Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46313 articles
Browse latest View live

BENKI YA KILIMO YATEMBELEA MIRADI YA JKT KITEULE CHA BULAMBA, BUNDA

$
0
0
 Afisa Kilimo na Ufugaji wa kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rwamkoma, Kapteni M. Kinana (kulia) akiongea na Ujumbe kutoka Benki ya Kilimo (hawapo pichani) walipotembelea mradi huo uliopo wilayani Bunda. Kushoto ni Msimamizi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha Bulamba, Luteni Kelvin Gondo.
 Maafisa wa Jeshi la Kujenga Taifa wanaotekeleza Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba wakifuatilia mkutano wa pamoja kati ya JKT na Ujumbe kutoka Benki ya Kilimo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bibi Rosebud Kurwijila (kulia) akizungumza wakati walipotembelea Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba uliopo wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Kushoto ni Afisa Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw. Steven Ochieng’.
 Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADB, Bw. Dome Malosha (kulia) akizungumza wakati walipotembelea Mradi wa Ufugaji wa Samaki kwa Vizimba Kiteule cha Bulamba uliopo wilaya ya Bunda, Mkoani Mara. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kushoto) na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Bw. Joseph Mutashubilwa (katikati).
 Afisa Uvuvi wa wilaya ya Bunda, Bw. Steven Ochieng’ (kushoto) akichangia wakati wa mazungumzo hayo. Anayemsikiliza ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kulia).
Msimamizi wa Mradi wa Ufugaji wa Samaki wa JKT Kiteule cha Bulamba, Luteni Kelvin Gondo akitoa maelezo juu ya maendeleo ya ufugaji wa samaki katika hatua mbalimbali.

Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetembelea mradi wa ufugaji wa vifaranga vya samaki unaotekelezwa na kikosi cha 822 Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rwamkoma wilaya ya Butiama kupitia Kiteule chake cha Bulamba, wilayani Bunda.

Akizungumza lengo la ziara hiyo, mkuu wa msafara huo ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila amesema lengo kubwa la kutembelea Mradi huo ni kujionea juhudi za serikali za kuchagiza mapinduzi ya kilimo hasa katika tasnia ya ufugaji na uvuvi wa samaki nchini.

Bibi Kurwijila aliongeza kuwa tasnia ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ni mojawapo ya minyororo ya mwanzo inayopatiwa mikopo kwa ajili ya uongezaji wa thamani mazao na mifugo mbalimbali hasa katika uongezaji wa thamani wa ufugaji wa samaki nchini.

Aliongeza kuwa Benki ya Kilimo imejipanga kuendeleza uongezaji wa thamani wa Ufugaji wa Samaki na uvuvi nchini ili ziweze kuchangia ukuaji wa uchumi nchini.

Mradi huo wa ufugaji wa samaki unaotekelezwa na JKT Wilaya ya Bunda, Kiteule cha Bulamba ulizinduliwa rasmi mwezi Novembea, 2014 kwa kupandikiza vifaranga vya samaki katika vizimba ndani ya Ziwa Victoria.
Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wakiwemo Economic Social Research Foundation (ESRF) na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

Ufugaji wa samaki kwa kutumia teknolojia ya vizimba ndani ya Ziwa Victoria, umekuwa maarufu zaidi katika nchi za Afrika Mashariki ikiwemo Uganda na Kenya ambapo umepunguza kwa kiasi kikubwa uvuvi haramu katika fukwe za ziwa hilo.


NLUPC YAANZA KUREJEA MWONGOZO WA UPANGAJI MATUMIZI YA ARDHI YA WILAYA

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Dkt. Stephen Nindi akielezea kwa ufupi malengo ya warsha kwa ajili ya kurejea mwongozo wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya ardhi ya Wilaya, Mjini Morogoro
 Kaimu Mkurugenzi wa Uratibu,Sera na Mawasiliano wa Tume Bi. Albina Burra akitoa maelezo mafupi kwa Mkurugenzi wa NLUPC Dkt. Stephen Nindi kuhusiana na kazi ya kurejea mwongozo wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya ardhi ya Wilaya.
 Makundi mbalimbali ya wana kikao kazi wakiwa wana rejea mwongozo wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya ardhi ya Wilaya kabla ya kutoa mrejesho
 Bw. Eugine Cylio Mtaalam kutoka NLUPC akitoa mawasilisho kwa niaba kundi lake.
 Bw. Paulo Tarimo kutoka Wizara ya Kilimo akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kusikiliza mrejesho wa majadiliano yaliyokuwa yanaendelea kutoka katika makundi mbalimbali.
 Afisa Programu kutoka Haki Ardhi Bw. Joseph Chiombola akitoa mawasilisho kwa niaba kundi lake.
 Bw. Angolile Rayson kutoka PELUM Tanzania akitoa mawasilisho kwa niaba kundi lake.

Afisa Miradi kutoka TNRF Bw. Daniel Ouma akichangia jambo kuhusu matumizi ya Ardhi na maendeleo endelevu.
 Afisa Sheria wa NLUPC Bi. Devotha Selukele akichangia jambo juu ya 'Participatory Land use Management'  (PLUM)
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Ufugaji Tanzania Bw. Joshua Lugaso (wa pilikulia) akichangia jambo kuhusu wafugaji wakati wa kikao kazi.

 Afisa Takwimu kutoka NLUPC Bi. Blandina Mahudi akichangia jambo kuhusiana na maswala ya Takwimu.

 Baadhi ya watumishi kutoka NLUPC, kuanzia kushoto ni Afisa Mipango Bw. Gerald Mwakipesile, Afisa Sheria Bi. Devotha Selukele, Afisa Tawala Bi. Nakivona Rajabu na Afisa Habari Bw. Geofrey Sima wakati wa Kikao kazi

Tume na wadau mbalimbali  kutoka Serikalini,Asasi za kiraia wamekutana Morogoro kwa ajili ya kutengeneza urejewa mwongozo wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya Ardhi ya Wilaya.

Akizungumza wakati wa mchakato huo Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya mipango na Matumizi ya Ardhi(NLUPC) Dkt. Stephen Nindi alisema kuwa NLUPC  ikishirikiana na Haki Ardhi pamoja na wadau mbalimbali wanaojihusisha na upangaji, utekelezaji  wa usimamizi wa mipango ya ardhi wamekutana kwa ajili ya kuanza kupitia namna ya upangaji wa matumizi ya Ardhi ya Wilaya ambapo mwongozo huo uliandaliwa tangu mwaka 2006.

“Kutokana na mambo mengi  kutokea kwa muda wa miaka kumi na moja (11), ambayo tungependa  yawepo katika muongozo huu wa namna ya kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi ya Wilaya, mambo hayo yaliyojitokeza ni kama mabadiliko ya tabianchi na athari zake kuwa kubwa inayopelekea mabadiliko ya hali ya kimazingira, ushirikishwaji wa jinsia pamoja na makundi mengine madogo madogo mfano watu wanaotegemea mizizi na wanaohama hama toka sehemu moja kwenda sehemu nyengine” Alisema Dkt. Nindi.

Aliongeza kuwa  Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt John Pombe Magufuli anayesisitiza kuwa  Nchi iwe  ya viwanda na uchumi wa kati, na katika muongozo wa kuandaa mpango wa  matumizi ya ardhi ya Wilaya haukuupa msukumo wa viwanda. Mwongozo huu utaangalia utaratibu wa  namna gani  viwanda vitaendelea katika ardhi ya Wilaya na vijiji.

