Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA JUMATANO LEO OCTOBER 18,2017


SERIKALI YA IRELAND YAPONGEZA TASAF KWA KUTEKELEZA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI KWA MAFANIKIO.

$
0
0

 Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF,Ladislaus Mwamanga akitoa maelezo kwa waziri wa Mambo ya nje wa Ireland namna shughuli za kuhawilisha fedha zinavyotekelezwa kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.
 Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland akizungumza na Mkurugenzi wa TASAF,Ladislaus Mwamanga  wakati waliposhuhudia zoezi la kulipa ruzuku kwa baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya masikini katika wilaya ya  Misungwi,mkoani Mwanza.
 Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland Ciaran akipata maelezo kutoka kwa baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini wilayani Misungwi unaotekelezwa na TASAF namna walivyonufaika na huduma za Mpango huo.
 Mkuu wa mkoa wa Mwanza,John Mongela akihutubia wananchi (hawapo pichani ) katika ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland( aliyeketi kushoto )
 Waziri wa Mambo ya nje wa Ireland aliyeshika kipaza sauti akiwahutubia baadhi ya walengwa wa TASAF (hawapo pichani) katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongela (aliyevaa kofia) akiwa na mgeni wake waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland wakiwa na baadhi ya walengwa wa TASAF wakiwa na vyeti vya bima ya afya ya jamii waliyopata baada ya kujiunga na bima hiyo kwa kutumia  sehemu ya ruzuku ya  TASAF.


NA ESTOM SANGA- MISUNGWI

Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa wa Ireland bwana Ciar`an Cannon T.D amepongeza jitihada za serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma za jamii na kuwajengea uwezo wa kiuchumi wananchi hususani wanaokabiliwa na umaskini .

Bwana Ciar`an ametoa pongezi hizo alipofanya ziara katika wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza ambako amekutana na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF na kupata ushuhuda wa namna walivyonufaika na Mpango huo.

Baadhi ya Wananchi wanaonufaika na huduma za TASAF wamemweleza waziri huyo kuwa tangu waorodheshwe kwenye Mpango wameboresha maisha yao kwa huku wakijengewa misingi ya kujitegemea kwa kuanzisha miradi midogo midogo ya kiuchumi,kuboresha na makazi yao .

Aidha baadhi ya walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini wameeleza kuwa wamepata mafanikio makubwa katika sekta ya elimu na afya katika kaya zao baada ya kujiunga na Mfuko wa Afya Jamii kwa kutumia fedha walizozipata kutoka TASAF na hivyo kuwapungizia mzigo mkubwa wa matibabu katika kipindi cha mwaka mzima,jambo ambalo wamesema limeboresha afya zao.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje wa Ireland amesema serikali yake imevutiwa na utekelezaji wa shughuli za TASAF na ili kuunga mkono juhudi hizo imepanga kuchangia kiasi cha shilingi bilioni 7.3 katika kipindi cha mwaka huu ili kufanikisha shughuli za Mpango huo ambao ni miongoni mwa mipango mikubwa ya huduma za kijamii inayotekelezwa barani Afrika.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Mwanza Bwana John Mongela amewataka walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kuendelea kuzitumia vizuri fedha na huduma nyingine wanazopata kupitia TASAF ili kupambana na umaskini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga ameishukuru serikali ya Ireland kwa kutambua jitihada za kupambana na umaskini na kuahidi kuwa Mfuko huo utaendelea kuzingatia maelekezo ya serikali ya Tanzania katika kuboresha huduma kwa kaya za walengwa wa Mpango huo zipatazo milioni 1.1 nchini kote.

PUBLIC NOTICE- ANNUAL ICT PROFESSIONALS CONFERENCE

$
0
0
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
MINISTRY OF WORKS, TRANSPORT AND COMMUNICATION
 INFORMATION AND COMMUNICATIONS TECHNOLOGY COMMISSION

 PUBLIC NOTICE

ANNUAL ICT PROFESSIONALS CONFERENCE, 2017 (AIPC-17)
         
1.INTRODUCTION
The Annual Conference for ICT Professionals 2017 (AIPC-17) is a platform for discussion, networking and raising awareness to ICT professionals and stakeholders on the global ICT affairs and skills needed by Tanzanians to cope with the dynamic digital economy. This year’s conference is the commencement of a series of annually held ICT Professionals Conference to be organised by the ICT Commission to discuss on topical developments in ICT especially on how to transform the dynamic growth of ICT into an opportunity for digital industrial development in Tanzania.The theme of this year’s conference is “Building the Tanzania Digital Industrial Economy”.
2.CONFERENCE TOPICAL ISSUESAIPC-17 seeks to strengthen the synergy between the Tanzanian ICT Professionals and other ICT stakeholders towards the advancement of professional competency and business development in the Tanzanian ICT Industry.  The conference will be a two days event held on 26th -27th October 2017 in Dar es Salaam at the Julius Nyerere International Conference Centre. The conference among other issues will discuss the following issues:
a.    Principals of profession accreditation in ICT: An introduction on the ICT Professionals Accreditation Framework outlining the recognition procedures and continuous skills development plan for ICT Professionals in Tanzania will be presented for discussion and adoption by participants.

b.    Trust and confidence in digital industrial economy: The conference will also examine the emerging global trends in the context of Cyber security and digital forensics and what further needs to be done to strengthen cyber security ecosystem in Tanzania and skills set needed towards achieving a truly secure and trustworthy cyberspace.
c.    Challenges and opportunities with evolving technologies: how can Internet of Things (IoT) can shape the future organizations and socio-economic development of Tanzania. The impact of IoT to individuals and businesses, and arising opportunities will be outlined. The future of Cloud and Big Data in Tanzania; the opportunities and challenges to the ICT industry, looking into Data Analytics in Cloud, Public Key Infrastructure, Artificial intelligence, and how the ICT industry can leverage open and big data will be topical discussions.

d.   Smart cities in digital industrial era: Innovation towards Smart Cities, how Governance must change to enable Smart City initiatives, role of public, private and development partners towards intelligent sustainable cities, technologies shaping the smart cities and how to position ICT towards Smart Cities will be presented.

e.    Digital agenda for Tanzania: Trends of digital transformation and its impact on future businesses and organization models will be held.

f.     Jobs and entrepreneurship in ICT: The Future Enterprise; Innovation Strategies and initiatives promoting new forms of Enterprises in the Digital Economy. What need to be done by ICT stakholders to enhance ICT Business innovation in Tanzania?

g.    Role of Private Sector in Mobilizing ICTs for social-economic development: The role of the private sector in mobilizing ICTs to achieve the country's Development Goals will be discussed.

