na wanakijii wakati wa ziara ya Jimbo la Mkuranga jana Mkoani Pwani.

WAFANYABIASHARA UFARANSA WATUA TANZANIA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA

0
0
Chemba ya viwanda, biashara na kilimo nchini (TCCIA ) imepokea ugeni wa wafanyabiashara kutoka nchini Ufaransa wenye lengo la kujadili na kupanua mianya ya biashara kati ya Tanzania na Ufaransa Ugeni huo kutoka nchini ufaransa umeambatana na wafanyabiashara pamoja na wamiliki wa makampuni makubwa ambapo lengo kuu la mkutano ni kutaka kutengeneza urafiki wa kibiashara baina ya nchi hizi mbili na kubadilishana uzoefu wa kibiashara pamoja kupanua fursa za uwekezaji baina ya Tanzania na Ufaransa
Makamu wa Rais wa TCCIA Ndg. Octavian Mshiu (katikati), kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa TCCIA Ndg. Gotfid Muganda,pamoja na wafanyabiashara kutoka ufaransa wakati wa mkutano
Makamu wa Rais wa TCCIA Bwana Octavian Mshiu amesema Tanzania imekuwa nchi yenye bahati ya kutembelewa na wafanyabiashara wakubwa kutoka nchi mbalimbali na hii ni kutokana na Tanzania kuwa na sifa kubwa kimataifa kama nchi yenye malighafi nyingi za kibiashara 
Makamu wa Rais wa TCCIA Ndg. Octavian Mshiu akisisitiza jambo wakati wa Mkutano na wafanyabishara kutoka ufaransa.Aidha Mshiu amesema kuwa ziara hii inatoa fursa nyingi kwa wafanya biashara nchini kutanua biashara zao kwenda kimataifa zaidi.Mshiu amewataka wafanyabiashara wakubwa na wadogo kutumia ujumbe huu wa wafanyabiashara kutoka Ufaransa kama njia ya kukuza biashara zao kwa manufaa yao na taifa kwa ujumla.

WCF YAPATA HATI SAFI KATIKA UKAGUZI WA TAARIFA YA FEDHA ULIOFANYWA NA CAG

0
0

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akifafanua baadhi ya mambo wakati viongozi wa Mfuko walipokuwa wakiwasilisha taarifa za utendaji wake kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Wadu kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC, jijini Arusha leo Novemba 30, 2017.