Kutokana na mabadiliko mbalimbali yaliyotokea nchini yakiwomo ya kiuchumi,kisiasa,kijamii,na ndani ya miaka hii kumi na moja kumekuwa na ukuaji wa mashamba ya saizi ya kati ekali 100 hadi 150 umeongezeka ambapo unahitaji muongozo mpya na namna ya kusimamia katika ngazi ya Wilaya,Miji mingi  watu wamezidi kuongezeka ambapo ukuaji huo unaonekana haukutiliwa mkazo wakati wa mwongozo wa awali ulio andaliwa miaka 11 iliyopita,ambapo sasa kuna kasi ya ongezeko ya ukuaji wa miji na vijiji, mwongozo huu utaangalia  namna gani mambo haya yote yataendelezwa vizuri.

Kwa upande wake Afisa Programu kutoka Haki Ardhi Bw. Joseph Chiombola ambao wanajihusisha na utafiti pamoja na utetezi wa maswala ya ardhi alisema kuwa Haki Ardhi ni jukwaa ambalo limekuwa likiendesha mijadala mbalimbali inayohusiana na maswala ya ardhi nchini Tanzania, na kwamba maswala ya matumizi ya ardhi yanahitaji mjadala mpana unaotakiwa kuwahusisha wananchi kwa ujumla.

“Moja ya malengo yetu ni pamoja na kuhakikisha kwamba kunafanyika mabadiliko ya Sera,Sheria,kanuni na miongozo mbalimbali, na hili swala la mipango na matumizi ya ardhi ni sehemu moja tunayo iangalia kwa sababu kama ikiendelezwa ipasavyo itasaidia kuweka ulinzi wa ardhi na wazalishaji wadogo ambayo ndio jukwaa tulilokuwa tukizungumzia sana kwa ajili ya haki zao kwa kipindi chote cha uwepo wetu” alisema Chiombola.

Aliongeza kuwa mipango hii ni muhimu kwa sababu inawagusa wazalishaji wa kila siku wakiwemo wakulima,wafugaji, waokota matunda,warina asali na wavuvi kwa kuwa wamekuwa wanahusika na ardhi kwa namna moja au nyengine. Hivyo mipango itakayokuwa kwa manufaa ya jamii hizo itakuwa na manufaa makubwa katika kuongeza kipato chao na kubadilisha hali ya maisha yao. 

Nae Naibu Katibu Mkuu wa wa Chama cha Wafugaji Tanzania Bw. Joshua Lugaso alisema kuwa kutengeneza urejewa mwongozo wa upangaji,utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya Ardhi ya Wilaya utakuwa ni mkombozi kwa mfugaji kutambulika katika maswala ya ardhi Tanzania jambo ambalo halijawahi kutokea kwa miaka mingi.

“Katika mwongozo huu mfugaji ameonekana sana na kuondoa dhana ya kila wakati wakulima kuonekana, tunaamini kwamba ni mpango unaoenda kufanya kazi  kwenye Wilaya tunaamini kwamba ikisimamiwa vizuri, migogoro ya wafugaji na wakulima itakwisha” alisema Lugaso.

Katika mwongozo  uliopita kulikuwa na mapungufu ambayo ni  pamoja na mkazo wa namna ya jamii zinavyokabiliana na mabadiliko ya Tabianchi haukuwa na mkazo mkubwa,hakukuwa na mkazo wa namna ya ardhi za Wilaya zinavyopangwa ili kuhakikisha kwamba kunakuwa kuna ukuwaji wa viwanda katika ardhi ya wilaya au ya vijiji, pia swala la ushirikishwaji katika upande wa jinsia na makundi madogo madogo wanaotumia ardhi ambao katika jamii hawana nguvu ya kisiasa,kiuchumi  kwa kuwa na wao wanatakiwa watambuliwe.

WAZIRI UMMY AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA KUANZISHA ZOEZI LA WAZI LA UCHUNGUZI WA SARATANI YA KIZAZI KWA WANAWAKE

$
0
0
 Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  leo jijini Dar es salaam .
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya vifaa vya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam.
 Waziri  wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akipokea moja ya nyenzo za  kufundishia juu ya uchunguzi wa saratani ya kizazi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran (kushoto) wakati wa makabidhiano ya vifaa vya kuchunguza saratani ya kizazi leo jijini Dar es salaam katikati ni Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .
 Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  leo jijini Dar es salaam .
Waziri  wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa  Wizara ya afya, Jpiego na USAID wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  leo jijini Dar es salaam wa tatu kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran na aliyevaa nguo ya pundamilia ni Afisa Afya kutoka USAID Bi. Ananth Thambinygan .picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

NA WAMJW-DAR ES SALAAM.

WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu amewaelekeza waganga wakuu wa mikoa yote nchini kuanzisha zoezi la wazi la uchunguzi wa saratani ya kizazi angalau mara moja katika mwezi ili kusaidia kutokomeza tatizo kwa wanawake hilo nchini.

Hayo amesema wakati wa kupokea vifaa vya kuchunguza saratani vyenye thamani ya shilingi milioni 98  ambavyo vimetolewa na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya JHPIEGO kwa kushirikiana na USAID ili kusaidia kupambana na tatizo hilo nchini.

“Angalau ifikapo Desemba 2018 nataka  vituo vya Afya vya Serikali  524  viwe vinatoa huduma ya matibabu ya awali ya Saratani ya mlango wa kizazi na kufikia  wanawake milioni 3 watakaopata huduma hii ili kuokoa wanawake wa vijijini  kwani mpaka sasa hivi tunavyo vituo vya afya  265 vinavyotoa huduma hii ” alisema Waziri Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa uchunguzi na kutoa chanjo ya Saratani ya mlango wa kikazi  kwa wasichana kuanzia miaka 9 mpaka 14 ili kuweza kupunguza vifo vitokanavyo na tatizo hilo kwani katika kila wanawake 100 vifo vinavyotokana na ugonjwa huo ni 32.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa katika kuongeza jitihada za  kupambana na ugonjwa huo Serikali imeongeza vituo vya afya 100 kutoka 343  hadi kufikia 443 mwaka huu ili kutokomeza tatizo hilo nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchini Tanzania Bw. Jeremia Zoungran amesema kuwa walianzisha mpango wa kupambana na tatizo hilo na kufanikiwa kuwafikia wanawake elfu 75 kwa mikoa 4 tangu mwaka 2009.

“Mbali na mikoa hiyo 4 bado tunalengo la kuongeza mikoa mingine 7 ili kuweza kutoa huduma hiyo kwa ajili ya kuunga mkono Juhudi za Serikali katika kupambana na Saratani ya mlango wa kizazi ili kuweza kuokoa wanawake wengi zaidi nchini” alisema Bw. Zoungran.