3.PARTICIPANTS
Participants to the Annual Conference for ICT Professionals will include ICT Professionals from both public and private sector, Senior Government Officials, Experts from ICT industry, Representatives from NGO’s, Academia, ICT Partners, Donor agencies, multinational and local ICT Companies

4.CONFERENCE OUTCOME
The outcomes of the conference is awareness to ICT Professionals on the global ICT industry set up, developments and existing ICT skills demand. ICT business promotion and investment opportunities towards a successful digital industrial economy in Tanzania is also considered the important outcome of the conference. Finally, advice resulting from deliberations from stakeholders and ICT Professionals will be shared with the Government for consideration towards successful ICT development in Tanzania.
5.CONFERENCE HOST
The conference is hosted by the Information and Communication Technology Commission, the government ICT promotion body under auspices of the Ministry of Works, Transport and Communications established in November 2015.The ICT Commission has been mandated to coordinate implementation of the National ICT Policy through fostering investment in ICT, build capacity and promote ICT professionals, advice and collaborate with other stakeholders through ICT research and foresight.

UKARABATI UWANJA WA NDEGE KIA KUKAMILIKA DESEMBA.

$
0
0
Serikali imesema ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu ambapo kwa sasa umefika zaidi ya asilimia Tisini. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mheshimiwa Elius Kwandikwa, mara baada ya kukagua ukarabati wa jengo la kupumzikia abiria na upanuzi wa maegesho ya ndege katika uwanja huo leo mkoani Kilimanjaro.

"Nimeridhishwa na ukarabati unaoendelea katika uwanja huu na nafikiri mmejionea wenyewe kazi inaendelea vizuri, hivyo naamini kutokana na hali hii kazi itakamilika hivi karibuni, amesema Naibu Waziri Kwandikwa.

Aidha, Naibu Waziri huyo amefafanua kuwa ukarabati huo ambao pia umehusisha maboresho ya mfumo wa maji taka unalenga kuleta tija kwa mkoa huo na Taifa kwa ujumla kutokana na kuwepo ongezeko la abiria, huduma za kijamii na kibiashara.

Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kukarabati na kujenga viwanja vya ndege nchini ili kurahisisha huduma za usafiri wa anga kwa wananchi wake lengo likiwa ni kuchochea fursa za kiuchumi ambazo zitasaidia kulipeleka Taifa katika uchumi wa kati.

Kwa upande wake, Meneja Miradi wa KIA, Mhandisi Mathew Ndossi, amesema kuwa maegesho yatakapokamilika yatakuwa na uwezo wa kuegesha jumla ya ndege kubwa 11 kwa wakati mmoja badala ya 6 zinazoegeshwa sasa.

Ameongeza kuwa abiria wanatarajiwa kuongezeka kutoka laki nane kwa mwaka hadi kufikia milioni moja na laki mbili mara baada ya kukamilika kwa uwanja huo.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Kwandikwa amekagua barabara ya Sakina - Tengeru (km 14.1) na barabara ya mchepuko ya Arusha (Arusha Bypass km 42.4) ambapo amesema kuwa kukamilika kwa barabara ya Sakina - Tengeru ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na wageni wanaoingia katika mkoa huo kwani kumepelekea kupungua kwa ajali na msongamano wa magari katika eneo hilo.

Ametoa wito kwa wananchi kuzitunza barabara na kutunza mazingira yanayozunguka barabara hizo ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Arusha Mhandisi, Johny Kalupale, amemhakikishia Naibu Waziri huyo kufanya kazi kwa ubora na kwa weledi ili kutimiza malengo ya Serikali ya kuwajengea wananchi miundombinu bora na ya kisasa.

Awamu ya pili ya mradi huo sehemu ya barabara ya mchepuo ya Arusha (Arusha Bypass), inayofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), inatarajiwa kukamilika mwakani na kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 67.

Naibu Waziri Kwandikwa amemaliza ziara ya kikazi katika mkoa wa Kilimanjaro na Arusha ambapo amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara yake.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. 
Meneja Miradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Mhandisi Mathew Ndossi, akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius Kwandikwa (Mb), (Kushoto), upanuzi wa maegesho ya ndege uliofanyika uwanjani hapo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius Kwandikwa (Mb), akikagua maboresho ya mfumo wa majitaka katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alipofika uwanjani hapo kujionea hatua zilizofikiwa za ukarabati wa uwanja huo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius Kwandikwa (Kulia), akitoa maelekezo kwa Meneja Miradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Mhandisi Mathew Ndossi (Katikati), alipofika uwanjani hapo kujionea hatua zilizofikiwa za ukarabati wa uwanja huo.
Mafundi wakiendelea na ukarabati katika jengo la abiria la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA). Ukarabati huo umefika zaidi ya asilimia Tisini na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba mwaka huu.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elius Kwandikwa,akifafanua jambo kwa Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoani Arusha, Mhandisi Johny Kalupale, alipokagua barabara ya Sakina – Tengeru (KM 14.1) na Barabara ya Mchepuko ya Arusha (Arusha Bypass KM 42.4) mkoani Arusha.
Muonekano wa Barabara ya Sakina – Tengeru (KM 14.1), mkoani Arusha,ambayo imekamilika kwa kiwango cha lami. Kukamilika kwake kumesaidia kupunguza ajali na msongamano katika eneo hilo.
Muonekano wa Daraja la Ndurumo lililopo katika barabara ya Sakina – Tengeru (KM 14.1), mkoani Arusha.

WAZIRI KAMWELWE AFURAHISHWA NA UTENDAJI WA MAMLAKA YA MAJI MOSHI

$
0
0
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Tenki la Maji la Njari.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira wakifungua bomba kuashiria uzinduzi wa Mradi wa Maji wa Mang’ana.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe amkimtua ndoo kichwani mama kutoka Kijiji cha Mang’ana, akiashiria kutimiza lengo la Serikali ‘‘kumtua mama ndoo kichwani’’ baada ya uzinduzi wa Mradi wa Mang’ana.
Msafara wa Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe ukielekea kwenye Chanzo cha Maji cha Mang’ana katika uzinduzi wa Mradi wa Mang’ana.



