Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

MKOA WA RUVUMA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA KUSOMESHA WANAFUNZI WA SAYANSI.

$
0
0
katika kuboresha huduma za afya mkoa wa ruvuma kupeleka wanafunzi wanaosomea masomo ya sayansi katika vyuo vya afya ili kuboresha huduma za afya mkoani hapo hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya songea POLOLETH MGEMA habri kamili hii hapa video yake  

SERIKALI YATUMIA BILIONI 85 KUPELEKA MAWASILIANO VIJIJINI

$
0
0
Serikali imesema kuwa imetumia shilingi Bilioni 85 kupeleka mawasiliano vijijini kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwa kuzipatia ruzuku kampuni za simu za mkononi ili kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata huduma za mawasiliano.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kwenye Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu mjini Dodoma.

“Mfuko huu unaendelea kuhakikisha kuwa mawasiliano bora yanafika katika maeneo mengi nchini hususan vijijini na kwenye maeneo ambayo hayana mvuto wa kibiashara ambapo Takwimu zinabainisha kuwa, tayari mawasiliano   yamefikishwa kwenye kata 443, vijiji 1,939  kuanzia mwezi Machi 2013 hadi Julai mwaka huu”, amefafanua Naibu Waziri Ngonyani.

Ameongeza kuwa tayari Mfuko umetiliana saini mkataba na kampuni za simu za mkononi mwezi Agosti mwaka huu kuhakikisha kuwa zinapeleka mawasiliano kwenye kata nyingine 75 na vijiji 154.

Aidha, ametanabaisha kuwa hadi hivi sasa asilimia 94 ya wananchi wanapata huduma ya mawasiliano nchini na kuongeza kuwa, Serikali kupitia mkataba wake na Kampuni ya Simu ya Halotel imefikisha mawasiliano kwenye jumla ya vijiji 3,069 kati ya vijiji 4,000 tangu walipoanza utekelezaji wa jukumu hilo mwezi Novemba, 2015 na wanatarajia kukamilisha kazi hiyo ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu Mhe. Moshi Kakoso, amezitaka kampuni za simu za mkononi zinazopeleka mawasiliano vijijini na maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara ambazo zinapatiwa ruzuku na Serikali kuhakikisha kuwa zinatoa taarifa sahihi kwa Mfuko huo ikiwemo hatua zilizofikiwa za ujenzi na usimikaji wa minara na uwepo wa mawasiliano kwenye vijiji husika.

 Amewataka UCSAF kujitangaza na kuweka mabango yao kwenye minara yote nchini iliyojengwa kupitia ruzuku ya Serikali ili kuwawezesha wananchi kutambua uwajibikaji wa Serikali katika kufikisha mawasiliano kwa wananchi wake.

Naye, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Eng. Angelina Madete, amesema kuwa Wizara kupitia UCSAF itahakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na mawasiliano kuendana na jukumu la msingi la Mfuko huo la kufikisha mawasiliano kwa wote.

Mtendaji Mkuu wa Mfuko huo Eng. Peter Ulanga, amewahakakikishia wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kuwa Taasisi yake itashirikiana na wataalam kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kuhakiki kazi zilizofanywa na kampuni za simu za mkononi za ujenzi na usimikaji wa minara na uwepo wa mawasiliano kwenye vijiji mbalimbali nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akifafanua jambo katika kikao na Kamati ya Bunge ya Miundombinu kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Moshi Kakoso na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano wa Wizara hiyo Eng. Angelina Madete. 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Eng. Angelina Madete akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu kuhusu miradi ya maendeleo ya mawasiliano vijijini katika kikao kilichofanyika mjini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Moshi Kasoso, akisisitiza jambo kwa wajumbe wa Kamati hiyo katika kikao kilichowakutanisha na uongozi wa Wizara ya  Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) mjini Dodoma. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Eng. Edwin Ngonyani.
Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Eng. Peter Ulanga akiwaonesha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu maeneo ya vijijini yaliyofikiwa na mawasiliano katika kikao na Kamati hiyo mjini Dodoma. Kulia ni Mhe. Dua Nkurua na kushoto ni Mhe. Rita Kabati wajumbe wa Kamati hiyo.


Sababu ya Eid al-Adha kuitwa ‘Sikukuu ya Kuchinja’

$
0
0

Na Jumia Travel Tanzania

Eid al-Adha ni miongoni mwa sikukuu kubwa kwa waumini wa dini ya Kiislamu ukiachana na Eid- al-Fitr inayosherehekewa kila mwaka duniani kote. Kwa mwaka huu sikukuu hii inatarajiwa kusherehekewa siku ya Ijumaa ya Septemba mosi ambapo kwa waumini wa dini hiyo ni kipindi cha kujitolea, kuonyesha ukarimu kwa marafiki, familia na watu wenye uhitaji.

Kama zilivyo sikukuu nyingine kuna baadhi ya watu huwa hawajui ni kwa nini huwa zinaseherehekewa namna zinavyosherehekewa. Jumia Travel kupitia makala haya imekukusanyia mambo ya msingi kuhusu maana ya sikukuu hii na namna ya kusherehekea.

Waislamu huisherekea sikukuu ya Eid al-Adha kwa kuchinja mnyama ikiwa ni kuheshimu kitendo alichokifanya Ibrahim au Abraham (anavyoitwa na Wakristu na Wayahudi). Ibrahim aliamriwa na Mungu kumtoa mtoto wake pekee kiume kama sadaka kwa kumchinja ambapo alikubali kutii amri hiyo bila ya kupinga. Kabla ya kumtoa sadaka mtoto wake sadaka, Mungu aliingilia kati kwa kumtuma Malaika wake ambaye altaka amchinje kondoo badala ya mtoto wake.

