Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

SPIKA JOB NDUGAI ATEMBELEWA NA BALOZI WA IRELAND NCHINI

$
0
0
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi wa Ireland nchini, Paul Sherlock (katikati) na Mshauri Mwandamizi wa Serikali hiyo, Ndg. Aran Corrington,  pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akimsikiliza Balozi wa Ireland nchini, Paul Sherlock (katikati) na kulia ni Mshauri mwandamizi wa serikali hiyo, Ndg. Aran Corrington,  pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. 

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akiagana na Balozi wa Ireland nchini, Paul Sherlock (kulia) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia)akiagana na Balozi wa Ireland nchini, Paul Sherlock (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi wa Ireland ulipotembelea Ofisi ya Bunge Mjini Dodoma, ukioongozwa na Balozi huyo.
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

WATU WA WILI WAMEUAWA NA POLISI MKOANI RUVUMA KATIKA MAJIBIZANO YA KURUSHIANA RISASI KATI YA POLISI NA WATU HAO.

$
0
0
Jeshi la polisi Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma limewaua watu wawili waisiojulikana kwa majina katika majibizano ya kurushiana risasi kati ya polisi na watu hao,Tukio hilo limetokea katika kijiji cha NANGURUKURU kata ya NANDEMBO tarafa ya NAMPUNGU .

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MATIBABU YA MHE. LISSU

MKURUGENZI WA MAENDELEO YA JAMII NCHINI AUNGANA NA WANANCHI WA KATA YA MONDO KATIKA UJENZI WA KITUO CHA AFYA

$
0
0
Attachments area Preview YouTube video MKURUGENZI WA MAENDELEO YA JAMII NCHINI ASHIRIKI KATIKA UJENZI WA KITUO CHA AFYA KATA YA MONDO.

UINGIZAJI WA MIFUGO KWENYE PORI LA AKIBA LA MKUNGUNERO UMEADHIRI UHIFADHI

$
0
0
Na mwandishi wetu, Kondoa
Uingizaji wa mifugo kwenye pori la akiba la Mkungunero lililoko wilayani Kondoa mkoani Dodoma umeathiri uhifadhi wa pori hilo na kusababisha kukauka kwa baadhi ya vyanzo vya maji na kutoweka kwa baadhi ya wanyamapori adimu.

Meneja wa Pori la akiba la Mkungunero, Emmanuel Bilaso akizungumza na a waandishi wa habari waliotembelea pori hilo hivi karibuni amesema pori hilo linalopakana na Hifadhi ya Taifa ya Tarangire lina vyanzo muhimu vya maji ambayo yanayotegemewa na wananchi wengi kwa shughuli za kijamii na kiuchumi.

Bilaso amesema pori hilo la Mkungunero pia lina vyanzo vya maji ya mto Tarangire ambao ndiyo uhai wa Hifadhi ya taifa ya Tarangire na akatoa wito kwa wananchi kutilia mkazo uhifadhi ambao una umuhimu mkubwa kwa jamii na maendeleo ya taifa.

Amesema operesheni inayoendelea katika pori hilo imefanikisha kukamata kwa mifugo mingi katika pori hilo ambayo inachunga humo kinyume na sheria ya uhifadhi ambayo inakataza shughuli za binadamu kwenye maeneo yaliyohifadhiwa.

“Tumekamata ng’ombe zaidi ya 230 ambao waliingizwa na wananchi kinyume cha sheria na wamefikishwa mahakamani na kutozwa faini ya zaidi ya shilingi milioni 6” alisema bwana Bilaso.

Aliongeza kuwa kuingiza ng’ombe ndani ya hifadhi ni kinyume cha sheria ya uhifadhi ambayo inatoa adhabu kali ikiwemo kutaifisha mifugo inayokamatwa ili iwe fundisho kwa watu wanaovunja sheria za uhifadhi.

Nae Mkuu wa mkoa wilaya ya Kondoa Sezaria Makota amewaonya wananchi wanaingiza mifugo katika pori hilo kuacha mara moja vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao ili iwe fundisho kwa watu wanaovunja sheria na kuingiza mifugo kwenye maeneo yaliyohifadhiwa.

Amesema  wilaya inaandaa mkakati wa uwepo wa makao makuu ya ncho Dodoma na kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Dodoma mpaka Babati kuwa fursa ya kiuchumi kwa wananchi na taifa.

“Tuna vivutio vingi vya utalii likiwemo pori la akiba la Mkungunero na mapango yenye michoro ya kale, ni matarajio yetu kwamba viongozi wengi na wabunge watapata fursa ya kutembelea na hasa kwa sasa ambapo barabara ya lami kutoka Dodoma mpaka Babati imekamilika´alisema mkuu wa wilaya.

lenye wanyamapori wengi wakiwemo simba, tembo, nyati na mimea adimu meneja wa pori la akiba la mkungunero emmanuel bilaso amesema watuhumiwa waliokamatwa

Nao baadhi ya wananchi wanaoishi kwenye vijiji kuzunguka pori hilo wameiomba serikali kuweka vipaumbele katika uhifadhi wa pori hilo la akiba la Mkungunero ikiwemo kulipa fidia kwa baadhi ya wananchi wanaotakiwa kupisha uhifadhi endelevu wa pori kama tathimini ilivyofanywa na serikali kwa mujibu wa sheria.

Diwani wa kata ya Itaswi  Said Mohamed Chobu alisema wananchi wanatambua umuhimu wa pori hilo lakini ni vizuri sasa wizara ya maliasili na utalii ikalipa fidia kwa wananchi kwenye vijiji kandokando ya hifadhi ili kuepuka uharibifu wa mazingira na migogoro baina ya wananchi na wahifadhi.