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA
MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) umepata hati safi katika taarifa ya hesabu zake za fedha katika kipinmdi cha mwaka 2015-2016 ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kuanzishwa kwake.
Katika taarifa hiyo mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2016 (mwaka wa kwanza tangu kuaza kufanya kazi zake), thamani ya Mfuko ilifikia shilingi bilioni 65.68 na mfanikio haya yaliweza kufikiwa kutokana na ubunifu na ushirikiano mkubwa kati ya Mtendaji Mkuu wa Mfuko na Bodi ya Udhamini, Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Mfuko huo, Bw.Bezil Kwala, aliwaambia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Wadau wa Mfuko huo unaoingia siku yake ya pili nay a mwisho kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC jijini Arusha, wakati akiwasilisha taarifa hiyo ya fedha leo Novemba 30, 2017.
Amesema Mfuko umekuwa ukiaandaa hesabu zake kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uaandaji wa hesabu za fedha na kwa mujibu wa sheria CAG ndiye mwenye mamlaka ya kufanya ukaguzi na Hati Safi ni uthibitisho wa taarifa ya fedha za Mfuko kuonyesha hali halisi na kutokuwa na dosari ya aina yoyote.
Amesema katika ukaguzi huo, CAG alishirikiana na kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PwC). Mwakilishi wa kutoka Ofisi ya CAG, Bw…….. amethibitishia wajumbe usahihi wa taarifa hiyo ya fedha ya WCF.
Mkutanmo huo ambao umeanza Novemba 29, 2017 na kubeba kauli mbiu isemayo, "Mafao ya Fidia: Haki ya Mfanyakazi na chachu katika kukuza uchumi wa viwanda”, pia ulipokea taarifa ya mipango ya uwekezaji ambapo Bw. Kwala aliwaambia wajumbe kuwa, katika kipindi kati ya mwaka 2017/18 – 2021/22, Mfuko umepanga kuwekeza kwenye miradi mbalimbali itakayoleta faida kwa mujibu wa tathmimi za kitaalamu zitakazofanyika.
“Maeneo tuliyoyaanisha katika uwekezaji kwenye sekta ya viwanda ni pamoja na kiwanda cha Grape Processing Factory kwa ushirikiano kati ya  GEPF na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, kiwanda cha Madawa mkoani Simiyu kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Kiwanda cha Morogoro Canvas Mills kwa kushirikiana na mifuko ya WCF, NSSF, PSPF, GEPF, na LAPF”. Alifafanua.
Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa Mfuko kuwekeza, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw.Masha Mshomba alisema, fedha zitokanazo na michango ya Wanachama ni kidogo ukilinganisha na mahitaji halisi ya ulipaji Mafao ya fidia na kwa hali hiyo, ni muhimu Mfuko kuwekeza ili kupanua wigo wa kuongeza mapato na hivyo kuendelea kutoa Mafao ya Fidia bila ya shaka yoyote.
 Baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Idara wa WCF wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, akizungumza
 Mkurugenzi wa Fedha WA WCF, Bw.Bezil Kwala, akiwasilisha ripoti ya fedha ya Mfuko kwa mwaka wa 2015-2016.
 Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Ofisi ya Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Johanes Joel Kisiri, akisikiliza uwasilishaji wa taarifa hiyo ya fedha.
 Mkuu wa Kitengo cha Sheria cha WCF, Bw.Abraham Siyovelwa, akitoa mada kuhusu Sheria juu ya kuanzishwa kwa Mfuko na jinsi unavyofanya kazi zake. Pamoja na mambo mengine Bw. Siyovelwa aliwaambia wajumbe kuwa,   Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoazishwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Sura Na. 263 (Marejeo ya 2015) na kuanza kazi rasmi tarehe 1 Julai 2015. Lengo la kuazishwa kwa Mfuko ni kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi waliopo katika sekta rasmi (Binafsi na Umma) Tanzania bara ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi
 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anslem Peter, akiwasilisha taarifa ya uendeshaji ya Mfuko katika kipindi cha uahai wake, ambapo alisema Mfuko umekuwa ukifanya vizuri ikiwa ni pamoja na usajili wa wanachama " katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015-2017 jumla ya Waajiri 5,178 walisajiliwa ikiwa ni asilimia 71.92 ya lengo la kusajili waajiri 7,200

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Dkt.Irene Isaka.
 Kiongozi wa chama cha Waajiri nchini (ATE), Bw. Aggrey Mlimuka, akizungumza kwenye mkutano huo.
 Bw. Hiroshi Yamabana kutoka Shirika mla Kazi Duniani, (ILO), akiuliza masuala mbalimbali kuhusu upembuzi juu ya usalama mahala pa kazi
 Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini, akizungumzia uzoefu wa masuala ya Mfuko wa Fidia kutoka nchini kwake

 Bw. Mshomba (kushoto), akizungumza jambo wakati wa mkutano huo. Kulia ni Bw.Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini,

 Mbunge wa jimbo la Mlalo Mkoani Tanga, Mhe. Rashiud Shangazi, (kushoto), akimsikiliza Meneja Uhusiano wa PPF, Bi. Lulu Mengele. Wote hao ni miongoni mwa wadau walioalikwa kushiriki mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wdhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, (kulia), akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Taifa wa Bima ya Afya, (MHIF), Bw. Afya, Bw. Bernard Konga.
Mkurugenzi wa Matekelezo na Uandikishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Lightness Mauki

