Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

Waziri Prof Makame Mbarawa akijibu hoja kuhusu muswada wa Sheria ya Shirika la Mawasiliano ya Simu Tanzania ya Mwaka 2017


VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMATANO LEO NOVEMBA 15,2017

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa

$
0
0
aziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage amekutana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa alieambatana na wawekezaji wa Kichina walioonesha nia ya kuwekeza katika mkoa wa Iringa.

katika Ziara hiyo, Mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe Bi. Amina Masenza ameelezea mikakati iliyopo katika mkoa wake ya kuhakikisha anapokea wawekezaji na kuwapatia maeneo ya kujenga Viwanda ili kuhahakisha wananchi wanaajiriwa kukuza kipato chao.

Mhe. Waziri amesifu jitihada zinazofanywa na Viongozi wa Mkoa wa Iringa katika kuhakikisha wanahimiza ujenzi wa Viwanda na kushirikiana na wawekezaji.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage (Mb) akimsikiliza kwa makini mkuu wa mkoa wa Iringa Mhe. Bi, Anna Masenza.
Wawekezaji walioonesha nia ya ya kuwekeza katika Mkoa wa Iringa, wakisikiliza kwa makini majadiliano yakiendelea katika ofisi ya Mhe. Waziri wa Viwanda.
Wajume kutoka Mkoa wa Iringa wakimsikiliza Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wakati wakujadili masuala mbalimbali ya uwekezaji katika mkoa wa Iringa.

MIAKA KUMI NA TANO YA THE FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY,MKURUGENZI AELEZA MIPANGO MIPYA

$
0
0
Shirika lisolo la kiserikali ya The Foundation For Civil society linalojihusisha na kujenga uwezo wa asasi za kiraia nchini Tanzania pamoja na Kutoa ruzuku kwa asasi hizo linatimiza miaka kumi na Tano tangu kuannzishwa kwake  na kuanza kufanya kazi.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hii Mkurugenzi mtendaji wa shirika hilo lenye ofisi zake Jijini Dar es salaam Ndugu Francis Kiwanga alisema kuwa kwa miaka kumi na tano ya uwepo wake nchini wamefanikiwa kufanya kazi na Asasi zisizopungua elfu tano nchini ikiwa ni mafanikio makubwa kwa shirika hilo lililojumuisha asasi tofauti.

Nakupa nafasi ya kumsikiliza mkurugenzi wa shirika hilo akieleza kwa undani,kazi walizozifanya kwamiaka 15,changamoto walizopitia nma mipango ya kuendelea kuihudumia jamii kwa sasa.Katibu--- 

MDAU MUGANYIZI BISHEKO ACHUKUA JIKO

$
0
0
Mkuu wa Masoko wa Bank of Africa - Tanzania Bw. Muganyizi Bisheko akiwa na furaha baada ya kufunga ndoa takatifu na Bi. Brenda Ngowo ambae ni mfanyakazi wa CRDB Bank. Ndoa hiyo ilifungwa mnamo wa tarehe 04/11/2017 katika Kanisa la Bungo KKKT, Morogoro.

Mkuu wa Masoko wa Bank of Africa - Tanzania Bw. Muganyizi Bisheko akiwa na furaha baada ya kufunga ndoa takatifu na Bi. Brenda Ngowo ambae ni mfanyakazi wa CRDB Bank. Ndoa hiyo ilifungwa mnamo wa tarehe 04/11/2017 katika Kanisa la Bungo KKKT, Morogoro.

Mkuu wa Masoko wa Bank of Africa - Tanzania Bw. Muganyizi Bisheko akiwa na furaha baada ya kufunga ndoa takatifu na Bi. Brenda Ngowo ambae ni mfanyakazi wa CRDB Bank. Ndoa hiyo ilifungwa mnamo wa tarehe 04/11/2017 katika Kanisa la Bungo KKKT, Morogoro.

Serikali Yaishukuru China

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiongea na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Bibi. Wang Ke (Kulia) katika ofisi za Wizara leo Mkoani Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Bibi. Wang Ke (Kulia) wakiweka saini makubaliano ya kukabidhiana vifaa vya ofisi vyenye thamani ya shilingi milioni 133 katika ofisi za Wizara leo Mkoani  Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Bibi. Wang Ke (wa pili kulia) pamoja na watendaji wa Wizara leo Mkoani Dodoma.Picha na Lorietha Laurence-WHUSM,DODOMA



Na Lorietha Laurence-WHUSM,Dodoma

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amemshukuru Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Bibi. Wang Ke kwa kuipatia wizara vitendea kazi vyenye thamani ya shilingi milioni 133.

Waziri Dkt. Mwakyembe ametoa shukrani hiyo leo Ofisini kwake Mkoani Dodoma alipokutana na Balozi huyo ambapo waliweka sahihi ya makabidhiano ya vifaa hivyo na kuhaidi kuendelea kuimarisha uhusiano huo uliodumu kwa muda mrefu .

“Nashukuru sana Balozi kwa kutupatia msaada wa vitendea kazi na tunaahidi kuendeleza ushirikiano uliopo baina ya nchi hizi mbili kwa manufaa ya taifa na watu wake” amesema Mhe.Dkt. Mwakyembe.