Article 0

$
0
0
Jeshi la Polisi likiwa limezungushia utepe eneo ambalo kuna kaburi ulimozikwa mwili ambao familia ya Mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo aliyepotea ,Humphrey Makundi ulitilia shaka.
Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyezikwa na Manispaa ya Moshi baada ya kuokotwa Mto Ghona jirani na ilipo shule ya Sekondari .
Askari Polisi wakishirikiana na ndugu wa Mwanafunzi aliyepotea Humphrey Makundi wakifukua Kaburi ulimozikwa mwili wa mtu aliyeokotwa Mto Ghona katika wilaya ya Moshi.
Kaburi likifukuliwa.
Baba mzazi wa Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Scolastica aliyepotea,Jackson Makundi (Katkati) akijadili jambo na wanandugu wakati zoezi la kufukua kaburi likiendelea.
Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akitizama mwili (haupo pichani) baada ya kaburi kufukuliwa.
Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akionekana akiwa amekaa chini baada ya kutizama mwili uliofukuliwa katika kaburi .
Askari Polisi na Wanandugu wa kijana aliyepotea wakijaribu kusaidia kumnyanyua mzazi wa Mwanafunzi huyo kutoka katika eneo lilipo kaburi lililofukuliwa .
Baba mzazi wa Mwanafunzi Humphrey ,Jackson Makundi (Mwenye suti nyeupe) akisindikizwa kutoka katika eneo la Makaburi ya Karanga katika manispaa ya Moshi.
Mwili uliofukulia katika Makaburi hayo ukiwekwa katika gari la Polisi kwa ajili ya kwenda kuhifadhiwa katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC.
Gari la Polisi likiwa na mwili uliofukuliwa katika Makaburi ya Karanga.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

 UTATA umeighubika familia ya Jackson Makundi ambayo kijana wake aliyetambulika kwa jina la Humphrey Makundi,Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Scolastica iliyopo mji mdogo wa Himo kupotea katika mazingira tatanishi.

 Utata wa kupotea kwa mwanafunzi huyo unatiliwa shaka zaidi na familia hiyo baada ya kufukuliwa kwa kaburi ulimozikwa mwili uliookotwa mto Ghona mita 300 ,jirani na shule hiyo ukidaiwa kushabihiana na wa mwanafunzi huyo

  Humphrey Makundi, mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari ya Scolastica anatajwa kupotea tangu Novemba 7 mwaka huu akiwa shuleni hapo huku wanafunzi wenzake wakiendelea na mitihani ya kidato cha Pili ya upimaji ya kitaifa .

 Familia ya kijana huyo yenye makazi yake mkoani Dodoma ikalazimika kutumia mitandao ya kijamii kutoa taarifa za kupotea kwake ikidai mazingira ya kutoweka kwake ni ya kutatanisha na baadae kuwasilisha taarifa katika kituo cha Polisi cha Himo .

Kutokana na kuwepo kwa taarifa za kuokotwa kwa mwili huo ,familia iliwasilisha maombi katika mahakama ya Hakimu Mkazi, Moshi na mahakama ikaamuru kufukuliwa kwa Kaburi hilo zoezi lililoanza majira ya saa 8:30 mchana na kudumu kwa zaidi ya saa moja.

Jeshi la Polisi liliongoza zoezi hilo katika makaburi ya Karanga huku likishuhudiwa na ndugu wa mtoto aliyepotea ambapo baada ya mwili kutolewa kaburini hali ya simanzi ilionekana katika nyuso za baadhi ya ndugu wa Mwanafunzi huyo akiwemo baba mzazi wa kijana huyo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa akathibitisha uwepo wa tukio hilo huku akieleza kuwa tayari jeshi la Polisi linawashikilia wati 11 akiwemo mmiliki wa shule hiyo Edward Shayo huku likifanya uchunguzi wa kina kuhusu matukio hayo mawili.

Mwili uliofukuliwa katika makaburi ya Karanga upande wa marehemu wasiokuwa na ndugu ulipelekewa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya KCMC kwa uchunguzi zaidi chini ya uangalizi wa jeshi la Polisi wakishirikiana na madaktari kutoka  KCMC.

Rais Magufuli hajatengua utengua uteuzi wa Dkt. Laurian Ndumbaro

MOI YAOKOA BILIONI 5 KWA KUPUNGUZA RUFAA ZA NJE YA NCHI.

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akizungumza na menejimenti ya MOI (hawapo pichani) katika ukumbi wa Mikutano wa MOI.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akimjulia hali mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji mkubwa wa mgongo, anayetoa ufafanuzi wa namna upasuaji huo ulivyofanyika ni Dkt. Nicephorus Rutabansibwa (Daktari bingwa wa Upasuaji wa Ubongo na Mgongo). Kushoto ni Mganga mkuu wa Serikali Profesa Muhamed Kambi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akikagua mashine mojawapo katika benki ya damu ya MOI.
Mtaalamu wa Maabara Bwana Mbuta Jackson akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya kuhusu namna benki mpya ya damu inavyofanya kazi kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa damu salama.
Watumishi wa MOI wakifuatilia hotuba ya katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto ( Sekta ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya (hayupo pichani) katika ukumbi wa Mikutano MOI.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akitoa maelekezo alipokua anakagua maeneo ya utoaji huduma katika jingo jipya la MOI (MOI phase III).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya ( katikati ) akiwa katika picha ya pamoja na menejimenti ya MOI.( Picha zote na MOI ).

……………………………………………………………………………..

Patrick Mvungi- MOI

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) imeokoa zaidi ya shilingi Bilioni 5 ambazo zingetumika kusafirisha wagonjwa nje ya nchi kufuata matibabu baada ya MOI kuanzisha huduma za kibingwa ambazo awali zilikua hazipatikani hapa nchini.

Hayo yamebainishwa katika ziara ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya alipotembelea MOI na kukagua hali ya utoaji wa huduma, mazingira , miundombinu na kuwajulia hali wagonjwa pamoja na kukutana na menejimenti.

Akizungumza na menejimenti ya MOI, Dkt. Ulisubisya amepongeza kazi nzuri na kubwa inayofanywa ambayo imepelekea watanzania kupata huduma bora za kibingwa ambazo wangepaswa kuzifuata nje ya nchi.

“Mnafanya kazi nzuri sana, jambo ambalo linatupa faraja kubwa sisi viongozi wenu, naomba muongeze ubunifu zaidi, hamtakiwi kuifikiria MOI kwenye ukanda huu wa Afrika pekee bali duniani, hii ni changamoto kwetu sote kuifikisha hapo ”alisisistiza Dkt. Ulisubisya

Aidha, Dkt Ulisubisya amesema MOI imepunguza rufaa za kwenda nje ya nchi kwa asilimia 95% na asilimia 5% iliyobaki MOI inaweza kuimaliza kabisa na kusiwepo mgonjwa wa kwenda nje ya nchi.

Pia, amewaelekeza viongozi wa MOI kushirikiana na Wizara ya Afya kutafuta namna ya kufuta rufaa kwa kutoa mapendekezo na ushauri utakaosaidia kutatuliwa kwa changamoto hiyo.

“Azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt John Pombe Magufuli ni kuhakikisha huduma zote za Afya zinapatikana hapa nchini na vyema sote tukamuunga mkono” amebainisha Dkt. Ulisubisya.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Muhamed Kambi amepongeza uongozi wa MOI kwa kuwa na maono ya mbali ya kuifanya MOI kuwa Taasisi bora barani Afrika na Duniani.

“Nimefurahi kwamba MOI mna maono ya mbali, mnafikiria kuitoa Taasisi hii hapa ilipo na kuifikisha sehemu ya juu zaidi, dira yenu ni kuwa Taasisi bora Afrika kufikia 2022 fanyeni kazi kwa bidii kufikia lengo hilo.” amesema Prof Muhamad Kambi

Awali akiwasilisha taarifa ya Utendaji, Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt Respicious Boniface amesema toka kuanzishwa kwa Taasisi hiyo imefanikiwa kuanzisha huduma za kibingwa za Upasuaji wa Nyonga, Magoti, Ubongo, Mgongo, Vibiongo, Usingizi ambazo zimesaidia kupunguza rufaa za nje ya nchi.

