Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live

TATU MZUKA YAMPONGEZA BI. BUJINGINYA KUTOKA NGARA KWA KUSHINDA MILIONI 50.

0
0
Pichani kulia ni Judith Bujinginya mkazi wa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera akizungumza jana jijini Dar mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani),namna alivyoibuka mshindi wa jackpot ya Tatu Mzuka  ya shilingi milioni 50 katika droo ya 15 iliyofanyika mwishoni mwa wiki.Pichani kati ni
mwakilishi wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akiwa pamoja na
Joseph Kofia ambaye alishinda kimaajabu shilingi milioni 68 kupitia droo ya kila saa.
Pichani kati ni mwakilishi wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akiwatambulisha Washindi wa mchezo  huo,mbele ya Waandishi wa habari mapema jana jijini Dar.
Mwakilishi wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi mfano wa hundi Bi.
Judith Bujinginya mkazi wa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera alieibuka  mshindi wa jackpot ya Tatu Mzuka  ya shilingi milioni 50 katika droo ya 15 iliyofanyika mwishoni mwa wiki

Mwakilishi wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba akimkabidhi mfano wa hundi,
Joseph Kofia ambaye alishinda kimaajabu shilingi milioni 68 kupitia droo ya kila saa.

Judith Bujinginya mkazi wa wilaya ya Ngara Mkoani Kagera ameibuka mshindi wa jackpot ya Tatu Mzuka  ya shilingi milioni 50 katika droo ya 15 iliyofanyika jumapili.

Bi Bujinginya, mama wa watoto wawili ambaye anaungana na washindi milioni 130  wa Tatumzuka amesafirishwa kwa ndege kutoka Ngara kuja Dar es Salaam ili kuchukua pesa yake ya ushindi  katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo Mikocheni.

 Baada ya kushinda mara chache katika droo ya kila saa, alipata msukumo wa kuendelea kucheza bila kukata tamaa. "Baada ya kuishi kwa kutafuta pesa ya mlo kila mwezi na miezi mingine bila pesa, Kiukweli sikujua itakavyokuwa ikifika Januari. Nimefurahi sana kwamba sasa naweza kutembea kwa kujiamini tena baada ya ushindi huu’ alikiri Bi Bujinginya.

Pia katika tukio la kukabidhi zawadi kwa mshindi alikuwepo Bwana Joseph Kofia ambaye alishinda kimaajabu shilingi milioni 68 kupitia droo ya kila saa.Dhamira ya Tatu Mzuka ya kubadilisha maisha ya watu haijabadilika ambapo zimebaki siku chache ili ichezeshwe droo kubwa ya Supa Mzuka jackpot ya milioni 150 jumapili ijayo. Tarehe 19 Novemba saa 3:30 usiku Mtanzania mmoja ataondoka na kitita cha milioni 150.

"Kila mtu ambaye umecheza tangu Tatumzuka izinduliwe na kutumia kuanzia shilingi 500 tu kupitia MPESA, TIGO PESA au AIRTEL MONEY, umeingia katika droo hii ambapo unaweza kujishindia milioni 150," alielezea mwakilishi wa Tatu Mzuka, Kemi Mutahaba.

Bi Mutahaba aliwahimiza watanzania kuendelea kucheza, akisisitiza kwamba bado washiriki hawajachelewa kujiwekea nafasi ya ushindi huo wa kihistoria.

MAHAFALI DUCE YAFANA, PROF MUKANDALA AWAAGA RASMI WANA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM

0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amewatunukia wahitimu 1443 wa ngazi mbalimbali kutoka Chuo Kikuu cha Elimu Dar es salaam (DUCE) kwenye mahafali ya 10 yaliyofanyika jana Jijini Dar es Salaam.

Katika mahafali hayo Mkuu wa Chuo Dkt Kikwete aliwatunukia wahitimu hao sambamba na kutoa zawadi kwa wanafunzi nane waliofanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho.

Rais wa Chuo Kikuu Kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam, Prof William Anangiyse amesema kuwa jumla ya wahitimu 1371 wametunukiwa digrii za awali katika fani mbalimbali na Wahitimu 72 ni wa ngazi ya stashahada ya uzamili katika elimu  (PGDE) na kutimiza idadi ya 1443.

Prof Anangisye amesema kuwa jumla ya 928 ni wanaume na 515 ni wanawake huku wahitimu 1015 wakitunukiwa digrii ya elimu ya jamii na ualimu (B.A.Ed), , 233 ni wahitimu wa Sayansi na Ualimu ( B.Sc.Ed), wahitimu 72 ni Elimu katika sayansi (B.Ed.Science) na Elimu katika elimu ya Jamii ( B.Ed.Arts) ni wahitimu 51.
Mbali na hilo, Mwenyekiti wa bodi ya Usimamizi ya Chuo Kikuu Kishirikishi  Cha Elimu Dar es Saalam, Prof. Rwekaza Mukandala kwenye mahafali ya 10 ya chuo hicho amewaaga rasmi wanajumuiya wa Chuo Kikuu Kishirikishi  baada ya kumaliza muda wake wa mwaka mmoja alioongezewa na Rais wa Awamu ya Tano Dkt John Pombe Magufuli kwenhe mahafali ya mwaka jana.

Mkuu wa Chuo Dkt Kikwete aliweza kutoa zawadi kwa wahitimu nane waliofanya vizuri katika mitihani yao ya mwisho pamoja na Emanuel Safari Dadi aliyefanya vizuri kwa ujumla na kumpongeza kwa juhudi kubwa alizozifanya katika kipindi chake cha masomo.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa amepiga picha na mhitimu Emanuel Safari Dadi aliyefanya vizuri katika mitihani yake yote na kupata GPA 5.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu  Dar es Salaam Peter Ngumbulu (Kulia), Rais wa Chuo Kikuu Kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam Prof William Anangyse, Mlau wa Chuo Kikuu Kishirikishi Cha Elimu Dar es Salaam Prof. Martha Qorro na wajumbe wengine katika mahafali ya 10 yaliyofanyika jana Jijini Dar es salaam.
 Wahitimu wakitoa kiapo cha utii na ahadi katika kulitumikia taifa na kulikuza
 Mhitimu bora Emanuel Safari Dadi akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya wahitimu wote.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akitoa zawadi kwa wahitimu nane waliofanya vizuri kwenye mitihani yao. Chini akiwa amepiga nao picha ya pamoja.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwatunukia wahitimu wa ngazi mbalimbali katika mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu Kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam yaliyofanyika jana Jijinj Dar es Salaam.


Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Rais wa awamu ya nne ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa mahafali akiongozana na viongozi wengine wa Chuo Kikuu kishirikishi cha Elimu Dar es Salaam jana katika mahafali ya 10.

SHIRIKA LA MAENDELEO LA UJERUMANI 'GIZ' NA SHUWASA WAENDESHA WARSHA KWA WADAU WA MAJI MANISPAA YA SHINYANGA

0
0
Mshauri wa masuala ya Maji na Mazingira kutoka Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’, Tina Eisele akielezea kuhusu mradi wa maji safi na mazingira katika maeneo ya wananchi wenye kipato cha chini unaotekelezwa na shirika hilo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA) katika kata ya Ndala na Masekelo manispaa ya Shinyanga - Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefungua warsha ya wadau wa maji na mazingira katika manispaa ya Shinyanga iliyoandaliwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’ kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA).
 
Lengo la warsha hiyo ni kuboresha huduma ya maji safi na usafi wa mazingira kwenye kata ya Ndala na Masekelo katika manispaa ya Shinyanga kupitia mradi wa huduma ya maji na usafi wa mazingira katika maeneo ya wananchi wenye kipato cha chini unaotekelezwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’ kwa kushirikiana na SHUWASA.
Akifungua warsha hiyo ya siku mbili inayofanyika katika ukumbi wa Karena Hotel Mjini Shinyanga ambayo imekutanisha wataalamu wa maji na mazingira na viongozi kuanzia ngazi ya mtaa hadi mkoa,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alisema mradi huo utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wenye kipato cha chini.
Matiro alilishukuru shirika la GIZ kwa kushirikiana na SHUWASA kuanzisha mikakati ya kushughulikia changamoto za maji na mazingira katika kata ya Ndala na Masekelo wakishirikiana na wadau mbalimbali.
Alisema lengo la serikali ni kusimamia sera za nchi ili kuondoa changamoto zinazowakabili wananchi na kwamba ipo tayari kushirikiana na wadau wote katika kukabiliana na changamoto zote zinazojitokeza.
“Mimi kama kiongozi mkuu wa wilaya hii,natoa shukrani za dhati kwa shrike la ‘GIZ’ kwa kuchagua mji wa Shinyanga kuwa moja ya miji mitatu nchini iliyopangwa kutekeleza mradi huu ikiwemo miji ya Korogwe na Dodoma,nawasihi kusimamia kikamilifu mradi huu ili uweze kunufaisha wananchi na pale mnapokwama msisite kuwasiliana na serikali”,alisema Matiro.
Naye Mshauri wa masuala ya Maji na Mazingira kutoka Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’, Tina Eisele aliishukuru serikali ya Tanzania kwa kuwaruhusu kutekeleza mradi huo ambao unatekelezwa katika maeneo ambako kuna wananchi wenye kipato cha chini.
Eisele alisema takwimu zinaonesha kuwa katika maeneo ambayo kuna wananchi wenye kipato duni,huduma za maji safi na usafi wa mazingira pia ni duni ndiyo maana wameamua kuanzisha mradi huo ambao utawalenga watu wenye kipato duni.
“Kupata maji safi na kuwa katika mazingira bora ni haki ya binadamu,tunataka maeneo yenye wananchi wenye kipato duni waangaliwe kwa jicho kama lile linalotumika kuangalia wananchi wenye kipato kikubwa,na hii ni miongoni mwa makubaliano ya mikataba mbalimbali ya kimataifa”,aliongeza Eisele.
Mkurugenzi wa SHUWASA,Injinia Sylivester Mahole alisema tayari mradi huo umeanza kutekelezwa huku akibainisha kuwa mradi huo utawanufaisha wananchi ambao walikuwa hawajafikiwa na huduma ya maji.
“Miongoni mwa changamoto katika utoaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira ni huduma kutowafikia wananchi wote na hivyo kusababisha makundi ya waliofikiwa na huduma na wasiofikiwa na huduma”,alieleza Injinia Mahole.
“Katika maeneo yanayotakiwa kupewa huduma kuna maeneo yanakaliwa na wananchi wenye kipato cha chini na hivyo kutokuwa na uwezo wa kuunganisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira majumbani mwao,hivyo kwa kushirikiana na shirika la GIZ tumeamua kukabiliana na changamoto hii”,aliongeza Injinia Mahole.
Naye Mwezeshaji katika warsha hiyo,Injinia Mutaekulwa Mutegeki alisema kata za Ndala na Masekelo zitatumika kama mfano wa utekelezaji wa mradi huo ambapo pamoja na mambo mengine vituo vya kuchotea maji “Magati” vitajengwa kwenye maeneo hayo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefungua warsha ya wadau wa maji na mazingira katika manispaa ya Shinyanga iliyoandaliwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’ kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA),katika ukumbi wa Karena Hotel mjini Shinyanga -Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa kufungua warsha ya wadau wa maji na mazingira katika manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwasisitiza wadau wa maji na mazingira kuhakikisha wanaungana katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili wananchi katika kupata huduma za maji safi na mazingira.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa SHUWASA ,Injinia Syliveter Mahole akifuatiwa na Erik Norremarle kutoka GFA.
Mshauri wa msuala ya Maji na Mazingira kutoka Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’, Tina Eisele akielezea kuhusu mradi wa huduma ya maji na usafi wa mazingira katika maeneo ya wananchi wenye kipato cha chini unaotekelezwa na shirika hilo katika kata ya Ndala na Masekeleo katika manispaa  ya Shinyanga kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira mjini Shinyanga (SHUWASA).
Mshauri wa masuala ya Maji na Mazingira kutoka Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’, Tina Eisele akiwasilisha mada kuhusu mradi huo wa maji.
Mshauri wa msuala ya Maji na Mazingira kutoka Shirika la Maendeleo la Ujerumani ‘GIZ’, Tina Eisele akiendelea kuwasilisha mada ukumbini.
Washiriki wa warsha hiyo wakifuatilia mada ukumbini.
Mwezeshaji katika warsha hiyo,Injinia Mutaekulwa Mutegeki akizungumza ukumbini.
Warsha inaendelea.
Washiriki wa warsha wakiwa ukumbini.
Washiriki wa warsha wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Maafisa kutoka SHUWASA wakiwa ukumbini.
Washiriki wa warsha wakiwa ukumbini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Shirika la WoteSawa lazindua mradi wa “Paza Sauti ya Mfanyakazi wa Nyumbani” wilayani Ilemela

