Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live

RAIS KIKWETE NA MARAIS WASTAAFU MZEE MWINYI NA MZEE MKAPA WAALIKWA FUTARI KWA KATIBU MKUU KIONGOZI

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjmani William Mkapa na Rais wa Awamu ya nne Alhaj Ali Hassan Mwinyi wakati wa futari iliyoandaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (wa pili kushoto) nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam Jumapili.
 Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefua akimshukuru Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjmani William Mkapa na Rais wa Awamu ya nne Alhaj Ali Hassan Mwinyi kwa kuhudhuruia  futari aliyoaiandaa nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam Jumapili
 Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Alhaj Alhad akiongoza dua kwa waalikwa waliohudhuyruia  futari aliyoaiandaa nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam Jumapili
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjmani William Mkapa na Rais wa Awamu ya nne Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada ya  futari iliyoandaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue Oysterbay jijini Dar es salaam Jumapili. 

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe Benjmani William Mkapa na Rais wa Awamu ya nne Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada ya  futari iliyoandaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (kushoto) nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es salaam Jumapili. CHA NA IKULU

NAPE: SIYO KILA MABADILIKO YANA FAIDA

$
0
0

NAPE NNAUYE
MWANZA, Tanzania .

KATIBU wa NEC, Itikadi na Uenezi, CCM, Nape Nnauye amesema japokuwa mabadiliko ni muhimu kwa maisha ya binadamu lakini lazima kila yanapohitajika yafanywe kwa umakini mkubwa ili yasiwe na madhara.

Amesema ni kutokana na sababu hiyo, ndiyo maana CCM imekuwa ikisisitiza umakini na busara kubwa vitumike wakati huu ambao Tanzania ipo katika mchakato wa kupata katiba mpya.

Nape amesema miongoni mwa mambo ambayo CCM inaona kwamba lazima yatazamwe kwa umakini na busara kubwa kabla ya hatua ya mwisho, ni kuhusu Tanzania kuwa na serikali ngapi, ambapo rasimu ya kwanza ya Katiba inapendekeza serikali tatu.

Nape ambaye alikuwa akizungumza wakati akifungua Kongamano la Vijana mkoani Mwanza lililofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Benki Kuu (BOT) Kapripoint jijini Mwanza, juzi, alisema, kwa upande wake CCM kuhusu kipengele hicho cha Tanzania kuwa na serikali ngapi, msimamo wake ni serikali mbili.

"Sisi CCM tunapotangaza msimamo wetu kwamba nchi hii inastahili kuwa ya serikali mbili, haina maana kwamba tunadharau au kuwaona wapuuzi  wanaopendekeza ziwe tatu, la, msimamo wetu huu tunaueleza kwa hoja ili hatimaye jamii ya Watanzania ikiziona zina mantiki watuunge mkono", alisema Nape.

Aidha Nape alisema, umuhimu wa kuwa makini na kutumia busara katika jamii kuhitaji mabadiliko unatokana na kwamba jamii ikiyapokea kwa pupa huambulia yasichotarajia, ikiwemo machafuko au uongozi wasiohitaji kwa ajili ya kukidhi matakwa yao ya maendeleo.

Nape alisema  katika pupa ya kutafuta mabadiliko, zipo baadhi ya nchi kama Misri ambazo hadi sasa zimekosa utulivu kutokana na kupokea vibaya dhana ya mabadiliko, wakaingia mitaani lakini bila kuchukua tahadhari, hatimaye wamejikuta mabadiliko waliyopata nayo hawayataki tena, wanataka mengine.

Akifafanua alisema, CCM inatambua kwamba, muundo wa serikali mbili ndio utafaa katika kudumisha Muungano, kuliko serikali tatu ambazo CCM inaona kwamba mbali ya kuwa mzigo zaidi kwa wananchi, pia ni kuongeza changamoto juu za zile zilizopo sasa kwenye muungano.

mchungaji peter msigwa atoa msaada wa chakula chuo cha kiislam kitanzini islamic center mkoani iringa leo.

$
0
0

MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini (CHADEMA),mchungaji Peter Msigwa ametoa msaada wa chakula cha futari chenye thamani ya shiling milion moja na laki nne katika chuo cha kiislam kiitwacho kitanzini Islamic Center kilichopo kitanzini mkoani humo.


Msingwa amesema kuwa lengo la kutoa msaada huo ni kuwapatia chakula cha futari wanachuo hao pamoja na uongozi mzima katika mwezi huu wa ramadhani na kuondoa ubaguzi na itikadi za kichama pamoja na za kidini na kuifanya Tanzania kuwa moja,


Sambamba na hayo Msigwa alibainisha kuwa kuwaelimisha wanachuo wanaosoma chuoni hapo ni moja ya maendeleo katika jamii nzima, kwa sababu ni wanafunzi wanaotoka katika mikoa yote ya Tanzania.


Kwa upande wake sheikh Mkuu wa mkoa wa Iringa, Ally Tagalile amesema kuwa anashukuru kwa kuwakumbuka na kuwajali wanachuo hao bila kujali itikadi ya dini ya mbunge wa jimbo hilo



Tagalile amesema kuwa viongozi waache kuwabagua waislam hasa katika mwezi huu mtukufu wa ramadhani, badala yake wawajali na kuwapa heshima kama wanavyo wapa wakiristu wakiwa katika mfungo.