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isack Kamwelwe ametoa pongezi nyingi kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Moshi (MUWSA) kwa kufanikiwa kutoa huduma ya majisafi na salama kwa asilimia 100 kwa Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Hayo aliyasema alipokuwa akizindua Mradi mkubwa wa Maji wa Manga’na, uliopo Kata ya Uru Kaskazini, utakaohudumia zaidi ya vijiji 11 katika Manispaa ya Moshi na Wilaya ya Moshi Vijijini baada ya kupokea taarifa ya hali ya huduma ya maji katika Mji wa Moshi.

“Nawapongeza MUWSA kwa kazi kubwa na nzuri mliyoifanya, kwa kuwa ndio lengo la Serikali, kuwa ifikapo mwaka 2020 maeneo ya vijijini huduma ya majisafi na salama ifikie asilimia 85 na mijini asilimia 95. Nyinyi leo hii mmeshavuka lengo hilo kwa Manispaa ya Moshi, kwa kweli nimefurahishwa sana na jambo hili na mnastahili pongezi nyingi’’, alisema Mhandisi Kamwelwe.

Waziri Kamwelwe aliendelea kusema kuwa kwa kufanikiwa lengo hilo, mamlaka hiyo sasa itaongezewa maeneo mengine zaidi, ili kufikisha huduma ya majisafi na salama kwa wakazi wengine wa Moshi Vijijini ambao hawajafikiwa na huduma ya maji, na kuahidi kama Waziri mwenye dhamana ya maji atawatafutia fedha kwa ajili ya kufanikisha lengo hilo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kamwelwe ameagiza halmashauri zote nchini, kuwa usifanyike ujenzi wowote wa miradi kabla ya kupata chanzo cha maji cha uhakika, ili kuondokana na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maji nchini.

Waziri Kamwelwe alisema ni ufisadi kutengeneza miundombinu ya maji, bila kuwa na chanzo cha uhakika cha maji. Sitakubali miradi ikamilike halafu isitoe maji, wakati umefanyika uwekezaji mkubwa wa fedha za Serikali. Hivyo, ni marufuku mradi wowote kukamilika bila kutoa maji.

Naye Mkurugenzi wa MUWSA, Joyce Msiru alisema katika taarifa yake kuwa mradi huo ni moja ya miradi mikubwa iliyotekelezwa na mamlaka yake, ukiwa umegharimu zaidi ya Sh. bilioni 2 na utahudumia zaidi ya wananchi 34,000.

Mkurugenzi Msiru alitaja baadhi ya vijiji vitakavyohudumiwa na mradi huo kuwa ni Kariwa, Longuo, Njari, Rau, Okaseni na Msuni.

VODACOM YAMKABIDHI MKWANJA WAKE SHAFIK BATAMBUZE WA SINGIDA UNITED

$
0
0
Mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara mwezi Septemba wa Singida United, Shafik Batambuze akiwa ameshikilia hundi yake yenye thamani ya shilingi Milioni 1/- baada ya kukabidhiwa rasmi na wadhamini wakuu wa ligi kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi huo.
 Meneja wa chapa wa Vodacom Tanzania,Yvonne Maruma(kushoto)akimkabidhi hundi yenye thamani ya Tsh.Milioni 1/=mchezaji bora wa mwezi septemba,Shafik Batambuze wa timu ya Singida United inayoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,Katikati ni Afisa Udhamini na Matukio wa kampuni hiyo,Ibrahim Kaude.

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC,Ambao ndiyo wadhamini wa ligi kuu Tanzania bara,Jana wamemkabidhi mchezaji bora wa ligi kwa  mwezi septemba wa Singida United,Shafik Batambuze hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 1/- kwa kuibuka mchezaji bora wa mwezi huo.

Akimkabidhi hundi hiyo Meneja wa Chapa wa kampuni hiyo,Yvonne Maruma alisema kwa mjibu wa taratibu unaofanywa na kamati ya Tuzo ya VPL iliyopo chini ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Vodacom ikiwa kama mdhamini mkuu haina budi kutekeleza matakwa yote yale yaliyopo katika mkataba na kuweza kutoa kitita cha shilingi milioni 1/-kwa mchezaji bora wa kila mwezi ikiwa na lengo la kuwapa motisha wachezaji wote wanaoshiriki ligi kikuu,Alisema Maruma.

“Kwa mjibu wa wa kikao cha kamati ya Tuzo ya VPL imeonesha kwamba mchezaji huyu alitoa mchango mkubwa kwa singida united kupata pointi 10 katika michezo mine,ambayo timu yake ilicheza kwa mwezi huo,matokeo ambayo yaliiwezesha Singida United kutoka nafasi ya 10 katika msimamo na kupanda hadi nafasi ya nne kwa mwezi huo wa Septemba,Singida United ndiyo timu iliyokusanya alama nyingi kwa mwezi huo ukilinganisha na timu nyingine 15 zinazoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara”,Alisema Maruma

Kwa upande wake Sharif Batambuze,aliishukuru kamati ya tuzo ya ligi na wadhamini wakuu kwa kumpatia fedha hizo na kusema atazitumia vizuri ili iwe kumbukumbu nzuri katika maisha yake kwa msimu wa 2017 Batambuze.

TACOSODE WATOA DIRA YA KUTATUA CHANGAMOTO ZA SEKTA YA AFYA HASA VIJIJINI

$
0
0

Na Fredy Mgunda,Iringa.

BARAZA la Vyama vya hiari na Maendeleo ya Jamii (TACOSODE) limesema wananchi wamekuwa na uelewa kuhamasisha bajeti kuwa na kipaumbele kwa changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga wakati akizungumza semina ya kujadilia jinsi gani ya kutatua changamoto zinazoikumba sekta ya afya iliyofanyika katika ukumbu wa valentine Manispaa ya Iringa.

