Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live

ASILIMIA 75% YA NCHI WANACHAMA WA INTERPOL, YAKUBALI KUJIUNGA KWA PALESTINA KATIKA TAASISI HIYO

0
0
Mwakilishi wa Palestina akipokea bendera kutoka kwa Rais wa Interpol Bw. Meng Hongwei kuashiria uanachama kamili wa Palestina ndani ya Taasisi ya Polisi ya Kimataifa ya kuzuia uhalifu wa kijinai duniani.


Mkutano Mkuu wa Taasisi ya Polisi wa kimataifa wa kuzuia uhalifu wa kijinai “Interpol”, umekubali kujiunga kwa Palestina katika taasisi hiyo,baada ya nchi wanachama 75 kulipigia kura ya ndio azimio hilo. Interpol imethibitisha kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa, Palestina na visiwa vya Solomon kuanzia sasa ni miongoni mwa wanachama wake.

Interpol ni taasisi kubwa zaidi ya kipolisi wa kimataifa iliyoasisiwa mwaka 1923, inajumuisha masuala ya nchi wanachama 190,huku makao makuu yake yakiwa mjini Lyon nchini Ufaransa.Aidha Interpol imekubali uanachama wa Palestina mnamo siku ya jumatatu iliyopita jioni kufuatia ombi la nchi hiyo, kabla ya kulijumuisha katika ajenda zake zitakazopigiwa kura katika Mkutano wake Mkuu,ambao uliketi nchini China Jumatano iliyopita na kuikubalia Palestina ombi lake hilo.

Kwa upande mwingine,Israeli na Marekani zilijaribu kukwamisha hatua hiyo ya kukubaliwa uanachama wa Palestina katika Interpol, kwa kutumia mashinikizo kadhaa juu ya taasisi hiyo ili isikubali ombi la Palestina kuwa mwanachama.

Wakati huo huo, Dr.Riyad Al-Maliki ambae ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Palestina, amepongeza hatua ya kuipigia kura ya ndio nchi yake na hatimae kukubaliwa uanachama wa Interpol,kupitia mkutano wake mkuu uliofanyika mjini Beijing nchini China. Amesisitiza kuwa hatua hiyo inathibitisha kuaminika uwezo wa Palestina katika kutekeleza sheria,dhamira halisi na maadili muhimu ya Interpol.

Waziri pia ameashiria kupatikana kwa ushindi huo,kumetokana na msimamo wa awali wa idadi kubwa ya nchi wanachama wa Interpol, iliyotetea sababu ya kuwepo kwa taasisi hiyo na kanuni zake za msingi,pale zilipokataa waziwazi kuupa nafasi ubabe wa kisiasa utawale. Huku waziri akiongeza kusema:"Leo haki na kanuni zimeshinda mambo mengine yote"."Leo, ukweli na kanuni zimeshinda mambo mengine yote.

Dr.Riyad Al-Maliki kwa niaba ya taifa la Palestina,amezishukuru nchi wanachama zilizoiunga mkono Palestina katika jitihada zake,huku akitilia mkazo kuendelea kwa nchi yake katika jitihada za kujiongezea hadhi na nafasi mbalimbali kimataifa,ikiwa ni pamoja na kutetea haki za Wapalestina,uhuru na amani yao kwa njia ya kidiplomasia na kisheria, ikiwa ni pamoja na kujiunga na taasisi husika za kimataifa.

Kwa mnasaba huu pia, Waziri Al-Maliki amesisitiza ahadi ya nchi yake ya Palestina katika kutimiza majukumu yake ya kuchangia kupambana na uhalifu na kuimarisha utawala wa sheria katika ngazi ya kimataifa. Huku ikishirikiana na nchi wanachama wa Interpol katika kukuza hadhi na nafasi ya taasisi hiyo, ushiriki wa kidhati kabisa wa kimataifa dhidi ya uhalifu unaohatarisha maisha wananchi na mustakabali wao duniani.

Aidha ameongeza kusema: "Nchi ya Palestina inauchukulia uanachama huu na majukumu yake kama ni sehemu ya wajibu wake kwa Wapalestina,pia ni wajibu wa kimaadili kwa walimwengu wote. Palestina ipo tayari na inaweza kubeba majukumu na wajibu huu kama mshirika wa dhati katika jamii ya kimataifa,itachangia hasa kuendeleza maadili yetu ya msingi ya pamoja kama mataifa. "

Uongozi mpya wa TFF watembelea SBL

0
0

Rais wa TFF ,Wallace Karia akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani

alipofanya ziara katika Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars.pembeni yake kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie na kulia ni Mkurungezi wa masoko wa SBL Ceaser Mloka na mwishoni ni Kocha mkuu wa Taifa stars Salum Manyanga,Mapema jana katika ofisi za makao makuu ya SBL Temeke Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie akifurahia jambo na Rais wa TFF ,Wallace Karia na Mkurungezi wa masoko wa SBL Ceaser Mloka wakati uongozi wa TFF ulipotembelea kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars.

Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie akimkabidhi zawadi Rais wa TFF ,Wallace Karia mapema jana alipotembelea kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars katika ofisi za kampuni hiyo Temeke Jijini Dar es salaam.


 Uongozi mpya wa Shirikisho la Soko Tanzania (TFF) ukiongozwa na Rais wake Wallace Karia, leo umetembelea Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambayo ni wadhamini wakuu wa Timu ya Taifa, Taifa Stars.

Ziara hii imefanywa na uongozi mpya wa TFF ikiwa ni wiki moja kabla ya mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayozikutanisha Taifa Stars na Malawi, mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Tangu imepata udhamini wa SBL mwezi Mei mwaka huu, Taifa Stars imecheza mechi nne za kimataifa na kufanikiwa kuweka rekodi nzuri kwenye mechi zote ilizocheza.

Akiongea wakati wa ziara hiyo, Rais wa mpya wa TFF aliishukuru SBL kwa udhamini wake kwa timu ya taifa na aliihakikishia SBL kuwa uongozi wake umeunda menejimenti ya Taifa Stars ili kuhakikisha kuwa timu ya taifa inapata ushindi kwenye kila mechi.

“Tunaishukuru SBL kwa kutoa msaada uliokuwa unahitajika sana na ambao umeiwezesha timu yetu ya taifa kujiandaa vyema na mechi na kufanya vizuri kwa ngazi ya kitaifa na kimataifa,” alisema Karia Karia alisisitiza kuwa fedha zilizotolewa kwa ajili ya udhamini wa timu ya taifa, zitatumika vizuri na kuongeza kuwa uongozi wa TFF unalenga kuongeza imani kwa wadhamini wa Taifa Stars na wadau wa soka kwa ujumla wake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Helene Weesie alimpongeza Rais mpya wa TFF pamoja na timu yake kwa kuchaguliwa na kueleza kuwa SBL itaendelea kutoa misaada inayolenga kuendeleza michezo hapa nchini.
“SBL inatambua mchango muhimu ambao michezo inatoa kwenye maendeleo ya kiuchumi na kijamii na ndiyo maana tunaamini kuwa tunapoidhamini Taifa Stars, tunachangia katika kuwaburudisha na kuwaunganisha Watanzania wakiwa na bia yao bora ya Serengeti ikwa na ujumbe wake wa sifa yetu, bia yetu, nchi yetu,” alisema

Mwezi Mei mwaka huu, TFF iliingia mkataba wa ufadhili kwa Taifa Stars utakaodumu kwa kipindi cha miaka 3 utagharimu shilingi blioni 2.1na kuifanya SBL kuwa mdhamini mkuu wa timu ya taifa.

Ikizalishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1996, bia ya Serengeti imetengenezwa na kimea kwa asilimia 100 huku ikiweza kushinda tuzo zaidi ya 10 kwa ngazi ya kitaifa na kimataifa kutokana na ubora wake wa kimataifa.

SEKTA YA MANUNUZI YA MTANDAONI NA CHANGAMOTO ZAKE NCHINI TANZANIA

0
0
SEKTA YA MANUNUZI YA MTANDAONI NA CHANGAMOTO ZAKE NCHINI TANZANIA


Na Jumia Travel Tanzania

Miongoni mwa sekta ambazo zimewapatia utajiri mkubwa wafanyabiashara mbalimbali duniani ni pamoja na biashara kwa njia ya mtandao. Leo hii ukiyataja majina ya kampuni kama vile Alibaba au Amazon ni watu wachache wasioyafahamu licha ya kutokuwepo nchini Tanzania. Waasisi wa makampuni hayo wamo kwenye orodha ya watu matajiri duniani, Bw. Jeff Bezos mwasisi wa Amazon ni tajiri nambari 3 huku Jack Ma ambaye ni mwasisi wa Alibaba yeye ni tajiri nambari 23.
Utajiri wa wafanyabiashara hawa sio kama wanamiliki biashara katika nchi mbalimbali bali uwezo wa makampuni yao kuwafikia wateja mahali popote walipo. Kuwafikia wateja hao Jumia Travel ingependa kukufahamisha si kwa njia nyingine bali ni kupitia mtandao wa intaneti. 


Kuja kwa mtandao wa intaneti kumerahisisha shughuli mbalimbali ikiwemo uendeshaji wa biashara. Mitandao kama Alibaba na Amazon iliona fursa kubwa kupitia intaneti ambazo inawezekana wafanyabiashara wenyewe hawakuziona. Fursa ambazo wao waliziona ni kwa kuwakutanisha wateja kutoka sehemu tofauti mtandaoni. 
Hivyo wao suluhu waliyoiona badala ya wafanyabiashara kutegemea wateja kuja moja kwa moja dukani, wao waliona ni vema wafanyabiashara kuziweka bidhaa zao mtandaoni zikiwa na taarifa kamili kama vile mwonekano wake, sifa, ubora, bei na namna ya kuzipata. Baada ya kufanya hivyo ndipo wateja wao wenyewe wapitie mtandaoni na kuchagua zile walizovutiwa nazo. 

Tafiti mbalimbali zilizofanywa na taasisi tofauti za kibiashara zimebaini kwamba kuna mambo ya msingi kadhaa ya kuzingatia pale unapotaka kufanya biashara kwa njia ya mtandao. Yapo masuala mbalimbali ambayo wafanyabiashara wanaaswa lakini yafuatayo ndiyo msingi mkuu zaidi.

Uharaka. Mojawapo ya changamoto kubwa ambayo manunuzi ya bidhaa mtandaoni imekuja kutatua ni upoteaji wa muda unaotumiwa na mteja kutoka eneo moja kwenda kwingine. Hivyo basi, ili kumshawishi mteja anunue bidhaa zako kwa mfumo huo lazima umhakikishie kwamba atatumia muda mchache mpaka kuipata huduma hiyo. Isiwe kwamba mteja anatumia muda mwingi kuipata bidhaa aliyoiagiza tofauti kama angeamua kuifuata mwenyewe dukani. Tafiti zinaonyesha kwamba wateja wapo tayari kulipa zaidi endapo kutakuwepo na uharaka mkubwa wa kufukiwa na huduma.    

Uaminifu. Je bidhaa aliyoiona na kuiagiza mteja ndiyo sahihi iliyomfikia? Je sifa ambazo alizoziona mtandaoni ndizo anazoziona mara baada ya bidhaa kumfikia? Je ni kweli bidhaa imemfikia kwa wakati kama alivyoahidiwa baada ya kufanya manunuzi? Haya ni maswali ya msingi ambayo mteja wa mara ya kwanza wa mtandaoni atakuwa anasubiri majibu. Majibu ya maswali hayo ndiyo yatakayozaa uaminifu baina ya mfanyabiashara na mteja ili aendelee kufanya manunuzi tena na tena. Kama mfanyabiashara, uaminifu ni kitu muhimu sana kwani kumbuka ni mtandao pekee ndio unaowaunganisha.       

Vifungashio (Packaging). Endapo ulikuwa haufahamu miongoni mwa vitu ambavyo huwavutia wateja ni pamoja na bidhaa inavyofungashwa. Hii inamaanisha kwamba vile bidhaa ungependa kumfungashia baada ya kufanya manunuzi kwa kuja dukani kwako iwe sawa ni vile itakavyokuwa kwa mtandaoni. Bila ya kujali mteja amemtumia kiasi gani kwenye manunuzi yake, vifungashio vya kuvutia humfanya  kuridhika zaidi na kuvutiwa kutumia tena huduma zako.       
Mbali na dunia kubadilika na kuhamia kwenye mifumo ya kimtandao bado kwa nchi zinazoendelea kama vile Tanzania ni changamoto. Baadhi ya sababu ambazo zimekuwa zikiwafanya watanzania kuwa wazito kidogo kufanya manunuzi ya bidhaa mtandaoni ni pamoja na: 

Kuiona bidhaa. Ni utamaduni sio tu wa watanzania bali hata waafrika wengi pia kufanya maamuzi juu ya bidhaa wanayotaka kuinunua mpaka kuiona. Hivyo basi zinahitajika jitihada za ziada katika kuwaaminisha wateja kwamba kile wanachokiona ndicho watakachokipata.    

Kuishika na kuijaribu bidhaa ili kujiridhisha. Kuiona tu bidhaa pekee haitoshi, watanzania wengi wana kawaida ya kuishika na hata kuijaribu bidhaa kabla ya kufanya maamuzi. Kwa kufanya hivyo wanaamini kwamba wanakuwa wamejiridhisha kwamba ni chaguo sahihi ndipo wafanye maamuzi. Kuitatua changamoto hii wafanyabiashara wanatakiwa kutoa elimu ya kutosha kwa wateja wao kuzifahamu kwa undani zaidi bidhaa wanazozihitaji ili kutokuwa na wasiwasi pale wanapofanya manunuzi. 

Ugumu katika kuitumia tekinolojia. Kutokana na changamoto ya tekinolojia hizi mpya sio watu wana ufahamu wa kutosha wa namna ya kuzitumia. Elimu ya kutosha inahitajika pamoja juu ya mifumo na urahisi kwenye kuitumia. Ili manunuzi ya mtandaoni yawe rahisi basi kuna umuhimu wa mifumo kuwa rafiki kwa wateja.

Hofu ya wizi wa mitandaoni. Kwa kuwa mifumo hii ni mipya miongoni mwa watanzania wengi, bado kuna hofu juu ya tahadhari za wizi unaoweza kutokea mitandaoni. Wafanyabiashara wa mitandaoni wanatakiwa kuwaelimisha na kuwaaminisha kwamba ni salama. Mbali na hapo inabidi kubuni njia salama zaidi za malipo au kutumia ile mifumo ambayo watanzania wanaiamini kama vile kulipia bidhaa pale zinapowafikia. 