0
0
Shirika la kutetea haki za watoto wafanyakazi wa nyumbani WoteSawa lenye makazi yake Jijini Mwanza, leo limezindua mradi wa kuwajengea uwezo wafanyakazi wa nyumbani katika Manispaa ya Ilemela ili kutetea haki na maslahi yao. Akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi huo uitwao “Paza Sauti ya Mfanyakazi wa Nyumbani”, Mkurugenzi wa shirika hilo Angel Benedicto amesema mradi huo pia utawasaidia wafanyakazi wa nyumbani kufichua changamoto zinazowakabiri. Mkurugenzi wa WoteSawa, Angel Benedicto akizungumza kwenye uzinduzi/ utambulisho wa mradi huo uliofanyika Monarch Hotel Mwanza. Wadau walioshiriki uzinduzi huo wakimsikiliza Mkurugenzi wa shirika la WoteSawa, Angel Benedicto.. Wadau walioshiriki uzinduzi huo wakimsikiliza Mkurugenzi wa shirika la WoteSawa, Angel Benedicto. Diwani wa Kata ya Kitangiri Manispaa ya Ilemela, Elizabert Wangaluka akizungumza wakati wa utambulisho wa mradi huo.. Rehema Mkinza ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Ilemela akieleza namna serikali inavyoshiriki ipasavyo katika kupambana na utumikishwaji wa mtoto. Washiriki wakifuatilia mada kwenye uzinduzi huo. Mratibu wa Shirika la Kutetea Haki za Wafanyakazi wa Nyumbani (Wotesawa) Elisha David akitambulisha mradi huo.

OPEC YAIPATIA TASAF DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 12 KUTEKELEZA MRADI WA KUPUNGUZA UMASKINI AWAMU YA TATU

0
0
 Mkurugenzi wa miradi wa TASAF ,Bw. Amadeus Kamagenge (aliyesimama) akifungua kikao kazi cha Mradi wa kupunguza Umasikini awamu ya Tatu,katika ukumbi wa mikutano wa TASAF jijini Dar es salaam.,Kulia kwake ni Mkurugenzi wa fedha, Bi. Chiku Thabiti,kushoto kwake ni meneja wa miradi ya miundombinu wa TASAF Mhandisi Elisifa Kinasha.
 

 Meneja wa miradi ya miundombinu wa TASAF,Mhandisi  Elisifa Kinasha (aliyesimama) akitoa maelezo ya kikao kazi cha Mradi wa kupunguza umasikini awamu ya tatu kwa wasimamizi wa halmashauri za wilaya za mikoa ya Arusha na Njombe yaliyoanza leo kwenye ukumbi wa mikutano wa TASAF jijini Dar es salaam.
 Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha mradi wa kupunguza  umasikini awamu ya tatu (TPRP) kwa wasimamizi wa halmashauri za wilaya za mikoa ya Arusha na Njombe.Kikao kazi hicho kinafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa TASAF jijini Dar es salaam.
 Washiriki wa kikao kazi cha mradi wa kupunguza  umasikini awamu ya tatu (TPRP) kwa wasimamizi wa halmashauri za wilaya za mikoa ya Arusha na Njombe wakisikiliza hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi hicho  kinachofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za makao makuu ya TASAF jijini Dar es salaam.
 
 
NA ESTOM SANGA-TASAF.

Umoja wa nchi zinazozalisha Mafuta kwa wingi OPEC- umeupatia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF kiasi cha Dola za kimarekani milioni 12 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kupunguza Umasikini Awamu ya Tatu katika mikoa ya Njombe na Arusha.

Akifungua kikao kazi cha mradi wa kupunguza Umasikini awamu ya tatu (TPRP III ) kwa wasimamizi wa halmashauri za wilaya za mikoa ya Njombe na Arusha kwenye ukumbi wa mikutano wa TASAF jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bwana Ladislaus Mwamanga, amesema kiasi hicho cha fedha kimetolewa ili kuendeleza miradi ya wananchi kwa jamii zenye upungufu wa huduma za jamii ,uhaba wa kipato na kujiongezea kipato.

Katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na mkurugenzi wa miradi wa TASAF,Bwana Amadeus Kamagenge, bwana Mwamanga amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa fedha hizo zinazowanufaisha walengwa na kusaidia kufanikisha mkakati wa serikali wa kupambana na umasikini nchini.

Aidha Bwana Mwamanga amesema takribani miradi 407 iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji baada ya kupatiwa fedha na kuwaagiza watendaji hao wa halmashauri kuongeza kasi ya kuibua miradi mingine kwenye maeneo yao ili kusaidia jitihada za serikali za kusogeza huduma za kijamii hususani elimu na afya karibu zaidi na walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.

Bwana Mwamanga pia ametoa wito maalumu kwa viongozi wa halmashauri za wilaya katika mikoa ya Njombe na Arusha kuendelea kuwahamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao hususani ile inayohitaji mchango wa jamii husika ili miradi hiyo iweze kuwa endelevu na yenye manufaa kwa wananchi.

Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini ambao pamoja na mambo mengine unajenga miundombinu hususani ile inayolenga moja kwa moja kaya za walengwa wa Mpango kwa kuongeza kasi ya kupunguza umasikini miongoni mwa wananchi.