“Unajua zamani wananchi hata viongozi wa sekta ya afya walikuwa wagumu kuelezea changamoto zinazowakabili lakini saizi wananchi na viongozi wamekuwa na elimu ya kutosha juu ya kueleza changamoto zilizopo katika sekta hiyo ndio maana vitu vingi vinaibuka muda huu” alisema Kapinga

Kapinga alisema licha ya serikali kufanya juhudi kutatua changamoto ili kuto huduma ya afya bora lakini bado sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinakwamisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

“Ukiangalia tafiti nyingi zinaonyesha kuwa serikali imekuwa ikishindwa kuongeza bajeti ya sekta ya afya ili kufikia asilimia 15 ya bajeti yote ya serikali kwa kuzingatia azimio la Abuja” alisema Kapinga

Aidha kapinga alisema kuwa moja ya changamoto kubwa ni uhaba wa kupatikana kwa dawa muhimu,vitendanish na vifaa tiba kulinganisha na utafiti wa mwaka 2012 ulifanywa na taasisi ya afya ya Ifakarana kugundua kuwa asilimia 41 ya dawa muhimu zinahitajika kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli aliwataka watumishi wa sekta ya afya kuzibaini changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi kushirikiana na serikali panoja na sekta binafsi.

“Unajua kweli kuna changamoto nyingi ambazo zinawakabili hivyo ni lazima muwe wabunifu kuzitafutia ufumbuzi lakini kwenye hizi sekta binafsi kuwa wasomi wengi ambao wanaweza kutoa ushauri mzuri wa kutatua changamoto zilizopo” alisema Kimuli 

Kimuli alisema kuwa wananchi wamekuwa na uelewa wa maswala ya afya kutokana na elimu waliopata katika mradi wa uhamasishaji wananchi kushiriki katika masuala ya afya katika kuangalia vipaumbele vya bajeti uliokuwa ukitekelezwa katika Mikoa ya Iringa pamoja na Dodoma.

Alisema kuwa wananchi mradi huo katika utekezwaji wake katika Halmashauri ya Iringa pamoja na Kongwa mkoani Dodoma wananchi wamekuwa na mwamko katika masuala ya afya ushiriki kwa kuchangia katika huduma za afya.

Kimuli alisema kuwa mradi huo wa miaka minne umekuwa na matokeo katika wilaya ambazo umetekelezwa kwa wananchi kuwa na mwamko katika masuala ya huduma za afya kwa kuchangia hata nguvu zao pale panapobidi.

Aidha amesema kuwa mradi huo ukiisha wanaweza kufanya katika sekta zingine ili kuwa maendeleo ya katika masuala mbalimbali kutatuliwa.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Abel Mgimwa alisema kuwa serikali ya awamu ya tano imejipanga kuahakikisha changamoto zinatatuliwa kimkakati kulinga na bajeti wanayokuwa wameipanga.

“Ukiangalia bajeti ya mwaka wa fedha mwaka huu imepanda hivyo ni dalili njema za kuanza kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikidumu kwa miaka mingi na kuwaomba wananchi na viongozi kuwa na subira katika kipindi hiki cha utatuzi wa changamoto hizo” alisema Mgimwa

Mgimwa aliwapongeza TACOSODE kwa mchango wao katika sekta ya afya ambayo imekuwa na changamoto nyingi hivyo sio rahisi kwa serikali kutatua kwa haraka hivyo.
 Mkurugenzi wa Miradi wa Tacosode, Theofrida Kapinga akizungumza jambo wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa valentine mkoani Iringa
Afisa mchechemzi wa mradi Abrahm Kimuli akiendelea kutoa elimu kwa wanasemina walikuwa wamehudhuria katika ukumbi wa valentine
 Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mijadala ya sekta ya afya na jinsi gani wanaweza kutatua changamoto zinazoweza kuikoa sekta ya afya hapa nchini

Kongamano la Vijana lafana Jijini Mwanza

$
0
0
Msanii Kala Jeremiah akitumbuiza kwenye Kongamano la Uzinduzi wa Mabaraza ya Vijana Jijini Mwanza, lililofanyika uwanja wa Furahisha jumapili Oktoba 15,2017.

Binagi Media Group
Kongamano hilo liliandaliwa na taasisi ya Youth & Environment Vision ya Jijini Mwanza kwa kushirikiana na taasisi ya Umoja wa Mataifa ya UNA Tanzania, The Foundation for Civil Society pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo Cocacola, TCRA, pepsi na Tecno.

Mgeni rasmi alikuwa Kaimu Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, William Mnyippembe ambaye aliwasisitiza vijana kujitambua kama ambavyo sera ya taifa ya vijana ya mwaka 2007 inavyosisitiza kwa kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo.

Aidha aliwataka kutumia vyema mitandao ya kijamii na kujiepusha na usambazaji wa jumbe zizizo na maadili katika jamii ikiwemo jumbe za uchochezi ambapo kongamano hilo liliwahusisha pia vijana kutoka shule mbalimbali Jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa taasisi ya Youth & Environment Vision, Jonathan Kassib alisema kongamano hilo lililenga kuwahamasisha vijana kuunda na kujiunga na mabaraza ya vijana katika mitaa yao kwa ajili ya utatuzi wa changamoto zinazowakabili ikiwemo kutumia fursa zinazowazunguka kupitia fedha za asilimia tano zinazotolewa na halmashauri kupitia mapato ya ndani.

Afisa Miradi kutoka UNA Tanzania, Saddam Khalfan alitoa wito kwa vijana kutilia maanani yale yanayopewa kipaumbele kupitia sera yao ya taifa kwa vijana na pia kuwa mstari wa mbele kujitafutia taarifa za kisera kwa ajili ya maendeleo yao.
Mgeni rasmi Kaimu Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, William Mnyipembe (kushoto) akizungumza kwenye kongamano hilo. Kulia ni Afisa Miradi UNA Tanzania, Saddam Khalfan.
Wanafunzi wa shule ya sekondari Mkolani wakitumbuiza kwenye kongamano hilo
Wanafunzi waliofanya vizuri kwenye michezo wakipokea zawadi kwenye kongamano hilo
Washindi wa michezo mbalimbali wakipokea zawadi kutoka kampuni ya simu ya Tecno

TAKATAKA KUGEUZWA KUWA MBOLEA

$
0
0
MANISPAA ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam, imetiliana saini  mkataba  wa sh.bilioni 5.56 na kampuni ya ukandarasi  ya  CRJE  ya nchini China  kwa ajili ya  kuanza ujenzi wa kiwanda  cha kuchakata taka kuwa mbolea aina ya mboji .