Sababu ya mwisho ingawa zipo nyinginezo ni muda unaotumika mpaka bidhaa kumfikia mteja. Kuzingatia uharaka kwenye kuwafikishia wateja bidhaa pale walipo ndio kitu cha kuzingatia zaidi katika biashara za mtandaoni. Na nadhani ndio sababu kubwa iliyopelekea mfumo wa biashara kuenea sehemu nyingi duniani. Kwa mfano, Dar es Salaam ni miongoni mwa jiji yanayokumbwa na changamoto ya foleni za magari barabarani. Hali hiyo hupelekea wakazi wake kupoteza muda mwingi ambao ungeweza kutumika sehemu nyingine. Hivyo kwa kulitambua hili wafanyabiashara wa manunuzi ya mtandaoni wanaweza kuitumia kama fursa kwa kuwafikishia huduma wateja pale walipo huku wao wakiendelea na shughuli nyingine za kujenga taifa.
Ni dhahiri kwamba tekinolojia imedabili shughuli nyingi sana na kuwafanya kuwa werevu ukilinganisha na kipindi cha nyuma. Jumia Travel inaamini wafanyabishara hawana budi kuyazingatia mambo ya msingi katika uendeshaji wa biashara za mitandaoni na kuzijua tamaduni za watanzania. Kikubwa zaidi ni kuwajua wateja ni watu wa aina gani, wana mitazamo ipi na vitu gani wanapendelea ni mwanzo wa kufanikiwa kwenye jambo lolote.#BIASHARA

AZAKI ZA ZANZIBAR ZAWEZESHWA NA FCS KUFANYA MAFUNZO YA KWA VITENDO MOROGORO

0
0
 Washiriki wa mafunzo kutoka Asasi za Kiraia za Visiwani Zanzibar, wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kutawanyika kila kundi kuelekea katika vijiji viwili tofauti vya Msowelo na Matombo kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.  
 Kundi lililokuwa likielekea Msowelo likipiga picha ya pamoja mbele ya gari lao
  Kundi lililokuwa likielekea Msowelo likipiga picha ya pamoja mbele ya gari lao
  Kundi lililokuwa likielekea Matombo likipiga picha ya pamoja mbele ya gari lao
 Wakiwasili Msowelo
Asasi za Kiraia kutoka Zanzibar zimeendelea na mafunzo ya siku mbili kuhusu Utetezi na Ushawishi wa Sera mkoani Morogoro. Asasi mbalimbali kutoka Zanzibar na Pemba ziko katika ziara ya Mafunzo iliyoratibiwa na Foundation for Civil Society (FCS) chini ya mwamvuli wa Association of Non Governmental Organizations of Zanzibar (ANGOZA) inakutanisha wawakilishi Zaidi ya 40 kutoka Zanzibar ambao wamekuja kujifunza namna mashirika ya MVIWATA (Muungano wa Vikundi vya Wakulima Wadogo Tanzania) na MPLC (Morogoro Para-Legal Center).

Katika siku ya pili washiriki hawa wamepata fursa ya kwenda uwandani ili kukutana na wanufaika wa kazi mbalimbali zinazofanywa na MVIWATA na MPLC. MVIWATA imewapeleka washiriki wilayani Kilosa katika kijiji cha Msowelo ambapo kijijini hapa kumekuwa na migogoro ya Wkulima na Wfugaji ambapo kijijini hapa MVIWATA imefanikiwa kutumia mtandao wake wa msingi kupaza sauti kwa serikali ili kutenga maeneo ya wakulima. Tayari wilayani hapa kuna mashamba 9, ambayo yamefutwa na yamekabidhiwa katika mamlaka ya wilaya ili yagawiwe kwa wananchi.

Kwa upande wa MPLC yenyewe inawaonesha washiriki hawa kazi zao katika eneo la Matombo ambako huko pia MPLC inafanya kazi za utetezi wa haki za umiliki wa ardhi kwa makundi mbalimbali yanayokabiliwa na changamoto hiyo. Shirika hilo limejizolea sifa kwa kazi zake mkoani Morogoro na pia ni shirika kongwe ambalo linafanya kazi za utetezi na ushawishi mkoani Morogoro.

Washiriki kutoka Zanzibar wanatumia nafasi hii kubaini changamoto mbalimbali zinazoyakumba makundi mbalimbali katika jamii ilhali kukiwa na mapungufu katika sera na maamuzi hali inahyowahitaji wananchi kufanya ushawishi na utetezi wa haki za kila kundi ili kuchochea jamii kubaki ikiishi kwa mani na ikiendesha maisha kwa mafanikio.

 Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa Msingi Msowelo, Zainab Kisegele, akizungumza na wanaasasi za Kiraia kutoka Visiwa vya Zanzibar,wakati walipofika kijijini hapo Msowelo kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kujifunza namna ya kupambana na changamoto za migogolo ya Ardhi na njia wanazoweza kutumia kutatua migogolo katika Kata za Vijiji.
 Mwenyekiti wa Mtandao wa Msingi Msowelo, Ally Omary, akizungumza na wanaasasi za Kiraia kutoka Visiwa vya Zanzibar,wakati walipofika kijijini hapo Msowelo kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kujifunza namna ya kupambana na changamoto za migogolo ya Ardhi na njia wanazoweza kutumia kutatua migogolo katika Kata za Vijiji.
 Washiri wakisikiliza kwa umakini
 Picha ya pamoja baada ya mafunzo kwa walioelekea Kijiji cha Msowelo
 Washiriki waliokuwa wakielekea Matombo wakiwa katika gari kuelekea katika mafunzo kwa vitendo.
 Wakiwa katika mafunzo
 Wakiuliza maswali kwa wenyeji wao ili kujifunza zaidi
 Mafunzo yakiendelea Matombo.....
 Mafunzo yakiendelea Matombo.....
Ushuhuda .......
Picha ya pamoja baada ya mafunzo kwa walioelekea Kijiji cha Matombo.
 Baada ya mafunzo kwa pande zote mbili Msowelo na Matombo, washiriki walikutana tena na kuungana kwa majadiliano baada ya mafunzo kwa vitendo
 
Washiriki wakijielezea jinsi walivyoweza kujifunza kutoka kwa wenzao walokokwenda.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 29,2017

0
0

































MAADHIMISHO YA SIKU YA MOYO DUNIANI TAASISI YA MOYO (JKCI) KUFANYA UPIMAJI KWA WANANCHI BILA MALIPO

0
0
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) katika kuadhimisha siku ya Moyo Duniani watafanya upimaji wa magonjwa ya Moyo bila malipo kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam na mikoa jirani. Upimaji huo utaenda sambamba na utoaji wa elimu ya lishe bora kwa afya bora ya Moyo.

Upimaji huu utafanyika katika viwanja vya Taasisi ya Moyo ambapo wananchi watapimwa urefu, uzito, shinikizo la damu (BP), sukari na kupewa ushauri. Kwa wale watakaokutwa na matatizo ya moyo watafanyiwa uchunguzi zaidi na kupatiwa matibabu. Kauli mbiu ya siku hii ni: “Moyo wenye Afya”.