Katika kuadhimisha tukio hilo kubwa la kiimani, kila mwaka sikukuu hii inaposherehekewa waumini wa Kiislamu huchinja mnyama halali kwa mujibu wa imani. Mnyama huyo anaweza kuwa ni ng’ombe, ngamia, mbuzi au kondoo inategemea na uwezo wa mtu. Baada ya kuchinja, nyama hugawanywa katika mafungu matatu ambapo la kwanza hubakia kwa familia; la pili hugawiwa kwa ndugu, jamaa na marafiki; na kisha la tatu hugawiwa kwa watu masikini na wenye uhitaji.

Hivyo basi sikukuu hii husherehekewa kama ni ishara ya kukumbuka utiifu wa Ibrahim mbele ya Mungu lakini pia huashiria tamati ya safari ya Hijja. Kila mwaka Waislamu wote duniani huenda kuhiji mjini Macca uliopo nchini Saudi Arabia. Eid al-Adha ni tofauti na Eid al-Fitr ambayo yenyewe husherehekewa baada ya kuisha kwa mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhan.

Katika kalenda ya mwezi wa Kiislamu, sikukuu ya Eid al-Adha hutukia siku ya 10 ya mwezi wa 12 na hudumu kwa muda wa siku nne mpaka siku ya 13. Kwa mwaka huu itaanza siku ya Ijumaa ya Septemba mosi na kufikia ukomo siku ya Jumanne ya Septemba 5. Maadhimisho ya sikukuu hii hubailika kila mwaka kulingana na mabadiliko ya kalenda, hivyo haimaanishi mwaka ujao sherehe zitaangukia tarehe sawa na za mwaka huu.

Kama ilivyo kwa Eid al-Fitr, Waislamu huanza kusherehekea Eid al-Adha asubuhi kwa kwenda msikitini kwa ajili ya sala, kusikiliza mawaidha kisha kufuatiwa na kutakiana heri ya sikukuu pamoja na kugawiana zawadi. Baada ya hapo wanyama huchinjwa ikiwa ni sehemu ya sherehe na kisha nyama hugawiwa kwa ndugu, jamaa na marafiki ikiwemo masikini na watu wasio na uwezo. Lakini pia watu wenye uwezo huwagawia pesa watu masikini na wasio na uwezo ili nao waweze kusherehekea kwa furaha kama watu wengine.

Kwa mfano, kwenye mitaa mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ni rahisi kugundua kwamba ni sikukuu kutokana na shamrashamra zinavyoonekana. Mitaa, maduka, migahawa, sehemu za kutembelea kama vile fukwe ya bahari ya Hindi hufurika watu wakifanya manunuzi, kula chakula na kufurahia kwani mara nyingi huwa ni mapumziko ya kitaifa. Jumia Travel inaamini kwamba utakuwa umeelewa ni nini maana ya Eid al-Adha na namna inavyosherehekewa ili kutopoteza maana yake.


WAKUFUNZI WA WADADISI WA UTAFITI WA KILIMO NA MIFUGO WAPIGWA MSASA

$
0
0
Na: Veronica Kazimoto-Mororgoro.

Jumla ya wakufunzi 52 wakiwemo Mameneja Takwimu wa mikoa yote nchini wamepewa mafunzo juu ya mbinu mbalimbali zinazotumika kufundishia wadadisi kwa ajili ya kupata takwimu bora za kilimo na mifugo.

Mafunzo hayo ya wiki moja yanayoendelea kufanyika mkoani morogoro, yanalenga kuwajengea uwezo wakufunzi hao ili waweze kuwafundisha wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa Mwaka 2017 kwa ajili ya kupata takwimu rasmi zitakazotumika katika kupanga mipango ya maendeleo.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya amewataka wakufunzi wao kuzingatia kwa makini mafunzo hayo ili waweze kuwafundisha kwa ufanisi wadadisi wakaokusanya taarifa za utafiti huo wa kilimo na mifugo.

"Ili kuiwezesha nchi yetu kupata takwimu bora za kilimo na mifugo inatakiwa ninyi wakufunzi kuzingatia kwa makini mafunzo haya ili muweze kuwafundisha kwa ufanisi mkubwa wadadisi ambao watazunguka nchi nzima kukusanya takwimu za kilimo na mifugo", amesema Ruyobya.

Utafiti wa Kilimo na Mifugo hufanyika kila mwaka ambapo utafiti wa mwaka huu utafanyika kuanzia mwezi Oktoba, 2017 chini ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Viwanda na Biashara.
 Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Irenius Ruyobya akizungumza leo na Wakufunzi wa Wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017 wakati wa mafunzo ya wakufunzi hao yanayoendelea kufanyika mkoani Morogoro. Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017 unatarajia kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Oktoba, 2017.

 Mtalaamu wa Kilimo na Mifugo kutoka Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi, Zanzibar Mzee M. Mzee akiwafundisha Wakufunzi wa Wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017. Mafunzo ya wakufunzi hao yanafanyika mkoani Morogoro ambapo utafiti huo unatarajia kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Oktoba, 2017.

 Mmoja wa Wakufunzi akiuliza swali wakati wa mafunzo ya Wakufunzi wa Wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017 yanayofanyika mkoani Morogoro.  Utafiti huo wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017 unatarajia kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Oktoba, 2017.

 Baadhi ya Wakufunzi wakijifunza mbinu mbalimbali zitazotumika kuwafundishia Wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017. Mafunzo ya wakufunzi hao yanafanyika mkoani Morogoro ambapo utafiti huo unatarajia kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Oktoba, 2017.
Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Irenius Ruyobya akitoa maelekezo kwa waratibu wa mafunzo ya Wakufunzi wa Wadadisi wa Utafiti wa Kilimo na Mifugo wa mwaka 2017. Mafunzo ya Wakufunzi hao yanafanyika mkoani Morogoro na utafiti huo unatarajia kufanyika nchi nzima kuanzia mwezi Oktoba, 2017. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).

Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI yapungua nchini, Dr. Zekeng

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Suzan Kolimba (Mb) akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI (UNAIDS), Bw. Dr. Leo Zekeng ofisini kwake jijini Dar Es Salaam leo. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Zekeng alisifu jitihada zinazofanywa na Tanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ambazo zimesaidia kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 25 na pia idadi ya watoto wanaozaliwa na virusi vya ukimwi imepungua kwa kiasi kikubwa. Dkt. Zekeng alisema kuwa kutokana na mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Bi Michel Sidibe anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini mwezi Oktoba 2017 .
Dkt. Zekeng akionesha takwimu zilizopo katika ripoti ya UNAIDS zinazoonesha namna maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI yalivyopungua nchini Tanzania. 
Mazungumzo yanaendelea 
Mhe. Naibu Waziri akiagana na Dkt. Zekeng baada ya kukamilisha mazungumzo yao 
Picha ya pamoja

WASANII NGULI NCHINI KUPIMANA MABAVU DIMBA CONCERT TRAVELNTINE MAGOMENI

$
0
0
 Meneja Tukio wa Tamasha la Dimba Concert , Mwani Nyangasa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya Tamasha litakalo wakutanisha Wakongwe wa Muziki wa Dansi nchini na bendi ya Msondo Ngoma katika ukumbi wa Traventine September 2 mwaka huu kwa kiingilio cha shilingi 10,000 na 20,000 kwa VIP.
 Mwenyekiti wa kamati ya Maandalizi Tamasha la Dimba Concert , Jimmy Chika akifafnua namna bendi hizo zitkavyotoa burudani kwa mashabiki na wadau wa Muziki wa dansi watakaofika katika ukumbi wa traventine siku ya Jumamosi
 Msanii wa Mkongwe wa Muziki wa dansi nchini, Husein Jumbe akiwatoa hofu Mashabiki wake kuwa muziki wao bado upo juu
 Mwanamuziki wa Mkongwe wa Double M Sound ,  Mwinyjuma Muumini akijigamba kwa tambo kuwa siku hiyo patachimbika kwa hiyo mashabiki wote wasikose kuhudhuria Tamasha hilo
 Mpiga gitaa la solo wa siku nyingi , Adolf Mbinga akionesha namna atakavyocharaza nyuzi siku ya Tamasha la Dimba Concert siku ya jumamosi
 Mwanamuziki Juma Kakere akieleza namna watakavyoweza kukonga nyoyo za Mashabiki kupitia nyimbo zake kadhaa ambazo ziliweza kutamba
 Rais wa Vijana wa Muziki wa Dansi nchini , Nyoshi Elsadat akieleza namna atakavyoweza kutoa burudani kwa wadau wa muziki wa Dansi na Mashabiki watakaofika siku hiyo
 Wanamuziki wakongwe wakiwa katika mazoezi yao wakionyesha namna watakavyoimba siku ya Dimba Concert  siku ya Jumamosi
 Rais wa Vijana wa Muziki wa Dansi nchini , Nyoshi Elsadat akiimba mbele ya waandishi wa habari namna atakavyofanya siku ya Dimba Concert itakayofanyika Sept 2 mwka huu katika ukumbi wa Traventine Magomeni

Na Agness Francis,Globu ya Jamii.

Wanamuziki wakongwe wa Muziki wa Dansi nchini wametambiana kuoneshana uwezo wa kuimba siku ya Tamasha la Dimba Concert litakalofanyika katika ukumbi wa Traventine Magomeni Septemba 2 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja tukio tamasha la  Dimba Concert,Mwani Nyangasa amesema kuwa maandalizi ya tamasha hilo yamekamilika kwa  Taifa muziki bendi kupambana na wanamuziki nguli wa Bendi ya Msondo ngoma.

“ Dhumuni la tamasha hili ni  kuendeleza muziki wa dansi hapa  nchini  kwa kutumia wasanii hawa wakongwe ili waweze kuonesha vijana,wapenzi na wadau kuwa muziki huu bado upo hai.” Amesema  Nyangasa.

 Nae msanii nguli nchini Hussen Jumbe ametanabaisha kuwa wadau na mashabiki wa muziki huo wafike kwa wingi siku hiyo pale Traveltine  septemba 2 mwaka huu ili kupata radha halisi ya muziki wa dansi.

Kwa upande wake  raisi wa vijana  sauti ya simba Nyoshi El Saadat, amewaomba mashabiki wa muziki huo kufika  kwenye tamasha hilo  na kuwaahidi kutowaangusha na kuwapa burudani ya kukata na shoka.

MAHAKAMA YAKATAA KUPOKEA VIPISI VIWILI VYA BANGI.

$
0
0
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu mapema leo imekataa  kupokea msokoto na vipisi viwili vya bangi vilivyotolewa na upande wa mashtaka kama vielelezo vya ushahidi dhidi ya tuhuma za matumizi ya dawa za kulevya imayomkabili Wema Sepetu na wenzake.

Uamuzi huo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba ambaye amesema mahakama haiwezi kupokea vielelezo hivyo kwa sababu vina kasoro.

Akitoa uamuzi wake amesema anakubaliana na hoja zilizotolewa  na upande wa mashtaka kwamba msokoto wa bangi na vipisi hivyo vina kasoro kwa kuwa shahidi hakuvifafanua mahakamani.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi September 12/2017.
Msanii wa Filamu hapa nchini na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akiwa na Wakili wake Peter Kibatara  wakiingia katika mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kwaajili ya kusikiliza mashtaka yanayo mkabili ya kutuhumiwa kutumia dawa za kulevya.
 Msanii wa Filamu hapa nchini na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri kusomewa mashtaka yanayomkabili jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Wakili Peter Kibatara na Kushoto ni Mama wa Wema Sepetu.
 Msanii wa Filamu hapa nchini na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akiwa na wafuasi wake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo wakati wakisubiri kusomewa Mashtaka yanayomkabili.
 Msanii wa Filamu hapa nchini na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu akiwa nche ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kusomewa mashtaka yanayo Mkabiri.
 Msanii wa Filamu hapa nchini na Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu  akiwa na wakili wake Peter Kibatara wakiwa nje ya Mahakama ja Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI NCHINI KUFANYIKA MKOANI DODOMA