Kiwanda hicho  ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchakata  takaka tani  tano (5) hadi 100 kwa siku kitajengwa katika eneo la Mabwepande.

Akizungumza wakati wa hafla ya utilianaji saini, Dar es Salaam,  Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Banjamin Sitta amesema kuwa kiwanda hicho ambacho ujenzi wake unaanza rasmi leo kitakuwa na uwezo wa kuchakata taka ngumu na laini kuwa  mbolea aina ya mboji.

Amesema manispaa  imekuwa ikitumia kati ya sh.milioni 500 hadi 600 kwa mwezi  kugharamia uzoaji wa taka ambazo hizo taka hazizalishi chochote.

Sitta amesema Manispaa ya Kinondoni  inazalisha   tani 22,000 kwa siku hivyo kutumia fedha nyingi kuwalipa makandarasi.

Amesema  zaidi ya wananchi 1000 wanatarajiwa kunufaika na ajira kupitia kiwanda hicho.

Aidha amesema  hatua hiyo kubwa ya kuitikia sera ya taifa ya kuelekea  uchumi wa viwanda na kinondoni tunakuwa kuzalisha mbolea aina ya mboji ambayo haina madhara  katika udongo ukilinganisha na mbolea za kemikali,”.

 Meneja wa Kanda  wa kampuni ya CRJE,  Bai Haochen amesema, ujenzi wa kiwanda hicho unaweza kuchukua muda wa miezi 12  hadi 18. 
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Banjamin Sitta na Meneja wa Kanda  wa kampuni ya CRJE,  Bai Haochen wakitiliana saini ya makubaliano ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata taka na kuwa mbolea leo jijini Dar es Salaam.
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Banjamin Sitta akizungumza na waandishi wa habari juu ya makubaliano na kampuni ya ukandarasi wa ujenzi wa kiwanda cha kuchakata taka kuwa mbolea leo jijini Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Banjamin Sitta na Meneja wa Kanda  wa kampuni ya CRJE,  Bai Haochen wakibadilishana hati za makubaliono leo jijini Dar es Salaam.

BODI YA MIKOPO YATOA MAJINA YA WALIOPATA MIKOPO MWAKA WA MASOMO 2017/2018

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Abdul-Razaq Badru akizungumza na waandishi wa habari kuhusu upangaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2017/2018 leo (Jumatano, Oktoba 18, 2017) katika ofisi za HESLB jijini Dar es salaam. Kushoto kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo wa HESLB Dkt. Veronica Nyahende (Picha: HESLB).

 WAOMBAJI wa mikopo ya elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2017/2018 kuwa, baada ya uchambuzi wa maombi yao, Orodha ya Awamu ya Kwanza yenye wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza waliofanikiwa kupangiwa mikopo imekamilika.

hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Bw. Abdul-Razaq Badru wakati akizungumza na waandshi wa habari jijini Dar es Saaam leo amesema kuwa
 Kiasi cha Tshs 34.6 bilioni kimetengwa kwa ajili ya wanafunzi hao 10,196. Kwa ujumla, Tshs 108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
  
Amesema kuwa "Orodha hiyo ya kwanza inapatikana kwenye tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz) na itatumwa kwa vyuo husika. Orodha nyingine (batches) zitafuata kadri taratibu za udahili na uchambuzi zinavyokamilika. Lengo ni kutoa majina ya wote waliofanikiwa kupata mkopo kabla ya vyuo kufunguliwa mwishoni mwa mwezi huu wa Oktoba, 2017."

Amesema kuwa Orodha hiyo ya wanafunzi 10,196 imepatikana baada ya kupokea na kuchambua Awamu ya Kwanza ya majina ya wanafunzi 32,495waliopata udahili katika chuo kimoja.

Wanafunzi waliopata udahili katika chuo zaidi ya kimoja na ambao wana sifa za kupata mikopo, watapangiwa mikopo baada ya kuchagua na kuthibitisha chuo watakachojiunga kwa ajili ya masomo.

 Tshs 318 bilioni zatengwa kwa ajili ya wanaoendelea na masomo.

amesema kuwa wanatarajia kuanza kutuma vyuoni fedha za mikopo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo ambao wamefaulu mitihani yao kuanzia leo, Jumatano, Oktoba 18, 2017.

Kiasi cha Tshs 318.6 bilioni kitatolewa kwa wanafunzi 93,295 wanaoendelea na masomo kwa mwaka wa masomo 2017/2018. Tayari Serikali imeshatoa fedha hizo na lengo la Bodi ni kuhakikisha fedha zinafika vyuoni kabla ya kufunguliwa kwa vyuo ili kuwaondoloea wanafunzi usumbufu.

Bodi ya Mikopo inawasihi waombaji wa mikopo kuwa na subira wakati ikiendelea kukamilisha maandalizi ya orodha zinazofuata za wanafunzi waliopata mikopo. Tutaendelea kutoa taarifa kwa vyombo vya habari na tovuti ya Bodi mara kwa mara.

TATUMZUKA YAWEKA HISTORIA KWA KUTOA MILIONI 150 KUPITIA DROO YA SUPA MZUKA ‘JACKPOT’

$
0
0
 
 Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akifafanua jambo mapema leo mchana,wakati akieleza namna Supa Mzuka Jackpot inavyofanyika na namna mshindi anavyopatikana.Maganga alisema

"Kwa Sasa kila wakati ukicheza Tatu Mzuka hadi tarehe 19 Novemba, unapata bure nafasi ya kujishindia Tzs.150 milioni za uhakika kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot" alisema na kuongeza kuwa Wiki iliyopita Juma Othman (pichani kushoto),aliibuka mshindi wa Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha Tz.55 milioni.
Pichani kulia ni Juma Othman mwenye umri wa miaka 21 tu, akitoa ushuhuda namna alivyoshinda Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha Tz.55 milioni. Mshindi huyo ambaye anaishi na mama yake wilayani Bagamoyo, aliishukuru Tatu Mzuka huku akibainisha kuwa ushindi huo umebadilisha maisha yake.
 Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi Juma Othman aliyeibuka mshindi wa Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha shilingi milioni 55 za Kitanzania.

 
Tatu Mzuka kwa mara nyingine wamevunja rekodi kwa kuwaletea Watanzania jackpot kubwa zaidi kuwahi kutokea nchin. 