Uhamiaji yapata msaada wa vitendea kazi toka Shirika la IOM

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala akipokea msaada wa vifaa mbalimbali uliotolewa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM. Anayekabidhi vifaa hivyo ni, Mwakilishi wa Shirika hilo nchini Tanzania Dkt. Qassim Sufi. Vifaa hivyo vinajumuisha Kompyuta, mashine za kutolea nakala na kuchapishia vyenye thamani ya Dola za Kimarekani elfu arobaini.

Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na wana habari Limefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Uhamiaji, Kurasini, Dar es Salaam. 

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Peter Makakala akibadilishana nyaraka za makabidhiano ya msaada wa vifaa mbalimbali uliotolewa na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM. Anayebadilishana naye ni Mwakilishi wa Shirika hilo nchini Tanzania Dkt. Qassim Sufi. Vifaa hivyo vinajumuisha Kompyuta, mashine za kutolea nakala na kuchapishia vyenye thamani ya Dola za Kimarekani elfu arobaini. Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na wanahabari Limefanyika katika Ukumbi wa Mikutano Makao Makuu yaUhamiaji, Kurasini, Dar es Salaam.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 15, 2017

Kukamata na kuchoma nyavu haitoshi, tuwachome wahalifu- RC Rukwa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafi Zelote Stephen ameionya idara ya uvuvi iliyo chini ya wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi nchini kuhakikisha wanawachukulia hatua wale wote wanaokamatwa na zana haramu za uvuvi na kutangaza hukumu zao na si kuishia kwenye kuchoma zana zao tu.

Ameyasema hayo wakati akijiandaa kushiriki zoezi la kuteketeza zana haramu zilizokamatwa kupitia doria katika vijiji vya Kabwe, Isaba, Chongokatete, mandakerenge, kolwe, lupata na kisenga katika wilaya ya Nkasi Mkoani humo. zoezi lililofanyika katika mwalo wa kijiji cha Kirando. 

“Kukamata na kuchoma haitoshi, kwasababu hii inaungua tu, nataka tuwachome wahalifu kwa kutumia sheria, nimechoma sana nyavu hizi na huu mtindo bado unaendelea, hii haina tija, kila tukichoma madhara yanatokea, mazingira yanaharibika, sasa tuseme basi, ningependa kusikia mhalifu kakamatwa kapelekwa mahakamani na kupewa adhabu,” Amesema

Katika kuhakikisha wahalifu hao wanapatika Mh. Zelote amewaasa watumishi wa idara hiyo kuachana na kupokea rushwa, jambo ambalo linaonekana kukwamisha juhudi za serikali katika kulinda rasilimali zake kwaajili ya faida ya kizazi hiki na kijacho.

Amesisitiza kuwa wananchi bado wanahitaji kuendelea kupatiwa elimu juu ya umuhimu wa rasilimali hizo na wajulishwe kuwa rasilimali hizo ni za watanzania wote na hatimae kuacha tabia kuvua samaki hao kwa zana zisizokubalika na sheria za serikali.

Mh. Zelote aliishauri idara hiyo kuwa panapokuwa na zoezi hilo linalofanyika mbele ya wananchi wahakikishe kunakuwa na nyavu halali zinazokidhi viwango vya serikali na kuwaelimisha wananchi tofauti iliyopo ili wasiojua nao wapate kufahamu matakwa ya serikali katika kuhifadhi mazingira.

Kutokana na doria hiyo iliyofanywa na kikosi cha usimamizi wa rasilimali za uvuvi Kijiji cha Kipili kwa kushirikiana na polisi pakmoja na kikosi cha jeshi la wanamaji wote wa kipili kuanzia Juni hadi September 2017 waliweza kukamatanyavu zisizokidhi viwango vya serikali zenye thamani ya shilingi milioni 57.6.

Miongoni mwa nyavu zilizokamatwa ni nyavu 32 za Makira (gilinets) zenye thamani ya shilingi milioni 38.4, nyavu za dagaa zenye macho chini ya 8mm zenye thamani ya shilingi milioni 16.5 na makokoro ya vyandarua yenye thamani ya shilingi milioni 2.7.

Awali akisoma taarifa hiyo fupi ya uteketezaji wa zana haramu za uvuvi kwa mgeni rasmi Afisa mfawidhi idara ya uvuvi kanda ya Rukwa Juma Makongoro alitaja kuwa kuna manufaa mengi yanayopatikana kutokana na rasilimali hiyo ikiwa ni pamoja na watu kujipatia ajira, kitoweo, fedha za kigeni na kuingizia serikali kodi ambayo hutumika kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mtaaafu Zelote Stephen (Kulia)akitoa maelekezo namna ya kuziteketeza nyavu haramu (hazimo kwenye picha) mbele ya maafisa aliongozana nao kushiriki uteketezaji wa zana hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mtaaafu Zelote Stephen (Katikati Mwenye suti ya ugoro) akiwasha moto tayari kwaajili ya kuzitekezeteza zana  haramu, kulia ni Juma Makongoro Afisa Mfawidhi Idara ya Uvuvi kanda ya Rukwa kushoto ni diwani wa kata ya kirando Kessy Sood


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mtaaafu Zelote Stephen kwa pamoja na  Mfawidhi Idara ya Uvuvi kanda ya Rukwa Juma makongoro pamoja na Diwani wa Kata ya Kirando Mh. Kessy Sood wakiteketeza zana haramu.
Nyavu zenye thamani ya shilingi milioni 57.6 zikiteketea kwa moto mbele ya wananchi, katika mwalo wa kijiji cha kirando, Ziwa Tanganyika, Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.