$
0
0
 Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Mhandisi Patrick Barozi (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati akieleza juu ya maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 7 hadi 8 mwezi Septemba.
Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Mhandisi Patrick Barozi (kushoto) akionesha kwa waandishi wa habari picha yenye mashine ya kushindilia barabara ambayo imegunduliwa na wahandisi wa hapa nchini na kupewa jina la Magufuli One, kulia ni Msajili Msaidizi wa bodi hiyo, Mhandisi Benedict Mukama .
Msajili Msaidizi wa Bodi ya Usajili wa Wahandisi, Mhandisi Benedict Mukama  (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akieleza juu ya maadhimisho ya Siku ya Wahandisi nchini ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Dodoma kuanzia tarehe 7 hadi 8 mwezi Septemba, kushoto ni Kaimu Msajili wa bodi hiyo, Mhandisi Patrick Barozi.
Picha na Eliphace Marwa - MAELEZO


MWIGULU AFUNGUA KIKAO CHA KUJADILI UREJESHAJI WA WAKIMBIZI WA BURUNDI WALIO TAYARI KUREJEA NCHINI KWAO

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani na Elimu ya Uzalendo kutoka nchini Burundi, Pascal Barandagiye, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi, ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi  Duniani (UNHCR) nchini Tanzania,Chansa Kapaya, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akipitia nyaraka mbalimbali wakatiKikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi,Harrison mseke.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba(watano kulia), Waziri wa Mambo ya Ndani na Elimu ya Uzalendo kutoka nchini Burundi, Pascal Barandagiye, (wasita kulia), na Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi  Duniani (UNHCR) nchini Tanzania,Chansa Kapaya(wanne kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kikao cha 19 kinachoshirikisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani(UNHCR),lengo ni kujadili na kuwekeana makubaliano juu ya Mpango wa Kuwarejesha Wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ambao wako tayari kurejea nchini kwao.Kikao hicho kimefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere,jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WATAKIWA KUFANYA KAZI ZAO KWA UFANISI

$
0
0
Na Mwandishi Maalum.

31/08/2017 Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa kufanya kazi kwa kujituma, kuongeza ufanisi na kutoa huduma bora kwa wagonjwa ili epukana na malalamiko yanayoweza kujitokeza.

Rai hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi wakati akizungumza katika kikao cha wafanyakazi kilichofanyika jijini Dar es Salaam.

Prof. Janabi pia aliwahimiza wafanyakazi wa Taasisi hiyo kuendelea kutunza vizuri kumbukumbu mbalimbali zikiwemo za wagonjwa na utendaji wa kazi zao za kila siku ili pale zitakapohitajika zipatikane kwa haraka.

“Mjitahidi kujaza fomu ya wazi ya mapitio na upimaji utendaji kazi (OPRAS) kwa wakati ili kusiwe na malalamiko ya upandaji wa vyeo kwani ujazaji wa fomu hizo ndiyo unaowezesha mfanyakazi kupimwa utendaji wake kwa kipindi cha mwaka mzima”, alihimiza Mkurugenzi Mtendaji huyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Godfrey Tamba aliupongeza uongozi wa Taasisi hiyo kwa kazi wanayoifanya ya kuhakikisha wafanyakazi wanafanya kazi zao katika mazingira bora.

Tamba alisisitiza, “Wafanyakazi wenzangu tunaodai haki zetu tukumbuke kutimiza wajibu wetu wa kazi kwa wakati, kwani uongozi wa TUGHE hautawatetea watu ambao hawatimizi wajibu wao ipasavyo”.

Hiki ni kikao cha pili cha wafanyakazi wote kufanyika tangu kuanza kwa mwaka huu ambapo katika kikao hicho mambo mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja na kuongeza ufanisi katika utendaji wa kazi.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA VIONGOZI MBALIMBALI WA ULINZI NA USALAMA WASASA NA WASTAAFU IKULU JIJINI DAR

$
0
0


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika chumba cha Mkutano kwa ajili ya kuzungumza na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya mazungumzo yao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, Omar Mahita(IGP Mstaafu), Said Mwema(IGP Mstaafu) pamoja na Ernest Mangu(IGP Mstaafu) Ikulu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Omar Mahita Ikulu jijini Dar es Salaam.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika chumba cha mkutano kwa ajili ya kuzungumza na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwakaribisha  viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na  viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu wakisimama kwa heshima kuomboleza msiba wa baba wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Mstaafu Jenerali  George Waitara wakati  alipokutana nao Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiendelea kuzungumza na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja  na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya mazungumzo yao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja  na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo pamoja na wakuu wastaafu wa Jeshi hilo Jenerali Mirisho Sarakikya (wa pili kushoto), Jenerali Davis Mwamunyange (kulia) na Jenerali  Robert Mboma (wa pili kulia) alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam mara baada ya mazungumzo yao.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Mirisho Sarakikya alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi mstaafu Jenerali Robert Mboma alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  mstaafu Jenerali Davis Mwamunyange alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro pamoja na IGP wastafu Omari Mahita, Saidi Mwem na Ernest Mangu alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Omari Mahita alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Saidi Mwema alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Ernest Mangu alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Kamishna Jenerali  wa Jeshi la Magereza Dkt Juma Malewa (kushoto) pamoja na Wakuu wa jeshi hilo wastaafu Simon Mwanguku (wa pili kushoto), Nicas Banzi (wa tatu kulia) Augostino Nanyaro na  John Casmir Minja (kulia) alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza Mstaafu Simon Mwanguku alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza Mstaafu Nicas Banzi alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza Mstaafu Augostino Nanyaro alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Kamishna Mkuu wa Jeshi la Magereza Mstaafu John Casmir Minja alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt.  Modestus Kapilimba (kushoto) pamoja na Wakurugenzi Wakuu wastaafu Cornel Apson (wa pili kushoto) na Kulia Rashid Othman alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa mstaafu Cornel Apson  alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt. Modestus Kapilimba  alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa mstaafu Rashid Othman  alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dkt Anna Peter Makakala (kushoto) na Kamishna Mkuu wa Uhamiaji Mstaafu Kinemo Kihomano alipokutana na Viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (kulia) na Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi hilo Mhandisi Pius Nyambacha alipokutana na Viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Kamishna Jenerali mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Mhandisi Pius Nyambacha alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na  Kamishna jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Omari Mahita alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na  Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa mstaafu Cornel Apson  alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wasasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Saidi Mwema akibadilishana mawazo wa Mkuu wa Jeshi la Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo (kulia), Kamishna Jenerali wa Magereza Dkt. Juma Malewa (wa pili kulia) na Kamishna Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala 
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Wakuu wa Jeshi la Polisi wastaafu Saidi Mwema na Omari Mahita alipokutana na viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Saidi Mwema akiongea na wanahabari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi baada ya kukutana na  viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wa sasa na wastaafu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Agosti 31, 2017. Picha zote na  IKULU