Aidha Waziri Dkt. Mwakyembe ameongeza kuwa tayari kumekuwa na juhudi za wazi zinafofanywa na Ubalozi huo kwa kutoa mafunzo ya kubadilishana utaalam kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa china kupitia sekta za filamu, habari,michezo na utamaduni.

Pia, Dkt. Mwakyembe alimueleza Balozi huyo kuwa Tanzania imepata nafasi ya kuwa Mwenyekiti wa programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika wenye lengo ya kuhifadhi kumbukumbu za harakati za kuikomboa Afrika ili kuwa na historia nzuri kwa kizazi kijacho.

“Tayari tumeanza maandalizi ya kuhifadhi historia ya wapigania uhuru ukizingatia Tanzania ilikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nchi za Bara la Afrika zinakuwa huru, hii ni hatua kubwa kwetu katika kuimarisha mahusiano baina ya nchi zetu ” amesema Mhe. Dkt. Mwakyembe.

Naye Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Bibi. Wang Ke ameeleza kufurahishwa na ushirikiano ulipo baina ya nchi hizo mbili ikiwemo kujifunza tamaduni za China.

“Nimefurahi kuona idadi kubwa ya watanzania wanaojifunza utamaduni wetu kupitia Chuo kikuu cha Dar es Salaama na Chuo kikuu cha Dodoma, ni hatua nzuri na ya msingi katika kuimarisha mahusiano ya nchi zetu” amesema Balozi Wang Ke.

Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China wamekuwa na ushirikiano wa karibu katika kuleta maendeleo tangu mwaka 1960 ambapo walishirikiana katika ujenzi wa reli ya TAZARA na sasa uhusiano huo umezidi kuimarishwa kupitia sekta za habari,filamu, sanaa na utamaduni.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKUTANA NA WABUNGE WANAOTOKA MIKOA INAYOLIMA PAMBA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa kwenye ukumbi wa Msekwa, bungeni Mjini Dodoma kabla ya kikao kati ya Waziri Mkuu na Wabunge wanaotoka mikoa inayolima pamba Novemba 14, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipokutana na wabunge wanaotoka mikoa inayolima pamba kwenye ukumbi wa Msekwa, bungeni mjini Dodoma Novemba 14, 2017. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.
Baadhi ya wabunge wanaotoka mikoa inayolima pamba wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Msekwa, bungeni mjini Dodoma Novemba 14, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wabunge kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma Novemba 14, 2017. Kutoka kushoto ni John Heche wa Tarime Vijijini, Marwa Ryoba wa Serengeti na Esther Matiko wa Tarime Mjini.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Kilimo ifanye utafiti wa kina ili kupata aina bora ya mbegu za pamba zitakazowanufaisha wakulima. Amesema ni lazima utafiti huo ufanyike kwa kuzingatia aina ya udongo unaopatikana katika kila mkoa unaolima pamba. Ametoa kauli hiyo jana jioni (Jumanne, Novemba 14, 2017) alipozungumza na wabunge wanaotoka katika mikoa inayolima pamba, Bungeni mjini Dodoma.

“Mbegu za pamba ziko nyingi na zina migogoro. Mbegu nyingine zina manyoya, nyingine zina vipara hivyo lazima utafiti wa kina ufanyike ili kupata aina bora.”

Alisema Wizara ya Kilimo itumie taasisi zake vikiwemo vyuo kufanya uchunguzi na kubaini ni aina gani za mbegu zinafaa kutumika kulingana na eneo husika. Alisema utafiti huo ambao utabainisha aina ya mbegu inayofaa kulingana na aina ya udongo katika kila eneo ili kumuwezesha mkulima kupata mazao ya kutosha. Pia aliwataka Maofisa Kilimo katika mikoa inayolima mazao makuu ya biashara waweke kipaumbele katika kuyasimia mazao hayo.

Waziri Mkuu alisema Maofisa hao lazima wahakikishe wanayasimamia vizuri mazao hayo ambayo ni korosho, chai, pamba, kahawa na tumbaku ili yawe na tija. Alisema Serikali imeweka mkakati wa kuimarisha mazao makuu ya biashara ambayo uzalishaji wake umeanza kupungua likiwemo na zao la pamba. Waziri Mkuu alisema Serikali inataka kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa zao la pamba kuanzia hatua za maandalizi ya shamba, pembejeo hadi masoko.

“Tunataka kulifanya zao hilo ambalo lilikuwa likijulikana kama dhahabu nyeupe lifikie kiwango cha juu cha uzalishaji, hivyo kuongeza tija kwa wakulima.”

Pia Waziri Mkuu aliwaagiza Maofisa Kilimo katika mikoa hiyo wafanye sensa ili kutambua idadi ya wakulima wa pamba na ukubwa wa mashamba yao. Alisema lengo la sensa hiyo ni kutambua idadi ya wakulima na ukubwa wa mashamba yao ili kurahisisha usambazaji wa pembejeo kulingana na mahitaji.Wakizungumza katika mkutano huo baadhi ya wabunge waliiomba Serikali kuhakikisha zao hilo linaboreshwa ikiwa ni pamoja na kuwafikishia wakulima pembejeo kwa wakati.

Kwa upande wake Mbunge wa Itilima Bw. Njalu Silanga aliiomba Serikali izibane Halmashauri ili kuhakikisha fedha za miradi ya kilimo zinatumika ipasavyo. Bw. Silanga alisema msukumo wa Serikali wa kufufua zao la pamba umeanza kuzaa matunda, hivyo aliiomba Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kutafuta masoko ya kutosha.