RAIS MSTAAFU DKT. JAKAYA KIKWETE AONGOZA MAHAFALI YA 10 YA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU (DUCE) CHA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

0
0


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, (pichani juu), ameongoza mahafali ya kumi (10), ya  Chuo kikuu kishiriki cha Elimu (DUCE) cha Chuo kikuu Dar es salaam kwenye viwanja vya chuo hicho, Chang’ombe jijini Dar es Salaam leo Novemba 15, 2017.
Katika mahafali hayo zaidi ya wanachuo 1,443 waliochukua mafunzo ya Shahada ya Elimu ya Jamii na Elimu, (BAED), Shahada ya Elimu ya Sayansi na Elimu, (Bsc) na Shahada ya Elimu (BED), pamoja na wahitimu waliojiendeleza (Post graduate), walitunukiwa shahada ya kwanza, ambapo mwanachuo Dadi Omary Safari, alipewa tuzo ya kuwa mwanachuo bora zaidi kitaaluma.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete, akimpongeza mmoja wa wahitimu wa Shahada ya Elimu ya Jamii na Elimu, (BAED) Amisa Hassan.
Baadhi ya wahitimu katika mahafali ya 10 ya ya  Chuo kikuu kishiriki cha Elimu (DUCE) cha Chuo kikuu Dar es salaamwakiwa kwenye mahafali hayo
Furahaya kuhitimu na kutunukiwa shahada.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala, akisoma hotuba yake.
Dkt. Kikwete, akipitia ratiba ya mahafali hayo.
Dkt. Kikwete akitangaza kuwatunuku shahada baadhi ya wanachuo hao.
Baadhi ya wanachuo wakisubiri kutunukiwa shahada zao na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete.
Dkt. Kikwete, akiteta jambo na Profesa Mukandala.
Dkt. Kikwete, akiipitia tuzo ya mwanachuo bora kitaaluma Dadi Emmanuel Safari kabla ya kumkabidhi.
Mwanachho bora kitaaluma Dadi Emmanuel Safari akiwa na tuzo yake.
 
Dkt. Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na mmoja wa wahitimu, Amisa Hassan, na baba mdogo wa muhitiumu huyo, Khalfan Said.

RC WA TANGA MARTINE SHIGELLA AZINDUA RASMI TAWI LA BENKI YA NMB MKATA WILAYANI HANDENI

0
0


Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh.Martine Shigella leo amezindua rasmi tawi la NMB benki lililopo Kata ya Mkata Wilayani Handeni na kuwataka wakazi wa  maeneo ya jirani kuacha kuhifadhi fedha nyumbani. 

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa ufunguzi wa tawi hilo la kibenki ni fursa kubwa kwa wakazi wa Mkata na maeneo ya jirani kwani huduma za kifedha zimesogezwa karibu na ni chachu ya ukuaji wa maendeleo na uchumi wa Mkata. 

Aliongeza kuwa Mkata ni eneo lenye mzunguko mkubwa wa kifedha kutokana na kuwa na wafanyabiashara mbalimbali, wakulima, wafugaji,wafanyabiashara wa matunda na biashara nyingine hivyo wanategemea kwa kiasi kikubwa huduma ya benki katika utunzaji wa fedha na usalama wao. 

Mh. Shigella alisema kuwa NMB Benki imesaidia sana wananchi kwa kutoa mikopo na misaaada mingine ya kijamii hivyo ni vyema kuitumia benki hiyo kwani kwa kufanya biashara na NMB ni kufanya biashara na serikali kwa sababu kwa upande mwingine NMB ni Serikali ambapo fedha zinazowekwa ndizo zinazorudi kwenye jamii kwa mtindo wa mishahara, ujenzi wa miundo mbinu na huduma nyingine za kijamii. 

”wananchi muweke utaratibu wa kuhifadhi fedha zenu kwenye benki badala ya kuzikumbatia ndani hali inayopelekea kuhatarisha usalma wa maisha yenu, NMB imefungua tawi kuwapunguzia kufuata huduma za benki mbali, tumieni fursa hii kupata mikopo ili kukuza uchumi wenu na Taifa kwa ujumla” Alisema Mkuu wa Mkoa. 

Aidha amewataka NMB Benki kujiandaa na fursa za miradi mikubwa ya Bomba la mafuta,Viwanda,Madini, Kilimo na Ufugaji iliyopo Wilayani Handeni na Mkoa wa Tanga ili kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi wote kwa kuongeza matawi mengi ili kuepusha wananachi kuzunguka na fedha mifukoni. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe ameshukuru uongozi wa NMB kwa kuona umuhimu wa kufungua tawi eneo la Mkata ambalo litawasaidia wakazi wa eneo hilo na jirani kutotembea urefu wa KM54 kufuata huduma za benki kwa kuzingatia kwamba eneo la Mkata linawafanayabiashara wengi na mzunguko wa fedha ni mkubwa. 

Wakati huohuo Meneja wa NMB kanda ya Kaskazini Bw.Salie Mlai ameahidi kuwa Benki yao itatoa msaada wa vifaa vya afya kwenye kituo cha afya cha Mkata vyenye thamani ya Milioni 10 ikiwa ni sehemu ya kurudisha faida waliyoipata kwa jamii wanayoihudumia. 

Benki ya NMB yenye kauli mbiu ya “Karibu Yako” yenye maana ya kuweka ukaribu wa huduma za fedha kwa wananchi na kutoa bidhaa inayoendana na mahitaji ya maeneo husika ili iweze kuwa karibu,rahisi na yenye mafanikio katika mambo ya ujenzi wa Taifa. 

NMB Benki imesambaa nchi nzima kwa asilimia 97 ambapo ina ATM zaidi ya 800, Matawi 213 na mawakala 4500 ambao wanarahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha.Mikopo ya wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa inatolewa ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo kuendana na aina ya mradi mfano Mikopo ya pembejeo za kilimo kwa wakulima. 

Imetolewa na: 
Kitengo cha Teknolojia, Habari na Mawasiliano 
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni. 
​Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Martine Shigella kushoto na Mkurugenzi wa NMB Benki Bi. Ineke Bismeka wakifungua kibao cha ufunguzi wa Tawi hilo​.
Mkuu wa Mkoa Tanga,Mh. Martin Shigela akizungumza na wananchi wa Mkata wakati wa ufunguzi wa Tawi la NMB
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akishukuru uongozi wa NMB kwa kuona umuhimu na kufungua Tawi eneo la Mkata.

TAARIFA YA AJALI YA NDEGE YA COASTAL AVIATION ILIYOTOKEA JANA

0
0

Baadhi ya Wananchi wakishuhudia ajali katika eneo la Empakai ilipotokea ajali ya ndege ya Coastal Aviation jana mkoani Arusha,ambapo katika ajali hiyo imethibitishwa kuwa watu 11 walipoteza maisha


TAKUKURU KILIMANJARO YAMSHIKILIA DAKTARI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA,MAWENZI KWA TUHUMA ZA RUSHWA

0
0
Anaandika Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini. 