POLEPOLE: TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA LONGIDO

$
0
0
Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
Aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Longido kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt Steven Kiruswa akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Chama cha Mapinduzi kimesema kuwa kipo tayari kuingia katika uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Longido Mkoani Arusha mara baada ya kutangazwa kuwa jimbo hilo lipo wazi kutokana na maamuzi ya mahakama ya Rufaa iliyobainisha kuwa uchaguzi wa mwaka 2015 haukuwa huru na haki hivyo kufuta matokeo ya uchaguzi huo.

CCM imeeleza kuwa kulikuwa na matumizi yasiyostahili kutumika kujazwa matokeo ya Ubunge, kwa kutumia fomu namba 21c za kujaza matokeo ya Udiwani na kujaza matokeo ya Ubunge, badala ya kutumia fomu namba 21b jambo lililopelekea kufungua kesi ya kupinga ushindi wa Ubunge katika Jimbo hilo.

Kauli ya CCM imetolewa na Katibu Wa Halmashauri Kuu Ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Polepole alisema kuwa vipo vyama vya siasa ambavyo kwa kawaida hulalamika kila vinaposikia kushindwa na mahakama kwa madai kuwa hakuna haki lakini vyama hivyo kila vinaposhinda vyenyewe husema mahakama imetenda haki.

Alisema kuwa kazi ya mahakama ni kutumia sheria zilizopo na kuamua juu ya malalamiko ya wananchi kwa kuhakikisha usawa mbele ya sheria kwa watu wote unatendeka hivyo maamuzi yaliyotolewa juu ya kuwa wazi kwa Jimbo la longido ni sehemu ya maamuzi huru na haki kwa mahakama ya Rufaa nchini.

Polepole alitoa Rai kwa mahakama zote nchini kuendelea kufanya kazi yake vizuri kwa uhuru na haki pasina kusikiliza kelele za watu wanaotaka mahakama kutekeleza matakwa yao kinyume na sheria za nchi.

Kwa upande wake aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Longido kupitia Chama Cha Mapinduzi Dkt Steven Kiruswa akizungumza katika mkutano huo na waandishi wa habari alisema kuwa pamoja na mapingamizi ya mara kwa mara katika kipindi chote tangu rufaa ilipoanza kusikilizwa aliamua kuwa mtulivu kwa kusubiri maamuzi yatakayotolewa na mahakama kama chombo huru nchini cha maamuzi.

Alisema kuwa kwa mara ya nne mahakama ya Tanzania imethibitisha kuwa inaongozwa kwa mujibu wa sheria na kujali haki ya mwenye haki ili isipotee bure.

Alisema CCM ilifungua kesi mwanzoni mwa mwezi Novemba 2015 ikiwa ni wiki mbili tangu kumalizika uchaguzi mkuu uliofanyika Octoba 25, 2015 ambapo mahakama kuu ya Arusha ilibaini kwamba uchaguzi haukuwa huru na haki na kufikia June 29, 2016 hukumu ikatolewa na ubunge kutenguliwa jambo ambalo liliwafanya Chadema kukata rufaa zaidi ya mara tatu.

Dkt Kiruswa alisema kuwa wananchi wa Longido wamenyanyasika katika kipindi cha miaka miwili pasina kuwa na muwakilishi wa kuwasemea bungeni hivyo maamuzi ya mahakama yataifanya Tume ya Uchaguzi kutangaza rasmi uchaguzi mdogo na hatimaye muwakilishi kupatikana kwa kura za haki.

Aidha, Polepole alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi katika muktadha wa CCM mpya Tanzania Mpya kinaendelea kusisitiza siasa safi na kutoa uongozi bora.

Alisema siasa za kutumia lugha isiyofaa, na Siasa za aina yoyote zenye mtazamo wa fitina hazina nafasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi katika kipindi hiki ambacho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe Dkt John Pombe Magufuli anaongoza kwani amedhamiria CCM kuwa chama cha wananchi wote chenye mtazamo chanya katika uwajibikaji.

Alitoa Rai kwa vyama vingine nchini kufanya siasa za weledi pasina kutumia lugha za kuudhi dhidi ya serikali na wananchi wake huku akiahidi kuwa chama chake hakiwezi kupoteza muda kujibu porojo za hila kwani kitakuwa hakitendi haki katika kuisimamia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015-2020 kwa kuwaletea maendeleo endelevu wananchi.

Polepole alisema kuwa CCM inaamini katika majibizano ya hoja kwani chama hicho kina deni kubwa kwa wananchi la kuwaletea maendeleo hivyo viongozi wote wa chama na wale wenye dhamana katika dola kuendelea kuishi misingi ya CCM Mpya ya Uadilifu, Uaminifu, Uchapakazi, Vita dhidi ya Rushwa, Vita dhidi ya ubadhilifu wa mali za chama na mali za Umma, Unyenyekevu na kusikiliza watu.