Naye Mbunge wa Tarime Mjini, Bi Ester Matiko ameiomba Serikali kuwaelimisha wananchi na kuwahamasisha kulima kilimo hicho ili waachane na kilimo cha bangi.

“Serikali ikitilia mkazo katika usimamizi wa mazao hayo tutasonga mbele na Tanzania ya viwanda tutaiona. Wakulima waelimishwe kuwa mazao hayo yana tija, hivyo wataachana na kilimo cha bangi.”

Bi. Ester alisema kati ya mazao makuu matano ya biashara manne yanalimwa katika jimbo lake ambayo ni chai, pamba, kahawa na tumbaku, hivyo wakulima wakipewa elimu ya kutosha juu za mazao hayo watapata tija.

MASHINDANO YA KUMUENZI MTAKATIFU GASPARI ITIGI

$
0
0
Ni baadhi ya washiriki wa mchezo wa kuvuta kamba kwenye mashindano ya maadhimisho ya kumuenzi Mtakatifu Gaspari,Itigi,wilayani Manyoni.(Picha Na Jumbe Ismailly)

MASHINDANO ya michezo ya maadhimisho ya siku kuu ya kumbukumbu ya kumuenzi Mtakatifu Gaspari Del Buffalo yaliyokuwa yakifanyika katika viwanja vya michezo vya kanisa, hatimaye yamefikia tamati,ambapo timu ya Wafanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Gaspari na chuo cha uuguzi iliyopo katika Mji mdogo wa Itigi,wilayani Manyoni imatawazwa kuwa mabingwa wa mpira wa miguu wa mashindano hayo mwaka huu.

Katika mashindano hayo yalizishirikisha jumla ya timu nane za wanaume za mpira wa miguu na mpira wa pete huku kukiwa na malalamiko yaliyotolewa na baadhi ya viongozi na wachezaji wa timu zilizoshiriki katika mashindano hayo.

Mmoja wa viongozi wa timu ya mpira wa pete kwa wanawake,Hayfat Hassani aliwashauri waandaaji wa mashindano hayo kwamba kwa kuwa timu nyingi zilizoshiriki hazikuwa na jezi,hivyo aliwataka kuangalia uwezekano wa kuzipatia jezi timu zitakazoshiriki katka mashindano ya mwaka ujao.

Aidha akizungumzia kuondokana na malalamiko ya upendeleo unaofanywa na waamuzi,Hayfat alishauri pia kwamba katika mashindano kama hayo kwa mwaka ujao ni vyema waamuzzi wa michezo hiyo wakatafutwa kutoka nje ya maeneo ya Halmashauri ya Itigi.

“Kwa sababu kulikuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wachezaji kuhusu kocha wa timu yetu ambaye naye alikuwa akichezesha kwenye mashindano hayo kuwa alikuwa hazitendei haki timu zingine pinzani na timu yake wakati zilipokuwa zikichuana huku yeye akiwa mwamuzzi wa mchezo huo”alifafanua Hayfat. 

Kwa upande wake kocha msaidizi wa timu ya wafanyakazi wa Hospitali na chuo ha uuguzi cha Mtakatifu Gaspari,Gabrieli Mathayo alipendekeza kuwepo sheria kali zitakazowabana viongozi pamoja na timu zao wenye tabia ya kupanga matokeo ya michezo wanayoshiriki.

Katika risala ya Watumishi wa Hospitali ya rufaa ya Mtakatifu Gaspari na Chuo cha Uuguzi iliyosomwa na Mwalimu Epafradito Frank ilieleza kwamba maadhimisho hayo hutanguliwa na michezo mbali mbali ambapo kipekee mwaka huu yamefanyika michezo ya mpira wa miguu,mpira wa pete,mchezo wa bao,mbio za baiskeli,mbio za maagunia,kuvuta kamba,kukimbia na yai kwenye kijiko na kufukuza kuku.

Naye Mratibu wa maadhimisho hayo mwaka huu,Dk.Peter Nyira aliitaja baadhi ya michezo iliyofanyika kuwa ni pamoja na mpira wa miguu na mpira wa pete ambapo jumla ya timu nane za wanaume zilishiriki mpira wa miguu huku Mkuu wa shirika la wamisionari wa damu Azizi ya Yesu kanda ya Tanzania,Fr,Chesco Msaga akiupongeza uongozi wa Hospitali hiyo kwa kujali sekta ya michezo.

Alpha Abdul ashinda kinyang'anyiro cha Tigo Fiesta Supa Nyota 2017 Mtwara

$
0
0
Mshindi wa Tigo Fiesta Supa Nyota toka mkoa Mtwara, Alpha Abdul akionesha umahiri wake wa kufokafoka kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka mshindi wa shindano hilo la kusaka vipaji kama sehemu ya shamrashamra za msimu wa Tigo Fiesta 2017.
Tano bora walioingia kwenye mchujo wa Tigo Fiesta Supa Nyota 2017 mkoani Mtwara.
Tatu bora walioingia kwenye mchujo wa Tigo Fiesta Supa Nyota Mtwara.
Majaji wakiongozwa na Nickson George (katikati) wakijadili jambo katika shindano la kusaka vipaji la Tigo Fiesta 2017 Super Nyota lililofanyika mjini Mtwara.