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)mkoani Kilimanjaro,imemtia mbaroni Daktari wa Hospital ya rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi akituhumiwa kudai na kupokea rushwa ya shilingi 150,000.

Daktari huyo,Deogratias Godfrey Urio,alikamatwa jana katika mji mdogo wa Himo kwenye baa maarufu ya Mombasa High Way baada ya kuwekewa mtego na makachero wa takukuru mkoani Kilimanjaro.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi kwa vyombo vya habari na Mkuu wa Takukuru mkoa wa Kilimanjaro(RBC),Holle Makungu imesema kuwa kukamatwa kwa daktari huyo kunatokana na malalamiko ya ndugu wa mgonjwa aliyekuwa akipigwa dana dana kupatiwa huduma ya upasuaji katika hospital hiyo.

Makungu ameeleza katika taarifa yake kuwa,mgonjwa huyo alikuwa akihitaji kufanyiwa upasuaji wa uvimbe katika kizazi chake tangu oktoba mwaka huu baada ya kufanyiwa vipimo kwenye hospital hiyo na kubainika kuwepo kwa uvimbe.

Lakini licha ya kubainika kuwepo na uvimbe huo,mgonjwa huyo hakuweza kupata tiba haraka baada ya kuelezwa na daktari huyo kuwa hawezi kufanyiwa upasuaji huo hadi hapo atakapotoa fedha hizo.

Makungu ameeleza kuwa,baada ya taarifa hizo kuwafikia,mtego uliandaliwa na daktari huyo aliweza kutiwa mbaroni jana Novemba 15 akiwa kwenye baa hiyo ya Mombasa High Way.

“Tunaendelea na uchunguzi wa tuhuma hizo na atafikishwa mahakamani mara tu uchunguzi utakapokamilika,takukuru inatoa rai kwa madaktari na wauguzi katika hospital ya Mawezi kuzingatia viapo vyao ili Mawenzi iwe hospital ya kuigwa kwa huduma bora”,amesema makungu.

Mkuu huyo wa Takukuru mkoa wa Kilimanjaro akahitimisha taarifa yake kwa kuonya kuwa kwa wale wachache watakaoendelea kutozingatia viapo vyao,watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria na pia kuwataka waajiri wao wachukue hatua kali za kinidhamu dhidi ya watumishi hao .

CHUO CHA KODI KUFANYA MAHAFALI YA KUMI JUMAMOSI NOVEMBA 18 2017

0
0
Chuo cha Kodi kitafanya mahafali ya Kumi Jumamosi tarehe 18 Novemba 2017 katika ukumbi wa chuo cha Kodi ambapo Mgeni rasmi katika mahafali hayo anatarajiwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango.

Katika mahafali hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mpango atatunuku vyeti, stashahada na shahada kwa wahitimu 520 ambao wamefuzu masomo yao mwaka 2016/2017 na kusathili kutunukiwa vyeti.

Dkt. Mpango pia atatoa zawadi mbalimbali kwa wahitimu 12 waliofanya vizuri zaidi katika masomo ikiwa ni utaratibu ambao chuo kimejiwekea ili kutambua jitihada nzuri ambazo zimefanywa na wanafunzi hao pamoja na kuwashajihisha wanafunzi wanaoendelea na masomo kufanya vizuri zaidi katika masomo. 

Jumla ya anafunzi watakao tunukiwa vyeti, stashahada na shahada katika mahafali ya Kumi ya Chuo cha Kodi ni wahitimu 82 wa Cheti cha Uwakala wa Forodha cha Afrika Mashariki yaani the ‘East African Customs and Freight Forwarding Practising Certificate (EACFFPC). Wahitimu 39 wa Cheti cha Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani ‘Basic Technician Certificate in Customs and Tax Management (CCTM). Stashahada ya Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani ‘Diploma in Customs and Tax Management – (DCTM)’ wahitimu – 147, Shahada ya Usimamizi wa Forodha na Kodi yaani ‘Bachelor of Customs and Tax Management (BCTM)’ Wahitimu – 134, ‘East African Community Postgraduate Certificate in Customs Administration (PGCCA)’ wahitimu 85 na Stashahada ya Uzamili katika Kodi yaani ‘Postgraduate Diploma in Taxation (PGDT) wahitimu - 33

Pamoja na kutunuku vyeti stashahada, na shahada kwa wahitimu, Mgeni Rasmi pia atatoa tuzo kwa wahadhiri wa Chuo cha Kodi waliofanya tafiti mbalimbali katika kipindi cha mwaka wa masomo wa 2016/2017 na kuchapishwa katika majarida mbalimbali ya kitaaluma, ikiwa ni pamoja na jarida la Chuo cha Kodi yaani ‘Journal of the Institute of Tax Administration’ (JITA).

Vilevile Chuo cha Kodi kinasherehekea miaka kumi tangu kipate ithibati (usajili) kutoka Baraza la Taifa la Vyuo vya Ufundi (NACTE).Chuo cha Kodi kinajivunia miaka kumi ya mafanikio katika kutoa mafunzo ya Forodha na Kodi yanayokidhi soko la ajira katika nyanja za forodha na Kodi ndani na nje ya nchi.

Tangu kipate usajili wa kudumu kutoka Baraza la Vyuo vya Ufundi (NACTE), Chuo kimepanua wigo wa taaluma kutoka kutoa mafunzo kwa watumishi wa TRA pekee hadi kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali wa masuala ya forodha na kodi kwa nchi za Mashariki Kati na Kusini mwa Afrika. 

Kikiwa katika hatua za mwisho za utekelezaji wa Mkakati wa Tatu, Chuo cha Kodi kinaendelea na maandalizi ya kuwa Kituo cha Umahiri wa Forodha na Kodi katika Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kukiteua Chuo cha Kodi kuwa Kituo cha Umahiri Afrika Mashariki

Nachukua fursa hii kuwakaribisha wahitimu pamoja wageni waalikwa wote pamoja na nyinyi waandishi wa habari katika mahafali haya ya Kumi yatakayofanyika katika Ukumbi wa Multipurpose Chuo cha Kodi tarehe 18 Novemba 2017 kuanzia saa tatu asubuhi.