MAENDELEO BANK YAWAZAWADIA WATEJA WAKE VIWANJA ,MABATI NA SARUJI

$
0
0
Maendeleo Bank leo imechezesha droo yake ya kwanza iliyotokana na kampeni ya Maendeleo Pamoja na Wewe iliyozinduliwa rasmi mwanzoni mwa mwezi Agosti 2017.
Promosheni hiyo ina malengo kadhaa;Kuwaweka wateja wake karibu kwa kutumia huduma mbalimbali za Maendeleo Bank Kuwajengea watanzania utaratibu wa kuweka akiba kwa njia ya kibenkiKukuza utamaduni wa kujiwekea malengo ya muda mfupi na mrefu kwa kuweka fedha kidogo kidogo katika akaunti ya WEKEZA ili kufanikisha malengo yao.
Kuwajengea wazazi utamaduni wa kuwawekea watoto wao akiba
Mkuu wa Idara ya Fedha wa benki hiyo Bw. Peter Tarimo alisema “Draw yetu ya Maendeleo Pamoja na Wewe awamu ya kwanza inahitimishwa leo kwa kuchezesha draw ambayo itatupatia washindi mbalimbali ikiwemo tani za simenti, kiwanja, mabati na ada ya shule”.
Draw hiyo imeibua washindi wane (4) ambao walishinda kiwanja, mabati 64 ,tani 3 za simenti pamoja na ada ya shule na kushudiwa na mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini Bw. Bakari Maggid.
Promosheni ya Maendeleo Pamoja na Wewe inasitishwa kwa sasa kupisha zoezi za uuzaji wa hisa za Maendeleo Bank na itaendeleo mara baada ya kuhitimisha uuzaji wa hisa za benki hiyo.
Mkuu wa Tehama na Uendeshaji Bw. George Wandwalo akibonyeza kitufe kuashiria kuanza kwa droo iliyomuibua mshindi wa kiwanja Bi. Dora Olotu katika droo iliyochezeshwa leo jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Bw. Bakari Maggid
Mkuu wa Tehama na Uendeshaji Bw. George Wandwalo akizungumza na mteja wa Maendeleo Bank kwa njia ya simu baada ya kuibuka kama mmoja wa washindi waliopatikana katika droo iliyoashiria kumalizika kwa awamu ya kwanza ya promosheni ya Maendeleo Pamoja na Wewe.C:\Users\EAG Group\Desktop\PRESS MAENDELEO BANK AUG 31 2017\1T4A9121.JPG
Mkuu wa Kitengo cha Fedha Bw. Peter Tarimo akizungumza na waandishi wa habari juu ya shindano na promosheni ya Maendeleo Pamoja na Wewe kabla ya kuanza kwa droo hiyo Dar es Salaam leo.

UJUMBE WA CPC ULIPOKUTANA NA MANGULA DAR NA ULIPOTEMBELEA ENEO LA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA SIASA CHA MWALIMU NYERERE, KIBAHA

$
0
0
Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole.
 Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Humphrey Polepole akiwa tayari kumpokea Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017.
 Katibu wa NEC, Iikadi na Uenezi Humphrey Polepole akimlaki Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Kulia ni Katibu wa NEC Siasa na Uhuisnao wa Kimataifa kanali Mstaafu Ngemela Lubinga
 TWENDE HUKU, Lubinga akionyesha njia ya kwenda mgeni huyo
Lubinga na Polepole wakimuongoza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, kwenda kukutana na Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017.
 Mgeni akiwa na Polepole
 Polepole akiendelea kumuongoza mgeni huyo
 Makamu Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimsubiri kwa hamu mgeni huyo
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje
wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya
CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi
Humphrey Polepole.
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula akimkaribisha Naibu Waziri za Mambo ya Nje
wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya
CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017. Katikati ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi
Humphrey Polepole
 Mzee Mangula na Mgeni wakiingia ukumbi wa mazungumzo
 Mangula na Lubinga wakiwaonyesha wageni eneo la kuketi kwa ajili ya kuanza mazungumzo
 Karibuni jamani wageni wetu. Mzee Mangula akimwambia mgeni kutoka Ubalozi wa China aliyeambatana na Naibu Waziri huyo wa CPC
 Ujumbe wa CPC kwenye mazungumzo
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017

 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akiongoza mazungumzo  baina yake na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Ujumbe wa CCM kwenye mazungumzo hayo
 Maofisa wa CCM kwenye mazungumzo hayo
 Maofisa wa CCM kwenye mazungumzo hayo 
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akimkabidhi zawadi maalum Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Makamau Mwenyekiti wa CCM-Bara Philip Mangula (kulia) akizawadiwa na Naibu Waziri za Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) Xu Luping (kulia) katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam, leo Agosti 31, 2017
 Mangula akizifurahia zawadi hizo
 Akimshuku kwa zawadi



 Mangula akimsindikiza mgeni wake. Kushoto ni Polepole na kulia ni Lubinga
 Byeee na karibu tena, Mangula akimuaga mgeni kabla ya mgeni huyo kuondoka rasmi kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. PICHA NYINGI ZAIDI/>BOFYA HAPA

MAMIA WAMIMINIKA KUJISAJILI KATIKA MFUKO WA FIDIA (WCF) IKIWA UTEKELEZAJI WA AGIZO LA WAZIRI JENISTA MHAGAMA

$
0
0
Meneja Matekelezo  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Bw.Victor Luvena, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na kulipa michango leo Agosti 31, 2017.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MUITIKIO wa waajiri kujisajili na kulipa michango katika Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF) umekuwa wa kuridhisha hususani Mwezi Agosti, Meneja Matekelezo Bw. Victor Luvena amesema leo Agosti 31, 2017.
Itakumbukwa ya kwamba, tarehe 23 Julai 2017 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama (Mb), alitoa siku 30 kwa waajiri wote nchini ambao walikuwa hawajasajili kuhakikisha wanajisajili katika Mfuko na wanawasilisha michango kwa wakati, vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao na kama Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi inavyoelekeza.
“Kwakweli tunamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa agizo alilolitoa kwani limetoa msukumo mkubwa, waajiri wengi wamejitokeza kutekeleza wajibu wao wa kisheria wa kujisajili na kuwasilisha michango katika Mfuko.” Alisema Bw. Luvena.
K-VIS Blog ilishuhudia idadi kubwa ya waajiri wakiwa wamejitokeza leo Agosti 31, 2017 ambayo ndiyo siku ya mwisho kwa waajiri kutekeleza agizo la Mheshimiwa waziri, wakiwa wamejazana kwenye ofisi za WCF  kujisajili na kuwasilisha michango, ambapo kazi hiyo ya kuwahudumia ilikuwa ikiongozwa na Meneja Matekelezo - WCF, Bw.Victor Ruvena.
 Waajiri, wakihudumiwa na maafisa wa WCF, leo Agosti 31, 2017.