REDESO YATOA MAFUNZO K WA WAZAILISHAJI NA WASINDIKAJI WA ZAO LA MKONGE MKOANI SIMIYU

$
0
0
 Mshauri wa kujitegemea, Steven Tilubuza kutoka Mwanza akitoa mada katika mafunzo hayo yaliyofanyika ukumbi wa Halmashauri Kishapu.
 Meneja wa Shirika la Msaada na Mandeleo ya Jamii (REDESO) Kishapu, Charles Buregeya akitoa ufafanuzi kuhusu mafunzo hayo kwa waashiriki.
Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephano Shadrack akitoa mada kuhusu ushirika katika mafunzo hayo.



Na Robert Hokororo, Kishapu DC.

Shirika la Msaada na Mandeleo ya Jamii (REDESO) katika Halmashauri ya wilaya ya Kishapu limewapa mafunzo wazalishaji na wasindikaji wa zao la mkonge kutoka Kishapu na Meatu mkoani Simiyu.

Mafunzo hayo yaliyofanyika ukumbi wa Halmashauri Kishapu yanalenga kuwajengea washiriki hao uwezo wa utumiaji rasilimali kwa tija katika kuzalisha na kukidhi mahitaji ya soko la bidhaa wanazozalisha katika maeneo yao.

Mafunzo hayo yalitolewa kwa pamoja na Mshauri wa kujitegemea, Steven Tilubuza kutoka Mwanza na Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephano Shadrack.Yanatarajiwa kuwapatia washiriki hao kutoka vikundi vya ujasiriamali elimu na ujuzi wa namna ya uanzishaji wa miradi ya maendeleo katika sekta mbalimbali kwenye maeneo hayo.

Meneja wa REDESO Kishapu, Charles Buregeya alisema washiriki hao kutoka vikundi vya ujasiriamali watanufaika na mafunzo hayo ambayo yatawajengea uwezo wa kutambua fursa mbalimbali waliko.“Kupitia mafunzo hayo washiriki wataweza kujikwamua kutoka umaskini na kuwa na fursa nzuri za kujipatia kipato kwani wataweza kuibua na kuanzisha miradi ya maendeleo,” alisema Buregeya.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa mafunzo hayo yatasaidia washiriki kupata elimu ya kubaini na kutafuta masoko ya bidhaa zao wanazozalisha hivyo kupata wigo mkubwa wa wateja.Utaalamu mwingine washiriki wanaopata kupitia mafunzo hayo ni pamoja na namna ya ufungashaji mzuri wa bidhaa zilizozalishwa pia kuzitangaza kupitia njia mbalimbali ili ziwafikie wateja.

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) yatoa zawadi kwa wafanyakazi bora wa mwezi wa tisa na wa kumi

$
0
0
 Daktari Bingwa wa Magojwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani akimkabidhi zawadi ya mfanyakazi bora wa mwezi wa tisa  Adilla  Musa ambaye ni mtunza kumbukumbu katika kikao cha asubuhi cha kujadili mabadiliko na maendeleo katika tasnia ya  magonjwa ya moyo kinachofanyika kila jumatano  katika Taasisi hiyo. Kulia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo Tulizo Shemu na kushoto ni Meneja wa kampuni ya uuzaji wa dawa za binadamu na vifaa tiba ya Samiro,  Masilamani Guru 
 Daktari Bingwa wa Magojwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani akimkabidhi zawadi ya Daktari bora wa mwezi wa  kumi Siza Ngomero  katika kikao cha asubuhi cha kujadili mabadiliko na maendeleo katika tasnia ya  magonjwa ya moyo kinachofanyika kila jumatano  katika Taasisi hiyo. Kulia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo Tulizo Shemu na kushoto ni Meneja wa kampuni ya uuzaji wa dawa za binadamu na vifaa tiba ya Samiro, Masilamani Guru .
 Daktari Bingwa wa Magojwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani akimkabidhi zawadi ya Mfanyakazi  bora wa mwezi wa  kumi Flora Kasembe ambaye ni Msimamizi wa Majengo   kwenye kikao cha asubuhi cha kujadili mabadiliko na maendeleo katika tasnia ya  magonjwa ya moyo kinachofanyika kila jumatano  katika Taasisi hiyo. Kulia ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo Tulizo Shemu na kushoto ni Meneja wa kampuni ya uuzaji wa dawa za binadamu na vifaa tiba ya Samiro,  Masilamani Guru .
 Baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakifuatilia utoaji wa zawadi kwa wafanyakazi bora wa mwezi wa tisa na kumi kwenye kikao cha asubuhi cha kujadili mabadiliko na maendeleo katika tasnia ya magonjwa ya moyo kinachofanyika kila jumatano  katika Taasisi hiyo.Picha na JKCI

Rais Dkt Magufuli awasili jijini Dar akitokea kijijini kwako Chato,mkoani Geita

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasili jijni Dar es salaam muda huu akitokea kijjini kwake Chato, mkoa wa Geita, na kupokelewa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul Makonda na viongozi wengine

WAFANYAKAZI WA BENKI YA CRDB WACHANGIA MILIONI 15 UJENZI WA OFISI ZA WALIMU JIJINI DAR

INTERNET GAME CHANGERS – TRUE REVOLUTION IN TANZANIA

$
0
0
Sometimes it can be painstaking when searching for the right Internet Service Provider (ISP) and your choice can make an enormous difference in your online experience – choose the right one and you are happy and likewise choose the wrong one, and you are left frustrated.