Donge nono la shilingi milioni 150 litatolewa kwa mshindi mmoja atakayebahatika siku ya tarehe 19 Novemba 2017, kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot.

Kupitia Supa Mzuka Jackpot, Watanzania wanashinda mara 1, si 2 bali nafasi 3 za kushinda kiasi kikubwa cha pesa kwa bei ya soda!

Njia tatu za kushinda na Tatu Mzuka ni;
1) Kushinda hadi milioni 6 kila saa, masaa 24 kwa siku

2) Kushinda Sh100,000,000 kupitia Mzuka Jackpot Jumapili hii, saa 9:30 usiku.

3) Kushinda Tzs.150,000,000 kupitia Supa Mzuka Jackpot tarehe 19 Novemba
Sebastian Maganga, Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka alielezea namna Supa Mzuka Jackpot inavyofanyika.

"Kwa Sasa kila wakati ukicheza Tatu Mzuka hadi tarehe 19 Novemba, unapata bure nafasi ya kujishindia Tzs.150 milioni za uhakika kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot" ilifafanua Maganga.

Wiki iliyopita Juma Othman, mshindi wa Mzuka Jackpot aliondoka na Tz.55 milioni. Othman mwenye umri wa miaka 21 tu, ambaye anaishi na mama yake wilayani Bagamoyo, aliishukuru Tatu Mzuka kwani ushindi huo umebadilisha maisha yake.

Tatu Mzuka imebadili maisha ya Watanzania hakika,hadi sasa imetengeneza mamilionea Zaidi ya 70 na kutoa zaidi ya bilioni 3 kwa zaidi ya washindi milioni 1 na laki tatu.

Homa ya Tatu mzuka inapoendelea kupanda, swali linabaki kuwa je? Nani ataondoka na donge kubwa Zaidi katika historia ya Tanzania.


RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA WAZIRI WA MAFUTA NA GESI WA OMAN MHE. DKT MOHAMED HAMAD Al RUMHY

NIC 'WAJICHIMBIA' ARUSHA KUPANGA MIKAKATI KABAMBE YA KIBIASHARA

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Ndugu Sam Kamanga akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Mameneja wa Shirika la Bima la Taifa unaoendelea mjini Arusha 
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya NIC wakiwa katika mkutano huo wa mameneja wa NIC unaoendelea jijini Arusha 
Mwenyekiti wa Bodi ya NIC Ndugu Laston Msongole akizungumza jambo wakati wa mkutano wa mameneja wa Shirika la Bima la Taifa unaoendelea mjini Arusha , kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Ndugu Sam Kamanga
Picha ya pamoja ya wajumbe wa Bodi na Mameneja wa Shirika la Bima la Taifa (NIC)unaoendela Jijini Arusha

NBC respected for supporting Vicoba Day

$
0
0

The Minister for Finance and Planning Hon. Dr. Philip Mpango sharing a light moment with the audience while delivering his key note address to 1,000 delegates during the first VICOBA Day launch in Dar es Salaam. NBC was one of the main sponsors of the VICOBA Day.
The Minister for Finance and Planning Hon. Dr. Philip Mpango presenting a certificate of appreciation to the NBC Retail Banking Director Filbert Mponzi for sponsoring the first VICOBA Day in Dar es Salaam. In between the two is Sihaba Nkinga Permanent Secretary in the ministry of Health, community Development, Gender, Elderly and Children. NBC was one of the main sponsors of the VICOBA Day.
The Executive Secretary of National Economic Empowerment Council (NEEC) Ben’gi Issa delivering her opening speech during the launch of the first VICOBA Day in Dar es Salaam. The VICOBA day was officially launched by the Minister for Finance and Planning Hon. Dr. Philip Mpango. NBC was one of the main sponsors of the VICOBA Day.
A cross section view of the 1,000 delegates attending the first VICOBA Day launch celebrations in Dar es Salaam. The VICOBA day was officially launched by the Minister for Finance and Planning Hon. Dr. Philip Mpango. NBC was one of the main sponsors.

MAZINGIRA YA UWEKEZAJI YAIMARISHWA TANZANIA-RIPOTI YA REPOA

$
0
0
 Mkurugenzi wa Repoa nchini, Donald Mmari, akizungumza mara baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya Nafasi ya Tanzania  katika kufanya Biashara Duniani
 Mtafiti Kutoka REPOA, Dk . Lucas Katera,Akiwasilisha   ripoti ya Nafasi ya nchi katika kufanya Biashara Duniani iliyotolewa na World Economic Forum na Repoa.
 Baadhi ya Watu waliohudhuria Uzinduzi wa Ripoti hiyo uliofanyika katika ukumbi wa Repoa.
 Mtafiti kutoka Repoa. Dk Blandina Kilama akizungumza mara baada ya kuwasilishwa Utafiti huo 
 Prof .Sufian Bukurura kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam akichangia mada mara baada ya kuwasilisha kwa ripoti .
 Mtafiti Kutoka Repoa Prof.Paschal Mihyo akichangia mada  mara baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya Nafasi ya Tanzania  katika kufanya Biashara Duniani



Katibu wa Kwanza wa sera na Uchumi  kutoka ubalozi Uholanzi Nchini, Eugene C.M Gies  akichangia mara baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya Nafasi ya Tanzania  katika kufanya Biashara Duniani
 Baadhi ya watu walioshiriki katika  uwasilishwaji kwa ripoti ya Nafasi ya Tanzania  katika kufanya Biashara Duniani.