 Afisa Matekelezo wa WCF, Bi. Gladness Madembwe, (kulia), akimkabidhi cheti cha usajili Bw.Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refregerator ya jijini Dar es Salaam.
 Afisa Matekelezo wa WCF, Bw.Edward Kerenge, (kushoto), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo wa WCF, Bw.Edward Kerenge, (kulia), akiwahudumia waajiri waliofika kujisajili na Mfuko leo Agosti 31, 2017.
 Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Bi.Emiliana J.Gwagilo, akimsikiliza Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo Msaidizi wa WCF, Bi.Emiliana J.Gwagilo, (kushoto), akimuhudumia Mwajiri huyu aliyefika kupatiwa huduma leo Agosti 31, 2017.
  Afisa Matekelezo wa WCF, Bi. Gladness Madembwe,(kushoto), akimuhudumia Bw. Sultani Ali kutoka kampuni ya Marifas Refrigeration, ya jijini Dar es Salaam.
 Meneja Matekelezo  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Bw.Victor Luvena, (kulia), akiwasikiliza waajiri waliofika leo Agosti 31, 2017 ili kupatiwa huduma ya usajili na uwasilishaji michango katika Mfuko huo.
 Maafisa wa WCF (kulia), wakimsikiliza Mama huyu mwajiri aliyefika kupatiwa huduma.




BANDARI KAVU YA KWALA –VIGWAZA KUANZA KUTUMIKA JANUARI MWAKANI

$
0
0
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kushoto), akifafanua jambo wakati akikagua mchoro wa Bandari kavu ya Kwala –Vigwaza Mkoani Pwani.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa (wa pili kulia), akitoa maelekezo kwa Eng. Charles Salu Ogare anayesimamia ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza Mkoani Pwani.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Eng. Deusdedit Kakoko akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa alipokagua maendeleo ya ujenzi wa bandari kavu ya Kwala –Vigwaza Mkoani Pwani.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasilino, Profesa Makame Mbarawa mwenye kofia ya njano akiwa katika majukumu ya ukaguzi wa ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza inayojengwa mkoani Pwani.
Muonekano wa bandari kavu inayojengwa na mkandarasi Suma-KJT katika eneo la Kwala-Vigwaza inayotarajiwa kuanza kutumika Januari mwakani ikiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini , Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ameelezea kuridhishwa kwake na kasi ya ujenzi wa bandari kavu katika eneo la Kwala Vigwaza Mkoani Pwani na kumtaka mkandarasi Suma JKT kuongeza kasi na kuzingatia ubora.

Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi huo ameiagiza Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), kushirikiana na Shirika la Reli Tanzania (TRL) na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) kuhakikisha wanaunganisha kwa haraka ili reli na barabara zinazoingia katika bandari kavu hiyo zinakamilika na hivyo kuiwezesha bandari kavu hiyo kuanza kutumika ifikapo Januari mwakani.

“TPA, TRL na TANROADS uzuri wote mko kwenye wizara moja shirikianeni na hakikisheni kilomita 15 za barabara inayoingia kwenye bandari kavu hii na kilomita moja ya reli zinajengwa haraka,” Amesema Profesa Mbarawa.

Profesa Mbarawa amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eng. Deusdedit Kakoko kuhakikisha ujenzi wa bandari kavu ya Kwala-Vigwaza unazingatia ubora na viwango vilivyopo katika mkataba ili kuiwezesha kuhudumia zaidi ya makontena milioni moja kwa mwaka na hivyo kupunguza msongamano katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

“Hakikisheni eneo la bandari kavu linakuwa na maegesho ya kutosha, taa, maji ya uhakika, gari la zimamoto, uzio na mashine ya ukaguzi wa mizigo scanner itakayowezesha kupima kila mzigo unaopandishwa na kushushwa katika eneo hili,” amesisitiza Profesa Mbarawa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA Eng. Kakoko amesema TPA imejipanga kuhakikisha ujenzi huo unatumia gharama nafuu na mifumo yote ya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA inakuwepo katika bandari hiyo ili kuiwezesaha kufanya kazi kisasa na kwa ufanisi zaidi.

“Tukifanikiwa kuhamia hapa mzigo uliokuwa unasafirishwa kwa siku saba sasa utatumia siku tatu kufika Mwanza hali itakayovutia wasafirishaji wengi kutumia bandari ya Dar es Salaam na hivyo kukuza uchumi wa nchi na kuibua fursa za ajira,” amesema Eng. Kakoko.

Bandari Kavu ya Kwala –Vigwaza inayojengwa na Mkandarasi SUMA JKT ambapo takribani kiasi cha shilingi bilioni 9 kinatarajiwa kutumika katika ujenzi huo ili kuboresha huduma za usafirishaji katika bandari ya Dar es Saalaam ambapo zaidi ya hekta 500 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi huo ambapo kwa kuanza hekta 120 sawa asilimia 24 zinajengwa katika awamu ya kwanza.

