Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

MANISPAA YA DODOMA YAANZA KUANDAA HATI MILIKI ZA ARDHI ZA MIAKA 99 KWA KASI, BARAZA LA MADIWANI LAPONGEZA

$
0
0
NA Ramadhani Juma,OFISI YA MKURUGENZI 

HALMASHAURI ya Manispaa ya Dodoma imekamilisha uandaaji wa hati 912 za umiliki wa ardhi za miaka 99 kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli Mei 15 mwaka huu wakati akitoa tamko la kuivunja iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) na shughuli zote kuhamishiwa katika Manispaa ya Dodoma. 

Akizungumza katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kilichopokea taarifa rasmi ya makabidhiano ya majukumu ya iliyokuwa CDA kuhamia Manispaa ya Dodoma jana, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Godwin Kunambi aliwaambia Madiwani na wananchi kwa ujumla waliohudhuria Baraza hilo kuwa, hatua hiyo imefikiwa katika kipindi cha miezi miwili ya Julai na Agosti, huku akiahidi kuwa,Manispaa hiyo itaendelea kutoa huduma hiyo na nyingine kwa kasi inayoendana na matarajio ya wananchi. 

Alisema kati ya hati hizo, hati 674 zilizowasilishwa kwa Kamishna Msaidizi wa Ardhi wa Wizara ya Ardhi zimeshasajiliwa na zipo tayari kwa ajili ya kukabidhiwa kwa wananchi husika, huku hati 238 zikiwa katika hatua ya kukaguliwa ili zisainiwe. 

Alifafaua zaidi kuwa, uandaaji huo wa hati unaenda sambamba na utoaji wa vibali vya ujenzi kwa haraka, ambapo mchakato wa kutoa kibali cha ujenzi unakamilishwa ndani ya siku saba tu baada ya maombi kupokelewa mpaka muombaji anakabidhiwa kibali chake. 

Kufuatia taarifa hiyo, wajumbe wa Baraza la Madiwani wakiongozwa na Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Profesa Davis Mwamfupe wameipongeza Menejimenti ya Halmashauri na watumishi wote na kuwataka waendelee na juhudi hizo ili pamoja na mambo mengine kuufanya mji wa Dodoma ukue kwa kasi kwa kuwawezesha wananchi na wadau wengine kujenga. 
Mkurugenzi wa wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kulia) ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi akizungumza wakati wa Baraza la Madiwani la Mnispaa hiyo.


Tanzania yakabidhiwa mashine ya kutoa dawa ya usingizi wakati wa upasuaji.

$
0
0
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisisitiza jambo wakati wa hafla ya kupokea msaada wa mashine ya kutoa dawa za usingizi zilizotolewa na Muungano wa Utepe Mweupe Tanzania (WRATZ). Mashine hiyo yenye thamani ya Sh. Mil.55 imetolewa na Kampuni ya Kas Medics Limited ikiwa ni matokeo ya uhamasishaji wa kupunguza vifo vya wakina mama na watoto leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Idara kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya na  Mratibu wa Taifa wa Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama (WRATZ) Rose  Mlay. 
Mratibu wa Taifa wa Muungano wa Utepe Mweupe wa Uzazi Salama (WRATZ) Rose  Mlay akielezea jambo wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa mashine ya kutoa dawa za usingizi iliyotolewa na Muungano wa Utepe Mweupe Tanzania (WRATZ). Mashine hiyo yenye thamani ya Sh. Mil.55 imetolewa na Kampuni ya Kas Medics Limited ikiwa ni matokeo ya uhamasishaji wa kupunguza vifo vya wakina mama na watoto leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Afya, Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Kas Medics Limited Nishitha Kulshreshtha  mara baada ya kukabidhiwa kukabidhiwa msaada wa mashine ya kutoa dawa za usingizi iliyotolewa na Muungano wa Utepe Mweupe Tanzania (WRATZ) kufuatia udhamini wa kampuni hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Mashine hiyo yenye thamani ya Sh. Mil.55 ni matokeo ya uhamasishaji wa kupunguza vifo vya wakina mama na watoto leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Idara kuu ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya.

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akipata maelezo kuhusu namna mashine ya kutolea dawa za usingizi inavyofanya kazi wakati wa hafla ya kukabidhiwa msaada wa mashine hiyo iliyotolewa na Muungano wa Utepe Mweupe Tanzania (WRATZ) leo Jijini Dar es Salaam. Mashine hiyo yenye thamani ya Sh. Mil.55 imetolewa na Kampuni ya Kas Medics Limited ikiwa ni matokeo ya uhamasishaji wa kupunguza vifo vya wakina mama na watoto leo Jijini Dar es Salaam.

Na.Paschal Dotto-MAELEZO.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imekabidhiwa mashine maalumu ya kutoa dawa za usingizi kwa mama wajawazito wenye uzazi pingamizi wakati wa upasuaji kwaajili ya kuokoa maisha yao.

Akizungumza katika makabidhiano hayo leo Jijini Dar es Salaam Waziri mwenye dhamana ya Afya Mh.Ummy Mwalimu alisema kuwa, hiyo ni hatua kubwa katika kupambana na vifo vya wakina mama wajawazito pamoja na watoto wachanga.

Waziri Ummy alitoa pongezi kwa watu waliojitolea kupanda mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuunga mkono kampeni ya kuokoa maisha ya mama na mtoto wakiongozwa na Dkt.Ahmed Mohamed Makuwani, ambapo alisema kuwa waliopanda mlima Kilimanjaro wamewezesha kupatikana kwa msaada wa mashine hiyo, hivyo akawashukuru na kuomba wadau wengine kuiga mfano huo.

“Tunawashukuru Utepe Mweupe wa Uzazi Salama kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya katika kushirikiana na serikali ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo kwa watoto wachanga, hatua hii inatufariji sana na naomba watanzania na wasio watanzania wenye mapenzi mema na afya ya mama na mtoto kuendelea kusaidia juhudi hizi ”, alisema Waziri Ummy.

Akieleza mafanikio katika sekta ya Afya waziri Ummy alisema kuwa kuna zaidi ya vituo vya afya 480 nchi nzima na kati ya hivyo vituo 109 vinavyumba vya upasuaji ambayo ni sawa na asilimia 20 huku akibainisha kuwa kufikia Juni, 2018 serikali inatarajia kujenga vyumba vya upasuaji 170 vitakavyosaidia upasuaji wa mama wenye uzazi pingamizi na idadi hiyo itaongezeka na kufikia vituo 279.

