TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UZINDUZI WA AWAMU YA PILI YA MRADI WA KULIJENGEA UWEZO BUNGE
↧
↧
Msisubiri Muda wa Kuchukua Leseni Kuisha - Dkt. Abbasi
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akielezea jambo wakati wa zoezi la kukabidhi Leseni za machapisho kwa Kampuni ya The Guardian Ltd leo Jijini Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula na kulia ni Mhariri Mkuu wa The Guardian Ltd Jesse Kwayu. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi Leseni za machapisho Mhariri Mkuu wa Kampuni ya The Guardian Ltd Jesse Kwayu (kulia) ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e).Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi Leseni za machapisho Meneja wa Sheria na Uhusiano wa Kampuni ya The Guardian Ltd Bw. Emmanuel Matondo(kulia) ikiwa ni muendelezo wa utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016 kifungu kidogo namba 5(e). Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi anayeshugulikia Usajili Patrick Kipangula. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi na Meneja wa Sheria na Uhusiano wa Kampuni ya The Guardian Ltd Bw. Emmanuel Matondo (kulia) wakionyesha Leseni ya machapisho aliyotolewa kwaa ajili ya gazeti la Nipashe mara baada ya kukabidhiwa leo Jijini Dar es Salaam.Utoaji wa Leseni unafuatia muitikio wa wamiliki wa machapisho kuzingatia matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 kifunga namba 5(e). Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
Mhariri Mkuu wa Kampuni ya The Guardian Ltd Bw. Jesse Kwayu na Meneja Sheria na Uhusiano wa kampuni hiyo Bw. Emmanuel Matondo wakiwa wameshika Leseni 10 za machapisho yanayomilikiwa na The Guarid baada ya kukabidhi wa Leseni kumi za machapisho yanayomilikiwa na Kampuni hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Kampuni hiyo inamiliki magazeti ya Nipashe, Nipashe Jumapili, Sema Usikike,The Guardian, The Guardian On Sunday, Kulikoni, Lete Raha, This Day, Alasiri na Taifa Letu.
Picha na: Idara ya Habari - MAELEZO
↧
BancABC yazindua akaunti mpya ya Hundi ya Jiongeze .
Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa akaunti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato yeyote ya mwisho wa mwezi. Kushoto ni Meneja Masoko wa benki hiyo Upendo Nkini.
Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa BancABC,Joyce Malai (kulia) na Meneja Masoko wa benki hiyo, Upendo Nkini, wakionyesha bango la uzinduzi wa akauti mpya ya Hundi ya Jiongeze isiyo na makato ya mwisho wa mwezi wakati wa hafla ya kuzindua akaunti hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Lengo ni kufikia Watanzania wengi na waweze kuwa na kaunti za hundi kwa bei nafuu.
Dar es Salaam Tanzania, BancABC imeendelea kuwa Benki inayojiogeza hapa nchini kwa kua wabunifu wa hali ya juu kwenye utoaji huduma zao pamoja na kuboresha huduma hizo za kibenki ili kuwawezesha wateja kupata huduma za kwa urahisi na hivyo kuwa suluhisho kwenye sekta ya fedha.
Dar es Salaam Tanzania, BancABC imeendelea kuwa Benki inayojiogeza hapa nchini kwa kua wabunifu wa hali ya juu kwenye utoaji huduma zao pamoja na kuboresha huduma hizo za kibenki ili kuwawezesha wateja kupata huduma za kwa urahisi na hivyo kuwa suluhisho kwenye sekta ya fedha.
Katika kuendelea kudhihirisha ubunifu wa bidhaa zao, BancABC leo imezindua akaunti mpya inayoitwa Jiongeze Hundi akaunti kwa lengo la kupunguza makato ya huduma za uendeshaji akaunti ya mwezi kwa mwezi kwa wateja wote watakaofungua Akaunti ya Jiongeze na Benki hiyo hapa nchini.
Akaunti ya Jiongeze inamfanya mteja aweze kuendesha akaunti ya kibiashara au ya mshahara mara nyingi bila makato ya mwisho wa mwezi kwa muda wa mwaka mmoja na hivyo kufanya wateja wa BancABC kuweza kufanya miamala mingi ya kibenki kwa Uhuru na urahisi zaidi.
Faida zingine wateja wa Jiongeze akaunti watafurahia ni pamoja na kuangalia salio sehemu yeyote kupitai simu yako ya mkononi, kuweka na kutoa fedha kupitia kwa zaidi ya mawakala 50 ambao wanapatikana sehemu mbali mbali za Dar es Salaam, kupitia mtandaoni na ATM mbali mbali zenye nembo ya visa na pia kupitia applikesheni ya BancABC aliogeza Mrs. Joyce Malai ambaye ni Meneja wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Biashara wa Benki hiyo.
Ikiwa ni benki iliyoshinda tuzo ya kuwa Benki inayokua kwa haraka kwa mwaka 2017, BancABC tunaendelea kuonyesha dhamira yetu ya dhati ya kujiimarisha zaidi kwa kuendelea kuzindua huduma bora na za kibunifu zinazopatikana kwa urahisi na kuendele kufikia Watanzania wengi ambao hawajafikiwa na huduma za kibenki, aliongeza Mrs. Malai.
"Ubunifu na huduma zetu ndio unafanya BancABC kuwa tofauti kwa hapa Tanzania. Tumeekeleza nguvu katika kukuza na kuongeza matawi yetu ya kibenki ili kila Mtanzania aweze kufikiwa na huduma za kibenki, alisema Mkuu wa Masoko BancABC Mrs. Upendo Nkini huku akitoa wito kwa Watanzania kujitokeza na kutumia hii fursa ya kufungua na kuendesha akaunti ya Jiongeze kwa mwaka mmoja bila makato yeyote ya mwezi.
Aliongeza kuwa BancABC inawakaribisha wafanya biashara na wajasiriamali, kufungua akaunti ya Hundi ya Jiongeze kwakua huduma hiyo itadumu kwa miezi miwili TU.
Benki ya ABC ambayo ni moja ya kampuni tanzu za Atlas Mara, ilishinda tuzo ya kuwa Benki bora inayokuwa hapa nchini Tanzania kwa mwaka 2017 na inatarajia kuzidi kukua hapa nchini kwa kufungua matawi mawili katika mkoa wa Dodoma na Mwanza ndani ya mwaka huu
↧
SPIKA JOB NDUGAI ATEMBELEWA NA BALOZI WA UINGEREZA NCHINI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. katikati ni Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (katikati) na Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy, pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (katikati) na kulia ni Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy, pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akiagana na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. katikati ni Mwakilishi Mkazi wa DFID hapa nchini, Ndg. Beth Arthy
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka ubalozi wa Uingereza uliomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma. ulioongozwa na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (watatu kulia).
Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) akimsikiliza Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (kushoto) pale ugeni kutoka ubalozi huo ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na ugeni kutoka Ubalozi wa Uingereza ulioongozwa na Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke (katikati) ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE)
↧
TRA YAONGEZA UFANISI WA UKUSANYAJI KODI YA MAJENGO
Serikali imeeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 Mamlaka ya Mapato Nchini, (TRA) imekusanya Kodi ya Majengo kwa ufanisi zaidi ikilinganishwa na kipindi ambacho kodi hiyo ilikuwa ikikusanywa na Halmashauri.
Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri waFedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Cecilia Paresso(CHADEMA), aliyetaka kujua baada ya TRA kupewa jukumu la kukusanya kodi za majengo basala ya Halshauri za Miji, Manispaa na Majiji, ufanisi wake umefikiwa kiasi gani ikilinganishwa na mapato yaliyokuwa yakikusanywa na Halmashauri zenyewe.
Katika swali hilo Mhe. Paresso alisema kuwa kodi hiyo ilikuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri hizo yaliyokuwa yakitumika katika kutekeleza majukumu ya kutoa huduma kwa wananchi.
“Baada ya TRA kupewa jukumu la kukusanya kodi ya majengo majukumu ya Halmashauri hizo hayajapungua, je Serikali imejipanga vipi kufidia vyanzo hivyo?,” alihoji.Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema ufanisi wa TRA katika kukusanya kodi ya majengo umeongezeka kwa asilimia 20.6 kutoka Sh. bilioni 28.28 mwaka 2015/16 hadi Sh. Bil 34.09 mwaka 2016/17.
Dkt. Kijaji alifafanua kuwa Serikali inatambua kuwa kodi ya majengo imekua ikichangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri husika katika kutekeleza mipango ya utoaji huduma za jamii na imeweka utaratibu wa kibajeti ambao unaziwezesha Halmashauri hizo kupata fedha za makusanyo ya kodi ya majengi iliyokusanywa na TRA ili kuziwezesha kutimiza majukumu yao.