“Baada ya kuanzisha huduma hizi za Kibingwa tumefanikiwa kuokoa shilingi Bilioni 5 ambazo zingetumika kuwapeleka wagonjwa nje ya nchi, tumepunguza rufaa kwa asilimia kubwa naomba nikuhakikishie hata hizi asilimia 5% zilizobaki tutashirikiana na Serikali na naamini zitakwisha kabisa.” amesema Dkt. Respicious Boniface.

Wabunge wawapongeza NSSF, PPF na magereza mradi wa kiwanda cha sukari cha Morogoro

$
0
0
KAMATI ya Bunge ya Katiba na Sheria imepongeza namna mifuko ya hifadhi ya jamii ya NSSF na PPF inavyotekeleza mradi wa pamoja wa ujenzi wa kiwanda cha sukari unaofahamika kama Mkulazi huku ikitoa wito kwa wadau hao kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kwa wakati ili kulinusuru taifa na uhaba wa bidhaa hiyo.

Mwisho mwa wiki kamati hiyo ilitembelea mradi huo unaotekelezwa katika gereza la Mbigiri, lililopo Dakawa mkoani Morogoro kupitia kampuni Hodhi ya Mkulazi Holding inayoshirikiana na Jeshi la Magereza nchini.

"Baada ya kusikiliza mpango mikakati na kisha kutembelea shamba husika kiukweli kamati yetu imeridhishwa sana na jinsi wadau hawa wanavyotekeleza mradi huu. Ni wazi kuwa walifanya utafiti wa kutosha kabla na matunda yake kiukweli yameanza kuonekana kikubwa tu tunachowaomba wamalize mradi huu kwa wakati .'' alisisitiza  Mwenyekiti wa kamati hiyo Bw Mohamedi Mchengelwa.

Aidha, wajumbe wa kamati hiyo walionyesha kuridhiswa zaidi na namna mradi huo unavyohusisha wananchi walio jirani na maeneo ya mradi ambao mbali na kupata ajira za moja kwa moja pia wamepatiwa fursa ya kulima miwa ili kukiuzia kiwanda hicho, hatua waliyosema kuwa itapunguza tatizo la ajira na kuongeza kipato cha wananchi.

"Kingine kikubwa zaidi kwa wadau hawa ni kuhakikisha kuwa mradi huu hauishii kwenye kuzalisha sukari tu bali pia bidhaa zitokanazo na mabaki ya malighafi za miwa ikiwemo ethanol, vyakula vya mifugo pamoja na uzalishaji wa nishati umeme,'' alisema mjumbe Selemani Zedi huku akiungwa mkono na wenzie akiwemo Mbunge wa Wawi Ali Salehe.

Akijibu baadhi ya hoja za wabunge hao ambao pia walitaka kufahamu uwezekano wa mifuko hiyo kuwekeza kwenye sekta ya uvuvi hapa nchini  Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  alisema uwezekano huo upo ikiwa mamlaka zinazosimamia mifuko hiyo zikiwemo bodi pamoja na Mamlaka ya usimamizi na udhibiti wa sekta ya hifadhi ya jamii (SSRA) zitaridhia miradi hiyo kwa kuangalia vigezo muhimu.

"Ili kuwekeza kwenye miradi mikubwa kama hii inahitaji ruhusa za mamlaka mbalimbali zinazosimamia mifuko hiyo kwa kuwa mamlaka hizo pia zinahitaji kujiridhisha pasipo kuacha chembe ya shaka kuwa utekelezaji wa miradi hii haihatarishi fedha za wanachama japo habari njema ni kwamba kati ya miradi 27 inayotarajiwa kutekelezwa na mifuko hii tayari miradi 15 imepatiwa ruhusa ya utekelezwaji na mamlaka hizi,'' alisema.

Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.William Erio, waliihakikishia kamati hiyo, serikali, wananchama na wadau wote wa mifuko hiyo kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwaka ujao mradi huo utakuwa tayari umeanza kuzalisha sukari pamoja na baadhi ya bidhaa ambatanishi kulingana na wito wa wabunge hao.

"Mradi huu mliotembelea leo unaolenga kuzalisha tani 50 za sukari kwa mwaka na ni sehemu tu ya mradi mkubwa unaotekelezwa na mifuko yetu miwili yaani NSSF na PPF ukiwepo mwingine mkubwa zaidi katika eneo la Ngerengere, Wilaya ya Morogoro Vijijini unaofahamika kama Mkulazi I ambao unaolenga kuzalisha tani 200,000 za sukari kwa mwaka,'' alisema Prof Kahyarara.

"Zaidi tuwahakikishie tu waheshimiwa wabunge kuwa hoja zenu tumezipokea na tutasimamia kuhakikisha kwamba mradi huu unakamilika kwa wakati na zaidi si tu kwamba tutalisha soko la ndani bali pia soko la nje hususani mataifa jirani ya Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,'' aliongeza Bw Erio.

Naye Mwakilishi wa jeshi la Magereza, Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro (RPO), Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP)Mzee Nyamka mbali na kuishukuru mifuko hiyo pia alitoa wito kwa mifuko mingine ya hifadhi ya jamii pamoja na  wadau wengine kujitokeza ili kushirikiana na Jeshi hilo katika utekelezaji wa miradi mingine huku akibainisha kuwa jeshi hilo lina eneo kubwa la ardhi pamoja na nguvu kazi ya kutosha.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk Stephen Kebwe alisema mkoa wake umekuwa ukiupa kipaumbele kikubwa mradi huo kuwa utekelezaji wake pamoja na mambo mengine unalenga kuongeza ajira kwa wananchi wa mkoa huo na kupunguza kabisa kasi ya mfumuko wa bei ya sukari kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa hiyo muhimu. 
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  (wa tatu kulia) akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria  kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria Bw Mohamedi Mchengelwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba kubwa la miwa lililopo katika gereza la Mbigiri lililopo Dakawa mkoani Morogoro ambalo ni sehemu ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha sukari kinachojengwa kwa ubia kati ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya NSSF, PPF na jeshi la Magereza nchini.
 Waziri wa Kazi, Ajira, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu, Jenista Mhagama  akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Mkulazi ambae pia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua shamba hilo. Kwa mujibu wa Prof. Kahyarara hadi kufikia mwishoni mwa mwaka ujao mradi huo utakuwa tayari umeanza kuzalisha sukari pamoja na baadhi ya bidhaa ambatanishi ikiwemo uzalishaji wa umeme.


WAKAZI WA MKOA WA DAR ES SALAAM WAJITOKEZA KUPATA HUDUMA KATIKA MELI YA CHINA


IGP SIRRO AKUTANA NA BALOZI WA CHINA NCHINI

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kulia), akizungumza na balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke, alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi hilo leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujitambulisha tangu alipoteuliwa kuwa Balozi hapa nchini. Picha na Jeshi la Polisi.
 Balozi wa  China nchini Mhe. Wang Ke, akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (kulia), alipomtembelea ofisini kwake Makao Makuu ya jeshi hilo leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujitambulisha tangu alipoteuliwa kuwa Balozi hapa nchini na kuahidi serikali ya nchi yake itaendelea kushirikiana na jeshi hilo. Picha na Jeshi la Polisi.

Waziri Kairuki, Benki ya Dunia Wajadili Rasilimali Madini

$
0
0


Na Rhoda James, DSM

Waziri wa Madini Angellah Kairuki mwishoni mwa wiki alikutana na Ujumbe wa Benki ya Dunia jijini Dar es Salaam kwa lengo la kufahamiana na kuangalia hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa Miradi ya Madini inayotekelezwa kupitia Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) unaofadhiliwa na Benki hiyo kwa kushirikiana na Serikali.