Aidha Waziri Ummy alisema kuwa licha ya kujenga vyumba hivyo watahakikisha upatikanaji wa vifaa, ujenzi wa maabara kubwa, wodi za kinamama pamoja na nyumba moja ya mtumishi katika vituo vya afya vyenye vyumba vya upasuaji.

Kutokana na mpango mkakati wa kupambana na vifo vya wajawazito na watoto wachanga Serikali inatarajia kufikia asilimia 50 mpaka asilimia 80 ifikapo mwaka 2020 ambayo ni kampeni ya Serikali ya Awamu ya Tano inayotarajia kuzinduliwa hivi karibuni ijulikanayo kama ‘Jiongeze Tukuvushe salama’ kampeni ambayo inalenga kuwasaidia wakina mama wajawazito popote walipo ili kuokoa maisha yao.

Naye Mratibu wa Utepe Mweupe Dkt. Rose Mlay alisema kuwa mashine hiyo ni maalum katika kunusuru maisha ya mama na mtoto lakini pia inaweza kutumika kwa mtu yeyote mwenye matatizo ya kufanyiwa upasuaji.

Kwa upande wake katibu mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya alisema mashine hiyo iliyotolewa na shirika la the Guardian Health yenye themani ya Shilingi milioni 55 ina ubora na kiwango cha kutosha katika kutoa huduma kwa mgonjwa wakati wa upasuaji.

“Mashine hii ni ya kipekee kwa sababu ina uwezo wa kutengeneza oksijeni na haihitaji mitungi ya gesi kwa hiyo ni mashine nzuri kwa wagonjwa na akinamama wenye uzazi pingamizi”, alisema Dkt.Mpoki.

Dkt. Mpoki alisema kilichopo sasa ni kufundisha wataalam watakaohusika na matumizi ya mashine hiyo ili waweze kuitumia ipasavyo na kuahidi kuwa atahakikisha inatunzwa ili iweze kudumu kwa muda mrefu.

PROF. MAGHEMBE AFUNGUA SIKU YA UTALII DUNIANI INAYOFANYIKA KITAIFA MKOANI IRINGA, ATOA WITO KWA WANANCHI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI KATIKA VITA DHIDI YA UJANGILI NCHNI

$
0
0
Na Hamza Temba-WMU
...............................................................
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe tarehe 30 Septemba, 2017 amefungua rasmi Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani yanayofanyika kitaifa mkoani Iringa na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana na Serikali katika kupambana na Majangili kwa kutoa taarifa za siri zitakazoweza kuwaibaini na kuchukuliwa hatua.

“Ili kulinda uwepo wa rasilimali za utalii zilizopo kwa vizazi vya sasa na vijavyo, ni lazima wananchi kushirikiana pamoja na Serikali katika mapambano dhidi ya ujangili, mkiona mtu ananyemeleanyemelea huko porini tuambieni tutamshukia kama mwewe, hizi rasilimali na zetu sote” alisisitiza Prof. Maghembe.

Alisema changamoto ya ujangili bado ipo katika baadhi ya maeneo hapa nchini, alitaja maeneo hayo kuwa ni upande wa Pori la Rugwa na Selous karibu na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ambapo watu huingiza mifugo hifadhini kwa kisingizio cha kutafuta malisho wakati huo huo wakifanya uhalifu wa kuua tembo.

Prof. Maghembe alifungua maadhimisho hayo pamoja na Maonesho ya Karibu Kusini na maonesho ya wajasiariamali wa viwanda vidogo SIDO yaliyoshirikisha wajasirimali kutoka mikoa ya nyanda zajuu kusini kwa lengo la kuonesha bidhaa zao zitakazoweza kutumiwa na watalii pamoja na watoa huduma hiyo. 

Akifungua maadhimisho hayo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Prof. Maghembe alisema, kaulimbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu kwa upande wa Siku ya Utalii Duniani ni “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo wakati ile ya Maonesho ya Karibu Kusini ikiwa ni “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”.

Alisema sekta ya utalii imechangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi kwa kuchangia asilimia kubwa ya mapato ya Serikali, kuongeza ajira, kipato cha jamii na kuchochea ukuaji wa sekta zingine. 

"Utalii ndio ndio sekta pekee inayoongoza kwa kuliingizia taifa fedha za kigeni kwa asilimia 25, Aidha, inachangia asilimia 17.5 ya pato la taifa na asilimia 11 ya ajira zote nchini" alisema prof. Maghembe. 

Alisema mapato yanayotokana na utalii yameongezeka kutoka Dola za Kimarekani milioni 1,353.29 mwaka 2011 hadi Dola za Kimarekani milioni 2,131.57 mwaka 2016.

Alisema mchango huo umechagizwa na ongezeko la watalii kutoka nje ya nchi ambao waliongezeka kutoka 867,994 mwaka 2011 na kufikia 1,284,279 mwaka 2016.

Hata hivyo, alisema mafanikio hayo yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na juhudi za Serikali katika usimamizi, uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali, utangazaji, mazingira bora ya uwekezaji na ushirikiano madhubuti baina ya sekta ya umma na binafsi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa wizara hiyo, Mhandisi Ramo Makani alisema Serikali imekusudua kuhakikisha kuwa utalii wa nyanda za juu kusini unakua juu zaidi uweze kutoa mchango stahiki kwenye pato la taifa. Alitoa wito kwa wananchi kutunza vivutio vya utalii vilivyopo, kuhifadhi mazingira na kupiga vita ujangili.

"Kwa upande wa sekta binafsi na wananchi kwa ujumla natoa witoe washirikiane na Serikali kuweka mazingira bora na ya kuvutia katika maeneo yenye vivutio  vya utalii ikiwemo hoteli za kisasa kwa ajili kuvutia watalii wa ndani na nje ya nchi kutembelea vivutia hivyo" alisema Mhandisi Makani.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina masenza alisema katika kuunga mkono azma ya Serikali ya kukuza na kufungua utalii wa Nyanda za Juu Kusini Serikali ya mkoa wake kwa kushirikiana na wadau wa utalii wameandaa Mpango Makakati wa kukuza sekta hiyo mkoani humo. Mpango huo umezinduliwa jana na Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe.