BANK OF AFRICA – TANZANIA yazindua program mpya ya kibenki ya “SWAHIBA MOBILE APP”

$
0
0
BANK OF AFRICA – TANZANIA imezindua programu yake mpya ya kibenki inayoitwa "SWAHIBA Mobile" kwenye soko la Tanzania. Huduma hii inakuja kama muendelezo wa programu ya B- Mobile, inayoruhusu watumiaji kufurahia huduma kamili za kibenki kupitia aina yoyote ya simu za mkononi, wakati wowote.

SWAHIBA Mobile App inawapa wateja urahisi wa kutumia huduma za kibenki katika simu kwani inakuja na muonekano mzuri Zaidi na sifa nyingi mpya zinanzowarahisishia wateja kufuatilia akaunti zao za binafsi na za kibiashara kwa wakati mmoja.

Huduma zipatikanazo kwenye programu hii ni: huduma za kuhamisha fedha, huduma za hundi, maombi ya mkopo wa papo hapo, malipo ya bili mbalimbali, huduma za utoaji fedha kwenye ATM bila kadi, kuongeza muda wa maongezi, usajili binafsi wa mobile banking na huduma za e-chama pamoja na nyingine nyingi.

Zaidi ya hayo, SWAHIBA Mobile APP inaweza kutumiwa na Mtanzania yoyote hata ambae si mteja wa BANK OF AFRICA. Hii ni kupitia huduma mbalimbali zinazopatikana kabla ya kuingia kwenye program yaani “without Log in services”. huduma hizi ni kama vile maelezo kuhusu Huduma mbalimbali zitolewazo na BANK OF AFRICA, Maombi ya Mikopo, maelekezo kuhusu yalipo Matawi ya BANK OF AFRICA na ATMs, pamoja na viwango vya ubadilishaji fedha za kigeni.

Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA - TANZANIA alisema Benki yake inajivunia kuanzisha programu hii mpya ya benki kiganjani katika wakati huu muhimu ambapo benki hiyo inaadhimisha miaka 10 ya biashara katika nchi ya Tanzania. "Uzinduzi wa SWAHIBA Mobile App ni namna ya kipekee ya kuwasilisha shukrani zetu kwa wateja, jamii, washirika, wamiliki na wadau wote, walio tupa ushirikiano wa kutosha katika kipindi cha miaka 10 ya kazi nchini ".

"Huduma hii pia inakuja kutia msistizo wa ahadi yetu ya kuweka mapendekezo ya wateja wetu kwanza na kuwaongezea uzoefu wa kidigitli Zaidi katika ukuwaji wa sayansi na technologia. Mkurugenzi aliendelea kueleza “Pia inathibitisha uamuzi wa benki wa kujenga uwepo wake wa kidigitali na kukidhi mahitaji ya haraka ya wateja wetu "

Bwana Emmanuel ameeleza: " katika dunia ya sasa kuna ongezeko kubwa sana la matumizi ya technologia pamoja na matumizi ya “Simu za kisasa na Tablets” tumeunda huduma hii katika ubunifu na uwezo wa hali ya juu sana na ambao mtanzania yoyote anaweza kutumia. Program hii inamuongezea mteja uzoefu wa kubenki kidigitali Zaidi huku akifurahia huduma maridhawa kwa uharaka zadid bila kujali kuhusu foleni benki au kufungwa kwa tawi.

Mbali na ongezeko la huduma SWAHIBA Mobile App inamfumo bora wa ulinzi wa fedha. “ Ulinzi wa fedha za wateja wetu ni kitu cha kwanza kabisa ambacho benki inaangalia kwenye programu hii benki imeingiza vipengele vya usalama wa hali ya juu kama vile vinavyopatikana kwenye benki ya mtandao (B WEB SMART) "alieleza Mr. Mshindo.

“Program yetu hii ni rahisi sana kutumia ikiwa imeundwa kwa kumzingatia mteja ili kumwezesha kuona machaguo mbalimbali punde tuu anapifungua program hii na hili limefanyika ili kupunguza mlolongo mrefu katika uchaguzi wa huduma ambayo mteja atakua anahitaji” alisema Mshindo, kwa sasa SWAHIBA MOBILE App, inaweza kupakuliwa kupitia “ Play store” kwa watumiaji wa Android na Apple iOS kwa watumiaji wa Iphone.

Sehemu ya wageni waalikwa wakiwa kwenye meza kuu.

Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA – TANZANIA, Mr. Ammishaddai Owusu-Amoah akizindua rasmi program ya SWAHIBA Mobile App. Kulia kwake ni mkuu wa kitengo cha rasilimali watu wa benki hiyo Ms. Mercy Msuya na Meneja Masoko, utafiti na maendeleo wa benki hiyo ndg. Muganyizi Bisheko.

Mr. Emmanuel Mshindo, Mkuu wakitengo cha Huduma mbadala za kibenki akitoa maelezo juu ya huduma mbalimbali zipatikanazo katika program ya SWAHIBA Mobile, wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma hiyo mapema hii leo.

Mkurugenzi Mkuu wa MaxCom Africa, watoaji wa huduma za Max Malipo pichani ndugu Jameson Kasati, ameipongeza BANK OF AFRICA kwa hatua za makusudi za kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma zake za kibenki. Aidha aliongeza Zaidi kua mtazamo wa BANK OF AFRICA wa kutumia mabadiliko ya kiteknolojia na kidigitali katika kusogeza huduma zake karibu Zaidi kwa watanzania unashabihiana na wa MaxCom.