NAIBU WAZIRI KAKUNDA AFANYA ZIARA KILWA

$
0
0

Mkurugenzi wa halmashauri ya Kilwa Zablon Bugingo kulia akitoamaelezo ya mradi mkubwa wa uoteshaji wa miche ya korosho kwa Naibu waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI George Kakunda alipofanya ziara leo Wilayani humo kushoto ni Mkuu wa wilaya hiyo Christopher Ngubiagai
Afisa kilimo na ushirika wilaya ya Kilwa John Mkinga kushoto akitoa taarifa ya mradi wa uoteshaji wa miche ya korosho mbele ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI George Kakunda alipofanya ziara leo Wilayani humo
Picha ikionyesha viriba vya kuoteshea miche ya korosho
Naibu waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI George Kakunda akiingia katika eneo la uoteshaji wa miche ya korosho,kushoto ni Wilayani humo kushoto ni Mkuu wa wilaya hiyo Christopher Ngubiagai



Pamela Mollel,Kilwa

Naibu waziri ofisi ya Rais TAMISEMI George Kakunda amewataka viongozi wa serikali wilayani Kilwa Mkoani Lindi kuhakikisha wanasimamia vyema upandaji wa miche mipya yazao la korosho hali ambayo itaongeza uzalishaji wa zao hilo kwa wananchi na kuinua uchumi wa Taifa

Hayo aliyasema jana wilayani Kilwa wakati wa ziara yake baada ya kuelezwa kuwa mkakati wa wilaya uliopo ni kuhakikisha wanazalisha na kupanda miche milioni moja kila mwaka hali ambayo itaongeza mashina ya zao hilo kutoka laki sita yaliyopo na zaidi kutokana na mpango huo kuwa wakudumu

Kufuatia hali hiyo Kakunda alisema ili miche hiyo iote vizuri na kustawi lazima uwepo usimamizi mkubwa kwa viongozi wote wa serikali wilayani humo kuliko kuacha usimamizi kwa wakulima peke yao ambao wanaweza kusababisha kukauka na kushindwa kufikia malengo

Awali Mkurugenzi wa halmashauri ya Kilwa Zablon Bugingo alisema tayari hatua za awali za kuotesha miche milioni moja kila mwaka zinaendelea ambazo miche hizo itagawiwa bure kwa wakulima hali ambayo itainua uchumi wao

Bugingo alisema mpango huo ni wakudumu ambapo kila mwaka wilaya itazalisha miche hiyo milioni moja na kuigawa kwa wakulima bure hali ambayo itakuwa zaidi ya mara mbili ya uzalishaji wa miche iliyopo ambayo kwa sasa ni laki sita tu iliyowaingizia shilingi Bilioni 13 na halmashauri kujipatia zaidi ya shilingi milioni220

Aliongeza kuwa mbali na kujipatia fedha kwa wakulima pia halmashauri itajiongezea mapato ya ushuru baada ya serikali kufuta baadhai ya vyanzo ikiwemo ya mabango iliyorudishwa serikali kuu hivyo zao hilo la korosho linaweza kuingizia halmashauri zaidi ya shilingi bilioni 40 kutokana na mpango huo kuwa zaidi ya mara mbili zaidi

Mbali na hali hiyo Waziri Kakunda ameupongeza mpango huo wa upandaji wa miche hiyo milioni moja kila mwaka kutokana na kuvuka malengo ya serikali ya kupanda miche elfu 50 kwa kila wilaya inayolima zao la korosho ingawa Afisa kilimo na ushirika wa halmashauri hiyo ya Kilwa John

Mkinga amesema changamoto iliyopo ni ucheleweshwaji wa mbegu hali inayosababisha zoezi la uoteshaji miche hiyo kwenda taratibu ingawa Kakunda amesema atawasiliana na wizara ya kilimo kumaliza tatizo hilo

NEC YASISITIZA WALIOPOTEZA VITAMBULISHO VYA KUPIGA KURA WATARUHUSIWA UCHAGUZI MDOGO WAKITUMIA VITAMBULISHO VINGINE.

$
0
0

NEC-DODOMA

Tume ya Taifa ya uchaguzi imesisitiza kuwa Leseni za udereva, Hati za Kusafiria na Vitambulisho vya Taifa vitatumika kwenye uchaguzi mdogo wa Madiwani wa Kata 43, utakaofanyika Novemba 26 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Ramadhan Kailima amesema wapiga kura wataruhusiwa kutumia vitambulisho hivyo kwa sharti ya kwamba picha, herufi na majina yaliyopo kwenye Leseni ya Udereva, Hati ya kusafiria na Kitambulisho cha Taifa yawe yanafana na majina na herufi zilizopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura

Kailima amesema kuwa ruhusa hiyo ya Tume ya matumizi ya vitambulisho hivyo imekuja kufuatia maoni ya wadau na baadhi ya wapiga Kura kupoteza kadi zao za kupigia Kura na wengine kadi zao kuharibika kutokana na sababu mbalimbali na hivyo kuwanyima haki na fursa ya kupiga Kura katika uchaguzi huo mdogo.

Amesema hatua hiyo inazingatia matakwa ya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kifungu Namba 61, kifungu kidogo cha 3a na Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Kifungu Namba 62 (a) ambavyo vinaipa Tume mamlaka ya kuruhusu kutumika kwa utambulisho mwingine wowote utakao msaidia mpiga kura aliyejiandikisha kuweza kupiga kura iwapo hana kadi.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI, MHE. JAPHET HASUNGA, AWASILI MAKAO MAKUU YA WIZARA MJINI DODOMA LEO

$
0
0
NA HAMZA TEMBA - WMU-DODOMA

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Ngailonga Hasunga leo tarehe 18 Oktoba, 2017 ameripoti rasmi Makao Makuu ya Wizara hiyo yaliyopo Mtaa wa Kilimani, Makao Makuu ya Nchi, Mjini Dodoma.

Mhe. Hasunga amepokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi na kuingia ofisini kwake kwa mara ya kwanza ambapo amesaini kitabu cha wageni na baadaye akapata fursa ya kuzungumza na watumishi wa Wizara hiyo waliopo Dodoma.

Akizungumza na watumishi hao baada ya kutambulishwa, Mhe. Hasunga aliwaomba ushirikiano katika kufanikisha majukumu ya Wizara ambayo ni kuhifadhi na kusimamia matumizi endelevu ya maliasili na malikale, na kuendeleza ufugaji nyuki na utalii.

“Nawaombeni ushirikiano tufanye kazi kama timu na tutekeleze majukumu yale ambayo tumepewa, nadhani kwa ushirikiano kwa pamoja tutaweza”. Alisema Mhe. Hasunga.

Naibu Waziri Hasunga ni mingoni mwa mawaziri wapya walioteuliwa na Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli na kuapishwa Oktoba 9, 2017 baada ya kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri. Awali nafasi hiyo ilikuwa imeshikiliwa na Mhe. Mhandisi Ramo Makani.