But what tickles your decision making? When I needed an ISP, I asked myself – Is it a good bargain? Are they charging me too much for what I’m getting? Do they provide faster speed? Are they easily available? Will I get online when I need to?

Like handsets, TVs or pair of shoes, you may have a range of ISP choices in your area and trust me I had a whole list of them. Then I realised, ultimately it all dawned back to two crucial things when it comes to internet – accessibility of service and price. I wanted a great bargain but it better work!

A lot of ISPs throw in extras to give you comfort you're getting a great value, free Wi-Fi hotspot access for experience, discounted or lowest packages, good customer care however don’t you agree none of these features matter if you can't use the service when you need to? Like the famous saying, cheap is expensive.

So it’s no wonder I find myself wanting to look at the revolution of internet services in Tanzania. One ISP caught my interest, Smile Communications. It does not represent the country as a whole of course but has been my personal bombshell.

If you recall, the coming of Smile Communications to Tanzania in 2012, for the first time Tanzania got the real taste of internet with no buffering or loading and immediately change came to Tanzania. With its promise for speed, quality and reliability, Smile set the trend of internet experience in a whole new level however their premium internet packages were quickly ridiculed in the market. Shortly after there was this noise about total internet freedom with the ISP’s launch of Unlimited packages with no data caps. You and I know where that went – now everyone can get unlimited bundles – total revolution I say!

Let me ask you something, if you had Tsh 1.4 Million today, imagine the hundreds of things you can use it for – family weekend in Zanzibar, buy one of the latest smartphones, or better yet buy a bodaboda or just crazy and change your wardrobe. But what if I were to ask you instead to recharge your mobile today with the 1.4 million worth of internet bundle, I am crazy right?

This is what it meant getting on SuperFast internet service in Tanzania. But I understand those are now days gone and forgotten. I bumped into an advert just the other day – Bei ya Ndizi – and I was like huh! Is there a new banana price in town? So I did some digging only to discover it’s another one of this ISP surprises. Smile was restructuring its bundle prices with a reduction of up to 80%.This one time bundle worth Tsh 1,400,000 for example is now a mere Tsh 275,000. I got to tell you, it knocked me off my feet. I had to verify it so I checked their website and behold, there it was! I even see you get some as low as Tsh 2,000.

I’m going to start some semi-regular series of “internet game changes”. These articles will largely follow my own buying decisions. The goal here is to dig into the specifics of buying habits of internet services and what drives that decision. Send me your questions and views on what works for you or what you think I should be searching for. I’m not (usually) going to make a specific recommendation however when I see one that speaks to me, well I feel obliged to show you what could be the best.

As an internet user, what’s your take? Talk to me.


Maafisa AAKIA wafurahishwa ulinzi JNIA

$
0
0
 Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Lugano Mwansasu (kulia), akitoa maelezo kwa Maafisa wa Idara mbalimbali kutoka kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume cha Zanzibar (AAKIA) waliofanya ziara ya mafunzo. Kushoto ni Msaidizi wa Mkuu wa kitengo cha Ulinzi na usalama JNIA, Bw. Hamis Mashaka.
 Maafisa wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume cha Zanzibar (AAKIA), Bw. Shaaban Kombo (kuanzia wa pili kulia), Bi. Zakhia Mohamed, Bw. Salehe Said na Bi. Fatma Yussuf wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Lugano Mwansasu (kulia) akiwaelekeza jambo wakati wa ziara yao ya mafunzo iliyofanyika jana.
  Msaidizi wa Mkuu wa kitengo cha Ulinzi na usalama wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Hamis Mashaka (kushoto), akitoa maelezo mbalimbali yanayohusiana na ulinzi na usalama kwa maafisa kutoka idara mbalimbali za Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume (AAKIA) cha Zanzibar jana walipofanya ziara ya mafunzo.
 Meneja Uendeshaji  cha Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Vedastus Fabian (kulia) akiwapa maelezo mbalimbali Maafisa kutoka Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume (AAKIA) walipofanya ziara ya mafunzo jana.
Afisa Habari katika jengo la Watu Mashuhuri la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (VIP-JNIA), Bw. Kenny Kwenga (kushoto) akitoa maelezo ya namna watu mashuhuri wanavyohudumiwa kwa maafisa kutoka Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume (AAKIA), walipofanya ziara jana. Kulia ni Msimamizi wa VIP, Bi. Josephine Mwaisukule. 
.
MAAFISA kutoka Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Abeid Amani Karume cha Zanzibar (AAKIA), wamefurahishwa na namna ulinzi na usalama wa abiria na mali zao unavyofanywa kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), imeelezwa.

Maafisa hao kutoka Idara mbalimbali walitoa kauli hiyo jana katika ziara ya siku moja ya mafunzo JNIA, ambapo walitembelea maeneo mbalimbali na kupata maelezo ya kina kutoka kwa maafisa husika.

Mkuu wa msafara wa maafisa hao, ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Ulinzi na Usalama cha AAKIA, Bw. Shaaban Kombo alisema JNIA inaulinzi madhubuti kwa abiria na mizigo hukaguliwa kwa kutumia mitambo maalum kabla ya kupanda ndege au kuingia ndani ya jengo kwa kazi mbalimbali, ambapo wameahidi kufuata nyayo hizo ili kuzuia uhalifu unaofanywa na baadhi ya watu wasiowaaminifu.