Naibu Mkurugenzi wa BANK OF AFRICA Bw. Wasia Mushi, akiongea na wageni waalikwa (hawapo pichani) katika hafla ya uzinduzi wa program ya SWAHIBA Mobile mapema hii leo.

Sehemu ya wageni waalikwa, uongozi na wafanyakazi wa BANK OF AFRICA wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya hafla ya uzinduzi rasmi wa Programu ya SWAHIBA Mobile.

Tanzania iko Tayari kuwa Mwenyeji wa Tamasha la JAMAFEST 2019-Dkt. Harrison Mwakyembe:

$
0
0
Naibu Waziri Mkuu ambaye ni Waziri wa Wizara ya Mambo ya Afrika Mashariki ya Uganda Mhe. Ali Kirunda Kivejinja akimkaribisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe kabla ya kumkabidhi Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kuashiria kuwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa ni zamu yake kukabidhiwa dhamana ya kuandaa Tamasha la Nne (4) la Utamaduni na Sanaa la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) litakalofanyika mwaka 2019.
Naibu Waziri Mkuu ambaye ni Waziri wa Wizara ya Mambo ya Afrika Mashariki ya Uganda Mhe. Ali Kirunda Kivejinja akabidhi Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe ikiashiria kuwa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ni zamu yake kukabidhiwa dhamana ya kuandaa Tamasha la Nne (4) la Utamaduni na Sanaa la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) litakalofanyika mwaka 2019 jana usiku hafla hyo ilifanyika katika Jumba la Sanaa la Taifa jijini Kampala Nchini Uganda.
Kaimu Balozi ambaye pia Naibu Balozi wa Tanzania Nchini Uganda Balozi Elibariki Nderimo Maleko aliyevaa shati la kitenge akiwaongoza Washiriki wa Tanzania katika Tamasha la Utamaduni na Sanaa la Afrika Mashariki pamoja na Watanzania wanaishi Uganda kusherehekea kupokea bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kukabidhiwa kutoka kwa Nchi ya Uganda


Na Benedict Liwenga-WHUSM, Kampala-Uganda.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amesema kwamba, Tanzania iko tayari kuwa wenyeji wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST kwa mwaka 2019.

Kauli hiyo ameitoa jana Mjini Kampala nchini Uganda wakati wa Ufungaji wa Tamasha hilo kwa mwaka 2017 ambapo wenyeji kwa mwaka huu walikuwa ni nchi ya Uganda.

Mhe. Mwakyembe amezipongeza nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo zimehudhuria tamasha hilo kwa ushirikiano wa hali ya juu katika kubadilishana uzoefu na ujuzi juu ya masuala mbalimbali yanayohusu utamaduni na sanaa kwakuwa yameongeza mahusiano mapya ya karibu baina ya nchi hizo.

Waziri Mwakyembe aliezea kufurahishwa kwake kwa kujionea ngoma mbalimbali za kitamaduni toka kwa nchi wanachama ambazo zinaakisi uhalisia wa utamaduni wa nchi hizo, pia amefurahishwa na kwa kujionea bidhaa mbalimbali adimu toka kwa nchi hizo jambo ambalo amesisitiza kwamba nchi wanachama hazinabudi kuendelea kushirikiana katika kuzilinda tamaduni hizo na kuendelea kujifunza ujuzi mbalimbali wa kazi za sanaa.

“Nilipotembelea Maonyesho ya Tamasha hili pale katika viwanja vya Kololo nilifurahi sana kujionea ngoma za kitamaduni toka kwa vikundi mbalimbali vya nchi wanachama wa Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki, hakika inapendeza sana, kwakweli tuzidi kuzilinda tamaduni zetu na kushirikiana kwa karibu zaidi”, alisema Mhe. Mwakyembe.

Akiongea kuhusu suala la Tanzania kukubali kuwa wenyeji wa Tamasha lijalo litakalofanyika mwaka 2019, Dkt. Mwakyembe alisema kwamba, Tanzania iko tayari kuwa wenyeji katika tamasha hilo lijalo na amezitaka nchi wanachama kujitahidi kushiriki pasipo kukosa wakiwa na bidhaa zao za kutosha huku akiwaahidi kuwa pindi wajapo Tanzania watafurahia mambo mengi na kujionea namna Watanzania wanavyo chapa kazi kutokana na kaulimbiu ya ‘HAPA KAZI TU’ iliyoasisiwa na Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

“Kwakuwa mwaka 2019 ni mzunguko wa Tamasha kama hili niwaambie kwamba, Tanzania iko tayari kuwa mwenyeji wa Tamasha hili na nawakaribisheni kwa dhati kabisa mje kujionea nchi yetu na namna tunavyofanya kazi kwa bidii, lakini pia mje na bidhaa nyingi zaidi kwa ajili ya kuwaonyesha Watanzania”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Tamasha la JAMAFEST lilianzishwa mwaka 2013 nchini Rwanda na baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kwa mwaka huu tamasha hilo linafanyika mjini Kampala nchini Uganda ambapo kwa mwaka 2019 linatarajiwa kufanyika nchini Tanzania.

TANZANIA BREWERIE’S GLOBAL BE(ER) RESPONSIBLE DAY PROMOTES SMART DRINKING

$
0
0
*Tanzania Breweries Limited (TBL) and AB InBev celebrated its annual Global Be(er) Responsible Day on Friday, 15th September 2017.