MGANGA WA KIENYEJI AUWAWA NA WATU WASIOJULIKANA MKOANI IRINGA.

$
0
0
MGANGA mmoja wa kienyeji  aliyefahamika kwa jina la George Tereva (55) amefariki dunia baada ya kupigwa risasi maeneo ya tumboni,kichwani na kwenye paji la uso kisha kukaktwa na panga kichwani na watu wawili wasiojulikana.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa moja na nusu katika kijiji cha Lungemba kata ya Lungemba wilaya ya Mufindi.


Kamanda alisema kuwa watuhumiwa wa tukio hilo wanatafutwa na jeshi la polisi na mara watakapopatikana watafikishwa kituoni uchunguzi utakapo kamilika . kamanda alibainisha kuwa chanzo cha tukio hilo hakijajulikana



KONGAMANO LA VIJANA NA RASILIMALI ZA TAIFA LAFANYIKA DAR

$
0
0
 Mwenyekiti wa Kongamano la Vijana na Rasilimali, lililofanyika leo RiverSide, Ubungo jijini Dar es Salaam, Christopher Ngubiagai, akifungua mjadala kuhusu mada mbalimbali. Kushoto ni Waziri wa Nishati na madini Profesa Sospeter Muhongo na watatu ni mtoa mada, Wakili Evod Mmanda ambaye pia ni Mjumbe wa NEC wa CCM. Ngubiagai pia ni Katibu wa CCM mkoa wa vyuo vya elimu ya Juu.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhomgo akitoa mada kuhusu rasilimali ya madini, wakati kwenye kongamano la vijana na rasilimali za taifa, leo Ubungo jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Katibu wa CCM, Vyuo vya elimu ya Juu, Christopher Ngubiagai ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa kongamano hilo na watatu ni mwanasheria Evod  Mmanda aliyetoa mada kuhusu rasimu ya Katiba.
Wakili Mmanda akitoa mada kwenye kongamano hilo
 Ngubiagai akizungumza kwenye kongamano hilo
 Baadhi ya viongozi wa Vijana wa CCM  kutoka mkoa wa vyuo vya elimu ya juu wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Baadhi ya wadau wakiwa kwenye kongamano hilo
 Baadhi ya wadau wakifuatilia mada kwenye kongamano hilo
 Wadau wakifuatilia hoja mbalimbali kwenye kongamano hilo
 Baadhi ya wawakilishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakichukua matukio kwenye kongamano hilo-
 Meza ya usajili wa waalilkwa waliofika kwenye kongamano hilo. Imetayarishwa na theNkoromo Blog

NSSF YAZIDI KUTOA ELIMU JUU YA FAIDA YA MFUKO HUO NDANI YA MAOENESHO YA NANE MJINI MOROGORO.

$
0
0
 
 MKUU wa idara ya Uhusiano NSSF Taifa Eunice Chiume (mwenye t-shirt ya kijani) akisikiliza malezo yanayotolewa kwa mmoja wa wanachama wa mfuko huo na Afisa mfawidhi Matekelezo NSSF Mkoa wa Morogoro Christopher Msagati  Katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere maarufu Nanenane nje kidogo ya Mji wa Morogoro.
Afisa mwandamizi wa mafao katika mfuko wa NSSF Mkoa wa Morogoro Adolfrida Mulokozi akitoa elimu ya faida ya mfuko huo kwa wanachama wapya ndani ya viwanja vya  Mwalimu Julius Nyerere maarufu Nanenane nje kidogo ya Mji wa Morogoro pembeni ni mwenye T-shirt ya kijani ni mkuu wa idara ya uhusiano NSSF Taifa Eunice Chiume.

grandmalt yafuturisha wadau wake.

$
0
0
Meneja masoko wa Tbl Fimbo Mohamed Buttala akizungumza na waandishi wa habari kwenye futari maalum iliyoandaliwa na kinywaji cxha GrandMalt ikiwa ni sehemu ya kutambua Mwezi mtukufu wa ramadhani ambapo futari hiyo iliandaliwa na kinywaji kisicho na kilevi cha GrandMalt.
 Mkurugenzi wa masoko wa TBL Kushilla Thomas mwenye shati jeupe akishirikiana na wadau mbalimbali katika futari maalum iliyoandaliwa kwaajili kufuturu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo futari hiyo iliandaliwa na kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt.
 Wadau mbalimbali wakiongozwa na Kabula Nshimbo (hayupo pichani) wakishirikiana na wadau mbalimbali katika futari maalum iliyoandaliwa kwaajili kufuturu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo futari hiyo iliandaliwa na kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt. 

MKUU WA MKOA WA RUKWA ATEMBELEA MAONESHO YA WAKULIMA NANENANE NYANDA ZA JUU KUSINI JIJINI MBEYA.