Bw. Kombo alisema pamoja na kupata mambo mengi ya msingi ya uendeshaji wa viwanja vya ndege, JNIA imekuwa darasa tosha, ambapo pia katika upande wa utoaji wa vitambulisho wamejifunza namna utoaji wa vitambulisho unavyofanyika, ukiwa ni tofauti na AAKIA ambao hutoa vitambulisho vya kudumu mara baada ya taratibu kukakamilika, wakati JNIA hutoa vitambulisho vya muda kwa muombaji ili aweze kuendelea na kazi, wakati akisubiri cha kudumu kikamilike kutengenezwa.

“Tumefaidika na mambo mengi ukiangalia sisi kwetu hii ya vitambulisho ni tofauti kabisa, ila kwetu kwa kipindi chote mteja anasubiri kitambulisho cha kudumu anakuwa hawezi kuendelea na kazi zake eneo la kiwanja hadi atakapopata cha kudumu, lakini hapa anakuwa na cha muda kinachomfanya aendelee na shughuli zake huku cha kudumu kikiwa katika matengenezo,” alisema Bw. Kombo.

Naye Mkuu wa kitengpo cha Ulinzi na Usalama cha JNIA, Bw. Lugano Mwansasu alisema ziara ya maafisa wa AAKIA imewafariji na kuanza ukurasa wa mahusiano katika ushirikiano, ambapo nao wamejifunza kulingana na maelezo ya uendeshaji wa AAKIA.

Bw. Lugano alitoa wito kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kuiga mfano huu wa kupeleka maafisa wake kwenye viwanja mbalimbali vya nje ya nchi kwa ajili ya kujifunza utendaji kwa lengo la kuboresha huduma za viwanja kwa ujumla. TAA inasimamia viwanja 58 vilivyopo chini ya serikali.

“Kila siku mambo ya uendeshaji yanabadilika, basi tunaiomba mamlaka yetu itusaidie na sisi kwenda kutembelea viwanja vya wenzetu tujifunze huko, zipo changamoto labda sisi hatujui zinatatuliwaje lakini kwa ziara za mafunzo tunaweza kupata mbinu kutoka kwa wenzetu,” alisema Bw. Lugano.
Katika hatua nyingine, Meneja Uendeshaji wa JNIA, Bw. Vedastus Fabian alisema faida ya ziara ya mafunzo ni kujijengea uwezo na mahusiano mazuri baina ya kiwanja kimoja na kingine.

Bw.Fabian alisema ziara hizo zinasaidia katika kutatua matatizo yanayovikumba viwanja vya ndege, ambapo kwa sasa kumekuwa na masuala ya ugaidi, uvushaji wa dawa za kulevia na nyara za serikali.

SHIRIKA LA PELUM TANZANIA NA HALMASHAURI YA MUFINDI KUTOA HATI MILIKI ZA KIMILA 795

$
0
0
 Mmoja wa wajumbe toka Kamati ya Usimamizi wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi (VLUMC) ya Kijiji cha Makungu akiwasilisha Mpango pendekezwa wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji hicho wakati wa Mkutano wa pamoja uliojadili na kupitisha Mpango wa Matumizi bora ya ardhi katika Kijiji hicho. Mafunzo hayo yaliyofanyika juzi Kijijini hapo yalifadhiliwa na Shirika la PELUM Tanzania. 
Mwanasheria kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa Mufundi, Method Msokeve akiwasomea wananchi wa Kijiji cha Mukungu Wilayani humo sheria ndogondogo zitakatumika wakati wa mipango mbalimbali ya matumizi ya ardhi Wilayani humo. Mafunzo hayo yaliyofanyika juzi Kijijini hapo yalifadhiliwa na Shirika la PELUM Tanzania. 
 Timu ya wataalamu toka Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, na Wafanyakazi wa Shirika la PELUM Tanzania, pamoja na Viongozi wa Serikali za Vijiji vya Kiyowela, Idete na Makungu alama ya Mipaka inayotenganisha vijijiji hivyo kabla ya kufanyika kwa Mpango wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji cha Makungu. Mafunzo hayo yaliyofanyika juzi Kijijini hapo yalifadhiliwa na Shirika la PELUM Tanzania.
Baadhi ya vibao vilivyowekwa katika baadhi ya maeneo ya kijiji cha Mukungu yakionesha mgawanyo wa matumizi ya ardhi katika kila eneo husika. Mafunzo hayo yaliyofanyika juzi Kijijini hapo yalifadhiliwa na Shirika la PELUM Tanzania.

Na Mwandishi Wetu 
SHIRIKA la PELUM Tanzania kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa kupitia linatarajia kutoa hati miliki za kimila 795 kwa wananchi wa Vijiji vya  Ugesa, Isaula, Magunguli na Usokami na Mukungu waliopimiwa ardhi zao kupitia Mpango wa Matumizi bora ya ardhi.

Hayo yamesemwa jana (juzi) Wilayani Mufindi na Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Leonard Jaka  wakati wa zoezi la upitishaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi uliofanywa katika kijiji hicho na Shirika la PELUM Tanzania kupitia mradi wa Ushiriki wa wananchi katika Sekta ya Kilimo (CEGO).