This year’s theme “Drink Smart Today, Celebrate Tomorrow”, is focused on bringing awareness to issues of harmful drinking and promoting smart drinking within the business, amongst the company’s partners and its consumers.

“Harmful drinking concerns us, and we know that more needs to be done by us, our industry, peers, civil society and government to reduce the harm caused by the misuse of alcohol. As a global brewer, TBL Group is committed to playing its part and working with communities and the public sector in finding effective solutions to the problem,” says Georgia Mutagahywa, Corporate Affairs Director, East Africa.

TBL Group has implemented several initiatives in partnership with private and public-sector partners, to tackle the problem of harm cause by the misuse of alcohol. These initiatives are embedded within the organization’s Better World sustainable development strategy under the Healthier World pillar with the aspiration of a healthier world where every experience with beer is a positive one.

These initiatives form part of the organization’s Global Smart Drinking Goals which encapsulate its efforts to make a deeper investment in programmes that measurably shift social norms and behaviors toward smart drinking.

The initiatives include:

•We have an internal program (Alcohol, Behavior and Communication), that trains all our employees on responsible consumption

•Road Safety Initiative, where we work with the Tanzania Police Force to help enforce our responsibility and safety messages, as well as test drivers of long distance routes to make sure they are in good health drive.

•Responsible Consumption trainings; we annually train the police force, the press and teachers on the dangers of drinking and driving.

•We also train and talk about responsible consumption messages at all and any forum we are invited to.

•Boda Boda (Motorcycle) drivers on responsible consumption.

•Partnership with select retailers to place posters with our smart drinking goals message. At TBL Group, we believe that smart drinking choices affect everyone, every day. “We are committed to helping foster a global culture of smart drinking to reduce the harmful use of alcohol, said Ms. Mutagahywa”

During TBL Group’s Global Be(er) Responsible Day, employees will be encouraged to think about the responsible and safety messages as well as take responsibility and drink moderately in social settings.
One of Boda Boda (Motorcycle) drivers safety training sponsored by the company last year.
Some of retailers in one of the Responsible Consumption trainings held in Dar es Salaam.
TBL sponsored teachers training on Road Safety in Mwanza last year.

UFAFANUZI JUU YA TUHUMA ZA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA KOREA KASKAZINI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari wakati akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ushirikiano wa Tanzania na Korea ya Kaskazini mapema hii leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (katikati) akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ushirikiano wa Tanzania na Korea ya Kaskazini, kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Aziz Mlima na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara hiyo Bi. Mindi Kasiga.
Mwandishi wa Habari toka kituo cha Televisheni cha Channel Ten, David Ramadhan akimuuliza swali Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (aliye kaa katikati) wakati Waziri huyo akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu ushirikiano wa Tanzania na Korea ya Kaskazini.


Picha na Eliphace Marwa – Maelezo

RC MAKONDA APIGA MARUFUKU WAGONJWA KULALA CHINI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda amepokea Magodoro 1,000 yenye thamani ya Shillingi Million 100 kutoka Kiwanda cha utengenezaji wa Magodoro ya Dodoma Asili kwa kushirikiana na Wadau wanaopendezwa na kazi kubwa anayoifanya katika kutatua kero Wananchi.

Makonda amekabidhiwa Magodoro hayo Mjini Dodoma na Kiwanda hicho mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Jordan Rugimbana.

Akizungumza baada ya Makabidhiano hayo Makonda amepiga Marufuku kitendo cha Wagonjwa kulazwa Chini Hospitalini kwakuwa Magodoro hayo yanaenda kutatua kero hiyo.
 Amesema kuwa Magodoro aliyopatiwa atayakabidhi kwenye Hospital zote za Mkoa wa Dar es Salaam kwakuwa baadhi zimekuwa na upungufu wa Magodoro hali inayofanya Wagonjwa kulala juu ya Vyuma vya kitanda na wengine kutandika Kanga na Nguo kwenye Sakafu.
 Amesema idadi kubwa ya Wananchi wamekuwa wakitoka Mikoani kufuata huduma za Afya Dar es Salaam kutokana na Wingi wa Hospital za Kisasa za Umma na Binafsi hivyo kusababisha Hospital kuwa na Wagonjwa wengi.
Licha ya Changamoto hiyo Makonda amesema Sekta ya Afya jijini Dar es Salaam imeimarika kwa kiasi kikubwa ambapo lengo lake ni kuona Mkoa huo unakuwa kinara kwenye utoaji wa huduma Bora za Afya.

Ameshukuru Kiwanda hicho na Wadau waliomuunga Mkono na kuwasihi Wananchi kununua Magodoro ya Dodoma Asili yanayotengene
zwa na Kiwanda cha Wazawa ili kukuza Uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mheshimiwa Jordan Rugimbana amempongeza RC Makonda kwa kazi kubwa anayoifanya katika Sekta mbalimbali ikiwemo Maboresho ya Jeshi la Polis na kusema ataenda Dar es salaam kujifunza namna walivyofanikiwa kwenye Ulinzi na Usalama.

Nae Mkurugenzi wa Kiwanda cha Magodoro ya Dodoma Asili Bwana Haider Gulamali amesema wataendelea kutoa ushirikiano kwa RC Makonda kwakuwa kazi anayoifanya ni kubwa na inawagusa Wananchi wote hususani wanyonge.