Kila mwaka nchi wanachama wa Shirika la Utalii Duniani huadhimisha Siku ya Utalii tarehe 27 Septemba kwa lengo la kuhanasisha umuhimu wa sekta hiyo katika kuleta maendeleo ya jamii, utamaduni, kukuza demokrasia, kutunza na kuhifadhi mazingira, kujenga uchumi na kuimarisha mahusiano ya kitaifa na kimataifa. Kilele cha Maadhimisho ni siku ya jumanne tarehe 2 Oktoba, 2017.
 Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (katikati),  Naibu Waziri, Mhandisi Ramo Makani (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) wakiimba wimbo wa Taifa katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Kauli Mbiu za maadhimisho hayo yatakayofikia tamati tarehe 2 Oktoba ni “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo na “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”. 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe, akitoa hotuba ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Kilele cha maadhimisho hayo ni tarehe 2, Oktoba. Kauli Mbiu za maadhimisho hayo yatakayofikia tamati tarehe 2 Oktoba ni “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo na “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”. 
Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani akizungumza katika maadhimisho hayo mkoani Iringa jana.
Mkuu wa Wilaya ya Iirnga, Richard Kasesela akiratibu shughuli nzima ya maadhimisho hayo.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Mkakati wa Utalii wa Mkoa wa Iringa ambao umeandaliwa kwa lengo kuunga mkono azma ya Serikali wa kufungua utalii wa Nyanda za Juu Kusini katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Kulia ni Mkuu wa Mkoa huo, Amina Masenza na Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Asia Abdallah. Kauli Mbiu za maadhimisho hayo yatakayofikia tamati tarehe 2 Oktoba ni “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo na “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”. 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto), Naibu Waziri, Mhandisi Ramo Makani (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (wa tatu kushoto) na viongozi wengine wa Serikali wakionesha Mkakati wa Utalii na Jarida la Iringa baada ya uzinduzi rasmi.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Philip Chitaunga akiwa na baadhi ya washiriki wengine kwenye ufunguzi wa maadhimisho hayo.
 Baadhi ya Machifu wa Iringa waliohudhuria ufunguzi wa maadhimisho hayo.
 Baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wakifuatila ufungunguzi wake.
Sehemu ya washiriki wa maadhimisho hayo ya Wiki ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini. Nyuma yao ni mabanda ya maonesho hayo.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto), Naibu Waziri, Mhandisi Ramo Makani (wa pili kulia), Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakielekea kukagua mabanda ya maonesho katika viwanja vya Kichangani Mkoani Iringa jana.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akipimwa afya katika banda la MSD wakati wa zoezi la kukagua mabanda katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. KKauli Mbiu za maadhimisho hayo yatakayofikia tamati tarehe 2 Oktoba ni  “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo na “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”. 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kushoto), akikagua bidhaa za wajasiriamali wakati wa zoezi la kukagua mabanda katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Anaeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa pili kushoto). 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kulia) akimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza moja ya bidhaa za wajasiriamali wakati wa zoezi la kukagua mabanda katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (wa nne kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatu kulia). Kauli Mbiu za maadhimisho hayo yatakayofikia tamati tarehe 2 Oktoba ni “Utalii Endelevu” – Ni chombo cha maendeleo na “Utalii endelevu ni nguzo ya Uchumi wa Viwanda”.
 Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto), akikagua kifaa maalum cha kuwashia umeme katika banda la VETA wakati wa zoezi la kukagua mabanda kwenye Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Anaeshuhudia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (kushoto). 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa tatu kushoto),  Naibu Waziri, Mhandisi Ramo Makani (kulia kwake) wakipata maelezo katika banda la Sido kuhusu huduma zinazotolewa na shirika hilo wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini yanayoendelea Mkoani Iringa.
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa tatu kushoto), akikagua gari maalum kwa ajili ya mafunzo katika banda la VETA wakati wa zoezi la kukagua mabanda katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. Wanaoshuhudia pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (wa tatno kulia). 
 Naibu Waziri wa Maliasili, Mhandisi Ramo Makani (kulia), Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (kulia kwake) na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza wakikagua vifaa vya mfumo wa umwagiliaji vilivyotengenezwa na VETA katika maadhimisho hayo.
 Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto), akisalimiana na Machifu wa Kabila la Wahehe katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani na Maonesho ya Karibu Kusini mkoani Iringa jana. 
Waziri wa Maliasili, Prof. Jumanne Maghembe akionesha picha za nyayo za Zamadamu wa Laetoli na Engaresero zilizogundulika Ngorongoro mkoani Arusha takribani miaka milioni 3.6 iliyopita kufuatia tafiti mbalimbali zilizofanyika kwa muda mrefu.
Katika maadhimisho hayo kuna fursa za kuwaona wanyamaori mbalimbali ikiwemo Simba kama wanavyoonekana kwenye banda lao maalum. (PICHA NA HAMZA TEMBA - WMU)

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 30,2017

DC WA KAKONKO KANALI NDAGALA APIGA MARUFUKU UNYANYASAJI KWA WAZEE,KUWATUHUMU WANAZUIA MVUA

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala amewaagiza Wananchi wa Wilaya ya Kakonko kuacha tabia ya kuwatuhumu baadhi ya wazee kuwa Wanazuia Mvua na kutaka kuwaondoa ikiwa ni pamoja na kuwauwa kwa kwa imani za kishirikina , na vikundi vitakavyo gundulika vinawatuhumu watachukuliwa hatua ili kukomesha vitendo hivyo.

Akizungumza na Wananchi jana katika maadhimisho ya siku yaWazee Wilayani humo katika kijiji cha Kasanda ,Ndagala alisema kumekuwa na tabia ya Wananchi wengi kuwatuhumu baadhi ya wazee kuwa wanazuia mvua, jambo ambalo ni imani za kizamani na zilizopitwa na wakati.
 
 "Kwa hiyo mimi nawaomba tuendelee kushirikiana na wazee wetu hawa kwa kuwa pia wana mchango wao mkubwa katika jamii,ni vyema tukawafanya wazee wetu waishi kwa amani na kuachana na imani hizo zinazoweza kuleta chuki na uhasama mkubwa baina yetu",alisema Ndagala.