Pamoja na mambo mengine yaliyojadiliwa katika kikao hicho, Waziri Kairuki aliitaka Benki ya Dunia kuona namna ya kuwaendeleza Wataalam wa Sekta ya Madini ili kuwezesha uwepo wa Watalaam wa kutosha hususan katika masuala ya Uthaminishaji wa Madini ya Almasi, tanzanite na madini mengine ya vito na pia masuala ya uongezaji thamani madini kwa ujumla.

Pia, alishauri umuhimu wa kuboreshwa kwa Mtandao wa Huduma za Leseni kwa Njia ya Mtandao (Online Mining Cadastre) ikiwa ni pamoja na kuunganisha mtandao huo na Mamlaka nyingine ikiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) ili taarifa zote zinazohusu madini na mapato yatokanayo na madini ziweze kupatikana kupitia mtandao huo.

Vilevile, aliishauri Benki hiyo kuhusu uuzwaji wa Madini ya Almas kwa njia ya Mnada kama vile inavyofanyika kwa Madini ya Tanzanite, lengo likiwa ni kuwezesha Serikali kunufaika na madini hayo.

Aliongeza kuwa, baada ya Serikali ya Tanzania kupitisha Marekebisho ya Sheria ya Madini kupitia Sheria ijulikanayo kama (The written laws (Miscellaneous Amendements) Act, 2017), alisema kuwa, baadhi ya wawekezaji wameonesha wasiwasi kuhusu marekebisho hayo.

Hivyo, Waziri Kairuki amewataka wawekezaji kutokuwa na hofu kwani mabadiliko hayo yanalenga kuhakikisha kuwa Serikali inanufaika ipasavyo kutokana na rasilimali zake za madini. Aidha,alisema kwamba, nia ya Serikali kuhusu kuvutia wawekezaji iko palepale ilimradi wazingatie Sheria na taratibu.

Vilevile, Waziri Kairuki alieleza kwamba, ni vema Benki ya Dunia ikaangalia namna bora ya kuhakikisha madini yote ya Tanzanite yanayouzwa nje ya nchi yanakuwa na Hati ya Uhalisia inayoonyesha chanzo cha madini hayo suala ambalo litawezesha Taifa kupata mapato stahiki kutokana na rasilimali hiyo.

Vievile, Waziri Kairuki alizungumzia suala la udhibiti wa utoroshaji madini na kusisitiza kuhusu kuwepo na namna bora ya kuzuia utoroshwaji wa madini ya Tanzanite ikiwemo kujulikana kwa idadi ya wachimbaji wadogo, wa kati, kiasi kinachopatikana na mahali madini hayo yanapouzwa. 

Pia, Waziri Kairuki aliishukuru Benki ya Dunia kutokana na ushirikiano ambao umekuwepo baina ya Serikali kwa kipindi chote na kueleza kuwa, Serikali iko tayari kutekeleza miradi husika kikamilifu kwa lengo la kukuza uchumi wa nchi.

Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Profesa Simon Msanjila aliiomba Benki ya Dunia kuleta Wataalam wa madini nchini ili waweze kutoa mafunzo katika vituo vya Madini nchini ikiwemo Chuo cha Madini Dodoma (MRI) na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) ili kuzalisha wataalam zaidi katika Sekta hiyo.

Kwa upande wake, Kamishna wa Madini Tanzania Mhandisi Benjamin Mchwampaka alisema kuwa, tayari Serikali imefanya jitihada kadhaa za kuanzisha mfumo wa utoaji wa leseni kwa njia ya Mtandao. Aliongeza kuwa, kinachotakiwa sasa ni kuimarisha zaidi mfumo huo ili taarifa zote zinazohitajika na umma zinazohusu madini na mapato ya kodi na mrabaha ziweze kupatikana kwa urahisi na kwa uhakika.

Aidha, Kamishna Mchwampaka aliiomba Benki ya Dunia kukijengea uwezo zaidi Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kilichopo jijini Arusha ili kiweze kutoa mafunzo ya Utambuzi wa madini na Uongezaji thamani kwa viwango vya Kimataifa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia Bella Bird alisema zipo fursa nyingi kwa Sekta ya madini na hivyo kuiomba Wizara ya Madini kuhakikisha kuwa inatumia fedha zilizopo katika miradi husika na kwa wakati.

Naye, Mwakilishi Mwandamizi Mradi kutoka Benki ya Dunia ambaye pia ni Mtaalamu wa Madini kutoka Idara ya Nishati Endelevu nchini Merekani, Mamadou Barry, alisema kuwa, Wizara ya Madini ihakikishe kuwa inakamilisha ujenzi wa Kituo cha Madini kinachotarajiwa kujengwa eneo la Mererani kwa wakati ili kuwezesha minada ya madini na maonesho ya madini kufanyika kwenye kituo hicho, na hivyo kudhibiti utoroshwaji wa madini.

Kwa upande wake, Mtaalamu wa Masula ya Madini kutoka benki hiyo Sheila Khama aliishauri Serikali ya Tanzania kuona namna ya kushirikiana na nchi nyingine kama Afrika Kusini hususan kwenye Mikutano ya Uwekezaji madini ya Indaba ili kuendelea kuwavutia wawekezaji.

Aidha, alishauri Tanzania kujifunza kutoka nchi ya Ethiopia kuhusu namna ya kudhibiti Wachimbaji Wadogo wa madini ya dhahabu kwa kuwa, nchi hiyo unao mfumo bora Barani Afrika.

Pia, alisisitiza kuhusu umuhimu wa ushirikishwaji wa wanawake katika shughuli za madini nchini.


MWANJELWA AMNADI MGOMBEA UDIWANI KATA YA IBIGI, APOKEA WANACHAMA WAPYA 21

$
0
0

Na Mathias Canal, Mbeya

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo amewasihi wananchi kwa kauli moja kuchagua kiongozi makini anayetokana na CCM.

Mhe Mwanjelwa alisema kuwa kumchagua diwani wa CCM ni dalili nzuri ya kumpongeza na kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anazozifanya kwa muktadha wa kuwaletea maendeleo watanzania wote.

Mjumbe huyo wa NEC, aliyasema hayo Leo Novemba 20, 2017 katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Bujinga A na B kilichopo Kata ya Ibigi, Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya ambapo alimnadi mgombea Udiwani wa Kata hiyo Bi Suma Ikenda Fyandomo.

(Mnec), Mhe Mwanjelwa aliwakumbusha wananchi waliojitokeza katika mkutano huo kuwa Hawachagui ilani mpya Bali wanachagua Diwani kwa ajili ya kutekeleza ilani ya Ushindi ya CCM ya Mwaka 2015-2020 ambayo wananchi waliiamini na kuichagua Octoba 25, 2015.

Alisema kuwa nchini Tanzania hakuna chama chenye uwezo wa kuwaletea maendeleo wananchi Bali Chama Cha Mapinduzi pekee ndicho chenye uwezo na jukumu la kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.

Katika Mkutano huo wanachama 21 walivutiwa na hotuba ya Mjumbe huyo wa Halmashauri kuu ya CCM wakati akimnadi mgombea hivyo kufanya maamuzi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na CCM ambapo wameahidi kushirikiana na mgombea udiwani wa CCM ili kuhakikisha anashinda kwa kishindo.