“Pamoja Tunajenga Taifa Letu”
Prof. Isaya J. Jairo
MKUU WA CHUO


Mkuu wa Chuo cha Kodi (ITA,) Profesa Isaya Jairo akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu mahafali ya kumi ya chuo hicho yanayotarajiwa kufanyika chuoni hapo Jumamosi Novemba 18 2017. Kushoto ni Afisa Uhusiano Mkuu wa chuo, Oliver Njunwa. (Picha na Robert Okanda wa Okanda blogs) 
Mkuu wa Chuo cha Kodi (ITA) Profesa Isaya Jairo akiongea na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu mahafali ya kumi ya chuo hicho yanayotarajiwa kufanyika chuoni hapo Jumamosi Novemba 18 2017. Kulia ni Kaimu Naibu Mkuu wa Chuo (Utawala), Emmanuel Masalu na Afisa Uhusiano Mkuu wa chuo, Oliver Njunwa.

TAMKO LA MHE. UMMY MWALIMU KUHUSU WIKI YA KUZUIA USUGU WA VIMELEA DHIDI YA DAWA ZA ANTIBIOTIKI TAREHE 13- 19 NOVEMBA, 2017

0
0

BENKI YA KILIMO YATEMBELEA ENEO LA MRADI LA UMWAGILIAJI LA MWAMANYILI WILAYANI BUSEGA

0
0
 Mkuu wa wilaya ya Busega, Tano Seif Mwera (kulia) akiwakaribisha wageni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania waliofika kijijini Mwamanyili kujionea chanzo cha maji na eneo litakalotumika kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji. Wageni hao waliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (kushoto).
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya (mbele kulia) akiwaongeza wageni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania kujionea chanzo cha maji kitakachotumika katika mradi wa umwagiliaji wa Mwamanyili.
 Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Eng. Tumbu akitoa maelekezo kwa ugeni kutoka TADB juu ya chanzo cha maji cha maji kitakachotumika katika mradi wa umwagiliaji wa Mwamanyili.
 Muonekano wa eneo likalotumika kwa ajili ya mradi wa kilimo umwagiliaji wa Mwamanyili.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Bibi Rosebud Kurwijila (aliyenyanyua mikono) akihimiza jambo wakati walipotembelea eneo likalotumika kwa ajili ya mradi wa kilimo umwagiliaji wa Mwamanyili.

Katika kutekeleza kwa vitendo maagizo ya serikali ya kuchochea mapinduzi ya kilimo, Bodi ya wakurugenzi ya Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imetembelea eneo utakaofanyika mradi wa kilimo cha kisasa cha  umwagiliaji la Mwamanyili Wilayani Busega mkoani Simiyu.

Akizungumza lengo la ziara hiyo, mkuu wa msafara huo ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila amesema lengo kubwa la kuanzishwa kwa Benki ya Kilimo ni kuunga mkono juhudi za serikali katika kuwakwamua wakulima nchini kutoka katika kilimo cha kujikimu na kwenda kwenye kilimo cha kibiashara ili waweze kujiongezea kipato.

Aliongeza kuwa Mradi huo wa kilimo cha umwagiliaji ukianza kufanya kazi utatimiza malengo hayo ya Benki kwani utasaidia kwa kiwango kikubwa katika kuwainua wananchi Kiuchumi na kukabiliana na upungufu wa chakula wakulima watakaolima katika skimu hiyo.

“Benki ya Kilimo ipo tayari kuunga mkono miradi ya aina hii ambayo inalenga katika kuendeleza miundombinu muhimu ikiwemo ya uendelezaji wa skimu za umwagiliaji, usafirishaji, hifadhi ya mazao, usindikaji, pamoja na masoko ili kumuongezea mkulima kipato,” alisema.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya mradi huo ambao unajumuisha zaidi ya ekari 2050, wananchi watakaolima katika skimu hiyo watazalisha mpunga kwa misimu miwili kwa mwaka na kupanda mazao mengine mbadala hususani ya jamii ya mikunde mara baada ya kuvuna mpunga, kwa ajili ya kurutubisha ardhi.

Kipindi cha Miaka miwili ya JPM madarakani, sehemu ya Pili.

0
0

TPDC CUP SASA RASMI SONGO SONGO

0
0
Mashindano yajulikanayo kama TPDC Bonanza yenye lengo la kuboresha na kuimarisha afya ya Wakazi wa Songo Songo, ushirikiano pamoja na kujenga vipaji vya michezo kwa vijana wa kike na kiume yanayodhaminiwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) yamezinduliwa rasmi tarehe 13 Novemba, 2017.

Mgeni Rasmi wa Uzinduzi wa Mashindano hayo ambaye ni Meneja Mawasiliano wa TPDC, Marie Msellemu ameeleza kuwa, “Shirika limefarijika sana kufanikiwa kuzindua Mashindano ya Michezo ya Mpira wa Miguu na Pete katika Kijiji cha Songo Songo kwa malengo ya kujenga afya bora kwa kuwa michezo ni nyenzo bora ya kuepuka magonjwa mengi yasiyoambukiza, kuibua vipaji vya michezo, kujenga na kuimarisha uhusiano bora kati ya TPDC na Wananchi.”
Meneja Mawasiliano TPDC akieleza umuhimu wa mashindano ya TPDC CUP katika kuboresha afya na uhusiano bora.

Bi Msellemu amefafanua kuwa, kuwepo kwa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia na Visima vya Gesi Asilia katika kijiji hicho kunaifanya TPDC kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za maendeleo ya jamii ya Kijiji hicho hivyo kwa kuanzishwa kwa mashindano hayo ambayo yatakuwa ya kifanyika kila mwaka ni moja ya sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa TPDC kwa Wananchi wa Songo Songo.

Aidha Meneja wa Mawasiliano ameongeza kuwa, “Mashindano haya yataambatana na zoezi la Upimaji Afya ambalo litaanza tarehe 23 hadi 25, Novemba 2017 kwa Wananchi wa Songo Songo ambalo linatarajiwa kujenga uelewa zaidi wa masula ya afya kwa wananchi wa Songo Songo na kuweza kujiepusha na maradhi mbalimbali na hivyo kujenga Jamii imara yenye Afya na Nguvu ambayo itaweza kuendesha Shughuli za Kiuchumi zitakazo jenga na kuimarisha uchumi wa Kijiji na Taifa kwa ujumla.”
Meneja wa Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia cha Songo Songo na Mgeni Rasmi wa Uzinduzi wa Mashindano ya TPDC CUP wakisalimiana na Timu ya Mpira wa Miguu ya Black Rhino kabla ya kuanza kwa mechi yao dhidi ya Heroes.