MAGEREZA SACCOS YAFANYA MKUTANO MKUU WA TANO, 2017 MKOANI DODOMA

0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa ambaye pia ni Mlezi wa Magereza SACCOS Nchini akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza SACCOS, Naibu Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana(wa pili kulia) alipowasili kwenye katika Ukumbi wa  Chuo cha Mipango Dodoma tayari kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara. Mkutano huo unafanyika kwa siku moja leo 30 Novemba, 2017 hapa mjini Dodoma. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza SACCOS, Naibu Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana(katikati) akimuongoza Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(kushoto) ambaye pia ni Mlezi wa Magereza SACCOS kuingia Ukumbini tayari kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara(kulia) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza, Gaston Sanga. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza SACCOS, Naibu Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufungua rasmi Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara ulifanyika katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango Dodoma..
Kaimu Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Bw. Charles Malunde akitoa hotuba ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara wakisikiliza hotuba ya Mgeni rasmi kama inavyoonekana katika picha. 
Mjumbe wa Mkutano huo ambaye pia ni Mkuu wa Magereza Mkoani Kagera, Naibu Kamishna wa Magereza, Jeremiah Nkondo akichangia mada katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tano wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara . 
Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga akitoa neno la shukrani mara baada ya ufunguzi wa Mkutano huo. 
Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa akiteta jambo na Mgeni rasmi Kaimu Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Bw. Charles Malunde kama inavyoonekana katika picha.
Kaimu Naibu Mrajis wa Vyama vya Ushirika nchini, Bw. Charles Malunde(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara(waliosimama). Walioketi(wa tatu toka kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya Magereza Saccos anayemaliza muda wake, Naibu Kamishna wa Magereza, Gideon Nkana(wa pili toka kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga mara baada ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Tano unaofanyika kwa siku moja Mkoani Dodoma(Picha zote na Kitengo cha Habari na Mawasiliano – Jeshi la Magereza).


Chama cha Ushirikia wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara (TPS SACCOS) kimefanya Mkutano wake Mkuu wa Tano wa Mwaka 2017 kwa ufanisi Mkoani Dodoma.Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere uliopo katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini,  Miyuji Dodoma leo Novemba 30,  2017.

Akiongea katika Mkutano huo Kaimu Naibu  Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini, Bw.  Charles Malunde kwa niaba ya Naibu Mrajisi ametoa angalizo kwa Vyama vya ushirika nchini kutokufanya biashara za Kibenki nje ya lengo la kuanzishwa kwa SACCOS.

Amesema kuwa katika  vyama vingi vya ushirika uzoefu umeonesha kuwa wakishakuwa na mtaji mkubwa huwa na wazo la kuanzisha Benki, ametoa angalizo kuwa masharti ya uendeshaji wa Benki ni tofauti kabisa na masharti ya uendeshaji wa vyama vya ushirika hivyo ameziasa Saccos zote nchini kutafakari vyema kabla ya kubadili vyama hivyo na kuwa Benki.
“ Ukianzisha Benki huduma za Saccos zitafifia, kumbukeni wateja wa Saccos ni pamoja na wale wa hali ya chini kabisa ikiwa benki hawa huenda mkawaacha” alisisitiza  Kaimu Mrajis Malunde.

Aidha,  amewaasa Magereza SACCOS pamoja na Saccos zote nchini kufanya shughuli zake kwa kufuata sheria  lakini pia kuheshimu na kusikiliza sana wenye mali ambao ni wanachama wa vyama hivyo vya ushirika.

Aliongeza kuwa kwakuwa Mkutano huu utahusisha uchaguzi wa wajumbe wa Bodi Bw. Charles Malunde pia amewaasa Wajumbe wa Mkutano Mkuu kuwa makini katika uchaguzi huo kwa kuchagua watu wenye weledi na wenye mapenzi ya dhati na ushiriki wao ili waweze kutimiza majukumu yanayokusudiwa.

Pia amewataka wagombea wote wanaowania nafasi mbalimbali za chama hicho kujiuliza mambo manne kama ifuatavyo;- Je, watumishi wa Jeshi la Magereza wote ni wanachama? na mnaweka Mkakati gani?, Je wanachama wanaweka akiba za kila mwezi?, Mnajiendesha kisayansi? Mtu akitaka mkopo anapata baada ya muda gani? na swali la mwisho uhusiano na vyama vingine vya ushiriki, SCULT, nje ya nchi ukoje?.

Awali akitoa taarifa ya Chama cha Ushirikia wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara (TPS SACCOS), Mwenyeki wa Bodi ya Magereza Saccos, DCP. Gideon Nkana amesema kuwa Idadi ya wanachama imeongezeka hadi kufikia wanachama zaidi ya 13,000 ikiwa na mtaji wa zaidi ya bilioni 18.