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya (katikati) akikagua mfumo wa umwagiliaji bustani za mbogamboga katika maonesho yanayoendelea ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.  
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akipokea maelezo kutoka kwa wataalam wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST) juu ya gari iliyotengenezewa mfumo wa nishati ya gesi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua bidhaa mbalimbali kwenye banda la Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya. Mkuu huyo wa Mkoa ameridhishwa na vifungashio vingi vilivyotumika katika maonesho hayo mwaka huu na wajasiriamali wa Mkoa wa Rukwa.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiangalia "shamba jiko" ambalo staili yake ni ya kupanda mbogamboga nyumbani katika eneo dogo kwenye maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua maji aina ya Dew Drop, maji pekee yanayotengenezwa Mkoani Rukwa Mjini Sumbawanga na Mjasiriamali wa ndani, maji ambayo wananchi na wadau wengi wanasifia ubora wake kuwa ni ya kiwango cha juu. Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima wakikagua banda la Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga ambalo limesifika kwa umaridadi wake.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikagua samaki mbalimbali waliopo katika moja ya banda la Wilaya ya Nkasi katika maonesho ya nanenane kanda ya nyanda za juu kusini jijini Mbeya. Samaki hao wamekaushwa kitaalam na wana uwezo wa kukaa mda mrefu bila kuharibika.

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima wakipata maelezo kwa mtaalam wa hali ya hewa walipotembelea kituo cha hali ya hewa kilichopo katika maonesho hayo. Kifaa kinachoonekana kinatumika kupima wingi wa mvua.
 TanSeed wakitangaza bidhaa zao za mbegu kwa staili ya aina yake.
 Ebony Fm Radio ya nyanda za juu kusini ambayo makao makuu yake ni Mjini Iringa ikifanya mahojiano ya moja kwa moja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya mara baada ya kiongozi huyo kuzungukia mabanda kuzungumzia maonesho hayo kwa ujumla wake.

Picha ya pamoja kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya na baadhi wafanyakazi wa Radio ya Ebony FM ya Mjini Iringa maara baada ya Interview.



MC MIMA, Misasi Marco akipaisha vokali zake.

Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akitangaza rasmi kuzaliwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya katika usiku wa maonesho ya nanenane "Rukwa Day" katika ukumbi wa JKT Nanenane Jijini Mbeya saa 12:01 Usiku wa tarehe 04/08/2013. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Ndugu Methew Sedoyyeka.

 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akiwa amebebwa juujuu na wananchi pamoja na watumishi walioshiriki hafla fupi ya "Rukwa Day" katika maonesha ya nanene nyanda za juu kusini Jijini Mbeya ikiwa ni pongezi kwake katika siku yake ya kuzaliwa ya tarehe 04/08.

Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa Ndugu Respich Maengo akimpongeza Mhe. Manyanya kwa siku yake ya kuzaliwa.

Simon Mutabazi Mkaguzi wa ndani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akimpongeza Mhe. Manyanya kwa siku yake ya kuzaliwa.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa "rukwareview.blogspot.com)

MPAMBANO WA MASUMBWI KUPIGWA MUHEZA TANGA SIKU YA IDI PILI

$
0
0

MPAMBANO  mwingine wa masumbwi unatarajia kufanyika Muheza mkoa wa Tanga wakati wa siku kuu ya idi pili kwa ajili  ya kutoa burudani kwa wakazi wa Muheza akizungumza kuhusu mpambano huo mratibu wake ambaye ndiye mwandaaji wa mpambano huo Hatibu Mwijuma amesema mpambano huo umeandaliwa maalumu kwa ajili ya kutoa burudani wakati wa sikukuu ya Idi na mpambano utafanyika katika viwanja vya jitegemee

Mpambano huo utakaowausisha mabondia kutoka Dar es salaam na wa Muheza, Mbena Rajabu wa Dar atakaeoneshana kazi na Jumanne Mohamedi mpambano wa raundi sita huku George Allan wa Muheza ataoneshana ubabe na  Muhamed Meme wa Tanga

na mapambano mengine mengi ya kukata na shoka uku kukiwa na burudani ya muziki alitaja kiingilio kwa siku hiyo kwa kuwa tunaitaji kila mtu aje kushudia mchezo wa ngumi kwani  ni nafasi ya pekee tuliyoipata kingilio kitakuwa ni 2000,kwa 1000,


ili watu waweze kuangalia ulinzi ni wa uwakika mchezo uho utakaosimamiwa na Oganaizeshani ya ngumi za Kulipwa nchini TPBO umereta faraja kwa wakazi wa muheza kwani wana kiu kubwa ya kuangalia mchezo huo wa masumbwi unaopenda na watu wengi

WAKAZI WA KIJIJI CHA KIWERE NA KIPERA MKOANI IRINGA WALAZIMIKA KUTEMBEA UMBALI WA KM 50 KUFUATIA KIVUKO CHAO KUZOLEWA NA MAJI

$
0
0
 Wakazi wa kijiji cha kiwere na Kipera vilivyopo kata ya Karenga wilaya ya Iringa wakitembea juu ya kivuko chao cha miti cha muda baada ya kivuko chao kuondolewa na maji,aidha Wakazi hao wanalazimika kutembea umbali wa km 50 baada ya daraja la mti kuzolewa na maji.