Alisema vitendo kama hivyo vilijitokeza mwaka jana, baadhi ya wazee walitaka kuuwawa kwa tuhuma hizo,aliema na kuongeza kuwa imani hizo zinapaswa kupuuzwa kwani zinaweza kuchochea uvunjifu wa amani Kwa Wazee hao ambao ni hadhina kubwa kwa jamii. 
 
"Niwaombe wananchi mshirikiane na Wazee waliopo katika maeneo yenu, tumeona mchango wao ni mkubwa sana katika jamii na Taifa kwa ujumla Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni thamini mchango wa wazee kwa maendeleo ya Nchi yetu, na serikali inalitambua hilo ndio maana inatoa kipaumbele kwa Wazee kwa kuhakikisha wanakuwa na Afya njema kwa kupatiwa matibabu bure kutokana na mchango wao", alisema Ndagala.
 
Aidha Ndagala alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuandaa watumishi watakao kuwa wakishughulikia masuala ya Wazee na kuhakikisha jamii ina tambua na kuthamini mchango wa wazee na kuihamasisha jamii kutambua umuhimu wa wazee na kuihamasisha jamii kuwathamini wazee na kuwapenda kwa kuweka mipango shirikishi kwa wazee na jamii ilikuweka usawa kati yao.

Alieleza kuwa Serikali inaendelea kuwajali wazee kwa kutoa huduma ya afya bure,Wilaya imeamua kuwatambua wazee na kutoa huduma za Afya bure kwa wazee 1700 wamepatiwa vitambulisho vya msamaa vya matibabu vya muda na kumuagiza Mkurugenzi kuandaa utaratibu mzuri wa wazee kupatiwa vitambulisho vy a kudumu.

Nao Wazee hao katika risala yao iliyo wasilishwa na Mwenyekiti wa chama cha wazee Wilaya ya Kakonko Mbonipa Kisama, waliishukuru Serikali ya awamu ta tano kwa kutambua umuhimu wa wazee na kuwapa kipaumbele kwakuwapatia matibabu bure na kuiomba serikali kuanza kutoa petion jamii waliyo ahidiwa kwa muda mrefu kwa Wazee iliwaweze kufanya shughuli ndogo ndogo za kujikimu katika kipindi hicho na kuondolewa tozo za kijamii kwa wazee.

Alisema Wazee wanamahitaji yao ya ziada iliwaweze kuishi bila wasiwasi wilaya ina wazee 7103 ambapo wazee wanawake ni 3135 na wanaume ni 3975 ambao ni Wanachama wa chama cha Wazee ambapo kupitia chama hicho serikali imeweza kitumia Wadau kufanya sensa ya kuwatambua wazee na mahitaji yao na kuweza kutoa msaada kwa Wazee wasio jiweza.

Aidha Wazee hao waliyashukuru mashirika ya Help age international na shirika la TCRS kwa kutoa misaada kwa wazee wasio jiweza na kuomba kuendelezwa kwa misaada ya kisheria na haki za wazee kuishi na kutoa mchango wa huduma za kijamii kwa Wazee na wanaamini maombi waliyatoa serikali itatue changamoto hizo ilikuondokana na changamoto hizo.

Hata hivyo katika maadhimisho hayo yaliadhimishwa kwa Wazee kucheza michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mpira wa miguu, uvutaji wa kamba na ukimbizwaji wa kuku ambapo mshindi alikabidhiwa mbuzi na kiasi cha shilingi 20,000/= na Mkuu huyo kuomba michezo hiyo kwa wazee kuendelezwa katika kila kata ili kuimarisha Afya za wazee hao .
 Baadhi ya Wazee wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye maadhimisho hayo
 Mkuu Wawilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akikabidhi zawadi ya Mbuzi kwa timu ya wazee wa kijiji cha Kasanda iliyofanya vizuri katika michezo wakati wa maadhimisho hayo ya Wazee.
  MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akikabizi vitambulisho vya matibabu kwa baadhi ya wazee wilayani Kakonko.
  MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala akikabizi vitambulisho vya matibabu kwa baadhi ya wazee wilayani Kakonko.
 Baadhi ya wazee wakicheza ngoma katika maadhimisho ya siku ya wazee.


ISANJABADUGU WAKABIDHI VITENDEA KAZI KWA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBOGWE.

$
0
0
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Mh Vicent Busiga.amepokea vinakilishi vitatu vyenye thamani ya Tsh 3,000,000 kutoka kwenye kikundi cha wachimbaji wadogo wadogo kinachoitwa Isanjabadugu kilichopo kwenye kata Nyakafulu wilayani Mbogwe.

Akiongea wakati wa makabidhiano, Mwenyekiti wa halmashauri amemshukuru Mungu kwa Neema ya machimbo mapya ya dhahabu yaliyogundulika hivi karibuni katika kata ya nyakafulu kwa kuwa ni neema ya pekee nakuwataka wachimbaji hao kusimamia vizuri eneo hilo na wahakikishe wanalipa kodi ya serikali kama inavyotakiwa,vilevile mwenyekiti amewataka waendelee kuihudumia jamii inayowazunguka na kuendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo ya wilaya hii kwani Wilaya bado ni changa na inakabiliwa na changamoto nyingi.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa kikundi hicho Bw Joseph Katemi Watwa, amesema wametoa msaada huo wa vinakilishi baada ya kutembelea ofisi za halmashauri na kugundua kuwa ofisi hizo zinakabiliwa na changamoto kubwa ya vitendea kazi vikiwemo vinakilishi hivyo wakaamua kuchuka hatua ya kutoa msaada wa vifaa hivyo ili kupunguza changamoto hiyo. Bw Joseph ameendelea kusema kuwa wataendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwenye shughuli zote za maendeleo ya wilaya pamoja na kulipa kodi zote za serika.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Elias Kayandabila ametoa shukrani kwa wachimbaji hao na kuwaomba waendelee kuunga mkono shughuli za maendeleo kwenye wilaya hii kwani wilaya bado ni changa na inakabiliwa na changamoto nyingi. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe Elias Kayandabila Akipokea Computer kutoka kwa Katibu wa Wachimbaji wadogo wadogo (Isanjabadugu).
Mwenyeki wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe mhe Vicent Busiga Akipokea computer kutoka kwa Mwenyekiti wa Isanjabadugu ndg Joseph Katemi watwa.
Uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe wakiwa na Uongozi wa wachimbaji Wadogo Wadogo

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM- Taifa) RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM-TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM.