Jaka alisema Wananchi wa kijiji cha Makungu pamoja na vijiji jirani katika Halmashauri hiyo kuchangamkia fursa hiyo ya kupima ardhi zao ili kuweza kuepekana na migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikiathiri shughuli za maendeleo ya wananchi Wilayani humo.

Jaka alisema mpango huo ni muhimu kwa kuwa unatoa kipaumbele kwa wajane, wagane, walemavu, wazee na watu wenye kipato cha chini kupata hati miliki ya ardhi na hivyo aliwataka wananchi ambao hawajapimiwa ardhi zao wahakikishe wanajipanga ili waweze kufikiwa na mpango huo.

“Kupimwa kwa ardhi zenu kutasaidia kuepukana na migogoro ya ardhi, kujihakikishia ulinzi wa ardhi,kuwa na umiliki halali wa kisheria wa ardhi, kuongezeka kwa thamani ya ardhi pamoja na kurahisisha upatakanaji wa mikopo kwa kuweka ardhi yako kama dhamana,” alisema Jaka.

 Aidha Jaka aliwakumbusha wananchi wa kijiji cha Makungu wajibu wao katika kusimamia kikamilifu mpango kwa kutoingilia au kuuuza maeneo ya huduma za kijamii ambayo yaliyopimwa na kuutaka Uongozi wa Serikali ya Kijiji kuchukua hatua za kisheria kwa wote watakaobainika kwenda kinyume na sheria ndogo walizojiwekea.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Makungu, Donatus Mnoga alisema kijiji chake pamoja na vijiji jirani wamekuwa katika hali ya sintofahamu ya kugombea mipaka toka mwaka 2008 bila ufumbuzi jambo lililokuwa lilileta mkanganyiko wa idadi halisi ya vitongoji vilivyopo katika mamlaka yake.

Alisema kupitia mradi wa CEGO unaotekelezwa kwa ushirikiano na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, hivi sasa Viongozi wa Serikali za Vijiji hivyo wameweza kukutanishwa na hatimaye kupata suluhu ya kudumu ya tatizo ikiwemo kurejeshwa kwa kitongoji cha Lole katika kijiji cha Makungu hatua inayokifanya kijiji hicho kuwa vitongoji vitatu kwa sasa.

Naye Mkazi wa Kijiji hicho cha Mukungu, Gaudensio Mwagala alilishukuru Shirika la PELUM Tanzania na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa kuweka utaratibu wa kuwapimia ardhi yake na kusema jambo litalosaidia kuondoa utata wa urithi wa umiliki wa ardhi yake katika siku za usoni.

Mradi wa Ushiriki wa wananchi katika Sekta ya Kilimo (CEGO) unaofadhiliwa na Shirika la Misaada La Marekani (USAID) unatekelezwa katika Halmashauri sita zilizopo katika Mikoa ya Dodoma, Morogoro na Iringa.

Serikali yalifungia shirika lisilo la kiserikali la TSSF

Rais Dkt Magufuli aagiza jengo la Makao makuu ya tanesco na Wizara ya Maji yawekwe x ili yabomolewa kupisha mradi wa ujenzi

$
0
0
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan walipokuwa wakitembelea na kukagua ujenzi wa barabara ya Flyover ya TAZARA mapema leo,kulia ni Mkuu wa mkoa Dar Mh Paul Makonda.Wakati huo huo  pia Rais Dkt Magufuli ametembelea mradi wa ujenzi wa barabara za juu za Ubungo ‘Ubungo Interchange’, katika ukaguzi wa Ubungo Rais Dkt Magufuli ameagiza jengo la makao makuu ya TANESCO lililopo eneo hilo pamoja na jengo la wizara ya maji ambalo liko mkabala na jengo la TANESCO, yawekwe alama ya ‘X’ ili yabomolewe kupisha ujenzi wa mradi huo.
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akizungumza mapema leo mbele ya baadhi ya Wananchi (hawapo pichani) walikuwepo katika eneno hilo, mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa barabara ya Flyover ya Tazara,kushoto ni Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh.Paul Makonda
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan wakiwa sambamba na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh.Paul Makonda walipokuwa wakiwasili maeneo ya Ubungo na kuanza kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa barabara za juu za Ubungo ‘Ubungo Interchange’, ambapo katika ukaguzi huo Rais Dkt Magufuli ameagiza jengo la makao makuu ya TANESCO lililopo eneo hilo pamoja na jengo la wizara ya maji ambalo liko mkabala na jengo la TANESCO, yawekwe alama ya ‘X’ ili yabomolewe kupisha ujenzi wa mradi huo.
  Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa ameambatana na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan wakimsikiliza mmoja wa Wakandarasi wa mradi huo wa ujenzi wa barabara za juu ‘Ubungo Interchange’,mapema leo 
Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi mbalimbali waliokuwa wamejitokeza mapema leo,wakati Rais Dkt John Pombe Magufuli (pichani kulia),alipokwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za juu za Ubungo ‘Ubungo Interchange’,mapema leo jijini Dar.
 Baadhi ya Wafanyakazi wa mradi huo wakishangilia wakati Rais Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza nao 
 Maendeleo ya Ujenzi wa Flyover ya Tazara jijini Dar Es Salaam kama unavyoonekana pichani mapema leo mchama,ambapo Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassani walitembelea na kujionea maendeleo yake,ambapo Mkandarasi wa mradi huo amesema kuwa asilimia 63 ya ujenzi umekamilia na kwamba Flyover hiyo inatarajiwa kufunguliwa Agosti 8,2018 badala ya Desemba 2018.