Makamba: Kila Mtanzania Anajukumu la Kuhifadhi Tabaka la Ozoni

$
0
0
Na: Lilian Lundo,MAELEZO-Dodoma

Serikali imesema kila Mtanzania anajukumu la kuhifadhi Tabaka la Ozoni kwa kutotumia bidhaa zenye madhara kwa Tabaka hilo katika biashara na shughuli za kila siku za majumbani.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba kupitia taarifa aliyoitoa leo, kwa vyombo vya habari juu ya Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni inayofanyika kila mwaka, Septemba 16.

“Kwa kuzingatia kauli mbiu ya mwaka huu ni muhimu tuzingatie kwamba juhudi za kila mmoja wetu zinatakiwa ili kupunguza na kuondosha madhara katika Tabaka la Ozoni yanayosababishwa na bidhaa tunazonunua na kutumia majumbani au sehemu za biashara ,” amefafanua Makamba kupitia taarifa hiyo.
Makamba amesema kuwa kila mwananchi anatakiwa kuepuka kuingiza nchini gesi zilizopigwa marufuku na vifaa vinavyotumia gesi haribifu kama vile majokofu na viyoyozi vilivyokwisha tumika (mitumba) na ambavyo vinatumia vipoozi aina ya Chlorofluorocarbons (R11 na R12).
Vile vile amewataka Watanzania kununua bidhaa zilizowekwa nembo rasmi isemayo “Ozone friendly” ikiashiria haina wala haikutengenezwa na kemikali zinazomong’onyoa Tabata la Ozoni.
Aidha amewaasa Watanzania kuepuka kutupa hovyo majokofu ya zamani ama vifaa vya kuzima moto vyenye kemikali zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni aina ya ” CFCs” na “halon”. Ila wanapotaka kutupa wanatakiwa kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa mafundi ama mamlaka zinazohusika.
Pia mafundi wa majokofu na viyoyozi wametakiwa kuhakikisha kuwa wananasa na kutumia tena vipoozi kutoka kwenye viyoyozi na majokofu wanayohudumia badala ya kuviacha huru visambae angani.Mafundi hao wanatakiwa kutoa elimu kwa wateja wao kuhusu njia rahisi ya kutambua uvujaji wa vipoozi kutoka katika majokofu na viyoyozi wavyotumia.
Kitaifa, maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni yatafanyika kwa njia ya uelimishaji Umma kuhusu Tabaka la Ozoni, faida zake, madhara ya kuharibika kwa Tabaka hilo na matumizi salama ya bidhaa zenye kemikali rafiki kwa Tabaka hilo.

Kauli mbiu ya mwaka huu katika kuadhimisha siku hiyo ni “Kutunza na Kulinda Viumbe Hai Duniani” ( Caring for All Life Under the Sun).

DKT. ASHATU KIJAJI AZINDUA KITABU CHA MWONGOZO KWA WANAMIPANGO

$
0
0
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (aliyeshika mkasi) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners handbook), Toleo la Pili, kilichoandikwa na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kwa kushirikiana na Taasisi ya Mafunzo ya Jamii ya nchini Uholanzi (ISS), tukio hilo limefanyika katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kampasi ya Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), (katikati), akionesha kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili,  baada ya kukizindua rasmi katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini-Dodoma. Wa pili kushoto ni Kaimu Balozi wa Uholanzi hapa nchini, Bi. Lianne Houben, na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo hicho Prof. Razack Lokina.
 Kaimu Balozi wa Uholanzi hapa Nchini, Bi. Lianne Hauben (kushoto), akifurahi wakati akikabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), nakala ya Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, mara baada ya kukizindua rasmi mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akimkabidhi Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Prof. Razack Lokina, nakala ya Kitabu cha Mwongozo kwa wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, mara baada ya kukizindua rasmi mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Prof. Hozen Mayaya, nakala ya Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, mara baada ya kukizindua rasmi mkoani Dodoma.
  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kituo cha Kanda ya Ziwa, Dkt. Benedict Kilobe, nakala ya Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, mara baada ya kukizindua rasmi mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akimkabidhi Makamu Mkuu wa Chuo-Mipango, Fedha na Utawala, Dkt. Vedastus Timothy, nakala ya Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners handbook), Toleo la Pili, kilichozinduliwa katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, mkoani Dodoma.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akiwaongoza wadau mbalimbali kunyanyua nakala ya kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners handbook), Toleo la Pili, kilichoandikwa na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kwa kushirikiana na Taasisi ya Mafunzo ya Jamii ya nchini Uholanzi (ISS), tukio hilo limefanyika katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini, Kampasi ya Dodoma.
 Mhadhiri Mstaafu wa Taasisi ya Kimataifa inayotoa elimu ya masuala ya kijamii (The International Institute of Social Studies (ISS), kutoka nchini Uholanzi, Prof. Leo de Haan, akitoa mhadhara kuhusu masuala ya umuhimu wa mipango katika jamii kabla ya kuzinduliwa rasmi kwa Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, tukio lililofanyika katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini-Dodoma.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) (katikati-walioketi), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi wa viongozi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini pamoja na wahadhiri kutoka Taasisi ya Elimu ya masuala ya Jamii (ISS) ya nchini Uholanzi, baada ya uzinduzi wa Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango (Planners Handbook), Toleo la Pili, tukio lililofanyika katika Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini-Dodoma.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)

Benny Mwaipaja, Dodoma
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, amezindua Kitabu cha Mwongozo kwa Wanamipango Tanzania, kilichoandaliwa na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kwa kushirikiana na Taasisi ya Mafunzo ya Jamii ya nchini Uholanzi (ISS), na kuwataka wataalamu wa mipango hapa nchini kuandaa mipango yenye tija itakayoiwezesha jamii kuondokana na umasikini.