$
0
0
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) kabla ya kufungua mkutano huo  jijini Dar es Salaam.


 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) kabla ya kufungua mkutano huo  jijini Dar es Salaam. 
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) Rais Mhe. Dkt. John Magufuli akijadiliana jambo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM kwa upande wa Tanzania Bara Rodrick Mpogolo kabla ya kufungua mkutano huo wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM)   jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) wakipiga makofi mara baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli kuwasili ukumbini hapo jijini Dar es Salaam. 
 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) wakipiga makofi mara baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli kuwasili ukumbini hapo jijini Dar es Salaam.

 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) wakipiga makofi mara baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli kuwasili ukumbini hapo jijini Dar es Salaam. 
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM-Taifa) Rais Mhe Dkt. John Magufuli akipiga makofi mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa mkutano wa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa jijini Dar es Salaam.
 Wajumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa wakiendelea na Kikao jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU. 

SIKU 40 ZA MAOMBI KUOMBE AMANI NA WANAFUNZI WATAKAOANZA MASOMO VYUONI ZA ZINDULIWA NA TAFES

$
0
0

 Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Felchesmi Mramba akizungumza na wanaTAFES  walikusanyika katika ukumbi wa mikutano wa benki kuu jijini Dar es salaam.BARAZA la taifa la TAFES hapa nchini limezindua siku 40 za maombi kwaajili ya kuombe amani hapa nchini pamoja na wanafunzi watakaoanza mwaka mpya wa masomo katika vyuo vikuu vyote hapa nchini.


Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa baraza la taifa la TAFES, Profesa Lazaro Busagala wakati akizungumza na wanafes waliohudhulia mkutano wa chama hicho jijini Dar es Salaam leo.

Nae Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ili kuwa na taifa lenye maadili lazima kuwe na taasisi za kidini na za kiroho zitakazokuwa zikiwalea watoto na vijana katika vyuo hapa nchini, pia amesema kuwa Baraza la taifa la Tafes ambalo linawalea wanafunzi wa vyuo vikuu wa madhehebu ya kiprotestandi yanafanya kazi kubwa sana kwa kuwalea wanafunzi hao wawapo vyuoni na kuwa na maadili yanayokubalika katika jamii.

Amesema kuwa ili kuwa na jamii yenye maadili lazima kuwepo na watu wenye karama ya kuwafunza wengine maadili ya kiroho.









Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akizungumza na wanachama wa Taasisi ya wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini wakati wa kuzindua siku 40 za maombi kuombea Nchi pamoja na wanafunzi watakao jiunga na vyuo vikuu wa dini za kiprostandi hapa nchini.Taasisi hiyo ambayo inasaidia kuwaandaa kiroho na kijamii wanafunzi ili kuwe na jamii adilifu pamoja na viongozi waadilifu.
Taasisi hiyo inamchango mkubwa katika kuitengeneza jamii kuondokana na jamii yenye watu wenye roho mbaya.


Mtoa maada Dk. Joshua Wathang'a akizungumza kuhusiana na kwanini huduma ya kiroho itolewe vyuoni kwa wanafunzi hii kwasababu elimu hii humwandaa mwanafunzi kukubalika katika jamii pamoja na kuwa na watu wenye hufu ya Mungu na wenye maadili mazuri.Wathang'a ameyasema hayo mbele ya wanachama wa TAFES waliohudulia katika mkutano huo jijini Dar es salaam.
Mnyekiti wa baraza la taifa la TAFES, Profesa Lazaro Busagala akizungumza na wanafes waliohudhulia mkutano wa chama hicho jijini Dar es Salaam Uliofanyika kwaajili ya Kuombea Taifa pamoja na wanafunzi watakaoanza mwaka mpya wa masoko katika vyuo vikuu hapa nchini.



Baadhi ya wageni waliohudhulia katika mkutano wa wanaTAFES wakimsikiliza Mgeni rasmi jijini Dar es Salaam.
  Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Felchesmi Mramba Akiwa katika mkutano wa wanatafes uliofanyika jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuliombea taifa amani pamoja na kuwaombe wanafunzi watakaoanza mwaka mpya wa masomo mwaka huu.







Baadhi ya wageni waliohudhulia katika mkutano wa wanaTAFES wakimsikiliza Mgeni rasmi jijini Dar es Salaam. 


Picha zote na Avila Kakingo,Globu ya jamii

TCCIA YAZINDUA MALIPO KWA NJIA YA MTANDAO

$
0
0

Rais wa TCIA akifafanua jambo mbele wa wafabiashara walioshirika katika mkutano mkuu wa mwaka.Chama cha wafanyakazi, kilimo na viwanda Tanzania kimefanya mkutano wake mkuu wa mwaka pamoja na kuzindua mfumo mpya wa ulipiaji bidhaa kwa njia ya mtandao ‘LIPA FASTA’ lengo kubwa likiwa ni kusaidia wafanyabiashara ambao wamekuwa wakisafirisha bidhaa zao nje ya nchi. Mfanyabiashara na mwanachama wa TCCIA ndugu mustafa hassanal akisalimiana na mgeni rasmi ndugu Raymond Mbilinyi katika mkutano mkuu wa mwaka, pembeni ni makamu Rais wa TCCIA ndugu Octavian Mshiu

Huduma hii imezinduliwa katika mkutano mkuu wa mwaka wa TCCIA ambapo wanachama wote wa TCCIA pamoja na wafanyabiashara mbalimbali walihudhuria mkutano huo kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa huduma hii ambayo itakuwa mkombozi kwa wafanyabiashara wengi.
Mkurugenzi Mtendaji wa TCCIA Gotfrid Muganda akiongea na wafanyabishara waliohudhuria katika mkutano mkuu wa mwaka