WAKAZI wa kijiji cha kiwere na Kipera vilivyopo kata ya karenga wilaya ya Iringa wanalazimika kutembea umbali wa km 50 baada ya daraja la mti kuzolewa na maji.
 Akizungumza mwenyekiti wa kijiji cha kiwere,Yustin  Lipita alisema kuwa kutokana na ubovu wa daraja ambalo linaunganisha vijiji hivyo viwili wanakijiji hao wanalazimika kutembea umbali mrefu ili kufuata zahanati ya serikali ambayo ipo katika kijiji cha kipera .
  
“tunaiomba serikali kutujengea daraja ili wakazi wa kiwere na kipera waondokane na adha ya kutembea umbali mrefu kupitia Mlambalasi mpakani mwa Tarafa ya Pawaga na Kalenga palipo na umbali wa klm.46 kufuata shughuli zao za kilimo pamoja na huduma muhimu za kijamii”alisema Lipita.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha kipera Bonifasi Mgomati alisema kuwa Changamoto nyingi zimejitokeza kutokana na ubovu wa kivuko hicho ni vifo vya wakazi wa vijiji hivyo pamoja na kupoteza vitu vingi kama mizigo na Baiskeli kuendana  maji.
    
“Ni kivuko cha mudamrefu katika eneo hili toka mwaka 1975 Ingawa kabla ya hapo ilitumika kamba ya katani iliofungwa Ng’ambo na Ng’ambo na mvukaji kuitegemea anapovuka “alisema mgomati.
Sambamba na hayo mkazi mmoja wa kijiji cha kipera Antoni Kigehe alisema wanalazimika kutumia kivukohicho wanapokwenda katika Mashamba yao yaumwagiliaji  yaliopo kijiji cha Kiwere jambo ambalo ni hatari kutokana na  mazingira ya Daraja hilo la Miti pia ni vigumu watoto wadogo kuvuka pekeyao kwakuhofia usalama.

Mhasibu Aibuka mshindi wa Nyumba kupitia promosheni ya Airtel yatosha

$
0
0


 Meneja Uhusiano wa Airtel  Bw, Jackson Mmbando , Msimamzi wa  bodi ya michezo ya Kubahatisha Tanzania Bw, Mrisho Milao kulia Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga wakisubiri draw ya kutafuta mshindi itafutenamba ya mshindi wakati wa kuchezesha droo ya kwanza ya kumsaka mshindi wa nyumba ya kwanza kupitia promosheni ya Airtel yatosha. 
Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga wakwanza kulia akiongea na mshindi wa nyumba mara baada  ya kupatikana katika draw ya mwenzi iliyofanyika katika makao makuu ya Airtel morocco ambapo bwana

Silvanus Juma kutoka mkoa wa iringa aliibuka mshindi wa nyumba hiyo wakishuhudia Msimamzi wa  bodi ya michezo ya Kubahatisha Tanzania Bw, Mrisho Milao katikati akifatiwa na Meneja Uhusiano wa Airtel  Bw,

Jackson Mmbando .

Meneja Uhusiano wa Airtel  Bw, Jackson Mmbando  akiongea wakati wa  kuchezesha droo ya kwanza ya kumsaka mshindi wa nyumba ya kwanza  kupitia promosheni ya Airtel yatosha , kushoto Msimamzi wa  bodi ya  michezo ya Kubahatisha Tanzania Bw, Mrisho Milao kulia Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga wakwanza kulia. Droo ya Airtel yatosha ilimpata mshindi wa nyumba bwana Silvanus Juma kutoka mkoa wa iringa.


=========   ========   =======
Airtel Tanzania imetangaza mshindi wa kwanza wa nyumba  kupitia
promosheni ya Airtel yatosha Shinda nyumba inayoendelea  na
kuwazawadia wateja wake kila siku.

Bwana Silvanus Juma mkazi wa Iringa mwenye umri wa miaka 33 ambaye ni
mhasibu katika shirila la Tanzania Rural women and children
development foundation - TARWOC ameibuka mshindi na kuzawadiwa  nyumba kisasa iliyojengwa na shirika na nyumba la taifa NHC iliyopo kigamboni jijini Dar es saalam.

Akiongea wakati wa kuchezesha droo hiyo Meneja Uhusiano wa Airtel
bwana Jackson Mmbando alisema" kama tulivyowangazia awali leo ndio ile
siku muhimu na maalumu ya kumpata mshindi wetu wa kwanza wa nyumba  na tumeshuhudia bwana Silvanus Juma  akiibuka mshindi kupitia droo ya kwanza tuliyoichezesha hapa.

Sambaba na hilo leo tunao washindi 7 wa wiki  kutoka katika mikoa
mbalimbali ambao hawa wataondoka na pesa taslimu shilingi  milioni
moja kila moja, washindi hawa ni pamoja na  Peter Ignasho kutoka
Muheza Tanga, Edita Rweyabura  kutoka Bukoba, Steven Maguro , Rakesh
Ali Mauji, Mwajuma Hassani kutoka Dar es Saalam, Siasa Yahaya Songo
kutoka Manyoni Singida and Vero Mispela Kiwango kutoka Bihalamulo.