FINLAND YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA BILIONI 75 KUENDELEZA MISITU, MAFUNZO YA UONGOZI NA UBUNIFU

0
0
Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

Serikali ya Tanzania na Finland zimetiliana saini mikataba mitatu yenye thamani ya Euro milioni 28.8 sawa na Shilingi bilioni 75 kwa ajili ya kuendeleza misitu, ubunifu na masuala ya uongozi.

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mikataba hiyo, Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James amesema, msaada huo kutoka Finland umetolewa ili kuendeleza  uwezo wa viongozi na kufanya maamuzi sahihi yenye tija kwa ukuaji wa uchumi wa Taifa, mradi ambao unasimamiwa na Taasisi ya Uongozi, ambapo kiasi cha Euro milioni 9.90 zimetolewa kuendeleza mradi huo.

Aidha Serikali ya Finland imetoa kiasi cha Euro milioni 8.95 kwa mradi wa  kuiimarisha mfumo wa ubunifu nchini kwa kutengeneza mazingira rafiki kwa wabunifu ili kuweza kubuni na kuendeleza ubunifu wao na kuchochea ukuaji wa viwanda. 

Bw. James alisema fedha hizo zitatumika kuwasaidia wabunifu kwa kuwapatia vifaa na msaada wa kitaalamu ili kuyaendeleza mawazo yao na kuyafanya yawe ya kibiashara na kuweza kusaidia kubadili mawazo hayo kuwa viwanda. 

“Fedha hizi zitasaidia kutatua changamoto katika viwanda vilivyopo nchini ili vifanye kazi kwa ufanisi kwa kuwaunganisha wanataaluma mbalimbali nchini, ikiwa ni pamoja na wabunifu wachanga, wataalamu kutoka vyuoni, wataalamu kutoka Serikalini na Sekta binafsi” Alisema Bw. Doto James

Eneo lingine lililonufaika na msaada huo ni programu ya misitu, ambayo imepatiwa Euro milioni 9.95 kwa lengo la utuzaji wa misitu na uongezaji thamani ya mazao yatokanayo na misitu ili kuongeza kipato kwa Wananchi, kupunguza umasikini na kulinda mazingira.

Katibu Mkuu amemshukuru balozi wa Finland Nchini, Mhe. Pekka Hukka kwa msaada walioutoa na kwa kuunga mkono shughuli za maendeleo za Serikali, na kuongeza kuwa Finland wamekuwa wakifadhili miradi mbalimbali nchini, ukiwemo mradi wa kilimo biashara Mkoani Lindi na Mtwara (LIMAS), uliogharimu Euro milioni 9, Mradi wa kuimarisha usambazaji na upatikanaji wa umeme wa uhakika Jijini Dar es Salaam, uliogharimu Euro milioni 25, na Programu ya maboresho ya Serikali za Mitaa, Euro milioni 10.5

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja aliiishukuru Serikali ya Finland kwa kuendelea kuisaidia Taasisi hiyo.
‘Hii ni mara ya tatu Finland wamekuwa wakitusaidia kuendeleza jitihada zilizoanzishwa na Serikali yetu ambapo awamu ya kwanza ilikuwa ni mwaka 2012 ambapo walitupatia Euro milioni 7, mwaka 2014 Euro milioni 12 na sasa wametupatia Euro milioni 9.90 huu ni msaada mkubwa’ alisema Profesa Semboja.

Aidha kwa upande wake Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendeleza ushirikiano na Serikali yake, na kuongeza kuwa msaada huo ni muhimu sana katika kutimiza malengo ya maendeleo ya nchi.Amesema msaada huo ukitumika ipasavyo hasa katika kuendeleza mnyororo wa thamani wa mazao ya misitu utasadia kuongeza ajira na kuongeza pato la Taifa.