Akizungumza kwenye mkutano huo Mkurungezi Mtendaji ndugu Gotrid Muganda alisema ‘LIPA FASTA ni mkombozi kwa wafanyabiashara wote katika kurahisisha njia zao za kufanya malipo. Kwa wafanyabiashara ambao wamekuwa wakisafirisha bidhaa zao nje ya nchi, sasa hawana haja ya kuwa na wasiwasi katika kufanya malipo kwani mfanyabiashara anaweza kufanya malipo akiwa ofisini kwake.Mfumo huu utasaidia wafanyabiashara kupata cheti cha uwasili kwa muda mfupi.Rais wa TCCIA ndugu John Mayanja akifafanua jambo katika mkutano hu0
Nae makamu wa Rais wa chama Ndugu Octavian Mshiu amesema’ mpango huo utaendeshwa na TCCIA kuanzia ngazi ya wilaya ili kuondoa vikwazo kwa wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa zao nje ya nchi’
LIPA FASTA ni zaidi ya njia ya malipo kwani hapa hata watanzania waishio nchi za nje ya nchi watapata nafasi ya kupata taarifa sahihi za soko, kuhifadhi taarifa sahihi za soko na bidhaa zilizopelekwa kwenye maitaifa mbalimbali pamoja na kumwezesha mfanyabiashara kufanya malipo popote alipo.Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mkutano mkuu wa mwaka wakifwatila mkutano

Tigo donated 1000 Mobile Smartphones for Mobile Birth registration for Lindi and Mtwara Regions

$
0
0




A RITA official explains to dignitaries including the Minister for Information, Arts, Culture and Sports Hon Dr. Harrison Mwakyembe, the Lindi Regional Commissioner Geodfrey Zambi, Tigo MD Simon Karikari and others  how the mobile birth registration works. This was during the launch of the Mobile Birth registration exercise for Lindi and Mtwara regions that happened in Tandahimba district in which Tigo donated 1,000 smartphones to ease the exercise.

Tandahimba residents line up to register their chidren.
Tigo MD Simon Karikari greets the audience
Tigo MD Simon Karikari addresses guests at the launch of the Mobile Birth Registration exercise for Lindi and Mtwara regions in Tandahimba district
Minister for Information, Arts, Culture and Sports Hon Dr. Harrison Mwakwyembe hands over a birth certificate to a resident of Tandahimba District during the launch of the mobile birth registration exercise for Lindi and Mtwara region. Looking on is the Tigo MD Simon Karikari (c) and other officials. Tigo donated 1,000 smartphones in  support of the child registration and certification  exercise.



Children perfom for guests during the launch of mobile birth registration exercise in Tandahimba.


Lindi Regional Commissioner Geodfrey Zambi, Minister for Information, Culture and Sports Dr Harrison Mwakyembe and RITA Advisory Board Chairperson Hamisi Dihenga show off one of the phones donated by Tigo.








Minister for Information, Culture and Sports Dr Harrison Mwakyembe hands over a phone donated by Tigo to Lindi Regional Commissioner Geodfrey Zambi. Left is RITA Advisory Board Chairperson Hamisi Dihenga.

KITUO KIPYA CHA KIMAREKANI CHAZINDULIWA MAKTABA KUU YA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Inmi Patterson na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya, wakikata utepe katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii. Hafla hii ilihudhuriwa pia na Mkurugenzi Mkuu wa Maktaba nchini, Dk. Alli Mcharazo.



Muonekano kituo  Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii

Muonekano kituo  Kituo Kipya cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu jijini Dar es Salaam Ijumaa hii




 Naibu waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya akihutuba katika uzinduzi wa kituo cha Kimarekani kilichoanzishwa kwa kushirikiana na Ubalozi wa  Marekani nchini Tanzania pamoja na serikali ya Tanzania. 

kikundi cha Ngoma kikisherehesha wakati wa uzinduzi wa kituo  hicho mapema jana.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi rasmi wa Kituo Kipya cha Kimarekani wakifuatilia kwa karibu hotuba zilitotolewa na wazungumzaji wakuu wa sherehe hizo jijini Dar es Salaam Ijumaa hii. Kituo hicho cha Kimarekani kimeanzishwa kwa ubia na Maktaba Kuu Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Injia Stella Manyanya ndiye alikuwa Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Maktaba nchini, Dk. Alli Mcharazo.

IGP SIRRO AWAKABIDHI BENDERA ASKARI WANAOKWENDA KUSHIRIKI SHUGHULI ZA ULINZI WA AMANI DARFUL NCHINI SUDAN

$
0
0
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Andrew Sattaa akiwakabidhi bendera ya Taifa kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi hilo (IGP) Simon Sirro, askari wa Jeshi hilo wanaokwenda Darful, nchini Sudani kushiriki shughuli za Ulinzi wa amani ambapo amewataka askari hao kufanya kazi kwa weledi na kwa kufuata taratibu kwa kipindi chote watakachokuwemo nchini  humo. Picha na Jeshi la Polisi
Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Adrew Satta, akimuwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiwaaga askari wanaokwenda kushiriki shughuli za Ulinzi wa Amani Darful Nchini Sudan, ambapo amewataka askari hao kufanya kazi kwa weledi na kwa kufuata taratibu kwa kipindi chote watakachokuwemo nchini  humo. Picha na Jeshi la Polisi.

HOTUBA YA MWENYEKITI WA CCM TAIFA, RAIS DKT. MAGUFULI ALIPOFUNGUA MKUTANO WA HALMASHAURI KUU YA CCM

PROF. KABUDI ATEMBELA UBALOZI WA TANZANIA UBELIGIJI

$
0
0
Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria ametembelea ubalozi wa Tanzania Brusels, Ubeligiji tarehe 29 Septemba, 2017. Prof. Kabudi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania Nchini Ubeligiji Mheshimiwa Joseph Edward Sokoine. 