Natoa wito kwa watanzania na wateja wetu kuendelea kutumia huduma ya
Airtel yatosha na kujiunga na vifurushi mbalimbali na kupata nafasi ya
kujishindia zawadi mbalimbali , kujiunga nirahisi piga  *149*99#
kisha nunua kifurushi chacko cha  siku, wiki au mwezi  na kisha
kuingizwa moja kwamoja kweny droo ya kuweza kushinda milioni moja kila
siku au zawadi kubwa ya Nyumba.

Akiongea mara baada ya kutangazwa mshindi Bwan Silvanus Juma
alisema"Ninayofuraha sana kupata zawadi hii kubwa kutoka Airtel
napenda kutoa wito kwa watanzania na wateja wa Airtel waendelee
kutumia huduma ya Airtel yatosha na waamini kuwa hakuna upendeleo.
Binafsi sijawahi kushinda Bahati nasibu yoyote na nilikuwa siamini
kama hakuna ubaguzi kwenye kushinda, lakini leo nashuhudia kwamba
ushindi ni wa uhakika usio na upendeleo wala ubaguzi hivyo wajaribu
nao wanaweza kuwa washindi.

Kwa upande wake moja ya wafanyakazi wenzake Bwana Beatus Magoti ambaye ni Mshauri wa fedha na utawala TARWOC alisema"  tumefurahi sana kuona kijana mgodo mwenzetu ambaye ni mchapa kazi ameweza kushinda nyumba kupitia promosheni ya Airtel yatosha.  Hii imetupa hamasa na sisi
kushiriki na kueneza habari kwa wengine kushiriki na kushinda kama
laivyoshinda Silvano.

Airtel inaendelea na promosheni ya Airtel yatosha shinda nyumba tatu
ikiwa na lengo la kuwazawadia wateja wake na kutoa huduma bora zenye
gharama nafuu kupitia huduma ya Airtel yatosha.  Sambamba na hilo
Airtel pia imewawezesha wateja wake nchi nzima  kutuma na kutoa pesa
bure bila makato yoyote.



Vodacom Foundation yakabidhi sadaka ya vyakula na vifaa vya shule gombani-pemba

$
0
0
 Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis(mwenye koti jeusi) na Mwenyekiti wa Vodacom Foundation Hassan Saleh (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Vodacom na baadhi ya wanafunzi wa Madrasa za Kisiwani Pemba mara baada ya zoezi la kukabidhi sadaka ya vyakula na vifaa vya shule kwa wanafunzi hao muda mfupi kabla ya wote kushiriki futrari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation kwenye uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba mwishoni mwa wiki.
 Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Jaffary Juma akikabidhi vyakula vilivyotolewa na Vodacom Foundation kwa wanafunzi wa madrasa mbalimbali za Kisiwani Pemba tukio lililohusisha pia futari kwa ajili ya wanafunzi hao na wadau wa Vodacom Kisiwani humo iliyofanyika uwanja wa Gombani mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis(mwenye koti jeusi) na Mwenyekiti wa Vodacom Foundation Hassan Saleh (kulia) na wafanyakazi wa Vodacom.
 Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim akizungumzia kampeni ya Pamoja na Vodacom namna inavyotekelezwa wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kuandaa futari na kutoa sadaka ya vyakula na vifaa vya shule kwa wanafunzi wa madrasa sehemu mbalimbali nchini. Mwaka huu Vodacom Foundation ilitenga Sh. 50 Milioni kwa ajili ya kampeni hiyo na kuwafikia wanafunzi zaidi ya 2500.
Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis akisalimiana na viongozi mbalimbali wa dini ya kiislamu wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Uwanja wa Gombani Pemba tayari kuongoza hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na Vodacom Foundation mwishoni mwa wiki kwa ajili ya wanafunzi wa Madrasa na wadau wa kampuni hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Vodacom Foundation Hassan Saleh

Grooveback Jumamosi Hii @ East 24/Arcade-Mikocheni

SuperSport yaja na burudani kemkem za ligi mbambali za soka katika msimu mpya unaoanza mwezi huu.