MAAFISA WA WIZARA YA USHIRIKIANO WA MAENDELEO YA UJERUMANI WATEMBELEA MAHAKAMA YA AFRIKA

$
0
0
Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR)Sukhdev Chatbar(kulia)akiwaongoza wageni kutoka Wizara ya ushirikiano wa maendeleo ya Ujerumani kupitia taasisi zake GIZ na AGA waliotembelea mahakama hiyo wamekua ni wadau wakubwa katika kusaidia miradi mbalimbali ya mahakama hiyo.
Mkutubi wa Maktaba ya mahakama hiyo,Revina Moshi akizungumza na maafisa kutoka
shirika la maendeleo ya kimataifa ya Ujerumani(GIZ),kutoka kushoto ni Afisa wa Wizara ya maendeleo ya Ujerumani anayehusika na Umoja wa Afrika(AU) ofisi ya Addis Ababa,Ethiopia,Barbara Schaefer,Janina Hasse kutoka Berlin,Mkuu wa taasisi za GIZ na AGA,Hartmut Krebs 
Mkuu wa taasisi za GIZ na AGA,Hartmut Krebs akiangalia sehemu ya machapisho kwenye maktaba ya AfCHPR. 
Msajiliwa mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR),Dk Robert Enno(kulia)akizungumza na ujumbe kutoka taasisi za Wizara ya maendeleo ya Ujerumani waliotembelea mahakama hiyo. 
Msajili wa mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu(AfCHPR),Dk Robert Enno akimkabidhi zawadi  Afisa wa Wizara ya maendeleo ya Ujerumani anayehusika na Umoja wa Afrika(AU) ofisi ya Ethiopia,Barbara Schaefer. 

MH. UMMY MWALIMU ANAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA

DKT PALLANGYO AKUTANA NA KAMPUNI YA M & P EXPLORATION PRODUCTION TANZANIA LIMITED

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akiongoza kikao kilichoshirikisha watendaji kutoka Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited, Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akizungumza na Meneja Mkuu kutoka Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited, Christophe Maitre ( kushoto) katika kikao hicho.
Sehemu ya watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (hayupo pichani) katika kikao hicho


…………………..


Leo Agosti 31, 2017 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo amekutana na Kampuni inayojihusisha na utafiti na uchimbaji wa gesi ya M & P Exploration Production Tanzania Limited kwenye Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini zilizopo jijini Dar es Salaam lengo likiwa ni kujadili namna ya kuendeleza gesi ya Mnazi Bay. Kikao hicho pia kilishirikisha watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)

WANANCHI WAONDOLEWA WASIWASI KUHUSU FIDIA YA MALI ZAO ZITAKAZOPITIWA NA BOMBA LA MAFUTA

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo akizungumza katika kikao na wataalamu watakaofanya uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mthamini wa ardhi kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Chiku Mkina (aliyevaa miwani) na wataalaamu wengine wakisikiliza kwa makini mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi akichangia mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.
Mkurugenzi wa kampuni ya Dighy Welly Dkt Jan Perold akiwasilisha mada katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mwakilishi wa Serikali katika zoezi la Uthamini kutoka Wizara ya Nishati na Madini Linus Kinyondo akizungumza na wataalamu wa mkoa wa Singida katika kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


Mhandisi wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Simwela Nuru Martin akifuatilia kwa makini kikao kilichohusu uthamini wa mali na ardhi kwa ajili ya fidia katika mradi wa bomba la mafuta la Kutoka Uganda hadi Tanga.


…………………….


Wananchi Mkoani Singida wameondolewa wasiwasi kuhusu fidia ya mali au ardhi yao ambayo itapitiwa na mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga kwakuwa hawatapunjwa bali itazingatia vigezo vya kimataifa na kitaifa.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Elias Tarimo amesema hayo mapema leo wakati wa kikao na wataalamu wanaofanya uthamini wa mali na ardhi ambayo itapitiwa na mradi huo.

Tarimo amesema wananchi na taasisi zote wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutaja gharama kulingana na thamani halisi ya mali zao na sio kuongeza gharama za juu kwakuwa vigezo vya kitaifa na kimataifa vitazingatiwa.

“wananchi wengine wasio waaminifu wananweza wakataja pesa kubwa au hata kuvamia maeneo ambayo siyo yao ilimradi wapate tu pesa, nawasihi wasifanye hivyo kwakua watakuwa wanakwamisha mradi huu muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu na majirani zetu Uganda”, amesema na kuongeza kuwa

“ Tunampongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John P Magufuli kwa kuhakikisha nchi yetu inapata mradi huu, tutoe ushirikiano wa kutosha ili mradi ufanikiwe kw kiwango kikubwa hasa kwa maeneo yote utakapopita kwa Mkoa wa Singida”, amesisitiza.

Tarimo ameongeza kuwa serikali ya Mkoa, wilaya, taasisi na wananchi wote wa Singida wamekuwa mstari wa mbele kutoa ushirikiano kwa miradi yote ya kitaifana kimataifa na hivyo basi wataalamu wanaofanya uthamini na wale watakaokuja kujenga wasiwe na wasiwasi wowote.

Ameongeza kuwa wananchina taasisi ziko tayari kunufaika na mradi huo kupita Mkoani Singida kwa kupata ajira za muda mfupi na mrefu, kufanya biashara pamoja na kutoa huduma mbalimbali.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt Angelina M Lutambi amewataka wataalmau hao kushirikiana na wataalamau wa ngazi zote kuanzia mkoa hadi vijiji ili zoezi la uthamini liende vizuri.

Dkt Lutambi amesema lengo la uthamini ni kuhakikisha wananchi hawapati madhara makubwa kutokana na kupita kwa mradi huo katika maeneo hayo pamoja na kuhakikisha sheria, miongozo na taratibu zote zinafuatwa.

Ameongeza kuwa wataalamu wanapaswa kuwa wazi kwa kushirikisha taasisi na mashirika ambayo kwa namna moja au nyingine yataguswa na mradi huo pamoja na kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kwa wote wanaohusika.

Wakichangia mada katika kikao hicho wataalamu kutoka Mkoa wa Singida wamesema uthamini uangalie athari zote ambazo zinaweza kutokea kutokana na mradi huo mfano athari ya kisaikolojia ya usumbufu wa kumhamisha mtu kutoka katika makazi yake pamoja na thari za maeneo kama vyanzo vya maji ambapo bomba litapita.
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images