Katika wiki hii ya maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani tuna kambi maalum ya upasuaji wa moyo wa bila kufungua kifua ambayo imeanza tarehe 25/09/2017 hadi tarehe 29/09/2017. Kambi hii tunaifanya kwa kushirikiana na Taasisi ya Madaktari Afrika ya nchini Marekani.

Hadi sasa tayari tumewafanyia upasuaji wa bila kufungua kifua kwa kutumia mtambo wa Cathlab (kwa jila la kitaalam Cathertarization) wagonjwa 23, siku ya kesho tutamalizia kuwafanyia upasuaji wagonjwa watano ili kufiokia idadi ya wagonjwa 28 tuliyolenga. Nia ya kambi hii ni kutoa huduma ya matibabu kwa wagonjwa na kubadilishana uzoefu wa kazi.

Wafanyakazi wa Taasisi hii tunahakikisha tunatoa huduma bora zaidi za magonjwa ya moyo kwa wananchi wenye matatizo hayo. Mpango wetu ni kutoa tiba ya moyo, upasuaji wa moyo na elimu kwa jamii ambayo itawasaidia wananchi kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusiana na magonjwa ya moyo ambayo ni moja ya magonjwa yasiyoambukiza na mtu anaweza kuyaepuka kwa kufuata ushauri wa kitaalam.

Tangu mwaka 2015 tumewafanyia upasuaji wa kupasua kifua, kuziba mishipa ya moyo, upasuaji wa mishipa ya moyo, upasuaji wa mishipa ya damu, kuweka vyuma ndani ya moyo, na kuweka kifaa maalum cha kuusaidia moyo ili uweze kufanya kazi vizuri (Pacemaker) zaidi ya wagonjwa 1500.

Hatua hiyo imewezesha Serikali kuokoa zaidi ya shilingi bilioni 45 fedha ambazo zingetumika kuwatibia wagonjwa wa moyo iwapo wangepelekwa njje ya nchi, hii ni sawa na asilimioa 85.Taasisi pia inatoa huduma ya uchunguzi wa kipimo cha magonjwa ya moyo kwa watoto wachanga waliopo tumboni mwa mama zao (FETAL ECHOCARDIOGRAPHY) ili kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la.

Tangu kuanza kutolewa kwa huduma hii mwezi wan ne mwaka huu jumla ya kinamama wajawazito 37 wameshafanyiwa uchunguzi wa kipimo hicho kati ya hao watoto watano walikutwa na matatizo ya moyo jambo ambalo litawawezesha kupata matibabu mapema pindi watakapozaliwa.

Tunawaomba wananchi waadhimishe siku hii kwa kujitokeza kwa wingi kupima afya zao hii itawasaidia kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la na hivyo kuanza matibabu mapema kwani asilimia kubwa ya wagonjwa tunaowapokea mioyo yao huo haiku katika hali nzuri.


Imetolewa na :

Kitengo cha Uhusiano na Masoko
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete

MTENDAJI MKUU WA TFS, PROF. DOS SANTOS SILAYO AFANYA ZIARA WILAYANI MKURANGA KWA AJILI YA KUIMARISHA UHIFADHI NA KUJADILI MIKAKATI YA KUZUIA WAVAMIZI KWENYE MISITU WA HIFADHI

0
0
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo alimpomtembelea jana Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga ofisini kwake akimuonesha baadhi ya maeneo kwenye ramani jinsi vyanzo vya maji vilivyoharibika kutokana na tabia ya baadhi ya wananchi kuvamia kwa kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Misitu. Mwingine ni Meneja Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wa Wilaya ya Mkuranga Christina Mohamed
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo akiteta neno na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga wakati wa ziara ya kujionea jinsi wananchi walivyovamia na kuanzisha shughuli za kibinadamu katika Hifadhi za Msitu wa Vikindu.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo kuu akisaini jana kitabu cha wageni mara alipotembelea ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga ikiwa lengo la ziara hiyo ni kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi
Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga akimuonesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo baadhi ya maeneo ya Hifadhi yaliyovamiwa na kuanzishwa shughuli za kibinadamu katika Hifadhi ya Msitu wa Vikindu. Lengo la ziara Mtendaji Mkuu wa TFS hiyo ilikuwa ni kuimarisha uhifadhi kwa kujadili mikakati ya kuzuia wavamizi kwenye msitu wa hifadhi

WATANZANIA WANG'ARA SHINDANO LA MWANDISHI BORA WA SAYANSI NA KILIMO AFRIKA

0
0
Mwandishi wa gazeti la Guardian, Gerald Kitabu ameshinda tuzo ya umahiri wa habari za sayansi katika eneo la magazeti huku akiwaashinda waandishi wengine kutoka nchi zingine saba za Afrika.

Kitabu alikuwa anachuana na waandishi kutoka nchi za Nigeria, Burkina Faso, Ghana, Ethiopia, Kenya, Tanzania na Uganda. Shindano hilo lilifanyika jana katika Hoteli ya Speke Resort Munyonyo iliyoko nje kidogo ya jiji la Kampala.

Kwa ushindi huo, Kitabu ambaye ni mshindi wa jumla wa shindano la Tanzania, alijinyakulia kitita cha dola za marekani 1,500 pamoja na simu aina ya iPhone 7+ yenye thamani za dola za Marekani 1,200. 

Mwandishi mwingine wa Tanzania aliyepata tuzo ni Koleta Makulwa kutoka Radio Free Afrika ambaye aliwashinda waandishi wengine ambao walikuwa wanashindana katika eneo la Radio. ambapo Tanzania ilizidi kung'ara baada ya Mwandishi wa Star Tv Dino Mgunda kuwa mshindi wa pili katika waandishi wa televisheni. 

Koleta aliondoka na kitita cha dola za Marekani 1,500, simu aina ya iPhone 7+ ya thamani ya dola za marekani 1,200 wakati Dino Mgunda alipata zawadi ya dola za marekani 1,000 na simu ya iPhone7+ ya thamani ya dola za marekani 1,000.

Katika shindano hilo jumla ya waandishi 20 waliwakilisha nchi hizo. waandishi hao ni wale ambao walikuwa washindi katika shindano la nchi mahalia, shindano ambalo lilifanyika mwanzoni mwa wiki hii katika nchi hizo ikiwemo tanzania. 

Shindano hilo liliandaliwa na Jukwaa la wazi la Bioteknolojia za Kilimo (OFAB) ambalo linahamasisha matumizi ya bioteknolojia katika kilimo ili kuwezesha nchi za Afrika ziweze kujitosheleza kwa chakula.Mshindi wa jumla katika shindano hilo la jana ni mtangazaji wa kituo cha TVC, Omolara Afolayan kutoka Nigeria. Washindi waliteuliwa na jopo la majai watano.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona (kushoto), akimkabidhi cheti Mwandishi wa Star Tv Dino Mgunda kuwa mshindi wa pili kwa waandishi wa Televisheni kwenye shindano hilo lililofanyika jana nchini Uganda.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona, akimkabidhi cheti Mwandishi wa Tanzania Koleta Makulwa kutoka Radio Free Afrika ambaye alipata tuzo na kuwashinda wenzake ambao walikuwa wanashindana katika eneo la Radio.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Uganda na Mjumbe wa Bodi ya ASARECA, Dr. Ambrose Agona, akimkabidhi cheti Mwandishi wa Tanzania wa gazeti la Guardian, Gerald Kitabu ambae alishinda tuzo ya umahiri wa habari za sayansi katika eneo la magazeti huku akiwaashinda waandishi wengine kutoka nchi zingine saba za Afrika. 
Keki ikikatwa katika hafla hiyo