“Utaratibu uliopo ni kwamba, Halmashauri zinatakiwa kuomba fedha hizo kutoka Serikali Kuu kwa kuzingatia makisio ya bajeti zao, kwa mantiki hiyo Halmashauri zinashauriwa kuzingatia utaratibu huo ili ziweze kupata fedha hizo,”alisema Dkt. Kijaji.
Alisisitiza kuwa hatua ya Serikali kuhamisha jukumu hilo la kukusanya kodi TRA halikulenga kuzinyang’anya Halmashauri vyanzo vya mapato bali ni kuimarisha ukusanyaji wake kwani takwimu zilizoainishwa hapo juu zinadhihirisha kuwa TRA imefanya vyema katika kukusanya mapato hayo ikilinganishwa na Halmashauri.
Imetolewa na:
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango
↧
↧
Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja ya Mkutano wa MakatibU Wakuu kutoka Nchi Wanachama wa Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine katika picha ni wawakilishi kutoka Nchi wanachama pamoja Makamishna na Wakuu wa Vituo vya Madini.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati) baada ya kufugua kikao cha Makatibu Wakuu kutoka Nchi Wanachama wakiwa katika Kituo cha Afrika Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine ni Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (kushoto) na Assa Mwakilembe (kulia).
Baadhi ya wawakilishi wa Bodi ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC), wa kwanza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa UNECA, Dkt. Koja Busia, Mwenyekiti wa Bodi, Masresha Gebreselassie, Mwenyekiti wa AUC, Frank Mugyenyi na Mkurugenzi Mkuu wa AMGC, Ibrahim Shaddad.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (anayeongea). Wengine ni washiriki katika kikao hicho.
Mshauri Mwelekezi wa AMGC, Timo Gawronski akitoa maelezo kwa washiriki wa kikao wakiwa katika maabara ya uchunguzi wa asili ya madini husika.
…………………..
Tanzania imekuwa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Masuala ya Kisera ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (African Minerals and Geosciences Center (AMGC) ambao unafanyika jijin Dar es Salaam.
Awali, mkutano huo ulianza kwa kuwakutanisha Wakurugenzi wa Bodi ya kituo hicho na kufuatiwa na mkutano wa tarehe 13 Agosti, 2017, uliowashirikisha Makatibu Wakuu kutoka nchi Wanachama wa kituo husika.
Akizungumza na Vyombo vya Habari wakati wa Mkutano wa Makatibu Wakuu, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe alisema lengo la kukutana ni kufanya tathmini na kuendeleza yale yaliyopangwa kutekelezwa na nchi wanachama ikiwemo kupanga mipango ya mwaka ujao na bajeti ya utekelezaji wa mipango hiyo.
Profesa Mdoe alisema kuwa yapo mambo ambayo waliyokubaliana katika mkutano wa 36 yakiwemo ujenzi ya Maabara ya kisasa kwa ajili ya nchi za Maziwa Makuu ambayo itasaidia katika shughuli za madini ikiwemo za uchunguzi wa madini, kukiwezesha kituo hicho kufanya shughuli zake vizuri na kusaidia nchi wanachama katika sekta husika.
Akizungumzia manufaa ya kituo hicho nchini, alisema kuwa kituo hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwa Tanzania hususan Taasisi za Vyuo Vikuu nchini ambazo zimekuwa zikikitumia Kituo hicho katika mafunzo mbalimbali.
“Sisi tumepata bahati kubwa ya kuwepo kwa kituo hiki hapa nchini. Tayari vipo Vyuo na wanafunzi ambao wamenufaika na uwepo wa kituo hiki. Kwetu sisi ni faida kwa sababu hatutumii gharama kubwa za kufuata huduma zinazotolewa na kituo hiki tofauti na nchi nyingine ambazo zipo mbali,” alisema Prof. Mdoe.
Aidha, alisema faida nyingine kwa nchi wanachama waliolipa ada kamili ni kupata punguzo la asilimia 40 la kutumia maabara za Kituo hicho.Akizungumzia malengo ya baadaye ya kituo hicho, alieleza kuwa ni kukifanya kuwa kituo bora zaidi ikiwemo kuongeza idadi ya wanachama kutoka nchi nane zilizopo sasa.
Hadi sasa nchi wanachama ni Tanzania, Msumbiji, Sudani Kaskazini, Ethiopia, Uganda, Kenya, Comoro na Angola.Sambamba na mkutano huo, itafanyika pia sherehe ya kuadhimisha miaka 40 ya kituo husika tangu kuanzishwa kwake.
↧
Serikali Imeanza Kujenga Mitambo ya FM Kuimarisha Usikivu Redio ya Taifa
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa Innocent Sebba Bilakwate leo Bugeni Mjini Dodoma lililohoji ni lini Serikali itawapatia Wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio TBC ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari badala ya sasa kusikiliza Redio Rwanda na Uganda.Picha na Frank Mvungi, MAELEZO, Dodoma
Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma
Serikali imeanza kutekeleza Mpango wa kujenga mitambo ya FM nchini kuimarisha usikivu maeneo mbalimbali ili wananchi waweze kupata matangazo kutoka redio yao ya Taifa (TBC).
Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kyerwa Innocent Sebba Bilakwate kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe, lililohoji ni lini Serikali itawapatia Wananchi wa Kyerwa haki yao ya kusikiliza Redio TBC ili kujua yanayoendelea katika nchi yao kama ilivyokuwa hapo awali kabla ya kubadilisha teknolojia ya habari badala ya sasa kusikiliza Redio Rwanda na Uganda.
Mpango huo unatekelezwa na Serikali kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ambao umeanza kutekelezwa katika wilaya za Kibondo, Nyasa, Longido, Tarime pamoja na Rombo na utaendelea katika wilaya nyingine ikiwemo Kyerwa kadiri bajeti inavyoendelea kuimarika.
“Kwa sasa kama ilivyobainishwa katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya mwaka 2017/2018, Serikali inaendelea kubadilisha mfumo wa urushaji matangazo kupitia satelaiti uweze kuwa wa kisasa ili kuboresha usikivu wa radio ya Taifa TBC hatua itakayosaidia wananchi kuendelea kupata habari kupitia viongozi wao” amesema Naibu Waziri Wambura.
Naibu Waziri Wambura amebainisha kuwa zipo wilaya 84 nchini ambazo usikivu wa TBC umeshuka na kusababisha baadhi ya maeneo kukosa matangazo ya redio kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa baadhi ya miundombinu ya radio, uwepo wa milima na uharibifu wa vifaa kutokana na radi wakati wa mvua.
Aidha, Naibu Waziri Wambura amewataka Wabunge na wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa endapo kutatokea uharibifu wa vifaa vya kusaidia upatikanaji na usikivu wa matangazo ya radio ya taifa TBC katika maeneo yao ili yaweze kufanyiwa marekebisho mapema na wananchi waendelee kupata habari mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa.
Wilaya ya Kyerwa iko katika Mkoa wa Kagera ambapo matangazo ya Redio yanapatikana kupitia mtambo wa TBC ulioko katika Manispaa ya Bukoba ambao unasafirisha mawimbi ya Redio katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.
↧
SEND OFF YA MKE MTARAJIWA WA CUTHBERT MIDALA,CATHERINE ILIVYOFANA DAR ES SALAAM, JANA
↧
TANZANIA IPO SALAMA NA IMARA -WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Septemba 13, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Bw. Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.
“Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote kutoka popote atakayejaribu kuvuruga amani yetu. Nawaomba wananchi muwe makini na muendelee kuidumisha amani yetu.”Amesema kwa sasa Serikali ipo katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi, rushwa, biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na wahujumu uchumi.
Waziri Mkuu amesema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, wameendelea kuwahamasisha wananchi wake kudumisha mshikamano.Amesema mbali ya kuimarisha amani nchini, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.
Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.Pia amewakaribisha raia wa Iran kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.
Kwa upande wake, Balozi Farhang ameipongeza Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi na kupambana na dawa za kulevya na ufisadi.Balozi huyo amesema Serikali ya Irani ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na vitendo vingine vya kihalifu.
Balozi Farhang ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Tanzania ifungue Ofisi ya Ubalozi nchini Iran ili kuimarisha uhusiano huo, ambapo Waziri Mkuu amekubali.Pia Bw. Farhang amesema aliwahi kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro na kusema kwamba ni maeneo mazuri ambayo hajawahi kuyaona tangu azaliwe.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, SEPTEMBA 13, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Balozi wa Iran. Mousa Farhang nakufanya mazungumzo ya kikazi leo Septemba 13/2017.Ofisini kwake Magogoni Dar es salaam. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ipo salama na imara na kwamba mtu yeyote atakayejaribu kutaka kuvuruga amani atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Septemba 13, 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Bw. Mousa Farhang jijini Dar es Salaam.
“Hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote kutoka popote atakayejaribu kuvuruga amani yetu. Nawaomba wananchi muwe makini na muendelee kuidumisha amani yetu.”Amesema kwa sasa Serikali ipo katika mapambano dhidi ya vitendo vya ufisadi, rushwa, biashara haramu ya dawa za kulevya pamoja na wahujumu uchumi.
Waziri Mkuu amesema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu wa kisiasa, wameendelea kuwahamasisha wananchi wake kudumisha mshikamano.Amesema mbali ya kuimarisha amani nchini, pia Serikali imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.
Hivyo ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchini Iran ili waje kuwekeza kwenye viwanda mbalimbali vikiwemo vya kuchakata mazao ya kilimo.Pia amewakaribisha raia wa Iran kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko nchini Tanzania kama mlima wa Kilimanjaro, fukwe, mali kale na mbuga za wanyama.
Kwa upande wake, Balozi Farhang ameipongeza Serikali kwa kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi na kupambana na dawa za kulevya na ufisadi.Balozi huyo amesema Serikali ya Irani ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, ufisadi pamoja na vitendo vingine vya kihalifu.
Balozi Farhang ametumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Tanzania ifungue Ofisi ya Ubalozi nchini Iran ili kuimarisha uhusiano huo, ambapo Waziri Mkuu amekubali.Pia Bw. Farhang amesema aliwahi kutembelea mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro na kusema kwamba ni maeneo mazuri ambayo hajawahi kuyaona tangu azaliwe.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, SEPTEMBA 13, 2017.
↧
↧
VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 14, 2017
↧
DKT.MWAKYEMBE AMEWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TANZANIA KWA KUSHIRIKI TAMASHA LA JAMAFEST KAMPALA, UGANDA
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akiangalia ngoma ya kiutamaduni iliyokuwa ikipigwa na Kikundi cha Sanaa na Utamaduni Tanzania (TaSUBA) katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza mjasiriamali wa Tanzania kuhusu baadhi ya bidhaa zilizopo katika banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akipokea zawadi ya shati toka kwa mjasiriamali wa Tanzania mara alipotembelea banda lao wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Utamaduni, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (mwenye tai nyekundu) akiangalia moja ya ubunifu wa picha iliyochongwa na mjasiriamali wa Tanzania wakati wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) linalofanyika mjini Kampala, Uganda 13 Septemba, 2017.PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewapongeza Wajasiriamali wa Tanzania kwa ushiriki wao katika Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST.
Dkt. Mwakyembe ametoa pongezi hizo leo mjini Kampala nchini Uganda katika viwanja vya Mashujaa Kololo alipotembelea kujionea namna tamasha hilo lilivyopokelewa na wadau wake walioiwakilisha Tanzania wakiwemo wajasiriamali toka vikundi mbalimbali, vikundi vya ngoma, vikundi vya sanaa ya maigizo pamoja na baadhi ya wasanii.
Katika tamasha hilo, Dkt. Mwakyembe pia alipata fursa ya kutembelea baadhi ya mabanda ya wajasiriamali hao pamoja na kuongea nao huku akijionea bidhaa mbalimbali zinazouzwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki jambo ambalo limemfurahisha sana hususani kwa upande wa watu kutoka Tanzania kwakuwa wamejaza mabanda yao kwa bidhaa kadha wa kadha.
“Tamasha hili linaonyesha utajiri mkubwa wa sanaa, utamaduni pamoja na bidhaa tulizonazo kama nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, na hapa tumekutana kwasababu tunabadilishana mawazo na kuonyeshana bidhaa mbalimbali za nchi zetu”, alisema Dkt. Mwakyembe.
Aidha, katika ziara hiyo, Dkt. Mwakyembe amewatoa wasiwasi wajasiriamali hao kuhusu suala la upatikanaji wa masoko huku akiwaahidi kuwatafutia fursa ya kuwapeleka wajasiriamali hao pamoja na bidhaa zao Bungeni mjini Dodoma ili ziweze kupata soko kwa urahisi kupitia wabunge.
“Niwatoe wasiwasi wajasiriamali wote wa Tanzania mliohudhuria hapa, nitahakikisha kuwa pindi tunaporudi nyumbani nitatafuta wasaa wa kulishawishi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili nyie mpate nafasi ya kuleta bidhaa zenu katika viwanja vya Bunge ili basi Wabunge wapate kujua haswa vitu vizuri mlivyonavyo nah ii itawasaidia kuviuza kwa urahisi zaidi na kujipatia vipato vyenu”, aliongeza Dkt. Mwakyembe.
Sambamba na hilo, Dkt, Mwakyembe amewahakikishia wajasiriamali hao kuhusu suala la kujitangaza kupitia vyombo vya habari akisema kwamba, atajitahidi kutoa ushawishi kwa vyombo vya habari nchini ili viweze kuwapatia muda wa kuwatangaza wajasiriamali hao ili wapate kujulikana ikiwemo shughuli wazifanyazo.
“Nitahakikisha kuwa siku mnapopewa nafasi ya kuja viwanja vya Bunge basi mnapata muda wa kutosha katika vyombo vya habari ili mpate kujulikana, hivyo kila mmoja wenu naamini atapewa nafasi ya kufanya mahojiano kwa kujieleza shughuli azifanyazo na mahali anapopatikana na hii itawasaidia kupata masoko zaidi toka kwa watu mbalimbali”, alisema Dkt. Mwakyembe.
Kwa upande wao wajasiriamali hao wameshukuru Waziri Mwakyembe kwa juhudi alizowafanyia hususani za kuhakikisha kwamba wanahudhuria kwa kiwango kikubwa katika tamasha hilo, lakini pia ahadi aliyowapa ya kuwapeleka Bungeni ili wakatangaze bidhaa zao na kuwatangaza katika vyombo vya habari nchini.
Tamasha la JAMAFEST lilianzishwa mwaka 2013 nchini Rwanda na baadhi ya Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo kwa mwaka huu tamasha hilo linafanyika mjini Kampala nchini Uganda ambapo pia tamasha hili linatarajiwa kufanyika tena katika moja ya nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) mwaka 2019.
↧
WAMILIKI WAAGIZWA KUHAKIKISHA USALAMA WA MIGODI YAO MKOANI SINGIDA
Wamiliki wote wa migodi inayofanya shughuli za uchimbaji wa madini Mkoani Singida wameagizwa kuhakikisha kuwa hakuna vifo wa majeruhi katika maeneo yao kutokana na uwepo wa miundombinu mibovu au uzembe wowote.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi ametoa agizo hilo alipotembelea mgodi wa madini katika Kijiji cha Konkilangi, Kata ya Ntwike, Tarafa ya Shelui, Wilaya ya Iramba kuona shughuli za uokoaji mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.
Dkt Nchimbi amesema wamiliki wa migodi wanatakiwa kuwekeza katika kuboreha miundombinu ya migodi ili wachimbaji waweze kufanya kazi katika mazingira ambayo si hatarishi.“Madini yanatakiwa kuleta neema na kukuza uchumi wa taifa letu na sio kuangamiza nguvu kazi na kuleta majonzi, serikali haiwezi kukubali kupoteza vijana kutokana na uzembe wa baadhi ya watu”, amesema.
Ameongeza kwa kumtaka Kamishna Msaidizi wa madini kanda ya kati Sostenes Masolla kuweka ratiba ya kutoa mafunzo kila wiki huku akitakiwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili wachimbaji wapewe semina na mafunzo ya juu ya usalama wao wawapo migodini.
Dkt Nchimbi pia amemtaka Kamishna huyo wa madini kufuatilia taaluma na sifa zinazotumika kuchagua wakaguzi wa migodi maarufu kama ‘inspekta’ kwakuwa wao ndio hutakiwa kwa kiwango kikubwa kuhakikisha kuwa shimo au duara liko salama kabla ya kuruhusu uchimbaji kufanyika.
“Hawa ma inspekta hawa wasituulie vijana kutokana na uzembe wao, unakuta hajakagua vizuri halafu anaruhusu watu walipue baruti matokeo yake ndio kama haya, hawa wakiwa makini ajali za kwenye migodi zitapungua sana”, amesisitiza.Aidha Dkt Nchimbi amewataka wachimbaji na wamiliki wa migodi kuachana na imani potofu kuwa endapo vifo vinatokea katika shimo la mgodi hapo panakuwa na madini mengi.
Amesema ikiwa atabaini kuwa imani hizo zinaendekezwa na kipa endapo patatokea tena kifo katika mgodi huo basi hatasita kufunga shughuli za uchimbaji katika mgodi huo.Kwa upande wao wachimbaji wameeleza kuwa ajali hiyo imesababishwa na uzembe wa mgakuzi wa shimo hilo ambaye aliruhusu ulipuaji wa baruti wakati mazingira yakiwa hayaruhusu.