Ushiriki wa kampeni hizo katika Kata ya Ibigi unajili wakati ambapo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo pamoja na mambo mengine Kesho Disemba 21, 2017 atashiriki ufunguzi wa Mkutano wa Makatibu Tawala na washauri wa kilimo wa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini juu ya mfumo wa ununuzi wa mbolea (BPS).

Mkutano huo utafanyika katika Ukumbi wa Benjamini Mkapa Jijini Mbeya.


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017. Picha Zote Na Mathias Canal
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akimvalisha kofia ya CCM kijana aliyehama Chadema wakati wa kampeni za Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe Mary Mwanjelwa (Mnec) ambaye ni Naibu Waziri wa kilimo akifurahi na wananchama wa CCM wakati wa mkutano wa kumnadi Mgombea Udiwani Kata ya Ibigi Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya Bi Suma Ikenda Fyandomo, Jana Novemba 20, 2017.

MEYA WA JIJI LA TANGA APOKEA VIFAA TIBA KUTOKA KUWAIT

$
0
0
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem (kushoto) akimkabidhi mabeseni 50 yenye vifaa tiba kwa ajili ya akina mama wajawazito na watoto wachanga, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhina Mustapha Selebosi ,kulia 
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem atia saini katika kitabu cha wageni mara alipowasili katika uzinduzi wa Kisima 
Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem akizungumza wakati wa uzinduzi huo

Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem amezindua visima sita vya maji safi na salama katika Mkoa wa tanga mwisho wa wiki ikiwemo shule ya Old Tanga Secondary School vilivyochimbwa na Jumuiya ya Direct Aid ya Kuwait ikiwa ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi huo




















Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem amezindua visima sita vya maji safi na salama mwisho wa wiki katika Mkoa wa tanga ikiwemo shule ya Old Tanga Secondary School vilivyochimbwa na Jumuiya ya Direct Aid ya Kuwait ikiwa ni mwendelezo wa mradi ulioanzishwa na Ubalozi wa Kuwait nchini unaofahamika kwa jina la “KISIMA CHA MAJI KATIKA KILA SHULE”, uzinduzi ambao ulihudhuriwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mhina Mustapha Selebosi, walimu, wanafunzi na wadau mbalimbali.

Aidha Balozi wa Kuwait alitembelea kituo cha afya cha Ngamiani ambapo alimkabidhi Mstahiki Meya wa Tanga mabeseni 50 yenye vifaa tiba kwa ajili ya akina mama wajawazito na watoto wachanga, mabeseni ambayo ni msaada kutoka taasisi ya Red Crescent ya Kuwait. Akiwa mjini Tanga Balozi Al-Najem alihudhuria mahafali ya kuhitimu wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Kheri ya wanawake.

Kwa upande wake Meya wa Tanga aliushukuru Ubalozi wa Kuwait nchini kwa msaada huo na akamuomba Balozi wa Kuwait pia aweze kusaidia katika shule za jiji hilo 98 za msingi na 32 za sekondari Rkupata huduma ya visima vya maji.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMANNE LEO NOVEMBA 21,2017

CHUO CHA MAFUNZO YA KIJESHI MONDULI CHAZINDUA KOZI MPYA YA SAYANSI YA KIJESHI

$
0
0
Na Pamela Mollel,Monduli

Katibu Mkuu wa wizara ya ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dokta Florens Turuka amesema kuwa jeshi hilo hivi sasa limejipanga katika kukabiliana na changamoto za ulinzi na usalama kwa
kuwapatia askari wake mafunzo maalumu ya sayansi ya kijeshi. 

Aliyasema hayo Jana wakati akizungumza katika uzinduzi wa shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi inayotekelezwa na chuo cha uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA). 

Alisema kuwa, kumekuwepo na matishio mengi ambayo yamekuwa yakijitokeza Kwa namna tofauti ambapo hivi sasa matishio hayo yamegeuka na kuhamia kwenye mitandao, hivyo kama jeshi wana wajibu wa kujipanga zaidi kwa kuwaandaa maaskari ili waweze kukabiliana na hali hiyo mahali popote. 

Dokta Turuka alisema kuwa, wao Kama jeshi ni wajibu wao kujipanga mapema kwa kuangalia namna ya kuwajengea uwezo hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia ili kuboresha ulinzi na usalama hapa nchini. 

Kwa upande wa Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo alisema kuwa wamekuwa wakitoa mafunzo hayo kwa maaskari wake kulingana na mabadiliko ya kidunia hasa katika maswala ya sayansi na teknolojia kwani ni eneo ambalo linahitaji elimu kubwa zaidi.  Alisema kuwa, ni lazima wasonge mbele na kwenda na wakati kwani wasipofanya hivyo watabaki nyuma na kamwe hawataweza kukabiliana na vitisho vilivyopo hivi sasa. 

Naye Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA), Dokta Paul Massao alisema kuwa, wamekuwa wakitoa masomo ya kijeshi na kiraia ili kuwaandaa vijana katika hatua ya ngazi za juu zaidi kielimu ambapo kwa kuanzia kozi hiyo watahiniwa 158 wataanza kozi hiyo mapema. 

Kwa upande wa Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi alisema kuwa, mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia ambayo yamekuwa yakileta manufaa makubwa Sana. 
Katibu Mkuu Wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Florens Turuka akisalimia na Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddy Kimanta mara baada ya kuwasili katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Mondoli(TMA) kwa ajili ya uzinduzi wa shahada ya kwanza ya mafunzo ya Sayansi ya kijeshi
iliyofanyika chuoni hapo leo(Picha na Pamela Mollel Arusha)
Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Tanzania Jenerali Vanance Mabeyo akisalimiana na Kaimu Mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha Dokt Faraji Kasidi, katikati ni Mkuu wa chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA), Dokta Paul Massao 
Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Florens Turuka akisalimia na Meja Jenerali Othman mara ya kuwasili katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Mondoli(TMA) kwa ajili ya uzinduzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo.
Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa Florens Turuka akisalimiana na Dr. Adolf B. Rutayuga ambaye ni kaimu mtendaji mkuu wa NACTE.
Katibu mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa Florens Turuka akizungumza katika uzinduzi wa uzinduzi wa shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo
Mkuu wa majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo akitoa hotuba fupi katika halfa ya uzinduzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo
Meja jenerali Paul Peter Masao ambaye ni mkuu wa chuo cha mafunzo ya maafisa wanafunzi jeshi la ulinzi la Tanzania(TMA).
Mwenyekiti wa Bodi ya chuo cha uhasibu Arusha Bi.Rukia Adam akisoma maelezo mafupi juu ya uzinduzi wa wafunzo ya shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi inayotekelezwa na chuo cha uhasibu Arusha kwa kushirikiana na Chuo cha mafunzo ya kijeshi Monduli (TMA). 
Kaimu mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha, Dokta Faraji Kasidi akizungumza katika uzinduzi huo ambapo alisema mahusiano kati yao na chuo hicho cha kijeshi yameanza muda mrefu ambapo wao wamekuwa wakifundisha askari hao mafunzo ya kiraia.
kushoto aliyevalia suti ni Profesa Johannes Monyoambaye aliwahi kuwa mkuu wa chuo cha uhasibu Arusha(IAA)
Wanafunzi wa mafunzo ya shahada ya kwanza ya Sayansi ya kijeshi iliyofanyika chuoni hapo leo
Maafisa wa jeshi wakitumbuiza wata wa uzinduzi wa wafunzo ya sayansi ya kijeshi.
Picha ya pamoja

USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA WAENDELEA MBEYA

$
0
0
Mamlaka ya Vitambuisho vya Taifa (NIDA) inaendelea na zoezi la Usajili na Utambuzi wa watu mkoani Mbeya ambapo wananchi wengi wamejitokeza ambapo kwa sasa usajili unaoendelea niwa mkupuo (mass registration) ambapo wananchi wanakusanyika kwenye mitaa na vijiji wanakoishi kusajiliwa ambapo Usajili huo unahusisha ujazaji fomu, uchukuaji alama za vidole picha na saini ya kielektroniki. 