Ameitaka Serikali kupitia Wizara ya nishati,  kushirikiana na sekta binafsi na kuitumia fursa hiyo ya kuboresha misitu ili kuiongezea nchi mapato zaidi yatakayotokana na makusanyo ya kodi.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kulia) akionesha kalamu aliyozawadiwa na Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka (kushoto) ambayo imetengenezwa kwa mbao, akionesha uzalendo wa matumizi ya misitu. Kutoka kulia ni Kamishna wa Bajeti Wizara ya Fedha na Mipango Bibi. Mary Maganga na Kamishna wa Fedha za Nje Bw. John Rubuga.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James (kulia) akitia saini moja kati ya mikataba mitatu yenye jumla ya shilingi bilioni 75 kama msaada kwa Tanzania, Kushoto ni Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka kwa pamoja wakisaini mikataba hiyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kulia) akibadilishana mkataba na Balozi wa Finland Bw.Pekka Hukka. Mkataba wa kwanza wa Euro milioni 9.9 ni kwa ajili ya kusaidia Taasisi ya Uongozi, wa pili wa Euro milioni 8.9 kwa ajili ya kuimarisha mfumo wa ubunifu na watatu wa Euro milioni 9.5 ni kwa ajili ya program ya misitu.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (kulia) pamoja na Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka (kushoto) wakionesha moja ya mikataba mara baada ya kumaliza kutia saini mikataba hiyo.
Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Prof. Joseph Semboja (Kulia) akiishukuru Serikali ya Finland kwa kuwapatia msaada wa Euro milioni 9.9 ambayo itawasaidia kuendesha shughuli mbalimbali za Taasisi hiyo. Kushoto ni Balozi wa Finland Bw. Pekka Hukka.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James (katikati, waliosimama mbele) akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya hafla ya utiaji saini mikataba mitatu ya jumla ya shilingi bilioni 75. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MENEJA WA COCA COLA AFRIKA MASHARIKI

0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Coca Cola Afrika Mashariki Bw. Ahmed Rady (kushoto) ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Coca Cola Afrika Mashariki Bw. Ahmed Rady (kushoto),Mkurugenzi Mtendaji wa Coca Cola nchini Bw. Basil Godzios na viongozi wengine wa kampuni hiyo mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WABUNGE WA CUF WALIOVULIWA UBUNGE

0
0

MTANDAO WA UTEPE MWEUPE (WHITE RIBBON) WAZUNGUMZA NA WAKAZI WA KIJIJI CHA MAORE JUUU YA VIFO VTOKANAVYO NA UZAZI KWA KINAMAMA NA WATOTO WACHANGA

0
0
Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe kitaifa  (The White Ribbon Alliance ) Rose Mlay akizungumza na wananchi katika kijiji cha Maore wilayani Same wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Taasisi ya Utepe mweupe (White Ribbon)  kujadili vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Maore wilayani Same akifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokuwa yakiendelea kuhusu vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Mganga Mkuu wa wilaya ya Same,Dkt Godfrey Andrew akizungumza wakati wa mkutano na wananchi ulioandaliwa na Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon) kujadili  vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Maore wilayani Same akifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokuwa yakiendelea kuhusu vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .
Mkutano ukiendelea katika jengo la Mahakama lililopo katika kijiji cha Maore wilayani Same.
Baadhi ya kina mama wakiwa na watoto wao katika mktano huo.

Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Maore wilayani Same wakichangia wakati wa mkutano uliondaliwa na Mtandao wa White Ribbon kuhusu vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga .

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

WANANCHI katika kijiji cha Maore wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro,wamesema tatizo la vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi pamoja na watoto wachanga vinachangiwa na upungufu wa watumishi katika zahanati ya kijiji pamoja na ufinyu wa wodi ya wazazi iliyopo.

Wakitoa maoni yao katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Taasisi ya Utepe mweupe (White Ribbon)  kujadili vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga katika kijiji cha Maore wilayani Same wananchi hao wameiomba serikali kuangalia namna ya kutatua changamoto hizo.

Mbali na changamoto hizo wakazi wa Maore wameeleza pia changamoto kubwa inayowakabili wanafunzi wa kike kupata ujauzito pindi wawapo shuleni kuna changiwa na wazazi kushindwa kuwaeleza ukweli  watoto wao kuhusu kuanza mahusiano wawapo shuleni .

Mganga Mkuu wa wilaya ya Same ,Dkt Godfrey  Andrew amesema vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi pamoja na watoto wachanga vimepungua wilayani Same hadi kufikia 15 mwaka huu ukilinganisha na vifo 60 vilivyotokea katika miaka miwili iliyopita ya 2015 na 2016 huku akibainisha mikakati iliyopo ya kupambana na changamoto za upungufu wa watumishi.

Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe kitaifa  (The White Ribbon Alliance ) Rose Mlay amesema  kuwekeza kwa mama mjauzito kunachangia kuzaliwa kwa kijana mwenye afya njema atakayechangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi na kulea maendeleo.

Same ni mojawapo ya wilaya saba zilizoko katika mkoa wa Kilimanjaro zinazokabiliwa na changamoto ya vifo vya akina mama wajawazito vitokanavyo na uzazi huku sababu ya vifo hivyo kwa kina mama ikielezwa kuwa ni Kifafa cha Mimba,kupasuka kwa mji wa mimba na kutokwa na damu nyingi.

CHINA YAAHIDI KUFADHILI UJENZI WA RELI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA (SGR)

0
0
Benny Mwaipaja, Dar es Salaam
BALOZI wa China hapa nchini, Wang Ke amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kushawishi taasisi za fedha ikiwemo Benki ya EXIM ya nchini humo kushiriki ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu wa mradi huo.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa mradi huo, unaokadiriwa utagharimu Dola za Marekani bilioni 7.6 hadi kukamilika kwake, utahitaji kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kukidhi masharti ya kupata mkopo kupitia Benki ya Exim na taasisi nyingine zitakazotaka kujenga mradi huo muhimu. 

“Mradi huu ni muhimu na wa kihistoria kwa nchi hizi mbili, China ingependa kuona mradi huo unaboreshwa ili uweze kutoa huduma ya kusafirisha mizigo na abiria na kwamba kuimarika kwake kutaokoa miundombinu ya barabara kwa kuwa shehena kubwa ya mizigo itasafirishwa kupitia reli hiyo.

Aidha, Balozi Ke alisema kuwa nchi yake inasubiri pia kukamilika kwa taratibu za ndani kati yake na Tanzania ili mradi wa reli ya TAZARA uanze  ili kuboresha usafiri na usafirishaji wa mizigo na abiria kati ya Tanzania na Zambia pamoja na nchi za maziwa makuu.

Balozi Ke alitumia fursa hiyo kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kukusanya kodi, kusimamia matumizi adili ya fedha za umma, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kupambana na rushwa.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo na mgeni wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alisema kuwa Serikali imeridhia uamuzi wa China wa kufanya upembuzi yakinifu wa mradi huo wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) ili China kupitia taasisi zake iweze kujenga sehemu ya mradi huo.

“Tayari mradi umeanza kujengwa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, kwahiyo kujitokeza kwa China kutaka kufadhili ujenzi wa mradi huo kutasaidia kukamilisha mradi huo muhimu kwa haraka na kwa wakati” Alisema Dkt. Mpango.

Alisema pia kuwa China imeonesha nia ya kusaidia kuujenga na kuupanga mji wa Dodoma kutokana na nchi hiyo kuwa na uzoefu wa kupanga miji ambapo nchi hiyo imeonesha nia ya  kujenga miundombinu ya elimu, barabara, uwanja wa ndege wa kimataifa-Msalato, kujenga mfumo wa maji safi na maji taka pamoja na majengo ya kisasa.

Kuhusu biashara, Dkt. Mpango alisema wamekubaliana kuwa China itaisaidia Tanzania kukuza kiwango cha biashara ambapo takwimu zilizoko zinaonesha kuwa urari wa biashara kati ya nchi hizo unaonesha kuwa Tanzania imekuwa ikinunua bidhaa nyingi kutoka nchini humo kuliko inavyo uza bidhaa na huduma zake.

“Mwaka 2016 Tanzania iliuza China bidhaa na huduma zenye thamani ya Dola za marekani milioni 460 wakati China iliuza hapa nchini bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.2, kiwango ambacho ni kikubwa karibu mara 5 ya kile tulichowauzia” Alisema Dkt. Mpango.

Ili kuvutia Sekta ya utalii, Tanzania imeiomba China kuanzisha safari ya ndege wa moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania ili kuvutia watalii wengi kutoka nchini humo na kwamba utaratibu utafanyika ili Mamlaka ya usafiri wa anga iweze iratibu na kusaini makubaliano ya ushirikiano na hivyo kufanikisha jambo hilo.