Wachimbaji hao wamemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa wamekosa amani kutokana na vifo hivyo ambavyo kwa kiwango kikubwa vimetokana na uzembe huku pia wakilalamikia utaratibu wa malipo yao.Mmoja wa wachimbaji hao Abuu Amiri amesema ma inspekta hao wamekuwa wakijali maslahi binafsi badala ya kuangalia usalama wa wachimbaji watakaoingia katika shimo hilo.
Mgodi ujulikanao kwa jina la Sekenke 1 katika kitalu namba 1, ambapo maduara matano yanayomilikiwa na Marijan Ramadhani na Jakobo Ntobi, yalititia mnamo tarehe tisa Septemba na kusababisha vifo kwa wachimbaji wawili huku mmoja tayari mwili wake ukiwa umepatikana na majeruhi watano.
Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akizungumza na wachimbaji alipotembelea mgodi wa madini katika Kijiji cha Konkilangi, Wilayani Iramba kuona shughuli za uokoaji mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki. Kushoto kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Iramba Emmanuel Luhahula.
Wachimbaji wakiendelea na shughuli za uokoaji katika Kijiji cha Konkilangi, Wilayani Iramba mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.
Wachimbaji wakiwa wanatazama shughuli za uokoaji zikiendelea katika Kijiji cha Konkilangi, Wilayani Iramba mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.
Mmoja wa wachimbaji Abuu Amiri akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi alipowatembelea kuona shughuli za uokoaji katika mgodi wa madini wa Kijiji cha Konkilangi, Wilayani Iramba mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.
Umati wa Wachimbaji uliojitokeza kumsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi alipowatembelea kuona shughuli za uokoaji katika mgodi wa madini wa Kijiji cha Konkilangi, Wilayani Iramba mara baada ya mgodi huo kutitia huku watu wawili wakihofiwa kufariki.
↧
TCRA YAWAASA WAMILIKI WA MITANDAO YA KIJAMII KUCHUJA HABARI ZAO KWA WEREDI
↧
↧
TUMEANZA KUIONJA SHUBIRI YA VITA YA UCHUMI.
Na Bashir Yakub.
Tumegusa uchumi wa bepari. Mara zote, na kote duniani bepari alipoguswa kwenye uchumi wake basi ametumia mbinu hizi hapa chini kuhakikisha anapambana na waliomzuia.
[a] Kumwita kiongozi anayeongoza vita ya uchumi Mvunjaji wa haki za binadamu na asiyefaa. Imetokea kwa Gaddafi baada ya kumnyima bepari mafuta, halikadhalika kwa Saddam Hussein.Pia ndilo tatizo la Mugabe na bepari baada ya kurudisha mashamba kwa wazawa ili wafaidi uchumi wao.
[b] Kuratibu na kufanikisha matukio ya ajabu kwenye jamii ili kuleta faraka,taharuki, chuki, uadui, na sintofahamu.Bepari analiweza sana hili hasa nchi za Afrika kutokana na uwezo wake mkubwa wa fedha na teknolojia.
Lengo la mbinu hii ni :
Mosi,kuwatoa kwenye ajenda ya vita dhidi yake na kuwaelekeza kwenye mijadala mingine.
Pili, kuchonganisha watu, serikali na viongozi wao.
Tatu, kupeleka ujumbe duniani kuwa kiongozi fulani na serikali yake hawafai tena.
Nne, kuligawa taifa kati ya upande unaoamini matukio kutekelezwa na fulani na upande unaoamini vingine.
[c] Kuandaa mapinduzi kwa kuwatumia wasaidizi wa rais na viongozi wenye tamaa.
[d] Kuandaa maandamamo makubwa ambayo mwisho wake ni kuuondoa utawala uliodhibiti uchumi .
Utaona waandamanaji wanalalamika kuchoshwa na mambo mbalimbali lakini nyuma yao ni fedha, mbinu na mipango ya bepari.
Bila hata waandamanaji kujua isipokuwa wachache/viongozi wao. Mbinu hii imetumika hivi karibuni kuondoa viongozi wengi wa Afrika ya Kaskazini waliodhibiti uchumi wao kwa mda mrefu.
[e] Kufadhili makundi ya waasi Mf. Congo, Sudani Kusini, Sierra Leone, Liberia nk. Mnajua kuwa hadi baadhi ya makundi ya kigaidi hufadhiliwa na hawa jamaa.
Badala ya kujadili udhibiti wa rasilimali zenu mnajadili amani itapatikana vipi huku bepari akitumia nafasi hiyo kuiba.
[f] Kufadhili na kuviimarisha vyama vya upinzani hasa vyenye tamaa ili hatimaye na kwa namna yoyote ile viondoe madarakani viongozi waliombana bepari.
[g] Kutafuta sababu na hatimaye kuweka vikwazo vya kiuchumi kwa nchi husika ili kulainisha au kumaliza kabisa misimamo ya serikali na viongozi dhidi ya rasirimali anazozitaka bepari.
Pia lengo ni kuwafanya wananchi wapate taabu ili wachoshwe na utawala uliombana bepari na hivyo kufanya maamuzi ya kuuondoa kwa namna yoyote. nk, nk, nk............
NINI MFANYE KTK KIPINDI KAMA HIKI.
[a] Kushikamana na kutokubali kutenganishwa kwa matukio.
[b]Kutokuwa na majibu ya haraka katika mambo makubwa.
[c] Vyombo vya usalama kujiimarisha kiulinzi na kuhakikisha vinafika kwenye majibu ya mzizi wa kila tukio na kutoa taarifa kwa wakati kwa umma.
[d] Vyombo vya usalama kutokubali kusaidiwa upelelezi na nchi za mabepari kwakuwa mwanya huo hutumika kutoa majawabu aidha yanayokwepesha(divert) ukweli au yanayokamilisha malengo yaliyokusudiwa.
[e] Kuepuka kabisa kuchanganya tofauti zetu za kisiasa za tokea huko nyuma na yanayotokea sasa.
YAPI MADHARA YA KUTOSHIKAMANA KIPINDI KAMA HIKI.
Bepari hana hasara, wenye hasara ni mimi na wewe. Mpango wa wagawe uwatawale "divide&rule" haikuishia kwenye ukoloni. Bado ungalipo.
Kama tutakubali kugawanywa na majaribu ya bepari , sawa na tugawanywe tu , ila ahadi ni hii kuwa kila mmoja ataonja joto la jiwe.
Wewe uliyekubali kugawanywa utaonja na ambaye hakukubali ataonja. Mtaona Iraq na Libya aliyeshiriki na ambaye hakushiriki wote wanaonja.
Hakuna atakayekuzuia kukomaa na msimamo wako. Hakuna atakayekuzuia kuamini mbowe ndiye aliyefanya tukio fulani ili kumzuia fulani kugombea uenyekiti. Hakuna atakayekuzuia kuamini kuwa Lowassa ndiye aliyefanya tukio fulani ili kumzuia fulani kugombea urais 2020. Lakini pia hakuna atakayekuzuia kuamini kuwa serikali ndiyo iliyofanya tukio fulani kwasababu yule au ofisi ile kuna wabaya au wakosoaji wake.
Wewe amini hivyohivyo unavyoamini ila kaa ukijua kuwa ikiwa tutagawanyika tu, basi kila mtu, kila familia, kila kundi, kila chama, na imani yako hiyohiyo uliyonayo yatakufika. Madhara ya bepari yanapokuja hayaangalii nani alikuwa akiamini nini, ama nani alitumia gani tukio kumsema nani.
Mtaona Libya kusini ina serikali yake, kaskazini ina serikali yake , magharibi yake na mashariki yake.Ni vipandevipande, shida juu ya shida. Na humo wamo wote walioshiriki na ambao hawakushiriki. Madhara ya bepari hayaangalii aliyeshiriki na ambaye hakushiriki.
Kwahiyo wewe msaidie tu bepari kwakujua au kutokujua kueneza propaganda zake kwa matukio anayoyaandaa ila ujue kuwa mwisho wa tamthilia tutakuwa wote tuu. Wala huna pa kwenda ndugu tutalia wote humuhumu.
Na mkishakuwa nyang’anyang’a, bepari ameshawashinda, na hamna tena la kumfanya, na sasa anawageuza anavyotaka, basi hapo bepari atakuja na kusema ukweli kuwa si fulani aliyefanya tukio fulani bali ni sisi kwa lengo fulani.
Mnakumbuka wale walioiharibu Iraq baadae walisema ukweli. Waliandika vitabu kuwa vita ile ilikuwa ya makosa na kule hakukuwa na silaha za sumu kabisa. Ni baada ya kuiharibu vibaya sana nchi hiyo na kuiletea dhiki na mashaka makubwa.