Prof. Kabudi yuko Mjini Brussels, Ubeligiji akiambatana na Mhe. Rais Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Uganda na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mawaziri na Makatibu Wakuu kutoka Tanzania, Kenya, Uganda na Burundi. Wakati akiwa Brussels, Prof. Kabudi ameshiriki mazungumzo baina ya Rais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Rais wa Kamisheni ya Jumuiya ya Ulaya kuhusu Mkataba wa Ubia wa Kiuchumi baina ya Jumuiya ya Ulaya na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mhe Prof. Palamagamba Kabudi,Waziri wa Katiba na Sheria akiwa kwenye picha ya pamoja Bw. Geoffrey Kabakaki, Mwambata Maalum (Minister Plenipotentiary) wakati alipotembea makazi ya Balozi.
Mhe. Prof Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria akisalimiana na Mhe. Balozi Joseph Sokoine katika Ofisi za Ubalozi zilizoko Mjini Brussels, Ubeligiji
Mhe. Prof Palamagamba John Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria akiwa kwenye picha ya Pamoja na Mhe. Balozi Joseph Sokoine katika Ofisi za Ubalozi zilizoko Mjini Brussels, Ubeligiji
Picha ya pamoja

ELIMU SOLUTION WASAFIRISHA WANAFUNZI 50 KWENDA KUSOMA NCHINI CHINA

$
0
0
 Mkurugenzi wa Elimu Solution, Neithan Swed akizungumza na  waandishi kuhusu kampuni ya Elimu Solution ilivyoweza kusafirisha wanafunzi hamsini(50) kwenda kusoma nchini China kwa miaka minne kwa ufadhili leo katika uwanja wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mwanadunzi anayekwenda kusoma nchini China, Osmund Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere kuhusu namna alivyoweza kufanikisha kuomba ufadhili wa kusoma nchini china kuputia kampuni ya Elimu Solution.
 Mmoja wa wazazi wa wanafunzi wanaokwenda kusoma nchini China, Marysponser Nhwan akizungumza na waandishi wa habari kuhusu furaha aliyonayo baada ya mtoto wake kupata nafasi ya kwenda kusoma nchini Chini akiwa na ufadhiri kwa takribani miaka minne(4).
  Mmoja wa wazazi wa wanafunzi wanaokwenda kusoma nchini China, Saimoni Mapunda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna walivyoweza kuomba ufadhili wa mwanae kwenda kusoma nchini China kupitia kampuni ya Elimu Sotion leo katika uwanja wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wanaokwenda kusoma China pamoja na wazao wao wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye uwanja wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo

MANISPAA KINONDONI YASAINI MIKATABA MIWILI YA UJENZI WA BARABARA YENYE THAMANI YA BILIONI 49

$
0
0
 Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni,Aron Kagurumjuli (kulia) akisaini mikataba miwili  ya ujenzi wa barabara yenye thamani ya sh. bilioni 49  na kampuni za ukandarasi za  Estim Constructions Company Limited ya hapa nchini na  kampuni ya CCEC ya China.katikati ni Meya wa Kinondoni,Benjamin Sitta
Picha ya pamoja.(picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii).
 Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Kinondoni,Aron Kagurumjuli akizungumza katika hafla ya utilianaji saini mikataba miwili  ya ujenzi wa barabara yenye thamani ya sh. bilioni 49  na kampuni za ukandarasi za  Estim Constructions Company Limited ya hapa nchini na  kampuni ya CCEC ya China,leo jijini Dar es Salaam.
 Meya wa Kinondoni,Benjamin Sitta, akizungumza katika hafla ya utilianaji saini mikataba miwili  ya ujenzi wa barabara yenye thamani ya sh. bilioni 49  na kampuni za ukandarasi za  Estim Constructions Company Limited ya hapa nchini na  kampuni ya CCEC ya China.

TAMASHA LA TIGO FIESTA LAFANA MKOANI TABORA

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akizungumza kuhusu usalama wa watu na mali zao ulivyoimalishwa  kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati wa tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana.
Benpol akiwapagawisha wakazi wa Mkoa wa Tabora katika Tamasha la Tigo Fiesta katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Msanii wa bongo fleva Mr Blue akitumbuiza kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora wakati wa tamasha la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana.
Chege akitumbuiza kaaika jukwaa la Tigo Fiesta
Darasa akitumbuiza kaaika jukwad la Tigo fiesta mapema usiku wa kuamkia leo mkoani  Tabora.
Omg Dimpoz akiburudisha wakaz wa Tabora waliojitokeza kwa wingi katika viwanja via.
Jux akitummbuiza wakazi wa Tabora.
Jux katika jukwaa la Tigo Fiesta  katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora
Maua Sama akiimba kwa hisia

Maelfu ya wakazi wa Tabora wakiwa katika Tamasha la Tigo Fiesta mapema usiku wa kuamkia jana.

DC SHINYANGA AWEKA JIWE LA MSINGI NA KUENDESHA HARAMBEE UJENZI WA BWALO LA CHAKULA SHULE YA LITTLE TREASURES

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Jumamosi Septemba 30,2017 ameweka jiwe la msingi katika jengo la Bwalo la Chakula katika shule ya msingi Little Treasures “Little Treasures Nursery & Primary School” iliyopo katika kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.

Mbali ya kuweka jiwe la msingi pia ameendesha harambee kwa ajili ya kupata shilingi milioni 200 kwa ajili kukamilisha ujenzi huo,ambapo wazazi na walezi wameshiriki katika harambee hiyo. 

Akizungumza katika shule hiyo,Matiro aliwapongeza wazazi na walezi wa wanafunzi kwa kujitoa kwa hali na mali kusaidia shule hiyo ambayo imejizolea sifa lukuki kwa utoaji wa elimu bora. 

“Shule hii imejizolea sifa nzuri,hii ni miongoni mwa shule bora kabisa nchini,kila mzazi anapenda mtoto wake asome kwenye shule nzuri,ukifika Shinyanga ukauliza shule gani nzuri,utatajiwa shule hii,nimeambiwa siri ya mafanikio haya inatokana na maono na utayari wa wazazi na marafiki kuisaidia shule hii”,alifafanua Matiro. 

“Sisi kama serikali tunaunga mkono sekta binafsi,kutokana na shule hii kufanya vizuri,ni ukweli usiopingika kuwa imeleta ushindani mkubwa kwa shule zetu za serikali,nasi kwa upande wa shule zetu za serikali hatuna budi kuiga, tuje kujifunza nini wanafanya hapa Little Treasures”,aliongeza Matiro. 



Aliwaasa wazazi na walezi mkoani Shinyanga kupeleka watoto shule kwani urithi pekee kwa watoto ni elimu na wala siyo mali ambazo hupotea kirahisi sana. 