IGP SIRRO AKABIDHIWA RAMANI YA NYUMBA ZA POLISI ZITAKAZOJENGWA ARUSHA

0
0
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo (wapili kulia), akimkabidhi Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro (katikati), mchoro wa ramani ya nyumba za Polisi za kisasa zitakazojengwa kufuatia za awali kuteketea kwa moto. Hatua ya ujenzi imeanza mara moja kufuatia Mhe. Rais Dkt. John Magufuli, kutoa kiasi cha shilingi milioni 260 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba hizo. Wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Makampuni ya Hanspaul, Kamaljit Singh, na kulia ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha (DCP) Charles Mkumbo na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Wakala ya Majengo Arusha Bw. Victor,. Picha na Jeshi la Polisi.
Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Simon Sirro, akiagana na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, alipomtembelea ofisini leo tayari kwa safari ya kurejea Dar es salaam, baada ya kuwapapole na kukagua eneo la nyumba za Polisi zilizoteketea kwa moto. Picha na Jeshi la Polisi.

MAADHIMISHO YA SIKU YA MOYO DUNIANI YAFANYIKA ZANZIBAR

0
0
Muakilishi wa Jimbo la Mpendae Said Mohd Dimwa wapili kushoto akifuatana na Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi katika Maandamano ya maadhimisho ya Siku ya Moyo Duniani yaliofanyika katika Ofisi ya Jumuiya ya watu wenye maradhi yasioambukiza (ZNCDA)Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja
Maandamano yalioongozwa na Bend ya Chipukizi yakielekea katika Ofisi ya Jumuia ya watu wenye maradhi yasioambukiza katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja
Vikundi mbalimbali vya mazoezi vikishajiisha suala zima la ufanyaji mazoezi ili kulinda afya na maradhi mbalimbali, katika siku ya maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
Makamo mwenyekiti wa ZNCDA Ali Zubeir Juma akitoa hotuba ya makaribisho kwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
Mgeni rasmi katika maadimisho ya siku ya Moyo Duniani Mwakilishi wa Jimbo la Mpendae Said Mohd Dimwa akitoa hotuba kuhusiana na kujikinga na maradhi mbalimbali yanayotokana na Ulaji,Unywaji wa Pombe na Uvutaji wa Tumbaku katika maadhimisho hayo yliofanyika katika Ofisi ya Jumuiya ya watu wenye maradhi yasioambukiza (ZNCDA)Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.
Wananchi mbalimbali waliojitokeza kupimwa afya zao katika maadhimisho ya Siku ya moyo Duniani 29/09/2017.Mpendae Wilaya ya Mjini Unguja.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.

Serikali Kuzichukulia Hatua Taasisi Zilizokiuka Taratibu za Manunuzi 2016/2017

0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Balozi Dkt. Matern Lumbanga (kushoto) akiongea wakati wakimkabidhi Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma,  Kulia ni Mjumbe wa Bodi hiyo Prof. Sufian Bukurura.
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Balozi Dkt. Matern Lumbanga wakati wa makabidhiano ya Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Balozi Dkt. Matern Lumbanga akimkabidhi Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akikata utembe baada ya kupokea Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma, Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Balozi Dkt. Matern Lumbanga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akionesha kwa wanahabari na wajumbe wengine wa Bodi(hawapo pichani) kitabu cha Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma, , Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Balozi Dkt. Matern Lumbanga. 
 Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiongea na wajumbe wa Bodi ya ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) baada ya kupokea Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma ambapo ameahidi kuzichukulia hatua taasisi zote zilizokiuka taratibu za manunuzi zilizoainishwa kwenye Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
 Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA) Dkt. Laurent Shirima akiongea, wakati wakimkabidhi Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango Ripoti ya Tathmini ya Utendaji kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 Leo Mjini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya ya Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi  ya  Umma (PPRA).PICHA NA IDARA YA HABARI-MAELEZO.


Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma

Serikali imesema itazichukulia hatua Taasisi zote zilizokiuka sheria na kanuni za manunuzi ya Umma pamoja na zile zenye viashiria vya rushwa ambazo zimebainika katika ripoti ya tathmini ya utendaji iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa mwaka wa Fedha 2016/17.

Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alipokuwa akipokea ripoti ya tathimini ya utendaji wa Taasisi za Serikali katika sekta ya Manunuzi iliyofanywa na PPRA kwa mwaka wa Fedha 2016/17.

“Tutazichukulia hatua na kuziwajibisha taasisi zote ambazo zimebainika katika ripoti hii kuwa na viashiria vya rushwa au kufanya malipo yenye utata katika manunuzi yao,” alisema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango amesema kuwa, zaidi ya 70% ya fedha za Umma zinatumika kununua vifaa na huduma mbalimbali hivyo Serikali haitavumilia kuona fedha hizo zinatumika bila kufuata sheria na kanuni zilizowekwa.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa PPRA Balozi Dkt. Matern Lumbanga amezitaja taasisi ambazo zimekiuka sheria na taratibu za manunuzi kwa mwaka 2016/2017 kuwa ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Taasisi ya Mifupa (MOI) pamoja na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Taasisi nyingine ni Shirika la Bima la Taifa (NIC), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mamlaka ya Anga (TCAA), Wizara ya Fedha na Mipango na Halmashauri ya Wilaya Kondoa. 

Balozi Lumbanga amesema kuwa uchunguzi wa zabuni mbili zenye thamani ya shilingi bilioni 160.5 ambazo zilikuwa zinatekelezwa na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja TCAA haukubainika mapungufu ya msingi na PPRA ilipendekeza utekelezaji wa miradi hiyo uendelee kama ilivyopangwa.

“Uchunguzi uliofanywa katika taasisi sita zilizobaki ulibaini kuwa Serikali ilipata hasara ya takribani shilingi milioni 12.15 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo, ucheleweshaji wa malipo kwa wakandarasi uliosababisha ongezeko la riba pamoja na faini zilizotokana na ukiukwaji wa taratibu za kijamii na mazingira kabla ya kuanza kwa utekelezaji wa kazi za ujenzi,” alisema Balozi Lumbanga.

Balozi Lumbanga amezitaja Taasisi zilizobainika na malipo yenye utata kuwa ni Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na Halmashauri ya Kwimba. Ukaguzi wa kupima upatikanaji wa thamani ya fedha ulibaini malipo yenye utata katika taasisi hizo tatu ambazo ni kiasi cha shilingi milioni 483.44 zililipwa kwa wakandarasi kwa kazi ambazo hazikuwa zimefanyika.

Vile vile amesema kuwa, miradi 33 katika taasisi 17 ilibainika kuwa na kiwango kikubwa cha viashiria vya rushwa. Taasisi hizo ni Mamlaka za Maji Safi na Maji Taka za Moshi (Muwasa), Mwanza (Mwauwasa) na Arusha (Auwasa) pamoja na Halmashauri ya Wilaya za Wilaya za Msalala, Kibondo na Moshi.

Taasisi byingine ni Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Chuo cha Ufundi Arusha, Halmashauri ya Mjia wa Kahama, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA), Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Halmashauri ya Mji wa MAsasi pamoja na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).