Dkt. Kijaji ameeleza kuwa nafasi ya wataalamu wa mipango katika kukuza uchumi wa nchi ni kubwa na kwamba kinachotakiwa ni kuandaa mipango shirikishi itakayochangia kuimarisha maisha ya wananchi ili waweze kujikwamua kiuchumi.

“Ni matumaini yangu makubwa kwamba kuzinduliwa kwa kitabu hiki cha mwongozo kwa wanamipango, kutakuwa chachu ya wataalamu wetu kuangalia namna ya kupeleka maendeleo vijijini na sehemu nyingine duniani kwa kutoa wataalamu waliobobea ili kuharakisha maendeleo ya nchi” alisistiza Dkt. Kijaji

Ameeleza kuwa maudhui ya kitabu hicho yapelekwe hadi ngazi za chini kupitia Serikali za Mitaa ili watu wengi waweze kukisoma na kuelekezwa namna bora ya kupanga mipango yao ya maendeleo.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijini, Prof. Hozen Mayaya, amesema kitabu hicho kimelenga kuwaongezea ujuzi wataalamu wa mipango kwa kuzingatia vitendo zaidi badala ya nadharia.

“Kitabu cha Mwongozo kwa wanamipango kitakuwa rejea ya nadharia nyingi na njia ambazo wataalamu wanapaswa kuzijua, namna ya kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuifanya mipango iweze kutekelezeka kama ilivyokusudiwa” alisema Prof. Mayaya.

Nae Kaimu Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Bi. Lianne Houben, ambaye kwa namna moja au nyingine nchi yake imefadhili uandishi na uchapaji wa mwongozo huo, toleo la pili, amesema nchi yake inajivunia uhusiano imara uliodumu kwa miongo kadhaa na Tanzania.

Alisema kuwa mtazamo wa ushirikiano wake na Tanzania kuanzia mwaka huu ni kujikita zaidi katika uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na kwamba uwekezaji wao mkubwa utalenga pia kuboresha kilimo na usalama wa chakula.

“Uholanzi ni nchi ya pili katika kufanya biashara na Tanzania ikitanguliwa na Marekani ambapo mwaka 2016, Uholanzi, imenunua bidhaa zenye thamani ya Euro bilioni 85” aliongeza Bi. Houben

Aidha, alieleza kuwa nchi yake imetoa mchango mkubwa katika kuendeleza rasilimali watu ambapo hadi sasa wanafunzi na wataalaamu katika fani mbalimbali wapatao 5,000, wamepata mafunzo kutoka katika vyuo mbalimbali nchini Uholanzi.

SERIKALI YA KARABATI VITUO VYA AFYA KWA FEDHA KUTOKA BENKI YA DUNIA.

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Seleman Jafo (Mb).

Na. Atley Kuni- TAMISEMI
SERIKALI imepanga kukarabati vituo vya afya 172 kutokana na fedha kutoka Benki ya Dunia na Ubalozi wa Canada ambapo wametoa jumla ya Dolla za Kimarekani Mil 88 sambamba na Bil.12 fedha za kitanzania zilizovuka katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Seleman Jafo (Mb) amesema lengo la serikali nikuhakikisha ifikapo Desemba 30, 2017 shughuli hiyo iwe imekamilika ipasavyo kwa kusimamiwa karibu na Waheshimwa Wakuu wa mikoa wakisaidiana na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya.

Jafo amesema kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Serikali imepokea Dolla za kimarekani  Mil. 66 kutoka Benki ya Dunia ambapo vituo 103 vitakarabatiwa aidha pia Serikali  kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI, imepata Msaada kutoka Ubalozi wa Canada wa dolla za kimarekani Mil 22, ambapo vituo 44 vya afya vitakarabatiwa kwa fedha hizo. 

Naibu waziri huyo alisema,  fedha zingine zitakazo tumika katika zoezi hilo ni zile zilizo vuka katika mwaka wa fedha uliopita.

“Vituo 25 vitafanyiwa ukarabati kupitia fedha za Benki ya Dunia na mfuko wa afya wa pamoja zilizovuka mwaka wa 2016/2017, ambapo Bil.12 za kitanzania zitatumika,” alisema Jafo na kuongeza  kwamba kila  “kituo kitapatiwa shilingi Mil. 500 za kitanzania na baada ya ukarabati serikali itakuwa na jukumu lakupeka vifaa katika maeneo hayo”.

Waziri Jafo amesema, Maeneo ya kipaumbele wakati wa ukarabati huo ni pamoja na  Upasuaji (Theater), Wodi za mama na Mtoto (Martenity), Maabara(Laboratory), pamja na Nyumba za watumishi sambamba na maeneo mengine ya kipaumbele kutokana na fedha zilizopo.

Katika hatua nyingine Jafo amewagiza Makatibu Tawala wa mikoa kuwasilisha Taarifa ya kila mwezi ofisini kwake juu ya maendeleo ya ukarabati, huku akiwataka Wakurugenzi na watendaji wengine kusimamia kwa ufasaha zoezi hilo. 

Naibu Waziri hakusita kuonya juu wale wote watakao kwenda kinyume na maagizo na maelekezo ya serikali yaliyotolewa  
“Nawaomba Wah. Wabunge na Madiwani kushirikiana bega kwa bega na watendaji katika kufanikisha zoezi hili kwa ufanisi, alisema Jafo na kuongeza kwamba,  “ofisi yangu haita mvumilia Kiongozi au Mtendaji yeyote atakaye onekana kutumia fedha hizo vibaya au kushindwa kutimiza wajibu wake na kisha kukwamisha shughuli hii muhimu yenye nia njema kwa maisha ya watanzania.