Katika hatua nyingine alizitaka shule za taasisi binafsi kutoza ada zinazoendana na hali ya uchumi wa wazazi huku akiwasihi wazazi kutoa ushirikiano katika shule akitolea mfano wa shule ya Little Treasures ambayo imekuwa karibu zaidi na wazazi na walezi wa wanafunzi. Mkurugenzi wa shule ya msingi Little Treasures,Lucy Dominic alisema ili kukamilika kwa jengo la bwalo la chakula jumla ya shilingi milioni 200 zinahitajika na tayari uongozi wa shule umetenga shilingi milioni 50 hivyo bado zinahitajika shilingi milioni 150. 

Naye Meneja wa shule hiyo,Wilfred Mwita alisema pindi jengo hilo litakapokamilika litatumika kama sehemu ya wanafunzi na wafanyakazi wa shule hiyo kula chakula lakini pia kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo michezo na mikutano. 

Akisoma risala,Mkuu wa shule hiyo,Paul Kiondo alisema shule hiyo yenye mchepuo wa Kiingereza ina wanafunzi wa bweni na kutwa ilianza na wanafunzi wanne pekee na sasa ina jumla ya wanafunzi 662 kati yao,wavulana ni 304 na wasichana 318 na imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani mbalimbali. 



Jumla ya shilingi milioni 15 zimepatikana katika harambee hiyo ya kuchangia ujenzi wa bwalo la chakula,ambapo wazazi na walezi pamoja na marafiki wa shule hiyo wamechangia huku Mkuu wa wilaya Shinyanga Josephine akitoa shilingi Milioni 2 pamoja na mifuko 30 ya saruji. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro (wa pili kulia) akiwasili katika shule ya msingi Little Treasures “Little Treasures Nursery & Primary School”.-Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiweka jiwe la msingi katika jengo la Bwalo la Chakula katika shule ya msingi Little Treasures “Little Treasures Nursery & Primary School”. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisoma maandishi baada ya kuweka jiwe la msingi katika jengo la Bwalo la Chakula katika shule ya msingi Little Treasures. 
Maandishi yakisomeka kwa lugha ya Kiingereza yakiwa na maana ya 'Jiwe la Msingi limewekwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro leo Septemba 30,2017'. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akipanda mti wa kumbukumbu baada ya kuweka jiwe la msingi katika jengo la Bwalo la Chakula katika shule ya msingi Little Treasures. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akimwagilia maji mti alioupanda katika shule ya Little Treasures. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiondoka katika eneo panapojengwa jengo la Bwalo la chakula katika shule ya msingi Little Treasures.Kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo,Tilulindwa Sulusi. 
Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakimwongoza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro katika maaandamano kuelekea eneo la mkutano kwa ajili ya harambee kuchangia ujenzi wa bwalo la chakula katika shule hiyo. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiwa katika maandamano hayo.Wa kwanza kushoto mbele ni Mkurugenzi wa shule ya msingi Little Treasures,Lucy Dominic,kulia ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo,Tilulindwa Sulusi. 
Meza kuu: Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Kulia ni Mkurugenzi wa shule ya msingi Little Treasures,Lucy Dominic,kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo,Tilulindwa Sulusi. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika shule ya msingi Little Treasures ambapo aliipongeza shule kuwa na mazingira mazuri ya kujifunzia wanafunzi. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika shule ya msingi Little Treasures ambapo alisema serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kuinua kiwango cha elimu. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliwasisitiza wazazi kupeleka watoto shule kwani ndiyo urithi unaofaa kwa watoto. 
Meneja wa shule ya Little Treasures Wilfred Mwita akizungumza wakati wa harambee hiyo ambapo aliwaomba wazazi na walezi wa wanafunzi pamoja na marafiki kuendelea kushirikiana na shule hiyo. 
Mkurugenzi wa shule ya msingi Little Treasures,Lucy Dominic akizungumza wakati wa harambee hiyo ambapo aliishukuru serikali kwa kuendelea kushirikiana shule hiyo ili kuboresha kiwango cha elimu mkoani Shinyanga na nchi kwa ujumla. 
Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Little Treasures,Tilulindwa Sulusi akitoa neno. 
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Little Treasures Paul Kiondo akisoma risala. 
Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakicheza ngoma ya Kijaluo mbele ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. 
Wanafunzi wakicheza muziki. 
Wazazi na walezi waliohudhuria mkutano huo wa harambee kuchangia ujenzi wa bwalo la chakula. 
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga,Said Pamui naye alikuwepo katika harambee hiyo ambapo alichangia shilingi 500,000/- kusaidia ujenzi wa bwalo la chakula katika shule hiyo. 
Wazazi wakipiga makofi. 
Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakicheza ngoma ya Kikurya. 
Wanafunzi wa shule ya msingi Little Treasures wakiimba ngonjera. 
Wazazi na walezi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea.
Wazazi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea. 
MC Mama Sabuni akifanya yake. 
Wazazi wakiwa katika eneo la tukio. 
Tunafuatilia kinachoendelea... 
Walimu wa shule ya msingi Little Treasures wakifuatilia yaliyokuwa yanajiri. 
Wazazi wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea. 
Waandishi wa habari wa magazeti ya Daily News na Habarileo,Suleiman Shagata na Kareny Masasy wakiwa katika eneo la tukio. 
Waandishi wa habari John Mponeja wa Channel Ten na Getruda Mallya wa Radio Faraja wakifurahia jambo. 
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga,Said Pamui (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa bodi ya shule ya msingi Little Treasures Tilulindwa Sulusi wakiondoka katika shule hiyo baada mkutano wa harambee. 
Picha ya kumbukumbu mbele ya jengo la utawala shule ya msingi Little Treasures.-Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI ACTOBA 1,2017

TANZIA:MTANGAZAJI WA E-FM AFARIKI DUNIA

$
0
0

"Uongozi na Wafanyakazi wa E-FM,TV-E kwa majonzi na masikitiko makubwa tunatangaza kuondokewa na Mwanafamilia Mwenzetu Dennis Rupia (Chogo),aliyefarika Dunia baada ya kuugua kwa kipindi cha muda mfupi.

Aidha kwa taarifa zaidi tataendelea kufahamishana taratibu za kumpumzisha mpendwa wetu kupitia vyanzo mbalimbali vya mawasiliano.

Hakika ni kipingi Kigumu kwetu,Wasikilizaji wa Redio na familia kwa ujumla tuendelee kuombea Mpendwa wetu" ,E-FM.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images