Aidha, katika uteuzi huo, Dkt. Magufuli alimteua pia Mhe. Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla kuwa Waziri wa Wizara hiyo akichukua nafasi ya Mhe. Prof. Jumanne Maghembe. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akikaribishwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (katikati) alipowasili kwa mara ya kwanza katika ofisi ya makao makuu ya wizara hiyo zilizopo mtaa wa Kilimani mjini Dodoma leo. Kulia anaeshuhudia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Tutubi Mangazeni.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jenerali Gaudence Milanzi (kushoto) akimtambulisha Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) kwa watumishi wa Wizara hiyo kabla ya kuzungumza nao leo mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na baadhi ya watumishi wa wizara hiyo baada ya kuwasili kwa mara ya kwanza katika ofisi ya makao makuu ya wizara hiyo zilizopo mtaa wa Kilimani mjini Dodoma leo. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na baadhi ya watumishi wa wizara hiyo baada ya kuwasili kwa mara ya kwanza katika ofisi ya makao makuu ya wizara hiyo zilizopo mtaa wa Kilimani mjini Dodoma leo.   
Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Maliasili wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga (hayuko pichani).
 Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Maliasili wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Japhet Hasunga (hayuko pichani).

NAIBU WAZIRI KWANDIKWA AMWAGIZA CHICO KUJENGA KIWANJA CHA NDEGE SHINYANGA.

$
0
0
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elius Kwandikwa akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Bi. Josephine Matiro (Watatu kushoto), alipofika mkoani humo kukagua  maendeleo ya kiwanja cha ndege cha Shinyanga kilichopo eneo la Ibadakuli. 
 Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Shinyanga, Bw. Julius Misollow akitoa taarifa ya maendeleo ya kiwanja hicho kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elius Kwandikwa, alipofika kiwanjani hapo kujionea maendeleo yake.
 Muonekano wa kiwanja cha Ndege cha Shinyanga ambacho kinatatrajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami na Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya kichina ya CHICO.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elius Kwandikwa akizungumza na wananchi wa Mwigumbi mkoani Shinyanga, alipofanya ziara ya kukagua barabara ya Mwigumbi – Maswa (KM 50.3), inayounganisha mkoa wa Shinyanga na Simiyu.
 Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoani Simiyu, Mhandisi Albert Kent, akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elius Kwandikwa kazi za ujenzi zinazoendelea katika barabara ya Mwigumbi – Maswa (KM 50.3).
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elius Kwandikwa akitoa maelekezo kwa Mkandarasi wa kampuni ya ujenzi ya kichina ya CHICO alipokuwa akikagua barabara ya Mwigumbi – Maswa (KM 50.3) inayounganisha mkoa wa Shinyanga na Simiyu.
Muonekano wa Barabara ya Mwigumbi – Maswa (KM 50.3), inayojengwa kwa kiwango cha lami  na mkandarasi CHICO kutoka nchini China. Barabara hii inaunganisha mkoa wa Shinyanga na Simiyu.Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mheshimiwa Elius Kwandikwa, amemtaka Mkandarasi wa kampuni ya ujenzi ya kichina ya CHICO aliyepewa zabuni ya ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Shinyanga kufika eneo la mradi na kuanza ujenzi wa kiwanja hicho haraka iwezekanavyo.
Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya kiwanja hicho katika eneo la Ibadakuli leo, mkoani Shinyanga, Naibu Waziri Kwandikwa, amesema kuwa haoni sababu ya mkandarasi huyo kuchelewa kuleta vifaa vyake katika eneo la mradi hadi sasa wakati tayari mkataba wa kuanza kazi hiyo umeshasainiwa.
"Mkandarasi hana sababu ya kuchelewa kuanza kazi wakati fedha zipo na zimeshatengwa kwa ajili ya mradi huu na mkataba umeshasainiwa,  sasa namwagiza mkandarasi huyu kuleta vifaa vyake na kuanza kazi mara moja", amesema Naibu Waziri Kwandikwa.

Aidha, Naibu Waziri huyo amemtaka Meneja wa kiwanja hicho kuhakikisha anatoa ushirikiano na kumsimamia mkandarasi huyo ili kuhakikisha kiwanja hicho kinakamilika mapema nakwa viwango vinavyotakiwa.
"Naamini tukimsimamia vizuri mkandarasi huyu tutapata kiwanja kizuri na imara hapa Shinyanga na tutafungua fursa mbalimbali za kiuchumi katika mkoa huu", amesisitiza Naibu Waziri Kwandikwa.
Kwa upande wake, Meneja wa kiwanja cha ndege cha Shinyanga, Julius Misollow, amemhakikishia Naibu Waziri huyo kutoa ushirikiano kwa mkandarasi huyo atakapowasili eneo la mradi.
Amefafanua kuwa mradi huo unatarajiwa kuhusisha ujenzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege, jengo la abiria, maeneo ya maegesho ya ndege na mnara wa kuongozea ndege.

Ameongeza kuwa ujenzi wa kiwanja hicho kwa kiwango cha lami chenye urefu wa kilomita mbili unatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi Bilioni 49.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Kwandikwa, amekagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Mwigumbi - Maswa (KM 50.3), mkoani Simiyu na kumsisitiza mkandarasi anayejenga barabara hiyo kuikamilisha kwa wakati na kwa viwango.

Amesisitiza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo ambayo ni kiungo kwa wananchi wa Maswa, Bariadi, Lamadi na Mwanza, kutarahisisha huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo katika maeneo hayo.

Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoani Simiyu, Mhandisi Albert Kent, amesema kuwa mradi upo katika hatua nzuri na unatarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili kutoka sasa.
Naibu Waziri Kwandikwa amefanya ziara ya kikazi katika mkoa wa Shinyanga na Simiyu ambapo amekagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wizara yake.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

KATIBU WA BUNGE NDG.KIGAIGAI AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA OFISI YA BUNGE KATIKA KIKAO CHA MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA BUNGE LEO MJINI DODOMA.

$
0
0
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kigaigai akizungumza na Menejimenti ya Utumishi wa Bunge katika kikao cha kufahamiana kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Spika Mjini Dodoma.
Watumishi wa Ofisi ya Bunge wakimsikiliza Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kigaigai (katikati) akizungumza wakati wa kikao cha kufahamiana na Menejimenti ya Utumishi wa Bunge kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Spika Mjini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images