Mnakumbuka walioiharibu Libya nao baadae walisema ukweli. Sasa wanasema wazi kuwa makundi waliyoyatumia kumg’oa Gaddaffi hayakuwa makundi sahihi bali ya imani kali.
Lakini mwanzoni walikataa kuwa hawako nyuma ya makundi yaliyoanzisha maandamano na kusema kuwa wananchi waliochoka udikteta wa Gaddaffi ndio wanaoandamana. Bepari akishakumaliza anakiri. Basi kwa kiwango gani mnakuwa mmedhalilika na kudharauliwa ndugu zangu. Ni lini wananchi wa Afrika tutajifunza kutoka matukio haya.
Tunawalaumu viongozi wetu waafrika lakini pia sisi wananchi wa Afrika kwa nafasi zetu kama wananchi tunayo mambo ya kujifunza na kushughulikia lakini hatufanyi hivyo. Ni lini basi tutaacha kudhalilishwa na bepari. Toka ukoloni mpaka uhuru hatujifunzi tuu ndugu zangu. Basi tutajifunza lini , makaburini ama.
Tujihadhari kwani kwetu tayari bepari ameanza kwa matukio ya hapa na pale. Tukimuunga mkono kwa vinywa vyetu huku tukijua tunamkomoa kiongozi fulani au chama fulani, basi atatuvuta taratibu taratibu mpaka huko Libya na Iraq halafu yeye aendelee kuiba kama alivyokuwa amezoea awali.
Ndugu zangu, tunawasifia Angola na Botswana kwa kumbana bepari na hatimaye kufaidi rasimali zao sasa.
Lazima tujue wamefikia hapo baada ya kushikamana na kuzishinda hila, fisadi, fitna,na mitihani ya bepari. Na sisi tunaweza.
TUTARAJIE MATUKIO ZAIDI.
Matukio bado , huu ni mwanzo tu. Hivi mlitarajia bepari abanwe halafu tubaki salama. Haiwezekani. Historia inakataa jambo hilo. Bepari lazima akutingishe.
Kama ingekuwa tumbane bepari halafu tubaki
salama basi isingeitwa Vita ya Uchumi bali Sherehe ama tafrija ya Uchumi. Yanini iitwe vita kama mmembana bepari na bado mkaendelea kuwa salama na kufurahia maisha. Hii ni vita na sasa mnaweza kuanza kuona taswira ya vita yenyewe.
Vitimbi na matukio yatakuja mengi. Lengo ni moja tu , kuua vita hii ili bepari aendeleze alikoishia.
Msishangae wakaanza kudhuliwa hata wanaoonekana wana mtazamo tofauti na mwenyekiti ndani ya chama tawala ili chama kigawanyike na hatimaye serikali igawanyike. Bepari anajua ukigawa chama kinachotawala umeigawa serikali kwakuwa wanachama wa chama tawala ndio huunda serikali.
Hivyo kwa kufanikiwa kukigawa chama kinachotawala bepari anajua atakuwa amefanikiwa kuigawa serikali.
Ukifanikiwa kuigawa serikali maana yake bepari amepunguza kasi ya vita dhidi yake lakini maana yake pia anakaribia kumwondoa kabisa adui aliyebana uchumi wake.
Bepari haoni tabu kumdhuru yeyote ama chochote ili kutimiza malengo yake. Bepari anajua ukimdhuru kiongozi mwenye mawazo tofauti ndani ya chama ama serikali , basi watanyoosheana vidole. Yule aliyedhuriwa atapata kundi lake wanaoamini ameonewa na wale wengine watabaki kundi jingine. Bepari anajua kuwa hata kiongozi awe mkali ama na msimamo kiasi gani hawezi kusimama kama wasaidizi wake wamegawanyika.
Ni vita ya uchumi , na sasa tunaonja shubiri yake. Ila tutashinda.
MWANDISHI WA MAKALA HAYA NI MWANASHERIA NA MCHAMBUZI WA MASUALA YA SIASA. 0784482959.
↧
MWANDISHI AANIKA SIRI MAUAJI YA ALBINO KWENYE KITABU, AHOAJIANA NA WAGANGA, WACHAWI NA MATAPELI
Jalada la kitabu cha ‘MIFUPA YA ALBINO’.
Mwandishi Daniel Mbega, akiwa ameshikilia Karunguyeye waliokaushwa nyumbani kwa mganga wa jadi.
MWANDISHI wa habari mwandamizi nchini, Daniel Mbega, amekamilisha kuandika kitabu kinachofichua siri zilizo nyuma ya pazia kuhusiana na mauaji ya vikongwe na albino nchini Tanzania na barani Afrika kwa ujumla.
Mwandishi huyo, ambaye alifanya utafiti kwa kipindi cha miezi nane mfululizo katika mikoa 10 ya Kanda ya Maziwa Makuu, amesema kitabu hiyo alichokipa jina la ‘MIFUPA YA ALBINO’ kinatarajiwa kuwaingia kiwandani wakati wowote na kwa sasa anatafuta msaada wa fedha za kuchapia.
“Nimekamilisha, lakini nimekwama kidogo kuhusu fedha za uchapaji na kama kuna taasisi yoyote au mtu anayeweza kunisaidia nitashukuru sana,” amesema mwanahabari huyo.“Yeyote mwenye nia njema na jamii ya Watanzania na anaguswa kusaidia uchapaji wa kitabu hiki, ninaomba awasiliane nami kwa namba hii 0656-331974, kwani naamini kitabu hiki kitakuwa msaada pia wa kiroho baada ya kujua mambo yanayofanywa hata na baadhi ya viongozi wa dini wanaotumia ushirikina,” aliongeza.
Bw. Mbega amesema kwamba, katika utafiti wake huo alifanikiwa kukutana na waganga wa jadi, wachawi na matapeli katika mikoa ya Shinyanga, Geita, Simiyu, Mwanza, Kagera, Mara, Kigoma, Tabora, Katavi na Rukwa, ambako alikaa kwa miezi miwili akifanya uchunguzi.
Aidha, amesema kwamba, katika uchunguzi wake huo alishiriki pia kikamilifu katika misako mbalimbali ya wahalifu walioshiriki kwenye matukio hayo na kushuhudia namna vyombo vya ulinzi na usalama vinavyotenda kazi.Kunusurika kifo kwa ajali ama kuzingirwa na baadhi ya wananchi ni moja ya hatari alizokumbana nazo wakati wa uchunguzi wake, huku akisafiri umbali wa zaidi ya kilometa 40,000 katika kipindi hicho.
“Wakati mwingine nilikosa usingizi hata kwa siku tano mfululizo, nililazimika kusafiri mchana na usiku katika mazingira mengi hatarishi nikikusanya habari,” alisema.Akaongeza: “Haikuwa kazi rahisi kuweza kufanya mahojiano na waganga wa jadi, achilia mbali wachawi ambao baadhi yao waliamua kujiweka wazi na kueleza mambo yanayotendeka katika ulimwengu wa giza na jinsi yanavyohusiana na mauaji ya wenye ualbino.”
Alisema katika uchunguzi huo alikumbana na mambo mengi ya ajabu ikiwa ni pamoja na kushika matunguli, pembe zinazofoka damu, damu na maiti, mifupa inayodhaniwa kuwa ya binadamu na mambo mengine kadha wa kadha.Aidha, alisema kwamba, alizungumza pia na wanamichezo, baadhi ya viongozi wa dini ambao nao wanatumia nguvu za giza ambapo waganga walieleza jinsi nao wanavyoshiriki katika matukio hayo ya mauaji ya wenye ualbino.
“Ni mtandao mpana sana, siyo Tanzania tu, bali hata katika nchi jirani za Kenya, Malawi, Burundi, Msumbiji, Afrika Kusini na Swaziland… naamini kkitabu hiki kitaiamsha jamii na kubadilisha mitazamo ya watu mara watakapojifunza yale niliyoyakusanya kutoka kwa vinywa vya wahusika wenyewe,” amesema na kusisitiza kwamba amepanga kitabu hicho kiwwe mtaani mwishoni mwa mwezi Septemba ikiwa atapata msaada wa kufanikisha uchapaji.
Mganga wa jadi akimpigia ramli mwandishi wa kitabu hiki (hayuko pichani) baada ya kutoa Shs. 2,000 akitaka amwangalizie kwanini 'mkewe' (askari mmoja wa kike aliyekwenda naye wakiwa kikazi) alikuwa hazai. Mganga alisema mwanamke huyo alikuwa 'amelogwa' na mwanamke aliyetaka kuolewa na mwandishi halafu yeye akamkataa, ambapo kiuhalisia hakuwepo mwanamke wa aina hiyo na hata huyo aliyekwenda naye walikutana kikazi na hawakuwa wakifahamiana kabisa.