ETIHAD AIRWAYS MARKS OPENING OF LOUVRE ABU DHABI WITH SPECTACULAR A380 FLY-BY

$
0
0
 An Etihad Airways Airbus A380 conducts a low-level fly-by of the new Louvre Abu Dhabi

‘From Abu Dhabi to the World’ - Airline celebrates capital’s new architectural wonder

Abu Dhabi, United Arab Emirates – Hundreds of visitors from around the world, attending yesterday’s official public opening celebrations of the Louvre Abu Dhabi, were treated to a low-level fly-by of the Jean Nouvel designed museum by one of Etihad Airways’ flagship Airbus A380 aircraft. 

Sporting the airline’s ‘Facets of Abu Dhabi’ livery, the aircraft chosen for the display now also features Louvre Abu Dhabi’s official logo on each of its four engines, to promote the opening of the institution.

Etihad Airways also took the opportunity to capture a series of spectacular images from the fly-by, and commissioned a short video directed by up-and-coming Emirati director, Ahmed Abdulqader, shot from the flight deck of the aircraft and from within Louvre Abu Dhabi, to celebrate the historic occasion. Two specially equipped helicopters were also positioned above the capital to capture air-to-air filming of the aircraft as it flew over the museum, located in the UAE capital’s Saadiyat Cultural District.

Peter Baumgartner, Etihad Airways Chief Executive Officer, said: “Echoing the sentiments from the signing of our landmark partnership agreement with Louvre Abu Dhabi last month, Etihad Airways is today honoured to play its part in the inauguration of this hugely important universal institution.

“Abu Dhabi can now proudly take its place among the world’s foremost cultural destinations, and we, as the UAE’s national airline, are poised to play our part in bringing millions of guests to our home to experience this modern wonder of art and humanity first-hand.”

The Etihad Airways Airbus A380 and Boeing 787 fleets feature multi award-winning interiors influenced by Abu Dhabi’s architecture and landscape. These include ceiling designs and light projections in the boarding zones, Lobby Lounge, First Class and The Residence cabins of the A380s, and stylised sconce lighting in the Business Studios of both aircraft types - all inspired by Louvre Abu Dhabi’s spectacular dome and its ‘Rain of Light’ effect, mimicking the way sunlight streams through the fronds of palm trees in a desert oasis.

Etihad Airways is the Louvre Abu Dhabi’s official airline partner, having signed the first exclusive platinum partnership in October.

As a Platinum partner, Etihad Airways will work closely with Louvre Abu Dhabi on areas of brand partnership, marketing, social media, public and media relations, events and exhibitions, cultural exchanges, cargo support, inflight programming, and travel trade support. Etihad Airways’ destination management company, Hala, will collaborate with the museum on bespoke tour packages in Abu Dhabi.

To coincide with the opening of Louvre Abu Dhabi, Etihad Holidays, the airline’s holiday division, is launching a set of all-inclusive destination packages which showcase the many varied attractions of Abu Dhabi and which feature the museum prominently.

ZAINA FOUNDATION HELP WOMEN TO ICREASE KNOWLEDGE IN CYBER SECURITY

$
0
0
Zaituni explained about password manager and how it can helps to secure  password, and reuse one password for many accounts and how to create strong password.
Zaituni facilitated about Mobile Safety:  She explained mobile rules and advantages and disadvantages of using smart phone and dump phone.
Some of Participants during reflection about day one before we started day 2 agenda.
Group photo with some participants with banners of different agenda of our workshop.


Recently Zaina Foundation hosted two days training about Digital Security for Women’s in Arusha Tanzania with great support from Internews,Defend Defenders from Kampala Uganda and trainers Mr. Paschal Masalu Founder us Elimika Wikiendi and Badru Juma from YUNA Tanzania. . The objective of workshop where to empower women’s and girls to be aware and get knowledge about digital security skills 

In that training twenty (20) participants and Zaituni safe sister fellow in East Africa was a facilitator, stay together and learn several topic about digital security skills and practiced all skills acquired by using their devices also participant learn and practiced new tools like Signal Mobile app in their phone. 

Online Safety was one of the topic covered during the workshop, in this participant learn about hackers who, how and why people get hacked in online this was important because women are at high risk when they are online compared to men, so they get knowledge on password and password manager which will help them to stay safe online.

Also due to the fact that we are in digital world, most of people are using Internet and especially in social media like Facebook, Twitter and instagram which are common to everyone due to this participant trained how to secure their accounts and teach them ten rules of social media and how to use social media in a positive way.

They also get knowledge about two factor authentication which help users to know someone who try to inter/log to your account, Computer hygiene securing computer with antivirus and how to be protected while we are in internet, Mobile Safety this was important because most of internet users they use through their mobile devices.

Other topic where topics were encryptions, full disk encryption, vera crypt and mail velop this was important because they wanted to make sure participants have end to end encryption in their communication in email and chats.

Lastly participants were introduced about cyber law in Tanzania and how to avoid cyber bulling; the law was signed since 2015 and from the workshop it help participants to be more aware about cyber security and they are more safe

Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images