$
0
0
DSC_0895
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar kuhusiana na msimu mpya  wa  ligi za soka katika SuperSport. Wengine katika picha kutoka kushoto ni  Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu Meneja Mauzo Salum Salum pamoja na Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi.
DSC_0882
Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi (wa pili kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema DStv imezidi kusogeza huduma kwa wateja wake ambapo hivi karibuni imefungua tawi jipya  Kariakoo barabara ya Msimbazi na kuongeza kuwa kuanzia sasa Channel ya SuperSport itakuwa ikionekana katika eneo lote la kusini mwa jangwa la Sahara.
DSC_0898
Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu  (kushoto) akizungumza na wanahabari ambapo amewataka wananchi kujiunga na huduma za DStv kwani bei zake ni nafuu na picha zake zinaonekana katika kiwango bora.
Kama mtu ni mteja aliyeunganishwa na DStv, sasa atapata msisimko zaidi akisikia kuwa kuanzia mwezi huu wa Agosti SuperSport’s football itawaletea mambo mengi na mazuri zaidi.
Katika msimu mpya, SuperSport itawaletea michapo yote inayohusu soka la Uingereza kwa sasa ambapo kocha mtata Jose Maurinho amerejea katika Ligi Kuu ya Uingereza.
Kama vile hiyo haitoshi pia Bundesliga itakuwa ikionekana katika SuperSport pekee katika eneo lote la Kusini mwa Jangwa la Sahara itakuwa ni ligi nyingine itakasisimu katika msimu mpya.
Kwa sasa Ligi hiyo ndio inayopewa kiwango cha juu barani Ulaya kufuatia mafanikio ya timu za Bayern Munich na Borussia Dortmund katika msimu uliopita wa michuano ya Ligi ya UEFA na sasa wanatamba kuwa na moja ya meneja mwenye mafanikio katika kipindi cha miaka mitano Pep Guardiola.
SuperSport ni mahali pekee kutazama ligi mbalimbali za soka.
Ligi hizo ni pamoja na English Premier League (EPL), Spanish La Liga, Italian Serie A, German Bundesliga, UEFA Champions League, UEFA Europa League, South African Premier Soccer League (PSL), Kenya Premier League (KPL), Uganda Super League (USL), Nigerian Premier League (NPL), Angolan Girabola, Ghana Premier League, Zambia Premier League na CAF Champions League.Habari picha kwa hisani ya dewjiblog

NAPE:CCM BADO INA IMANI KUBWA NA TUME YA KATIBA

$
0
0

Nape Nnauye
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) kimesema bado kina imani na Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini, katika mchakato unaoendelea wa kupata katiba mpya.

Imesema licha ya CCM kutofautiana kimawazo katika baadhi ya maeneo katika rasimu ya kwanza ya  katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, lakini haina ugomvi na tume hiyo.

Hayo yamesemwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.

 "Tunawaheshimu sana wajumbe wa tume hii, na kwa kweli tunamatumaini nao sana kuwa watatimiza wajibu wao kwa weledi mkubwa", alisema Nape.

Nape alibainisha kwamba  pamoja na maeneo mengine ya rasimu ya kwanza ya katiba ,  CCM ina mawazo tofauti kwenye suala la Muundo wa Muungano ambapo wakati rasimu inapendekeza muundo wa serikali tatu, CCM yenyewe inapendekeza  serikali mbili.

"Kama mnavyoona katika hili, wakati tume inapendekeza muundo wa serikali tatu sisi CCM tunapendekeza muundo wa serikali mbili, lakini hii haitufanyi tuwapuuze au tugombane na wale wenye mawazo tofauti na yetu", alisema Nape na kuongeza;

"Kumekuwepo na ripoti na makala kadhaa zinazojaribu kuonyesha kama vile kuna mvutano kati ya tume na CCM, au CCM na wengine wenye mawazo tofauti na CCM. Ukweli ni kuwa hali hiyo inayojaribu kujengwa kwa nguvu si ya kweli. Tuache hoja zishindane kwa hoja na nguvu ya hoja ndio iwe msingi wa ushindani".

Nape alitaka ushindani uwe kwenye hoja bila kushutumiana ili jatimaye mawazo ya wengi yasikilizwe na kuzingatiwa.

Alisema, CCM inasisitiza kuwa itaheshimu mawazo ya Watanzania, kwani katiba inayotengenezwa ni ya watanzania wote bila ya kujali itikadi zao.

"Naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru wale wote wanaounga mkono baadhi ya hoja za CCM hasa hoja ya serikali mbili. Tumeshuhudia maoni ya wajumbe wengi wa  mabaraza na wananchi kwa ujumla wakiunga mkono mawazo haya ya CCM ya muundo wa muungano wa serikali mbili na hoja kadhaa zingine", alisema Nape na kuongeza;

"CCM tunapenda kuwashukuru wote. Tujadili kwa kuvumiliana, tukipendana na kuheshimiana. Tanzania yenye neema tele inawezekana".

MKOA WA NJOMBE UNAONGOZA KWA MAAMBUKIZI MAKUBWA YA VIRUSI VYA UKIMWI-TACAIDS

$
0
0

TUME ya Kudhibiti UKIMWI nchini (TACAIDS) imesema mkoa wa Njombe unaongoza kwa kuwa na maambukizi makubwa ya Virusi vya UKIMWI kwa asilimia 14.8 ikifuatiwa na Iringa kwa asilimia 9.1. 

Mkoa wa Mbeya unashika nafasi ya nne kwa asilimia tisa ukifuatiwa na Ruvuma (7.2), Shinyanga (7.4), Dar es Salaam (6.9) Rukwa (6.2), Katavi (5.9), Pwani (5.9),Tabora (5.1), Kagera (4.8) na Geita (4.7).

Msemaji wa TACAIDS, Glory Mziray alisema hayo jana Dar es Salaam na wakati akizungumza na waandishi wa habari. 

Mikoa mingine na viwango vyake ni Mara (4.5), Mwanza (4.2),Mtwara (4.10), Kilimanjaro (3.8), Kigoma (3.4), Simiyu (3.6), Morogoro (3.8), Singida (3.3), Dodoma (2.9), Manyara (1.5), Lindi (2.9), Tanga (2.4), Unguja (1.9) na Pemba (0.3).