Akihitimisha maagizo hayo  Naibu waziri Suleima Jafo, amezishukuru  Wizara zote za kisekta katika kusukuma gurudumu la maendeleo  na kwenda sambamba na kasi ya Rais  Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ya HAPA KAZI TU,  ikiwapo, Wizara ya Afya, Fedha na Mipango pamoja na watendaji wa Ofisi yake ambao walikuwa bega kwa bega katika mchakato wote wa kupatikana kwa fedha.

RC SHIGELA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA UMOJA WA KLABU ZA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA -UTPC MKOANI TANGA

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela leo Ijumaa Septemba 15,2017 amefungua mkutano Mkuu wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (Union of Tanzania Press Clubs- UTPC) mwaka 2017. 

Mkutano huo uliokutanisha viongozi wa Klabu za Waandishi wa Habari kutoka mikoa 27 nchini unafanyika katika ukumbi wa Tanga Beach Resort mkoani Tanga. 

Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo ambao utafanyika kwa muda wa siku mbili (Septemba 15 na 16,2017),Shigela alisema serikali inatambua umuhimu wa vyombo vya habari katika maendeleo ya jamii. 

“Ukitaka maendeleo katika jamii lazima ushirikiane na vyombo vya habari,na hata tunapoelekea katika Tanzania ya viwanda ni vyema vyombo vya habari vihusike”,alieleza. 

Alitumia fursa hiyo kuwataka waandishi wa habari nchini kuzingatia maadili katika kazi yao ya uandishi wa habari huku akiwaasa kujiendeleza kielimu ili kufanya vizuri zaidi katika kazi yao. 

“Vyombo vya habari vinafundisha,vinaelimisha,vinahamasisha ,vinakosoa na kufichua maovu na ili kutimiza haya ni vyema mkazingatia maadili yenu,mfanye kazi kwa usawa bila upendeleo lakini pia ni vyema mkawa wazalendo”,aliongeza. 

Kwa Upande wake rais wa UTPC,Deogratius Nsokolo alisema miongoni mwa changamoto zinazoikabili tasnia ya habari ni uwepo wa sera na sheria zinazobinya uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo sheria ya Habari ya habari ambayo baadhi ya vifungu vyake siyo rafiki kwa waandishi wa habari. 

“Tunaiomba serikali ifanye marekebisho katika baadhi ya vifungu kwenye sheria hii ambavyo siyo rafiki kwa vyombo vya habari”,aliongeza Nsokolo. 

Awali akizungumza katika mkutano huo,Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC,Abubakar Karsan alisema mkutano huo umekutanisha pamoja wadau mbalimbali wa habari nchini na viongozi wa klabu za waandishi wa habari kutoka mikoa 27 ya Tanzania bara na Zanzibar ukifadhiliwa na SIDA. 

Alisema katika mkutano huo wajumbe wanoshiriki watafanya majadiliano mbalimbali kuhusu masuala mbalimbali yanayowahusu waandishi wa habari. Habari na Kadama Malunde- Malunde1 blog,Picha zote na Oscar Assenga- Tanga Raha Blog 
Mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigela akifungua mkutano mkuu wa UTPC
Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC,Abubakar Karsan akizungumza wakati wa mkutano huo
Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilakwa akizungumza ukumbini
Rais wa UTPC,Deogratius Nsokolo akitoa hotuba
Makamu wa Rais wa UTPC,Jane Mihanji akizungumza ukumbini

Mkutano wa 37 wa AGMC wafanyika jijini Dar es Salaam

$
0
0
 Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe akihutubia wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Kituo cha Madini na Kijiosayansi cha Afrika (AMGC) jijini Dar es Salaam baada ya Kituo hicho kutimiza miaka 40 tangu kuanzishwa kwake. 
 Mwakilishi Mkazi wa Masuala ya Uchumi kutoka Ubalozi wa China, Lin Zhiyong mmoja wa wafadhili wa AMGC akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Kituo, Ibrahim Shaddad kwa ushirikiano mwema uliopo kati yao.
 Balozi wa Msumbiji Nchini Tanzania, Monica Patricio Clemente akichangia hoja katika Mkutano wa Baraza la Uongozi wa AMGC jijini Dar es salaam.
Wajumbe mbalimbali wa Mkutano wa Baraza la Uongozi wa AMGC wakiwa katika kikao cha 37 nchini Tanzania.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILISHA HOTUBA YA KUAHIRISHA BUNGE

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasilisha hotuba ya kuahirisha Bunge mjini Dodoma Septemba 15, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipongezwa na Wabunge baada ya kuwasilisha hotuba ya kuahirisha Bunge mjini Dodoma Septemba 15, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiteta na Spika wa Bunge, Job Ndugai kwenye ukumbi wa Spika baada ya kuwasilisha hotuba ya kuahirisha Bunge mjini Dodoma Septemba 15, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

PICHA ZA MATUKIO YA OFISI YA WAZIRI MKUU BUNGENI.

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde akisalimiana na baadhi ya walimu wa Shule ya Sekondari ya Jamhuri walipotembelea Bungeni Septemba, 2017 Mjini Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde (wa tatu kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu wa Shule ya Sekondari ya Jamhuri waliotembelea Bungeni Septemba, 2017 Mjini Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Vijana), Mhe. Antony Mavunde akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jamhuri waliotembelea Bungeni tarehe 13 Septemba, 2017 Mjini Dodoma. (PICHA NA OFISI OFISI YA WAZIRI MKUU - DODOMA)
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images