Mtoto Baraka Cosmas akiwa amelazwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mbeya baada ya kukatwa kitanga cha mkono Machi 7, 2015.
Mwandishi Daniel Mbega (mwenye fulana nyekundu na kofia ya sweta) akiwa sambamba na wanausalama katika nyumba ambamo Baraka Cosmas alikatwa kitanga cha mkono Machi 7, 2015.
Mtuhumiwa Sajenti Kalinga Malonji akiwa chini ya ulinzi baada ya kukishusha kiganja cha Baraka Cosmas kwenye mti nyumbani kwake kijijini Hanseketwa, Mbozi siku ya Jumapili, Aprili 26, 2015. Sajenti tayari amehukumiwa miaka nane jela na wenzake wamehukumiwa vifungo vya hadi miaka 20 jela.
Mwandishi Daniel Mbega, akiwa kwa mganga huko Kachwamba, wilayani Chato wakati akifanya uchunguzi wa mauaji ya albino.
↧
SHIRIKA LA EMPOWER SOCIETY TRANSFORMM LIVES LAANZA KUTOA ELIMU JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI MKOANI SINGIDA
Na Jumbe Ismailly SINGIDA
SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la Empower Society Transform Lives (ESTL) la Mkoani Singida limesema kwamba ukeketaji wa wanawake na watoto ni tatizo kubwa Afrika,Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi 28 zinazotajwa kuendeleza mila hiyo mbaya.
Hayo yalisemwa na Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo Mkoani Singida,Joshua Ntandu kwenye risala aliyosoma wakati wa uzinduzi wa mradi wa kutokomeza ukeketaji katika vijiji 14 vilivyopo katika kata za Itaja,Mgori,Ntonge na Ughandi,uliofadhiliwa na The Foundation For Civil Society na kufanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.
Aidha Ntandu alifafanua kwamba inakadiriwa kuwa Tanzania ina zaidi ya wanawake milioni 7.9 waliogundulika kuwa wamekeketwa huku Mkoa wa Singida ukishika nafasi tano za juu za mikoa inayoongoza kwa ukeketaji hapa nchini.
Alisema tafiti zinaonyesha pia kwamba vitendo hivyo vinaendelea kuongezeka katika Mkoa wa Singida na sababu kubwa zinazotajwa ni pamoja na imani kwamba ukeketaji ni sehemu ya makuzi ya mtoto wa kike na kwamba humzuia mtoto wa kike asiingie katika mahusiano ya mapenzi kabla ya kuolewa.Hata hivyo Ntandu alisisitiza kuwa jamii pia huamini kwamba ukeketaji ni tiba ya ugonjwa unaojulikana kama lawalawa kwa watoto wa kike (Vaginal or Urinary Tract Infection (UTI).
“Kadhalika kuna mbinu mpya ambayo imeshamiri ya ukeketaji wa watoto wachanga mara tu wanapozaliwa na kabla ya kufikia umri wa mwaka mmoja,na hii hufanywa ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria na vyombo vya dola”alisisitiza Mtendaji mkuu huyo wa ESTL.
Akizindua mradi huo kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida,Afisa Ustawi wa jamii wa Mkoa wa Singida,Shukurani Mbago,pamoja na kusikitishwa na mbinu mpya iliyoshamiri ya ukeketaji wa watoto wachanga,alizitaja baadhi ya sababu za kuongezeka kwa vitendo hivyo kuwa ni imani kuwa ukeketaji ni sehemu ya makuzi ya mtoto wa kike na kwamba kumzuia mtoto wa kike asiingie katika mahusiano ya mapenzi kabla ya ndoa.
“Jamii pia huamini kuwa ukeketaji ni tiba ya ugonjwa ujulikanao kwa jina la lawalawa kwa watoto wa kike mara tu wanapozaliwa na kabla ya kufikia umri wa mwaka mmoja.”alifafanua Katibu tawala huyo wa Mkoa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya ESTL Mkoa wa Singida,Rose Mjema aliweka bayana kwamba mpaka sasa wameshaunda kamati za kutokomeza ukeketaji katika ngazi za vijiji na kata kutokana na watu waliopo katika ngazi hizo kuonyesha utayari wa kufanyakazi na wao.
Kwa mujibu wa Mjema wajumbe waliopo katika kamati hizo ni ni vijana tu kwa ngazi ya kata na vijiji,viongozi wa jadi,wakunga wa tiba asilia na wakunga wa jadi kwa kuwaandalia vikundi vya kupiga vita masuala ya ukeketaji kwenye maeneo yao.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida,Elia Digha akizungumza na washiriki wa semina hiyo alishauri kwamba ili kukabiliana na vitendo hivyo kuanzia ngazi za serikali za vijiji pamoja na Halmashauri waanze kuandaa sheria ndogo itakayosimamia udhibiti wa ukeketaji katika Halmashauri ya wilaya hiyo.
Ni Mwenyekiti wa Bodi ya ESTL,Bi Rose Mjema akiwasilisha mada kwa washiriki wa mafunzo ya kupinga vitendo vya ukeketaji huku akitoa tahadhari juu ya madhara yatokanayo na vitendo hivyo vya ukeketaji.(Picha zote Na Jumbe Ismailly).
Ni baadhi ya Mangariba na wakunga wa jadi kutoka katika Tarafa ya Mgori,wilayani Singida ambao wameamua kuachana na shughuli za kukeketa baada ya kupatiwa elimu na Shirika lisilokuwa la kiserikali la ESTL la Mkoani Singida,wakitoa ushuhuda kwenye uzinduzi wa mradi wa kutokomeza ukeketaji kwa wanawake katika Mkoa wa Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.
↧
HOSPITALI YA WATOTO YA HUNAN YAWAFUNDA MADAKTARI NA WAUGUZI WA ZANZIBAR
Na Ramadhani Ali – Maelezo 13.9.2017
Makamu wa Raiswa Hospitali ya watoto ya Hunan Chini China Zhu Lihui ameahidi kuwa Hospitali hiyo itaendelea kushirikiana na Hospitali ya Mnazimmoja ya Zanzibar kuwajengea uwezo wafanyakazi na kuimarisha Utawala wa Hospitali.
Zhu ameeleza hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku kumi yanayowashirikisha madaktari na wauguzi 25 wanaoshughulikia watoto kutoka Hospitali ya Mnazimmoja, Kivunge na Makunduchi.
Amesema Hospitali ya watoto ya Hunan imewahi kutoa mafunzo kwa wafanyakazi 26 katika vipindi tofauti nchini China imeamua kufanya mafunzo Zanzibar kwa kushirikiana na Wizara ya Afya iliwafanya kazi wengi waweze kufaidika.
Ameeleza matarajio yake kuwa wafanyakazi waliopata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo wataenda kuwaelimisha wafanyakazi wenzao ambao hawakubahatika kushiriki.
Aidha amesema kuja kwamadaktari bingwa kutoka jimbo la Hunan kutoa mafunzo hapa Zanzibar kutaongeza mashirikiano kati ya Hospitali ya Mnazimmoja na kubadilishana uzoefu katika kuimarisha afya za wananchi na kuimarisha masuala ya utawala.
Balozi mdogo wa China aliepo Zanzibar Xie Xiawu amesema ushirikiano baina ya China na Zanzibar niwamuda mrefu na nchi yake itaendelea kusaidia Zanzibar katika kuimarisha na kukuza maendeleo ya wananchi.
Alisema mafunzo yatakayotolewa na wataalamu kutoka Hospitaliya watoto ya Hunan yatawajengea uwezo watendaji wa wodi za watoto na kuimarisha afya ya mama baada ya kujifungua na watoto wanaozaliwa.
Akifungua mafunzo hayo yanayofanyika Hospitali mpya ya wazazi ya Mnazimmoja, Naibu Waziri wa Afya Harusi Saidi Suleiman aliishukuru Hospitali ya watoto ya Hunan kwa kusaidia kuwaongezea ujuzi wafanyakazi wanaoshughulikia matatizo ya watoto na kuimarisha utawalawa Hospitali.
Aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kuwa wasikivu na kufuatilia kwa karibu masomo watakayo someshwa ili nao kuja kuwa walimu kwa wengine baada ya kumaliza na kuwawezesha wataalamu wa China kusomesha kada nyengine za afya.
Makamu wa Rais wa Hospitali ya Watoto ya Hunan nchini China akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku 10 ya Madaktari na wauguzi wanaoshughulikia watoto katika Hospitali ya Kivunge, Makunduchi na Mnazimmoja mafunzo yanayofanyika Mnazimmoja Mjini Zanzibar.
Balozi mdogo wa china aliepo Zanzibar XieXiawu akitoa hutuba katika ufunguzi wa mafunzo ya siku 10 ya kuwajengea uwezo madaktari na wauguzi wanaofanyakazi wodi za watoto za Hospitali ya Kivunge, Makunduchi na Kivunge.