Alisema takwimu hizo zinatokana na utafiti uliofanyika mwaka juzi hadi mwaka jana. Kutokana na matokeo hayo, alisema maambukizi ya UKIMWI yamepungua kwa kasi ndogo.

Alisema watanzania walioonesha kuwa na ufahamu sahihi wa elimu kuhusu Virusi vya ukimwi na UKIMWI wanafikia asilimia 60 jambo linalosababisha kuwepo mwamko mdogo wa kubadili tabia.

Kuhusu tohara kwa wanaume endapo inapunguza maambukizi ya UKIMWI alisema inapunguza kwa asilimia 60 na kusisitiza kuwa ipo haja kutoa elimu zaidi juuya uelewa wa ugonjwa huo.

TAMASHA LA IDD MOSI DAR LIVE: WASANII, MABONDIA WALONGA NA WANAHABARI

$
0
0
Meneja wa Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kulia) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu burudani mbalimbali zitakazokuwepo Dar Live sikukuu ya Idd Mosi. 
Mratibu wa mapambano ya ndondi, Abdallah Yasin 'Ustaadh' (kulia) akiongea na wanahabari. Kushoto ni Abdallah Mrisho.
Mwanamuziki Ali Kiba (kulia) akipeana 'hi' na Ustaadh wakati wa mkutano huo.

WASANII wa muziki watakaopanda katika jukwaa la kisasa la Dar Live sikukuu ya Idd Mosi pamoja na mabondia leo wamelonga na wanahabari kwenye mkutano uliowakutanisha ambao umefanyika katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wasanii wametambiana kila mmoja akitamba kuwa atamfunika mwenzake. Vilevile mabondia nao wametunishiana misuli hali inayoonyesha kuwa kutakuwa na bonge la burudani katika sikukuu hiyo ya Idd Mosi.

Katika sikukuu hiyo wasanii Ali Kiba, H-Baba, Chegge, Temba, Dogo Aslay, Bi. Cheka na Bendi ya Mapacha Watatu watashusha bonge la burudani na kuwapa raha mashabiki watakaohudhuria shoo hiyo. Kwa Upande wa masumbwi bondia Francis Miyeyusho atazipiga na Darius Lupupa kutoka nchini Zambia, Chupaki Chipindi atapigana na Ramadhan Kido. Vilevile mabondia wa kike Ester Kimbe na Irene Kimaro wataonyeshana moto siku hiyo.



 Mwanamuziki H - Baba akitamba mbele ya wanahabari (hawapo pichani) kuwa atafunika mbovu siku hiyo.
Bondia Francis Miyeyusho akitunisha misuli. Bondia huyu atapigana na Mzambia Darius Lupupa.
Bondia Chupaki Chipindi atakayezipiga na Ramadhan Kido.
Ramadhan Kido atakayepambana na Chupaki Chipindi siku hiyo.
Mabondia wa kike Ester Kimbe (kushoto) na Irene Kimaro wakijaribu kuzipiga.
Mabondia Francis Miyeyusho (kulia) na Ramadhan Kido (kushoto) wakifuatilia mkutano huo.
Chupaki Chipindi kutoka mkoani Iringa akiwa kwenye pozi.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo.
Bondia Ester katika pozi.
Bondia Irene naye akiwa kwenye picha ya pozi.
H - Baba katika pozi la kusimama.
Ester ndani ya gloves.

WASANII wa muziki watakaopanda katika jukwaa la kisasa la Dar Live sikukuu ya Idd Mosi pamoja na mabondia leo wamelonga na wanahabari kwenye mkutano uliowakutanisha ambao umefanyika katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza Afrikasana jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo wasanii wametambiana kila mmoja akitamba kuwa atamfunika mwenzake. Vilevile mabondia nao wametunishiana misuli hali inayoonyesha kuwa kutakuwa na bonge la burudani katika sikukuu hiyo ya Idd Mosi.
Katika sikukuu hiyo wasanii Ali Kiba, H-Baba, Chegge, Temba, Dogo Aslay, Bi. Cheka na Bendi ya Mapacha Watatu watashusha bonge la burudani na kuwapa raha mashabiki watakaohudhuria shoo hiyo. Kwa Upande wa masumbwi bondia Francis Miyeyusho atazipiga na Darius Lupupa kutoka nchini Zambia, Chupaki Chipindi atapigana na Ramadhan Kido. Vilevile mabondia wa kike Ester Kimbe na Irene Kimaro wataonyeshana moto siku hiyo.

(PICHA: SHAKOOR JONGO /GPL)

SERIKALI YAHIMIZA UFUGAJI NYUKI

$
0
0
Naibu Waziri wa Maendeleao ya Mifugio na Uvuvi, Mhe. Benedict Ole Nangoro (MB) (mwenye suti) akipokea zawadi kutoka kwa mmoja wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii kutoka kikundi cha SULEDO. 
========   =========  ========
Serikali imeimiza wananchi kujikita katika miradi ya ufugaji nyuki inayohitaji uwekezaji mdogo na faida kubwa ili kufikia lengo la kuwa na maisha bora kwa kila mtanzania.