Awali Meneja wa Kiwanda cha Kuchataka Gesi Asilia ndugu Kondoro Nteminyanda akiwa anamkaribisha Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa mashindano hayo alieleza kuwa uhusiano katika ya Shirika na Jamii ya Wananchi wa Songo Songo ni muhimu kwanza kwasababu wote tunategemeana katika shughuli zetu za kila siku na ili Kiwanda kiweze kifanye kazi yake kwa ufanisi kinahitaji mahusiano bora kati ya Shirika na Wananchi na hivyo shughuli kama hizi za kijamii zinazodhaminiwa na Shirika pamoja manufaa mengine lakini ni muhimu saana katika kujenga na kuendeleza ujirani mwema na ushirikiano wenye tija katika ya Kijiji na Kiwanda.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Songo Songo alieleza kuwa ni furaha ya pekee kwa Kijiji kwa Ushirikiano unaotoka TPDC haswa katika kuanishwa kwa mashindano hayo ya michezo ambayo imeleta hamasa kubwa na furaha kwa wananchi wa Songo Songo.
Mgeni Rasmi akizindua rasmi mashindano ya TPDC CUP katika Uwanja wa Mpira Songo Songo tarehe 13 Novemba, 2017.
“Ndugu zangu wachezaji wa timu zetu pamoja na mashabiki nawaomba tushiriki mashindano haya kwa kufuata Sheria za Uendeshaji wa Michezo za FIFA na Mamlaka nyingine za michezo ili tucheze kwa Amani, furaha na upendo hadi mwisho wa michuano na aliyeshindwa akubali kushindwa ili tumpe hamasa TPDC kuweza kuendelea kudhamini mashindano haya kila mwaka” alifafanua Mwenyekiti wa Kijiji.

Aidha pamoja na kulishukuru Shirika, Mwenyekiti aliomba michezo hiyo pamoja na zoezi la upimaji wa afya liwe la kudumu kama walivyopokea taarifa hapo awali.

Uzinduzi huo ulishuhudia pambano kali lililozikutanisha timu za Black Rhino na Heroes ambapo hadi mwisho wa mchezo timu Black Rhino ilifanikiwa kuitupa nje ya mashindano timu ya Heroes kwa ushindi wa gori moja kwa sifuri.

Katika Mashindano hayo Mshindi wa Kwanza wa Mpira wa Miguu atapata zawadi ya Mbuzi, Jozi moja ya Jezi na Mipira Minne, Mshindi wa Pili atapata Jozi moja ya Jezi na Mipira Miwili na Mshindi wa Tatu atapata Jozi moja ya Jezi na Mpira mmoja.Kwa upande wa Mpira wa Pete, Mshindi wa Kwanza atapata jozi moja ya Jezi na mipira miwili na Mshindi wa Pili atapata Jezi jozi moja pekee.

MHASIBU TAKUKURU, GODFFREY GUGAI APANDISHWA KIZIMBANI NA KUSOMEWA MASHTAKA 43

0
0

Kubeza dhana ya Viwanda ni Mtazamo Finyu na Uliopitwa na Wakati-Waziri Jenista Mhagama

0
0

LAYING WREATH CEREMONY ON 12TH NOV. 2017, TO COMMEMORATES THE FIRST WORLD WAR (1914-18) AT SOKOINE OLD POST OFFICE IN DAR ES SALAAM - THE EAST AFRICA SIGNALS MEMORIAL AND HISTORICAL CENTER

0
0
Richard Painton an Ex- South Africa Corps Engineer blowing the bag pis as a official signs to open the ceremony. 
One of the officials from British High Commision (L), makes a welcome remarks to officiate the ceremony.
The acting Postmaster General, Deo Kwiyukwa (L), speaking during the ceremony.
The Acting Postmaster General Mr. Deo Kwiyukwa infront of memorial plague of ex-soldiers and members of Post Office whose died during the First World War (1914-1918).
The British High Comissioner M/s Sarah Cooke (L), adressing the audience.
The UK deffence attache Lt Col.Ally Kern laying wreath at Sokoine Drive- Old Post Office.
Acting Postmaser General and TPC- Dares salaam Regional Manager M/s Margreth Mlyomi laying a wreath at the Old Post office (Sokoine Drive Post ffice) during the ceremony.
Acting Postmaser General and TPC- Dares salaam Regional Manager M/s Margreth Mlyomi laying a wreath at the Old Post office (Sokoine Drive Post ffice) during the ceremony.
The British High Commissioner m/s Sarah Cooke (Center) with  defence attache Lt. Col. Ally Kern (L) and Acting  
Postmaster General Mr. Deo Kwiyukwa remembering  the  1914-18 East  African Signal  Service  at  the Sokoine drive -Old  Post Office, Dar es Salaam, on 12 November.
Acting Postamaster General Deo Kwiyukwa share a light moment with some of the guests.
Acting Postamaster General Deo Kwiyukwa and Ex-South African Corps Engeneer  Richard Painton  farewell after ceremony.
Group photograph of some TPC staff and members of Tanzania  legions & club.
 Group photograph of Acting Postmaster General (second left) and members of Tanzania Legion&Club.
Acting Postmaster General  and members of Legion&Club of Dar es salaam share a light moment as they leave the wreath laying ceremony.
Group photograph after ceremony. (All photos by Joseph Ngowi of TPC)


*Wartime Askaris, Porters and Signallers honoured in Tanzania

A WEARTH laying ceremony in the historical centre of Dar es Salaam on Sunday remembered the First World War’s East African campaign that claimed thousands of lives in the bitter battles fought in places such as Tanga, Bukoba and Kibata. The ceremony was held at the Old Post Office on Sokoine Drive which houses a monument dedicated to the 234 men of the Royal Engineers Signal Service who died across East Africa in the 1914-18 conflict.

Communication remained difficult throughout the East African campaign. Most commanders relied on dispatch runners, occasionally supplemented by airplanes, or more frequently, dispatch riders on motorcycles.