Akitoa elimu kwa umma kuhusu taratibu za Usajili mwakilishi wa kitengo cha Mawasiliano NIDA Bw. Deodatus Alexander Mchaki amesema zoezi hilo ni fursa ya kipekee kwa wananchi kutambuliwa na kusajiliwa.

Amesisitiza zoezi la usajili ni Bure na wananchi hawatakiwa kutozwa gharama zozote Ili kusajiliwa mwananchi ni lazima afike na nakala (photocopy) ya nyaraka/viambatisho vifuatavyo kuthibitisha Umri, Uraia na Makazi yake ikiwemo cheti cha kuzaliwa, Passport (Pasi ya kusafiria), Kadi ya kupigia kura, leseni ya udereva, ID ya Mzanzibar mkazi, TIN, Pasi ya kusafiria na vyeti vya elimu.
Mmoja wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete akiweka saini kwenye mashine maalumu ya uchukuliaji alama za kibaiolojia, picha na saini ya kielektroniki.
Wanaoonekana kwenye picha ni Baadhi ya Maafisa Usajili wa NIDA wakiendelea na zoezi la kuwasajili wananchi wa Kata ya Mwakidete mkoani Mbeya. Kushoto ni Afisa Usajili Wilaya ya Mbeya Bi. Alavuya Ntalimwa akitabasamu jambo na wananchi wa Mtaa wa Mwakidete.
Mwananchi akichukuliwa alama za Vidole na afisa Usajili wa NIDA wakati zoezi la kuwasajili wanannchi likiendelea. 
Msururu wa wananchi wa Mtaa wa Mwakidete wakisubiri huduma ya usajili.
Wananchi wa Kata ya Mwakidete mtaa wa Mwakidete mkoani Mbeya wakiendelea na Usajili Vitambulisho vya Taifa.


UJENZI MAGOMENI KOTA KUKAMILIKA MACHI MWAKANI

$
0
0
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (katikati), akitoa maelekezo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Msanifu Majengo Elius Mwakalinga (kulia) wakati akikagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Msanifu Majengo Elius Mwakalinga (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (katikati), kuhusu hatua zilizofikiwa katika utelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, wakati akikagua maendeleo ya ujenzi huo, jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa mtambo wa kuchakata zege unaotumiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota, jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa baadhi ya vitalu vya makazi eneo la Magomeni Kota zinazojengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 35.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na menejimenti ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), wakati alipowatembelea wakala huo leo, jijini Dar es Salaam.
Meneja Rasilimali Watu kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Bi. Gerwalda Luoga, akitoa neno la shukrani kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (hayupo pichani) mara baada ya kikao kazi na Naibu Waziri huyo, jijini Dar es Salaam.


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa (Mb), ameutaka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kufanya kazi kwa bidii katika miradi yote inayopewa na Serikali ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa.

Akikagua hatua zilizofikiwa katika mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni kota, Naibu Waziri Kwandikwa, amesema kuwa Serikali itaendelea kuanisha miradi mingine ili kuhakikisha fedha za Serikali zinaokolewa na kusimamiwa kwa uzalendo.

“Hakikisheni mnafanya kazi zenu kwa weledi, uzalendo na kukamilisha miradi kwa wakati na kuokoa fedha ambazo zitatumika katika utekelezaji wa miradi mingine hapa nchini”, amesisitiza Mhe. Kwandikwa.

Ametoa wito kwa wataalamu wengine kuja kupata mafunzo kwa TBA ambao ni chachu ya utekelezaji wa miradi mingi hapa nchini kwa kuwa wanatumia mfumo wa kisayansi na mitambo yenye kusaidia kupunguza gharama za ujenzi.

Aidha, Naibu Waziri huyo ameushukuru uongozi wa TBA kwa kutoa ajira za vibarua takribani 200 kwa siku katika mradi huo na kuwataka wafanyakazi hao kuwa waadilifu na waaminifu ili kuwa na sifa za kupata ajira za kudumu.

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Msanifu Majengo Elius Mwakalinga, amemhakikishia Naibu Waziri Kwandikwa kukamilika mradi huo kwa wakati, ubora na kwa gharama nafuu.

Amefafanua kuwa mradi huo utakuwa una jumla ya vitalu vitano ambapo vitalu vinne vina majengo ya ghorofa nane na kitalu kimoja kina jengo la ghorofa tisa na hivyo mradi utatoa makazi kwa kaya 656.

Mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi eneo la Magomeni Kota unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Machi mwakani na utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 20 zote ikiwa ni fedha za Serikali.

Mama Salma Kikwete ashiriki ufunguzi wa mkutano "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" mjini Beijing nchini China.

$
0
0

 Mmoja wa wadau akizungumza kwenye mkutano huo wa "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" ulioanza kufanyika leo Beijing nchini China,ambapo Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB),ameshiriki
 Washiriki wa mkutano "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ndani ya ukumbi huo.
Pichani kulia ni  Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB), pamoja na washiriki wengine wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" uliofunguliwa leo mjini Beijing nchini China.
Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mhe. Mama Salma Kikwete (MB), akiwa katika picha ya pamoja na mshiriki mwenza wa mkutano wa "First Silk Road NGO Corporation Network Forum" uliofunguliwa leo mjini Beijing nchini China.

DC HANDENI ATOA SIKU 14 WATAALAMU WA ARDHI KUAINISHA MPAKA UNAOTTENGANISHA HALMASHAURI YA WILAYA NA MJI KATA YA MISIMA.

$
0
0
Baadhi ya wafugaji na wakulima walioshiriki mkutano wa hadhara.
 mmoja wa wafugaji akitoa malalamiko yake kuhusu wakulima kuvamia eneo la mifugo na kuanza kulima kinyume na taratibu na kuomba kuanishiwa mipaka kuepuka muingiliano.
 Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw.William Makufwe akiwaeleza wafugaji wa Kijiji cha Msomera kuwa  wakulima kuingia kwenye eneo la kufugia mifugo kunatokana na baadhi ya viongozi kutokuwa waadilifu kwa kuuza maeneo bila kufuata taratibu na kuwataka kushirikisha wananchi kwa kila jambo kwani viongozi sio watu wenye maamuzi ya mwisho.
 Kaimu  Mkuu wa Idara ya  Ardhi na Maliasili Bw. Napoleone Mlowe akithibitisha kuwa Kijiji cha Msomera kinatambulika kisheria na ni eneo lililotengwa kwaajili ya wafugaji kulingana na mpango bora wa matumizi ya ardhi.
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe akizungumza na wafugaji   wa Kijiji cha Msomera na akiwasisitiza kuwa Kuwa Kijiji hicho ni cha wafugaji wote bila kujali kabila.
Diwani wa Kata ya Misima Mh. Mariamu Killo akizungumza na wananchi wa  Kijiji cha Msomera na kuwataka kuwa wavumilivu hadi hapo mipaka itakapoainishwa.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh.Godwin Gondwe amewapa siku 14 wataalamu wa ardhi wa Wilaya kuainisha mipaka baina ya Kata ya Misima iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Mji ili kuondoa mkanganyiko wa mpaka uliodumu kwa muda mrefu.