Rai hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Maendeleao ya Mifugio na Uvuvi, Mhe. Benedict Ole Nangoro (MB) muda mfupi kabla ya kuzindua mashindano ya Mifugo na Maonesho ya Ufugaji Nyuki Kitaifa mwaka huu katika Uwanja wa Maonyesho ya Kilimo wa Nzuguni mjini Dodoma.


Mhe. Nangoro alisema shughuli za ufugaji nyuki ni nzuri na endelevu kutokana na kutohitaji mtaji mkubwa wakuanzia na hata uvunaji, usindikaji wa asali na mazao mengine yatokanayo na nyuki hutumia tekinologia rahisi.


“Utunzaji ama ufugaji nyuki ni shughuli inayomwezesha mwananchi kupata kipato cha kutosha bila kuwekeza mtaji mkubwa lakini pia tekinolojia yake ni rahisi kwani haina madai ya ajabu ajabu,” alisema Mhe. Naibu Waziri.


Mhe. Nangoro alisema shughuli za ufugaji nyuki ni eneo lingine ambalo watu wakielekeza ujasiriamali wao watanufaika bila madai makubwa na hivyo kujiongezea kipato katika kaya, kuchangia lishe, tiba, uboreshaji wa mazingira na utunzaji wa habitanti inayohitajika na nyuki kuzalisha asali.


Aidha, Mhe. Naibu Waziri na vingozi waandamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii walipata fursa ya kutembelea Mradi wa Ufugaji Nyuki wa Chama cha Ushirika cha Huduma, Mtandao wa Askari wa kike Tanzania wilayani Chamwino kujionea shughuli mbalimbali za kikundi hicho.


Akielezea mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Bi. Fatma Ally alisema, walianzisha mradi huo mwezi Oktoba 2012 ili kupata fedha za kuendesha huduma kwa akina mama na watoto wanaofanyiwa ukatili na unyanyasaji wa kimwili, kiuchumi na kiakili.


Alisema mradi huo una jumla ya mizinga 543 yenye uwezo wa kuzalisha wastani wa lita 5000 za asali zenye thamani ya tshs 50, 000, 00/= kwa mwaka.


Aidha, alisema wanatarajia mradi huo kutumika kama shamba darasa kanda ya kati na kuwa na mizinga zaidi ya 1000 ifikapo Desemba 2013; na kuendelea kuhamasisha uanzishwaji wa vikundi vingine vya ufugaji nyuki ndani na nje ya mkoa wa Dodoma.


Kufuatia mafanikio ya kikundi hicho, Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu ilitoa mizinga 10 kwa wanakikundi hao.


Akitoa mizinga hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Nuru Millao alisema Wizara imefarijika na mafanikio ya wanakikundi na hivyo imeamua kuwapa mizinga 10 ili waweze kufikia malengo ya kutimiza mizinga 1000.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Maendeleao ya Mifugio na Uvuvi, Mhe. Benedict Ole Nangoro (MB) aliwataka wanakikundi hao kuzingatia nidhamu kwenye kundi, kutunza mazingira ili waweze kupata asali yakutosha na kuepuka kulina asali kabla haijaiva.


Sherehe za Nane Nane zinafanyika Kitaifa mjini Dodoma katika Uwanja wa Maonyesho ya Kilimo wa Nzuguni uliopo kilomita saba kandokando mwa barabara ya Dar es Salaam kwenda Dodoma. Kauli mbio ya sherehe hizi mwaka huu ni “zalisha mazao ya kilimo na mifugo kwa kulenga mahitaji ya soko”.

RAIS KIKWETE AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU JIJINI DAR LEO.

$
0
0

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha baraza la Mawaziri kilichofanyika ikulu jijini Da es Salaam leo.Wapili Kulia ni Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na watu kulia ni Katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue.(Picha na Freddy Maro).

MKOA WA VYUO VYA ELIMU YA JUU CCM WAFANYA KUBWA LA WASOMI WA VYUO VIKUU KUJADILI RASIMU YA KATIBA,GESI

$
0
0
 Sehemu ya Vijana wa Vyuo Vikuu walioshiriki Kongamano la kujadili Rasimu ya Katiba Mpya na Rasilimali za nchi yetu.
 Baadhi ya Mafisa wa Mkoa wa Vyuo Vya Elimu ya Juu CCM wakiwa na mgeni rasmi wa Kongamano,Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo,katika ukumbi wa Riverside,Ubungo.
 Baadhi ya washiriki wa Kongamano wakifuatilia kwa makini hotuba ya Profesa Muhongo alipokuwa akichambua masuala ya gesi na uchumi.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo mbali mbali nchini wakichukua habari za Kongamano la Kujadili rasimu ya Katiba mpya na rasilimali lililofanyika katika ukumbi wa  Riverside Ubungo, ambalo liliratibiwa na Mkoa wa Vyuo Vya Elimu ya Juu CCM tarehe 5 Agosti 2013. 
Viewing all 46371 articles
Browse latest View live




Latest Images