Ripoti hiyo ni ripoti ya 11 kuwasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango tangu PPRA ilipoanzishwa.

KIITEC LAUNCHED SOLAR POWER PLANT AND SOLAR LABORATORY

0
0
Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania (C) cuts a ribbon to officiate the launch of Solar Power plant and laboratory at KIITEC in Arusha, others in photo are senior officials from the partners institutions supporting the Institute. 
FTE President Fransis Bronchon,(R) briefing invited guests on Solar Project at KITEEK during the launch event at Arusha. 
Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania(C) got briefing on project from, Albert Mtana, (R)-Teacher of Electrical and Solar Photovoltaic System (L) is Michel Ramser-VP Strategic Marketing and Sponsorship (ADEI). 
Solar panel installed at the centre. The Kilimanjaro International Institute for Telecommunications, Electronics and Computers (KIITEC) has launched 30KW solar power plant and solar laboratory at its training centre in Arusha recently. The Guest of Honour at launch event was Her Excellency Malika Berak, Ambassador of France in Tanzania, also the event brought together the partners that have supported KIITEC for many years. 

These are: Schneider Electric East Africa, the Schneider Electric Foundation, ADEI, EDF Help and the Foundation for Technical Education (FTE). Speaking during the event, KIITEC Director of studies, Mr. Daniel Mtana, said the opening of this solar power plant speaks to the accomplishment of institute’s vision to become the centre of training excellence for renewable energy, particularly solar photovoltaic systems in East Africa. 

“Committed to true hands-on experience, KIITEC has now invested heavily in photovoltaic solutions and strives to be recognized as the premier provider of quality technical education in a student-centered community.” General manager at Schneider Electric East Africa, Mr. Mr. Edouard Heripret, said in most sub-Saharan countries, the rate of enrolment in formal secondary technical and vocational training and education (TVET) does not exceed 5%. 

“Vocational training has always been at the heart of Schneider Electric’s DNA. In East Africa, we have been committed to support technical training since 2009. Kiitec was one of our first training partners and I am pleased today to participate in the inauguration of the solar plant and laboratory, as these new components will allow students to have a full set of competencies to enter the labour market and will support access to energy for everyone.” Mr. 

Heripret added “At Schneider Electric, we are building sustainable communities through energy knowledge and leadership, thanks to the Schneider Electric Foundation. Its aim is to contribute to the development of people and societies through education, innovation, awareness-raising and vocational training related to energy. 

It acts, anywhere in the world where the company is present, through its three programmes. KIITEC is an international technical institution, was founded in 2004 by French engineers and has produced some of the most competent technicians in the country. Two NGOs, the Foundation for Technical Education (FTE-Swiss) and Action Development Education International (ADEI-French), support the institution. Schneider Electric assists ADEI in its support of KIITEC. 

The institute is a pilot centre, with the goal of transposing and exporting its model from Tanzania, to Kenya. It provides its students with the basic skills in telecommunications, electronics, information science, networks and industrial automation systems. 

The training lasts over two years. It comprises lectures complemented by practical training, project design, and a three-month outplacement in a company. As of today, 350 young people, comprising 90% of the students, have obtained their diploma, the ‘National Technical Award’, which is recognized by the local government, and have all found jobs, mainly in the industrial maintenance sector.

SERIKALI YALIFUNGIA GAZETI LA RAIA MWEMA KWA SIKU 90

0
0







Kituo cha Mabasi Ubungo kuzalisha ajira 20,000

0
0
NA CHRISTINA MWAGALA, OFISI YA MEYA WA JIJI

MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amekutana na ugeni kutoka Jiji la Shanghai nchini China na kujadili mambo mbalimbali yamaendeleo jijini hapa ikiwemo suala la uboreshaji wa kituo cha Mabasi Ubungo.

Ugeni huo uliambatana na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Linghang Cathy Wang ambayo ndiyo imeingia mkataba na Halmashauri ya jiji kwa ujenzi wa kituo hicho.Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo hayo, Meya Mwita alisema kuwa ugeni huo umeridhia kuwekeza katika nyanja mbalimbali ikiwemo kituo cha mabasi ubungo.

Alifafanua kuwa jiji la Dar es Salaam linakaribia kunza kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa kubadilisha kituo cha mabasi ubungo na kwamba hatua mbalimbli zimeshakamilika ili kupisha mradai huo.Alisema kuwa mara baada ya kukamilika kwa mradi huo jumla ya watanzania 20,000 watapata ajira jambo ambalo litawezesha kuongeza kipato kwa wananchi na hivyo pia kuwezesha vijana kuondokana kwenye makundi ambayo sio salama.

Alisema kufanikisha kwa mradi huo, utasaidia pia kuongeza mzunguko wa fedha jijini hapa kutokana na kuwepo kwa fursa nyingi za kibiashara.“ Leo nimekutana na ugeni ambapo kwa kiasi kikubwa mnafahamu ndugu zetu hawa wamekuwa na urafiki mkubwa katika nchini yetu, tumejadiliana mambo mengi ambayo yote ni yakuleta maendeleo katika jiji letu.

“ Lakini kubwa zaidi ni kuhusu ujenzi wa kituo cha mabasi Ubungo, ambapo hivi karibuni tunatarajia kuanza kwa mradi huo, na wananchi pia watajulisha, nitumie fursa hii kuwaeleza wananchi kuwa jiji linafuata utaratibu katika kutekeleza mradi huo” alisema Meya Mwita.

“ Fursa hii ni kubwa ambayo tumeipata, watanzania watapata ajira, mzunguko wa fedha kwenye jiji letu utaongezeka, kama Meya wa jiji hili nimewakaribisha tufanye kazi pamoja, lengo likiwa nikuweka jiji kwenye muonekano mzuri” aliongeza.Kwaupande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya Linghang Cathy Wang alimpongeza Meya Mwita kutokana na aina ya utendaji wake wa kazi nakuahidi kuonyesha ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo.

Alisema kuwa Meya Mwita ni kiongozi anayefanya kazi kwa bidii na umakini na kwamba kutokana na jitihada hizo za kulijenga jiji , kampuni yao itafanya  kazi na kumuhakikisha kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa.

BBC Tanzania watembelea wadau wake

0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa BBC, Idhaa ya Kiswahili kwa upande wa Tanzania, Bw. John Solombi leo katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje. Timu ya BBC imeanza ziara kuwatembelea wadau wake wakubwa katika masuala ya kupashana habari na wameanza kwa kuitembelea Wizara ya Mambo ya Nje na baadaye walielekea kwa msemaji wa Jeshi la Polisi nchini. Katika mazungumzo hayo, wawili hao walikubaliana kufanya kazi kwa karibu kwa maslahi ya kuuelimisha na kuuhabarisha umma. 
Bw. Solombi akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo. 
Mazungumzo yanaendelea. Katika picha anaonekana Bw. Aboubkar Famau, Mtangazaji wa BBC na Mkuu wa Kitengo cha Uratibu wa Vipindi, akichangia jambo katika mazungumzo hayo. Kulia kwake ni Bw. Ally Kondo, Afisa Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya Nje na aliyekaa peke yake ni Bi. Halima Nyanza, Mtangazaji wa BBC. 
Picha ya pamoja 
Timu ya BBC baada ya kukutana na Kitengo cha Mawasiliano ilipata fursa ya kusalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba (Mb). Pichani anaoenekana Mhe. Naibu Waziri akiwapa neno la shukrani Team ya BBC kwa uamuzi wao wa kuichagua Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuwa mdau wa kwanza kutembelewa.
Mhe. Naibu Waziri akiwa katika picha ya pamoja na Team ya BBC na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali cha Wizara ya Mambo ya Nje

UFAFANUZI KUHUSU KATIBU MKUU WA CCM, KINANA

0
0
Chama Cha Mapinduzi, kimefafanua kuhusu Katibu Mkuu wa Chama hicho, ABDULRAHMAN KINANA, kutohudhuria Kikao cha Kamati Kuu, kikisema kwamba hakuhudhuria Kikao hicho kutokana na kupata Dharura ya Kihali ya Ki-Utu.