Mkuu wa Wilaya ameyazungumza hayo jana alipokuwa kwenye mkutano wa Hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Msomera Kata ya Misima baada ya uongozi wa Kijiji hicho kuomba msaada wa kusikilizwa ili kuainishiwa mipaka baina ya Kata na Vijiji ili kuondoa muingiliano.

Mh. Gondwe alisema kuwa wataalamuwa ardhi watapima na kuonesha mipaka baina ya Halmashauri ya Mji na Wilaya ili wafahamu mipaka yao na kutambua wanapaswa kuitika wapi na kuondoa migongano inayokwamisha wananchi kushiriki katika maendeleo.

Alisema kuwa Msomera ni Kijiji kilichoanzishwa kisheria na kipo kwenye mpango wa matumizi bora ya ardhi hivyo wananchi wote wanapaswa kuheshimu na kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa sheria na kuwataka wananchi wote wanaokuja kwenye Kijiji hicho na maeneo mengine kufuata masharti ya maeneo husika kwani Tanazania ni huru kuishi kwa kila mwananchi isipokuwa kwa kufuata taratibu zilizowekwa.

Aliongeza kuwa Kijiji cha Msomera kilitengwa maalumu kwa mifugo, wakulima ambao walikuwepo kabla ya kijiji hicho kupangwa kuwa kwaaajili ya mifugo watambuliwe na hawataondolewa, wakulima waliokuja baada ya kijiji kutambulika kuwa ni cha mifugo wataondolewa.

Aidha Mkuu wa Wilaya amewataka wanakijiji cha Msomera kufuata utaratibu linapokuja suala la kuuza ardhi na kuingiza mifugo mipya kwa kushirikisha uongozi wa Kijiji na kufanya mikutano mikuu ya maamuzi ili kuwe na maaamuzi ya pamoja hata kama ardhi inayouzwa ni ya mtu binafsi.

“Kijiji kikipangiwa matumizi bora kitumike kama ilivyokusudiwa ili kuondoa migogoro, tunzeni ardhi yenu na rasilimali zenu kwa ustawi wa vizazi vyenu,haijalishi kama mnaleta ndugu zenu, taratibu lazima zifutwe kinyume na hapo sheria itachukua mkondo wake” amesema Mkuu wa Wilaya.

Imetolewa na:
Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni
21/11/2017

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, MHE. JAPHET HASUNGA AKABIDHI MSAADA WA MABATI KWA SHULE YA MSINGI ILIYOATHIRIKA NA KIMBUNGA MKOANI IRINGA

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakitwanga Kinu wakati wa ziara yake katika Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) jana Mkoani humo.

Na Hamza Temba - WMU
....................................................................
Katika jiihada za Serikali za kuendeleza ushirikiano na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi nchini, Wizara ya Maliasili na Utalii imetoa msaada wa mabati sitini kwa ajili ya kuezeka madarasa ya shule ya msingi Kipanga baada ya kuezuliwa na kimbunga hivi karibuni katika kijiji cha Ubwachana Wilaya ya Iringa mkoani Iringa.

Msaada huo umetolewa jana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga alipotembelea kituo cha Malikale cha Isimila mkoani humo ambacho kinapakana na shule hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja Mkoani humo.

Akikabidhi mabati hayo, Naibu Waziri Hasunga alisema  Serikali inatambua mchango wa wananchi wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi kwenye uhifadhi shirikishi hivyo ni jukumu la Serikali kuwaunga mkono pale wanapopatwa na majanga ya aina mbalimbali.

Aidha, aliwataka baadhi ya wananchi wanaochimba mchanga kwenye maeneo ya vivutio katika kituo hicho waache mara moja kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria kwakuwa wanahatarisha uhai wa kingo za miamba ya kale ambayo na kivutio kikubwa cha utalii wa asili katika ukanda wa kusini.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya mambo ya Kale wa Wizara hiyo, Bi. Digna Tillya alitoa rai kwa wananchi wanaozunguka kituo hicho kushirikiana na Serikali katika uhifadhi na ulinzi wa kituo hicho na kujiepusha na vitendo vya uharibifu wa mazingira.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akiwa amevaa “musk’ mfano wa vazi la kabila la wahehe wa Mkoa wa Iringa wakati wa ziara yake katika Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa huo (Boma) jana.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (wa tatu kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa Kijiji cha Ubwachana, Donatus Lihoha mabati 60 kwa ajili ya kuezeka vyumba vya madarasa vya shule ya msingi Kipanga ambayo iliezuliwa na kimbunga hivi karibuni ikiwa ni kutambua mchango wa wananchi katika uhifadhi shirikishi wa Kituo cha Mali Kale cha Isimila jana Mkoani Iringa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akimsikiliza Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga ambaye pia ni Meneja Msaidizi wa Mradi wa Fahari Yetu unaojishughulisha na Uhuishaji, Uendelezaji na Utangazaji wa utalii Nyanda za Juu Kusini kuhusu Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) wakati wa ziara yake jana Mkoani humo. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale wa Wizara hiyo Digna Tillya.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga ambaye pia ni Meneja Msaidizi wa Mradi wa Fahari Yetu unaojishughulisha na Uhuishaji, Uendelezaji na Utangazaji wa utalii Nyanda za Juu Kusini wakati akitoa maelezo kuhusu Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa  (Boma) wakati wa ziara yake jana Mkoani humo. Anayeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (kulia kwake).
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akizungumza na watumishi wa Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) alipotembelea Makumbusho hiyo jana wilayani Iringa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa pili kulia) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela kuhusu Makumbusho ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa (Boma) wakati wa ziara yake jana Mkoani humo. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wapili kushoto) akisalimiana na wafanyakazi wa  (Kituo cha Mali Kale cha Isimila) alipotembelea kituo hicho jana mkoani Iringa.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) akimpa maelekezo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya (kulia) alipotembelea Kituo cha Mali Kale cha Isimila mkoani Iringa jana.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Kale wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Digna Tilya akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi mabati.
Baadhi wa washiriki wa hafla hiyo.
Baadhi ya washiriki wa hafla hiyo.

NEWZ ALERT: JENGO LA CLOUDS MEDIA GROUP LAWAKA MOTO MAPEMA LEO.

$
0
0
 Magari ya ya Jeshi la zimamoto yakiwa yamefika eneo la tukio,katika jengo la Ofisi za Clouds Media Group lililopo Mikocheni jijini Dar, kukabiliana na moto uliozuka mapema leo kwenye moja chumba cha ofisi na kusababisha baadhi ya vifaa kuungua na kuharibika kabisa,aidha mpaka sasa Globu ya jamii haijaelezwa haswa chanzo cha moto ni nini.Hivyo Tunaendelea kufuatilia na kupata taarifa kamili.
 Sehemu ya jengo la Ofisi za Clouds Media Group kama lionekanavyo pichani huku shughuli za uzimaji moto huo ukiendelea .
  Mmoja wa Askari wa jeshi la Zimamoto  akiendelea kuudhibiti  moto uliokuwa umezuka ndani ya moja ya Ofisi za jengo hilo
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Clouds Media Group pamoja na baadhi ya ndugu jamaa na marafiki wa Clouds wakiwa nje ya jengo hilo wakifuatilia tukio la uzimaji moto uliozuka katika jengo hilo mapema leo,Mikocheni jijini Dar.



Viewing all 46313 articles
Browse latest View live




Latest Images