Naibu Waziri wa Afya Arusi Said Suleiman akifungua mafunzo ya madaktari na wauguzi wanaoshughulikia watoto na kuimarisha utawala wa Hospitali, mafunzo yanayofanyika Hospitali kuu ya Mnazimmoja.
Washiriki wa mafunzo kutoka Hospitali ya Mnazimmoja, Kivunge na Makunduchi wakiwa pamoja na wakufunzi wao kutoka Hospitali ya Hunan China wakifuatilia hotuba ya ufunguzi iliyotolewa na Naibu Waziri wa Afya Bi. Arusi Said Suleiman (hayupo pichani).Picha na Makame Mshenga.
↧
↧
MSHITAKIWA SETH ALALAMIKIA MAHAKAMA KUWA HAJAPATA MATIBABU
Na KaramaKenyunko, Glogu ya jamii
MSHITAKIWA Herbinder Seth leo ameileza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa, bado hajapelekwa Hospital ya Muhimbili kutibiwa kama amri ya mahakama ilivyoagiza.
Mshtakiwa Seth ameyasema hayo leo baada ya wakili wake wa utetezi, Melchisedeck Lutema kuileza mahakama kuwa bado mteja wake huyo anayeshtakiwa katika kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha inayomkabili yeye na mwenzake James Rugemalira bado hajapelekwa Hospital ya Muhimbili
mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, Lutema ameomba upande wa mashtaka ueleze kwanini mshtakiwa hapelekwi hospitali, kwani katika mashauri yaliyopita mahakama imetoa amri mara kadhaa zote zikielekeza mshitakiwa huyo apelekwe Hospitali ya Muhimbili lakini haijatekelezwa.
ameiomba mahakama itumie busara ili kuhakikisha mshtakiwa anapekwa hospitali na kwamba wakuthibitisha kama ametibiwa au la ni mshtakiwa mwenyewe.
Habinder amedai hayo baada ya Wakili wa Serikali, Leonard Swai akisaidiana na Vitalis Peter kudai kuwa shauri limekuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
akiongea kuhusu matibabu, alidai mshtakiwa alipelekwa hospital ya magereza na kwamba alitibiwa na mtaalamu Dotto Pakacha ambaye anampatia matibabu kila anapolalamika huwa wanamuona na kwamba yeye mwenyewe alifuatilia kupata uhakika kuwa anapatiwa matibabu kwani hata akipata shinikizo la damu huwa wanamuona.
"Tunaendelea na upelelezi kwasababu kuna mashtaka ya kugushi yanahusisha taasisi zaidi ya moja tunaomba mahakama itupe muda ili tukamilishe upelelezi"alidai
Hata hivyo, Hakimu Shaidi amesisitiza mshitakiwa Seth apelekwe katika hospitali ya Muhimbili kama ilivyotoa maagizo awali na kwamba inaonyesha wazi amri ya mahakama haifuatwi, “ oda ya mahakama lazima ifuatwe, haiwezekani kila siku tukija hapa tunaongea kitu kimoja tu hii haipendezi" amesema hakimu Shaidi.
Aidha, Wakili anayemtetea James Rugemarila, Pascal Kamala amedai kuwa washtakiwa walifikishwa mahakamani hapo juni 19 mwaka huu hadi leo ni siku 87 wako ndani na makosa wanayoshtakiwa nayo hayana dhamana na upelelezi haujakamilika, ili haki iweze kutendeka kwa pande zote mbili wanaomba upelelezi ukamilike mapema na haki iweze kutendeka.
Kesi hiyo itatajwa Septemba 29 mwaka huu.
Seth na Rugemarila wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu , kighushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kuisababisha hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.
Upelelezi wakamilika kesi ya Manji tuhuma za ‘unga’
Hata hivyo, wakati upande wa Jamhuri ukitoa taarifa ya upelelezi kukamilika dhidi ya mfanyabiashara huyo, mshtakiwa huyo hakuwapo mahakamani.
Wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Cyprian Mkeha, kwamba mshtakiwa ni mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
"Mheshimiwa mteja wangu ameshindwa kuja mahakamani kusikiliza kesi yake kwa sababu mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Muhimbili," alidai Mgongolwa mahakamani hapo.
Kabla ya kutolewa taarifa ya ugonjwa wa mshtakiwa huyo, Wakili wa Serikali Mkuu, Timon Vitalis, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba upande wa Jamhuri unaomba tarehe nyingine ya kusikiliza maelezo ya awali.
Hakimu Mkeha alisema kwa kuwa mshtakiwa ni mgonjwa, kesi hiyo itaanza kusikilizwa Agosti 10, mwaka huu.
Katika kesi ya msingi, Manji ambaye pia ni Diwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam na mfanyabiashara maarufu nchini, anakabiliwa na mashtaka ya kutumia dawa za kulevya.
Ilidaiwa kuwa kati ya Februari 6 na 9 mwaka huu, eneo la Upanga Sea View jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.
Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana.
Hata hivyo, wakati Manji akiwa nje kwa dhamana katika kesi hiyo ya tuhuma za utumiaji dawa za kulevya, mfanyabiashara huyo alikosa dhamana juzi katika kesi nyingine inayohusiana na uhujumu uchumi.
Katika kesi hiyo ambayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilihamishia shughuli zake Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa Manji kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Manji na wenzake watatu walikosa dhamana baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), akiomba washtakiwa wasipewe dhamana kwa usalama wao na maslahi ya taifa.
Pia DPP alieleza sababu nyingine ya Manji kunyimwa dhamana kuwa ni mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kushughulikia dhamana dhidi ya kesi hiyo. Washtakiwa wengine ni Ofisa Rasilimaliwatu Deogratias Kisinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Mtunza Stoo msaidizi, Thobias Fwele (43).
Ilidaiwa katika shtaka la kwanza kuwa Juni 30, mwaka huu eneo la Chang'ombe Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Manji na wenzake walikutwa na askari polisi wakiwa na mabunda (majora) 35 ya vitambaa vinavyotengezea sare za JWTZ vyenye thamani ya Sh. milioni 192.5 na kwamba vilipatikana isivyo halali.
Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A' Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na askari polisi wakiwa na mabando nane ya sare za JWTZ zenye thamani ya Sh. milioni 44.
Upande huo wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa, Juni 30, mwaka huu eneo la tukio la kwanza, washtakiwa walikutwa na mhuri wa JWTZ uliokuwa na maandishi 'Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha Jeshi JWTZ' bila kuwa na uhalali, kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Katika shtaka la nne, ilidaiwa kuwa siku ya tukio la tatu, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na mhuri wenye maandishi "Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupora Dodoma" bila uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Katika shtaka la tano, ilidaiwa siku ya tukio la tatu na la nne, mshtakiwa alikutwa na mhuri wenye maandishi "Comanding Officer 835 KJ Mgambo P.O BOX 224 Korogwe" bila kuwa na uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Ilidaiwa katika shtaka la sita, Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A', washtakiwa wote walikutwa na namba za gari zenye usajili wa SU 383 iliyopatikana isivyo halali.
Katika shtaka la saba, eneo la tukio la sita, washtakiwa walikutwa na namba za gari zenye namba ya usajili SM 8573 iliyopatikana isivyo halali.
Kwa mujibu wa mashtaka hayo yaliyofunguliwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi na Usalama wa Taifa, washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yao.
Hakimu Mkazi Huruma Shaidi alisema kesi hiyo itatajwa Julai 19 na washtakiwa watatu walipelekwa mahabusu ya Keko huku Manji akiwa chini ya ulinzi wa polisi wodini hapo.
Wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Cyprian Mkeha, kwamba mshtakiwa ni mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.
"Mheshimiwa mteja wangu ameshindwa kuja mahakamani kusikiliza kesi yake kwa sababu mgonjwa na amelazwa katika Hospitali ya Muhimbili," alidai Mgongolwa mahakamani hapo.
Kabla ya kutolewa taarifa ya ugonjwa wa mshtakiwa huyo, Wakili wa Serikali Mkuu, Timon Vitalis, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba upande wa Jamhuri unaomba tarehe nyingine ya kusikiliza maelezo ya awali.
Hakimu Mkeha alisema kwa kuwa mshtakiwa ni mgonjwa, kesi hiyo itaanza kusikilizwa Agosti 10, mwaka huu.
Katika kesi ya msingi, Manji ambaye pia ni Diwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam na mfanyabiashara maarufu nchini, anakabiliwa na mashtaka ya kutumia dawa za kulevya.
Ilidaiwa kuwa kati ya Februari 6 na 9 mwaka huu, eneo la Upanga Sea View jijini Dar es Salaam, Manji alitumia dawa za kulevya aina ya heroin.
Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana.
Hata hivyo, wakati Manji akiwa nje kwa dhamana katika kesi hiyo ya tuhuma za utumiaji dawa za kulevya, mfanyabiashara huyo alikosa dhamana juzi katika kesi nyingine inayohusiana na uhujumu uchumi.
Katika kesi hiyo ambayo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilihamishia shughuli zake Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikolazwa Manji kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Manji na wenzake watatu walikosa dhamana baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), akiomba washtakiwa wasipewe dhamana kwa usalama wao na maslahi ya taifa.
Pia DPP alieleza sababu nyingine ya Manji kunyimwa dhamana kuwa ni mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kushughulikia dhamana dhidi ya kesi hiyo. Washtakiwa wengine ni Ofisa Rasilimaliwatu Deogratias Kisinda (28), Mtunza Stoo, Abdallah Sangey (46) na Mtunza Stoo msaidizi, Thobias Fwele (43).
Ilidaiwa katika shtaka la kwanza kuwa Juni 30, mwaka huu eneo la Chang'ombe Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Manji na wenzake walikutwa na askari polisi wakiwa na mabunda (majora) 35 ya vitambaa vinavyotengezea sare za JWTZ vyenye thamani ya Sh. milioni 192.5 na kwamba vilipatikana isivyo halali.
Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A' Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na askari polisi wakiwa na mabando nane ya sare za JWTZ zenye thamani ya Sh. milioni 44.
Upande huo wa Jamhuri uliendelea kudai kuwa, Juni 30, mwaka huu eneo la tukio la kwanza, washtakiwa walikutwa na mhuri wa JWTZ uliokuwa na maandishi 'Mkuu wa Kikosi 121 Kikosi cha Jeshi JWTZ' bila kuwa na uhalali, kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Katika shtaka la nne, ilidaiwa kuwa siku ya tukio la tatu, washtakiwa wote kwa pamoja walikutwa na mhuri wenye maandishi "Kamanda Kikosi 834 KJ Makutupora Dodoma" bila uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Katika shtaka la tano, ilidaiwa siku ya tukio la tatu na la nne, mshtakiwa alikutwa na mhuri wenye maandishi "Comanding Officer 835 KJ Mgambo P.O BOX 224 Korogwe" bila kuwa na uhalali kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa nchi.
Ilidaiwa katika shtaka la sita, Julai Mosi, mwaka huu eneo la Chang'ombe 'A', washtakiwa wote walikutwa na namba za gari zenye usajili wa SU 383 iliyopatikana isivyo halali.
Katika shtaka la saba, eneo la tukio la sita, washtakiwa walikutwa na namba za gari zenye namba ya usajili SM 8573 iliyopatikana isivyo halali.
Kwa mujibu wa mashtaka hayo yaliyofunguliwa chini ya Sheria ya Uhujumu Uchumi na Usalama wa Taifa, washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi yao.
Hakimu Mkazi Huruma Shaidi alisema kesi hiyo itatajwa Julai 19 na washtakiwa watatu walipelekwa mahabusu ya Keko huku Manji akiwa chini ya ulinzi wa polisi wodini hapo.
↧
MFUMO WA KUPOKEA PESA BAADA YA KUPOKEA MZINGO WALETWA NA JUMIA.
Kampuni inayojihusisha na huduma za manunuzi ya bidhaa mbalimbali kwa njia ya mtandao nchini, Jumia Tanzania imewaondolea hofu wateja wake kwamba sasa wanaweza kulipia bidhaa pale zinapowafikia baada ya kufanya manunuzi kupitia tovuti yao.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja Masoko wa Jumia Tanzania, Bw. Albany James amebainisha kwamba wameona ni vema kuutambulisha mfumo huo mpya kwa wateja wao ili kuwaondolea hofu na kuwajengea uaminifu kwa huduma zote za manunuzi wanazozifanya kwa njia ya mtandao.
“Jumia Tanzania inayo furaha kuwajulisha wateja wao wote kwamba hivi sasa wanaweza kulipia bidhaa wanazozinunua kwa njia ya mtandao pindi zinapowafikia. Tumeona ni vema kuwapa wateja wetu chaguo hilo kwa kuzingatia mila na tamaduni tulizonazo watanzania kwamba tumezoea kununua bidhaa baada ya kujiridhisha kwa kuiona kwa macho. Mbali na hapo bado teknolojia ya huduma na manunuzi kwa njia ya mtandao ni ngeni miongoni mwa watanzania wengi hivyo wanakuwa na hofu kwamba wanaweza kuwa wanatapeliwa,” alisema Bw. James.
“Faida nyingine mbali na mteja kuiona bidhaa aliyoiagiza na kujiridhisha ndiyo alipie pia mteja atapata fursa ya kuweza kubadilisha kama hatoridhika. Tumekuwa tukipokea changamoto kwa baadhi ya wateja wetu kwamba wamekuwa wakipelekewa bidhaa ambazo zimekuwa tofauti kidogo na walivyoagiza. Ingawa tunawasisitiza sana kuwa makini na kuzingatia taarifa muhimu za bidhaa wananozitaka lakini katika kuwathibitishia kwamba Jumia Market sio wababaishaji tumeamua kuwajulisha kwamba wana chaguo la aidha kulipia kwa njia ya mtandao au pale bidhaa inapomfikia,” aliongezea Meneja Masoko huyo wa Jumia Tanzania.
Aliendelea mbele kwa kuongeza zaidi kwamba tofauti ya Jumia Tanzania na kampuni zingine zinazojihusisha na huduma za mauzo ya bidhaa kwa njia ya mtandao ni kwamba wao pekee ndio wanawapa wateja wao chaguo la kulipia bidhaa pale zinapowafikia. Na pale mteja asiporidhika na bidhaa aliyopelekewa anao uwezo wa kuomba kubadilishiwa na kuletewa bila ya kudaiwa malipo yoyote.
“Ningependa kutoa wito kwa watanzania kuchangamkia ofa mbalimbali za manunuzi ya bidhaa kwenye tovuti yetu na mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Twitter na Instagram. Lakini pia kwa wafanyabiashara wa kitanzania kuhamia kwenye njia za mitandao ili kupanua wigo wa wateja wao. Kuna faida nyingi za kujiunga nasi zikiwemo kujiongezea wateja wengi tofauti na wale wanaotembelea maduka yao moja kwa moja lakini pia kutangazwa bure kabisa bila ya malipo yoyote kwenye mtandao wetu,” alihitimisha Bw. James.
Jumia Tanzania ina amini kuwa tekinolojia inavyokua kwa kasi inatubidi kwenda nayo sambamba hasa kwenye manunuzi ya bidhaa tajwa hapo juu ili kuepuka usumbufu wa kuzunguka duka hadi duka pamoja na kuokoa muda kwasababu bidhaa zote zinazoagizwa hupelekwa hadi pale mteja alipo.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Jumia Tanzania, Mikolaj Kucia akizungumza na waandishi wa habari namna ya malipo yanavyofanyika hasa pale tu mtu anapopokea bidhaa wanzaouza mtandaoni pamoja na namna wanavyofikisha bidhaa kwa wateja wao kwenye mkutano uliofanyika katika ofisi zao Kinondoni Jijini Dar es Salaam leo.
Maneja Masoko wa Jumia Tanzania, Albany James akizungumza na waandishi wa habari kuhusu jinsi Kampuni ya Jumia Tanzania inavyoweza kurudisha imani kwa watanzania namna ya kununua bidhaa mtandaoni kwa kutumia mfumo wa malipo baada ya mteja kupokea bidhaa yake kwenye ofisi zao Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
↧
9 of 43 Tigo Biashara Yakutana na Wafanyabiashara Wakubwa Kuzindua Bidhaa Mpya Bidhaa na huduma za kipekee kuongeza ufanisi, ukuaji na faida kwa biashara.
Kaimu Meneja Mkuu wa Tigo, Simon Karikari akielezea jambo katika mkutano na waandishi wa habari katika uzinduzi wa huduma mpya za Tigo Business zinazowasadia wafanyabiasahra kuongeza ufanisi wa kazi zao. Kulia ni Afisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, Hugh Sonn.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Tigo, Hugh Sonn akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari kuzindua huduma mpya za Tigo Business zinazowasaidia wafanyabiashara kurahisisha mawasiliano na kuongeza ufanisi wa biashara zao. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari.
Meneja wa Biashara wa Tigo, David Sekwao akifafanua jambo katika mkutano na waandishi wa habari kuzindua huduma mpya za Tigo Business zinazowasaidia wafanyabiashara kurahisisha mawasiliano na kuongeza ufanisi wa biashara zao. Kushoto ni Mkuu wa Mauzo wa Tigo, Kadambara Maita.
↧
More Pages to Explore .....