The British relied on heliographic signals in East Africa using an appliance by which the sun’s rays can be reflected by means of mirrors. Using telegraph networks in remote locations with limited resources proved especially challenging with forces sometimes improvising with barbed wire and using beer bottles or animal bones for insulation.

Radio was used extensively in East Africa because of the distances involved while telephone lines were used over shorter distances. Overhead telephone lines, known as airlines, suffered from damage caused by giraffes running through them. Raising the height helped solve the problem.

RJ Katunda, chairman of the UK Alumni in Tanzania network, who co-organised the ceremony commented:

‘I thank the CEO of the TPC and his team present today for remembering the work of the East African Signal Service that forms part of the postal and telecommunications history of this country.’ He also observed that many of the men who died had been postal or telegraph workers in civilian life across the UK, South Africa and India. Mr Katunda is keen to explore ways to digitise the life stories of the men named on the monument and contribute this to wider heritage initiatives across the city.

A special tribute was also paid at the ceremony to the men of the Tanganyika Labour Corps who lost an estimated 14,000 personnel in four years of conflict. “The vital military labour force provided support to the Royal Engineers and other units from the Commonwealth” explained Antony Shaw, co-organiser of the ceremony ahead of the event that included families of linked to the King’s African Rifles and other British East African Forces, predecessors to the Tanganyika Rifles and present day Tanzania People’s Defence Force.

British Legion Tanganyika Club Secretary David Sawe, who attended the occasion along with the British High Commissioner, explained that Britain’s Remembrance Sunday was observed across the world where Commonwealth forces have died in war. The men from Tanganyika who served with the British in both world wars should not be forgotten said Mr Sawe: ‘The relevance of Remembrance Sunday for modern day Tanzania is that this country’s existence was influenced by the wars that they fought.’

(Ceremony preparation in collaboration with Tanzania Posts Corporation, British High Commision and UK Alumni in Tanzania Networks)

Mhariri Mtendaji wa TSN Afurahishwa na Jarida la Nchi Yetu

0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi nakala ya Jarida la Nchi Yetu Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonaz alipotembelea Ofisi za Idara hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Jarida hilo nit oleo maalum la mwezi Novemba ambalo limeangazia miaka miwili ya uongozi wa Rais Dkt, John Pombe Magufuli.Picha na: MAELEZO

taarifa kwa umma

0
0

TATU MZUKA YACHANGIA MILIONI 100 KUFANYA DODOMA KIJANI

0
0
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba ( katikati) akizungumzia mikakati ya Serikali kuufanya mji wa Dodoma kuwa Kijani wakati akipokea hundi ya shilingi milioni mia moja kutoka Kampuni ya The Net Work kupitia mchezo wa bahati nasibu wa Tatu Mzuka ili kusaidia katika kukabiliana na Changamoto zinazokabili mazingira hapa nchini mapema leo mjini Dodoma. Kulia ni Mkuu wa Mawasiliano Kampuni ya Tatu Mzuka Bw. Sebastian Maganga.kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Injinia Joseph Malongo.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba akipokea hundi ya shilingi milioni mia moja kutoka Kampuni ya The Net Work kupitia mchezo wa bahati nasibu wa Tatu Mzuka mapema leo mjini Dodoma ikiwa ni mchango wa Kampuni hiyo katika kuunga mkono juhudi za Serikali katika kulinda mazingira. Kulia ni Mkuu wa Mawasiliano Kampuni ya Tatu Mzuka Bw. Sebastian Maganga.kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Injinia Joseph Malongo.

Mkuu wa Mawasiliano Kampuni ya Tatu Mzuka Bw. Sebastian Maganga (kushoto) akieleza mikakati ya Kampuni hiyo katika Kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutatua changamoto mbalimbali kabla ya kukabidhi hundi ya shilingi milioni mia moja ili kusaidia Serikali kupambana na changamotozinazokabili mazingira mapema leo mjini Dodoma.Katikati Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba.
Meneja wa TEHAMA wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania Bw. Kabora Mboya ( kulia) akitoa maelezo kuhusu mchango wa michezo ya Kubahatisha katika kujenga uchumi.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia Mkutano wa Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba wakati akipokea hundi ya shilingi milioni mia moja kutoka Kampuni ya Tatu Mzuka ili kusaidia katika kukabiliana na Changamoto zinazokabili mazingira hapa nchini mapema leo mjini Dodoma.

Picha zote na Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma

………………

Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma

Serikali imepokea hundi ya Shilingi milioni mia moja kutoka kampuni ya The Net Work inayochezesha mchezo wa Kubahatisha wa Tatu Mzuka leo Mjini Dodoma kama hatua ya kuunga mkono juhudi za serikali katika Kuboresha Mazingira.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya hundi ya fedha hizo, Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Januari Makamba amesema kuwa fedha hizo zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

” Kwa kuzingatia umuhimu wa Serikali kuhamia Dodoma, tumeamua kuwa fedha hizi zitatumika katika kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani kupitia mpango maalum ambao tulishauandaa kama Serikali na sasa tunashukuru wadau hawa kwa kutuunga mkono” Alifahamisha Makamba.

Akifafanua, Mhe. Makamba amesema serikali imejipanga kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika dhana ya mazingira hapa nchini, hasa kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi.

Aliongeza kuwa sasa ni wakati muafaka kwa wadau kujitokeza kushiriki kikamilifu katika Kulinda mazingira kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.

Kwa upande wake Mkuu wa Mawasiliano wa kampuni hiyo Bw. Sebastian Maganga amesema kuwa Kampuni yake itaendelea kuunga mkono Serikali kwa kuhakikisha kuwa wanachangia katika shughuli za maendeleo katika sekta mbalimbali ikiwemo mazingira.

” Mpango wetu umeanza kwa kuchangia shilingi milioni 100 kwa Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, mchango wetu unalenga kusaidia uboreshaji na ulinzi wa mazingira ambayo ni muhimu kwa maisha ya Watanzania wote” Alisisitiza Maganga

Akifafanua, Maganga amesema kuwa Kampuni yake imetenga milioni 150 katika kusaidia jamii katika sekta za Afya, Elimu na michezo.

Tatu Mzuka ni mchezo wa Kubahatisha ambao umechangia zaidi ya shilingi bilioni 1.2 kama kodi hivyo kuchangia katika kukuza uchumi.
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live




Latest Images