“China imeandaa maonesho makubwa ya uwekezaji na biashara ya bidhaa na huduma mbalimbali mwezi Novemba, 2018, hivyo wafanyabiashara wa Tanzania pamoja na  Bodi ya Utalii nchini wahakikishe wanashiriki kikamilifu kwenye maonesho hayo ili kutumia nafasi hiyo kujitangaza” Alisistiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango alieleza kuwa Balozi Wang Ke, amesema kuwa Nchi yake itashiriki katika ujenzi wa miradi ya bandari ili kukuza masuala ya usafiri kwa kuboresha bandari za Tanga, Bagamoyo, Kigoma, Bagamoyo, Dar es Salaam, Mtwara na katika Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika.

Waziri huyo wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alitoa wito kwa wawekezaji kutoka China na nchi nyingine kuja kuwekeza nchini katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaipeleka nchi katika uchumi wa viwanda.

Miradi mikubwa ambayo China imewekeza na kufadhili hadi sasa hapa nchini ni Reli ya TAZARA, Kiwanda cha Urafiki, ujenzi wa barabara, majengo, ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi dar es Salaam, Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dare Salaam, Ujenzi wa Mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na miradi mingine kadha wa kadha.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (katikati),  Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke (wa pili kulia), Mwakilishi wa masuala ya Uchumi na Biashara wa Ubalozi wa China Bw. Lin Zhiyong (wa pili kushoto) pamoja na maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango  wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya pande hizo kuhusu Biashara, uwekezaji na ushirikiano, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Kulia) na mgeni wake Bi. Wang Ke, wakitoka nje ya Jengo la Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao uliohusu masuala mtambuka ya ushirikiano kati ya Tanzania na China.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke,  wakiagana   baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao ambapo balozi huyo aliahidi kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kati nchi hizo mbili, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akiagana na Mwakilishi wa masuala ya Uchumi na Biashara wa Ubalozi wa China  nchini Tanzania Bw. Lin Zhiyong baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya Waziri huyo na Balozi wa nchi hiyo Bi. Wang Ke (hayupo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Kamishina wa Fedha za Nje Bw. John Rubuga (kushoto) na Afisa anayeshughulikia masuala ya nje katika dawati la China Bw. Alfonce Mayala kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kwa makini majadiliano kati ya Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke,  na Waziri wa Fedha na Mipango (hawapo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa pili kulia akieleza kuhusu fursa zilizopo katika Sekta ya Utalii wakati wa  Mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam, kulia ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. John Rubuga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa tatu kulia akiwa katika mkutano na  Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke (wa pili kushoto) ambapo walikubaliana kuendeleza ushirikiano katika Biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande hizo mbili, mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akieleza kuhusu kuwa na uwiano wa kibiashara kati ya Tanzania na China kwa manufaa ya pande hizo mbili wakati wa mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China hapa Nchini Bi. Wang Ke, (katikati) akiongoza maafisa wake wa ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini wakati wa mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa China hapa nchini, Bi. Wang Ke, akisisitiza jambo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango)

Rais Magufuli amteua Bi Stelli Chagi kuwa Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba wa Wilaya

0
0

WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA MGENI RASMI MAHAFALI YA 33 YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA

0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda,  baada ya kuwasili kwenye Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania mjini Singida ambapo alikuwa mgeni rasmi, Novemba 30, 2017.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida Novemba 30, 2017. Kushoto ni Mkuu wa Chuo Kikuu hicho na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda.
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (mwenye miwani mbele) akiwa na wahitimu wenzake katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida, Novemba 30, 2017.
 Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamili Katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master Of Education in Administration, Planning and Policy Studies), Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (kushoto) katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida, Novemba 30, 2017. Wapili kulia ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Watatu kulia ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinoloji, Profesa Joyce Ndalichako. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akitelemka kutoka kwenye jukwaa baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili Katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master of Education in Administration, Planning and Policy Studies) na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Waziri Mkuu MStaafu, Mizengo Pinda (kulia)  huku  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishuhudia. 
 Mke wa  Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa   akipokea ua kutoka kwa mwanae, Saad Majaliwa Kassim baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili katika Elimu ya Utawala, Mipango na Sera (Master of Education in Administraion, Planning and Policy Studies) katika Mahafali ya 33 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika mjini Singida Novemba 30, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Viewing all 46194 articles
Browse latest View live




Latest Images