Hata hivyo, kimesema kazi yote ya Maandalizi ya Kikao cha Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa-NEC, kinachoanza kesho imefanywa na KINANA.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, HUMPHREY POLEPOLE, amesema Kamati Kuu katika kikao chake ilipata taarifa rasmi kupitia kwa Mwenyekiti Rais JOHN MAGUFULI kwamba Katibu Mkuu ameomba udhuru wa kihali.

Katika hatua nyingine, Wajumbe wa Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa-NEC, wameanza kuwasili jijini Dar es salaam, katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba kwa ajili ya kukamilisha taratibu muhimu kabla ya kuanza kwa Vikao hivyo muhimu vya Chama.

Kuanza kwa kikao hicho kesho kunatokana na kumalizika kwa Kikao cha Kamati Kuu ambacho kilikuwa chini ya Mwenyekiti wake, Rais JOHN MAGUFULI.

Pamoja na mambo mengine, POLEPOLE, amesema vikao hivyo vya maamuzi vina kazi ya kujadili, kupitisha na kufanya uteuzi wa mwisho wa wana-CCM-wanaoomba ridhaa ya nafasi ya Uenyekiti wa CCM ngazi ya Wilaya.

Kikao cha NEC kitafanyika kwa siku Mbili, Jumamosi na Jumapili.

Serikali Yaipongeza Muhimbili kwa Kutoa Huduma Bora

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulusubisya (kulia) akitembelea Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo ili kuona maeneo mbalimbali yaliokarabatiwa vikiwamo vyumba vya upasuaji na vyumba vya kulaza wagonjwa wa figo. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Profesa Lawrence Museru.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulusubisya akizungumza na wafanyakazi wa Idara ya Uzingizi leo pamoja na watumishi wengine wa hospitali hiyo
Baadhi ya wafanyakazi wa idara hiyo pamoja na watumishi wengine mbalimbali wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Ulusubisya leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Profesa Lawrence Museru akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Ulusubisya kuzungumza na wafanyakazi wa idara hiyo leo.
Wafanyakazi wa Muhimbili wakiwamo wa Idara ya Usingizi wakimsikiliza Mkurugenzi wa Muhimbili, Profesa Museru.Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili


Serikali imepongeza juhudi zinazofanywa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) za kuboresha huduma sanjari na kuwawezesha watalaam kusoma ili wapate ujuzi zaidi na kutoa huduma bora na za kibingwa.

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulusubisya wakati akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo kupitia Idara ya Usingizi.

Dk. Mpoki amesema serikali inatambua juhudi zinazofanywa na uongozi wa hospitali na kwamba hatua hiyo inaleta faraja kwa Watanzania kwani sasa wana uhakika wa kupata huduma bora .

“Naona mabadiliko makubwa hapa Muhimbili, mmeongeza vyumba vya upasuaji, Vyumba vya wagonjwa mahutuni (ICU) na pia mnaendelea kuboresha huduma zingine kwakweli hatua hii ni ya kupongezwa na ninaomba muendelee kujituma kwani hospitali hii inategemewa kwa sababu mna watalaam wengi waliobobea hapa,’’ amesema Dk. Mpoki.

Kuhusu kusomesha wataalam, Katibu Mkuu amesema hatua hiyo ni nzuri kwani watalaam hao watapata fursa ya kuwatawafundisha wengine ili nao wapate ujuzi .

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru amesema MNH inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa wataalam katika Idara ya Usingizi na kwamba hospitali inaendelea kutatua changamoto hizo.

Dk. Mpoki ambaye ameambatana na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Dk. Doroth Gwajima pamoja na mambo mengine wamepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali ya Taifa Muhimbili ikiwemo vyumba vya upasuaji, wodi ya wagonjwa mahututi na wodi ya watoto.

CHINA YAIPATIA TANZANIA MSAADA WA SH. BILIONI 29.4 KWA AJILI YA MIRADI YA MAENDELEO

0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (wa pili kulia) na Kaimu Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Gou Haodong (wa tatu kushoto) wakisaini makubaliano ya msaada wa Sh. bilioni 29.4 kwa ajili ya miradi ya Ujenzi wa Chuo cha VETA Mkoani Kagera, Utalii wa Kijilojia na Ukarabati wa Uwanja wa Taifa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Gou Haodong (kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) wakibadilishana hati ya makubaliano ya msaada wa Sh. bilioni 29.4 kwa ajili ya miradi ya Ujenzi wa Chuo cha Ufundi (VETA), Mkoani Kagera, Utalii wa Kijiolojia na Ukarabati wa Uwanja wa Taifa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Gou Haodong (kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (kulia) wakiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) hati ya makubaliano ya msaada wa Sh. bilioni 29.4 uliotolewa na Serikali ya China kwa ajili ya miradi ya Ujenzi wa Chuo cha Ufundi (VETA) Mkoani Kagera, Utalii wa Kijiolojia na Ukarabati wa Uwanja wa Taifa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Amina Khamis Shaaban (kushoto) na Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bw. John Rubuga (kulia) wakishuhudia utiliwaji saini makubaliano ya msaada wa Sh. bilioni 29.4 uliotolewa na China kwa ajili ya miradi ya Ujenzi wa Chuo cha Ufundi (VETA) Mkoani Kagera, Utalii wa Miamba na Ukarabati wa Uwanja wa Taifa, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James (katikati), Kaimu Balozi wa China Nchini Tanzania, Mhe. Gou Haodong (wa pili kulia) na Maafisa waandamizi kutoka Tanzania na China wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kusainiwa makubaliano ya msaada wa Sh. bilioni 29.4 uliotolewa na Serikali ya China kwa ajili ya miradi mbalimbali katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikali Wizara ya Fedha na Mipango


Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
SERIKALI ya China imeipatia Tanzania msaada wa Shilingi bilioni 29.4 kwa ajili ya kusaidia sekta ya elimu ya ufundi stadi, utalii wa kijiolojia na kukarabati wa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Makubaliano ya msaada huo yametiwa saini Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, kwa niaba ya Serikali, na Kaimu Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Gou Haodong.
Bw. Doto James alisema kuwa kiasi cha Shilingi bilioni 22.4 cha msaada huo kitatumika kujenga Chuo cha Ufundi Stadi-VETA wilayani Ngara mkoani Kagera, ambacho kitakapo kamilika kitadahili zaidi ya wanafunzi 400.
“Fedha hizo zitatumika kujenga vyumba 19 vya madarasa, ujenzi wa karakana 9 za kutolea mafunzo ya elektroniki, ufundi bomba, useremala, ufundi uashi na upakaji rangi” alisema Bw. James
Alieleza kuwa kiasi hicho pia kitatumika kujenga majengo ya utawala, mabweni, nyumba za walimu na miundombinu mingine itakayosaidia kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia kwenye chuo hicho.
“Tunaamini kwamba msaada huo utakuwa sehemu ya kusaidia jitihada za Serikali za kujenga uwezo wa wataalamu wake watakaochangia kukuza sekta ya uzalishaji na hatimaye kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira kwa vijana nchini” alisema Bw. James
Katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James alibainisha kuwa katika makubaliano ya msaada huo, Jamhuri ya watu wa China, itatoa kiasi cha shilingi bilioni 6.7 kwa ajili ya kuukarabati Uwanja wa Taifa wa Michezo wa Dar es Salaam.
“Katika makubaliano yetu ya msaada wa kuendeleza Uwanja wa Taifa wenye uwezo wa kuingiza watu 60,000, China itatoa msaada wa kiufundi na vifaa vya kisasa vya michezo na utaalamu katika usimamizi na ukarabati wa uwanja” Alifafanua Bw. James
Bw. Doto James alisema kuwa kiasi kingine cha shilingi  milioni 300 kitatumika kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu wa kuanzishwa kwa aina mpya ya utalii ujulikanao kama utalii wa kijiolojia “Geopark Project” katika Hifadhi ya Taifa Ngorongoro, mkoani Arusha.
Alisema lengo la utafiti huo ni kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika na maajabu mbalimbali ya kitalii yaliyopo nchini ambayo hayajatumika kikamilifu kuvutia watalii watakaoongeza pato la Taifa
“Tanzania ina kila sababu ya kujifunza kutoka katika Hifadhi ya Kimataifa ya Jiolojia ya Jiaozuo ya Yuntaishan ya China, iliyoanzishwa mwaka 2000 ambayo inaongeza asilimia 37.2 ya watalii kila mwaka na huchangia asilimia 12 ya pato la Taifa la nchi hiyo” aliongeza Bw. Doto James.
Aliishukuru China kwa ushirikiano wake wa dhati na Tanzania tangu miaka ya 1960 na kwamba mpaka sasa nchi hiyo imeendelea kuipiga jeki Serikali katika ujenzi wa miradi mbalimbali ukiwemo upanuzi wa Chuo cha Polisi Moshi, Ujenzi wa Maktaba mpya katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Kwa upande wake Kaimu Balozi wa China hapa nchini, Mhe. Gou Haodong, amesema kuwa nchi yake inatarajia kwamba ujenzi wa Chuo Cha Ufundi VETA huko Ngara mkoani Kagera utaanza haraka kama ilivyopangwa.
Kuhusu masauala ya utalii wa kijiolojia katika Hifadhi ya Taifa Ngorongoro, alisema Tanzania ina bahati ya kuwa na vivutio vingi vya utalii lakini haijavutia idadi kubwa ya watalii kutoka China kuja kuvitembelea.
“Zaidi ya watalii milioni moja kutoka China wanatembelea nchi mbalimbali dunia lakini kati ya hao, Tanzania inapokea watalii elfu 20 tu kila mwaka kutoka China, lakini kwa kuanzisha mradi huu, watalii wengi kutoka China watavutiwa kuja nchini kufurahia utalii wa miamba, mandhari nzuri, urithi wa dunia, na kutembelea hifadhi za Taifa” aliongeza Mhe. Haodong
Akizungumzia masuala ya uchumi, Balozi huyo alisema kuwa hivi sasa China imekuwa mwekezaji mkubwa zaidi nchini Tanzania kwa kuwekeza kiasi cha Dola za Marekani bilioni 1.77 na kukuza ajira nchini.
Ameitaja baadhi ya miradi mikubwa iliyowekezwa kuwa ni pamoja na mradi wa miundombinu ya mtandao (Tanzania ICT Broadband backbone), Bomba la gesi la kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam, mradi wa kuboresha miundombinu ya Bandari, barabara na madaraja.
Hafla hiyo imehudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo, ambaye alisema kuwa msaada wa ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA mkoani Kagera kitaongeza watalaamu watakaosaidia kuendeleza sekta ya viwanda nchini.

UTIAJI SAINI WA MKATABA WA UJENZI WA MRADI WA RELI YA KISASA

0
0
  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja Kadogosa (kulia) na pamoja na Mjumbe wa Bodi  kutoka Kampuni ya Ukandarasi ya Yapi Merkezi Insaat ya nchini Uturuki wakisaini Mkataba wa ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja Kadogosa (kulia) na pamoja na Mjumbe wa Bodi  kutoka Kampuni ya Ukandarasi ya Yapi Merkezi Insaat ya nchini Uturuki wakibadilishana Mkataba wa ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
   Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja Kadogosa (kulia) na pamoja na Mjumbe wa Bodi  kutoka Kampuni ya Ukandarasi ya Yapi Merkezi Insaat ya nchini Uturuki wakionyesha kwa waandishi wa habari  Mkataba wa ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
     Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja Kadogosa akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
   Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hawa Ghasia akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
   Baadhi ya Wahandisi kutoka kampuni ya Ukandarasi ya Yapi Merkezi Insaat ya nchini Uturuki wakifuatilia hafla ya utiaji saini saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
   Baadhi ya Wafanyakazi kutoka shirika la Reli Nchini (TRL) na kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) wakifuatilia hafla ya utiaji saini saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.

   Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Uchukuzi) Dkt. Leonard Chamuriho akizungumza akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akibadilishana mawazo na Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya Ukandarasi ya Yapi Merkezi Insaat ya nchini Uturuki, Erdem Ariogl  pamoja na Kaimu Balozi wa nchini hiyo Yunus Belet wakati wa utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.
1.    Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro- Makutopora (Dodoma). Halfa hiyo ilifanyika leo Septemba 29, 2017.(PICHA NA MAELEZO)


VIWANDA MOROGORO VYA PONGEZWA KWA KUNUSURU UHARIBIFU WA MAZINGIRA

0
0
 Katikati Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Mhe. Luhaga Mpina, Mbele yake ni Bw. George Mratibu wa Kiwanda cha Ngozi Morogoro , cha ACE LATHER TANZANIA LTD, wakiwa katika ukaguzi wa mtambo wa kisasa wa kutibu majitaka kiwandani hapo ambapo Mpina yupo Mkoani Morogoro katika ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Sheria ya Mazingira na kanuni zake, kufuatia maagizo aliyoatoa awali katika ziara ya viwanda hivyo.

 Kushoto kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na maji Taka mjini Mororgoro, inginia Halima Mbiru, akimuonyesha Naibu Waziri Mpina Mpaka wa mabwawa ya maji taka mali ya mamlaka hiyo, hayapo katika picha. Mhe. Mpina alifanya ziara ya ukaguzi wa mabwawa hayo mapema leo.
 Katika picha ni washiriki katika ziara ya Naibu Waziri Mpina alipokagua Mabwawa ya majitaka kama yanavyoonekana katika picha.
Kushoto, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina kulia ni Mwenyeji wake  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Steven Kebwe katika kikao kabla ya kuanza ziara ya ukaguzi wa viwanda Mkoani hum oleo. (Picha na Evelyn Mkokoi)
Viewing all 46201 articles
Browse latest View live




Latest Images